Makanisa ya kikristo ya Mungu

[257]

 

 

 

Amri Kuu ya Pili

(Chapisho La 3.0 19981008-19990526-20070228-20120804)

 

Amri hii Kuu ya Pili inafanana na ile ya Kwanza. Nayo inasema: Nawe mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Amri Kumi za Mungu zimegawanyika kwenye Amri Kuu Mbili. Mfumo wake unonekana kirahisi, na kwamba kundi la kwanza linafungasha anri nne zinazohusika na upendo kwa Mungu na kundi la mwisho.linajumla ya amri sita ambazo zinahusika na upendo kwa mwanadamu mwenzako au jirani..

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hakimiliki © 1998, 1999, 2007, 2012 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki..

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 


Amri Kuu ya Pili

 


 [jarida hili linatakiwa lisomwe kabla ya kulifafanua ile ya Tano na ambayo ni Amri nyingine zinazofuatia.]

 

Mungu alimpa Musa utaratibu wa Torati kwenye maandiko yaliyo kwenye Kutoka 20. Amri Kumi ziligawanyika katika amri kuu mbili kama tulivyoona kwenye tathimini ya Amri Kuu Kwanza (soma jarida la Amri Kuu ya Kwanza (Na. 252) [The First Great Commandment (No. 252)].

 

Kutoka 20:1-17 Mungu akanena maneno haya yote akasema, 2 Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

[I] 3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.

[II] 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

[III] 7 Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure

[IV] 8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 11 Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa..

[V] 12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

[VI] 13 Usiue.

[VII] 14 Usizini.

[VIII] 15 Usiibe.

[IX] 16 Usimshuhudie jirani yako uongo.

[X] 17Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.  

 

Mgawanyo wa sheria za Torati kwa sehemu mbili za Amri Kuu ulifanywa baadae na Kumbukumbu la Torati. Muundo wake umeonyeshwa kwa wazi sana, kwa kuzifanya zile amri nne za kwanza zihusike na kuonyesha kwetu upendo wetu kwa Mungu, na zile sita za mwisho zihusike na upendo wetu kwa wengine au majirani zetu. Kwa hiyo sheria hizi zilifungamanishwa kwa utaratibu ulio muhimu na dhahiri.

 

Wajibu wetu ni kwa Mungu na pia kwa wanadamu wenzetu. Wajibu wet uni kuwa tunaofaa na wenye mapokeo mema kwa Mungu wetu aliye Hai. Yeye ni Mungu wa waliohai na sio wa wafu.

Mathayo 22:29-40 inasema: Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu. 30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni. 31 Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema, 32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. 33 Na makutano waliposikia, walishangaa kwa mafunzo yake. 34 Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja. 35 Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu; 36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? 37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. 38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. 39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. 40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.

 

Sehemu ya kwanza ya torati inashughulika na upendo wetu kwa Mungu. Inatakiwa tufanye hivyo kwa mioyo yetu yote na kwa akili zetu zote na kwa roho zetu zote. Sehemu ya pili ni kumpenda jirani yetu, kama nafsi zetu. Kwa kuwa kama hatutampenda jirani yetu ambaye tunamuona, tutawezaje kupenda Mungu ambaye hatumuoni?

1Yohana 4:20-21 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. 21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.

 

Muundo wa Amri Kuu ya Kwanza inaweka misingi ya Amri Kuu ya Pili, na kwa amri hizi mbili zinategemeza Torati yote na manabii. Kwa hiyo, Amri Kumi ni muunganiko wa makundi madogo mawili, na kwa sehemu iliyobakia ya sheria ama torati ni pea nyingine ndogo ya hizi amri kumi.

 

Amri Kuu ya Pili imetokana na amri sita zilizo kwenye zile Amri Kumi. Ni katika tendo letu la kuziua kiroho kwa hii Amri Kuu ya Pili ambapo tunaonyesha uwezekano kwa sisi kuingia hukumuni kwa kiwango kikubwa cha mambo ya Sheia au Torati.

 

Muundo wa hii ya Pili unatokana na mlolongo huo huo wa kufikiri mambo ya msingi yanayotokana na Amri Kuu ya Kwanza. Ni kama Mungu alivyo kiini au mhusika kwenye ile ya Kwanza, na familia ya mwanadamu akiwa kama elohim ni mlengwa wa kundi hili la Amri Kuu ya Pili. Amri zote Mbili zinatangaza na kuonyesha chakato wa Mungu (kama Eloa) na kuwa Elohim ambao kwao unafanya mionekano yote miliwi ya kimbinguni na mwonekano wa kiduniani au kimwili.

 

[V] 12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

Amri ya Pili ina ahadi inayohusiana na mpango wa maisha ya kimilele ya elohim. Ilipaswa kuwa hivyo tangu mwanzo.

 

[VI] 13 Usiue.

Tendo la kuua linatokana na dhambi na hamu ya kujionea uharibifu wa kuharibu viumbe vingine. Mawazo haya yanatoka kwa adui na nshitaki wetu ibilisi. Si mpango wa Mungu kumfanya kiumbe yeyote aangamie, kwa kuwa wataokolewa wote kwa wakati wake muafaka, hata Malaika zake. Kwa kuwa upendo wa Mungu ni mkamilifu na hana upendeleo (soma jarida la Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199) {Lost Sheep and the Prodigal Son (No. 199)].

 

[VII] 14 Usizini.

Tendo la kulinda maadili ya familia na uaminifu wa umoja ni ashirio au mwonekano asilia wa tabia ya uadilifu na uaminifu ya Mungu. Ndoa ni mfano ashirio wa uhusiano kati ya Kristo na Kanisa. Hatuwezi kuivunja moja bila ya kuiathiri nyingine. Uhusiano wowote ambao unaingilia maadili ya familia, kupunguza wajibu na mamlaka ya mume nay a mwanamke, ni uzinifu na yanaathiri na kuhatarisha kwa kuendeleza fikra potofu za kiuzinzi kwa mwanamke. Mwanaume ni kuhani kwenye nyumba yake hasa akiwa kama ataitii Sheria au Torati hii ya Mungu. nyingi ya hizi imani zinazoitwa leo kuwa za Kikristo zinaendeleza fikra hizi potofu na wanawapa huduma za kikuhani au majukumu ya kikuhani na zifanywe na wote yaani wababa au wanaume na wanawake. Baadhi ya dini hizi zimefikia kiasi cha kutokemea na kuchukuliana na matendo ya uasherati na hata yamewekwa kwenye moja wapo ya matendo ya kufanya ili kukamilisha sharti za ibada zao.

 

Ukubwa wa dini hizi au itikadi ya maisha ya useja kwa makasisi vinaonekana kuwa haviwezi kuwafanya kuokoka mbali na matendo haya.

 

[VIII] 15 Usiibe.

Mambo ya mtu binafsi yake yanaonyesha kwenye muundo wa Torati, kama inavyohusiana na uwezekano wa kumlinda kila mtu kutokana na bidii yake binafsi, na kwa maisha ambayo wamelazimika kuingia mkumboni. Jamii na mpangilio wake wa kimuundo vinamuibia mtu kwa namna iliyopangiliwa nay a kijanja sana zaidi ya wahalifu tulinaowajua na tuliowazoea kwenye jamii zetu za leo. Katika siku hizi za mwisho, dhuluma na udanganyifu ni vitu vinavyopigwa vita sana na kuonekana havifai, lakini kuna vitu vyenye madhara makubwa zaidi kuliko hivi. Tunakaribia kushuhudia kihoro kikubwa cha mfumo wa dini ya uwongo katika siku za mwisho.

 

[IX] 16 Usimshuhudie jirani yako uongo.

Mfumo mzima wote wa mambo ya haki unatuama kwenye kweli. Mfumo wote wa mpango wa wokovu unaweza kuwa salama tu iwapo kama utaendana na ulivyo, na kulindwa na kweli. Tunalazimika kuushuhudia mpango wa Sheria au Torati ya Mungu na kweli yake.

 

[X] 17Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.  

 

Mambo ya kiroho yanayoihusu Totati yameorodheshwa kwenye mambo haya yaliyoandikwa kwenye Amri Kumi, ambayo kwamba namna zote za kujaribu kuzivunja ni matokeo ya mawazo ya kibinadamu na ni kuivunja Torati hii yote. Ni kwa kuyazuia majaribu tu yatokanayo na mawazo kunaweza kutufanya tujifunza kikweli kumpenda mwenzako na kupendana sisi sote kwa roho na kweli.

 

1Wakorintho 13:1-13 inasema: Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 9 Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; 10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika. 11 Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. 12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana. 13 Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.

 

Ukamilifu wa Sheria au Torati ni upendo na kuhudumiana. Torati yenyewe imewekwa kwa nia ya kumlinda mtu na mambo yaliyo kwenye taratibu za kidunia au za kimwili, wakti Roho Mtakatifu ameletwa ili kuhudumia yale yaliyo kwenye mlolongo wa kiroho. Roho Mtakatifu ni wa muhimu ili tuweze kuifuata vema na kikamilifu Sheria ya Kamilifu ya Uhuru.

 

Sheria Kamilifu ya Mungu ya Uhuru imewekwa ili kutuwezesha sisi tuwe kwenye mahusiano kamilifu nay eye na kwa kila mmoja wetu. Kwa hiyo, amri ile ya sita na nyingine zote zinazofuatia zinaelekea kwenye mwisho huu, na kwamba sisi tupendane sote na tumpende jirani yetu kama tunavyojipenda wenyewe.

 

q