Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[CB20b]

 

 

 

 

Jinsi ya Kuipangilia

Kalenda ya Mungu

 

(Toleo La  1.0 20061106-20061106)

 

Jarida hili linaelezea kanuni na taratibu za kuhesabu zilizotumika kuziweka au kuzipangilia siku na tarehe za Kalenda Takatifu ya Mungu.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Sheria ya Hatimiliki © 2007 Jacques Guérard, ed. Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Jinsi ya Kuipangilia Kalenda ya Mungu


 

Kwenye jarida hili tutaonyesha kanuni ya msingi, taratibu na jinsi ya kuhesabu kukovyotumiwa ili kupata msingi wa kuamua jinsi ya kuipangilia Kalenda Takatifu ya Mungu na jinsi ya kuupata mwezi wa Kwanza wa Mwaka Mpya kwa mujibu wa vipindi vya mpito vya vipindi vya kutoonekana mwezi vya Mwezi Mpya vya taasisi ya elimu ya mambo ya anga na nyota. Mizunguko hii ya mwezi imeainishwa vyema na dondoo zote za kimahesabu zinaweza kupatikana kwenye vyanzo rasmi vya kisayansi kama vile taasisi ya NASA na nyinginezo. Maana na tafsiri ya maneno yaliyotumika kwenye kuamua mpangilio wa kalenda yametolewa mwishoni mwa jarida ili kuyaona na kuyasoma kiurahisi.

 

Kalenda ya Mungu inakwendana na Uumbaji wake – kwa kuweka mianga midogo na mikubwa. Haitegemei waka kutuama kwenye kitu kingine chochote kilichotengenezwa na mwanadamu, kama vile kwenye kalenda ya Kigregoriani au kalenda ya Kiyahudi ya Hilleli. Kalenda ya kweli ya Mungu inashabihiana na mwandamo na mzunguko wa mwezi, kwa hiyo inaendana na mizunguko ya mwezi, ambavyo ni, mzunguko wa mwezi mwandamo. Ili kujifunza kwa kina kuhusu Kalenda hii ya Mungu, tafadhali soma majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. CB20) na Siku Takatifu za Mungu (Na. CB22).

 

Kwanza kabisa, tutaona majedwali fulani kadhaa na dondoo za vipindi vya mpito vya muunganiko kati ya miezi na siku za kulingana masaa usiku na mchana za majira ya baridi yaliyopo kutokana na utambuzi wa mamlaka maalumu ya kisayansi. Pili, tutatathimini kanuni za msingi ili kupangilia siku za Miandamo ya Mwezi Mpya za kuzishika baada ya kuzipata siku hizo kutoka kwenye taasisi ya Saa za Ulimwengu mzima zijulikanazo kama Universal Time (au Greenwich Mean Time) na kuziweka kwenye saa za kimahalia za Yerusalemu. Tatu, tutaziona dondoo za ikwinoks ya majira ya baridi ili kupangilia tarehe au siku ya kuutangaza Mwaka Mpya au mwanzo wa mwezi wa Kwanza majira ya baridi.

 

Kutangazwa kwa tarehe au siku ya Mwezi Mpya kwenye maeneo yote mahalia na makanisa yaliyoko ulimwenguni kote kunategemea na siku ya Mwezi Mpya na Siku Takatifu wakati kunapozama juna na kuanza giza kwetu sisi mahali popote tunapoishi.

 

Isaya 2:3 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu. (sawa pia na  Mika 4:2).

 

MAJEDWALI NA DONDOO

 

1. VIPINDI VYA MUUNGANIKO WA MIEZI, MIAKA YA 2001-2100 BK

 

Tuna chanzo cha kuzipata siku za miunganiko ya mwezi mmoja hadi mwingine kwenye tovuti ifuatayi na taasisi ya NASA ifuatayo: http://aa.usno.navy.mil/data/docs/MoonPhase.html

 

Tarehe zote zimeandikwa kwa kufuata kalenda ya Kigregorian na masaa yameandikwa kwa kufuata majira ya Saa za Ulimwengu zijulikanazo kama Universal Time (yaani mstari wa Greenwich). Dondoo hizi zimetumika katika kuipangilia siku ya kwanza ya mwezi mpya kwenye Kalenda ya Mungu.

 

2. IKWINOKS ZA  MAJIRA YA BARIDI ZA MIAKA YA 1992-2020 BK

 

Ikwinoks ni wakati ambao jua linapita au kukatiza Dunia kwenye mstari wa Ikweta, ambapo inafanya usiku na mchana Ulimwenguni kote kuwa sawasawa masaa au urefu wake. Tukio hili hutokea kwenye tarehe za March 20 au 21 na pia tarehe 22 Septemba. Ikwinoks inatusaidia kupangilia kuanza kwa mwaka. Kama saa 9:00 alasiri. Dhabihu ya siku ya 14 Abibu haifanyiki au kutolewa hadi baada ya ikwinoks ya majira ya baridi, tunafanya nyongeza au kuongeza mwezi wa 13.

 

Chanzo cha dondoo za ikwinoks za majira ya baridi zinapatikana kutoka kwenye tovuti ifuatayo ya taasisi ya Jeshi la Marekani ifuatayo: http://aa.usno.navy.mil/data/docs/EarthSeasons

 

Kufuatia kanuni hiyohiyo kwa ajili ya Miandamo ya Mwezi Mpya kama ilivyo hapo juu 20 March, kwa mujibu wa ainisho la Mungu.

 

3. DONDOO YA MAJIYA AU MASAA YA EENT HUKO YERUSALEMU

 

Neno la Mwisho wa Majira ya Jua Kuchwa Jioni, au End Evening Nautical Twilight (EENT) ni neno la kisayansi la kipindi halisi ambacho giza linaanza upande fulani maalumu. Muda huu ni wakati siku mpya inaanza na siku iliyopita inaisha kwa mujibu wa uumbaji wa Mungu. Soma jarida la Kuanza Kwa Mwezi na Siku (Na. 203). Jedwali la nyakati au masaa ya EENT huko Yerusalemu laweza kupangiliwa kwenye Kompyuta kwa kipindi cha mwaka mmoja – au siku 365 – moja kwa moja kutoka kwenye tovuti ya Interneti ya  http://aa.usno.navy.mil/data/docs/RS_OneYear.php kwa kutumia dondoo zifuatazo: mstari ulalo au longitude Mashariki nyuzi 35’ 19, mstari ulalo au latitude Kaskazini nyuzi 32’ 34, na masaa 2 mashariki mwa Greenwich.

 

4. KUAMUA MPANGILIO WA TAREHE AU SIKU ZA MWEZI MPYA

 

A. Pata siku ya mpito ya muunganiko kwenye dondoo za Mwezi Mpya.

 

Utumiaji wa dondoo kupata siku za miunganiko ya miezi, tunaweza kuamua kupangilia siku za Mwezi Mpya za kushika huko Yerusalemu. Kwa mfano, tutaamua kupangilia siku ya Mwezi Mpya kuwa ni Mwezi wa Kwanza wa Kalenda Takatifu ya Mungu katika mwaka 2008, au mwaka wa 31 wa Yubilee ya 120. Tunaukuta Mwezi Mpya saa 11 jioni siku ya 14 ya ushirika wa meza ya Bwana tarehe 7 March 2008. http://aa.usno.navy.mil/data/docs/MoonPhase.php

 

B. Amua kupangilia Mwezi Mpya kwa masaa mahalia ya Yerusalemu.

 

Yatupasa kulinganisha saa ya kuanza kwa muunganiko wa Mwezi Mpya kulikoonyeshwa kwenye jedwali kutokana na Masaa ya Kimataifa ya Universal Time (UT) na masaa mahalia ya Yerusalemu kwa kuongeza tu masaa 2 na kufikia saa 1 jioni, siku ya14 (saa 1:14 jioni) kwa masaa mahalia ya mwanzo wa Mwezi Mpya huko Yerusalemu.

 

Wakati yanapoongezwa masaa 2 kwa kukatiza kwenye usiku wa manane (saa 6:00 usiku), yatupasa kusogeza siku vizuri, ambavyo ni, kwa kuifanya iwe siku inayofuata ya kalenda ya Georgian. Hii kwa hiyo ni kuusogeza mbele muda wa dondoo la jedwali.

 

C. Pata masaa ya EENT ya Yerusalemu kwenye jedwali la mwaka 2008.

 

Kwenye tarehe 7 March 2008, tunakuta kuwa saa 12:34 jioni (saa 12:34 jioni) kwenye jedwali la masaa yaliyowekwa kwenye Kompyuta ya EENT likitumia masaa 2 mashariki mwa mstari wa Greenwich.

http://aa.usno.navy.mil/cgi-bin/aa_rstablew.pl

 

D. Kurekebisha tarehe kama mwanzo wa Mwezi Mpya utakuwa kati ya masaa ya EENT na usiku wa manane, yaani saa 6:00 usiku.

 

Wakati mwingine tunapaswa kurekebisha tarehe ya siku ya kuadhimisha wakati siku asilia ya Mungu inapoanzia wakati wa giza wakati mwanadamu anapofanya mwanzo usiku wa manane. Kwa hiyo kunakuwa na tofauti ya masaa 6 kati ya maana mbili yanayoendana na kipindi cha kati ya masaa ya EENT huko Yerusalemu na usiku wa manane. Hata hivyo, majira ya baridi siku inaweza kuishia mapema sana kama saa 11:00 jioni (saa 11:00 jioni) na majira ya joto inaweza kuishia muda mrefu wa saa 4:00 usiku (saa 4:00 usiku) kwenye maeneo mengine ya dunia. jambo la msingi na muhimu kukumbuka hapa ni kwamba siku ya Mungu huanza na kuishia jua linapozama na giza kuanza. Kwa lengo la kufafanua dhana ya “tangu kuzama jua na kuingia giza hadi usiku wa manane” tutauita muda huu kuwa ni kipindi cha masaa 6, tukijua kwamba muda linapoanza kuingia “giza” hutofautiana kwa mwaka mzima.

 

Kwa hiyo twaweza kusema siku ya Mungu huanza na kuishia kwenye wastani wa masaa 6 kabla ya tafsiri aliyoifanya mwanadamu hivi karibuni. Wakati Mwezi Mpya unapojitokeza kwenye kipindi hiki cha masaa 6, yatupasa kupeleka mbele siku iliyoonyeshwa kwenye jedwali na kuihamishia kwenye siku inayofuatia ili kuishika siku sawasawa na maana aliyoiagiza Mungu. 

 

Kwenye mfano wetu, siku inabadilishwa hadi siku inayofuatia kwenye jedwali la siku kwa kuwa muda wa kuanza Mwezi Mpya wa tarehe 7 March ulikuwa ni baada ya masaa ya EENT ya siku ile.

 

Kwa hiyo, kwa kuwa mwanzo wa Mwezi Mpya wa tarehe 7 March 2008 ilikuwa saa 1:14 jioni (1:14 jioni), ambayo ni baada ya saa za EENT (12:34jioni, au saa 12:34 jioni), mwanzo wa Mwezi Mpya uliadhimishwa tarehe 8 March.

 

5. JINSI YA KUAMUA MWANZO WA MWAKA MPYA (ABIBU 1)

 

Maamuzi ya ni mwezi gani wa Kwanza na siku ya Kwanza ya mwaka, yatupasa kuupata kwanza Mwezi wa Kwanza ulio karibu sana na ikwinoks ya majira ya baridi. Siku ya 14 ya mwezi wa Abibu unaweza kuwa ndio huohuo wenye siku ya ikwinoks, lakini haiwezi kuadhimishwa KABLA ya ikwinoks ya majira ya baridi. Hii ni kwa ajili ya kutoa sadaka mbili za Pasaka zinazotokea kwenye mwaka huohuo wa kalenda. Hata hivyo, inapasa iwe katia siku ya 14 inayotokea kabla ya siku ya ikwinoks, mwezi wa kumi na tatu unapasa uongezwe ili kuzuia kutokea kwa hilo. Kimsingi, pia ina maana kwamba siku ya 15 ya mwezi wa Abibu ni budi kila mara itokee baada ya siku za ikwinoks.

 

A. Pata majira ya ikwinoks ya majira ya baridi.

 

Kwenye majedwali kwa ajili ya mwaka 2008 iliyowekwa kwenye tovuti ya: http://aa.usno.navy.mil/data/docs/EarthSeasons.html siku ya ikwinoks ya majira ya baridi au ya joto kwenye Ncha ya Kaskazini mwa dunia ni March 20, saa 11:48 asubuhi kwa saa za UT. Ikwinoks ya majira ya joto inatokea karibia kwenye siku hiyohiyo kila mwaka. Tunaongeza siku 2 ili kuifanya iendane na muda mahalia wa masaa ya Yerusalemu saa 1:48 asubuhi. Kwa kufuata kanuni hiyohiyo kwa mionekano ya Mwezi Mpya hapo juu, tunaamua kuipanga siku ya ikwinoks kuwa ni tarehe 20 March sawasawa na malengo ya Mungu.

 

B. Pata mwanzo wa Miezi Mipya ya kabla na baada ya ikwinoks ya majira ya baridi.

 

Kutokana na majedwali ya kwenye tovuti ya http://aa.usno.navy.mil/data/docs/MoonPhase.html, tunakuta siku ya kuanza Mwezi Mpya kukitokea hata kabla ya siku ya ikwinoks, March 20, na mwanzo wa Mwezi Mpya ukifanyika mara tu baada March 20. Siku ya Mwezi Mpya iliyo karibu sana na ikwinoks ndiyo hufanyika kuwa ni mwezi mpya wa Mwaka wa Kwanza, ambayo ndiyo Siku ya Kwanza iitwayo siku ya 1 Abibu. Katika mwaka 2008, tulikuwa na mwonekano wa Mwezi Mpya tarehe 7 March, saa 11:14 jioni saa za UT (saa 1:14 saa za Yerusalemu) na kuonekana kwa Mwezi Mpya kulikuwa Aprili 6 saa 9:55 alfajiri (11:55 majira ya Yerusalemu). Tunakuta kwamba Mwezi Mpya ulikuwa siku ya March 7 ukiwa ni mwezi wa karibu zaidi na ikwinoks ya majira ya baridi ya March 20. Kwa kuwa Mwezi Mpya ulianza saa 1:14, baada ya saa za EENT (12:34) huko Yerusalemu na kabla ya usiku wa manane, tunaisogeza siku hadi siku inayofuatia. Kwa hiyo, March 8 ikafanyika kuwa ni Siku ya Kwanza ya Mwaka, yaani, mwanzo wa Mwaka Mpya, siku ya 1 Abibu.

 

Hili ni hitimisho la utaratibu wa kuamua jinsi ya kuipangilia Kalenda ya Mungu. Siku zote za mwanzo wa Kalenda ya Miezi Mipya na Mwaka Mpya inaweza kupatikana kwenye jarida la Kalenda ya Mwezi Mpya na Siku Takatifu (Na. C3).

 

Na tuombe basi ili Baba na Mwumbaji wetu, Eloah afundishe watu wote kuhusu Kalenda yake ili kwamba wote wamuabudu yeye kama inavyotakiwa na kwa siku sahihi.

 

Soma pia kwenye jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156).

 

***************

 

Maana ya Maneno yaliyotumika:

 

Utusitusi wa Mawio na Machweo ya Jua [Astronomical twilight]: kunatokea wakati wa jioni mara tu jua linapokuwa limefikia kiwango cha zaidi ya nyuzi 18° chini ya upeo wa macho na huzama wakati jua linapofikia kwenye nyuzi 18° za upeo wa macho majira ya asubuhi.

 

Kipindi cha Muunganiko Kati ya Mwezi wa Zamani na Mwezi Mpya [Conjunction]: mkutaniko au muunganiko wa muundo wa mbinguni kwenye mstari huohuo wa wima au uliosimama wima, yaani, hali ya mihimili miwili au zaidi ya mbingu wakati mistari ya wima ni ile ile – inaonekana kuwa kwenye mstari wa kila mmoja wapo.

 

Utusitusi wa Nchi [Civil twilight]: unaanza majira ya asubuhi wakati kitovu cha jua kinapokuwa chini ya nyuzi 6° chini ya upeo wa macho, na kuishia kwenye mawio ya jua. Utusitusi wa nchi wa jioni unaanzia jua linapokuchwa na huishia wakati kitovu cha jua kikiwa zaidi ya nyuzi 6° chini ya upeo wa macho.

 

Utusitusi wa Ukomo wa Zamu ya Jioni ya Mabaharia [EENT]: Utusitusi wa Ukomo wa Zamu ya Jioni ya Mabaharia ni muda halisi ambao giza linaanza kwenye maeneo fulani maalumu.

 

Ikwinoks [Equinox]: ikwinoks ni kipindi ambacho jua linavuka kwa kupita kwenye mhimili wa Dunia wa ikweta, kikifanya usiku na mchana karibu Ulimwenguni kote kuwa na urefu sawa. Hali hii inatokea mara mbili kwa mwaka: mmoja hutokea majira ya baridi na hii hutokea kwenye tarehe za 20/21 March na nyingine hutokea majira ya joto mnamo tarehe 22 Septemba.

Majira yajulikanayo kama Greenwich Mean Time: maana yake ni masaa au majira yatokanayo na mwelekeo wa jua ukanda wa meridian kupitia mstari wa Greenwich, huko Uingereza.

Kalenda ya Gregorian [Gregorian Calendar]: kalenda iliyotokana na marekebisho ya kalenda ya mwanzoni ya  Julian iliyotengenezwa na kuanzishwa na tume ya Papa Gregory XIII na inayotumika sasa. Kwa mujibu wa kalenda hii, mwaka wa kawaida una siku 365 (miezi 12), na aiku 366 kwa miaka mirefu. Siku zake zinaanzia usiku wa manane kalenda hii ya Gregorian.

 

Kuongeza Mwezo wa Ziada [Intercalation]: ku-intercalate maana yake ni kuingiza mwezi wa ziada ili kuufanya mwaka wa kalenda ulingane na kalenda ya mfumo wa mwaka wa mzunguko wa jua.

 

Mstari wa Mlalo [Latitude]: umbali uliowekwa wa mastari wa wima wa kaskazini au kusini kutoka kwenye mstari wa ikweta unaoonesha uso wa Dunia, unaopimwa kwenye nyuzi za umbali.

 

Mstari wa Wima [Longitude]: umbali uliowekwa wa mastari wa wima wa mashariki mwa uso wa Dunia, uliopimwa kwenye nyuzi au digrii kutoka kwenye ukanda fulani wa mstari unaozitenganisha kanda (mstari wa kutoka Kaskazini hadi Ncha ya Kusini mwa Dunia). kwa kawaida, mstari huu unaotenganisha kutoka ukanda wa Greenwich, Uingereza inatumika.

 

Mchanganyiko wa Mwezi na Jua [Lunisolar]: inahusiana au inatokana na uhusiano wa mseto wa mwezi na jua (mfano, mzungko wenye mseto wa mwezi na jua).

 

Kalenda ya Mchanganyiko wa Mwezi na Jua [Lunisolar calendar]: ni kalenda ambayo tarehe au siku zake zinaashiria vyote viwili, yaani mwonekano wa mwezi na nyakati za jua. Kwa kawaida kuna nyongeza ya lazima ambayo kwamba mwaka una idadi yote ya miezi lakini, na kwa namna yoyote, kila mwaka una miezi 12 bali kila mwaka wa pili au wa tatu una miezi 13. Mara saba kwenye kipindi cha miaka 19 tuna mwaka wenye miezi 13.

 

Kukomaa na Kupanda kwa Mwezi/ Kuweka nyakati [Moonrise/set times]: nyakati hizi zinategemea na mwelekeo wa mwezi – yaani mwezi mpya wenye giza kamili, mwezi kamili na robo ya kwanza na ya pili. Mwezi unainuka na kuchwa kila siku ni kama lifanyavyo jua. Kwa habari zaidi kuhusu mwelekeo huu wa mwezi, soma tovuti ifuatayo: http://www.calculatorcat.com/moon_phases/moon_phases.phtml

 

Utusitusi wa Kubadilishana Zamu ya Jioni ya Mabaharia [Nautical twilight]: inamaaniha kuwa ni wakati kiini cha jua kiko zaidi ya 6° chini ya upeo wa macho lakini chini kuliko nyuzi 12°. Kipindi hiki asubuhi mara nyingi kinaitwa kuwa “nuru ya kwanza” kabla ya mapambazuko, na kwa jioni kinajulikana kuwa cha “kuingia usiku” baada ya magharibi. Kipindi hiki cha Utusitusi Jioni ya Muda wa Kubadilishna Zamu Mabaharia unafanana na ule wa EENT.

 

Mwezi Mpya [New Moon]: Mwezi Mpya wa wataalamu wa elimu ya nyota na anga, wakati mwingine unajulikana kama mwezi wa giza, hutoke kimwelekeo na kipindi cha mpito cha kutooekana mwezi kwenye uficho kwa tukio la kupatwa kwa mwezi na Jua kwenye mstari wa wima, wakati Mwezi unapoacha kuonekana kutoka Duniani.

 

Majira ya Jua [Solar time]: hupimwa au huamuliwa kwa mwenendo wa Dunia kwa kuhusiana na jua.

 

Mawio ya Jua [Sunrise]: muonekano wa kwanza wa jua wakati wa asubuhi.

 

Machweo ya Jua [Sunset]: kuzama chini kwa jua – mwonekano wa mwisho wa jua jioni.

 

Masaa ya Ulimwengu [Universal Time]: mfumo wa masaa unaopimwa kwa kutegemea mfumo Kuanza kwa Masaa Kutokanako na Majira ya mstari wa Greenwich, lakini yanahesabiwa tangu saa 0, ambayo ni sawasawa na usiku wa manane ya mfumo wa Masaa ya mstari wa Greenwich.

 

q