Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[187B]

 

 

Majukumu ya Familia 

(Toleo La 2.0 20071112-20071204)

Ni kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu wafanye kazi kama jumuia inayotenda kazi? Maandiko Matakatofu yanafunua kwamba muundo wa familia uliwekwa kwenye ulimwengu wa kiroho hata kabla ya kuubwa kwa mwanadamu. Maandiko yanatufunulia pia kwamba mwajibiko ulitolewa kwa wana wa kiroho wa Mungu walioumbwa ili kulinda familia ya mwanadamu kwa uhusiano bora na wa upendo na Baha wa uumbaji. Kwenye familia ya mwanadamu pia, Mungu aliweka mwajibiko kuwapa baba, mama, kaka, dada na mabibi na mababu kwa ili kuweza kuiweka sawa mambo ya kiroho na kimwili ya familia. Je, ni majukumu gani hayo basi? Jarida hili linakwenda kujibu maswali yahoo yote. Ni muhimu kwa uwepo na ustawi wa jamii ili kuiwezesha kuyajua mapenzi ya Mungu kwa familia, na umuhimu wa kujua wajibu wa kila mshiriki kwenye muundo wa familia.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2007 Tom Schardt and Jeremy Hatchett, ed. Wade Cox)

(tr. 2013) 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Majukumu ya Familia


 

Mungu Aliyejuu Sana Aliifanya Familia

Kabla ya kuumbwa kwake mwandamu, familia ya Mungu ilikuwepo. Mwonekano wa muundo wa kifamilia ulianza na kuwepo wakati Mungu Aliyejuu Sana ilifangiliwa kwa umakini mkubwa na kuweka familia endelevu ya wana wa kiroho. Neno la Kiebrania kuelezea mwana ni ben (SHD 1121). Limetumika zaidi ya mara 5,000 kwenye Maandiko Matakatifu, na linatumika kwa namna mbalimbali na wanadamu pamoja na wana wa Mungu walioko mbinguni. Agano la Kale linaelezea baraza la mbinguni kuwa ni mjumuiko wa “wana wa Mungu” (Ayubu 1:6, 2:1). 

 

Andiko hili la Ayubu 1:6 kwenye Biblia ya the New Living Translation (NLT) inasomeka hivi: “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.” Kwa kuongezea, lugha ya Zaburi 82:6-7 inafanya iwe wazi zaidi na ijulikane kwamba hawa wana ni wakimbinguni, lakini ukweli huu umepotea kwenye uelewa wa Ukristo wa sasa.

 

Mungu aliwatukuza wana hawa kwa kupitia uweza wa Roho Mtakatifu. Ni kwa kupitia Roho Mtakatifu ndipo Mungu huyu Mmoja na asiye na mshiriki aliunganika ma wana wake wa kiroho ili kuiunda familia au baraza la Mungu, kama Elohim (SHD 430). Utajaji wa neno hili “wana wa Mungu” wenye Kitabu cha Ayubu usingekuwa na maana kabisa iwapo kama muundo wa kifamilia usingekuwepo kwenye baraza la elohim, na kama wana hawa wasingekuwa na mwanzo wao kwa kuumbwa au kufanyizwa na Baba. Hata hivyo, wana hawa wa roho walioumbwa wana Baba, na wana mwanzo wao kama viumbe wenye nguvu wa Baba. Mungu Aliye Juu Sana ambaye jina lake ni Eloa (SHD 433), ndiye Baba yao (Mithali 30:4-5). Kwenye Waebrania 12:9, anatajwa kuwa ni “Baba wa Roho zote”.

 

Kwa kulielezea kwa undani tukio hili la ajabu linalozunguka uumbaji wa wana hawa wanaoendelea kuwepo wa kiroho wa Eloa, na

 

jinsi wanavyounganika kwa kupitia Roho wake Mtakatifu, tazama majarida ya Jinsi Mungu Anavyofanyika Kuwa Familia (Na. 187) na Roho Mtakatifu (Na. 117) [How God Became a Family (No. 187), and The Holy Spirit (No. 117)].

 

Eloa aliweka muundo wa familia kwa utaratibu mwandamano akianzia kwanza na familia yake ya kiroho. Muundo wa familia ya mbinguni hatimaye uliowekwa kwenye muundo wa mambo ya kawaida nay a kimwili pamoja na uwekaji wa familia ya mwanadamu. Ni muhimu kuelewa mlolongo huu ambao kwao Eloa alipanga kuifanya familia yake yote, makundi yote mawili, yaani wale walioumbwa kiroho na kimwili, na kuuelewa umuhimu wa muundo wake. Aliweka kwanza familia yake ya kiroho na mpango wa wana wake ambao kwa ujumla wawe na mtazamo chanya, upendo na uhusiano wa kufundisha kwenye familia ya wanadamu, ambao waliumbwa kipindi cha mbele zaidi.

 

Waefeso 3:14-15 kwenye tafsiri ya Philips inasomeka hivi:

14 Kwa hiyo nampigia Baba magoti, 15 ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,

 Eloa alisababisha wanadamu kuumbwa kwa uwakilishi wa wana wake kwenye Baraza la Elohim uweza wa kuianzisha familia ya mwanadamu “Na tumfanye mtu kwa mfano wetu” (Mwanzo 1:26) ni usemi unaoelezea uweza huu wa uumbaji uliotolewa na Eloa kwa kupitia kwa Roho wake Mtakatifu kwa elohim kumuumba mwanadamu. 

Ni kwa kupitia kwa wana wake wa kiroho ndipo Bwana Mungu, Eloa alijifunua mwenyewe, asili yake ya kweli na Torati yake kwa wanadamu. Wakati Mungu aliposababisha kuumbwa kwa wanadamu, wana wake wa kiroho walipewa wajibu wa kuwa ni wajumbe na horo watumikiao kwenye huduma yake kwa wanadamu (Waebrania 1: 14). Kwenye Matendo 7:35-38 tunaona kwamba ilikuwa ni Malaika huyu wa Bwana ndiye aliyeongea na nabii Musa kwenye kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto na ndiye aliyewapa Torati Israeli pale Sinai. Wana wa Eloa wanapaswa kuhudumu na kusimamia maongozi ya Torati ya Baba yenye amri na maelekezo kwa mwanadamu.

 

Kwa hakika, ili kuelewa muundo wa familia ulivyo kwenye familia ya kiroho ni jambo gumu sana kuelewa sawa na kama ilivyo kuijua asili ya kweli ya Mungu Aliye Juu Sana Mwenyewe, na asili ya watoto wake wa kiroho. Ingawa inapingwa na kukataliwa na dini kongwe na za kale za Kikristo, Elohim ni jina lililo kwenye nafsi ya umoja na siko ya Mungu mwenye nafsi ya uwingi inayojulikana kama Eloa inayowataja viumbe wa mbinguni wenye mamlaka ya Mungu. Elohim anajumuisha wana wengi wa Eloa wanaounda baraza la familia ya mbinguni (Ayubu 38:4-7).

 

Ni Eloa peke yake, Baba wa uhai na Mwanzilishi wa mpango wa familia, ndiye aliye na sifa ya kutokufa na ndiye asiye na mwanzo (1Timotheo 6:16). Ni yeye tu ndiye mwenye kujua kila kitu (Isaya 46:8-10), na haonekani kwa macho ya kibinadamu (Yohana 1:18; 1Timotheo1:17), na hakuna yeyote mwenye mwili aliyewahi kuisikia sauti yake wala kuliona umbo lake (Yohana 5:37). Tazama jarida la Mungu Tunayemuabudu (Na. 2) [The God we Worship (No. 2)].

 

Eloa ni Mungu wa miungu tunayemsoma habari zake kwenye Zaburi 136:2 kusema:

Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.

 

Kwenye Isaya 46:9-10 tunasoma:      

kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; 10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.

 

Eloa ndye Mungu mwenyezi, aliye Mkuu na ni Baba wa wana wa kiroho, wakiwemo mwana wake wa kiroho aliyejulikana kwa wanadaamu kuwa ni Yesu Kristo. Masihi alimwambia Mariamu Magdalena baada ya kufufuka kwake kuwa, ufufuo aliomfanyia Mungu na Baba yake kuwa:

Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu. (Yohana 20:17)

 

kwenye Yohana 20:17, Kristo anasema kwamba yeye ana Mungu, ambaye ndiye Baba yake. Ni suala tu linaloeleweka kuwa yeye aliye na Mungu hawezi tena yeye mwenyewe kuwa Mungu. Basi ni Baba peke yake, Eloa, ndiye aliyekamilika kwa sifa ya kuwa Mungu na ndiye ambaye peke yake hahitaji msaada wala ushauri na mamlaka nyingine ya juu yake. Yeye ndiye asili ya maisha yetu sote, yaani kwa ya aina zote mbili, yaani ya kiroho nay a kimwili. Maisha na uhai viliwekwa na huyu Mungu wa Pekee na wa Kweli, Eloa, ambaye ndiye baba wa Kristo pia, na Baba yetu sisi pia (Yohana 5:26). Amefunuliwa kwetu kupitia Kristo Mwana Wake wa pekee (Mathayo 11:25-27; Luka 10:21-22). Soma jarida la TUwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Kimwili (Na. 243) [The Pre-Existence of Jesus Christ (No. 243)].

 

Eloa ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli, ambaye ndiye pekee anayestahili kuabudiwa (Kutoka 20:3; 34:14; Mathayo 4:10; Yohana 4:21-24; 1Wakorintho 14:25; Ufunuo 4:8-11; 5:13-14; Ufunuo 22:8-9). Roho wa Eloah aliwezesha wana kuwa na uwezo wa kuwa miungu wadogo kwa kuzitenda kazi zake (Zaburi 82:1-6; 1Wakorintho 8:5).

 

Imani-dhana ya Waamini Utatu kuhusu asili ya Mungu inatafsiri vibaya asili hii ya Baba na inazusha imani ya uwongo ya kumuweka Elohim kwenye mtazamo wa kuwepo kwa hypostases watatu au muunganiko wa watu watatu na kwamba wanastahili kufanyika na kuonekana kuwa wanaumilele sawa na wana hadhi sawa na mamlaka kwenye muundo huu wa kiutatu. Ni sawa na imani na mafundisho mapotofu ya Wabinitariani na Waditheisti wanayoendelea kufundisha na kuamini siku hizi kuhusu asili ya Mungu kwa kudai kwamba kuwa viumbe wawili wenye hadhi sawa ya kimungu katika Elohim mmoja. Imani na mafundisho haya ni ya makosa kwa kuwa yanatafsiri vibaya familia ya kiroho ya Mungu. Wanakataa na kupinga ukweli na uhalisia wa Mungu wa Pekee wa Kweli (Zaburi 82:1-8; Isaya 46:8-10) ikiweka familia, kuanzia kwanza kwenye chimbuko la watoto wake wengi wa kiroho, kama tunavyoona kwenye Ayubu 1:6, 2:1 na 38:4-7.

 

Dhana potofu kuhusu asili ya Mungu pia inamzuia mtu asiujue mpango wa Eloa wa kujumuisha uumbaji wa mwandamu kwenye familia ya Elohim. Ni hatima ya mwanadamu kwa mapenzi ya Eloa kuwa afanyike kuwa mmoja wapo kwenye familia ijayo ya viumbe hai wasiokufa. Wanadamu walioumbwa watapewa fursa ya kupewa uwezo wa kutokufa na kuwa pamoja na Elohim wakiwa na Yesu Kristo (Zaburi 82:6; Yohana 6:51-58; 10:34; 1Wakorintho 15:22-27).  Soma jarida la Watakatifu Kama Elohim (Na. 1) [The Elect as Elohim (No. 1)] kwa mjadala wa kina kuhusu dhana hii ya mwanadamu kufanyika kuwa mshiriki mmojawapo kwenye familia ya Mungu.

 

Majukumu kwenye familia ya kiroho

 Wana wa Eloa wanapaswa kuwa na mikakati ya kusimamia na kufundisha Sheria au Torati ya Amri na maagizo kwa mwanadamu. Tangu kipindi cha uumbaji wa Adamu na Hawa kwenye Bustani ya Edeni, na kwa maongozi na maelekezo ya Eloa, watoto wake walipewa majukumu ya kuwafundisha hawa ‘wazazi wetu wa kwanza’.

 

Maana ya neno miti ile iliyokuwepo Bustanini inatumika kama neno linalomaanisha viumbe wa kiroho. Jambo hili limechanganuliwa kwa kina kwenye jarida la Fundisho Kuhusu Dhambi ya Asili Sehemu ya 1, Bustani ya Edeni (Na. 246) [The Doctrine of Original Sin Part I The Garden of Eden (No. 246)]. 

 

Kwenye Matendo 7:35-38 tunaona kwamba alikuwa ni Malaika wa Bwana ndiye aliyesema na Musa kwenye kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto, na ndiye aliyetoa Sheria za Torati kwa Israeli pale Sinai. Huyu Mwana wa Mungu alihitimisha au kukamilisha kanuni na majukumu muhimu za kuwatumikia watu kwa maongozi na kumuwakilisha Baba yake. Ni muhimu pia kumjua huyu Mwana huyu kuwa ni nani hasa na namna alivyotumikia akiwa kama Mjumbe wa Mungu, anayetokea mara nyingi sana kwenye Agano la Kale (soma jarida la Malaika wa YHWH (Na. 24) [The Angel of YHVH (No. 24)].

 

Waebrania 2:2 Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa. 2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,

 

Kinyume kabisa na mafundisho ya Kristo, wahubiri na watumishi wa uwongo wanadai kwamba Sheria ama Torati ya Mungu haina umuhimu na maana tena na haina umuhimu kuishika kwa siku zetu hizi. Lakini tunaona jinsi Kristo alivyomjibu yule kijana alipomuuliza swali kuhusiana na jambo hili kwenye Mathayo 19.

Mathayo 19:16-19 inasema: Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? 17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. 18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, 19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

 

Kristo mwenyewe alisema kwamba hakuja kuitangua Torati ya Baba yake (Mathayo 5:17-19).

 

Waliojumuishwa kwenye mjumuiko huu wa wana wa kiroho ni yule malaika aliyeasi ambaye hatimaye alikuja kujulikana kwa jina la bilisi au Shetani na Mshitaki wetu. Huyu mwana muasi alitenda mambo na kuwaza kinyume kabisa na Mpago wa Baba yake. Kwa ubatili wake huu wa mawazo, alichukua fursa ya kuwa mshitaki na mharibifu dhidi ya Mipango ya Baba yake kwenye familia ya kiroho na kuwa na ushawishi chanya katika kuitumikia na kuiongoza familia ya mwanadamu kwenye uhusiano wa haki na wakiutakatifu na Baba yao (soma Isaya 14:12-15; Ezekieli 28:14-19). Badala ya kuwa ni chombo cha haki na utakatifu cha kuilisha na kuiendeleza familia yenye kudumu siku zote hadi ifikie kwenye kiwango kinachohitajika kwenye urithi wa vipawa au cha Baba cha kuurithi uzima wa milele kwenye muundo wa kiroho, Shetani amekuwa ni chombo cha kuleta mauti na kuwa ni baba wa uwongo (Yohana 8:44).

 

Shetani aliwekeza nguvu zake kwenye mkakati wa kuiangamiza na kuiharibu familia ya mwanadamu baada ya jaribio lake lililoshindwa la kuuharibu na kuuangamiza muundo wa familia ya kiroho. Alijaribu kukiinua kiti chake cha enzi juu zaidi ya nyota nyingine zote (wana wengine) wa Baba yake (Isaya 14:14). Anaendelea kuwadanganya wanadamu hata leo kwa kueneza mafundisho ya uwongo yanayoonekana kufanana na muundo wa familia ya kiroho na kuwazuia wanadamu wasiijue asili ya Baba yao na asili halisi ya Yesu Kristo na nafasi yake. 

 

Alikuwepo Bustanini na kuwadanganya wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, ili wafanye dhambi kwa kumuasi Mungu (Mwanzo 3:1-24). Soma jarida la Amri ya Kwanza: Dhambi ya Shetani (Na. 153) ;The First Commandment: The Sin of Satan (No.153)].

 

Pia tazama majarida ya: Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya 2, Kizazi cha Adamu (Na. 248) na Msalaba: Chanzo Chake na Maana Yake (Na. 39) [Doctrine of Original Sin Part 2 The Generations of Adam (No. 248), and The Cross: Its Origin and Significance (No. 39)] kwa kuwafanya wajadili kuhusu ulivyokuwa na maana ya ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya kwenye Bustani ya Edeni mshitaki huyu ametumia mbinu ile ile kufanikiwa kushawishi mawazo na nia za kidini za wanadamu kuendelea kufikiri hivyo hadi leo.

 

Wakati Eloa alipowatawanya watu na kuwaweka kwenye mipaka mbalimbali na kuwapa urithi, aliwapa kila mmoja wa watoto wake wa kiume uwezo wa kuongoza na kuyaelekeza mataifa Sheria au Kanuni zake, na jinsi ya kumuabudu yeye ambaye ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli, na ambaye ndiye Baba yao. Mwana wake ambaye hatimaye alikuja kuzaliwa kimwili hapa duniani na ambaye alikuwa na uweza wa kipekee wa kimungu maishani mwake, yaani Yesu KRisto, alitumwa kwao Israeli. Kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8-9 tunasoma hivi: 

Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, Alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Israeli. 9 Maana, sehemu ya Bwana ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake.

 

Ni huyu mwana wa kiroho, Yesu Kristo, aliyewekwa wakfu tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu (1Petro 1:18-20) ili kuachana kabisa na wadhiwa wake wa kiroho wa kuwa na kufanyika kuwa mwanadamu aliyezaliwa hadi kuweza kuishi maisha yasiyo na dhambi katika mwili na hatimaye kutolewa sadaka. Alipewa wajibu mzito na wakuogofya ili kuyatoa sadaka maisha yake ili kuwapatanisha wanadamu, wote wawili, yaani wana wa kiroho Mbinguni waliotenda dhambi na idadi nzima ya wanadamu watenda dhambi.

 

Kwa kuyafuata Maandiko Matakatifu tunajua kwamba wana wa kiroho walioanguka dhambini wa Eloa wana fursa ya kutubu kutokana na dhambi zao na kuikubali dhabihu iliyotolewa kupitia kwa Kristo kwa niaba yao kwa kusamehewa kwa dhambi zao.

 

Wakolosai 1:19-20 kwenye Biblia inayoitwa  Complete Jewish Bible (CJB) kuwa:

Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae; 20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.

 

Kristo alikwenda kuzimuni na kuwahubiria Malaika walioanguka dhambini na kuwekwa kifungoni huko Tartaros.

 

1Petro 3:18-19 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa, 19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;

Na kwamba ndiko alihubiri kwenye kiwango cha kueleweka na umuhimu wa kila mmoja kupitia kwenye wokovu. Kwa hiyo mapepo wanaweza kuokolewa kama walivyokuwa (na kama walivyo) walengwa kwenye huduma ya Yesu Kristo. Ili kuelewa kwa kina zaidi kuhusiana na hilo, soma jarida la Hukumu ya Mapepo (Na. 80) [The Judgment of the Demons (No. 80)].

Ni kutokana na imani ya Kristo kwa Baba yake na utii wake kwake jambo lililomfanya ainuliwe juu kwa wenzake, amavyo ni juu ya wote ambao ni wana wengine wa kiroho wa Eloa. Zaburi 45:7 na Waebrania 1:9 vinamtaja Kristo kuwa ameinuliwa juu baada ya kufufuka kwake na Baba yake. Maandiko haya Matakatifu yanasema kuwa “Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio..

 

Ukristo wa itikadi za kikale—yakiwemo na makanisa ya Mungu ya leo—wameshindwa kushikilia maana yaliyolengwa kwenye maandiko haya Matakatifu. Kitendo chao cha kuyaeneza dhana ya uwongo ya kwamba Kristo anasifa sawa ya umilele na Baba yake ni madai na mafundisho ya kipuuzi nay a uwongo yaliyochukuliwa kutoka kwenye fikra za kidunia za falsafa ya imani ya Kihellemism na Kinostiki iliyokubalika na kuaminiwa na ulimwengu mchanganyiko wa Wayunani wenye asili ya Kirumi mapema kabla ya kuja na kuzaliwa kwa Kristo kimeili hapa duniani. Kwa makosa kabisa alitangazwa kwenye imani yao kuwa yuko sawa na Baba yake kwenye muundo wa kiimani wa Waamini miungu Miwili au wa Binitariani kuhusiana na Uungu kwenye Baraza la kidini la Nicea lililoketi mwaka 325 BK. Baraza hili liligushi maamuzi ya Baraza la Chalcedon ya mwaka 451 BK ambayo yaliwaingiza Kristo na Roho Mtakatifu wa Eloa kwenye muundo wa Kiuungu. Na sasa Shetani anajaribu na kuendeleza mkakati kwenye jaribio lake na imani ya Kanisa lake lenye mchanganyiko wa Kiyunani na Kirumi ili kuharibu uelewa wote maarifa ya asili ya Baba yake na kusudi la kufanyizwa kwa familia ya Mungu.

 

Wana wa kiroho wa Mungu walioanguka dhambini wanajua ya kwamba huyu ni Mungu wa Pekee wa Kweli, ambaye ndiye Baba yao, na wanatetemeka mbele yake. Ndiyo kitu kinachowasubiria kwa ajili ya uasi wao na uvunjifu au uasi wa kanuni na mwenendho wao ambavyo kwayo inawafanya watetemeke. Yakobo 2:19 inasema: Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka.

 

Kristo haoni aibu kuitwa kuwa ni ndugu zake wa kike na wakiume wale wote wanaoitwa sasa na kuingizwa kwenye Mwili wa Kristo, kwa mujibu wa makusudi ya Baba yetu wa mbinguni. Waebrania 2:10-17 inasema:

Kwa kuwa ilimpasa yeye, ambaye kwa ajili yake na kwa njia yake vitu vyote vimekuwapo, akileta wana wengi waufikilie utukufu, kumkamilisha kiongozi mkuu wa wokovu wao kwa njia ya mateso. 11 Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake; 12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa. 13 Na tena, Nitakuwa nimemtumaini yeye. Na tena, Tazama,mimi nipo hapa na watoto niliopewa na Mungu. 14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, 15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa. 16 Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu. 17 Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye suluhu kwa dhambi za watu wake.

 

Majukumu ya Wazazi

 Kutoka mwanzo wakati Eloa alipowaumba hawa wana wa kiroho, alipanga kwa umahiri sana kueneza kwenye mamlaka ya familia ya mwanadamu kupitia kwa mume wan a mke Baraka zote za kuzaana na kuongezeka katika maisha ya mwanadamu na kulisha na kuwalea watoto. Baraka ya inayofuatana na kuwa na familia inafanya na kusababisha mwajibiko mkubwa na haipaswi kuchukuliwa kijujuu. Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kuwa wawe na uhusiano wa karibu na Mungu wa Pekee na wa Kweli, Eloa na wazijue na kuzitii Sheria na amri zake.

 

Agizo la msingi kuhusu majukumu haya ya wazazi limetolewa kwenye Kumbukumbu la Torati  6:4-9 ikisema:

Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. 6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; 7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. 8 Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. 9 Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.

 

Wazazi wachamungu wanapewa thawabu kuu kwa ajili ya mtoto mwenye busara (Mwanzo 27:46; Mithali 10:1). Msisitizo mkubwa umewekwa kwenye majukumu ya wazazi kuwaelekeza watoto wao kuzishika na kuheshimu Sheria za Mungu (Kutoka 13:14; 20:10; Kumbukumbu la Torati 11:19; Yoshua 4:6). Kwa upande wao, watoto wanawajibu na kupaswa kuwatii wazazi wao. Kwenye uhusiano huu ni muhimu sana kujua kwamba kijineno kisemacho kutii kinapoandikwa mahali pengine popote kwenye Agano la Kale kinachukulia kuwa ni kitu muhimu kwa mtu au au kile ambacho ni tabia za lazima. 

 

Eloa hakuumba mtoto wake yeyote na kisha awaangamize. Bali anaumba kutokana na tabia na asili yake, ambayo ni upendo, na anawalisha watoto wake kwa kusukumwa na upendo. Inawapasa wazazi pia kufuata mfano wake. Na ndiyo maana kitendo cha kutoa mimba ni kibaya na kinachukuliwa kuwa ni uuaji, isipokuwa pale tu inapoonekana kuwa mama atakuwa hatarini kama haitatolewa. Sheria ua Torati yake Eloa inaendeleza na kufafanua asili yake na yeye haui yeyote kati ya watoto wake. Uytoaji mimba unaofanywa kwa lengo la kuzuia tu kuzaa mtoto kunaharibu lengo safi la kijamii na dhamira njema kwenye jamii zetu.

 

Ni muhimu kwa wazazi kuyaelewa maana neno “kuabudu” na matumizi yake yalivyo kwenye Maandiko Matakatifu ili yaweze kuchukuliwa katika kuwafundisha watoto Yule anayestahili wao wamuombe dua zao na kumuabudu. Kuomba dua ni namna mojawapo ya kuabudu, jambo linalostahili kumfanyia Baba peke yake. Mathayo 6:6 tunasoma: 

Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

 

Shetani alimpeleka Kristo jangwani ili amjaribu kwa kuahidi kumpa falme zote za hapa duniani iwapo tu kama Kriisto angeinama tu chini ili kumsujudia. Shetani alikuwa anajaribu kumtia majaribuni Kristo ili atende dhambi—na angetenda dhambi kama asingesimama imara. Kristo alimkemea Shetani. Mathayo 4:10 inasema:

Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 

 

Krisssto kamwe hakuelekeza dua zake ama kumuabudu au kujitukuza mwenyewe. Kamwe hakudai kuwa yeye ni Mungu. Bali kitu alichokifanya tu ni kwamba alijiita kuwa yeye ni Mwana wa Mungu.

Yohana 10:36 inasema: je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?

 

Neno la Kiyunani linaloelezea kuabudu ni proskuneo (SGD 4352) linalotokana na neno pros, ambalo ni kuelekea, na kuneo, hadi kwenye busu. Neno Proskuneo linanekana mara kwa mara likimaanisha “kuabudu” na lina maana tofauti. Linamaanisha kufanya kusujudu. Kuonyesha kumheshimu mtu. Linatumika kama tendo la kuonyesha utii au heshima kuu.

 

Kuabudu kunaweza pia kuelezewa kwa vebu mbalimbali za lugha ya Kiyunani. Nazo ni kama:

 

Tangazo la: (1) Tendo la kumuabudu Mungu halijaelezwa popote kwenye Maandiko Matakatifu. Kitecho cha kuzitilia maanani vebu za hapo juu kunaonyesha kwamba halikuhusiana na kusifu, kwa kiasi kikubwa linaweza kuchukuliwa kuwa ni utambuzi wa moja kwa moja kuhusu Mungu, kwenye asili yake, tabia zake, njia au namna zake na matakwa yake, iwe ni kwa kuonyesha kwa nje ya moyo kwa kumsifu na shukurani au kwa matendo yaliyofanywa kwa kutambua hivyo. (2) kwenye Matendo 17:25 therapeuo, "kutumikia, kumtumikia" (kwa hiyo RV), inasema "anaabudiwa."

 

(maelezo yaliyoko hapo juu yanatokana na kamusi maarufu ya Vine's Expository Dictionary of Biblical Words.)

 

Majukumu kwenye Ndoa

 Mungu aliweka muundo wa kifamilia kwa wanadamu na kumpa kipaumbele cha kwanza mwanaume na mwanamke wakiwa ni mmume na mke tangu wale wa kwanza (Mwanzo 2:24). Kwa kujibu wa amri ya Mungu, mwanaume anapaswa kuwaacha baba yake na mama yake na kuambatana na mke wake na kuwa mwili mmoja. Kwenye kitabu cha Mwanzo 2:25, usemi wa “Mwanaume na mke wake” ni mwongozo dhahiri wa uhusiano wa mwanadamu uliokusudiwa kuwa na mwanamke. Mwongozo huu wa Mungu unapingana na ushauri wa kwanza wa Mtume Paulo kuhusu mwanaume unaoonekana kwenye 1Wakorintho 7:6, kama inavyosema, “sio kwa amri,” bali zaidi sana ni kwamba ni wazo la kwanza tu la Pauulo khusisna na suala hili. Soma pia kwenye jarida la Ndoa (Na. 289) [Marriage (No. 289)].

 

Kutoka kwenye Mwanzo 1:26-28, tunaon pale ambapo elohim alimfanya mtu kwa sura na mfano wake. Tangu kuumbwa kwa mwanadamu haikuwa tu kwa sisi kufanana na Mungu kwenye mwonekano wa kimwili na viumbe wa mbinguni au elohim bali pia ilipangwa kuwa sisi tuwe kama miungu midogo au elohim kwa mchakato wa hatua moja hadi nyingine, kwa kupewa kwanza wajibu na elohim wa kuwalisha na kuwaelekeza wale walioumbwa kwa sura na mfano wake kwenye uhusiano wa kifamilia. Tunayajua hayo kutokana na maneno ya Kristo mwenyewe alisema, “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);” (Yohana 10:34-35), akinukuu kutoka kwenye Zaburi 82:6 inakosema: Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia.

 

Kwa hiyo, sisi tunaungana na ndugu zetu wa kiroho walio elohim, kuwa ni wana wa Mungu Aliye Juu Sana. Tukiwa ni viumbe wanadamu tuliofanyika kupitia Kristo. Kristo pia anajulikana kuwa ni kaka yetu, kwa hiyo ulikuwa ni uweza wa Baba yake ambaye ni Baba yetu pia, Mungu wake ambaye ni Mungu wetu pia (Yohana 20:17), hicho ilikuwa ndicho chanzo cha kuumbwa kwa mwanadamu.

 

Warumi 8:29 inasema: Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.

 

Sisi tunajulikana pia kama ndugu wa malaika wote waliobakia kwenye ulimwengu wa roho wa baba yetu wa Mbinguni.

 

Ufunuo 12:10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

 

Amri ya Mungu kwa mwanaume kwenye Mwanzo 1:28 ilikuwa ni kuzaa na kuongezeka kuijaza Nchi kwa njia ya kuzaa kunakotokana na mpangilio wa kifamilia ulioonyeshwa kwenye Mwanzo 2:24 mpangilio wa kuwa mume na mke. Je, ni kwa nini Mungu alimpa mwanaume amri hii? Mwanaume alitakiwa kujifunza kutokana na yaliyopo kwenye nchi anayoikaa duniani ambayo alitwaliwa kutoka kwayo, chini ya Sheria za Mungu, somo la kiroho kuhusu Ufalme au familia ya Mungu. Mfano wake ukiwa ni hizi Siku Takatifu ambazo ni siku za hapahapa duniani na nyakati zake ambazo hutufundisha masomo makubwa sana yanayoonyesha na kuashiria hatua ya Mpango wa Mungu katika kuwaleta watoto wa kimwili wa Mungu kwenye familia ya kiroho ya Ufalme wake. Kwa kuwa Mungu alianzisha utaratibu mkamilifu wa kijamii wa mume na mke, unaashiria taswira ya uhusiano uliopo kati ya Kristo na Kanisa ulioonyeshwa kwenye waraka kwa Waefeso ambako inasema hivi.

 

Waefeso 5:22-33 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. 25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. 29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. 33 Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.

 

Soma majarida ya Torati na Amri ya Saba (Na. 260), Mithali 31 (Na. 114) na Wimbo Ulio Bora (Na. 145) [Law and the Seventh Commandment (No 260); Proverbs 31 (No. 114) and Song of Songs (No. 145)].

 

Kutokana na Maandiko haya Matakatifu tunaweza kujionea wazi kwamba Yesu Kristo aliwajibika kwenye uongozi wa Kanisa, ambalo ni sehemu ya Mungu, familia ya Baba yetu. Wajibu wa wanaume ni kuiongoza familia wakifuata mfano wa Kristo. Kristo anatajwa pia kuwa ni Adamu wa mwisho (1Wakorintho 15:45,47). Hii inamaana kwamba Adamu wa kwanza alikuwa na majukumu hayahaya, ila alishindwa kuyatimiliza.

1Wakorintho 15:45-47 Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha. 46 Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho. 47 Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni. Thus it is written,

 

Ni kwa kuwa Adamu alishindwa kuongoza sawa na maelekezo aliyopewa kwa hiyo ilimpasa Kristo aje na kuyatimiliza majukumu hayo. Kitendo hicho kinaelezwa kuwa ni siri kubwa na Mtume Paulo.

 

Waefeso 5:29-32 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa.

 

Adamu wa kwanza alipaswa kumchunga mke wake kwa namna sawa na vile Kristo alivyolitunza Kanisa lake la kweli la Mungu. Adamu wa kwanza alishindwa, bali Adamu wa pili amefanikiwa, sawa na tunavyojionea kwenye Mathayo 16:18.

Mathayo 16: 18 …. nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

 

Kristo ni mfano wetu wa uongozi tunapoelewa kile ambacho wanaume wanachokitarajia kukifanya kwenye mahusiano yao mema na familia zao.

 

Katika Efeso 5:23, tunaona kwamba mwanaume ni “kichwa cha mkewe”, ambavyo inamaanisha kwamba ana mamlaka yote mawili pamoja na jukumu kwa familia yake yote, akianzia kwa mke wake. Ni kwa bahati sana, kuna wanaumme wengi wanaoonyesha mamlaka yao lakini pasipo kuonyesha maana yoyote ya uwajibikaji. Watu hawa wachache wamefanyika kuwa sababu ya wanawake wengi kudai haki ya uhuru na kutotii miwajibiko yao na kuuasi utaratibu wa muwajibiko wa kifamilia. Matokeo yake ya mwisho ni kwamba familia inapata mateso kwa njia moja au nyingine, pamoja na jamii nzima yote kwa ujumla. Ongezeko la kiwango cha matukio ya kuachana na kupeana talaka kunaonysha mporomoko wa maadili kimataifa. Uamuzi wa kuachana ni machukizo na unamadhara makubwa kwa watoto wetu na kunawasababishia kuteseka yakiwa ni matokeo yatakayoishia kukumbukwa maishani mote.

 

Kutokana na 1Wakorintho 11:3 tunaona kwamba Mungu, Baba yetu alimpa mamlaka Kristo, na Kristo amewapa mamlaka haya wanaume, na kwa hiyo wanaume wanawajibika kuwapangia kazi na mambo yakufanya yaliyo wajibu wao wanawake ili kukamilisha malengo ya namna zote na matarajio yanayohitajika kwenye familia (sawa na isemavyo 1Petro 3:7). 

1Wakorintho 11:3 Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu. [yaani Baba].

 

1Petro 3:7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.

 

Inawapasa wanaume wagawe majukumu kama anavyofanya Mungu na Kristo wake. Haitakiwi mwanaume azembee kwenye wajukumu yote. Adamu alizembea kuwajibika kwenye Bustani ya Edeni. Hawa akaachwa akabiliane kujadilina na nguvu ambayo alikosa uwezo wa kuishinda. Matokeo yake “milango ya mauti” iliimshinda mwanamke na kwa wanadamu wote kwa ujumla (Mwanzo 3:1).

 

Wanaume wanapaswa kuwaongoza wake zao na kuwafundisha watoto wao. Kwenye jukumu hili wanaume wanatakiwa kuwafundisha watoto wao kwa namna ya mfano na kuitunza Kalenda ya Mungu kiusahihi na kuwaelezea maana na umuhimu wa kutunza Sabato, Miandamo ya Mwezi, Sikukuu zote na Siku nyingine Takatifu zilizoamriwa na Mungu.

 

Hebu na tuangalie sasa uanzaji wa ndoa kama ulivyotiliwa mkazo na Yesu Kristo  (Mathayo 19:1-12).

Mathayo 19:1-12  Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng'ambo ya Yordani. 2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko. 3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu? 4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, 5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? 6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe. 7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha? 8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. 9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini. 10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa. 11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa. 12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.

 

Kwenye aya ya 5, Kristo anasema kwamba wanaume na wanawake wanatakiwa waishi maisha yenye uhusiano wa mke na mume mmoja tu “na wawili hawa watakuwa mwili mmoja”, sio watatu au zaidi ya hawa wawili, na ni kwenye mambo ya ndoa tu, “ataungana na mke wake”. Kristo anafafanua pia kwamba mwanaume na mke wasiendelee tena kufanya mambo yao kiufichouficho na ubinafsi na wanapaswa sasa kuishi kwa mtindo wa watu wenye hisia mbili, kama inavyosema kwa wazi aya ya 6 kwamba: “nao sio wawili tena bali ni mwili mmoja”. Na kwa kuwa ni kifo tu ndicho kitakachomtenganisha mtu kutoka kwenye kifungo hiki cha kimwili, na ndiyo maana ndiyo maana umewekwa utaratibu huu wa mke na mume mmoja na Kristo.

 

Kwa ajili hii, Mungu ameamuru kwamba kila aina yoyote ya muunganiko wa kingono nje ya ndoa hii iliyohalali ni dhambi na uasi na ni kinyume kabisa na maisha wanayopaswa kuishi kwenye familia ya Mungu. Iwapo kama mtu atakiuka na kuiasi Sheria hii ya Mungu na kuamua kuuandama kukahaba au uzinifu, matokeo yake yako wazi kwa kila mtu, ambapo kwamba ataumbuliwa kwa kukumbwa na magonjwa na kuendelea kuyaandama maisha yasiyo ya uaminifu tena kwenye ndoa kiasi cha kufikia kufanya matendo ya kuzalisha watoto wa kuuza kwenye masoko ya magendo, na matukio mengine ya kusikitisha ya utoaji mimba na kuua vichnga. Moja wapo ya mapatilizo an madhara ya kuendekeza ngono za uzinifu nje ya ndoa na moja ya sababu za maadili kupua kwenye  jamii na uharibifu mkubwa imeelezewa vizuri kwenye makala ya Familia kwenye Biblia ya the International Standard Bible Encyclopedia (ISBE) kwenye kifungu kinachoiongelea amri ya 7 ikisema. 

“Wakati iliwa ni kweli kwamba kwenye sheria za uhusiano wa kingono katika Israeli kwa mtu anayetenda dhambi hii nje ya mahusiano yaliyopo ya kifamilia alitendewa vikali ili awe mfano kwa wote, na tena tunapokumbuka ni mapema kiasi gani maishani ndoa ilifanyia katika siku hizo za kale, na pia uchumba kwenye umri wa utoto ulivyochukuliwa kuwa ni kitu kitakatifu sawa tu na kama ilivyokuwa ndoa, tunaona kwa sasa juhudi za kuifuta amri ilikuwa iko kwenye kiwango cha juu cha kimataifa ingawa ni kitu kilichosaidia kwa kiasi kikubwa kuzilinda familia. Familia ni taasisi iliyoanza aiku nyingi sana nay a kwanza na inayomfanya mwanadamu kuwa-na uwezo mkubwa na kutakasika sana. Ni kwa taasisi hii ndipo amri hii inasimama kuisimamia. Inawazuia watu wasiivunje na kumfanya mtu aondolewe na kutengwa mbali na uharibifu na upweke. Hebu fikiria jinsi watoto wote wanavyozaliwa, na unataswira kiwango kidogo alichonacho cha unyama ambacho mambo yote yanayohusu majukumu ya kijamii ya kibaba yakiondoka, na ikiwa hata yale ya umama yakipungua kwa kufanya malezi na uangalizi wa kawaida tu katika kipindi kifupi tu kijacho ns kumuacha akiwa ni kichanga kisicho na msaada tena. Hebu na ujiulize sasa kwamba ile dhana ya kuwa ndoa itakuwa ni kitu cha watu wote na kwamba watoto wanaozaliwa kwenye ndoa wanapaswa kushikamana nayo kwa umakini mkubwa nawe sasa una mbingu mpya na nchi mpya kwenye kupapatikia ngono ya wanadamu wasiojali.”

 

Kwa mujibu wa utaratibu wa mafunzo wa Mungu wa mambo ya kawaida ya kimwili yanayowakilisha mambo ya kiroho, maongozi ya kifamilia waliyopewa wanadamu yanakuwa ni mafundisho pia yanayoelekea uhusiano wa kiroho ulio kati ya Malaika walio na umoja na Baba na hadi kwake.

 

Mungu amempa mwanadamu wajibu wa kuzaana na kuongezeka: Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi (Mwanzo 1:28). Kwa hiyo, kwa ajili hii, mwanaume ana wajibu mkubwa wa kuieneza na kuikuza familia ya Mungu kwa kujifunza uhusiano wa kibaba ba kiumama katika kuwalisha watoto, kuwafundiisha Sheria za Mungu na kuwaongoza wafuate njia hiyohiyo ya kuwafanya watoto wao kuwa wazazi na mababu wazuri kutoka kizazi kimoja hadi kingine wakiwa kwenye malezi ya ndoa ya baba ba mama mmoja.

 

Hebu na tuone sasa uhusiano wa kila mmoja wao kama Mungu alivyokusudia kwenye uumaji wake wa vitu.

 

Jukumu la Baba

Jukumu la baba kwenye familia ni kuwa kama mwakilishi wa Mwenyezi Mungu na Baba. Wajibu wake ni kuwa mleta mahitaji na huduma zote kwa mahitaji yote ya kifamilia, kuweka mahusiano mema na kusimamia masuala yote ya kiroho.

 

Sio jambo dogo kama baba atakataa kutoa mahitaji kumhudumia mke wake na watoto, kama tunavyoona kutoka kwenye makemeo ya Mtume Paulo kuhusu wale wasiojali kuhudumia familia zao kwa kuwapatia mahitaji yao.

 

1Timotheo 5:8  Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

 

Hii inaonekana pia kwenye madhihaka ya Sulemani anapomdhihaki mwanaume mvivu akimhamasisha awe mchapakazi kwenye Mithali 6:6-11.

 

Wakati majukumu ya mleta mkate yanapotolewa kwa baba hapo Mungu alupomwambia Adamu kuwa atapata mkate kwa jasho uso wake (Mwanzo 3:19), anawajibika pia na hawezi kukataa ama kupuuzia utoaji wa huduma za kiroho kwa familia yake. 

 

Kabla ya kuwekwa kwa huduma za kikuhani katika Israeli, baba alikuwa na jukumu la kutoa dhabihu za wanyama kwa ajili ya familia yake, kama tunavyouona mfano wa Ibrahimu kwenye Mwanzo 12:8 na kwenye Ayubu 1:5. Akiwa kama mkufunzi-mwenza pamoja na mama wa watoto, baba amepewa jukumu kubwa wa kuiongoza familia kwa kuifundisha Sheria na maelekezo au kanuni za Mungu (Kutoka 12:26-27; Kumbukumbu la Torati 6:6-7; Mithali 22:6; Waefeso 6:4).

Kumbukumbu la Torati 6:6-7 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; 7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.

 

Waefeso 6:4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

 

Mithali 22:6  Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

 

Kiongozi wa kiroho, ambaye bi baba, ana wajibu kama mlinzi wa kiroho wa kuwaelimisha dhidi ya matendo maovu na tabia za dunia zinazofanyika na kuonekana kuwa za kawaida na kuchukua kipaumbele kwa watoto wetu na marafiki zao, wanapokuwa wanatenda mambo yaliyo kinyume na maelekezo ya Torati ya Mungu. 

 

Warumi 16:19 Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya.

 

Ikiwa tutakuwa hatuna hatia kwenye mambo mabaya na kuwafundisha watoto wetu hivyohivyo ndipo itatupasa kuwakataza wasijihudhurishe kwenye kila aina ya mambo ya burudani kwenye vituo vya runinga, michezo ya kuigiza au picha za video na kuangalia wavuti za Intanet zilizo kinyume na Sheria za Mungu. Ni rahisi kutumia vyombo vya habari na mawasiliano vya kisasa na maonyesho ya burudani na kuvifanya mbadala wa wazazi, lakini hata kama jumbe zake zikiwa murua, kila moja ya hizi zinapoingia bado zitafanya mchosho kwenye tabia za mtoto. Soma jarida la Mitindo ya Ibilisi (Na. 42) [The Devil's Designs (No. 43)].

 

Kwenye jukumu hili la kuwa kiongozi wa kiroho pia kunakuja na wajibu wa kuwaadibisha watoto. Tunajifunza kutoka kwenye Zaburi na Mithali kwamba watoto hawana asili ya kurithi mambo mema, na kwamba kwa asili wana tabia tafaruku za kupenda kufuata tabia na matendo maovu kama ilivyo tabia iliyoko kwenye kila mwanadamu. Daudi alikiri kufanya dhambi hii asilia ya kibinadamu ambayo ilianza kutoka kipindi cha kuzaliwa kwake.

 

Zaburi 51:5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.

 

Aya nyingi zilizo kwenye kitabu cha Mithali zinalitaja hitaji na umuhimu wa kumuonya na kumkanya mtoto aziache njia zake mbaya za dhambi.

 

Mithali 22:15  Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

 

Mithali 23:13-14  Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.

 

Kwa kuwakanya watoto wetu kwa kutumia fimbo ya kuwakanyia tunayotakiwa kuwapiga kwa upendo basi sio tu kwamba tutakuwa tunayaepusha maisha yao au uhai wao usiingie kaburini kabla ya umri wao, bali pia tunakilinda kizazi chetu au hata na wajuu zetu pia.

 

1Samweli 3:13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye hakuwazuia.

 

Kila mtoto anatakiwa afundishwe kwamba anatarajiwa na wao na pale ambapo mipaka hii inawekwa, ni sawa kama baba yetu wa mbinguni anavyotufanyia sisi kwa kutupa Sheria zake. Mara tu baada yam toto kutahadharishwa juu ya viwango hivi ndipo ahdabu inatakiwa itolewe, kwa ajili ya kukiuka na nilazima ajulishwe kwanza na aliue kosa lake, vinginevyo mtoto atakuwa na tabia ya kutoiogopa haki na kuwaheshimu walio na mamlaka. Kumkanya mara kwa mara kutamfanya ajue kuwa Baba yetu aliye Mbinguni anamaanisha kile anachokisema, na kwamba hafanyi hukumu isiyo ya haki na kumuonea mtu. Kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu ni kwamba, ili kuruhusiwa na kushika njia yenye upinzani mdogo pale maonyo yanapotakiwa kufanyika, ni chanzo cha kuchukizwa kwa watoto wetu. 

 

Mithali 13:24 Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.

 

Ni wazi kabisa kwamba baba anawajibika kuwazuia watoto wasitende dhambi na tabia za namna hiyo kwa kuwaadhibu.

 

Kwa mfano tunaojifunza kwenye kitabu cha Waamuzi ambao tunaona kilichotokea mababa wachamungu waliposhindwa kuwafanya watoto wao wamche Mungu.

 

Waamuzi 2:10-22 inasema: Tena watu wote wa kizazi hicho nao walikusanywa waende kwa baba zao; kikainuka kizazi kingine nyuma yao, ambacho hakikumjua Bwana, wala hawakuijua hiyo kazi ambayo alikuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli. 11 Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali. 12 Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika.13 Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi. 14 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui zao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao. 15 Kila walikokwenda mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana. 16 Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara. 17 Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo. 18 Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua. 19 Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi. 20 Basi hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akasema, Kwa kuwa taifa hili wamelihalifu agano langu nililowaamuru baba zao, wala hawakuisikiliza sauti yangu; 21 mimi nami tokea sasa sitalifukuza taifa mojawapo la hayo aliyoyaacha Yoshua alipokufa; 22 ili kwa njia ya hayo nipate kuwajaribu Israeli, kwamba wataishika njia ya Bwana kwenda katika njia hiyo, au sivyo.

 

Katika tawala za dunia yetu leo, Ukomunisti, Usoshalisti na hata na Udemokratiki/Urepacliki vimeipa Nchi wajibu wa kuwaelimisha watoto walio kwenye mataifa yao, na wameenda hatua zaidi kwa kutumia sheria ili kudhoofisha wajibu huu wa baba kwenye familia kwa kumuondoea mamlaka yake kwa watoto wakiwa kwenye umri mdogo. Kitendo hiki kimeondoa jambo la msingi na muhimu kwenye jamii na kuliweka mbali sana na familia na kuwaweza karibu na mtu mwingine. Machapisho yetu, vyombo vya habari na hata shule zetu vimekazana sana kuwekeza dhana hii potofu ya kila mtu kuwa bora na hahitaji wa kumuonya, na huku serikali zetu zikisaidia mkakati huu kwa kupitisha sheria zinazolenga kulidhoofisha wajibu huu muhimu wa baba na mama kwenye familia. Matokeo yake, hesima na utiifu wa watoto kwa wazazi wao umepungua, huku kukiacha ubaradhuli mkubwa wa kimatakaba ya watu kwenye taifa, licha ya kihoro kikubwa kilichofanyika kutokana na mtenganisho mpangilio maalumu wa majukumu ya kifamilia na utaratibu aliouweka Mungu kwa viumbe wake.

 

Kwa uasi huu ulioongezeka dhidi ya uadibishaji majumbani, ongezeko la uzembe na ukengeufu vinajitokeza, ambavyo ni matokeo ya kuonbgezeka kwa kiwango cha upungufu wa utajiri au mali zilizotunzwa kwa ajili ya watoto kwa kazi za mikono ya baba zao na babu zao. Ni kizazi kidogo tu kilichopo na mamlaka ya mababa zilizopotea, na jamii inaanza kupungua nguvu zake kwa kwenda chini. 

 

Maandiko ya Charles de Ribbe kwenye kitabu chake cha Le Play’s studies kwenye sehemu aliyoiandika kuhusiana na mwili wa binadamu anaweka msisitizo linganifu wa kizazi hiki cha familia iliyopungukiwa na mamlaka kamili na serikali zetu zinazounga mkono hali hii akisema.

 

“Kama tukirudisha mamlaka kwa baba, basi tutairudisha upya huduma ya Mungu kwa utaratibu wa muda nfupi…. Kadiri muda unapopita zaidi, ndipo tunapojua kwamba ni muhimu kurudisha mamlaka kwenye familia. Haiwezekani kuiweka serikali bora kwa kutumia kanuni zenye makosa zilizofanywa na wanadamu. Kwenye nchi iliyo na huzuni ambayo tunajikuta sisi wenyewe, wokovu unaweza tu kuja kutoka kwenye mamlaka ile iliyomahiri na iliyoungana, ambayo inaheshimu sheria asilia, na kubakia tiifu kwa watumishi wake saidizi. Ni mamlaka ya kifamilia tu ndiyo inaweza kuhitimiliza hilo ambalo ni kipaumbele na bora zaidi kulazimisha kila mamlaka ya watu iliyoko.”

 

Maandiko Matakatifu yanaweka wazi kwamba mipakai ya mamlaka imewekwa na Mungu na ni ya muhimu katika kuimarisha familia na nchi.

 

Warumi 13:1-7 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu. 3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake; 4 kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu. 5 Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri. 6 Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo. 7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima.

 

Onyo kutoka kwa Mungu linakuja kwa kupitia nabii wake Malaki kuhusu kizazi hiki cha wanadamu.

“Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya. 6 Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.” (Malaki 4:5-6)

 

Ni wazi kabisa kutokana na aya hii kwamba mababa na watoto wao katika siku za mwisho watashindana na kuchukiana na watapoteza mwelekeo wa uhusiano wao ambao uliwekwa na Mungu kwa kuzishika Sheria zake, na kwamba nabii Eliya alitabiriwa kuwa atakuja na ataileta kweli hii ya muundo wa kifamilia na kuurudisha tena

 

Maisha ya baba ni mfano wa kile watoto wanachotakiwa kufanya na kwamba mabinti wanatakiwa kuomba kuwapata wa kuwaoa. Mwanamume ni nguzo ya mamlaka kwa familia na ni mfano wa kweli wa Mwenyezi Mungu, ambaye ni Baba wa wote wenye mwili. Baba kwa mamlaka aliyopewa na Mungu, ni muhusika wa usalama wa maisha ya watoto wake na ni mhusika muhimu kwenye unusurishaji wa maisha, ni kama Mungu Baba anavyotushughulikia wakati wote. Sambamba na hilo, watoto wanakuwa wametakaswa kutokana na busara yake na kwa mafundisho ya Torati (2Nyakati 13:18; Yohana 17:19; 1Wakorintho 7:14).  Yeye ni mfano wa Mungu Baba wa wote na anatakiwa aenende kwa mfano wa sifa hii akiwa ni mwakilishi, kama mhusika na ustawi wa maisha na mhusika kuhakikisha ustawi wa maisha hayo kwa kuwalea kwenye kumjua na kumpenda Mungu na baba wa Milele. Watoto hawa wataonekana kuwa ni taswira njema kwa muumba na baba yao kwa maisha ya mfano waanayoyaona kwa  baba zao. Soma jarida la Ukristo na Malezi ya Watoto (Na. 186) [Christianity and Childrearing (No. 186)].

 

Jukumu la Mama

Jukumu la mama ni yeye ndiye anayenyonyesha na ndiye mtu ambaye uhai wa mtu unaanzia. Baba na mama ndiyo wanaowezesha kupatikana kwa watoto, ni mfano wa kama Baba na Mwana wake walivyoumba mtu hapo mwanzo. Mungu akasema, “Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.” (kutokana na Mwanzo 1:26-27). Kila mtoto aliyezaliwa ameumbwa kwa mfano na sura ya baba na mama yake wa kimwili  

 

Kwenye Yohana 1:3-4 inaongelea kuhusu wana wa Eloa, ambaye ni neno la Mungu, Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. 4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.(LITV). Kama Baba Mungu alivyompa uhai mwanadamu kupitia Neno, ndiposa pia kwamba baba ni mtoa uzima anayepitia mwili wake kwa watoto kupitia kwa mama. Kisha mama anachukua jukumu kubwa la kumpa uhai mtoto kwa kumbeba kwenye mimba tumboni kwa kipindi chake cha kuwa kiumbe cha tumboni, na kuendelea kuaribu mkubwa kwa hiki kiumbe kichanga ambacho kwacho anatakiwa akitunze hadi kipate uzima. Na mara anapozaliwa tu, ndipo anakuwa na jukumu la kuhakikisha anamtunza kwanza na anafanya hivyo kwa kumnyonyesha mtoto na kumlisha na kumchangamsha akihakikisha kuwa mtoto anakua akiwa na hali njema ambaye hatimaye anaweza kumrithi au kuchukua mahala pa baba yake au mama yake kwenye kazi hii ya majukumu ya kiuongozi ya uzaaji na ufundishaji kama ilivyofanyika kwenye familia yao.

 

1Timotheo 5:14 Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu.

 

Mithali 29:15 Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

 

Kutokana na fungu hiki la maandiko la kitabu cha Mithali tunaona kwamba ni wajibu wa mama kuelimisha watoto washike Sheria za Mungu kama sehemu ya malezi ya mtoto. Akikosa kufanya hivyo atajiletea aibu hatimaye.

 

Kwenye miaka ya mwanzoni ya maisha ya watoto, baba humsaidia mama kwenye majukumu ya utunzaji na kumlea mtoto sambamba na kuwa mshauri na kuwa chanzo cha kuitia familia. Kadiri watoto wanapoendelea kukua na kuendeleza jukumu hili la kielimu ndivyo itakavyokuwa pia kwamba watoto watakuwa wakivutiwa sana na baba yao zao na dada zao na mama zao. Kila maendeleo yam toto yatashamirishwa na umoja kati ya baba na mama. Kuna mengi ya kufaidika kwenye uimara na ulinzi wa maisha ya watoto kwa kushuhudia upendo wan je na kushuhudia matendo ya mume anavyomfanyia mkewake na akifanya hivyohivyo kwa kumletea zawadi na kumuonyesha upendo kila siku kunaweza kuwafanya wengine wajione kuwa ni wa muhimu na waaina yake na wanapendwa.

 

Sambamba na hali hii ya kushirikishana majukumu ya kuwalea watoto, mama/mke pia anawajibu wa kuyatunza na kusimamia mambo ya nyumbani kwenye familia yake, ambayo ni pamoja na kuweka vitu kwenye mpangilio wa kupendeza na kuandaa chakula chenye virutubisho na afya njema na kwa mujibu wa maagizo ya Torati na Sheria za Mungu. Anamsaidia pia mume wake kwenye masuala ya utoaji zaka, kuzitii Sheria na Torati ya Munguna maandalizi yenye kuhakikisha kuwa wanazitunza Sabato za Mungu vizuri na kwa utakatifu wake. Soma jarida la Jukumu la Wanawake wa Kikristo (Na. 62) [Role of the Christian Woman (No 62)].

 

Jukumu la Watoto

Majukumu yam toto wa kiume na wa kike ndiyo yanayowafanya hatimaye na wao wafanyike kuwa baba na mama, na hatimaye wawe babu na bibi. Ni mchakato unaowapelekea wawe wanafunzi kwanza na hatimaye kuwa waalimu. Kwa namna hiyohiyo wanadamu wanafundishwa na Mungu ingawaje watoto hawa wa kiroho au elohim haya wafanyike kuwa wasaidizi wazuri, yaani elohim. Hii inaweza kuwa ni taswira kwa jukumu la wengine, yaani anaweza kuwa ni kaka yake mkubwa au dada yao mwenye mamlaka yanayoendelea kutoka kwa wazazi wao ya kuwasaidia kuwaelimisha wadogo zao kwenye familia yao. Wakati mamlaka haya yaliyotolewa kwa kaka au dada mkubwa yanapotumiwa vibaya kwa kuchukuliwa kijuujuu bila kutilia maanani au hata yanapodhalilishwa, yanaenda sambamba na kitendo cha kuwaadhibu wana wa kiroho wa Mungu wanapoasi. Kiongozi mkubwa wao anapokuwa mzembe kwa kupuuzia na kutotilia maanani mamlaka yachukue mkondo wake kwa kiwango cha kumaanisha kabisa, inaweza kufananishwa na jukumu alililolifanya kaka yetu mkubwa Yesu Kristo.

 

Baba yetu wa Milele anapenda utii (1Samweli 15:22). “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu”. Na anapendu kuwa waonyeshwe utii mababa na wamama kutoka kwa watoto wao moja kwa moja ameagiza hili kutoka kwenye Amri ya Tano (Kutoka 20:12 na Kumbukumbu la Torati. 5:16, sawa na Waefeso 6:2-3).

 

Kutoka 20:12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

 

Kumbukumbu la Torati 5:16 Waheshimu baba yako na mama yako; kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

 

Kwa ajili ya asili ya kimaumbile iliyopo kwenye upendo unaoendelea kwa mtiririko ukitokea kwa Baba kwenda kwa watoto wake, umuhimu wa Amri hii ni mkubwa sana kuliko kazi ya wazazi kwa watoto wao.

 

Baba ametajwa kwanza hapa kwenye mifano hii miwili, ila mama ametajwa kwenye Mambo ya Walawi 19:3:

Kila mtu na amche mama yake, na baba yake, nanyi mtazitunza Sabato zangu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.  

 

Kwenye aya zote tatu, baba na mama wanachukuliwa na kuonekana kuwa wako sawa. Baraka za mama ziko wazi, na yeyote anayemtii na kumheshimu baba anazipokea sawa na kwa kumfanyia mama. Yuko sawa na anapokea stahili sawa za kuheshimiwa kulikoamriwa kwenye amri ya Mungu.

 

Agano Jipya pia linasisitiza kuwatii wazazi kufanywe na watoto wao.

Waefeso 6:1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

 

Wakolosai 3:20 Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.

 

Soma pia jarida la Torati na Amri ya Tano (Na. 258) [Law and the Fifth Commandment (No. 258)].

 

Amri hii ya Mungu ya kuwaasa watoto wawatii wazazi wao kwa ahadi ya kuongezewa siku zao hapa duniani, Mungu anatuagiza hata sisi pia. Mapatilizo ya kumuasi Mungu kwa kuidhihali Amri hii nay a kutowatii wazazi wetu ni maisha yetu kufupishwa hapa duniani. Kumuonyesha mzazi kutomtii, kwa Mungu ni dhambi na kosa bay asana.

 

Kutoka 21:15 Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa.

 

Utii na heshima iliyoagizwa wafanyiwe wazazi, ndyo hiyohiyo pia iliyoamriwa kufanyiwa mababu na mabibi wakubwa.

 

Mambo ya Walawi 19:32 Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana

 

Wakati kijana anapokoacha kutii na kujionyesha kwenye jamii kuwa anamajivuno au kuzidharau sheria kutowaheshimu wala kuwatii wanaostahili kupewa heshima na wazee ndipo jamii isiyojali na isiyo na utaratibu inajikita hapa duniani.

Isaya 3:5 Nao watu wataonewa, kila mtu na mwenziwe, na kila mtu na jirani yake; mtoto atajivuna mbele ya mzee, na mtu mnyonge mbele ya mtu mwenye heshima.

 

Jukumu la Bibi na Babu

Mababu na mabibi wana majukumu ya kuiwezesa familia iendelee vizuri na kuiefanya iendelee na bidii ya kuziheshime Amri na Sheria za Mungu sawa na mazingira waliyolelewa kwayo na kufundisha. Wanawajibika kuifanya familia ijikite na kuendelea kuzipenda Sheria za Mungu ili kuifanya isisobwe wala kuyumbishwa na mawimbi mengine ya kimafundisho ya uwongo ya kidini kwa pande hii hadi ile nyingine na desturi au mapokeo ya wana wa dunia hii.

 

Mababu na mabibi hawa wana wajibika kuhakikisha kwamba watoto wao wanaendele kudumu kwenye njia nyembamba na kuwaongoza watoto wao kwenye maongozi ambayo vizazi vyao vilivyopita walilelewa kwayo.

 

Kwenye kizazi cha hivi karibuni aha jamii za kimagharibi za Kimarekani na ongezeko la famila kubwa za watu wanaoishi pamoja na kutembeleana, watoto wameanza kujitenga na wazazi wao mara tu baada ya kufikia umri wao wa ujana. Wakati jamii inapochukua hatamu za familia zao, watoto wetu watapelekwa mbali mashuleni kwa ajili ya kupata elimu ya juu, ambako wataanza mchakato endelevu wa kuwatenganisha na maisha ya kifamilia ambayo ndiyo ilikuwa kiini cha na msingi wa kumfundishia Sheria za Mungu. Utaratibu huu unaoanza na kuchukua hatamu hatimaye unaendelea hadi kwenye kipindi cha ajira ya mtu, na hata kama ajira itakuwa ni ya kwenye jamii ile ile. Mwajiriwa anakuwa ndiye wa kulaumiwa au kuondolewa wakati matatizo yanapotokea kwenye kazi yake ya wakati huo. Na ndipo anatafuta maeneo mengine ya kupata ajira mpya au kujiajiri mwenyewe, na hapo ndipo anaweza kuichukua au anasiweze kuichua familia yake na kwenda nayo pamoja naye. Wakati mwingine mtenganiko huu wa familia na baba unachukua kipindi cha miezi kadhaa, kisha unachukua miaka, hatimaye inafikia hata utelekezaji na hatimaye unaishia kwenye kuacbana na kupeana talaka ambayo inaigawa katikati hata familia ya watoto wengi yenyewe.

 

Kwa kukosekana familia za wengi kuishi pamoja kwenye jamii zetu ambayo ndiyo umti wa mgongo kwenye ukoo, kabila, na hata taifa, ndyipo tunaposhuka chini kwenye maadili ya kupendana na kuzua chuki na hali ya kuwa watu tuio na heshima na adabu, jambo ambalo limeonywa sana kwenye Isaya 3:5. Kweye familia zinazokaa pamoja kwa kundi watu wake mali na raslimali zote stahiki huwa chini ya mamlaka ya mababu na wanaacha wafe wakiwa mbali na watoto na wajukuu zao ambao walikuwa wakiwategemea. Na kwa kuwa walikuwa wanakosa upendo na taabu zilizosababishwa na kizazi chao, na kuamua kuondoka na kwenda mbali siku za mwisho huku waakiwaacha watoto waliowazaa kwenye nyumba za ndugu zao wa zamani. Kwenye mifano kadhaa mingine kutokana na udhaifu wa akili na kimawazo na hali mbaya ya kiafya, masuala mengine ya kiuangalizi kama vile vifaa vya kulishia vinatakiwa wasaidiwe, bali dhana kuhusu wazee walioko kwenye jamii zetu kuonekana kama wasio na umuhimu na kero kwenye familia za kimakundi inaendelea kukua zaidi na zaidi na kuonekana kuwa ni kitu marufu. Madhara yanayotokana na kupuuzia kuishika Amri ya Tano yanazidi kujitokeza na kuonekana kila mahali na siku za kuishi watu hapa duniani zinazidi kupungua katika kila aina ya jamii za watu ambazo zinaendelea kuipuuzia na kuivunja Sheria hii ya Mungu.

 

Urudishaji mtazamo wa kuwaheshimu wazee walio kwenye familia zetu kwa kuwajali na kuwahudumia wazazi wetu wakiwa kwenye miaka yao ya mwisho ya kuishi kwao hapa duniani kutafanyika kwa kuruhusu utamadunishaji ulio kwenye Sheria na Amri za Mungu uendelezwe kutoka kizazi kimoja hadi kingine, na kuweka msisisitizo zaidi kwa watoto wawatii na kuwaheshimu walio kwenye mamlaka kuanzia viongozi na wakubwa wao na kwa Mungu.

 

Hitimisho

Majukumu haya ya kila mmoja kwenye utaratibu wa familia aliouweka Mungu yana maana tu na mashiko kwa watoto wake wa kiroho na kimwili waliochaguliwa kwa mujibu wa Torati yake. Wakati mwanadamu kwa ujumla wake anapoishi kinyume na maelekezo ya Baba yetu wa mbinguni, fikra hii huonekana kuwa ni jambo lisilowezekana kabisa kuifikia. Msingi wake unapaswa kwanza ujengwe imara kwenye maoongozi ya Torati au Sheria za Mungu, pamoja na mwanaume aungane na mkewe na kuwa mwil mmoja na hatimaye iendelee kwenye mtandao wa vizazi viwili ya familia hii iliyobarikiwa na utaratibu unaweza kuanzishwa, kukubalika kwamba kila mwana familia anaitilia maanani na kuitia moyoni mwake amri inayoagiza kuungana kwenye ndoa kwa wale wanaizishika Amri za Baba wa Mbinguni (2Wakorintho 6:14-18).

2Wakorintho 6:14-18 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. [Mambo ya Walawi 26:12; Ezekieli 37:27]  17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. [Isaya 52:11]  18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike, [2 Samweli 7:8, 14; Isaya 43:6].

 

Wakati kipengele chochote mojawapo ya hizi kikiondolewa hali ya kutojiamini na masikitiko hutokea na hatimaye familia huishi maisha yaliyo kinyume na mapenzi ya Mungu wakiwa kama watoto waliomuasi Mungu kwa sasa. Kristo alitabiri kutatokea mateso yatakayotokana na wanafamilia na marafiki ambao wanaishi kinyume na mapenzi ya Mungu.

 

Luka 21:16-17 Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu. 17 Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu.

 

Tunatakiwa kufanya kile kilicho ndani ya uwezo wetu ili kuendeleza utaratibu wa kifamilia ambao Mungu ameuweka ili kumfanya mwanadamu aweze kuzaliana na hatimaye kumheshimu Mungu. Hata hivyo, kaka yetu mkubwa Kristo anasema kwamba utimilifu wa uhusiano wa familia kwa kila mmoja kwa mwingine huonda hali ya udanganyifu miongoni mwa walio kwenye familia ya watoto watiifu wa Mungu. Kwa kuwa hawa ni wana na mabinti wa Bwana, na Mungu Mwenyezi na ndugu wa kiume na wa kike wa mzaliwa wa kwanza Kristo.

 

Mathayo 12:46-50 Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye. 47 Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe. 48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani? 49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu! 50 Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu.

                                                                                Amina

q