Makanisa ya
kikristo ya Mungu
[258]
Torati na Amri ya Tano
(Toleo La 2.0
19981008-19990526-20120522)
Imeandikwa: Waheshimu baba yako na
mama yako;
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 1998, 1999, 2012 Wade
Cox)
(tr. 2012)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote
kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Torati na Amri ya Tano
Amri hii ya Tano imeandikwa kwenye Kutoka 20 na Kumbukumbu la Torati 5.
Kutoka 20:12 Waheshimu baba yako na mama yako;
Kumbukumbu la Torati 5:16 Waheshimu baba yako na mama yako;
Amri hii ya Tano
ni amri pekee nay a kwanza yenye ahadi. Ni amri ya kwanza au ni kiini cha amri
zote na hufungamanisha na ile Amri Kuu na ya Pili inayotuamuru kumpenda jirani
Mathayo 19:18-19 Akamwambia, Zipi? Yesu
akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, 19
Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako
Waefeso 6:1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
Wakolosai 3:20: Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.
Familia kama kiini cha
jamii
Uumbaji ulitegemezwa kwenye mfumo wa kifamilia kwenye Bustani ya Edeni (soma jarida la Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya 1, Bustani ya Edeni (Na. 246) [The Doctrine of Original Sin Part I The Garden of Eden (No. 246)] na Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya 2, Kizazi cha Adamu (Na. 248) [The Doctrine of Original Sin Part 2 The Generations of Adam (No. 248)]. Familia hutengeneza tofali lililo kiini cha jengo la kwenye jamii zetu. Familia ya kibinadamu ilianzishwa na Mungu, na ilikusudiwa iongezeke na kuendeleza hali ya kufanyika kuwa mfano wa Mungu, na kufanyika kuwa ni hekalu la Mungu (sawa na Mwanzo 1:27-30; Mwanzo 2:7,18).
Baba ni nguzo ya nyumba
Familia pia ina wajibu mpana kwa mujibu wa sheria, ambayo haitakiwi kudharauliwa au kuchukuliwa ki juu juu tu na ki wepesi. Kwa ajili hii alama ya mtumwa ni kitu kilicho kwenye jamii, inaonyeshwa kwa alama ya mwewe anayeruka hewani (Kutoka 21:6). Kwa jinsi hiyohiyo, kiongozi wa nyumba hubeba wajibu mkubwa kwa mujibu wa sheria (Kutoka 22:8). Kwa ajili hii, tunaendelea kuwa ni watoto wa Mungu aliye Juu na wana wa Mungu. Haijaandikwa kuwa “Je, sikusema kuwa ninyi ni miungu?” …wana wa Aliye Juu ninyi nyote” na Maandiko hayawezi kutanguka (sawa na Zaburi 82:1-6; Yohana 10:35).
Zaburi 82:1-6: Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati
ya miungu anahukumu. 2 Hata lini mtahukumu
kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya? 3 Mfanyieni
hukumu maskini na yatima; Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara; 4 Mwokoeni maskini na mhitaji; Mwopoeni mikononi mwa
wadhalimu. 5 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;
Misingi yote ya nchi imetikisika. 6 Mimi nimesema, Ndinyi
miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia.
Utaratibu na mfumo mzima wote ni kwa familia ya wana wa Mungu, ya aina zote mbili yaani kiroho na kimwili.
Viumbe wote humtegemea mwanadamu
1Petro 3:1-7: Kadhalika ninyi wake, watiini
waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake
zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu
Kuwaasi wazazi kuna ahadi yake pia.
Mithali 30:17: Jicho la mtu amdhihakiye
babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga
vya tai watalila.
Familia hufanyika kuwa kiini cha kwanza kaeika jamii. Jamii kama utaratibu imeonyeshwa kwenye familia, kwa njia ya neema na inaonekana kuwa Mungu alitupeleka tukiwa na sura na tabia zake, kwa mwana wake tumjuaye ambaye ni Yesu Kristo.
Tito 2:1-15: 1 Lakini wewe nena mambo yapasayo
mafundisho yenye uzima; 2 ya kwamba wazee wawe wenye
kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika
saburi. 3 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na
mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi,
bali wafundishao mema; 4 ili wawatie wanawake vijana
akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; 5 na
kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii
waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe. 6 Vivyo
hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi; 7 katika
mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na
katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, 8 na
maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga
atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu. 9 Watumwa
na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu, 10 wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili
wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote. 11 Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;
12 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za
kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa
sasa; 13 tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo
ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; 14 ambaye
alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na
kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo
mema. 15 Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa
mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.
Kwa ajili hii
wazazi wanatakiwa kujiangalia na kuwapa watoto wao na kuwaandalia hatima
2Wakorintho 12:14: Tazama, hii ni mara ya tatu ya mimi kuwa tayari kuja kwenu, wala sitawalemea. Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi; maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto.
Kwa jinsi hii, kuna mzaliwa wa kwanza mmoja tu mwenye stahili ya kurithi kwenye familia, jambo ambalo halitegemei na idadi ya wake waliopo kuwa ni wangapi (Kumbukumbu la Torati 21:15-17).
Kumbukumbu la Torati 21:15-17: Akiwa mtu yuna wake wawili, mmoja ampenda, mmoja hampendi, nao wamemzalia
watoto, ampendaye na asiyempenda wote wawili; na yule mzaliwa wa kwanza akiwa
ni wa mke asiyependwa; 16 ndipo itakapokuwa ya
kwamba siku atakayowarithisha wanawe alivyo navyo, asimweke mwana wa ampendaye
kuwa mzaliwa wa kwanza mbele ya mwana wa asiyempenda, naye ndiye mzaliwa wa
kwanza huyu; 17 lakini amkubali mzaliwa wa kwanza mwana
wa yule asiyempenda, kwa kumpa mafungu mawili katika vyote alivyo navyo; kwa
maana ndiye mwanzo wa nguvu zake; haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
Watoto wanawajibu pia
kwa wazazi wao ambao kama wakikosea adhabu
Kumbukumbu la
Torati 21:18-23: Mtu
akiwa na mwana mkaidi, mshupavu, asiyetii sauti ya baba yake, wala sauti ya
mama yake, nao wajapomwadhibu hawasikizi, 19 ndipo
babaye na mamaye na wamkamate, na kumpeleka kwa wazee wa mji wake, katika lango
la mahali pake; 20 wawaambie wazee wa mji wake, Huyu mwana
wetu ni mkaidi, mshupavu, hasikizi sauti yetu; ni mwasherati, tena ni mlevi. 21 Waume wote wa mji wake na wamtupie mawe, afe; ndivyo
utakavyoondoa uovu katikati yako; na Israeli wote watasikia na kuogopa. 22 Akiwa mtu ametenda dhambi ipasayo kufa, akauawa, nawe
ukamtundika juu ya mti; 23 mzoga wake usikae
usiku kucha juu ya mti; lazima utamzika siku iyo hiyo; kwani aliyetundikwa
amelaaniwa na Mungu; usije ukatia unajisi katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu
wako, iwe urithi wako.
Tunaona sasa
kwamba msingi wa jamii ni familia na familia ni tofali la jengo la taifa. Nidhamu
ya jamii inategemea na familia ikiwa
Amri inayotutaka kuwa
watakatifu
Kwa kuwa familia inafanya kazi kwa njia za kawaida, wajibu wa kazi ya Mungu ni wa kiroho. Tuna Baba yetu mmoja tu.
Malaki 2:10: Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba
siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana,
tukilinajisi agano la baba zetu?
Mungu ametuumba sisi na kwa mapenzi yake tunaishi na tumeumbwa.
Ufunuo 5:8-10: Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu. 9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, 10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.
Kumbuka jinsi maandiko yanavyosema kuwa “watatawala hapa duniani.”
Yeye anayetakasa na yule anayetakaswa wana wana chanzo kimoja.
Waebrania 2:11: Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa
wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake;
Hatupaswi kumuita mtu yeyote baba, kwa kuwa baba yetu ni Mungu peke yake na aliyeko mbinguni, naye ndiye Mungu wetu na Baba yetu naye ndiye Baba Mungu na Baba wa Yesu Kristo aliyemtuma.
Mathayo 23:9: Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.
Yeye ndiye pekee anayepaswa kuwa mlengwa kwenye kujitoa kwetu na kwenye maombi yetu.
Mathayo 6:1-15 inasema: Angalieni msifanye
wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya
Uhusiano na Baba
Mungu ni jambo muhimu na la kwanza, lakini ni kwa Amri ile Kuu nay a Kwanza
tunagundua umuhimu wa Amri Kuu nay a
Kutoka 22:31: Nanyi mtakuwa watu watakatifu
kwangu mimi; kwa hiyo msiile nyama yo yote iliyoraruliwa huko kondeni na mnyama
wa mwitu; mtawatupia mbwa nyama hiyo.
Mambo ya Walawi 11:44 Kwa kuwa mimi ni Bwana, Mungu wenu; takaseni nafsi zenu basi; iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu; wala msitie uchafu nafsi zenu kwa kitu kitambaacho cha aina yo yote, kiendacho juu ya nchi.
Mtu binafsi ni mtakatifu na hapaswi kunajisika, kwa kuwa ilikuwa ni Mungu ndiye aliyetuokoa na kutufanya kuwa watakatifu.
Mambo ya Walawi 11:45 Kwa kuwa mimi ni Bwana niliyewaleta kutoka nchi ya Misri, ili kwamba niwe Mungu wenu; basi mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu.
Mambo ya Walawi 20:26: Nanyi mtakuwa watakatifu kwangu mimi; kwa kuwa mimi Bwana ni mtakatifu nami nimewatenga ninyi na mataifa, ili kwamba mwe wangu
Kusudi
la kuumbwa kwa mwanadamu
Familia takatifu
Kama Israeli ilivyotakatifu, na ndivyo familia ilivyo ni takatifu. Taifa ni la Mungu, na ufalme umewekwa kwa Kristo aliye wa uzao wa Daudi, ufalme utakaodumu milele. Sisi ni watu wa nyumbani mwa familia moja, na familia ile inatawaliwa na waamuzi walio kwenye nyumba ya Daudi, ambayo ni ya Masihi nay a ukuhani wa Melkizedeki. Kwa kuwa mfalme wangu ni mtakatifu (Melkzedeki) au Bwana wangu ni mtakatifu (Adonizedeki) ni cheo cha kumtukuza mfalme wa milele wa Yerusalemu (sawa na zinavyosema Mwanzo 14:18; Zaburi 110:4; Yoshua 10:1; na pia G. Vermes, kitabu chake cha kilichoandikwa kwa lugha ya Kiingereza cha The Dead Sea Scrolls in English [(Gombo la Kiingereza lililopatikana kwenye Bahari Mfu) linalomwelezea Melchizedek na maana yake)].
2Samweli 7:10-16: Tena nitawaagizia mahali
watu wangu Israeli, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe,
wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena, kama hapo kwanza; 11 naam,
15 lakini fadhili zangu hazitamwondoka,
Kwa hiyo Masihi amepewa cheo cha ubaba kwa wana wa wanadamu walio wana wa Mungu.
Isaya 9:6-7 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa
kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu
mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. 7 Maongeo
ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha
Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki,
Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.
Ataitwa mwana wa Mungu.
Luka 1:32-35: 31 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. 33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. 34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? 35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.
Kwa yeye, haki imewekwa kwa familia ya
wanadamu (Isaya 11:4, 5)
Kwa Adamu wa kwanza tuchukua taswira ya kidunia, na kwa Adamu wa pili tunachukua taswira ya kimbinguni.
1Wakorintho 15:45-49: Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha. 46 Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho. 47 Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni. 48 Kama alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni. 49 Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni.
(sawa na Mathayo 28:18,19; Ezekieli 21:27)
Familia yake ni familia yetu kwa kuwa tunayafanya mapenzi ya Mungu (Yohana 19:25-27). Kwa hiyo, familia ina viwango viwili ambavyo ni vya familia ya kidunia na vya kimbinguni.
Mathayo 12:46-50: Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama
yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye.
47 Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako
wamesimama nje, wanataka kusema nawe. 48 Akajibu,
akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina
nani? 49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake,
akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu! 50 Kwa
maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye
ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu.
Kwa hiyo, sisi sio wana wa mwanamke mtumwa
bali ni wana wa uzao wa kweli na kwa hiyo sisi ni warithi (Wanzo 21:10;
25:1-6). Tofauti hii ni ya mstari wa wana walio
kwenye imani, katika urithi wa Mungu, uolioainishwa kwenye sheria, ikiwa ni
utofautidhaji na yule asiye mwaminifu.
Mambo ya Walawi 25:45-46: Tena katika wana wa wageni wakaao kati yenu mtajinunulia, na katika jamaa zao walio pamoja nanyi, waliowazaa katika nchi yenu; wao watakuwa milki yenu. 46 Nanyi mtawafanya kuwa urithi kwa watoto wenu baada yenu, wawe milki yao; siku zote mtatwaa watumwa wenu katika hao; lakini msitawale kwa nguvu juu ya ndugu zenu, hao wana wa Israeli, wenyewe kwa wenyewe.
Kwa hiyo uanzishaji wa taifa lionekanalo huanzia kwenye masuala ya kiroho, na utofautishaji wake umefanywa ili kuonyesha kuwa ni kwa njia ya wokovu peke yake na kuingia kwa taifa ndipo watu wote watakuwa kwenye milki ya uzima wa milele.
Ili tuweze kuonekana
kuwa tunaliweza
Zekaria 12:8: Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa
Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo;
nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele
Kufuatiwa na ufufuo
wa pili na kipindi cha kuwafundisha viumbe wote (Isaya 65:20), ndipo sisi sote
kwa kila mmoja na viume wote tutakwenda mbele kuelekea kwenye hatima yetu. Na
ndipo Mungu hatimaye atafanyika kuwa wote ndani ya yote na katika yote, nasi
tutakuwa ni mahala pa makao ya Mungu, tukiwa
Waefeso 4:6: Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya
yote na katika yote na ndani ya yote.
Haya ni matukio ya mwisho ya vile Mungu anavyokwenda kuwa (Kutoka 3:14).
Utakaso na usafishaji
Kwenye mchakato huu tunapaswa kutakaswa na
kuwa
Amri inayohusu vyakula inapatikana kwenye Mambo
ya Walawi 11:1-47 na Kumbukumbu la Torati 14:1-21 (soma jarida la Sheria ya
Vyakula (Na. 15) [The
Food Laws (No. 15)].
Taifa na watu walitakaswa na kutenga mbali ili kwamba Mungu awatembelee. Hata hivyo, kwa taifa la kimwili linaloonekana, aliweka viapo na kuongea nao kwa kupitia malaika wa Yahova. Kanmuni hizi zimeorodheshwa kwenye kitabu cha Kutoka 19:10-25,
Andiko kamili ambalo tunaweza kulisoma katika
mwaka wa saba. Sheria hizi zinaelezea jinsi Mungu anavyoweza kufanya kazi
kupitia taifa na kupitia Kanisa. Sheria hii hapo mwanzoni walipewa watu sabini
na hatimaye kwa taifa. Watu walitakaswa kwanza na mchakato wa utakaso unafanywa
na Kanisa na taifa kwa mwelekeo wa kila mwaka ulianzia Siku ya
Kwa hiyo, utakaso ni sehemu ya mchakato unaomfanya mtu kuwa mtakatifu na mwenye kukubalika katika kumuishia Mungu aliye hai.
Mambo ya Walawi 20:7: Jitakaseni basi, iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Kuweka ka mamlaka
Mungu ameweka malmaka yake hapa dunia kwa kupitia viongozi wake aliowawachagua na kuwaweka. Mungu aliongea na watu kwa kupitia watumishi wake waliosimama kati yake na wanadamu ambao walikuwa ni manabii (Amosi 3:7). Tendo hili lilifanyika kwa mwelekeo endelevu wa mamlaka yaliyotoka kwa manabii wa Mungu na kuwaendela viongozi wa mataifa.
Kutoka 4:11-23 inasema: Bwana akamwambia, Ni
nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au
kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? 12 Basi
sasa, enenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na kukufundisha
utakalolinena. 13 Akasema, Ee Bwana, nakuomba, tuma
kwa mkono wake huyo utakayemtuma. 14 Hasira ya Bwana
ikawaka juu ya Musa, akasema, Je! Hayuko Haruni, ndugu yako, Mlawi? Najua ya
kuwa yeye aweza kusema vizuri. Pamoja na hayo, tazama, anakuja kukulaki; naye
atakapokuona, atafurahi moyoni mwake. 15 Nawe utasema
naye, na kuyatia maneno kinywani mwake; nami nitakuwa pamoja na kinywa chako,
na pamoja na kinywa chake, na kuwafundisheni mtakayofanya. 16
Naye atakuwa msemaji wako kwa watu, hata yeye atakuwa mfano wa kinywa
kwako, nawe utakuwa mfano wa Mungu kwake. 17 Nawe
utatwaa fimbo hii mkononi mwako, na kwa hiyo utazifanya zile ishara. 18 Basi Musa akaenda na kurejea kwa Yethro mkwewe, na
kumwambia, Nipe ruhusa niende, nakusihi, niwarudie hao ndugu zangu walioko
Misri, nipate kuwaona kwamba wako hai hata sasa. Yethro akamwambia Musa, Haya,
nenda kwa amani. 19 Bwana akamwambia Musa huko
Midiani, Haya, nenda, karudi Misri; kwa kuwa wale watu wote waliokutaka uhai
wako wamekwisha kufa. 20 Basi Musa akamchukua mkewe na
wanawe, na kuwapandisha juu ya punda, naye akarudi mpaka nchi ya Misri; na Musa
akaichukua ile fimbo ya Mungu mkononi mwake. 21 Bwana
akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile
ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye
hatawapa ruhusa hao watu waende zao. 22 Nawe umwambie
Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu; 23 nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate
kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua
mwanao, mzaliwa wa kwanza wako.
Mungu ndiye aliyekuwa anawachagua na kuwaweka viongozi katika Israeli.
Hesabu 27:12-23 inasema: Bwana
akamwambia Musa, Panda wewe juu ya mlima huu wa Abarimu, uitazame nchi niliyowapa
wana wa Israeli. 13 Na ukiisha kuiona, wewe nawe utakusanyika
pamoja na baba zako, kama Haruni ndugu yako alivyokusanyika; 14 kwa sababu mliasi juu ya neno langu katika jangwa la
Sini wakati wa mateto ya mkutano, wala hamkunistahi, hapo majini, mbele ya
macho yao. (Maji hayo ndiyo maji ya Meriba ya Kadeshi katika jangwa la Sini.) 15 Musa akanena na Bwana akisema, 16 Bwana,
Mungu wa roho za wenye mwili wote, na aweke mtu juu ya mkutano, 17 atakayetoka mbele yao, na kuingia mbele yao;
atakayewaongoza watokapo, na kuwaleta ndani; ili mkutano wa Bwana wasiwe kama
kondoo wasio na mchungaji. 18 Bwana akamwambia
Musa, Mtwae Yoshua, mwana wa Nuni, mtu mwenye roho ndani yake, ukamwekee mkono
wako; 19 kisha ukamweke mbele ya Eleazari kuhani,
na mbele ya mkutano wote; ukampe mausia mbele ya macho yao. 20 Nawe
utaweka juu yake sehemu ya heshima yako, ili mkutano wote wa wana wa Israeli
wapate kutii. 21 Naye atasimama mbele ya Eleazari kuhani,
naye atamwulizia kwa hukumu ya ile Urimu mbele za Bwana; kwa neno lake
watatoka, na kwa neno lake wataingia; yeye na wana wa Israeli wote pamoja naye,
mkutano wote pia. 22 Musa akafanya kama
Bwana alivyomwamuru; akamtwaa Yoshua, akamweka mbele ya Eleazari kuhani, na
mbele ya mkutano wote; 23 kisha akaweka mikono
yake juu yake, akampa mausia, kama Bwana alivyosema kwa mkono wa Musa.
Kwa hiyo, uchaguzi
uliofanywa na makuhani wakitumia Urimu na Thumimu, ulisimama kuwa
Kumbukumbu la Torati 17:14-20 inasema: Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo
Bwana, Mungu wako ukaimiliki, na kukaa humo; nawe utakaposema, itaweka mfalme
juu yangu mfano wa mataifa yote yaliyo kando-kando yangu; 15 usiache
kumweka yule atakayechaguliwa na Bwana, Mungu wako, awe mfalme juu yako; umweke
mmoja katika ndugu zako awe mfalme juu yako; usimtawaze mgeni juu yako, ambaye
si ndugu yako. 16 Ila asifanye farasi wake kuwa wengi, wala
asiwarudishe watu Misri, ili apate kufanya farasi kuwa wengi; kwa kuwa Bwana
amewaambia, Tangu sasa msirudie tena njia ile. 17 Wala
asijizidishie wake, ili moyo wake usikengeuke; wala asifanye fedha zake na
dhahabu kuwa nyingi mno. 18 Tena na iwe, zamani
aketipo juu ya kiti cha ufalme wake, ajiandikie nakala ya torati hii katika
chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi; 19 na
awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha Bwana,
Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii na amri hizi, kwa kuyafanya; 20 moyo wake usije ukainuliwa juu ya ndugu zake, wala
asikengeuke katika maagizo, kwa mkono wa kuume wala wa kushoto; ili apate
kuzifanya siku zake kuwa nyingi katika ufalme wake, yeye na wanawe, katikati ya
Israeli.
Ni mtu yule tu aliye wa kabila la Israeli ndiye atawatawala Israeli. Mfalme anafungiwa kwenye maongozi ya torati au sheria za Mungu na kwenye maelekezo yote yaliyoagizwa kwenye torati.
Agano la kufanya
tohara liliwahusu Israeli na manabii walilijua hili kuwa ni kama mfano wa
maumivu yaliyotokana na maisha
Kutoka 4:25-28: Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi. 26 Basi akamwacha. Ndipo huyo mkewe akanena, U bwana arusi wa damu wewe, kwa ajili ya kutahiri. 27 Bwana akamwambia Haruni, Nenda jangwani uonane na Musa. Naye akaenda, akamkuta katika mlima wa Mungu, akambusu. 28 Musa akamwambia Haruni hayo maneno yote ya Bwana ambayo alimtuma aende nayo, na ishara hizo zote alizomwagiza.
Agano la tohara
lililenga kwenye agano la mioyo
Tendo hili la kuwatahiri watoto wa familia zao alilopewa Ibrahimu na likaanzisha tena na kuedelezwa na Musa na Yoshua (soma Yoshua 5:8; Yohana 7:22) zinazoelezea kuhusu kutahiriwa kwa njia ya Roho Mtakatifu na wajibu wa wateule (soma Matendo 7:8; 10:45-11:2). Wamataifa waliambiwa haikuwa lazima kwao kutahiriwa wanapoingia kwenye mkutano wa Israeli kwa Roho Mtakatifu. Kwa kuwa kwa amri kuu twaweza kusema kwamba sio kila alyetahiriwa alikuwa Muisraeli na sio kila asiyetahiriwa alitengwa mbali na agano hili la Ubaba na Mungu wa Israeli.
Kutoka 12:49: Sheria ni hiyo moja kwa mtu aliyezaliwa kwenu, na kwa mgeni akaaye kati yenu ugenini.
Wakati ule Musa alipowakusanya wazee wa Israeli na Musa na Haruni akasema nao (Kutoka 4:29-31).
Kutoka 4:29-31: Musa na Haruni wakaenda,
wakawakusanya wazee wote wa watu wa Israeli. 30 Haruni
akawaambia maneno yote Bwana aliyonena na Musa akazifanya zile ishara mbele ya
watu. 31 Watu wakaamini, na waliposikia ya kuwa Bwana
amewajilia wana wa Israeli, na ya kuwa ameyaona mateso
Mamlaka ya taifa ndiyo njia ambayo Mungu alishughulika nayo pia katika kuieneza na kuweka utaratibu wa familia.
Hesabu 12:1-16 inasema: Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa
sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke
Mkushi. 2 Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa
tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno
Jukumu la kuweka na kuyatendea kazi mzmlaka ni la Mungu. Ndiyo maana inanenwa kamba uasi ni sawa na dhambi ya uchawi, kwa kuwa tendo hili la kuasi linaanzisha nia ya moyo wa mtu ya kupingana na mapenzi ya Mungu na ni matokeo ya mtu kuwa mwabudu miungu wengi (soma 1Samweli 15:23).
Kazi ya mamlaka
Hata watiwa mafuta wa Mungu waliwajibika
kuzitunza sheria hizi zilizo kwenye amri ya tano na jinnsi zinavyohusiana na
familia na ndoa. Wazazi wa Musa pia waliwajibika kuzitunza hivyo hivyo. Kwa
hiyo, busara kubwa itokea kwa kuhani na nabii mwingine. Kwenye kitabu cha
Kutoka 18 tunaona kwamba Musa alikuwa amewamini mke wake na wanawe na mkwa wake
mzee Yethro aliyekuwa kuhani wa Midiani, akairudisha familia ya Musa na kuwapa
ushauri wa jinsi ya kuwahukumu Israeli na utaratibu wake wa kuwapatia watu haki
zao na jinsi ya utawala.
Kutoka 18:1-27 inasema: Basi Yethro, kuhani wa Midiani, mkwewe
Musa, alisikia habari ya mambo hayo yote Mungu aliyokuwa amemtendea Musa, na
Waisraeli watu wake, jinsi Bwana alivyowaleta Israeli watoke Misri. 2 Ndipo Yethro mkwewe Musa akamtwaa Sipora, mke wa Musa,
baada ya yeye kumrudisha, 3 pamoja na wanawe wawili;
katika hao, jina la mmoja ni Gershomu, maana alisema, Mimi nimekuwa mgeni
katika nchi ya ugenini; 4 na jina la wa pili ni
Eliezeri, kwa kuwa alisema, Yeye Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu,
akaniokoa na upanga wa Farao. 5 Basi Yethro, mkwewe
Musa, pamoja na mke wa Musa na wanawe wawili wakamwendea Musa huko nyikani,
hapo alipokuwa amepanga, kwenye mlima wa Mungu; 6 naye
akamwambia Musa, Mimi Yethro mkweo nimekuja kwako, na mkeo, na wanawe wawili
pamoja naye. 7 Basi Musa akatoka nje ili amlaki
mkwewe, akasujudia na kumbusu; nao wakaulizana habari; kisha wakaingia hemani. 8 Musa akamwambia mkwewe mambo hayo yote Bwana aliyomtenda
Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na mambo mazito yote yaliyowapata
njiani, na jinsi Bwana alivyowaokoa. 9 Yethro
alifurahi kwa ajili ya wema wote Bwana aliowatendea Israeli, kwa alivyo waokoa
mikononi mwa Wamisri. 10 Kisha Yethro akasema, Na
ahimidiwe Bwana aliyewaokoa na mikono ya Wamisri, na mkono wa Farao;
aliyewaokoa watu hao watoke mikononi mwa Wamisri. 11 Sasa
najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu yote; naam, katika jambo
Musa alikuwa anawajibika kumtumikia Mungu akiwa kama mwombezi wao, na watu waliokuwa hawana tuhuma za wizi na ubadhirifu walichaguliwa kuwa maakida wa makumi, wa hamsini, wa mamia na wa maelfu, na watu hawa walifanyika kuwa ni maakida wa Israeli. Mambo yaliyokuwa makuu tu kwao ndiyo walimpelekea Musa aliyekuwa na wale waliokuwa kwenye malmaka makuu.
Kutokana na utaratibu huu, tunaona kuwa familia zinapangwa kwa kufuata makundi ya kumikumi, na kumi wa hamsini, na kisha kwa mamia, na halafu kwa maefu na kutoka hapo kwa wakuu wa maelfu na hatimaye kwa wakuu wa makabila. Makundi yaha yalikuwa ni ya watu 28,000. Kutoka kwenye makabila haya ambako kisha tunapata watu sabini walio wajumbe wa Elohim mwenye HAki. Kwa hiyo kwa muundo huu wa familia ndio uliunda tifa, ambayo hatimaye ilifanyika kuwa ni familia ya mataifa, yote yakiwa kwenye utaratibu na kwenye mamlaka yanayoilinda na kwendana.na mapenzi ya Mungu na Torati yake.
Chini ya mamlaka
yake tunafanya mambo kwa jina
1Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi
mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Tumeita wote ili kufanyika kuwa wana na
Mungu aliye Hai (Hosea 1:10). Eloa amejiongeza mwenyewe na kuwa
Elohim
Kumbukumbu la Torati 6:13: Mche Bwana, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake.
Jina la Mungu ni kitu chenye mamlaka ya mapana yake kati ya watu wake, kwa jinsi ya kiroho na kimwili. Kwa hiyo neno elohim linawahusu Malaika wa mbinguni na waamuzi na watawala wa taifa la kidunia la Israeli (Kutoka 22:18).
Kumbukumbu la Torati 16:18-20 Weka waamuzi na maakida katika malango
yako yote akupayo Bwana, Mungu wako, kwa hesabu ya kabila zako; nao wawaamue
watu kwa maamuzi ya haki. 19 Usipotoe maamuzi;
wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha
macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki. 20 Yaliyo
haki kabisa ndiyo utakayoyafuata, ili upate kuishi na kuirithi nchi upewayo na
Bwana, Mungu wako.
Kutakuwa na haki kwenye hukumu zetu zote tunazozifanya kwa hukumu ya haki.
Malaika wa Mungu wote wanaitwa Hayoha wanapokuwa wakifanya kazi zake alizowatuma (ndivyo ilivyoandikwa kwenye Mwanzo 18:3, 27; neno hili linafanywa kwa kuwaongeza viumbe kwenye uwingi kwenye maandiko yote ya Mwanzo 19 kwa mfano). Yahova ilitumika pia kwa malaika wengine wawili waliokuja na viumbe wengine watatu walioitwa Yahova. Alibakia na Ibrahimu alipokwenda kwa Lutu huko Sodoma, ambako alitajwa pia kuwa ni Yahova (soma jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24) [Angel of YHVH (No. 24)]. Tangu kipindi cha Sethi ambaye ni mtoto wa Adamu, ndipo watu walianza kuliitia jina la Yahova (Mwanzo 4:26).
Tunaona kwamba kutoka amri hii ya tatu,
ndipo tunaendelea hadi kwenye amri ya nne iliyo
Mambo ya Walawi 19:1-3: Bwana akanena na Musa, akamwambia, 2 Nena na mkutano wote wa wana wa Israeli, uwaambie, Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wenu, ni mtakatifu. 3 Kila mtu na amche mama yake, na baba yake, nanyi mtazitunza Sabato zangu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Kutoka kwenye Amri Kuu ya
Mamlaka ya kuupa
uweza wa kutendea kazi au kuchukulia hatua yamewekwa kwa mtu mmoja na sio kwa
wawili. Hii inamaanisha ni kwa Mungu na kwa Wateule, ambao wote wanafanya chini
ya mapenzi yake yeye Mungu, aliye wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3). Kwa hiyo,
Kristo hawezi kufanya neno lolote kwa aonavyo yeye (Yohana 5:30). Kuelelewa
jambo
Kunapokuwa na
mgongano, ndipo kiapo au nadhiri ya mke haiwezi kuifunga familia. Na ndivyo
ilivyo, kuwa ni kweli hata mapenzi ya Mungu hushinda zaidi ya yale ya Wateule
wake. Tunaona kuwa sheria hii imeandikwa kwenye kitabu cha Hesabu 30:1-16, inayoagiza
kusomwa kwa Torati kila ufikapo mwaka wa
Kwa hiyo, mwnamke yu chini ya mume wake.
Kwa kuwa amechukuliwa kutoka kwenye familia moja na kukabidhiwa kwenye familia
nyingine ambayo ni ya mume wake. Ni mfano ulio sawa tu na Kanisa ambalo limechukuliwa
kutoka kwenye kabila la mzazi na kuwekwa au kupelekwa kwenye kabila la mume,
kwenye familia inyomtii Mungu wa Pekee na wa Kweli. Na
Kichwa cha kila mwanamke ni mwanaume (kwenye familia) na kichwa cha kila mwanaume ni Masihi, na kichwa cha Kristo mtiwa mafuta ni Munbu.
1Wakorintho 11:3: Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu
Familia ya kimwili
inaendelea na kuenea tu hadi kifo, bali ile ya kiroho huendelea hadi umilele,
ambako hatutaoa wala kuolewa, bali tutakuwa kama malaika (Luka 20:34-35)
Familia kama kabila la
Familia zinafanywa na makabila na kwa vikundi vilivyo ndani ya makabila. Hii inaonekana kwenye Hesabu 2.
Hesabu 2:1-33 inasema: Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia, 2 Wana wa Israeli watapanga kila mtu penye beramu yake
mwenyewe, na alama za nyumba za baba zao; kuikabili hema ya kukutania ndiko
watakakopanga kwa kuizunguka pande zote. 3 Na hao
watakaopanga upande wa mashariki, kwa kuelekea maawio ya jua, ndio wale wa
beramu ya marago ya Yuda, kwa majeshi yao; na mkuu wa wana wa Yuda atakuwa
Nashoni mwana wa Aminadabu. 4 Na jeshi lake, na wale
waliohesabiwa kwao, walikuwa sabini na nne elfu na mia sita. 5
Na hao watakaopanga karibu naye ni kabila ya Isakari; na mkuu wa wana wa
Isakari atakuwa Nethaneli mwana wa Suari; 6 na jeshi
lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa hamsini na nne elfu na mia nne; 7 na kabila ya Zabuloni; na mkuu wa wana wa Zabuloni atakuwa
Eliabu mwana wa Heloni; 8 na jeshi lake, na wale
waliohesabiwa kwao, walikuwa hamsini na saba elfu na mia nne. 9 Hao wote waliohesabiwa katika marago ya Yuda walikuwa mia
na themanini na sita elfu na mia nne, kwa majeshi
Makabila haya kumi
yapo kwenye makundi kumi manne ya makabila matatu. Makundi haya yana maana zake
pia kwa muunganiko wake.
Biblia inayaelezea jinsi makabila haya yalivyokuwa yanahesaabiwa na kupangiliwa. Milki ya kila kabila ilitolewa kulingana na ukubwa.wa kabila ulivyo, na kwa idadi ya majina ya wanaume waliokuweko na waliofikia umri wa kwenda vitani, ambao ni kuanzia umri wa miaka ishirini na kwenda mbele.
Hesabu 26:1-62 inasema: Ikawa baada ya hilo pigo, Bwana akanena na
Musa na Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, na kuwaambia,
2 Fanya jumla ya mkutano wote wa wana wa Israeli,
tangu umri wa miaka ishirini, na zaidi, kwa nyumba za baba zao, hao wote katika
Israeli wawezao kutoka kuenenda vitani. 3 Kisha Musa
na Eleazari kuhani wakanena nao katika nchi tambarare za Moabu karibu na mto wa
Yordani, huko Yeriko, wakawaambia, 4 Fanyeni jumla ya
watu, tangu umri wa miaka ishirini, na zaidi; kama Bwana alivyomwagiza Musa na
wana wa Israeli, hao waliotoka nchi ya Misri. 5 Reubeni
mzaliwa wa kwanza wa Israeli, wana wa Reubeni; wa Hanoki, jamaa ya Wahanoki; na
wa Palu, jamaa ya Wapalu; 6 na wa Hesroni, jamaa ya
Wahesroni; na wa Karmi, jamaa ya Wakarmi. 7 Hizi ndizo
jamaa za Wareubeni; na hao waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tatu elfu na
mia saba na thelathini. 8 Na wana wa Palu; Eliabu. 9 Na wana wa Eliabu; Nemueli, na Dathani, na Abiramu. Hawa
ndio Dathani na Abiramu waliochaguliwa na mkutano, ambao walishindana na Musa
na Haruni katika mkutano wa Kora, hapo waliposhindana na Bwana; 10 nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza pamoja na Kora,
mkutano huo ulipokufa; wakati moto ulipowateketeza watu mia mbili na hamsini,
nao wakawa ishara. 11 Pamoja na hayo, hao wana wa Kora
hawakufa. 12 Na wana wa Simeoni kwa jamaa zao; wa
Yemueli, jamaa ya Wayemueli; wa Yamini, jamaa ya Wayamini; na Yakini, jamaa ya
Wayakini; 13 wa Sohari, jamaa ya Wasohari; wa Shauli,
jamaa ya Washauli. 14 Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu
ishirini na mbili elfu na mia mbili. 15 Na wana wa
Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa
Shuni, jamaa ya Washuni; 16 wa Ezboni, jamaa ya
Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri; 17 wa Arodi, jamaa
ya Waarodi; wa Areli, jamaa ya Waareli. 18 Hizi ndizo
jamaa za wana wa Gadi
Ardhi iligawanywa
kwa kura au kwa vipimo, jambo ambalo ni adimu
Kwa watu hawa waliohesabiwa huko Sinai, hawakuwa ni wale wanaume walioachwa wakati wanahesabiwa kwenye uwanda wa Moabu, hesabu ambayo iliwacha Kalebu wana wa Yefume na Yoshua mwana wa Nuni, kwa sababu zake Bwana na kuwa wengine wote wafe wangekufa hakika jangwani.
Hesabu 26:63-65: Hao ndio waliohesabiwa na Musa na Eleazari
kuhani; ambao waliwahesabu wana wa Israeli katika nchi tambarare za Moabu,
karibu na Yordani, hapo Yeriko. 64 Lakini katika watu
hao hapakuwa na mtu hata mmoja wa wale waliohesabiwa na Musa na Haruni kuhani;
waliowahesabu wana wa Israeli katika bara ya Sinai. 65 Kwa
kuwa Bwana alisema juu
Hii ilikususia kwa wote ambao hawakupenda kuingia kwenye Nchi ya Hahadi kwa njia ya ubatizo wa Roho Mtakatifu, kwa kipindi chote cha Yubile arobaini za kanisa kuwa jangwani, kwa kipindi tangu kifo cha Masihi hadi kipindi cha kuja Kwake mara ya pili. Wale ambao hawajatubu na kukubali kubatizwa hawakuingia kwenye nchi ya Israeli na kurithi milki ya Mungu, bali waliangamia jangwani. Na ingawaje wao ni miongoni mwa makabila haya, watu hawa hawataingia kwenye familia ya Mungu hadi kwenye Ufufuo wa Pili.
Kuitii sheria
Taifa limefanywa kwa utaratibu wa familia.
Hesabu 2:34 Ndivyo walivyofanya wana wa
Israeli;
Upatanisho kwa njia ya sadaka ya damu ulifanyika kufuatana na nyuma ya kila familia.
Familia na taifa yanalinwa kupitia na utii wao kwenye sheria hizi za Mungu. Hakuna taifa lililoruhusiwa kuwa liabudu sanamu, na taifa la Israeli ndilo limebahatika kuwa msingi wa sheria hii. Kwa ajili hii, familia za wote wawili, yaani mwanadamu na ya mnyama wanalindwa (Kutoka 23:24-26).
Kutoka 23:26 Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala
aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza
Adhabu waliyoahidiwa itawapata kwa kuabudu sanamu ilikuwa ni kwenda utumwani na kuangamizwa na kufutwa kizazi chao na taifa lao (soma Amosi 5:25-27; pia jarida la Torati na Amri ya Pili (Na. 254) [Law and the Second Commandment (No. 254)].
Torati ilifundishwa kwenye familia na watoto waliiheshimiwa na kuitii tangu wakiwa kwenye umri mdogo wa utoto wao.
Kumbukubu la Torati 32:46: akawaambia, Yawekeni mioyoni mwenu maneno yote ambayo nashuhudia kwenu hivi leo; nayo waamuruni watoto wenu, wayatunze na kuyafanya maneno yote ya torati hii.
Maisha ya kila mmoja wao kwenye familia na taifa yalirefushwa kwa kutilia kwao maanani jambo hili.
Kumbukumbu la Torati 32:47: Kwa maana si jambo lisilofaa kwenu; maana, ni maisha yenu, na kwa jambo hili mtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi mwivukiayo Yordani kuimiliki.
Hii ndiyo kiini msingi cha torati yote na manabii. Torati haipaswi itafsiriwe kwa kufuata mapokeo ya watu (Marko 7:10-13), bali ni kwa mujibu wan eno la Mungu lililonenwa na watumishi wake manabii.
Kikomo cha mamlaka ya mwanadamu
Mamlaka na uweza wote ukiwemo ule aliopewa Masihi, vilitoka nab ado vinatoka kwa Mungu, ikiwa ni hekima na uelewa wake (sawa na Mathayo 21:23; Zaburi 62:11).
Danieli 2:20-22 Danielii akajibu, akasema, Na lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na uweza ni wake. 21 Yeye hubadili majira na nyakati; huuzulu wafalme na kuwamilikisha wafalme; huwapa hekima wenye hekima; huwapa wenye ufahamu maarifa; 22 yeye hufunua mambo ya fumbo na ya siri; huyajua yaliyo gizani, na nuru hukaa kwake.
Mungu Mwenyezi humpa mamlaka na uweza mtu
yeyote anayempenda na
Mungu anapaswa kuheshimiwa na kumtii kwa kila anachokiamuru na hata pale ambapo mapenzi ya wanadamu nayayazidi yale ya Mungu, bado Mungu anapaswa kuheshimiwa na kumtii tu.
Matendo 5:29: Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa
kumtii Mungu kuliko wanadamu
Tendo la kumtii Mungu
Wakati mamlaka ya Mungu inapotolewa na kupewa wanadamu na wakati mfalme anapopewa mamlaka ya kututawala, ndipo mamlaka hii haitakiwi apewe (sawa na Kumbukumbu la Torati 17:14-20 lisemavyo hapo juu). Hakuna mtu aliyetakiwa apewe utawala mpaka awe anaendana na sifa zilizoandikwa kwenye totati ya Mungu. Watoto wake ni lazima pia waendane na kutii amri zilizoandikwa kwenye torati hii.
Maoni na mashauri ya familia yanatakiwa kutafutwa (Mithali 23:22, 25). Familia pia inawajibu wa kutoa masahihisho ya kwanza kikamilifu. Nidhamu na kuuadhisha pia ni wajibu mmojawapo wa familia na sio busara au vema kujiondoa na matendo na kuonyesha ukarimu au kuadhibu kwa kutumia fimbo kwa kumuonya mtoto (Mithali 13:24; 19:18; 23:13-16; 22:15). Kila asikiaye maonyo hupata maarifa na hekima (Mithali 15:32, 33).
Mithali 15:32-33: Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe;
Waebrania 12:11: Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
Marekebisho yoyote
yatakayofanywa kwa vijana yatatapa ijara au malipo yake siku za mbele kwa
mwenendo huo uliorekebishwa. Hali ya kutomrekebisha motto au kijana itasababisha
athari ya jamii yote kuharibika. Tatizo kuu kwenye jamii yetu inayoonekana
ukosefu wa maelekezo au mafundisho ya kibiblia na kutoadibishwa kwenye miaka ya
mwanzoni, na mambo ambayo vijana wanakutana nayo kwenye masomo
Mithali 22:6: Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha,
hata atakapokuwa mzee
Elimu ya kijana haiwezi kupewa kwa wengine kwa mafanikio. Ni wajibu wa wazazi kuwaelimisha na kuwaadibisha watoto wao. Inapotokea kuwa wajibu huu unapoondolewa au kutotiliwa maanani au kudharauliwa, ndipo jamii inapoanza kuwa isiyoaminika nay a watenda maovu.
Mithali 29:15: Fimbo na maonyo hutia hekima;
Na hii ndiyo maana talaka ni jambo la
hatari
Hali hii ya kurekebishwa au kuadibishwa inatakiwa ienee kwa watu wa ngazi zote na umri wote kwenye jamii yetu.
Mithali 1:7: Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa,
Maadili ya watu hutoka kwenye familia na familia inatuama kwenye sheria. Na hii ndiyo sababu moja wapo inayoweka umuhimu wa kusomwa Torati katika mwaka wa saba ambao pia ni wa Sabato.
Kumbukumbu la Torati 4:7-9 Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na
Mungu aliye karibu nao,
Sambamba yake, amri hii inapaswa isomwe kwa kurudiwa rudiwa kwenye familia na kwa wote wanaoishi kwenye nyumba zetu (soma Mithali 4:10).
Kumbukumbu la Torari 6:6-7: Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa
katika moyo wako; 7 nawe
uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na
utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.
Mkakati huu wa kusoma na kufundisha torati unapaswa kufanywa katika kila miaka saba, na unatakiwa ufanywe kwa taifa zima (Kumgukumgu la Torati 31:10-13). Tendo hili la kusoma linafanywa ili kujitathmini matendo yetu yote.
Kuyalinda mazingira pia ni jambo muhimu na
limeagizwa na torati, pasi kujali kwa familia kuwa ni ya wafugaji au la, au ni
kwa muda waliodumu wakizitii sheria na amri hizi za Mungu (Kumbukumbu la Torati 22:6-7). Hii inalenga kote kuwili bila kujali
Mambo ya Walawi 22:28 Tena kama ni ng'ombe, au
Hii inaenda mbali hadi kukataza tendo la kumtoa ndama kwa nguvu anaponyonya maziwa ya mama yake. Hii ni kuonyesha kwa wazi sana kuwa tendo la kupika lilikuwa limekatazwa, kwa kuwa linapingana kabisa na dhana inayohusu familia, pia inaonekana kuwa na uhusiano fulani na mafundisho ya dini ya kipagani ya urutubisho na dini ya mafumbo ya urisi.
Kutoka 23:19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na
kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika
maziwa ya mama yake.
Utaratibu mzima wa
torati unatakiwa ushikwe ili kumfanya kila mtu binafsi na familia waweze kuvumilia
(Kumbukumbu la Torati 4:20).
Kumbukumbu la Torati 5:29: Laiti wangekuwa na moyo kama huu ndani
Amri ya jinsi ya
kuenenda
Kumbukumbu la Torati 7:12-26 inasema: 12 Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiliza hukumu hizi,
na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimilizia agano na
rehema aliyowaapia baba zako; 13 naye atakupenda na
kukubarikia na kukuongeza tena ataubarikia uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi
yako, nafaka zako na divai yako, na mafuta yako, maongeo ya ng'ombe zako, na
wadogo wa kondoo zako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwa atakupa. 14 Utabarikiwa kuliko mataifa yote; hakutakuwa na mtu mume
wala mke aliye tasa kati yenu; wala kati ya wanyama wenu wa mifugo. 15 Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu
yako maradhi yo yote mabaya uyajuayo ya Misri, lakini atayaweka juu ya wote
wakuchukiao. 16 Nawe angamiza mataifa yote atakayokupa
Bwana, Mungu wako; jicho lako lisiwahurumie, wala usiitumikie miungu yao; kwani
litakuwa ni mtego kwako jambo hilo. 17 Nawe kama ukisema
moyoni mwako, Mataifa haya ni mengi kunipita mimi; nitawatoaje katika milki
yao? 18 Usiwaogope; kumbuka sana Bwana, Mungu
wako, alivyomfanya Farao na Misri yote; 19 uyakumbuke
hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na
mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo
atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa. 20 Tena Bwana, Mungu wako, atampeleka mavu kati yao, hata
hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako. 21 Usiingiwe
na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu
mkuu, mwenye utisho. 22 Naye Bwana, Mungu
wako, atayatupia nje mataifa yale mbele yako kidogo kidogo; haikupasi
kuwaangamiza kwa mara moja, wasije wakaongezeka kwako wanyama wa mwitu. 23 Ila Bwana, Mungu wako, atawatoa mbele yako, atawatia
mashaka, mashaka makuu, hata waishe kuangamizwa. 24 Na
wafalme wao atakutilia mkononi mwako, nawe utalipoteza jina lao litoke chini ya
mbingu; hapana mtu atakayeweza kusimama mbele yako, hata utakapokwisha
kuwaangamiza. 25 Sanamu za kuchonga za miungu yao
mtaziteketeza kwa moto; usitamani fedha wala dhahabu iliyo juu yao, wala
usiitwae iwe yako usije ukanaswa nayo; kwa maana ni machukizo kwa Bwana, Mungu
wako; 26 na machukizo usitie ndani ya nyumba yako,
usije wewe kuwa kitu cha haramu mfano wake; ukichukie kabisa, na kukikataa
kabisa; kwa kuwa ni kitu kilichoharimishwa.
Amri hizi walipewa Israeli, kwa kuwa waliokuwa wenyeji asilia wan chi ya Kanaani walikuwa wamelaaniwa kwa ajili ya kuabudu kwao sanamu.
Utaratibu huu wote wa familia, taifa na sheria ulimlenga Masihi, familia ikiwa ni wanaoitunza tu kwa kielelezo.
Yohana 10:7-16 inasema: Basi Yesu aliwaambia
tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo. 8
Wote walionitangulia ni wevi na wanyang'anyi; lakini kondoo
hawakuwasikia. 9 Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa
mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi
nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. 11 Mimi
ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. 12 Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si
Kwa hiyo,
utaratibu wote mzima wa familia na sheria vinakuwa kielelezo cha taifa moja
lililo
Kuiasi sheria au torati
Tendo la kuziasi sheria au totati
kwa familia ni jambo linalopelekea hukumu na hukumu yake ni kifo (Kumbukumbu la
Torati 21:18-23)
Kumbukumbu la Torati 17:6-7: Huyo atakayeuawa na auawe kwa midomo ya mashahidi wawili, au mashahidi watatu; asiuawe kwa mdomo wa shahidi mmoja. 7 Mikono ya wale mashahidi na iwe juu yake kwanza kwa kumwua, kisha mikono ya watu wote. Uondoe vivyo uovu katikati yako.
Familia ilikuwa inapimwa kwa kufuatana na
sheria au torati. Machukizo ya kufanya ukahaba, usagaji na ufiraji yamekatazwa
kufanyika kwenye familia, na kuendelea kuyafanya kumekatazwa kabisa kwa walio
kwenye Nyumba ya Mungu. Hakuna kahaba wala afanyaye ushoga (na mapato
Kumbukumbu la Torati 23:17-18: Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.
Familia yote inawajibika kuisimamia sheria na hukumu ya kifo.
Kumbukumbu la Torati 13:6-10: Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako,
mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au
rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine
usiyoijua wewe wala baba zako; 7 katika miungu ya
mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya
dunia hata ncha ya pili ya dunia; 8 usimkubalie wala
usimsikize; wala jicho lako lisimwonee huruma, wala usimwache, wala usimfiche; 9 mwue kweli; mkono wako na uwe wa kwanza juu yake katika
kumwua, na baadaye mikono ya watu wote. 10 Nawe
mtupie mawe hata afe; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako
aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa,
Masihi alituonyesha mtazamo sahihi wa torati wakati torati ilipokuwa imepotoshwa na kuvunjwa na mapokeo ya Mafarisayo na shule za marabi. Hii ilitokea kwa tendo lake la uponyaji walivyokshutumu kuwa alikuwa anaihalifu au kuivunja torati.
Marko 7:6-13 inasema: Akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi
wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa huniheshimu kwa midomo Ila mioyo
Kwa ajili hii iliwapelekea Yuda na Walawi
kuondolewa mbali ma kwenda utumwani kwa karne kadhaa, nako bado waliendelea na
shingo ngumu wasilisikie neno la Mungu aliye Hai, bali wakajifanyia amri zao
wenyewe zilizoyafuata mapokeo ya wanadamu (Kumbukumbu
la Torati 28:58-68).
Mamlaka kwenye familia
Mamlaka ya kwenye familia hupangiliwa na
baba, ikiwa
Mambo ya Walawi 22:19-20: ili mpate kukubaliwa, mtaleta mume mkamilifu, katika ng'ombe, au katika kondoo, au katika mbuzi. 20 Lakini mnyama ye yote aliye na kilema msimtoe; kwa kuwa hatakubaliwa kwa ajili yenu.
Sisi tu malimbuko
ya Mavuno ya Mungu. Na
Wawakilishi hawa wote wamewekwa kwenye familia na wazazi kwa mfano wa kwanza. Kwa jinsi hii Mungu anawajibika kuwapatia watoto wake kwa sheria zake mwenyewe. Kwa hiyo, Wateule wote anapewa kwa uweza wake wa kuwa anajua kila jambo na uwezo wake wa kila jambo na kwa mapenzi yake na upendo wake mkamilifu. Kiumbe yule ambaye hajuia mambo yote yajayo hawezi kuwa Mungu. Kwa hiyo, Mungu akiwa ni kiumbe anayeyajua mambo yote, amewapa watoto wake upendo wake kamili unaotokana na sheria na Amri Kuu mbili Hesabu 30:1-16 na jarida la Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199) [Lost Sheep and the Prodigal Son (No. 199)].
Mamlaka ya familia yanaanzia kwenye kichwa.
Kwa hiyo nadiri cha mwanamke kinaweza kutanguliwa na yeye aliye kichwa cha
nyumba, kukionekana kuna mgongano fulani wa maslahi ya familia. Kukaa kimya
kutachukuliwa kuwa ni ishara ya kukubaliana na uamuzi huo au utata (
Kumuapia Mungu
Kanisani ni jambo linalotufunga na hukumu yake ni kifo iwapo kama itafanywa kwa
Roho Mtakatifu, kama ilivyowatokea kina Anania na mke wake Safira ambao wote
wawili walikuwa wanajaribu kuvunja sehemu ya nadhiri
Wajibu kwa familia
Wazazi wanawajibika kuitunza familia. Yeye asiyewatunza watu wa nyubani mwake mwenyeweni mbaya kuliko asiye amini. Wajibu huu amepewa baba kwa upande wa kwanza, na mama ni kwa sehemu ya pili, mjukuu ni kwa tatu na hatimaye ni kwa familia yote mzima kama ni ya watu wengi au Kanisa.
1Timotheo 5:1-16 inasema: Mzee usimkemee,
bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; 2 wanawake
wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote. 3 Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli. 4 Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze
kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi
wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu. 5 Basi
yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini
lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku. 6
7 Mambo hayo pia uyaagize, ili wasiwe na lawama.
8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani,
wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu
asiyeamini. 9 Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake
amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja;
10 naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea
watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa
amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema. 11 Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana,
wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa; 12 nao
wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza.
13 Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu,
wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi
na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa. 14 Basi
napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya
nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu. 15 Kwa
maana wengine wamekwisha kugeuka na kumfuata Shetani. 16 Mwanamke
aaminiye, akiwa ana wajane, na awasaidie mwenyewe, Kanisa lisilemewe; ili
liwasaidie wale walio wajane kweli kweli.
Neno
mjukuu (kwenye aya ya 4) ambalo kwa
Kiyunani ni ekgonos, ambalo
limetafsiriwa wapwaze kwenye farisi
ya KJV. Ijulikane kwamba ayah ii ilitafsiriwa kutoka kwenye tafsiri ya
Kiingereza ilikuwa ni kawaida kutumia neno wapwaze walipokuwa wanamaanisha
wajukuu (sawa na kitabu cha Shakespeare cha Othello).
Familia ni mtoaji,
lakini Kanisa familia kamilifu na kiini cha imani. Ni wajibu wa wanawake vijana
kuolewa na kuzaa watoto
Haki ya kuishi kwenye familia
Wajibu wa kulinda maisha kwenye familia
wamepewa wazazi na mara nyingi wajibu huu umehakikishwa na Munbu,
Kutoka 2:1-10 inasema: Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa
binti mmoja wa Lawi. 2 Yule mwanamke akachukua mimba
akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu. 3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha
manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika
majani kando ya mto. 4 Umbu
Mungu wa dunia hii anausongo
Ni wajibu wa familia kulinda uhai wa taifa.
Mungu atatuletea wokovu: Masihi atakuja kuwaokoa wale wote wanaomngojea kwa
hamu kubwa. Hadi kipindi kile, Kanisa litakuwa linapitia kwenye maajaribu
yatakayolifanya kupitia kwenye tanuu la moto wa mateso. Na kila mtoto
atakayeyatishia maisha ya wazazi wake kwa kuhangaikia uhai wake au wa wa mttoto
huyo
Maingiliano ya kijamii
Kila mtu anawajibika kwa nwenendo wake na jinsi ya kuishi kimahusiano kwenye familia yake, awe mwanamke au mwanaume na mfano wa kwanza ukiwa ni mahusiano ya ndani (Kutoka 21:15), na ni kote kuwili, yaani kwenye familia na kwenye jamii ikiwa ni mfano wa pili.
Kutoka 21:17: Yeye amwapizaye baba yake au
mama yake, sharti atauawa.
Mambo ya Walawi 20:9: Kwa maana kila mtu
amlaaniye baba yake au mama yake hakika atauawa, amemlaani baba yake na mama
yake; damu yake itakuwa juu yake
Maelekezo haya yametolewa kwa marudio kwa mara tatu ili kusisitiza umuhimu wake.
Kumbukumbu la Torati 27:16: Na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina.
Umri unapaswa
kuheshimiwa.
Mambo ya Walwi 19:32: Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana.
Kuwalinda waheni
Wana wa Yakobo walikuwa nafsi sabini.
Kipindi cha Musa, wazee hawa waliwakilisha wana wa Yakobo na serikali ya
Israeli. Tunamuona pia Masihi kuwa alikuwa na wanafunzi sabini, na mapepo
waliwatii wakiwa
Ulinzi wa familia kwa
mambo yanayohusu hisia za kimaeneno
Familia ni kiini cha kundi la kabila ambalo
ni utaratibu wa familia enezi. Kwa hiyo, kabila ndilo linalounda taifa makabila
yanalindwa kwenye ardhi zao kwa mujibu wa tirati ya Mungu. Ilinzi huu wa
makabila umeandikwa kwenye kitabu cha Hesabu 27:1-11 kwenye hadithi inayowahusu
mabinti wa Selofehadi. Selofehadi alifia jangwani kwa dhambi zake alizozitenda
mwenyewe na hakuwa wa wana wa kiume. Urithi wake ulilindwa na kupewa binti zake
ambao walikuwa na urithi uliokuwa ni haki
Kwa hiyo, wale walio na urithi wataoa ndani ya kabila la
baba yake, na ndipo kabila na familia italindwa ndani yake (soma Hesabu
36:1-12). Kwa jinsi hii, familia inayotoka Familia ya Kifalme italindwa na ardhi yote itakayotunzwa
kipindi cha Yubile (soma Ezekieli 46:16-18). Hakuna kitakachochukuliwa kwa dhuluma,
na mchakato wake ni endelevu.
Kuwalinda wajane na
yatima
Mungu ndiye Mlinzi wa wale wote wasio na ulinzi na malipo yanafuata toka kwa Mungu.
Yohana 19:26: Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao.
Kwa hiyo Kanisa ndilo lenye wajibu wa kwanza wa familia. Mariamu alikuwa na watoto wa kiume wane na idadi kadhaa ya watoto wa kike wakti Kristo alipomwambia Yohana maneno yafuatayo.
Yohana 19:27: Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.
Nduguyake Kristo alikuja na kujiunga na Kanisa na akafanya mambo makuu akiwa ni mzee wa Kanisa, bali hii haikuathiri msimamo uliowekwa hapa.
Zaburi 68:5-6: Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, Mungu katika
kao
Mungu
atashughulika na mahitaji ya wajane na yatima (soma Isaya 10:2; Yeremia 49:11).
Kwa mujibu wa nabii Ezekieli, Mungu anakemea
Kutoka 22:21-24: Usimwonee mgeni, wala kumtendea jeuri; kwa kuwa
ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri. 22 Usimtese
mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima. 23 Ukiwatesa
watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia
kilio chao, 24 na hasira yangu itawaka moto, nami
nitawaua ninyi kwa upanga; na wake wenu watakuwa wajane, na watoto wenu
mayatima
Kuwalinda wageni na
walioajiriwa kwenye familia ya Mungu
Kuna sheria inayohusu jinsi ya kuwalinda ili wasidhulumiwe watumishi walioajiriwa, kuwaachilia huru watumwa na kusamehe madeni na kuwalinda wageni.
Mambo ya Walawi 25:14-17:
Tena kama ukimwuzia
jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako,
msidanganyane wenyewe kwa wenyewe; 15 kwa hesabu ya miaka
iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na
Kutoka 23:9 Usimwonee mgeni; maana, ninyi mwajua moyo wa mgeni
ulivyo, kwa kuwa ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri
Tuna Baba mmoja
tu, Mungu Maoja aliyetuumba sisi sote (Malaki 2:10). Mungu kama Baba yetu
anawaokoa wana wa Israeli na kuwarrejeza tena kwake (soma Isaya 49:15-26). Hata
maadui zetu wanapaswa kulindwa kutoka kwenye manyanyaso na uovu wao (Kutoka 23:5).
“Basi, mpendeni mgeni, kwa sababu ninyi wenyewe mlikuwa
wageni katika nchi ya Misri.”
Kumbukumbu la Torati 10:18-19 Huwafanyia yatima na mjane hukumu ya haki,
naye humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi. 19 Basi,
mpendeni mgeni, kwa sababu ninyi wenyewe mlikuwa wageni katika nchi ya Misri.
Mambo ya Walawi 19:33-34: Na mgeni akikaa pamoja nawe katika nchi
yako, usimdhulumu. 34 Mgeni
akaaye pamoja nawe atakuwa kama mzalia kwenu; mpende kama nafsi yako; kwa maana
ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri; Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Mataifa
wanaoabudu sanamu wawakuruhusiwa kuachiliwa nyumba zao na iliamriwa watokomezwe
kabisa kutoka kwa wana wa Israeli na wana wa Mungu aliye Hai. (Kumbukumbu la
Torati 7:1-26). Sio kwa kuwa Israeli walikuwa ni wazuri
Mgogoro huu mkubwa
na wa dhahiri kwa kile torati inachotaka unaelekewa
Sheria kuhsu familia na
uthibi wa kijamii kupitia mahakama
Sheria kuhusu familia
ni ya mpango kazi muhimu wa kisheria
Zinaa ipo kwenye
kundi la mambo yanayotoa ruhusa kwa wanandoa kuachana na ni tendo linalouhusisha
mwili ukishiriki na ni sawa na ibada ya sanamu. Nabii Malaki alitumwa Yuda kwa
kuwa katika kpindi hiki taifa lilikuwa limeanza kufanya ibada ya kigeni ndani
ya Israeli na walikuwa wamewaoa binti za Mungu mgeni, jambo lililowapelekea wao
kwenda utumwani. Kwa hiyo, mtazamo wa kila mmoja wetu ni wajibu wa wazazi. Mamlaka
makubwa waliyonayo wazazi na Mungu anayelihukumu taifa na likiwa
Watu waliruhusiwa kuachana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao na hali yao ya kutotahiriwa mioyo yao na kuongoka, na hali ya upotofu wa hisia na fikra zao, lakini haipaswi iwe hivyo kwa wateule.
Maranyingi kuna
viwango aina mbili za ndoa kwenye jamii zetu. Ya kwanza ni ile iliyoko kati ya
wasio batizwa au kati ya mteule na mwanandoa asiyebatizwa bado. Na ya pili ni
ile ya kati ya watu wawili wa imani moja. Mwanzoni kabisa ilionekana kwamba
mapenzi ya Mungu yalikuwa kwamba kila mwanaume awe na mke mmoja tu (Mwanzo
2:24), lakini mtazamo huu ulionekana kuachwa mbali na mababa zetu waliofanya
agano na Mungu. Utaratibu wa kuoa umewekewa mfano wake kwenye uhusiano wa mtu
mmoja na taifa na Mungu, na kwa hiyo uaminifu ni kitu muhimu cha kuangalia
Kwa mujibu wa Torati na tafsiri inayohusinisha na Kristo, kuna mambo kadhaa yanayohitaji kuyatolea maelezo na ufafanuzi kuhusu amri ya saba. Kikomo cha idadi ya wake kwa mwanaume mmoja nawake unaweza kuwa ni mambo yanaendana na jinsi sheria na tatatibu za kila taifa ilivyo. Korani (Qur’an) inafuata mengi yaliyokuwa kwenye mapokeo ya marabi, ambayo yanaweka idadi ya wake wane (baadhi ya marabi walivuka hadi kuchukua wake watano) kwa mtu wa kawaida, na kumi na nane kwa mfalme.
Agano Jipya
linaweka kikomo cha mke mmoja tu kwa mzee wa Kanisa, na kwamba mtu haruhusiwi
kuwa mzee wa kanisa
Uhusiano kwa familia huishia kwenye ndoa, na kwa hiyo ridhiaa ya wazazi inahitajika kwa mujibu wa torati ya Mungu.
Kutoka 22:16-17: Mtu akimshawishi mwanamwali, aliyeposwa na mume, na kulala naye, lazima atatoa mahari kwa ajili yake ili awe mkewe. 17 Ikiwa baba yake huyo mwanamwali akataa kabisa kumpa, atalipa fedha kama hesabu ya mahari ya mwanamwali ilivyo.
Kwa mujibu wa Torati, ridhaa ya wazazi ni
ya muhimu kwa binti
Viapo vya ndoa ni
vikali
Amri ya tano
inamlenga Masihi, anayefanya kazi
“Kiti chako cha enzi, Mungu, Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.” (Zaburi 45:6-7; Waebrania 1:8-9).
Kwake tunatarajia kutoka kwake kichwa hiki cha milele wa familia na mfalme wa amani. Biblia inatuambia kuwa kuna mababa wengi (Waefeso 3:14), na wote wako chini ya Mungu Mmoja na Wapekee wa Kweli (Yohana 17:3).
Sisi ni daraja la
Kristo na chini ya manuni zake tutaielimisha na kuifundisha dunia,
Ni kwa kulielewa hilo tu ndipo tunalazimika kuwa wa familia iliyo ya Mungu, na Mungu akifanya kazi ndani yetu tukiwa kama viumbe wenye mfumo enezi ambao tumeitwa na kufanya kazi kama Mungu, na tunayoyajua malengo ya Amri Kuu nay a Pili inayosema: “Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe” Tumekusudiwa kuwa watu wake Mungu sisi sote ni wana wa yeye Aliye Juu—na Maandiko Matakatifu hayawezi kntanguka (Yohana 10:34-35).
q