Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[CB23]
Siku za Ibada za Shetani
(Toleo La 2.0 20030312-20061223-20140209)
Watu wengi sana duniani wanaadhimisha sikukuu za Krismas, Easter na Mwaka
Mpya, lakini je, kuna msingi wowote wa kimaandiko unaotuamuru kuzishika sikukuu
hizi? Na kama hakuna, je, tunaweza basi kuziadhimisha Siku za Mungu sambasamba
na huku tukizishika sikukuu hizi za uwongo na potofu za kidini?
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2003, 2006 Diane Flanagan, ed. Wade Cox)
(rev.
2014)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili linapatikana Ulimwenguni
kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Siku za Ibada za Shetani
Watakatifu wa
Mungu ni wale wanaozishika Amri za Munguna Ushuhuda wa Yesu Kristo (Ufunuo
12:17; 14:12; 22:14). Wanamuabudu Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli (Kum. 6:4;
Yohana 1:18; 17:3; 1Timotheo 6:16; 1Yohana 5:20). Wanazitii Sheria na Torati
yote na wanamuabudu Mungu kwa siku zake sahihi zilizoagizwa kwa namna ambayo
ameiamuru Mungu.
Shetani Mfalme wa
mamlaka ya uweza wa anga (Waefeso 2:2). Hii inamaana kwamba Shetani ana uwezo
wa kushawishi fahamu na uelewa wa watu na fikra zao. Shetani anapenda kugeuza
na kupingana na Mipango ya Mungu. Kwa kweli, Mungu hatakubali hilo litokee.
Lakini kwa kipindi cha miaka 6,000 ambayo Shetani ameruhusiwa kutawala hapa
Duniani ,Sameanzisha mafundisho mengi sana ya uwongo, na kwa kufanya kwake
hivyo amewapata watu wengi sana.
Shetani ameweka
mchanganyiko wa sehemu ya ukweli na uwongo. Au amechukua imani na desturi za
kipagani za kale na kuyachanganya na kiasi fulani cha ukweli. Shetani
amewafanya pia watu waamini kwamba Mungu anakamilika kwa muunganiko wa viumbe
watatu, imani inayoitwa ya Utatu. Tunajionea wazi kabisa kutoka kwenye Timotheoy
6:16 inasema wazi kabisa kwamba kuna Mungu Mooja tu wa Pekee na wa Kweli (soma
jarida la Mungu ni Nini? Na. CB 1 [Who is God? (No.
CB1)]. Ni huyu Mungu wa Pekee na wa Kweli ndiyw
tunayemuabudu kwenye zile siku alizozitenga na kuzibarikia kuwa ni Siku
Takatifu na kutuamuru tumfanyie makusantiko Matakatifu. Ingawa Shetani aliumbwa
mkamilifu, aliasi. Alimuasi Mungu na kujaribu kukitwa Kiti cha Enzi cha Mungu (Isaya
14:13). Alipokuwa ameumbwa kwanza jina lake lilikuwa ni Lusifeli, ambalo
linamaansisha Mleta Nuru, lakini
Mungu alilibadilisha na akaitwa Shetani, ambalo maana yake ni Mshitaki au Mlleta mashitaka (1Petro 5:8; Rev. 12:10). Ili kujifunza zaidi
kuhusu uasi huu, soma jaridea la Uumbaji wa Familia ya Mungu (Na. CB4 [The Creation of the Family of God (No. CB4)].
Kwa vipindi fulani mbalimbali Shetani amefanya mjaribio mbalimbali ili kuusimamisha Mpango wa Mungu. Mara tu baada ya kifo cha Kristo, Shetani alianzisha dini na imani mbalimbali zilizonuia kukomesha ushikaji wa Sheria au Torati. Ndipo aliweka mafundisho yanayobadilisha asili ya Mungu tunayemuabudu, na kujumuisha mafundisho mengine yanayotokana na imani za kale za kipagani na kuyaingiza kwenye Ukristo. Wapagani ni watu wanaoabudu miungu mingi mbalimbali, lakini hawana uhusiano na Mungu wa Pekee wa Kweli (Eloa). Kwenye maeneo mbalimbali ya duniani miungu hawa wengi wa Utatu (imani ya miungu wanaojumuisha viumbe watatu) wanaabudiwa. Kwenye kipindi cha zamani sana kabla ya kufa kwa Kristo, imani hii ya Utatu ilifanikiwa kuingizwa kwenye Kanisa Katoliki la Roma
Watu wengi sana leo wanaamini kuwa Mungu anatokana
na muunganiko wa viumbe watatu kwa kile kinachoitwa—Baba, Mwana na Roho
Mtakatifu. Huu ni uwongo mkubwa sana. Bali kuna Mungu Baba mmoja, na ndiye
Muumbaji wa vitu vyote na ni yeye tu peke yake ndiye tunayetakiwa kumuabudu.
Pia kuna Yesu Kristo, Mwanae, ambaye alikuja hapa Duniani akiwa kama Malaika wa
Yahova na kuongea na nabii Musa na manabii wengine, kama Biblia inavyotuambia.
Hatimaye, Kristo alitwaa mwili wa kibinadamu na akafanya ishara mpya kwa njia
ya maadhimisho ya Pasaka. Akafanyika kuwa ni sadaka kamilifu na takatifu ambayo
iliwapatanisha na Watakatifu kwa Mungu Baba. Soma jarida la Mungu ni Nini? Na. CB2) [Who is Jesus? (No. CB2)].
Roho Mtakatifu ni
uweza tu wa Mungu. Anatusaidia
kuwasiliana na Mungu na anatusaidia pia kuyajua mapenzi ya Mungu na anayotaka
tuyafanye. Lakini hii isitufanye sisi tumruhusu mtu yeyote ajaribu kutudanganya
kwa kutuambia kwamba miungu hii mitatu inafanya jumla ya Mungu mmoja. Shetani hajali jinsi
anavyowapotosha watu mbali na Mungu wa Kweli. Soma
jarida la Roho Mtakatifu Ninini?
(Na. CB3) [What is the Holy Spirit? (No. CB3)].
Kuibadili kalenda na mwanzo wa siku
Mungu anatuambia kwamba mwaka mpya unaanzia mwezi wa Abibu, mwezi ambao wana wa Israeli walitolewa utumwani Misri (Kutoka 13:4). Kwenye kalenda ya Kirumi huu ni mwezi wao wa Machi au Aprili kutegemea na mwaka ulivyo. Ili kuelewa kikamilifu kuhusu Kalenda, soma jarida la Kalenda Takatifu ya Mungu (Na. CB20) [God’s Sacred Calendar (No. CB20)]. Kalenda ya kale zaidi ya Kirumi pia mwaka wake ulikuwa unaanza mwezi wa Machi/Aprili. Kwa kipindi kifupi tu, Shetani alifanikiwa kuwashawishi karibu watu wote duniani kubadilisha mwanzo wa mwaka hadi kwenye mwezi wa Januari, kama unavyojulikana leo kwenye kalenda ya Wagregoriani.
Karibu miezi yote ya mwaka mzima imeitwa kwa majina ya miungu ya kipagani, watawala au idadi ya miezi kutokea mwezi wa kwanza wa kalenda:
(Hii hi kwa mujibu wa Kamusi ya kitabu cha Fafanuzi kiitwacho The Living Webster Encyclopedic Dictionary of the English Language 1977.)
Mungu anatumia hesabu au idadi ili kuitambulisha miezi yake (Kutoka 12:2; 13:4; 2Nyakati 30:2; Nehemia 8:2). Katika kipindi hiki tutaona majina yaliyotumiwa kuitaja miezi kwenye Kalenda ya Mungu. Majina haya yana asili ya Kikanaani au Kibabelonia na yaliingia kwenye lugha ya Kiyahudi.
Mungu anatumia
pia idadi katika kutambulisha siku za juma. Siku iliyotajwa kwa jina tofauti ni Sabato tu.
Sabato ni siku ya saba ya juma, lakini imetajwa kuwa ni Sabato.
Mfumo wa Shetani
pia unatumia majina ya miungu kwenye majina ya siku za juma:
Kama tunavyoona
kwamba Shetani aamejaribu kubadilisha vitu na mambo yote ambayo Mungu
ameyapanga ili sisi tuweze kujua ni kipindi gani kilicho sahihi kumuabudu.
Kitendo cha kuabudu siku isiyopangwa au kuamriwa hakimaanishi wala kuonyesha
kuwa tunamheshimu au kumuabudu yeye Mungu Baba yetu na kuzitii Amri zake.
Biblia inatuambia
kwamba siku inaanzia majira ya kuzama jua (Walawi 23:32; Nehemia 13:19; Matendo
27:27-33). Siku nyingi sana zilizopita watu walijua kwamba siku ilianzia muda
jua linapozama giza likianza. Lakini Shetani alimudu kunpata mtu wa kuongoza
mkakati huu wa kubadilisha majira ya kuanza kwa siku. Hivi sasa siku inaanzia
usiku wa manane. Hili ni jaribio lingine la Shetani katika kuwachanganya watu
na kuichanganya siku wanayopaswa kumfanyia ibada Mungu.
Kama
hatutamuabudu huyu Mungu wa Pekee na wa Kweli katika siku alizoziweka na
kutuamuru, basi tujue kwamba tunamuasi au hatumpi heshima yake yeye Mungu!
Kwa kujaribu
zaidi kuuharibu Mpango wa Mungu, Shetani alijaribu kuzibadili siku ambazo
tulipaswa kumfanyia Mungu ibada. Na ndiyo maana wengine wanasema kwamba siku
tunayopaswa kumuabudu Mungu ni Jumapili. Siku za kale, watu waliliabudu jua
siku hii kwa kuwa kilikuwa ndiyo kitu wanachikiona na walijua kwamba jua lilikuwa
ni la mihimu sana katika kuwapa uhai wao na mazao yao. Siku hii ya Jumapili
ilikuwa rasmi kwa kuliabudu jua. Tangu ksrne ya pili, ibada hii ya kuliabudu
jua ilianza huko Roma sambamba na ibada ya Sabato. Katika kipindi cha takriban
karne ya 3 na 4, watu fulani walijaribu kuibadili Sabato na kuitukuza Jumapili
na waliwashawishi wengine kuukubali na kuueneza uwongo huu. Soma jarida la Siku ya Sabato (Na. CB21) [The Sabbath Day (No.
CB21)].
Kuingiza
sikukuu za upotofu zichukue mahala pa Siku Takatifu za Kila Mwaka Zilizoamriwa
na Mungu
Karibu sikukuu
zote za zinaendana na majira ya kukua mazao. Miaka imegawanywa kwa kufuatia
vipindi vya ikwinoks, vya usiku kuwa mrefu cha solstices na siku za robo mwaka.
Kipindi cha ikwinoks kinatokea wakati jua linapopita kwenye mstari wa ikweta na
siku hii masaa ya usiku na mchana yanalingana urefu wake duniani kote. Ikwinoks
ya majira ya baridi inatokea mnamo tarehe 21 Machi na ile ya majira ya joto
inatokea Septemba 23. Majira haya ya solistais yanakuwa jua linapokuwa mbali
sana kutoka kwenye mstari wa ikweta. Linafika upande wa kaskazini zaidi ya dunia
tarehe 21 Juni, ambayo ni siku ndefu zaidi ya mwaka kwa upande Ukanda wa
Kaskazini, na Desemba 21, ambayo ndiyo siku fupi zaidi ya mwaka kwenye Ukanda
wa Kaskazini. Kwenye Ukanda wa Kusini, siku ndefu kuliko zote ni tarehe Desemba
21 na siku fupi zaidi ya zote ni Juni 21. Siku zinazoangukia robo ya mwaka
zinakuwa ni kati ya siku ya usiku mrefu zaidi maarufu kama solstice na kila cha
ikwinoksi.
Ikwinoksi ya Majira ya
Baridi ya March 21 na Maadhimisho ya Ostra/ Easter
Ni kama
lilivyofanywa jaribio la kuibadili siku ya Sabato na kuwa Jumapili, baadhi ya
watu walijaribu kuibadili Pasaka na kuiadhimisha Easter. Kwa kweli, jaribio la kuibadili
siku ya Sabato kuwa Jumapili lilifanyika kutokana na imani na taratibu za zamani za kipagani, ambayo
iliendana au kuhitinishwa na maadhimisho ya Easter. Easter ni sikukuu ya
kipagani ya mungu Ishtar au Ashtorethi. Mungu mke huyu alikuwa na majina mengi
sana mbalimbali kokote kule duniani. Baadhi ya majina yake ni: Cybele,
Shingmoo, Isis, Diana, Nuria, Vensus, Nana, na Disa. Kwenye Kiingereza cha
Zamani, alijulikana kwa jina Easter, na hapa ndipo jina la Kiingereza la
sikukuu hii lilitokana kwayo.
Sungura wa Easter ilikuwa ni takatifu kwa mungu mke huyu
na kuangua mayai ya watoto wema. Easter inaashiria maisha mapya na alama yake ni sungura wengi, mayai na
vinginevyo. Ni wazi kabisa kwamba Biblia haisemi wala kutuamuru sisi
tuiadhimishe sikukuu hii ya Easter. Baadhi ya watu wamekwenda mbali kiasi cha
hata kubadili maandiko fulani ya Biblia kwa kujaribu kuwashawishi watu
kuiadhimisha sikukuu hii ya Easter. Kwenye Biblia ya Kiingereza Tafsiri ya
Mfalme Yakobo maarufu kama the English King James Version of the Bible (KJV),
Matendo 12:4 imeandikwa kimakosa na upotoshaji wa makusudi kwa kuliandika neno
"Easter". Mtu akiangalia na kulinganisha na tafsiri nyingine kama
vile ya Revised Standard Version (RSV) au nyinginezo zilizotafsiriwa kiusahihi
unaweza kuipata maana halisi ya neno liliortumiwa.
Visingizio vya
kusema kwamba eti Kristo alifufuka kutoka kwa wafu siku ya Jumapili alfajiri ni
jitihada tu za kurudisha upya mapokeo ambayo kwamba makuhani wa Easter walikuwa
wanafanya ibada ya kuliabudu jua siku hiyo. Desturi ya kuila nyama ya paja la
nguruwe wa Easter inaonekana kutokana na viumbe wa zamakale ambaye alikuja kuwa
ni mungu Tammuzi, ambaye aliuawa na dume la nguruwe pori, ambaye ni nguruwe. Mungu
anatuambia nguruwe ni mnyama najisi kwetu na tusimle. Tafadhali soma ba
kujifunza zaidi kwenye jarida la Sheria ya Vyakula ya Biblia (Na. CB18 [The Biblical Food Laws (No. CB19)].
Attis alikuwa
mungu mwingine aliyekuwa na mfanano mkubwa na Kristo. Kulizuliwa uzushi kwamba
Attis alizaliwa pasipo kuwa na Baba, na kwamba alikuja kuwakomboa watu wake,
alisulibiwa kwenye mti wa msonobari, akazikwa na kufufuka siku ya 3 toka kwa
wafu. Kifo cha Arris hapo zamani kilisherehekewa
tarehe 25 Machi. Kwa kweli walikuwa na maadhimisho ya juma zima yaliyoitwa Hilaria
(kwa mujibu wa Barbara Walker, The Woman’s Encyclopedia of Myths and Secrets,
New York: Harper Collins, 1983, pp.267, 268, 403). Maadhimisho haya
yalibadilishwa na kuitwa maombolezo ya mateso ya kusulibiwa ya Ijumaa hadi
ufufuo wa Jumapili, shamrashamra zilizopamba moto sana na tunazozijua siku hizi
na ambayo yamepewa jina la uwongo la Ukristo.
Kwa imani ya Makanisa
Makongwe, kipindi kinachojulikana kama Lenti kinaanzia siku wanayopakazwa
Majivu kwa imani ya kidini ya Jumatano hadi mwishoni mwa maadhimisho ya Easter
siku ya Jumapili. Kipindi hiki cha Lent kinamaanisha siku 40 za kujitafakari
kwa maandalizi ya Easter. Watu wengi wanaiadhimisha Lenti kwa kufunga, kutoa
sadaka, kujinyima kula baadhi ya vyakula na kujinyima na kiburudisho, nk.
Hata hivyo, wale
wanaoifuata Kalenda ya kweli ya Mungu wanajua kwamba maadhimisho haya ya Lenti
ni upotoshaji unaokusudia kufunika maandalizi ya Mwezi wa Kwanza (Abibu)
kipindi tunachojiandaa na kuiadhimisha Pasaka kwa mujibu wa Torati ya Mungu.
Imani ya kipagani iliichukua hii kama ilivyofanya kwa Easter pamoja na sikukuu
nyingine nyingi \zilizoanzishwa na wanadamu.
Haya ni
maadhimisho yanayofanyika kwa mapambo ya rangi yanayofanyika Jumanne inayotangulia
Maombolezo ya Kwaresma, siku inategemeana na tarehe itakayoadhimishwa Easter.
Maadhimisho yanafantika mwishoni mwa sherehe ndefu ya inayoanzia tarehe 6
Januari au Usiku wa Ishirini. Mardi Gras ni neno la Kifaransa ambalo maana yake ni Jumanne Nene. Neno hili linatokana desturi ya kumswaga ng\ombe dume
kwenye mitaa ya mjini Paris siku ya Jumanne inayotuatia Kwaresma.
Sherehe hizi za
Mardi Gras yanaenda hadi nyuma kwenye desturi za zama za Warumi wa kale za
kufunga ndoa kabla ya kipindi cha kufunga saumu. (kwa mujibu wa jarida la World
Book Encyclopedia, 1989 Ed.)
Maadhimisho haya
ya Jumatano ya Majivu yanayofanywa na makanisa kale makongwe, kunakuwa na
majivu ambayo waumini wake wanapakwa kwenye vipaji vya nyuso zao na makasisi
wao au wahudumu waliochaguliwa kufanya kazi hiyo. Wanavyos3ema wenyewe ni
kwamba ibada na tendo hili vinalenga kuwawakumbusha waumini wao kuwa maisha yao
hapa duniani ni mafupi na umuhimu wa wao kujindaa kwa kifo kinachokwenda
kuwafuatia.
Lakini ibada hii
haitokani na mapokeo wala imani ya Kanisa la kwanza bali chanzo chake
kinatokana na imani za kipagani iliyochukuliwa na kuingizwa pamoja na maadhimisho
ya Easter katika karne ya pili. Maadhimisho au ibada hii ya Jumatano ya Majivu
haina uhusiano wowote na maagizo ya kwenye Biblia. Mwanzoni kabisa Jumatano hii
ya Majivu ilikuwa ni siku ya kumuombolezea mungu aliyekufa na kifo cha kuteswa kipindi
hiki cha pilikapilika za sikukuu. Ni wakati walipokuwa wanachoma matawi ya
mitende ndipo hapo ndipo majivu haya yalipotokea.
Sherehe za Hilaria
ziliishia mwezi Aprili tarehe 1. Siku hii watu walienda huku na huko waliwa na
hali ya kujibadili mwonekano wao na kwa ujumla watu wangeweza kusema au
walifanya kitu chochote walichotamani kukifanya (ibid., pp.79,403).
Siku ya Mei 1 au ya
Belatine/ Mei Dei
Huko Ujerumani,
siku hii ilijulikana kama Walpurgisnacht, huko Ireland na Scotland ilijulikana
kama Beltaine au Baltein, siku ambayo mungu Baali, Beli au Balder alipochomwa
moto na kuteketezwa sanamu yake. Wakati mwingine siku hii iliadhimishwa kwa mtu
kuchaguliwa na kukatwa na kutupwa achomwe moto mahali palipokuwa panaitwa
tanuru la tita la Baler kwenye maeneo ya mashambani ya nchi za Scandinavia
(ibid., pp. 624-626). Wengi wa wasomaji wangu mnakumbuka kuhusu alivyotajwa
Baali kwenye Maandiko Matakatifu.
Zamani sana hata
Israeli walimtumikia huyu Baali. "Wakaziacha amri zote za Bwana, Mungu wao,
wakajifanyizia sanamu za kusubu, yaani, ndama mbili, wakafanya na Ashera,
wakaliabudu jeshi lote la mbinguni, wakamtumikia Baali." (2Wafalme 17:16). Soma pia Waamuzi 2:13.
Lakini Mungu alimwambia nini nabii Eliya? "Lakini ile jawabu ya Mungu
yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali" (Warumi
11:4). Sisi pia tunapaswa kuwa ni miongoni mwa hao waliobakia kuwa waaminifu kwa Mungu wa Pekee na
wa Kweli na tusiojitoa kuiabudu miungu mingine wala kuitumikia.
Hiki ndicho
kipindi ambacho mungu mke wa uchawi na ushirikina alikuwa anafikia kilele chake
cha uweza wake wote. Mabiwi makubwa yaliwashwa ili kumkaribisha huyu mungu mke.
Nabii Yeremia anatuambia kwamba wakati mwingine mioto hii iliwashwa kwa
minajiri ya kutolea kafara za watu, “nao wamemjengea Baali mahali pake palipo juu, ili
kuwachoma moto wana wao, wawe sadaka za kuteketezwa kwa Baali; tendo
nisiloliamuru mimi, wala kulinena, wala halikuingia moyoni mwangu" (Yeremia 19:5). Tunajua kwa wazi
kabisa kwamba hii haikuwa Kanuni wala maagizo ya Mungu wala sio napenzi yake.
Uchezaji wa Mziki
unaojulikana kama Maypole ni alama iliyoashiria alama ya urutubisho na ngoma.
Ngoma hii ilichezwa kwa kipindi kirefu kwa kuingiliana wachezaji wakiashiriana
mambo maovu. Mziki au ngoma hii ya Maypole ilitokana na wachezaji waliojipangwa
sawasawa Upande wa Kuume na Kushoto, ambako wanaume na wanawake walipita
katikati na kutoka kwenda kwenye duara walizozifanya huku walipeperusha
vitambaa juu walivyovifunga kwenye vinara vidogovidogo (Walker, ibid., pp.
25,26).
Sherehe ya solstaisi
ya majira ya hari ilikuwa kama ya ikwinoksi za majira ya machipuko. Matita ya
nyasi yalichomwa usiku kucha ili kulitia moyo jua lirudi. Kulikuwa na michezo
ya mashambani na iliyopangiliwa kwa mistari.
Siku ya Uhuru ya Julai
4 huko Marekani
Hii ni siku
nyingine ya utoaji kafara kwa kalenda ya kipagani. Ilipelekwa kwenye siku hii
ya tarehe 4 Julai ili ikidhi matakwa ya kalenda ya wachawi au washirikina wa
kale waliojulikana kama Wiccan, ambayo ilikuwa ni siku ya kutoa kafara za watu
au wanadamu.
Siku ya August 1 ya Lughnasad
/ Lammas
Lammas maana yake
ni Sikukuu ya Mikate. Lilikuwa ni
jina la Mkristo la mpagani Lugnasad, Mceltiki "Michezo ya Lug"
(ibid., pp. 556-556). Lug alikuwa mungu wa
nafaka aliyetolewa kafara na kufufuka ili ampe heshima heshima Mama wa Mavuno
mwanzoni mwa mwezi August.
Hii ni siki
nyingine ya kipagani ya uroaji wa kafara iliyokuwa kwenye kalenda ya kipagani.
Halloween ya Octoba 31 –
Siku ya Roho Zote ya Novemba 1
Halloween au Siku
ya Mazimwi ilikuwa ni ile iliyokuwa inaitwa kwenye nakala za Wakristo wa
Damhain kuwa ni sikukuu ya madhehebu ya Kiceltiki na ni sikukuu ya wafu.
Iliitwa na Aryan Lord kuwa ni ya Wafu. Wazo la wapagani lilitaka kuifanya kuwa
ni ya kipindi fulani maalumu tu cha majira ya "mavunjiko" iliyofunguliwa
ya majira ya frabic yaliyo kati ya “ulimwengu wa wafu na mazimwi” na ulimwengu
wa walio hai (ibid., pp. 371-372). Tunajua kutokana na Maandiko
Matakatifu kwamba sehemu walioko wafu ni pale wanapolala (Mathayo 9:24; Luuka
8:52); na kwamba hakuna wanachokijua (Mhubiri 9:5); na kwamba wako kimwa (Zaburi
115:17); na kwamba wako gizani (Zaburi 143:3). Hapo kale sana, watu wengi
waliamini kuwa roho haifi. Hii ilimaanisha kuwa wangeishi milele wakiwa kwenye
mwili wa kiroho (mizimu). Hata sasa bado watu wanaamini uwongo huu. Alama kama
za kunguru, popo nap aka ni ishara zinazofafa na maroho haya.
Alama ya pembe
yenye kumwaga tunu, inayoonekana kwenye wazi kwenye maadhumisho haya ya Siku ya
utoaji shukurani huko Marekani, ilikuwa hapo kwanza inaashishia pembe ya Mama
Mkuu akiwa kwenye umbo lake la ng’ome au la mbuzi. Majina yake yalikuwa ni Io,
Ceres, Hera, na Hathor. Waliamini kwamba kila jambo jema lilitokea kwenye pembe
yale tukufu, ambayo ilikuwa ni ishara ya maombi aliyokuwa anaombwa huyu mungu
mke. Cornucopias bado wanaonekana mara kwa mara kama mapambo ingawa watu wengi hawajui
maana yake ya kipagani na kwamba hii ni sikukuu takatifu ya dini ya kipagani
(ibid., p. 90). Siku asilia iliyokuwa imewekwa kusherehekea siku hii ya Utoaji
shukurani ilibadilishwa na kupangiwa siku hii kwa
kukidhi sababu za
kipagani na dini inayoendesha mambo kisirisiri ya Wamarekani tangu zamani.
Biblia haituambii
wala kutuamuru kuiadhimisha sikukuu yoyote katika mwezi wa 11 au mwezi
Desemba. Lakini kwa mara nyingine tena, Shetani aliingiza sikukuu hii ya
kipagani iliyojulikana hapo mwanzoni kama Saturnalia, na kuiunganisha kwa
kisingizio kinachodaiwa kuwa ni siku ya kuzaliwa kwa Kristo na hadithi za Santa
Claus. Soma jarida la Sababu Zinazotufanya Tusisherehekee Krismas (Na. CB24) [Why we don’t
celebrate Christmas (No. CB24)].
Kuna taratibu
nyingi za kidini ya kipagani zilizofungamanishwa kwenye kajira haya ya solstaisi
ya majira ya baridi iliyoanzishwa kipindi cha maelfu ya miaka iliyopita.
Kwenye kalenda ya
kale ya Warumi, Mwaka Mpya ulikuwa unaanzia siku iliyojulikana kama Ides,
ambayo ni katikati ya mwezi ya Machi. Kwa ujumla siku hii iliaminiwa kuwa ni
siku ya kufanya sherehe au tafrija mbalimbaloi za maporini na kunywa na kulewa
bila mipaka kwa kuwa walikuwa wanausherehekea ujio wa Mwaka Mpya ambao kwamba
ungeweza kuwasamehe makosa na dhambi zao zote walizozifanya huko nyuma. Hadi
siku hizi huko Ulaya, kipindi cha kabla ya Lenti kinaadhimishwa kama cha
tafrija za maporini kutenda dhambi na maovu yote mbalimbali. Baada ya
kubadilika kwa kalenda ya Warumi, Siku hii ya Mwaka Mpya ilisherehekewa baada
ya solstice ya majira ya baridi na inaangakia kipindi cha mungu Januas. Janus alikuwa
ni mungu aliyekuwa na vipaji viwili vya uso au sura mbili, moja iliangalia
mbele na nyingine myuma na hakuwa na kisogo. Walimtukuza kama Mama wa Majira na
Nyakati, aliyekuwa anatawala Vitu vya Kimbinguni akiukinga na kuuzuia Upepo
unaotokea pande za Kaskazini ambao watu walikuwa wanauogopa (ibid., p. 208).
Februari 1: Siku ya Imbolg/ya
Kuwasha Mishumaa/ Siku ya Ground hog
Hapo kale, siku
hii ya Kuwasha Mishumaa ilikuwa inaadhimishwa na Warumi ikilenga kumtukuza
mungu Juno Februata waliyemuita kuwa ni mwanakme bikira wa Mars. Waumini wa
dini hii ya kipagani walikwenda kuhiji mjini Roma ambako waliuzunguka wakiwa
wamebeba mishumaa mikononi mwao wakimuomba na kumtukuza mungu Februa. Waceltiki
walimuita Imblog, lakini ni huyuhuyu (ibid., p. 171).
Tabia za wanyama
zilichukuliwa kama dalili njema au ishara ya hali ya hewa (Sam Epstein, Spring
Holidays, Champaign, Illinois. 1964, pp. 5-11). Kwa hiyo yale maadhimisho
ya siku ya nguruwe pori, yanayoadhimishwa Marekani yanamaanisha sherehe hii na
chanzo chake ni ya kipagani.
Siku ya Valentine,
February 14
St. Valentine alichukuliwa
kama ni kiranja wa wapendanao, desturi iliyounganishwa na imani ya kale iliyotiliwa
chumvi kwamba pia kuna ndege wanaoruka kwa kufuatana wawiliwawili siku hii ya Februari
14. Au iliweza kuunganishwa na sherehe ya kipagani ya mungu wa urutubisho,
Lupercalia. Hii ilikuwa ni sherehe ambayo wanaume vijana waliwachagua wachumba
wanawake kwa kuandika majina yao na kuwaahidi kushirikiana nao kingono na mambo
mengineyo yote (kwa mujibu wa kamusi ya Oxford Australian Reference
Dictionary).
Kila tarehe 17 Machi
ilikuwa inahusishwa na wa Leprechauns ambao walikuwa ni watoto wanavaa nguo za
kijani na ambao walisababiha matatizo. Kijani inaashiria rangi asilia. Washillelagn
au Washillelagh walikuwa ni watumishi au wanachama wenye sauti kwenye kundi la
wabuni mambo yanayotumiwa na watu lakini yenye maana za kisiri maarufu kama
Occult. Ilijulikana pia kama fimbo yenye manyoya, pembe ya mnyama wa ajabu
mwenye umbo la farasi ainayeitwa unicorn, Pembe ya Moloch na Pembe ya Wataliano.
Sufuria au majungu makubwa yalitumika na wachawi kwa jinsi zilivyotengenezwa na
zinavyoashiria kwa Baraka za kifedha za Moloch.
Maandiko
Matakatifu yanasema kwamba siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa (Mhubiri
7:1). Hakuna mahali kwenye Biblia paliposema wala kuagiza watu kusherehekea siku
ya kuzaliwa. Na kwa kweli, mifano iliyoko kwenye Biblia inaonyesha kwamba haturuhusiwi
kuadhimisha siku za kuzaliwa (Mwanzo 40:20; Ayubu 1:4; Mathayo 14:6; Marko
6:21). Biblia ya Shetani imeorodhesha ikionyesha kwamba siku mtu
anaposherehekea kuzaliwa kwake anapanda daraja na kuwa kama mungu mdogo. Ingawa
tunaweza kuwa waumini tuliohesabiwa kwenye Familia ya Mungu, tujua kwamba hatu
wezi kabisa kuwa mingu sawa na Mungu kwa kuwa Mungu ni Mungu tu. Kitendo hiki
cha kusherehekea siku ya kuzaliwa ni mojawapo ya uwongo mwingine alioutunga
Shetani unaokusudia kumkufuru Muumba wetu.
Tendo linguine
linalofanyika sambamba na sherehe hii ya kuzaliwa ni kuwekwa kwa kitu
kinachoitwa Piñata. Hii pia inatokana na asili ya kipagani na hatupaswi kuwa
matendo kama haya. Hapo mwanzoni kabisa, hii Piñata ilitengenezwa kwa umbo la
nguva jike, ingawa haitengenezwi kila mara kwa umbo hili la nguva jike siku
hizi. Wakati mwingine inatengenezwa na nyota inayoonekan kwa namna sita mbalimbali.
Nyota hii inayomwakikisha mungu inatokana na chanzo kilekile walichomchukulia huyu
nguva jike. Hii ni miungu ya kipagani.
Nguva jike
alipingwa kwa fimbo ili kumvunja Piñata au kifurushi cha mbegu, ambacho alikuwa
nacho, ili kuzifanya mbegu zimwagike chini ya Ardhi na ndipo ziweze kuota. Na ndiyo sababu Piñata inamseto wa pipi/peremende
zinazoashiria mbegu.
Katika siku za
kale, waliweka ngozi ya mwandamu na kuipiga. Mara nyingi sherehe hizi
ziliendana na utoaji wa kafara za wanadamu.
Dini
inayosisitiza usawa wa kijinsia kwa Wamama na Wababa na kufana maadhimisho kwa
kutenga siku maalumu za watu hawa ilianziishwa na Warumi. Ni miongoni mwa dini
zinazoadhimisha mambo ya urutubisho, ambayo iliwakilishwa na imani ya Utatu.
Mungu wa Utatu wa Warumi alikuwa kwenye muunganiko wa Utatu na Jupita ambaye
alikuwa anaashiiwa kwa umbo la mwanaume mwenye uzazi mwingi aliyeonekana kwa
ishara ya Genii, au muunganiko wa watu wenye akili nyingi wa Dola ya Rumi.
Mungu mke Juno alionekana kwa umbo la mwanamke mzazi. Kitu cha tatu kilikuwa ni
kile Kisule kinachoonekana kimezunguka kichwa kwa juu kilichotokana na imani ya
watu wa Mashariki na kimewezesha kuleta ushawishi kwa mungu mke alikuwa bikira
aliyeonekana kuungana na miungu wengine wawili walio kwenye muundo huu wa
kiutatu. Imani hii inawakilisha nguvu au uweza wa kiroho alionao Lusifeli. Na
hii ndiyo sababu inayofanya kuwekwe madoli ya kike yenye mabawa kwenye miti ya
Krismas
Siku hizi za
Wamama na Wababa za siku hizi zinatofautiana kutoka taifa moja hadi lingine. Sehemu
kubwa ya maadhimisho haya yanafanyika kibiashara, bali baadhi yake yanaendana
sawa na chanzo chake asilia cha upagani uliokuwa kwenye dini za kale kabisa.
Kuna sikukuu
nyingine nyingi ambazo hatupaswi sisi kuziadhimisha. Kama tukiwa hatuna hakika
na sababu za maadhimisho ya siku au sikuu yoyote ile, basi na tuwaulize wazazi
wetu watuambia maana hasa ya maadhimisho ya siku ile ili tuone na kuamua iwapo
kama haina madhara yoyote kwetu kuziadhimisha.
Kumbuka kuwa
tunapokuwa na hata mzazi mmoja tu aliyeamini na kubatizwa na anamwamini Mungu
wa Pekee na wa Kweli, basi watoto wote tunatakaswa, au tunatengwa mbali na
maasi ya dunia (1Wakorintho 7:14). Kile wanachotufundisha wazazi wetu
walioamini au wanachotuambia na kutuadibisha kwa mujibu wa Biblia ndicho
kitakachotulinda dhidi ya yale tunayofundishwa na dunia.
Tunapaswa kijiepusha
kujifunza njia za mataifa.
Yeremia 10:2 Bwana asema hivi, Msijifunze njia ya mataifa, wala msishangae kwa sababu ya
ishara za mbinguni; maana mataifa hushangaa kwa sababu ya ishara hizo.
Ni jukumu letu
kumfundisha kila mmoja wetu ajifunze kumcha na kumuabudu Mungu kwa usahihi
zaidi na kwa kila mara yale tunayojifunza na kuyaamini husuan juu ya Siku zake
Takatifu zilizoamriwa na kwa nyakati zake za kuziadhimisha. Soma jarida la Siku
Takatifu za Mungu (Na. CB22) [The Holy Days of God (No. CB22)].