Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[092]
Roho
(Toleo La 3.0 19950225-20010127-20071215)
Fundisho kuhusu Roho ni dhana iliyoanzishwa kutokana kosa la uasi inayosema kwamba mwanadamu hawezi kufa tu moja kwa moja. Kwa ujumla, mfumo ya imani ya walimwengu ulimwenguni kote hudai na kuamini kuwa roho huishi milele. Mtazamo wa kimafundisho wa Kibiblia kuhusu roho umegeuzwa na mporomoko wa kiroho wa Kanisa la kwanza, kama tunavyojionea kwenye mafundisho yaliyo kwenye jarida hili.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1995, 2000, 2001, 2007 Wade Cox)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Roho
Mafundisho ya
kibiblia kuhusu Roho yako wazi na ni mafundisho rahisi, ambayo yamegeuzwa mporomoko
wa kiroho uliojitokeza kwenye Kanisa la kwanza. Mafundisho ya imani ya kidini
kwa ujumla yamekuwa ni moja ya kile kinachodaiwa na kuaminiwa kuwa roho ni kitu
kinachodumu milele. Haya siyo mafundisho ya kweli ya kibiblia. Mwendelezo wa
kile kinachaitwa mtazamo wa Kikristo na uhusiano wake na mtazamo wa kibiblia
ndiyo mambo yanayotazamwa na kufafanuliwa hapa.
Roho na Biblia
Kama ilivyoelezewa
na Cox, kwenye jarida lake la Uumbaji: Kutoka Kwenye Teolojia ya
Kianthropomorfiki hadi Kwenye Anthropolojia ya Kiteomorfiki (Na. B5) [Creation:
From Anthropomorphic Theology to Theomorphic Anthropology (No. B5)], dhana hii ya kuamini kuwa roho
inaendelea kuishi ikiwa kama kitu kinachoendelea kuishi baada ya kifo imekuwa ni
kisa cha mara kwa mara kinachotokana na imani za Waaminism za Kibabeloni, na
ambazo zinatokana kwenye chimbuko la mafundisho ya kiteolojia ya Wakaldayo. Na
dhana yenyewe inatuama kwenye itikadi ya kuamini miungu mingi na iliyoanzishwa
na waabudu miungu mingi. Biblia inaeleza wazi kabisa kwamba wafu wanabakia
hivyo hivyo hadi kipindi cha ufufuo wa wafu, uwe ule wa Kwanza ama ule Ufufuo
wa Pili. Hakuna mtu aliyewahi kufufuka kutoka kwa wafu zaidi ya Kristo; wateule
wengine wote wanabakia kuwa bado wamelala tu mautini (1Wathesalonike 4:13-18). Ila
wafu walioko mautini watafufuliwa kutoka kwa wafu:
1Wakorintho 15:16-18
Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka. 17 Na
kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu. 18 Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.
Kwa kweli, Kristo
alifufuka kutoka kwa wafu akiwa ni malimbuko ya waliolala mautini (1Wakorintho
15:20). Daudi alikufa na akazikwa na kaburi
lake tunalo hadi siku hii ya leo (Matendo 2:29).
Yohana 3:13 Wala
hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana
wa Adamu.
Umuhimu wa
ufufuko wetu au wa miili unatokana na fundisho hili. Kitendo cha kukana ufufuo
wa wafu au wa miili ambayo imekuwa ni kitu cha kimtindo tu kwenye imani ya
Watrinitariani, sio jambo sahihi, inawa hali hiyo inatokana na kuelewa kimakosa
maana na matukio yanayo ambatana na maadhimisho ya dhabihu ya Pasaka na sadaka
yake. Ni muhimu kushughulika na ufufuo kwa undani wake hapa ili kufikia kiwango
cha kuuelewa uhusiano wake na Kristo na wanadamu na Mungu, na maana ambayo kwayo
Biblia inasema kwamba mwanadamu ataurithi uzima wa mileie.
Fundisho kuhusu
Roho linaonekana kufanyiwa propaganda kwa lengo la kuliwekeza mioyoni na
akilini mwa wanadamu waamini kuwa mtu anaendelea kuishi baada ya kufa kwake jambo
ambalo ni uwongo kabisa, na ukweli ukiwa ni kwamba wanamngojea Mungu tu ndiye
atakayeweza kuwafufua na ndipo watakapoendelea kuishi. Maelezo ya kibiblia kuhusu
ushawishi au dhana hii ya ujuzi huu wa kuwasiliana na wafu au ibada hizi za
kuwasiliana na kuwauliza mashauri wafu inaeleza kwamba ni udanganyifu
uliozoeleka kiasi cha kuonekana kuwa ni kitu cha kawaida, na kazi ya
udanganyifu inayofanywa na Malaika walioasi au mashetani. Na ilikuwa ni
kutokana na imani hii ndiyo ilimpelekea mfalme Sauli aende kumuona mwanamke mchawi
wa Aendori. Mwanamke huyu mchawi aliaminikiwa kuwa alikuwa na roho ya utambuzi
iliyojulikana kama "&! Öwb au obe, kwenye kipindi chake cha kupagawa kwake na mashetani
au yanapompagawisha na kuwavuta walengwa kwa njia ya kijichupa au gudulia,
jambo lililokuwa linatumiwa na watu wenye kutumia mbinu za kupeleka sauti ya mwangwi
au na waomba mizimu wanaotumia mbinu hizi ili kudanganya watu wakijifanya kama
ni mizimu inaongea au roho za utambuzi kwa udanganyifu. Fikra potofu za kudhani
kwamba roho za wafu zinaweza kuitwa kutoka kuzimuni ziliko inachukuliwa
kuaminika zaidi na wengi wanadiriki kuifananisha kimakosa na andiko
linaloonyesha kama Samweli aliitwa akaja kutoka kwa wafu. Na pia madai
yanayoendelea kutolewa kuwa mtu yule alikuwa ni pepo kuwa ndiye Yule mwanamke
aliyemuona; hata hivyo mwanamke Yule alistushwa na kile alichokiona:
1Samweli 28:13 Mfalme
akamwambia Usiogope; waona nini? Yule mwanamke akamwambia Sauli, Naona mungu
anatoka katika nchi.
Neno alilolitumia kuelezea miungu hapa ni elohim, lenye maana ya kiumbe mmoja (au viumbe) na aliyesema na
Sauli alikuwa ni elohim aliyemuondolea
Sauli ufalme wake na kumtangazia hukumu yake. Kitendo cha kuwasiliana na
roho hizi za utambuzi bi ushirikina kwa kuwa kinaivunja Amri ya Kwanza ya
Mwenyezi Mungu na ni kitecho cha uasi kwa Mungu (1Samweli 15:23).
Akitaja kwa hofu
aliyokuwa nayo, alihitimisha kuwa haukuwa uweza au nguvu aliyoijua au aliyokuwa
anashindana nayo. Hakuna pepo wala shetani angaliyeweza kumuondoa Sauli kutoka
kwenye ufalme wake, na wasingeweza kuchukua madaraka. Madai ya kwamba mtu huyu
alikuwa ni malaika waovu au pepo yanaweza kutuama tu kwenye mtazamo wa kwa pale
ambapo kiumbe hiki kinafanya kazi yake kinyume na mapenzi ya Mungu, basi kiumbe
hicho mara moja kitakuwa kwenye mamlaka ya malaika au elohim waovu. Mfano huu
unaonekana kuwa kinyume na maneno aliyoyasema Paulo, ambaye alilijua swali hili
kwa mtazamo wa kimafundisho. Elohim mwenye mamlaka hii kwa mara moja lazima awe
ni miongoni mwa Malaika waliowatiifu kwa Mungu. Makosa ya kiuelewa kwa jambo
hili huenda yanatokana na makosa ya kitafsiri yaliyoko kwenye tafsiri ya Biblia
za NKJV, na NIV, na kadhalika kwa kuwa waliozitafsiri hawakujua maana ya neno
elohim na walikuwa kwenye imani na mafundisho yanayosema kuwa Roho inaendelea kuishi baada ya mtu kufa. Mtu
huyu kwa namna yeyote ile ni elohim, anawezakuwa ni wa mrengo wa Malaika
watiifu au ule wa Malaika waovu na waasi, na kwamwe haikuwa ni roho ya nabii
Samweli.
Kwenye sababu
zilizoainishwa kwenye jarida la Uumbaji
(Na. B5) na za hapo juu. Fundisho
linalodai kuwa roho haifi na inadumu milele ni la uwongo na linatokana na
mafundisho potofu ya teolojia ya Kikaldayo. Ukombozi na kuchaguliwa kwa namna
ya kushirikishana Roho ni dhana iliyo kwenye mchakato wa muundo wa kiroho wa
kiumbe. Ni kwa nini basi Mungu aunde muundo wa kulinda uhai wenye utata sana
kuliko unavyohitajika, ukihusisha na muundo ulio na utata zaidi wa uharibifu? Utata
unahitajika kwenye mlolongo wa kiumbe ukihusisha vyote viwili yaani mwanadamu
na roho, na uharibifu mkubwa zaidi na mbaya wa mtu wa ulimwengu wa kiroho.
Kutokana na maandiko mengine ya biblia, yalielezea kwa kina ukweli wa kwamba, kwenye
ufufuo wa wafu roho itaitafanyizwa na kuwa ni mwanadamu wa kimwili ili
washughulikiwe pamoja na Shetani ambaye atafanyika kuwa mwanadamu na hakuna
namna nyingine bali alikuwa mwenye dhambi. Mwanadamu wa kiroho atafanywa kuwa
wa kimwili na atakufa iwapo kama waliasi kwa kutenda dhambi. Waasi
watendadhambi wote watakufa na watatupwa kwenye ziwa la moto na kuungua huko
kama makapi, sawa na itakavyowapata watu wengine wote waliokataa kutubu.
Watakomeshwa kabisa na hawataishi. Fundisho la Roho kuendelea kuishi ni kitu
kinachokusudia kuendelea kuwafanya watu waamini kuwa kuna mchakato endelevu wa
mzunguko wa maisha usiojali mapenzi mema ya Mungu, neema ya Mungu na uweza
wake. Inaonekana kana kwamba inamwambia Mungu kwamba “Mimi naenda kuishi, iwe
umependa au hupendi na hakuna utakalonifanya kunizuia mimi kuendelea kuishi.”
Mabishano haya yote
yamepata upenyo wake kwenye teolojia ya uhuru wa Kimashariki ya uingiliaji.
Ilipata mpenyo wake kwenye teolojia ya Dini kuu na uingiaji nchini na
watembeleaji. Watu waliiamini imani hii ingawa ilikuwa ni ya uwongo na
udanganyifu. Waliiamini kwakuwa walikuwa ni watu waliokuwa na hamu kubwa ya
kidini. Fundisho la kibiblia kutoka kwenye Mhubiri 12:7 ni kwamba roho inamrudia
Mungu aliyewapa, lakini hii haina maana kuwa ni viumbe vinavyoishi, lakini wafu
hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao
limesahauliwa. (Mhubiri 9:5). Hata hivyo, fundisho lililoko linaendelea kubaki
hivyo kwenye aya zote za biblia ambayo ni kwamba kuna ufufuo wa miili wa wafu (Ayubu
19:26; Ezekieli 37:1).
Kitabu cha Ufunuo
kinaonyesha aina mbili za ufufuo wa wafu. Wa kwanza utatokea kipindi cha kurudi
kwake Masihi mwanzoni mwa Millennia. Umeelezewa kwenye Ufunuo 20:4 na unahusiana
hasa na kufufuliwa kwa wateule, ambao watafanya kazi ya kumsaidia Kristo kwenye
utawala wake wa Milenia. Usaidizi huu utakuwa unaandaa tendo la pili la kuweka
kiwango ambacho kwacho mapepo watahukumiwa nacho kwenye Kiti Kikubwa Cheupe cha Hukumu, ambayo imeelezwa kwenye Ufunuo 20:5.
Ukweli ulioko kuhusu
jinsi sisi tutakavyohusika kwenye utawala wa miaka elfu moja ni jambo
linaloeleweka sana. Shetani asingeweza kuhukumiwa hadi pale Jesu Kristo
alipokuja hapa na kuja kufanya kazi na kuyatoa uhai wake kwa ajili ya watu aliowaokoa.
Alipaswa kujaribiwa jangwani. Wakati Kristo alipojaribiwa na kutakiwa amtende
dhambi Mungu na amuabudu Shetani, alikataa. Kwa hiyo, Shetani alihukumiwa kwa
mujibu wa kile alichokifanya Kristo. Kwa namna hiyo hiyo, ndvyo mapepo wengine
waliobakia watahukumiwa kwa jinsi tunavyotenda na kuishi sisi. Mwishoni mwa
Milenia, watu wote waliowahi kuweko ulimwenguni kote watafufuliwa na
kushughulikiwa kweny kipindi kwenye kipindi chote kitakachowekwa cha hukumu na
cha kuadibishwa, ambacho kinaonekana kuwa huenda kitakuwa ni cha urefu wa miaka
mia moja, kwa mujibu wa Isaya 65:20. Fundisho hili la roho kuishi milele halina nafasi wala mashiko kwenye mfundisho na
imani ya kibiblia. Fundisgo lililopo la Biblia linasema kwamba Mungu anafanya
kazi na wanadamu na kuwahukumu kama ilivyoaelezewa kwa kina kwenye jarida la Tatizo la Uovu.
Mhubiri 9:5 kwa
sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote,
wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.
Dhana na
mafundisho ya zama Baada ya Utawanyiko kuhusu Kristo na Ufufuo wa wafu
Pia uangalifu
ulikuwepo kwenye kazi ya uandishi ya Uumbaji
na mafundisho ya kiteolojia kuhusu nafasi ya usaidizi ya Kristo ya
wanazuoni Watetea dini wa kwanza aliokuwako baada ya zama za utawanyiko wa
Wayahudi huko Yerusalemu mwaka 70 BK. Ilikuwa ni kipindi hiki ndipo Kanisa
lilianza kuingiliwa au kushambuliwa na fundisho hili na kuwapinga moja kwa moja
wale waliokuwa wanafundisha elimu hii inayotokana na wakufundi wa elimu ya dini
zas ulimwengu kwa kutumia vigezo vyenye mashiko. Pia umakini uliwekwa kwa mwandishi
Anders Nygren kwenye kitabu chake cha Upendo
wa Agape na wa Eros [Agape and Eros (kilichotafsiriwa na Philip S. Watson,
Harper Torchbooks, New York, 1969)], ambacho kwacho mfia dini maarufu aitwaye Justin Martyr alionyesha tofauti kubwa
iliyokuwepo kati ya Mungu na mwonekano wa neno, Logos akisema yafuatayo:
Logos liko njiani
kuwa la kimungu lakini sio neno lenye mkazo sana... Ni Baba tu ndiye peke yake hajazaliwa
na hakosei wala hawezi kutenda dhambi na ni ndiye Mungu. Yeye ndiye Muumbaji na
ni Baba wa vitu vyote (Dial. lvi.
1.).
Hajaja kwetu,
emebakia kila mara juu mbinguni na hajajitokeza kamwe kwa mtu yeyote na
hajashirikiana wala hana ushirikiano na mtu yeyote. (Dial. v. 4.)
Kimahusiano nay eye,
Kristo ndiye aliye wa cheo cha chini yake, ambaye ni *,bJ,D@H 2,`H [deuteros
theos], 'Mungu mwingine mbali na yeye aliyeviumba vitu vyote.' (Dial. lvi. 1.)
Nygren anasema
kwamba:
Patano hili la usaidizi
kwenye elimu ya teolojia kuhusu Ktisto ya Watetea dini bila shaka ilichukuliwa
kutoka kwenye mawazo na imani ya Wayunani kuhusu Mungu (ukurasa wa 280).
Kama ilivyosemwa
kwenye Uumbaji, Nygren amekosea
kuhusu jambo hili, kama itakavyokwenda kuonwa kwenye tathmini ya mafundisho ya Agano
la Kale na Jipya lilivyoonyeshwa hapo juu. Mfia dini Justin Martyr yoko karibu
kidogo kuliko yeye; hata hivyo, tofauti na matendo ya uumbaji vinahusiana Logos,
na sehemu yake haieleweki na hawa wanaomhukumu Nygren kina Loofs kuwa sahihi
anapowataja hawa Watetea dini kuwa:
Fundisho lao kuhusu
neno au Logos sio fundisho ‘kuu’ la teolojia inayomhusu Kristo zaidi ya kuwa ya
kawaida tu, bali zaidi sana kuwa ni ya kima cha chini sana zaidi ya tathmini
halisi ya Kikristo juu ya Kristo. Sio Mungu aliyejidhihirisha kwa Kristo, bali ni
Logos yaani (depotenzierte) au uvuvio wa Mungu, Mungu ambaye ni Mungu
aliyejishusha kutoka kwa yeye Mungu aliye juu. (Loofs: Leitfaden zum Studium
der Dogmengeschichte, 4 Aufl. 1906, p. 129, ibid.)
Lakini hawa wote,
kina Nygren na Loofs wamekosea kwenye tathmini yao kuhusu kile kilichokuwa
sahihi na halisi kwenye Ukristo. Walikuwa wanajaribu kuyatafsiri upya
mafundisho ya Nikea kuhusu Kristo, maarufu kama ya ki Ante-Nicene, ambayo
yanafuata kwa ukaribu sana mafundisho ya kibiblia kwenye mtzamo wa kisasa, na
ambayo hayahusini kabisa na maandiko matakatifu.
Malaika wa
Ukombozi alikuwa ni mmoja kati ya washiriki wa
Maraza la Elohim, wakiwa chini ya Elohim mwenyewe, ambaye Eloa (Baba
Mungu na Muumbaji). Malaika huyu wa Ukombozi alifanyika kuwa ni Nyota ya
Alfajiri akichukua mahala pa Shetani, aliyekuwa hapo zamani kuwa ni Nyota ya Asubuhi.
Kwa kupitia matendo yake ya unyenyekevu Kristo alimhukumu Shetani, na ndiye
pekeyake kati ya Jeshi la Malaika atayehukumiwa na Biblia (Yohana 16:11). Nukuu
kwenye 1Henoko inasema kwamba takriban Mashetani 20 wamekwisha tiwa hatiani (tazama
sura ya 3). Hata hivyo, Biblia inaonyesha kuwa ni moja tu, na kwa kweli umuhimu
wa mafuatano yenye mashiko ya hukumu ndiyo yangeelekea hili kufanyika kisahihi.
Katika kushughulika
na fikara ya Nyota wa Alfajiri huyu mpya na Yule wa kale na kipindi cha mpito
au cha ukombozi, inaweza kuwa ni jambo linalochanganya kumuacha mmoja wa hawa
malaika waovu na mwenye nguvu kuliko wote (Kerubi Mwenye Kufunika Mbawa) kwenye
amri, na kumuweka elohim mwingine duniani aliondolewa kwenye ukuhani na
kumchagua na kumfunza kwa kipindi cha ghafla mahala alipokuwa huyu malaika
muasi, na mataifa haya yote yaliyo chini ya uangalizi kupitia kwenye uasi. Hata
hivyo mchakato wa ukombozi na wa kimafundisho vimepunguzwa kwa namna hii. Umuhimu
wa kutendeka hukumu ya haki na isiyo na upendeleo kwa kutoa mfano imeonyeshwa
pia. Ni kwa sababu hii ndipo Kristo, kwa ulazima angeweza kutenda dhambi, na
ndipo Mungu angeonekana kuwa anao upendeleo kwenye hukumu na kwamba ni kweli
kabisa kwa vile Shetani alivyojaribu kumkosea kiumbe ambaye alikuwa ni kama
sawa tu na roboti.
Hakuna kiasi chochote
cha fikra ambacho kingelazimisha wazo la kuishusha kiwango na kuiharibu sayari
(ambayo inatokea kila siku siku hizi) mara tu baada ya mchakato umekwisha wekwa
tayari kwenye mwenendo. Hakuna dalili za majadiliano na malaika muasi iliyoweza
kuonyesha maangamizi yasiyo na maana kama matokeo ya itikadi na imani yao ya kuamini
na kuabudu miungu mingi au wepo wa nje ya mapenzi, asili na upendo wa agape wa Mungu. Ni sawa na imani ya
mwanadamu inafikia kwenye kiwango cha kutorudi zaidi ya yale wasiyoweza
kufikiwa kwayo au kuitwa kwenye toba katika zama hii na kwa hiyo wamekusudiwa
kuangamizwa ili waweze kukombolewa katika mazingira mema kwenye Ufufuo wa Pili
wa wafu. Na hii ndiyo maana ufufuo huu wa wafu unapaswa utendeke katika mwili.
Fumbo lililo
kwenye Mpango wa Wokovu na ufufuo ni kitu kingine ninachogonga uelewa wa wwatu
wengi kuhusu mwendelezo mzuri kama ilivyo kuwa ni utata kuelewa juu ya Malaika
walioasi wakiwa kwenye mwili wa kigoroti. Shetani na Malaika walioasi wanajifanya
kuwa kama Malaika wa Nuru (2Wakorintho 11:14), na hakuna tofauti ya kibiblia, hakuna
kumbukumbu ya tofauti ya mwonekano wao na uwezo wa kujizuia. Wanadhaniwa kuwa
na uwezo wa kuchukua maumbo ya kibinadamu au maumbo mengine mengi na wanaweza
kujitokeza kwenye ndoto na kwenye maono. Vita na matokeo yake vinaonekana kuweko
mawazoni na ni tabia ya mwanadamu, na ili kulinda matumizi mabaya au upotevu wanarudiwa
tena katika mwili kwenye ufufuo wa wafu. Hawana maisha yasiyoweza kufa (tazama
jarida la Uumbaji). Nygren aliijua
hatua hii kwa usahih sana pale aliposema:
Kanisa la kale
linatofautiana kwa kiasi kikubwa sana na Uhellenism kwenye imani yake kwenye
Ufufuo wa wafu. Mapokeo ya Wakristo yanaamini juu ya ‘Ufufuo wa Miili,’ imani
ambayo Watetea dini waliyapinga na kuyashabikia mafundisho ya Kihellenisti
yanayoamini ‘Roho kuendelea kuishi bila kufa.’ Tabasiri yake ilikuwa macho na
kimakusudio, na kwa bila sababu kama hivi ilikuwa ni upinzani wao dhidi ya roho
ya Ehellenisti uliohisiwa na kanisa la kwanza. Mafundisho ya Kihellekini na
Kiplatoniki ua kuwa roho haifi ilionekana na Watetea dini kuwa sio fundisho la
kimungu na ni la kufuru, ambalo zaidi ya yote linatakiwa kushambuliwa na
kukomeshwa kabisa.
(kitabu cha Justin, Dial. lxxx. 3-4) kauli mbiu yao kwa
jambo hili ingelazimu kuwa ni neno la Tatian: 'Hakuna Kutokufa, O Kiyunani, ni
roho iliyo ndani yake yenyewe, bali ni kufa. Ndipo haiwezekani kabisa kutokufa.'
(Tatian, Oratio ad Graecos, xiii. 1).
Tofauti kati ya Ukristo na usio Ukristo kwa jambo hili ni kubwa sana ya imani
ile ya ‘Ufufuo wa miili' ingekuwa ni alama yake. Mtu anayeamini juu ya ‘Roho
kutokufa’ anaonyesha kwahiyo kuwa yeye sio Mkristo. Ni kama alivysema Justin kuwa:
'Iwapo kama wewe umeanguka kwa wale wanaoitwa Wakristo... na wanaosema kwamba
hakuna ufufuo wa wafu, lakini kwamba roho zao, wanapokufa, zinachukuliwa na
kwenda mbinguni, wasichukuliwe kama ni Wakristo (Dial. lxxx. 4) (ibid., pp. 280-281).
Mabwana hawa
wawili hapo juu wanaweweka kwa wazi sana hatua muhimu na ya kuvutia kati ya
Mkristo na falsafa ya uwongo ya Kikristo. Kama ilivyosemwa kwenye jarida la Uumbaji:
… tofauti za msingi
za kifalsafa kati ya Ukristo wa Uwongo na mafundisho ya ‘Roho kuto Kufa’, na
ile ya Wakristo wa kale na mafundisho yake ya ;Ufufuo wa Miili’, ni kwamba fundisho
hili la Roho ni la majigambo la kimwili binafsi na hili la Ufufuo wa Miili ni
lina mashiko ya Kiteolojia. Kwa hiyo ni lazima kwamba kutakuwa na mgongano kati
ya lengo lililosemwa la mfumo na tafsiri yake ya maelezo ya kibiblia ambayi
hayaungi mkono na maridhiano na ni juu ya utaratibu unaodaiwa kuwa ni msingi
wake (ukurasa 62).
Hapo mwanzoni
kabisa ilisemwa kwamba ni masomo ya kina ya kibiblia ndiyo kwayo yangeweza
kufunua falsafa na pia mgongano endelevu. Mlinganisho huu ungeweza kufanya
tathmini yenye mgongano. Kwa kuendelea kutoka kwenye Uumbaji, tunagundua kwamba fundisho hili la Roho kuendelea kuishi linakutikana
kwenye mafundisho ya Plato maarufu kama Plato's Timaeus, ambako kila roho inasemekana kuwa imeunganika na nyota
yake moja inayoishi na ambayo imekuwa ni chanzo cha kuwepo kwake humu Duniani
na ambayo inarudi wakati wa kufa (41dff.). David Ulansey analielezea wazo hili
kwenye kitabu chake cha The Origins of
the Mithraic Mysteries (Oxford, 1989, pp. 86-87), ambako anasema yafuatayo:
'Tunalikuta wazo
lililoendelezwa kikamilifu kwenye mafundisho yanayojulikana kama Empedotimus ya
mwanafunzi wa Plato aitwaye Heraclides Ponticus, ambayo kwayo Nia ya Maziwa
inaonekana kuwa ndiye njia ambayo roho inapitia kwenye chini kwenye uhai mpya. (Kwenye
kitabu cha Heraclides Ponticus, tunawaona Burkert, Lore na Science, ukurasa wa.
366; na Gottschalk, Heraclides wa Pontus, ukurasa wa 98)
Wazo hili la roho
kutokufa lilifanyika kuwa lenye kutetewa sana kipindi hiki cha Wah ellenistiki
hadi kipindi cha kuhukumiwa kwa Franz Cumont, na Warumi kilipokuja kuwa ni
taswira maarufu ya maisha baada ya kufa.
Kwa mujibu wa
Cumont, anasema 'ingawaje kumbukumbu na mwonekano wa kuishi kwa imani ya kwanza
ni kwenye maisha ya wafu makaburini na na kushukia taratibu kwenye shimo
kuzimuni ingeweza kuaminiwa, bali fundisho lingaliloweza kuaminiwa tangia hapo
na kuendelea lilikuwa ni la kidini la roho kuendelea kuishi’ (kitabu cha Franz
Cumont, cha Chimbuko la Dini Mbalimbali kwenye Upagani wa Kirumi wa huko New
York: Dover, 1956, ukurasa wa 39). Ni sawa tu kama kwenye mkazo wa maandiko ya Gnostiki
tunaona kwamba safari ya roho ingawaje mambo ya mbinguni yameruhusu au kuachilia
na kuonyesha kuwa ni hatari na kwamba nguvu za kuzimuni zinahitaji kuzimwa
kwenye kila hatua' (tazama mfano kitabu cha Liturujia ya Mithras Liturgy, cha
huko Meyer, maarufu kama Dini za Kisiri
za Kale, kurasa za 211-21).
Mvutiwo wetu kwa
jambo hili ni kwamba dhana hii ya roho kuendelea kuishi imeelezwa na kutajwa na
mababa wa kanisa la kwanza aitwaye Origen (akimnukuu mwandishi wa riwaya za
kipagani Celsus) ambayo yalikuwa ni mafundisho ya dini ya kipagani ya Mithra. Kwa
mujibu wa Celsus, kwenye Dini hii ya Kisiri ya Mithra, kuna ishara ya vitu
viwili mbinguni, ishara moja wapo ni ya nyota zilizowekwa sawia na nyingine ni
ile iliyoonekana kwenye sayari nay a kiwango cha roho inayoonekana kule. Ishara
ni kwamba kuna ngazi na malango saba na juu yake kuna malango mengine manane.
(Origen, Contra Celsum, ukurasa 334 (6.22)). Kwa kuongezea hapo, mtazamo wa
Uplato Mamboleo unaonyesha kuwa imani ya Umithraism ni fundisho lenye utata kusema
kuwa rohi unadmmu pasipo kufa ikienda na kutoka kuzimuni na kuifanya iweze
kumuingia kiumbe mwingine anayezaliwa.
Jinsi ilivyosemwa
huko nyuma:
… hii inachukua
mahala pa udanganyifu aliofanyiwa Adamu kwenye kitabu cha Mwanzo akiambiwa kuwa
‘Hakika hutakufa’ imani inayotokana na Dini za kipagani za Kisiri za
Wababelonia na jinsi walivyozifanya upya tena kutoka kwenye dini za Waariyani
wa Kihindu nay a Wayunani nay a watu wa Mashariki.
Ni mfumo unaotokana
na falsafa ya kujiona au kujifikiria wenyewe ambayo inazidisha imani juu ya
miungu mingi na ambayo inaongeza kwa kiasi kikubwa tofauti ya tabaka kutoka
kwenye mfumo wa kitabaka wakihusisha imani ya Mungu. Mpangilio huu wa kitabaka
unasababisha madhara makubwa kwenye mfumo mzima. Mwambatano wake unazidi na kwa
kweli mtengano na mtafaruku. Kimantiki, mchakato huu unangukia kwenye Majivuno
ya Kisaikolojia na Uherodi, ambavvyo vinaendana kws pamoja kwa kweli.
Mfumo wowote unaotuama
kwenye mtazamo wa ubinafsi na kwenyendo na unaofuatilia kiwango cha kadiri cha
kila mtu hatimaye utashindwa na uwekezaji wa kadiri. Dhana hii ya miungu mingi
unaweza kuwa ni chanzo cha aina ya mtazamo wa kimungu unaoweza kuonekana kukirudiwa
mara kwa mara kwa kuwa uanzishajiwa mafundisho uko kwenye kiwango kikubwa. Mafundisho
haya kimsingi yalipinga ukweli wa Mungu kuwa kiini na mwaamini Mungu yeyote analazimika
kuwapinga. Kwa usemi rahisi ni kwamba huwezi kuamini katika imani ya roho
kusihi milele na halafu ukawa ni Muamini Mungu mzuri (imenukuliwa kwenye jarida
la Uumbaji (Na.B5), ukurasa 63).
Dhana hii
ilihusika na kwenye umri na hukumu iliyoongelewa na kufafanuliwa kwenye jarida
la Matatizo ya Uovu. Kipengele kilichonukuliwa
hapa kinaonyesha asili ya mafundisho yaliyoko hadi kwenye zama ya Watetea dini
wa kwanza.
Madhara ya fundisho
hili la Roho kutokufa yalikuwa makubwa sana hasa kwenye kipindi cha karne ya
tano, ambapo Augustine alisema kwamba miili
ya kiroho sio roho, bali ni miili tu ambayo:
… sio kwa ajili ya
kupungukiwa na virutubisho vya asilia, bsli ni kwa bahati ya kiwango na ubora
wake [utakuwa] unaishi mbinguni wenyewe (Mji wa Mungu, xiii.23).
Augustine aliandika
kwenye ukurasa wa (xxii.29) kuwa:
Ndipo Mungu [baada
ya ufufuo wa wafu] ataonekana na yale macho kwenye uhalisia wa milki yao (kwenye
mazingira haya ya kufanyika kwao upya) ya kitu chenye kiwango kinachofahamika, uweza
wa kupambanua mambo yaliyo sio ya asili ya visivyo na uhai. Tena, ni vigumu
kama sio haiwezekani kabisa, kuliunga mkono wazo hili kwa ushahidi wowote wa
kifungu cha Maandiko Matakatifu.
Mtu anaweza kuuliza
kuwa ni kwa namna gani mchakato huu wa mabadiliko wa uelewa wenye msingi wa
muundo wa mambo ya maisha baada ya kifo unavyweza kutokea. Umuhimu wa uelewa pia
ulikuwa na maana kuu sana kwenye uelewa wa mambo yenye matukio muhimu ya Agano
Jipya. ght well ask how this process of change in mfuatano wa matukio unaitwa
kuwa Matukio ya Kristo au kerygma na wanateolojia. Mtazamo kuhusu
roho na uhusiano wake na Uungu unaathiri uelewa wa dhana ya kuzaliwa upya kwa
Yesu Kristo. Kuelewa kikamilifu kwa mfumo wa mwili, ni jambo la muhimu la
kwanza ili kufanyiza mafundisana kiusahihi kuhusu kuja dunianai na kuzaliwa ho
ya kibiblia kwa jambo hili.
Kuja duniani
na kuzaliwa kwa Yesu, jinsi neno au Logosalifanyika Mwanadamu
Kutokana na
Yohana 4:24, tunaona kwamba Mungu ni Roho. Tafsiri ya Yohana 4:24 inasema kuwa Mungu ni Roho kwenye Biblia zote, yaani
NKJV, NIV, NASB, NEB, JB, TEV, RSV, Moffatt, Zwingli. Andiko hili limetafsiriwa
Mungu ni roho kwenye biblia za KJV,
RV, Noli, J.F.B. kitabu cha Fafanuzi cha Commentary, Vincent's Word Studies
in the New Testament. Biblia ya Amplified Bible inalitafsiri andiko hili
kuwa Mungu ni roho (inaonyesha ni Kiumbe aliye wa Kiroho). Nukuu
ya Origen kwenye Yohana 4:24 imetafsiri kuwa Mungu ni roho na kwenye baraza la Nikea lijulikanalo kama Ante-Nicene Fathers kwa Kumpinga Celsus, Bk. 2, Sura ya 71 (ANF, Vol. 4, uk. 460); Bk. 6, Sura 70 (ANF, Vol. 4, uk. 605); De
Principis Bk. 1, Sura 1 (ANF,
Vol. 4, uk. 242). Tafsiri ya ANF inalitafsiri
andiko hili pia kama alivyolitafsiri Tatian Akifanya
rejea kwenye lugha ya Kiyunani (ANF, Vol. 2, uk. 66) na pia kwa
Tertullian kwenye kitabu chake cha Kumpinga
Praxeas, Sura 7 (ANF, Vol. 3, uk. 602); na Dhidi ya Hermogenes Sura 32 (ANF, Vol. 3, uk. 495). Kwa hiyo
Tertullian alielewa lugha ya Kiyunani kwa namna hii pia. Kulinganisha na uandishi
wa Kiyunani kuhusu “Mungu” mwingine
kwenye maandiko haya yanafanya kwa mfano, 1Yohana 4:8, 1Yohana 4:16, 1Yohana
1:5. Nia ya kumfanya Mungu kuwa ni Roha pekee inatokana na muundo wa imani ya
Waplatoniki kukiwemo na fikara ya Wademiurge, na Wastoiki fikara ya Kidunia ya Wafilo
inayochanganika na ya Kiyahudi ya Shekina na ya Memra iliyotokana na wazo lake
la Logos. Imani ya Kibiblia ina idadi ya matamko ya msingi yanayobeba dodoso au
dalili ya utofauti. Kwa mfano, Kristo alikuwa na wanamna yake peke yake ambaye
alikuwa kwenye mikono ya Mungu alipokuwa anakufa.
Luka. 23:46 mikononi mwako naiweka roho yangu.
Roho hii ni
tofauti na Roho Mtakatifu, ambaye ni Roho wa Kweli na anayetokana na Baba (Yohana
5:26), lakini inaonekana kuwa na uhusiano wa kimshikamano naye na kwa kweli
inategemeana nayo. Muundo wa mchakato huu unaonekana kutokana na kufuata
kikamilifu na mlolongo uliowekwa kwa wanadamu na ulioonyeshwa hapo juu– ambao
kwamba kila mwenye mwili atakufa. Kristo alikufa pia (Yohana 3:16; Warumi 5:8;
2Wakorintho 5:14-15; 1Petro 2:24). Kristo alikubali kuutoa uhai wake kama
ilivyoeleza hapo juu.
Yohana 15:13 Hakuna
aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki
zake.
Uhai wa Kristo
ulitolewa kama sadaka ya kuondoa makosa ya wengi (Mathayo 20:28; Marko 10:45).
1Petro 3:18 inasema kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi na kondoo (tazama
Yohana 10:11). Paulo anasema kwamba Kristo alikufa na kufufuka na kwamba
ufufuko na kupaa mbinguni kwa Kristo ni mambo muhimu ya msingi kwa Imani yetu,
kama ulivyo ufufuo wa wote wenye mwili.
1Wakorintho 15:12-14
Basi, ikiwa Kristo
anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba
hakuna kiyama ya wafu? 13 Lakini kama hakuna
kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka; 14 tena
kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.
Ufufuo wa wafu
Wote
Mashiko yaliyo
kwenye usemi huu wa Mtume Paulo ni kwamba namna ya kifo na ufufuko wa Kristo ni
sawa tu na ilivyo na itakavyokuwa kwa wateule, aliowafia (1Yohana 3:16). Ufufuo
wa wafu, umeandikwa kwenye Ufunuo 20:4 nk, kisha inafuatiwa na watu wote kwa
ujumla wao. Kristo alikuwa na uzima ndani yake ambao aliruzukiwa na Baba (Yohana
5:26). alisemekana kuwa ni Adamu wa mwisho. Mtume Paulo anajibu maswali
yaliyoko kuhusu ufufuo wa wafu akisema:
1Wakorintho 15:35-49
Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani? 36 Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa; 37 nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila
chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo; 38 lakini
Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake. 39 Nyama
yote si nyama moja; ila nyingine ni ya wanadamu, nyingine ya hayawani, nyingine
ya ndege, nyingine ya samaki 40 Tena kuna miili ya
mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na
fahari yake ile ya duniani ni mbali. 41 Kuna fahari moja ya
jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko
tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota. 42 Kadhalika
na kiyama ya watu. hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika;
43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa
katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu; 44 hupandwa
mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho
pia uko. 45 Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza,
Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha. 46 Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili;
baadaye huja ule wa roho. 47 Mtu wa kwanza atoka
katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni. 48 Kama
alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama alivyo yeye wa
mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni. 49 Na
kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake
yeye aliye wa mbinguni.
Paulo anasema kwamba mwili na damu
haviwezi kuurithi Ufalme wa Mungu, wala uharibifu kuurithi kutokuharibika (aya
ya 50). Hali halisi inajulikana kuitangulia kutoka kwenye hali ya mwili hadi
kwenye kuzaliwa upya kunakofanyika kwa njia ya ubatizo baada ya kutubu, akiwa
anajua na kutubu akiwa mtu mzima anapoitwa na Mungu. Kwa hiyo basi, ubatizo unaweza tu kufanyika baada
ya toba na mtumzima. Wakati maandiko yaliyo kwenye Marko 16 tangia aya za 9-20 zinakubaliana
kwa ujumla kuwa ama imeandikwa kama nyongeza kutoka kwenye maandiko asilia au
marekebisho ya aya (na ambayo inaonekana ingeweza kuondolewa kwenye kipindi
cha zamani), andiko lililo kwenye aya ya 16 inaonyesha kuwa dhana ya kufanya
toba kwa njia ya imani ilikuwa ni ya muhimu ili kuupata wokovu Asiyeamini atahukumiwa inaonyesha kuwa
toba na imani vilikuwa ni vitu muhimu ili kustahili kubatizwa. Na ndiyo maana
watoto wameondolewa haki hiyo kwa kuwa hawawezi kufikia kwenye kiwango cha
kujua mabaya na kuweza kufanya toba. Kwa hiyo, ubatizo wa watoto wadogo ni
kitendo kilicho kinyume kabisa na hali yenye maana inayohitajika kufanyiwa
ubatizo na ilikuja julikana kwenye zama za karne chache tu zilizopita.
Kuzaliwa Tena
Kwa Njia ya Ubatizo
Maisha ya kiroho ya mwanadamu na muungo au imani juu ya kuzaliwa mara ya pili na kuijua gennao vimeelezwa vizuri sana kwenye
jarida la Uuumbaji. Itikadi hii ya kuzaliwa mara ya pili kwa njia ya ubatizo
katika toba kumpokea Roho Mtakatifu ni muhimu ili mtu aweze kuuingia Ufalme wa
Mungu (Yohana 3:3-5). Kutokana na Warumi 8:23, tunda la kwanza la Roho
linatolewa na mtu hulipokea kwenye ubatizo, lakini tendo la kufanywa Wana
linatokea kwa tendo la ukombozi wa mwili. Tendo la kuzaliwa mara ya pili linafanyika wakati
wa ubatizo kwa ishara ya kifo na kufufuliwa ambayo uzamishaji wa mwili wote hufanyika.
Kitendo hiki cha kumzamisha mtu mwili wote majini kiliaminika kuwa ni tendo
endelevu na cha lazima sio tu kwa Kanisa bali pia ni ishara ya ubatizo wa
Yohana aliyoitumia alipokuwa anawabatiza watu kwenye Mto Yordani. Kristo
alienda kwa kupitia mchakato huu na Roho Mtakatifu alimshukia kutoka kwa Baba
kwa umbo la njiwa (Mathayo 3:16; Marko 1:10; Luka 3:22; Yohana 1:32). Kila
Injili inathibitisha mchakato huu. Kwa kweli, ukweli unajitokeza na kuonekana ili
kwamba mchakato wenyewe umethibitika kuwa ni muhimu katika Kristo ukiwa ni
mfano wa kwanza au tunda la kwanza. Kuna watu wengine wanaoonekana kwenye Agano
la Kale ambao walimpokea Roho Mtakatifu pasipo kufuata utaratibu wa kawaida
unaojulikana na kuzoeleka wa kuwekewa mikono uliozoeleka. na mtu. Daudi aliomba
kwamba Roho Mtakatifu asiondolewe kutoka kwake (Zaburi 51:11). Daudi alitiwa
mafuta na Samweli Hata hivyo, wengine hawakutiwa mafuta kwa wazi au kikamilifu.
Biblia yenyewe
inatuambia kwamba ufufuo wa wafu na uelewa wa muundo wa kiroho vilikuwa kwenye
mabishano ndani ya vikundi vya kidini au madhehebu ya Kiyahudi. Masadukayo
walifundisha kwamba hakutakuwepo na ufufuo wa wafu, wala hakuna malaika, wala
hakuna roho (Matendo 23:8). Mafarisayo walikubali na kuamini mambo haya yote
mawili (Matendo 23:8), na Kristo aliwakubali mafarisayo na kusema kuwa ni wao ndio
walioketi kwenye kiti cha Musa na kwamba wanastahili kuheshimiwa na watu
kuwatii (Mathayo 23:2).
Inaonekana kuwa
Mafarisayo walikumbwa na mtindo wa kupenda mali na utajiri jambo ambalo
linapaswa kuepukwa suala hili la kujilimbikizia mali na utajiri. Mtume Paulo
aliendeleza mtazamo usioendana na waumini kujikita kwenye mahangaiko ya
kutafuta mali Kristo atakapokuja. Ni jambo lililo dhahiri kwa kila msomaji wa
Biblia kwamba kipindi cha takriban miaka elfu mbili kimeshuhudia wateule wengi
wakifa. Mchakato huu, kwa ajili ya dhana na fundisho la kumpokea Roho Mtakatifu
kwenye ubatizo, jambo hili la kufa lilijulikana kama kulala mautini au usingizini.
Mtu wa kale alikufa kwenye ubatizo, na mtu mmoja mwingine aliyezaliwa upya au
aliyezaliwa kwa roho. Mtume Paulo anasema:
1Wakorintho 15:51-53
Angalieni, nawaambia ninyi
siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, 52 kwa
dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana
parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.
53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu
wa kufa uvae kutokufa.
Mchakato unaoongelewa
hapa ni Ufufuo wa wafu wa Kwanza ulioelezwa kwenye Ufunuo 20:4. Ufufuo wa Pili
ni ule utakaofanyika baada ya miaka elfu wa hii dunia kuwa chini ya utawala wa
Kristo. Huu ni ufufuo wa jumla wa wote waliokufa huko nyuma ambao unatajwa
kwenye Ufunuo 20:11-15. Kwenye 1Wathesalonike 4:15, Paulo anasema kwamba hatuta
‘zuia’ au kuwatangulia waliolala. Kristo atakuja na wafu waliokufa katika
Kristo – wale waliobatizwa na kisha wakafa – watafufuliwa kwanza na kisha
watakuwa pamoja na wale walio hai, watabadilishwa na kuwa wakiroho kabisa.
Jinsi mchakato huu utakavyokuwa imefafanuliwa kwenye jarida la Tatizo la Uovu. Hawa watakaobadilishwa
na kuwa kwenye hali ya kiroho ndipo watakutanika pamoja na Kristo huko
Yerusalemu ambako kutoka hapo ulimwengu wote utatawaliwa kutoka hapo katika
utawala wa Kristo kwa kipindi cha millennia au miaka elfu. Zekaria 14 inaelezea
mambo yatakvyokuwa kipindi hiki. Mchakato wa kuanzishwa kwake umeainishwa
kwenye Zekaria 14:1-15. Ulazima wa kwenda kuadhimisha huko Yerusalemu na kuishika
Sikukuu ya Vibanda ili mvua inyeshe kwa majira
yake sahihi umetajwa. Kwa hiyo, kutokana na Maandiko haya Matakatifu,
kuwepo kwa makundi mawili ya watu yatakayojitokeza hapa duniani kipindi hiki
cha miaka elfu baada ya kurudi kwa Kristo. Hawa ni wateule wa kiroho
watakaokuwa chini ya Kristo, na ni watu waliosalia kutokana na Vita vya Siku za
Mwisho ambao watapewa ulinzi kwa kuiweka vizuri tena sayari hii. Wateule
watakuwa ndyo walinzi wa mambo yatakavyokuwa na watu watakaobakia (Isaya
30:21).
Kama kundi,
Wasabato wa Kiadventista wana mkakati wa makusudi kabisa wa kutoweza au
kupuuzia kuamini juu ya utawala huu wa milania As a group, Seventh-Day
Adventists have a serious inability to comprehend the millennial structure (tazama
sehemu ya Nyongeza). Kwa mujibu wa maandiko ya Ellen G. White, wanatafsiri na
kukifanya kuwa ni cha kiroho tu kipindi hiki cha Milenia na kwa hiyo hawawezi
kuhesabu kukamilifu kwa manabii. Waamini unyakuo wengine wana tatizo kama
hilihili pia.
Mchakato ambao Biblia
unautumia katika kuwashughulikia wale watakaobaki Kristo ajapo ni kwamba ni kubadilishwa miili. Wafu watafufuliwa na
kubalidishwa miili yao pamoja na wale watakaobakia hai bado. Ni sawa na hilo,
wale watakaokuwa mwishoni mwa kipindi hiki cha utawala wa milenia wa Kristo na
ambao hawakuasi, na wale walio kwenye Ufufuo wa Pili waliofufuliwa watapelekwa
hukumuni kwa kipindi kinachooneka kuwa kuenda kitakuwa cha miaka mia moja (kutoka
kwenye Isaya 65:20). Mwishoni mwa miaka hii mia moja, waongofu waliookoka watabadilishwa miili yao. Watenda dhambi
wasiotubu wataruhusiwa kufa na watatupwa kwenye Jehenamu ya moto; au kwa maneno
mengine, miili yao itaunguzwa. Sababu inayofanya kuwa ni muhimu kuuelezea
mchakato huu hapa ni kwamba mchakato na mlolongo wa uvunaji matunda ni muhimu
katika kuelewa uji wa Kristo wa kuzaliwa kwake. Kufa na kufufuka kwake Kristo.
Krristo alikuwa
ni limbuko la wote wenye mwili. Alikuwa ni mfano wa kile kitakachotokea kwa
wateule, na kisha kwa wanadamu kwa ujumla. Kristo ndiye pekee aliyezaliwa na
Mungu na Mwana wa Mungu (monogenes theos
na uion; Yohana 1:18; 3:16; 1Yohana
4:9; pia tazama Luka 7:12, 8:42, 9:38; Waebrania 11:17 kwa kulinganisha au
kuainisha). Alikuwa ni mzaliwa wa pekee (prototokos)
wa viumbe wote (Wakolosai 1:15), kwa hiyo, mwanzo wa uumbaji wa Mungu (Ufunuo
3:14, sio kama ilivyoandikwa kwenye tafsiri ya NIV; tazama hapo juu). Fundisho
la kibiblia ni kwamba Kristo alikuwa ni Mwana wa Mungu na alikuwa ni tofauti na
Mungu, ambaye ametajwa kuwa ni Mungu Baba.
Wakati Kristo alipokufa alidumu na kuendelea kuwa na mwili uliokufa kwa siku
tatu, bali hakuruhusiwa auone uharibifu au kuoza (Zaburi 16:10). Hata hivyo,
roho yake ilimrudia Mungu wake, ambaye ni Baba. Na Baba akamfufua kutoka kwa
wafu kwa mamlaka yake au amri yake, ambayo alimpa Kristo kabla ya kufa kwake (Yohana
10:18), na ambavyo ndivyo alivyoamua hata kabla ya kuwekwa kwa msingi wa dunia (Ufunuo
13:8). Umuhimu wa sadaka hii na kwa hiyo pia wa ufufuo wake vimekusudiwa kwa
kuutoa uhai wake au kwa kuweka msingi (kataboles)
wa dunia (kosmou).
Dhana na Fikra
Potofu ya Kisasa
Kinachojulikana na
kisicho na shaka ni kwamba Kristo alikuwa ni mtumishi mtiifu. Kutokana ilivyo
hapo juu, kifo na kufufuka kwake vilikuwa ni lazima kwenye Imani yetu. Mchakato
wote huu unafanya taswira ya kile kinachojulikana kuwapata wateule, na hatimaye
kwa watu wote kwa ujumla. Ukristo ulioko leo umetuama kwenye idadi ya mambo na
mafundisho ya uwongo, yaliyoelezwa hapo chini. Kwa ufupi, unajaribu kudai mambo
yafuatayo:
1: Mungu na Masihi (na Roho Mtakatifu) ni
wamoja wanaotokana na kila mmoja wao kuwa na nafsi yake na wanauweza sawa na
haiba sawa na mawazo na ni vigumu sana kuelezea Utu na muungano wao. Pia kwamba
huyu elohim anagawanyika kwenye nafsi mbili na Roho, wakiacha kutilia maanani
tofauti iliyopo kati ya Eloa na Baraza lake. Kutokana na uchambuzi uliofanyika hapo
juu, huu ni uwongo.
2: Kwamba mwonekano wake na kazi za kipindi
cha kabla ya kuzaliwa kwake katika mwili Kristo hakuwa malaika wa YHVH.
3: Kwamba Kristo alikuwa ni Mwana pekee wa
Mungu kalba ya uumbaji wa dunia (tazama Ayubu 1:6; 2:1; 38:7). Madai haya ni ya
uwongo. Ni lazima kuwe kuna mchakato mahsusi wa kuja kwake duniani kwa kuzaliwa
kimwili uliofanywa kwa ajili ya Kristo akiwa tofauti nae, na ni tofauti kutoka
na Mungu. Ukristo wa leo haulielezi jambo hili.
Kristo na Shetani
walikuwa sio Nyota mbili za Asubuhi peke yao (tazama Ayubu 38:7; Isaya 14:12; Ufunuo
2:28; 22:16). Madai na uhakika wa kuwepo Nyota wengi ws Asubuhi na Baraza la
Elohim yanaonyesha uenezaji na uimarishaji wa mamlaka kwenye mifumo mingi. Kila
mmoja wa watu hawa anauhusiano na utambulisho na Baba ambao hauwezi kubaguliwa na
ule uhusiano wa Kristo. Ukweli wa kuwa Kristo ni mshiriki kwa watu hawa
unamaanisha kuwa hawezi kuwa Mungu wao. Kwa hiyo, uhusiano wake na Baba ni way
eye kuwa mdogo. Kwa hiyo, ujio wake na kuzaliwa katika mwili hapa duniani
hauwezi kukamilika kwa namna ya madai yao ya kumfanya kuwa ni mshiriki sawa
kwenye cheo cha Uungu. Kwa hiyo, andiko linadai kwa kusema hivi:
4: Kwamba Kristo ni
Mungu kwa namna hii hii kwamba Mungu kama Mungu ni ya uwongo.
Yeye ni mdogo kwa
Mungu na ni mtumishi tu (Waebrania 1:9), aliyetumwa na Bwana wa Majeshi (Zekaria
2:10-11). Kwa hiyo hawezi kuchukuliwa au kuwekwa uzani sawa wa kuabudiwa na
Mungu au kufanyiwa dua, kinyume kabisa na Kutoka 34:14, Mathayo 4:10 nk.
Upuuzi mwingine
unaofuatia ulioendelezwa kutoka kwenye madai ya kuwepo kwa Kristo na kumfanya
kuwa tofauti, na zaidi sana kuliko kwenye hali ya kuzaliwa kwake hapa duniani
ni kwamba angeweza kujiomba yeye mwenyewe kama Mungu. Fikra ya namna hiyo inakataa
kabisa tofauti iliyopo kati ya Baba na Mwana na ukamilifu wa mpango mkamilifu wa
ufufuo. Haya ni mafundisho ya Mpingakristo (1Yohana 2:22; 4:3; 2Yohana 7). Mabishano
haya yameendelea hadi kwenye fikra ya kudhania kwamba kwamba Kristo na Mungu walikuwa na matakwa mamoja na kwamba Kristo hakuwa na mapenzi tofauti ambayo
kwayo alimshirikisha Mungu kwa utii aliokuwa nao. Hili limekanushwa kwenye sura
ya 2. Wazi hili ndipo liliendelezwa kwa kusema kuwa:
5: Asili ya kimbinguni inakubali kwamba
hakuna faida wala hasara kwa Kristo (fikra hii ni tofauti kutoka ilivyo hapo
juu).
Dhana iliyoko
kwenye jambo hili ni kwamba:
6: Kwamba Roho Mtakatifu ametolewa kwa
kipimo (kinyume na ilivyoandikwa kwenye Yohana 3:34, RSV; Warumi 12:6); na
kwamba
7: Kristo asingeweza kutenda dhambi (kutoka
kwenye sababu au madai ya uwongo kuhusu uasilia wa kimbinguni inatokubali kuwa
hakuna faida wala hakuna hasara zaidi tu ya uweza wa Mungu wa kuelewa kila
kitu, ambaye alijua tangu mwanzo kuwa Kristo asingeweza kutenda dhambi); tazama
hapo juu.
Maendeleo ya
mabishano haya yanaendelea kwenye madai haya:
8: Kwamba Kristo alikuwa na cheo sawa na
Mungu kwa namna ambayo kwamba alikuwa sawa na mwenye umilele sawa na Mungu, madai yaliyo kinyume kabisa na andiko
la Wafilipi 2:6 na 1Timotheo 6:16, yanayoonyesha kwamba Mungu huishi milele
bila kufa. Umilele wa Kristo au uzima wa aioonion
(1Yohana 1:2), na kwamba Viumbe wote wametokana na yeye ambaye ni Mungu wa
Kweli (Yohana 5:20).
Wote wawili,
yaani Kristo na malaika wateule wana asili moja tu (Waebrania 2:11, RSV) wakiwa
na sifa ya kuishi na kutokufa kutokana na utiifu uliotakiwa kwa Baba (Yohana
5:19-30), alioyetuumba sisi sote
(Malaki 2:10-15). Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo
hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake.
(Yohana 5:26), na sisi ni
warithi pamoja naye, tuliochaguliwa kuwa na uzima ndani yetu kwa mamlaka ya
Mungu. Inakuwa lazima kwa Wakrito wa leo kufanya madai ya uwongo kuwa:
9: Kwamba malaika
wateule sio Wana wa Mungu kwa namna iliyoko ya sawa na Kristo alivyo kuwa ni
Mwana wa Mungu na kwamba sio warithi pamoja naye, kinyume na inavyosema Warumi 8:17; Wagalatia 3:29; Tito
3:7; Waebrania 1:14; 6:17; 11:9; Yakobo 2:5; 1Petro 3:7.
Katika kuiunga
mkono jambo hili, matumizi yake yamekuwa ya kimakosa:
10: Kwamba Mungu Mtukufu mwenyewe alishuka
hapa chini katika mwili na
kuishi pamoja na wanadamu (wakiyachukulia maandiko yasiyo rasmi na
yasiyoandikwa na mwandishi asilia yaliyo kwenye 1Timotheo 3:16 kwenye fasiri ya
Codex A, iliyofanyizwa kwenye fasiri ya KJV na iliyoingizwa na kutiliwa mkazo
kwenye mhutasari wa biblia ya NIV) kinyume na Yohana 1:18 (na Yohana 1:14 ambapo
ilikuwa ni logos, au memra, aliyefanyika kuwa mwili) na maandiko
mengine kadhaa yanayomuweka mbali Kristo na Mungu wa Pekee wa Kweli (Eloa au
Theon, ambaye ni Mungu Baba), Mungu wa Yesu Kristo (Yohana 17:3, 20:17; 1Wakorintho
8:6; 2Wakorintho 1:3), anayesimama kwenye Jina Lake (Mika 5:5).
Maelezo
yaliyokosewa yaliyoko hapo juu ya Ukristo mambo leo yanaathiri uelewa kuhusu
dhana ya kuja kwa mwokozi na kuzaliwa kimwili hapa duniani. Hii inatokana
ukweli kwamba fikra ya jinsi Mungu alivyo mmoja
inaeleweka vibaya na wamini Utatu. Shema
(Kumbukumbu la Torati 6:4) imetathminiwa baadae. Huyu aliyetajwa kwenye
Kumbukumbu la Torati 6:5 anajulikana kama Mungu
Aliye Juu Sana, Mungu aliyemtia mafuta Kristo kama Elohi wa Israeli, kwenye
Zaburi 45:6-7. Umoja wa Mungu ni muhimu sana kwa imani juu ya Mungu mmoja au
Umonotheism, na ni sharti endelevu iliyo kwenye umoja ulio chini ya mapenzi
mhimilifu kwa makubaliano na mwingiliano wa kiroho kupitia Roho na Uweza wa
Mungu (1Wakorintho 2:4-14) ambayo kupitia Kristo, ni kuelekea kwa Mungu
(2Wakorintho 3:3-4). Imani ya Utatu hukataa umoja muhimu kwenye imani juu ya
Mungu mmoja au Umonotheism na kwa kweli ni waamini miungu mingi. Inadaiwa kuwa
ilitokea kwa sababu watawala hawakuelewa,
kuwa havijavuviwa na roho (1Korintho 2:8,14). Kristo aliweza kujifanya kuwa
Mungu, na alimudu kufikia kima cha utimilifu wa Kiuungu kwa uweza wa Roho
Mtakatifu.
Fundisho la
Kanisa la Kwanza
Namna ya hili tendo
la kuja duniani na kuzaliwa katika mwili imebakia kuwa ni fumbo kubwa. Hata
hivyo, hakuna shaka kwamba hatushughuliki na sehemu tu ya matendo kwa Kiumbe
ambaye kwa namna fulani ameacha asili yake Mbinguni kana kwamba angekuwa na
sayari mbili tofauti za kuishi kwa muda. Dhana na fikra kama hii haina mashiko
ya kibiblia kabisa. Tukiwa tumewekwa kwenye misingi na imani ya kibiblia kwenye
kipindi cha Kristo, tunaweza kujionea jinsi fundisho hili lilikuwepo kindi cha
karne ya kwanza nay a pili. Kutokana na maandiko tuliyonayo ya Justin Martyr na
Irenaeus, tunajua kwamba uelewa umeongezeka kwenye Kanisa la kwanza. Justin
Martyr anasema kuwa Mungu alifundisha kitu hichohicho kwa manabii kama Musa nah
ii ilikuja jitokeza hapo juu (tazama kitabu cha Dial. na Trypho, Sura ya XXVII, ANF,
Vol. I, ukurasa 207). Justin alifundisha kwamba Mungu alianzisha, kama huko
mwanzoni, nguvu ya namna fulani, kutokana yeye mwenyewe ambayo inaitwa Roho
Mtakatifu” sasa Utukufu wa Bwana, sasa ni Mwana, na tena ni Hekima, tena
Malaika, kisha Mungu (theos), na kisha Bwana na Logos. Justin anamuonyesha yeye
kuwa kama Kapteni wa Jeshi la Bwana aliyemtokea Yoshua (ibid., LXI). Eneo hili
lilichukuliwa ili kuonyesha kilichoandikwa kwenye mithali 8:21. Ambapo Hekima
ilitajwa kuwa ni Masihi, aliyefanywa na Mungu. Mapenzi ya Mungu hatimaye
yatimilizwa na Masihi. Justin (ibid., LXII) anaendelea kusema kwamba, kwenye
uumbaji Mungu alifunikwa na viumbe wengi waliokuwa tofauti nay eye mwenyewe. Na
kwa hiyo Musa aliaminika kutangaza kwamba uumbaji ulihusika na yapata viumbe
wawili ambao wasifa wao ulikuwa ni tofauti na wasiofanana. Waditheists wanajaribu
kutenganisha watu hawa na kuwa wawili, na waamini Utatu wanaigawa hii kwenye
viumbe vitatu vilivyo tufauti hypostases.
Ikitolewa na Watrinitarian wenyewe, mabishano kati ya Wabinitariani na
Watrinitariani huenda yakawa hayana maana. Hawa elohimu kwa kweli walikuwa ni
wengi, kutoka kwenye maandiko mengine yaliyotajwa hapo juu, hususan Zaburi 45:6-7,
walioitwa kuwa ni washika wa Kristo.
Irenaeus (mwaka
125-203 BK) aliandika juu ya swala hili la wasifa enezi wa elohim (au theoi kwa
Kiyunani) kwa wanadamu. Irenaeus ni wa muhimu kwa kuwa alikuwa mwanafunzi wa
Polycarp, mwanafunzi wa Yohana (tazama kitabu cha Butler, cha Maisha ya Watakatifu (Lives of the Saints),
Burns & Oates, U.K., 1991, ukurasa 56). Kwa hiyo tunaweza kuwa wasafi kwa
namna fulani tukisema kwamba uelewa wa Irenaeus (aliyeuawa kwa ajili ya
kughushi) aliweka wastani wa Kanisa la kwanza. Kwa kweli aliwasaidia Waquartodecimans
na kuwatete kuhusiana na utata uliojitokeza kuhusu maadhimisho ya Pasaka (Butler,
ibid., ukurasa 197), ingawaje alitengwa mbali ya Asia Ndogo, akapelekwa huko Lyon.
Kwenye kitabu chake kiitwacho Dhidi ya
Uzushi (Against Heresies) alifundisha ukweli kwamba wateule au malaika
wangeishi kama elohim. Irenaeus alishikilia kuamini kwamba malaika na muumbaji
wa ulimwengu walikuwa sio viumbe wasiomjua Mungu mwenyezi wakionekana kuwa
walikuwa ni viumbe wake pia na waliumbwa na yeye (Bk. II, Ch. VI, ANF, ukurasa 365). Irenaeus hakumtaja
muumbaji wa ulimwengu, ambaye alikuwa ni Masihi, kama Mungu aliye Juu Sana au
Mwenyezi (Sura ya VI, ibid.). kutokana na kazi hii ineonekana kwamba fikra za
Wayunani kuhusu Demiurge na Pleroma yameshambulia mawazo yao ambayo yaliitwa Aeons,
na yalikusudia kuvutia fikra za kibiblia ambayo wanamifano wa Kiyunani, kwayo
yanaharibu maana yake. Wagnoistiki walilazimika kwa chinichini kuwa sehemu ya
dini ya Siri. Mwendelezo wa mwisho wa kwenye imani ya Utatu umeelezewa baadae.
Irenaeus (na
Justin) walifundisha kwamba ufufuo wa wafu ulikuwa ni wa kimwili, na kwamba
Mungu atailinda miili isioze na idumu bila kufa (jarida la ANF, Vol. I, uk. 403). Mungu anaaminika kuwa ni Muumbaji (ibid., uk.
404), ikimpingwa Kristo aliyeumba ulimwengu kwa mamlaka ya Mungu (uk. 405).
Irenaeus anafundisha kwamba Roho Mtakatifu alihusika na wote wawili, yaani Baba
na Mwana (kutoka Zaburi 45:6-7) akiwa Elohim au Theoi; Baba anamtuma Mwana
Irenaeus alifundisha kwamba Zaburi 82:1 ilikuwa inawataja Baba, Mwana na
malaika (ambao ndio walengwa wa Kanisa) pale aliposema:
Mungu alisimama
katikati ya Kutaniko la miungu (theoi), akiwahukumu miungu (Adv. Her., Bk. III, sra ya VI, ANF, Vol. I, uk. 419).
Anaonekana
kutokuwa na uelewa mkamilifu eneo la udugu wa wateule, ambao ulienea kwa
Malaika wote wakiwa ni wapendwa kwenye Ufalme. Yohana alionyeshwa Ufunuo akiwa kisiwani
Patmo alipofungwa akiwa amekwisha mfundisha tayari Polycarp. Ufunuo 12:10 inasema
kuwa malaika ni ndugu zao wateule. Ufunuo 4 na 5 inaonysha kuwa wateule
wamejumuishwa na Baraza la Wazee ili kuwa wafalme na makuhani kati ya Malaika. Kristo
alisema kwamba wateule watafanana na malaika (isaggelos: kutokana
na neno isos na aggelos, ambayo
yana nadharia ya kuwa sehemu yao wakiwa
sawa).
Irenaeus aliamini
kuwa Kanisa lilikuwa ni sinagogi ya Mungu, ambalo Mwana alikutanika kwa ajili
yake mwenyewe. Mungu wa miungu Zaburi
50:1 inaonekana kumtaja Mungu. Bwana wetu na Masihi alikuwa ni theos au Mungu atakayekuja kwa ujio wa
wazi na hatakuja kwa uficho wala hatanyamaza (Zaburi 50:3), na aliyeonekana
wazi kwa wale wasiomtafuta (Isaya 65:1). Jina miungu lililo kwenye Zaburi 50:1 linawahusu wateule ambao Kristo
anaaminika kuwa aliwasema kuwa: “Ninyi miungi nanyi ni wana wa Aliye Juu” (Yohana 10:34-35 sawa na Zaburi
82:6). Kwa hiyo ni makosa makubwa kwa Kanisa kusema kuwa kwa kipindi chake cha
millennia ambayo Kristo amekuwa akilitumia andiko ambalo limekuwa likiwataja mahakimu
wote wa Yerusalemu, wakati mwanafunzi wa Polycarp waliamini kuwa alikuwa
anawataja wateule kama elohim. Wale waliomwamini Kristo waliaminika na Iranaeus
kuwa walikuwa ni Wana wa Mungu walio warithi pamoja na Kristo, na ndio elohim.
Iranaeus anaamini pia kwamba Kristo alikuwa Mwana wa Mungu aliye Mimi Niko Ambaye Niko (YHVH) (kutokana
na Kutoka 3:14). Kwa hiyo, uchukuaji wa jina hili ulikuwa kwa ajili ya kupewa
au kuruzukiwa. Irenaeus alimnukuu Isaya hivi:
Isaya 43:10 Ninyi
ni mashahidi wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na
kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye
yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo
Soncino analieleza
jambo hili kama hivi:
Ninyi ni mashahidi
wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na
kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu (EI) awaye yote, wala
baada yangu mimi hatakuwapo
Nukuu kutoka kwa Irenaeus
na Soncino zinatofautiana, ambazo
kwa kuzidi au kwa upungufu Irenaeus, anaonyesha kuwa ‘MIMI’ inamaanisha kumtaja
Mungu, ambaye ni Baba. Akitajwa kama mtumishi
kwenye Soncino inaonekana na Irenaeus
kumtaja Masihi.
Soncino inajaribu
kufananisha jina Mtumishi Wangu na mashahidi wa kale wa Israeli, ingawaje
hakuna mamlaka ya kirabi yanayotajwa. Kinachuonekana kuwa ni hakika ni kwamba
andiko hili lilionekana kama linaashiria kwamba ni Mungu pekee, na sio Masiri,
ndiye alikuwepo huko nyuma kabla ya yote. Baba, Masihi wanatofautiana na Mungu.
Irenaeus anaonysha kwamba uelewa wake katika Isaya 44:9 na Yeremia 10:11 kuhusu
suala la vinyago au sanamu ilikuwa ni kwamba vinyago hivi vilikuwa ni sanamu za
mashetani (Adv. Her., Bk. III, Ch.
VI, ANF, p. 419). Mashetani hawa
waliondolewa kutoka kwa theoi au elohim. Akifananisha na Yeremia 10:11,
Irenaeus ananukuu hivi:
Miungu ambao hawajaumba
mbingu na nchi, na waangamie kwenye dunia iliyo chini ya mbingu. Kwa kuwa kutokana
na ukweli wa yeye kuwa mshiriki aliyeunganishwa na maangamivu yao anawaonyesha
kuwa hakuna miungu (elohim au theoi) yeyote.
Kwa hiyo sanamu
zenyewe zilonyeshwa kueleweka kuwa sio sanamu za kawaida, bali zaidi sana ni
zilikuwa na miili ya mashetani ambazo (tazama pia kitabu cha Bk. III, Ch.
XII:6, ibid., uk. 432). Hiki ndicho kilikuwa kipimo kilichoeleweka kipindi cha
ulimwengu wa kale. Kwa hiyo kitendo cha kuwaondoa mapepo hawa kusafisha na hatimaye
kuhukumiwa kuliwaondoa kwenye kundi la elohim.
Irenaeus anaonyesha
kwa maelezo Kutoka 7:1 kwamba Musa alikuwa kwa kweli amefanywa kuwa elohim kwa
Farao, lakini hakuweza kutajwa kikamilifu kuwa ni Bwana au Mungu na
manabii. Zaidi tu ni kwamba Musa anatajwa na Roho kama Musa, mtu na mtumishi wa Mungu mwaminifu (Waebrania 3:5; Hesabu
12:7), ambavyo ndivyo pia alivyotajwa Masihi kwenye maandiko. Kwa hiyo, kila
elohim ni mtumishi mwaminifu wa Eloa, Elyon.
Irenaeus (uk.
421) anasema kwamba Kristo alikiri kuwa ‘ya kaisari apewe Kaisari’ na ‘ya Mungu
apewe Mungu;, kwenye Mathayo 6:24, katika kumtumikia Mungu na sio mungu mammon.
Kwa hiyo, Kristo alijiweka kando kutokana na kudai kuwa yeye ni Mungu (tazama
ukurasa 422). Aliinukuu Wafilipi 2:8, Irenaeus anaonyesha kuwa uhusiano kati ya
Kristo na Mungu na Mwamuzi ulitokana na Mungu
wa Wote kwa kuwa alikuwa mtii hadi kufa (Sura ya XII:8, uk. 433). Irenaeus anainukuu
Septuagint (LXX) kwenye Isaya 9:6 akisema kwamba Masihi alikuwa ni Emmanueli mjumbe [au Malaika] wa Shauri Kuu la Baba (Sura
ya XVI:3, ibid., uk. 441). Kwa hiyo alionyesha kwamba Malaika wa Shauri Kuu wa
Agano la Kale (LXX) alikuwa anajulikana kuwa ni Kristo. Irenaeus anakataa wazo
la kwamba mateso ya Yesu yanaweza kumtenganisha na Masihi kwa madai kwamba
Kristo alitajwa kuwa ni mwenye huruma na kuteseka. Kwa maneno mengine, anakataa
jaribio kwa kudai kwamba mwili wa kimbinguni wa Masihi ungeweza kutofautishwa
na Yesu mwanadamu hapa Duniani. Hili lilifanyika kuwa ni fundisho la dini ya
Wagnostiki likiibadilisha Injili ya Marko na kuzipuuzia na nyingine.
Pia Irenaeus anaonyesha
misingi wa makosa ya dini hizi potofu. Waebioni wanadaiwa kuwa waliitumia
Injili ya Mathayo peke yake. Kwa hiyo walifanya hitimisho zenye makosa
kuhusiana na nafasi ya Kristo. Waathanathias au Watrinitariani walilitumia jina
Waebioni baadae kama kujaribu
kufanyiza mafundisho udogo kicheo au wanaoamini hivyo wakitumia kila namna ya
ushawishi kwenye kila msitari na namna yeyote ya kizushi za hawa Waebioni kwa
kila namna iliyotumika kwenye mabishano ya mtaguso wa nikea ambao uliitwa kwa
jina la Waarian. Madai haya ni ya uwongo kutoka kwenye mahojiano yaliyofanywa
na waandishi wa Kanisa la kwanza na ambao walikuwepo siku za kabla ya mtaguso
wa Nikea, na kugundua walikuwa wasabonist.
Irenaeus alikuwa
anasisitiza kwamba kulikuwa na Mungu mmoja tu au Baba, aitwaye Mungu Baba. Masihi alikuwa ni Mwana
wake. Anasema pia kuwa Marcion aliiongeza Injili ya Luka ili kuwekeza mafundisho
yake. Wavalentinia waliitumia Injili ya Yohana kuzikanganya nyingine na pia kwa
kuzijumuisha injili za uwongo. Ukweli ni kwamba basi, kama sasa, Maandiko matakatifu
yanapaswa kutumika pamoja, kwa bidii na sio kwa kuyachagua. Irenaeus anaonyesha
uelewa mkubwa wa asili iliyoko kwenye Injili hizi nne na maana zake kwa
kuhusianisha na Makerubi (ibid., Bk. III, Ch. XI:8, kurasa 428-429). Irenaeus alikataa
dhana ya kuwa Yesu aliweza kuteseka na kufa na kufufuka tena, na kwamba yeye
aliyewahi kuruka na kwenda mbinguni alikuwa ni mwingine. Irenaeus aliamini
kwamba “Kristo ambaye Mungu alimuahidi kumtuma, alimtuma katika Yesu,
waliyemsulibisha na Mungu akamfufua (ibid.,
Ch. XII:2,4,5; kurasa 430, 431).
Hakuna mchanganyo
kati ya Mungu na Kristo kwenye mawazo ya huyua mwana teolojia na anasema hapa
wazi kabisa, kwamba Mitume hawakumbadili Mungu, bali Kristo alitumwa na Mungu. Irenaeus
anasema:
Wapenzi, msiiamini
kila roho, Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu
Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. (sura ya. XVI:8 akiinukuu Yohana
1 Yohana 4:1,2. Kumbuka: Tafsiri ya Vulgate
na Origen zinakubaliana na Irenaeus, Tertullian inaonekana kukubaliana na
maandiko yote mawili). Socrates anasema (VII:32, uk. 381) kwamba kifungu
kiliharibiwa na wale waliotaka kutofautisha ubinadamu wa Kristo kutoka kwenye
ule wa kimbinguni. Polycarp (Ep., c, vii) anaonekana kukubaliana na Irenaeus
na ndivyo alivyofanya Ignatius pia (Ep.
Smyr., c,v) (tazama ANF, ibid., uk.
443, iliyonukuliwa pia na Burton, kwenye kitabu chake cha Shuhuda za Ante-Nicene hazi Umbinguni wa Kristo (Ante-Nicene
Testimonies to the Divinity of Christ)].
Kwa hiyo, kila fundisho
linalotafuta kumtenganisha Kristo kwa kumuunganisha kwenye eneo linguine na
wote wawili, yaani mamlaka ya kidunia na kimbinguni lilichukuliwa na Kanisa la
kwanza kuwa ni Fundisho la Mpingakristo. Tendo la kuyabadili au kuyageuza maandiko
linaonekana kuwa na lenye asili ya Kimashariki. Maandiko ya Biblia bado
hayajasahihishwa hadi leo.
Irenaeus anasema
kwamba Roho wa Mungu alimshukia Kristo kwa umbo la njiwa ili aweze kutimiliza
yaliyoatabiriwa kwenye Isaya 11:2 kusema: Na
roho ya Bwana atakaa juu yake, na pia Isaya
61:1: Roho
ya Bwana MUNGU i juu yangu; Kwa hiyo sio
yeye aliyekuwa anaongea bali ni Roho wa Baba yenu ndiye anayeongea ndani yenu (Mathayo 10:20) (Sura ya XVII:1, ibid., uk.
444). Kwa hiyo, Roho Mtakatifu alijulikana kuwa ni wa Mungu na sio alitoka kwa
Kristo, bali zaidi sana ni kwa kupitia Kristo kama ilivyoelezwa hapo juu. Hii
ilikuwa ni kwamba:
… Mwana wa Mungu,
alifanyika kuwa Mwana wa Adamu akifanyika kuwa kwenye udugu na mkutaniko naye
ili aishi kwenye ulimwengu wa wanadamu, ili aishi na wanadamu na kuwa kati yao
alizifanya kazi za Mungu, akiyatumikia mapenzi ya Baba kwao, na kuwarejesha kutoka
kwenye tabia na miendendo yao ya zamani hadi kwenye upya wa Kristo (ibid.).
Irenaeus alifundisha
kwamba wateule wangewekwa kwenye maisha yasiyo na kifo ili wapokee hali ya kufanywa
wana kama Wana (Sura XIX:1). Roho aliwaunganisha wateule kwa Mungu, akiyaleta
makabila mbalimbali kweny umoja na kuwatoa kwa Baba malimbo ya mataifa yote (ibid.,
XIX:2). Kristo alikuwa ni chombo cha matendo yake, lakini hakuwa ni mlengwa
kwenye ibada au kuabudiwa na wala sio msanifu mkuu wa mambo yake. Hata hivyo,
alikuwa ni Mshauri wa Ajabu na Mungu mwenye Nguvu aliyeandikwa kwenye Isaya
9:6, na Hakimu kwenye Danieli 7:13
(ibid.). Hata hivyo, Kristo alimtambua na kumheshimu Baba kuwa ndiye Mungu
wake, kama alivyofanya Daudi, (tukiinukuu Zaburi 22:1) ambapo Daudi alisema:
Mungu wangu Mungu
wangu mbona umeniacha?
Kristo tena
alisema haya alipokuwa mtini, kama ilivyonukuliwa kwenye Mathayo 27:46 na Marko
15:34. Maandiko haya yote mawili yanamtaja Eloa, Mungu Mkuu na ni Mungu na Baba
wa Kristo. Maneno yaliyotumiwa na Kristo ni ya Kiaramu, wakati aliposikika
akisema:
Eloi, Eloi, la'ma
sabaki-th'a'ni.
Hii ni tafsiri ya
kimaandiko ya lugha ya Kiingereza iliyotokana na fasiri ya kiimandishi ya Kiyunani
yenye chanzo asilia cha lugha ya Kiaramu inayosema 'eli, 'eli lamah 'azabthani. Neno linalomtaja Mungu hapo ni la Kiaramu la El hapo kama Mungu anayeelezea mapenzi yake kwa Mwanae. Mungu hakumsahau
wala kumuacha Kristo kama inavyosema Zaburi 22:24 kuwa:
Maana hakulidharau
teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake, Bali
alipomlilia
Kwa hiyo unaona
hapa kuwa Mungu na Kristo walikuwa watu tofauti hapa. Kristo hakuwa anaongea tu
hapa kimasihi kama sauti ya Mungu, ni kama ulivyokuweko ulazima wa kutofautiana
uliopo kwenye Maandiko Matakatifu yanayohitaji utendaji wa kimbinguni kwenye
usaidizi na ambao hauwezr kutangiliwa. Hakuna mwingine bali Kristo na wateule
waliitwa na Mungu (elohim) kwa kuwazidisha. Irenaeus anasema yafuatayo:
Hakuna mwingine
aliyeitwa Mungu kwenye Maandiko Matakatifu isipokuwa Baba wa wote, na Mwana ba
wale waliopewa uwana (Adv. Her., Bk.
IV, Pref. 4, ANF, p. 463): [na pia]
[Sura ya ] 1. Kwa
kuwa hii ni hakika na imara (sic), kwamba hakuna Mungu mwingine au Bwana
aliyetangazwa na Roho, isipokuwa yeye ambaye ndiye Mungu, atawalaye juu ya
yote, pamoja na Neno wake, na wale wanaompokea Roho wa kufanywa wana [tazama iii.
6,1], kwamba ni wale wanaomwamini Mungu mmoja na wa pekee, na Yesu Kristo Mwana
wa Mungu, na ni kama walivyofanya kwao wenyewe wakisema kuwa hakuna aliye kama
Mungu, au jina [hakuna jingine] aliye kama Bwana, na ni kitu gani kilicho
muhimu zaidi, [kwa kuwa ni kweli (sic)] kwamba Bwana wetu [alitenda sawa na], aliyetuamuru
sisi kuwa kutomkiri mwingine yeyote ila Baba, isipokuwa yeye tu aliyeko mbinguni,
ambaye ni Mungu mmoja na Baba mmoja;...(ibid., uk. 463).
Kwa hiyo ni
upuuzi kudai kujaribu kudhani kuwa kuelewa kuwa ni wateule ndio watakaokuwa
elohim haikueleweka kama fundisho asilia la karne mbili za kwanza za Kanisa,
ikichukuliwa kwamba Irenaeus alikuwa ni kiunganisho cha karibu sana tuliyenaye na
mafundisho yake, na yuko wazi sana anasema na kuamini. Zaidi sana, inaonekana
pasipo na shaka kwamba imani ile ni mpango muhimu wa Maandiko Matakatifu, na
sio tu kuwa ni wa Maandiko Matakatifu kikamilifu – ambao tafsiri ya kibiblia
ilikuwa ni Agano la Kale (Danieli 10:21; Mathayo 21:42; 22:29; 26:54; Marko
12:10,24; 14:49; 15:28; Luka 4:21; 24:27,32,45; Yohana 2:22; 5:39; 7:38; nk.) – lakini pia kwenye Injili na kwenye maandiko ya
Agano Jipya. Kwenye ukurasa huuhuu kunaelezea kuhusu wateule wa elohim, waliotajwa
kwenye Yohana 10:35, Kristo anaonyesha fikara yah ii kwamba Maandiko Matakatifu
hayawezi kutanguka. Kutokana na hapo juu, mafundisho ya Kanisa la kwanza
yanaonekana wazi kuwa ni ya mfumo wa mkubwa na mdogo, yakihusisha pia fundisho
la uzima wa milele unaotegemea kwa Roho Mtakatifu anayewezesha kazi ya ufufuo
wa wateule wakiwa kama theoi au elohim kwenye Ufufuo wa Kwanza wa
wafu wakati Masihi atakaporudi.
Fundisho kuhusu
Roho kwa hiyo liliwaingia wateule sana baadae sambamba na dini ya Siri nay a
Mungu wa Utatu. Kanisa asilia la kwanza lilishikilia kuamini juu ya ufufuo wa
wafu na kikikataa mafundisho ya Roho kuendelea kuishi na kuyachukulia kuwa ni
ya kipagani. Mabishano juu ya kukubaliana na Kanisa la Kikristo lenye
mafundisho ya Kihelleniki na kuwaona kuwa wako sahihi zaidi ya ilivyokuwa imani
ya mwanzoni ya Kiyahudi, sawa na wale walioyageukia mafundisho na imani ya Ebionite,
au kuondolewa wakichukuliwa kuwa wamebobea kwenye Ukristo wa itikadi ya Kiyudea
ambayo kwa kweli ilitoa mwanya kwenye Ukristo wa itikadi kali nay a wastani
uliokuwa chini ya uangalizi wa Wamataifa kama ilivyoelekezwa na Mtume Paulo,
jambo ambalo ni uwongo. Mabishano haya yalileta kile kilichosemwa na Paulo
kwenye nyaraka zake mbili zote wa Wakolosai na wa Wagalatia. Mabishano kama
hayahaya yametumika kuingiza makosa ya fundisho la Roho kutokufa (tazama jarida
la Mafundisho ya Kisocrati ya Roho (Na. B6) [The Socratic Doctrine of the Soul (No. B6))].
Fundisho hili la
Roho ni dhana ya uasi unaorithiwa unayosema kwamba hakika mwanadamu hatakufa (Mwanzo 3:4). Ni jaribio la kuchukua nadharia
ya hukumu kwa ajili ya dhambi isiwepo kwa wanadamu. Dhana ya kwamba mwanadamu
atakuwa kama elohim katika kuelewa
peke yake iliingizwa na Shetani kwa mujibu wa Mwanzo 3:5. Uwezo wa kuwa kama elohim
kwa ujumla unategemea na ufufuo wa wafu, kupitia kwenye neema iokoayo Yoshua au
Yesu Kristo akiwa Masihi. Kitendo cha kupinga kuwepo kwa kipindi cha utawala wa
Milenia ni sehemu ya udanganyifu na kujaribu kudai urithi usiojulikana kanuni
yake wa uzima wa milele. Uzima wa milele unaweza kupatikana tu kwa kumjua Mungu
wa Pekee na wa Kweli na mwana waike Yesu Kristo. Hakuna kitu kama hicho ya
‘roho isiyokufa’. Ni uwongo unaotokana na imani za Kibabelonia, na ambayo
imeenea ulimwenguni kote. Watu wanaamini uwongo kwa kuwa hawamwamini wala
kumtii Mungu. Pasipo na Roho Mtakatifu, mawazo yao yanamchukia Mungu (Warumi
8:7), na hayawezi kumtii Mungu au kumudu kuwa kwenye asili yake. Wateule wamechukua
asili ya Mungu wakiwa kama warithi pamoja na Yesu Kristo (2Petro 1:4). Ni Mungu
tu ndiye asiyeweza kufa (1Timotheo 6:16). Anakaa kwenye nuru inayofikiwa na
hakuna mwanadamu aliyewahi kumuona wala anayeweza kumuona. Ni kwa njia ya Roho
tu ndipo tunavyoweza kumaribia Mungu na hiyo inategemea na utii wetu na dhabihu
ya Yesu Kristo, ambaye ndiye muombezi wetu na Mungu Mmoja na wa Kweli (Yohana
17:3; 1Yohana 5:20; Wagalatia 3:19-20; 1Timotheo 2:5; Waebrania 8:6; 9:15;
12:24).
Tunapaswa
kutarajia ufufuo wa wafu ili tuweze kuwa wanadamu katika ulimwengu wa roho
tukiwa kama wana wa Mungu, wakati tutakapomuona Mungu na kumkaribia kwa dhahiri
na kwa matendo. Kwa hiyo sasa tunakikaribia Kiti cha Enzi cha neema kwa njia ya
roho.
Nyongeza
Kushindwa kwa
Waadventista Wasabato ( Wa-SDA) kuelewa na kuendana kama unavyosema unabii wa Isaya
na Zekaria unatokana na wao kujikita kwenye maandiko mapotofu ya Ellen G.
White, ambayo yamechukulia kipindi cha millennia kuwa ni cha kiroho na kuyatafsiri
mambo yote kwa mtazamo huu wa kiroho na kudhania kwamba Shetani atakuwa hapa
duniani peke yake. Huu ni uwongo wa dhahiri kabisa umesababishwa na ukosefu wa
kuelewa wa waandishi wao ambao wameyaelezea maneno ya manabii Isaya na Zekaria yanayoonyesha
kuwa Kristo atakuja kuzianzisha tena ulimwenguni kote ibada za Sabato, Miandamo
ya Mwezi na Sikukuu Zilizoamriwa zinazokutikana kwenye mambo ya Walawi 23 (sawa
na Isaya 66:23; Zekaria 14:16-19). Kama mfano wa kushindwa huku kuelewa
marejesho yatakayokuweko kipindi cha milenia yanaonekana kwenye kitabu cha Robert
D. Brinsmead, aliyeandika mengi kuhusu suala la Usabato na Torati (tazama
makala yake ya Kuutathmini Upya Usabato, (Sabbatarianism Re-examined, la Juni
1981). Brinsmead anashambulia mafundisho kadhaa na imani ya Wa-SDA na anajaribu
kukana fundisho linaloelezea mtawanyiko wa Waingereza, ila ameweka sawa mtazamo
wake kuhusu unabii unaolingana na elimu ya mambo na mwenendo wa mambo ya
ulimwengu, na kusema kuwa Maandiko Matakatifu yalikuwa yanaeleza mambo kiroho
na siyo kimwili, wakati ambapo kwa mfano, nabii Isaya alimuainisha kuwa alikuwa
anataja matukio yatakayotokea kimwili kabisa.
Wa-SDA
wanaonekana hawajachukua kwenye na kupeleka kwenye mabaraza yao wazo lolote
lile linalohusika na ukweli kuhusu kipindi hiki cha millennia, na ya kuwa
kitafanyika kiukweli na sio kiroho na utawala wake na Kristo utakuwa hapa
duniani kwa miaka elfu. Badala yake, Ellen G. White na Wa-SDA walizua fundisho la
kunyakuliwa kwenda mbinguni, ambapo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu watenda
dhambi wote watauawa na kwamba wenye haki wote watanyakuliwa na kupelekwa
Mbinguni na kwamba Shetani ataachwa peke yake hapa Duniani kwa kipindi cha
miaka elfu moja, akingojea hadi ile hukumu ya mwisho. Na hii ndiyo
wanavyoamini, ambavyo ni kinyume kabisa na maelekezo chambuzi ya Maanago ya
Kale na Jipya. Hivi wanavyoamini hakuna msingi wala mashiko ya Kibiblia lakini
wao wanaamini tu hivyo.
Maranyingi sana,
tunapowapata watu wakishughulikia mambo haya wanakuwa hawausomi unabii wa Agano
la Kale kama tunavyousoma sisi. Wanasema na kudhani kuwa hakuna ukweli kwenye
unabii wowote wa Agano la Kale, unaoelezea marejesho ya kweli ya Israeli hapa
duniani. Wanasoma wakiwa na mifano ya kiroho, kwa hiyo kwa watu hawa unabii
hauwezi kuwaeleza au kuwaonyesha kile unachokikusudia au kinachousema. Maranyingim
tunaokuwa kwenye andiko la 66:23 linalosema kuwa Sabato na Miandamo ya Mwezi
vitarejeshwa na kuadhimishwa, wanasema kuwa huenda kuna mkazo wa kiroho
umaonishwa na kukaziwa hapa. Ila haviendi kurejeshwa Sabato zenyewe na kwa hiyo
ndipo hata Brinsmead anaweza kuziondoa Sabato zilizowekwa msingi wake kwenye
andiko hili, ambalo linasema wazi sana kwamba Kristo atakuja kuzirejesha upya.
Ni upingaji na msimamo chuki tu kichwani na ambao ni suala linaloleta maswali
mengi sana kujiuliza juu yake. Ni msimamo ambao hauna nafasi kwenye akili za
mtu imara. Hakuna ukweli kwao wanaoujua au kuushikilia kutokana na unabii wa
biblia kwa namna yoyote ile kuhusu marejesho yanayokwenda kufanywa siku zijazo
za mwisho. Wanalisikia neno la kweli na la uzima ila wana udanganyifu unaowafanya
waendelee kupotoka na kutoliamini jambo hili. Bali wamekuwa wakiuamini uwongo tu
na kuupenda.
Imani ya Brinsmead
kuhusu andiko la Isaya 40:3-4 hadi Yohana Mbatizaji peke yake (tazama Sura ya
7) inaonyesha kuwa haelewi ukweli Ujio ws Masihi kwa hatua mbili, na Mfalme
Masihi ni mtu halisi atakayekuja kutawala Siku za Mwisho. Tafsiri ya The
Companion Bible inaionyesha Isaya
40:3 ikionysha kwamba andiko hili halijatimilika bado. Tafsiri ya kiroho ya
Wa-SDA kuhusu kipindi cha millennia inawasuta wao wenyewe na waandishi wao. Kwa
kweli tafsiri hii ya uwongo inakwenda kuiangamiza imani hata ya Brinsmead mwenyewe.
Brinsmead anashikilia kuamini kwamba, “mara tu baada ya imani ya kweli ya
kikatoliki inavyopasa kuingia kila mahali, ndivyo inavyopaswa pia kupenya kila
wakati. Hakuna wakati ulio mtakatifu kwa wenyewe tu kama ulivyo tena zaidi ya
kila mahali ni patakatifu au kila kitu ni najisi. Kwa hakika sheria zilizokuwa
zinahusiana na mahali na nyakati zilikuwa ni za kipindi kifupi tu zilizowekwa
kwenye huduma au kanuni za kidini hadi kipindi cha matengenezo”
(Sura ya10, uk. 37).
Kwa hiyo, tunaona
kule anakokwenda hadi kipindi hiki. Anauchukulia kimakosa ukweli wenye msingi
wa kisayansi kuhusu sheria ya vyakula ukweli kuhusu utofautishaji kati ya mambo
matakatifu na yaliyo najisi, akidhania kwamba Kristo amebatilisha tofauti zote
kati ya yaliyo ya kidunia. Basi hakuna maana ya kusema tokeni ndani yake na muwe watakatifu; kwa kuwa ninyi ni watakatifu wa watakatifu na kwamba Hekalu la Mungu li ndani
yetu. Nasi tu Hekalu la Mungu. Na kwamba utofauti huu hauna maana, licha ya
ukweli kwamba ni fundisho la kibiblia.
Malumbano haya
yanasababishwa na uwepo wa uweza wa Kristo wa kubadilisha nyakati na Sheria kwa
mintaarafu sawa na Mungu, na ni Utrintari uliorithiwa. Zaidi sana, ukengeufu
umetabiriwa kutokea kwenye Danieli 7:25, na ni machukizo kwa Mungu Aliye Juu
Sana. Malumbano yote, mawili yote kutoka kwenye imani ya Kiadventista na kutoka
kwenye imani ya Utatu, inatuama kwenye fundisho la Roho kutokufa.
Marejesho mapya yatakayofanywa na Kristo yanaonyesha kwamba kuna aina mbili ya viumbe. Wale wa daraja la kwanza, wanaoitwa wateule, watakaofufuka kwenye Ufufuo wa Kwanza na ambao watafanyika kuwa viumbe katika roho wakati Kristo akija. Kundi la pili ni lile ni la wale watakaokuwepo kwenye Ufufuo wa Pili utakaotokea baada ya kipindi cha utawala wa millennia, na linawajumuisha watu walioishi kipindi cha Milenia na wale waliokufa ambao hawakuwa na sehemu kwenye mafundisho ya wale walio na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza (Ufunuo 20:1-6). Tazama jarida la Ufufuo wa Wafu (Na. 143) [The Resurrection of the Dead (No. 143)].
Shetani atafunguliwa baada ya miaka elfu na anakwenda kuwadanganya mataifa, walio pande nne za Dunia (Ufunuo 20:8-9). Imani ya Kiadventa haioni masshiko yoyote kwenye maandiko haya kwa ajili ya maandiko mapotofu ya Ellen G. White. Hawezi kuuelewa ufufuo wa miili wa dunia nzima, na teolojia yake inapingana na asili ya uwepo wa Mungu.
q