Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[270]
Jumbe za Ufunuo 14
(Toleo La 2.0 19981114-20080514)
Jumbe za malaika wanne wa Ufunuo 14 ni
za muhimu katika kutuelekeza na kutuongoza kwenye ujio wa Masihi. Zinabeba
umuhimu wenye maana re katika kutuhabarisha, kutuelekeza, na msukumo au jukumu
la Kanisa katika Siku za Mwisho.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1998, 2008 Wade Cox )
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ufunuo 14 una
jumbe nne za pamoja, ambazo zinahusiana na ujio wa Masihi na harakati za Kanisa
kwa maongozi ya Mungu kupitia Yesu Kristo na watumishi na wahudumu wa mambo ya
rohoni ambao Mungu amempa.
Ujumbe wa tano
unahusu hasira ya Mungu itakayomwagika wakati atakapokuja.
Hehemu ya kwanza inahusisha
wale 144,000 wanaotokea kwenye Mlima wa Sayuni.
Ufunuo 14:1-7 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya
mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake
na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao. 2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji
mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti
ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao; 3 na kuimba
wimbo mpya mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na
wale wazee; wala hapana mtu aliyeweza kujifunza wimbo ule, ila wale mia na
arobaini na nne elfu, walionunuliwa katika nchi. 4 Hawa
ndio wasiotiwa unajisi pamoja na wanawake, kwa maana ni bikira. Hawa ndio
wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko
kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 5 Na katika vinywa vyao
haukuonekana uongo. Maana hawana mawaa. 6 Kisha
nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele,
awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, 7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa
maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi
na bahari na chemchemi za maji.
Ujumbe huu una maana mbili. Unahusu wale 144,000 waliotengwa na kupewa
Masihi na wale waliosimama pamoja nay eye juu ya lima Sayuni. Kwa mtazamo wa
haraka unaweza kuona kana kwamba ni wote wapo pmoja na kwa mahali pamoja na
kwamba tukio hili linaonyesha nyakati za mwisho huko Yerusalemu. Machakato
wenyewe kwa kweli unahusu mwandamano wa matukio ya nyakati tangu kuanza kwa utimilifu
wa unabii ulio kwenye Isaya 61:1-2 uliotimilika mwaka 27 BK na mwisho wa ujio
wake wa pili au ujio wa Masihi.
Isaya 61:1-2 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia
mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga
waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za
kufunguliwa kwao. 2 Kutangaza mwaka wa Bwana
uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;
Kutokana na
maandiko ya tafsiri ya KJV tunaona kwamba huu umeonekana kama Mwaka wa Bwana Uliokubalika, ambao
ilikuwa unamaanisha wa Yubile. Unabii huu kwa kweli ulitimilika mwaka 27 BK
baada ya kujaribiwa kwake jangwani, kulikofuatia baada ya kubatizwa kwake Kristo.
Luka 4:16-21 Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa;
na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake,
akasimama ili asome. 17 Akapewa chuo cha nabii Isaya,
akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa,
18 Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia
mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa
kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, 19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. 20 Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu
wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21 Akaanza
kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.
Kwenye andiko
hili pia alizungumzia kutoka kwenye Isaya 58:6, ambalo lilikuwa ni muunganiko
wa maandiko mawili. (Maandiko yote yameruka maneno kuziponya roho zalizovunjiika yanayopatikana kwenye tafsiri ya KJV;
sawa na kwenye maandiko ya The Companion
Bible kuhusu andiko hili)
Kutoka hatua hii,
katika kukamilisha unabii, anaitangaza pia Yubile. Andiko hili kuhusu Mwaka wa Bwana Uliokubalika ni maelekezo
ya moja kwa moja ya Yubile (sawa na Mambo ya Walawi 25:8-17). Pia kuna swali
kuhusuma andiko haya kwenye Ufunuo 16:7; 18:10; 19:2).
Tumeona kwamba
utaratibu wa Yubile unaweza kujulikana kutoka kwenye Maandiko Matakatifu, kutoka
kwenye maandiko mawili ya Agano la Kale pia. Ka kwanzz kwenye Ezekieli 1:1 ambapo
mwaka wa kumi na tatu umewekwa au kutajwa kama mwaka wa tano wa mambo
aliyoyafana Yehoyakini. Andiko hili linachanganya kidogo tunaposhughulika na
kufafanua kuhusu Adari 2 na kwa hiyo mwaka unaweza kukosewa kirahisi.
Mtajo wa pili
unaonekana kwenye usomaji wa Torati uliofanywa na Ezra na Nehemia. Ili
kulielewa andiko hili sawasawa na wakati wake muafaka, historia ya ujenzi mpya
wa Hekalu inapaswa ieleweke vizuri pia na usomaji ufanyike katika mwaka sahihi.
Jambo hili lote limefafanuliwa kwa kina kwenye majarida ya: Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13); Maana ya
Maono ya Ezekieli (Na. 108) na Usomaji wa
Torati Uliofanywa na Ezra na Nehemia (Na. 250) [The Sign of Jonah and the
History of the Reconstruction of the Temple (No. 13); The Meaning of Ezekiel's Vision (No. 108); and Reading the Law with Ezra and Nehemiah
(No. 250)].
Mchakato huu wa
kipindi unafaa ukiwekwa kwenye dhana halisia kuwa ni mwaka 27 BK unaonyesha
kwamba hii kweli ilikuwa ni Yubile na Kristo alikuwa anatimiza unabii wa Isaya
61.
Hata hivyo, ujumbe
ulio kwanye Ufunuo 14:7 unaelezea jambo lililoelezwa kwenye Isaya kwamba Kristo
hakunukuu na kuendelea mbele katika nyakati za mwisho. Ili kuelewa vyema maana
na matendo ya andiko, tunatakiwa kuandalia kile alichokisema Kristo na maandiko
ya Agano la Kale ambako ndiko alichukua mifano yake.
Luka 4:22-30 Wakamshuhudia wote, wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka
kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu? 23 Akawaambia,
Hapana shaka mtaniambia mithali hii, Tabibu, jiponye nafsi yako; mambo yote
tuliyosikia kwamba yametendeka Kapernaumu, yatende na hapa pia katika nchi yako
mwenyewe. 24 Akasema, Amin, nawaambia ya kwamba,
Hakuna nabii mwenye kukubaliwa katika nchi yake mwenyewe. 25 Lakini,
kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za
Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia
nchi nzima; 26 wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila
kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni. 27 Tena,
palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala
hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu.28 Wakajaa
ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo. 29
Wakaondoka wakamtoa nje ya mji, wakampeleka mpaka ukingo wa kilima ambacho
mji wao umejengwa juu yake, wapate kumtupa chini; 30 lakini
yeye alipita katikati yao, akaenda zake.
Walikuwa na njaa
kwa kuwa kwenye mifano hii miwili alikuwa anaonysha kuwa Kristgo alikuwa
anatangaza wokovu kuwa utakuwa kwa Wamataifa. Mifano yote miwili ilikuwa
inalihusu Kanisa, kama tutakavyojionea. Mfano wa kwanza ulikuwa unamtaja
mwanamke wa Kisidoni aliyebarikiwa na nabii Eliya. Wa pili unamtaja Naaman, mtu
mwenye ukoma Mshami, aliyeponywa na nabii Elisha kwa imani yake.
2Wafalme 5:1-27 Basi Naamani, jemadari wa jeshi
la mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa mbele ya bwana wake, na mwenye
kuheshimiwa, kwa sababu kwa mkono wake Bwana alikuwa amewapa Washami kushinda;
tena alikuwa mtu hodari wa vita; lakini alikuwa mwenye ukoma. 2 Na Washami walikuwa wametoka vikosi, wakachukua mfungwa
mmoja kijana mwanamke kutoka nchi ya Israeli; naye akamhudumia mkewe Naamani. 3 Akamwambia bibi yake, Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na
yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake. 4 Mtu
mmoja akaingia, akamwambia bwana wake, akasema, Yule kijana mwanamke aliyetoka
nchi ya Israeli asema hivi na hivi. 5 Mfalme wa Shamu
akasema, Haya! Basi, mimi nitampelekea mfalme wa Israeli waraka. Basi akaenda
zake, akachukua mikononi mwake talanta kumi za fedha, na vipande vya dhahabu
elfu sita, na mavazi kumi. 6 Akampelekea mfalme wa
Israeli waraka ule, kusema, Waraka huu utakapokuwasilia, tazama, nimemtuma
mtumishi wangu Naamani kwako, ili upate kumponya ukoma wake. 7
Ikawa, mfalme wa Israeli alipousoma waraka, alirarua mavazi yake,
akasema, Je! Mimi ni Mungu, niue na kuhuisha, hata mtu huyu akanipelekea mtu
nimponye ukoma wake? Fahamuni, basi, nakusihini, mwone ya kuwa mtu huyu anataka
kugombana nami.
Kulikuwa na uhaba
au imani ndogo katika Israeli na mfalme aliichukulia hii kama ni chanzo cha
kule chokochoko ya kuanzisha vita na Washami.
8 Ikawa, Elisha, yule mtu wa Mungu, aliposikia kwamba mfalme wa Israeli
ameyararua mavazi yake, ndipo akatuma mtu kwa mfalme, akisema, Mbona umeyararua
mavazi yako? Na aje sasa kwangu mimi, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika
Israeli. 9 Basi Naamani akaja na farasi wake na magari
yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha. 10 Naye
Elisha akampelekea mjumbe, akisema, Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na
nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi. 11 Lakini
Naamani akakasirika, akaondoka, akasema, Tazama, nalidhania, Bila shaka atatoka
kwangu, na kusimama, na kuomba kwa jina la Bwana, Mungu wake, na kupitisha
mkono wake mahali penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma. 12 Je! Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko
maji yote ya Israeli? Je! Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka,
akaondoka kwa hasira.
Watu wengi
hujidhania kuwa wao ni muhimu kuliko wengine na kwamba kuna vitu rahisi
vilivyoko ndani yao. Naamani alitarajia changamoto kubwa kwa kuwa aliyatazama
mambo kwa mtazamo huo. Suala la kumtakasa watu wote lilikuwa rahisi, na
lilikuwa kwenye maji ya uponyaji katika Israeli katika ubatizo wa Roho wa Mungu
kupitia kwa Masihi.
13 Watumishi wake wakamkaribia, wakamwambia, wakasema, Baba yangu, kama yule
nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi,
akikuambia, Jioshe, uwe safi?14 Ndipo akashuka,
akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu;
nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga,
akawa safi. 15 Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na
mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa tazama, najua
ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli; basi nakuomba upokee
mbaraka kwa mtumwa wako. 16 Lakini akasema, Kama Bwana
aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake, sipokei kitu. Akamshurutisha apokee;
lakini akakataa. 17 Naamani akasema; Kama sivyo,
lakini mtumwa wako na apewe mzigo wa udongo wa baghala wawili; kwa maana mtumwa
wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila
kwa Bwana. 18 Jambo hili Bwana amwachilie mtumwa wako;
bwana wangu akiingia nyumbani mwa Rimoni ili aabudu humo, naye akitegemea mkononi
mwangu, nami nikijiinama nyumbani mwa Rimoni, hapo ninapojiinama nyumbani mwa
Rimoni, Bwana amwachilie mtumwa wako jambo hili. 19 Akamwambia,
Enenda kwa amani
Wengi wetu, kama
watumwa wa mfumo huu wa mambo ya dunia, inatupasa kuwa kwenye mazingira ambayo kwayo
tusingeweza kuwepo kwa hali zetu wenyewe tulizonazo.
Basi akamwondokea mbali kidogo. 20 Lakini Gehazi,
mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akasema, Tazama, bwana wangu amemwachilia huyo
Naamani Mshami, asivipokee mikononi mwake vile vitu alivyovileta; kama Bwana
aishivyo, mimi nitamfuata mbio, nipokee kitu kwake. 21 Basi
Gehazi akamfuata Naamani. Naye Naamani, alipoona mtu apigaye mbio anakuja nyuma
yake, alishuka garini amlaki, akasema, Je! Ni amani? 22 Akasema,
Amani. Bwana wangu amenituma, kusema, Tazama, sasa hivi wamenijia kutoka
milimani mwa Efraimu vijana wawili wa wana na manabii; uwape, nakuomba, talanta
ya fedha, na mavazi mawili. 23 Naamani akasema, Uwe
radhi, ukatwae talanta mbili. Akamshurutisha, akafunga talanta mbili za fedha
ndani ya mifuko miwili, na mavazi mawili, akawatwika watumishi wake wawili; nao
wakayachukua mbele yake.24 Naye alipofika kilimani,
alivitwaa mikononi mwao, akaviweka nyumbani; akawaacha wale watu kuondoka, nao
wakaenda zao. 25 Lakini yeye akaingia, akasimama mbele
ya bwana wake. Elisha akamwambia, Watoka wapi, Gehazi? Akanena, Mtumwa wako
hakuenda mahali. 26 Akamwambia, Je! Moyo wangu
haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu
ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na
mizabibu, na kondoo, na ng'ombe, na watumwa, na wajakazi? 27 Basi
ukoma wa Naamani utakushika wewe, na wazao wako hata milele. Naye akatoka usoni
pake mwenye ukoma kama theluji
Gehazi aliadhibiwa
kwa kuwa alijaribu kujipatia faida mbali na utaratibu halali ambavyo ulitolewa
kama lulu visivyo kulipia gharama yoyote. Alipewa mikasa au maradhi ambayo ya
mtu aliyeponywa kwayo. Simon Mchawi pia alijaribu kujipatia faida kutokana na
udhirisho wa uweza wa Roho Mtakatifu, ambao lilipewa Kanisa, na aliondolewa-mbali.
Ukuhani mpya unachukua mahala pa ule wa kwanza.
Hadidhi ya
Naamani iliyofananishwa na wokovu wa Wamataifa Kanisani. Kitendo cha kuingia
majini mara saba kinafananishwa na nguvu ya ubatizo yaliyopewa Makanisa saba na
roho saba za Mungu. Inasemekana kwamba Naamani aliuchukua udongo wa mahala pale
nyumbani, akimaanisha kwamba awe na sehemu ya ardhi ya Israeli na Mlima Mtakatifu
wa kufanyia maombi, inafananishwa na dhana ya kwamba nchi za utawanyiko za
mbali na Sayuni zifanyike kuwa sahihi kwa Mataifa walio uhamishoni mbali, kwa
imani, wawe kama ni Hekalu la Mungu. Ili kulielewa andiko hili kwa usahihi na
ndiyo maana andiko hili limeandikwa kwenye Ufunuo 14:1ff., tunhitaji tuende kwenye
Waebrania 12:1-29.
Waebrania 12:1-29 Basi na sisi
pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke
kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa
saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, 2 tukimtazama
Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya
furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye
ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. 3 Maana
mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi
juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu. 4 Hamjafanya
vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi; 5 tena
mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu,
usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; 6 Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga
kila mwana amkubaliye. 7 Ni kwa ajili ya kurudiwa
mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na
babaye? 8 Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni
fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. 9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili
walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa
roho zetu na kuishi? 10 Maana ni hakika, hao kwa siku
chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili
tuushiriki utakatifu wake. 11 Kila adhabu wakati wake
haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao
waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani. 12 Kwa
hiyo inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza, 13 mkaifanyie
miguu yenu njia za kunyoka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali
kiponywe. 14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu
wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; 15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la
uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa
hilo. 16 Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama
Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja. 17 Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi
baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana
kwa machozi. 18 Maana hamkufikilia mlima uwezao
kuguswa, uliowaka moto, wala wingu jeusi, na giza, na tufani, 19 na mlio wa baragumu na sauti ya maneno; ambayo wale
walioisikia walisihi wasiambiwe neno lo lote lingine; 20 maana
hawakuweza kustahimili neno lile lililoamriwa, Hata mnyama akiugusa huo mlima
atapigwa kwa mawe. 21 Na hayo yaliyoonekana jinsi
yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka. 22 Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu
aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi, 23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa
mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki
waliokamilika, 24 na Yesu mjumbe wa agano jipya, na
damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili. 25 Angalieni
msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye
aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye
atuonyaye kutoka mbinguni; 26 ambaye sauti yake
iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena
nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia. 27 Lakini
neno lile, Mara moja tena, ladhihirisha kuhamishwa vile viwezavyo kutetemeshwa,
kama vitu vilivyoumbwa, vitu visivyoweza kutetemeshwa vikae. 28
Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema,
ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na
kicho; 29 maana Mungu wetu ni moto ulao.
Kutoka kwenye aya
ya 22, tunaona kwamba tangu wongofu hadi kwenye Kanisa la karne ya kwanza,
Wamataifa walikuwa wanaletwa Mlimani na Mjin wa Mungu. Na kwa hiyo, walikuwa
wanaachwa ndani ya Mji na kwenye Mlima Mtakatifu tangu kipindi cha kuongoka
kwao. Mlima ni mfano wa kiroho ambao watakatifu wanasimama kwapo, kwa kipindi
cha zaidi ya miaka elfu mbili ya kuitwa kwao kutoka umataifani. Hawa 144,000 wamejumuishwa
kwenye uongozi imara. Pia hawa 144,000 wamejumuishwa kwenye baraza la wazee 72
(sawa na isemavyo Hebdomekonta[duo]ya maandik
o kwenye Luka 10:1,17). Hili lilikuwa ni Baraza la wazee sabini. Baraza la Sanhedrin
katika Israeli liliwekwa mbadala na Sanhedrin ya Kanisa tangu kuwekwa wakfu kwao
na Kristo, na kwa uweza wa Roho Mtakatifu tangu Pentekoste. Walikuwa na mamlaka
juu ya mapepo tangu kuchaguliwa na kuwekwa wakfu kwao. Tangu Pentekoste, Wana
wa Skewa, japo walikuwa ni watoto wa Kuhani Mkuu, hawakuwa na uwezo wowote wa
kuwakabili Malaika hawa Waovu au mapepo (Matendo 19:14 ff.).
Hawa wazee 72 wanawakilisha
dhabihu kuu ya mwaka wa kinabii ambao ni sawa na Sabato 52, Miandamo ya Mwezi
na sadaka za Sikukuu, amoja na Mganda wa Kutikiswa.
Mkutano au umati
Mkuu unaoonekana kwenye Ufunuo 7:9. Unawakilisha sadaka za daima, lakini hakuna
mtu anayeweza kuwahesabu.
Jumbe za Ufunuo 14
ni uwajibiko wa wale 144,000. Jumbe walizopewa hawa 144,000 zinaenda hadi
kwenye kipindi cha zama saba za makanisa zilizotolewa kwene Ufunuo sura za 2 na
3. Miaka elfu mbili kwa kipindi chote cha Yubile arobaini yangu mwaka 27 BK hadi
2027 BK.
Malaika wa Kwanza
ni Injili ya Milele ambayo itatolewa kwa kipindi hadi nyakati za mwisho.
Mwishoni, utimilifu au hitimisho la Ujumbe wa Isaya 61:1-2 umetolewa (sawa na
Ufunuo 14:1-7).
Unabii ulinenwa
na Isaya ulinenwa na Masihi na uliishia kwa sehemu kwenye Isaya 61:2, kwa
maandiko yote, kwa kuwa mwisho wa unabii unatokea mwishoni mwa zama au
ukamilifu wa dahari.
Isaya 61:2-7 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha
Mungu wetu; kuwafariji wote waliao; 3 kuwaagizia hao
waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha
badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya
haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe. 4 Nao
watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa
zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya
kizazi. 5 Na wageni watasimama na kulisha makundi yenu,
na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu
yenu. 6 Bali ninyi mtaitwa makuhani wa Bwana; watu
watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia
utukufu wao. 7 Badala ya aibu yenu mtapata maradufu,
na badala ya fedheha wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki
maradufu; furaha yao itakuwa ya milele.
Ili kuelewa zama
hizi kwa kina tunahitajika kuendelea kwenye Ujumbe wa Malaika wa Pili.
Sehemu ya II
Ujumbe wa Malaika wa
Pili
Ujumbe wa Malaika
wa Pili unaonyesha Ujumbe wa Malaika wa Kwanza. Ni matokeo ya kuondolewa kwa
Ujumbe wa Malaika wa Kwanza ili Ujumbe wa Malaika wa Pili uweze kutolewa kwa
uhakika na mafanikio. Mwishoni mwa shughuli ya kuwtia mhuri hawa 144,000, Dunia
itapitia maumivu makali.
Habari kamili
kuhusu jinsi hili litakavyotokea imechambuliwa kwa kina kwenye maandiko mengine
ya Ufunuo na kwingineko.
Mfumo na dini
yote ya Kibabeloni vitashamiri katika Siku za Mwisho kabla ya kipindi cha
mwisho.
Ufunuo 14:8 Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka,
umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote
mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake.
Huyu ndiye Yule
Kahaba Mkuu anayeyaendesha au kuyaongoza mataifa na ametajwa kwenye Ufunuo 17. Ataangamizwa
na umoja au muungano wa wafalme kumi ambao watapokea mamlaka kwa saa moja na
Mnyama, katika Siku za Mwisho (Ufunuo 17:12-18).
Saa hili la
kinabii, ni kipindi kifupi sana kitakachotokea. Kinaweza kutokea kwa mtindo wa
kweli wa masaa ishirini na manne tunayoyajua na sehemu ya ishirini na nne ya
siku ya mwaka wa kinabii – kama majuma mawili, nk. Au kinaweza kuwa ni kipindi
kitakachokuwa chini au ndani ya mwaka mmoja. Lakini, hata hivyo, ni muda mfupi
ambacho nabii hizi na nguvu hizi zitajikusanya ama kutokea kwa pamoja. Nguvu ya
uharibifu ya mifumo au dini hii ni kubwa. Inafanya uharibifu kama uliofanyika
kwene Vita Kuu ya II ya Dunia ya miaka sita, basi itakuwaje itakapofanyika kwa
kutumia zana za nyukilia kwa mwaka mmoja?
Ili kujua kile
kinachotokea inatubidi tuende kwenye hadithi ya Gideon, Gideon alisimama
katikati ya imani ya dini ya Baali na alikuwa ni mtu wa kutegemewa na kutizamwa
na wengi, kama dini na mfumo huu utakavyokuwa na kuonekana katika Siku za
Mwisho.
Waamuzi 6:32-40 32 Basi akamwita Yerubaali siku
hiyo, akisema, Baali na atete naye kwa ajili ya nafsi yake, kwa sababu
ameibomoa madhabahu yake. 33 Wakati huo Wamidiani na
Waamaleki, na hao wana wa mashariki walikutana pamoja; wakavuka na kupanga hema
zao katika bonde la Yezreeli. 34 Lakini roho ya Bwana
ikaja juu yake Gideoni; naye akapiga tarumbeta; na Abiezeri walikutanika na
kumfuata. 35 Kisha akatuma wajumbe waende kati ya
Manase yote; wao nao walikutana pamoja ili kumfuata; kisha akatuma wajumbe
waende kwa Asheri, na kwa Zabuloni, na kwa Naftali; nao wakakwea ili kumlaki. 36 Gideoni akamwambia Mungu, Ikiwa wewe utawaokoa Israeli
kwa mkono wangu, kama ulivyosema, 37 tazama, nitaweka
ngozi ya kondoo katika kiwanja cha kupuria; na kama ukiwapo umande juu ya ngozi
tu, na nchi yote ikiwa kavu, basi, hapo ndipo nitakapojua ya kuwa utawaokoa
Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema. 38 Ikawa
hivyo; kwa maana aliondoka asubuhi na mapema, akaikamua ile ngozi, akautoa ule
umande katika ile ngozi, bakuli zima la maji. 39 Gideoni
akamwambia Mungu, Hasira yako isiwake juu yangu, nami nitasema mara hii tu;
nakuomba, nijaribu kwa ngozi hii mara hii tu; sasa ngozi tu na iwe kavu, na uwe
umande juu ya nchi yote. 40 Mungu akafanya hivyo usiku
ule; maana ile ngozi tu ilikuwa kavu, napo palikuwa na umande juu ya nchi yote.
Gideon, au Yerubaali,
alipindua madhabahu ya Baali na alipewa amri kujaribu au kuthibitisha mapenzi
ya Bwana.
Akiwa na Wenzake,
aliwakusanya pia wale waliokwua katika Asheri na Zabuloni na Naftali. Hii pia
inahusiana na kufanana na Siku za Mwisho na kazi za makabila haya kwenye
mchakato huu. Mbali na makabila haya walichaguliwa wale ambao walitumiwa na
Mungu.
Waamuzi 7:1-25 Kisha Yerubaali,
yaani Gideoni, na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaondoka na mapema, wakapiga
kambi yao karibu na kijito cha Harodi; na kambi ya Midiani ilikuwa upande wao
wa kaskazini, karibu na mlima wa More, bondeni. 2 Bwana
akamwambia Gideoni, Watu hawa walio pamoja nawe ni wengi mno hata nikawatie
Wamidiani katika mikono yao, wasije Israeli wakajivuna juu yangu wakisema,
Mkono wangu mwenyewe ndio ulioniokoa. 3 Basi sasa
enda, tangaza habari masikioni mwa watu hawa, na kusema, Mtu awaye yote
anayeogopa na kutetemeka, na arudi aondoke katika mlima wa Gileadi. Ndipo watu
ishirini na mbili elfu wakarudi katika watu hao, wakabaki watu elfu kumi. 4 Bwana akamwambia Gideoni; Hata sasa watu hawa ni wengi
mno; uwalete chini majini, nami nitawajaribu huko kwa ajili yako; kisha itakuwa
ya kwamba yule nitakayekuambia, Huyu atakwenda pamoja nawe, ndiye atakayekwenda
pamoja nawe; na mtu yule nitakayekuambia, Huyu hatakwenda pamoja nawe, basi mtu
huyo hatakwenda. 5 Basi akawaleta watu chini majini.
Bwana akamwambia Gideoni, Kila mtu atakayeyaramba maji kwa ulimi wake, kama
vile arambavyo mbwa, huyo utamweka kando; kadhalika kila mtu apigaye magoti
kunywa. 6 Na hesabu ya hao waliokunywa kwa
kuramba-ramba, wakipeleka mkono kinywani, ilikuwa watu mia tatu; bali watu
wengine wote walipiga magoti kunywa maji. 7 Bwana
akamwambia Gideoni, Kwa watu hawa mia tatu walioyaramba maji nitawaokoa, nami
nitawatia Wamidiani katika mikono yako; lakini watu hawa wote wengine na waende
zao, kila mtu mahali pake. 8 Basi wale watu wakachukua
vyakula vyao mikononi mwao, na tarumbeta zao; naye akawapeleka watu wote wa
Israeli, kila mtu hemani kwake; bali aliwazuia wale watu mia tatu; na kambi ya
Wamidiani ilikuwa chini yake, bondeni.
Kutokana na
uchaguzi huu, kupunguzwa kwa idadi ya watu kulifanyika. Hii ilfanyika ili
ushindi usichukuliwe kuwa umetokana na uweza
bali ni kwa roho wake, asema Bwana wa Majeshi (Zekaria 4:6).
Jaribio lilikuwa
ni kupambanua katika Roho Mtakatifu. Maji yalikuwa ni mfano wa Roho Mtakatifu
alitenda kazi zake kupitia kwa Yesu Kristo. Namna waliyochukulia ilionyesha
mpambanuo ulioonyesha kumjua Mungu Mmoja na Wapekee wa Kweli na Yesu Kristo
aliyemtuma (Yohana 17:3).
Makundi matatu
yaliundwa kutoka kwenye kundi ambayo yalikuwa yamechaguliwa kutok kwenye kundi
ambalo limepunguzwa tayari, ikimaanisha sio Israeli wote wameitwa. Wale
waliorepotiwa kazini ndio walioitwa. Thelathini na mbili elfu waliripoti kwenda
vitani na, kwa mujibu wa Torati kutokana na maagizo ya Kumbukumbu la Torati 20,
wale waliokuwa wanaogopa kwenda vitani waliruhusiwa warudi majumbani kwao. Watu
elfu kumi walijiondoa na kurudi nyumbani. Waliobakia hatimaye wakapewa jaribio
la kwenye maji mtoni. Ndipo hatimaye watu 300 tu walibakia.
Jambo la ajabu na
la tofauti hapa lilikuwa ni tofauti kati ya 4 kwa 1.waliongezeka dhidi yao hadi
watu 13 kwa 1, na kisha hadi kufikia watu 450 kwa 1.
Tofauti ya mwisho
kiuwiano ilikuwa kubwa sana sawa na idadi ya makuhani wa Baali waliokuwa
wanakula mezani kwa Yezebeli, kwenye
dini yao, wakati Eliya alikabiliananao peke yake (1Wafalme 18:19). Pia Eliya
alikabiliana na manabii mia nne wa ashera. Miingano huu unamaana yake, hata
hivyo, kwa kuwa ni Kahaba Mkuu atakayepinduliwa na kuangamizwa katika Siku za
Mwisho.
Roho hii ya Eliya
inatendakazi kwene Kanisa na mfumo au imani yake yote linaporuka na kuendelea
kupambana dhidi ya mfumo au imani ya dini ya uwongo kwa kipindi cha zaidi ya
miaka elfu mbili. Ni katika Siku za Mwisho tu ndipo litafanikiwa, na pia sio
kikamilifu kwa matendo yake lenyewe.
9 Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Ondoka, shuka kambini; maana nimeitia
katika mikono yako. 10 Lakini, ukiogopa kushuka, shuka
pamoja na Pura mtumishi wako kambini; 11 nawe utasikia
wanayoyasema, na baada ya haya mikono yako itatiwa nguvu; ushuke kambini. Ndipo
akashuka pamoja na Pura mtumishi wake hata kufikilia mwisho wa watu wenye
silaha waliokuwa kambini. 12 Nao Wamidiani na
Waamaleki na, hao wana wa mashariki walikuwa wametua bondeni, mfano wa nzige
kwa wingi; na ngamia zao walikuwa hawana hesabu; mfano wa mchanga wa ufuoni,
kwa wingi. 13 Hata Gideoni alipofika, tazama, palikuwa
na mtu mmoja aliyekuwa akimhadithia mwenziwe ndoto, akasema, Tazama, naliota
ndoto, na tazama, mkate wa shayiri ulianguka katika kambi ya Wamidiani, ukafika
hata hema moja, ukaipiga hata ikaanguka, nao ukaipindua, hata ikalala chini. 14 Mwenzake akamjibu akasema, Habari hii haikosi kuwa upanga
wa Gideoni, mwana wa Yoashi, mtu wa Israeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi
lote katika mkono wake.
Unabii huu
ulitolewa na Mungu kwenye mikono ya adui na wakapunguzwa nguvu kabisa nao, ili
waweze kutiwa moyo wakati adui akiwa amekata tamaa.
15 Ikawa, aliposikia habari ya ile ndoto, na kufasiriwa kwake, akasujudu;
akarudi katika jeshi la Israeli akasema, Inukeni, kwa maana Bwana amelitia
jeshi la Midiani mikononi mwenu.16 Kisha akawapanga
wale watu mia tatu wawe vikosi vitatu, akatia tarumbeta katika mikono ya watu
wote, na mitungi isiyo maji, na mienge ndani ya hiyo mitungi. 17 Akawaambia, Nitazameni, mkafanye kama nifanyavyo mimi;
angalieni, nitakapofika mwisho wa kambi, itakuwa, nifanyavyo mimi nanyi fanyeni
kadhalika. 18 Nitakapopiga tarumbeta, mimi na wote
walio pamoja nami, basi ninyi nanyi zipigeni tarumbeta pande zote za kambi,
mkaseme, Kwa Bwana, na kwa Gideoni. 19 Basi Gideoni,
na wale watu mia waliokuwa pamoja naye, wakafika mwisho wa kambi, mwanzo wa
zamu ya kati, wakati walipokuwa wamebadili wenye zamu; wakazipiga hizo
tarumbeta, wakaivunja vipande vipande ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao. 20 Vile vikosi vitatu wakapiga tarumbeta, wakaivunja
mitungi, wakaishika mienge kwa mikono yao ya kushoto, na zile tarumbeta katika
mikono yao ya kuume ili kuzipiga; wakapiga kelele, Upanga wa Bwana na wa
Gideoni. 21 Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka
kambi pande zote; jeshi lote wakakimbia; nao wakapiga kelele, wakawakimbiza. 22 Wakazipiga zile tarumbeta mia tatu, naye Bwana akaufanya
upanga wa kila mtu uwe juu ya mwenziwe, na juu ya jeshi lote, jeshi likakimbia
mpaka Bethshita, kuendelea Serera, hata mpaka wa Abel-Mehola, karibu na
Tabathi.23 Wanaume wa Israeli walikuwa wamekusanyika
kutoka Naftali, na kutoka Asheri, na kutoka Manase yote, wakawafuata Midiani.
Akiwa na wanaume
mia tatu aliwapanga kwa uzuri na kwa makini kwenye makundi matatu, na
akafanikiwa kufanya jambo la kushangaza. akisaidiwa na \mungu mwenye nguvu
aliwaondoa woga mioyoni mwao na akawasababisha wafanye mauaji makuu kwa adui
mmoja baada ya mwingine.
Kisha Waefraimu
wakaitwa kama kundi kuwashughulikia na walijisikia uchungu kuachwa nje ya tukio
hili. Hata hivyo, unabii mwingine ulionyesha dalili ya kwamba Dani/Efraimu pia
walihusika kwenye harakati hizi za kuwaonya
watu duniani katika Siku za Mwisaho (Yeremia 4:15) (sawa na jarida la Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44) [The Warning of the Last Days (No. 44)].
24 Kisha Gideoni akapeleka wajumbe katika nchi yote ya vilima vilima ya
Efraimu, akisema, Haya, telemkeni juu ya Midiani, na kuyashika hayo maji mbele
yao, mpaka Bethbara, maana, huo mto wa Yordani. Basi watu waume wote wa Efraimu
walikutana pamoja, wakayashika maji mpaka Bethbara, maana, huo mto wa Yordani. 25 Wakawashika hao wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu;
wakamwua huyo Orebu pale penye jabali la Orebu, na huyo Zeebu wakamwua hapo
penye shinikizo la divai la Zeebu, kisha wakawaandamia Wamidiani; vichwa vya
Orebu na Zeebu wakamletea Gideoni huko ng'ambo ya pili ya Yordani.
Kwa hiyo, dini ya
Baali katika siku za mwisho imepinduliwa na kuangushwa. Lakini ni kina nani
basi hawa manabii wa Baali katika siku za mwisho? Ni rahisi kuwajua kutokana na
maandiko ya bibliaical text.
Ni makasisi
waliovaa mavazi meusi. Inawezakuwa ndiyo utambulisho wao wa kimavazi kwenye
milenia.
Sefania 1:4 4 Nami nitaunyosha mkono wangu juu ya
Yuda, na juu ya watu wote wakaao Yerusalemu; nami nitayakatilia mbali mabaki ya
Baali, yasionekane mahali hapa, na hilo jina la Wakemari pamoja na makuhani;
Ni rahisi mno
kuona kwenye tafsiri ya KJV.
Sefania 1:4 4 Nami nitaunyosha mkono wangu juu ya
Yuda, na juu ya watu wote wakaao Yerusalemu; nami nitayakatilia mbali mabaki ya
Baali, yasionekane mahali hapa, na hilo jina la Wakemari pamoja na makuhani;
Je, ni kina nani
huyu Mkerani? Neno hili limeachwa pasi kutafsiriwa kwenye tafsiri ya
KJV, na linalenga makasisi waabudu sanamu
kwenye tafsiri ya RSV, kwa kuwa inamaanisha moja kwa moja mwene vazi jeusi; na tafsiri iliyo kwene KJV wote ni sehemu ya
makasisi au makuhani wa dini yenye mavazi meusi, kwa hiyo, ni kwa makusudi kabisa
imeacha bila ya kutafsiriwa. Bullinger ana la maana aliloandika kuhusiana na
tafsiri ya The Companion Bible.
Maandiko kwenye Hosea 10:3 pia yameachwa bila kutafsiriwa, kama yalivyo kwenye 2Wafalme
23:5.
Hosea 10:3-5 Yakini sasa watasema, Hatuna mfalme; kwa maana hatumchi Bwana;
na mfalme huyu je! Aweza kututendea nini? 4 Hunena
maneno yasiyo na maana; huapa kwa uongo wafanyapo maagano; basi ndipo hukumu
huchipuka kama mbaruti katika matuta ya shamba. 5 Wakaao
Samaria wataona hofu kwa ajili ya ndama za Beth-Aveni; kwa maana watu wa mji
huo wataulilia, na makuhani wake walioufurahia, kwa sababu ya utukufu wake; kwa
maana umetoweka.
Neno makuhani lililopo kwenye aya ya 5 kwa
kweli linamaanisha Kemarim au Chemarim, linalomaanisha mwenye vazi jeusi. Neno hili mara zote limekuwa halieleweki kuwa linamaaiisha
makuhani wa Baali, ndiyo peke yao waliokuwa wanavaa mavazi au majoho haya meusi.
2Wafalme 23:5 Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme
wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya
Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia
uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni.
Makuhani waabudu
sanamu wanaoonyeshwa hapa ni sawa tu na Kemarim aliyeko kokote kule.
Wanachukuliwa kama makuhani waabudu sanamu ili kuficha ukweli wa mambo.
Makuhani au makasisi wanaomtumikia Mungu wa Pekee na wa Kweli, kamwe hawakuvaa
na hadi sasa havai majoho meusi. Mara zote walivaa meupe.
Wenye majoho
meusi wamekuwa wakijaribu kuumiliki Yerusalemu tangu kipindi Daudi alipoingia
humo mwaka 1005 KK nab ado wangaliko kule wakijaribu kufanya hivyo.
Katika Siku za
Mwisho, makuhani wavaa majoho meusi wa Mwanamke Kahaba wataangamizwa, na
kuondolewa usoni pa Dunia kabla ya utaratibu na dini ya Masihi haijachukua
mkondo wake kikamilifu, na kazi hiyo itafanywa na utawala wa Mnyama ambao
alijaribu kuumiliki.
Ni jukumu na kazi
ya Kanisa kuhubiri Ujumbe wa Malaika wa Kwanza na kuifunua dini na itikadi hii
katika Siku hizi za Mwisho kwenye Ujumbe wa Malaika wa Pili (sawa na isemavyo
Ufunuo sura ya 17 na 18).
Ujumbe wa Malaika wa
Tatu
Ufunuo 14:9-20 9 Na mwingine, malaika wa tatu,
akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na
sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono
wake, 10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu
ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira
yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele
za Mwana-Kondoo. 11 Na moshi wa maumivu yao hupanda
juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo
huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake. 12 Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao
amri za Mungu, na imani ya Yesu. 13 Nikasikia sauti
kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam,
asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana
nao.
Mazingira hapa ni
kwamba Mnyama ataweka mfumo utakaofanya maangamizo ya wazi kati ya Mungu na
mfumo au dini yake na ule wa kishetani wa Mnyama. Sehemu kubwa ya dunia
inaonekana kufuata ama kwenda kwenye mfumo au dini hii.
Uvumilivu wa
watakatifu umetolewa nwito kuwepo, na tofauti ya alama ya watakatifu ni amri za
Mungu na imani ya Yesu. Imani
ya Kristo ni ile kwamba hakupenda maisha yake hadi kufa. Na ndivyo ilivyo pia
kwa wateule tutapitia mateso katika nyakati hizi za mwisho. Msimamo huu wa
mwisho wa dola ya Mnyama utakuwa ni tukio kuu sana la kuifunga kinywa dunia yote.
14 Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na
juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu
ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali. 15 Na
malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa
ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna
imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa. 16 Na yeye
aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa. 17 Kisha malaika mwingine akatoka katika lile hekalu
lililoko mbinguni, yeye naye ana mundu mkali. 18 Na
malaika mwingine akatoka katika ile madhabahu, yule mwenye mamlaka juu ya moto;
naye akamlilia kwa sauti kuu yule mwenye mundu ule mkali, akisema, Tia mundu
wako mkali, ukachume vichala vya mzabibu wa nchi, maana zabibu zake zimeiva
sana. 19 Malaika yule akautupa mundu wake hata nchi,
akauchuma mzabibu wa nchi, akazitupa zabibu katika shinikizo hilo kubwa la
ghadhabu ya Mungu. 20 Shinikizo lile likakanyagwa nje
ya mji, damu ikatoka katika shinikizo mpaka kwenye hatamu za farasi, kama
mwendo wa maili mia mbili.
Mambo haya mawili
yanaonyesha mavuno ya Mwana wa Adamu, ambayo ndiyo mavuno ya mwisho, na kisha
mavuno ya shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu.
Kuna matukio mawili tofauti kwene jumbe mbili tofauti na viumbe. Ziko kwene
maelekezo na maongozi ya Mungu, ambayo yanaonyesha matukio mawili kwenye
matukio maalumu zinazochukuliwa na wajumbe au malaika wawili kwa nyakati
tofauti.
Kwa hiyo, imani
katika Siku za Mwisho imefunuliwa kupitia mchakato wa mafundo manne unaohitiisha
Siri za Mungu.
Ujumbe wa Malaika
wa Kwanza ni Injili ya Milele na kama ilivyo, haihitajiki kuibadilisha, na ina
muundo na utaratibu ule ule tangu kipindi cha Kristo na Mitume. Kwa hiyo
haiwezi kuwa ni imani ile ya makanisa makongwe ya kale inayotuama au kwendana
na mafundisho potofu ya wanadamu au yaliyotungwa na Mabaraza ya Makanisa.
Ujumbe wa Malaika
wa Pili unauvunjavunja mfumo na dini ya Kibabeloni. Ujumbe ule unatuama au
kujengwa juu ya kazi ya mwisho ya Injili yote iliyo kwenye Ujumbe wa Malaika wa
Kwanza.
Ujumbe wa Malaika wa Tatu unatoa maonyo juu ya mfumo au dini ya Mnyama,
ambaye atamuangamiza Mwanamke Kahaba.
Jumbe za Malaika wa Nne
na wa Tano
Ujumbe wa Malaika wa Nne una sehemu mbili, ya kwanza ikiwa ni mavuno au
mshahara wa (mtu ambaye kuonekana kwake ni kama) Mwana wa Mungu).
Sehemu ya Pili ya
Ujumbe wa Malaika wa Kwanza ni shinikizo la kikombe cha ghadhabu ya Mungu.
Kwa michakato hii
ya jumbe tano, ndipi kipindi cha Milenia kitafunika jumla ya miaka 1,000-ya
utawala wa Kristo.
Soma pia majarida
yafuatayo:
Vita Kuu ya III ya
Dunia: Sehemu ya I Dola ya Mnyama (Na. 299A) [World War III: Part I The Empire of the Beast (No. 299A)]
Vita Kuu ya III ya Dunia: Mwanamke Hakaba na
Mnyama (Na. 299B) [WWIII Part
II: The Whore and the Beast (No. 299B)]
Mwaka 2012 na Mpingaktisto )Na. 299D)
[2012 and the Antichrist (No. 299D)]
Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300) [The Golden Jubilee and the Millennium
(No. 300)]
q