Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[279]
Waraka wa Yakobo
(Toleo La 1.0 20060501-20060501)
Matatizo
mengi yanayotokea kwenye Makanisa ya Mungu yanaweza kukomesha kwa kufuata
kanuni zilizowekwa na kuelekezwa kwenye Waraka wa Yakobo ulioandikiwa makanisa
yaliyokuwa kwenye hali ya mtawanyiko mahala pengi.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2006 Wade Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Waraka wa Yakobo
Waraka huu uliandikwa ukiyalenga makabila kumi na mawili yaliyokuwa kwene hali ya
utawanyiko, kwa wale waliokuwa Uhamishoni, ambao wengi wao walikuuwa huko
Uyunani (kama ilivyo pia kwenye Yohana 7:35). Idadi ya makabila imekamilika,
bila shaka ni waliogawanyika Yuda na Galilaya, na kama ilivyokuuwa. Inaonekana
kuwa ndivyo utakavyokuwa mkakati wa kuliunganisha tena taifa chini ya Yesu
Kristo.
Yakobo 1:1-27
Yakobo, mtumwa wa
Mungu, na wa Bwana Yesu Kristo, kwa kabila kumi na mbili waliotawanyika;
salamu. 2 Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha
tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; 3 mkifahamu
ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. 4 Saburi
na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa
na neno.
Kila majaribu au mateso (yanayojulikana kama majaribu)
ambayo yako mbele yetu yanakusudia kutuimarisha na kutukamilisha. Tunajifunza
kutokana na makosa yote tuyafanyayo na kwa kila jaribu na misukosuko
tunayoipitia. Huu ni mchakato wa kujaribiwa (dokimion). Kwenye mchakato ule
tunajifunza uvumilivu au subira ya watakatifu.
5 Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na
hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye
atapewa. 6 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo
yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na
kupeperushwa huku na huku. 7 Maana mtu kama yule
asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana. 8 Mtu wa nia
mbili husita-sita katika njia zake zote. 9 Lakini
ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa; 10 bali
tajiri kwa kuwa ameshushwa; kwa maana kama ua la majani atatoweka
Mungu anaiimarisha imani kwa kupitia hekima kwa wale
wanaoihitaji. Imani Kanisani inaanza, lakini kwa wale walio wa daraja la chini
na walio matajiri. Mungu hana upendeleo kwa mtu yeyote. Kusudi la busara au
hekima ya imani ni kutufanya sote tufikiri vizuri. Kuwa na mawazo mawili au
njia mbili mawazoni mwetu ni kuonyesha kukerwa na kuvutia mchakato au
mwendelezo dhaifu au kutokuwa na afya njema. Hivi ndivyo ilivyo dhana au maana
ya mtu wa kuwa na njia mbili au kutangatanga na asiye imara kiimani. Tumeitwa
ili kujitoa kikamilifu, na busara, na kuchukuliana na uimara.
11
Maana jua huchomoza
kwa hari, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo
hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.
Utajiri wa kidunia au wa duniani hapa ni kitu cha kupita
tu na sio vitu vya kuhangaikia sana au kutafutwa kwa nguvu zote zaidi ya imani.
Maelezo yaliyo kwenye Injili zote yako wazi sana kwamba ni rahisi kwa ngamia
kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia kwenye ufalme wa Mungu.
Mitego iliyopo ni kwamba wanaikinza imani na kuwadhanganya wale wanaoitangaza.
Majaribu yanatupata kutokana na tama za miili yetu na
udhaifu na kujaribiwa na dunia inayotuzunguka. Jukumu letu ni kuyavumilia
majaribu ili hatimaye tupokee taji ya uzima. Majaribu hayaji kutoka kwa Mungu,
lakini uwezo wa kuyavumilia unatoka kupitia Roho wa Mungu.
12
Heri mtu astahimiliye
majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana
aliyowaahidia wampendao. 13 Mtu ajaribiwapo, asiseme,
Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye
mwenyewe hamjaribu mtu. 14 Lakini kila mmoja
hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. 15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na
ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. 16 Ndugu zangu
wapenzi, msidanganyike. 17 Kila kutoa kuliko kwema, na
kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake
hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
Mungu anatupa sisi vitu vilivyo na ulazima kwa ustawi wa
maisha yetu na wokovu wetu. Usiwaangalie wanadamu kama kigezo chako bali
mwangalie Mungu. Ni kwa kupitia mapenzi ya Mungu sisi tuliumbwa, ili tuwe
malimbuko ya jamii yote ya Wanadamu kwa Mungu.
18
Kwa kupenda kwake
mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake. 19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe
mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
Kila mmoja wetu
anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia mambo lakini sio wepesi kunena, tunapaswa kuwa
tulio rahisi kuchukulika na kulisubiri Kanisa na kuwapa heshima stahiki wazee
wanaotuongoza katika imani. Wagundue wale wanaoleta au kusababisha migawanyiko
na mambo ya kughadhibisha katika imani kwa kuwa huo sio utkatifu wala sio haki
na uchaji wa Mungu.
20
kwa maana hasira ya
mwanadamu haiitendi haki ya Mungu. 21 Kwa hiyo wekeeni
mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa
ndani, liwezalo kuziokoa roho zenu.
Watumishi wa Siri
za Mungu wamepewa hekima ili waweze kutuandaa vizuri na kutuongoza au
kutuelekeza kwenye imani. Je,
Mungu anaweza kuandaa imani na kuiacha kwa walinzi wa imani wasio na busara?
Hapana, Hafanyi hivyo, na maishani mwetu Kanisani tunapaswa kuonyesha
uvumilivu, heshima na upendo ili kwamba tusiweze kutumiwa na adui wetu. Basi na tusiwe tunasema tu habari ya imani
na neno la Mungu. Basi na tufanye sasa!
22
Lakini iweni watendaji
wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. 23 Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si
mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. 24 Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi
alivyo.
Mwenendo wetu na
uwe sawasawa na Sheria kamilifu ya Uhuru. Miriamu alikuwa amenia makuu na aliadhibiwa kwa
kuwa hivyo. Aliadhibiwa kwa kuwa na ukoma na akapelekwa nje ya Marago yao na
kutengwa kwa muda wa siku saba, sawasawa na maelekezo yaliyo kwenye Torati ya
Mungu, ambayo ni Sheria kamilifu ya Uhuru. Usiende mbele zaidi ya wajibu wako
na mamlaka yako ambayo tumepewa na kuminiwa nayo. Na tuuzizuie ndimi zetu
kuyanena, kwa kuwa kila yanayotutoka mioyoni mwetu ndiyo yanayotutia unajisi.
25
Lakini aliyeitazama
sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali
mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake. 26 Mtu
akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali
akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.
Kama hatutazizuia
ndimi zetu ndipo dini yetu haitakuwa na maana yoyote. Shetani ni mshitaki wa
ndugu zetu. Ni kazi ya malaika hawa walioasi kutushitaki sisi. Kazi yetu ni
kusaidiana na kupendana. Yakobo anatuambia kuhusu tunachotakiwa kufanya kwa
usahihi.
27
Dini iliyo safi, isiyo
na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika
dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Katika sura ya 2
Yakobo anaendelea kwa kuielezea umuhimu wa imani na matendo.
Yakobo 2:1-17
Ndugu zangu, imani
ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe nayo kwa kupendelea watu.
Kuhusu tabia ya
kuwapendelea watu inaeelezewa kwenye mwendelezo wa sura ya 2 na ni muhimu
kuielezea au kuikemea kwa kuwa kupendelea watu ni dhambi. Tutakuwa wote tunaivunja amri na Sheria kwa
kutenda dhambi hii. Kanisa linaweza kuathirika vibaya na hata kumeguka kwa
ajili ya tabia hii ya kuwapendelea watuwenye fedha au uwezo.
2 Maana akiingia katika sinagogi lenu mtu
mwenye pete ya dhahabu na mavazi mazuri; kisha akiingia na maskini, mwenye
mavazi mabovu; 3 nanyi mkimstahi yule aliyevaa mavazi
mazuri, na kumwambia, Keti wewe hapa mahali pazuri; na kumwambia yule maskini,
Simama wewe pale, au keti miguuni pangu, 4 je!
Hamkufanya hitilafu mioyoni mwenu, mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu?
Mungu ametuchagua
sisi tulio dhaifu na wanyonge, ili awaaibishe wenye nguvu. Yatupasa tuwe
matajiri wa imani kama waridhi wa ufalme wa Mungu na tuonyeshe kuwa
tunaheshimiana bila kujali hali ya mtu. Na tusiruhusu kuingia kwenye mtego wa mambo
ya mali na utajiri.
4 je! Hamkufanya hitilafu mioyoni mwenu,
mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu? 5 Ndugu zangu
wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa
imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao? 6 Bali
ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri hawawaonei ninyi na kuwavuta
mbele ya viti vya hukumu? 7 Hawalitukani jina lile
zuri mliloitwa?
Tusipunjane na
kufanyiana mabaya katika hukumu. Tunapohudumiana inatupaswa tuhukumiane kwa
haki na sio kwa kuoneana wala kwa kushitakiana kwa uwongo. Shahidi wa uwongo
hatabakia salama pasipo kuhukumiwa.
8 Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani
yako kama nafsi yako, mwatenda vema. 9 Bali
mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji.
Kitendo cha
kumpendelea mtu ni dhambi. Uvunjaji wa sheria ni mojawapo ya uovu na uvunjifu
wa sheria zote.
10
Maana mtu awaye yote
atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema,
Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.
Inatupasa kunena
na kutenda kama sheria zinavyotutaka kufanya kwa kuwa tutahkumiwa kwa Torati ya
Mungu.
12
Semeni ninyi, na
kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.
Kwenye hukumu
zote tunapaswa kuonyesha rehema na tunapaswa kuwajali na kuwainua ndugu wengine
kwa kuwarekebisha na kwa mafundisho yote.
13
Maana hukumu haina
huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.
Kwenye matendo
yote tunapaswa kuonyesha imani yetu na kwa kazi zetu. Kazi hizo zote
zinajumuisha huduma za ndugu wapendwa kwa namna zote.
14
Ndugu zangu, yafaa
nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani
yaweza kumwokoa? 15 Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu
mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki, 16 na mtu
wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini
asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini?
Haya
“mambo”yaliyotajwa hapa sio ya kimwili tu peke yake; bali ni ya kiroho pia.
Watu wanahitaji kufanikiwa, kimwili na kiroho na ni wajibu wa Kanisa kuendeleza
na kutiamoyo zaidi kuliko kukatisha tamaa au kulaumu kusiko na maana wala
lazima.
14
Ndugu zangu, yafaa
nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani
yaweza kumwokoa?
Matendo
yanathibitisha au kuonyesha imani. Tunahitajika kuhitimisha sheria kimwili na
kiroho na kuhudumiana kwa imani.
17
Vivyo hivyo na imani,
isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake. 18 Lakini
mtu atasema, Wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo
matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.
Haitoshi
kumuamini tu Mungu Mmoja na Wapekee na wa Kweli. Mapepo yanaujua ukweli huo na
kwa kutetemeka.
19
Wewe waamini ya kuwa
Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka.
Chanzo kikubwa
cha mambo hapa ni pale Yakobo anaposema kwamba imani bila matendo imekufa.
20
Lakini wataka kujua,
wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai?
Sura ya Imani kwenye Waebrania 11 imewekwa kwenye mwonekano hapa
ambapo imani ya Ibrahimu ulioneshwa kwa matendo, kama ilivyokuwa imani ya kila
mtu ambayo ilionekana kuwa waliishi kwa imani.
21
Je! Baba yetu Ibrahimu
hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka mwanawe juu ya
madhabahu? 22 Waona kwamba imani ilitenda kazi pamoja
na matendo yake, na ya kwamba imani ile ilikamilishwa kwa njia ya matendo yale.
23 Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu
alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu.
24 Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki
kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. 25 Vivyo
hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo,
hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine? 26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na
imani pasipo matendo imekufa.
Kwa hiyo mwili
pasipo na Roho Mtakatifu umekufa. Na ndivyo ilivyo pia kuwa imani bila matendo imekufa. Kama tutamhuzunisha
Roho na kumzima tunakuwa tumekufa.
Ulimi
Kwenye sura ya 3, Yakobo anaendelea dhana nyingine kuhusu ulimi. Ulimi ni
kiungo kikubwa na cha muhimu sana ambacho Shetani anakitumia sana pia Kanisani.
Tumejionea na kushuhudia maasi Kanisani yanayotokana na masengenyo au uzushi na
ndimi zinazoshuhudia mambo ya uwongo. Watu wengi wamekuwa wakiangamia kwa
masengenyo na mambo ya kuzuliana mabaya. Kumekuwa na mambo yasiyofaa
yaliyoanzishwa na ya kukwaza kwenye Sikukuu moja hadi nyingine kwa aina ile ile
ya masengenyo mabaya. Namna hii haiwezi kuvumilika ya yanapaswa kupelekwa
kwenye uongozi. Wakati Mungu anapoamua kushughulikia jambo hili, watu
wanaondolewa kutoka Kanisani, wakati mwingine kwa idadi kumbwa ya wale
walioliathiri.
Tumejionea masengenyo yakitokea Kanisani ambayo yanaonekana kutokuwa na
mwisho na yasiyo kemewa. Ushahidi wa uwongo umeendelea kuwashutumu viongozi au
hali ya kutokuwa na mtangamano wa kiakili unaotokana na hali ya kuwapendelea
watu, mashitaka au shutuma zinazotokana na hukumu mbaya ya nabaraza ya Makanisa
na matmizi mabaya ya fedha miongoni mwa watu wanaofanyakazi kwa kujitolea
wakiwatumikia ndugu wapendwa wenzao wengine.
Ushahidi wa uwongo unaweza kuendelea na kuwa masengenyo yenye kuharibu watu
nyuma yake yakilenga kuanzisha aina fulani ya mwndelezo wa shutuma ambayo
hatima yake yanakuwa ni uasi. Yanafanikiwa tu wakati yanaporuhusiwa kufanikiwa
kupitia udhaifu wa kiroho wa baraza la Kanisa. Sio vizuri sana kuona au
kuliachia Kanisa likiharibiwa na matumizi haya mabaya ya ulimi. Mungu anachukua
hatua ya kulisafisha Kanisa kwa kutumia matokeo mabaya ya dhambi hiyohiyo
yenyewe kwa udhaifu wa kiroho ili kuwaondoa. Wakati mwingine wale walio wapya
kwenye imani wanadanganyika pia.
Yakobo anatuambia sisi kuwanyenyekea viongozi wetu kwakuwa kutonyenyekea ni
tatizo kwenye Kanisa lililoharibiwa na masenhenyo. Kwenye aya ya 1 anatuambia
tusinie makuu kwa kuwa kunapelekea hukumuni na lawamani.
Hatimaye Yakobo anaonyesha kile ambacho ulimi unachoweza kukisababisha au
madhara yake yalivyo kutokana na amri na maelekezo ya Kanisa la Mungu.
Yakobo 3:1-18 inasema:
Ndugu zangu, msiwe
waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi. 2 Maana
twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo
ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu. 3 Angalieni, twatia lijamu katika vinywa vya farasi, ili
wamtii, hivi twageuza mwili wao wote. 4 Tena angalieni
merikebu; ingawa ni kubwa kama nini, na kuchukuliwa na pepo kali, zageuzwa na
usukani mdogo sana, ko kote anakoazimia kwenda nahodha. 5 Vivyo
hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi
moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. 6 Nao ulimi ni
moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio
uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto
na jehanum. 7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege,
na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha
kufugwa na wanadamu. 8 Bali ulimi hakuna awezaye
kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. 9 Kwa
huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa
mfano wa Mungu.10 Katika kinywa kile kile hutoka
baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. 11
Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? 12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu
kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.
Ujuzi Kanisani
unaonekana kwa jinsi mtu anavyonena kwa upole na busara.
13
N'nani aliye na hekima
na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzu. na wivu wenye
uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. 15 Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu,
bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. 16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo
machafuko, na kila tendo baya.
Chuki na
mabishano ni uwanja ambao Shetani anautumia ili kufikia malengo ya kujiinua na
majivuno na chuki. Kanisa limejionea tunda la matendo ya watu wenye kunaia
makuu na wanawake waongo wanapofanya kazi pamoja ili kuliharibu kanisa. Watu
wengi wameharibiwa na hali hii. Inaonekana kuwa ili kufanikisha malengo haya,
hakuna mashitaka au shutuma za pamoja yaliyo makubwa kuliko mengine. tumejionea
pia hali hii ya kuwapendelea watu ikishindwa kushughulikia mambo. Tunahukumiwa
dhamiri zetu na dhambi hizi zote. Tumejionea makanisa yakinunuliwa kwa fedha na
yakiandaliwa kumharibu au kumuangamiza mtu yeyote na kitu chochote na kuvunja
sheria yoyote.
17
Lakini hekima itokayo
juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya
watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. 18 Na tunda la haki hupandwa katika amani na
wale wafanyao amani.
Tunda la haki
limepandwa kwa amani yao inayoweka amani kwa kuwa wao wamefanyiwa kwa upole na
kwa urahisi sana. Kunai makuu na tama ni kitu kinacholeta au kusababisha vita
na kuushinda uovu na chuki. Wivu na kutamani kitu alichonacho mwingine, wakati
kwamba chuki ni hukusudia kuharibu mambo yote mawili na mtu anayekuwanayo.
Mungu atatupa
kile tunachomuomba kama tutafanya sawasawa na mapenzi yake na tukimuomba kwa
haki. Mambo mengi tunayomuomba kila mara yanakuwa sio sahihi kwa mambo
tusiyoyahitaji.
Yakobo 4:1-16
Vita vyatoka wapi,
na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu
zifanyazo vita katika viungo vyenu? 2 Mwatamani, wala
hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na
kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3 Hata
mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.
Sote tuna tatizo
na dhambi. Sisi sote
tumeondolewa kwenye tamaa ya mali nay a kimwili.
4 Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki
wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia
hujifanya kuwa adui wa Mungu. 5 Au mwadhani ya kwamba
maandiko yasema bure? Huyo Roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona
wivu? 6 Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa
hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. 7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
Huenda hii ni
changamoto kubwa sana tuliyonayo sisi sote. Hebu na tujitoe na kujinenyekesha kwa Mungu na
tumshinde adui.
8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.
Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye
nia mbili. 9 Huzunikeni na kuomboleza na kulia.
Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu. 10 Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza. 11 Ndugu, msisingiziane; amsingiziaye ndugu yake, au
kumhukumu ndugu yake, huisingizia sheria na kuihukumu sheria. Lakini ukiihukumu
sheria, huwi mtenda sheria, bali umekuwa hakimu.
Kanisa
linashughulika na utendaji wa hukumu na sheria. Kanisa linaweka kwenye jumuia
yake utaratibu wa kuhukumu mambo. Hebu na tuone kwenye Mathayo 18.
Mathayo 18:10-35
inasema:
Angalieni msidharau
mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku
zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni. 11 [Kwa
maana Mwana wa Adamu alikuja kukiokoa kilichopotea.] 12 Mwaonaje?
Mtu akiwa na kondoo mia, mmoja akampotea, je! Hawaachi wale tisa na tisini,
akaenda milimani, na kumtafuta yule aliyepotea? 13 Hata
akipata kumwona, amin, nawaambia, amfurahia huyo zaidi, kuliko wale tisa na
tisini wasiopotea. 14 Vivyo hivyo haipendezi mbele za
Baba yenu aliye mbinguni kwamba mmoja wa wadogo hawa apotee.
Mojawapo kati ya
matatizo tunayokutana nayo kwenye mabo haya ya kiroho ambayo yanasababisha
chuki na shutuma au lawama miongoni mwa wapendwa. Mafundisho poofu nay a uwongo
huja Kanisani na watu wenye tabia hii ya kunai makuu. Wanasababisha watu
kuanguka na kuiacha imani au kukengeuka. Kwa mfano, wakati Mungu alipoigawanya
Israeli na Yuda na mgawanyiko ule ulikuwa na ruhusa ya Mungu, Aliyachukua
makabila ya kaskazini na kuyatenda na Yuda na ufalme wao wakiongozwa na
Yeroboam. Yeroboamu akaenda huko Shekemu, lakini kwa kipindi cha majuma tu
walianza ksimamisha sanamu za ndama wa dhahabu huko Betheli na Dani. Kwa hiyo,
dini ya uwongo na potofu ilianzishwa kwa kipindi kifupi sana. Ili kuzuia wazo
la kuinganisha tena Kanisa, Yeroboamu akaiweka kalenda kutoka moyoni mwake na
ambayo inafanana na ile ya Mwandamo wa Mwezi Mpya iliyoanzia baada ya kipindi
cha ikwinoks, na ambayo iliwekwa ikianzia tahere 25 Machi. Kalenda hii
inajulikana hata leo kama Kalenda ya Wasamaria.
Kuna watu kwene
Kanisa la Mungu wanaopenda kuitambulisha na kuuingiza kalenda ya Wasamaria na
wanaotaka kuwapotosha watu kwa mafundisho ya uwongo. Ni kwa jinsi hiyohiyo,
watu wanaotaka kuingiza mafundisho ya mwezi mchanga wanatafuta jinsi ya
kuligawa Kanisa la Mungu.
Wanauadhimisha
wakati mwingine hata hapa nchini Australia, wakati mwezi mkamilifu uliwa kwenye
siku ya 15 wakati ukiwa haujawa mwezi mkamilifu sana bado. Jambo hili
halimaanishi kwamba siku ile haijawa ni ya mwezi mkamilifu. Wakati mwezi
mkamilifu ukiwa kwenye hatua iliyochelewa ya mwendelezo wake, haufikii kwenye
wastani wake hasa hadi unapokuwa kwenye mzunguko wa upande mwingine wa dunia.
Watu wanatumia
jambo hilo ili kujaribu kuieneza kalenda ya Hilleli na wakitafuta kusababisha
migawanyiko na kuligawanya Kanisa. Mambo haya yote yanafanyika kwa lengo la
kuligawanya Kanisa na kuliharibu kwa kupitia mafundisho ya uwongo na
imethibitika kufanikiwa miongoni mwa watu wasioelimika.
Kwenye aya ya 15,
inaendelea kusema yafuatayo:
15
Na ndugu yako
akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata
nduguyo. 16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena
mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno
lithibitike.
Utaratibu huo
umekuwa umewekwa Kanisani kwa kiwango cha kuheshimika na ni mara chache sana
umekuwa ukipingwa au kukataliwa.
17
Na asipowasikiliza
wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa
mataifa na mtoza ushuru.
Tumeona watu
wakidiriki kuyashutumu mabaraza ya Kanisa kwa kuwapendelea watu, kwa kutotoa
hukumu au kuizungusha hukumu kwa jinsi isiyo ya haki au kuwa ni ‘wajumbe
ndiyo’. Malalamiko haya yamekuwa yakitolewa kwa wazi na hadharani au pengine
kwa uficho, na machoni pa Kanisa lenyewe lililotoa hukumu hiyo. Wakati Kanisa
linapojikanganya kwenye hukumu, wale wasioathirika wanapenda kwenda kwenye
sheria, wakikata rufaa kwenye vyombo vya sheria dhidi ya hukumu iliotoewa
Kanisani inapokuwa inawafaa wao. Kwetu sisi watu hawa tunawachukulia kama
wapagani au wamataifa waso na Mungu mioyoni na maishani mwao.
18
Amin, nawaambieni, yo
yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote
mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. 19 Tena
nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote
watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. 20 Kwa
kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo
katikati yao.
Hii ni ahadi ya
Mungu, kwa kupitia Kristo, kwa Kanisa na kwamba sisi tutawahukumu malaika. Ni
kwa kiasi gani basi tunaweza kuhukumu mambo ya watu walio Kanisani.
21
Kisha Petro akamwendea
akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara
saba? 22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba,
bali hata saba mara sabini.
Msamaha
unahitajika kwa kiasi endelevu, kwetu sisi wote. Hata hivyo, kunapaswa kuwepo na toba. Tunasamehe
kutoka mioyoni mwetu na tunapata kutokana na kazi tuliyoifanywa kwa mikono
yetu. Tukiwasamehe wengine, na ndipo Mungu hutusamehe sisi pia. Lakini ili mtu
aweze kuaminiwa, kunabidi lionekane kwanza tunda la toba ndani yake. Kusamehe
ni jambo linalotulazimu kuwanalo, yaani kumsamehe mtu aliyetuksea.
23
Kwa sababu hii ufalme
wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.
24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye
talanta elfu kumi. 25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana
wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo,
ikalipwe ile deni. 26 Basi yule mtumwa akaanguka,
akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. 27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe
ile deni. 28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa
wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe
uwiwacho. 29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake,
akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. 30 Lakini
hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni. 31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika
sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka. 32 Ndipo
bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile
yote, uliponisihi; 33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu
mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe? 34 Bwana
wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote. 35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi,
msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.
Hatuwezi
kumsamehe mtu na huku tukishikilia aina fulani ya malipo au fidia itolewe nao,
au huku tukinung’unika au kuyashikilia mambo tunayoyatenda. Na wala tusipende
kuwalaumu vikali ndugu zetu. Hakuna mtu anateweza kukizuia kile kilicho katika
Roho. Hakuna mtu anayeweza kuishi sawa sawa na vile ilivyo kwenye Kanisa.
Italila Kanisa kama inavyofanya saratani.
Wazo la
kujinyenyekesha sisi wenyewe kwa Mungu ni moja ya amani na wanadamu kwenye
mapenzi ya Mungu. Inatupasa kumpinga Shetani naye atatukimbia. Tunapaswa
kumkaribia Mungu naye atatukaribia. Na tuisafishe mikono yetu, sisi ni wenye
dhambi wakubwa; na tuitakase mioyo yetu, na tusiwe watu wa kutangatanga au
wenye nia mbili. Tumeambiwa tujitese, na tuomboeze na kuhuzunika; na kicheko
chetu kigeuke kuwa maombolezo ay huzuni na furaha yetu kuwa huzuni, na
tujinyenyekeshe machoni pa Bwana, naye
atatuinua juu au kututukuza. Wala tusidanganyane wala kusemana vibaya,
wapendwa. Yeye amneneaye mwenzake vibaya na kumhukumu ndugu yake, basi anainene
vibaya sheria, na anaihukumu sheria; bali kama tutaihukumu sheria, ndipo mioyo
yetu hitakuwa watendaji wa sheria, bali ni wenye kuhukumu tu.
Hakuna
aliyemchagua mtu mwingine kuwa ni hakimu wake, isipokuwa ni mahakama ya Kanisa.
Na hukumu hii na itendeke kwa haki na utakatifu na watu wenye roho na
walioitendea kazi imani kwa miaka mingi. Tusitafute wala tusipende kulaumiana au kueneza lawana na
kuchafuana au kutafuta kumshushia hadhi mtu yeyote miongoni mwetu kama
ilivyowahi kutokea. Na usijaribu kuwa hakimu hadi utakapochaguliwa kuwa hakimu
wa Kanisa.
Na pia tusijaribu
kutafuta faida au kufaidika kwa kumshuhudia ushuhuda mbaya au wa uwongo mtu
mwingine wakati kukiwa hakuna mashitaka. Hakuna aliye wa muhimu kiasi cha kuwa
mhukumu au hakimu isipokuwa kwenye mahakama ya Kanisa.
Yakobo 4:12
inaendelea kwa kusema:
12
Mtoa sheria na mwenye
kuhukumu ni mmoja tu, ndiye awezaye kuokoa na kuangamiza. U nani wewe
umhukumuye mtu mwingine? 13 Haya basi, ninyi msemao,
Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya
biashara na kupata faida; 14 walakini hamjui
yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa
kitambo, kisha hutoweka. 15 Badala ya kusema, Bwana
akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi. 16 Lakini
sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya. 17 Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala
hayatendi, kwake huyo ni dhambi.
Kwa maneno
mengine ni kusema, kama tutakuwa tunajua mambo, basi tunapaswa kuyafanya, na
kama hatutayafanya, itakuwa dhambi. Tumetenda yale ambayo Bwana alitutaka
tuyafanye tangu mwanzo. Tunajua kwamba Bwana analitaka Kanisa kwa kipindi
kingine cha zaidi ya miaka saba mingine ijayo. Tutaihitiwisha il kazi. Mungu na
atatusaidia, na haitakuwa ni kitu cha kukanganya.
Yakobo 5:1-20
Haya basi, enyi
matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia. 2 Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa
na nondo. 3 Dhahabu yenu na fedha
yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama
moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. 4 Angalieni,
ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga
kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. 5 Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa;
mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. 6 Mmehukumu
mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi. 7 Kwa
hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya
nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya
kwanza na ya mwisho. 8 Nanyi vumilieni, mthibitishe
mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia. 9 Ndugu,
msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya
milango. 10 Ndugu, watwaeni
manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa
uvumilivu.11 Angalieni, twawaita
heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa
Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma. 12 Lakini
zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, wala kwa mbingu wala kwa nchi; wala kwa
kiapo kinginecho chote; bali ndiyo yenu na iwe ndiyo, na siyo yenu iwe siyo,
msije mkaangukia hukumu. 13 Mtu wa kwenu
amepatikana na mabaya? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi. 14 Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite
wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. 15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa
mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
Sio kazi ya kulilalamikia
Kanisa tu linapoitendea kazi dhambi inapojitokeza miongoni mwetu na kuyatoa
majukumu ya kuyafuta. Mungu hutusamehe dhambi zetu tunapobatizwa na kwene
maadhimisho ya Pasaka. Maombi ya mwenye imani htmuokoa sisi na yanatuunganisha
pamoja na hulisaidia Kanisa. Sisi sio wengi hapa duniani. Kila adhimisho la
Sikukuu, mara tatu kwa mwaka, ni hija ambako tunakutana kila mmoja wetu kwa
watu wale wale hadi pale Mungu amchague na kumuongeza mtu kwenye ushirika hu.
Ni kazi na wajibu wetu kuutunza mwili huu, na kama kuna mtu aliyepotea kwa
ajili ya sisi kumkwaza ni makosa yetu. Tusijione kuwa ni wenyewe tu na
kutoutilia maanani ukweli kwamba kuna watu wamefanyiwa hila hadi waondoke
kwenye imani. Mungu hutuongeza na ni yeye ndiyr anayewachukua kutoka kwetu.
Hatari iliyoko ni
kwamba, tunajiona vizuri tu wakati Mungu anapowaondoa watu kutoka kwetu. Hata
hivyo, baadhi ya watu wanaondolewa kutoka kwetu kimakosa wananyonywa na wale
wanaotgaka kutuangamiza. Wala tusiwalaumu. Bali na tumlaumu mshitaki wa ndugu
zetu anayetushambulia.
16 Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na
kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa
bidii.
Sisi miongoni
mwetu ambao hatuna uwezo wa kusaidia kimwili tunaweza kuomba kwa bidii kwa kuwa
maombi yananguvu na yanathiri karibu kazi zetu kama sio zote.
17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja
na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda
wa miaka mitatu na miezi sita. 18 Akaomba tena,
mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake. 19 Ndugu
zangu, ikiwa mtu wa kwenu amepotelea mbali na kweli, na mtu mwingine
akamrejeza; 20 jueni ya kuwa yeye amrejezaye
mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na
kufunika wingi wa dhambi.
Hii haimaanishi
kuwa kila mtu amepangiwa kukosoa au kurekebisha au kusahihisha mawazo yasiyo
sahihi na mwenendo wa wapendwa. Kila kitu tunachokifanya kinapaswa kitendeke
kwa kuzingatia upendo na wema, na sio kwa shutuma na sio kwa kupenda
kujitafutia lawama au mashitaka dhidi ya ndugu zetu.
Ni bahati mbaya
sana kwamba ni Yakobo peke yhake tu ndiye aliandika waraka mmoja tu kwa kuwa
uelewa wake ulikuwa ni kmubwa sana kuliko wa Paulo. Uwezo wake ulikuwa ni
mkubwa sana kwa kuwa pia alikuwa ni mtume kiongozi na ndugu yake Kristo. Kwenye
uelewa wake wa sheria na sheria kamilidu ya uhuru anatupa muongozo kwamba
tunapaswa kuzishika na kuzitenda sheria na tuendende kwazo. Tunapaswa
kuchukuliana na ushirika ambao Yakobo anauelezea kwa kuwa ulikuwa unaenenda
kinyume na waraka huu wa Yakobo na alipoona kwamba Kanisa lilikuwa linakaribia
kwenye uangamifu au uharibifu.
Kitendo cha
kuwapendlea watu hupelekea kuwepo kwa mgawanyiko na mafarakano. Tabia hii ya
kuwapendelea watu au upendeleo imebaka kuwa ni dhambi moja kubwa kabisa kubakia
kwenye Makanisa ya Mungu.
q