Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[040]

 

 

 

Heri

(Toleo La 3.0 19940702-19991127-20070202)

 

Jarida hili linatafakari neno Heri na maana yake. Kila moja ya Heri hizi imefafanuliwa kwa utaratibu muafaka. Utimilifu wa Injili inayosisitiza afya na uzima yn utajiri au mafanikio kumetathiminiwa pia. Nafasi ya Nafasi ya katika utendaji wa mambo ya kimaongozi imejadiliwa pia.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1994, 1996, 1999, 2007 Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Heri


 


Heri zilizotajwa na kutolewa ni za maana sana. Mahubiri haya aliyoyafanya Kristo na kuandika kwenye Mathayo 5 yananguvu na matokeo makubwa sana.

 

Heri hizi ni mibaraka kwa Kanisa lake, na kwa watu wake. Zimechukuliwa kama mfano wa kuufuata au kigezo cha maisha na matendo ya wateule. Hata hivyo, zinaelezewa na Wakristo wa makanisa kongwe ya kale kwa namna dhaifu na potofu; kanuni zake zikilinganishwa na Injili ya udhaifu au yenye mapunguvu. Kusudi la kuandika jarida hili ni kufafanua jinsi tunavyoweza kujifunza kutokana na Heri hizi kwa namna bora, njema na imara.

 

Inasema kwenye Mathayo 5:1-12:

Mathayo 5:1-12 Naye alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia; 2 akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema, 3 Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 4 Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika. 5 Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi. 6 Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa. 7 Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema. 8 Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu. 9 Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu. 10 Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. 12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

 

Kristo analiambia Kanisa hapa, kitu kilicho cha hakika au cha kwanza kukifuata au kukifanya wanafunzi wake. Kisha anaendelea kuelezea kuhusu chumvi.

Mathayo 5:13-16 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu. 14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. 15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. 16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.

 

Kristo haishii hapa tu. Wakristo wengi wamesikia mambo haya huko nyuma, lakini wameshindwa kuyachambua kwa ujumla na kuweka kwenye mifuko midogo. Hawaichambui. Kristo anaongelea kwa mfuatano wa mambo kwa ujumbe halisi. Anaendelea kwa kusema hivi:

Mathayo 5:17-20 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. 19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. 20 Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Hawa ni watu kwenye Kanisa la Mungu, na wamekuwepo kwa kipindi cha karne kadhaa, na ni ambao wamefundishwa umuhimu wa kuzishika Sheria au Torati kwa namna mbalimbali. Wamefundishwa na kufundisha kwamba hatuna sababu ya kuzishika au pengine idadi nyingine ya mambo ya Kitorati. Kwa kweli kuna mambo mengine yahusuyo Amri na Torati ambazo hatuendelei kuzishika leo kwa sababu ya desturi za jamii inayotuzunguka tunayoishi nayo. Hata hivyo, hii sio ni kwa sababu amri na Sheria hizo zimetanguka la hasha, bali ni jamii tunayoishi nayo ndiyo imezikataa na kuziondolea mbali na kuzifanya zisitumike. Tena, katika siku fulani kadhaa zilizopita, baadhi ya Makanisa ya Mungu yametumia utetezi wa kwamba, kwa kuwa hatuzishiki tena hata mojawapo ya maagizo haya ya Torati, basi hatuhitaji kushika agizo linguine lolote la amri hizi leo. Kwa mfano, imeenezwa ushawishi kuwa hizi Siku Takatifu hazihitajiki kuadhimishwa kwa kuwa eneo au nafasi ya Torati hii inapotakiwa kuadhimishwa haliadhimishi tena.

 

Udadisi huu umefanywa kwa msingi kwamba jamii inakataza biashara ya kuuza mabinti (Kutoka 21:7) na maisha ya ndoa za wake wengi (Kutoka 21:10). Swali la kujiuliza ni kwamba Siku Takatifu (Kutoka 23:10-19) hazihitajiki kuadhimishwa. Mchakato huu huu wenye mashiko unaedelea hadi kwenye Sabato na Amri za Mungu (Kutoka 20:1-17; 23:1-13). Kama tulivyojadili kwenye maeneo yaliyopita, Torati haijatganguka bado kukiwepo na ndoa za matala, uuzaji wa mabinti au kuhusu uvaaji wa riboni za bluu kwenye nguo zetu (Hesabu 15:37-38; soma jarida la Amri ya Kwanza: Dhambi ya Shetani (Na. 153) [The First Commandment: the Sin of Satan (No. 153)]. Torati bado upo kwenye ukamilifu wake na hakuna hata yodi moja au kinukta kidogo kitakachopita. Sheria za kutoa sadaka za wanyama hazitumiki leo kwa kuwa sisi ni Hekalu. Wakati atakapokuja Masihi ataaiamsha tena imani na kuizisha tena. Lakini sio jukumu letu. Masihi alikuwa ni dhabihu ya ondoleo la dhambi na sadaka yake inatosha kututakasa na ambayo imetolewa mara moja tu kwa wote. Hii ndiyo Sheria pekee ambayo imehitimishwa katika ukamilifu wake. Sheria zingine hazitumiki kwa kuwa jamii haiuzi tena mabinti zao. Sheria za Australia na karibuni nchi zzote za magharibi haziruhusu ndoa za mitala lakini Sheria zipo pale kwa ajili ya wanajamii wazitende, na ndoa za mitala hazijakatazwa kwenye Biblia. Zaidi tu ni kwamba zimeruhusiwa.

 

Mfano huu umetumiwa sio kwa nia ya kutia moyo ndoa hizi ila ni kwa nia ya kuonyesha jinsi sheria inapofanya kazi na kudumu kwenye ubunifu au tunzi mbalimbali za jamii ya wanadamu. Kutakuja kipindi ambacho jamii zatu haitakuwa imara na Mungu atashughulika na sisi moja kwa moja na kuziharibu njia. Ataruhusu tushughulikiwe na mataifa, kwa baraka na laana zilizoandikwa kwenye Kumbukumbu la Torati 28 (soma jarida la Baraka na Laana (Na. 75) [The Blessings and the Curses (No. 75)].

 

Wakati watu wetu wanapokufa kabisa kati ya mamilioni (Isaya 3:25) na wanawake wanapotembea wakifanya uzinifu na watoto haramu waliozaliwa nje ya ndoa kwenye mataifa yetu, watazishika pindo za nguo zao na huku wakiwaambia wakisema: "Mtuondolee aibu yetu" (Isaya 4:1). Haya ni Maandiko Matakatifu, na Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka (Yohana 10:35).

 

Mambo haya yote yanafanyika ili kutimiliza makusudi maalumu ya Masihi na kuzifanya jamii za wanadamu ziende sawasawa na mapenzi ya Mungu. Na hii ndiyo sababu iliyopelekea tupewe Torati.

 

Tutazitathmini hizi Heri na kwenda moja kwa moja kwenye lengo lililoko nyuma yake na kuuona uweza inayokuwanayo.

 

Heri ya kwanza inasema: Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

 

Huu ni mkanganyo wa wazi. Sisi tu maskini wa roho kwa hiyo tunakwenda kuurithi Ufalme wa Mbinguni. Wakati kwamba kila tulichofundishwa kinasema kuwa tunapaswa kuwa matajiri wa roho. Inatupasa tufanye kazi na kujishughulisha ili kutimiliza na kuishi katika roho na kukua katika roho. Je, mambo haya yanawezekanaje? Je, inamaana kuwa tu kwamba kuwa maskini war oho kunamaanisha kuwa ni umaskini kwa maana ya udhaifu au uduni katika roho? Hapana, haimaanishi hivyo. Kuwa maskini wa roho kunamaanisha kwamba ni sisi kujitoa kikamilifu na kwa hiyari yetu kuwa sadaka kwa kadiri tuwezavyo kwa jirani zetu, ndugu zetu—na hapo tunakuwa maskini kwa hiyari kwa kujinyenyekeza na kuachilia mambo yetu yenye faida kwa watu tunaowatumikia. Inamaana kwamba utajiri, kama ulivyo tu peke yake, sio kigezo cha mtu kuonekana kuwa ni mteule. Mtazamo huu unapingana moja kwa moja na injili zinazohubiriwa siku hizi zinazosisitiza utajiri na mafanikio kuwa ni kigezo cha imani.

 

Katika miaka ya hivi karibuni, mambo mengi sana ya namna tofauti yamekuwa yakifundishwa na Kanisa la Mungu kuwa kuna injili inayosisitiza utajiri, mali na mafanikio – ikiwa ni falsafa ya kwamba magonjwa yanatokana na dhambi na kwamba mafanikio ni matokeo ya utakatifu. Imani au fundisho la kwamba magonjwa yanatokana na dhambi yanatokana na imani ya Kishamanism; na ni mafundisho potofu nay a kizushi. Ni mafundisho ya mapepo na tunakutana na mafundisho hayo kwenye makabila ya watu waliorudi nyuma wa jamii ya Kiasia wanaoishi chini ya imani ya kishetani ya kimapepo. Magonjwa yanayoila hii dunia yametokana na athari zilizotokea takriban miaka 6,000 ya uasi dhidi ya Sheria au Torati ya Mungu.

 

Baadhi yao, kama sio wote, miongoni mwa watu wetu kwa kiasi fulani wanaathari za kijenetiki kwa sababu ya maasi haya. Baadhi ya watu wanalazimika kwa njia ya ajira hadi kuwa kwenye mazingira yanaayowafanya waugue na wanahitaji kusaidiwa na kuonewa huruma. Watu wetu makanisani mwetu siku za huko nyuma walikuwa madaktari. Waliieneza Injili kwenye bara lote la Ulaya walitembelea majumbani, wakiwaponywa watu na kuwasaidia kwa namna mbalimbali. Magonjwa na maradhi hayakuchukuliwa kuwa ni matokeo ya dhambi na wazee wetu hawa wa imani waliohudumu huko nyuma. Bali waliwapenda watu walijaribu kuwaokoa. Waliwaponya, kuwalisha, kuwavalisha nguo na waliyahatarisha maisha yao ili kuwaokoa kwa kuwahubiria neno la Mungu. Walikubali kutoa mali zao, kujitoa sadaka na kujikana, na walisafiri ulimwenguni kote wakitembea kwa miguu, na walijinyenyekesha na kuyatoa maisha yao na maisha yao mazuri wakayatoa kwa faida ya wengine ulimwenguni. Walijaribu kuwaleta watu wote kwa Kristo, wakifanya hivyo kutokana na upendo waliokuwanao kwa watu wote na kujitoa kikamilifu na huku wakizidi kupendana kama ndugu.

 

Watu wetu waliyatoa maisha na nafsi zao kikamilifu kwa ajili yaw engine kwa kipindi cha karne kadhaa. Mwenye makanisa mengi ya karne ya kwanza walikuwa na ushirikiano mwema. Mitume waliweka utaratibu ambaokwamba walitoa fedha zao zote kwenye mfuko wa ushirika wao ambao ni kanisa na waliishi pamoja.

 

Hii haikutokana na jambo lingine lolote. Kama tutajaribu kufanya hivyo kwenye karne hii basi watu wengi wangeondoka na kuachana kabisa hata kabla hatujaanza. Tumesikia ikisemwa, wapende ndugu zako wapendwa wote, lakini kuna wengine unapaswa kuwapenda kwa mbali. Mtazamo kama huo unonyesha kuna matatizo makubwa sana ya kiroho, sio kwa hawa wanaosema hivyo tu, bali na wale waliosababisha kutokea mawazo haya. Watu wengine hawajui matokeo yanayoletwa na miendendo yao.

 

Kwa hiyo, tunaona hapa kwamba fundisho la kuwa maskini wa roho halimaanishi kuwa duni au kuwa na kiwango cha chini kiroho. Bali inamaanisha mtu kuwa maskini kwa kuweka maslahi yaw engine mbele, na kazi za Yesu Kristo kuiweka juu zaidi ya maslahi yetu binafsi.

 

Heri ya pili inasema: Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika.

 

Ni wapi basi tunapotapa wazo la kujlia kwa kuomboleza? Kwani kulia huku kwa kuomboleza ni nini? Je, kulia kwa kuomboleza kunawezaje kuwa baraka? Kulia na kuomboleza kunatokana na kupotelewa na kitu; au sivyo? Kwenye Ezekieli 9:4 tunapata wazo la maana yake. Kristo kwa kweli anaendeleza tu dhana hii ya kile alichokuwa anakisema Ezekieli. Tunaanza kutoka aya ya 1. Kichwa chake cha somo ni Mauaji ya Kuwachinja Waabudu Sanamu.

Ezekieli 9:1-11 Kisha akalia kwa sauti kuu masikioni mwangu, akisema, Waamuru wale wanaousimamia mji wakaribie, kila mmoja na awe na kitu chake cha kuangamiza mkononi mwake. 2 Na tazama, watu sita wakaja, wakitokea kwa njia ya lango la juu, lielekealo upande wa kaskazini, kila mmoja ana kitu chake cha kufisha mkononi mwake; na mtu mmoja kati yao amevaa bafta, naye ana kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. Wakaingia, wakasimama karibu na madhabahu ya shaba. 3 Na huo utukufu wa Bwana wa Israeli ulikuwa umepanda juu kutoka kwa kerubi, ambaye ulikuwa juu yake, mpaka kizingiti cha nyumba; akamwita mtu yule aliyekuwa amevaa bafta, mwenye kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. 4 Bwana akamwambia, Pita kati ya mji, kati ya Yerusalemu, ukatie alama katika vipaji vya nyuso vya watu wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika kati yake. 5 Na hao wengine aliwaambia, nami nalisikia, Piteni kati ya mji nyuma yake, mkapige; jicho lenu lisiachilie, wala msione huruma; 6 Waueni kabisa, mzee, na kijana, na msichana, na watoto wachanga, na wanawake; lakini msimkaribie mtu ye yote mwenye hiyo alama; tena anzeni katika patakatifu pangu. Basi, wakaanza kwa wazee waliokuwa mbele ya nyumba. 7 Akawaambia, itieni nyumba unajisi, mkazijaze nyua mizoga ya hao waliouawa; haya, enendeni. Wakaenenda, wakapiga-piga katika mji. 8 Tena ikawa, walipokuwa wakipiga, nami nikiachwa, nalianguka kifudifudi, nikalia, nikasema, Ee Bwana MUNGU! Utaangamiza mabaki yote ya Israeli, wakati wa kumwaga ghadhabu yako juu ya Yerusalemu? 9 Ndipo akaniambia, Uovu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni mwingi sana, nayo nchi imejaa damu, nao mji umejaa kupotosha hukumu; maana husema, Bwana ameiacha nchi hii, naye Bwana haoni. 10 Nami, jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; lakini nitaleta njia yao juu ya vichwa vyao. 11 Na tazama, mtu yule aliyevaa bafta, mwenye kidau cha wino kiunoni, akaleta habari, akisema, Nimefanya kama ulivyoniamuru.

 

Mchakato huu unaanzia kutoka kwa walio na vyeo vya juu sana vya wateule hawahawa na unaendelea kwa kushuka chini hadi kwa watu wetu. Tumepigwa mhuri ili tulie na kuombolea kadri tuwezavyo na kupiga kite kwa huzuni, tukilia na kutubu na kushinda. Wale ambao hawatalia na kuomboleza na kutubu watauawa: wanaume, wanawake na watoto. Huu sio ujumbe kwa wenye dhambi na waovu. Taifa la Australia, kwa mfano, litatiishwa na kunyenyekeshwa kwa upanga. Mji wa Sydney utatubia maadhimisho yake ya kikuu yake ya kipagani ya Mardi Gras. Mambo haya ni machukizo machoni pa Mungu na wataondolewa mbali nazo; na siyo mbaya kusema kwamba neno la Mungu linasimama. Watu hawa wanayaita mambo mema kuwa ni mabaya nay ale mabaya huyaita mema. Ni machukizo machoni pa Mungu na yanachoma mianzi ya pua yeke. Mungu atawaacha waangamizwe.

 

Kazi na wajibu wetu ni kuwaonya watu na kuzumbea kuahirisha kufanya hivyo kunamaanisha kuwa watoto watakufa. Na hii nd iyo maana tunabarikiwa kama tutalia na kuombolea na kuhuzunika na kunyongeka. Lakini tunapaswa kufanya hivyo kwa matendo, na sio kwa kujionyesha. Tunapaswa kuwa kimbelembele kwa kile tunachokifanya, na tusitende. Sio ni suala la kuonyesha kuhuzunika kwetu tu. Inatupasa tuondoke na kutoka hapo na kwenda kuwaambia. Inatupasa kutoa wito wa kutubu kwenye taifa hili – libadili mioyo ya mababa, au vinginevyo nchi hii itakufa. Huu sio mkosolewo wa kurithi tulionao lakini ni kuyapigia mstari tu matatizo muhimu. Uwezo wetu wa kuishi kama taifa na idadi ya watu wetu kwenye Milenia unategemea kwa kile tunachokifanya sasa. Hata idadi ya Wamataifa inategemea ni kwa kiasi gani tunafanya vizuri kazi yetu. Tuna zana chache na kuna watu wengi sana wamebalia na makosa ya zamani, kwa kuzembea na kujihesabia haki mwenyewe.

 

Heri ya tatu inasema: Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.

 

Inakanganya kusema tunapaswa kulipa changamoto wazo hili na ulimwengu, lakini je, tunapaswa kuwa wapole? Je, kuwa mpole maana yake ni nini? Je, upole ni dhambi au uhdaifu? Hapana! Upole sio ugoigoi au udhaifu.

 

Musa alikuwa mpole kuliko watu wote, lakini hakuna, kwa kuonyesha fikra yoyote, aliweza kusema kuwa alikuwa dhaifu. Kwa jinsi hiyohiyo, nguvu haitokani na wala haielezeki kwa namna ya, madai ya kimapokeo au nguvu za kutumia silaha, au matumizi ya wadhifa au cheo, au kwa kutumia mamlaka. Nguvu hazimaanishi kuwa na nafasi ya kiwadhifa na kutumbua au kutoa nje matumbo ya mtu aliye chini yetu. Nguvu inasababisha vifo vya watu wetu. 1Wakorintho 13 ni sura ya upendo, kama tujuavyo wote. Kusaidia, kwa maana ya upendo, unaofanyika bila masharti hujulikana kama ni upendo wa agape ambao ni wa Mungu. Ni suala la kimapendo ambalo limenenwa kinywani mwa Kristo alipokuwa mtini akisulibiwa wakati aliposema: “Baba wasamehe maana hawajui watendalo. Upendo huu ni upendo wa aina aliyousema Stefano midomoni mwake walipokuwa wanampiga kwa mawe hadi kufa. Alionyeshwa maono ya Ufalme yakimjia kupitia upendo huu. Jambo hili limeelezwa kwa kina kwenye swali lililo kwenye Heri mbili za mwisho.

 

Kutoka kwenye 1Wakorintho 13 tunaweza kupata wazo la kile alichokuwa anakisema Kristo kwa namna ya kusema juu ya upole huu na kuirithi Nchi. Ni aina ya upole unaotokana na kujifanya kuwa mdogo na chini ya wapendwa ndugu zetu.

Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

Kunapaswa kuwa na mwonekano wa wazi ya majukumu yetu. Ni maneno matupu, ni kwa kupayukapayuka tu, ndiyo ya kuongelea kuhusu imani yetu na kutofanya lolote. 1Wakorintho 13 inaongelea uweza wa kinabii, ili kuelewa siri na uelewa. Inaelezea kuhusu imani inayoweza kuondoa milima. Hata hivyo, kama tukikosa upendo ambao unaendana na imani yetu umekosa malengo, kwa kuwa nguvu zote za Roho Mtakatifu zimetolewa kwa watu hao wanaoweza kuelezea kwa upole – kwa kupendana kila mtu na mwenzake. Hatujapewa Roho kwa umbo lolote lile au nguvu hadi tujue jinsi ya kuielekeza kwa kila mmoja kwa upendo.

 

Tutapewa karama za kutosha zitusaidie. Kiwango cha chini cha upendo tunachokionyesha, ndipo kumzima Roho Mtakatifu itakapokuwa. Kama hatutashinda udhaifu huo, tutakapompoteza Roho Mtakatifu.

 

Tumewaona watu watu wakijaribiwa kwenye uelewa wao juu ya Uungu. Wale wasiopatana na jaribio hili kama wanavyostahili na kufanya maamuzi mabaya, hupoteza kile walichokuwa wakikijuua tayari.

 

Hatua ya kwanza ni Amri Kuu ya Kwanza (imeelezewa kwenye amri nne za kwanza) ambayo ni: mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa akili zako zote na kwa roho yako yote. Upole ni aina ya mwenendo unaotuama kila kitu kwenye usaidizi wa Amri ya Kwanza.

 

Watu wa Mungu wameachana na ndoa zao, ndugu zao, mambo yao ya usitawi, mali zao, na kila kitu kwenye Kanisa. Kila mmoja wetu ameitwa ili atoe sadaka kitu fulani. Kila mmoja wetu ameitwa na ameitwa kutumikiana ili tuweze kuendeleza na kukuza upendo na nguvu katika Roho Mtakatifu. Tutairithin nchi kwa kuwa Bwana wetu Yesu Kristo, atapewa, na amepewa uweza ule na ufalme na mamlaka akiwa kama Nyota ya Asubuhi. Nasi tutapewa uweza huu pia, kama kiti chake cha enzi (Ufunuo 2:26-28; 3:12,21). Tutafanya hivyo kwa ajili ya asili yake au nafasi ya kujinyenyekesha na kuachilia faida na nafsi zetu, na kutumikiana.

 

Ni lazima tuendeleze mambo haya kwa          kiwango cha juu sana tuwezavyo. Wakati mwingine inatokana na shughuli za kutafuta mahitaji ya wengine. Ni namna ya kuonyesha upendo wetu ili kutegemea kupata mahitaji ya wengine. Tuna familia kubwa na tunapaswa kuyaona mahitaji ya kila mmoja wetu hata kabla mtu hajayaeleza. Kwa kufanya hivyo kutaondoa hali ya kupoa kwa upendo kama dunia inavyoona na kufanya kuwa ni tunda la wajibu unaoendelea. Ni kipimo cha kuonyesha upendo, kuonyesha kuwa tun ajali. Kuona na kutarajia kitu fulani ni zawadi isiyoelezeka, kwa kuwa tunawaondoa ndugu zetu umuhimu wa kuweza kuuliza. Hakuna mmoja wetu anayestahili kuuliza kitu chochote.

 

Kinachofuatia kutokana suala la upole, tunaendelea kwenye suala la mapigano. Bwana wetu ana uweza wa kuamua kutuokoa au kutotuokoa. Anauwezo wa kuamua kutupeleka utumwani au kutotupeleka utumwani. Ni kwa namna hiyohiyo, anaweza kuwatendea wale wote wanaotegemea nguvu zao na wasimtumikie Mungu kwa mioyo yao yote na nia zao zote na kwa roho zao zote, hatimaye watashindwa. Watakwenda ama kwenye utumwa wa kihalisi wa Israeli, au kwenye ule utumwa wa Ufufuo wa Pili.

 

Ufufuo wa Pili ni shule ya uadibisho ambayo kwamba watu wote hujifunza kumpenda Mungu kwayo na wataona matokeo ya kile wanachokifanya. Bwana wetu alishalipa gharama ili kutuweka huru sisi kutokana na hayo na kutupa sisi fursa ya kuongoza. Tunaongoza kwa kupitia upole na uvumilivu wetu dhidi ya majaribu.

 

Kwenye Ufunuo 6, tunaona jinsi dhana hii inavyoendelea. Mihuri hii imeelezewa kwa kina kwenye majarida ya Mihuri Saba (Na. 140) na  Baragumu Saba (Na. 141) [T he Seven Seals (No. 140) and The Seven Trumpets (No. 141)]. Hapa tunaona suala la kushindwa kuwa mpole. Kile kinachotokea kwenye mchakato wa kugongwa muhuri ni kwamba mihuri hii inatokana moja kwa moja na hizi Heri. Mihuri hii ni matokeo ya wazi ya kushindwa kuishika Amri Kuu nay a Kwanza, na Amri Kuu ya Pili ambayo ni kumpend jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Kwa pamoja, hizi zimefungamanishwa kwenye Amri Kumi za Mungu (sawa na yanavyosisitiza majarida ya Torati ya Mungu (N. L1) na Mlolongo wa Majarida ya Torati au Sheria (Na.252-Na. 263) [T he Law of God (L1) and the Law series (No. 252-No. 263)].

 

Mhuri wa kwanza unaendelea kutoka kwenye dini ya uwongo – kutoka kwenye mfumo unaochukua mbadala wa kiserikali ulio juu ya misingi na utaratibu wa kibiblia na Torati ya Bwana na Mungu wetu.

 

Mihuri hii imefunguliwa ki makamio kutokana na uvunjifu wa Sheria za Mungu na kuzikataa kwao Heri zilizotolewa.

 

Kama zilivyovunjwa, mhuri wa kwanza umefunguliwa kwenye dini ya uwongo kwa kuwa haina upole. Hakuna nia wala haja ya kujinyenyekeza na kuachilia matakwa na faida za kibinafsi na kuwasaidia watu wote. Kwa kuwa dini ya uwongo iliyosimamishwa pale haina nia moja ya kumtumikia Mungu Mmoja Wapekee na wa Kweli na maamrisho ya Torati yake. Mafarakano yanayosababishwa na mifumo ya vyeo vya uongozi ya kidini ya vikundi vya kidola hulazimisha hali ya kukosa usawa ambao unaendeleza tena hali ya kushindwa kufikia vigezo vilivyo kwenye Heri mioyoni mwetu. Kupenda kunageuka kuwa tamaa mbaya ya ngono, ambayo inapelekea migongano. Hatimaye kunatokea Vita. Kutoka vita huja magonjwa, vifo na njaa. Hii ni mihuri minne ya kwanza na ni ya mwisho. Kama moja iliondoka na nyingine huondoka pia.

 

Kinachofuatia hatimaye, ni kwamba wanavunja mhuri wa tano wa mateso ya kidini, kwa kuwa kama tukiwa na dini ya uwongo, tunakuwa na pande mbili za imani na tunakuwa namungu wa uwongo. Tunapokuwa na dini ya uwongo tunakuwa na muwako wa tamaa mbaya za madaraka. Tukikosa upole, tutateseka.

 

Mhuri wa tano ni matokeo ya mateso yanayoinuka, yanayofuatia hali ya ukosefu wa upole, na unatokana na hamu ya maumivu na kuwadhuru wale wasiokubaliana nasi.

 

Mhuri wa sita ni ishara za mbinguni. Zitaonyesha kuwa Kriso atashughulika na mambo na kuingilia mara moja kwa utaratibu endelevu.

 

Kwa ishara, Kristo anaonyesha kuwa ataukomesha mfumo uliopo hapa duniani kwa kutumia mabavu haya haya na tama na mamlaka ya watu wale ambao watapingana na kupigana.

 

Katika kipindi kile wote wataletwa kwenye Bonde la Kukata Maneno na kuangamizwa kwa nguvu za silaha zao wenyewe. Kristo hatawaua, kwa maana kwamba atafanya hayo kwa maamrisho ya moja kwa moja ya Mungu ili kuwaangamiza tu na hatimaye kuwaua watu hawa. Wanaruhusiwa kuendelea na dhambi zao, ambazo zinatokana na kushindwa kwao kuzishika kanuni za Heri. Watauana, mwanaume, mwanamke na mtoto, kwa mamilioni, ambayo karibu yataangamiza sayari hii yote.

 

Dunia inahamasisha itikazi za ukabila. Watu wanaoongea Kiingereza pia wanahamasisha kwa namna hii. Mawazo ya watu wetu yameharibiwa kimpangilio wa kihila kwa kutumia maonyesho ya sinema za Hollywood na vyombo vya habari, kwa kuonyeshwa matukio ya machafuko sambamba na matukio mengine yasiyojenga fikra zetu.

 

Ulaya imejitangazia vita kupigana wenye kwa wenyewe takriban mara mbili katika karne ya 20 kwa kitendo cha kiwendawazimu mkubwa. Baadae ikafuatiwa na kipindi cha Vita Baridi cha miaka 50 kilichotokea kama matokeo ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Kwa sasa inakaribia kulipuka tena kutokana na ubabarianism au ushenzi na udhulumaji. Imekuwa na itikadi ya kibaguzi tena. Watu wa jamii ya kiaborigini wanashambuliwa.  Kile kinachoonekana kama usafishaji wa kimaadili na ubabariani wa kikabila uliofanywa kwa vita vya Balkani ni dalili tosha inayoashiria Vita Kuu ya Tatu ya Dunia, kama Vita ya Wenyewe kwa Wenyewe huko Uhispania ilivyokuwa kiashirio cha Vita Kuu ta Pili ya Dunia. Kushindikana kwa uwezo wa kisiasa wa kukabiliana au kumthibiti Mnyama kumesababisha kuwepo kwa mlolongo wa matukio yanayoleta mhemko. Watu hawa wanapelekeshwa na roho ya kupenda mali na utajiri na misisimko, kupitia tama zao mbaya, kupenda kwao vyeo na umaarufu, na majigambo, mambo ambayo yatawaangamiza wenyewe na sayari yote hii.

 

Wapole watairithi Nchi kwa kuwa hakutakuwepo na mtu atakayesalia akiwa hai. Kristo ataingilia kati uwendawazimu huu na kukifupisha kipindi hiki kwa ajili ya wateule kwa Mpango wa Mungu (Mathayo 24:22).

 

Wakati wa kila awamu ya kufanyiwa kazi kwa mihuri hii saba, dunia ingeweza kutubu. Kwenye mhuri wa saba kuna baragumu saba, halafu vitasa saba, na vitasa hivi saba vinaiwakilisha ghadhabu ya Mungu. Na katika kila kimoja inasema: na wala hawakutubu (Ufunuo 16:9). Wakati wa kipindi hiki hakuna mtu atakayeruhusiwa kuingia Hekaluni mwa Mungu hadi kutokee mapigo saba ya tauni na hitimike (Ufunuo 15:8). Kwahiyo, pasipo tona hakuna wongofu au wale wasiotubu hakuna atakayeongoka.

 

Kwene kila moja ya mapigo hayo, Mungu ataruhusu kuwepo na mahali pa salama pa kukimbilia. Ni sawa tu na kama tunavyokuwa na mtu aliyeangukia kwenye kitanzi, na kisha tukasema: “Je, umeumia?” naye akasema “Hapana!” kwa kweli, mwanadamu umejiweka kwnye kitanzi na kinamyonga taratibutaratibu hadi kufa, jeraha la kujitesa kwa makusudi. Mungu anasema kwa ukali sana kwamba “usijipige risasi ya mguunimwako wewe mwenyewe, itakuumiza”, kwa kuwa hatujipigi risasi miguuni mwetu kwa mapigo endelevu.

 

Heri ya nne inasema: Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.

Hamu ya namna hii ni ya kuwa na njaa na kiu ya kumjua Mungu. Zaburi 119 inaonyesha wazo lililo kwenye Torati, na haki na utauwa unaotokana na Sheria za Mungu. Wateule wamejazwa Roho Mtakatifu lakini kumekuwa na bidii kwenye hali yao ya njaa na kiu chao. Hawali chakula cha kimwili; bali wanakula chakula cha kiroho.

 

Majarida yenye vichwa vya maneno Roho Mtakatifu (Na. 117) na  Tunda la Roho Mtakatifu (Na. 146) [The Holy Spirit (No. 117) and Fruit of the Holy Spirit (No. 146)] inapasa yaonekane kuhusiana na Heri hizi na kujazwa na Roho. Ni Roho Mtakatifu na matunda yake yote yaliyoelezewa kwenye 1Wsakorintho 13, na kwenye maandiko menhineyo yote yanayomlenga Paulo, inaonyesha kuwa ni kujazwa na Roho tu ndiko kunakochukua mkondo wake.

 

Heri hizi0zinafungua mlango, na kunafuatia nyingine nyuma yake kwa kiwango tuwezacho ili tuonekane kuwa ni chumvi ya Dunia na kuwa ni nuru zaa Hekalu. Tunaweza kufanyika kuwa nuru kwa Wamatgaifa.

 

Hata hivyo, sio watu wengi miongoni mwetu. Chumni hutiwa tu kwenye chakula au ni sehemu ndogo kwenyekiungo au kiambato. Wazo hilohilo linakutwa kwenye habari za Gideoni naa wale 300. Sisi tu wachache; tumeitwa mmoja kutumika mjini, na wawili wa kutoka kwenye familia (Yeremia 3:14).

Yeremia 3:14 Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; maana mimi ni mume wenu; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni;

Na hii ndiyo sababu kuna watu wachache sana wanaoielewa kazi kwa kipindi hiki cha mwisho. Mungu anamwaga Roho wake kwa wanadamu kwanza kabisa kupitia kwa wateule wake (Matendo 2:1-33) na hii inaendelea kwenye Siku hizi za Mwisho (Yoeli 2:28-32; Matendo 2:17-21).

 

Eliya alidhani kuwa alikuwa ni mtu wa mwisho aliyebakia. Kwa uchungu alikuwa aksema kwamba: “hakuna mwingine aliyebakia. Lakini ee, Mungu wangu, niko peke yangu hapa; Mimi ni wa muhimu”. Alikuwa na upweke na hali ya upweke na kushuhudia ubatili kwa ajili ya majukumu ya kazi au huduma yake. Paulo alimuua Stefano, lakini yeye alisema, wakati inapotokea hali ya chini ya – kutokulaumika (Wafilipi 3:6). Aliandika kwamba baada ya kuongoka kwake na baada ya kuuawa kwake Stefano! Kulikuwa na mtu mmoja mnyofu, Yesu Kristo na sisi sote ni wenye dhambi. Kristo, hata hivyo, alisema hakuna aliye mwema ila ni Mungu peke yake (Mathayo 19:16-17). Wote wamepungukiwa na utukufu wa Mungu, Paulo alihitimisha. Dhambi ni dhambi na inaendelea kkutoka kwenye dhambi na uovu wa mawazo na moyoni. Wateule wengine waliomtangulia Masihi, kaka vile wazazi wa Yohana Mbatizaji, walikuwa watachaji wa Mungu na wasiolaumiwa kutokana na desturi za wakati ule (Luka 1:6). Yatupasa sote kuwa ni watu tusioshitakiwa neno baada ya kuongoka kwetu (1Wakorintho 1:8; Wafilipi 2:15; 1Wathesalonike 5:23; 1Timotheo 3:2,10; 5:7; Tito 1:6,7; 2Petro 3:14).

 

Paulo, hata hivyo, alikujakuelewa baadae kwamba alikuwa ni mwenye dhambi mkubwa (Warumi 7:1-25).

 

Baadhi yetu tunatenda dhambi mioyoni mwetu. Dhambi nyingine ni za kweli na na za kukusudia. Lakini tumapimwa kutoka mioyoni mwetu na sio kwa yale tunayoyafanya tu peke yake. Hili ni wazo la kusikitisha na la kutisha. Moyo unatoa fursa kubwa wa kutenda dhambi. Mara nyingi tunashangazwa na kwango yanachowaza mawazo yetu. Vyombo vya habari vya leo zinatoa fursa ya kuwaza na kutenda dhambi ya mawazo ambayo yaliendelea kutoka siku za zamani huko nyuma.

 

Swali hili hatimaye linaendelea hadi kwenye suala la rehema. Sio jambo la bahati mbaya kuwa neema inafuatia baada ya kuwa na njaa na kiu ya haki kwenye utaratibu huu wa hizi Heri. Yatupasa kuwa wapole ili tupate au tustahili kupata, kile tunachotakiwa kukijua na kwamba tunamhitaji Roho Mtakatifu, neema ya Mungu na sadaka ikomboayo ya Kristo. Tunahitaji kujazwa Roho ili tuweze kuzinyenyekeza nafsi zetu. Ubatili wetu na kujiamini kwetu vinakuwa vimeshushwa na kumtegemea Kristo. Baadhi yetu kwa hakika tunahitaji kunyenyekeshwa kimwili ili tuweze kuingia kwenye Ufalme wa Mungu. Baadhi yetu tumeandikiwa kujeruhiwa na kupata hasara ili kuweka mawazo yetu mahala ambapo tunaweza kushughulikiwa na Mungu mwenyewe. Kila jambo linafanyika kwa nia nzuri kwa wale wanaompenda na kumtumikia Mungu, na kwa wale walioitwa kwa makusudi yake (Warumi 8:28).

 

Heri ya tano ni: Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema

 

Zekaria 7:8-10 Kisha neno la Bwana likamjia Zekaria, kusema, 9 Bwana wa majeshi amesema hivi, ya kwamba, Fanyeni hukumu za kweli, kila mtu na amwonee ndugu yake rehema na huruma; 10 tena msimdhulumu mjane, wala yatima, wala mgeni, wala maskini; wala mtu awaye yote miongoni mwenu asiwaze mabaya juu ya ndugu yake moyoni mwake.

 

Limekuwa ni fundisho linalofundishwa na makanisa ya Kiutatu au Utrinitariani kwamba yatuna haja ya kuishika imani pamojja na watu wasiokuwa wa dhehebu letu. Walifundisha kwamba tuna namna iliyotofauti ya kuwashughulikia watu kama tutakuwa wa imani moja. Kwa masuala ya uaminifu na ya wajane na yatima na masikini kwa mujibu wa Torati, jambo ambalo sio sahihi wala sio kweli. Mungu hanaupendeleo wala haangalii sura ya mtu (Matendo 10:34).

 

Watu shirika, Wamataifa, wanatuamini kwa kuwa hatuna upendeleo wala hatumuonei huyu na kumchukia Yule, kwa mujibu wa amri za Torati. Hukumu ya Torati itatoka na kuendelea mbele ikikatiza ulimwengu huu pasi kujali madaraja ya watu, rangi ya ngozi aliyonayo mtu, au daraja la maisha aliyonayo mtu kwenye jamii.

 

Zekaria 7:11-13 Lakini hao walikataa kusikiliza, wakageuza bega lao, wakaziba masikio yao ili wasisikie. 12 Naam, walifanya mioyo yao kuwa kama jiwe gumu, wasije wakaisikia sheria na maneno ya Bwana wa majeshi, aliyoyapeleka kwa roho yake kwa mkono wa manabii wa kwanza; kwa sababu hiyo ghadhabu kuu ikatoka kwa Bwana wa majeshi. 13 Ikawa kwa sababu alilia, wao wasitake kusikiliza; basi, wao nao watalia, wala mimi sitasikiliza, asema Bwana wa majeshi.

Kunakwenda kuwa na muda ambapo Bwana wa Majeshi hatakuwa anasikia. Hatakwenda kuyasikiliza mataifa yatakapomlilia na itashughulikiwa kisawasawa na kwa haki wakati ambapo yatayageykia mataifa mengine yatakayopewa mioyo ya jiwe ili yatushughulikie.

Zekaria 7:14 Lakini nitawatawanya kwa upepo wa kisulisuli, katikati ya mataifa yote wasiowajua. Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa ukiwa nchi baada yao, hata hapakuwa na mtu aliyepita kati yake, wala aliyerudi; maana waliifanya nchi iliyopendeza sana kuwa ukiwa.

 

Maangamizo na vita vitafuatia kutokana na kushindwa kulishika kwa bidii neno la Mungu.

 

Zekaria 8:1-6 Neno la Bwana wa majeshi likanijia, kusema, 2 Bwana wa majeshi asema hivi, Mimi nina wivu kwa ajili ya Sayuni, wivu mkuu, nami nina wivu kwa ajili yake kwa ghadhabu kuu. 3 Bwana asema hivi, Mimi nimerudi Sayuni, nami nitakaa katikati ya Yerusalemu; na Yerusalemu utaitwa, Mji wa kweli; na Mlima wa Bwana wa majeshi utaitwa, Mlima mtakatifu. 4 Bwana wa majeshi asema hivi, Wazee wanaume na wazee wanawake watakaa tena katika njia za Yerusalemu, kila mtu ana mkongojo wake mkononi, kwa kuwa ni mzee sana. 5 Na hizo njia za mji zitajaa wavulana, na wasichana, wakicheza katika njia zake. 6 Bwana wa majeshi asema hivi, Ingawa hili ni neno lililo gumu mbele ya macho ya mabaki ya watu hawa katika siku hizo, je! Liwe neno gumu mbele ya macho yangu? Asema Bwana wa majeshi.

 

Inaonekana kuwa kwa mwanadamu haiwezekani, lakini sio kuwa haiwezekani hivyo pia kwa Mungu. Mungu anaweza kumuinulia watoto Ibrahimu kutoka kwenye mawe yaliyoko nyikani, na atafanya hivyo. Tupo kwenye kujengwa tayari kwa kuanzisha kipindi na utawala wa Milenia. Haya yote yanahusiana na Masihi na kuuanzisha Ufalme wa Mungu. Ndipo suala la haki na rehema linafuatia kwenye uwezo wetu wa kushughulikia na kusaidiana kila mmoja wetu na mwingine kwa njia ya haki.

 

Heri ya sita ni: Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.

 

Kwa kuvionyesha vigezo na viwango hivi katika Roho Mtakatifu kama watu tuliokwisha kubatizwa katika Roho Mtakatifu na kama watoto tuliozaliwa wa Mungu, ndipo tutaupokeo mhuri wa Mungu. Kwa kupokea kwetu mhuri huu wa Mungu tutaweza kuzipokea nguvu za Roho na tutamuona Mungu. Paulo aliandika kwamba hakuna, wala kwa umbo la kimwili, aliyewahi kumuona Mungu na hatakuwepo mtu wa namna hiyo kamwe (1Timotheo 6:16). Na hii ndiyo dhana mojawapo ya kuwa Paulo na Yohana waliifanyia kazi; kusema kwamba hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu, kwa kuwa Mungu ni uweza wa kiroho. Tunapaswa kuwe kwanza kwenye umbo hili la kiroho ili tuweze kumuona Mungu, na hakuna mtu anayeweza kuwa wa namna hiyo. Ni umbo ambalo litawezekana tu kuwanalo baada ya ufufuko wa wafu.

 

Heri ya saba inasema hivi: Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

 

Kupatanisha ni mojawapo ya kuonyesha uwepo wa Roro Mtakatifu. Kuleta amani ndiyo njia atakayoitumia Yesu Kristo katika kuitawala hii dunia. Utawala wake utaiunganisha dunia yote na kunai mamoja kwa maongozi ya Mungu. Imani hii ya kuamini kuwa Mungu ni Mmoja iitwayo Umonotheism haimaanaishi kuwa Mungu ni mmoja lakini ana vichwa vitatu, hapana. Bali Umonotheism ni itikadi inayoamini kuwa Mungu ni Mmoja, kwa kuwa kila mtu, yaani Yesu Kristo na wengine wote akiwemo Roho Mtakatifu, wamejishusha na kwa Mungu na kujidunisha. Wanayashiriki mapenzi ya Mungu, umbo na uwezo wa kupenda na kupenda. Tumeitwa kwenye mfumo wa kushiriki na kuyatenda mapenzi yake na maagizo yake na upendo wake. Yesu Kristo mwenyewe alisema: "Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, [nikaimalize kazi yake]" (Yohana 4:34). Hili linapaswa kuwa jambo muhimu kwetu. Na ndiyo maana imani hii ya Kimonotheism ilivyo na inavyofundisha na kuamini. Sisi sote tuna Roho mmoja aliyetoka kwa Mungu na ndiye anayemuwezesha na kumfanya Yesu Kristo kuwa wamoja na Mungu. Ndiye anayetufanya hata sisi kuwa ni sehemu ya Mwili wa Yesu Kristo ambaye ndiye kiongozi na kichwa wetu, kutufanya sisi sote tuwe ni sehemu ya Mungu ambaye ni yote katiks yote na ndani ya yote (Waefeso 4:6). Yeye siyo wa Utatu, wala hana nafsi nyingine zaidi yake. Imani ya Utatu in atuzuia kwa kupingamiza sisi tusimuone Mungu na tusiwe wamoja na Mungu, kwa namna ileile moja kama alivyo Yesu Kristo kuwa ni mmoja na mshiriki wa karibu kwa Mungu. Imani ya Kibinitarianism inaendeleza makosa hayohayo ya Watrinitarian ya hapo juu.

 

Ili kufanyika kuwa watoto wa Mungu tunapaswa kuwa wapatanishi na tuonyeshe tunda la Roho Mtakatifu. Je, tunawezaje basi kuwa wapatanishi? Ni kwa kuyaona na kuyajali mahitaji na kuguswa nayo na kuwajibika. Kujinyenyekesha na kujishusha na kuwainua ndugu zetu. Tunaweza kusema kuwa, “Siwezi kufanya kitu kwa ajili ya ndugu yangu. Sipendi kufanya kitu chochote nje ya mapenzi ya Baba yangu. Sipendi kufanya mambo zaidi kwenye Mwili huu ambalo ni kanisa la Bwana wangu na kwa mapenzi ya Baba yangu. Kama Baba ameamua kutoingilia kati, nami basi nitakufa kwenye mchakato huo, na basi hayo ndiyo mapenzi ya baba yangu, lakini nitaishi na kuwa imara zaidi ya huko nyuma na kinyume na watu walivyotarajia”.

 

Tunapatanisha lakini sio kwa kuwa kunatishwa na mtu yeyote hapa duniani. Roho Mtakatifu ni roho wa uweza na wa akili timamu – na siyo roho wa woga na ulegevu. Ni kwamba baadhi yet utu wadhaifu kimwili na hatuwezi kupigana na kundi kubwa na kubeba vitu vizito bali vidogo. Sisi sote tu dhaifu kimwili kwa namna fulani na nguvu zetu zinatokana na uweza wa Mungu. Ukweli wa kwamba Kristo ametuweka kwenye nafasi ambayo hatuwezi kuyashusha na kuyatiisha mataifa (kuangamizwa kabisa kwa sayari hii) ni muhimu kwa kuwa kuna ndugu na wapendwa wengi ambao walihukumu kimakosa na kwa upendeleo. Iwapo kama wangekuwa wanafanya maonyesho kungekuwa na viumbe wengi wa aina isiyojamiiana na kungekuwa pia na maiti nyingi za watu. Baadhi ya makanisa yangechoma moto kila kitabu kilichopo hapa duniani kama alikuwa wanafanya maonyesho haya kwa kipindi cha miaka ishirini iliyopita; na wengine wangependa bado kufanya hivyo. Wanawake wengi wangeuawa kwa kuchomwa moto kwa ajili ya ulozi na kungekuwa na kiwango kidogo cha tabaka karibuni. Ni kama tujuavyo sisi sote, miji mingi yenye matendo maovu nay a kikatili imewekwa wakfu kwa jina la Mungu.

 

Kwenye Heri ya nane, Kristo alisema: Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

 

Mauji ya ushuhuda ya Stefano kwenye kitabu cha Matendo ni ya muhimu sana. Stefano analiambia Baraza la kidini kwenye Matendo 7. Mara tu baada ya kumaliza kusema hayo, walikasirika sana na kusaga meno yao. Wakasema, Amesemaje? Kwenye Matendo 7:51 aliwaambia, akisema:

Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio

 

Walijua kuhusu tohara ya mioyo maana yake. Nabii Isaya aliwaambia wote hawa kuhusu jambo hili na walijua, hayakuwa mafundisho mapya. Kristo alikuwa amekwishaonekana kwa kutambulishwa na manabii. Lakini hawakumsikiliza. Hiki ndicho alichokuwa anakisema Stefano naye hawakupenda kuambiwa hivyo.

 

Katika Mathayo 23:31,37 na Luka 11:50, Kristo alimaanisha kabisa kuwauliza Mafarisayo kwa kusema: "Ni yupi kati ya manabii ambaye mababa zenu hawakumtesa?" Haisemi hapa kwamba, "Nathani mliwafanyia hivyo karibia wote". Bali aliwauliza wamwambie ni yupi miongoni mwao ambaye hawakummtesa? Manabii wote pamoja na kila aliyenena kwa Jina la Mungu waliteswa na bado wanaendelea kuteswa hata leo. Waliwaua wale waliowatabiria juu ya ujio wa mwenye haki ambaye Stefano aliwaambia kuwa wamemtaliti na kumuua. Aliwaambia akisema: "ninyi mlioipokea torati kwa agizo la malaika msiishike" (Matendo 7:53). Ulikuwa ni utambulisho wa Mafarisayo wa Kiyahudi. Walikuwa na Torati ila hawakuishika wala kuiweka mioyoni mwao.

 

Basi waliposikia maneno haya, wakachomwa mioyo, wakamsagia meno. Lakini yeye akijaa Roho Mtakatifu, akakaza macho yake, akitazama mbinguni, akauona utukufu wa Mungu, na Yesu akisimama upande wa mkono wa kuume wa Mungu. Akasema, Tazama! Naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu. Wakapiga kelele kwa sauti kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja, wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni pa kijana mmoja aliyeitwa Sauli.

 

Wakati wakiwa wanampiga mawe, Stefano aliomba akisema:

Bwana Yesu, pokea roho yangu. 60 Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona vema kwa kuuawa kwake.

Sauli alikkuwepo akishuhudia wanapomuua. Nguo zake ziliwekwa miguuni mwake kwa kuwa yeye alikuwa ni Farisayo aliyepewa wajibu wa kushuhudia au kusimamia mauji haya. Iliamriwa kuwa mtu asiuawe kwa ushadi wa kuonwa na mtu mmoja tu au wakili mmoja peke yake, ni lazima kuwe na ushihidi wa wengi. Wakati wa zama za Kushitakiwa watu kwa kupinga mafundisho ya dini, mamlaka ya kiutawala iliweka kigezo kutoka kwa Wawakilishi au Mahaliafa wa Papa. Lakini Sauli alimuua Stefano kwa kumrushia jiwe la kwanza na ilikuwa mhalifu ni kazi yake na wajibu wake kumrushia jiwe la kwanza. Kmsingi, shahidi ndiye alikuwa ntu wa kwanza kumrushia jiwe ili auawe. Bila kufanya hivyo, wauaji wa Stefano wasingekuwa na udhuru wa kujitetea. Paulo angekuwa ametubu kikamilifu kwa ajili ya jambo lile, badala ya kusema tu maneno ya kutokuwa na hatia. Hakuwa safi na kwamba hakuwa na hatia kwa kuwa alikuwa ameivunja Amri ya Mungu iyosema: Usiuwe. Alimuua mtu asiye na hatia.

 

Hatimaye, kwenye Heri ya tisa, tunasoma: Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu..

 

Kristo aliweka wazi hilo. Alifundisha kuwa mateso yatatokea na kumpata kila mtele. Watu waliowatesa wateule ni wale walio kwenye mamlaka au tuseme ni wale walio kwenye madaraka yanayojiita Makanisa au Makutaniko ya Mungu. Hii ndiyo imani ya Kiyahudi lakini mateso makubwa yalikuja kutokea kwenye kile kinachoitwa leo kama Ukristo mkongwe wa siku nyingi. Yanaendelea kwenye kwenye imani za Kiprotestant na hata kwene Makanisa haya ya Mungu. Hawa ni wale wanaosema kuwa ni Wakristo, na kumbe sio. Wale walionje ya Makanisa haya makongwe ya kale na huku wakidai kuwa nayo ni Makanisa ya Mungu yanayowatesa wateule kwakuwa hawamjui Bwana wetu.

 

Isaya 66:5 anasema:

Lisikilizeni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina langu, wamesema, Na atukuzwe Bwana, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika.

 

Kwa kweli, wateule wamekataliwa na Sinagogi ya wale wanaodhani kuwa kwa kufanya hivyo wanampendeza Kristo. Wanafikia hata kiwango cha kujaribu kuwaua wateule. Ni nani aliyemuua nabii Isaya kwa kile kinachodaiwa kuwa alichanwa vipande viwili kwa msumeno? Ilikuwa ni makuhani. Ni nani alimpiga mawe hadi kumuua nabii Yeremia? Mapokeo yanatuambia kuwa ni manabii wa Anathothi. Ni watu hawahawa wanaojiita kuwa ni nguzo za nuru ndiyo wanaorudia kututesa sisi kwa kuwa hawamjui Bwana wetu. Wanadhani kuwa wao ni watakatifu lakini hawana Roho Mtakatifu. Haishiki Torati kwakuwa mawao ya kimwili waliyonayo ni adui wa Mungu (Warumi 8:7). Sio tu suala la kwamba watu hawa ni maadui wa Mungu. Bila ya Roho Mtakatigu na kuwa karibu na Mungu hatuwezi kuzishika Sheria na Amri za Mungu kwa kuwa zinashabihiana na asili alisia ya Mungu. Mungu anachokisema na kukazia ni kwama: “Nimeweka utaratibu. Nimewaumba watu ninyi na hamkuwepo hpo kabla ya mimi kuwapa Roho wangu.

 

Mlingano wake unafanana sana na mfano wa kuwa na meli bandarini ikiwa na jenereta yake ikiwaka. Taa zake pia zote zinawaka, lakini imesimama tu pasipo kwenda mahala popote na ni mota ndogo ya usaidizi ikiwa inaunguruma. Mota kuu ikiwa hata haijawashwa. Watu hawa hawawezi kujisaidia walichonacho. Hawajaweza hata kujifunga mikanda yao. Wanaendelea kuwasha ile ndogo ya kusaidia na huu ni mfano unaofanana na ulio sawa nayo. Ipo karibu nusu ya uwezo wake; hawana nguvu. Taa ziko zimewashwa, lakini hakuna kinachoendelea. Ni wakati tunapoanza kuwasha injini kwa Roho Mtakatifu na ndipo tunapoweza kufanya kazi. Na ndipo tunapoweza kuondoka bandarini na kuendelea na safari tukienda mahala kokote katika mapenzi ya Baba yetu.

 

Kusema maneno yote maovu kinyume chetu kwa kutushitaki kwa uwongo kwa sababu ya imani yetu kwa Kristo sio kitu kigeni. Iliyoko hapo juu ni mifano ya aina ya mashutumu uliyoyapitia kwa kipindi cha zaidi ya karne kadhaa. Kwakuwa hatukuwa na uwezo wa kuandika vitabu, basi hatujuweza kuwa na toleo la vitu vyetu kwa watu walionje ya imani. Walichoma moto maandiko na vitabu vyetu, wakiita maandishi maovu nay a waovu na kusema kuwa yale tunayoyafanya ni hatari na machukizo makubwa kama vile kumuabudu Mungu Mmoja wa Kweli, kufunga saumu, kuzishika Sabato, na kuvaa mavazi yasiyoonyesha kujitukuza. Walituua kwa kututundika mitini na kwa kutuchoma moto, kwa sababu ya mambo haya. Ulikuwa ni mtindo wao kuvaa kama ndege tausi. Ukristo huu wa zamakale ulitutesa na kutuchukia kwa ajili ya mambo haya yote. Walikuwa na kiwango kidogo sana cha mambo ya kutushitaki au kutulaumu kwenye Imani yetu (soma jarida la Wajibu wa Amri ya Nne jibu wa Amri ya Nne Kwenye Makanisa ya Mungu yanayshika Sabato (Na. 170)  [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)] na jarida linguine la Migawanyo ya Jumla ya Makanisa yanayozishika Sabato (Na. 122) [General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122)].

 

Watu wetu wengi wameitwa watoke dhambini. Mara nyingi dunia huwalaumu watenda dhambi. Hata hivyo, wanapoongoka na wanapokubalika na kusamehewa kwa kupitia Makanisa ya Wapendwa. Kukubalika huku kusiko na masharti kwa wenye dhambi kwenye neema iokoayoya ubatizo wa Yesu Kristo ni mhuri na alama ya Kanisa la Mungu na wateule wake.

 

Kristo alisema, Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

 

Basi na tuchukuliane na mateso ya dunia kwenye nuru ya matumaini iliyoko ndani yetu. Basi na tukazane kwa bidii yote ili kuifanya kazi ya Mungu.

 

Inatupasa kuwa chumvi ya Dunia na nuru ya Ulimwengu. Yesu Kristo ni nuru ya ulimwengu na kwa kupitia sisi anaieneza injili. Mungu amechagua kututumia sisi zaidi kuliko kazi nyingine yoyote. Ametuita ili kutupa uweza ilituwe wenye nguvu. Ametuita tuingie, sisi wadhaifu na msingi. Baadhi yet uni wadhaifu, wengine ni imara na wengine wako kotekote kuwili. Lakini ametuita sisi sote tuingie, na sio kutuacha tukiwa kwenye hali ile, bali kutufikisha mahali pa kupata nguvu kwa kupitia Roho Mtakatifu.

 

Kipimo cha nguvu ile ni hizi Heri na kwa jinsi tunavyoweza kuachilia mambo yenye faida kwetu binafsi kwa ajili ya Mungu na wapendwa wetu waliomo Kanisani. Wale miongoni mwetu wanaishi peke yao wapo kwenye familia zetu; na wale waio na watoto miongoni mwetu, ni wazazi na wale kati yetu walio peke yao basi hawapo pekeyao tena. Bali sisi sote ni familia kubwa, yenye nguvu, katika Roho mmoja. Kristo anatuambia kwenye hizi Heri jinsi ya kufuka pale na jinsi ya kuitensa kazi zake. Tumetwa sio kwa udhaifu au kufanywa wadhaifu, bali kupewa nguvu au uweza.

 

q