Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[256]

 

 

 

Sheria na Amri ya Nne

(Toleo La 4.0 19981007-20050717-20080320-20120711)

 

 

Amri ya Nne ya Mungu inahusu Sabato au pumziko. Hii inajumlisha na Sabato ya kila Siku ya Saba ya Juma, Siku Takatifu, Sabato ya kila Mwaka wa Saba ya Mapumziko ya Ardhi na Utaratibu wa Yubile. Hizi zote zimefungamanishwa kutokana na Kalenda ya Mwandamo wa Mwezi na Mwelekeo wa Nyota na ni za muhimu kuadhimishwa kwa manufaa ya wote wenye mwili (Mk.2:27). Zinasimama pamoja au zinaanguka pamoja (Kol.2:16-17).

 

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Haki Miliki © 1998-2012 Christian Churches of God, ed. Wade Cox)

 

Masomo haya yanaeza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Sheria na Amri ya Nne

 


“Siku ya Sabato ni Takatifu kwa Bwana kwa mujibu wa Amri ya Nne ya Mungu (Kutoka 20:8-11). Amri hii imewekwa ili kuwafanya watu wote wapumzike (Kumbukumbu la Torati 5:14). Siku hii inajulikana kama siku ya Jumamosi kwa mujibu wa mpangilio wake wa kimahesabu uliotokana kwa mujibu wa chanzo chake cha tangu uumbaji. Inajulikana na mataifa yote kama ni siku ya Sabato na kwamba inaangukia siku ya Jumamosi ya kalenda iliyoko sasa ya juma. Siku hii ya saba iko kwenye mzunguzo endelevu na haiwezi kuwekwa kwenye siku nyingine yoyote” (Cox, W.E., “A” kwenye jarida lake la Sabato (Na. 31) [The Sabbath (No. 31)], lililochapishwa na CCG. 1994-2008, ukurasa wa 2).

Siku ya Sabato

Utaratibu wa jinsi ya kuitunza Sabato hii ya juma umeainishwa kwenye kitabu cha Kutoka 20 na Kumbukumbu la Torati 5.

Kutoka 20:8-11 inasema:

Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 11 Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.

 

Kumbukumbu la Torati 5:12-15 inasema:

Ishike siku ya Sabato uitakase, kama BWAA, Mungu wako, alivyokuamuru. 13 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 14 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala ng’ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako yeyote, wala mgeni aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vilevile kama wewe. 15 Nawe utakumbuka ya kuwa wewe ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, na ya kuwa BWANA, Mungu wako, alikutoa huko na mkono wenye nguvu, na mkono ulionyoshwa; kwa sababu hiyo, BWANA, Mungu wako, alikuamuru uishike Sabato.

 

Katika Kamusi ya Kiebrania iitwayo Strong Hebrew’s Dictionary (SHD 7676), neno sabbat linamaana ya kupumzika yaani kutoka kwenye shughuli ngumu za mahangaiko, (kusababuisha kuacha, kujiachia, kujifanyiza) kusimama au kuachana na shereheko: (kufanya kuwa) mapumziko, kupumzika, kutoshughulika, kuachana au kuachilia.

Kutoka 23:12 inasema: "Siku sita utafanya kazi yako, na siku ya saba utapumzika; ili kwamba ng'ombe wako na punda wako wapate kupumzika, kisha mwana wa mjakazi wako na mgeni wapate kuburudika”.

 

“Maadhimisho ya Sabato yanaendana na kicho kwa Bwana na kupaheshimu Patakatifu pake (mambo ya Walawi 19:30), jambo ambalo sisi tunalifanya. Kwa hiyo, siku hii ya Sabato iliwekwa kwa ajili ya wanadamu ili kuitakatifusha Maskani yake Bwana na kuifanya iwe mahali maalumu na muafaka pa kuweka makazi yake Mungu. Sambamba na hilo, Sabato inaendana na tendo la kuwaheshimu mama na baba (Mambo ya Walawi 19:3)” (Cox, “A”, kitabu hichohicho, ukurasa wa 4).

 

Siku ya saba huanzia mwishoni mwa siku ya sita ya juma, ambayo ni Ijumaa kama tulivyozoea kuiita, wakati giza linapoanza (EETN) (Mwanzo 1:5; Zaburi 104:20; Mambo ya Walawi 23:32. Matendo 27:27-33). Sabato hii ya siku ya saba inabakia kwa wanaoiadhimisha na kuitunza ambao pia ni watu wanaolirejesha u[ya agano (Waebrania 4:9; Wakolosai 2:16-17).

Waebrania 4:9-11 inasema: Basi, imesalia raha ya Sabato [SGD4520] kwa watu wa Mungu. 10 Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake. 11 Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu ye yote asije akaanguka kwa ,fano huohuo wa kuasi.

 

“Tendo hili la kuitunza Sabato linaendana na ukusanyikaji pamoja na kufanya ibada, kama ilivyofundishwa na Mtume Paulo (Waebrania 10:23-25). Tendo la kukusanyika siku ta Sabato limeamriwa na Mungu kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi:

Mambo ya Walawi 23:1-3 inasema: Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia, 2 Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Sikukuu za BWANA, ambazo mtazipigia mbiu kuwa ni makusanyiko matakatifu; hizi ni sikukuu zangu. 3 Mtafanya kazi siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, kusanyiko takatifu, msifanye kazi ya namna yoyote; ni Sabato kwa BWANA katika makao yenu yote.

 

Neno la Kiebrania litumikalo kuelezea mapunziko ni migra, ambalo maana yake ni kuitisha makutano na kukutanika (pamoja), na kwa mujibu wa Kitabu cha fasiri cha Young’s Analytical Concordance, neno Migra ndilo lililotumika kwenye Mambo ya Walawi 23:4-44 kuyaelezea makutaniko yote matakatifu yaliyoamriwa na Mungu kuwa ni Sabato zake kuu na takatifu. Ili kuwasaidia watu wake wazitunze Sabato zake na kuzitakatifuza, Mungu aliwapa siku ya sita kuwa ni siku ya maandalio (kama inavyosema Kutoka 16:1-21).”

 

Maadhimisho ya Sabato

 

Maandalio ya Sabato

“Tumeamriwa kufanya maandalio au kuiandaa Sabato ifikapo siku ya sita ya juma (kama inavyosema Luka 23:54). Kwa kufanya maandalio maalumu na halisi tunaweza sote kuwa na mapumziko muafaka ya Sabato kwa kadri alivyotuamuru Mungu, na kuitunza Sabato hii kwa hali yake takatifu. Wakati baba yetu amri ya kuitenga siku ya kufanya maandalio na amri ya kuitunza Sabato, alikuwa anatutengenezea njia ya kumfuata yeye na kuyashika mapenzi yake (sawa na ilivyo kwenye Mwanzo 2:2-3). Kama tutazitii amri zake na kuacha kuyafanya yanayotupendeza wenyewe na yenye ‘kutufaidisha’ sisi wenyewe siku ya Sabato, ndipo tutaweza kumjua Mungu wa Kweli na Kristo wake, jambo linalotupelekea kuupata uzima wa milele (Yohana 17:3). Pia soma jarida la Uzima wa Milele (Na. 133) [Eternal Life (No. 133)].

 

Tunapoitumia siku hii ya maandalio kwa kuitafakari na kuichukulia Sabato kuwa ni siku ya kuwa karibu na Mungu na kujitenga na dunia na mambo yake yote na kuweka kando mambo yetu mengine yote, na kuwa mbali na mambo yetu mengine yote ya kidunia na kutojihusisha nayo na kuyafanya wakati Sabato itakapoanza. Na tunapokutanika pamoja katika siku hii ya Sabato na kujifunza kujifunza Neno takatifu la Mungu kama alivyofanya Mariamu, tunakuwa tumeamua ‘kuchagua uamuzi mzuri’” (Kwa mujibu wa Cox, W.E., “B” jarida lake la Ijumaa: Maandalio ya Sabato (Na. 285) [The Juma’ah: Preparing for the Sabbath (No. 285)], na kitabu chake cha CCG, 1999-2008, ukurasa wa 2,9).

 

Hakuna Kufanyakazi Siku ya Sabato

“Hatupaswi kuwa wavivu na kutofanyakazi. Chochote tunachoweza kukifanya kwa mikono yetu, na tukifanye kwa bidii na nguvu zetu zote (Mhubiri 9:10). Kwa kuwa kile tunachokipanda ndicho tunachokivuna (Wagalatia 6:7). Pia tunatakiwa kuwatumikia na kuwasaidia ndugu zetu wapendwa wengine wote, hususan walio wageni miongoni mwetu (3Yohana 5-7).

 

Hakutakiwi kufanywa kazi yoyote siku ya Sabato kwa mtu yeyote binafsi yake wala kwa kikundi chochote kwenye jamii kilichopo kwenye milki ya Israeli. Bali Amri na Sheria ilitakiwa itunzwe ama kuadhimishwa na Israeli wote—kwa mgeni na kwa Muisraeli wote amri ilikuwa ni moja tu. Nehemia anatupa mfano kwa dhana hii ya jinsi sheria au amri inavyopaswa kutunza na kuadhimishwa siku ya Sabato gives us examples as to the manner in which.

Nehemia 10:28-31 inasema: Na watu waliosalia, makuhani, walawi, mabawabu, waimbaji, Wamethini, na hao wote waliojitenga katika watu wa nchi kwa torati ya Mungu; wake zao, na wana wao, na binti zao, kila mwenye maarifa na akili; 29 wakaambatana na ndugu zao, wakuu zao nao wakaingia katika laana na kiapo, ya kuwa wataiendea torati ya Mungu, iliyotolewa kwa mkono wa Musa, mtumishi wa Mungu, na kuziangalia, na kuzitenda, amri zote za BWANA, Bwana wetu, na hukumu zake na sheria zake; 30 wala tusiwaoze watu wan chi binti zetu, wala kuwatwalia wana wetu binti zao; 31 tena watu wan chi wakitembeza biashara,  au chakula chochote, siku ya Sabato, tusinunue kwao siku ya Sabato, au siku takatifu; tena kwamba tuuache mwaka wa saba, na madai ya kila deni

 

Hairuhusiwi kubeba mzigo wowote siku hii ya Sabato, wala haukuruhusiwa kuingizwa kwenye mji wa Yerusalemu (Yeremia 17:21). Kwa hiyo tunapaswa kufurahia siku hii ya Sabato na kuleta furaha kwenye Nyumba ya Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo, hata kufanya kazi kwenye mali za mtu kumekatazwa pia siku hii ya Sabato. Inatakiwa iwe hivyo ili kuipisha na kuitakativusha Sabato na ndiyo inayotakiwa itukuzwe peke yake.

 

Kuishika Sabato ni sharti la muhimu kwa mwanadamu ili aweze kuurithi ufalme wa Mungu wa Israeli. Hakuna mzigo ulioletwa ama kuingizwa ndani ya malango ya mji. Wafalme na Wana wa ufalme wote wataketi kwenye kiti cha enzi cha Daudi. Na kama maonyo haya hayatatiliwa maanani ndipo mji utaangamizwa kwa moto (Yeremia 17:27). Kwa hiyo, Sabato ni ishara na chanzo cha kubezwa na kuteswa kwa wale walio wa Nyumbani mwake Mungu. Mfale na kuhani wawaka hasira kwa kutiwaunajisi Sabato (Maombolezo 2:6).

Maombolezo 2:6 inasema: Naye ameondoa maskani yake kwa nguvu, Kana kwamba ni ya bustani tu; Ameziharibu sikukuu zake; Bwana amezisahauzisha katika Sayuni Sikukuu za makini na sabato; Naye amewadharau mfalme na kuhani Katika uchungu wa hasira yake.

 

Kwa hiyo, sabato inajulikana kuwa inawakilisha mfumo wa kipekee kwa watu wa Mungu. Inaendelea kuwa ya muhimu kwao wote na hakuwezi kuwa na kufanyika mauzo au biashara siku hii ya Sabato au kwenye Siku Takatifu yoyote iliyoamriwa, kwa mtu yeyote mongoni mwao au hata kumruhusu Mmataifa (asiye miongoni mwa aweaminio).

 

Yeyote anayeitia unajisi Sabato sharti lililowekwa ni kuuawa (Kutoka 31:14; Hesabu 15:32-36). Hukumu hii inamaanisha au kuashiria ufalme wa milele walioahidiwa ama kupewa wateule. Wanakatiliwa mbali na watu wao, ambayo kutouingia uzima wa milele. Hii ni ishara kati ya Mungu na wana wa Israeli milele (Kutoka 31:17). Neno milele maana yake ni Olam (SHD 5769) na linamaanisha tendo la wakati wote, lisilokoma, la milele, lenye kudumu hivyo (milele), lisolo na mwisho, nk.

 

Kazi ya Makuhani Siku ya Sabato

Ni jambo la kawaida sana kwamba makuhani wakiwa Hekaluni wanaweza kuihalifu Sabato (na ni kawaida) na hawahesabiwi kuwa na hatia (Mathayo 12:5; sawa na Hesabu 28:9-10; pia tazama Nehemia 13:7; Ezekieli 24:21; Yohana 7:22-23). Kwa hiyo, kazi zozote tunazozifanya sisi wateule zinazohusiana na kumfanyia Mungu ibada siku hii ya sabato haina makosa wala haihesabiwi hatia. Na kwa kweli, kulikuwa na dhabihu nyingi sana zilizokuwa zikiletwa Hekaluni siku ya Sabato kuliko siku nyingine yoyote ile ya juma.

 

Sadaka ya kuteketezwa motoni ililetwa na kutolewa na kuhani kwa niaba ya wana wote wa Israeli siku ya Sabato, kuwa sadaka ya milele kwao (Mambo ya Walawi 24:8). Sadaka hii iliamriwa kutolewa na wateule kwamba waitoe na kuiombea na kutoa shukjurani wao kwa Bwana kila siku ya Sabato. Kwa hiyo tumeamriwa kutoa sadaka zetu tunapokusanyika. Kinachoelezewa inazidi kwenye ayah ii ya mambo ya Walawi 24:1-4 ni kwamba inampasa kuhani ahakikishe kuwa taa zote ziwe zijazwa mafuta safi ya kila siku yaliyofanywa kwa kukamua mzeituni. Kwa hiyo inatukumbusha leo kuwa maandalizi ya wateule ni wajibu wa kila siku, na taa za wanawali ni lazima zitengenezwe na ni kazi ya kila siku, yaani Sabato hadi sabato nyingine. Wanatakiwa na ni wajibu wao kabisa kuzitunza na kuziadhimisha Sabato hizi za Mungu (Ezekieli 44:24).

 

Nehemia aliamuru kuwa hata wageni wazitunze pia Sabato. Huyu ni mfano wetu kwa jinsi tunavyopaswa kuitunza Amri hii inavyopaswa kufuatwa na kuishika. Nehemia 13:22 inaonyesha kuwa ni wajibu wa Bwana—kuhani mpya wa wateule—kujitakasa wenyewe na kulinda malango ili kuhakikisha Sabato zinaadhimishwa katika utakatifu wake.

 

Kadiri tunwezavyo, tujitahidi kuwa tunaacha kufanya kazi, au kusimamisha shughuli zetu zote siku ya Sabato, na tusinunue wala kuuza, na tunapaswa kufanya hivyo, na tunapaswa kupingana na kushinda aina yoyote ya upinzani. Hatupaswi kununua pia kwenye Siku Takatifu. Tusiende kwenye mikahawa siku za Sabato na Siku Takatifu za Bwana.

Nehemia 13:15  Siku hizo naliona katika Yuda watu wengine waliokanyaga mashinikizo ya mvinyo siku ya sabato, na wengine waliochukua miganda, na kuwapakia punda zao; tena na mvinyo, na zabibu, na tini, na namna zote za mizigo, waliyoileta Yerusalemu, siku ya sabato; nami nikashuhudia juu yao siku ile waliyouza vyakula.

 

Nehemia 13:19 Ikawa malango ya Yerusalemu yalipoanza kuwa na giza kabla ya sabato, naliamuru milango ifungwe, nikaamuru isifunguliwe hata sabato iishe; na baadhi ya watumishi wangu nikawaweka juu ya malango, ili usiingizwe mzigo wo wote siku ya sabato.

 

Nehemia 10:31 tena watu wa nchi wakitembeza biashara, au chakula cho chote, siku ya sabato, tusinunue kwao siku ya sabato, au siku takatifu; tena kwamba tuuache mwaka wa saba, na madai ya kila deni.

 

Kuwasha moto siku ya Sabato

Amri isemayo, “Hamtawasha moto katika nyumba zenu kwa siku ya Sabato” inamaanisha tendo la kuwasha kwa mnajiri wa kikazi au kuwasha kwa nje na sio kuwasha majumbani na kwa matumizi ya nyumbani (Kutoka 35:1-3). Hata Hekaluni kulikuwa na dhabihu za daima. Watu walikuwa wanawasha moto muda wote. Na kama tukirudi nyuma na kuangalia aya za kwanza asilia, na kuona jinsi Sheria hii ilivyotolewa, amri hii ilikuwa inahusika na dhana ya kufanikisha na kufanikisha. Hakuna kazi ya ujenzi au ubomoaji uliofanyika au kuruhusiwa kufanywa Siku ya Sabato” (Cox, “A”, op. cit., kurasa za 2, 3, 4, 5).

 

Aya zilizo kwenye Kutoka 35:4-35 zinafafanua kazi kubwa inayoonyeshwa kwamba kwazo moto isiwashwe siku za Sabato.

 

“Hii pia haiathiri uwashaji wa moto kwa lengo la kupasha maji moto au kupasha moto kwa aina yoyote, ambao ni muhimu kwa ajili ya uzima wa watu kunakutumika sehemu nyingi za Dunia zenye hali ya hewa baridi. Inavyotokea hivyo, basi siku ya maandalio itumike kwa kazi ya kukusanya kuni au kununua mafuta na kwa ajili ya kupikia, lakini siku ya Sabato kumekatazwa kabisa. Ni kwa sababu hii ndiyo maana Kristo alikula masuke mashambani siku ya Sabato (Mathayo 12:2). Hukumu kwa asiyeenda kujihudhurisha na kumwabudu Mungu siku ya Sabato ni kifo. Kwa hiyo, kazi yoyote ya namna hii kuifanya Siku ya Sabato ni tendo la kuivunja Sheria na kuiwekwa kwenye Ufufuo wa Pili na kupelekea kwenye mauti ya pili” (sawa na Hesabu 15:32-36)” (Cox, “B”, op. cit., ukurasa wa 6).

 

“Ndipo hapa kwamba lile tendo la Bwana la kuchuma masuke siku ya Sabato lililaumiwa. Hata hivyo, Bwana alionyesha kwa matendo kwamba yeye alikuwa ndiye Bwana wa Sabato na sio kwamba alikuwa anakusudia kuonyesha kuwa Sabato haina umuhimu kuitunza kama ilivyoelekezwa hapo mwanzoni. Ni jambo muhimu kuwa na tabia ya kuandaa chakula cha kutosha ili kukila siku ya Sabato kama inavyoelekezwa kwenye ayah ii na pia kwenye Aheria na Amri za Agano Jipya (Mathayo 12:1-12).

 

Kuwatunza wagonjwa siku ya Sabato

Kristo alitoa pia amri inayohusu kuwaponya wagonjwa. Amri hii inapaswa ifanywe siku ya Sabato. Kwa hiyo, vi jambo jema sana kuwaponya na kuwalisha au kuwahudumia wagonjwa siku ya Sabato.

Yohana 7:23 Basi ikiwa mtu hupashwa tohara siku ya sabato, ili torati ya Musa isije ikavunjika, mbona mnanikasirikia mimi kwa sababu nalimfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato?

 

Marko 3:1-5 Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza; 2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki. 3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati. 4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza. 5 Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.

(sawa na Luka 6:8-10; 13:14-16; 14:3; Mathayo 12:10-13).

 

Kama inavyoruhusiwa kufanya tohara siku ya Sabato, ndivyo pia inaruhusiwa kufanya tohara ya mioyo yetu kwa njia ya kutoa na kwa uweza wa Roho. Hebu na tuhukumiane kwa hukumu ya haki kwa kutathmini mema tuyafanyayo siku hii ya Sabato (Yohana 7:21-24).

 

Ng’ombe anapotumbukia shimoni

Fundisho la ng’ombe au punda kutumbukia shimoni ni jambo la dharura na nadra kutokea. Haitoshi kufanya jambo lililopangwa mapema hapo kabla nyuma yake. Luka 14:5 inaonyesha kwamba ni muhimu kushughulika mabo ya dharura siku ya Sabato. Na kwa kweli, hii inahusu na dhana au hali ya kuwaponya watu siku ya Sabato. Tendo la kuwahudumia vizuri wagonjwa siku ya Sabato ni tatizo kubwa sana. Kwenye Kumbukumbu la Torati 5:14, kunaonekana kabisa kwamba Amri na Sheria hii imewekwa wazi kwa wote, yaani wanadamu na wanyama.

 

Moyo na nia safi kuhusu Sabato

Moyo safi unatakiwa siku ya Sanato. Haipaswi mtu kuyaangalia maslahi na mambo yake na kushughulikanayo, kwa kuwa kwa kujiepusha na hayo kutamfanya awe na hali ya uaminifu, kujitolea na kujitoa na kuwasaidia wengine (Amosi 8:5).

 

Sabato inapaswa itunzwe kwa usafi wa moyo (Isaya 1:13). Haitakiwi itiwe unajisi (Isaya 56:2, 4-7).

Isaya 56:2  Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje, auzuiaye mkono wake usifanye uovu wo wote.

 

Siku ya Sabato ni ya furaha, na sio ya maombolezo (Isaya 58:13-14). Sabato ni ya kuifurahia na kuifanya ifurahiwe na wote walio kwenye nyumba ya Mungu (Zaburi 118:24).

Isaya 56:4-7 inasema:  Kwa maana Bwana awaambia hivi matowashi, wanaozishika sabato zangu, na kuyachagua mambo yanipendezayo, na kulishika sana agano langu; 5 Nitawapa hawa nyumbani mwangu, na ndani ya kuta zangu, kumbukumbu na jina, lililo jema kuliko kuwa na wana na binti; nitawapa jina lidumulo milele, lisilokatiliwa mbali. 6 Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; 7 Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.

 

Kristo alikuwa ni mkuu kuliko Hekalu, kama sisi tulivyo wakuu kuliko Hekalu lililojengwas la kimwili. Sisi ni Hekalu na Hekalu lilijengwa kwa ajili yetu (Marko 2:27), ili tuweze kuzitunza Sabato kama maandalio ya nyumba ili kutufanya sisi tuwe haiba ya Mungu” (Cox, “A”, op. cit., kurasa za 2,3,4,5).

 

Sabato kama ishara-alama ya Kanisa

Sabato imeorodheshwa kuwa ni alama muhimu ya watu wa Mungu. Ni ishara kati yetu sisi na Mungu atutakasaye. Kwa mujibu wa (SHD 226), neno ishara linaitwa owth au oth na linamaana ya ishara, alama, kielekezi, ushahidi, nk. Mungu hutumia ishara au alama fulani ili kuwatofautisha na kuwambulisha watu wake kwa uhusiano wake maalumu naye.

Kutoka 31:12-17 inasema: Bwana akasema na Musa, na kumwambia, 13 Kisha, nena wewe na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi. 14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. 15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa Bwana; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa. 16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato, kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele. 17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Bwana alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.

 

“Utazishika Sabato zangu” (nyingi). “Sabato zinaelekea hadi kwenye kilele chote cha ibada zinazofanywa kwenye Siku Takatifu zilizoorodheshwa na kutajwa kuwa ni Sabato za Mungu. Hukumu ya kifo ni ya kiroho.

 

Sabato haiwezi kutenganishwa na ishara ya Kanisa. Pia ni ishara ya wana wa agano ambao hawajaitwa bado na kujiunga na Kanisa. Iwapo kama ilikuwa ni ishara ya wateule, basi imani ya Kiyahudi ingekuwa na sehemu katika Ufufuo wa Kwanza, jambo ambalo halipo hivyo.

 

Hali ya kuiweka Imani pamoja lilikuwa ni fundisho muhimu la Mungu. Sabato, Miandamo ya Mwezi na Sikukuu zilizoamriwa na Mungu yalikuwa ni mambo yasiyoweza kutofautishwa katika kumwabudu Mungu. Hii pia ilikuwa inaenda sambamba au kupewa mshiko na kutambua umuhimu wa sheria ya vyakula kwa hali ya undani na umuhimu wake kwa ujumla (soma jarida la Sheria Kuhusu Vyakula (Na. 15) [The Food Laws (No. 15)]. Kwa hiyo, Sabato nay ale yanayofuatananayo yote yalikuwa ni ishara ya ibada ya kweli iliyolenga kumwabudu Mungu wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3). Mungu huyu ambaye pia huitwa Eloah, alikuwa ni yeye yule aliyeabudiwa na watu wa Yuda na ndiye aliyefunuliwa kwenye Agano Jipya. Pia angalia na kulisoma jarida la Mungu Tunayemwabudu (Na. 2) [The God We Worship (No. 2)].

 

Msingi wa kibiblia kuhusu mafundisho asilia umetuama kwenye Amri Iliyokuu na ya Kwanza (kama ilivyoelezewa kwenye jarida la Amri Iliyokuu nay a Kwanza (Na. 252) [The First Great Commandment (No. 252)]. Kwa jinsi hii tunaona kwamba amri hii ya nne ndiyo amri pekee yenye sara au mtazamo mkuu na wenye muundo mkuu na muhimu. Sabato na Siku Takatifu ni sehemu ya muundo wa amri hii ya nne na inamuingiliano na amri nyingine zote.

 

Kutokana na neno linalotoka kwa Yesu Kristo mwenyewe, Baba Mungu anakuwa ndani yake na lengo la kwanza muhimu na hukamilisha lengo la Imani (Mathayo 22:37-38; Marko 12:30; Ufunuo 1:8). Ufunop wa kumjua Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli ni muhimu katika kuupata uzima wa milele (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20). Kwa hiyo, Amri hii ya nne haiishii kwake yenyewe tu bali ni ashirio la kwanza la mteule na ukweli wa utii wao kwa Mungu.

 

Amri hii ya nne pia inaendelea mbele hadi kuufanya mfumo wote wa ibada za kibiblia za Miandamo ya Mwezi, Sikukuu zilizoamriwa na Siku Takatifu na pia kwenye utoaji wa zaka. Soma jarida la Utoaji wa Zaka (Na. 161) [Tithing (No. 161)] ambayo inahusiana na mfumo wa malimbuko na Agano la Mavuno (saoma pia jarida la Agano la Mungu (Na. 152) [The Covenant of God (No. 152)].

 

Sabato ni ishara ya Kanisa la kweli la Mungu. Sio ni dalili. Ishara ya kwanza ni Imani juu ya Uungu, ambao unatokana na fundisho la kibiblia la Imani ya kuwa Mungu ni Mmoja ya muundo na mwonekano wa Kiunitari.  

 

Ishara nyingine za Wateule

Ishara inayoonekana kwa nje ya wateule ni utunzaji wa Sabato, na ushiriki wa Meza ya Bwana au Mlo wa Pasaka, vikifuatiwa na adhimisho la Mwandamo wa Mwezi na maadhimisho ya Siku zote Takatifu zilizoamriwa. Ubatizo ni ishara ya pili kumpokea Roho Mtakatifu ni mhuri au ishara ya ndani. “Ishara muhimu na ya kwanza ya agano kwa watu ilikuwa ni tohara (Mwanzo 17:10-14). Hii ilitimilizwa kwa amri au utaratibu wa ubatizo (soma jarida la Toba na Ubatizo (Na. 52) [Repentance and Baptism (No. 52)](Cox, W.E., “C” na Wajibu wa Amri ya Nne katika Historia ya Makanisa ya Mungu ya Watunza—Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)], CCG, 1996-2000, ukurasa wa 2,3,18).

 

Kama ilivyokuwa tangu siku za Kristo, ubatizo wetu ndio ukiri na agano letu la kudumu kwenye agano hili. Ubatizo huu ni ishara kwa mataifa, ambao unafanya mambo kwa namna ile ile kama ilivyokuwa ishara ya zamani ya tohara iliyofanywa na Israeli. Alama hii ashirio ilichukuliwa kutokana na desturi ya kufanya tohara ya kimwili na kufanywa kuwa ni tohara ya kiroho ya mioyoni. Kanisa liliwekwa kwenye kiwango cha mwajibiko wa utii kwa Amri za Mungu, ambapo linafanya hivyo kwa kufanya tohara ya mioyo (Kumgukumgu la Torati 30:6; Yeremia 4:4)” (Cox, W.E., “D” kwenye jarida la Agano la Mungu (Na. 152) [The Covenant of God (No. 152)], CCG, 1996-1999, pp. 2,13).

Kumbukumbu la Torati 30:6 BWANA, Mungu wako, atautahiri moyo wako, na moyo wa uzao wako, ili umpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, upate kuwa hai. (sawa pia na Kumbukumbu la Torati 10:15-16)

 

“Ubatizo wa Roho Mtaakatifu ni siahara ya kwanza pia ya wateule kupitia kwa Yesu Kristo katika Mwili mmoja (Mathayo 28:19; Matendo 1:5; 11:16; Warumi 6:3; 1Wakorintho 12:13; Waebrania 9:11-28).” Ishara nyingine ni adhimisho la Pasaka na Mikate Isiyotiwa chachu, kama tunavyojionea kwenye kitabu cha Kutoka 13:9-16.

Kutoka 13:9-16 inasema: Nayo itakuwa ishara kwako katika mkono wako, na kwa ukumbusho kati ya macho yako, ili kwamba sheria ya Bwana ipate kuwa kinywani mwako; kwani Bwana alikutoa utoke Misri kwa mkono wenye uwezo. 10 Kwa hiyo utaitunza amri hii kwa wakati wake mwaka baada ya mwaka. 11 Itakuwa hapo Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, kama alivyokuapia wewe na baba zako, na kukupa, 12 ndipo utamwekea Bwana kila afunguaye tumbo, na kila mzaliwa wa kwanza uliye naye, azaliwaye na mnyama; hao waume watakuwa ni wa Bwana. 13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo; na kwamba hutaki kumkomboa, utamvunja shingo; na kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu katika wanao utamkomboa. 14 Kisha itakuwa hapo mwanao atakapokuuliza keshoni, akisema, Ni nini hivi? Utamwambia, Bwana alimtoa Misri, kutoka ile nyumba ya utumwa, kwa uwezo wa mkono wake; 15 basi ilikuwa hapo Farao alipojifanya kuwa mgumu ili asitupe ruhusa kuondoka, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote waliokuwa katika nchi ya Misri, wa binadamu na wa mnyama; kwa ajili ya hayo namtolea Bwana wote wafunguao tumbo, wakiwa waume; lakini wazaliwa wa kwanza wote wa wana wangu nawakomboa. 16 Jambo hilo litakuwa ni ishara mkononi mwako, na utepe katikati ya macho yako; kwa kuwa Bwana alitutoa Misri kwa uwezo wa mkono wake.

 

“Mwendelezo huu wa amri ya nne unakusudia kuweka mkazo wa sheria na amri za Mungu kwenye matendo yetu (mikononi) na kwenye fikra zetu (kwenye vipaji vya nyuso, kati ya macho). Ni ishara ya amri ya Bwana (Kumbukumbu la Torati 6:8) na jinsi alivyowaokoa Israeli (Kumbukumbu la Torati 6:10).

 

Ishara hizi za maadhimisho ya Sabato na Pasaka ni mhuri uliogongwa mkononi na kwenye paji la uso kwa Wateule wa Bwana Mungu. Pamoja na Roho Mtakatifu wanaweka msingi wa mhuri wa wana wa Mungu uliotajwa kwenye Ufunuo 7:3. kwa hiyo, ishara ya wateule inatuama kwenye amri ya kwanza. Kristo alisema, “Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake (au kumtumikia)” (Mathayo 4:10; Luka 4:8). Kumtumikia ni lile tendo la kumfanyia ibada kwa mujibu wa isemavyo biblia.

 

Adhimisho la siku ya Upatanisho ni ishara nyingine ya agano la watu. Tendo la kushindwa kuitunza siku hii ya Upatanisho limewekewa hukumu ya kumtenga mtu huyo mbali na watu wake, au kwa maneno mengine ni kwamba mtu huyu atengwe mbali na mwili au bodi ya wana wa maagano wa Israeli ambao ni Kanisa la Mungu leo (Mambo ya Walawi 23:29) (Cox, “C”, kitabu hicho hicho, ukurasa wa 3).

 

 Ili kufanya ukumbusho wa maagano yetu ya kuzishika amri za Mungu, Biblia inatuamuru pia kuwa tuvae utepe wa rangi ya bluu kwenye kingo au mwishoni mwa mavazi yetu (sawa na isemavyo Hesabu 15:37-41).

 

Kwa kuwa sheria hii haihusiani na kipindi chochote cha muda wowote, au mahali haisemi mahali au shughuli zinazohusiana nayo, inabakia kuwa ni uamuzi wa mtu binafsi kuendelea kufanya hivyo ama la. Na zaidi sana ni kwamba hakuna adhabu iliyotajwa kufanyiwa mtu asiyefanya hivyo. Bali ikiwa ni ukumbusho wa kila mtu binafsi yake, agizo hili linaeleza tu jinsi haja ya kumkumbuka, kumpenda na kutimiliza amri za Mungu kwa kuzishika” (McElwain, T., et.al., “E” jarida la Utepe wa Bluu (Na. 273) [Blue Ribbons (No. 273)], iliyoandikwa na CCG, 1998, ukurasa wa 1, 4).

 

Jinsi ya kuitendea kazi Sheria hii

Kwa kuhitimisha ni kwamba, “Sabato hii ya siku ya saba ya juma inatakiwa itunzwe na kuadhimishwa (kama isemavyo Kutoka 20:8-11; Kumbukumbu la Torati 5:12-15) ikiwa ni amri ya daima ya Bwana Mungu wetu ambayo ni mojawapo ya Amri Kumi za Mungu. Amri hii haipaswi kuitia unajisi na mtu yeyote milele. Sabato ni takatifu. Na kila anayeitia unajisi Sabato adhabu yake ni kifo na kukatiliwa mbaliau kutengwa na watu wake (Kutoka 31:14-15).

 

Ni agano la milele kati ya Mungu na wana wa Israeli na ni ishara ya milele kati yao na Mungu, ili wamjue kuwa yeye ndiye muumbaji (Kutoka 31:15-16). Wakristo wote ni Israeli wa kiroho na Wamataifa wote wanapaswa kuja kwenye taifa hili la Israeli. Kwa hiyo, Sabato ni ishara kati ya Mungu na wanadamu au watu wake wote na ni kwa wakati wote milele. Adhabu au hukumu iliyoagizwa kufanyiwa mtu anayeitia unajisi Sabato ni kuuawa iliwa ni pamoja na yule anayemkufuru Roho Mtakatifu na kuwa hana sehemu kwenye ufufuo wa kwanza bali ule wa pili wa hukumu (soma Ufunuo 20:5). Sabato ni siku ya furaha na inapaswa iheshimiwe kama ni Siku Takatifu ya Bwana. Sio siku ya kuyafanya mambo yako mwenyewe au ya kutimilizia haja zako bali ni ya kuitisha makutaniko matakatifu (Isaya 58:13-14). Hakuna kazi inayotakiwa ifanywe wala mzigo unaoruhusiwa kubebwa siku hii ya Sabato (Yeremia 17:21-22).” Wala haturuhusiwi kununua (Nehemia 10:31) wala kuuza (Nehemia 13:15) siku hii ya Sabato (soma jarida la Tangazo la Imani ya Imani ya Kikristo (Na. A1) [Statement of Beliefs of the Christian Faith (No. A1

)], ya CCG, toleo la 4., mwaka 1997, ukurasa wa 22).

 

“Amri ya Sabato haitengani na amri ya kwanza na amri nyinginezo. Taifa la Israeli liliadhibiwa kwa ajili ya kushindwa kwao kuyatunza maagizo na amri za Mungu” (Zekaria 14:16-19). Hata hivyo, Sabato zinakataliwa na wanadamu kwa ajili ya imani yao iliyoshamiri mioyoni mwao ya kuabudu sanamu” (Cox, “C”, op. cit., ukurasa wa 18).

 

Miandamo ya Mwezi

“Siku ya Mwandamo wa Mwezi ni mojawapo ya Sikukuu zilizoamriwa na Bwana Mungu. Imeorodhesha kwenye kitabu cha Hesabu 10:10.

Hesabu 10:10 inasema: Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizo amriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu, mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

 

Aya hii inatuambia kwamba pia baragumu zilikuwa zinapigwa siku zote za Kuandama kwa Mwezi, kwenye Siku Takatifu na siku ya Sabato wakati kulivyokuwa kunatolewa sadaka za kuteketezwa na za amani (Soma pia jarida la Baragumu ya Pembe za Kondoo na ya Fedha (Na. 47) [The Shofar and the Silver Trumpets (No. 47)]. Dhabihu hii ilitimilizwa katika Kristo. Sikukuu na Sabato hizi zinabakia kama zilivyo, hazikukoma au kubatilishwa.

 

Siku hii ya Mwandamo wa Mwezi iliadhimishwa sawa na Shabbatown au Sabato Takatifu. Dhabihu zilikuwa zinatolewa kuwa ni ukumbusho kama tulivyojionea hapo juu” (sawa na kwenye Hesabu 28:11-15).

 

Jinsi hiyohiyo ya kuadhimisha hutumika kwenye Miandamo ya Mwezi kama inavyofanywa pia kwenye Sikukuu nyingine zote na Sabato.

1Mambo ya Nyakati 23:31  na kumtolea BWANA sadaka zote za kuteketezwa, katika siku za Sabato, na mwezi mpya na sikukuu zilizoagizwa, kwa hesabu, kadiri ya agizo lake, daima mbele za BWANA

 

Kwa hiyo tunaona kwamba Miandamo ya Mwezi ndiyo inayopelekea au kuamua ni majira gani yatakuwa Sabato na Sikukuu. Sawa kama zilivyo Sikukuu na Sabato, umuhimu wa kutoa dhabihu siku ya Miandamo ya Mwezi vilitimilizwa kwa kuja kwake Masihi, lakini maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi yenyewe hayakukomeshwa ama kuondolewa.

2Mambo ya Nyakati 31:3 Tena akaweka sehemu ya mfalme ya mali zake kwa sadaka ya kuteketezwa, yaani, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni, na sadaka za kuteketezwa za Sabato na mwezi mpya na sikukuu, kama ilivyoandikwa katika torati ya BWANA.

 

Tunaona pia kwamba maadhimisho na ibada hizi za Miandamo ya Mwezi zilirejeshwa tena na Ezra (soma Ezra 3:5). Kwa hiyo, marejesho makuu yalihusisha maadhimisho na ibada hizi za Miandamo ya Mwezi.

Ezra 3:5  Na baadae sadaka ya kuteketezwa ya daima, na za mwandamo wa mwezi, na za sikukuu za BWANA, zilizoamriwa na kuwekwa wakfu, na za kila mtu aliye mtolea BWANA sadaka kwa hiari yake.

 

Maadhimisho haya yasieleweke vibaya au kutafsiriwa kuwa ni ibada za kuabudu mwezi, jambo ambalo limekatazwa kabisa.

Kumbukumbu la Torati 4:19  Tena usije ukainua macho yako hata mbinguni, na ulionapo jua, na mwezi, na nyota, jeshi la mbinguni lote pia, ukashawishwa na kuviabudu, na kuvitumikia, ambavyo Bwana, Mungu wako amewagawanyia watu wote chini ya mbingu zote.

 

Kumbukumbu la Torati 17:3 Naye amekwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu, au jua, au mwezi, au vilivyo katika jeshi la mbinguni vyo vyote, nisivyoagiza mimi;

 

Tendo la kuziadhimisha Sabato na Miandamo ya Mwezi pamoja na Sikukuu zilizoamriwa kumefanya Mpango wa Mungu na mwenendo mzima wa mzunguko wa dunia au uumbaji wake. Kalenda ya jua haina uwezo huo. Kalenda inayofuata miandamo ya mwezi ni alama ya watu watakatifu. Alipokuwa anaitafakari Kutoka 12:2, Mekilta alisema kwamba “mataifa” yanajulikana kwa jua, bali Israeli wanajulikana kwa mwezi.

 

“Mwandamo wa Mwezi ndiyo mwanzo wa siku ya kwanza ya mwezi mpya (Hesabu 10:10; 28:11). Hakuna mfumo wowote unaotegemea kwenye mzunguko wa mwezi uliopo leo. Kalenda ya Hilleli imekoma na kutoweka kabisa kwa ajili hii.

 

Siku ya Mwandamo wa Mwezi ilijulikana kama siku kuafaka kwa kutoa maono na unabii, huenda kama inavyoonekana kwenye 2Wafalme 4:23 lakini hasa kwenye Ezekieli 26:1; 29:17; 31:1; 32:1 (na kwenye Isaya 47:13; Hagai 1:1). Hii inaipinga kabisa dhana waliyokuwanayo wanajimu na wachawi wa Babeli na taratibu zao, kama tunavyoona kwenye Isaya 47:13.

 

Sabato na Miandamo ya Mwezi zote ziliadhimishwa kwa kufanya mapumziko kwa kuacha kufanya kazi, kama tunavyoona kwenye Amosi 8:5. Ilikuwa ni siku ya furaha. Vicheko vivyokusudiwa kusikika Siku Takatifu, Mwezi Mpya na Sabato viliondolewa kama tunavyoona kwenye Hosea 2:11.

Hosea 2:11 Tena nitaikomesha furaha yake yote, na sikukuu zake, na siku zake za mwandamo wa mwezi, na Sabato zake na makutaniko yake yote yaliyo amriwa.

 

Hii ni kwa sababu ya kutokuwa waaminifu kwao na ibada ya sanamu. Mungu huwaangamiza watu wake kwa sababu hawakuzishika sheria zake. Hatimaye ni kwamba aliuharibu utajiri wa taifa.

 

Hosea 2:12 inasema:

12 Nami nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema, Hii ndio ujira wangu niliopewa na wapenzi wangu; nami nitaifanya kuwa misitu, na wanyama porini wataila

 

“Tunaona kutoka kwenye aya fulani kadhaa kwamba Mwandamo wa Mwezi wa mwezi fulani unaadhimishwa kwa namna yake maalumu (1Samweli 20:5; Ezekieli 45:18-20).

Ezekieli 45:18-20  Bwana MUNGU asema hivi; Mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utatwaa ng'ombe mchanga mume mkamilifu; nawe utapatakasa mahali patakatifu. 19 Na kuhani atatwaa baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi, na kuitia juu ya miimo ya milango ya nyumba, na juu ya pembe nne za daraja ya madhabahu, na juu ya miimo ya lango la ua wa ndani. 20 Nawe utafanya vivyo hivyo katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi kwa ajili ya kila mtu akosaye, na kwa ajili ya mtu aliye mjinga, ndivyo mtakavyoifanyia nyumba upatanisho.

Tendo la kuisafisha maskani linalotangulia kufanyika siku ya Mwandamo wa Mwezi wa mwezi wa Kwanza (Nisan) mwanzoni mwa Mwaka Mtakatifu (soma jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [Sanctification of the Temple of God (No. 241)]. Utakaso huu wa uwa wa ndani ambao ulikuwa ni inawaonyesha watakatifu kwa mwonekano wa gurudumu la ndani la maono ya nabii Ezekieli. Utakaso kwa ajili ya dhambi zilizofanywa bila kukusudia ama za kupotoshwa ulifanywa kikamilifu tangu Siku ya Saba ya Mwezi wa Kwanza ambao pia huitwa wa Nisan. Makuhani walipaswa kujiandaa na taifa pia.

 

Siku ya kwanza ya Mwandamo wa Mwezi wa Saba (Tishri) ulikuwa wa muhimu sana pia (pia soma jarida la Baragumu (Na. 136) [Trumpets (No. 136)].

Mambo ya Walawi 23:24  Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi, kutakuwa na kustarehe kabisa kwenu, ni ukumbusho wa kuzipiga baragumu, ni kusanyiko takatifu.

 

Nehemia 8:2  Naye Ezra, kuhani, akaileta torati mbele ya kusanyiko, la wanaume na wanawake, na wote walioweza kusikia na kufahamu, siku ya kwanza na mwezi wa saba.

 

Siku ya Mwandamo wa Mwezi wa Saba ambao ni mwanzo wa marejesho ya amri ya Usomaji wa Torati unaofanyika katika kila mwaka wa saba wa mzunguko wa Yubile wa kila siku za Sikukuu ya Vibanda (soma Kumbukumbu la Torati 31:10-12 na pia soma jarida la Jinsi Walivyosoma Torati Ezra na Nehemia (Na. 250) [Reading the Law with Ezra and Nehemiah (No. 250)].

 

Nehemia 8:18 Tena siku baada ya siku, tangu siku ya kwanza hata siku ya mwisho, akasoma katika kitabu cha torati ya Mungu. Wakafanya sikukuu muda wa siku saba; na siku ya nane palikuwa na kusanyiko la makini, kama ilivyoagizwa.  

 

Alama ashirio hapa ni kwamba mwaka wa saba au wa Sabato unaonysha mzunguko wa milenia wa miaka elfu, unaoanzia na kurudi kwa Masihi, ambaye atafanya utawala wa Sheria atakazoziamuru kutoka Yerusalemu. Na Sheria hizi zitaenea ulimwenguni kote na zikiyafanya mataifa yajinyenyejeshe kwake. Usomaji wa Torati kwenye Sikukuu ya Baragumu kulikofanywa na Nehemia ilikuwa ni kitendo kinachoashiria marejeo ya Masihi yatakayoambatana na mlio wa Baragumu (sawa na ilivyoandikwa kenye jarida la Mlolongo wa Ratiba ya Nyakati (Na 272) [Outline Timetable of the Age (No. 272)].

 

Kutoka kwenye kipindi cha zama jangwa cha utawanyiko, hatimaye Mungu atashughulika na Israeli na kuirejesha upya. Ikumbukwe kwamba wateule wake Kristo ni sehemu ya hawa Israeli na watachukuliwa kama taifa (Hosea 2:14-23).

 

Miandamo ya Mwezi iliadhimishwa na Kanisa la Wakristo wa kwanza waliokuwa na Mitume na hata walipokuwa kwenye zama ya utawanyiko na jinsi walivyokuwa wanaadhimisha sio jambo tunalopaswa kulitolea hukumu. Walikuwa wanaendela bado kuadhimisha ibada hizi huko Ulaya kwenye karne na kumi na saba (soma jarida la Mgawanyo wa Jumla wa Makanisa Yanayoshika Sabato (Na. 122) [General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122)]; na kitabu cha Wasabato wa Transylvania (The Sabbatarians In Transylvania) kilichoandikwa na Samuel Kohn (1894), ambacho nakala yake ya tafsiri ya Kiingereza imechapishwa na idara ya machapisho ya  CCG, mwaka 1998).

Wakolosai 2:16-17 Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; 17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

 

Miandamo ya Mwezi ni muhimu kwa ustawi wa wanadamu. Kalenda hii imepuuzwa na mahala pake kuchukuliwa na ile inayoitwa ni kalenda ya wanadamu au ya walimwengu iliyopewa siku za kipagani zinazoendana na kuwatukuza wanadamu. Nchini Marekani, kalenda hii ya wanadamu imepambwa kwa kuwekewa siku muhimu za mapumziko kwenye siku za kipagani. Jambo hili halipaswi kupuuzwa au kufumbiwa macho.

 

Siku hizi za Sabato na Miandamo ya Mwezi ziliadhimishwa kwa uzito sawa kwa masuala ya kibiashara na shughuli zote. Shughuli za kibiashara au za kununua na kuuza zilikatazwa siku hizo nz hata leo zisifanyike katika siku zote, yaani za Mwandamo wa Mwezi na za Sabato.

Amosi 8:4-6 inasema: Lisikieni hili, ninyi mnaopenda kuwameza wahitaji, na kuwakomesha maskini wa nchi, 5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandika ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu; 6 tupate kuwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu; na kuziuza takataka za ngano.

 

Katazo hili ni tatizo kubwa kwa Waisraeli wa leo. Hatahivyo na kwa kweli, hakuna uwezekano wowote wala mahala panapoonyesha kuwa Sabato na Miandamo ya Mwezi zinaweza kuonyesha tofauti ya maadhimisho yake, zaid kama ilivyo kwenye Sikukuu ambazo zimeorodheshwa mbali na Amri Kumi, na ambazo zinachukuliwa kama Shabbatown – ambazo ni lazima ziadhimishwe zote.

 

Nabii Amosi anaendela kuelezea na kuwaonya Israeli kwa kukosa kwao kuzitunza Sabato na Miandamo ya Mwezi kikamilifu.

Amosi 8:8-12 inasema: Kwa ajili ya hayo, je! Haitatetemeka nchi, na kuomboleza kila mtu akaaye ndani yake? Naam, itainuka yote pia kama huo Mto; nayo itataabika na kupwa tena kama Mto wa Misri. 9 Tena itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri, nami nitaitia nchi giza wakati wa nuru ya mchana. 10 Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote, na upaa katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu. 11 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana. 12 Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione.

 

Adhabu ya moja kwa moja kwa wanaoyaasi maneno ya Mungu ni kile tulichokipokea. Njaa ya kukosa kulisikia neno la Mungu hutokea kama adhabu kwa wanaomuasi Mungu. Tendo la kuzitia unajisi Sabato na Miandamo ya Mwezi kwa kufanya matembezi na kufanya biashara kwa makusudi ya kuzivunja Amri ni sababu za kwanza. Nyumba ya Yakobo walikumbwa na machukizo haya ingawaje walihifadhiwa salama na hawakuangamizwa, kama nafaka zinavyopeperushwa kwenye chombo cha kupepetea (Amosi 9:8-15).

 (Cox, W.E., “F” jarida la Miandamo ya Mwezi (Na.125) [The New Moons (No. 125)], CCG, 1995-2007, kurasa za 5-10).

 

Maana ya Miandamo ya Mwezi Kwenye Mpango za Mungu

Mwanzo 1:14 inaonyesha kuwa Mungu aliweka mwanga katika mbingu ili kufanya tofauti kati ya mchana na usiku na kama ishara ya majira. Mwezi Mpya hutupa utaratibu na muda wa Sikukuu na hasahasa hutanguliwa na Sabato, ambayo husimamia tando la kukamilisha siku saba, wakati Miezi huanzia kutoka siku ya nne. Nuru hutenga nuru na giza (Mwa.1:18). Mwezi huashiria nuru ya nuru ya ulimwengu katika giza ambalo huitawala. Jua lilitumia kufananisha na Kristo (Malaki 4:2).

Malaki 4:2-5  Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini. 3 Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema BWANA wa majeshi. 4 Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu niliyomwamuru huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote, naam amri na hukumu.. 5 Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya.

 

Mwezi unamaana pia kwa kuwa uko kwenye mwonekano. Mwandamo wa Mwezi ni alama ashirio ya kuanza kwa shughuli ngingine kwenye kila mzunguko. Kuna miezi kumi na miwili katika kila mwaka (mbali na ule mwaka mkubwa) (1Wafalme 4:7; 1Nyakati 27:1-15). Miezi hii inachukuliwa kwa ujumla kuwa na urefu wa siku 30 kila mmoja (Mwanzo 7:11; 8:3-4; Hesabu 20:29; Kumbukumbu la Torati 21:13; 34:8; Esta 4:11; Danilei 6:7-13). Pia tazama jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156) [God’s Calendar (No. 156)].

 

Mwandamo wa Mwezi ni “mwanzo wa mwezi mwandamo, ujulikanao kama kipindi kilicho kati kati ya kipindi giza ambacho mwezi hauonekani hadi kingine kinachofuatia, urefu ambao kwa kweli hauhesabiwi kwenye shule zinazoshughulika na elimu ya mambo anga au nyota.” (Judaeus Philo, kwenye kitabu chake cha Kanuni Mahususi, II, XXVI, 140 (The Special Laws, II, XXVI, 140, F.H.) cha Colson, kwenye Machapisho ya Chuo Kikuu cha Harvard, huko Cambridge mwaka 1737 (Harvard University Press, Cambridge MA, 1937).  

 

Kwa kuongezea nukuu hii kunamaandiko mengine yanayohusu Miandamo ya Mwezi na jinsi ya kuanza kwake ambayo inaitaja siku halisi hasa ma Kuandama kwa Mwezi.

 

Maadhimisho ya Sikukuu kwa mujubu wa Philo

Tunaposhughulikia suala la maadhimisho ya Sikukuu kwa mujibu wa amri za Mungu, tunaona pia kwamba Philo ana la kusema akilinganisha na Shria Muhimu zinazoihusu amri ya nne na jinsi inavyoshabihiana kwa jisi ifuatayo:

 

SHERIA MUHIMU, II*

{**Lichwa cha somo cha kitabu cha Yonge, kinachoandika kwa alama, Kingamo la Amri Muhimu aina yake, ambazo Zilielezewa kwa Maandako chapisho Matatu ya Mdahalo, Ilioitwa ni ya Tatu, ya Nne na ya Tano Kuhusu Viapo na Makumbushio yake Yanayoyahusu; Kuhusu Sabato Takatifu, Kuhusu Heshima Inayotakiwa Wapewe Wazazi).

....

Tafsiri ya Yonge inahusisha ufanyiaji kazi kwenye hatua hii. Kwa Nambari Saba. Mgawanyo wake unaofuatia unaanzia na kuishia na numerali za kirumi I (= X kwenye Loeb). Loeb nyingine zinazofuatia zimewekewa nambari.

X. (39) Amri inayofuatia ni ile inayohusu siku saba takatifu, ambazo zimewekewa nambari kinyumbulisho ya kuwa ni sikukuu za muhimu sana. Kwa mfano, kuna kuachiliwa kwa wanaume ambao kwa asili walikuwa huru, lakini ambao walidhania baadhi ya nyakati muhimu zisizoonekana, ambazo wamekuwa ni watumwa na ambao uwekwaji huru huu unakuwa kila kipindi cha miaka saba. Na tena kuna madeni ya kibinadamu unaowahusu wadeni, kama wanavyowasamehe wadeni ndugu zao, ambao wanawasamehe madeni yao kila mwaka wa saba. Pia kuna mapumziko yanayotolewa kwa ardhi yenye rutuba, bila kujali kama ipo kwenye maeneo ya milimani au kwenye utambarare au mabondeni, mapumziko ambayo yanakuwa kila baada ya mwaka wa saba. Zaidi ya yote, kuna amri nyinginezo ambazo zilianzishwa kwa kuuadhimisha mwaka wa hamsini. Na kwa mambo yote haya huleta mnyumbulisho (pasipo kuangalia maana yoyote ya kimafumbo) inatosha kuwaongoza wale wote walioachwa kwenye ujuzi kamilifu, na kuwafanya hqata wale walio na mashaka au wagumu kwenye mitazamo yao wakubaliane zaidi na kupendezwa. (40) Sasa tumeishasema tayari kwa upana wa kiasi fulani kuhusu umuhimu wa namba saba, tukielezea ni nini asili yake kuelekea kwenye namba kumi, na pia jinsi uhusiano wake ulivyo kwa muongo mmoja wenyewe, na pia kwa namba nne, ambayo ni msingi wa muongo mmoja. Na sasa, inapokuwa imehusishwa kwenye mwito wa kawaida kutoka kwenye kiini chake, ni mchakato wa wito wa kawaida kuona kuwa namba ya kawaida ishirini na nane; ambayo inazidishwa kwa hali sawa na mlingano wa kawaida ulio sawa na maeneo yote, ambayo inafanya kikomo chake kuwa ni kote kuwili yaani mzingo na mlingano pembe. Pia nilionyesha jinsi zilivyo idadi ya nambari za mambo ya uzuri ambayzo zinaweza kuzidi kutoka kwenye mabo yanayoizidia, na ambayo hatujawa na muda wa kuyaangalia kwa sasa. Bali tunapaswa kuyahoji na kuyachunguza kila kimoja wapo miongoni mwa mambo haya muhimu yaliyoko mbele yetu kama yako pamoja, ikianzia na kile cha kwanza. Jambo la kwanza linalotakiwa kutiliwa maanani ni lile la maadhimisho ya Sikukuu. [Tafsiri ya Yonge inahusisha ufanyiaji kazi kwenye hatua hii. Kuonyesha Kwamba Sikukuu Zipo Kumi Idadi yake. “Mgawanyo” huu unaanzia na numerali ya kirumi I (= XI kwenye Loeb); ikionyesha kila moja ya sikukuu hizi kumi peke yake na kuendelea kupitia kwenye nambari za Loeb 214. aya nyingine zinazofuatia numerali za Loeb)

XI. (41) Sasa kuna idadi ya sikukuu kumi, kama sheria zinavyoziandika na kuziorodhesha.

Ya kwanza ni ile ambayo huenda mtu anaweza kushangazwa kuisikia ikiitwa sikukuu. Sikukuu hii ni ya kila siku.

Sikukuu nyingine ya pili ni ile ya siku ya saba, ambayo Waebrania kwa lugha yao huuita Sabato.

Ya tatu ni ile inayokuwa kipindi cha baada ya kipindi cha kutoonekana mwezi au cha muunganisho wa mwezi ambayo inatokea siku ya kuandama kwa mwezi wa kila mwezi.

Ya nne ni ile ijulikanayo kama Pasaka ambayo pia inaitwa Pasaka.

Ya tano ni ile ya malimbuko ya mazao ambayo kwayo hutikiswa mganda mtakatifu (Kumbuka kuwa Mganda wa Kutikiswa ni moja ya Sikukuu kumi zilizokuwa na mashiko makubwa zama hizi za Hekalu).

Ya sita ni ile ya Mikate Isiyotiwa Chachu, inayoadhimishwa baada maadhimisho ya sikukuu yamekwisha tayari.

Ya saba ni ile inayoadhimishwa siku ya saba ya majuma saba.

Ya nane ni sikukuu inayoaadhimishwa sambamba na mwandamo wa mwezi, ambayo ni sikukuu ya baragumu.

Ya tisa ni ile inayoadhimishwa kwa kufunga saumu.

Ya kumi ni sikukuu ya vibanda, ambayo ni ya mwisho miongoni mwa sikukuu zote za mwaka, inashoishilia kwa kukamilisha idadi ya kumi. Tunatakiwa sasa kuanza na sikukuu ya kwanza.

[Kumbuka kuwa, hapa Philo anajumuisha na Siku ya Mkutano wa Makini na Sikukuu ya Vibanda na kuzifanya ziwe kumi badala ya kumi na moja.]

 

Tunagundua hapa kwamba katika kutambulishwa kuhusu Sikukuu hii ya tatu inayojulikana kama ya Mwandamo wa Mwezi, Philo anatumia neno ambalo halijawahi kuonekana anaposema baada ya kipindi cha kutoonekana mwezi au cha muunganiko cha mpito na wengine wameitaja kama kipindi kinachofuata kwa maana ya “kwa mujibu wa” au “kama alivyokusudiwa na” kipindi cha mpito. Hata hivyo, anastahili kwa jinsi hii kwa kusema inayotokea siku ya Mwandamo wa Mwezi wa kila mwezi. Kwa hiyo andiko hili liko wazi sana kwamba Mwandamo wa Mwezi ni suku ambayo kipindi hiki cha mpito hutokea. Kwa mafafanuzi Philo kwa hiyo anaendelea kuelezea kwamba mwezi unahesabiwa tangu kipindi kimoja cha kutoonekana mwezi hadi kingine kama kinavyoamriwa na wanazuoni wa shule za utafiti wa mambo ya anga na nyota, kama ilivyoandikwa hapo juu.

 

Tafsiri ya Yonge inapungukiwa na sehemu ya 140 na maandiko 142-144 (ambayo yametolewa hapo chini) na anaelezea kipindi na teolojia iliyo nyuma ya Mwandamo wa Mwezi na sababu inayopelekea kuendelea kwa mujibu wa kipindi hiki cha kutoonekana mwezi, na siku ya Kundama kwa Mwezi kuwa ni ile siku ya giza.

 

SIKUKUU YA TATU

XXVI. (140) Kufuattana na kanuni tuliyoichukua, tunaendelea kuiongelea sikukuu ya tatu, ambayo ni ya mwandamo wa mwezi. Kwanza kabisa na kabla ya mambo yote, kwa kuwa ni mwanzo wa mwezi, na ni mwanzo wa idadi au majira, ya mwelekeo wa kuufikia mwezi wa Pili, kwa kuwa katika kipindi hiki kunakuwa hakuna mwangaza wowote angani kote. (141) Tatu, kwa kuwa kwenye kipindi hiki uweza wa mwili wote wenye nguvu na wa muhimu hupulinguzia sehemu yake ya msaada ulio muhimu kwa mwili uliodhaifu na usio wa muhimu sana, kwa kuwa kipindi cha kuandama mwezi ndicho jua linaanza kuuangazia mwezi kwa nuru ambayo inaangaza kwa mwonekano wa nje, na kisha kuufanya uonekane mzuri kwa mng’ao wake kwa wanaoutazama. Na hii, ni kama inavyoonekana kuwa ni fundisho la dhahiri la wema na unyenyekevu kwa mwanadamu, kuwafundisha kuwa hawapaswi kufanya jitihada ya kuwashirikisha mema yao mazuri kwa wengine, bali ni kuwaiga viumbe wa mbinguni, jambo linaloweza kusababisha wivu na kuitesa Roho. {17}{sehemu ya 142-144 zilirukwa kwenye tafsiri ya Yonge kwa kuwa chapisho ambalo ndiyo Yonge aliitegemea alipokuwa anatafsiriwa, Mangey, alikosa matirio yake. Mistari hii imetafsiriwa upya kwa toleo hili.} (142) Sababu ya nne ni kwamba vitu vyote vilivyo mawinguni, mwezi unazunguka kwa kupitia kwenye ukanda wa sayari unaopitia sayari zote kuu, yaani ukanda wa zodiaki kwa kipindi cha chini ya jinsi ilivyopangiwa; na unakamilisha mzunguko wake kwa mzingo wa kile mwezi. Kwa ajili hii sheria imeheishimu mzingo, kipindi ambacho mwezi umekamilisha kutoka kwenye chanzo chake ambapo ndipo ilianzia mzunguko wake, kwa kuiita siku ile kuwa ni sikukuu ili kwamba iweze kutufundisha tena somo jema ili kwenye mambo yanayohusu maisha tuweze kufikia kikomo cha uwiano mwanzo wake. Hii itatokea iwapo kama tutashika hatamu kwenye msukumo wetu wa kwanza wenye nguvu ya maana na haiwaruhusu kukataa hatamu na kukimbia tukiwa huru kama wanyama pasipo mtu yeyote wa kuwaongoza wanyama.

http://www.earlyjewishwritings.com/text/philo/book28.html

 

Kwa hiyo sio makosa. Mwandamo wa Mwezi huwa ni kipindi kile cha mpito cha giza la kutoonekana mwezi kama inavyoaminika na wanazuoni wa shule za elimu ya mambo anga na nyota huko Yerusalemu. Tendo la kuahirisha Mwandamo wa Mwezi lililofanywa na imani ya Kiyahudi kunamaanisha kuahirisha sikukuu zote na kuzifanya kuwa hazina maana. Huko ni sawa na kutia Mungu kidole puani kwa kutumia Sheria na Amri zake. Kwa hiyo, Mwezi unapokuwa Unaandama ndipo mfumo na utaratibu wa sikukuu unapoanzia.

 

Mpango mzima wa Wokovu unaonekana kwenye kila Mwandamo Mpya wa Mwezi kupitia utaratibu wa hesabu ya Sikukuu na mwonekano wake kwenye mzunguko wa mavuno halisi ya uvunaji mazao” (Cox, W.E., “G” jarida lake la Mwandamo wa Miezi Katika Israeli (Na.132) [The New Moons of Israel (No. 132)], CCG, 1995-2008, ukusara wa 3,5,6,7).

 

“Mkutano mzima – viongozi na watu – wanaamriwa kufanya ibada kwa siku zote mbili, yaani kwenye Sabato na Miandamo ya Mwezi (soma pia Ezekieli 46:6,9-10).

Ezekieli 46:1-3 inasema: Bwana MUNGU asema hivi; Lango la ua wa ndani, lielekealo upande wa mashariki litafungwa siku sita za kazi; lakini siku ya sabato litafunguliwa, na siku ya mwezi mpya litafunguliwa. 2 Naye mkuu ataingia kwa njia ya ukumbi wa lango lile, upande wa nje, naye atasimama karibu na mwimo wa lango, nao makuhani wataitengeneza sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka zake za amani, naye ataabudu penye kizingiti cha lango; kisha atatoka; lakini lango lile halitafungwa hata wakati wa jioni. 3 Watu wa nchi nao wataabudu mbele ya mlango wa lile lango mbele za Bwana, siku za sabato, na siku za mwezi mpya.

 

Utoaji dhabihu siku ya Mwandamo wa Mwezi kwa kweli jambo kuu na muhimu zaidi kuliko lile la siku ya Sabato (Ezekieli 46:4,6). Hakuna tofauti iliyofanywa kati ya Mwandamo wa Mwezi na Sabato ya juma, bali siku zote mbili ni takatifu na haziruhusiwi kufanya biashara siku hizo.

Amosi 8:5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandika ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu;

(Cox, W.E., “H” jarida la Mavuno ya Mungu, Dhabihu ya Mwandamo wa Mwezi, na Wale 144,000 (Na. 120) [The Harvests of God, the New Moon Sacrifices, and the 144,000 (No. 120)], CCG, 1995-2007, ukurasa 13).

 

“Mwandamo wa Mwezi ni tukio muhimu katika mfumo wa mambo anga na ambalo linatabirika kamilifu pasipo makosa. Linapaswa lichukuliwe mwanzo wake kutoka kipindi linapotokea huko mjini Yerusalemu ili kufanya umoja wa ibada za kidini ulimwenguni kote, ili kuweko na ongezeko la kimawasiliano. Hii inafanyika kwa kufuata jinsi yanavyosema Maandiko Matakatifu ambayo yanauita mji wa Yerusalemu kuwa ni Kiti cha enzi cha Mungu (Yeremia 3:17), ni kitovu cha sheria na ni kituo ambacho kwacho zitatoka kwenye kipindi cha utawala wa Masihi (Isaya 2:3), na kwa maji ya Roho Mtakatifu (Zekaria 8:22; 14:8-21). Mungu ameliweka jina lake pale milele (2Nyakati 33:4)” (Cox, W.E.,”I” jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156) [God’s Calendar (No. 156)], CCG, 1996-2008, ukurasa 13)

 

Siku Takatifu na Sikukuu

Siku Takatifu za kila mwaka zinapatikana katika Walawi 23:1-44, Hesabu 28:16-29, 35 na katika Kumbukumbu la torati 16:1-16. Siku hizi Takatifu za kila mwaka ni taswira ya Mpango wa Wokovu wa Bwana . ni za muhimu na lazima na zinaweka umuhimu wake fulani wa kiishara kati ya Mungu na watu wake. Siku hizi Takatifu zinaadhimishwa na kuchukuliwa sawa na Sabato.

 

Siku hizi Takatifu ni:

Pasaka na Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu (Law. 23:7; Hes.28:18, 25);

Pentekoste (Law.23:21;  Hes.28:26);

Baragumu (Law.23:23; Hes.29:1);

Upatanisho (Law.23:26; Hes.29:7)

Vibanda (Law.23:35; Hes.29:12);

Siku ya Mkutano wa Makini (Law.23:36; Hes.29:35).”

Jarida la (Msingi wa Imani wa Imani ya Kikristo (Na. A1) [Statement of Beliefs of the Christian Faith (No. A1)], CCG, toleo la 4 ed., 1997, ukurasa wa 24.)

 

Sikukuu Tatu za Kila Mwaka

Sikukuu tatu zilizoamriwa kuadhimishwa kila mwaka ni Pasaka na Mikate isiyotiwa Chachu, Pentekoste au Idi ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda

Kumbukumbu la Torati 16:16 "Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu.”

 

Kutoka 23:14  " Mara tatu kila mwaka utaniwekea sikukuu.

 

Pasaka

Sikukuu ya Pasaka ni ishara ya wanadamu wakikombolewa kutoka kwenye utumwa wa dhambi na adhimishola Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu inawakilisha ishara ya kuondoa dhambi na kutoshiriki tena miongoni mwetu na ni ishara waliyoifanywa Israeli na hizi ni Siku mbili Takatifu zilizo tofauti. Pasaka huishia siku ya kumi na nne jioni, na si ku ya mwisho ya Mikaye Isiyo na Chachu ni siku ya ishirini na moja ya mwezi wa Kwanza (Abibu).

Kumbukumbu la Torati 16:1-2 Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako. 2 Nawe umchinjie pasaka Bwana, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng'ombe, mahali atakapochagua Bwana apakalishe jina lake.

 

Masaa 36 ya kwanza ya maadhimisho ya Pasaka pamoja na Ushirika wa Meza ya Bwana na mlo wa siku ya 15 havitakiwi kufanyika majumbani au ndani ya malango yetu. Matukio haya hufanywa kwa kutanguliwa na siku ya maandalizi ambayo ni siku ya 14 ya mwezi huo huo wa Nisan.

Kumbukumbu la Torati 16:5-7 Usimchinje pasaka ndani ya malango yako yote akupayo Bwana, Mungu wako; 6 ila mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinja pasaka jioni, katika machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri. 7 Nawe umwoke na kumla mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; kisha asubuhi yake ugeuke uende hemani mwako.

 

Mlo wa Meza ya Bwana

“Mahala panapolazimu kushuriki ili kuitii na kudhimisha amri hizi na utaratibu ambao Kristo mwenyewe alionyesha mfano kwa kuanzisha na kushiriki Meza ya Bwana na Mlo wa Pasaka. Kama hatutaishiriki ibada na maadhimisho haya, basi tunakuwa hatuna ushirika na Yesu Kristo (Yohana 13:8).

Yohana 6:53-56 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. 54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. 55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.

 

Adhimisho la kwanza la Ushirika wa Meza ya Bwana ni kufanyika kwa utaratibu wa kuoshana miguu, ambalo linafuatiwa na tendo la kushiriki kuumega mkate na kunywa divai. “Ishara hiyohiyo iliyoifanywa kwa dhaihu ya aliyojitoa Kristo imeonekana kwa mifano hii miwili ya kula mkate na kunywa divai” (Cox, W.E., “J” jarida la Ushirika wa Meza ya Bwana (Na. 103) [The Lord’s Supper (No. 103)], CCG, 1995-2008, ukurasa wa 4-5).

 

Mkate wenye chachu hautakiwi kabisa kutumika kwenye ibada ya maadhimisho haya ya Meza ya Bwana (sawa na ilivyoandikwa kwenye Kutoka 23:18).

Kutoka 34:25   " Usisongeze damu ya sadaka yangu pamoja na mkate uliotiwa chachu; wala hiyo sadaka ya sikukuu ya pasaka haitasazwa hata asubuhi..

Pia sona jarida la Maana ya Kuoshana Miguu (Na. 99) na Maana ya Mkate na Divai (Na. 100) [Significance of the Footwashing (No. 99) and Significance of the Bread and Wine (No. 100)].

 

Maelekezo ya jinsi ya Kuadhimisha Pasaka

Maelekezo yaleyale yahusuyo Pasaka yanapatikana kwenye kitabu cha Kutoka 12.

Kutoka 12:1-51 inasema: Bwana akanena na Musa na Haruni katika nchi ya Misri, akawaambia, 2 Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu; utakuwa ni mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu. 3 Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja; 4 na ikiwa watu wa nyumba ni wachache kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu, ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-kondoo. 5 Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi. 6 Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni. 7 Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba watakazomla. 8 Watakula nyama yake usiku ule ule, imeokwa motoni, pamoja na mkate usiotiwa chachu; tena pamoja na mboga zenye uchungu. 9 Msiile mbichi, wala ya kutokoswa majini, bali imeokwa motoni; kichwa chake pamoja na miguu yake, na nyama zake za ndani. 10 Wala msisaze kitu chake cho chote hata asubuhi, bali kitu kitakachosalia hata asubuhi mtakichoma kwa moto. 11 Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya Bwana. 12 Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana. 13 Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri. 14 Na siku hii itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi mtaifanya iwe sikukuu kwa Bwana; mtaifanya iwe sikukuu katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele 15 Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba; siku hiyo ya kwanza mtaondoa chachu yote isiwe katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula mkate uliochachwa tangu siku hiyo ya kwanza hata siku ya saba, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na Israeli. 16 Siku ya kwanza kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na siku ya saba kutakuwa kusanyiko takatifu; haitafanywa kazi yo yote katika siku hizo, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu. 17 Nanyi mtaitunza ile sikukuu ya mikate isiyochachwa; kwa kuwa katika siku iyo hiyo mimi nimeyatoa majeshi yenu katika nchi ya Misri; kwa hiyo mtaitunza siku hiyo katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele. 18 Mwezi wa kwanza, siku ya mwezi kumi na nne, wakati wa jioni, mtakula mikate isiyochachwa, hata siku ya mwezi ishirini na moja jioni. 19 Muda wa siku saba isionekane chachu katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula hiyo iliyotiwa chachu, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na mkutano wa Israeli, akiwa mwenye kukaa hali ya ugeni, au akiwa mtu aliyezaliwa katika nchi. 20 Msile kitu chochote kilichochachwa; mtakula mikate isiyochachwa katika makao yenu yote. 21 Hapo ndipo Musa akawaita wazee wa Israeli, na kuwaambia, Nendeni, mkajitwalie wana-kondoo kama jamaa zenu zilivyo mkamchinje pasaka. 22 Nanyi twaeni tawi la hisopu, mkalichovye katika ile damu iliyo bakulini na kukipiga kizingiti cha juu, na miimo miwili ya mlango, kwa hiyo damu iliyo katika bakuli; tena mtu ye yote miongoni mwenu asitoke mlangoni mwa nyumba yake hata asubuhi. 23 Kwa kuwa Bwana atapita ili awapige hao Wamisri; na hapo atakapoiona hiyo damu katika kizingiti cha juu, na katika ile miimo miwili, Bwana atapita juu ya mlango, wala hatamwacha mwenye kuharibu aingie nyumbani mwenu kuwapiga ninyi. 24 Nanyi mtalitunza jambo hili kuwa ni amri kwako na kwa wanao milele. 25 Itakuwa hapo mtakapoifikilia hiyo nchi, Bwana atakayowapa, kama alivyoahidi, ndipo mtakapoushika utumishi huu. 26 Kisha itakuwa, hapo watoto wenu watakapowauliza, N'nini maana yake utumishi huu kwenu? 27 Ndipo mtawaambia, Ni dhabihu ya pasaka ya Bwana, kwa kuwa alipita juu ya nyumba za wana wa Israeli huko Misri, hapo alipowapiga Wamisri, akaziokoa nyumba zetu. Hao watu wakainama vichwa na kusujudia. 28 Basi wana wa Israeli wakaenda na kufanya mambo hayo; vile vile kama Bwana alivyowaamuru Musa na Haruni, ndivyo walivyofanya. 29 Hata ikawa, usiku wa manane Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, tangu mzaliwa wa kwanza wa Farao aliyeketi katika kiti chake cha enzi, hata mzaliwa wa kwanza wa mtu aliyefungwa katika nyumba ya wafungwa; na wazaliwa wa kwanza wote wa wanyama. 30 Farao akaondoka usiku, yeye na watumishi wake wote, na Wamisri wote; pakawa na kilio kikuu katika Misri; maana hapakuwa na nyumba hata moja asimokufa mtu. 31 Akawaita Musa na Haruni usiku, akasema, Ondokeni tokeni katika watu wangu, ninyi na wana wa Israeli; enendeni, kamtumikieni Bwana kama mlivyosema. 32 Twaeni kondoo zenu na ng'ombe zenu kama mlivyosema, enendeni zenu, mkanibariki mimi pia. 33 Wamisri nao wakawahimiza watu, kuwatoa katika nchi kwa haraka, maana walisema, Tumekwisha kufa sote. 34 Watu wakauchukua unga wa mikate yao kabla haijatiwa chachu, na vyombo vyao vya kukandia wakavitia ndani ya nguo zao mabegani. 35 Wana wa Israeli wakafanya kama neno lile la Musa; wakataka kwa Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu, na mavazi. 36 Bwana akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara. 37 Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi, walipata hesabu yao kama watu sita mia elfu watu waume waliokwenda kwa miguu, bila kuhesabu watoto. 38 Na kundi kubwa la watu waliochangamana mno wakakwea pamoja nao; na kondoo na ng'ombe, wanyama wengi sana. 39 Nao wakaoka mikate isiyochachwa ya ule unga waliouchukua walipotoka Misri, maana, haukutiwa chachu, kwa sababu walitolewa watoke Misri, wasiweze kukawia, nao walikuwa hawajajifanyia tayari chakula. 40 Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa ni miaka mia nne na thelathini. 41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo mia nne na thelathini, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri. 42 Ni usiku wa kuangaliwa sana mbele za Bwana kwa sababu ya kuwatoa katika nchi ya Misri; huu ndio usiku wa Bwana, ambao wapasa kuangaliwa sana na wana wa Israeli wote katika vizazi vyao. 43 Bwana akawaambia Musa na Haruni, Amri ya pasaka ni hii; mtu mgeni asimle; 44 lakini mtumishi wa mtu awaye yote aliyenunuliwa kwa fedha, ukiisha kumtahiri, ndipo hapo atamla pasaka. 45 Akaaye kwenu hali ya ugeni, na mtumishi aliyeajiriwa, wasimle pasaka. 46 Na aliwe ndani ya nyumba moja; usiichukue nje ya nyumba nyama yake yo yote; wala msivunje mfupa wake uwao wote. 47 Na wafanye jambo hili mkutano wa Israeli wote. 48 Na mgeni atakapoketi pamoja nawe, na kupenda kumfanyia Bwana pasaka, waume wake wote na watahiriwe, ndipo hapo akaribie na kufanya pasaka; naye atakuwa mfano mmoja na mtu aliyezaliwa katika nchi; lakini mtu ye yote asiyetahiriwa asimle. 49 Sheria ni hiyo moja kwa mtu aliyezaliwa kwenu, na kwa mgeni akaaye kati yenu ugenini. 50 Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli wote; kama Bwana alivyowaagiza Musa na Haruni, ndivyo walivyofanya. 51 Ilikuwa siku ile ile moja, Bwana akawatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri kwa majeshi yao.

The First Passover Instituted

 

Sikukuu hii inatakiwa iadhimishwe kwa kutokula mikate isiyotiwa chachu kipindi chote hiki (Kutoka 12:8, 15-20; 12:3,6; 23:15; Mambo ya Walawi 23:6; Hesabu 9:11; 28:17; Kumbukumbu la Torati 16:3, 4; Marko 14:12; Luka 22:7; Matendo 12:3; 1Wakorintho 5:8). Adhabu kwa mtu anayedharau na kuitia unajisi Sikukuu hii ni kukatiliwa mbali na watu wake au kutengwa kutoka kwenye mkutano wa wateule (Hesabu 9:13), isipokuwa kama kuna unajisi au safari iliyoainishwa hapo juu. Kuna amri moja tu kwa wote, yaani kwa mgeni na kwa mpita njia (Hesabu 9:14).

Kumbukumbu la Torati 16:3-4 inasema: Usimle pamoja na mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka; ili upate kukumbuka siku uliyotoka nchi ya Misri, siku zote za maisha yako.  4 Wala isionekane kwako chachu muda wa siku saba katika mipaka yako yote; wala katika hiyo nyama uchinjayo siku ya kwanza jioni, kisilale cho chote usiku kucha hata asubuhi.

 

Wale ambao hawajajiandaa kushiriki kuila Pasaka au wale wanaosafiri wanatakwa kuila Pasaka kwenye mwezi unaofuatia (Hesabu 9:6-12; 2Nyakati 30:2-4).

Hesabu 9:1-23 inasema: Kisha Bwana akanena na Musa katika bara ya Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka kwao katika nchi ya Misri, akamwambia, 2 Tena, wana wa Israeli na washike sikukuu ya Pasaka kwa wakati wake ulioagizwa. 3 Siku ya kumi na nne ya mwezi huu, wakati wa jioni, mtaishika kwa wakati wake ulioagizwa; kwa amri zake zote, na kama hukumu zake zote zilivyo, ndivyo mtakavyoishika. 4 Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli kwamba waishike sikukuu hiyo ya Pasaka; 5 Nao wakaishika Pasaka katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, katika bara ya Sinai vile vile kama hayo yote Bwana aliyomwagiza Musa, ndivyo walivyofanya wana wa Israeli. 6 Basi walikuwako watu waume kadha wa kadha waliokuwa na unajisi kwa ajili ya maiti wa mtu, hata wasiweze kuishika Pasaka siku hiyo; nao wakaenda mbele ya Musa na Haruni, siku hiyo hao watu wakamwambia, 7 Sisi tu hali ya unajisi kwa ajili ya maiti wa mtu; nasi tumezuiwa kwa nini hata tusipate kumtolea Bwana matoleo kwa wakati wake ulioagizwa, kati ya wana wa Israeli? 8 Musa akawaambia, Ngojeni hapo; hata nipate sikiza Bwana atakaloagiza juu yenu. 9 Bwana akanena na Musa, akamwambia, 10 Nena na wana wa Israeli, kuwaambia, Mtu wa kwenu, au wa vizazi vyenu, ye yote atakayekuwa na unajisi kwa ajili ya maiti, au akiwako mbali katika safari, na haya yote, ataishika Pasaka kwa Bwana; 11 mwezi wa pili, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, wataishika; watamla pamoja na mikate isiyotiwa chachu na mboga za uchungu; 12 wasisaze kitu chake cho chote hata asubuhi, wala wasimvunje mfupa wake; kama hiyo sheria yote ya Pasaka ilivyo ndivyo watakavyoishika. 13 Lakini mtu aliye safi, wala hakuwa katika safari, naye amekosa kuishika Pasaka, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake; kwa sababu hakumtolea Bwana matoleo kwa wakati wake ulioamriwa, mtu huyo atachukua dhambi yake. 14 Na kama mgeni akiketi kati yenu ugenini, naye ataka kuishika Pasaka kwa Bwana; kama hiyo sheria ya Pasaka ilivyo, na kama amri yake ilivyo, ndivyo atakavyofanya; mtakuwa na sheria moja, kwa huyo aliye mgeni, na kwa huyo aliyezaliwa katika nchi. 15 Na siku hiyo maskani iliposimamishwa, lile wingu likaifunika maskani, yaani, hema ya kukutania; wakati wa jioni likawa juu ya maskani, mfano wa moto, hata asubuhi. 16 Ndivyo ilivyokuwa sikuzote; lile wingu liliifunika kwa mfano wa moto usiku. 17 Na kila lilipoinuliwa lile wingu juu ya ile Hema ndipo wana wa Israeli waliposafiri; na mahali lilipokaa lile wingu, ndipo wana wa Israeli walipopiga kambi yao. 18 Kwa amri ya Bwana Wana wa Israeli walisafiri, na kwa amri ya Bwana walipiga kambi; wakati lile wingu ilipokaa juu ya maskani walikaa katika kambi yao. 19 Na lile wingu lilipokawia juu ya maskani siku nyingi, ndipo wana wa Israeli walipolinda malinzi ya Bwana, wala hawakusafiri. 20 Na pengine lile wingu lilikaa juu ya maskani siku chache; ndipo kwa amri ya Bwana walikaa katika kambi yao, tena kwa amri ya Bwana walisafiri. 21 Na pengine lile wingu lilikaa tangu jioni hata asubuhi; na lile wingu lilipoinuliwa asubuhi walisafiri, au kama likikaa usiku na mchana pia, lilipoinuliwa lile wingu, ndipo waliposafiri. 22 Ikiwa lile wingu lilikawia, likikaa juu ya maskani siku mbili, au mwezi, au mwaka, wana wa Israeli walikaa katika kambi yao, wasisafiri; 23 bali lilipoinuliwa walisafiri. Kwa amri ya Bwana walipiga kambi yao, na kwa amri ya Bwana walisafiri; wakayalinda malinzi ya Bwana, kwa mkono wa Musa.

Tumeamriwa kuhakikisha tunaziadhimisha sikukuu hizi sawa sawa na ilivyoagizwa na kwa kipindi kizima cha siku saba kamili. Kwenye Kutoka 12:16 hapo juu tumeona kwamba inasema kwamba siku ya kwanza na ile ya saba tunatakiwa kuitisha kutaniko takatifu na kazi isifanywe siku hizo zote, bali twaweza kuzifanya zile ambazo kwazo twaweza kuwezeshwa kula tu.

Kumbukumbu la Torati 16:8 Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote.

 

Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa

Sadaka hii ya Mganda wa Kutikiswa inatolewa katika siku ya kwanza ya juma, maarufu kama Jumapili (majira ya saa 9 kamili asubuhi) wakati au ndani ya kipindi cha Idi ya Mikate isiyotiwa Chachu. Sadaka hii inaashiria tendo la Kristo kuingia kwenye chumba cha Kiti cha Enzi cha Mungu ili akubaliwe baada ya ufufuko wake kutoka kwa wafu kama ilivyoonyeshwa kwenye kitabu cha Danieli 7:13-14 na Yohana 20:17. Kristo alifanyika kuwa ni sadaka ya kutikiswa, ambayo ni malimbuko wa mavuno yote (Kutoka 29:24-27; pia tazama Mambo ya Walawi 7:30, 34; 8:27, 29; 9:21; 10:14, 15; 14:12, 24; 23:11-20; Hesabu 5:25; 6:20; 18:11, 18)” (Cox, W.E.,  “K” jarida la Pasaka (Na. 98) [The Passover (No. 98)], CCG, 1995-2008, ukurasa 2,3,8,9).

 

“Adhimisho la Mganda wa Kutikiswa ni amri ya lazima linaloendana na adhimisho la Sikukuu ya Pasaka na inahusiana na zote mbili za kipindi cha Pentekoste na ulaji wa mavuno mapya” (Mambo ya Walawi 23:9-14) (Cox, W.E., “L” jarida la (Mganda wa Kutikiswa (Na. 106b) [The Wave Sheaf Offering (No. 106b)], CCG, 1995-2008, ukurasa 2).

 

Pentekoste

Idi ya Majuma au Pentekoste (Kutoka 23:16; 34:22) hufanyika siku ya hamsini tangia siku ya kutolwa kwa Mganda wa Kutikiswa ambayo huwa katika siku ya kwanza ya juma, au Jumapili ilifuatiwa na Sabato saba kamili. Idi hii ya Majuma ni ishara mavuno ya wateule, ambayo inafananishwa na mavuno ya ngano. Soma jarida la Jinsi ya Kuhesabu Kufikia Pentekoste (Na. 173) [The Omer Count to Pentecost (No. 173)].

 

Siku ya Baragumu

Idi hii ya Ukumbusho wa Kuzipiga baragumu huadhimishwa siku ya Kwanza ya mwezi wa Saba (Tishri) ni siku ya mapumziko na kufanya mkutano mtakatifu (Mambo ya Walawi 23:24). Siku hii Takatifu kwa kawaida inaonekana kuwa ni ashirio la baragumu ijayo itakayopigwa na Malaika Mkuu Mikaeli na kwenye Maknisa ya Mungu inawakilisha kurudi kwa Masihi. Pia soma jarida la Baragumu (Na. 136) [Trumpets (No. 136)].

 

Siku ya Upatanisho

Siku ya Upatanisho ni ya kuitisha kusanyiko takatifu na kwenye siku hii tunazitesa nafsi zetu (Mambo ya Walawi 23:27). Inaangukia katika siku ya 10 ya mwezi wa Saba na inamaana ya upatanisho wa Israeli na Mungu hapa Duniani kipindi cha kuja kwake Masihi. Soma pia jarida la Upatanisho (Na. 138) [Atonement (No. 138)].

 

Sikukuu ya Vibanda

Kumbukumbu la Torati 16:13-15 Fanya sikukuu ya vibanda siku saba, utakapokwisha kuyakusanya yatokayo katika sakafu yako ya nafaka, na katika kinu chako cha divai; 14 nawe utafurahi katika sikukuu yako, wewe, na mwanao, na binti yako, na mtumwa wako, na mjakazi wako, na Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako. 15 Siku saba mfanyie sikukuu Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, atakubarikia katika maongeo yako yote, na katika kazi zote za mikono yako, nawe uwe katika kufurahi kabisa.

 

Sikukuu ya Vibanda au Sikukuu ya Kukusanyika (Kutoka 23:16; Kumbukumbula Torati 29:12-40) ni kiashirio cha zama ya utawala wa milenia ambapo Masihi atakuwa ni mtawala. Sikukuu hii huwa inaanza tangu siku ya kumi na Tano ya wezi wa Saba ambayo pia ni Siku Takatifu. Inafuatiwa na Sikukuu nyiungine inayokwenda kipindi kimoja katika siku ya 22 inayoitwa ni Siku ya Mkunato wa Makini ambayo ni Sikukuu muhimu sana kuiadhimisha pia. (Mambo ya Walawi 23:34; Kumbukumbu la Torati 16:13-15; 31:12-13). Sikukuu hii ya Mkutano wa Makini huashiria ufufuo wa pili na wa mwisho utakaofanyika baada ya kipindi cha miaka efu moja kinachojulikana pia kama Molenia na cha ujio wa Mji Mtakatifu wa Mungu. Soma jarida la Maadhimisho ya Sikukuu (Na. 56) [Keeping the Feasts (No. 56)].

 

Maandalio ya Kuadhimisha Sikukuu

“Kuna taratibu zinazotuongoza katika kufanya maandalizi ya jinzi ya kuadhimisha Sikukuu hizi. Haitosho tu kwa sisi kufanya maamuzi ya kuacha kufanya kazi zetu na kwenda kushika sikukuu hizi, bali tunapaswa kujua kwamba sisi sote tunapaswa kujiandaa kifedha na kimwili pia. Hii inamaanisha kwamba tunatakiwa tufanye maandalizi kwanza na ndipo tuende kuziadhimisha Sikukuu hizi. Kumbukumbu la Torati 12:17-19 inasema kuna utaratibu na kanuni za kutumia zaka ya pili. Tunatakiwa kuitenga kando zaka ya pili ili tuitumie tunapokwenda kwenye Sikukuu hizi.

Kumbukumbu la Torati 12:17-19  Usile ndani ya malango yako zaka ya nafaka zako, wala ya divai yako, wala ya mafuta yako, wala wazaliwa wa kwanza wa makundi yako, ya ng'ombe wala ya kondoo, wala nadhiri zako uwekazo zo zote, wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya mkono wako; 18 lakini hivyo mtakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, wewe, na mwanao mume na mke, na mtumwa wako mume na mke, na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako, katika yote utakayotia mkono wako. 19 Jilinde nafsi yako usimwache Mlawi siku zote uishizo katika nchi yako.

(Cox, W.E, “M” Keeping the Feasts (No. 56), CCG, 1994-2007, ukurasa wa 8).

 

Zaka hii ya pili inatakiwa itumike kwenye kipindi hiki tunachojihudhurisha kwenye Sikukuu hizi kwenye maeneo yetu wakati umbali unapokuwa mkubwa kufikia kwenye mahali palipochaguliwa kufanyika Idi hizi.

Kumbukumbu la Torati 12:21 Na mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apaweke jina lake, pakiwa mbali nawe mno, ndipo utakapochinja katika kundi lako la ng'ombe na kondoo alilokupa Bwana kama nilivyokuagiza, nawe utakula ndani ya malango yako, kwa kufuata yote inayotamani roho yako.

 

Kama tunavyowea kujinea, utaratibu wa kujiwekea akiba ya zaka hii umefungamanishwa na maadhimisho haya ya Sikukuu.

Kumbukumbu la Torati 14:22-29 inasema: "Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka. 23 Nawe utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wako, daima. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako; 25 ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; 26 na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng'ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula huko mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako; 27 na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani hana fungu wala urithi pamoja nawe. 28 Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako; 29 na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba Bwana, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.

Sikukuu hizi zinafanya kazi ndani ya mfumo wa Yubile. Soma pia jarida la Sikukuu za Mungu na Jinsi Zinavyohusiana na Uumbaji (Na. 227) [God's Feasts as they relate to the Creation (No. 227)].

 

Jinsi Sikukuu hizi zinavyohusika kuwa ni sehemu ya Mpango wa Wokovu wetu

Kusudi la Mpango wa Mungu limefunuliwa na utaratibu na mpangilio wa hizi Sikukuu, kwa namna zilivyopangiliwa zikiwa ni amri mhumu kuagizwa na Biblia. Sikukuu hizi ziliamriwa na Yahova (Yehova) na akapewa maagizo yake nabii Musa. Sikukuu hizi ziliamriwa kuwa zitangazwe kwa kupigiwa mbiu kuwa ni siku takatifu na ambazo wanatakiwa kufanya ,akutaniko matakatifu kwa Bwana. Ikumbukwe pia kwamba Sikukuu hizi ni za Bwana na aliziita mwenyewe kuwa hizi ni Sikukuu Zangu (Law. 23:2). Zimeitwa na kujulikana kuwa ni Sikukuu za Bwana kwenye Mambo ya Walawi 23 na 2Nyakati 2:4. Neno sikukuu zenu lilitumika pia kwenye kitabu cha Hesabu 15:3 na 29:39. Neno sikukuu zao limetumika kwenye  kitabu cha Isaya 1:14 na 5:12 kwa matumizi yaliyo kinyume na ukweli halisi ulivyoandikwa kwenye nakala hasilia za kale. Sikukuu hizi hazina uhusiano wowote na mambo ya kidunia wala hazihusiani na mifumo yoyote ya watu wa dunia hii. Na haziwezi kubadiilika kwa sababu yoyote ile au kuondolewa hadi utakapokuja Mpango wale kamili wa Wokovu, ambao kwazo huwakilisha, kipindi ambacho mpango wake huu utakapokuwa umeondolewa au kufikia tamati yake.

Mambo ya Walawi 23:2-44 inasema: "Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Sikukuu za Bwana, ambazo mtazipigia mbiu kuwa ni makusanyiko matakatifu; hizi ni sikukuu zangu. 3 Mtafanya kazi siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, kusanyiko takatifu; msifanye kazi ya namna yo yote; ni Sabato kwa Bwana katika makao yenu yote. 4 Sikukuu za Bwana ni hizi, ni makusanyiko matakatifu, ambayo mtayapigia mbiu kwa nyakati zake. 5 Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi wakati wa jioni, ni pasaka ya Bwana. 6 Na siku ya kumi na tano ya mwezi ule ule ni sikukuu kwa Bwana ya mkate usiotiwa chachu; mtaila mikate isiyochachwa muda wa siku saba. 7 Siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu msifanye kazi yo yote ya utumishi. 8 Lakini mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto siku saba; siku ya saba ni kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi. 9 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 10 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa malimbuko ya mavuno yenu; 11 naye atautikisa mganda mbele za Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada ya Sabato kuhani atautikisa. 12 Na siku hiyo mtakayoutikisa mganda, mtamsongeza mwana-kondoo wa kiume mkamilifu wa mwaka wa kwanza awe sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana. 13 Na sadaka yake ya unga itakuwa sehemu za kumi mbili za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, ni kafara iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto kuwa harufu ya kupendeza; na sadaka yake ya kinywaji itakuwa ni divai, robo ya hini. 14 Nanyi msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote. 15 Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba; 16 hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya. 17 Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba, itaokwa na chachu, iwe malimbuko kwa Bwana. 18 Nanyi, pamoja na hiyo mikate, mtasongeza wana-kondoo saba, walio wakamilifu, wa mwaka wa kwanza, na ng'ombe mume mmoja, na kondoo waume wawili; watakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, pamoja na sadaka yao ya unga, na sadaka zao za kinywaji, sadaka ya harufu ya kupendeza iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. 19 Nanyi mtasongeza mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wana-kondoo wawili waume wa mwaka wa kwanza kuwa dhabihu ya sadaka za amani. 20 Kisha kuhani atawatikisa pamoja na hiyo mikate ya malimbuko kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana, pamoja na wale wana-kondoo wawili; watakuwa watakatifu kwa Bwana, wawe wa huyo kuhani. 21 Nanyi mtapiga mbiu siku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yo yote ya utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu. 22 Nanyi hapo mtakapovuna mavuno ya nchi yenu, usivune kabisa kabisa pembe za shamba lako, wala msiyakusanye masazo ya mavuno yako; utayaacha kwa ajili ya huyo maskini, na mgeni; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 23 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 24 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi, kutakuwa na kustarehe kabisa kwenu, ni ukumbusho wa kuzipiga baragumu, ni kusanyiko takatifu. 25 Msifanye kazi yo yote ya utumishi; nanyi mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto. 26 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 27 Lakini siku ya kumi ya mwezi huo wa saba ni siku ya upatanisho; itakuwa kusanyiko takatifu kwenu, nanyi mtazitesa nafsi zenu; nanyi mtasongeza sadaka kwa Bwana kwa njia ya moto. 28 Nanyi msifanye kazi yo yote siku hiyo; kwa kuwa ni siku ya upatanisho, ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu mbele za Bwana, Mungu wenu. 29 Kwa kuwa mtu awaye yote asiyejitesa mwenyewe siku iyo hiyo, atakatiliwa mbali na watu wake. 30 Na mtu ye yote afanyaye kazi ya namna yo yote siku hiyo, mtu huyo nitamwangamiza atoke katika watu wake. 31 Msifanye kazi ya namna yo yote; ni amri ya milele katika vizazi vyenu, katika makao yenu yote. 32 Itakuwa kwenu sabato ya kustarehe kabisa, nanyi mtazitesa nafsi zenu; siku ya kenda ya mwezi wakati wa jioni, tangu jioni hata jioni, mtaishika hiyo Sabato yenu. 33 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa Bwana. 35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi. 36 Mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yo yote ya utumishi. 37 Sikukuu za Bwana ni hizi, ambazo mtazipigia mbiu ya kuwa ni makusanyiko matakatifu, ili mmsongezee Bwana sadaka kwa moto, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga, na dhabihu, na sadaka za kinywaji, kila sadaka kwa siku yake; 38 zaidi ya hizo Sabato za Bwana, na zaidi ya matoleo yenu, na zaidi ya hizo nadhiri zenu zote, na zaidi ya sadaka zenu za hiari, ambazo mwampa Bwana. 39 Lakini siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, hapo mtakapokuwa mmekwisha kuyachuma mavuno ya nchi, mtaweka sikukuu ya Bwana muda wa siku saba; siku ya kwanza kutakuwa na kustarehe kabisa, na siku ya nane kutakuwa na kustarehe kabisa. 40 Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matunda ya miti mizuri, na makuti ya mitende, na matawi ya miti minene, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele za Bwana, Mungu wenu, muda wa siku saba. 41 Nanyi mtaishika kuwa sikukuu kwa Bwana muda wa siku saba katika mwaka; ni amri ya milele katika vizazi vyenu; mtaishika katika mwezi wa saba. 42 Mtakaa katika vibanda muda wa siku saba; wazalia wote wa Israeli watakaa katika vibanda; 43 ili vizazi vyenu vipate kujua ya kuwa niliwaketisha wana wa Israeli katika vibanda, hapo nilipowaleta kutoka nchi ya Misri; mimi ndimi Bwana Mungu wenu. 44 Naye Musa akawaambia wana wa Israeli hizo sikukuu za Bwana.

 

Kristo aliziadhimisha zote, yaani Sabato ya juma, Miandamo ya Mwezi na Sikukuu zote hizi. Kanisa la Mitume pia waliadhimisha Sabato, Miandamo ya Mwezi na Sikukuu zote hizi (Makolosai 2:16) na ndivyo lilivyofanya kanisa kwa kipindi chote cha zaidi ya miaka elfu mbili. Katika kipindi cha Milenia mataifa yote pia wataziadhimisha Sabato zote hizi, yaani za juma, na Miandamo ya Mwezi na Sikukuu zote (Isaya 66:23; Zekaria 14:16-19).

 

Mchakato mzima wa kuzielezea na kuwafanya wateule wajulikane miongoni mwa vikundi vyote vinavyojiita Wakristo unatimilika kwa kutegemea kama wanaziadhimisha au kuzijua Siku hizi Takatifu zinapokuwa zinatikea hadi kutakapofika Ufufuo Mkuu au wa Pili ambao ni wa watu wote. Siku hizi takatifu hazitaweza kukoma hadi siku ile ya Mkutano Mkuu wa makini utakapokamilisha sehemu ya mpango wake. Kila Sikukuu inawakilisha utaratibu huu endelevu wa Mpango wa Mungu na kwa tafsiri nyingine huitwa mfumo wa mavuno ambao bado unadumu na kwa sasa umefunuliwa kwetu.

1Petro 2:5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

 

Ukristo Mamboleo wa sasa hauuna habari na wala hauzijui na kuziadhimisha Sikukuu hizi hali inayowafanya washindwe kuelewa lolote lililo kwenye Mpango huu wa kibiblia. Makanisa haya ya kisasa hayatilii maanani maelekezo au amri hizi ambazo Biblia (ambayo ni msingi wa dini ya Ukristo wa Kiyahudi) inaonyesha kuwa ziliwekwa tangu mwanzo wa uumbaji kama ulivyoelezwa kwenye kitabu cha Mwanzo na hatimaye zinatolewa na kuamriwa na Mungu kupitia nabii Musa na watumishi wake wengine waliofuatia. Sheria hizi zinaelezea kwa kina jinsi ya kuiishia Imani na kuelezea umuhimu wa Sikukuu zake.

 

Sikukuu hizi zimeamriwa na Mungu kwa kupitia Kristo na Kristo ameziendeleza na kuaiwekea utaratibu kwa kuweka maelekezo yake kwa wateule na hatimaye kwa watu wa mataifa yote kwa utaratibu mwelekeo wa Milenia. Kristo ni yeye yule, jana leo, kesho na hata milele (Waebrania 13:8). Mungu hana kigeugeu (Malaki 3:6; Yakobo 1:17). Kwa hiyo, hakuna mabadiliko na kwa hiyo, siku wanazozishikilia kuwa ni takatifu kwa wanadamu zilizotolewa na kuelekezwa kwenye Sheria na amri hazibadiliki.

 

Siku hizi Takatifu na Sabato zimesusiwa na kupotezewa naama na umuhimu yake kwa makusudi kabisa. Hiyo ndiyo ahadi ambayo Mungu mwenyewe ameiweka kwa kupitia manabii wake watakatifu. Mungu alisema hivyo kupitia nabii Amosi kwa kulilinganisha taifa la Israeli kwenye Siku za Mwisho sawa na kapu la matunda ya wakati wa hari (Amosi 8:1). Trndo la kushindwa kumtii Mungu ni chanzo kikubwa. Adhabu inayotokana na hali hii ya kumuasi Mungu ni kwamba maadhimisho haya ya Sabato na Sikukuu kubadilika kuwa ni maombolezo. Hii inafuatia na kukumbwa na njaa ya kukosa kulisikia neno la Yahova (Yehova) (Amosi 8:11-14). Ni kwa ajili ya kushindwa kuelewa asili ya Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20) watu wanaadhibiwa (Hosea 8:5-9).

 

Wateule wanahukumiwa kutokana na jinsi wanavyomjua Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli, jambo ambalo kanuni ya aheria inavyotaka na kuwa ikamilike ndani ya mioyo ya watu kwa jinsi ya kila mtu peke yake na binafsi yake.

 

Jambo kuu hapa siyo Sabato au Sikukuu au Sheria au Amri, bali ukweli wa kwamba Mungu, baba yetu ni Mmoja na wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20) na kwamba, ni yeye tu peke yake hawezi kufa (1Timotheo 6:16). Mtu anaweza kuitunza Sabato nab ado anaweza kuwa ni mtu mwenye imani potofu. Iwapo kama hatuta shikilia kwa bidii ukweli huu tutaondolewa mbali kutoka kwa wateule na tukatolewa kwenye upotevu mkuu na tukaamini uwongo (2Wathesalonike 2:11).

(Cox, W.E., “N” The Holy Days of God (No. 97), CCG, 1995-2007, kurasa za 2,5,6,7,8,11).

 

Sadaka au Dhabihu za Sikukuu

“Moja wapo ya maandalizi ya Sikukuu hizi zote ni tendo la kutafakari na kushukuru kwa baraka zote ambazo Mungu, baba yetu ametubarikia amabazo hatimaye zinafanyika kuwa ni sadaka tunazomtolea kama kumrushia yeye mwenyewe aliyetukirimia. Hatuwezi kujionyesha tu tukijihudhurisha kwenye Sikukuu kwa kufanya maamuzi ya wakti ule tu kwa kulinganisha na kile tulichonacho mifukoni mwetu kwa wakati ule, au kwa kuandika hawala ya kuchukulia fedha benki na tukifikiri kuwa tumetimiza wajibu wetu kama Wakristo.

2Wakorintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

 

Tunapaswa kutilia maanani kile ambacho Mungu alichotufantia kwa kutoa sadaka inayoendana na ukweli wa baraka zake alizoturuzukia.

Kumbukumbu la Torati 16:17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa.

 

Mara tatu kila mwaka Mungu ametuamuru tukutanike mahali alipolikalisha jina lake, na na kamwe tusiende mbele zake Bwana mikono mitupu.

Kumbukumbu la Torati  16:16 "Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu.

 

Neno hili la “mahali alipopachagua” limebadilishwa kwa mara nyingi na linategemea kwa mahali kwenye mataifa ambayo Mungu ametupa kuyamiliki. Sikukuu hizi zinaadhimishwa na kusherehekewa kwenye mataifa tuliyopewa na haitegemei kuwa ni mjini Yerusalemu” (Cox, W.E., “O” jarida la Sadaka au Dhabihu (Na. 275) [Offering (No. 275)], CCG, 2006, ukurasa wa 2,3).

 

“Maelekezo kuhusu jinsi ya kupachagua mahali hapa yanapatikana kwenye kitabu cha Kutoka 23:17-19.

Kutoka 23:17-19 Mara tatu katika mwaka watu waume wako wote watahudhuria mbele ya Bwana MUNGU. 18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi. 19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

“Mafuta” ni dhabihu mojawapo itolewayo kwenye Sikukuu. Haina maana kuwa ni mafuta yale yaliyokatazwa kwenye Sheria  ndiyo yaliwe hapa (kama ilivyoandikwa kwenye Mambo ya Walawi 3:17). Neno hilohilo ndilo linaloonekana kwenye kitabu cha Mwanzo 45:18 na Nehemia 8:10.

Mambo ya Walawi 3:17 Neno hili litakuwa amri ya daima, katika vizazi vyenu vyote, ndani ya nyumba zenu zote, ya kwamba hamtakula mafuta wala damu kabisa.

 

“Kwa mujibu wa Amri na Sheria zake, sadaka zinaweza kutolewa mara tatu kila mwaka—na siyo kila Siku Takatifu. Pia utoaji na makusanyo yanatakiwa yafanyike katika kila siku ya kwanza ya Sikukuu hizi jioni yake ya kwanza ya kila Sikukuu, na isibakizwe hata asubuhi yake. Kuna maana nzuri kufanya hivyo, yaani ni kwamba ili kuwafanya masikini na Walawi wale na maandalio yalifanywa kabla ya Sikukuu. Masihiataurudisha utaraibu huu kwenye kipindi cha utawala wa Milenia, lakini hii ni mojawapo ya sheria na amri za Mungu zinazotakiwa kufanywa hata leo” (soma pia jarida la Makutaniko (Na. 139) [Ingathering (No. 139)].

 

Sikukuu ya Ukumbusho wa Kuzipiga Baragumu haikuandikwa kwenye Kumbukumbu la Torati 16. Sambamba na hilo kumekatazwa kabisa kutoa aina yoyote ya sadaka tunapojihudhurisha kuiadhimisha Siku ya Upatanisho. Kwa hiyo, kutajwa tu kuwa ni mara tatu kwa mwaka na ndivyo ilivyagizwa na inamaana hiyohiyo tu. Mahusiano yake yanalenga kuelezea mavuno makuu matatu ya Mungu ambayo ni: Masihi akiwa kama ni sadaka ya Mganda wa Kutikiswa, Wateule wakiwa kama ni wahusika wa ufufuo wa Kwanza (sawa na mavuno ya ngano ya wakati wa Pentekoste), na mavuno makuu ya mwisho wa dunia yaliyo kwenye taswira ya Sikukuu ya Vibanda.

 

Tendo la kufanya machangizo na kutoa sadaka za kila juma kufanywa Kanisani ni kinyume na amri na sheria za Mungu. Changizo analolitaja mtume Paulo kuwa lifanyike siku ya kwanza ya juma, au Jumapili, halikuwa ni agizo au ashirip la kuwekwa kwa sheria nyingine ya kuabudu siku ya Jumapili na wala hakumaanisha kuanzishwa kwa utaratibu mpya wa kutoa sadaka kwa kila juma (1Wakorintho 16:2-4)” (Cox, W.E. “P” jarida la Zaka (Na. Tithing (No. 161), CCG, 1996-2007, kurasa za 12,13).

 

“Sadaka iliyotakiwa iligeuzwa kutoka umuhumu wake hadi kufanyika kuwa sadaka ya kiroho ya kila siku zilizo kwenye mfumo wa Siku Takatifu, tangia Sabato, Miandamo ya Mwezi na Sikukuu. Dhabihu zitolewazo kwa mujibu wa amri na Sheria ziliamriwa kwa kufanyika makusanyo au changizo maalumu yaliyoratibiwa kwa mujibu wa mamlaka ya kitaifa. Matoleo au changizo la Mfalme limeelezwa kwenye jarida la Zaka (Na. 161) [Tithing (No. 161)].

Ezekieli 45:14-17 na sehemu ya mafuta iliyoamriwa, katika bathi ya mafuta, itakuwa sehemu ya kumi ya bathi katika kori moja, ambayo ni bathi kumi, yaani homeri; maana bathi kumi ni homeri moja; 15 na mwana-kondoo mmoja wa kundi katika mia mbili, katika malisho ya Israeli yenye maji; kwa sadaka ya unga, na kwa sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka za amani, ili kuwafanyia upatanisho, asema Bwana MUNGU. 16 Watu wote wa nchi watatoa toleo hili kwa ajili ya mkuu katika Israeli. 17 Tena itakuwa kazi ya mkuu kutoa hizo sadaka za kuteketezwa, na sadaka za unga, na sadaka za vinywaji, katika sikukuu, na katika mwezi mpya, na katika sabato, katika sikukuu zote za nyumba ya Israeli zilizoamriwa; atatengeneza sadaka ya dhambi, na sadaka ya unga, na sadaka ya kuteketezwa, na sadaka za amani, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.

 

Sadaka hii zilikuwa ni zaka ya zaka ya mafuta na nusu sadaka ya zaka ya dhabihu ya nyama. Mfalme aliifanya iwepo na kutolewa katika Sabato, Miandamo ya Mwezi, Siku Takatifu na dhabihu. Kwa hiyo, sio sahihi kudai kwamba zaka iliondolewa na mahala pake kuchukuliwa na sadaka kwa kuwa kwa sababu zilitolewa na hali mtengano” (Cox, “F”, op. cit., p. 5).

Hesabu 31:50-54 inasema: Nasi tumeleta matoleo ya Bwana, aliyopata kila mtu, ya vyombo vya dhahabu, na mitali, na timbi, na pete za muhuri, na vipini, na vikuku, ili kuzifanyia upatanisho nafsi zetu mbele ya Bwana. 51 Musa na Eleazari kuhani wakapokea kwao hiyo dhahabu, maana, vile vyombo vyote vilivyofanyizwa. 52 Na dhahabu yote ya sadaka ya kuinuliwa waliyosongeza kwa Bwana, ya maakida wa elfu elfu, na maakida wa mia mia, ilikuwa shekeli kumi na sita elfu na mia saba na hamsini. 53 (Kwa kuwa hao watu wa vita walikuwa wametwaa nyara, kila mtu nafsi yake.) 54 Basi Musa na Eleazari kuhani wakapokea hiyo dhahabu mikononi mwa hao maakida wa elfu elfu na wa mia mia, na kuileta ndani ya hema ya kukutania, ili iwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.

 

Hesabu 3:44-51inasema: Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 45 Uwatwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza katika wana wa Israeli, na wanyama wa Walawi badala ya wanyama wao; na hao Walawi watakuwa wangu mimi; mimi ndimi Bwana. 46 Tena kwa kuwakomboa hao watu mia mbili na sabini na watatu, wa hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli, ambao wamezidi ile hesabu ya Walawi, 47 utatwaa shekeli tano kwa kichwa cha kila mtu kwa hiyo shekeli ya mahali patakatifu (shekeli ni gera ishirini); 48 na hizo fedha ambazo waliosalia wamekombolewa kwazo utampa Haruni na wanawe. 49 Basi Musa akawatoza fedha za ukombozi, hao waliozidi hesabu ya wale waliokombolewa na Walawi; 50 akatwaa hizo fedha kwa wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli; shekeli elfu moja na mia tatu na sitini na tano kwa shekeli ya mahali patakatifu; 51 kisha hizo fedha za ukombozi Musa akampa Haruni na wanawe, kama neno la Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Musa.

 

Zaka hii ya zaka zote alipewa Kuhani Mkuu ili kumfanya aendelee kulihudumia Hekalu na adumu kwenye huduma na maongozi yake (2Wafalme 12:1-19; 22:5-6; Ezra 6:8).

 

Mwaka wa Saba au Mwaka wa Sabato na wa Mapumziko ya Ardhi

Dhana hii inajumuisha na:

1. Mwaka wa saba wa maachilio ambao watu wanaachiliwa kutoka kwenye shughuli za utumwa na shokoa (Kutoka 21:2-6, Kumbukumbu la Torati 15:12-18),

2. Kusameheana madeni (Kumbukumbu la Torati 15:1-6), na

3. Ni Sabato au mapumziko ya Ardhi (Kutoka 23:10-11; Mambo ya Walawi 25:1-7, 19-24).

 

Kwenye mwaka huu wa Sabato au mwaka wa Saba, tunauadhimisha kwa kuisoma Torati ya Mungu kila siku hasa kwenye maadhimisho ya Sikukuu ya Vibanda (Kumbukumbu la Totati 31:10-13; Nehemia 7:73; 8:1-18).

 

Kumbukumbu la Torati 30:10 ukiwa utaifuata sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa kuyashika maagizo yake, na amri zake zilizoandikwa katika chuo hiki cha torati; ukimwelekea Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote.

 

“Neno linalotakiwa kutumika kukitaja kitabu hiki cha Sheria za Mungu ni Torah au Gombo la Torati. Bullinger anafanya mlingano kama huohuo na pia anakielezea kama kilivyoandikwa kwenye 2Wafalme 22:8 na 23:25, na anaiweka hoja yake kutoka kwenye Kutoka 17:14 hadi anapoichukulia kwenye 2Wafalme 22:8-13 kwa kulinganisha na 23:25 ambapo inaonyesha kwamba Kitabu chote kizima cha Torati kilipaswa kiheshimiwe na kwa kuwa sio taifa tu lingaliloadhibiwa (sawa na aya ya 14).

 

Tunaona kutoka kwenye Nehemia 8:18 kuwa Torati ilisomwa kila siku na kwamba haipaswi isomwe tu katika siku ya mwisho ya Mkutano wa Makini, au kwa siku nyingine yoyote peke yake. Sikukuu iliadhimishwa kila siku na kwa mujibu wa ilivyoagizwa na Torati, na siku ya Nane kulikuwa na kusanyiko takatifu iliyojulikana kama ni Siku Kubwa ya Mkutano wa Makini (sawa na Mambo ya Walawi 23:36; Hesabu 29:35) iliyofanywa kwa sadaka zake maalumu (sawa na ilivyoandikwa na Soncino).

 

Tendo hili la kusomwa kwa Torati linaondoa uwezekano na hatari ya kujipenyeza imani za kimapokeo na pia husaidia kulinda na kurejesha maadhimisho ya Yubile na Sabato za Mapumziko ya Ardhi. Pia inaonyesha utii wetu kwenye mapenzi ya Mungu na huwatia nguvu watu wetu na kuwapa maono ya Mpango wa Wokovu” (Cox, W.E., “Q” jarida la Jinsi Usomaji wa Torati ulivyofanywa na Ezra na Nehemia (Na. 250) [Reading the Law with Ezra and Nehemiah (No. 250)], CCG, 1998-2007, ukurasa 11).

 

Mapumziko ya Mwisho

“Mwaka huu wa Sabato huendana na ardhi kupumzishwa kutoilima wala kuichimbwa kwa matumizi ya kibiashara au mavuno. Maelekezo ya mari hii yameandikwa kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi 25:1-7 ambayo yanakataza upandaji wowote wa mazao ya aina yoyote mashambani au kuvuna zabibu au vichala vya mizabibu (Kutoka 23:10). Maongeo ya mashambani na zabibu za vichala zilivyokaa wazi pia havitakiwi kukusanywa kwenye mwaka huu wa saba wa mzunguko wa miaka hii mitakatifu. Bali zinaweza kutumiwa kama chakula na wamiliki wenyewe, watu wa nyumbani wake na watu masikini au wageni wapitao au waliokuja kwenye nchi yao. Kwa hiyo, nchi inatakiwa iwe huru na isifanyiwe kazi yoyote ingawaje itamea mazao ya namna fulani ambayo yatamea yenyewe tu pasipo kupandwa wala kulimiwa na mtu” (Cox, “P”, op.cit., ukurasa wa 13).

 

Nchi au ardhi yote ni ya Mungu na haitakiwi kuuzwa kwa kipindi cha kudumu. Sisi ni wa milki yake Mungu.

Mambo ya Walawi 25:23 Nayo nchi haitauzwa kabisa kabisa; kwani nchi ni yangu mimi; maana ninyi ni wageni na wasafiri wangu

 

Hatupaswi kudai umiliki wa mito, kwa kuwa ni Mungu aliyeifanya hiyo na ni milki.

Ezekieli 29:9 Nayo nchi ya Misri itakuwa ukiwa na jangwa; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; kwa sababu amesema, Mto huu ni wangu, nami nimeufanya.

 

Wakati ardhi inaponajisika Mungu huihukumu nchi nzima na wakazi wake kutapikwa kwa kufukuziliwa mbali watoke mbali na nchi hiyo.

Mambo ya Walawi 18:25-30 … na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa. 26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu. 29 Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, nafsi hizo zitakazoyafanya zitakatiliwa mbali na watu wao. 30 Kwa ajili ya hayo yashikeni mausia yangu, ili kwamba msifanye kabisa desturi hizi zichukizazo mojawapo, zilizotangulia kufanywa mbele zenu, wala msijitie unajisi katika mambo hayo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

 

Tendo la kuzivunja amri ma sheria za Mungu zilizoandikwa kwenye Torati yake Mungu husababisha hukumu. Adhabu na matukio yatakayofuatia kama hatutasikiliza na kuishika Torati hii, vimeandikwa kwenye Mambo ya Walawi 26:14-33.

Mambo ya Walawi 26:14-15 " Lakini msiponisikiza, wala hamtaki kuyafanya maagizo hayo yote; 15 nanyi mkizikataa amri zangu, na roho yenu ikichukia hukumu zangu, hata ikawa hamtaki kuyafanya maagizo yangu yote, bali mwalivunja agano langu;

 

Mambo ya Walawi 26:43 Nchi nayo itaachwa na wao, nayo itazifurahia Sabato zake, itakapokuwa ukiwa pasipokuwa na wao; nao wataikubali adhabu ya uovu wao; kwa sababu, naam, ni kwa sababu wamezikataa hukumu zangu, na roho zao zimezichukia amri zangu.

 

Tunapokuwa tukipanda aina yoyote ile ya miti ya matunda, matunda yamekatazwa kuliwa yanapokuwa yanatoa mazao yake ya kwanza yatokayo kwenye mwaka wa kwanza.

Mambo ya Walawi 19:23-25 Nanyi hapo mtakapoingia nchi ile, mkiwa mmepanda miti ya namna zote kwa ajili ya chakula, ndipo mtayahesabu matunda yake kama ni kutotahiriwa; muda wa miaka mitatu miti hiyo itakuwa kwenu kama kutotahiriwa; matunda yake hayataliwa. 24 Lakini mwaka wa nne matunda yake yote yatakuwa ni matakatifu, kwa ajili ya kumpa Bwana shukrani. 25 Na katika mwaka wa tano mtakula katika matunda yake, ili ipate kuwapa maongeo yake; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

 

Vilevile kama tunavyojionea kwenye kwenye mwaka wa nne matunda yote yanachukuliwa kuwa ni matakatifu ya yanatakiwa yapelekwe kwa makuhani yakiwa kama sadaka kwa Bwana.

Hesabu 5:9-10 Tena kila sadaka ya kuinuliwa, ya vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, watakavyosongeza kwa kuhani, itakuwa ni yake. 10 Tena vitu vilivyowekwa wakfu na mtu awaye yote, vitakuwa ni vya kuhani; kitu cho chote mtu atakachompa kuhani, kitakuwa chake.

 

“Tendo la kuiadhimisha Sabato hii ya Mapumziko ya ardhi ni la muhimu, ingawa linashutumiwa na kuonekana kuwa linaenda kinyume na maendeleo ya uchumi au ustawi endelevy wa taifa. Hukumu kwa kutoitunza sheria hii ya Sabato na mapumziko ya ardhi na kutoutunza mwaka wa Yubile ni nchi au taifa zima kwenda utumwani (Mambo ya Walawi 26:33-35).

Mambo ya Walawi 26:34-35 Hapo ndipo nchi itakapozifurahia Sabato zake, wakati itakapokuwa hali ya ukiwa, nanyi mtakapokuwa katika nchi ya adui zenu; ndipo nchi itakapopumzika, na kuzifurahia Sabato zake. 35 Wakati wote itakapokuwa na ukiwa, itapumzika; ni hayo mapumziko ambayo haikuwa nayo katika Sabato zenu, hapo mlipokaa katika nchi hiyo

 

Yuda walikwenda utumwani kwa kuwa roho ya kuzipenda amri za Mungu iliondoka kwao na wakanajisika. Yaani ni kusema kwamba, walizitia unajisi Sabato za nchi na utaratibu wa Yubile ulipotea kiasi cha kwamba Wayahudi walikuwa wanauza ardhi yao kwa mtindo wa kujodisha ufikapo mwaka wa Saba, na kumpa mtu asiye Myahudi alilime na hata kwa mtu wa tatu zaidi alilime na hatimaye wakarudi na kuyadai mashamba yao mwaka unaofuatia, na hali kadhalika walifanya hivyohivyo kwa shughuli nyingine za kibiashara ambazo walifanya kwa kukodisha au kuweka poni kipindi chote cha Sikukuu kikifika, na kadhalika wa kadhalika. Hii ilionyesha kuwa walikuwa wanamdhihaki Mungu.

2Nyakati 36:20-21 Na wale waliookoka na upanga akawachukua mpaka Babeli; wakamtumikia yeye na wanawe hata kulipoingia milki ya Uajemi; 21 ili kulitimiza neno la Bwana kwa kinywa cha Yeremia, hata nchi itakapofurahia sabato zake; kwa maana siku zote ilipokaa ukiwa ilishika sabato, kutimiza miaka sabini.

 

Kwenye kitabu cha 2Nyakati 36:20-21, tunaona kwamba lengo la unabii uliotolewa na nabii Yeremia (Yeremia 29:10), ilikuwa ni kwamba Yuda walichukuliwa na kupelekwa utumwani na Yerusalemu na nchi ya Yuda vikabakia ukiwa kwa kipindi cha miaka 70, ili kuifanya nchi na arhi yake vipumzike na kuzifurahia Sabato zake—kwa kuwa Yuda waliacha kuzitunza Sabato na hawakuzishika sheria zake kikamilifu kwenye kipindi kama hicho hicho cha majuma ya miaka 70 iliyokuweko huko nyuma yao, kama vila; tangu kujengwa kwa Hekalu la Sulemani, ambayo ilikuwa ni kipindi cha historia yenye kutukuka ya Israeli iliyofanywa maana yake na Makerubi aliyoonyeshwa nabii Ezekieli kwa njia ya maono. Inapaswa ijulikane pia kwamba taifa lililotumiwa kuiadhibu na kuihusuru Yuda hatimaye lilianguka na Yuda ikarejea na kufanywa upya” (Cox, W.E., “R” kwenye jarida lake la Maana ya Maono ya Ezekieli (Na. 108) [The Meaning of Ezekiel’s Vision (No. 108)], CCG, 1995-2008, ukurasa wa 3, 4).

 

Milki mbalimbali za maeneo au nchi waliyopewa makabila ya Israeli zinaonekana kwenye kitabu cha Yoshua sura zile za 14 hadi 19.

Yoshua 18:1-10 inasema: Kisha mkutano mzima wa wana wa Israeli walikutana pamoja hapo Shilo, wakasimamisha hema ya kukutania kuko; nayo nchi ilikuwa imeshindwa mbele zao. 2 Zilisalia katika wana wa Israeli kabila saba ambazo hazijagawanyiwa bado urithi wao. 3 Yoshua akawauliza wana wa Israeli, akasema, Je! Hata lini mtakuwa walegevu katika kuingia kwenu na kuimiliki hiyo nchi, ambayo yeye Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa? 4 Haya, jichagulieni watu watatu kwa ajili ya kila kabila; nami nitawatuma, nao watainuka waende kati ya hiyo nchi, na kuiandika kama urithi wao ulivyo; kisha watanijilia mimi. 5 Watu hao wataigawanya nchi iwe mafungu saba; Yuda atakaa katika mpaka wake huko upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu watakaa katika mpaka wao upande wa kaskazini. 6 Nanyi mtaiandika nchi iwe mafungu saba, kisha hayo maandiko yake mtaniletea mimi hapa; nami nitawapigia kura hapa mbele ya Bwana, Mungu wetu. 7 Kwa maana Walawi hawana fungu kati yenu; Kwa kuwa huo ukuhani wa Bwana ndio urithi wao; tena Gadi, na Reubeni, na hiyo nusu ya kabila ya Manase, wamekwisha pata urithi wao ng'ambo ya pili ya Yordani upande wa mashariki, ambao walipewa na Musa, mtumishi wa Bwana. 8 Basi watu hao wakainuka wakaenda; kisha Yoshua aliwaagiza wale waliokwenda kuiandika nchi, akawaambia, Endeni, mkapite katikati ya nchi, na kuiandika habari zake, kisha mnijie tena hapa, nami nitawapigia kura kwa ajili yenu hapo mbele za Bwana huko Shilo. 9 Basi watu hao wakaenda, wakapita katikati ya nchi, wakaandika habari zake katika chuo, na kuigawanya kwa miji yake, hata iwe mafungu saba, kisha wakamrejea Yoshua maragoni huko Shilo. 10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao hapo mbele za Bwana katika Shilo; huko Yoshua akawagawanyia wana wa Israeli hiyo nchi sawasawa na mafungu yao.

 

Yoshua 19:51 Hizi ndizo nchi, ambazo Eleazari kuhani, na Yoshua huyo mwana wa Nuni, pamoja na hao vichwa vya nyumba za mababa ya kabila za wana wa Israeli, walizigawanya kwa njia ya kupiga kura, ziwe urithi, huko Shilo mbele ya Bwana, hapo mlangoni mwa hema ya kukutania. Basi hivyo wakamaliza kazi ya kuigawanya hiyo nchi.

 

Miji ya makimbilio imeelezewa kwenye sura yote ya 48 ambako kunajumuisha pia wajibu wanaotakiwa kuufanya katika kugawiwa milki ya ardhi kwa makabila haya.

Yoshua 20:2-9 inasema: "Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie, Haya, toeni hiyo miji ya makimbilio, ambayo niliwaambia habari zake kwa mkono wa Musa; 3 ili kwamba mwenye kuua mtu, aliyemwua mtu awaye yote pasipo kukusudia, na pasipo kujua, apate kukimbilia kuko; nayo itakuwa ni mahali pa kukimbilia kwenu, kumkimbia huyo ajilipizaye kisasi cha damu. 4 Naye ataikimbilia miji hiyo mmojawapo, naye atasimama hapo penye maingilio ya lango la huo mji, kisha atanena neno lake masikioni mwa wazee wa mji; nao watamtia kwao ndani ya mji, na kumpa mahali, ili apate kukaa kati yao. 5 Na kama huyo mwenye kujilipiza kisasi cha damu akimwandamia, ndipo hawatamtoa huyo mwuaji kumtia mkononi mwake huyo; kwa sababu alimpiga mwenziwe naye hakujua, wala hakumchukia tangu hapo. 6 Naye atakaa katika mji huo, hata hapo atakaposimama mbele ya mkutano kuhukumiwa, hata kifo chake kuhani mkuu mwenye kuwapo siku hizo; ndipo yule mwuaji atarudi, na kuuendea mji wake mwenyewe, na nyumba yake mwenyewe, hata mji huo alioutoka hapo alipokimbia. 7 Nao wakaweka Kedeshi katika Galilaya katika nchi ya vilima ya Naftali, na Shekemu katika nchi ya vilima ya Efraimu, na Kiriath-arba (ndio Hebroni) katika nchi ya vilima ya Yuda. 8 Tena ng'ambo ya pili ya Yordani pande za Yeriko upande wa kuelekea mashariki wakaweka Bezeri ulioko nyikani, katika nchi tambarare ya kabila ya Reubeni, na Ramothi katika Gileadi katika kabila ya Gadi, na Golani katika Bashani katika kabila ya Manase. 9 Miji hiyo ndiyo miji iliyoamriwa kwa ajili ya wana wa Israeli wote, na kwa ajili ya mgeni akaaye kati yao ugenini, ili kwamba mtu awaye yote atakayemwua mtu pasipo kukusudia apate kimbilia huko, asife kwa mkono wa mwenye kujilipiza kisasi cha damu, hata hapo atakapokuwa amekwisha simama mbele ya mkutano.

“Miji iliyochaguliwa ilikuwa ni ile ambayo pia walipewa Walawi, ambako kwa kawaida sheria za Mungu zilitakiwa zijulikane sana na kuheshimiwa au kuogopwa” (sawa na tunavyoona kwenye Yoshua 20, hasa ukisoma Biblia inayoitwa The NIV Study Bible, ukurasa wa 318).

 

Aina ya Sabato

“Mwaka wa Sabato unaruhusu kila mtu awe huru kutokana na kazi zote shokoa na za kitumwa zilizoandikwa kwenye amri hii ya nne kufanywa kwenye siku zote za wiki kwa mwaka wote, isipokuwa tu siku za Sikukuu, Miandamo ya Mwezi na Sabato na zile wanazozifanya siku za kawaida na walizotakiwa kuzifanya kila siku na zinazofanywa kwenye jamii zao. Watu wanaweza kuutumia mwaka wa Sabato kwa kujisomea masomo waliyoyachagua kujifunza, na hasa yale yanayoihusu Biblia na ambayo yanaweza kuwasaidia kuwapa maarifa ya kupata faida ya kiuchumi. Katika mwaka wa kawaida, mtu anapoamua kuutumia mwaka mzima wote kwa mapumziko na kuacha kufanya kazi yoyote, basi ajua kwamba anaivunja amri hii ya nne.

 

Umuhimu wa kujiepusha kutokana na kufanya biashara ya kuiuza ardhi na mazao yanayopatikana kila mwaka unapifika mwaka huu unamtaka kila mmoja aache kufanya shughuli za aina yoyote zinazomfanya mtu aweze kutoa zaka ambayo alikuwa anapata kwa kazi zake za kawaida. Ni ukweli usiopingika kwamba sio watu wote ni wakulima na sio wote wanategemea kuendesha maisha yao kutokana na mazao au maongeo ya ardhi. Kwenye jamii zetu za leo watu wengi wanafanya shughuli za kawaida na ni wachache sana miongoni mwao wanaoweza kupata fursa ya kupewa likizo na kulipwa kwa ajili ya Sabato. Hata hivyo, hii hafanyi kutoa fursa au udhuru kwa watu kutoishika sheria hii au haki yake mbayo kila mtu ameamriwa kuitunza kwa mujibu wa Amri na sheria hii. Ni suala la kuamua tu kwa mtu kuamua ama kufanya kazi na kuingiza mapato yake kwa kufanya kazi zaidi ya kushughulikia shughuli na biashara ya mazao.

 

Mungu ameahidi kwamba tutapata mazao mrngi sana kwenye miaka inautangulia miaka hii ya Sabato na Yubile. Hii ilikuwa ni kuwahakikishia kuwepo kwa akiba kubwa ya zaka na mazao yaliyotolewa zaka ingekuwepo ili kutuwezesha tuweze kuitunza miaka hii ya Sabato na Yubile.

 

“Kwa uhuru huu mkubwa waliokuwanao watu kwenye mwaka huu wa Sabato, utaratibu na mfumo wa utoaji zaka uliwekwa huru kwa mtu kutoa ulimwachia mtu mwenyewe aamue kama anakitu kimpasacho kukitoa zaka ama la.

 

“Ni juu ya kila mmoja kuamua kile anachoweza kukiweka wakfu na kukitenga mbali kama zaka yake ya pili kwa mapato aliyoyapata katika miaka sita iliyotangulia nyuma yake na kama bado kimesalia hadi kwenye mwaka huu wa Saba ambao pia ni wa Sabato. Katika miaka hii mitakatifu ya Sabato, fedha zote zinazotolewa Kanisani zinahesabiwa kama sadaka tu ya kawaida(Cox, “P”, op. cit., ukurasa wa 13,14).

 

Sheria ya Kusamehe Madeni

“Mungu ameweka amri maalumu inayohusiana na madeni na wadeni wetu na jinsi ya kusameheana ufikapo Mwaka huu wa Sabato, sheria inayo julikana kama ni ya “mwaka wa maachilio”

 

Imeandikwa kwamba:

Kumbukumbu la Torati 15:1-17 Kila miaka saba, mwisho wake, fanya maachilio. 2 Na jinsi ya maachilio ni hii, kila mkopeshaji na akiache alichomkopesha mwenziwe, wala asimlipize mwenziwe wala nduguye; kwa kuwa imepigwa mbiu ya maachilio ya Bwana.

 

Tunatakiwa sote kusamehe madeni kwa wadeni wetu wote kwenye mwaka huu wa Sabato, hasa kama tutaombwa tuwasamehe.

3 Waweza kumtoza mgeni; lakini kila uwiacho kwa nduguyo mkono wako utamwachilia. 4 Lakini hawatakuwako maskini kwenu; (kwa kuwa Bwana atakubarikia kweli katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako;)  

 

Hata hivyo, tutaendelea kuwadai madeni yetu wale ambao hawapo kwenye imani moja nasi na ambao sio wapendwa wenzetu.

5 kwamba utaisikiza tu kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, uyatunze maagizo haya yote nikuagizayo leo, kuyafanya. 6 Kwani Bwana, Mungu wako, atakubarikia, kama alivyokuahidi; nawe utakopesha mataifa mengi, lakini hutakopa; tena utayatawala mataifa mengi, usitawaliwe na wao.

 

Torati ya Mungu inatukataza tusiende kuwakopa mataifa wasio ndugu zetu wa imani moja. Hii itakuwa hivyo hasa kwa ajili ya baraka alizotuahidia kuwa atatupa kwa wingi, na kwa hiyo kamwe tusiwaendee na kuwakopa. Hata hivyo, tumeamriwa pia tusitoze riba wala faida yoyote tunapokopesha. Mungu amesema kwenye Zaburi 15:5, kwa hiyo ni kila mtu binafsi yake atasimama kwenye kutaniko la Bwana. Inasema: “Yeye ambaye hautii mkono wake katika kutafuta faida kwa riba, na wala hachukui zawadi dhidi ya asiye na hatia. Yeye afanyaye hivyo hataondolewa kamwe.”

 

  7 Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe, nduguzo mmojawapo, ndani ya malango yako mojawapo, katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini; 8 lakini mfumbulie mkono wako kwa kweli, umkopeshe kwa kweli yatoshayo haja yake katika ahitajiayo. 9 Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia Bwana juu yako, ikawa ni dhambi kwako.

 

Iwapo kama tutawaona watu wakiwa kwenye uhitaji tumeamriwa kuwakopesha. “Ikiwa kama mwaka wa Sabato umekaribia tumeonywa kwamba tusiifanye migumu mioyo yetu kwa kutowakopesha ndugu zetu walio kwenye imani moja nasi. 

10 Mpe kwa kweli, wala moyo wako usisikitike utakapompa; kwa kuwa atakubarikia Bwana, Mungu wako, kwa neno hili katika kazi yako yote, na katika kila utakalotia mkono wako. 11 Kwa maana maskini hawatakoma katika nchi milele; ndipo ninakuamuru na kukuambia, Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, maskini wako, katika nchi yako. 12 Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.

 

Watu wa mataifa na Wayahudi wote wanamiliki na kufanya shughuli za kibenki na wanaenda kinyume na sheria au amri hii ya Mungu na kuitumia vibaya na kinyume amri hii inayohusu jinsi ya kuwafanyia wajirani na Waebrania (aya ya1-11) na hii ni kinyume na utumwa (aya ya 12). Mmonaki au mtawa wa Kiingereza alianzisha mfumo huu kwa nia ya kuweka ili kusaidia vita. Lakini utaratibu huu inaenda kinyume kabisa na sheria za Mungu na utakomeshwa hatimaye kipindi cha Yubile atakayoianzisha Masihi katika kipindi cha utawala wake (Cox, “P”, op. cit., ukurasa wa 14).

13 Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu; 14 umwangalie kwa wema katika kundi lako, na sakafu yako ya nafaka, na kinu chako cha divai; mpe kama alivyokubarikia Bwana, Mungu wako. 15 Nawe kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, akakukomboa Bwana, Mungu wako; kwa hiyo mimi nakuamuru neno hili hivi leo. 16 Hata itakuwa, akikuambia, Siondoki kwako; kwa sababu akupenda wewe na nyumba yako, kwa kuwa yu hali njema kwako; 17 ndipo utwae uma, uupenyeze katika sikio lake uingie katika ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako milele. Na kijakazi chako naye mfanye vivyo.

 

kwa hiyo, tunaweza kuwakopesha watu lakini sio kuwawekea riba. Ni vibaya sana kuwasababishia watu wafilisike na kuwatoza riba watu binafsi au hata mataifa au kufanya aina zozote za kujipatia faida kubwa kutoka kwao. Kwa hiyo tendo la kuyafutia madeni mataifa yanayoendelea ni jema na la muhimu kwa kila mtu au taifa linalodai wanaiamini Biblia.

 

Kila taifa linawajibika kujitawla na kujihudumia lenyewe kwa mujibu wa sheria za Mungu na yanapaswa kujimudu kifedha yenyewe. Iwapo kama yatashindwa kujimudu yenyewe, ndipo wanapojikuta yakiishi kaisha yasiyopaswa kuwa hivyo kwao au maisha ya kitumwa.

 

Pia kuna masharti waliyopewa ndugu zetu kutoka mataifa yote ambayo ni agizo la kujisaidia wenyewe na sio kudumu wakiwoomba fedha ndugu zao wengine walio mahala pengine kwa kufanya hivyo kila mara na pasipo kukoma. Hatutaweza kuwafanya watumwa watu wetu kwa kuwatoza riba kwa ajili ya kuwapa wenzetu kwa mtindo wa kuwafanya wenzetu kuwa watumwa. Kila mmoja wetu atahukumiwa kwa jinsi anavyowafanyia wenzake wengine, kwa namna zote mbili yaani kama taifa na kama mtu binafsi.

 

Jinsi ulimwengu ulivyo kwa siku hizi kwa mfumo wake shirikishi ambao ni kama hauko sawa. Utaanguka na kukoma kwa uzito wake wenyewe na mfumo wake mbaya uluojiwekea. Mungu ataruhusu uanguke na ataurejesha upya. Ataurudisha upya kwa kuweka amri na sheria zake katika kipindi cha mwisho wa mateso na misukosuko.

 

Pasipo kutoza riba na kwa mujibu wa Torati ya Mungu tunaweza kupata utajiri na kuishi maisha ya kheri kabisa. Tunapoishi kinyume na utaratibu ndipo tunajifanyia maovu na dhambi. Sheria ya Mungu na taratibu zake hufanya kazi kwa namna inayoonekana kama ya kiamri na sio ya haki huria.”

http://www.ccg.org/_domain/ccg.org/Sabbath/2005/S_07_09_05.htm

 

Kutokana na Maandiko Matakatifu hapo chini tunaona kwamba kitendo cha kukopesha fedha kwa nia ya kutoza riba kumekatazwa kwenye maandiko haya ya Agano la Kale. Riba hii isichukuliwe kwa namna yoyote ile ya utoaji wa fedha, kimsaada au mali ya mtu. “Riba ni kiasi cha fedha kinacholipwa pamoja na fedha iliyokopeshwa (ni kikanuni), au hutolewa kama kiasi kilichozidi kutokana na deni lililotolewa” (kwa mujibu wa Kamusi maarufu ya Macquarie ABC Dictionary).

Kutoka 22:25  "Ukimkopesha mtu aliye maskini, katika watu wangu walio pamoja nawe; usiwe kwake mfano wa mwenye kumdai; wala hutamwandikia faida.

 

Mambo ya Walawi 35:36-37 Usitake riba kwake wala faida, bali mche Mungu wako, ili ndugu yako akae nawe. 37 Usimpe fedha yako upate riba, wala usimpe vyakula vyako kwa kujitakia faida. .

 

Kumbukumbu la Torati 23:19 "Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;

 

Riba au faida ya ziada huitwa tokos (kwa mujibu wa SGD 5110) na imetumika mara mbili kwenye maandiko ya Agano la Kale, kitabu cha Mathayo 25:27 na Luka 19:23, kwenye mfano wa talanta.

Mathayo 25:27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo angu na faida yake.

Ieleweke kuwa, Kristo hakuwa anabariki tendo hili la kudai faida ya ziada au riba kwenye Maandiko haya Matakatifu. Maana aliyoikusudia Kristo kwa kutoa mfano huu ilikuwa ni kusisitizia juu ya Ufalme wa Mungu na hakumaanisha masuala ya fedha.

 

Tendo la kukopesha fedha ili upate kitu cha nyongeza ni riba pia na wizi na Mungu amekataza matendo haya na ametangaza hukumu kwa wanaofanya hivyo. Katika kipindi cha utawa;a wa Masihi, kila mtu anayekopesha fedha kwa kufanya mambo haya ya riba atatiwa hukumuni na atafanywa alipe tena kama atakavyoamriwa atakapohukumiwa kwa hukumu itakayochukuliwa kama wizi na utapeli kulingana na Sheria. Pia soma jarida la Torati na Amri ya Nane (Na. 261) [Law and the Eighth Commandment (No. 261)].

 

Yubile

Wakati Adamu na Hawa walipotenda dhambi, sio tu kuwa walitolewa tu kutoka Bustani ya Edeni, bali Mungu pia aliilaani ardhi ambayo waliishi ndani yake na kula kutokana kwayo (Wanzo 3:17-18). Hata hivyo, ili kumlinda mwanadamu na sayari hadi atakapokuja na kuirejeza upya Masihi yote kwa Mungu mwishoni mwa miaka 7000, mfumo wa Yubile unaendelea kufanya kazi kwa faida ya sayari hii yote tunapokuwa tunazifuata na kuzitii Amri za Mungu.

 

“Mfumo wote wa Kalenda unatuama kwenye Yubile. Yubile moja ni mzunguko wa kipindi cha miaka hamsini, am,bacho kinaonekana kwenye ujenzi wa Hekalu na Kanisa lililo kwenye utaratibu wa Biblia. Inafanywa kwa mizunguko sana ambayo kila mmoja una miaka saba. Yubile huashiria mwelekeo wa maisha ya mwanadamu na ukuaji wake wa miaka hamsini.

 

Mwaka wa Yubile huesabiwa kutoka Siku ya Upatanisho ya mwaka wa Arobaini na tisa au Yubile, wakati ardhi yote inarejeshwa kwa makabila ya wamiliki wake asilia. Thamani yote ya ardhi huamuliwa kwa mtindo huu wa ulingano (Mambo ya Walawi 25:15). Mwaka huu huadhimishwa na Yubile hupigiwa mbiu kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka wa Arobaini na tisa (Mambo ya Walawi 25:8-9), na kisha kuadhimishwa mtakatifu kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka wa Hamsini (Mambo ya Walawi 25:9-13), ili kwamba ardhi ianze kulimwa tena na kupandwa kwa mavuno ya majira ya baridi ya mwezi wa Abibu wa mwaka wa Kwanza wa Yubile inayofuatia. Mwaka huu (wa 50) ni wa nane kwa kufuata utaratibu wa mzunguko wa miaka ya kawaida (Mambo ya Walawi 25:22) (Cox, W.E., “P”, op. cit., kurasa za 27, 28).

 

Kwa mujibu wa kitabu cha fasiri cha (SHD 6944, kodesh) neno takatifu lina maana moja na linapaswa tendo la kula kile ambacho kimekatazwa au kitu haramu kutoka kwenye maongeo ya mavuno ya tatu ya mwaka uliopita wa Sabato na maongeo yaliyohifadhiwa ya mavuno.

 

“Mtazamo huohuo wa kujitoa na kujiandaa kwa ajili ya kuutunza utaratibu wa Sabato umeenea hadi kwenye kipindi chote kizima cha Yubile na kinaendelea hadi hata kwenye mavuno makuu ya mwaka unaotangulia kabla ya Sabato ya saba ya Yubile. Katika mwaka ule, Mungu kuwabarikia watu wake mavuno maradufu yatakayoweza kutosheleza kwa kipindi cha Miaka Miwili mitakatifu inayofuatia mbele yake.”

 

Kwa maneno mengine, mavuno makuu mara tatu yanavunwa katika mwaka wa Arobaini na nane wa Yubile katika mwaka wa sita wa mzunguko wa mwisho ili kwamba miaka mingine miwili ya Sabato na Yubile iweze kutumika pasipo kupungukiwa au kuwa ba uhitaji.

 

“Mchakato huu hutokea kwenye kila mwaka wa saba wa mzunguko huu kwenye mwaka wa sita na ndipo mavuno maradufu hutokea, lakini kwenye mwaka wa kabla ya maadhimisho ya Yubile tunajionea mavuno makuu mara tatu kulingana na kawaida yake kama ilivyoahidiwa. Kwenye mwaka wa Yubile, ambao hapa unaitwa na kujulikana kama mwaka wa nane katika mzunguko, inaruhusiwa kupanda mbegu mashambani baada tu ya kupita Siku ya Upatanisho tangu Pasaka ya mwaka wa tisa.

 

Mungu kuachilia baraka za kimwili kwa Israeli wanapozitii amri zake. Ndivyo anavyowabarikia pia Israeli wote wa kiroho wanaotembea kwenye njia zake kwa maarifa makuu na kuelewa na kwa uweza wake katika Roho Mtakatofu” (Cox, “B”, op. cit., ukurasa wa 6).

 

Kila mmoja wetu ni mali ya Mungu (soma Mambo ya Walawi 11:2, 11, 21).

Kutoka 19:5 ' Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu,

 

Walawi hawakupewa ardhi ya kuimiliki katika Israeli. Ila kulikuwa na miji na maeneo ya malisho ya wanyama iliyotengwa rasmi kwa kutumiwa na Walawi, pamoja na zaka zote na baadhi ya sadaka au dhabihu zilizotolewa walipewa wao.

Kumbukumbu la Torati 18:1-8 inasema: "Makuhani Walawi, kabila yote ya Lawi, wasiwe na fungu wala urithi pamoja na Israeli; watakula sadaka za Bwana zifanywazo kwa moto, na urithi wake. 2 Wala wasiwe na urithi kati ya ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaambia. 3 Na hii itakuwa haki ya makuhani kwa watu hao wasongezao sadaka, ikiwa ni ng'ombe au kondoo wampe kuhani mkono, na mashavu mawili, na tumbo. 4 Malimbuko ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na manyoya ya kwanza ya kondoo zako, umpe. 5 Kwani Bwana, Mungu wako, amemchagua katika kabila zako zote, asimame atumike kwa jina la Bwana, yeye na wanawe milele. 6 Na akija Mlawi atokaye katika malango yako mojawapo, katika Israeli yote alipokuwa akikaa, akaja kwa mapenzi yote ya nafsi yake mahali atakapochagua Bwana; 7 na atumike kwa jina la Bwana, Mungu wake, kama wafanyavyo ndugu zake wote, Walawi wasimamao huko mbele za Bwana. 8 Wawe na fungu sawasawa la kula, pamoja na haya yaliyomfikilia kwa kuuzwa urithi wa baba zake.

 

Binti za Selofehadi, aliyekufa bila kuacha mtoto wa kiume, walifikiriwa kupewa milki yao na jina la baba yao kwenye ukoo wake.

Hesabu 27:1-11 inasema: Wakati huo wakakaribia hao binti za Selofehadi, mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa jamaa za Manase mwana wa Yusufu; na majina ya hao binti za Selofehadi ni haya; Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa. 2 Nao wakasimama mbele ya Musa, na mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya wakuu, na mkutano wote, mlangoni pa hema ya kukutania, wakasema, 3 Babaetu alikufa nyikani, naye hakuwamo katika mkutano wa hao waliojikutanisha kinyume cha Bwana katika mkutano wa Kora; lakini akafa katika dhambi zake mwenyewe; naye alikuwa hana wana wa kiume. 4 Kwa nini basi jina la babaetu kufutwa katika jamaa zake kwa sababu alikuwa hana mwana wa kiume? Tupe sisi urithi pamoja na ndugu zake babaetu. 5 Basi Musa akaleta neno lao mbele ya Bwana 6 Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 7 Hao binti za Selofehadi wananena lililo haki; kweli utawapa milki ya urithi pamoja na ndugu za baba yao; nawe utawapa urithi wa baba yao. 8 Kisha utanena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Mtu akifa, naye hana mwana wa kiume, ndipo utampa binti yake urithi wake. 9 Tena ikiwa hana binti, mtawapa nduguze urithi wake. 10 Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za babaye huo urithi wake. 11 Tena ikiwa babaye hana ndugu, utampa huyo aliye karibu naye katika jamaa zake huo urithi wake, naye atakuwa nao; na neno hili litakuwa ni amri ya hukumu kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Musa.

Kama tuonavyo hapo juu, kutokana na jinsi Musa alivyomuuliza Bwana hukusu milki ya nchi ulipaswa kubakia kwenye ukoo wa baba yake hadi kuwafikia mabinti zake. Waume zao waliokuja baadae waliwachukua majina ya kike ya jamaa yao. Milki yao hii inategemea kwenye mlolongo wa uzao wa jamii yao.

 

Mungu amemchukulia Israeli kama mtoto wazaliwa wake wa kwanza (Kutoka 4:22). Kwa hiyo, wazaliwa wote wa kwanza katika Israeli ni wake.

Kutoka 13:2 "Nitakasie mimi wazaliwa wa kwanza wote, kila afunguaye tumbo katika wana wa Israeli, wa binadamu na wa mnyama; ni wangu huyo"

 

Wazaliwa wa kwanza walibidi kukombolewa. Wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa kufugwa pia walikombolewa kwa dhabihu ya mwana kondoo. Wanadamu walitakaswa kwa Bwana kwa uhai wao wenyewe, na sio kwa kuuawa (soma mfano wake kwenye kitabu cha Kutoka 13:13, hasa kwenye tafsiri ya The NIV Study Bible, ukurasa wa 105).

Kutoka 13:13-22 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo; na kwamba hutaki kumkomboa, utamvunja shingo; na kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu katika wanao utamkomboa. 14 Kisha itakuwa hapo mwanao atakapokuuliza keshoni, akisema, Ni nini hivi? Utamwambia, Bwana alimtoa Misri, kutoka ile nyumba ya utumwa, kwa uwezo wa mkono wake; 15 basi ilikuwa hapo Farao alipojifanya kuwa mgumu ili asitupe ruhusa kuondoka, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote waliokuwa katika nchi ya Misri, wa binadamu na wa mnyama; kwa ajili ya hayo namtolea Bwana wote wafunguao tumbo, wakiwa waume; lakini wazaliwa wa kwanza wote wa wana wangu nawakomboa. 16 Jambo hilo litakuwa ni ishara mkononi mwako, na utepe katikati ya macho yako; kwa kuwa Bwana alitutoa Misri kwa uwezo wa mkono wake. 17 Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri; 18 lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa silaha. 19 Musa akaichukua ile mifupa ya Yusufu pamoja naye; maana, alikuwa amewaapisha sana wana wa Israeli, akisema, Mungu hana budi atawajilia ninyi; nanyi mtaichukua mfupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi. 20 Nao wakasafiri kutoka Sukothi, wakapiga kambi Ethamu, kwenye mpaka wa ile jangwa. 21 Bwana naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia; na usiku, ndani ya moto mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru; wapate kusafiri mchana na usiku; 22 ile nguzo ya wingu haikuondoka mchana, wala ile nguzo ya moto haikuondoka usiku, mbele ya hao watu.

 

Mwana mzaliwa wa kwanza wa kiume au mkubwa kuliko wote alipewa urithi mara dufu ya mali zote zinazorithishwa.

Kumbukumbu la Torati 21:17 lakini amkubali mzaliwa wa kwanza mwana wa yule asiyempenda, kwa kumpa mafungu mawili katika vyote alivyo navyo; kwa maana ndiye mwanzo wa nguvu zake; haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.

 

Nabii Ezekieli anaonyesha urithi milki wa ardhi. Urithi wa familia umelindwa kwa utaratibu huu wa Yubile na hakuna atakayeweza kunyang’anywa au kudhulumiwa mali zake.

Ezekieli 46:16-18 "Bwana MUNGU asema hivi; Mkuu akimpa mwanawe awaye yote zawadi, ni urithi wake, itakuwa mali ya wanawe; ni milki yao kwa kurithiwa. 17 Bali akimpa mmoja wa watumishi wake baadhi ya urithi wake, itakuwa mali yake mpaka mwaka wa kuacha huru; ndipo itakapomrudia mkuu; lakini urithi wake, huo utakuwa wa wanawe. 18 Tena mkuu hatawaondolea watu urithi wao, hata kuwatoa kwa nguvu katika milki yao; atawapa wanawe urithi katika mali yake mwenyewe, watu wangu wasije wakatawanyika, kila mtu mbali na milki yake”

 

Tunakumbushwa kuwa kuna adhabu kubwa imewekwa kwa kuivunja na kupuuzia kuiadhimisha Yubile.

Yeremia 34:17 Basi Bwana asema hivi, Hamkunisikiliza kumtangazia uhuru kila mtu ndugu yake, na kila mtu jirani yake; tazama, mimi nawatangazieni uhuru, asema Bwana, yaani, wa upanga, na njaa, na tauni; nami nitawatoa ninyi mtupwe huko na huko katika falme zote za dunia.

 

Kama tunavyojionea hapo juu utaratibu wa umiliki unaotuama kwenye Yubile unalinda vizazi vyetu kwenye safu ya uzao wetu. Hata hivyo, kaswali mapya yanajitokeza kutoka kwenye hesabu ya binti za (walioitwa ili wamiliki ardhi ya baba yao, kama tunavyoona kwenye kitabu cha Hesabu 27:1-11), kama ni kitu gani kingepaswa kutokea kwenye ardhi ya jamii yao kama wangeolewa na watu wa makabila mengine.

Hesabu 36:1-4 Kisha wale wakuu wa nyumba za mababa ya jamaa ya wana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, katika jamaa za wana wa Yusufu, wakakaribia, na kunena mbele ya Musa, na mbele ya wakuu walio juu ya nyumba za mababa ya wana wa Israeli; 2 wakasema, Bwana alimwagiza bwana wangu awape wana wa Israeli nchi kwa kupiga kura iwe urithi wao; tena bwana wangu aliagizwa na Bwana awape binti za Selofehadi ndugu yetu huo urithi wa baba yao. 3 Wakiolewa na watu wa wana wa hizo kabila nyingine za wana wa Israeli, ndipo urithi wao utatwaliwa na kuondolewa katika urithi wa baba zetu, na hiyo kabila watakayotiwa ndani yake itaongezewa urithi wao; basi urithi huo utaondolewa katika kura ya urithi wetu. 4 Tena itakapokuwapo hiyo yubile ya wana wa Israeli, ndipo urithi wa hiyo kabila ambayo wamekuwa ndani yake utaongezewa huo urithi wao; hivyo urithi wao utaondolewa katika urithi wa kabila ya baba zetu."

 

Uamuzi ulikuwa ni kwamba kila binti aliyepata irithi kutoka kwenye kabila la baba yake alipaswa kuolewa na mtu kutoka kwenye kabila lake hilohilo ili kwamba familia na kabila viweze kulindwa. 

Hesabu 36:5-9 Basi Musa akawaagiza wana wa Israeli kama neno la Bwana lilivyokuwa, akasema, Kabila ya wana wa Yusufu imenena yaliyo haki. 6 Bwana ameagiza neno hili katika habari ya binti za Selofehadi, akasema, Na waolewe na waume wawapendao; lakini na waolewe katika jamaa ya kabila ya baba zao. 7 Hivyo hapana urithi wo wote wa wana wa Israeli utakaotoka kabila hii kwenda kabila hii; kwa kuwa wana wa Israeli watashikamana kila mtu na urithi wa kabila ya baba zake. 8 Na kila binti atakayemiliki urithi katika kabila yo yote katika wana wa Israeli, ataolewa katika jamaa moja ya kabila ya baba yake, ili wana wa Israeli wapate kumiliki kila mtu urithi wa baba zake. 9 Hivyo hapatakuwa na urithi uwao wote utakaotoka kabila hii kwenda kabila hii; kwa kuwa kabila za wana wa Israeli zitashikamana kila mmoja na urithi wake mwenyewe.'"

 

Binti hawa wa Selofeadi walikubali na kutii kama Bwana alivyowaamuru, na milki zao aikabakia kwenye jamaa ya baba zao.

Hesabu 36:10-12 Basi hao binti za Selofehadi wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Musa; 11 kwa kuwa Mala, na Tirsa, na Hogla, na Milka, na Noa, binti za Selofehadi waliolewa na waume, wana wa ndugu za baba yao. 12 Waliolewa katika jamaa za wana wa Manase, mwana wa Yusufu, na urithi wao ukakaa katika kabila ya jamaa ya baba yao.

 

Mungu aliahidi kwamba mtu fulani kwenye ukoo wa jamaa zao wa Rekabu hadi wa Yonahabu ndio watasimama kila mara mbele zake.

Yeremia 35:16-18 Basi, kwa kuwa wana wa Yonadabu, mwana wa Rekabu, wameitimiza amri ya baba yao aliyowaamuru, lakini watu hawa hawakunisikiliza mimi; 17 kwa sababu hiyo, asema Bwana, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli; Tazama nitaleta juu ya Yuda, na juu ya wenyeji wote wa Yerusalemu, mabaya yote niliyoyatamka juu yao; kwa sababu nimesema nao, wasinisikilize; nimewaita, wala hawakuniitikia. 18 Naye Yeremia akawaambia watu wa nyumba ya Warekabi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa sababu mmeitii amri ya Yonadabu, baba yenu, na kuyashika maagizo yake yote, na kutenda sawasawa na yote aliyowaamuru; basi, kwa sababu hiyo, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Yonadabu, mwana wa Rekabu, hatakosa kuwa na mtu wa kusimama mbele zangu hata milele"

Ukoo wa familia hii utabakia kwa kuwa walifuata amri ya baba yao. Watoto wetu watapokea faida ya muda mrefu kutokana na jinsi tunavyozitii amri za Baba yetu wa Mbinguni, na hakuna hata moja ya amri zake zitakazoweza kukomeshwa au kutanguliwa.

Mathayo 5:18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. 

 

Mpango wote mzima haujakamilika bado na amri hii itabakia imekamilika. Sadaka au dhabihu iliyokubalika ya Masihi haikutangua torati bali imefungua awamu nyingine ya Mpango huu na kuwaruhusu Mataifa wasio Wayahudi kupata fursa ya kuingia kwenye mpango wa Roho mtakatifu wa kufanywa wana na kufanywa kuuwa ni Israeli wa kiroho.

 

Wana wa Rekabu waliotii amri za baba yao walifanywa kuwa mfano wa watu wa Yuda waliomuasi Mungu.

Yeremia 35:12-15 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema, 13 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Enenda ukawaambie wana wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, Je! Hamtaki kupokea mafundisho, myasikilize maneno yangu? Asema Bwana. 14 Maneno ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, aliyowaamuru wanawe, kwamba wasinywe divai, yametimizwa, na hata leo hawanywi; maana waitii hiyo amri ya baba yao; lakini mimi nimesema nanyi, nikiamka mapema na kunena, bali ninyi hamkunisikiliza mimi. 15 Pia naliwapeleka watumishi wangu wote, manabii, kwenu ninyi, nikiamka mapema na kuwapeleka, nikisema, Rudini sasa, kila mtu na aiache njia yake mbaya, mkatengeneze matendo yenu, wala msiwafuate miungu mingine, ili kuwatumikia, nanyi mtakaa katika nchi hii, niliyowapa ninyi na baba zenu; lakini hamkutega masikio yenu, wala hamkunisikiliza.

 

Jinsi ya Kuthaminisha Mali

Iwapo kama mtu ataiweka wakfu nyumba yake kwa Bwana, thamani yoyote ambayo kuhani ataiweka ndiyo itakayodumu na kubakia hivyo. Na inwapo kama mtu atapenda kuikomboa ndipo mtu huyo atalazimika kuongeza sehemu ya tano (20%) kutoka kwenye thamani iliyowekwa na nyuma hiyo itabakia tena kuwa yake (Mambo ya Walawi 27:14-15).

Mambo ya Walawi 27:14-15 "Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa. 15 Tena mtu huyo aliyeweka nyumba yake iwe wakfu kama akitaka kuikomboa, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano ya hiyo fedha ya hesabu yako, nayo itakuwa mali yake

 

Nyumba zilizojengwa kwenye miji yenye maboma huwa ni milki ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Hazirudishwi kwa mwenyewe unapofika mwaka wa Yubile. Lakini nyumba zinazojengwa vijiji visivyozungushiwa na boma yanahusika na sheria inavyosema kuhusu mwaka wa Yubile. (mfano ni inavyoelekezwa kwenye Mambo ya Walawi 25:29-31 hapa chini).

 

Sheria na utaratibu wa YubileMaelekezo kamili ya jinsi ya kufanya ukifika mwaka wa Yubile yanakutikana kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi 25 hapa chini.

Mambo ya Walawi 25:9-55 inasema:  Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote. 10 Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote wanayokaa; itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake. 11 Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabibu za mizabibu isiyopelewa. 12 Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani. 13 Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake. 14 Tena kama ukimwuzia jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe; 15 kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe. 16 Kama hesabu ya miaka ilivyo ni nyingi ndivyo utakavyoongeza bei yake, na kama hesabu ya miaka ilivyo ni chache ndivyo utakavyopunguza bei yake; kwani yeye akuuzia mavuno kama hesabu yake ilivyo. 17 Wala msidanganyane; lakini utamcha Mungu wako; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 18 Kwa sababu hii zitendeni amri zangu, mkazishike hukumu zangu, na kuzifanya; nanyi mtakaa katika hiyo nchi salama. 19 Nayo nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba, na kuketi humo salama. 20 Na kama mkisema, Je! Mwaka wa saba tutakula nini? Angalieni hatutapanda mbegu, wala kukusanya maongeo yetu; 21 ndipo nitawaamria baraka yangu iwe juu yenu mwaka wa sita, nayo utazaa matunda hesabu ya miaka mitatu. 22 Na mwaka wa nane mtapanda mbegu, na kuyala yale matunda, akiba hiyo ya zamani, hata mwaka wa kenda, hata matunda yake yatakapoletwa ndani, mtakula hiyo akiba ya zamani. 23 Nayo nchi haitauzwa kabisa kabisa; kwani nchi ni yangu mimi; maana ninyi ni wageni na wasafiri wangu. 24 Nanyi mtatoa ukombozi kwa ajili ya nchi, katika nchi yote ya milki yenu. 25 Kwamba nduguyo amekuwa maskini, na kuuza sehemu ya milki yake, ndipo jamaa yake aliye karibu naye atakuja, naye ataikomboa ile aliyoiuza nduguye. 26 Na kama mtu hana atakayeikomboa, naye mwenyewe amepata mali na kujiona kuwa anayo ya kutosha kuikomboa; 27 ndipo na aihesabu hiyo miaka ya kuuzwa kwake, na kilichozidi kumrudishia huyo mtu aliyeinunua; naye atairejea milki yake. 28 Lakini asipoweza kujipatia mwenyewe, ndipo hiyo iliyouzwa itakaa mkononi mwake huyo aliyeinunua, hata mwaka wa yubile; na katika yubile itatoka, naye atairejea milki yake. 29 Tena kwamba mtu anauza nyumba ya kukaa, iliyo ndani ya mji wenye kuta, ndipo ana ruhusa kuikomboa katika mwaka mmoja mzima baada ya kuiuza; atakuwa na amri ya kuikomboa muda wa mwaka mzima. 30 Na kama haikukombolewa katika muda wa mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyo ndani ya mji wenye kuta itathibitishwa milele kuwa ya huyo aliyeinunua, katika vizazi vyake; nayo haitatoka katika yubile. 31 Lakini nyumba za vijiji, ambavyo havikuzingirwa na kuta, zitahesabiwa pamoja na mashamba ya nchi; nazo zina ruhusa ya kukombolewa, nazo zitatoka katika yubile. 32 Pamoja na hayo, miji ya Walawi, nyumba za miji ya milki yao, Walawi wana ruhusa ya kuzikomboa majira yo yote. 33 Tena kama mtu mmoja wa hao Walawi akikomboa, ndipo nyumba iliyouzwa, na mji wa milki yake, itatoka katika yubile; maana, hizo nyumba za miji ya Walawi ni milki yao kati ya wana wa Israeli. 34 Lakini konde la malisho ya miji yao lisiuzwe kwa kuwa ni milki yao ya daima. 35 Na ikiwa ndugu yako amekuwa maskini, na mkono wake umelegea kwako, ndipo utamsaidia, atakaa nawe kama mgeni, na msafiri. 36 Usitake riba kwake wala faida, bali mche Mungu wako, ili ndugu yako akae nawe. 37 Usimpe fedha yako upate riba, wala usimpe vyakula vyako kwa kujitakia faida. 38 Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, niliyewatoa katika nchi ya Misri ili niwape nchi ya Kanaani, nipate kuwa Mungu wenu. 39 Tena kwamba nduguyo amekuwa maskini pamoja nawe, akajiuza kwako; usimtumikishe mfano wa mtumwa; 40 kwako wewe atakuwa mfano wa mtumishi aliyeajiriwa, au mfano wa msafiri; naye atatumika kwako hata mwaka wa yubile; 41 ndipo atakapotoka kwako aende zake, yeye na wanawe pamoja naye, naye atairejea jamaa yake mwenyewe, tena atairejea milki ya baba zake. 42 Kwa kuwa hao ni watumishi wangu, niliowaleta watoke nchi ya Misri; wasiuzwe mfano wa watumwa. 43 Usitawale juu yake kwa nguvu; ila umche Mungu wako. 44 Tena katika habari za watumwa wako na wajakazi wako, utakaokuwa nao; mataifa walio kando-kando yenu, katika hao mtanunua watumwa na wajakazi. 45 Tena katika wana wa wageni wakaao kati yenu mtajinunulia, na katika jamaa zao walio pamoja nanyi, waliowazaa katika nchi yenu; wao watakuwa milki yenu. 46 Nanyi mtawafanya kuwa urithi kwa watoto wenu baada yenu, wawe milki yao; siku zote mtatwaa watumwa wenu katika hao; lakini msitawale kwa nguvu juu ya ndugu zenu, hao wana wa Israeli, wenyewe kwa wenyewe. 47 Tena kama mgeni au mtu akaaye nawe akitajirika, na nduguyo amekuwa maskini karibu naye, akajiuza kwa huyo mgeni, au kwa huyo akaaye kwako, au kwa ukoo wa jamaa ya huyo mgeni; 48 baada ya kuuzwa aweza kukombolewa; mtu mmoja miongoni mwa ndugu zake ana ruhusa kumkomboa; 49 au mjomba wake, au mwana wa mjomba wake, ana ruhusa ya kumkomboa, au mtu awaye yote aliye karibu naye wa jamaa yake, ana ruhusa ya kumkomboa; au kwamba yeye mwenyewe amepata mali, ana ruhusa ya kujikomboa mwenyewe. 50 Naye atafanya hesabu na huyo aliyemnunua, tangu mwaka huo aliojiuza hata mwaka wa yubile; na ile bei ya kuuzwa kwake itakuwa kama hesabu ya hiyo miaka ilivyo; atakuwa pamoja naye kama majira ya mtumishi aliyeajiriwa yalivyo. 51 Kwamba ikali imesalia miaka mingi, kama hesabu yake ilivyo ndivyo atakavyolipa bei ya ukombozi wake, katika hiyo fedha ambayo alinunuliwa kwayo. 52 Tena kwamba imesalia miaka michache tu hata mwaka wa yubile, ndipo atafanya hesabu naye, kama hesabu ya miaka yake ilivyo, ndivyo atakavyolipa tena bei ya ukombozi wake. 53 Kama mtumishi aliyeajiriwa mwaka hata mwaka, ndivyo atakavyokuwa pamoja naye; asitawale juu yake kwa nguvu mbele ya macho yako. 54 Tena kwamba hakukombolewa kwa njia hizi mojawapo, ndipo atatoka katika mwaka wa yubile, yeye, na watoto wake pamoja naye. 55 Kwa kuwa wana wa Israeli ni watumishi; ni watumishi wangu niliowaleta watoke katika nchi ya Misri; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

 

Uthibitisho kwenye Agano Jipya

Kuna sehemu mbili zenye maandiko yanayoielezea Yubile na ambayo yanaweza kuchukuliwa sawa na yale waliyoyaeleza kina Ezra na Nehemia tunapowaona nukuu za jinsi walivyoisoma Torati. Nukuu moja inatoka kwenye Agano la Kale na lingine ni utimilifu wa unabii ulitolewa kwenye Agano la Kale kwenye Agano Jipya unaomlenga Masihi.

 

Nukuu ya maandiko ya Agano la Kale iko kwenye Ezekieli 1:1-3.

Ezekieli 1:1-3 inasema: Ikawa katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa pamoja na watu waliohamishwa, karibu na mto Kebari, mbingu zilifunuka, nikaona maono ya Mungu. 2 Siku ya tano ya mwezi, nao ulikuwa ni mwaka wa tano wa kuhamishwa kwake mfalme Yehoyakini, 3 neno la Bwana lilimjia Ezekielii, kuhani, mwana wa Buzi, kwa dhahiri, katika nchi ya Wakaldayo, karibu na mto Kebari; na mkono wa Bwana ulikuwa hapo juu yake.

 

Kwa hiyo basi, tunapolingakisha na majenzi na marejesho mapya yaliyoonekana nyakati za nabii Ezekieli ya Yubile yalikuwa ni yale yaliyoangukia mwaka wa 574/3 na pia yale ya mwaka 524/3, na tena mwaka 74/3 na 24/3 kwenye karne za nyakati za Kabla ya Kuzaliwa Kristo (BCE), na 27/28 na 77/78 kwenya kipindi cha nyakti hizi. Mtazamo huu unapata mashiko kwa kusaidiwa na ukweli mwingine mkuu wa unabii unaomhusisha Masihi.

 

Baada ya kutangulia miaka kumi na tano ya kufawala kwake Mfalme Tiberio, ambao haukuwa mapema sana na mwaka wa kidunia na tarehe ya Oktoba, 27 BK, Yohana Mbatizaji alianza kuhubiri na kuwabatiza watu ubatizowa toba (Luka 3:1-22). Ndipo Roho Mtakatifu alimwita Yesu kutoka Nazareti ili akabatizwe na Yohana kipindi fulani na kitambo baada ya Yohana kuanza huduma yake, au kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa tangu mwezi Oktoba ya mwaka wa 27 BK. Mara tu baada ya Kristo kubatizwa ndipo aliongozwa na Roho kwenda nyikani ambako alijaribiwa na Ibilisi kwa siku arobaini (Luka 4:1-2). Baada ya kurudi kwake maana na ilieleweka kidogo maana ya unabii kuhusu yeye kuwa unakamilika.

Luka 4:13-21 inasema: Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda. 14 Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando. 15 Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote. 16 Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome. 17 Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa, 18 Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, 19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. 20 Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21 Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.

 

Kisha, Masihi alirudi Galilaya kutoka kwenye majaribu yake, na kufika mjini Nazareti akiwa ametimiliza unabii alioutoa Mungu kupitia kwa nabii Isaya. Andiko hili linapatikana kwenye Isaya 61:1-2 na linapatikana tena kwenye Isaya 58:6.

Isaya 61:1-2 "Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. 2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;”

 

Kwa hiyo, tendo alilolifanya la ‘Kusoma maandiko kutoka gombo la nabii Isaya’ alililolifanya lilifanyika katika mwaka wa Yubile, ambalo lilienda sambamba na kipindi alichotabiri nabii Ezekieli, na fasiri ,aarufu ya Biblia inayoitwa Naves Topical Bible inayaelezea maandiko haya kuwa yamehusiana kabisa na tukio la Yubile (sawa na alivoandika kwenye kitabu chake cha Yubile, ukurasa wa 755). Huu pia ulikuwa Mwaka wa Maachilio wa watu kusamehewa na kuwa huru (sawa na Ezekieli 46:17). Kwa hiyo, ndio Kristo alipoitangaza Yubile ya mwaka 27 BK, mapema kabla haujaja mwaka mpya na siku ya 1 Nisan. Andiko hili kuhusu Masihi linabakia kuwa ni ushahidi usiopingika wa pili kutoka kwenye Ezekieli, na linathibitisha ufafanuzi wake wa majira yaliyoandikwa kwenye gombo la Nehemia linaloelezea yanayojiri kwenye mfumo na taratibu za Sabato na Yubile” (Cox, “R”, op. cit., ukurasa wa 3).

 

“Yubile hutokea kwenye miaka ya 24 na 74 KK na 27 na 77 BK ya kila karne. Yubile iliyofuatia ambayo ni Yubile ya arobaini tangu kuanza kwa huduma ya Masihi na Yubile ya arobaini na nane tangu kujengwa upya kwa Hekalu na majeresho mapya ya usomaji wa Torati yaliyofanywa na kina Ezra na Nehemia, yatafanyika mnamo Mwaka Mtakatifu wa 2027/8. Mwaka 2028 utakuwa ni mwanzo wa kipindi cha Yubile ya Yubile na cha Milenia mpya ya utawala wa Masihi na ambao utakuwa pia ni mwaka wa kwanza wa miaka mingine hamsihi, yaani 1/50” (Cox, “I”, op. cit., ukurasa wa 28).

 

Yubile ya Dhahabu

“Tangu Siku ya Upatanisho ya mwaka wa 2027 dunia itakuwa imeishaingia kwenye kipindi chake cha milki ya Milenia ya nchi yote. Tendo hili litatanguliwa na maadhimisho ya Yubile ya Dhahabu, au huitwa pia Yubile ya Yubile.

 

Ifikapo siku ya Kumi ya mwezi wa Saba ya mwaka wa 49 ya Yubile ya 120, au Jumapili ya tarehe 20 Septemba 2026, kuanzia jua linapozama na kupisha giza ya siku iliyotangulia, ndipo mwaka wa Yubile utaanza. Kwa kipindi cha mwaka huu, mataifa yatapangwa upya na kuwekwa sawa na milki zao stahiki. Kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka wa Hamsini wa Yubile ya 120, mbiu ya Yubile itapigwa, na ifikapo siku ya 23 ya mwaka wa Saba, inayofuatia mara tu baada ya Siku Kuu ya Mkutano wa Makini mwishoni mwa Sikukuu ya Vibanda, ndipo marejesho ya ardhi kwa wamiliki wake asili yatafanyika. Watu wote watarejeshewa ardhi au mashamba yao.

 

Ndipo wataanza kulima na kupanda kwa mavuno ya kwanza kuvunwa kipindi hiki cha Milenia kwenye Pasaka ya mwaka 2028. Mavuno makuu yatakayovunwa kwenye Ukanda-dunia wa pande za Kusini (Southern Hemisphere) itakuwa imefanyizwa upya na kufuata majira yake na mavuno yake. Ukanda-dunia wa Pande za Kaskazini (Northern Hemisphere) utakuwa umeharibiwa vibaya sana kwa ajili ya vita vilivyopiganwa. Itabidi Dunia ifanywe upya tangu mwaka 2028 hadi 2077. Kipindi hiki kitashuhudiwa kikipitwa na mabadiliko makubwa yatakayobadili mitazamo yote na mwenendo wa ongezeko la watu duniani” (Cox. W.E., “S” jarida la Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300) [The Golden Jubilee and the Millennium (No. 300)], CCG, 2006, kurasa za 4-5).

 

Utendaji sahihi wa mwaka huu wa mfumo huu wa kibiblia wa aina zote mbili, yaani wa kutoa zaka na sheria unategemea na kwendana na Yubile. Mfumo huu unaoenda pamoja na usomaji kiusahihi na makini wa Torati. Kwa hiyo, tuna agizo endelevu na lisilokoma la kuiheshimu na kuyashika maagizo ya Torati, amri ambayo haitakoma wala kutanguka, wala kubadilika (Mathayo 5:18; Luka 16:17). Torati hii ya Mungu inatangulia kutoka kwenye asili na hali asilia ya Mungu na itadumu kuwa hivyo milele, kama Mungu alivyo na sifa ya tabia ya kutobadilika.

1Yohna 5:3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

Pia soma jarida la Uhusiano kati ya Dhana ya Wokovu kwa Neema na Torati (Na. 82) [The Relationship between Salvation by Grace and the Law (No. 82)].

 

Baraka na Laana

Kuba baraka na laana zinazoweza kuwapata Israeli wote kwa jinsi watakavyoamua kati ya kuzitunza ama kuacha kuzitunza amri hizi za Mungu. Imeandikwa hivyo kwenye Kumbukumbu la Torati 28:1-68, tendo la kuzishika amri hizi ni jambo lililowazi sana kwamba linaonyesha jinsi mtu anastahili kusaidiwa au kukataliwa na Mungu. Hata hivyo, kuziasi amri za Mungu hupekelea adhabu kwa wote wawili, yaani kwa mtu binafsi na kwa taifa na kwa wote.

 

Laana itamuandama mtu anayeasi maagizo yaliyoandikwa kwenye Torati hii ya Mungu. Mungu huyafanyia mataifa ka hali sawa na jinsi anavyozifanyia familia. Mataifa yahoo pia huadhibiwa, yakifanika kuwa ni Wenyeji wanaowatumikisha au kuwafanyia watu kwa namna isiyo sawa. Amri hizi zote na sheria zake zinapaswa kuheshimiwa. Adhabu ya kutofanya hivyo ni jambo endelevu lisilo na mwisho kwa wale wote wanaoziasi, jambo linaloonekana kwenye maongeo ya ardhi. Taifa lnafanyiwa sawa kama wanavyofanyiwa watu. Watu watakumbwa na baa la njaa. Mambo yanavyokuwa hapa duniani yanauhusiano mkubwa na sheria na amri za Mungu.

 

Baraka na laana ni ishara na dalili za jinsi Israeli walivyo na zitabakia kuwa hivyo milele. Tunavyosema Israeli tunawajumuisha pia wale watu wa kiroho; kwa hiyo baraka na laana zitabakia zikiwa hivyo milele kwa wale wanaoliitia jina la Yesu Kristo na kuingia hukumuni. Kwa hiyo, kuna ahadi waliyopewa Israeli  kwenye mambo yao yote somo hili hutolewa ili kutufanya tujionee hatari yote itokanayo na kukosa kwetu na tunavyoshindwa kuwafanyia vizuri watu wetu . soma jarida la Baraka na Laana (Na. 75) [The Blessings and the Curses (No. 75)].

 

Kwenye Siku Zijazo

“Sabato zitakuwa zinaadhimishwa na wote wenye mwili wakati watakapokuwa wanajihudhurisha kwenye ibada mbele za Bwana, kwa Mwandamo mmoja wa mwezi hadi mwingine na toka Sabato moja hadi ile nyingine (Isaya 66:23)” (Cox, “A”, op. cit., ukurasa wa 5).

Isaya 66:18-23 inasema: "Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu. 19 Nami nitaweka ishara kati yao, nami nitawatuma hao waliookoka kwa mataifa, Tarshishi, na Puli, na Ludi, wavutao upinde, kwa Tubali na Yavani, visiwa vilivyo mbali; watu wasioisikia habari yangu, wala kuuona utukufu wangu; nao watahubiri utukufu wangu katika mataifa. 20 Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema Bwana; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka yao nyumbani kwa Bwana katika chombo safi. 21 Na baadhi ya hao nitawatwaa kuwa makuhani na Walawi, asema Bwana. 22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.

 

“Marejesho haya mapya ya Sabato na Miandamo ya Mwezi yataendana na marejesho mapya ya maadhimisho ya Sikukuu hizi zilizoamriwa na Mungu.

Zekaria 14:16-19 Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda. 17 Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, mvua haitanyesha kwao. 18 Na kama jamaa ya Misri hawakwei, wala hawaji, pia haitanyesha kwao; itakuwako tauni, ambayo Bwana atawapiga mataifa, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 19 Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa yote, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda.  

 

“Kwa hiyo, kutakuwa na marejesho mapya yaliyo kamili hadi pale maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi yatakayofanywa panoja na maadhimisho ya Sikukuu. Kwenye jumuia hii ya kisasa, jambo hili huonekana kuwa ni gumu sana. Na ndiyo maana Masihi ataushusha chini utaratibu wote huu wa kidunia wakati atakapokuja. Mataifa yatafanywa upya kwa sheria za Torati zitakazoamriwa kutoka mjini Yerusalemu” (Cox, “F”, op. cit., ukurasa wa 9). .

 

************

Bibliography/Tulikotohoa:

Christian Churches of God, Statement of Beliefs of the Christian Faith (No. A1), CCG, 1994-1997

Cox, W.E., “A”, The Sabbath (No. 31), CCG, 1994-2008

Cox, W.E., “B”, The Juna’ah: Preparing for the Sabbath (No. 285), CCG, 1999-2008

Cox, W.E., “C”, The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170), CCG, 1996-2000

Cox, W.E., “D”, The Covenant of God (No. 152), CCG, 1996-1999

McElwain, T., et.al., “E”, Blue Ribbons (No. 273), CCG, 1998

Cox, W.E., “F”, The New Moons (No. 125), CCG. 1995-2007

Cox, W.E., “G”, The New Moons of Israel (No. 132), CCG, 1995-2008

Cox, W.E., “H”, The Harvests of God, the New Moon Sacrifices, and the 144,000 (No. 120), CCG, 1995-2007

Cox, W.E., I”, God’s Calendar (No. 156), CCG, 1996-2008

Cox, W.E., “J”, The Lord’s Supper (No. 103), CCG, 1995-2008

Cox, W.E., “K”, The Passover (No. 98), CCG, 1995-2008

Cox, W.E., “L”, The Wave Sheaf Offering (No. 106b)

Cox, W.E, “M”, Keeping the Feasts (No. 56), CCG, 1994-2007

Cox, W.E., “N”, The Holy Days of God (No. 97), CCG, 1995-2007

Cox, W.E., “O”, Offering (No. 275), CCG, 2006

Cox, W.E., “P”, Tithing (No. 161), CCG, 1996-2007

Cox, W.E., “Q”, Reading the Law with Ezra and Nehemiah (No. 250)

Cox, W.E., “R”, The Meaning of Ezekiel’s Vision (No. 108)

Cox, W.E.,”S”, The Golden Jubilee and the Millennium (No. 300), CCG, 1996-2008

Cox, S., The Shofar and the Silver Trumpets (No. 47), CCG, 2003

Cox, W.E., Atonement (No. 138), CCG, 1994-2007

Cox, W.E., Eternal Life (No. 133), CCG, 1995, 2000

Cox, W.E., General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122), CCG, 1995-1999

Cox, W.E., God's Feasts as they relate to the Creation (No. 227), CCG, 1998, 2007 (based on a paper by A. Williams, 1997)

Cox, W.E., Ingathering (No. 139), CCG, 1994-1999, 2007

Cox, W.E., Law and the Eighth Commandment (No. 261), CCG, 1998, 1999

Cox, W.E., Outline Timetable of the Age (No. 272), CCG, 1998, 2002, 2006

Cox, W.E., Reading the Law with Ezra and Nehemiah (No. 250), CCG, 1998, 2007

Cox, W.E., Repentance and Baptism (No. 52), CCG, 1994, 1998, 2007

Cox, W.E., Sanctification of the Temple of God (No. 241), CCG, 1998, 2000, 2007

Cox, W.E., Significance of the Bread and Wine (No. 100), CCG, 1995-2007

Cox, W.E., The Blessings and the Curses (No. 75), CCG, 1994-2007

Cox, W.E., The First Great Commandment (No. 252), CCG, 1998, 1999

Cox, W.E., The God We Worship (No. 2), CCG, 1994,1998

Cox, W.E., The Food Laws (No. 15), CCG, 1994-2008

Cox, W.E., The Omer Count to Pentecost (No. 173), CCG, 1996-2009

Cox, W.E., The Relationship between Salvation by Grace and the Law (No. 82), CCG, 1994-2007

Cox, W.E., Trumpets (No. 136), CCG, 1994-2007

Johnson, B., Significance of the Footwashing (No. 99), CCG, 1995, (ed. Cox. W.E., 1999, 2007)

Kohn, Dr. S., Die Sabbatharier in Siebenburgen, Budapest, 1894, tr. McElwain, T., & Rook, B., Intro. Cox, W.E., CCG Publishing, 1998

Sabbath Message: http://www.ccg.org/_domain/ccg.org/Sabbath/2005/S_07_09_05.htm

Early Jewish Writings: http://www.earlyjewishwritings.com/text/philo/book28.html

Judaeus Philo, The Special Laws, II, XXVI, 140, F.H. Colson, Harvard University Press, Cambridge MA, 1937

The NIV Study Bible, Zondervan Bible Publishers, MI, USA, 1985



 

q