Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[191]
Yeroboam na Kalenda ya Hilleli
(Toleo
la 3.0 19970118-19990612-20070907)
Jarida hili linamuelezea Mfalme Yeroboam, mfalme
wa kwanza wa makabila kumi ya Israeli, na jinsi alivyouchukua ufalme kutoka kwa
mtoto wa Sulemani kwa sababu ya kitendo cha kuabudu na kuzitumikia sanamu
kilichofanywa na babayake yaani mfalme Sulemani. Pia linaelezea dhambi alizofanya
Yeroboam kwa masuala ya Sikukuu na ibada za sanamu. Linaelezea pia kuhusu
vuguvugu la wa Quartodeciman na halafu maadhimisho ya Easter kwa Kanisa la
zamani na jinsi ya kuamua kuanza kwa mwezi wa Nisani kulivyofanywa na kanuni za
kale. Hii imepatikana kinyume na matendo ya mwanzoni ya Yuda ambayo kwayo yamepelekea
kuanzisha kwa kile kinachoitwa leo kuwa ni Kalenda ya Hilleli.
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
1997, 1999, 2007 Wade Cox)
(tr. 2013)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Kuna wafalme
wawili wa Israeli wenye jina hili la Yeroboam. Wa kwanza ni Yeroboam mwana wa Nebati
na Zerua, kutoka kwenye mji wa Zereda huko Efraim (kwa mujibu wa Encyc. Judaica, Vol. 9, ukurasa 1371.). wa
pili ni Yeroboam mwana wa Yehoashi au Yoashi. Mtu tunayemzungumzia na kuelezea
habari zake ni Yeroboam mwana wa Nebati. Alikuwa ni Muefraimu, ambao walikuwa
ni tofauti na Waefraimu wa Bethelehemu. Jina lake lina maana ya Yeye anayepigana vita ya watu au watu watashindana (SHD 3379; kutoka
7378, ruwb – kushikamana na 5971, ’niko
au watu). Yerubaali (Baali atashindana)
pia ni ishara au inamaanisha sawa na jina la Gideon (SHD 3378). Yeroboam au Yeroboamu
(halina herufi J kwenye Kiebrania) alimkimbia
Sulemani na akaenda Misri hali alipokufa mfalme Sulemani.
1Wafalme 11:26-27 Na Yeroboamu wa Nebati, Mwefraimu wa
Sereda, mtumwa wake Sulemani; ambaye jina lake mamaye aliitwa Serua, mwanamke
aliyefiwa na mumewe; yeye naye akainua mkono wake juu ya mfalme. 27 Na hii ndiyo
sababu ya yeye kumwinulia mfalme mkono. Sulemani aliijenga Milo, akapafunga
palipobomoka pa mji wa baba yake Daudi.
Neno Millo
limechukuliwa kwenye Kiebrania likimaanisha kutia
au kujaza, na linatokana na neno
la Kiashuru mulu, ambalo maana yake ni trrasse
au terrace.
Shekemu pia alikuwa na nyumba huko Millo (Waamuzi 9:6). Nji wa Millo unatajwa ukijumuishwa
na mzingiro wa boma uliofanywa na Daudi baada ya kuuteka mji wa Yerusalemu (2Samweli
5:9; 1Wakorintho 11:8). Ujenzi wake hapo kwanza uliamriwa na Sulemani (1Wafalme
9:15,24; 11:27). Inatajwa kuwa ni nyumba
ya Millo kwenye Waamuzi 9:6 na pia inatajwa kwenye kifo cha Yoashi (2Wafalme
12:20 – Henda na 12:21). Mji huu yaonyesha kuwa ulikuwa upande wa magharibi ya
mji wa
Daudi ukiunganisha maeneo kati ya Yebu na Moria.
Hezekia aliuimarisha (kama inavyosema 2Nyakati 32:54).
Inaonekana kuwa
kuzungushia ukuta au ngome kwenye miteremko iliyojitokeza inaweza kuwa ndiyo
maana yake pia. Kunawezekana kuwa kulikuwepo na utaratibu wa kikanuni kama
alivyochukua Yeroboam na kuwa ni sababu ya mashambulizi linaweza kuwa na
uhusiano na mungu wa ngome au wa vita na kulifanya liashirie ibada ya sanamu.
Maana yake haieleweki vizuri. Maelezo yake yanamfanya mtu afikirie ujenzi wa
mahekalu kwenye viwanja vya kuta zilizozungushiwa kuta za boma ya mji wa Uru.
Kutoka Agada,
tunaona kwamba Yeroboam anamkemea Sulemani kwa kufunga milango iliyowekwa
kwenye kuta za Yerusalemu zilizojengwa na Daudi, ili kwamba Israeli wote waweze
kutembelea mjini Yerusalemu na kuhudhuria Sikukuu. Inaonekana kwamba Sulemani
aliifunga milango hii ili kuwapendeza binti za Farao (Sanh. 101b). Hali hii ilikuwa ni kongwa kubwa sana ambayo aliitumia
Yeroboam kuruzukiwa kwa ajili ya juhudi zake za kupigania haki ya uhuru wa
kuabudu wa watu, lakini alipopata ufalme slijaribiwa kuzuia kufanyika kwa matu
wasiende tion is quite ironic in that Jeroboam wasembezi haya haya akiwazuilia
watu wasiende Yerusalemu. Jambo ambalo alilipigania sana watu kuwa na uhuru wa kuabudu
(pia tazama kitabu cha TJ. Av. Zar.
1:1, 39a; Sanh. 101b; cf. Encyc.
Judaica, ibid.).
Tunaendelea
kwenye 1Wafalme 11.
1Wafalme 11:28-43
inasema: Na huyo Yeroboamu alikuwa mtu hodari, shujaa; Sulemani akaona ya kuwa
kijana huyo ni mtu mwenye bidii, akamweka juu ya kazi yote ya nyumba ya Yusufu.
29 Ikawa zamani zile Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii
Ahiya, Mshiloni, alikutana naye njiani; naye Ahiya amevaa vazi jipya, na hao
wawili walikuwa peke yao mashambani. 30 Ahiya akalishika lile vazi jipya alilokuwa
amelivaa, akalirarua vipande kumi na viwili. 31 Akamwambia Yeroboamu, Twaa wewe vipande
kumi, maana Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nitaurarua ufalme, na kuuondoa
katika mkono wa Sulemani, nami nitakupa wewe kabila kumi, 32 (lakini yeye
atakuwa na kabila moja kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya
Yerusalemu mji ule iliouchagua katika miji yote ya kabila za Israeli); 33 kwa sababu
wameniacha mimi wakaabudu Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni, na Kemoshi, mungu
wa Wamoabi, na Milkomu, mungu wa wana wa Amoni wala hawakuenda katika njia
zangu, kutenda mema machoni pangu, kuzishika sheria zangu na hukumu zangu, kama
Daudi baba yake. 34 Walakini sitauondoa ufalme wote katika mkono wake; lakini nitamfanya awe
mkuu siku zote za maisha yake, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi niliyemchagua
kwa maana alizishika amri zangu na sheria zangu, 35 lakini nitauondoa ufalme katika mkono wa
mwanawe, nami nitakupa wewe kabila kumi. 36 Nami nitampa mwana wake kabila moja, ili
Daudi, mtumishi wangu, apate kuwa na taa siku zote mbele zangu katika
Yerusalemu, mji ule niliouchagua niweke jina langu huko. 37 Nami nitakutwaa
wewe, nawe utatawala kama roho yako inavyotamani, nawe utakuwa mfalme juu ya
Israeli. 38 Tena itakuwa, ukiyasikia yote nitakayokuamuru, na kuenda katika njia zangu,
na kutenda yaliyo mema machoni pangu, ili kuzishika amri zangu na hukumu zangu
kama Daudi mtumishi wangu alivyotenda, basi, nitakuwa pamoja nawe, nitakujengea
nyumba iliyo imara, kama nilivyomjengea Daudi, nami nitakupa wewe Israeli. 39 Tena nitawatesa
wazao wa Daudi kwa sababu hii, lakini si daima. 40 Basi Sulemani akataka kumwua Yeroboamu,
lakini Yeroboamu akaondoka, akakimbilia Misri, kwa Shishaki, mfalme wa Misri,
akakaa katika Misri hata wakati wa kufa kwake Sulemani. 41 Nayo
yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je!
Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani? 42 Na siku
alizotawala Sulemani katika Yerusalemu juu ya Israeli wote zilikuwa miaka
arobaini. 43 Naye Sulemani akalala na baba zake, akazikwa katika mji wa Daudi baba yake;
na Rehoboamu mwanawe akatawala mahali pake.
Tunaona hapa kwamba Yeroboam alitoroka kwakuwa Sulemani alikuwa anatafuta
kumuua. Huenda hii ndiyo hatimaye ilisababisha maasi. Kitabu cha Wafalme
hakiliweki wazi sana jambo hili, lakini tafsiri ya Septuagint inasema kwamba Yeroboam alifanikiwa
kuanzisha kikosi cha askari wa magari wapatao 300 na alikuwa na ngome yake kwenye
mji wa Zereda (au Serera). Maasi yalishindwa na Yeroboam akalazimika kukimbilia
Misri (pia tazama kitabu cha Encyc.
Judaica, ibid.). Tafsiri ya Biblia ijulikanayo kama LXX pia kinanukuu
kwamba Shishaki alimtoa shemeji yake kwa Yeroboam ili awe mkewe, na Abiya
alikuja kwenye muungano huu.
Yeroboam alikuwa mtiwa mafuta wa Bwana. Sulemani alifikia kuwa ni mwabudu sanamu
na uzao wake uliadhibiwa. Kwenye andiko hili, inaonekana kuwa ni kama Shishaki wa
Misri alikuwa ni shemeji yake Sulemani. Huenda yeye ni mrithi asiyefaa. Na sasa
tunaendelea kuangalia namna ambayo kwamba Mungu aliuathiri nguvu na ukubwa wake
ufalme huu wa mwana wa Sulemani, yaani Rehoboam.
1Wafalme 12:1-15 Rehoboamu akaenda Shekemu; maana Israeli wote
walikuwa wamekwenda Shekemu, ili kumfanya mfalme. 2 Ikawa Yeroboamu mwana wa Nebati alipopata
habari (maana alikuwa akaliko Misri, huko alikokimbilia awe mbali na mfalme
Sulemani; Yeroboamu akakaa huko Misri, 3 wakapeleka watu kwenda kumwita); basi
Yeroboamu na jamii yote ya Israeli wakaenda, wakamwambia Rehoboamu, wakasema, 4 Baba yako
alilifanya zito kongwa letu; basi sasa utupunguzie utumwa mzito tuliotumikishwa
na baba yako, na lile kongwa zito alilotutwika, nasi tutakutumikia. 5 Akawaambia,
Enendeni zenu hata siku ya tatu, kisha mnirudie tena. Watu wakaenda zao. 6 Mfalme Rehoboamu
akataka shauri kwa wazee waliokuwa wakisimama mbele ya Sulemani, baba yake,
alipokuwa hai, akasema, Mwanipa shauri gani ili niwajibu watu hawa? 7 Wakamwambia
wakasema, Ukikubali kuwa mtumishi wa watu hawa leo, na kuwatumikia, na
kuwajibu, na kuwapa maneno mazuri, basi watakuwa watumishi wako daima. 8 Lakini akaliacha
shauri lile la wazee, walilompa, akataka shauri kwa wale vijana waliokua pamoja
naye, na kusimama mbele yake. 9 Akawaambia, Mwanipa shauri gani ili
tuwajibu watu hawa, waliosema nami, wakinena Utufanyie jepesi kongwa lile alilotutwika
baba yako? 10 Na wale vijana waliokua pamoja naye wakamwambia, wakasema, Uwaambie hivi
watu wale waliokuambia, wakisema, Baba yako alilifanya zito kongwa letu, bali
wewe utufanyie jepesi, uwaambie hivi, Kidole changu cha mwisho ni kinene kuliko
kiuno cha baba yangu. 11 Basi kama vile baba yangu alivyowatwika kongwa zito, mimi nitaongeza kongwa
lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge. 12 Basi, Yeroboamu
na watu wote wakamfikia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyoamuru,
akisema, Mnirudie siku ya tatu. 13 Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali,
akaliacha shauri lile wazee walilompa; 14 akawajibu kama vile walivyomshauri vijana,
akasema, Baba yangu alilifanya zito kongwa lenu, bali mimi nitaongeza kongwa
lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge. 15 Basi mfalme
hakuwasikia wale watu; maana jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili alitimize neno
lake, Bwana alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kwa kinywa cha Ahiya Mshilon
Yeroboam aliwekwa
mahala pake na Mungu ili aweze kuligawanya kwa mrithi wakuu – lakini hili halikueleweka
hadi kipindi cha baadae sana. Upuuzi wa kiushauri wa vijana uliongezeka sana. Kazi
na uzungushaji ngome vilikuwa vimekwisha fanywa na Daudi na Sulemani. Angeweza
kupunguza uzito wa kongwa na akawa mfalme, lakini Mungu hakupenda iwe hivyo. Masharti
ya ufalme wa Sulemani yalikuwa ni awe mtiifu kwa Mungu na kwa Sheria na Torati
yake. Jambo hili lilipelekea maana kubwa kama tutakavyojionea baadae.
1Wafalme 12:16-20 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme
hakuwasikia, hao watu walimjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika
Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya! Nendeni zenu hemani
kwenu, enyi Israeli; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi. Hivyo Israeli
wakaenda zao hemani kwao. 17 Lakini kwa habari za wana wa Israeli
waliokaa katika miji ya Yuda, Rehoboamu aliwatawala wao. 18 Ndipo mfalme
Rehoboamu akampeleka Adoramu, aliyekuwa juu ya shokoa, nao Israeli wote
wakampiga kwa mawe hata akafa. Mfalme Rehoboamu akafanya haraka kupanda katika
gari, ili akimbilie Yerusalemu. 19 Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya
Daudi hata leo. 20 Ikawa, Israeli wote waliposikia ya kwamba Yeroboamu amerudi, wakapeleka
watu wakamwita aje mkutanoni, wakamfanya mfalme juu ya Israeli wote; wala
hapakuwa na mtu aliyeshikamana na nyumba ya Daudi, ila kabila ya Yuda peke
yake.
Mungu alitenda
jambo litokee na Mpango wake ulifanikiwa. Watu wenyewe hawakugundua kile
kilichokuwa kinatokea. Yeroboam ndiye alikuwa mrithi aliyestahili na ndiye angaliyeweza
kuyaunganisha makabila chini ya Efraimu, ila Mungu alijua kuwa angeshindwa.
Hata hivyo, alimfanya kuwa mfalme.
1Wafalme 12:21-24 Hata Rehoboamu
alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda, pamoja na kabila ya
Benyamini, watu wateule mia na themanini elfu, waliokuwa watu wa vita, ili
wapigane na nyumba ya Israeli, waurudishe ufalme tena kwa Rehoboamu mwana wa
Sulemani. 22 Lakini likaja neno la Mungu kwa Shemaya mtu wa Mungu, kusema, 23 Mwambie
Rehoboamu mwana wa Sulemani, mfalme wa Yuda, na jamaa yote ya Yuda na
Benyamini, na watu waliosalia, ukisema, 24 Bwana asema hivi, Msiende, wala msipigane
na ndugu zenu wana wa Israeli; rudini kila mtu nyumbani kwake; kwa kuwa jambo
hili limetoka kwangu. Basi, wakalisikiliza neno la Bwana, wakarudi, wakaenda
zao, sawasawa na neno la Bwana.
Mungu pia alizuia
umwagaji damu usio wa lazima kwa kuwarudisha myumbani Yuda na Benyamin kwa
upande mwingine, na makabila mengine kumi kwa upande mwingine.
Ingawa Yeroboam
alifanywa kuwa mfalme na Mungu na akatumika kuchukua mahala pa nyumba hii
iliyogeukia na kuabudu sanamu chini ya Sulemani, bado hakuwa na imani ya
kutosha kwa Mungu kuwa angeweza kumlinda na kumfanya awe huko.
1Wafalme 12:25-33 Ndipo
Yeroboamu akajenga Shekemu katika milima ya Efraimu, akakaa huko. Akatoka huko
akajenga Penueli. 26 Yeroboamu akasema moyoni mwake, Basi ufalme utairudia nyumba ya Daudi.27 Kama watu hawa
wakipanda kwenda kutoa dhabihu katika nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, ndipo
mioyo ya watu hawa itamrudia bwana wao, yaani Rehoboamu, mfalme wa Yuda; nao
wataniua mimi, na kumrudia Rehoboamu, mfalme wa Yuda. 28 Kwa hiyo mfalme akafanya shauri,
akafanyiza ng'ombe wawili wa dhahabu, akawaambia watu, Ni vigumu kwenu kupanda
kwenda Yerusalemu; tazama, hii ndiyo miungu yenu, enyi Israeli, iliyowapandisha
kutoka nchi ya Misri. 29 Akamweka mmoja katika Betheli, na wa pili akamweka katika Dani. 30 Jambo hili
likawa dhambi, maana watu walikwenda kuabudu mbele ya kila mmoja, hata huko
Dani. 31 Tena akafanya nyumba za mahali pa juu, akafanya na watu wo wote, watu wasio
wa wana wa Lawi, kuwa makuhani. 32 Yeroboamu akaamuru kushika sikukuu katika
mwezi wa nane, siku ya kumi na tano ya mwezi, mfano wa sikukuu iliyokuwa katika
Yuda, akapanda juu ili kuiendea madhabahu. Akafanya vivyo katika Betheli
akiwatolea dhabihu wale ng'ombe aliowafanya; akawaweka katika Betheli wale
makuhani wa mahali pa juu alipokuwa amepafanya. 33 Akatoa dhabihu juu ya ile madhabahu
aliyoifanya katika Betheli, siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi
aliouwaza moyoni mwake mwenyewe; akawaamuru wana wa Israeli waishike sikukuu
hiyo, akapanda kuiendea madhabahu, ili kufukiza uvumba.
Aliujenga Shekemu
na kisha akauzungushia boma mji wa Penueli uliokuwa mashariki mwa ukingo wa
Yordani (1Wafalme 12:25), na hatimaye alionekana pia kuwa alikwenda Tirza (1Wafalme
14:17; sawa na. 1Wafalme 15:21).
Yeroboam aliamua
kuanzisha mfumo wa kidini ambao kwa kweli ulikuwa ni wa ibada za sanamu.
Alianzisha imani ambayo ilikuwa karibu sawa na ile iliyokuweko Hekaluni ya
ibada asilia ya Yerusalemu ikiwa na Sikukuu zided to reintroduce a religious
system that was inlezile lakini kiini na kituo cha kufanyia ibada ilikuwa na
msingi wake kwenye sanamu ya ndama wa dhahabu, ambaye anakiweko ambacho pembeni
yake amesimama Mungu (Encyc. Judaica, ibid.). dini hii waliijua Israeli tangu
siku walizokuwa jangwani. Kutokana na kile tunachokijua sasa kuwa ni utaratibu
wa ibada za watu wa Uru, ndama alikuwa ndiye alama ya ibada za watu wa Uru – inayoonekana
kwenye majumba ya kujiliwaza yaliyo nje ya mji wa Alaka Huyuki (tazama kitabu
ccch Wataalamu wa Uchimbuzi (Archaeological
Diggings), Vol. 3, Na. 6, Dec 96/Jan 97, ukurasa. 41). Waajemi wameifanyiza
upya sanamu hii ili kufanya yule ng’ombe dume aliyekuwa anamuwakilisha Ahriman,
ambaye ni mungu wa giza. Mtazamo huu wa kiulimwengu wa mapigano kwenye sayari
za juu bilashaka ni alama ya dume la ng’ombe aliyechinjwa ni alama ashirio ya dini
na ibada za mungu Mithras, iliyochukuliwa kutoka kwa wa Zoroastrian na kufuatiwa
na elimu-dunia (sawa na ilivyoandikwa kwenye jarida la Mdama wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No. 222)].
Mji wa Dani kwa
upande wa kaskazini na Betheli kwa upande wa kusini ilikuwa ni mahali
patakatifu pa imani po ofu ya dini hii kabla ya kipindi cha kuanzishwa kwa utawala
wa wafalme (Encyc. Judaica, ibid.).
Inaonekana kuwa Yeroboam
alitengwa na baraza la kidini la Sanhedrin kwa kuwa matendo yake yote aliyoyafanya
ikiwemo na kupaweka tena mahali pa juu katika Dani na Betheli, kulituama kwnyre
mtazamo wa kuchukulina na uvumilivu wa kidini uliopelekea kutumia kuabudu ndama
jambo ambalo ni kinyume na amri ya Torati (TJ.
Av. Zar. na Sanh, loc. cit., cf. Encyc. Judaica, ibid.). hii ni hali sawa na jinsi tulivyo leo. Hata hivyo,
makabila haya hawakudanganjika na dini hii isipokuwa kabila la Dani, ambalo
liliabudu sanamu iliyochongwa na Mika katika zama hizi za makabila (Hesabu 2:10). Inaonekana kuwa Walawi
walijitahidi kupinga na kuzuia ibada hizi za sanamu na ndipo Yeroboam akaanzisha
mfumo mpya mwingine wa Makuhani ambao uliwaweka kando Walawi (TJ. Av. Zar., loc. cit.). walawi
waliandika habari kwamba Yeroboam aliweka walinzi ili kuzuia—maumivu ya kifo—ya
wanaokwenda kuzitunza sikukuu mjini Yerusalemu (Tosef., Ta’an. 4:7; Sanh. 102a). Watu na hata mtoto wa
mfalme, walizihalifu amri hizie (MK
28b, cf. Encyc. Judaica, loc. cit.).
Katika mwaka wa
hamsini wa utawala wa Yeroboam, Shishaki, mfalme wa Misri, aliamua kuishambulia
Israeli. Mikakati yake iliyoandikwa kwenye Biblia ilisababisha kile kiliccchotokea
huko Yuda (1Wafalme 14:25-28; 2Nyakati 12:2-12). Hebu na turudi kwenye yale michoro
ya ukutani mwa hekalu la Karnaki huko Misri ili kuona ni miji gani iliyokuwa
imetekwa na Shishaki, na tutaona kwamba inaonekana kuwa Israeli walitaabika sana.
Kwa hiyo, mlingano na muonekano huu sio tu kwamba unafanana tu kwenye Biblia
bali pia unafika mbali kutupa taarifa za huko. Shishaki alishambulia jimbo la
kusini la Ufalme wa Israeli kupitia huko Gezeri na Gibeon, kupenyeza bonde la Sukoth na kisha kugeukia upande wa Beth-Shean
na bonde la Yezreeli, hatimaye akarudi Misri kwa njia ya uwanda wa pwani. Uweza
wa nguvu za kijeshi za Misri ulikoma kwa utekwaji rahisi na usiotarajiwa. Wataalamu
wa uchimbuzi wa mambo ya kale wamegundua kwamba Gezeri, Beth-Shean, Taanaki na
Megido ziliangamizwa kipindi cha kampeni hii. Kwa hiyo mafanikio ya Abiya kuyashinda
majimbo ya Israeli yanatakiwa kuonekana kwenye wepesi wa udhaifu iliyoikumba kampeni
ya Wamisri, lakini pia ni kwa shinikizo juu ya hili kutoka kwa Aram-Damascus wa
kaskazini mashariki na Wafilisti wa kusini magharibi. Hii inaweza pia kuwa iliungwa
mkono na mapigano na majimbo ya Trans-Jordan ambayo yalikuja kuwa huru zaidi (Encyc. Judaica, op. cit., ukurasa 1373).
Pia Yeroboam aliamua
kubadilisha maadhimisho ya Sikukuu ya Vibanda kutoka nyakati zake asilia za
Mwezi wa Saba na kuisogeza hadi mwezi wa Nane alifanya hivyo kwa kusudi la
kufanya ibada ionekane kuwa ni sawa na ni ile ile, lakini ikiwa isiyo sawa na ile
iliyo kwenye taratibu asilia za Hekaluni. Jambo hili lina fundisho lenye madhara
makubwa kwa Kanisa la siku hizi ambayo Mungu anaonyesha kwa matendo yake hapa
kwamba hawezi kuuvumilia wala kusamehe na kuachia uendelee utaratibu wa ibada wenye
mjumuisho na ushirika wa namna za ibada za sanamu, au unabadili utaratibu
uliowekwa wa maadhimisho ya Sikukuu kwa kuiweka kwenye majira mengine mbali na
mwezi uliowekwa na ambao ameuweka mwenyewe kwa mujibu wa ishara za mbinguni. Kalenda
ya Mungu haitegemei na hesabu na mipangilio na muafaka wa kibinadamu. Imewekwa
na inadumu kwa nyakati zote na uumbaji unaonyesha mpangilio wa mabadiliko ya
nyakati na majira. Mwandamo wa Mwezi Mpya unaunganisha mipangilio kati ya jua,
mwezi mwandamo na Dunia, na unaweza kupimwa kiuhakika hadi kwenye kipindi
kingine cha karne kadhaa zijazo. Tukio hili la kipindi cha kutoonekana mwezi,
pamoja na lile la mwezi mkamilifu na robo ya kwanza nay a mwisho, vimepandiliwa
kwa mujibu wa maji kujaa na kupwa.
Tunaweza kufanya mabatiyo
tusiyoweza kuyajua kupata hakika jinsi mfumo huu wa dini mpya ulivyokusudia
kubadili hadi kwenye namna mpya iliyoanzishwa tangu kale na ambayo inaendelea
kudumu hadi leo, na hii ndiyo chanzo cha kuanzishwa kwa kalenda ya watu wa
Samaria. Ilianza siku za kale zaidi kuliko ile inayojulikana kama kalenda ya
Hilleli na inarudi nyuma zaidi hadi kipindi cha zama za Hekalu kabla ya Kristo.
Imani au Dini
ya Wasamaria
Kwenye jarida la Malumbano ya Wa-Quartodeciman (Na. 277) [The Quartodeciman Disputes (No.
277)], tuligundua uwiano wenye kufanana wa Wasamaria na ule wa Masadukayo katika
kuamua namna ya kuiweka kalenda ya Hekalu na kupanga majira ya kuadhimisha Pasaka
wakati wa kipindi cha Hekalu na siku za Kanisa la kwanza tunarudia hapa baadhi
ya maandiko hayo.
Kuandama kwa Mwezi Mpya kulikuwa ndiyo jambo la muhimu sana katika kuamua
kuanza kwa miezi, na Mwandamo wa Mwezi wa Kwanza wa Abibu au wa Nisani, (na sio
wa mezi wa Saba wa Ethanimu au wa Tishri), ndiko kilikuwa kigezo cha kutangazwa
kwa mwezi wa kwanza wa mwaka mpya, kama ilivyofanywa na kujulikana na Wayahudi kutoka
karne ya tatu ya zama hizi. Mfumo wa Rosh HaShanah, ulio kwenye utaratibu wa
leo wa kuamua kutangazwa kwa mwaka mpya, hauwezi kuchukuliwa kuwa ni wa
kibiblia au ulichukuliwa kwenye maadhimisho ya zama za Hekalu, wala kuchukuliwa
kuwa ni maadhimisho sahihi ya Wakristo—Wayahudi.
Kitabu maarufu kiitwacho
Filo wa Alexandria, yaani Philo of Alexandria [kilichotafsiriwa na F.
H. Colson, (Harvard University Press, Loeb Classical Library, Cambridge, MA,
1937), The Special Laws, II, XI, 41] kinatuambia
kwamba: “[Sikukuu] ya tatu kwenye mwandamo wa mwezi mpya uliofuatia kipindi cha
mwezi kutoonekana na jua”. Na kwenye chapisho la II, XXVI, 140: “Huu ni Mwandamo wa Mwezi, au mwanzo wa mwezi
mwandamo, unaojulikana kuwa ni kipindi kilicho katikati ya kipindi cha
kutoonekana mwezi na kinachofuatia, urefu ambao umehesabiwa kikamilifu pasi kukosewa
na wanazuoni wa elimu ya anga nyota”. Yapaswa ijulikane pia Kitabu maarufu
kilichochapishwa cha Hendrickson Publishers toleo la (1993) la tafsiri ya C. D.
Jonge ya mwaka 1854 haina taaarifa sawa kama iliyoko kwenye tafsiri ya Colson na
jinsi inavyotuambia. Dalili zilizoko ni kwamba vipindi vya kutoonekana mwezi viliamuliwa
ili kuamua ama kuashiria mwanzo wa mwezi.
Wasamaria na Masadukayo makundi yote mawili yaliaweka kalenda kwa kuanzia
kipindi cha mwezi kutoonekana, maadhimisho ya Mwandamo wa Mwezi yalitangazwa na
kufanyika kwa kutegemea majira haya ya kutoonekana kwa mwezi kwa namna yoyote
ile kwenye kipindi cha Hekalu, isipokuwa kwa Essene tu aliyekuwa na kalenda
isiyobadilika ambayo kwamba siku ya 14 Abibu iliangukia siku ya Jumanne ya kila
mwaka kwenye mzunguko wa kamilifu wa kalenda. Wasamaria bado wanatangaza siku ya
kwanza kwa kufuata kipindi cha kutoonekana mwezi hadi leo (sawa na
ilivyoandikwa kwenye jarida la Kalenda ya Mundu (Na. 156) [God’s Calendar (No. 156)].
Wasamaria walianzisha makosa kwenye kalenda yao walipoanzisha utaratibu wa
kutangaza mwanzo wa Mwezi wa Kwanza kwa kusema kwamba Mwandamo wa Mwezi kila
mara ni lazima uwe kwenye majira ambayo saa za usiku na za mchana ni sawa au
baadae kidogo, ambayo walitangaza kuwa kinaangukia kila mwaka tarehe 25 Machi. Uhesabuji
wa miaka ya (1988-2163 BK), kama ulivyoonyeshwa na Kasisi Eleazar ben Tsedeka, umejumuishwa
kwenye kitabu cha maombi kuhusu Pasaka na Mazzot, Knws tplwt hg hpsh whg
hmswt (Holon, 1964, pp. 332-336; sawa na Reinhard Pummer Samaritan
Rituals and Customs, kurasa 681-682, fn. 201 in Alan D. Crown Ed. The
Samaritans, 1989, J. C. B. Mohr (Paul Siebeck) Tübingen). Ukweli huu
unaonyesha pia kuwa tunatazamia chanzo asilia cha kale, ambacho msingi wake ni
kwenye kalenda inayotumika wakati siku hii ya usiku na mchana masaa kuwa sawa iliangukia
tarehe 25 Machi. Tarehe hii ilitangulia siku
nyingi kabla ya kipindi cha Kristo na ilikubalika kwa kuweka uwiano wa kalenda
ya kaisari Yulio au Julius Caesar (sawa na. David Ewing Duncan, The Calendar,
4th Estate London, 1998, uk. 81).
Hii inaonekana kuwa huenda ni chanzo cha kuwapo makosa haya. Kitendo cha watu
wa kale kuamua siku ya mwezi kutoonekana ya tarehe 25 Machi kinaonekana kuwa
kilichukuliwa kutoka kwenye mapokeo ya kipindi cha kwanza cha Hekalu la Kwanza
na la Pili na inaonyesha kwamba huenda sisi tunaangalia suala zima la Kalenda
ya Yeroboam. Kitendo chake cha kuamuru Sikukuu iadhimishwe mwezi wa
Nane—kililaaniwa na Biblia—na kingeweza kufanikiwa kutokea kwa tendo la kufanya
Mwandamo wa Mwezi ufanyike kwenye kipindi cha masaa ya jua kuwa sawa usiku na
mchana au baadae kidogo. Hii inaonyesha kuwa haikuweza kubadilishwa kwa suala
la Wasamaria tangia kuanguka kwa taifa la Israeli. Na kwa sababu hii
waliangukia kwenye laana na wamebakia kuwa ni masalia pekee ya Israeli ambao
hawajabarikiwa na ahadi ya uzaliwa wa kwanza ya Yusufu. Kazi ya kuhesabu ya
Wasamaria ilifanywa kwa siri, huenda ni kwa kulifanyia uangalifu jambo hili. Hata
hivyo, wao pamoja na Mafarisayo kila mara waliamua mambo ya kalenda kwa
kutegemeza na siku ambayo mwezi hauonekani, ambavyo ndivyo ilivvofanyika
kipindi chote cha zama za Hekalu.
Kalenda ya Wasamaria kwa hiyo iliondoka kwenye msingi sahihi wa uelewa wa
Mwandamo wa Mwezi na Msingi wake, bali ulichukuliwa kwenye baraza lenye makosa
ya uwekaji kwa usahihi na kuweka siku ya mwanzo wa mwaka kimakosa. Kwenye miaka
hiyohiyo wakati wa Mwandamo wa Mwezi wa Mwezi wa Kwanza ulioangukia kabla ya
siku hii ya masaa kuwa sawa usiku na mchana, waliamua kutangaza kuanza kwa
mwaka mpya kwenye Mwezi wa Pili na kufanya Sikukuu iadhimishwe mwezi wa Nane badala
ya Mwezi wa Saba wa kweli na sahihi kwa mujibu wa mwaka unaofuata mwezi
mwandamo. Huenda hii ilikuwa ni chanzo cha makosa yaliyofanywa kwenye imani na
mtazamo wa Yeroboam. Na kwa kweli, ili kugundua kakosa kunabidi kukubali kuwa
Wasamaria ni masalio ya mfumo huu wa zamani wa Israeli na sio wote
waliojichanganya na hatimaye kuzuka kwa makabila ya Cutheans na Wamedi, ikiwa
kama ni propaganda ya Wayahudi ambayo inaumiza sana kuiongelea. Ukweli ni
kwamba, wanachanganyika na nasaba zote mbili.
Utaratibu huu wa ibada uliofanywa na kupangwa na wanadamu, siku hizi
imeshika hatamu, kwa kuwa utaratibu wa kuabudu wa Wayahudi ulioanzishwa na
kalenda ya Hilleli umefuata kikamilifu sana kile alichokifanya Yeroboam. Kwa mfano,
mnamo mwaka 1997 – ulikuwa ni wa kuadhimisha kikamilifu mtindo na muono wa
kibinadamu uliojulikana kama wa maahirisho ya--kalenda ya Hilleli
yaliyotangulia kwenye mwezi wa kweli wa Pili na sio katika mwzui wa Kwanza na,
kwa hiyo Sikukuu ikaadhimishwa mwezi mmoja kwa wote. Chini ya utaratibu wa Hilleli,
Sikukuu ya Vibanda ya mwaka 1997 ilifanyika mwezi wa Nane na sio mwezi wa Saba.
Makosa haya yalitokana na utaratibu huu unaojulikana kama wa ahirisho na ambao
hauna mashiko wala maagizo yoyote kwenye Biblia. Utaratibu wote wa uwekaji wa
utaratibu wa Kalenda umetolewa kwenye majarida ya GKalenda ya Mungu (Na. 156) na pia Tishri na
Uhusiano Wake na Siku ya Masaa ya Usiku na Mchana Kuwa Sawasawa (Na. 175) [God’s
Calendar (No. 156) and also Tishri in Relation to the Equinox (No. 175)].
Kanuni za siku za kale ziko rahisi na wazi sana. Mwansamo wa Mwezi wa
Nisani unachukuliwa kuwa ni ule unaoandama majira yaliyo karibu na siku ya
masaa ya usiku na mchana kuwa sawa. Siku Takatifu ya kwanza ya Mikate Isiyotiwa
Chachu (siku ya 15 Nisani) inapaswa kila mara iwe baada ya siku ya masaa
kulingana usiku na mchana. Siku ya 14 Nisani inaweza kuangukia siku hii ya
masaa kulingana usiku na mchana, lakini – siku ya 15 Nisani haiwezi. Hii inahesabiwa
wakati jua linapokuwa kwenye umbo la Aries (tazama kitabu cha Schürer, History of the Jewish People in the Age of
Jesus Christ, Calendar Appendix III, (Historia
ya Wayahudi Kipindi cha Yesu Kristo, Kaleanda na Nyongeza III), na pia
majarida tuliyoyataja hapo juu). Kwa hiyo, Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu
haiwezi kufanyika siku hii ya usiku na mchana kuwa sawa au kabla yake na
haiwezi kufanyika zaidi ya tarehe 20-21 Aprili. Hakuna maadhimisho ya Pasaka
yanayoruhusiwa kufanyika baada ya tarehe 20-21 Aprili (kama ilivyoainishwa pia
kwenye jarida la Mwezi na Mwaka Mpya (Na. 213) [The Moon and the New Year (No. 213)].
Hii inajulikana na inaadhimishwa na matawi yote ya Kanisa tangu kipindi cha
Kristo. Tangia karne ya pili na cha malumbano ya Waquartodeciman (tazama jarida
la Pasaka (Na. 98) [The Passover (No. 98)], kanisa huko Roma lilianza kuadhimisha sikukuu ya
Easter, lakini bado alikuwa wanaendelea kuzishika sheria za zama kale kwa
kuichukulia Nisani kuwa ni mwezi wa maadhimisho ya Easter kwa kuwa ilikuwa
inaangukia pia kwenye mwezi huu wa Nisani.
Kanisa huko Roma, hata hivyo lilifanya mabadiliko ya sheria. Siku ya Ijumaa
ilifanywa kuwa iwe ni siku ya kusulibiwa na sio siku ya 14 Nisani (aambayo ni
Jumatano ambayo Krsto alisulibiwa kwayo; tazama jarida la Kipindi cha Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159) [Timing
of the Crucifixion and the Resurrection (No. 159)]. Kalenda iliyojulikana mapema zaidi ya kanisa la
kale la mrengo wa Jumapili katika kujitahidi kwake kuifanya iwepo ni ile ambayo
ilimilikiwa na Willibrord, aliyekuwa mtume wa Kkiingereza aliyehudumu hko Frisians
(Askofu aliyewekwa wakfu mwaka 695 BK, aliyetajwa kwenye maandiko). Kalenda ile
inaweka siku ya kusulibiwa kwa Kristo kuwa ni tarehe 25 Machi na Yakobo ndugu
yake kuwa alisulibiwa pia tarehe hiyohiyo (akifuatiwa na Tertullian). 25
Machi ilikuwa ni siku iliyokubalika kwa kare kadhaa, ila ilikataliwa na Kanisa
Katoliki la Roma kwa kuwa inaharibu na kupinga juhudi za kuiaminisha dhana na
fundisho la kusulibiwa siku ya Ijumaa. Tehere 25 Machi ilikuwa ni Jumapili
katika mwaka wa 31 BK na huenda ilitokana na kazi ya kuhesabu kwenda nyuma hadi
mwaka 31 BK ukiwa kama mwaka uliofikiriwa kuwa ndio alisulibiwa kwawo. Tarehe 25
Machi, 31 BK ilikuwa siku ya 14 Nisan kwa mujibu wa Mwandamo wa mwezi na
ikiwa ni siku ya kweli ya mwezi kutoonekana ya utaratibu wa kale wa kalenda ya Hilleli.
Kwa jinsi ilivyo, inaonekana kama utaratibu wa kuahirisha haukulazimishwa.
Makosa aliyyafanya Tertullian huenda yalisababishwa na maandiko ya Josephus ambayo
yalimyanya kuamini kuwa ni mwaka 31 BK badala ya mwaka 30 BK. Mnamo mwaka
30 BK, tarehe 14 Nisan iliangukia siku ya Jumatano, na tena iliangukia kwenye
siku halisi ya mpito cha Kuandama Mwezi pasipo ahirisho. Huenda Tertullian alifanya
makosa ya kimahesabu kwa mwaka wa kumi na tano wa Tiberius (kama ilivyoelezwa
kwenye jarida la Kipindi cha Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159) [Timing
of the Crucifixion and the Resurrection (No. 159)] (pia tazama kwenye kitabu cha Cath. Encyc., Vol. III, art. ‘Calendaar’, p. 163 kwa tarehe, ingawaje
elimu ya wafiadni maarufu kama Syriac Martyriology inasema kuwa kina Yohana na
Yakobo waliuawa tarehe 27 Desemba, kwenye kitabu hicho cha hapo juu., ukurasa
162).
Tarehe za Tertullian zinaonyesha mambo mawili. La kwanza ni kwamba
hakukubali kuwa kusulibiwa kulifanyika siku ya Ijumaa kwenye miaka hii
inayoonewa mashaka (14 Nisan iliangkia tarehe 25 Machi tu mwaka 31 BK). Hata
hivyo, tarehe 25 Machi 31 BK ilikuwa siku ya Jumapili. Kwa hiyo kuhesabu kwa
namna hiyo hakuwezi kwendana na jinsi Injili inavyosema (tazama jarida la Kipindi cha Kusuibiwa na Kufufuka
tulilolitaja hapo). Pili, ni kam Tertullian alivyoandika siku nyingi kabla ya 358
BK, tunajua kuwa uahirishaji haukutiliwa maanani mapema kabla ya kalenda ya
Hilleli ilipofanyiwa hesabu kutoka hitimisho. Tarehe ya 25 Machi pia ina maana
yake kwenye ibada za mungu Attis, na kuingizwa kwenye Ukristo kupitia dini za
fumbo (sawa na ilivyoandikwa kwenye jarida la Chimbuko la Krismas na Easter
(Na. 235) The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].
Kansa lililoluwa huko Roma lilibadilisha kutoka kuifanya Pasaka iwe Sikukuu
ya Kwanza ya Mikate Isiyotiwa Chachu kuwa inaichukua mahali pa siku ya mchana
na usiku kuwa sawa na kwenye kipindi ambacho Easter ilikuwa ni Jumapili ya
Kwanza iliyoifuatia Mwezi Mwandamo wa Pasaka (ambayo ni kipindi cha Mwezi
Kamili, siku ya 15 Nisan). Mwandamo wa Mwezi uliganyika kabla ya siku kulingana
masaa usiku na mchana, bali Mwezi Mkamilifu haukuangukia kipindi cha kabla ya
siku hii ya masaa kulingana. Kwa hiyo, siku ya 14 Nisan inawezekana iliangukia
siku ya masaa kulingana, ila siku ya 15 Nisan iliangukia siku ya masaa
kulingana.
Katika karne ya pili Kanisa liliingia kwenye malumbano kuhusu kubadili
maadhimisho ya Pasaka kutoka siku za 14-15 Nisan hadi Easter, ikaamuliwa kama
tunavyoona hapo juu. Hili lilikuwa ndilo hasa jambo lililosababisha utata kwa wa
Quartodeciman. Utata huu uliendelea na kuenea kati ya askofu Anicetus wa Roma (aliyemfuatia
Pius mwaka 157 BK) na Polycarp, mwanafunzi wa Yohana na askofu wa Smirna. Alikuja
Roma (yapata mwaka 160-162) kwenye uzee wake kushirikiana pamoja na Anicetus kuhusu
kuanzusha kwa mafundisho mapotofu ya Easter. Kanisa la Mashariki kila mara
lilipenda kuendelea na Pasaka tangu siku ya 14 Nisan haijalishi ni siku gani ya
juma iliangukia. Huko Roma kulianza kujulikana siku ya Ijumaa na Jumapili.
ambayo ilikuwa ni maadhimisho Easter ya kipagani au Ishtar (kama iliyoandika
kwenye Cath. Encyc., art. ‘Anicetus’, Vol. I, p. 514). Polycarp hakufanikiwa
kumshawishi Anicetus akiwa anakata tama na wazo lake la kipagani na kurudi,
bali uhusiano kati yao uliliimarishwa na kulindwa (ibid.). hali hii iliendelea hadi
takriban mwaka 190 BK. Eusebius anaandika kwenye kitabu chake (Eccl. Hist., V, xxiii) kwamba wakati au
kipindi cha utawala wa Papa Victor kwamba:
Swali kuhusu kitu
kidogo muhimu liliibuka kipindi kile. Dayosisi ya Asia yote, kama kutoka kwenye
mapokeo yao ya kale, ilishikilia kwamba siku ya kumi na nne ya mwezi, kwenye
ile siku ambayo Wayahudi waliamriwa kumtoa sadaka mwanakondoo, ndiyo inayofaa kilamara
iadhimishe kuwa ni sikukuu ya kutoa uhai au Pasaka [epi tes tou sõterion Pascha eotes], sambamba na hilo ikaamuriwa
mkwacba ndiyo iwe siku ambayo kwamba kipindi cha mafungo walichojiwekea kihitimishwe
siku hii, yaani siku yoyote ya juma inaweza kufanyika tendo hili (Cath. Encyc., Vol. V, art. ‘Easter’, p. 228).
Makanisa kayika Asia yalihitimisha mafungo siku ya 14 Nisan kwa kushiriki
Ushirika Mtakatibu wa Meza ya Bwana ili kwamba Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu
ifuatie baada ya Siku hii ya Ushirika wa Meza ya Bwana. Maanalio ya mlo
yalifanywa na mlo wa Kutoka 12 uliandaliwa mahsusi kwa ajili ya siku ya 15
Nisan. Dini ya Warumi hata hivyo ilianzisha utaratibu wa kuhitimisha mfungo
siku ya Jumapili (tazama kitabu hikihiki cha Eusebius, ibid.; sawa na ilivyosndikwa kwenye Cath. Encyc., ibid.) kinachohusisha imani hii na imani ya kumuabudu
mungu mke Easter au Astarte/Ishtar.
Tendo hili la kubadilisha na kuiadhimisha Easter badala ya Pasaka lililofanywa
huko Rumi linaonekana kuwa lilifanyika kipindi cha Sixtus, askofu wa Roma takriban
mwaka 120 BK (tazama waraka wa Irenaeus unavyosema kuhusu jambo hili; sawa na Cath. Encyc., ibid.). Irenaeus anasema
kwamba Polycarp alikuja kutoka Roma akiwa na swali hili mnamo takriban mwaka
150.
Ni kwa jinsi hii ndipo Irenaeus aliwakataa na kuwapinga wa Quartodeciman na
itikadi yao ila hathubutu kabisa kumshutumu au kumlaumu Victor (takriban mwaka
189-199) kwa kuwatenga wafuasi wa Asiatics na kwa kutoifuatia tabia ya kuvumiliana
ya waliomtangulia. Ukweli unaoonyeshwa hapa uko dhahiri kabisa. Irenaeus hakupenda
kutengwa na kwa hiyo anadaiwa kuwa aliikubali Easter ichukue mahala pa Pasaka
kwa kuwa Roma ilisimama kati yake na pande za Mashariki. Ni kama ilivyo kwa
watu wengi Kanisani leo, yeye alikubali kukabiliana na mateso ya nje bali
hakuweza kukabiliana na ukengeufu uliokuwa ndani yake.
Baada ya juhudi za Victor za kuwakomesha wa Quartodecimans kuwakomesha na kuwaondolea mbali. Kwa
mujibu wa kitabu cha Origen (cha Philosphumena,
VIII, xviii) inaonekana kuwa aliwachukulia ni watu dhaifu kwa utendaji kazi walio na umahiri usiona na maana (sawa
na Cath. Encyc., op. cit.).
Hakuna mwandishi kwenye siku za kabla ya Justin Martyr (takriban mwaka 140)
aliyewahi kuitaja Jumapili kuwa ni siku inayofaa kufanyiwa maadhimisho haya ya
Pasaka kwa Kanisa (Cath. Encyc.,
ibid., p. 159). Tendo la kutenga kipindi cha ,mafungo ya Pasaka ya maandalizi
pia hakikuwa ni cha siku arobaini tu kama kilivyo kwenye siku za leo. Ulikuwa
ni utaratibu wa kiimani wa maandalizi yaliyopelekea kwenye maadhimisho ya
Pasaka (kwa mujibu wa Cath. Encyc.,
ibid.). Utaratibu wa kikanuni wa Mitume na Maendelezo
nya Mitume viliifanya Pasaka au Easter kuwa ni maadhimisho makubwa na
maarufu miongoni mwa Sikukuu zote. Kwa mujibu wa Tertullian, matukio ya mateso
na ufufuko wa Bwana vilichukuliwa kwa uzito sawa na neno Pascha (au Pasaka) viliwekwa kwenye siku zote mbili au kwenye kipindi
kilichokuwa kati ya ufufuko na siku ya Jumapili (ambayo ilikuwa ni siku ya
Mganda wa Kutikiswa na ambacho ndicho kwacho, hesabue ya kuelekea siku ya
Pentekoste inaanza kwayo) (ibid., p. 159).
Utaratbu wa kuhesabu na kuigiza imani ya sikukuu ya Easter na maadhimisho yake
kwa watu ulifanywa kwa mujibu wa Baraza la Mtaguso wa Nicaea, lakini hakuna kumbukumbu
kwenye utaratibu wa Kikanuni wa maamuzi haya (kwa mujibu wa kitabu cha Cath. Encyc., ibid., p. 160; cf. Turner, Monumenta Nicaeana 152; cf. Vol. V, art.
‘Easter’, p. 228). Rekodi imechukuliwa
kutoka kwenye madai ya nyongeza yaliyofanywa kwenye kitabu cha Eusebius
kiitwacho Life of Constantine (III,
xviii, et. seq.). Constantine alitafuta kutoka kwenye dokumenti hii kufanya
hali ya uwiano usiokuwepo na kuiweka mbali itikadi ambayo Wayahudi wanasema
kwamba:
Na kwanza na kabla ya yote kabisa inaonekana kuwa ni kitu kisicho sahihi kusherehekea sikukuu hii muhimu sana na takatifu na kwamba tulipaswa kufuata wanavyofanya Wayahudi, bali bila woga kabisa tumeinajisi mikono yao kwa dhambi kuu...kwa kuwa tumepokea kutoka kwa Mwokozi wetu namna nyjngine...
Watu
wengi (kutoka Roma katika Italia na Misri na Afrika) walikumbwa na wimbi hili
la kuikubali sikukuu hii ya Easter, lakini makanisa katika Syria na
Mesopotamia, pamoja na kituo chao kikuu katika Antiokia, walikuwa hawajaachana
na mafundisho na itikadi ya wa Quartodeciman. Kanuni hii ilirenukuliwa na
kuandikwa kwenye nyaraka zinazohusu mabishano haya kwamba kwenye maadhimisho ya
kale ya Wayahudi, siku ya 14 Nisan inapaswa kuwa siku kabla ya ile ya masaa
kulingana usiku na mchana. Na kwa hiyo, siku ya 14 Nisan inaweza kuangukia siku
ya masaa usiku na mchana kulingana na siku ya 15 Nisan inapaswa kila mara
iangukie siku hii ya masaa ya usiku na mchana kulingana. Jambo linguine tunalopaswa
kulijua ni kwamba Constantine, kwenye waraka
unaohusu mabishano yanayopinga uadhimishaji wa Easter na wa Quartodeciman yaliyoelezwa hapo juu, anasema kwa masikitiko
makubwa sana kwamba Wayahudi “wakatimwingine waliadhimisha Paschas mbili
kwa mwaka mmoja, akimaanisha kwamba Paschas mbili ambazo wakati mwingine
ziliangukia kati ya kipindi kimoja cha masaa ya usiki na mchana kulingana hadi
cha pili chake" (kwa mujibu wa kitabu cha Cath. Encyc., Vol. V, op.
cit.).
Maadhimisho
haya yanaonekana kwamba itikadi ya marabi ilikuwa imetanguliwa na kitendo cha
kuongeza mwezi mmoja na kuwa na mwaka mrefu. Sababu pekee kwa kufanyika kwake hivyo
ilikuwa ni kuwezesha mapokeo yake yashikwe na kuepuka marejeo ya Sabato
zinazohesabiwa nyuma kwa nyuma. Kalenda hii ya Hilleli haikuwepo huko nyuma
hadi mwaka 358 BK, au 344 ilipoanzishwa huko Babeloni. Na hivyo basi tuaweza kuhitimisha
kwa kusema kwmba utaratibu huu wa kuhesabu wa kalenmda hii ya Hilleli haikuwa
ikitumika wala kujulikana kama ilivyoanza tu mwaka 325 BK. Wasamaria kila mara
walianza mwaka tangia kuonekana kwa Mwezi Mwandamo wa baada ya tarehe 25 Machi.
Auamuzi
uliofanywa na baraza ulikuwa ni kwamba "Easter na iadhimishwe katika
Jumapili ya kwanza baada ya kipindi cha kwanza cha mwezi mkamilifu
kinachofuatia siku ya masaa ya usiku na mchana kulingana" (Vol. III, op. cit.). utaratibu huu unafanya
maadhimisho ya Easter yaangukie kipindi cha mapema sana cha tarehe 22 Machi
na cha mapema zaidi ya tarehe 25 Aprili (ikimaanisha kuwa ni tehere ya
mapema sana iwezekanavyo ya Jumapili na ndiyo ifanyike Sikukuu hii ambayo
itaangukia kwenye kipindi cha siku saba za baada ya Pasaka). Hii ni kitu
kingine tofauti na Pasaka na taratibu zake tena kuna mabadiliko na mpishano ulio tofauti kati yake kuhusiana na tarehe
iliyowekwa na ile ya zamani asilia. Utaratibu wa Helleli kwa hakika, unaweka
mifumo miwili hii mbali kwa kipindi cha takriban zaidi ya mwezi mmoja (kama
ilivyotokea mwaka 1997). Maamuzi ya Baraza ka kuweka Kanuni la Nicaea yalifanywa
huko mjini Constantinople (mwaka 381) lakini nyaraka za Constantine zanaonyesha
dhahiri kuwa ziliandikwa kabla ya mkutano huu uliounda Kanuni I ya Mtaguso wa Antioki
a wa mwaka 341 ikionyesha kwamba maaskofu wa Syria kangia kipindi hiki
walikubaliana na mafundisho na itikadi ya Warumi, ambayo kwa kweli yalitokana
na maamuzi yaliyopitishwa huko Alexandria. Kanuni na sheria zilijulikana kuwa
ni kama ifuatavyo:
1. Easter ni
lazima iadhimishwe na watu wote ulimwenguni kote na ni siku hiyohiyo ya
Jumapili;
2. Jumapili hii
ni lazima iwe ile inayofuatia siku ya kumi na nne ya mwezi inaoadhimishwa Paschal;
3. Mwezi ndio
uwe kigezo cha upangaji wa maaadhimisho ya paschal [au Pasaka] ambavyo ni siku
ya kumi na tano inayofuatia siku ya masaa ya mchana na usiku kulingana majira
ya baridi [kutokana na sheria za kale ni siku ya 14 Nisan iliangukia kwenye
siku ya masaa ya usiku na mchana kulingana majira ya baridi na sio kabla yake;
nah ii ndiyo maana ya usemi huu kwamba inayofuatia
baada ya siku ya usiku na mchana kulingana masaa ya majira ya baidi];
4. Ni kwamba
matoleo mengine yanapaswa yafanyike – huenda na makanisa ya Alexandria ambayo
yamebobea sana kwenye elimu ya kuhesabu nyota na mambo ya angani – ili kuweza
kuweka majira kamilifu na tarehe ya kuadhimisha Easter na kuwasiliana na
ulimwengu mwingine uliobakia (tazama jarida liitwalo Leo to the Emperor Marcian
in Migne, P. L., LIV, 1055).
Kwa hiyo uwekaji
wa siku ya kuadhimisha Easter unaofanywa na waumini wa mrengo wa Jumapili
ulitokana na imani na itikadi za kale ya uhesabuji wa mwezi wa Nisan, na
uliutangulia utaratibu wa kalenda ya Hilleli. Ufafanuzi kuhusu jinsi
walivyoamua na kuweka unaonyesha kwamba utaratibu wa Hilleli haukuwa unatumika
hata kwa namna ya kiusaidizi, zaidi ya kuwa tu ya ile ya uahirisho na mara
nyingine hata kwenye kiwango cha kupuuzia nyongeza ya mwezi mmoja, jambo ambalo
kwa kweli lilikuwa ni sahihi.
Kwa
hakika, Kanisa lilikuwa likiiadhimisha Paska kiusahihi hadi kufikia kipindi cha
Polycarp na cha mabishano ya wa Quartodeciman kipindi ambacho karibu Kanisa liparaganyike
mapande mawili. Nusu ya waumini wa Kanisa waliitunza vyema hadi kufikia
takriban mwaka 190 BK.
Wakiweka
msingi wao kutoka kwenye mtaguso huu wa Nicaea, makanisa ya mrengo wa Jumapili
yanashikilia msimamo wao kuwa sikukuu ya Easter ya mwaka 1997 iliyofanyika kwenye
siku mbili za mwisho za Mikate Isiyotiwa Chachu na sio siku ya kwanza kama
walivyofanya tangu mwanzoni. Hata hivyo, wanaendelea bado kuhesabu kwenye mwezi
wa Nisan kwa mujibu wa kanuni hizohizo walizozitumia siku za kale. Walikuwa
wanafanya hivyo kwa kipindi cha takriban miaka 200 kabla ya kuanzishwa kwa kalenda
ya Hilleli iliyoanzishwa mwaka 358 BK kwa kuwa ilichukuliwa kuwa ni iliyotokana
na markebisho ya siku za karibuni zaidi na kukiuka sheria zinazosimamia
uataratibu wa kupanga siku ya maadhimisho ya Sikukuu.
Hakuna
kanisa lilote, liwe la Kiutatu ama lenye kuamini Mungu mmoja lililochuua utaratibu
uliofuatia wa Wayahudi au wa Hilleli. Haikufanyika hivyo hadi ilipofika
takriban karne ya ishirini ndipo utaratibu huu wakimakosa wa kupanga kalenda
ulichukuliwa na Kanisa, na ni kwenye tawi peke yake. Hakuna wakati wowote ambao
Kanisa lilifuata utaratibu wa Wasamaria wa kupangilia mwaka kutoka tarehe 25
Machi. Hata hivyo, tutajionea hilo kwenye jarida la Mwezi na Mwaka Mpya
(Na. 213) [The Moon and the New Year (No. 213)] ambao hatimaye ulikuja
kuwa ni Mwaka Mpya kwenye mataifa yaliyo kwenye nchi zinazojulikana kama za Anglo-Saxons
na kwenye nchi ningine nyingi hatimaye.
Utaratibu
Mpotofu Kuhusu Mwezi wa Nane
Tutakwenda
kujionea sasa ni kwanini Mungu alimshughulikia Yeroboamu kwa kitendo chake cha
kuweka utaratibu mbaya wa maadhimisho ya mwezi wa Nane.
1Wafalme 13:1-3 Na tazama, akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba. 2 Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa katika nyumba ya Daudi, jina lake Yosia; na juu yako atawachinja makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu yako. 3 Akatoa ishara siku ile ile, akasema, Hii ndiyo ishara aliyoinena Bwana, Tazama, madhabahu itapasuka, na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.
Mungu
anatoa mafundisho kadhaa hapa kwenye andiko hili. Anasema kwamba anamtia mafuta
mtu mwingine, na anatabiri marejesho mapya yatakayofanywa na Yosia. Kwa hiyo
kwa kupitia unabii anamtaja Yule atakayekuwa mtiwa mafuta wake anayetuatia na
kuwa atakuwa nani. Hii ilitokea wakati mfalme alipokuwa yungali madarakani bado.
Yeroboam
alidhania kuwa angeweza kumuua nabii huyu wa Mungu. Hakujua kuwa ni Mungu peke
yake ndiye anayeshughulika na manabii zake, na wanaweza kuuawa tu pale
anapoamua na kuona kuwa wamekwisha timiliza mapenzi yake na ndipo vifo vyao
vinaweza kuwa ni mfano au ushuhuda dhidi ya imani ile ambayo kwayo wametumwa
kuionya.
1Wafalme 13:4-10 Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena. 5 Madhabahu ikapasuka, majivu ya madhabahuni yakamwagika, sawasawa na ishara aliyoitoa mtu wa Mungu kwa neno la Bwana. 6 Mfalme akajibu, akamwambia yule mtu wa Mungu, Umsihi sasa Bwana, Mungu wako, ukaniombee, ili nirudishiwe mkono wangu tena. Yule mtu wa Mungu akamwomba Bwana mkono wa mfalme ukarudishwa tena, ukawa kama ulivyokuwa kwanza. 7 Mfalme akamwambia mtu wa Mungu, Karibu nyumbani kwangu ujiburudishe, nami nitakupa thawabu. 8 Mtu wa Mungu akamwambia mfalme, Ujaponipa nusu ya nyumba yako, sitaingia pamoja nawe, wala sitakula chakula, wala sitakunywa maji mahali hapa; 9 maana ndivyo nilivyoagizwa kwa neno la Bwana, kusema, Usile chakula cho chote wala usinywe maji, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia. 10 Basi akaenda zake kwa njia nyingine, wala hakurudi kwa njia ile aliyoijia Betheli.
Somo linalomhusu
huyu nabii ni la muhimu. Mungu anawatumia watumishi wake manabii wawaelekeze na inawapasa kuyatii.
Tukio hili zima limefanywa kuwa kama somo kwetu katika utii wetu kwa Mungu.
Mkosaji anaweza kurejeshwa upya tu kwa kupitia kwa msemaji aliyepewa ujumbe na
Bwana. Ayubu alikuwa mfano wa jambo hili, na Yeroboam aliujua ukweli huo ksms
tunsvyomuona akiomba aponywe.
1Wafalme 13:11-32 inasema: Basi nabii mmoja
mzee alikuwa akikaa katika Betheli; na wanawe wakamwendea wakamwambia kila neno
alilolitenda yule mtu wa Mungu siku ile katika Betheli; na maneno aliyomwambia
mfalme, hayo nayo walimwambia baba yao. 12 Baba
yao akawaambia, Amekwenda zake kwa njia ipi? Kwa maana wanawe walikuwa wameiona njia ile
aliyoiendea yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda. 13 Akawaambia wanawe, Nitandikieni punda.
Wakamtandikia punda, naye akampanda. 14 Akamfuata mtu wa Mungu, akamkuta ameketi
chini ya mwaloni, akamwambia, Je! Wewe ndiwe yule mtu wa Mungu aliyetoka katika
Yuda? Akamwambia, Mimi ndiye. 15 Akamwambia, Karibu kwangu nyumbani, ule
chakula.16 Naye akamwambia, Siwezi kurudi pamoja nawe, wala kuingia pamoja nawe; wala
sili chakula wala sinywi maji pamoja nawe hapa; 17 kwani nimeambiwa kwa neno la Bwana, Usile
chakula wala usinywe maji huko, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia. 18 Akamwambia,
Mimi nami ni nabii kama wewe, na malaika akaniambia kwa neno la Bwana, kusema,
Mrudishe pamoja nawe nyumbani kwako, ale chakula, akanywe maji. Lakini alisema
uongo. 19 Basi mtu yule akarudi pamoja naye, akala chakula, akanywa maji nyumbani
mwake. 20 Hata ikawa, walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia nabii yule
aliyemrudisha; 21 akamlilia yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda, akinena, Bwana asema
hivi, Kwa sababu umeiasi kauli ya Bwana, wala hukuishika amri ile aliyokuamuru
Bwana, Mungu wako, 22 bali umerudi, ukala chakula ukanywa maji, hapo alipokuambia, Usile chakula,
wala usinywe maji; maiti yako haitaliingia kaburi la baba zako. 23 Basi ikawa,
alipokwisha kula chakula na kunywa maji, yule nabii aliyemrudisha akamtandikia
punda. 24 Na alipokuwa amekwenda zake, simba alimkuta njiani, akamwua. Maiti yake
ikatupwa njiani, na yule punda akasimama karibu naye; na yule simba naye
akasimama karibu na maiti. 25 Na tazama, watu wakapita, wakauona mzoga
umetupwa njiani, na yule simba akisimama karibu na mzoga, wakaenda, wakatoa
habari katika mji ule alimokaa yule nabii mzee. 26 Na yule nabii aliyemrudisha njiani
alipopata habari, akasema; Ndiye yule mtu wa Mungu, aliyeiasi kauli ya Bwana;
kwa hiyo Bwana amempambanisha na simba, simba akamrarua, akamwua, sawasawa na
neno la Bwana alilomwambia. 27 Akawaambia wanawe, akasema, Nitandikieni
punda. Wakamtandikia. 28 Akaenda, akamwona yule maiti ametupwa njiani, na punda na simba wamesimama
karibu na maiti; yule simba alikuwa hakumla maiti, wala hakumrarua punda. 29 Nabii yule
akamtwaa maiti wa yule mtu wa Mungu, akamweka juu ya punda wake, akamrudisha;
yule nabii mzee akaenda mjini mwake, kukaa matanga, na kumzika. 30 Akamweka maiti
katika kaburi lake mwenyewe; wakamlilia, wakisema, Aa! Ndugu yangu! 31 Hata ikawa,
alipokwisha kumzika, akawaambia wanawe, akasema, Nikifa mimi, nizikeni katika
kaburi hili alimozikwa yule mtu wa Mungu; iwekeni mifupa yangu kando ya mifupa
yake. 32 Kwa maana neno hilo alilolia juu ya madhabahu katika Betheli, kwa neno la
Bwana, na juu ya nyumba zote za mahali pa juu zilizo katika miji ya Samaria,
hakika litatimizwa.
Nabii alijaribiwa
ili kumfanya awe mtiifu. Nabii mwingine akaje kumdanganya. Aliruhusiwa afanye
hivyo ili iwe mfano wa mashahidi wa uwongo. Nabii wa kwanza alikuwa ni mfano
wan eno la Bwana na akashuhudia nguvu za matendo yake. Ila hatimaye alipokabiliana
na nabii mwingine aliyenena maneno kinyume na maelekezo aliyopewa na Mungu,
alimuamini mtu mwingine na sio neno la Mungu alilolijua kuwa ni la kweli. Alilipa
gharama ya kosa hili kwa uhai wake. Ili kuonyesha kuwa ametilimiza unabii,
kakuzikwa kwenye makaburi ya baba zake, bali manabii walimzika kwenye kaburi
lake mwenyewe, ambalo hatimaye angeweza kuzikiwa na Yule aliyesababisha kifo
chake. Jambo hili linafanyika hata
kwenye siku zetu hizi na kwenye mazingira yetu pia. Tumeona maelekezo ya neno
la Mungu. Tumejionea jinsi tulivyoitwa na uweza wa Mungu, lakini bado tunafuata
maelekezo ya wanadamu na sio neno la Mungu. Hili limekuwa ni tatizo kwa muda
mrefu sasa kwenye nchi hii, na Mungu anatenda kazi akishughulika na Kanisa.
Waumini walio kwenye Kanisa la Mungu wajiepushe kuwa kama alivyokuwa Yeroboam,
vinginevyo, au kila mmoja wao, awe mkubwa au mdogo, watapoteza na kukosa kuwa
na sehemu katika Ufalme wa Mungu.
1Wafalme 13:33-34 Baada ya hayo Yeroboamu hakuiacha njia yake mbovu,
lakini akafanya tena makuhani wa mahali pa juu, wa watu wo wote. 34 Kila aliyetaka
akamfanya wakfu, ili wawepo makuhani wa mahali pa juu. Jambo hilo likawa dhambi
kwa nyumba ya Yeroboamu, hata kuiharibu, na kuifuta usoni pa nchi.
Ni kama Yeroboam
alivyowaweka utumishini waalimu wa uwongo waliofundisha na kuzua mafundisho ya
uwongo na kushamirisha ibada za sanamu, ndivyo ilivyotokea pia kwa Kanisa
lilijichanganya kwa kuyapa nafasi mafundisho ya uwongo, kwa kuliona neno la
Mungu halina nguvu na kufundisha mawazo ya wanadamu. Watu wanaofundisha kwa
lengo la kujipatia ajira ndio hasa waliofuata mafundisho haya ya uwongo. Mijada
ya uwongo imeshamiri sana ikilenga kuhalalisha mafundisho ya uwongo. Moja ya
mifano kuhusu wajumbe au watumishi wa Mungu (tazama jarida la Watumishi wa Mungu (Na. 184) [The Oracles of God (No. 184)]. Mijadala imeenea kwa kusema kuwa
Wayahudi wana manabii wa Mungu na kwamba wanahusika na mambo yote ya Kalenda.
Kama hilo ni kweli, ni kwa nini watu hawahawa wanalikubalia Agano Jipya lililokataliwa
na imani ya Kiyahudi? Ne, ni kwa nini wanaiadhimisha Pentekoste siku ya
Jumapili wakati Wayahudi wanaitunza siku ya 6 Siwani?
Waalimu hawahawa
wenye mafundisho ya uwongo wanasema kile kilicho muafaka na sio kile kilicho
sahihi.
Yeroboam bado
hajatubu kwa uovu wake huu.
1Wafalme 14:1-5 Siku zile akaugua
Abiya, mwana wa Yeroboamu. 2 Yeroboamu akamwambia mkewe, Ondoka,
tafadhali, ujibadilishe, wasikujue kuwa mkewe Yeroboamu; ukaende Shilo; tazama,
yuko huko Ahiya nabii, aliyeninena mimi ya kwamba nitakuwa mfalme juu ya watu
hawa. 3 Twaa mkononi mikate kumi, na kaki, na mtungi wa asali, ukamwendee; naye
atakuambia kijana atakuwaje. 4 Akafanya hivi mkewe Yeroboamu, akaondoka,
akaenda Shilo, akaja nyumbani kwa Ahiya. Basi Ahiya hakuweza kuona; kwa kuwa
macho yake yamepofuka kwa sababu ya uzee wake. 5 Bwana akamwambia Ahiya, Angalia, mkewe
Yeroboamu anakuja akuulize mambo ya mwanawe; kwa maana hawezi; hivi na hivi
umwambie; kwani itakuwa akiingia atajifanya kuwa mwanamke mwingine.
Watu hao
hawakumuogopa Mungu. Nguvu za Mungu na uhusiano wa Mungu na watumishi wake
manabii haikueleweka. Yeroboam alitaka kuwaomba msaada na ushauri manabii, bali
hakuamini kamwe kuwa walikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Mungu. Ni
makuhani waliowekwa wakfu tu peke yao ndio walichukuliwa kuwa na umuhimu wa
muda mrefu wa kudumu. Na hii ndiyo sababu manabii walikuwa wanauawa. Walichagua
kumtii Mungu na sio wanadamu.
1Wafalme 14:5-16 Bwana akamwambia Ahiya, Angalia, mkewe Yeroboamu
anakuja akuulize mambo ya mwanawe; kwa maana hawezi; hivi na hivi umwambie;
kwani itakuwa akiingia atajifanya kuwa mwanamke mwingine. 6 Ikawa, Ahiya
alipoisikia sauti ya miguu yake, akiingia mlangoni, alisema, Karibu, mkewe
Yeroboamu; mbona wajifanya kuwa mwingine maana nimetumwa kwako wewe, mwenye
maneno mazito. 7 Nenda, umwambie Yeroboamu, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa kuwa
nilikutukuza miongoni mwa watu, nikakufanya uwe mkuu juu ya watu wangu Israeli,
8 nikaurarulia mbali ufalme utoke nyumba yake Daudi, na kukupa wewe; walakini
wewe hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, aliyezishika amri zangu, na kunifuata
kwa moyo wake wote, asifanye lo lote ila yaliyo mema machoni pangu; 9 lakini umekosa
kuliko wote waliokutangulia, umekwenda kujifanyia miungu mingine, na sanamu
zilizoyeyuka, unikasirishe, na kunitupa nyuma yako; 10 tazama, kwa hiyo mimi nitaleta mabaya juu
ya nyumba yake Yeroboamu, nami nitamkatia Yeroboamu kila mwanamume, aliyefungwa
na aliyeachwa katika Israeli, nami kuondoa nitawaondoa waliobaki wa nyumba yake
Yeroboamu, kama mtu aondoavyo mavi, hata itakapokwisha pia. 11 Yeye afaye wa
Yeroboamu mjini mbwa watamla; afaye mashambani ndege wa angani watamla; kwa
kuwa Bwana amelinena hilo. 12 Basi ondoka, urudi nyumbani kwako; na
miguu yako itakapoingia mjini huyo kijana atakufa. 13 Na Israeli wote watamlilia, na kumzika,
kwa maana ndiye peke yake wa Yeroboamu atakayeingia kaburini; kwa sababu
limeonekana ndani yake jambo lililo jema kwa Bwana, Mungu wa Israeli, nyumbani
mwa Yeroboamu. 14 Tena Bwana atajiinulia mfalme wa Israeli atakayeiharibu nyumba ya Yeroboamu
siku ile; na nini tena hata sasa? 15 Kwa kuwa Bwana atawapiga Israeli kama
manyasi yatikiswavyo majini; naye atawang'oa Israeli katika nchi hii njema,
aliyowapa baba zao, naye atawatawanya ng'ambo ya Mto; kwa sababu wamejifanyia maashera
yao, wakimkasirisha Bwana. 16 Naye atawatoa Israeli kwa ajili ya makosa
ya Yeroboamu, aliyoyakosa, ambayo kwa hayo amewakosesha Israeli.
Dhambi za
viongozi wa watu ziliwafikia watu wao. Dhambi za Yeroboam zilikuwa ni kubwa
sana. Ya kwanza ilikuwa ni ile ya kubadili maadhimisho ya Sikukuu hadi mwezi wa
Nane. Alihukumiwa kwa ajili ya jambo hili. Hata hivyo, hakukata tamaa kuiabudu
miungu yake ya uwongo na kwa sababu hiyo na kwa Maashera, Israeli walifukuzwa
na kupelekwa mbali utumwani, nyumba ya Yeroboam ilihukumiwa na kulikuwa na vita
na Yuda siku zote za uhai wake, kwa wote wawili, yaani na rehoboam na Abiya (1Wafalme
15:6-7).
1Wafalme 14:17-20 Basi
mkewe Yeroboamu akaondoka, akaenda zake, akafika Tirza; naye alipofika
kizingitini kwa nyumba, huyo kijana akafa. 18 Israeli wote wakamzika, wakamlilia;
sawasawa na neno la Bwana, alilolinena kwa mkono wa mtumishi wake Ahiya nabii. 19 Na mambo yake
Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika
kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli. 20 Na siku alizotawala Yeroboamu zilikuwa
miaka ishirini na miwili; akalala na babaze, naye Nadabu mwanawe akatawala
mahali pake.
Yeroboam
aliwasababisha Israeli wafukuzwe na kwenda mbali utumwani kwa ajili ya uongozi
wake mbovu na dini yake ya uwongo. Yuda nao hawakuwa na afadhali yoyote, na
mabaki au masalio ya Wasamaria walikuwa ni wachache na kundi dogo na wakiwa
wamebakia kwa ajili ya kutimiliza usemi na ni mchanganyo wa moja kwa moja
kuhusu haki ya uzaliwa wa kwanza ya Efraimu, ambaye kwaye wanadai kuwa ni wazao
wake. Efraimu ni donge aminifu. Uzao wake utafanyika kuwa mataifa mengi (Mwanzo
48:19; 49:26). Masihi atarudi hivi karibuni na Wasamaria na Wayahudi watafanywa
wayajue makosa yao kwenye kipindi hiki cha muhimu sana ambacho ulimwengu wote
utamuabudu Mungu Mmoja ma Wapekee na wa Kweli.
Israeli wanarithi
ahadi waliyopewa licha yakustahili na kujitoa kwao. Mungu atayafungua macho yao
na watayaona makosa yao zitakapofika Siku Hizo.
q