Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[278]
Dhabihu Sadaka
(Toleo
La 1.1 19990623-19990717)
Dhana au wazo la utoaji wa dhabihu na sadaka halijaeleweka kwa usahihi sana
makanisani. Ni kwa miaka mingi sana makanisa ya Mungu yamekuwa haiishiki Idi ya
Penyekoste kiusahihi na kwa kweli hayajafikia kiasi cha kuelewa vyema ya yale
yanayotakiwa kufanyika kwenye Sikukuu na dhabihu zake. Mtu anapaswa aishi kwa
kila neno litokalo kinywani mwa Mungu. Jarida hili linaangalia juu ya dhana ya
ni nini hasa dhabihu na ni nini hasa maana ya hizi Sikukuu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1999 Wade Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Dhabihu za Sadaka
Jarida hili
linakwenda kufafanua kwa kina kuhusu dhana na utoaji wa sadaka.
Kutoka 23:14ff.
Kutoka 23:14-20 Mara tatu kila mwaka utaniwekea sikukuu. 15 Utaiweka sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu; utakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba kama nilivyokuagiza, kwa wakati uliowekwa, mwezi wa Abibu (kwa maana ndio mwezi uliotoka Misri); wala hapana mtu atakayeonekana mbele yangu na mikono mitupu;
Sasa hilo
linamaana sana na liko wazi. Hakuna hata mtu mmoja, atakayekuja mbele za Bwana
mikono mitupu
16 tena, sikukuu ya mavuno, hayo malimbuko ya kazi zako za kupanda mashambani; tena, sikukuu ya kukusanya, mwisho wa mwaka, hapo utakapokusanya hayo uliyoyataabikia shambani. 17 Mara tatu katika mwaka watu waume wako wote watahudhuria mbele ya Bwana MUNGU. 18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi. 19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Dhana iliyo kwenye
aya za 14 na 15 linahusiana na agizo lisemalo kuja mbele zangu. Neno-dhana lililo kwene tafsiri ya Companion
Bible ni kwamba hii ni neno lililoandikwa kwa Kiebrania cha kisasa, lakini hili
na vifungu kumi vingine zilikuwepo tayari kwenye tafsiri ya Sopherim na ni kwa
kuonyesha tu. Maandiko ya
zamakale yanasomeka (ya yanapasa yasomeke) “kuuona uso wangu”. Dhana yote nzima
kukuhusu Uso wa Mungu ilitumika kama mfano au Synecdoche kwa mujibu wa
Bullinger kwenye Biblia ya the Companion, lakini ukweli wa mambo ulikuwa ni
kwamba huu Uso wa Mungu alikuwa ni Malaika wa Yahova. Kwenye aya ya 20 inaendelea
mbele kwa musema:
20 Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele
yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.
Uso wa Mungu alikuwa ni Kiumbe wa Uwepo wake; ambaye ni
Yahova aliyewatokea Isrfaeli na kuwaendesha Israeli kwa kuwafundisha Torati.
Dhana nzima iliyo kwenye andiko hili ni kwamba haturuhusiwi kwenda huko na kuwa
mbele za Uso wa Bwana na hata mahala pengine kwenye sikukuu hizi mikono mitupu.
Idi ya Majuma (au
Pentekoste) ni ya pili kati ya hizo tatu zinazotolewa sadaka. Tunawajibu wa
kukutanika pamoja ili kuiadhimisha Pentekoste na hatupaswi kwenda tukiwa mikono
mitupu.
Kwenye
Matendo 2:1 tunaona kwamba kunaulazima wa kukutanika kama Kanisa kwenye sikukuu
ya Pentekoste.
Matendo 2:1
Hata ilipotimia
siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
Ni
Sikukuu ambayo tunalazimika kwa moyo
mmoja na mahali pamoja. Kwa hiyo, sio suala tu la kuisika nyumbani. Tumeamriwa
na Mungu kujihudhurisha kwenye Sikukuu ya Pentekoste kwenye mahali alipopachagua,
kwa namna hiyohiyo na kwenye Sikukuu mbili nyingine ziadhimishwe pia,
zinazojulikana kama Pasaka na Idi ya Vibanda, na tusijitokeze mikono mitupu (Kumbukumbu
la Torati 16:16).
Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwepo wote mahali pamoja.
Kwa maneno mengine, yawezekana kuwa walikutanika pamoja tangu siku ya Sabato na
huenda walikusanyika pamoja kwa ajili ya Sikukuu ya Pentekoste. Huenda hii ni
dhana ya kuhusu Sabato ya pili baada ya Pentekoste baada ya (the Sabbatton deuteropro) iliyo kwenye Luka
6:1.
Tangu
maadhimisho ya kwanza ya Kanisa ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliwashukia wale
waliokuwepo kwa nguvu nyingi. Waliweza kunena kwa lugha nyingine na kunena
maneno ya kinabii na kutumia au kutumiwa na Roho Mtakatifu. Ilipasa isemwe
kwamba ni kuadhimisha visivyo sahihi sikukuu hii ya Pentekoste kunazuia uwezo
wa Kanisa kutumiwa na Roho Mtakatifu aweze kuzuia na kukingwa kutoka kwenye
hali ya uasi na tama za mwili.
Kutokana na
maelezo na maagizo ya Kumbukumbu la Torati 16 tunaona kutoka kwenye aya ya 1 amri
inaanza kutoka mwezi wa kwanza na inasema:
Kumbukumbu la Torati
16:1 Utunze mwezi wa Abibu,
ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu
alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako.
Haya ni marudio
ya kile kinachosemwa kwenye Kutoka 23.
Kumbukumbu la Torati
16:2-6 Nawe umchinjie pasaka
Bwana, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng'ombe, mahali atakapochagua
Bwana apakalishe jina lake. 3 Usimle pamoja na
mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa chachu, nayo
ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka; ili upate
kukumbuka siku uliyotoka nchi ya Misri, siku zote za maisha yako
Ni dhahiri sana
na wazi sana kwamba ilipoandikwa hakukuwa na mahali maalumu ambapo
palichaguliwa na Bwana ili aliweke jina lake. Hakuwa ameliweka jina lake huko
Yerusalemu kikamilifu. Wakati Torati ilipoandikwa, iliandikwa kwa ajili ya
nyakati zote, kwa kuwa Yerusalemu haikuwa inakwenda kuwa ni mahali ambapo Bwana
amelikalisha jina lake kikamilifu na kwa wakati wote. Tangu mwaka 70 BK,
Yerusalemu imekuwa ikiangamia na Kanisa na Hekalu vimekuwa jangwani. Ni wazi
sana kuwa agizo tulilopewa la kuamrishwa la kulifanya jina la Bwana kuwa ndicho
lengo kwenye maadhimisho ya Idi hizi tatu: Pasaka na Siku za Mikate Isiyo na
Chachu, Pentekoste na Idi ya Vibanda na Mkutano wa Makini. Kanisa lipewa wajibu
wa kuliweka jina la Mungu mahali pake stahiki na tumeamriwa kuhudhuria kwa
kuwepo huko.
Inaendelea:
4 Wala isionekane kwako chachu muda wa siku saba
katika mipaka yako yote; wala katika hiyo nyama uchinjayo siku ya kwanza jioni,
kisilale cho chote usiku kucha hata asubuhi. 5 Usimchinje
pasaka ndani ya malango yako yote akupayo Bwana, Mungu wako;
Ni wazi kabisa
kwamba inatupasa kuwa nje ya nyumba zetu tunapoziadhimisha Idi za Paasaka na tutaona
pia kuwa tumeamriwa pia kuadhimisha Pentekoste na Idi ya Vibanda. Huu sio
wakati wa kukitofaautishaganisha kitu kwa mtu binafsi, wala kitu chakulitofauisha
au kulinganisha Kanisa. Kanisa na viongozi wake wanatakiwa kupachagua mahali pa
kuliweka jina la Bwana mahali maalumu. Pasaka imeelezzewa kwa wazi kuwa
haipaswi kuadhimishwa au kuliwa ndani ya marago au nyumba zetu. Maelezo haya
yanapelekea hadi kwenye Sikukuu nyingine kama tutakavyoona.
6 ila mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako,
apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinja pasaka jioni, katika machweo ya jua,
kwa wakati kama uliotoka Misri. 7 Nawe umwoke na kumla
mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; kisha asubuhi yake ugeuke uende hemani
mwako.
Kwa hiyo tunawea
kurejea hemani mwetu au kwenye makazi yetu katika Siku Takatifu ya kwanza, lakini
hatupaswi kuwa majumbani mwetu au maskani mwetu wakati wa maadhimisho ya Pasaka.
Inaendela:
8 Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku
ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote. 9 Jihesabie majuma
saba; tangu wakati uanzao kutia mundu katika mmea utaanza kuhesabu majuma saba.
Mwanzoni mwa
mavuno ya shayiri wakati wa mwanzoni mwa miganda au masuke ya kijani kibichi ya
shayiri yanakusanywa ili yaweze kuchomwa. Hayavunwi ili yatwangwe au kusagwa; kwa
kuwa yako ya kijani bado. Tendo hili hufanyika siku ya Jumapili kwenye juma la
maadhimisho ya Mikate Isiyo na Chachu. Wanaendelea kuhesabu kuanzia wakati huu.
Kishe tnajihesabia
majuma saba. Hii ni muhimu na tutakwenda kuiona sababu au maana ya kuhesabu majuma
haya saba baadae.
10 Nawe sikukuu ya majuma umfanyie Bwana,
Mungu wako, kwa kutoa sadaka ya hiari ya mkono wako, utakayotoa kwa kadiri
akubarikiavyo Bwana, Mungu wako;
Kwa hiyo
hatutakiwi kuja mble za Bwana mikono mitupu na tunapaswa kwenda mahali ambapo
Bwana amelikalisha jina lake. Agio hili ni kwa watu wote. Viongozi wa kanisa
wanaowajibu wa kupaandaa mahali ambapo watu watajihudhurisha kwa maadhimisho
haya na hakuna mtu anayeruhusiwa kwenda au kujihudhurisha hapo akiwa mikono
mitupu. Kuna utoaji wa sadaka; sadaka ya hiyari mikononi mwetu
... Kila mtu na atoe
kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa.
Katika
kuziangalia Baraka za Bwana, sadaka hii inapaswa iwe inatolewa kwa hiyari, na
isiwe ikitolewa huku mtu akimnung’unikia Mungu kama hatukufanikiwa tungependa
kuwa kama tulivyokuwa miaka ya nyuma
11 nawe utafurahi mbele ya Bwana, Mungu wako,
wewe na mwana wako na binti yako, na mtumwa wako na mjakazi wako, na Mlawi
aliye ndani ya malango yako, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na
mumewe, walio katikati yako, katika mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako,
apakalishe jina lake.
Ni wazi kabisa
hapa kwamba agizo la wanaume wote waende mbele a Bwana ni amri ya lazima, lakini pia
wanasindikizwa na wake zao na binti zao. Wanawake kwa mazingir fulani wanazuiwa
kusafiri kwenda maeneo fulani, au vinginevyo wahudumiwe kwa uangalizi kama wa
watoto; kwa hiyo Torati haijatubebesha mzigo wowote sisi ambao tusioweza
kuubeba. Sheria iko wazi sana kuhusu wanawake. Mungu amewaambia wanaume waende
peke yao iwapo kama wake zao hawataweza kuhudhuria. Inaenda kinyume na watumishi
walio kwenye familia za Walawi na wageni na mayatima na wajane walio katikati
yetu, mahali ambapo Bwana Mungu wetu amepachagua ili alikalishe jina lake hapo.
Kwa hiyo, ni
dhahiri sana kuwa kuna agizo na umuhimu linalotutaka kupachagua mahali pa
kujihudhurisha na mwingine yeyote anayehusika kwenye jamii na nyumba na watu wote
wanaojiri kwenye huduma za familia zetu. Walawi wanategemea matoleo yetu pia.
Kwa hiyo, dhana yote nima lililo kwenye kanisa likionekana kama ni idara ya
kikuhani na watu wote wanaohusiana na kanisa. Sio sehemu inayowapasa Walawi na
wala zaka hii sio sehemu ya Walawi. Ibrahimu alitoa zaka yake kwa Melkizedeki kwenye
zama ambayo hata Lawi alikuwa haja zaliwa, na ukuhani wet uni wa mfano wa
Melkizedeki ,bna sio wa Lawi. Lawi alikuwa ni kuhani wa mpito, ambaye
alifanyika kuwa ni sehemu ya shirika au ukuhani mkubwa na mpana linaloitwa
Ukuhani wa mfano wa Melkizedeki, ambao kwa huo, Ibwahimu baba yetu alitoa aka
yake kwa huo, wakati sisi tulipokuwa viunoni mwake. Ukuhani wet uni pamoja na
Melkiedeki, na utoaji wa aka haujakoma au kutanguliwa; na sio tangu siku za
Nuhu.
Kwa hiyo tunakwenda
kwenye Sikukuu ya Vibanda, jambo ambalo sio linaloongelewa hapa.
Kwenye Mambo ya Walawi sura ya 23 tutaona utaratibu na amri fulani sasa
kutoka kwenye maadhimisho ya Mganda wa kutikiswa. Tunaelezea utaratibu wa
kuhesabu hadi Pentekoste, ambacho ni kipindi maalumu cha kuhesabu kuanzia saa tatu
kamili asubuhi ya Jumapili. Hii ni kwa mujibu wa ilivyokuwa inafanyika katika
kipindi cha Hekalu chini ya Masadukayo. Marabi wa Kiyahudi (waliotokana na
Mafarisayo) walianza kuadhimisha kimakosa tangu walipoondoka Israeli, wakati
walipokwenda uhamishoni. Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa mara zote ilitolewa siku
ya Kwanza ya Juma katika kipindi cha Hekalu; na kila mara ilikuwa ni saa tatu
asubuhi na ndipo ilichukuliwa rasmi kuwa ni wakati wa kuhesabu hadi kufikia
hesabu ya hamsini yangu muda huu wa saa tatu za asubuhi na ni tangu Jumapili
hadi Jumapili. Hivi ndivyo’ilivyokuwa ikifanyika katika kipindi cha kamba ya
kubomolewa Hekalu cha takriban miaka 1,500. Hivi ndivyo Wasamaria na Masadukayo
walivyokuwa wakifanya. Haikukoma hadi kwa warithi wa Mafarisayo walipoanza
kuichezea kalenda na kibadilisha kwenye takriban karne ya pili BK.
Mambo ya Walawi 23:9-12
Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 10 Nena
na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi
niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa
malimbuko ya mavuno yenu; 11 naye atautikisa
mganda mbele za Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada
ya Sabato kuhani atautikisa.
Siku inayofuatia
baada ya Sabato ilikuwa ni siku ya kwanza ya juma, ambayo siku hizi tunaiita
Jumapili.
12 Na siku hiyo mtakayoutikisa mganda,
mtamsongeza mwana-kondoo wa kiume mkamilifu wa mwaka wa kwanza awe sadaka ya
kuteketezwa kwa Bwana. 13 Na sadaka yake ya
unga itakuwa sehemu za kumi mbili za efa za unga mwembamba uliochanganywa na
mafuta, ni kafara iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto kuwa harufu ya kupendeza; na
sadaka yake ya kinywaji itakuwa ni divai, robo ya hini. 14 Nanyi
msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata
mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika
vizazi vyenu katika makao yenu yote..
Katazo hili la
kula bisi bado linaendelea kwenye Mganda wa Kutikiswa. Haturuhusiwi kula bisi
ya mavuno mapya hadi ifikapo siku ya Mganda wa Kutikiswa. Tunakula bisi za
mavuno ya miaka iliyopita hadi kufikia mavuno ya malimbuko ya Mganda wa
Kutikiswa. Tutaona kwamba walipokuwa Israeli wanaiteka na kuikalia nchi ya
ahadi chini ya Yoshua.
15 Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili
baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa;
zitatimia Sabato saba; 16 hata siku ya pili ya
hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya
unga mpya.
Kwa hiyo kuna
siku hamsini zenye Sabato saba kamili ndani yake. Sabato au Sabatoni hizi saba kamili. Kuna siku
sita za kazi inaopelekea kwenye siku ya saba ya juma, ambayo ni siku ya
mapumziko ya Sabato. Sabato saba kamili inatufikisha kwenye Sabatoa ya saba na
halafu siku inayofuatia (kesho yake au siku inayofuatia baada ya Sabato) ni
siku ya kwanza ya Juma, ambayo tunaiita Jumapili. Marazote Pentekoste inaangukia
siku ya Jumapili ikiandhimisha na kanisa kwa kipindi cha zaidi ya miaka 2000,
isipokuwa kwa kosa moja tu dogo kwenye karne yak mi na moja.
17 Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya
kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba,
itaokwa na chachu, iwe malimbuko kwa Bwana.
Sasa hii
inapendeza kwamba mikate hii miwili, ndiyo mikate miwili pekee kati ya
utaratibu wote wa sadaka ambayo ndiyo imeagizzwa itengenewe kwa kuitia chachu
na kuwa mikate yenye chachu ndani yake, ikiashiria Roho Mtakatifu waliyempokea
siku ya Pentekoste takriban mwaka 30 BK, baada ya kusulibiwa kwa Kristo, wakati
Roho Mtakatifu alipoingia kwenye jingo lile kwa lugha na moto na kwapa uweza
ndugu wapendwa na kuwaongoa.
18 Nanyi, pamoja na hiyo mikate, mtasongeza
wana-kondoo saba, walio wakamilifu, wa mwaka wa kwanza, na ng'ombe mume mmoja,
na kondoo waume wawili; watakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, pamoja na
sadaka yao ya unga, na sadaka zao za kinywaji, sadaka ya harufu ya kupendeza
iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. 19 Nanyi
mtasongeza mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wana-kondoo wawili waume
wa mwaka wa kwanza kuwa dhabihu ya sadaka za amani. 20 Kisha
kuhani atawatikisa pamoja na hiyo mikate ya malimbuko kuwa sadaka ya kutikiswa
mbele za Bwana, pamoja na wale wana-kondoo wawili; watakuwa watakatifu kwa
Bwana, wawe wa huyo kuhani. 21 Nanyi mtapiga mbiu
siku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yo yote ya
utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu. 22 Nanyi hapo mtakapovuna mavuno ya nchi yenu, usivune
kabisa kabisa pembe za shamba lako, wala msiyakusanye masazo ya mavuno yako;
utayaacha kwa ajili ya huyo maskini, na mgeni; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Jambo hili linaendelea
kupitia kwenye sadaka ya Mganda wa Kutikiswa hapa ukiwa kwa Makuhani wale
walioitwa na kuchaguliwa na baada ya ule wenye mfano wa Melkizedeki, siku ya
Pentekoste na hadi kwenye Idi ya Vibanda. Kwa hiyo, katika miaka hii 2,000,
Kanisa lina Makuhani na Wafalme, waliochaguuliwa na kutengwa mbali, kuteuliwa
na kulindwa na kutikiswa tangu saa 3:00 asubuhi sadaka ya kutikiswa ya Pentekoste.
Kwa hiyo, tuna sadaka ya Mganda wa Kutikiswa inayotolewa siku ya Jumapili
wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu na sadaka hii nyingine ya Kutikiswa
hutolewa siku ya Pentekoste. Sadaka ya Pentekoste ni kubwa zaidi ya ile ya Mganda wa Kutikiswa.
Kwa hiyo, ni wazi
sana kwamba tunashughulika na mwendelezo wa dhana hii ya Mganda wa Kutikiswa.
Haya yote, yanamaanayake katika kulielewa kanisa na nafasi yetu. Tunatakiwa
kukutanika pamoja na kusafiri na kuwa wamoja ili kuiadhimisha sadaka hii na
Sikukuu hii ya Pentekoste kwa roho njema kama ilivyokuwa inaadhimishwa.
Inapaswa kuwa mahali ambapo Bwana Mungu wetu atapachagua na sio kwenye makazi na
majumbani mwetu. Sikukuu yote ya Pentekoste iliadhimishwa kwa siku moja, lakini
tuna Sabato pia.
Sabato na
siku Pentekoste zinafanya kuwa sikukuu mbili kwa pamoja, na inatupasa kufunga
safari na kuhudhuria kama sikukuu mbili zilizo pamoja. Andiko halisemi kuwa
mara mbili kila mwaka na Pentekoste iwapo kama tutakuwa karibu na mahali hapa
palipochaguliwa. Bali inasema kuwa ya mwisho ni Idi ya Vibanda. Maandiko
hayasemi Idi ya Vibanda au labda Pasaka na Pentekoste kama tunadhani kuwa hiyo
ni sahihi sana. Bali andiko linasema ishike Idi ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa
Chachu kwa muda wa siku saba na haturuhusiwi kuila Pasaka tukiwa majumbani mwetu.
Watu wengi wakati mwingine hudhani kuwa hii ni tafsiri inayojitegemea. Lugha
hii ni lugha iliyowazi. Kwa kuwa baadhi ya Makanisa ya Mungu hayaishiki Idi za Pasaka
na Pentekoste vizuri kwenye mashirika yao ya mwanzoni na sasa wanakabiliana na
ukweli wa kuishika kisahihi, na haifanyi kuwa na tafsiri ya kipekee. Inamaana
kwamba walikosea kabisa huko nyuma, na kwamba walikuwa hawamtii Mungu bali walikuwa
wanamausi. Sio suala la tafsiri ya kipekee nay a jinsi mtu anavyojionea au ni
maamuzi yetu. Hatuna la kusema kuhusu hili. Tunazishika sheria na amri za Mungu
na kwenda kwenye Sikukuu au vinginevyo tutakuwa tunajiondoa wenyewe mbali na
Ufalme wa Mungu. Kuna chaguo moja tu; Kumtii Mungu au kutomtii Mungu. Na iwapo
kama Bwana ni Mungu ndipo basin a umuabudu yeye, sawa sawa na anavyoamuru.
Tutaona
kwenye Mhubiri 12.
Mhubiri 12:12-14
Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna
mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. 13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche
Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu. 14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na
kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.
Kwa hiyo hakuna
shaka kabisa hapa kuwa hizi ni amri za Mungu nah ii ndiyo kazi yote nzima ya mwanadamu
na anachotakiwa ni kuzitenda amri hizi. Tunachotakiwa kuamia ni iwapo kama
tutamtii Mungu au kama hatutamtii. Kanisa linapaswa kuzitenda kazi lilizopewa
kwa kuzishika amri za Mungu, na kwa kufanya kwetu hivyo ndipo tunaweza kufanya
maamuzi na kuyafanya mambo ambayo tumeamriwa. Iwapo kama tukiamua kuwa shindano
limekuwa gumu sana na tunakata tama kwalo, hayo ni maamuzi yetu. Inatupasa
kushindana kana kwamba ttashinda na inatupasa kuendelea kushindania bila kukona.
Inatupasa kupia hatua na
kusonga mbele ili tuweze kuvumilia hadi mwisho. Watu wengi wanakimbia kwa hatua
ndogo na bila kufika mbali. Watu wengi hudhani kuwa ni dhana ya kiakili au
zoezi linayohitaji kutumia akili nyingi. Wanaisoma Biblia na wanadhania kwamba
kwa kuisoma kwao tu inatisha na hawahitaji kufanya chochote zaidi, au wanakuwa
wapata malengo tofauti, au kuna mtu mwingine anayewaambia visivyo au vinginevyo.
Mungu ameiweka
kalenda na ametupa sisi sheria ili tujue kile anchokifanya. Tumewekwa kwenye
mahala ma maana sana. Tumepewa fursa ya kuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza
wa wafu na fursa ya kuuingia Ufalme wa Mungu juu ya mamilioni kwa mamilioni ya
watu. Litakuwa ni jambo la kijinga kuitupa na kuipoteza fursa hii kwa kufanya
mambo yenye kuleta madhara makubwa, kwa kuwa tulikuwa ni wazembe na wavivu sana
wa kwenda kwenye Sikukuu, kanakwamba iliamriwa kuwa tusiende, au kwamba hatukupenda
kwenda, au ni kama hatujawahi kufanya hivyo huko nyuma. Mtu yeyote
anayezidharau amri za Mungu, atahesabiwa kuwa ni mdogo kwenye Ufalme wa Mungu. Watu
wanaofanya hivyo, wao wenyewe hawatakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa
wafu. Na kwene ufufuo wa pili wa wafu, watu walioitupilia mbali fursa hii
watakabiliana na fursa ya kusema tu kuwa ‘lakini nilimfuata’. Lakini walimfuata
kwenye ufufuo wa pili wa wafu lakini watakuwa wamechelewa sana walipambiwa
ukweli ule kwenye ufufuo wa pili. Fusra yet uni sasa na tutakuwa ni wajinga
sana tukiipoteza
Yatupasa kufikiri
yale tunayoyafanya. Kanisa lina wajibu wa kutusaidia na sote tunawajibu wa
kukutana na hatutakiwi tukutanike tukiwa mikono mitupu tunapojihudhurisha kwenye
kila moja ya sikukuu hizi. Sikukuu zote zinapaswa kuzingatiwa na kuadhimishwa.
Kama tukijitoa na
kumkabidhi Mungu njia zetu, atathibitisha mawazo yetu. Sio kwa njia nyingine
yoyote iliyopo. Basi na tuzishike sikukuu hizi kikamilifu naye atatupa ueklewa
zaidi.
q