Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[CB28]

 

 

 

Jeshi la Mbinguni

 

(Nakala 1.0 20060715-20060715)

 

Mungu Mmoja wa kweli (Eloah) akawa Baba hapo alipoumba Wana wake wa Kiroho. Katika Somo hili tutaangalia kwa kifupi vyeo na kazi za asili ya Uumbaji wa Ulimwengu wa Kiroho.

Familia ya Mungu.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Haki milki © 2006, Makanisa ya Kikristo ya Mungu, ed. Wade Cox)

 

Somo hili linaruhusiwa kunukuliwa, na kusambazwa kwa yeyote mradi tu kama litanukuliwa kikamilifu, bila kubadilishwa au kuondoa namna halisi, Jina la Mchapishaji na anuani yake na tangazo la hati milki lazima vijumlishwe. Hakuna gharama yoyote ipaswayo kuchangiwa na mtumiaji na hairuhusiwi kuuzwa nakala zake kwa msomaji. Nukuu chache zaweza kuchukukuliwa katika makala zinazo tofautiana kimtazamo na kimaoni bila kukiuka maadili ya haki milki.

 

Somo hili linapatikana pia katika Tovuti zetu popote Duniani

 

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


 

 

Jeshi la Mbinguni

 


Biblia inatufundisha ya kwamba Mungu Mmoja wa kweli ni Mungu asiyeonekana kwa macho, na hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote au kusikia sauti yake (Yn. 1:18; 5:37). Mungu (Eloah) ana uzima nafsini mwake. Kwa hiyo hakuhitaji kuthibitika kwa kuonekana, maana Uzima hutoka kwake. Uzima pekee ni jambo la kushuhudia ya kwamba Mungu Yuko na yu Hai, na ni uzima wa milele, maana kitu ambacho si hai hakiwezi kutoa uhai. Uhai ni uzima utokao, mahali pale tu palipo na Uhai, na Uzima. Hivyo Mungu ni Uzima, tena ni Uhai maana vyote hivi vinamshuhudia Yeye, na vyote vyatoka Kwake (Yn. 5:26; 1Tim. 6:16). Daima alikuwako, na Daima atakuwako, na Daima Yuko wakati wote. Mungu aliyeko na Aliyekuwako na Atakayekuja, Mwenyezi. Kuna wakati Mungu alikuwa peke yake, lakini aliamua kuzaa Familia kwa ajili yake Mwenyewe. Angalia Somo la Mungu ni Nani? (Na. CB1).

 

Kitu cha kwanza kabisa kutoka kwa Mungu na ambacho yeye Mwenyewe alitoa kutoka kwake alikuwa ni Roho Mtakatifu. Katika Roho Mtakatifu Uumbaji wote uliofuata baadaye ukifungamana kwa Mungu kwa sababu hakuna chochote kilichofanyika pasipo Roho Mtakatifu wa Mungu, na Roho Mtakatifu alitoka kwa Mungu. (Roho ndiyo itiayo uzima, ni Roho tena ni Uzima. Kutoka hapo Mungu alizaa (aliumba) Wana wa Kiroho katika uwezo wa Roho Mtakatifu na wote waliungana na Mungu katika Roho Mtakatifu, na waliweza kutenda kazi sawasawa na Mapenzi ya Mungu kwa maana waliongozwa na Roho Mtakatifu ambaye ni Roho wa Mungu aliyetoka kwa Mungu. Ilikuwa ndiyo sababu ya Mungu kuwa Baba wa Wana wa Kiroho maana amezaa Wana kwaa njia ya Roho mtakatifu (Ebr.12:9). Angalia Somo la Roho Mtakatifu ni nini? (Na. CB3).

 

Hawa ni Wana wa Mungu aliye Juu sana wote wanaitwa elohim (kutoka Zab. 82:1) kwa ngazi za utendaji tofauti tofauti. Waliumbwa Wakamilifu, na kwa kuendelea kumtii Mungu (Eloah). Na wataendelea kuishi milele kama Wana wa Kiroho wa Mungu.

 

Malaika ni nani au ni wa namna gani?

Malaika ni wajumbe wa Mungu wanaotumwa kutenda kazi za Mungu. Wana wa Kiroho wa Mungu hawakuitwa malaika mpaka baada ya Uumbaji wa Adamu. Kwa sababu kabla ya Adamu, hakuna yeyote aliyehitaji kupelekewa ujumbe, kwa hiyo hapakuwa na sababu ya kuwapo kwa wajumbe ambao ni Malaika.

 

Malaika waliumbwa katika Roho na ni Roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi Wokovu (Ebr. 1:14). Mungu aliwaumba Wana wake wa Kiroho kabla ya Uumbaji wa nchi (Ayubu 38:4-7). Kuna zaidi ya malaika milioni 100 (Angalia Dan. 7:9-10; Mt. 26:53; Lk 2:13; Ebr. 12:22; Ufu. 5:11). Malaika wameumbwa katika hali ya mmoja mmoja (individuals) ambao wana uhuru wa kuchagua, ambao ndiyo unahitajika katika kukua kwa tabia.

 

Neno la Kiebrania, mjumbe (messenger) katika Agano la Kale ni Malaika na linatafsiriwa kama Malaika (angel) katika Biblia za Kingereza. Neno linatumika katika kuonyesha wajumbe wa Kiroho waiotumiwa na Mungu. (Mwa. 32:1-2) na pia lilitumika kwa wajumbe wanadamu waliotumwa na Yakobo (Mwa.32:3).

 

Katika Agano Jipya, neno la Kigriki, mjumbe (messenger) ni aggelos, ambapo tunapata neno katika kiingereza angel yaani malaika, au mjumbe. Neno hili pia linatumika katika sehemu zote katika wajumbe wa kibinadamu na wajumbe wa Kiroho.

 

Mungu alituma wajumbe mbalimbali. Kwanza kulikuwa na wajumbe wa manabii na wa wanadamu (2 Nya. 36:15-16). Pili, kulikuwa pia na wajumbe wa Kiroho (malaika) waliotumwa na Mungu kwenda kwa wanadamu kwa madhmuni ya kupeleka ujumbe maalumu au kwa madhumuni ya kutenda kazi.

 

Kama mawakili wa Mungu walitumwa duniani kutoka mbinguni, kuchukua au kuleta maamuzi ya Mungu, juu ya wanadamu katika kutimiza adhabu ya Mungu kwa wanadamu, na katika kuwafundisha wanadamu (kut.12:23; Zab. 104:4; 2 Sam. 24:16; 2 Fal. 19:35; 1 Nya. 21:16; Matendo 12:23; Ebr. 11:28; 1 Kor. 10:10).

 

Malaika pia walichukua ujumbe wa Mungu kuwapelekea manabii wa Mungu na kuwalinda watu wa Mungu (Zab. 34:7; 91:11; Dan. 6:22; Mt. 18:10; Ebr. 1:14). Malaika walioonekana kwa wanadamu daima walikuwa katika umbo la kibinadamu (Mwa. 18:2; 19:1,10; Lk.24:4; Mdo. 1:10).

 

Wana wa Kiroho wa Mungu pia wanatofautiana katika ngazi na katika uwezo wa utendaji, (Zek. 1:9,11; Dan. 10:13; 12:1; Efe. 1:21; Kol. 1:16; 1 The. 4:16; Yuda 1:9). Malaika wamepewa uwezo na nguvu ya utendaji (2 The.1:7); “wanaitwa wenye nguvu na uwezo mwingi” (Zab.103:20). Ni “Watakatifu” (Lk 9:26), ni “Wateule” (1 Tim. 5:21). Hawasitahili kuabudiwa au kusujudiwa (Kol 2:18; Ufu. 19:10).

 

Malaika wengine wana mabawa na wengine wanafanana kama sanamu wakiwa na sura za nyuso mbili, ambapo uso mwingine unaweza kuwa ni uso unaofanana na nyuso za wanyama na uso mwingine unaofanana na wanadamu. (Eze. 1:4-14; Isa. 6:1-3) wanaweza kubadilika katika maumbile yao na kufanana na maumbile ya kibinadamu wanapoonekana kwa wanadamu (Ebr. 13:2). Wakati wote wana miili ya kung’aa na wanavaa mavazi meupe (Mdo 1:9-11; 22:6-9; 2 Sam 22:13).

 

Wanadamu hawaruhusiwi kumwona Mungu, kwa hiyo Malaika wanawasaidia wanadamu katika kumjua Mungu Mmoja wa kweli, (Eloah).

 

Malaika katika Agano la Kale

Mjumbe muhimu anayetumwa na Mungu anayeitwa “Malaika wa Bwana”, au “Malaika wa Mungu” katika Biblia za Kingereza. Majina haya yenye vyeo hivi huitwa Malaika Maalumu (au wajumbe) ambao wanamwakilisha Mungu. Alikuwa mara kwa mara anaitwa Yehova.

 

Watu wa Agano la Kale walimtambua huyu Mjumbe au Malaika aliyetoka kwa Mungu kuwa hakuwa Mungu Mmoja wa kweli. Walijua ya kwamba Mungu (Eloah) alijifunuwa na kujidhihirisha kwao kwa kupitia kwa hao malaika wa Mungu, ambaye pia walimwita Elohim. Wakati malaika wa Yehova alikuwa pamoja nao, ilimaanisha ya kwamba Mungu (Eloah) alikuwa yuko pia pamoja nao. Malaika alisema na kutenda kwa niaba ya Mungu Mmoja wa kweli.

 

Malaika wa Yehova ambaye mara kwa mara alishughulika na wanadamu, alikuwa ni mungu (god) wa Waisraeli (k.m. Elohim). Alimwakilisha (Eloah), Mungu Mmoja wa kweli ambaye Waisraeli walimwabudu. Huyu Malaika wa Yehova, aliyeshughulika na wandamu ndiye yeye ambaye baadaye alijidhihirisha, na kuwa mwanadamu Yesu Kristo. Tazama katika Somo la Yesu ni nani? (Na. CB2).

 

Hebu tuangalie matukio mengine mengi, ambayo Malaika huyu, alionekana na kuzungumza na wanadamu katika nyakati za zamani.

     Malaika alizungumza na Hajiri mara mbili (Mwa. 16:7-13; 21:17-18)

     Malaika alizungumza na Ibrahim (Mwa. 12:1-3; 22:11-18).

     Malaika alizungumza na Yakobo katika ndoto (Mwa. 28:11-21; na 31:11-13; Angalia pia Mwa. 32:24-30).

     Malaika alimtokea na kuzungumza na Musa (Kut 3:1-6; 24:12-16).

     Malaika katika mawingu (kut. 13:21; 14:24)

     Malaika akiwa kama mhifadhi, Mlinzi na Mwokoaji (zab. 34:7; 35:5-6).

 

Biblia inasema alikuwa ni Malaika wa Yehova, ambaye ni Yesu Kristo, ndiye aliyetenda haya yote (Mdo. 7:30-38, 53; Gal. 3:19).

 

Mtume Paulo alisema ya kwamba alikuwa ni Kristo ambaye, ndiye aliyewavusha wana wa Israel katika bahari (1 Kor. 10:1-4). Paulo pia anamtambulisaha Malaika wa Mungu kama Yesu Kristo katika Wagalatia 4:14. Tazama somo la Malaika wa Yehova (CB24).

 

Matukio mengine ambayo Malaika aliwatokea Wanadamu;

     Baalamu na Malaika (Hes. 22:22-35)

     Yoshua na Malaika (Yos. 5:15)

     Gidioni na Malaika (Amu. 6:12-24)

     Wazazi wa Samsoni na Malaika (Amu. 13:2-20)

     Daudi na Malaika (2 Sam. 24:16-17)

     Eliya na Malaika (1 Fal. 19:5-12 na 2 Fal. 1:15)

     Malaika na Daniel (Dan. 3:24-25, 28)

     Malaika na Zekaria (Zek. 1:9,13-14,18-21; 2:3; 4:1,4-5; 5:5,10)

 

Malaika katika Agano Jipya:

Tunaona ya kwamba Malaika walimhudumia Yesu wakati alipokuwa katika nchi (duniani) (Mt. 4:11, Lk. 22:43). Malaika alimtokea Yusufu na kumwarifu habari za kuzaliwa kwake Yesu (Mt. 1:20, Lk 1:26-38). Malaika walikuwepo katika ufufuo wa Yesu (Mt 28:2-8; Yn. 20:12). Na walizungumzia wakati wa kupaa kwakeYesu Kristo (Mdo 1:9-11). Malaika wanatoa  huduma za Kiroho kwa watu wa Mungu  (Ebr. 1:14; Mt. 18:10; Mdo 5:19; 8:26; 10:3; 12:7; 27:23).  Malaika hufurahi mwenye dhambi anapotubu (Lk. 15:10).

 

Katika Agano Jipya, Kristo kama mwanadamu bado alitenda kama mtu aliye  mdhihirisha na kumfunua Mungu. Na alitenda kwa ukamilifu akifuata asili ya Mungu na tabia ya Mungu. Kama Mpatanishi kati ya Mungu na Wanadamu, kumwona Yesu ni sawa na kumwona Mungu, na kusikia na kumtii Yesu ni kumsikia na kutii Mungu (Eloah). Maneno aliyozungumza hayakuwa maneno yake mwenyewe bali maneno ya Mungu yaliyotoka kwa Mungu. (Yn. 14:8-10)

 

Vyeo mbalimbali vya Jeshi la Mbinguni

 

Malaika wana vyeo, uwezo na nguvu zinazotofautiana katika utendaji wa kazi mbalimbali.  (Zek. 1:7-11; Dan.10:13; 12:1; 1The. 4:16; Yuda 1:9; Efe. 1:22; Kol 1:16).

 

Enzi Utawala, Nguvu, Mamlaka,

 

Tunajua ya kwamba Kristo alikuwa ni mzaliwa wa kwanza katika uumbaji, ambapo baada ya hapo Mungu hakuumba Wana wake wengine bali katika Yesu Kristo  aliumba (k.m. alitengeneza) enzi, utawala  (ufalme) mamlaka na Serikali. Hizi ni katika mambo ya utawala wa kimwili na sio katika mambo ya utawala wa Kiroho. Lakini vyote vyatokana katika Kristo (Kol.1:16-17 ).

 

Maserafi:

 

Kuna maserafi na wana mabawa sita (angalia Isa. 6:2,6). Wana nguvu uwezo wa kuondoa makosa yaletayo dhambi na kuwandaa manabii kwa kuwatakasa (Isa. 6:7).Kuwa na mabawa sita  inadhihirisha ukuu na uwezo wao katika katika utendaji wao wa kazi mbalimbali.

 

Neno maserafi ni neno la wingi wa neno saraph (SHD 8314) likiwa na maana ya mwenye kuchoma kwa moto. Kwa sababu ya nyoka katika Hesabu 21:6,8 walikuwa na sumu inayochoma kama moto wakati wanapouma, kwa hiyo wakaitwa maserafi. Kwa hiyo hawa maserafi ni “nyoka wa  moto wa  mbinguni” (linganisha pia Kum. 8:15; Isa. 14:29; 30:6). Mungu aliwatuma ili waweze kuwadhibu watu waliotenda dhambi. Maumbile yao walionekana kuwa kama wandamu kwa vile walikuwa na nyuso, mikono na miguu juu ya umbile lao la kuwa na mabawa. Wanawakilishwa kama wenye “kusimama wakati wote” juu ya wote. Mfalme anaposimamisha enzi yake, tayari kwa kumhudumia.

 

Hawa ndiyo Malaika Wakuu na wana nafasi muhimu sana katika Jeshi la mbinguni. Ni Malaika wakuu ndiyo mara nyingi hutumwa katika nchi kuleta ujumbe wa Mungu na maonyo kwa wanadamu na kwa manabii.

 

Katika kitabu cha Henoko kinataja majina ya  Malaika wakuu sita:

Mikaeli (Mkuu wa sehemu mhimu sana ya wanadamu) Gabriel (Mkuu wa Majoka, Bustani na wa Makerubi), Urieli Malaika Mkuu wa dunia na watu wakali) na Raphaeli (Malaika Mkuu wa Roho za wanadamu), Ragueli (ambaye analipiza kisasi juu ya dunia na mwangaza) na Saragaeli (Malaika Mkuu wa watoto wa wanadamu, ambao Roho zao wametenda dhambi).

Kitabu cha Henoko, sura ya 20, R.H Charles, 2002).

 

Malaika hawa pia wanaitwa Malaika Walinzi.

 

Malaika Mkuu Gabriel:

 

     Alitafsiri  maono ya Danieli (Dan. 8:16, 26; 9:20-27)

     Alitangaza  juu ya kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji (Lk. 1:11-20)

     Alitangaza  kuzaliwa kwa Yesu (Lk. 1:26-38).

 

Malaika Mkuu Mikaeli:

 

Mikaeli Mwana mkuu wa Mfalme, ametajwa mara nyingi katika Agano la Kale.

     Katika Daniel 10:13 ametajwa “Jemedari mkuu aliyekuja kunisaidia.” Angalia pia Daniel 12:1

 

     Yuda 1:9 Mikaeli Malaika Mkuu, anagombana na Shetani kuhusiana na Mwili wa Musa.

 

     Ufunuo 12:7-8 Mikaeli pamoja na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake.

 

Hawa maserafi wanatambulikana kama makerubi wanaokizunguka Kiti cha Enzi cha Mungu kama tunavyoona sasa.

 

Makerubi:

 

Kiti cha Enzi cha Mungu kinazungukwa na wanyama wane wenye vichwa tofauti. Hawa ni Simba, Ndama, Tai na Mwanadamu, wanatambulikana kama Makerubi (umoja Kerubi) wako wanne katika jumla ya hesabu yao na wana mabawa sita wanakizunguka Kiti cha Enzi cha Mungu (Ufu. 4:6-9). Waliubwa wakiwa wanne (tazama mwisho wa Biblia ya Companion Uk 10). Maelezo ya makerubi yanaelezewa katika Ezekiel 1:5-14; 10:20; na Ufunuo 4:6-9. Ambapo wameumbika katika viungo mchanganyiko katika Ezekieli wakiwa walinzi wa Yehova wa Israeli na wanaonekana wenye mabawa manne katika viwiliwii vyao vya juu. Hapa hawajatajwa kuwa na mabawa mawili katika miguu yao kama wale makerubi wanaokizunguka Kiti cha Enzi cha Mungu, au wale wa moto katika Agano la Kale. Idadi ya hao makerubi kuwa wanne inatokana na Uumbaji. Wakati makerubi hawa wanapotumwa katika nchi, kwa ajili ya Yehova wa Israeli, na kutenda kwa pamoja huwa na mabawa manne na wanatembea pamoja katika gari daima wakiangalia sehemu moja. Makerubi wanaokizunguka Kiti cha Enzi cha Mungu wana mabawa sita kama maserufi.

 

Mfano wa vichwa vya viumbe wanaokizunguka Kiti cha Enzi cha Mungu wanatabulikana kama makerubi katika Ezekieli 1:1-28. Angalia Somo la Maono ya Ezekieli (Na. 108).

 

Vichwa vya wanyama vinaashiria vita vya Wana wa Israeli na mgawanyiko wa makabila katika idadi ya 10 na 11. Angalia Somo la Uumbaji wa Familia ya Mungu (Na. CB4).

 

Tangu mwanzo kulikuwa na makerubi wanne, makerubi wawili wanakizunguka na makerubi wawili wakisimama nyuma ya Kiti cha Enzi cha Mungu. Ezekieli 1:4-14 anaelezea juu ya makerubi wane; na hii ndiyo idadi ya “viumbe wane wenye uhai” wanaotajwa katika Ufunuo 4:6

 

Makerubi wanatajwa katika kitabu cha Mwanzo 3:24 ambapo tunasoma ya kwamba Mungu alimfukuza mwanadamu kutoka katika Bustani ya Edeni na kuweka Makerubi, na upanga uwakao moto katika sehemu ya Mashariki ya Bustani ya Edeni, kumzuia mwanadamu asirudi na kula tunda la mti wa uzima.

 

Katika 2 Samweli 22:11; Zab. 18:10 na Ezekiel sura 1,9 na 10 inaonekana ya kwamba uzima wa milele umesimama juu ya makerubi wanne.

 

Tunaona mifano ya Makerubi inavyotumika, katika Hema ya kukutania pamoja na kwenye Hekalu. Wale waliyo katika Sanduku la Agano wanaitwa “Makerubi wa Utukufu” (Ebr 9:5), kutoka kwa hao Makerubi Utukufu wa Mungu unaoonekana hukaa kwao.

 

Makerubi wawili walitengenezwa kwa dhahabu, na wakiangaliana na mabawa yao yakiwa yameinuliwa, huwekwa juu ya sanduku la Agano (Kut. 25:17-20). Mungu (kwa kupitia katika malaika wake aliahidi kuzungumza na Musa “kutoka kati ya Makerubi” (kut. 25:22). Mifano ya makerubi iliwekwa katika mapazia ya Hema ya kukutania (Kut.26:1,31).

 

Mfalme Sulemani alikukuwa na makerubi wawili waliotengenezwa kutokana na mbao za mzeituni, na kuwekwa Hekaluni. Makerubi pia waliwekwa milangoni na kwenye sehemu za ukutani katika Hekalu, na mifano ya makerubi iliweza kushonewa katika nguo zilizotumika Hekaluni (1 Fal. 6:23-35; 2 Nya. Sura ya 3).

 

Ingawaje Biblia inatwambia ya kwamba tusijifanyie sanamu ya kitu chochote cha mbinguni au cha duniani (Kut. 20:4; Kum. 4:16), Wana wa Israeli waliamriwa kufanya picha za makerubi katika kuta za hema ya kukutania. Hizi zilikuwa ni mifano tu na hazikuwa za kuwabudiwa. Hema ya kukutania ambayo Musa alijenga na Hekalu alilojenga Sulemani ilikuwa mifano halisi inayowakilisha mambo ya mbinguni.

 

Nyota ya Asubuhi

 

Nyota ya Asubuhi, Nyota ya Mchana au Mleta Nuru ni sifa tu za Jeshi la Kiroho na wala si majina yao (Ayubu 38:1-7).

 

Nyota ya Asubuhi ilionekana kutenda kazi kama Makerubi. Nyota ya Asubuhi ya sasa, Lusifa, alikuwa ni mmoja wa makerubi watiwa mafuta kabla ya kuasi kwake. Cheo hiki alichokuanacho Lusifa, pamoja na mamlaka na nguvu ya Kishetani aliyonayo kama mungu, (god) wa Sayari hii itaondolewa na kuvuliwa hapo Kristo atakaporudi mara ya Pili. Tazama Ufunuo 22:16.

 

Mbali na shetani na Kristo kuna viumbe wengine katika Jeshi la Kiroho wanaotenda kazi katika cheo kimoja. Angalia Somo la Lusifa: Nuru ing’aayo na Nyota ya Asubuhi (Na. 223). Katika Uumbaji wa Sayari, nyota za Asubuhi zilikusanyiaka pamoja na kuimba pamoja, na kupiga kelele na kushangilia kwa furaha pamoja na Wana wa Mungu. (Ayubu 38:4).

 

Je, Mungu ndiye aliyemuumba shetani?

 

Mungu aliwaumba Wana wake wakiwa Wakamilifu na Watakatifu, lakini walikuwa na uhuru wa kuchagua Kumtii Mungu au Kutomtii Mungu. Tunajua ya kwamba wengine kati yao walitenda dhambi, na Biblia inawataja kama “Malaika walioanguka” (Mwa. 6:2,4; Yuda. 1:6)

 

Lusifa alikuwa amejaa hekima na alikuwa Mkamilifu katika uzuri wote, lakini aliingia katika majivuno na kuwa asiyefaa kitu na kugeuka kuendelea katika njia ya dhambi, (Ezekieli 28:12-15). Alifikiri angeweza kujiinua juu ya Kiti cha Enzi cha Mungu (Isa. 14:12-14). Maasi yake yalishindwa na kutupwa chini, duniani katika nchi (Lk 10:18; pia katika Ufu.12:7,9). Lusifa alishawishi theluthi ya malaika kumfuata katika maasi yake. Ambao alifukuzwa nao na jina lake likabadilika na kuitwa shetani, yule joka mkubwa (Ibilisi) na malaika waliofuatana naye wanajulikana kama pepo wachafu (demons). Wote wanajulikana kama “Jeshi lililoanguka”. Angalia katika Somo la Shetani ni nani? (Na. CB60).

 

Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata itakapokuja ile hukumu (1 pet. 3:18-20; 2 Pet. 2:4-5; Yuda 1:6). Mapepo wengine wachafu, huzunguka zunguka katika dunia hii wakitafuta watu ili wawameze (Ayubu 1:6-12; Lk 8:30-32).

 

Ni nini kitakachotokea kati ya shetani na mapepo wabaya?

 

Kristo alihitimu katika kumkomboa mwanadamu na jeshi lililoanguka. Alilipa adhabu na fidia, pale msalabani kwa dhambi zetu zote (Kol.1:19). Ni Mapenzi ya Mungu ya kwamba hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wapate kutubu (2 Pet. 3:9).

 

Kwa hiyo ni dhahiri ya kwamba mapepo wabaya wote watahukumiwa katika Ufufuo wa pili wa wafu. Na yule Ibilisi, ambapo watakuwa katika umbo la kimwili kama wanadamu watakao fufuliwa. Watakuwa na nafasi ya kutubu na kubadilika kuwa wana wa kroho wa Mungu. Soma Biblia inasema nini katika Isaya 14:11-17. Tunaona shetani anatajwa kama mwanadamu anaetoka katika shimo katika msitari wa 14. Tunaelewa ya kwamba Kristo kama Mwana wa kroho wa kwanza wa mwanzo alifanyika mwanadamu na akafa katika kifo cha kimwili. Kwa hiyo hilo pia linawezekana kwa shetani na mapepo. Walakini, katika matokeo ya dhambi ya shetani na mapepo hawatahachwa bila kuadhibiwa. Jambo moja hawatarudishwa tena katika nafasi zao walizokuwanazo kabla ya kuasi.

 

Mwisho wa Mwanadamu

 

Mungu ni Roho na kilichozaliwa kwa Roho ni Roho, Kwa hiyo Uumbaji wa kwanza wa Mungu ulikuwa ni Uumbaji wa viumbe vya Kiroho (Yn. 3:6). Mtu wa kwanza aliumbwa na Mungu, lakini alitoka katika  mavumbi ya ardhini, kwa hiyo aliumbwa kama kiumbe kinachoonekana katika mwili. (kiumbe chenye mwili unaoonekana) pia akaitwa mwana wa Mungu (Lk 3:38). Uumbaji wa kimwili katika umbo la mwanadamu ilikuwa ni uumbaji wa pili wa Mungu.

 

Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili, (Yn. 3:6) na mwili na damu haviwezi kurithi Ufalme wa Mungu (1 Kor. 15:50). Lakini mwisho wa wanadamu ni kuwa ‘wana wa Mungu’, k.m kuwa Wana wa Mungu wa Kiroho. Wote wanomjua Mungu Mmoja wa kweli na Yesu Kristo, Mwanae aliyetumwa na Yeye, na kutubu na kubatizwa na kupokea Neema ya Roho Mtakatifu wa Mungu wanayo haki ya kuwa Wana wa Mungu  (Yn. 1:13; Rum. 8:14-15; 1Yoh 3:1).

 

Wale watakaofufuliwa katika ufufuo wa kwanza watabadilika na kuvaa miili ya Kiroho na kutawala kama warithi pamoja na Kristo katika kipindi cha miaka elfu moja ya Mileniamu. Wale watakaofufuliwa katika ufufuo wa pili ambao ni ufufuo wa marekebisho na hukumu, iwapo wataonekana ya kwamba wanafaa na kuhitimu kwa kuwa na sifa yakuwa Wana wa Mungu, basi watabadilishwa na kuvikwa miili ya Kiroho.

 

Mpango wa Mungu wa Uumbaji wa Familia yake, hautakuwa umekamilika mpaka baada ya kumalizika kwa hukumu ya mwisho, na kubadilika kabisa kwa sayari yote (dunia). Hapo sayari yote (dunia)itakapobadilika katika Uumbaji mpya yaani Mbingu Mpya Na Nchi Mpya, wote watakuwa Wana wa Mungu kama Elohim katika Roho Mtakatifu, wote watakuwa wamekamilika katika Umoja wa Uungu, kama Familia ya Mungu waliyounganishwa katika Roho mtakatifu na kuungana na Mungu kama Familia ya Mungu.

 

Kwa maelezo zaidi na mafunzo zaidi soma somo la

Serikali ya Mungu (Na. 174)

Jinsi  Mungu anavyokuwa  Familia (Na. 187)

Hukumu ya Pepo wachafu (Na. 80)

q