Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[CB30]

 

 

 

Mpango wa Mungu wa Wokovu

(Toleo La 2.0 20020701-20061216)

Mara nyingi watoto wanauliza maswali mengi sana kuhusu Mungu na jinsi anavyotuwazia au Mpango wake Kwetu sisi. Jarida hili linajibu maswali haya na kuelezea sababu inayotufanya sisi tuhitaji Mpango wa Mungu wa Wokovu, na mpango huo ni nini na jinsi tunavyotakiwa kuwa ili tuweze kustahili kuwa nao.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 2002, 2006 Carrie Farris and Wade Cox)

(tr. 2014)

 

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au ku

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya::
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 

Mpango wa Mungu wa Wokovu

 


Kwa nini tunahitaji Mpango wa Mungu wa Wokovu?

Wakati Mungu alipomuumba mwanadamu kwanza, alimuumba kwa sura na mfano wake na kwa kunafafa na yeye.

Mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba

 

Adamu na Hawa walikuwa ni wanadamu wa kwanza aliowaumba Mungu. Walikuwa ni sehemu ya familia yake. Waliishi kwenye Bustani ya Edeni na hawakuwa na dhambi yoyote aliyomfanyia Mungu, ambayo maana yake ni kwamba hawakuivunja amri yoyote katika Torati ya Mungu. Hivi ndivyo ilivyokuwa hadi ale Hawa alipojaribiwa kula matunda ya mti ambao Mungu aliwaambia wasile.

Mwanzo 2:16-17 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

 

Wakati Hawa alipolichukua lile tunda lililokatazwa, alitanda dhambi. Aliivunja Amri ya Mungu. Pia alimmegea kipande Adamu naye akala lile tuna naye akatenda dhambi (Mwanzo 3:1-6).

 

Kwa kuwa Adamu na Hawa walimuasi Mungu kwa kuvunja Sheria yake, walifukuzwa watoke bustanini na Mungu akawalaani na kuiweka laana juu yao.

Mwanzo 3:16-19 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala. 17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; 18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; 19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

 

Laana hii haikuwa kwa ajili ya Adamu na Hawa peke yao. Bali ilikuwa ni kwa wanadamu wote watakao wafuata wao kutenda matendo haya ya uasi, hadi kwetu sisi leo pia. Laana inatuambia sisis kwamba tutapatwa na maumivu na mateso sisi sote na kwamba hatimaye tutakufa sote na miili yetu itayarudia mavumbi. Kutokana na dhambi hii ya kwanza, ndipo mauti ikaja; na pia iliwafanya watoto wa Adamu kuwa wana wa wanadamu na sio tena kuwa wana wa Mungu kama ilivyokuwa imekusudiwa hapo kabla.

Warumi 5:12 Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;

 

Kama hatukuwa na Mpango wa Mungu wa Wokovu, basi tungekufa na kusingekuwa na kingine zaidi. Tungerudi tu kwenye mavumbi ya Nchi na hivyo ndivyo ingalivyokuwa tu. Lakini Mungu hapendi mtu yeyote apotee milele.

2Petro 3:9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.

 

Ili tuweze kuishi, au tusife milele, Mungu aliweka Mpango wa Wokovu kwa ajili yetu, ili kutufanya tuwe kwa mara nyingine sehemu ya familia yake.

 

Je, Huu Mpango wa Mungu wa Wokovu Ni kitu gani?

Baada ya Adamu, Mungu alifanya agano na watu wake. Mwanzoni kabisa, alilifanya na Mababa wa imani, na ndio peke yao waliokuwa wanazishika Amri zake. Dunia ilijaa maovu kiasi ilistahili kuangamia kwa gharika. Nuhu na familia yake waliokoka na kuanzisha ulimwengu mpya usio na maovu yaliyokuweko huko nyuma. Kupia Ibrahimu Mungu aliandaa kundi la mataifa na kuwachagua Israeli kuwa taifa lake teule, ambalo kupitia kwalo aliweza kufuua Mpango wake. Aliwapa Torati iwaongoze na walimtolea sadaka za dhambi ili wasamehewe. Pia aliwapa Siku zake Takatifu. Hizi Siku Takatifu zimetolewa ili kutuonyesha jinsi Mpango wa Mungu ulivyo. Katika siku hizi,  watu wa Mungu walimtolea Mungu sadaka za aina mbalimbali za kuteketezwa. Tunaweza kujisomea kwa kina zaidi kuhusu siku hizi Takatifu kwenye jarida la Siku Takatifu za Mungu (Na. CB22) [God’s Holy Days (No. CB22)].

 

Mungu alijua kuwa agano hili lisingeweza kufanya kazi pasipo msaada wa Roho Mtakatifu kuwepo ndani ya mwanadamu, kwa kuwa alijua kwamba mwanadamu angeendelea kutenda dhambi. Ingawa mtenda dhambi alikatiliwa mbali na Mungu wa Pekee na wa Kweli. Kwa hiyo Mungu alitabiri kwamba mfumo mpya wa Agano lake ungeanzishwa na agano kuwekwa kama maagano mengi madogomadogo au ahadi na makubaliano vikiwemo ndani yake (Soma jarida la Maagano ya Mungu (Na. 152) [The Covenants of God (No. 152)]. Utaratibu huu mpya wa agano uloiwekwa katika Kristo, ulileta tumaini na wokovu.

Yeremia 31:31-34 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. 32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana. 33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.

 

Ilitabiriwa pia kwenye Biblia kwamba Mungu atamtuma Masihi wake, ambaye ni Mtiwa Mafuta wake, kuja kuwaokoa watu wake.

Yeremia 23:5-6 Tazama siku zinakuja, asema Bwana, nitakapomchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi. 6 Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, Bwana ni haki yetu.

 

Aya hizi zilikuwa zinatabiri ujio wa Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, na ujio wa Roho Mtakatifu, ambaye Mungu alikuwa anakwenda kuwapa watu wote waliomuamini Mwanae wa Pekee.

 

Yesu alikuja kuwafundisha watu kuhusu utaratibu huu mpya wa agano na Mungu. Hakuja kuitangua Torati ambayo Mungu alikuwa ameiweka na kuwapa watu wake. Bali alikuja kuwafundisha watu na kuwasisitiza kuishika Torati na kuwafikisha kwenye toba watubie dhambi zao walizomtenda Mungu.

Mathayo 5:17-18 17 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie.

 

 

Toba maana yake ni kujisikia vibaya na kujutia mambo mabaya tuliyoyatenda na kuondoka kwenye kutenda mabaya na kutenda mema, au kumrudia Mungu na kuyafanya mapenzi yake.

 

Yesu alifundisha pia kwamba inatupasa kubatizwa, ambayo maana yake ni kwamba baada ya kutubu kwetu na maisha yetu kumrudia Mungu, tunatakiwa kuzamishwa majini kwa dakika kadhaa, kitendo kinachomaanisha ishara ya kuyafisha matendo yetu ya zamani na kufufuka na maisha mapya na Mungu.

Mathayo 28:19-20 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; 20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.

 

Tunaweza kubatizwa tu tunapokuwa na umri wa mtu mzima. Bali wakati huohuo, iwapo kama tuna wazazi waaminio tunakuwa tumetakaswa kupitia wao (1Wakorintho 7:14). Hii inamaana kwamba Mungu hutuangalia kwa upendo mkubwa tunapokuwa chini ya ulinzi wa wazazi wetu. Inaamikika kuwa wazazi waaminio huwafundisha watoto wao Torati ya Mungu, na kwa watoto hawa watakuwa wanaendelea kuzishika Sheria au Torati hii hadi watakavyokuwa watu wazima au wazee. Kwenye Kanisa la Mungu watoto huwa hawabatizwi. Hii inamaanisha kwamba tunatakiwa kwanza tuzijue dhambi zetu na kujutia matendo yote mabaya tuliyoyatenda, kabla hatujaenda kwenye kisima au mto wa maji au pahali popote enye maji mengi ili kubatizwa na tukahuishwa na kuwa hai (kutakaswa).

 

Yesu pia alikuja ili awe Mwokozi wetu. Hii inamaana kwamba alikuja ili atufie ili atuoshe au kutusafisha dhambi zetu. Wakati Kristo alipokufa alifanyika kuwa Mwanakondoo wetu wa Pasaka. Hakufanya dhambi yoyote kamwe, bali alilipa gharama ya wenye dhambi, ambayo ni mauti. Alifanya iwezekane kwa sisi kumwendea Mungu sisi wenyewe bila kuwaendea makuhani au kasisi. Yeye pia alikuwa ni dhabihu ya mwisho, ambayo maana yake ni kwamba hatuhitaji tena kumtolea Mungu dhabihu nyingine yoyote ya wanama.

Kwa hiyo Kristo alifufuka kutoka kwa wafu akiwa ni malimbuko ya mavuno ya Mungu. Hii inamaanisha kwamba yeye ni wa kwanza miongoni mwa wengi wataofufuliwa toka kwa wafu na kuishi tena kwenye Mbingu Mpya na Nchi Mpya.

1Wakorintho 15:20 Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.

 

Ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

 

Pia Kristo alifanya iwezekane karama za Roho Mtakatifu wazipate wana wa Mungu. Roho Mtakatifu ni uweza au nguvu za Mungu, inayotuwezesha kupata asili ya Mungu mwenyewe na ni kipawa anayoitoa bure kwa yeyote anayeiomba. Tunaweza kujisomea zaidi kuhusu Roho Mtakatifu kwenye jarida la Roho Mtakatifu Ninini? (Na. CB3) [What is the Holy Spirit? (No. CB3)].

 

Kristo, kwa kupitia Roho Mtakatifu, ndpo tunavyoweza kuyaelewa Maandiko Matakatifu au Biblia na ndvyo Mungu anavyotuonyesha yalle anayotaka tuyafanye. Mungu anatuonyesha kwamba ameliweka Agano lake Jipya ambalo aliliongelea kwenye Yeremia 11. Warumi 2:14-15 ikimaanisha kwamba kwa sasa Roho Mtakatifu anaongoza mawazo na matendo ya watu wa Mungu.

Warumi 2:14-15 Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria wamekuwa sheria kwa nafsi zao wenyewe. 15 Hao waionyesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;

 

Yesu pia alisema kuhusu kurudi kwake Duniani, na kwamba atawakusanya wateule wa Mungu kutoka kokote waliko Duniani. Wateule ni watu wanaoyafanya mapenzi ya Mungu na maagizo yake. Yesu pia anasema kwamba hakuna ajuae kipindi au siku ya kuja kwake ila Baba yake peke yake.

Marko 13:26-27 Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu. 27 Ndipo atakapowatuma malaika na kuwakusanya wateule wake toka pepo nne, toka upande wa mwisho wa nchi hata upande wa mwisho wa mbingu.

 

Marko 13:32 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.

 

Wakati Kristo atakapokuja atatawala kama Mfalme wetu kwa kipindi cha miaka elfu. Wateule watasaidia utawala wake wakiwa kama makuhani. Watu hawa watakuwepo kwenye kile kinachoitwa kuwa ni Ufufuo wa Kwanza wa wafu—kwa maneno mengine ni kwamba watakuwa ni wafu wa wa kwanza kufufuliwa na kuwa hai tena kai ya wafu waliolala mauti.

Ufunuo 20:4-6 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.

 

Watu wengine wote waliosalia ambao waliishi bali hawakuyatenda yale aliyoyapenda Mungu wayafanye, watafufuliwa tena baada ya miaka elfu ya utawala wa Kristo akiwa ni Mfalme. Huu unaitwa Ufufuo wa Pili wa wafu. Watu kwenye Ufufuo wa Pili wa wafundishwa kuishi sawa na maongozi ya Torati ya Mungu na wataweza kuwa na fursa ya kuwa ni sehemu ya familia ya Mungu. Hii inaitwa hukumu. Kama hawatamrudia Mungu, hakika watakufa kwa mara ya nwisho na hawataweza kuwa hai tena.

 

Tunawezaje kuwa sahihi kwenye Mpango wa Mungu?

Mungu anatupenda, na sisi sote. Hapendi hata mmoja wetu apotee kama tulivyokwisha jionea tayari. Bali pia anatupenda kiasi cha kutosha kwa kutupa Mwanae wa pekee ili awe ni sadaka yetu ya dhambi, ili sisi tuwe sehemu ya familia yake tena. Ila sio watu wengi wanaoelewa jambo hili sasa.

Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

 

1Yohana 3:1-2 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.

 

Siku moja sisi sote tutabadilika na kuwa viumbe wa kiroho. Hakutakuwa na mwanaume wala mwanamke, bali ni kama malaika au viumbe wenye miili ya kiroho. Sote tutafanyika kuwa ni Wana wa Mungu na tutafana kazi pamoja na Kristo. Kristo alitufia ili kwamba tutakapoamka kutoka malaloni mwetu (kifo) tuishi pamoja naye (1Wathesalonike 5:10). Hebu fikiria na kutarajia kwamba siku moja tutamuona Kristo na kuwa pamoja naye pamoja na viumbe wengine wenye miili ya kiroho.

 

Namna pekee ya kufanyika kuwa familia ya Mungu ni kumuamini yeye na Mwanae wa Pekee, Yesu Kristo. Tunapaswa pia kuitii Torati yake, kutubu dhambi zetu, na kubatizwa tunapofikia umri wa utu uzima. Hili ni jambo ambalo tunapaswa wote tuliangalie kwa kina.

 

Kumbuka kuwa jambo ambalo Mungu anatutaka tukifanye ni kumpenda na kumtii yeye. Kadiri tunavyofanya hivyo ndipo tutakuwa ni sehemu ya familia yake milele.

Kumbukumbu la Torati 7:9 Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu;  

 

q