Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[025]

 

 

 

Alama ya Mnyama

(Toleo La 2.0 20010525-20060703)

 

Fundisho kuhusu Alama ya Mnyama limekuwa ni mojawapo ya nyama inayoendelea na tarajio la sehemu ya ile wanaodaiwa kuwa ni imani ya Kikristo. Hata hivyo, dhana na fundisho hili limekuwa likikosewa kuleweka kwakr kwa kiasi kikubwa sana kulinganisha na unabii wote wa Biblia. Umakini katika usomaji wa Maandiko Matakatifu na kuiruhuru Biblia ijitafsiri yenyewe kutampelekea mtu kuelewa kuwa ni jambo tofauti sana na mafundisho makongwe na yakizamani ya makanisa ya zama kale. Ingawaje kuelewa kuhusu huyu Mnyama ni nani na ishara ya alama yake ni ipi ni muhimu sana na inasaidia katika kumpeleka mtu kwenye uelewa mzuri na kamilifu wa nabii nyingine nyingi na mchakato mzima wote ulio kwenye Mpango wa Mungu.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 2001, 2006 Scott Rambo, ed. Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Alama ya Mnyama


 


Kwa kipindi chote cha takriban miaka 1900 au zaidi watu wamekuwa wakitangatanga kutaka kujua kuhusu ni nini hasa maana ya alama ya Mnyama. Je, ni nini hasa maana ya alama hii ambayo watu wanaiogopa sana kuipokea, alama hii ambayo wakati wake watu hawataweza kuuza wala kununua? Je, ni kiolezo cha compyuta ndicho kitakachochokewa kitaalamu kwenye nyuso za watu au mikononi? Je, ni kitu kitakachokuja kwa mwonekano kama wa tatuu au chanjo? Je, ni nini hasa alama hii ya Mnyama?

 

Onyo kuhusu alama hii ya Mnyama limetolewa na kuandikwa kwenye nabii nyingi kadhaa za kitabu cha Ufunuo.

 

Ufunuo 13:16-17 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao; 17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.

 

Ufunuo 14:9-11 Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, 10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo. 11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake.

 

Kwa hiyo, ni je, alama hii inamaana gani au inataja nini? Je, jana la mnyama huyu ni lipi, na tarakumu hii y jina lake ni kitu gani basi? Ili kuelewa maswali haya inatupasa kutafakari maana ya neno na dhana nzima ya hii alama na ya mnyama kama zilivyoelezewa kwenye Biblia. Haitakuwa vizuri kubahatisha au kinadharia kuhusu maana ya maneno haya. Mtume Petro alisema, “Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.” (2Petro 1:20). Hii ni pointi ya msingi ya kwa nini suala hili la alama ya mnyama limeshindwa kueleweka kabisa na kupotoshwa. Badala ya kuyaacha Maandiko Matakatifu yajitafsiri yenyewe, watu wanapenda kuitafsiri Biblia kwa kufuata mujibu wa imani zao zinavyopenda na kuelekeza. Kwa sababu hii ndipo ulimwengu umejionea manabii wengi wa uwongo wakitokea mmoja baada ya mwingine wakitoa ama kufundisha nabii za uwongo kuhusiana na maana ya alama hii ya mnyama. Namna pekee ya kuelewa kinachomaanishwa kwenye neno hili “alama ya mnyama” ni kwa kuyasoma Maandiko Matakatifu kama nabii Isaya alivyosema hebu na tuiruhusu Biblia ijitafsiri yenyewe.

 

Isaya 28:9-13 Atamfundisha nani maarifa? Atamfahamisha nani habari hii? Je! Ni wale walioachishwa maziwa, walioondolewa matitini? 10 Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo. 11 La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa; 12 ambao aliwaambia, Hii ndiyo raha yenu, mpeni raha yeye aliyechoka; huku ndiko kuburudika; lakini hawakutaka kusikia. 13 Kwa sababu hiyo neno la Bwana kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.

 

Kwa kuangalia kwa karibu na kwa kuweka kituo hadi kituo, mstari hadi mstari, tunaweza kujipatia uelewa mzuri wa somo hili. Kwa kufanya hivyo, tutaona kwamba matumizi ya biblia ya neno alama linatumika tu pale inapokusudia kwa kumaanisha au kwa mtazamo wa kutiwa alama kwenye vipaji vya nyuso au mkononi. Tutajionea pia kwamba matumizi ya biblia ya neno mnyama ni sawa na kama linavyotumika kwenye unabii.

 

Tunahitaji kuona maana ya kimaandiko ya Maandiko Matakatifu mengine tofauti tofauti ili kuelewa kikamilifu maana hii ya alama ya mnyama. Mawazo haya yamefungamana na mifano ya vitu na mifano au mionekano ya kiroho kwa pale inapotaka kuchambuliwa ili kuweza kuelewa kikamilifu migawanyo ya nabii hizi. Haiwezekani kuelewa kinachoendelea na alama hii ya mnyama kwa kutumia tafsiri ya moja kwa moja ya kimwili ya Biblia. Haya ni mawazo yanayohusiana na ambayo yamefunuliwa tu pale mtu anapochimba kwa kupitia kina-ardhi cha moja kwa moja ya kimwili na kwenye kina ya kiroho.

 

Mji wa Yerusalemu Mpya una milango ya lulu (Ufunuo 21:21). Maana inayohukuliwa na milango hii ya lulu ni kama ifuatavyo. Milango ya mji ni njia ya kuingilia mjini. Lulu  tunayoijua imetengenezwa kwa kupitia magamba/ ya chaza ambayo imechukuliwa kutoka kwenye kipande cha changarawe na hatimaye ilifanyika mchakato wa mahali pa tabaka la lulumizi karibu na jiwe la changarawe hadi lulu hafifu na isiyo na dhamani iundike. Na ndivyo pia siri za Mungu zinaeleweka kama habari ya ukweli uliodhahiri ambao umewekewa tabaka na maana za kiroho makusudio yake. Ili kuelewa maana hizi za kiroho ni kuiona milngo ya mji wa Mungu (pia jisomee jarida la Mji wa Mungu (Na. 180) [The City of God (No. 180)]. Na hii ndiyo sababu pia Kristo alisema tusitupe lulu mbele za nguruwe, wasije wakazikanyaga kwa miguu yao na wakaturudi na kuturarua.

 

Mathayo 7:6 Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.

 

Kristo alikuwa anasema kuwa tusiyafunuo mambo yaliyo kwenye fumbo za Mungu kwa nguruwe waliopo, kama tutakavyoonyesha baadae, hawa ni wale Malaika walokengeuka pamoja na wafuasi wao, wasijewakaitumia elimu ile tena na kuwapotosha wateul wote. Na hii ndiyo sababu siri za Mungu zimefunuliwa kwa sehemu na kwa utaratibu na zote ni kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu. Kwa kweli malaika wenyewe wanatamani kuziona siri hizi.

 

1Petro 1:12 Wakafunuliwa ya kuwa si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Mambo hayo malaika wanatamani kuyachungulia.

 

Nyingi ya siri hizi zimetiwa mhuri na kufungwa hadi ufike watati wenyewe muafaka uliokusudiwa wa mwisho, ambao ndiyo huu tulionao sasa (soma jarida la Mchakato wa Ratiba ya Kipindi-Zama (Na. 272) [Outline Timetable of the Age (No. 272)].

 

Alama

Neno la Kiyunani lililotumika kwenye Ufunuo ambalo kwenye lugh ya Kiingereza limetumika kuadikwa “Mark” yaani Alama, ni neno charagma {khar'-ag-mah} kutoka kwenye Kamusi ya Kiyunani ijulikanayo kama Strong’s Greek Dictionary #5480 maana yake ni:

1) stemp au mhuri, au alama iliyochapwa

1a) ya stempu au mhuri uliogongwa kwenye kipaji cha uso au kwenye mkono wa kuume uliwa ni alama au ishara ya wafuasi wa Mpingakristo

1b) mhuri au alama iliyochapwa kwa farasi

2) vitu vilivyochongwa, na kuwa sanamu, kazi ya kuchongwa

2a) sanamu ya kuabudiwa

Neno la Kiebrania linalofanana na neno hili Alama kwenye Agano la Kale ni neno 'owth' {oth}, kwa mujibu wa Kamusi ya Kiebrania ya Strong’s Hebrew Dictionary #0226 ikimaanisha:

1) ishara, dalili au kiashirio

1a) ni mhuri au alama inayotofautisha

1b) bango au bendera

1c) ukumbusho

1d) ishara ya kimiujiza

1e) ishara

1f) onyo

2) kete, tepe, kiwango, miujiza, uthibitisho

Neno hili limetafsiriwa kama ishara kwenye fafanuzi au maana nyingi, lakini pia linamaanisha alama inayotofautisha. Kuna ishara au alama iliyotolewa na Mungu kwa wale wanaozishika Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu na Torati.

 

Kutoka 13:6-10 6 Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba, nayo siku ya saba itakuwa ni sikukuu ya Bwana. 7 Mikate isiyochachwa italiwa katika hizo siku saba; mkate uliotiwa chachu usionekane kwako, wala chachu isionekane kwako, ndani ya mipaka yako yote. 8 Nawe utamwambia mwanao siku hiyo, ukisema, Ni kwa sababu ya hayo Bwana aliyonifanyia hapo nilipotoka Misri. 9 Nayo itakuwa ishara kwako katika mkono wako, na kwa ukumbusho kati ya macho yako, ili kwamba sheria ya Bwana ipate kuwa kinywani mwako; kwani Bwana alikutoa utoke Misri kwa mkono wenye uwezo. 10 Kwa hiyo utaitunza amri hii kwa wakati wake mwaka baada ya mwaka.

 

Kumbukumbu la Torati 6:1-9 Na hii ndiyo sheria, na amri, na hukumu, alizoziamuru Bwana, Mungu wenu, mfundishwe, mpate kuzitenda katika nchi ile mnayoivukia kuimiliki; 2 upate kumcha Bwana, Mungu wako, kushika amri zake zote, na sheria zake, ninazokuamuru, wewe na mwanao, na mwana wa mwanao, siku zote za maisha yako; tena siku zako ziongezwe. 3 Sikiza basi, Ee Israeli, ukaangalie kuzitenda; upate kufanikiwa, mpate kuongezeka sana, kama Bwana, Mungu wa baba zako, alivyokuahidi, katika nchi ijaayo maziwa na asali. 4 Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. 6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; 7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. 8 Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. 9 Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.

 

Ni kama mnyama wa Ufunuo alivyo na alama inayotiwa kwenye vipaji vya nyuso na mikononi mwa wale wanaomuabudu, na ndivyo hivyohivyo pia Mungu anayo alama au mhuri inayotiwa kwenye vipaji ya nyuso na mikono ya wale wanaomuabudu. Suala hili limetathminiwa kwa kina kwenye jarida la Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)]. Mhuri au alama hii inwekwa upande paji la uso kwa kuwa hapo ndipo mawazo ya mtu yanatungwa. Mhuri au alama hii pia inapigwa kwenye mkono kwa kuwa hapo ndipo mawazo ya moyo wa mtu hutekelezewa na kutedewa kazi. Ni kwa kuzifuata hizi Amri za Mungu, kwa namna zote mbili, yaani kwa moyo na kwa matendo, ndipo mtu anapokea alama hii ya Mungu. Ni kama ilivyoandikwa kwenye Kutoka 13:6-10, amri hizi zinajumuisha pamoja ushikaji wa taratibu zilizowekwa na Mungu za imani na ibada, kwa mfano, kuziadhimisha Sikukuu kama vile Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu na nyinginezo.

 

Ishara na alama hii ya Mungu siyo ya kimwili, ya kawaida; ila ni ishara na alama za kiroho. Hakuna hata mmoja kati ya manabii wala Yesu Kristo mwenewe aliyeyekuwa na alama ya kimwili kwenye vipaji vya nyuso zao wala mikononi mwao zilizowaonyesha kuwa wao ni watu wa Mungu. Zaidi tu ni kwamba walikuwa na alama za kiroho, ikiwa kama msaidizi wake wa kimwili katika matumizi ya chapa ya ng’ombe, inayoonesha umiliki na raslimali unaohakikishwa kwa alama, na utii na madai halali ya umiliki kwa yule aliye na alama au ishara yake.

 

Tunaona mahali pngine kwenye kitabu cha Kutoka inaposema kwamba Sabato ni alama au ishara nyingine pia.

Kutoka 31:12-17 Bwana akasema na Musa, na kumwambia, 13 Kisha, nena wewe na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi. 14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. 15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa Bwana; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa. 16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato, kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele. 17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Bwana alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.

 

Sabato, ikiwa kama ni moja ya siku zilizoamriwa na Mungu kuwa watu kuziadhimishe, ni ishara pia kati Mungu na watu wake (soma jarida la Sabato (Na. 31) [The Sabbath (No. 31)]. Kumbuka pia kwamba hii ni ishara ya milele. Haitakoma hata na kuja kwake Masihi. Haijabadilishwa kamwe kuwa siku ya Jumapili na Mungu wala na Yesu Kristo. Jumapili wakati wote ilikuwa nab ado inaendelea kuwa siku ya ibada ya wale waliomuasi Mwenyezi Mungu na walioziasi Amri na Sheria zake. Ni bahati mbaya sana, kuwa wengi wa wale wanaojiita kuwa Wakristo wa siku hizi, wanaichukulia Jumapili kuwa ni Siku ya Bwana. Yesu Kristo mwenyewe alisema kuwa yeye ni Bwana wa Sabato, na sio Bwana wa Jumapili wala wa siku nyingineyo yote (soma jarida la Siku ya Bwana na Siku za Mwisho (Na. 192) [The Day of the Lord and the Last Days (No. 192)]

 

Mathayo 12:8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

 

Na hata utunzaji huu na kuabudu siku za Sabato umepuuzwa pia na wanaoiadhimisha ibada za Juma'a au Ijumaa, badala yake, yaani umma wa  Waislamu ambao wanahatia kubwa kwa kuamua kwao kufanya hivyo. Mtume wao aitwaye Muhammadi, kamwe hakukusudia waumini wake waihalifu Sabato na badala yake wameifanya ile siku ya maandalio kuwa siku takatifu kwa kuzingatia haki yao wenyewe (soma jarida la Ijuma’a Kwa Maandalio ya Sabato (Na. 285) [The Juma'ah: Preparing for the Sabbath (No. 285)].

 

Sabato ni adhimisho la siku ya saba ya juma la uumbaji, siku ambayo Mungu alistarehe na kupumzika katika kazi zake zote. Ni siku ambayo inaashiria pia tukio kuu la mapumziko ya kipindi cha miaka 1,000 ya millennia. Sabato oilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, na sio mwanadamu sio kinyume chake, yaani mwanadamu kwa ajili ya Sabato, na sio siku nyingine (Marko 2:27).

 

Alama na mhuri wa Mungu kwa hiyo imetolewa kwa wale wanaozishika amri za Mungu na kwa wale wanaomuabudu yeye sawasawa na jinsi alivyoamuru na sio kwa jinsi wanvyoona sawa kumuabudu yeye. Wale waliotiwa mhuri wa Mungu wanamuabudu kwa kuzishika amri zake na kwa kuzishika Sikukuu zilizoamriwa na sio kwa kuyaiga matendo ya mipagani na kuyaita matendo hayo kuwa ni ya Kikristo. Tunajua kwamba Mungu hapendi watu wamuabudu kwa jinsi namna hiyo, yaani kwa jinsi wanavyoona vyema wenyewe.

 

Kumbukumbu la Torati 12:29-32 Bwana, Mungu wako, atakapoyakatilia mbali hayo mataifa mbele yako, huko uingiako kuyamiliki, nawe ukawatwaa, na kuketi katika nchi yao; 30 ujiangalie, usije ukanaswa ukawafuata, wakiisha kuangamizwa mbele yako; wala usije ukauliza habari za miungu yao, ukisema, Mataifa haya waitumikiaje miungu yao? Nami nifanye vivyo. 31 Usimtende kama haya Bwana, Mungu wako; kwani kila yaliyo machukizo kwa Bwana, ayachukiayo yeye, wameifanyia miungu yao; kwa maana hata wana wao na binti zao huiteketezea hiyo miungu yao ndani ya moto. 32 Neno niwaagizalo lo lote liangalieni kulifanya; usiliongeze, wala usilipunguze.

 

Tunapaswa kufanya na kuadhimisha kile Mungu anachotuagiza. Hii haiwezi kufanyika kwa kudai tu kwamba maagano yote mawili, yaani Agano la Kale na Jipya yamegeuzwa kwa kiasi kwamba hatujui kile ambacho maandiko asilia yanavyosema, kama unavyofanya Uislamu. Gombo la Chuo lililogunduliwa kwenye Bahari ya Chumvi linathibitisha kuwa tuna maandiko yaliyoandikwa kwenye wakati wenyewe muafaka sasa kama yalivyokuwapo hata kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammadi. Kuran (Kora) haiwezi kueleweka pasipo kuitumia sambamba Biblia. Ni kwakuielewa Torati tu na ushuhuda wa manabii wa nyakati zote mbili, Agano la Kale na Jipya, ndipo Kurani inaweza kueleweka vizuri. Na hii ndiyo maana Mtume mwenyewe aliagiza usomaji wa Maandiko Matakatifu.

 

Maana iliyoko kwenye Kumbukumbu la Torati 12 inapaswa iwe ya wazi sana vya kutosha kwa watu wote kuona. Inafanyika kwa Wakristo (Israeli wa kiroho), kiasi chochote kidogo knachofanyika kwenye taifa la kimwili la Israeli. Kama Waislamu wa kweli, kwa kile kilichofundishwa na mtume na Makhalifa Wanne waliokuwa mkono wake wa Kuume na Viongozi, mwanzo wake ulikuwa ni tawi la Ukristo, na hii inatendeka sawasawa na wale wanaodai kuwa wana imani ya Kiislamu. Mungu habadiliki. Ni yeye yule, jana, leo na hata milele. Matendo mengine ya kipagani ambayo alichukizwa nayo hata kabla ya kuja kwa Masihi, pia alikuwa amechukizwa baada ya kufa kwake Msihi. Wakiwa kama Israeli wa kimwili hawakupaswa kunaswa na mitego wa matendo haya ya kipagani, na ndivyo tunavyopaswa kuwa sisi kama Israeli wa kiroho, yaani, kama Kanisa tusiingie mtegoni kukumbatia imani na matendo haya ya kipagani.

 

Kwa kuzibadilisha amri na Sikukuu zalizoamriwa na Mungu, imani zote hizi mbili, yaani Ukristo mkongwe wa kale na Uislamu wamejikana wenyewe mhuri halisia wa Mungu. Hakuna mahali kwenye Biblia inaposema kwamba Mungu amemtia alama kwa yeyote anayemuabudu kwa namna wanazoabudu mataifa ya kipagani. Kwa makosa/default na bahati mbaya sana, wale wanaoitwa Wakristo na Waislamu wamejinyima wenyewe mhuri huu wa Mungu. Hawazishiki Sabato, wala Idi za Mikate Isiyotiwa Chachu, au sheria za Mungu, zote ambazo Maandiko Matakatifu yanasema ni ishara ya mhuri wa Mungu. Badala yake, tuna Ukristo wa zama kale unaodai kwamba sheria na amri za Mungu zimegongolomewa mtini wengine huita msalabani wakati zilikuwa ni chierographon —yaani nakala ya uhuru ambazo kwazo tunawiwa na Mungu kwa dhambi zetu – zizilopigiliwa mtini. Kwa bahati mbaya, wanadai kuwa sheria zinapaswa kushikwa na kisha wanaendelea kusema kwamba siku ya kwanza ya juma ndiyo Sabato ya sasa ikichukua mahali a Sabato ya kweli ya siku ya saba ya juma. Wanakataa kusikiliza kwa uwazi na maneno yenyewe ya Masihi pale aliposema kuwa hakuja kuitangua torati.

 

Mathayo 5:17-19 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. 19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.

 

Anisa Katoliki la Roma linadai kwamba lina mamlaka ya kuzibadilisha Sheria. Hata hivyo, Masihi anasema kuwa wale wanaofanya hivyo, na kuwafundisha wengine kufana hivyo, watakuwa duni kwene Ufalme wa Mungu.

 

Katika siku za mwisho dunia haitaruhusiwa kupata madhara hadi idadi kamili ya watumishi wake Mungu watiwe mhuri wake.

 

Ufunuo 7:2-3 Nikaona malaika mwingine, akipanda kutoka maawio ya jua, mwenye muhuri ya Mungu aliye hai; akawapigia kelele kwa sauti kuu wale malaika wanne waliopewa kuidhuru nchi na bahari, 3 akisema, Msiidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao.

 

Watumishi hawa wa Munguj katika siku za mwisho wanatiwa mhuri kwenye vipaji vya  yuso zao kwa kuwa wanasheria za Mungu mioyoni mwao, na, kwa kipindi kirefu wamekuwa wanazishika amri hizi kwa matendo. Hawa ndio wale waliotabiriwa na nabii Yeremia.

 

Yeremia 31:33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

 

Kutaniko la Mungu katika siku za mwisho ni wale waliorudia agano. Hawa ni wale ambao Mungu ameziweka sheria zake ndani yao. Hii ndiyo kusudi ya mfano wa Sanduku la Agano. Sanduku liie, ambalo Mungu alimpa Musa na kazi ya watu ilikuwa ni kuwaelekezea wateule. Ni kama alivyosema Mtume Paulo kuwa wateule ni Hekalu la Mungu.

2Wakorintho 6:16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

 

Sanduku hili lilisimamishwa ndani ya hekalu. Sanduku hili lilikuwa ni ishara mioyo ya wateule (soma jarida la Sanduku la Agano (Na. 196) [The Ark of the Covenant (No. 196)]. Ni ndani ya mioyo ya wateule ndimo Mungu aweka Sheria zake, ni sawa tu kama zile mbao zilizoandikwa Toarti zilivyotiwa ndani ya sanduku la agano. Torati ya Mungu inaanzia na zile amri kuu mbili za Mungu. Amri hizi kuu mbili zilisisitizwa na Kristo.

 

Marko 12:28-31 Na mmojawapo wa waandishi akafika, akawasikia wakisemezana naye, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza? 29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; 30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. 31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.

 

Yesu alisema kuwa sheria zote na yote yale yaliyosemwa na manabii yanatuama kwenye amri hizi mbili kuu. Utaratibu wote wa ibada umefungamanishwa na amri hizi kuu mbili. Zimevunjwavunjwa kwenye vipande na kuwa Amri Kumi, ambazo zimeandikwa kwenye vibao ambazo ziingizwa kwenye Sanduku la Agano. Kila moja ya Amri hizi Kumi zilikuwa zimeelekezwa zaidi na Musa na manabii. Kumuabudu Mungu kwa kuzisika Sabato, Sikukuu zalizoamriwa na Siku Takatifu, kumeungamanishwa moja kwa moja na Amri Kuu ya Kwanza. Kwa hiyo, ni kama Yesu alivyosema, ili kuupata uzima wa milele, ni lazima mtu azishike amri.

 

Mathayo19:17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.

 

Wale waliotiwa mhuri na Malaika wa Mungu na kuwa na mhuri wa Mungu ndio wale watakaokuwa wanazishika Sabato, Miandamo wa Mwe zi Mpya, na Sikukuu alizoziamuru Mungu, pamoja na amri nyingine zote zilizobakia (sokma jarida la Torati ya Mungu (Na. L1) [The Law of God (No. L1)].

 

Kinyume chake, alama ya mnyama ni alama ya wale ambao hawamuabudu Mungu kama alivyoamuru, bali wanamuabudu mungu wa uwongo sawasawa na imani na mifumo ya uwongo ya ibada. Lakini ni huyu mnyama ndiye watu wengi karibu ulimwenguni kote humuabudu? Ili kuuelewa mfumo wa mnyama katika siku za mwisho yatupasa turudi nyuma kwenye kitabu cha Mwanzo.

 

Wanyama wa Kondeni

Tunajua sote historia ya Adamu na Hawa kwenye Bustani ya Edeni (soma jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni (Na. 246) [The Doctrine of Original Sin Part I The Garden of Eden (No. 246)]. Kuna mambo mengi sana yanayoendelea kuhusu habari hii zaidi ya zile zilizodhahiri zijulikanazo. Mtu asipochimba kwa kina kiroho ya habari hii, kijuujuu inaonekana kuwa ni kama hadithi au simulizi tu inayosimuliwa ili mashiko kidogo nje ya mwanadamu halisi na kinachotufanya tutofautiane na viumbe wengine duniani. Kwenye Mwanzo 3:1 nyoka aaliyemdanganya Hawa anatajwa kuwa “mwerevu kuliko kuliko hayawani wengine wote, aqliyewaumba Bwana Mungu”.

Mwanzo 3:1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

 

Huyu sio nyoka halisi wa kimwili anayenena hapa, lakini ni kiumbe ambaye alikuwa ni Kerubi aliyemuasi Mungu. Neno la kiebrania litumikalo kumtaja nyoka ni nachash {naw-khawsh'}, limechukuliwa kwenye neno ambalo shina lake ni nachash {naw-khash'} ambalo maana yake ni mwenye nuru na limeitwa serpent kwa Kiingereza, yaani nyoka kwa Kiswahili.

 

Huyu mwenye kutoa nuru ni Kerubi Mwenye Mabawa Yafunikayo; Malaika wa Nuru au Mleta Nuru au Lusifeli aliyeandikwa kwenye Isaya 14 na kwenye Ezekieli 28:13-17.

 

Ni kwa namna hiyohiyo imetumiwa kwa nyoka wenye sumu kali walioandikwa kwenye Hesabu 21:6,9. Wametakwa kama nachashim maserafi. Nyoka wakali waliitwa hivyo kwa sababu ya muwako wa hisia kutoka kwenye majeruhi waliyoumwa, lakini inawezekana kuwa huenda pia walielekezwa na malaika wakati Waisraeli walipowanenea Musa na Mungu maneno mabaya wakiwanung’unikia kwa kuwaleta kangwani. Neno sarafi maana yake ni kuwaka. Serafi aliyeandikwa kwenye Isaya 6:2 waliitwa mwenye kuwaka. Kwa hiyo, malaika hawa walikuwa wakali au mwenye haiba ya ukali na wa shaba ing’aayo.

 

Nyoka wa zamani (2Wakorintho 11:3) anajigeuza kama malaika wa nuru (2Wakorintho 11:14). Kwa hiyo nyoka anatumika kama mfano wa Shetani aliyeongea na mwanamke na kumdanganya yeye Hawa.

 

Nyuka huhu au kerubi mwenye mbawa zifunikazo alisemekana kuwa alikuwa mwerevu (maana yake nyingine ni mlaghai au mjanja) kuliko hayawani wote wa kondeni. Kuna kitu kuhusu usemi huu kinachoonekana cha tofauti kidogo. Tunajua kwamba nyoka ni kiwakilisho cha Shetani, Kerubi mpakwa mafuta na mwenye mabawa yafunikayo. Tunaambiwa kwenye Ezekieli kuhusu hekima yake.

 

Ezekieli 28:12-15 Mwanadamu, umfanyie maombolezo mfalme wa Tiro, umwambie, Bwana MUNGU asema hivi; Wewe wakitia muhuri kipimo, umejaa hekima, na ukamilifu wa uzuri. 13 Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari. 14 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako.

 

Huyu mfalme wa Tiro aliyetajwa hapa ni jina lingine la fumbo la Shetani. Ilikuwa ni yeye aliyekuwa pale Bustanini Edeni, ambaye alikuwa mkamilifu tangu siku ya kuumbwa kwake hadi uovu ulipoonekana ndani yake. Kerubi huyu mwenye mbawa zifunikazo alizingirwa na idadi ya wengi, na hekima nyingi. Kutokana na hili kulionekana maneno yasiyo na maana na yakipumbavu kulinganisha hekima yake na ile ya hayawani wa kondeni, kama usemi huu wa wamyama wa kondeni inapaswa ichukuliwe moja kwa moja kuwa ni wanyama. Ufafanuzi wa hapa ni kwamba wanyama hawa wengine wa kondeni wanahusiana na viumbe wengine wa kiroho walioasi pamoja na Shetani. Tutaona baadae jinsi wanama hawa wa kondeni wanavyohusiana na wanyama wa kwenye viabu vya Ufunuo na Danieli. Aina hii ya mifano inaonekana pia inapotajwa miti ya bustanini (soma jarida la Lusifa: Mpeleka Nuru na Nyota ya Asubuhi (Na. 223) [Lucifer: Light Bearer and Morning Star (No. 223)]. Kutoka kwenye Ezekieli 31 tunaona kwamba Farao na Waashuru wanafananishwa na miti.

 

Ezekieli 31:2-18 Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri, na jamii ya watu wake, Je! Umefanana na nani katika ukuu wako? 3 Tazama, Mwashuri alikuwa mwerezi katika Lebanoni, wenye matawi mazuri, na kifuniko chenye uvuli, na kimo kirefu; na kilele chake kilikuwa kati ya matawi mapana. 4 Maji yalimlisha, vilindi vilimsitawisha; mito yake ilipita pande zote za miche yake; naye akapeleka mifereji yake kwa miti yote ya kondeni. 5 Basi kimo chake kilitukuzwa kuliko miti yote ya kondeni, na vitanzu vyake viliongezeka; matawi yake yakawa marefu, kwa sababu ya maji mengi, alipoyachipuza. 6 Ndege wote wa angani walifanya vioto vyao katika vitanzu vyake, na chini ya matawi yake wanyama wote wa kondeni walizaa watoto wao, na chini ya uvuli wake mataifa makuu yote walikaa. 7 Basi hivyo alikuwa mzuri katika ukuu wake, katika urefu wa matawi yake; maana mizizi yake ilikuwa karibu na maji mengi. 8 Mierezi ya bustani ya Mungu haikuweza kumficha; misunobari haikuwa kama vitanzu vyake, na miamori haikuwa kama matawi yake, wala bustanini mwa Mungu hamkuwa na mti wo wote uliofanana naye kwa uzuri. 9 Nalimfanya kuwa mzuri kwa wingi wa matawi yake; hata miti yote ya Adeni, iliyokuwa ndani ya bustani ya Mungu, ilimwonea wivu. 10 Basi Bwana MUNGU asema hivi; kwa kuwa umetukuzwa kimo chako, naye ameweka kilele chake kati ya mawingu, na moyo wake umeinuka kwa urefu wake; 11 mimi nitamtia katika mikono yake aliye mkuu kati ya mataifa; naye atamtenda mambo; nimemfukuza kwa sababu ya uovu wake. 12 Na wageni, watu wa mataifa watishao, wamemkatilia mbali na kumwacha; juu ya milima na katika mabonde yote matawi yake yameanguka, na vitanzu vyake vimevunjika karibu na mifereji yote ya nchi; na watu wote wa dunia wameshuka, wakitoka katika uvuli wake na kumwacha. 13 Juu ya magofu yake ndege wote wa angani watakaa, na wanyama wote wa jangwani watakuwa juu ya matawi yake; 14 kusudi mti wo wote, ulio karibu na maji, usijitukuze kwa sababu ya kimo chake, wala usitie kilele chake kati ya mawingu, wala mashujaa wake wasisimame katika kimo chao kirefu, naam, wote wanywao maji; maana wote wametolewa wafe, waende pande za chini za nchi, kati ya wanadamu, pamoja nao washukao shimoni. 15 Bwana MUNGU asema hivi, Katika siku ile alipotelemka mpaka kuzimu naliamuru matanga, nalikifunika kilindi kwa ajili yake, nikiizuia mito yake, nayo maji makuu yalizuiwa; naliamuru Lebanoni kumwombolezea, na miti yote ya kondeni ilizimia kwa ajili yake. 16 Niliwatetemesha mataifa kwa mshindo wa kuanguka kwake, hapo nilipomtupa chini mpaka kuzimu, pamoja nao washukao shimoni; na miti yote ya Adeni, miti iliyo miteule na iliyo mizuri ya Lebanoni, yote inywayo maji, ilifarijika pande za chini za nchi. 17 Hao nao walitelemka kuzimuni pamoja naye kwa watu waliouawa kwa upanga; naam, wale waliokuwa mkono wake, waliokaa chini ya uvuli wake kati ya mataifa. 18 Umefanana na nani, hivi katika utukufu na ukuu, kati ya miti ya Adeni? Lakini utashushwa pamoja na miti ya Adeni, hata pande za chini za nchi; utalala kati ya hao wasiotahiriwa; pamoja na hao waliouawa kwa upanga. Huyu ndiye Farao, na jamii yote ya watu wake, asema Bwana MUNGU.

 

Miti hii na wanyama wa kondeni ina maana ya kiroho, iliyoelezewa kwa kina kwenye jarida la Kuanguka Kwa Misri (Na. 36) [The Fall of Egypt (No. 36)]. Aina hii ya mifano inaonekana kwa kupitia Biblia na inafunuliwa kwa watumishi wa Mungu katika siku hizi za mwisho (Danieli 12:9-10). Mawazo haya sio rahisi kuelewa na hayajafunuliwa hadi mtu apite kipengele kimoja hadi kingine, mstari hadi mstari. Mtu anaweza pia kuona muunganiko hapa kati wanyama wa kondeni na Malaika waovu wsalioanguka kwa matendo ya Masihi.

 

Mathayo 8:28-32 Naye alipofika ng'ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. 29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu? 30 Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha. 31 Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe. 32 Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini.

 

Marko 5:1-13 Wakafika ng'ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. 2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; 3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; 4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda. 5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe. 6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia; 7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese. 8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu. 9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi. 10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile. 11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha. 12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao. 13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini.

 

Mara nyingi Yesu Kristo ametajwa kama pepo aliyetupwa nje ya watu. Je, ni wapi alipelekwa wapi? Waliamriwa wakawaingie nguruwe, wanyama wa kondeni, ambao hatimaye waliingia na kutumbukia majini na wakafa. Maji yale ambayo ni wanyama asilia walikoenda kufananishwa na maji ya roho, ambao watachukuliana na kuwaangamiza Malaika walioasi, sawa na kama maji ya Bahari ya Shamu yalivyowlifunika na kuliangamiza jeshi la Wamisri. Yesu Kristo kwa kweli alikuwa anatoa unabii ya kile ambacho hatimaye kingetokea na kuwapata Malaika hawa walioasi. Kwa kuwakomesha mapepo (wanyama wa kondeni wa kiroho) kwa kuwaamuru waingie kwa nguruwe (wanyama asilia wa kondeni) Masihi alikuwa anaonyesha kuwa maangamizo yangewafuatia Shetani na mapepo zake. Kwa hiyo, ni uweza wa Masihi alioruzukiwa na Mungu, kuwakomesha Malaika hawa waasi kwa kuwaamuru waende na kuwaingia wanyama na kuwaua majini, sawa na kama mtu wa kale anapokufa kwenye maji ya ubatizo na kupewa upya wa uzima. Malaika waasi watapewa pia fursa ya ubatizo kubatizwa na kuufikia uzima mpya. Waasi wataangamizwa na kukomeshwa kabisa na wale wanaohusika watashushwa chini hadi shimoni, na watakuwa ni viumbe wanaoonekana, na kwa kuyubu kwao na kubatizwa kwenye maji ya Roho Mtakatifu watarudishwa kwenye upya wa uzima kupitia kwa Masihi kwa nguvu za Roho Mtakatifu.hii ndiyo kile kinachojulikana hapa kuwa ni kukemea mapepo. Dhana hi inaonekana pia kwenye kitabu cha Waamuzi wakati Samsoni alipochukua asali kutoka kwenye mzoga wa simba ambaye alimuua hapo kwanza.

Waamuzi 14:5-11 5 Ndipo Samsoni na baba yake na mama yake wakatelemkia Timna, wakafika mashamba ya mizabibu huko Timna; na tazama, mwana-simba akamngurumia. 6 Roho ya Bwana ikamjilia kwa nguvu, naye akampasua kana kwamba anampasua mwana-mbuzi, wala hakuwa na kitu cho chote mkononi mwake; lakini hakuwaambia baba yake na mama yake aliyoyafanya. 7 Basi akatelemka na kuzungumza na huyo mwanamke; naye akampendeza Samsoni sana. 8 Kisha baadaye akarudi ili kumtwaa, naye akageuka kando kuuangalia mzoga wa huyo simba; na tazama, nyuki wengi walikuwamo ndani ya mzoga wa simba, na asali. 9 Akatwaa asali mikononi mwake akaenda mbele, huku akila alipokuwa akienenda, akawafikilia babaye na mamaye, akawapa, nao wakala; lakini hakuwaambia ya kuwa ameitwaa hiyo asali katika mzoga wa simba. 10 Basi babaye akamtelemkia huyo mwanamke; Samsoni naye akafanya karamu huko; kwa kuwa vijana ndivyo walivyokuwa wakifanya. 11 Basi ikawa hapo walipomwona, wakamletea wenziwe thelathini, wawe pamoja naye.

 

Marafiki au washirika thelathini ni mfano wa baraza la ndani la Malaika. Kitendo cha kurina asali kutoka kwenye mzoga wa simba kunamaanisha hali ya kusafisha na kukila kitu ambacho ni najisi na kisichoweza kujisafisha chenyewe.

 

Hapa tuna mifano miwili na yote inamuashiria Masihi akishughulika na kitu safi (soma marida la Samsoni na Waamuzi (Na. 73) [Samson and the Judges (No. 73)].

 

Na turudi nyuma kwenye dhana ya kuhusu mnyama. Neno mnyam lililotumika kwenye Mwanzo 3:1 ni la Kiebrania ambal ni chay {khah'-ee} kwa mujibu wa kamusi ya Strong’s Hebrew Dictionary #2416. Neno hili linatumika kama ifuatavyo kwenye tafsiri ya King James Version: ishi 197, ihai 144, mnyama 76, kuwa hai 31, kiumbe 15, kukimbia 7, kitu chene uhai 6, tepetepe 6, misc 19.

 

Kwa hiyo, inamaana, zaidi ya kile tunachokitaja kuwa ni mnyama. Nyoka (au nachash) alilaaniwa zaidi kuliko hayawani wote wa kondeni. Hayawani wa kondeni walilaaniwa pia, lakini nyoka ilibidi alaaniwe zaidi kuliko hayawani wengine wote waliokuwepo.

 

Mwanzo 3:14 14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;

 

Nano kulaaniwa ni la Kiebrania la 'arar {aw-rar'} kwa mujibu wa kamusi ya Strong’s Hebrew Dictionary #0776 lenye maana ya:

1)      Kulaani
1a) (Qal)
1a1) kulaani
1a2) na alaaniwe (kijineno kinachotumika kama laana)
1b) (Niphal) kulaaniwa, laaniwa
1c) (Piel) kulaani, kuwa chini ya laana, kutamka laana kwa ajili ya kitu au mtu
1d) (Hophal) kulaanika, kulaaniwa

 

Inatum ka kwa namna ya kama Mungu kuwalaani wale ambao wanamrudia na kufuata njia zake.

 

Zaburi 119:21 Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako.

 

Yeremia 11:3 ukawaambie, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Na alaaniwe mtu asiyeyasikia maneno ya maagano haya,

 

Malaki 2:2 Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema Bwana wa majeshi, basi nitawapelekeeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.

 

Hebu na turudi kwenye andiko la Mwanzo 1:26, tunaona kwamba mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu (ambaye ni Elohim), na alipata mamlaka ya kutawala kila kitambaacho.

 

Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

 

Hakukuwa na watu wawili kwenye aya hii. Kwanza kabisa, ilikuwa ni kwa namna ya kimwili ukweli kuhusu uumbwaji wa mwanadamu na kwamba alikuwa na uwezo wa kutiisha na kuwatawala hayawani wote walioko duniani. Maana haya yanatambulika sana. Pili, aya hii ilikuwa ni unabii pia wenye maana ya kiroho na utendaji, ambao ni kwamba mtu huyu hatimaye atakuwa na mamlaka wa kuwatawala Malaika walioasi – wanyama wa kiroho wa kondeni. Wakati idadi kamili ya wateule wanakombolewa kutoka duniani na wakifanyika kuwa wafalme na makuhani kwenye ufalme wa Mungu, ndipo hatimaye watatawala hapa duniani pamoja na Kristo.

 

Ufunuo 20:4-6 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.

 

Ni katika kipindi hiki ambapo unabii wa 1Wakorintho utatimilika pia, na Malaika walioasi watahukumiwa na watakatifu (soma jarida la Hukumu ya Mapepo (Na. 20) [The Judgment of the Demons (No. 80)].

 

1Wakorintho 6:2-3 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?

 

Ili kuwa waangalizi au walinzi wa sayari yetu hii na Yesu Kristo na kuanzisha sheria za haki za Mungu, mwenendo wa wateule utatumiwa kama kigezo cha kuwahukumu Malaika walioasi. Hatimaye watakapokuwa wanahukumiwa na kukutwa wakitaka, watashughulikiwa na Mungu. Hii itafanyika kwenye Ufufuo wa Pilo wa wafu. Inawezekana kabisa kuwa hii ingechukua mkondo wake mapema sana iwapo kama Adamu na Hawa wasingeasi na kumfuata Shetani. Hata hivyo, tunajua kwamba uasi wao ulijulikana tangu mwanzoni na Mungu na kwamba yeye alishakuwa na mpango tayari ambao hatimaye ungefanikisha kuhitimisha mapenzi yake, pamoja na yale yaliyotajwa kwenye Mwanzo 1:26.

 

Wakati wa Ufufuo wa Pili wa wafu, Malaika hawa waasi watashushwa chini hadi kuzimu shimoni (Ezekieli 31). Watalazimika kwa shuruti kuwa na miili ya kibinadamu kwa namna sawa tu na kama Masihi alivyojigeuza, na kuuacha mwili wa kimbinguni na kuwepo kwake kule, na kuchukua umbo na hali ya utumwa na mtumishi na kuwa mwanadamu (Wafilipi 2:6-8). Ukweli ni kwamba, Yesu Kristo aliamua kufanya hivyo kwa hiyari yake kwa kumtii Mungu, wakati kwamba Malaika walioasi watashurutishwa kubadilika kwa nguvu za Mungu. Ni katika kipindi hiki ambapo ndipo watajionea mshahara wa dhambi zao za uasi. Katika kipindi hiki watapewa fursa ya kutubu na kusamehewa kwa rehema kubwa na kwa upendo wa Mungu (soma jarida la Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199) [Lost Sheep and the Prodigal Son (No. 199)].

 

Mapenzi haya kwa hakika yanapaswa kufundishwa tena jinsi ya kyafuata na kufundisha sheria za Mungu, sawasawa na zilivyofundishwa na kukaziwa umuhimu wake na \Yesu Kristo na wateule wake. Kwa hiyo jambo la pili kuhusu unabii ulio kwenye Mwanzo 1:26 litatimilika miaka elfu saba tangu kipindi cha Adamu. Ndipo maangamizo ya Malaika walioasi yalikuwa yanawekewa mfano ama ashirio na matenzo au kazi za Masihi aliokuwa anayafukuza mapepo na kuyaamuru yawaingie nguruwe, na kwa Samsoni alipokula asali iliyotoka kwenye mzoga wa simba. Pia tunajionea tena matukio ya kimwili kama yalivyoandikwa kwenye Biblia yakitupa njia ya utimilifu wake wa kiroho.

 

Mnyama

Neno hili la mnyama limeandikwa tena kwenye kitabu cha nabii Danieli sura ya 7. Hapa tunaona kuna wanyama wanne ambao wote wanatokea baharini.

 

Danieli 7:2-7 Danielii akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa. 3 Ndipo wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna mbalimbali. 4 Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu. 5 Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele. 6 Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka. 7 Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.

 

Wanyama hawa wanne tena hawatajwi kwa maana ya viumbe wa kimwili, bali ni viumbe wanaotajwa kwa mfano tu hapa. Tunaambiwa kwenye Danieli 7:17 kwamba wanyama hawa ni wafalme wanne ambao wataiuka na kuwepo duniani. Wanyama wanne hawa habari zo zinafanana na sehemu nne za madini tofauti tofauti za sanamu aliyoiona ndotoni mfalme Nebukadneza kwenye Danieli sura ya 2.

 

Danieli 2:31-45 Wewe, Ee Mfalme, uliona, na tazama, sanamu kubwa sana. Sanamu hii, iliyokuwa kubwa sana, na mwangaza wake mwingi sana, ilisimama mbele yako; na umbo lake lilikuwa lenye kutisha. 32 Na sanamu hii kichwa chake kilikuwa ni cha dhahabu safi; kifua chake na mikono yake ni ya fedha; tumbo lake na viuno vyake ni vya shaba; 33 miguu yake ni ya chuma; na nyayo za miguu yake nusu ya chuma na nusu ya udongo. 34 Nawe ukatazama hata jiwe likachongwa bila kazi ya mikono, nalo jiwe hilo likaipiga sanamu miguu yake, iliyokuwa ya chuma na udongo, likaivunja vipande vipande. 35 Ndipo kile chuma, na ule udongo, na ile shaba, na ile fedha, na ile dhahabu, vilivunjwa vipande vipande pamoja vikawa kama makapi ya viwanja vya kupepetea wakati wa hari; upepo ukavipeperusha hata pasionekane mahali pake; na lile jiwe lililoipiga hiyo sanamu likawa milima mikubwa, likaijaza dunia yote. 36 Hii ndiyo ile ndoto, nasi tutaihubiri tafsiri yake mbele ya mfalme. 37 Wewe, Ee mfalme, u mfalme wa wafalme, na Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, na uwezo, na nguvu, na utukufu; 38 na kila mahali wakaapo wanadamu, wanyama wa kondeni na ndege wa angani amewatia mkononi mwako, naye amekumilikisha juu ya hao wote; wewe u kichwa kile cha dhahabu.39 Na baada ya zamani zako utainuka ufalme mwingine mdogo kuliko wewe; na ufalme mwingine wa tatu wa shaba, utakaoitawala dunia yote. 40 Na ufalme wa nne utakuwa na nguvu mfano wa chuma; kwa maana chuma huvunja vitu vyote na kuvishinda; na kama chuma kisetavyo vitu hivi vyote, ndivyo utakavyovunja-vunja na kuseta. 41 Na kama vile ulivyoziona hizo nyayo za miguu na vidole vyake, kuwa nusu udongo wa mfinyanzi, na nusu chuma, ufalme ule utakuwa ufalme uliogawanyika; lakini ndani yake zitakuwako nguvu za chuma, kama vile ulivyoona kile chuma kimechanganyika na udongo wa matope. 42 Na kama vidole vya zile nyayo vilikuwa nusu chuma na nusu udongo, kadhalika ufalme ule utakuwa nusu yake una nguvu, na nusu yake umevunjika. 43 Na kama vile ulivyokiona kile chuma kimechanganyika na udongo wa matope, watajichanganya nafsi zao kwa mbegu za wanadamu; lakini hawatashikamana, kama vile chuma kisivyoshikamana na udongo. 44 Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele. 45 Na kama vile ulivyoona ya kuwa jiwe lilichongwa mlimani bila kazi ya mikono, na ya kuwa lilivunja-vunja kile chuma, na ile shaba na ule udongo, na ile fedha, na ile dhahabu; basi Mungu aliye mkuu amemjulisha mfalme mambo yatakayokuwa baadaye; na ndoto hii ni ya hakika, na tafsiri yake ni thabiti.

 

Maeneo haya ya sanamu hii, yanajumuisha madini mbalimbali yanayopungua thamani yake kadiri yanavyoshuka kutoka kichwani kwenda chini hadi kwenye vidole, yakimaanisha falme nne ambazo zimetawala hapa duniani, kuanzia kwa yeye mwenyewe Nebkadreza wa Babeli aliwa ndiye kile kichwa na kushuka hadi chini kwenye ufalme wa vidole kumi, ambao utaangamizwa mwishoni mwa zama hizi. Ufalme huu wa mwisho utaangushwa na kuangamizwa kwa jiwe lishukalo toka mbinguni ambalo halikuchongwa kwa mikono ya mwanadamu. Jiwe hili si mwingine ila ni Masihi. Yeye ndiye jiwe kuu la pembeni la Hekalu.

 

Matendo 4:10-12 jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. 11 Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni. 12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

 

Kwa hiyo tuna mnyama wa Ufunuo mwenye vichwa saba na pmbe kumi, na tuna ufalme wa mwisho wa sanamu ya Danieli sura ya pili yenye vidole kumi. Hivi ni vitu viwili vinavyowakilisha wazo moja. Kwa hiyo ni kwamba katika siku za mwisho kabla ya kurudi kwake Masihi na kuja kutawala hapa duniani, kutakuwa na ufalme unaotajwa kama mnyama, na ambao utakuwa na mungano ama utajumuisha wafalme kumi ambao watayatoa mamlaka yao kwa huyu mnyama mmoja ili kumpa nguvu na uweza, na watafanyan hivyo kwa saa moja au wakati mmoja (Ufunuo 17:13). Watawala hawa kumi wanafanana au wanamaana moja na wana kumi wa Hamani walioangikwa kwenye mti uliochongwa ambao habari zao zipo kwenye Kitabu cha Esta (soma jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Esta (Na. 63) [Commentary on Esther (No. 63)]. Waliangikwa wote kwa pamoja kwa kuwa kwa pamoja wanafanya muungano huu wa vidole kumi vya Danieli sura ya 2, na pembe kumi za Ufunuo 13 za katika siku za mwisho.

 

Ufunuo 13:1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.

 

Watafanya vita na Mwanakondoo, lakini Mwanakondoo atawashinde.

 

Ufunuo 17:14: Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu.

 

Wanyama hawa kwa hiyo wanaonekana kuwa kama falme za dunia hii, ambazo zilikuja kuwa na nguvu juu ya watu wote wa duniani hapa. Sehemu muhimu au jambo la msingi linaloonekana kuendena nayo inapatikana kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8.

 

Kumbukumbu la Torati 32:8-9 Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, Alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Israeli. 9 Maana, sehemu ya Bwana ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake.

 

Hapa tunaambiwa kwamba wakati wana wa Adamu walipotawanyika na kupewa urithi wao (hapa ni kwenye mnara wa Babeli) mipaka yao iliwekwa sawasawa na idadi ya wana wa Mungu. Hii inaonekana kwenye tafsiri za RSV, the Septuagint na the Dead Sea Scrolls. Hii ilijulikana vizuri sana kwamba kulikuwa na mataifa sabini pale, na kila moja likiwa chini ya himaya ya kiumbe fulani wa kiroho, mwangalizi, mmoja wa wana wa Mungu. Mojawapo ya mataifa haya lilikuwa ni la Israeli ambalo lilichaguliwa na Yahova. Tunajua kuwa kiumbe huyu ni Mwana wa Mungu aliyefanyika kuwa mwanadamu na aliyekufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, ni yeye ambaye kwa lugha ya Kiingereza anaitwa Jesus Christ, yaani Yesu Kristo  (soma jarida la Malaika ya YHVH (Na. 24) [The Angel of YHVH (No. 24)].

 

Viumbe wa kiroho walio na mamlaka juu ya mataifa walikuwa ni hayawani wa wa kondeni waliotajwa kwenye kitabu cha Mwanzo. Kwa mujibu wa nabii Danieli kulikuwako wanyama wanne waliotabiriwa watainuka na kufanya dola au falme kubwa. Wa mwisho kati ya wanyama hawa wanne atakuwa na atakuwa na vichwa saba na pembe kumi. Vichwa hivi saba vinasemekana kuwa ni milima saba ambayo yule mwanamke (kahaba aliyeandikwa kwenye Ufunuo aliyelewa kwa damu ya watakatifu) anaketi, lakini hawa ni wafalme saba pia. Hii milima saba ni zote mbili zipo kwenye muonekano wa kimwili wa milima ya duniani, lakini pia kwa lugha ya kimafumbo ni kama falme saba au urejesho wa ufalme huohuo kulingana na urefu wa vipindi vya nyakati. Pembe kumi zinawakilisha ia wafalme kumi, ambao watampa nguvu zao na mamlaka yao yote huyu mnyama.

 

Kitu cha muhimu kukumbuka hapa ni sanamu ya Danieli 2. Pale tunaona sanamu moja yenye madini ya namna mbalimbali. Ilikuwa ni moja kumbwa na iliyounganika kikamilifu kwa kila upande ukiwa umeungana na sehemu iliyotangulia kama kuirithi nyuma yake. Kwa hiyo, hizi falme nne hazikuwa ni falme zimetengana kabisa, zikiwa hazina la kusaidiana wala kutegemeana kila mmoja na mwenzake, bali zilikuwa zimeunganishwa zote na kuwa sehemu moja ya mfumo mzima wote. Mfumo huu mmoja ulianzia kwa Wababeloniani, na ukaendelea hadi kwa Wamedi na Waajemi, hadi kwa Wayunani wa Makedonia, na hatimaye utaishia kwa mnyama wa mwisho, ambaye ni Dolan a mfumo wa Kirumi (soma jarida la Dini za Siri Sura ya 1 Kuenea Kwa Imani za Siri za Wababeloniani  (Na.B7 1) [Mysticism Chapter 1 Spreading the Babylonian Mysteries (No. B7_1)].wakati wa Dola hizi, mfumo wa uwongo na potofu wa ibada ulianufaika. Ni kama ilivyoandikwa ma kusemwa kwenye Danieli 7:25, mnyama huyu ataazimu kubadili majira ya sheria. Hivi ndivyo ilivyotokea chini ya mfumo wa mnyama wa Kirumi na mwanamke kahaba uliombeba akiuendesha.

 

Marira au nyakati zilizozibadilishwa ni zile zinazoihusu kalenda. Kalenda inayotumika na iliyomaarufu leo ulimwenguni kote imechukuliwa kama ni kitu cha kawaida tu na kama ni sahihi, lakini ni ishara ya kuibuka au kubuniwa kwa mfumo huu wa Kirumi. Ikaondoa na kuyabadili maelekezo ya Biblia ya siku kuanza jioni wakati wa kuzama jua, bali hii ikawaelekeza watu kuwa siku inaanza usiku wa manane. Ibadadilisha maelekezo ya Biblia ya kwamba mwaka mpya uanze tangia Mwandamo wa Mwezi Mpya ulinaofuatiwa na ikwinoks ya majira ya baridi ili kwamba Pasaka iadhimishwe katika kipindi hiki, lakini mwaka wa hawa unaanzia katikati ya majira ya baridi ya maeneo yaliyo kwenye ncha za kaskazini. Kalenda hii ikabadilisha utaratibu wa Kibiblia wa mianzo ya miezi ijulikane kwa kigezo cha Kuandama kwa Mwezi Mpya kama neno la Mungu linavyosema, lakini miezi ya hawa ikawa inaanza siku yoyote tu pasipo kuzingatia utaratibu huo wa Maandiko Makatatifu, na badala yake miezi yao ikaanzia tu kwa kutegemea na uholela wa idadi ya siku iliyowekwa kwenye mwezi wa kalenda ya Kirumi.

 

Mnyama huhu anasemekana kuwa na mke ambaye ni kahaba aliyempanda juu yake akimuendesha. Neno kahaba limetumika kwenye Agano la Kale kwa kuwataja wateule wa Mungu, yaani Israeli. Ndipo, kama vile Israeli wa kimwili walivyofanya ukahaba na Wamisri na Wababeloni, na ndivyo ilivyo pia kwa Israeli wa Kiroho wanavyofanya ukahaba. Huyu mwanamke kahaba mwenyewe ana jina lililoandikwa kwenye paja la uso wake linalosomeka: BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI. (Ufunuo 17:1-5). Ni rahisi sana kuona sababu ya hili kuwa ndilo la kahaba huyu. Amechapwa mhuri wa Wababelonia kwenye paji la uso wake. Mafundisho yake yanatokana na imani za kale za kifumbo za dini za kale za Wababeloni. Imani na mafundisho mapotofu na ya uwongo Nebukadreza wa Babeli yalitiririka yakishuka kutoka kwenye kichwa cha dhahabu yakashuka chini yakipitia kwenye madini mengine yote yaliyooneshwa kuwa ni dola zilizofuatia kwenye Danieli sura ya 2.

 

Wakati alipoyaingiza na kuyachanganya mafundisho haya ya imani fumbo za Kibabeioni kwenye dini yake mpya inayojiita kuwa ni Ukristo, ndipo kahaba huyu mkuu aliazimu kuibadili Sabato kutoka siku ya saba ya juma iliyoamriwa iadhimishwe kwenye maandiko, akaweka ibada nyingine zilizoadhimishwa siku ya kwanza ya juma. Jambo hili liliwafanya hata wale wanaodai kuwa wanamuabudu Mungu wa Pekee na wa Kweli wapoteze kigezo cha kuwafanya wastahili kutiwa mhuri wa Mungu. Kahaba huyu anayeendesha akiwa amempanda mnyama hakuishia hapa. Alidiriki pia kuzibadilisha sheria ambazo pia ni torati ya Mungu. Aliziunganisha pamoja amri ya Pili ya Mungu na ile ya Kwanza, akazifanya kuwa ni moja, na kisha akaigawanya ile ya Kumi na kuifanya ziwe mbili, ili kuzifanya zionekane zimetimia zote kumi. Alifanya haya yote ili kumruhusu kutamani sanamu wa wapagani na avinyago vya dhahabu na fedha ambazo alijipamba kwazo yeye mwenyewe, sawa na kama Mtume Yohana alivyoonyesha kahaba huyu kwenye maono ya Ufunuo 17:4. Alimkufuru Mungu kwa kuyapotosha mataifa yote aliyoyashinda kwenye vita. Aliyaingiza maovu na mapotovu yote kwenye kile alichokiita Ukristo na akaendelea kuwadanganya wale wote ambao walikuwa hawajaitwa wala kuchaguliwa na Mungu. Kwa kuwalaghai kwake kuwapa thamani ya Ukristo au jina hilo na huku akiwapotosha kwa kuwafanya waendelee na taratibu na imani za mataifa walizozitumia kuabudu na kuitumikia miungu yao, aliupotosha kabisa ulimwengu wa Kikristo. Ikawa watu hawa wanaojiita kuwa Wakristo hawaziadhimishi tena Sikukuu zilizoamriwa na Mungu na kuzichukulia kuwa ni siku takatifu, na badala yake wakaziadhimisha sikukuu na siku za miungu wa kipagani (soma majarida ya Malumbano ya Wakwuartodeciman (Na. 277) na Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235) [The Quartodeciman Disputes (No. 277) and The Origins of Christmas and Easter (No. 235)]. Matokeo mabaya ya hili yalikuwa ni kutoujua tena mpango wa Mungu wa wokovu kwa wanadamu, ambao unajulikana tu kwa kuzijua na kuziadhimisha Sikukuu zake alizotuamuru kutitunza.

 

Shetia za Mungu za ulaji wa vyakula zilipaswa kushikwa na ualaji wa vyakula najisi ulibidi uepukwe (soma jarida la Sheria za Vyakula (Na. 15) [The Food Laws (No. 15)]. Huenda ulaji wa vyakula safi na najisi zina mashiko ya kiroho ambayo yanauhusiano na kuonyesha utii wetu kwa Mungu nwa kwenye Amri na Sheria zake. Ni kama Hawa alivyomfuata Shetani kwa kumsikiliza na kumuasi Mungu na akala tunda kutoka kwenye mti uliokatazwa, na vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa walio kwenye ibada na imani hii wanamfuata Shetani katika kumuasi Mungu na kula vyakula najisi. Vyakula najisi vinamaana sawa tu na ibada najisi. Tunajionea tena mlingano wa wanyama wa kondeni sambamba  na vyakula najisi. Ni kama walivyo wanyama wavkundeni waliopo walivyo safi kuwala na baadhi yao sio safi. Wale walio safi kama Masihi alivyosafi kwa chakula cha kroho. Yeye ni mkate wa kiroho wa uzima. Na hii ndiyo sababu sheria za vyakula ziliwekwa kama kama zilivyokuwa. Na kwa mara nyingine tena, zikaonyeshwa dhahiri kwa kiroho.

 

Mambo haya yote yakuchukiza aliyafanya kahaba huyu kwa nguvu na utukufu, asijue kwama matendo ya kipagani na aina ya ibada ambazo aliziingiza kutoka kwenye imani za mataifa ya kipagani na kuzifanya kuwa kama zake mwenyewe, yalikuwa yanafanyika kwa ushawishi wa miungu hii ya kipagani, Malaika walioasi, amao walikuwa na mamlaka hay ohayo juu ya mataif haya ya kipagani. Badala ya kushika ukamilifu na utakatifu na kuifuata njia nyembamba na iliyopindapinda na kuzishika amri za Mungu, pasipo kuchepuka na kwenda upande wa kuume wala wa kushoto, akajichukulia njia yake mwenyewe.Alifanya ukahaba na wafalme wa dunia, na mamlaka za kiroho za mahali pa juu. Na kama hiyo haikufosha aliwaua na kuwaondolea mbali watakatifu wa kweli wake yeye Mungu, aliye juu kama ilivyotabiriwa kwenye Danieli 7:25. Alipewa mamlaka kwa wakati ,Snakati mbili na nusu wakati. Hii hi miaka 1260 ya kudumu kwake iliyojulikana hapo zamani kama Dola Takatifu ya Kirumi iliyoanzia mwaka 590 BK hadi mwaka 1850 BK. Wakati wa kipindi hiki alilewa kwa damu za watakatifu na mashahidi wa Yesu Kristo (Ufunuo 17:7) (sawa na majarida ya Migawanyo Mikuu ya Makanisa ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na. 122) na Vita vya Waunitarian na Watrinitarian (Na. 268) [General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122) and The Unitarian/Trinitarian Wars (No. 268)]. Isitoshe, aliwafanya wote wakaao duniani walew au aliwalewesha kwa mvinyo wa uasherati wake (Ufunuo 17:2). Mvinyo huu ni mafundisho yake, misingi ya imani yake, na mfumo wake wa ibada na kuabudu, ambazo zote zilichukuliwa kutoka kwenye mitindo ya ibada za miungu ya kipagani.

 

Hatimaye, kahaba huyu alichanganikiwa kwa kuona kuwa wengi wa aliowalevya mvinto wa uasherati wake hawakuendelea kumfuata. Walitafuta njia za kujiondoa kutoka kwake na kujitenga naye. Kwa hiyo, haya makanisa yote ya Kiprotestant ni mabinti wa huyu kahaba aliyetajwa kwenye Ufunuo 17:5. Badala ya kuachana nao mafundisho yake mapotofu ya kizushi na kurudi kwenye njia iliyopindapinda na nyembamba (imani ya kweli iliyofundishwa na Yesu Kristo) hatimaye wakajiunga na kuendelea kuendeshwa na yeye na wakijifanya kuwa wamejitanga na kuachana na matendo yake, na huku wakiendelea kuyashika karibu mafundisho yake yote na wakiwa na kiu cha kunywa damu ya watakatifu kama afanyavyo yeye. Walianza kumuabudu Mungu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu (Mathayo 15:9).

 

Kwa hiyo, mnyama wa mwisho wa Danieli na Ufunuo kwa kipidi cha miaka 1260 likuwa akiendeshwa akiwa amepandwa juu na huyu kahaba. Alibadili sheria na nyakati au majira kiasi cha kwamba dunia yote ilidanganyika. Mfumo wa mwisho utakuwa ni tofauti sana kutoka kwenye mfumo wa ufalme wa Mungu na kwamba utakuwa wa tofauti na vigumu saba kwa watu wa Mungu kutoka nje ya yeye na kumuacha kama walivyoamriwa kufanya hivyo (Ufunuo 18:4). Ili kutoka nje na kuachana naye inambidi mtu kufuata mfumo ambao umepingwa sana hapa duniani na mfumo au imani ya mnyama. Inampasa mtu kuzishika siku za maadhimisho ya Sikukuu zilizoamriwa na Mungu, na siyo sikukuu za kipagani zilizowekwa kwa heshima ya miungu wa kipagani. Kwa hiyo, ni uamuzi wa mtu, aidha kutiwa mhuri wa Mungu kwa kuzishika na kuziadhimisha amri zake na Siku zake Takatifu, au kupigwa chapa ya mnyama kwa kuzifuata amri zake na sikukuu za kipagani. Mwishoni kulikuwa na kipindi cha mateso wakati wa Mhuri wa Tano wa Ufunuo. Hii ilikuwa ni Mauji Makubwa ya Kuangamiza Wayahudi na waamini Sabato huko Ulaya yaliyopewa jina la  Holocaust yaliyofanyika katika karne ya 20 na yataendelea hata kwenye karne hii ya 21 na hatmaye tutashuhudia kuuawa au kuangamizwa kwa yule mwanamke kahaba ambaye ataangamizwa na yule mnyama mwenyewe (soma jarida la Ujumbe wa Ufunuo 14 (Na. 270) [The Messages of Revelation 14 (No. 270)].

 

Kipindi hiki itakuwa vigumu kumudu kununua au kuuza bila kuwa na alama ya mnyama. Na kwa watu wengi, ni vigumu sana kutofanya kazi au kufunga biashara siku za Sabato, Miandamo ya Mwezi, katika Siku Takatifu za Mungu, na kubakia na ajira yenye manufaa makubwa. Hata hivyo, wakati umewadia na unakuja upesi ambao ni kama inavyosema Ufunuo 13:17, kwamba hakuna mtu atakayeweza kununua au kuuza asipokuwa na alama hii ya mnyama. Ambavyo kwamba, mtu asipokuwa tayari kufanyakazi siku za Sabato, Miandamo ya Mwezi na Siku Takatifu zilizoamriwa na Mungu, mtu hataweza kubakia na ajira yake au na shughuli ama biashara yake. Kwa mambo haya yote muhimu yanayoendana na maisha ya kisasa, kama vile kodi ya serikali, pango ya nyumba, huduma za bima, nk, itakuwa ni vigumu kubakia bado umetiwa mhuri wa Mungu na huku ukiendana sambamba kufanikisha mambo yako kwenye mfumo huu utakaowekwa na huyu mnyama.

 

Je, alama hii ya mnyama itakuwa ni kitu kinachoonekana wazi kama vile kimelea cha compyuta itakayoingzwa miilini mwa watu. Huenda inweza kuja kwa njia hiyo, lakini hii itakuwa ni alama inayoonekana wazi tu. Alama yenyewe hasa ni ya kiroho ambayo watu wanagongwa na kuwanayo hata sasa na wanakuwanayo asipo hata wenyewe kujijua! Kwa hiyo, wakati watu wengi wanapoogopa na kujiwekea tahadhari wakidhania kuwa huenda kutakuwa na siku moja watalazimika kupokea alama hii ya mnyaka kwa namna iliyo wazi na kama kitu kinayoonekana wazi wakitiwa kwenye vipaji vya nyuso zao au mikononi mwao, watakuwa wameikwisha tiwa alama hii kiroho kwenye vipaji vya nyuso zao na mikononi mwao. Hivi ndivyo Ufunuo 12:9 inavyosema: “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.” Joka huyu mkubwa kwa kweli anaudanganya ulimwengu wote, hata na wale wanaojiwekea tahadhari kubwa kutopenda kuipokea alama hii ya mnyama.

 

Tarakimu ya Mnyama

Chanzo kingine kilichopelekea kutolewa kwa nabii za uwongo kwa miaka mingi kinahusu tarakimu ya mnyama. Tunaambiwa kwene Ufunuo 13:18 kwamba Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita (666). Inaeleweka vyema na,imeandikwa vizuri kwamba tarakimu hii ya 666 inahusiana na imani za kidini na mifumo ya Kibabeli. Alama ya mungu Isis ni SSS ambayo ina tarakimu inayofanana na hii ya 666’ alama hii imekuwa ikitumiwa kama ishara au alama ya dini za waabudu jua tangu zama za Wababeloni hadi sasa. Makuhani wa zamani wa Kibabeloni waliigawana mbingu kwa vilimia/thelathini na sita. Inajulikana kwamba hesabu ya tarakimu ya kwanza ya thelathini na sita ni 666. Makuhani wa kipagani walikuwa na namna ya kuiwakilisha au kuitumia migawanyo ya tarakimu thelathini na sita kwa kuzipangilia kila moja ya fungu la idadi ya thelathini kwenye meza yenye mistari sita kwa mafundu sita, ambazo walizitunda kwenye tasbihi au kamba maalumu ambazo walizivaa shingoni mwao. Kila mstari na kila fungu pamoja na kila mzingo ziliongezwa haki kufikia 111. Idadi ya mistari yote na mafungu yote kwa hiyo ilikuwa ni 666. Kwa hiyo, tunaona kwamba makuhani hawa wa zamani wa kipagani sio tu kuwa walikuwa wanaijua tarakimu hii bali pia waliitumia kama sehemu ya elimu yao wa mambo ya nyota na kama chombo cha kufanyia ubashiri na ulozi. Elimu ya nyota na anga pamoja na ubashiri au ulozi ni sehemu ya imani na mifumo ya Wababeloni.

 

Ufunuo 13:8 inasema kwamba tarakimu hii ya 666 sio tu kuwa ni ya mnyama, bali hii pia ni hesabu au tarakimu ya kibinadamu. Maelezo ya jinsi ya kuliewa jambo hili yametolewa na nabii Isaya.

 

Isaya 14:4-17 utatunga mithali hii juu ya mfalme wa Babeli, na kusema, Jinsi alivyokoma mwenye kuonea; Jinsi ulivyokoma mji ule wenye jeuri! 5 Bwana amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala. 6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu. 7 Dunia yote inastarehe na kutulia; Hata huanzilisha kuimba. 8 Naam, misunobari inakufurahia, Na mierezi ya Lebanoni, ikisema, Tokea wakati ulipolazwa chini wewe, Hapana mkata miti aliyetujia. 9 Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako, Ili kukulaki utakapokuja; Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako, Naam, walio wakuu wote wa dunia; Huwainua wafalme wote wa mataifa, Watoke katika viti vyao vya enzi. 10 Hao wote watajibu na kukuambia, Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi! 11 Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika. 12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. 16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?

 

Aya elekezi ili kuelewa jambo hili ni ile ya kumi na sita inayosema: " Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme". Kwa kweli, Shetani atatazamwa kama ni mtu aliyeifanya dunia itetemeke. Yeye alikuwa ni Kerubi kwenye mabawa yafunikayo anayeonekana kwenye dini za kipagani kwa umbo la mtu mwenye vichwa vinne (soma jarida la Serikali ya Mungu (Na. 174) [The Government of God (No. 174)]. Kushushwa huku kwa Shetani kutafanyika mwishoni mwa kipindi cha Milenia kwenye Ufufuo wa Pili wa wafu (aya ya 9).

 

Ilikuwa ni Shetani aliyekuwa kiongozi au Malaika Mkuu anayeonekana akionyeshwa kwa umbo la mtu asiye na kichwa au aliyeondolewa kichwa chake kwenye dini hizi potofu aliyeanguka kutoka kwenye neema na kutoka mbinguni. Yeye ndiye yule mtu ambaye tarakimu yake ni 666. Tarakimu hii imekuwa ikitumika na kuwekwa au kujumuishwa kwenye falme zote za ulimwenguni ikiwa imeanzia huko Babeli.

 

Wakati kukiwa hakuna shaka kuwa tarakimu hii 666 kuwa inahusika na harakati za dini za siri za kishetani, kuna tarakimu nyingine iliyoandikwa kwenye moja ya maandiko yaliyopendwa sana ya maandiko ya zamani ambayo ilitumika kama mbadala wa hii namba 666. Kama alivyosema Del Washburn kwenye kitabu chake Theomatics II ukurasa wa 500, “kwenye kitabu kilichochapishwa mjini London mwaka 1932, na kupewa kichwa cha jina Kitabu Cha Ufunuo, Chanzo cha Chimbuko la Ukristo [The Book of Revelation, A Key to Christian Origins], maelezo haya ya chini kwa kitabu ya ufafanuzi yanayoonesha kuendelea kwa maasi yanaonekana yakisema hivi.

 

Tarakimu ya 616 imetolewa kwenye moja ya maandiko mawili mazuri sana. C (Codex Ephraemi Rescriptus, Paris), na toleo la Kilatini la Tyconius (DCXVI. ed. Souter kwenye Jarida la Theo., SE la Aprili, 1913), na kwenye toleo la zamani la Kimarekani la (ed. Conybeare, 1907). Irenaeus alilijua hili [ masomo ya mwaka 616], lakini hakuchukuliana nayo wala kuiiga (Haer. v, 30,3); Jerome aliiiga na kuichukua (De Monogramm, ed. Dom G. Morin ya Rev. Benedictine, 1903) huenda ni ya kihalisia. Tarakimu hii ya 666 imewekwa mbadala wa tarakimu ya 616 na huenda kwa kuilinganisha na tarakimu nyingine ya 888, namba ya Yesu (Deissmann), au kwakuwa ina umbo la mzingo, tarakimu ya 36 za kwanza (1+2+3+4+5+6...+36=666).”

 

Huenda kunawezakuwa na umuhimu hapa kuangalia kichwa cha maneno cha Kitheomatikia. Theomatikia imefafanuliwa na Washburn kuwa ni tarakimu au hesabu za Mungu. Ni sawasawa tu na Gematria, lakini haishabihiani na hii. Theomatics ni elimu ya jinsi wazo linavyoendana au kushabihiana kwenye Biblia, iwe kwenye Kiebrania au Kiyunani, linapotokea kwenye uandishi kwa namna ambayo thamani ya herufi ya maneno yaliyo kwenye dhana maalumu yanaongezeka hadi kwenye nambari fulani au kwa kuizidiaha namba ile. Kwa mfano, kuna idadi kadhaa ya majina ya Shetani kwenye lugha zote mbili, Kiebrania na Kiyunani ambayo yote yanahitimika kwenye tarakimu ya 276. Muonekano huu halingani kila mara, bali unashikamana na tarakimu iliyoko ndani ya kiwango cha nyongeza au kupunguza au kutoa mbili. Kwene kitabu hiki, Washburn aliweza kuonysha kwa ushawishi mkubwa sana (na kwa mujibu wa kanuni zilizoanzishwa za kisayansi za kusawazjsha) kwamba miunganiko hii ya neno na kifungu hulinganishwa hapo kwa mtindo au mwonekano, na isingeweza kufanywa kwa kutokea tu bahati njema.

 

Sasa basi, kama tukiichukua tarakimu ya 616 kuwa ni namba ya mnyama, basi tutaona uwepo wa vifungu vingi na maneno kutoka kwenye maagano yote mawili, yaani la Kale na Jipya ambavyo vitakuwa na thamani ya kitheomatiki iliyosawa na namba 616 au namba 616 nyingi. Hapa kuna baadhi ya vifungu vinavyoonyesha thamani ya kitheomatiki ya namba 616:

Mwanzo 1:25 aliumba hayawani wa duniani baada ya aina zake; Mwanzo 1:26 aliumba kila kiumbe kitambacho juu ya nchi; Mwanzo 1:28 akatawale kila kiumbe kilicho hai na kitambaacho; Mwanzo 2:19 kutoka katika nchi kila hayawani; Mwanzo 3:1 wanyama wa kondeni ambao; 2Wakorintho 11:3 inasema isijekuwa kwa namna fulani kama nyoka alivyodanganya; 2Wakorintho 11:3 akashawishika au kudanganyika; 1Timotheo 2:14 kudanganyika; Ufunuo 17:1 kabaha mkuu aketiye juu yake; 1Wakorintho 6:16 kahaba; Ufunuo 17:5 Babeli ya siri na machukizo ya nchi; Mathayo 10:15 kila Sodoma na Gomora; Ufunuo 18:4 kushiritiki dhambi zake; Ufunuo 17:17 kila moja ya zifuatazo mnyama, kahaba, uovu (udhaifu au uchafuko); Mwanzo 3:14 ulimlaani mnyama; Ezekieli 28:14 kerubi mpakwa mafuta; Mambo ya Walawi 11:41 kila kiumbe atambaaye; Marko 1:23 unajisi; Warumi 1:23 wanyama na watambaao; Mathayo 6:32 giza; Yohana 3:6 wenye mwili; Danieli 7:17 wanyama wakubwa; Luka 16:8 kwa wana wa kizazi hiki; Waesfeso 5:6 kwa wana watiio; Mathayo 13:38 magugu ni wana.

 

Kuna linaloshangaza kwa namna yoyote ile kusikia kwama mpakwa mafuta huhu ambaye pia ni Kerubi mwenye mabaya yafunikayo, joka, anashirikiana na mnyama, pamoja na giza, na kahaba, na uwongo, na Babeli ya Siri, pamoja na Sodoma na Gomora na nyingine, na wengine, na wengine? Kutoka kwenye mirejesho yote hii tunaweza kuona dalili za kiroho. Tunajua kuwa Shetani ni mfalme wa nguvu za anga. Tunajua pia kwamba ameudanganya ulimwengu wote. Tunajua pia kwamba matukio yaliyotokea kwenye Agano la Kale ni mafundisho kwetu na tuyapambanue au tuyachuje. Ni kwa kuyajua mambo haya tu mdipo tunaweza kuona jinsi ulimwengu mzima wote ulivyodangwanywa. Matukio halisi ambayo sio ya kiroho ya Agano la Kale yalifanyika ili kuwapa jinsi ya kutimilika kwake kiroho kwenye Agano Jipya. Mfano mmojawapo kuhusu hili ni Pasaka. Damu halisia iliyokuwa inamwagika ya Mwanakondoo wa Pasaka ambayo iliwalinda Israeli kutoka kwa Malaika wa kifo ilikuwa ni mfano tu uliokuwa unaashiria damu ya Masihi ambayo itawaokoa wateule kutokana na mauti ya pili. Tunajonea hayo pia tunapofananisha matukio ya kimwili ya kitabu cha Mwanzo na utilifu wake kwenye Ufunuo. Nyoka aliyemdanganya Hawa kwenye Mwanzo ni mnyama yuleyule anayemdanganya huyu mwanamke kahaba na ulimwengu wote kama tunavyoona kwenye kitabu cha Ufunuo. Ni kama alivyodanganyika Hawa hadi akala tunda la mti uliokatazwa kwa ulaghai wake na hekima yake potofu na kwa ujanja wake, na ndivyo anavyomdanganya huyu kahaba kwa kupitia mbinu hizihizi kama zilivyoelezewa na na falme za mnyama. Ni kwa dini za kimafumbo na kisirisiri za Wababeloni, kama zilivyoingizwa na kushirikishwa kwenye falme zote za ulimwenguni za huyu mnyama, na ndivyo pia Kanisa lilivyorubuniwa ili limfuate nyoka. Ni kama mwanamke Hawa alivyoumbwa kutokana na Adamu, mwanadamu wa kwanza, na akadanganywa na nyoka, na ndivyo ilivyo kwa mwanamke huyu ambaye ni Kanisa alivyochukuliwa na taifa ambalo lilikuwa ni mzaliwa wa kwanza wa Mungu, taifa la Israeli, na likadanganywa ya nyoka huyuhuyu. Ni kama vile Hawa alivyokula tunda kutoka kwenye mti uliokatazwa kinyume na mapenzi ya Mungu waliyoelekezwa, na ndivyo alivyofanya pia huyu kahaba, anakula chakula cha kiroho kilichokatazwa ambacho ni vyakula na wanyama waliokatazwa, na na kushiriki matendo yaliyokatazwa na kuiabudu miungu ya uwongo, vitendo ambavyo vinapingana moja kwa moja na mapenzi ya Mungu. Ni kama Hawa alivyomsababishia Adamu kutenda dhambi, na ndivyo alivyofanya kahaba huyu, anamsababishia mwanadamu kutenda dhambi kwa kuzifuata njia za kahaba huyu. Na ni kama masalio walivyoondolewa nje ya uzao wa Hawa na kutengwa mbali wakiwa kama wateule wake Mungu, na ndivyo ilivyo kwamba kuna masalio waliotolewa watoke nje mfumo wa imani na dini ya huyu mnyama ambao unaongozwa na huyu kahaba, na wametengwa na kuwekwa mbali wakiwa kama ni watu wateule wake Mungu.

 

Huyu joka amejaribu kwa jitihada kubwa kuwadanganya na kuwapotosha wanadamu tangu mwanzo na kuwaondoleambali wale alioshindwa kuwadanganya. Amejaribu kwa namna zake zote alizoweza kuwaangamiza wanadamu na kuwaweka mbali kutoka kwenye makusudi na lengo alilowawekea Mungu wao. Kwa ni jambo kubwa somo hilo kuliendeleza kwenye jarida hili, lakini na tutoe mifano michache ya majaribio yaliyofanywa ya mapenzi na nia za Shetani inayotosha kuonyesha jinsi alivyojaribu kubadilisha unabii wa kuangamia kwake uliotolewa kwenye Mwanzo 1:26, na Mwanzo 3:6.

 

Kumdanganya Hawa lilikuwa ni jaribio lake la kwanza. Na huenda hakuonambali asijue kwamba Mungu tayari alishaandaa mpango wa kuwakomboa wanadamu kutoka kwenye mshahara wa dhambi zao, au huenda alidhania kuwa angefanikiwa kuutokomeza mpango huo. Jaribio la pili ni lile la Abeli (ambaye sadaka yake ilikuwaliwa na Mungu) aliyeuawa na ndugu yake Kaini ambaye sadaka yake haikukubaliwa. Hadithi hii pekeyake inamlinganisho kati ya wana wawili wa Mungu, Yesu Kristo  (au Yahova Elohim) na Shetani. Kwa kuwa ilikuwa ni sadaka ya Yesu Kristo kama Mwanakondoo wa Mungu ambayo ndiyo inakubalika na Mungu. Shetani hakuandaliwa kuyatoa maisha yake kwa kutoa sadaka. Kwa hiyo, ni kama vile Kaini alivyomuua ndugu yake Abeli, ndivyo Shetani alivyomuua Kristo. Katika kipindi cha Nuhu wengi waliotokana na uzao wa kinasaba ya wanadamu walijiingiza na kujichanganya na Wana wa Mungu wakichanganya damu na binti za wana wa wanadamu (Mwanzo 6:4) kwa kiasi kwamba ni Nuhu peke yake ndiye alikuwa ndiye mkamilifu kwenye kizazi hiki chote, na hii inamaanisha katika mchanganyo wa kinasaba. Na hii ndiyo sababu iliyompelekea Mungu kuingamiza dunia yote kwa gharika ya mvua ili kwamba Nuhu tu na familia yake waendelee kuijaza Dunia wakiwa na mbegu isiyochanganyika. Katika kipindi cha Kanisa, baada ya kujaribu baada ya kujaribu tena na tena kwa kipindi cha takriban miaka 4,000 kuwaangamiza wateule wake Mungu, ndipo sasa anawafuatia masalia ya yule mwanamke wa Ufunuo 12:6. Anamtumia mwanamke kahaba wa imani kongwe ya Kikristo ili kuwafuatilia kwa mfululizo na kuwakomesha pasipo huruma au kwa ukatili mkubwa mawasali wale wachache waliobakia ambao ni Ekklesia au Kanisa la kweli, ambao wangali bado wakizishika amri za Mungu na Ushuhuda wa Kristo.

 

Kwa hiyo, hebu na turudi nyuma hadi kwenye wazo letu la tarakimu ya 666 ambayo Shetani mwenyewe aleigonga kwenye falme zake mwenyewe, na namba 616, ambayo kama ikichukuliwa kitheomatiki inaonekana kumuonyesha moja kwa moja Shetani na udanganyifu wake kwa wanadamu. Huenda tarakimu zote mbili zinauhusiano na mnyama, moja ni ile ambayo Shetani mwenyewe anapenda itumike na nyingine ni inayotuama kwenye tarakimu za kitheomatiki za Maandiko Matakatifu na ambayo inamlenga moja kwa moja Shetani akwa kama mnyama wa kiroho anayeziongoza falme za huyu mnyama wa duniani. Cha kufurahisha zaidi kutokana na tarakimu hizi za gematria ni kwamba, namba 666 inapungua hadi tisa na namba 616 hadi nne (soma jarida la Maana ya Namba au Tarakimu (Na. 7) [Symbolism of Numbers (No. 7)]. Namba Nne inawakilisha kazi ya uumbaji na inahusu uumbaji wa dunia na vitu vilivyoumbwa ndani yake. Namba Sita inaaminika kuwa ni namba ya Kibinadamu. Mwanadamu aliumbwa siku ya sita. Matumizi ya tarakimu hii na uwingi au uzidishaji wake wote umehusiana na uumbaji na ni matokeo ya kazi ya mwanadamu na mfumo wa uumbaji. Namba Tisa ni namba ya ukamilifu au hitimisho la mchakato wa hukumu. Ni 3x3 na huu ni ukamilifu wa muundo  wa harakati. Tarakimu hii inakutikana kwenye mambo yote yahusuyo hukumu. Namba tatu inamaanisha ukamilisho kwa maana ya mistari mitatu ya alama. Siku ya Tatu ilikamilisha mambo ya msingi wa uumbaji. Kwa hiyo, inonekana kwamba, kwa kujumuisha namba 666 na mfumo wake wa dini yake ya uwongo, Hsetani anajaribu kumtoa mwanadamu (6) na kwa kukamilisha mfumo wake wa dini ya uwongo (3) akiwapeleka wanadamu wote hukumuni (9) kwa kiasi kwamba watashindwa hukumu ile na wasiweze kumuweka mbadala wake na wale waliomuasi. Hata hivyo, tunajua kwamba Yesu Kristo hatashindwa, na ndipo kwa kutumia tarakimu hii 616 kumuelezea au kumuonysha Shetani na kazi zake mbovu. Mungu anasema kwamba Shetani atashindwa na hatimaye atakuwa ni sehemu ya viumbe wenye kuonekana dhahiri (4).

 

Tunapoiweka Kumbukumbu la Torati 32:8 pamoja na Ufunuo na Danieli, tunaweza kuona wanyama waliotabiriwa ni falme za ulimwengu huu zinazoongozwa na viumbe lio kwenye ulimwengu wa kiroho. Kuna mnyama mmoja kwa wastani, Shetani, aliye na uthibiti wote kamili wa falme hizi zote. Na hata angeutoa ufalme wake wote kwa Masihi iwapo tu kama angemuabudu. Na hii ndiyo sababu mtume Paulo alifanya rejea kwa kiasi kwamba tunapigana vita vya kiroho dhidi ya majeshi yaliyo kwenye ulimwengu wa roho. Majeshi haya yaliyo kwenye ulimwengu wa roho yana uwezo wa kutawala mawazo na nia ya mwanadamu. Ni aina hii ya uthibiti ndio unawezesha Malaika hawa waasi kuanzisha au kuweka mfumo wa uwongo wa kidini na ibada kwa wanadamu. Malaika hawa waasi (hayawani wa kondeni) wanajaribu kwa makusudi kabisa kuukomesha au kuuharibu mpango wa Mungu ambao ulikuwa ni, kama ulivyoonekana kwenye Mwanzo 1:28, wa kumpa mwandamu mamlaka ya kuwatawala samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kwa kila kiumbe kilichohai kitambaacho juu ya nchi. Mamlaka haya ni pamoja na kuwatawala Makaila hawa wasioasi. Kwa kufanya hayo yasitokee, wamejaribu kwa kipindi cha takriban miaka 6,000 sasa kumfanya mwanadamu atengane na kuwa mbali na Mungu. Wameuinua ufalme mmoja baada ya mwingine hapa duniani, ambazo zilitumika kuwafundisha wanadamu uwongo na kuwapotosha.

 

Wakati huu, Yesu Kristo (Yahova Elohim) amekuwa akifanya kazi ili kuweka idadi kamili ya wateule hasi mahali ambapo watakuwa tayari kuchukua maongozi ya sayari hii na kuanzisha ufalme utakaoongozwa na Yesu Kristo mwenyewe. Kazi yake yote imefanywa kwa maelekezo Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli. Ufalme huu utaanzishwa na kuongozwa kwa mujibu wa sheria au Torati ya Mungu iliyotolewa na Malaika wa Agano, ambaye anadhaniwa na baadhi ya watu kuwa alikuwa ni Yesu Kristo (soma majarida ya Malaika wa YHVH (Na. 24) na  Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi (Na. 243) [The Angel of YHVH (No. 24) and The Pre-Existence of Jesus Christ (No. 243)]. Atayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma. Atakapokuja atawakusanya wateule, wale walitiwa alama au mhuri wa Mungu, na atafanya vita na mnyama na wale waliopigwa mhuri wake. Ataazianzisha sheria zote za Mungu ambazo yeye mwenewe alimkabidhi nabii Musa, ni torati ileile ambayo huyu kahaba na binti zake wanadai kuwa zimeondolewa na hazifai kuzishika tena na ambazo hata Waislamu wanazipuuzia kutozishika.

 

Wsasa tungeweza kujua vya kutosha kuhusu habari za alama ya mnyama na tujiuze sisi wenyewe swali hili: “Je, mimi namuabudu mnyama, au ninamuabudu Mungu Mmoja aliye Wapekee na wa Kweli?” Basi, na Tokeni kati yake anyi watu wangu!!

 

q