Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[054]
Jina La Mungu Kwenye Uislamu
(Toleo La
1.0 20020126-20020126)
Kutoka Septemba tarehe 11 mwaka 2001
kumekuwa na kiasi kikubwa cha ufichaji wa habari na visingizio vya kitoto
ikitokea kama matokeo ya kuelekea kwenye historia na midahalo huko Marekani, hususan
kwenye mifumo na imani zake za kidini. Utumiaji wa jina la Mungu ni mojawapo ya mfano huo.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 2002 Wade Cox)
(Imetafsiriwa
Mwaka 2009; rev. 2017)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Jina La Mungu Kwenye Uislamu
Mara nyingi mtu
anaweza kupumbazwa na kukerwa na kiwango kikubwa cha ujinda wa kutokujua wa
imani za kidini za ulimwenguni humu. Kwenye majadiliano ya siku nyingi kumekuwa
na kiwango kikubwa na kisicho cha kawaida cha kisingizio cha imani ya Kiislamu
iliyotiliwa mkazo, au ni kama ni matokeo yake, ndipo mashambulizi ya kigaidi
yanatokea kwenye imani za Waafghani chini ya Wataliban na mtandao wa Bin Laden majibu
ya kimatokeo makubwa ya Washirika wao. Majarida mengi yamekuwa yakizungushwa
ambayo ni ya uwongo sana, lakini tena yamewakilishwa kwa njia ya kimadai,
ambaye ni mwanazuoni msomi wa Dini Zinazolingana mambo yake angeweza kucheka
ayaonapo madai haya. Hata hivyo, idadi ya watu, ambao hawajajulishwa vya
kutosha, wanakuwa wamechukuliwa kwenye maandishi au nakala za kidini.
Hadithi moja kama
maelezo na alama au maandishi hayo yanahusu jina la Mungu au Allah kwa Kiislamu.
Tutaangalia
baadhi ya madai yahusuyo mambo haya. Huenda tunaweza kupata ukweli kidogo na
sababu kulingana na ukweli wa mambo yanayobishaniwa.
Dai mojawapo kuhusiana
na jina hili la Allah ni kufanya mizunguko ifuatayo.
“Iwapo kama hii ingekuwa ni historia ya iliyothibitishwa, basi kitabu
kidogo cha maandiko kingeeleza kwamba mungu wa Muhammadi alikuwa ni kazi iliyobuniwa
na wanadamu. Saudi Arabia lilikuwa ni taifa la kipagani lililoabudu zaidi ya miungu
300. Mmojawapo kati ya miungu hiyo alikuwa ni mungu mwezi aliyejulikana kama
al-ilah. Hadithi zinasema kwamba huyu mungu mwezi aliolewa na mungu wa jua na
walizaa mabinti wawili, na hawa wawili nao waliabudiwa kama miungu midogo ya
kike. Wakati Muhammadi alipodai kuwa ameonyeshwa au kupokea ‘maono’ yake na ‘ufunuo
kutoka kwa Gabrieli’ alimchagua al-ilah kama ndiye mungu kujenga jeshi lake
karibu. Muhammadi alilifupisha jina hili la al-ilah na kuwa Allah, na
kumtangaza kwamba ni yeye peke yake ndiye anayefaa kuabudiwa. Alikataza na kupiga
marufuku ibada za kuwaomba wale mabinti. Mpaka siku hii ya leo, sanamu ya mwezi
mwandamo mchanga inaweza kuonekana mbele au juu au mahala popote muhimu kwenye
kila msikiti, ikiwa ni ishara ya kukubali kwamba Allah alikuwepo na ni mungu wa
mwezi. Haya yote yamekosekana kuandikwa kwenye maandiko ya makala ya Houghton-Mifflin”
Sasa machoni mwa
malumbano haya ingeonekana kuwa ni hoja yenye kukubalika kwa wasiojulishwa na
kwa kweli imeenea kwa baadhi kuwa ni mtazamo hakisi na sahihi.
Kumbuka mwandishi
anashambulia maelezo na hoja za Houghton-Mifflin kwa kuwa hazina kile
kinachowakilishwa kama ni ukweli unaothibitika. Inataka kudai na kutafuta maeneo
ya kushindwa kwa watunzi ili kuonyesha amani hii ya thamani ya habari. Haishangazi
kuona kwamba maelezo hayo hayana rejea kama hizi, kama madai hayo ni ya uwongo
yote kabisa, kama tutakavyokwenda kuona.
Majina
ya Mungu Mwezi na Mwezi Wake Jua
Jina la Mungu Mwezi
hapo mwanzoni liilikuwa Sin alivyojulikana kwa Waisraeli. Waarabu walimpatia mungu
huyu mume jina la Qamar na mwenzi wake walimuita Shamsi. Nabari zake kwa kina zinapatikana
kwenye jarida la (Ndama wa Dhahabu (Na. 222)).
Mungu jua alikuwa
ni mwenza wa kike. Majina tunayoyapata
miongoni mwa Selti yanatokana na majina haya. Kwa mfano jina James, yaani
Yakobo linatokana na aina ya jina hili la Shamus na linatokana na imani hii.
Ndivyo ilivyo pia kwa miungu ya Milkomu na Kemoshi ya kipagani ya wana wa Lutu.
Mungu Milkomu anahusiana katika jina la Malkomu.
Jina Al ilati linalozungushwa
na kuenea kama tunavyoona hapo juu ni upotoshaji wa mmoja wapo kati ya miungu
mike mitatu ya kike. Jina Al ilati ni muundo wa kizamani sana wa Mungu jua
aliyetajwa kwenye maandiko ya Herodotus i. 131, iii, 8. Huyu alikujakuwa Al lati ama Allati na maana yake
ni mungu mke. Alikuwa anaabudiwa na Waarabu
wa peninsula ya Sinai na hasa hasa wa jamii ya Nabateani na Palmyrenesi.
Herodotus anadai kwenye ukurasa wa pili kwamba ‘alilati na ‘arotalti ni
miungu mikuu wa Waarabu. Noldeke (ERE
I, ukurasa wa 661) kinatuofanya tulione jina kuwa ni kama mtindo wa kizamani
sana wa jina Allati na kinalinganisha na jina Al’ilah, ambalo ni jina la kale la
Allah. Kwenye vifungu vyote viwili vya Herodotus vinamuonyesha yeye na Ούρανίη na hivyo basi mungu mke mkuu wa kuheshimiwa na kustahili.
Maelezo ya uthibitisho
kwamba al itati mungumke hahusiani na
Allah ni taarifa iliyotolewa na Muhammadi mwenyewe kwenye Korani katika sura ya
1iii:19, ambapo anamwelezea al ilati
kama ni mmoja wapo wa miungu mitatu ya mbinguni, Ali Lat, Al Uzza, na Manati
kama wa tatu. Alikanusha uhusiano na mshikamano wao na kumuweka Allah kuwa ni
kama Mungu mmoja wa Kweli. Kwenye Sura hii anaendelea mbele kwa kukanusha
kuombwa na kuabudiwa au kutukuzwa kwa Sirius (Sura ya 1iii, 50) katika kuilaani
imani ya kwamba Siriusi mwenyewe alikuwa
na nguvu za kimungu.
Al Lati pia
anajulikana au kutajwa kwenye maelezo katika Safa kama LT na pengine HLT. Anajulikana
kama ni Mama wa Miungu. Jina hili linaonekana wazi kutamkwa kama Hallati.
Alipewa heshima kubwa na kutukuzwa miongoni mwa Warabu wa baadaye.
Mungu jua aliyechukuliwa
jupokea heshima maalum kwa Wanabateanis na kutambuliwa na Strabo (784) pia ilijulikana
kuwa Al Lat (ERE ibid.).
Dini potofu ilikuwa
huko Ta’if hadi mashariki mwa Maka na kabila la Thaqif lilimwongelea yeye kuwa
ni kama mkunga.
Dini potofu nuhimu
ya nyakati zilizofuatia pia ilikuwa ni dini ya Al Uzza, ambayo ilikuwa ni ya
kuiabudu sayari ya Zuhura yaani Venus. Jina hili kwa maana nyepesi limaanisha “Nguvu au Uweza”.
Manat huenda alihusiana
na mungu wa Meni (Isaya 65:11). Manati alikuwa anaheshimiwa na kuabudiwa na
kutukuzwa na kabila la Hudhaili karibu na Maka na hasa hasa miongoni mwa
wakaazi wa Yathribi (Madina). Tukio la jina lake liko wazi kwamba dini hii
potofu ilipatikana kwenye sehemu kubwa ya Saudi Arabia.
Kwa sababu hii Mtume
Khasimu (aliyeitwa Muhammadi) alibidi ashambulie matendo ya kuiabudu miungu
hii, Katika kulielezea tatizo alikiweka kipindi hiki cha kuabudu miungu katika
nyakati za Nuhu na hivyo kuwahusianisha wao na imani zilizokuwa huko Babeli
kama zinavyoonekana kwenye kitabu cha Mwanzo. Mingu iliyowekwa ilikuwa ni hii
ifuatayo:
Yaghuthi (msaidizi) (Sura ya lxxi. 23)
(Robertson Smith
anamwelezea mungu huyu na Ye’ushi mzee na babu wa Waedomu aliyetajwa kwenye
Mwanzo 36 na mahali peinginepo pote kwenye Agano la Kale). Ni baadae tu kidogo
tunaposikia kuhusu kinyago hiki cha mungu kikiwa kinahusiana kwenye makabila Yamen.
Ya’uq na Suwa (huenda linamaana ya mbakizaji) dini iliyokuwepo na kupata nguvu
sana huko Yamen (Sura ya lxxi 20).
Hubal na Dhu Shara
Kuna miungu
miwili ambayo inashabihiana sana na hoja au mjadala huu: Hubali na Dhu Shara.
Dhu Shara ama kwa
usahihi zaidi ni Dhu ‘sh – Shara, ambayo
maana yake ni “inayotokana na ash–Shara” ana uhusiano wa moja kwa moja na neno Ashera la kwenye Bibilia. Ni mungu ambaye
alikuwa anaabudiwa na Wanabateani katika mji mkuu wao wa Petra. Alikuwa anaonyeshwa
kwa tofali la pembe nne la jiwe jeusi lisilochongwa lenye urefu wa futi nne kwenda
juu na upana wa futi mbili. Damu ya vitu vilivyotolewa sadaka ilimwagwa juu
yake na mbele yake. Chini yake kulisimamishwa kiwiko cha dhahabu na maskani
yote ilingarishwa na dhahabu na sadaka zilizopigiwa kura na za kuvutia (ERE makala ua 1, ukurasa wa 663). Rekodi
au maandishi ya Kiyunani vinamuonyesha mungu huyu kuwa ni Dusares. Epiphaneus
anasema kuwa sherehe au sikukuu ya Dusares ilisherehekewa huko Petra katika
tarehe 25 Desemba ambayo iliyokuwa majira ya baridi wakati jua linapokuwa
upande wa kaskazini kabisa mwa Ikweta. ERE inaelezea na kutambua jambo hili ni
kama kuna muungano au uhusiano na ibada za jua (Ibid) (sawa na ilivyodadavuliwa
kwenye jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235)).
Katikati ya nyumba
ya dini potofu ya As shera (ambayo ni
Miti au Kijimsitu) alitambuliwa na Dionysus. Muungano au uhusiano wa dini
hii potofu na wala mbogamboga kwa kustarehe ni ule wa waabudu jua, ibada
zilizofanyika kwa kuzuguka miduara. Miungu hii ilikuja omyeshwa kwa kuchongewa sanamu
kwenye kabila la Dausi siyo mbali sana na Maka.
Jiwe jeusi la Dusaresi
ama Dionysus mungu wa Wanabateani huko Petra lilichukuliwa na kupelekwa au kufanywa
Ka’aba na kuganywa kwamba kitu cha kutumika kidini kama kigezo huko na hata
Muhammadi alishindwa kuliondoa. Kidogo kidogo hatimaye likakuzwa habari na
umuhimu wake na Hadithi za Kiislamu na kwenye ibada za mungu wa kipagani zikafanyika
kuwa ni kitovu cha kutembelea mahujaji wa huko Maka.
Mungu wa pili ajaye
kutoka Kaskazini alikuwa ni yule wa Hubali. “Amr b. Luhai anajulikana kuwa alileta
sanamu zake hadi Maka kutoka Moabu (Ma’ab) na kuliweka katika Ka’aba. Mwanzoni lilikuwa
katika muundo wa binadamu. Pamoja nail kulikuwa na mishale ya kufanyia ubashiri
kwa njia za nguvu za mapepo.
Kabila la Kalbi la
Wasyria wa Jangwani walilitumia jina la Habuli kwa kumwita mtu ama ukoo na pia
walitumia Isafi na Na’ila, ambao walikuwa miungu mingine miwli waliojulikana
sana huko Maka.
‘Amr. b Kuhai nachukuliwa
kuwa ni mwakilishi wa Huza’a ambalo ndilo lilikuwa kabila waliokaa huko Maka
kabla ya Makureshi (ERE ibid., ikuasa
wa 664).
Hivyo basi
tunaweza kusema au kuona kwamba kwamba Huza’a alianzisha dini za kipagani huko
Maka ingawa Noldeke anachukulia kuwa haiwezekani kwamba ‘Amr. B Luhai anafaa
kupongezwa na mwenendo huu lakini haelezi bayana sababu, akituacha tudhanie
kwamba ilianza kabla yake.
Neno El lilitumika
na Waarabu wa mwanzoni kama jina la kipekee la mungu akiwa ni kama Mungu kwa namna hiyohiyo lilivyotumika kwenye
Bibilia. Neno hili likafanyika kuwa iyal
kama muundo wa kiuwingi wa mtukufu.
Kwa namna hiyohiyo,
neno la Bwana, Baali, kama Bwana likafanyika kuwa jina la mungu na inaonekana kuwa
la kawaida hasa kwenye imani ya Kisemiti. Kivumishi ba’ila (kutatizwa) inamaanisha kwa hakika kumtwalia Mungu Ba’ali (huenda
pia makusanyo au madeni au bili zetu).
Kwenye maelezo ya
neno Hallah linalomaanisha Mungu kunaingia mtungo wa majina kadhaa
ya kipekee ya Wanabateani na ya Waarabu mbalimbali wa Kaskazini wa nyakati za
zamani na za mwanzoni sana na neno hili lilikuwa likitumika hata miongoni mwa
wapagani waliokuwepo kipindi cha kabla ya kuanza kwa Uislamu na wapagani wa Kiarabu.
Allah likafanyika kuwa limezoeleka kutumiwa kwenye matumizi ya maandiko kadha
wa kadha yaliyokuwa ya muhimu ya wapagani wa Kiarabu. Kozani yenyewe
inashuhudia kwa mtazamo wa kwamba zama za kabla ya Uislamu na wapani wa Kiarabu
wenyewe walimchukulia Allah kama Kiumbe Mkuu. Walimrudia Allah wakati mambo na
walipokuwa mashakani (Sura x, 23, xxix, 65, xxxi, 31). Viapo vya muhimu viliapwa
kwa jina lake (S. vi, 109, xvi, 40, xxxv, 40). Anatambuliwa na wanadamu kama Muumbaji, na Mtoaji wa
mvua (xxxi, 61ff). Makosa yao ni kwamba wanaabudu mingu mingine zaidi ya yeye;
ijulikanayo kama miungu mitatu ya kike Al lati, Al Uzza na Manati ambao
wanaaminiwa kuwa ni mabinti zake (xvi 59ff).
Miji ya
Wawellhausan ina idadi kubwa ya vifungu ambazo kwamba Waarabu walioishi kabla
ya Uislamu walimtaja Allah kuwa ni mungu mkuu. Kuna wengi sana hata kama
tutawaondoa wengine nje kama mashaka bado wanabakia wengi wa kutufanya tusione
shaka kuamini kwamba neno Allah ni neno lililokuwepo na limekuwa likitumika
hata kipindi cha kabla ya harakati za Mahammadi.
Neno hilo ni jina
la kawaida la Mungu wa Waarabu wote, wapagani na wengineo. Tena licha ya
ushahidi huo kuthibitisha, Wellhausen bado anaendelea mbele akijaribu na
kuanzisha muunganiko unaosema kuwa jina Allah linatokana na ibada ya Hubali wa
Wamoabu. Hii inaonekana kuwa ni hombwe au mkanganyiko wa kidini usio na msingi
kwenye ukweli wa kihistoria ambao mtu anaweza kuwa tayari sana kuuona. Kwa kweli
ushahidi wenyewe unatofautiana sana. Ni kutoka kwa huyu Wallhausen ndiko hoja
hizi za uwongo zinatokea (ERE ibid.).
Mkanganyiko
kwenye unatokana na hatari iliyoko ya udogo au ufinyu wa maarifa wa baadhi ya
misingi iliyopotoshwa na Wallhauseni.
Kwa kuwa
tunarudiarudia kulikuta jina la mungu likifuatiwa na jina Alaha, au mungu, Wallhauseni
ilipinga kwamba Warabu wa miaka ya baadaye yawezekana kuwa walichukua kiambishi
cha jina Allah kuwa ni kama Mungu kwa idadi ya miungu tofauti na
kwamba, kwa maana hiyo, kutoka kuwa kiunganisho peke yake hadi kuwa ni jina la
mungu mkuu, ndipo yawezekana kuwa kidogokidogo likafanyika kuwa ni jina la
Mungu Mkuu.
Hoja hii inaibua
au kuzidisha hali ya kulipuuzia andiko la Biblia na mtindo wa kizamani wa ulimu
ya lugha kuhusiana na majina ya Mungu kwa lugha za Kiebrania, Kikaldayo, Kiaramu
na Kiarabu.
Wakati Ka’aba ilipokuwa
inasafishwa nje ya Maka kulikuwa na vinyago au sanamu 167 hapo. Sanamu ya mfano
wa samba miongoni mwa Waarabu ilihitajika sana, ingawaje iliwekwa kwa wingi
kwenye miungu ya mitatu, na Siriusi. Mtindo mingi na taratibu wa ibada za
kipagani vimeingizwa kwenye Uislamu kama tutakanyoona lakini haikuhusisha Jina
la Mungu.
Mohammadi alitokea
kwenye familia ambayo kwa sehemu kubwa ilikuwa ya Ukristo wa Kuamini Mungu
Mmoja, yaani Uyunitarian na ilikuwa ni lengo lake kuonyesha mfumo ulio kwenye
Biblia.
Alikusudia
kuondoa miungu hii mitatu hadi wafikie kwwenye ibada ya Mungu mmoja wa kweli. Kwanza
kabisa alinuia kukomesha ibada za kipagani kutoka kwenye makabila ya Kiarabu.
Kisha alikabiliana na harakati za kiupinzani na kuubomoa mfumo wa Kiutatu, ambao
ulikuwa umejiingiza ukitokea Mashariki kutoka Costantinople ukiwa kama kifaa
cha imani ya Kirumi. Alikuwa pia na jukumu la kuwatoa na kuwaweka huru Waarabu
kutokana na itikadi za kiastrokrasi na za kifalme za Kiyahudi, itikadi na fikra
zilizokuwa zinatawala fikra za watu wa Mashariki ya Kati kwa wakati huo. Nyingi
za ushawishi huu ulienea hadi kwa Wakhazaria na ndipo tulijioea uwongofu wa
Wakhazaria, Waashikenazi wakiingia kwenye imani ya Kiyahudi katika karne
iliyofuatia mnamo mwaka 740BK.
Muhammadi alianza
kufundisha mnamo mwaka 610 BK na ilipofikia mwaka 632, Uislamu ulianzishwa rasmi
baada ya kile kilichojulikana kama Hijra au kukimbia kutoka Maka mpaka Madina.
Ni ukweli kwamba
misikiti ya Kiislamu ina alama ya mwezi mchanga inayoshikirishwa nayo lakini ni
sawa tu na kama yafanyavyo Makanisa mengi ya Wakristo waamini Utatu pia. Hatahivyo,
majina hayo hayana uhusiano wowote na jina la Allah. Ujenzi wa miskiti mingi
unahusianishwa pia na kuweka kwa siri maziwa au matiti ya mungu mke upande wa
juu ya mapaa na kitendo hicho ni cha kipagani moja kwa moja, lakini hii
haihusiani sana na Mtume na kwenye Uislamu wa kweli.
Kama tunavyoona
Al’ilah lilikuwa ni aina nyingine ya kuandika jina la Allah. Huyu hakuwa na
uhusiano wowote kabisa na Mungu Mwezi na wala miungu mke aliyejulikana na
kuabudiwa sana aitwaye Al ilat au Al Lat iwe kwa namna yoyote ile.
Lugha za Kiebrania
na ya Kiarabu zinahusiana kwa njia hii. Kiebrania kilikuwa ni mwanzilishi wa
mtindo wa Kiaramu cha magharibi, ambacho kiliongelewa baada ya zama za utumwa
wa Babeli badala au mahali pa Kiebrania. Lugha ya Wasemiti ya Wakaldayo
ikafanyika kuwa ni ya Waaramu wa mashariki na ndiko kilikotokea Kiarabu cha
siku hizi.
Eloah (kwa namna
ya umoja); na
Elohim (kwa
wingi).
El ilikuwa ni kifupi
cha uandishi na iliemaanisha uweza kama alionao mtu.
Majina ya Mungu
kwa Kikaldayo yalikuwa:
Elohi (kwa umoja)
(= Kiebrania. Eloah)
Elahhim (kwa
wingi) (= Kiebrania, Elohim).
El ilikuwa na
maana sawa. Kwa lugha zote mbili, yaani Kiebrania na Kikaldayo zinaonekana kwenye
maandiko ya Biblia zikitumia mitindo hii. Kitabu cha Ezra kinaonyesha kwamba
jina Eloah
ni jina la cheo la Mungu wa Hekalu aliyeko Yerusalemu. Jina hili ni umoja na linakubali
na kuthibitisha kutokuwa na aina yoyote ya uwingi. Linamtaja na kumrejelea Mungu
mmoja na wa ukweli peke yake.
Kwenye Kiaramu
cha mashariki, Elahh mmoja au wa pekee ailikuwa Allah kwa Kiarabu kwa namna hii.
Elahh alitajwa kama Al Elahh au Mungu
kwa umoja kama inavyoonekana kwenye maandiko ya Biblia na kwenye Kikaldayo. Kwa
hiyo alikuja kuwa Al’ilah kwa muundo wa Kiarabu ambacho ndicho Kiaramu cha
mashariki, herufi mbili za hh zinaelezwa kuwa ni kama kihamasisho au kiambishi
cha herufi za mwishoni h cha Allah. Kwa hiyo, mtindo wa Kiarabu cha zamani uliokuwa
Al’ilah ulikuwa unabadilisha sauti ya h mbili. Uislamu chini ya Muhammadi uliendeleza
jina Allah kwa sababu lilikuwa la umoja na linakubaliana kutokuwa na uwingi.
Hakuna tashishwi
kwamba jina Eloah wa Biblia na Allah wa Kiarabu lilitujia kutoka kwrmur lugha
ya Kisemiti kupitia Kiebrania cha Kale na Kikaldayo cha Kale kwa kipekee na inamaanisha
kitu hichohicho kimoja.
Jina Yahovah ni la
kisheo au mamlaka linalomtaja au kumhusu Eloah kama muundo wa nafsi ya tatu ya
kiambishi inayomaanisha “Anafanya Ikawa”.
Mtazamo huu unathibitishwa na maandiko ya bangokitita kwenye maandiko ya Kutoka
3:14 katika tafsiri ya Annotated Oxford RSV. Jina lililoelezewa kwenye andiko la
Kutoka 3:14 inamaanisha “Mimi Niko Ambaye
Niko (‘eyeh ‘asher ‘eyeh sawa na
Bulhinger fn kwenye tafsiri ya Companio Bible pia). Inaonyesha au kuelezea kitendo
cha uumbaji kwa kujieneza mwenyewe na Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli sawasawa
na mapenzi yake na mipango yake. Kwa jinsi hiyo watu wote watafanyika kuwa wana
wa Mungu.
Kwa hiyo ni jina
linalotumika au kumhusu msemaji wa Mungu Mmoja wa Pekee wa Kweli ambaye anajulikana
kama Yahovih (SHD 3069) au Yahovah ya Majeshi. Yahovah (SHD 3068) inatumika kuwataja
miungu wadogowadogo au wasaidizi na wakati mwingine ni miungu wengi kwa wakati
huohuo mmoja. Kwa maneno mengine ni kwamba wote hao wanatenda kazi kwa niaba ya
Mungu mmoja wa Kweli, Eloah kama elohim. Kwa hiyo watu wote watafanyika kuwa miungu wa kiroho au elohim kama wana wa
Mungu (soma jarida la Wateule Kama Elohim (Na. 1)).
Jina Yahovah limetumika
kwa takriban viumbe mwanne, watatu wao wakiwa ni malaika au wajumbe wa Mungu wa
Mbinguni kwa wakati huo huo kama tunavyoona kwa mfano kwa Ibrahimu na Lutu, na
kuangamizwa kwa Sodoma na Gomora. Mambo haya yote yameelezewa kwa kina kwenye majarida
ya Malaika wa YHVH (Na. 24); Majina ya Mungu (Na. 116); Uwepo wa Yesu Kristo Kwenye Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi
Duniani (Na. 243); na Ibrahimu na Sodoma (Na. 91).
Hii ni kutokana na
hali ya kutojua chimbuko la majina kwenye lugha zake na shauku ya kudanganya
kwa kujihesabia haki kamili kwenye imani ya Kikristo ambako tunaona makosa na
udanyanyifu ukiibuka. Kutofahamu kwa Waislamu kumetuama kwenye mapokeo ya
wanadamu ambayo yanaongoza hali ya chuki kwa kiasi kikubwa sana.
Kwa nini watu wanalishambulia jina Allah? Ni nini maana ya jina hili?
Tatizo halisi
linatuama kutoka kwenye teolojia potofu na ya uwongo iliyouingia Ukristo na
kutafuta meelezo yake leo yakifundishwa kwenye Makanisa ya Mungu.
Imani ya Utatu au
Utrinitarian ilitokana na imani ya Kibinitariani na ni mwendelezo wake tu,
ambayo ilijikuta ikiingizwa rasmi kwenye Halmashauri Kuu ya Mtaguso wa Nicaea mwaka
325 BK. Utrinitarian uliendelezwa na Wakapadokiani, Gregory wa Nysaa, Gregory
wa Nizianzus na Basili. Teolojia hii iliingizwa mwaka 381 BK na iliuzinga Ukristo
kiteolojia. Augustine wa Hippo naye alianzisha teolojia potofu akiianikiza kwa
kutumia maandishi yake.
Makanisa ya Mungu
yamekuwa hata hayana udhuru kwa upotofu huu. Waliiendeleza na kuikuza, chini ya
Herbet Armstrong katika miaka ya karne ya ishirini, wakafundisha imani ya uditheism
ambayo ilikuwa chanzo cha teolojia potofu iliyofundisha kuwepo wa miungu wawili
wenye hadhi na mamlaka sawa. Waalimu hawa wa uwongo wanakabiliwa na utata wa
maneno ya Biblia kuhusu jina Eloah kuwa ni jina la Mungu katika umoja na ambalo
linaweza tumika tu kwa Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli aliyemtuma Yesu Kristo
(Yohana 17:3). Kwa hiyo ndipo wanakataa na kushambulia matumizi ya jina la Eloah
kuwa ni kama Mungu wa Pekee wa Kweli. Wanafanya hivyo kwa kuhanganya majina ya
Eloah na Allah, ambapo ni muunganiko sahihi, lakini wanadai kuwa linahusiana na
za Mungu mwezi katika Uislamu kwa sababu ya mwingilio wa kipagani kwenye misikiti
kulikofanywa na dini za siri. Ni kweli kabisa kwamba Uislamu, kama ulivyo Ukristo
uliokuwepo kabla yake, umepotoka kwa kupaganishwa kwake lakini hiyo halina
uhusiano wowote na matumizi ya jina Allah kwenye Ku’rani.
Makanisa mengine
kama Kanisa la Mungu (la Siku ya Saba) wakati lilipoingiliwa na imani ya Utatu
ama Utrinitarian huko Marekani lilianza kwa kukubaliana na Ubinitarian kama
njia rahisi kwao na bila shaka litaishia kwenye Utrinitarian. Kanisa la Seventh
Day Baptists bado wangali waamini Mungu mmoja yaani Wayunitarian ni kama
walivyokuwa hivyo wakati wote kimsimamo kwenye Makao yao Makuu ya Kimataifa, lakini
wamejikuta wakiingia kwenye Utrinitarian kwenye Halmashauri yao ya Kanisa la
Marekani kuanzia katikati ya miaka ya sabini. Kiteolojia ni wadhaifu sana.
Makanisa ya Mungu pamoja na kanisa la Seventh Day Baptists mwanzoni walikuwa
waamini Mungu Mmoja au Wayunitarian kwa madhehebu mengine yote likiwemo kanisa la
Waadventista Wasabato au Seventh Day Adventists. Armstrong aliwekwa wakfu na
kukubaliwa kuwa mtumishi kwenye kanisa lijulikanalo kama Church of God (Seventh
Day) wakati lilipokuwa bado ni la mrengo wa kuamini Mungu Mmoja au Uyunitarian
mwishoni mwa miaka ya 1970.
Watu hawahawa
wanakabiliwa sasa na ukweli wa kwamba wameanzisha mafundisho ya uwongo na
kuyapotosha Makanisa ya Mungu kwa upotovu.
Ilikuwa kwa sababu
hii katika karne za mwanzoni kwa kufuatia teolojia potofu ta Kitrinitarian kwenye
Ukristo ndipo Uislamu ukasisitiza kumrejelea Mungu Mmoja, wa Pekee wa Kweli
kuwa ni Allah, kuliko mungu wa uwingi ellahhim, kwa kuwa jina lenyewe
linakubaliana kutokuwa na uwingi wa aina yoyote ile.
Badala yake linakubaliana
na kuwaonyesha kwamba wamepotoka, waalimuwa wa Kibinitarian, Kiditheist na
Kitrinitarian wa Makanisa kadhaa mbalimbali ya Mungu walianzisha malumbano wakiwekea
msingi wake kwenye uwongo na kuwasingizia mambo ya uwongo wale waliopingana nao
na kutoamini hoja na mafundisho yao. Matendo haya ni kinyume kabisa na Biblia
na hata sasa kwenye Sheria za Marekani pamoja na za mataifa mengine pia.
Upotovu kadhaa wa
teolojia hii umeainishwa kwa kina kwenye jarida lihusulo Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Uislamu (Na. 55).
.
Fikira ya kwamba
Alla siyo Mungu wa kwenye Biblia, ambaye jina lake kwa kweli ni Yahweh kama
inavyosemekana, ni fikira ambazo zimetokana na teolojia ya Majina Matakatifu zinazofundishwa
au zilizotokea nchini Marekani na ni ya uwongo. Imeshindwa kuyajua majina ya
Mungu yalivyo kwenye Biblia na nafasi au mahali pa Eloah – Elohim na tofauti
yao hapa.
Kwenye makala au tahakiki moja tunakutana na
fafanuzi au maoni ya kama vile
“Kwa watu wa Maandiko” ama “wa kitabu” Waislamu wameambiwa
waseme. “Tuna imani kwa kile ambacho kimefunuliwa kwetu na kwa kile ambacho
kimefunuliwa kwenu. Mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja, na kwenu ninyi tumetulia”
Kurani 29:46.
Je Waislamu wavinamini vitabu vyote
viwili, yaani Korani (Kurani) na Biblia?
Tunaona.
Sasa malumbano na
hoja hii ni mwelekeo wa muhimu. Inaonyesha umuhimu wa kuiuliza Korani na kuona
kuna tofauti ipi kati ya dini hizi mbili.
Kurani kwa hakika
inamtaka Muislamu wa kweli kuvifuata vitabu vyote viwili, yaani Kurani na Biblia.
Hii ina maana na nguvu sana na ingeweza kuwa ni uthibitisho wa kwa dini zingeweza
kusuluhishwa na kwenda sambamba. Mfano wa dhana inayoyaacha Makanisa ya Mungu
kwa wakati huu ni hii ifuatayo:
Asili ya Allah ni nini – Allah - wa Waislamu? Je, yeye ni sawa tu na Yahweh
wa kwenye Maandiko Matakatifu?
Kama ilivyoripotiwa kwenye taarifa ya jarida lijulikanalo kama Battle Cry la Januari na Fenruari 2000, mlinganisho
kati ya Allah na Yahweh, wakiwekea msingi wa kuionyesha Kurani na Biblia kwa
ujumla, ni mafunzo ya kupinga tu.
Kinachojulikana na kukubalika: Allah ni mkuu, hana mfano wala mipaka, aliyetukuka
sana na kwamba hakuma mtu anayeweza binafsi yake kumjua Allah. Yahweh, kwa upande
mwingine ni kwamba alimtuma Mwana wake Yesu Kristo duniani ili kutuwezesha
tumjue Mungu kila mtu nafsini mwake, Yohana
17:3 (kwa mujibu wa jarida la R Nickels la Uislamu na Wewe, Somo Na. 185).
Bibilia inasema
wazi kwamba hakuna mtu aliyewahi
kumuona Mungu kwamwe. Alichagua kujifunua mwenyewe kwa kupitia watumishi wake
manabii na akamtuma Yesu Kristo. Mwandishi anaonekana kuwa hajui lolote kabisa
kuhusu jina Eloah kwa jinsi linavyotumika kwenye Biblia. Pia anaonekana kutolijua
kabisa neno Yahovah au Yaweh kwa vile anavyodai kuwa limetumika kuwaelezea au
kuwahusu Malaika wa Agano la Kale, ambao mmoja wao, Mwamba wa kiroho ambaye alikuwa
pamoja na wana wa Israeli Jangwani (1Wakorintho 10:4) ulikuwa ni Yesu Kristo.
Ezra anaonyesha,
kwenye matengenezo na marejesho makuu kwamba Nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu
ilikuwa ni Nyumba ya Eloah (Ezra 4:24) na siyo Nyumba ya ‘Yaweh.’ Ezra
anamtambulisha Eloah kuwa ni Eloah wa Israeli. (Ezra 5:1). Manabii walikuwa ni manabii
wa Eloah (Ezra 5:2). Yeye ni Eloah wa Wayahudi (Ezra 5:5). Yeye ni Eloah mkuu
ambaye kwaye Nyumba ilijengwa (Ezra 5:8). Yeye ndiye Eloah wa Mbinguni na Duniani
(Ezra 5:11). Alikuwa ni Eloah huyu ambaye mababu zetu walimkasirisha kwa hasira
na akawapeleka utumwani (Ezra 5:12) Koreshi alitoa amri kwamba nyumba ya Eloah
ikajengwe, na vyombo vya dhahabu na fedha viingizwe ndani yake (Ezra 5:13-17;
6:5).
Nyumba ya Eloah
ililindwa na iliamriwa ijengwe na watawala wa dola kwa kuwa Eloah alikuwa amemchagua
Koreshi aanzishe mchakato huu wa ujenzi. Dario II aliumalizia na Ahauswero II
aliamuru mng’aro wake. Ezra na Nehemia waliurejesha upya utaratibu wa huduma za
Hekalu na Ezra alifariki mnamo mwaka 323KK. Hakukuwa na mashaka kwenye mawazo
ya mtu yeyote kwamba lilikuwa ni Hekalu la Eloah, Mungu wa Mbingu na Dunia. Sio
mara moja tu jina Yahweh limetajwa kwa jambo hili. Kwa kweli, neno Yahweh linatokana
na kosa la kimatamshi ya jina lenye kwenye kila tukio.
Kutoka hapo juu
tunaona kwamba majina ya Eloah na Allah kama yanatokana na sehemu mbili tofauti
zenye muundo na mfumo mmoja wa lugha Eloah na Allah ni Mungu huyuhuyu mmoja ambayo
kutokana na huyo ndipo linatoa jina Allah. Kwa kupewa ukweli huu wa muhimu ndipo
kwa hiyo tunaweza kwenda kwenye msimamo wa kawaida na kujenga uelewa uliosawa
kwa pande mbili zote.
Allah ni muundo
wa kijina wa Kirabu wa Mungu Mmoja wa Kweli, Eloah anayejieneza mwenyewe kufanyika
kuwa elohim kwa kupitia watu aliowaita kwenye mfumo wake.
Kurani inashikilia
kusema kwamba Wakristo wapo karibu sana na wao. Hawakubaliani na wala
hawatakubaliana na mapokeo yoyote yanayojumuisha imani ya Utatu na Ubinitarian.
Kimsingi wao wamekaza mtazamo wao kwa kutomkubali Mungu mwenye mjumuiko na
viumbe wengine na mdahalo kama huu hauleti maana wala kutupeleka kwenye malengo
yoyote zaidi ya kusababisha mafarakano na kuzidisha chuki miongoni mwetu.
q