Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[055]
Mwaswali Yaulizwayo Mara kwa Mara Kwenye Uislamu
(Toleo La 1.0 20080612-20120121)
Huu ni
msingi wa muhimu sana katika kuieea Korani. Kwa kuwa Kanisa na huduma zake zimeachwa
kuandikwa au kuondolewa na maandishi vitabu vya Hadithi, maana ya Korani
(Kurani) yamekuwa yakifanywa kiutatu na kupotoshwa ili kwamba wafuasi wa imani
ya Uislamu wasiweze kuelewa vizuri kutoka kwayo.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 2008, 2012 Wade Cox
with input by Jean-Alphonse Armand)
(tr.
2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Mwaswali Yaulizwayo Mara kwa Mara Kwenye Uislamu
1: Nabii
aliitwa jina lake Muhammadi
Swali la 1. Ni jina gani sahihi la Nabii kwa Waarabu?
A. Kwenye karne ya sita Kanisa
la Mungu la Sabato kwa upande wa Mashariki lilienea kutoka kwenye kingo za maji
yam to Nile hadi Uarabuni na Asia Ndogo hadi India na Mashariki ya Kati. Mnamo
mwaka 610 mwongofu wa Kkristo wa Kimonophysite aliinuka na kuelimishwa, Huenda
alikuwa kama kasisi (Abu) lakini mwanae wa kwanza wa kiume alimuita pia jina
lake kuwa Al Qasim. Aliitwa Qasim bin ‘Abdullah, bin ‘Abdul-Muttalib bin Hashim wa kabila la kundi la Hashim babu wa
baba yake. Aliongoka na kuwa muumini wa Kanisa la S (soma pia jarida la
Wana wa Ibrahimu, Sehemu ya III: Ishimaeli (Nao. 212C)).
Hamasa yake
ya pupa na hamu kubwa ya kuitafuta kweli kwenye Maandiko Matakatifu ilimsababishia
matatizo kwenye mtazamo wake wa mafundisho ya Kimonophysite Nasaari, ambayo
yalionekana kupingana na maandiko asilia yenyewe. Kimsingi, Roho alikuwa
anaanza kumuita kwa njia ya isiyo wazi, ambayo iliitwa na kujulikana kama “Evangelion”.
Akalitafuta Kanisa la kweli. Maandiko ya Purana ya Kihindi yanaashiria kuwa
aliwahi kujulikana kwenye Makanisa ya Mungu yaliyokuwapo huko. Sababu
iliyomfanya Muhammad atoke kwenye Kanisa ilikuwa ni ndoto, na Mtume huyu wa
Waarabu alipata maono wakati alipokuwa anatafakari kwenye pango. Maono haya
yalimtisha sana lakini yalimhamasisha. Kisha alifanyika kuwa ni Msabato Mwamini
Mungu mmoja wa mrengo wa Kiyunitariani wa Kanisa lile lililokuwapo huko
Uarabuni, ambako alibatizwa (tena) mapema kabla ya utumishi au utume wake. Akiwa
hatokani na uzao wa Haruni wala wa Lawi, alijiambatanisha na kwenye uzao wa AhlulBayt
mabibi arusi wa Rasulullah kama Nasraani Sabi (TheoSebes/QEO-SEBHS/sebovmenoi = Mwabudu au Mcha Mungu) Mursal. Hadithi Nyingi,
Kadhaa zimetuama kwenye ukweli kwamba alifanyika kuwa Sabi. Akiwa kama Mursal
(Bibi arusi wa Rasulullah) alipata hekima zaidi na zaidi. Hatimaye,
alipobatizwa kwake, alitiwa nguvu na kupata uweza kwa Roho Mtakatifu (Ahmed) na
kufikia kwenye cheo cha kuwa Mmahmoodan na kawa Muhammad akiwa ni Mkristo wa kweli kwenye Makanisa ya
Mungu.
Swali la 2. Inadaiwa
kuwa jina la Mwenyesifa (au Ahmed) ni mojawapo ya majina ya Mtume, aliyojiita mwenyewe,
lakini linamtaja Roho au Mfariji, na wengine wanasema kuwa linamaana mbili zote
na ni ushahidi wa kukubalika kwa Mtume. Kwa hiyo, Ahmad ndiye nani hasa?
Jibu. Waislamu wengi hawajui kwamba Ahmed sio jina lake Qasim bali linamaana ya
Roho Mtakatifu, kwa kuwa hawasomi Biblia, na hawahawa andiko la Yohana kwenye
lugha ya Kiaramu.
Ingeshangaza sana kuona kuwa Mtume haijui kazi ya Roho Mtakatifu na kwa
bahati mbaya kwamba alijaribu kujiochukulia yeye mwenyewe majukumu ya Roho
Mtakatifu.
Kwenye Sura
61:6 tunaona kuwa Kristo anatangazwa kuwa Mtume wa Mungu. Habari njema kuhusu Ahmed
ilikuwa kuwa ni "Mfariji" ambaye alitumwa kwenye Kanisa. Roho Mtakatifu
alionekana kuwa na nguvu au uweza wa Mungu akiwa kama mjumbe au mfariji wa Kanisa
aliyewashukia siku ya Pentekoste, mwaka wa 30 BK, lakini uweza wake ulipuuzwa
au kubezwa na wengi. anut the power of it was rejected or mocked by many. The
text refers to the Seiko linafanya rejea yake kwene Matendo sura ya 2 (sawa na
Matendo 8:11 nk.). hadithi zimegeuza na kupotosha kwa makusudi uelewa wa watu.
Swali la 3. Je, tunaujuao mstari wa kweli wa uzao wa
Mtume?
Jibu. Mstari wa uzao wake ni wa Ishmaeli hadi
Kinana hadi Quraish, hadi Hashim hadi Qasim (sawa na majarida ya Muslim
(Mwislamu) 2/245; Tirmidhi 2/201). Hatimaye alitajwa kimakosa kuwa ni Muhammad ambalo
halikuwa jina lake kabisa bali lilikuwa ni jina la kicheo la bodi ya Kanisa la
Mungu.
Mtume
alikuwa amevutiwa au kushawishika na ukoo wa baba yake na misafar yake kadhaa
ya mara kwa mar ya kutembelea Maka, Madina na Taif, ambao walikujakuwa ni
waamini Mungu mmoja. Hivyo, waliwajumuisha baadhi ya watu wengine wasioamini Umonophysite
wa Utatu ulioingizwa kwene Ukristo, na lakini walioku sio Waamini Utatu wa
Kiathanasiani, ambao walikuwa na ushawishi wa kuabudu waliowaita watakatifu na
kushirikisha masalia ya viungo kama wanavyofanya kwenye imani ya kianimism ya
Wakaldayo. Walikuwa wametohoa ibada za miungu ya kipagani ya “Maria”, kwa dhana
iliyokuwa imejengeka kwenye dini ya mungu Mama, iliyochukuliwa kutoka kwenye dini
za kale za Waarabu waliokuwa wanamwabudu Astarte na kuhusianishwa na Jua akiwa
kama mungu wa kike kwenye baadhi ya dini potofu za kisirisiri (soma jarida la Imani za Dini za Siri, Sura ya 5 Uislamu (Na.
B7_5)).
Swali
la 4. Tunaona
na kusikia kila mahali, kwenye vyombo vya
habari na kwenye maisha ya kila siku, akitajwa “mtume wa Waislamu Muhammad"
au Mahomet au Mohammed, nk. Je, jina hili "MAHOMET" halimaanishi kuwa
yeye siyestahili kusifiw. Unaweza kufafanua
mkanganyo huu wa wazi?
Jibu. Muhammad ni dini ya ki Uungu (soma Sura 48:29) ambaye ni sura na mfano wa
Mungu wa Pekee wa Kweli kwa Roho wa Mungu. Muhammad ni alama ya mitume kwa
mujibu wa Sura ya 33:40. Jina la mhubiri anayeulizwa habari zake asichanganwe
na matumizi ya neno Muhammad kwa kuwa huyu ni alama tu au chisince this is just
a seal cheo.
Hapo mwanzoni, Muhammad halikuwa jina kabisa. Neno Muhammad ni sawa na maana ya kiuwingi: watu
waliotetewa. Tunaona kwamba maana ya neno la cheo la Muhammad kwa
kweli ni la kufanana na vyeo vyovyote vinavyoweza kutolewa na kupewa watu
wowote walibarikiwa kwenye Malimbuko.
Muhammad
(Sura za 3:144, 33:40, 47:2, 48:29) na Mahmoodan (Sura ya 17:79) inaonyesha
wazi kuhusiana na Ahmed, lakini anaweza kuwa tofauti na kile tunachokitarajia
sawa na kwa Kiingereza.
Swali la 5. Kuna wanaosema
kuwa Safari ya Usiku ya Mtume iliyomfana
kufika hadi Yerusalemu, na pia Paradiso, ilikuwa ni ya kimaono tu. Je, kuna
maana gani hasa ya hatithi hii ya Safari
ya Usiku?
Jibu. Hadithi imelipotosha andiko hili la Korani kwenye Sura 17:1 mahali ambapo
mtume alidai kuwa alipokea maono wakati alipochukuliwa usiku “Mahali pasipotiwa
unajisi pa Ibada” (palipotafsiriwa kama Maka) hadi “Mahali Pengine pa Ibada” (palipotafsiriwa
kama Hekalu la Mlimani huko Yerusalemu). Maono haya yalikusudia kupadhihirisha mahala
Wana wa Israeli kwenye Maandiko Matakatifu. Mapokeo ya Hadithi yanadai kwamba huyu
ilikuwa ni farasi mwenye mabawa anayeweza kuruka aitwaye “Buraq” na kutoka hapa
mtume alitwaliwa na kupelekwa hadi mbinguni na kurudishwa. Uelewa wa kwanza
asilia ulikuwa ni kama ulivyoonyeshwa kwenye tafsiri ya Pickthall katika
kuifahamisha Sura, wakati ilikuwa imeeleweka kuwa alikuwa amesafirishwa hadi
mbinguni hadi kwenye mbingu ya saba na hadi kwenye makazi akaayo Mungu mwenyewe
kwenye maono, ni kwa namna hiyohiyo kama walivyoandika kina Paulo na Yohana
kwenye Agano Jipya.
Mengi yasiyo na maana wala umuhimu yameandikwa kuhusu siku ya 27 Rajab. Baadhi
ya wanazuoni wafafanuzi wa Kimarekani hata wanadai kuwa kwenye siku hii mtume
alipaa kutoka kwenye msikiti wa Al Aksa kwenda mbinguni, jambo ambalo ni la
kimaandiko na kiteolojia haiwezekani kwa namna zozoye.
2: Uislamu
Swali la 1. Tunajua kwamba Waislamu wanamuabudu Mungu
mmoja, lakini dini yao ni ipi? Je, Korani ilikusudia nini kuweka msingi wa dini
mpya?
Jibu. Kundi hili pia
lililoitwa “Muhammad” lilianzisha kanisa la Waliojisalimisha
kwa Mungu au Al Islam. Kuna dini moja tu na namna moja
ya kuabudu nayo ni Uislamu na ambao ndiyo
waliopewa Nuhu, Ibrahimu na Isaka na Musa na Haruni, na kwa manabii na kwa
manabii au mitume na kwa Kristo na Qasim na kwa kanisa ambalo ni “Muhammad” na kwa Makanisa ya Mungu na hadi wakati
huu wa sasa. Korani inato mlolongo huo wa matukio kwenye Sura ya 37 As Saffat “Wale wanapanga Vyeo.”
Wakati imani ilipokuwa inashambuliwa,
makundi yote mawili, yaani Waamini Utatu na Wayahudi wa huko Uarabuni, mtume Qasim,
na kanisa lililoitwa "Muhammad", waliongezeka huko Uarabuni kutoka
kwa Wakristo wa mrengo wa Kiyunitari hapa, kuushughulikia mafundisho ya uwongo
yanayoshambulia Umoja wa Mungu na matendo mapotofu ya waamini Utatu yaliyoingizwa.
Qasim na Baraza la Wazee walianzisha mafafanuzi au mahubiri ya kimafundisho ya
Biblia wakiwasimika viongozi kwenye makabila ya jangwani.
Chini ya
uongozi wa Qasim waliwafundisha makabila ya Waarabu kumhusu Kristo na wakaweka
mfumo wa viongozi wa kanisa wakiwa chini ya mamlaka ya mitume kumi na mbili. Huyu
ndiye Muhammad. Walipambana na mamlaka ya kifalme ya Wayahudi waliokuwa kwenye
makabila ya Kiarabu na wapagani waliouawa na wao. Qasim lirithiwa Papohapo na Makhalifa Viongozi wanne au warithi
wake. Kisha imani hii iliharibiwa na
wale waliojulikana kama “waongofu” ambao kwa kweli walikuwa ni wapagani wa
Kiarabu walioanzisha itikadi ya uwongo waliyoiita kuwa ni Hadithi na kuharibu
maana na muundo wa uandishi ambao waliandika kama rekodi ya kanisa la Waarabu.
Mauaji ya Ali yalifanyika ili kuizima imani ya kweli huko Uarabuni. Soma jarila
la Kuanzishwa kwa Mkakati wa Kuifafanua Korani (Na. Q1).
Swali la 2. Waislamu wengi
wanaiita dini yao kama Al Islam. Je, Al Islam ni nini na ina maana
gani?
Jibu. Alislam, maana yake ni Unyenekevu au Kujiachia, ni
neno lililotumika ili kuonyesha mfumo wa kidini na kwa kweli likajakuwa jina la
dini. Hata hivyo, kwa hakika ni jina la utaratibu wa kisheria na halali au Dini
(Sura 3:19, 85; 5:3; 61:7-9). Inaitwa imani ya Kweli. Kwenye Agano Jipya
ilikuwa ni dini yenye wafuasi wake. Njia au
Imani Waliopewa Watakatifu Mara Moja Tu na
ndiyo mtazamo uliotumika kwenye Sura ya 61:7-9. Ni wazi kwamba kutokana na
matumizi ya Kikorani, na ikilinganishwa na Agano Jipya, kwamba KRISTO ndiye
mfano wetu au dini yetu akiwa kama ufunuo wa Mungu kwa Mariamu, mama yake. Kwenye
nyaraka za Paulo, kwa mfano tunasoma kuwa Kristo ndiye Ukristo. Wakristo ni
wafuasi wa Kristo, sio wafuasi wa Ukristo. Dini hii pia iliitwa “Ukumbusho wa Allah"
na Kweli. Ushuhuda wa Jesu ni “Roho ya Unabii”. Kuna jambo linguine
linaloonekana kuweza pia kuwa kama ishara ya Gabrieli (Sura 2:97). Kimakosa
Gabrieli anatajwa kuwa kama Roho wa Ameen (Sura 26:193) au Roho wa Kweli,
ambaye ni Roho Mtakatifu (soma Yohana 14:17, 15:26, 16:13). Malaika wa Bwana
alimtokea Yohana huko Patmo akiwa kama mtu aliye kama mwanadamu (Ufunuo 1:13). Baada
ya kutungwa kwake mimba Kristo kiumbe huyu alijulikana kama Gabrieli, Malaika
aliyetumwa kwa Manabii na kwa Kanisa (Danieli 8:15-12:13), sawasawa na kwa Mtume
huyu Mwarau alipokuwa pangoni.
Swali la
3. Mimi ni Mwislamu na nina sababu ya kuchambua kile kilichoandikwa kwenye
Agano la Kale – kwa kuwa linafanana kwa ukaribu na hadithi
nyingi zilizoandikwa kwenye Korani. Sasa ni kwamba, siwezi kabisa kujua hata pa
kuanzia kwenye Agano Jipya. Ni kina nani walioliandika hili? Walishi miaka mingapi
baada ya Yesu? Kwa hiyo, Wakristohi wote wanayapa uzito stahiki maagano yote
mawili, yaani la Kale na Jipya? Nauliza hivyo kwa kuwa waongofu wengi wanapenda
kupata taarifa au habari zake kiusahihi sana baada ya kuamua kwao kuwa
Waislamu. Nadhani kwamba tunataka dini kuiweka kwenye namna moja ya historia.
Jibu: jibu linaweza kupatikana pia kwenye Korani. Wakati lilipoandikwa Agano
Jipya, Maandiko Matakatifu yalikuwa ni yale ya Agano la Kale peke yake. Agano
Jipya ni ufafanuzi wa lengo la kinabii la Agano la Kale. Kwa hiye answers can also be found
in the Koran. When the NT was written, Scripture was the OT. The NT is explanation,
ni ufafanuzi tu wa Torati au Sheria za Mungu.
Agano la Kale linafafanuliwa na Agano Jipya, na ndivyo ilivyo hata Korani,
kwamba haiwezi kueleweka pasipo kutumia Biblia kwa kuwa huo ni ufafanuzi tu.
Kuna Al Islam mmoja tu aliyetolewa tangu mwanzo na watu wote wanahitajika
kuzishika sheria za Mungu aliyehai, Eloah au Allah’. Huwezi kuwa Muislamu wa
kweli ukiwa huishiki Sabato.
Kutoka kwenye Sura isemayo: Wale waliosimama kwenye nyadhifa, tunaona kwamba Ufunuo wa Mungu
alipewa Adamu na Nuhu na Ibrahimu na Isaka na Yakobo, na Musa, Kristo na
Manabii wa Agano la Kale na Mitume wa
Agano Jipya na kwenye Korani.
Muhammad, kama Qasim na Wazee, na Makhalifa waliofuatia wanne walisimama
wakiwa Al Islam. Baada ya hapo, ulianguka kutokana na kushindwa kwa utakaso wa
imani yake ya msingi.
Swali la 4.
Pale inapodaiwa kwamba: "Uislamu ndiyo dini pekee inayokubaliwa na Mungu",
usemi huohuo kutoka kwenye tafsiri nzuri zaidi ingekuwa: "Unyenyekevu tu ndio unaokubalika na
Mungu". Ndivyo sawasawa?
Jibu. Uislamu naana yake ni kujinyenyekeza
kwa kuiachilia kwa Mungu. Kama hujitoi au kujisalimisha kwa Mungu na kuzitii
amri zake basi wewe si Mwislamu, haijalishi kuwa unapinga kwa kiasi gani.
Unakuwa ni punda uliyelemewa na uzito wa vitabu vya dhahabu, na usijue kitu
chochote.
Wale
wanaozishika amri za Mungu na imani au ushuhuda wa Yesu Kristo ni wateule (Ufunuo
14:12; 12:17).
Swali la 5. Kwa maana na mtazamo wa jumla, neno Jihadi
maana yake ni Vita Vitakatifu. Je, unaweza kunifafanulia maana yake hasa ya neno hili?
Jibu. Haikuwa na maana ningine zaidi ya kuwa ni Vita
Vitakatifu tu (kama ilivyoandikwa kwenye Sura za 2:218; 3:142; 8:72,74; nk.). Wateule wako vitani dhidi ya dhambi
kwa namna mbili. Tunapambana na tamaa za mwili yetu (1Petro 2:11) na pia
yatupasa kujizuia na kuishinda asili ya dhambi, na kumshinda mwanzilisho have
to resist thei wake, Shetani au Ibilisi (soma jarida la Hatua za
Kuishinda Dhambi (Na. 11)). Wateule wameitwa ili kushinda (Ufunuo 2:7; 3:12; Sura ya 9:19,20), bakia kwenye njia za Mungu.
3: Kur’ani (Korani)
Swali la 1. Unaweza kufafanua
maana ya neno Kur’ani na yule
aliyeiandika?
Jibu. Korani (maana
yake ni "Mkusanyo" au "Maarifa au hazina") ina maana ya mkusanyiko
wa mamia ya mafunuo yaliyokuja kwa kupitia mitume na manabii wa Kanisa kwa miaka
mingi. Mjumuiko huu ndio unaopelekea mapokeo mengine kusema kwamba Mtume huyu wa
Waarabu alikuwa Sabi. Sabiyah ni jina la Kiaramu linalomaanisha mtu au
watu wasiotokana na nasaba ya uzao wa Waisraeli na ambaye hajatimiza vigezo vya
kukubalika kuwa mwongofu au pengine aliitwa Nabi; na inamaanisha kuwa ni wale
waliojipachia kwenye Kanisa kwa njia ya ubatizo, lakini wakati mwingine
wanadaiwa kuwataja wafuasi au wanafunzi wa Yohana Mbatizaji. Hata hivyo, madai
yaliyofuatia baadae hayawezekani kuokana na ushuhuda wa Maandiko Matakatifu na
historia za Kanisa. Sabiyah inamaanisha kuwa ni Kanisa linaloishika Sabato la
Roho Mtakatifu. Mafunuo haya yote yalikusanywa pamoja na kuwekwa kwenye kitabu
kimoja huko Uarabuni, huenda kwa uangalizi wa Usman au ndiye aliyeifanya kazi
hii.
Swali la 2. Waislamu wengi wa leo wanasema kwamba kitabu cha kweli na kikamilifu cha
Mungu ni Kur’ani na sio Biblia, na kwamba Biblia tuliyonayo leo imepotoshwa.
Je, kuna ukweli wowote kwenye madai haya kwamba maandiko ya Torati na au Injili
imetosheleza?
Jibu. kur’ani
inawataka wafuasi wake kuyaamini na kuyasoma maandiko ya kwenye Biblia zikiwemo
Injili na maandiko yanayofate nya kanoni zzilizokubalika kwenye Maandiko
Matakatifu ya Wakristo (Sura 5:68). Hakuna mtu anayeweza kudai kuwa ni mfuasi
wa Uislamu na kuyakataa mafundisho ya Biblia, kama tutakavyoweza kuona kutoka
kwenye maneno ya Korani yenyewe.
Mwislamu wa sasa
anajifanya kwamba vitabu ambavyo Mtume anasoma sio yaleyale kama wale wlioko
leo na hivyo, hawapasi kufuata amri za Mtume kwenye usomaji wa Torati na maandiko
ikikusanya Agano Jipya. Biblia imekuwa ikilindwa na Mungu kama tujuavyo kwa
uhakika kutokana na yaliyokutanika kwenye kile kilichoitwa Gombo la Bahari ya
Chumvi maarufu kama the Dead
Sea Scrolls na maanndiko ya zamani ya historia. Wale wanaodai kuwa Biblia
imepotoa na kupoteza mwelekeo kwa kulitia unajisi jina na uweza wa Mungu wa
Pekee wa Kweli, Eloa au Allah'.
Yatupasa kufana
na kushika kile Mungu alichokiamuru. Hii haiwezi kufanyika kwa kudai kuwa
magano yote mawili, yaani la Kale na Jipya yamepotoshwa kwa kiasi cha kwamba
hatujui kile ambacho maandiko ya asili yanachosema, ni kama unavyofanya Uislamu
wa sasa. Gombo lijulikanalo kama the Dead Sea Scrolls linathibitisha kwamba
tuna maandiko halisia na yenyewe yaleyale yadumuyo hata kabla ya kuzaliwa kwa
nabii Qasim na kundi linaloitwa ‘Muhammad.” kur’ani (Korani) haiwezi kueleweka
bila kuitumia Biblia. Ni kwa kuwa na uelewa wa sheria na ushuhuda wa manabii wa
maagano yote mawili, yaani la Kale na Jipya ndipo Kur’ani inaeleweka vizuri. Na
ndiyo maana nabii mwenyewe alisisitiza usomaji wa Maandiko haya Matakatifu.
Swali la 3. Je, ni
kweli kuwa Kur’ani ni Neno la huyu Mungu wa Pekee wa Kweli?
Jibu. Korani ni kitabu cha ufafanuzi tu wa Maandiko Matakatifu na inayathibitisha
au kuyaunga mkono Maandiko Mtakatifu sawasawa na Torati na Manabii na Mitume
walioitangulia. Inashughulikia matatizo ambayo Kanisa la Uarabuni ambali
lilikuwa limechanganyika na makabila ya Wayahudi waliouwa wanajaribu
kuukwamisha na hata kuutokomeza Ukristo, na waliowatumia wapagani wa Kiarabu
kuwasaidia.
Wale
wasioyafuata Maandiko Matakatifu na wanaitumia Kori waalimu wa uwongo na Allah atawahukumu.
Wameuharibu na kuupotosha Uislamu kama waamini Utatu walivyoupotosha Ukristo na
Marabi walivyoipotosha imani au dini ya Kiyahudi.
Korani inapasa
isomwe sambamba na Biblia na ifuatst be read in conjunction wiiwe na Torati ya Mungu. Mtu asiisome Korani na kuiacha Biblia yote na akategemea
ataelewa. Na ndiyo maana Maimamu wa waalimu wa Kiislamu hawajui vya kutosha na
wanafundisha kuwa inaruhusiwa kuongopa ili kuapata au kuwafanya watu wajiunge na
kuingia kwene dini yao au waukatae na kuushambulia Ukristo. Kuongopa ni kuipuuzia
au kutoijali Torati au sheria ya Mungu na kuivunja Amri ya Nane ya Mungu.
Swali la 4. Kuna tofauti gani kati ya Kur’ani na Suna? Au Suna imeitwa hivyo ili kuipa mashiko zaidi
Kur’ani?
Jibu. Suna za Allah ni zinatokana na kabisa na Torati, Zaburi, Injili na Vitabu
vya Manabii. Wao wanaviita Tawrat, Zabur, Injil na Sahaif kabisa. Kwa maneno
mengine, ni Maandiko yote Matakatrfu.
Kama wewe
huisomi Biblia huwezi kuielewa Korani. Korani haiwezi kitenganishwa na Biblia.
Madai ya kwamba inawezekana yanafanywa na Mwislamu asiyeelewa lolote na
aliyepotoka imani.
Waislamu wa siku hizi hata wanadai kuwa Biblia iliokuwepo hadi mwaka 632 BK
alipoanza huduma Mtume na imani imepotea. Wanafana hivyo ili kuwafanya waipinge
na kuikataa Biblia na hii inapotosha imani yao. Mtume anawaita watu kama hawa
kuwa ni waalimu wa uwongo, punda mwitu au punda waliobeba shehena na vitabu vya
dhahabu. Wanavibeba kwa uchovu mwingi na wasielewe chochote kilichoandikwa
ndani yake.
Swali la 5. Je,
kuna tofauti yoyote kati ya Biblia na Kur’ani?
(kumbuka kuwa Biblia ilifunuliwa kwa zaidi ya manabii 40
na kwa kipindi cha zaidi ya miaka 1,500. Kur’ani inadaiwa kuwa alifunuliwa
mtume mmoja tu, peke yake kwa kipindi cha miaka 33, ambavyo ni uwongo kama
tulivyojionea hapo juu.)
Jibu. Watu wanajiita kuwa ni Waislamu, sasa wanadai kuwa Biblia imepotea nah ii
iliyoko sasa sio yenyewe asilia. Torati inatajwa kwenye Korani. Wanafanya madai
haya ya uwongo kwenye nadharia
iliyoingizwa baadae na Makhalifa walioeneza uvumi huu wa kuwa imepotea kwenye
Mabaraza yao ya Kikhalifa na kisha uvumi huu wa kipuuzi umerejea nyuma kwenye
maandi ko ya Yeremia 8:8, yanayowakemea waandishi wa nyakati zake kwa
kuyakanganya maandiko. Kwa namna hiyohiyo, Watrinitari waliichukua Biblia kwa
kudai yahusuyo uandishi wa nyaraka za Mtume Paulo, na madai wa Wanostiki wa
Kiantinomia au watu wanaotegemea maarifa na ujuzi ili kuupata wokovu, na huku
wakiyashika mapokeo ya imani za Kimafumbo na Dini za waabudu Jua. Imani zote
mbili msingi wake ni uwongo na hazina uhusiano wowote na sheria au torati ya
Mungu na itapelekea kwenye vita vyaa dunia.
Korani ina ujumbe ulio wazi sana kuhusu Biblia au
Maandiko Matakatifu na Torati na Agano. Korani inathibitisha ujumbe ulio kwenye
Biblia na Torati na Ushuhuda na Agano la Mungu. Hakuna anayedai kuwa Muislamu
anayeweza kuwa na Imani pasipo kujikita kwenye Maandiko Matakatifu na Torati ya
Mungu na kuyaamini na kubatizwa kwenye ushirika wa Kanisa la Mungu.
Korani au Kur’ani ni kitabu cha ufafanuzi tu wa
Maandiko Matakatifu iliyoandikwa na viongozi wa Makanisa ya Mungu katika karne
ya saba ya Zama Zetu za Sasa huko Uarabuni. Itafunuliwa na kufundishwa uhusiano
wake na Maandiko Matakatifu. Uhusiano uliopo na maandiko ni wa muhimu sana. Ina
nafasi yake kwenye historia ya Kanisa, kama zilivyo hizi nyaraka za mitume
kwenye historia ya Kanisa kwenye karne ya kwanza.
Swali la 6. Kuokana na
Sura za 2:4-6, 41-42, 89-91, 101 na 136, tunaweza kudai kuwa kile wanachokuwanacho
Watu wa Kitabu, wakati wa uhai wa Mtume, inaonekana inatia hamasa kubwa sana
kwenye Kur’ani?
Jibu. Familia ya Mtume ilikuwa
na maandiko ya Biblia. Tunajua
kuwa wakati zilipokuwa zinaandikwa na tunajua mwamba maandiko yote yako sahihi.
Magombo yajulikanayo kama the Dead Sea Scrolls yanatuonyesha kuwa maandiko
ambayo watu wa Mashariki ya Kati na kanisa na viongozi wake walikuwanayo, na
kwamba yalikuwa ni yaleyale kama yalivyokuwa wakati wa Kristo na ule wa Eloa habadiliki.
Fikra hii ilisema kwamba maandiko asilia yamepotezwa na Makhalifa waliofuatia
ili kukwepa kuzishika sheria. Waliaanza kudai kuwa Qasim na Muhammad walikuwa
na maandiko halisi vinginevyo wangekuwa wamejulishwa kama Korani inavyowataja
kuwa ni Watu wa Kitabu na kudai kuwa kama kuna mashaka yoyote kwenye Maandiko
inabidi wawaulize ikiwa ni kama maamuzi yao ya mwisho.
Agano Jipya
liliandikwa na watu wa kanisa la karne ya kwanza. Mitue Mathayo na Yohana
waliandika injili zao na wanafunzi Marko na Luka waliandika za kwao. Nyaraka za
Paulo ziko sahihi na Kitabu cha Waebrania kinadaiwa kuwa kuwa kiliandikwa na
Paulo na kumaliziwa na mwanafunzi mwingine, inadhaniwa kuwa huenda alikuwa ni
Barnaba. Yohana anachukuliwa kuwa aliandika injili, nyaraka na kitabu cha
Ufunuo kwa neema aliyopewa na Masihi kukiandika.
Historia ya
kanoni imeelezwa kwa kina kwenye jarida la Biblia (Na.
164). Jarida hili litakupa dodoso zaidi. Watu asilia walioitwa kuwa ni watu wa
kitabu bado wapo, bali ni wachache sana. Imeandikwa: “kwa hakika tulimpa Musa
Maandiko Matakatifu na tulifanya mlolongo wa mafuatano kwa wajumbe waliofuatia
baada yake, na tulimpa Yesu mwana wa Mariamu [kimakosa wanamuita Maria waamini
Utatu] ushahidi wa wazi na tulimsaidia kwa njia ya Roho Mtakatifu. Ni kwa hiyo
kwamba atakapokujia wewe mjumbe pamoja naye ambaye wewe mwenyewe humpendi,
akajitukuza kwa majivuno nawe usimuamini na wengine watamuua?”
Swali la 7. Inaonekana
kuwa na tofauti za muhimu kati ya Biblia na Kur’ani. Watu wameamini kwa hiyo kwamba
ilikuwa ni muhimu kuikataa moja na kuiamini au kuipa nafasi nyingine, au
kuchukua kidogo upande moja na kuiweka kwenye kidogo kilicho kwene nyingine.
Je, ushauri wako ni upi kwa hili?
Jibu. Inapochukuliwa na kusomwa kwa kutenganishwa, Korani, kama Agano
Jipya, inaweza kukanganyika na haitaepukika kabisa kufanyika kuwa ni chanzo cha
migawanyiko, chuki, mteso na hata vita. Wakati vitabu vyote vitatu vinaposomwa
kwa pamoja, ni kama vinavyotakiwa kuwa, inawezekana kuvielewa na mpango kamili
wa wokovu unaoongelewa hauwezi kutafsiriwa kimakosa.
Korani kama kitabu kingine chochote kwenye Kanisa
la Agano Jipya iliandikwa kwa Waarabu miaka takriban mia sita baada ya Agano
Jipya la Karne ya Kwanza na sasa linajumuishwa kwenye Kitabu Kimoja kiitwacho
Biblia.
Swali la 8. Je,
Kur’ani imefaniwa marekebisho au/na imekuwa ikipitia vipindi kadhaa vya
kurekebishwa kwa karne fulani kadhaa?
Jibu. Usmani alichoma ushahidi
wowote wa Kanisa ambao uliokuwa unakwenda kinume na mipango yake na akaenda
,bali kwa kufanya kila aliloliweza ili kawdanganya “kondoo” kwa hatua moja kwa
kila wakati pasipo kukamatwa na wengi. Hata hivyo, upende wa Ali ulichukua
mamlaka, lakini wafuasi wa Usmani walikuwa na nguvu kuliko hawa wengine. Ali
akauawa na hatimaye Kanisa liliendesha shughuli zake kichinichini tena. Kuuawa
kwa Ali yalifanyika ili kufanilisha mkakati wa kuikomesha imani ya kweli huko
Uarabuni.
Maelezo ya kina kuhusu habari hii yanakutikana kwenye
jarida la Utangulizi Kuhusu Ufafanuzi wa Kur’ani (Q1).
4:
Allah
Swali la 1. Ni nini asili ya mungu – Allah – wa
Waislamu? Ni moja tu nay a Yahweh wa kwenye Maandiko Matakatifu?
Jibu. Jina Yahovah (Yahweh) linatumika kuwaita viumbe wanne, watatu wao wakiwa ni
malaika, au wajumbe wa Mungu wa Mbinguni kwa wakati mmoja kama tunavyoona
kwenye mfano wa Ibrahimu na Lutu, na kuangamizwa kwa Sodoma na Gomora. Mambo
haya yote yameelezewa kwa kina kwenye majarida ya: Malaika wa YHVH (Na. 24); Majina ya Mungu (Na. 116); Uwepo wa Jesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa
Kwake Duniani (Na. 243) na Ibrahimu na Sodoma (Na. 91).
Kuna majina mbalimbali ya Mungu kwenye vitabu
vyote viwili, yaani Biblia na Kur’ani. kur’ani inatumia jina la Kiarabu la
Allah’ ambalo ni la umoja kabisa na linaonyesha na kukubaliana kwamba halina
umoja kabisa. Ni la “uweza” (au laa Uungu) ambaye ni Mungu.
Yeyote asiyeelewa ukweli kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Kweli yupo kwenye
mafundisho za uzushi. Uyunitari wa Kibiblia haukubaliani kwamba Yesu Kristo
alikuwa kuna umilele au usawa na Baba Eloah. Kuna MUNGU MMOJA TU WA KWELI naye
ni Baba wa wote na alimtuma Jesu Kristo (Yohana 17:3). Kwa kuujua ukweli huo ni
muhimu kwa ajili ya kuupata uzima wa milele.
Jina Allah’ ni la
Kiarabu linalomaanisha Mungu wa Pekee wa Kweli, Eloah anayejieneza mwenyewe kuwa
ni elohim kwa kupitia watu aliyejiita kwenye imani yake. Kulijua jina hili la
Mungu ni jaribio la kumwelewa Roho Mtakatifu. Waditheist au Wabinitarian walishindwa
jaribio hili.
Swali la 2. Kama naelewa
sawasawa, Waislamu wanamwabudu Allah. Je, huyu ndiye Mungu wa pekee na kama ni
hivyo, walipataje jina hili lake?
Jibu. Majina ya Eloah na Allah’ yametoholewa kutoka kwenye
tofauti mbili za muundo wa lugha hiyohiyo.
Kwa jina la Kiarabu, “Allah' ” limetokana na lugha ya Kiaramu cha Mashariki
na cha Kikaldayo cha zamani, “Elahh.” Ni jina la umoja na inakubaliana kuwa si
jina la uwingi. Yeye ni Mungu wa Pekee wa Kweli wa kwenye Biblia, “Eloah.” Neno
la umoja “Eloah” na kwa Kikaldayo ni “Elahh” linakuwa ni neno la umoja “Elohim”
kwenye Kiebrania na “Elahhin” kwa Kikaldayo. Huyu ni kiumbe anayejieneza ambaye
ni Mungu na Wana wa Mungu ambaye ni malaika wa mbinguni.
Jina “Elohim” linatumika kwa ni umoja kwenye kulitumia na kisha linatumika
kumtaja “mmoja wa Elohim.” Mahali linapotumika kwa maana ya “Eloah” kwa kawaida
linatumiwa kama “ha Elohim” au “Elohim” au “Mungu.” Kwa Kiyunani, kitendo hiki
kinaendelea kwenye Koine kama “Ho Theos” na “Theos” au mwenyekulaumiwa au
kushutumiwa “ton Theon” na ni kama “theos” ni jina linalomlenga au kumtaja elohim.
Kwenye uwingi huitwa elohim limefanyika kumaanisha “theoi.” Mwislamu anamjua
Mungu Mmoja wa Kweli aliyeandikwa kwenye Yohana 17:3 kama “Allah' ” maana ya
jina hili kutokana maana yake asilia linatokana na
maana ya moja kwa moja kutoka kwenye lugha asilia ya kale ambalo kwa hakika linamaana
ya Mungu kama “Nguvu au Uweza.” Inamaana ya liherufi el, ambacho kinaweza kutumika kumtaja mwenye nguvu au Mwenyezi na
pia kwa kisarufi linachomaanisha au kinachotuama kwenye uwingi kama hizi au wale walio miongoni mwetu. Kwa maana hii ina maana hiyohiyo moja
kwenye Kiebrania na Kikaldayo na hata kwenye Kiaramu na nyingine nyingi
mbalimbali. Kwa maana hii ni kwa umoja tu wakati linapotumika kama “hivi” au “wao.” Kwa jinsi hii ni ajabu kuwa ni uwingi kwenye kamuzi ya SHD
429 inapoandikwa kama ‘elleh kwa Kikaldayo
ila limeunganishwa au kujumuishwa kwenye namna ya umoja ya Eloah. Neno hili ni
hilohilo la kama Eloah (au Eloahh) au Elowahh kwa Kiebrania na linataja na
kumaanisha umoja wa Mungu mmoja wa kweli. Maana ya uwingi elohim au elahhin ni neno
la Kikaldayo kwenye uwingi isipikuwa pale kipengele kinachoelezewa linatumika
kulifanya hilo Ha elohim maana yake
ni Mungu (sawa na kwenye kamusi ya SHD
430 na notisi zake). Kwa hiyo, Mungu ni uweza unaoenea na kuendelea kwenye
viumbe vingine vya mbinguni ambao ni malaika na wanadumu kuwepo kama wale walio wamoja wetu. Kwa hiyo, jina elohim
na yahovah yanatumika kama viumbe wengi
kama viumbe wa Mungu wa Pekee wa Kweli, na wote wanamtumikia yeye. Maana yake
ni hiyohiyo iliyo kwenye lugha ya Kikaldayo au Kiebrania au lugha nyingine
mbalimbali yaliyotoholewa kwenye lugha hizo. Jina Allah’ ni aina tu ya inayotambulisha maana hii ya Nguvu moja inayotenda kazi katikati
yetu. Inajumuisha dhana ya uwingi pekee kwa namna nyingine ikiwa ni kama mawakala
wa Nguvu itendayo kazi kwa niaba yake
na inajumuisha mambo ya ngvu zake.
Propaganda
zinazoenezwa na Wabinitariani na waamini Utatu au Watrinitariani wa Magharibi
wanalichukulia jina la Mungu kwenye Uislamu kama habari au taarifa za zisizo na
mashiko na zisizojulishwa na zinazopasa kuchanganuliwa kwa namna yoyote
iwezekanavyo kuiita (soma majarida ya Majina ya Mungu (Na. 116) na Jina la Mungu Kwenye Uislamu (Na. 54)).
Swali la 3. Je, Mtume alimjua Mungu wa Wayahudi kuwa ndiye
Mungu wa Pekee wa Kweli?
Jibu. Imani ya Kiislamu inamtaja Mungu Mmoja wa Kweli kuwa ni Allah. Imani
iliyoko kwenye imani ya Kiislamu (Shahaadah) ni sahihi ya kwamba hakuna Eloah mwingine
ila Eloah (La Elaaha Ella Allah (soma pia Sura za 37:35; 47:19). Waislamu
waliochanganyikiwa wanasisitiza kuongeza “Shahaadah” ya pili wakitangaza kwamba
Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Hii ni kwa kuielezea kuwa ni ‘Kwepa’ (ibada
za sanamu) na uasi wa wazi kwa Mungu na ya mjumbe au wajumbe wake. Korani inasema
kwamba imani haifanyi utofauti wowote kati ya manabii (Sura ya 3:83-84). Manabii wote wako sawa kwenye mahasa yao kutoka
kwa Mungu.
Muhammad na
mahalifa wake wanne wa kwanza waliitwa mahalifa
viongozi waliokuwepo wakati huohuo ambao walikuwa ndio Waislamu asilia
pekee waliofundishwa vizuri kuwaongoza Waislamu. Baada yao, Uislamu ulipotoka
na ulikengeushwa kwa mapokeo ya kitamaduni (yaliyoitwa
Hadithi au Ahadith) kama ulivyofanywa kwenye imani ya Kiyahudi na
Ukristo zilizoutangulia.
Qasim na Muhammad alianza kuhubiri vizuri sana
akijiepusha na imani ya na mafundisho ya Watrinitariani, Waathanasiani,
mafundisho waliyoyaona wao kama uzushi, na kuwaunganisha Waarabu kwenye imani
ya Kimonotheism. Korani huwaweka pamoja Wakristo kwa aina mbili za majina,
yaani – Watu wa Kitabu au Maandiko Matakatifu na Wakristo kwa ujumla. Tofauti
hizi kwa sasa zimepotea kwa kuwa Wakristo wa leo hawajui tofauti zilizopo kwa
wakati ule. Tofauti zenyewe zinahusu Watrinitariani waliopigana na Uislamu na
kulitesa Kanisa la Pergamo, lililoungana na Uislamu.
Swali la 4. Kuna Mkristo aliyeniambia kwamba Allah alikuwa na moyo kama mwanadamu. Je, Allah alikuwa
na roho ya kama malaika, au mwanadamu na viumbe wengine, tukiona kwamba wote
waliumbwa kama alivyo Mungu? Je, roho inaumbwa au sivyo?
Jibu. Biblia inaongelea kuhusu roho iliyo ndani
ya mwanadamu. Ni tofauti na alivyo Roho wa Mungu. Ni kama pumzi yetu. Ni zawadi
au kipawa cha uzima toka kwa Mungu (Zekaria 12:1). Wakati tunapokufa roho ya mwanadamu
hututoka (Zaburi 146:4). Inarudi kwa Mungu (Mhubiri 12:7). Wakati Mungu
alipomuumba Adamu Alimpulizia puani mwake
pumzi ya uzima, na mtu akawa kiumbe hai. (Mwanzo 2:7; 1Wakorintho 15:45).
Kwa
hiyo, roho hii ya ndani ya mwanadamu sio roho anayeishi “Mbingun” tunapokufa.
Biblia inasema sema kuwa mtu akafanika
kiumbe hai au nafsi. Roho inaweza kufa (Ezekieli 20:18). Wakati Biblia
inaposema kuhusu roho ni hakika kuwa inaongelea juu ya maisha ya mwili. Roho inaweza
kumaanisha kuwa kiumbe, au mtu au uzima. Wote wawili, yaani mwanadamu na mnyama
hufa kwa namna hiyohiyo, ila mwanadamu atakujaishi tena. Kwa hiyo, roho ya
mwanadamu ndiyo inayotutofautisha sisi na wanyama.
Mungu
si mwanadamu; bali ni kiumbe mwenye Roho njema nay a kweli. Kufundisha kuwa Mungu
ana roho ndani yake ni jaribio lingine la kudai kwamba roho inaishi milele.
Fundisho la roho kuishi milele ni uwongo mwingine, ni sawa na uwongo mwingine
unaoendelezwa wa kwamba mapepo au mashetani hawafi na kwamba hawawezi kutubu.
Swali la 5. Roho Mtakatifu ni nani kwenye Kur’ani? Je, neno la Kiarabu la ruh al-qodos linamaana
ya Roho Mtakatifu, kama lilivyo sawa na neno Roho Mtakatifu na neno la
Kiebrania limtajal Rohfu na neno la Kiebrania limtajal Roho Mtakatifu la, ruach al qodesh?
Jibu. Kwa kweli, Ahmed maana yake ni Mtetezi au Wakili au “Mwenye Kusifiwa Sana” na ina maana ya Roho Mtakatifu
ambapo Yesu (Yahoshua/Yoshua) alikuwa ni Mleta Habari. Kanisa
liliongozwa na Roho Mtakatifu na huyu ndiye Ahmed/Wakili aliyetajwa kwenye Korani.
Swali la 6. Wakati anapotajwa Mungu, kwa nini Korani
inatumia viambishi vyote viwili vya “Mimi” na “SISI?” Wengine wanasema ni
mtazamo wa mtindo wa moja kwa moja kwa Kiarabu, au mtu aliyekusudiwa kwa
kutumia kiambishi cha “sisi” kwa kutilia maanani na kwa utukufu. Tafadhali
nishauri ili nijibu kwa usahihi kwa wasioamini wanaouliza swali hili.
Jibu. Korani inaelezewa kwa kupitia Jina la Uungu –Smillahalrahmanalrahim.
Kila sura inatanguliwa na muundo ulio sawa “Na Allah-Alrahman-jina la Alrahim's”
(Ku’rani:1).
Mwanzoni mwa
sura ya 9 kumepotezwa na ndiyo maana neno Bismillah halipo hapo. Neno Bismillah
ni si sehemu ya ufunuo isipikuwa pale panapoonekana kwenye mabishano.
Sehemu
kubwa ya Korani, Jina la sifa za Mungu aliye juu ya mengine yote (Ku’rani 1:5).
Zaidi sana, Jina la Mungu kila mara limekuwa likibadilishwa badilishwa kati ya anapotajwa
kwenye nafsi ya kwanza ya umoja na kwenye nafsi ya kwanza ya uwingi na kurudi
tena hata kwenye sentensi hiyohiyo (Ku’rani 2:38). Mambo haya yanamlingano wa
moja kwa moja na maneno ya Bwana alipokuwa anafananisha na maneno ya Elohim kwa
kupitia kwa Manabii wa zamani. Ni kama “maneno” aliyoyasema Bwana kwenye Kutoka
4:22 na kwenye Yeremia 31:9 kuhusu Israeli, Jina la Mungu anenaye nasi kama
watoto wake Ku’rani 31:16-19.
Kwenye
Ku’rani 90:3, Jina la mtu huyu anaonekana akiapa kwa nafsi yake mwenyewe na kwa
Yesu (Ku’rani 19:15 na 33) inaonyesha kabisa kuwa ni mzaaji na mzaliwa ambaye
Waebrania 1:8-9 inaonyesha kuwa hakika ni yule “Elohim” (au Zaburi 45:6-7) ni
msaidizi au mdogo wa Mungu Mwenezi.
Kwenye
Ku’rani 43:57-60, Jina la Mungu analolitaja na kuwaelezea Yesu kuwa ni kama
Mtumishi na Khalifa, kwa namna nyingine ni kama kuujaribu uungu wake au mamlaka
yake ya kimbinguni. Mungu kwa upande mwingine wakati inapofanyika kuwa ni
chanzo cha Roho (Ku’rani 4:171, Ku’rani 58:22) asiye na mtoto (Ku’rani 10:68, Ku’rani
17:111, Ku’rani 18:4, Ku’rani 19:35, Ku’rani 19:88-92, Ku’rani 21:26, Ku’rani 23:91,
Ku’rani 25:2, Ku’rani 37:152, Ku’rani 43:81, Ku’rani 72:3) – aliyeokolewa kwa
kufanywa mwana au kuasiliwa (Ku’rani 39:4) – lakini hata wakati madai
yanapotangazwa kwa uzazi wa kweli (Ku’rani 33:5). Wala jahazaliwa (Ku’rani 112:3)
ingawa hakuna mungu ila yeye (Ku’rani 2:163). Lakini bado jambo linapokuwa mama
yetu, Roho ni Baba yetu, akati Mungu
sio mwwnzetu au hayupo kama sisi (Ku’rani 6:101). Hata hivyo, Jina la Mungu
ndiye Baba Yetu, na jina lake Mungu ni mlinzi wetu.
Swali la 7. Sura ya 12:87
ina maneno ya Kiarabu ruh Allah, yaliyoandikwa kwenye baadhi ya
tafsiri kama rehema za Allah. Ina maana gani?
Jibu. Neno lililo kwenye Sura
ya 12 kwenye ayat 87 si ruh Allah kama
lilivyopotoshwa kimakosa. Bali ni rauh.
Abdullah Yusuf Ali kwenye tafsiri yake ya 1762 anaweka maneno haya akidai
kwamba watafsiri wengi wamepotosha kimakosa neno hili. Anasema kwamba: “Rauh inajumuisha dhana ya Rehema
linalopotosha au kupunguza maana hali yetu halisi na ni sahihi sana kwa hakika
hapa midomoni mwa Yakobo.”
5: Kristo
kwenye Korani
Swali la 1. Tukiachana
au mbali na tafsiri ya Talmudi ya Kiyahudi ambayo haimtambui Masihi, Je, Mtume
huyu wa Waislamu alimtambua Yesu Kristo kuwa ni Masihi ajaye?
Jibu. Familia ya Kasimu
ilikuwa ilikuwa na ushawishi na ilikubaliana na mafundisho ya Kikristo na
walikuwa Wakristo, ila hawakuwa Watrinitariani na hivi ndivyo Uislamu ulivyoanza
na jinsi Korani ilivyoandikwa. Yapasa ikumbukwe kwamba Mtume huyu wa Mwarabu alikuwa
anaandika ili kupinga imani na mafundisho ya kizushi ya Watrinitariani
watrinitariani walidai kwamba Kristo ni Mungu wa kweli, wakati Biblia iko wazi
sana kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Kweli na kwamba Kristo ni mwana wake
aliyemtuma (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20). Yapasa Korani isommwe kwa nuru au mtazamo huo
wa kimaandiko aliyonayo Kasimu na baraza lote la uongozi wa Muhammad.
Hakuna
Mwislamu anayejiteua mwenyewe anaweza kuisoma Ku’rani na akaikataa Torati, au
Injili au Zaburi au vitabu vya Manabii.
Swali la 2. Inamaana
kwamba Sura ya 4:171, Ku’rani
inamtambua Yesu kama Neno wa Mungu aliyetumwa kwa Mariamu (sio Maria). Je, hii
ni tafsiri nzuri ya kujua maana ya Sura hii?
Jibu. Ndiyo, ni ruach ha qodes wake na
neno lake ambalo Allah alilieneza ndani ya Kristo (kama ilivyo kwenye Sura za.
2:87; 3:45; 4:171; 5:46). Huyu ayat ameelezewa na watu wa Kitabu au wa
Maandiko. Kwenye waraka alioandikiwa Negus, mfalme wa Abyssinia (Ethiopia),
Muhammad alisema: "... Yesu ndiye ni mtumishi wake [Allah] na mjumbe wake na ni roho wake na ni
neno lake aliyemtia ndani ya Maria." Yussuf Ali pia kwenye
kifungu cha 676 anafanya rejea kwenye Sura ya 3:59 anasema kuwa yeye ni roho
anayetangulia kutoka kwa Mungu lakin sio Mungu wa Pekee wa Kweli. Andiko hili
lina maneno yaliyoongezwa yasemayo: Kwa kuwa Mungu ni mmoja: Utukufu ni wake (Na
Atukuzwe Sana) zaidi ya kuwa na mwana, yaani, ‘Atukuzwe Sana yeye’ imeongezwa
ili kuligeuza andiko ambal linasema tu Na
Apewe Utkufu zaidi ya kuwa na mwana. Andiko hili halimkani mwana ila
linampa utukufu wote Mungu peke yake.
Swali la 3. Korani inakataa kwa nguvu zote umbunguni wa Kristo na uwana wa Mungu wake.
Je, kwani Korani inafundishaje kuhusu Kristo, na je, Uislamu una sehemu kwenye
imani waliyopewa watakatifu mara moja tu?
Jibu. Kama ilivyo Biblia,
Korani lazima itatilia maanani na haiwezi kusomeka ikiwatenganishwa mbali na Biblia. Maandiko yaliyo kwenye Korani
yaliyo mbali kwa kweli yamaonekana kuupinga au kukataa ukweli wa Kristo kuwa ni
Mwana wa Mungu kama tunavyoona mara moja hapo juu lakini andiko limeongezwa
sana baadae. (soma jarida la Kristo na Korani (Na. 163)).
Hakuna
nabii au mtume anayeweza kukataa au kuipinga torati na kile kilichofunuliwa
kabla yake kwenye ushuhuda (Isaya 8:20). Ujumbe wa mtume au nabii yeyote ni
ufafanuzi au mwendelezo wa kile kilichotangulia kabla yake, na ufunuo wa Mungu wa
kile kinachojiri kutokea. Hadithi za Kiislamu zimeanzisha tafsiri
zinazoikangana Korani, pamoja na Maandiko Matakatifu. Ndivyo ilivyo pia hata
Wakristo wengi wanakataa au kupinga ushikaji wa Sheria za Torati na Ushuhuda.
Wakristo hata hawazitii Amri Kumi za Mungu. Yuda hata hawawezi kujua kwamba
walimuua Masihi wakati Maandiko |Matakatifu yalisema kwamba wangemuua, na Agano
Jipya linashuhudia kuwa walimuua.
Swali la 4. Kwa nini Masihi wa kwenye Korani
anaonekana kuwa alizaliwa kwa minajiri sawa na mwanadamu mwingine yeyote; je,
hakuwa mwana wa pekee wa Mungu?
Jibu. Huu ni mtazamo
wa Korani, unaosema kuwa Kristo sio mwana pekee wa Mungu kwa jinsi yoyote ya
kimwili (sawa na Sura ya 19:34; 4:171) lakinibut God simply said: Be! And he was in the body of Mariamu na kitoto cha kibinadamu (Sura ya
3:59). Kwa jinsi hii, Neno akafanyika mwili na akaishi kati yetu (Sura ya
4:171; Yohana 1:14).
Swali la 5. Je, kwenye Kur’ani, kunasema kuwa Yesu alizaliwa kama mwanadamu mwenye
kuweza kutenda dhambi?
Jibu. Kristo
angeweza kutenda dhambi au vinginevyo angekuwa ni roboti na hapa kusingekuwa na
kuhukumiwa kwa Shetani. Kwa namna zote alijaribiwa kama tufanywavyo sisi (Waebrania
4:15; soma jarida la Kusudi la Uumbaji na Dhabighu ya
Kristo (Na. 160)). Hakuna mahali popote kwenye Korani panaposema au
kuonyesha kuwa hakuwa na uwezo wa kutenda dhambi, na sadaka yake na wokovu wetu
unategemea jambo hili. Nawezaje kuwa Masihi basi kama Korani inavyomtangaza
yeye kuwa hivyo?
Swali la 6. Ni kwa nini mafundisho ya Korani
yanasema kwamba Kristo hakusulibiwa bali aliyesulibiwa alikuwa ni mtesulibiwa
alikuwa ni mtu mwingine tu na wakati huo huo inamuonyesha Yesu kuwa ni
Masihiwakati huo huo inamuonyesha Yesu kuwa ni Masihi? Andiko hili linatofautiana na injili.
Jibu. Kwenye Sura za 3:55
and 5:117, zinasema wazi sana kuwa Mungu aliruhusu Yesu afe na kwamba Yesu
alifufuliwa na Mungu wake, aliyemrejesha kwake. Waislamu wa siku hizi ndio
wanaokataa kumkubali Masihi na hata wanazikataa Injili walizoambiwa wazisome.
Waislamu wa siku hizi kwa kweli hawapendi hata kutii na kufanya kama walivyoagizwa
na Korani.
Swali la 7. Kwenye Sura ya 5:110, Kur’ani inafana rejea kwa Yesu na inasema kwamba
aliwahubiria wanadamu kutoka akiwa mtoto mdogo. Je, unaweza kulielezea hilo?
Jibu. Andiko lenyewe linasema:
Ili kwamba uweze kunena kwa watu ukiwa
mtoto mdogo na ukuapo (soma pia kwenye Yussuf Ali kifungu cha 817 na 3:46 na
fungu la 388 kwa ajili ya andiko hilo). Ni rejea ya Injili (Luka 2:46) ambapo
Kristo aliongea na wazee Hekaluni na ambao walimshangaa sana. Andiko linaendelea
kwa kusema kuwa Mungu alinena na Yesu Kristo kuwa Tazama! Nilikufundisha
Kitabu na Hekima (yaani kwenye Sura ya 3:48), Torati na Injili. Kwenye andiko hili
pia linaonyesha uponyaji aliofanyiwa kipofu na wakoma na ufufuko wa wafu kulikofanyika
kwa mapenzi ya Mungu na sio kwa mapenzi ya Kristo wala kwa uweza wake binafsi
yake. Utumiaji wake udongo alioufanya katika kuwaponya watu kunatajwa pia
kwenye andiko hili.
6: Biblia na Ukristo
Swali la 1. Je,
Waislamu wanawamini Mungu huyuhuyu mmojawanaomuamini Wakristo?
Jibu. Imani ya Kiislamu inamlenga Mungu Mmoja wa Kweli wanaomuita Allah. Ni raisi
kwa wote kuona kwamba hakuna Mungu mwingine ila ni huyu Mungu Mmoja wa Kweli
peke yake na Yesu Kristo aliyemtuma (Yohana 17:3).
Kile ambacho Mtume huyu Mwarabu anachokifanya ni kuiharibu na kuifutilia
mbali kabisa nadharia na mafundisho ya Waathanasiani ya
Utatu, ambayo hayakuwepo kabisa na wala kufundishwa na Kanisa la Kwanza, na
mbayo kwa kuyapinga kwao watu wengi walikuwa wanaendelea kuteswa na kuuawa.
Imani ya Utatu imejengwa kwenye msingi wa uwongo wa Ubinitariani
ulioingizwa kwenye mtaguso wa Nicea mwaka 325 BK. Nadharia au dhana na Undumila
Kuwili kwenye imani ya Kristo na Mungu unatokana na upotoe huu (soma jarida la Upotofu wa Kufafanua Ubinitariani na Utrinitariani
wa Teolojia ya Kwanza Kuhusu Uungu (Na. 127b)). Mtume Kasim alikabiliwa na
ukanusshaji wa upotofu huu kila mara, kutkana na kuyaeneza kwake mafundisho ya
uwongo (soma jarida la Kristo na Korani (Na. 163)).
Kristo
hakuwa tu kuwa alikuwepo hata kabla ya kuzaliwa kwake rasmi, bali aliuwa nab
ado ni elohim au Elohi wa Israeli, kams Yahova, aliyetumwa na Yahovih au Yahova wa Majeshi, Elyon au
Mungu Mwenyezi Aliye Juu Sana. Kiumbe huhu, Mungu wa pekee wa kweli, ni
Eloah. Yeye ndiye mlengwa na anayestahili kuombwa kwenye Hekalu kama HaElohim
wa Elohim au Mungu. Kristo
sio huyu Mungu mmoja, wa pekee wa kweli. Ni huyu peke yake, Eloa (Elahh kwa
Wakaldayo na Allah’ kwa Waislamu) alisimama peke yake akidumu milele
akiwa hana wa kulingana naye wala kufanana naye ile ni yeye mwenyewe tu peke
yake (sawa na lisemavyo jarida la Teolojia ya Kwanza Kuhusu Uungu (Na. 127)). Ha Elohim (au Elohim) alikuwa ni Eloah.
Alikuwa ni Mungu wa Masihi na alimtia mafuta kuwa elohim kwa mafuta ya furaha
juu zaidi kuliko wenzake wote (sawa na Zaburi 45:6-7; Waebrania 1:8-9) na
Kristo alikuwa mwaminifu kwa yeye aliyemuumba (kama isemavyo Waebrania 3:2 Kamusi
ya Marshall’s Greek English Interlinear RSV).
Swali la 2. Tafsiri
nyingi za Kur’ani hutumia neno dini au
dini ya Allah. Je, neno hili dini
linpatikana kwenye kwenye nakala asilia ya Kur’ani?
Jibu. Korani imetafsiriwa kimakosa mara nyingi
ili kuficha maana inayofanana kati yake, yaani Korani na the Biblia.
Sura ya Ng’ombe
[2.138] (Pokea) ubatizo wa
Allah, na ni nani aliye bora zaidi ya Allah kwenye ubatizo? na yeye tunayemtumikia.
Roho Kur'ani, iliyotafsiriwa na M.H. Shakir na kuchapishwa na Tahrike
Tarsile Qur'an, Inc., in 1983.
Tafsiri nyingine nyingi zimeorodheshwa hapa chini
zikisema yafuatayo.
Tafsiri ya Pickthall: (Tunachukua) rangi yetu
kutoka kwa Allah, na ni nani aliye bora zaidi kuliko Allah kwa rangi. Sisi ni
wafanya ibada tu.
Tafsiri ya Darabadi: Tuliyonayo ni rangi iliyotiwa
na Allah! Na ni nani aliye bora kwenye utiaji wa rangi kuliko Allah! Nasi ni
wamwabuduo.
Tafsiri ya Mohammed Asad: [Sema: “Maisha yetu yanapakwa yake] rangi toka kwa Mungu! Na ni
nani anayeweza kutia rangi (ya maishani) kuliko Mungu, ikiwa sisi ni wamwabuduo
halisi yeye?
Tafsiri ya Yusufali: (Dini yet uni) Rangi ya Allah:
na ni nani anawezaye kutia rangi vizuri kuliko Allah? Na ni yeye ndiye
tunayemuabudu.
Ufafanuzi: Sibghah
ص ب غ: maana asilia inaonyesha kuwa ni upakaji au utiaji rangi, ikimaanisha kuwa
ni Wakristo Waarabu waliochanganya rangi kwenye maji ya ubatizo, ikimaanisha
mtu aliyebatizwa aliyepata rangi nyingine mpya maishani mwake. Yusuf Ali.
Neno “Sibghatun” maana yake ni kuchovya au
kupaka rangi, kutia rangi. Kwa hiyo, maneno haya yametoholewa au yanatokana na
shina la herufi yanayomaanisha: kuchovya, kupaka rangi, kubatiza, kuzamisha,
kutia yote, kupaka, kuchukua tabia, mtindo, ukuzi, kifungu cha sheria, dini.
Kwenye Aya ya 138 ya Sura ya
Al-Baqaraah ya Kur’ani sifa za Allah na Gombo la Sheria linaitwa Sibghah
ya Allah.
Korani inaamuru
kwamba mwaminifu ni yule aliyetubu na kubatizwa. Hadithi za siku hizi
zinafundisha kwamba ubatizo si kitu cha lazima, na wanatumia andiko kuashiria
kuwa Allah anabatiza kuliko ubatizo mwingine wowote wa kimwili unaohitajika,
ambavyo ni kinyume sana kabisa na malengo ya Korani na Biblia. Ujumbe wa Korani
yapasa utafsiriwe kutokana na mahudhui ya Maandiko Matakatifu. Ubatizo ni kitu
cha muhimu kwa wateule ili kuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Wale
wanaofundisha kinyume chake, hawatauingia Ufalme wa Mungu wala hawataingia
kwenye Bustani ya Ufufuo wa Kwanza wa wafu,wao wenyewe, na wanawazuia wale
wanaowasikiliza kuwa na sehemu hiyo pia.
Biblia inasewa wazi
sana kwamba kuna Imani moja, Ubatizo mmoja, Bwana mmoja, Mungu mmoja na Baba
mmoja wa wote na aliye ndani ya yote na wa kila kitu (Waefeso 4:5; Korani Sura
ya 2:138; 5:73; 6:82). Karibu ulimwengu wote kwa hakika hawajabatizwa kabisa.
Swali la 3. Ni wapi
panapoonekana kuwa yeye ni "mtume mmataifa" ambaye Kur’ani inamwelezea
kwenye Vitabu? Nimekuwa nikimtafuta... Sura ya 7:157. Hoja ni kwamba, neno Ummi na kutoholewa
kwake halimaanishi "mtu asiyejua kusoma wala kuandika," bali
linamaanisha "Mmataifa." Tunapotafuta rejea zote za neno hili na
kutoholewa kwake (mara saba)—mifano yote inaonekana kutiririka vizuri na
kwendana na tafsiri ya Mmataifa. Nilipaona sehemu moja ambapo wanazuoni wa
Kiislamu wa siku hizi wanadai kuwa panataja—lakini sivyo ilivyo kwenye Torati
au kwenye Injili zote. Bali ni kwenye
Isaya 42. Inapendeza kwa kuwa inaonyesha moja kwa moja mahali (ilipo
Kedar) ambapo panaonekana kama ni makazi ya Waarabu.
Jibu. Sura ya 7:157-9 inalionyesha au kulitaja Kanisa ambalo linazishika sheria au
maagizo ya toreati ya Musa (159) (soma Pickthall).
Wanazuoni wa Kiislamu wanajaribu kulifanya andiko
hili limaanishe mtume asiyeandikwa kuwa ndiye anayetajwa hapa aitwaye Kasim
(Muhammad) wa kanisa la Waarabu na Yusuf Ali anatajwa hapa kwenye (1127) na
rejea nyuma kwenye fafanuzi za Musa mahali anaposema kuwa Bwana Mungu wako
atakuinulia nabii katikati ya ndugu zako kama mimi. Anaruka maelezo yaliyonenwa
na Musa kwenye Kumbukumbu la Torati 18:15. Kasim hakuwa mtoto au mwana wa Israeli
na hakuwa ndugu na wana wa Israeli na aingeweza kutajwa hapa.
Aya za 16-18 zinaonyesha kuwa Mungu anasema wazi
kwamba atamuinua nabii kutoka katika Israeli na yeyote atakayepuuza
kumsikiliza, atahukumiwa na nabii Yule atakayenena neno lolote kwa kujikinai
akiwa hajamwagiza, nabii huyo atakufa.
Andiko hili linaeleza tu habari za Kristo na wala
sio Kasimu na Waislamu wanalitumia andiko hili ili kukwepa au kuepuka umuhimu
wa kufuata na kushika sheria.
Swali la 4. Je, Biblia ina
unabii wowote unaomtaja nabii wa Waislamu?
Jibu. Ili kuelewa vizuri maandiko yahusuyo imani, yakupasa uwe mnyenyekevu kwa
Mungu na utubu na kubatizwa na kumpokea Roho Mtakatifu au uwe kwenye mchakato
huo (tazama jarida la Toba na Ubatizo (Na. 52)). Shetani ni mungu wa ulimwengu huu (2Wakorintho
4:4) na ameanzisha imani hii ya dini ya kiutatu yenye Uwongo wa Kiyahudi,
Ukristo wa Uwongo na Uislamu wa Uwongo ili kukanganya, imani isijulikane wala
kueleweka na matengano yatumike katika siku za mwisho ili kuanzisha dini potofu
ya Mnyama na kuwaangamiza kabisa wanadamu.
Swali la 5. Ni nani hawa
“Watu wa Kitabu”?
Jibu. Kile kinachokuja mawazoni unapoisoma
Korani ni kwamba tunaongelea juu ya Ukristo wa aina tatu, aina mbili yake ikiwa
ni isiyopatana kabisa kuhusu Mungu. Kanisa la Kikristo huko Mashariki lilijumuisha
na makanlsa yenyewe asilia yaliyoanzishwa na Mitume, ambao ni Yohana huko Efeso
na Smirna, na pia mengine mengi ambayo yalikuwa ni machipukizi yaliyokumbwa na
wimbi kubwa la mafundisho ya kizushi, pamoja na Wanestoriani na vikundi
mbalimbali vingine vilivyojulikana baadae kama Wamonophysite.
Imani ya Kimonophysitism, hata hivyo,
ilikuja kuwa hatimaye vikundi vya mafundisho ya kizushi vilivyotokana na dini
asilia au kanisa la Mitume. Imani ya Kimonophysitism ilikuwa na mambo yote
mawili, yaani Uyunitarian (ambao mara nyingi waliitwa pia kama Waarians) na pia
Waasians. Waathanasians walipingwa upande wa magharibi na Wakristo wa mrengo wa
Kiyunitarian ambao pia waliitwa Wakristo wa Kiarian, na Watrinitarians wa Roma.
Watu wa
Maandiko wanaonekana kutoka kwenye Sura za 2:105, 111nk., 120, 144; 3:23,
64nk., 98f.,110nk., 186f., 199; 4:44nk., 123, 153nk., 171; 5:5, 15, 19nk., 59,
65, 68, 77, 29:46; 33: 26 nk.; XCVIII 1 hadi mwishoni; LVII: 29. Historia yao
imeelezewa kwenye majarida ya Migawanyiko Mikuu ya Makanisa Yanayozishika Sabato (Na. 122) na Kazi ya Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozishika
Sabato (Na. 170).
Swali la 6. Unazarayo ni kitu gani, na unatokana
na nini? Je, Uislamu ni aina ya Unazarayo wa Kiarabu?
Jibu. Wanazarayo walikuwa ni moja ya namna mbili za kuufanya Ukristo uendane na
imani ya Kiyahudi huko Mashariki ya Kati. Wenyewe walijitenga mbali kabisa na
Ukristo wa Wamataifa. Mwanzoni walijulikana kama Waebionite. Waliikubali injili moja tu ya Mtakatifu Mathayo,
walimkataa Paulo kuwa mtume na walimchukulia kama anayefundisha uzushi (na
walikataa uungu wa Kristo kama walivyomuona Watrinitariani).
Wanazarayo walikubaliana umuhimu wa kuzishika sheria au
“Torati ya Musa” na waliona kuwa ni sharti muhimu kwa Wakristo wanaotokana na
nasaba ya Kiyahudi, lakini waliwaruhusu Wakristo Wamataifa kuwa ni kama lango
la waongofu (sawa na ERE, art. “Judaizing”, Vol. 7, p. 611a).
Kwa hiyo
hawakuonekana kama ni sehemu ya kanisa au Uislamu wa mwazo.
Swali la 7. Je, hawa Wanazarayo wako tofauti na
Wakristo Wayahudi?
Jibu. Wanazarayo kwa kweli walikuwa ni Wayahudi wanaomwamini Masihi walioziamini
na kuzishika sheria au Torati yote ya Musa na walianzisha na kuendeleza kwa
kiasi kikubwa tofauti kwenye imani ya Kikristo huko Mashariki ya Kati. Kwa
hiyo, hawakuwa Waislamu kwa maana ya kuwa kanisa linaloendesha huduma zake.
Swali la 8. Je, huyu Theofilo alikuwa nani? Kazi yake ilikuwa nini kwenye Ukristo wa kwanza
huko Uarabuni na imani yake?
Jibu. Theofilo Mhindi alikuja akitokea kwenye kisiwa cha Dibous na alichaguliwa
kuwa liwali na Mfalme Contantius (mnamo Novemba 3, 361) ambaye alikuwa ni
Mfalme wa Roma tangu mwaka 337 hadi 361. Alikuwa ni Muarian lakini kama
alivyokuwa baba yake Constantine hakuwa amebatizwa hadi alipokuwa karibu na
kufa na alibatizwa kwenye imani ya Kiarian na kwa kweli aliiendeleza sana imani
hii ya Uarian wakati wote wa utawala wake. Hayajulikani mambo mengi sana kwa
hakika kama walivyo wanateolojia waliofuatia baadae wa mrengo wa Kitritarian
waliokashfu wote na kudai kwamba Constantius na askofu wa Antiokia wakati huo
walikuwa wanaitwa wafiasi wa Arians. Hili lilikuwa ni jina na kikundi ambacho
hakikujulikana hadi wakati wa Mtaguso wa Constantinople mwaka 381 na ni hakika.
Alitenda kinyume na mapenzi na maslahi ya Wayahudi kwa kuwakataza tabia ya
kumiliki watumwa au kuwamiliki waongofu wa Kikristo na kuwarudisha kwenye imani
ya Kiyahudi kama watumwa wao. Waandishi waliohudumu kwa ukaribu kipindi chao
walishuhudia sana kwamba alikuwa Muarian kabisa na historia ya Wafalme inaonyesha
kuwa hakuwa na imani nyingine yoyote ile. Hata hivyo, bado alikuwa mpagani pia
na alijitwalia cheo cha Kipapa cha Pontificus Maximus na akamchagua Julian Mkengeufu
aue Apostate kuwa mrithi wake mnamo Novemba 361. Theophilus wa Dibous alichaguliwa
na yeye aende Asia Ndogo apitie upande
wa Kusini na Kusini Mashariki hasahasa na hadi Ethiopia kaba ya lufa kwake
Constantius na inaelezwa kuwa ilikuwa muongo wa sita, uliomaanisha kuwa
alipangiwa kipindi fulani cha mwaka 360 na yaweza kuwa ni kabla ya Novemba ya
mwaka 361. Anaaminika pia kwamba alikwenda kutoka Asia Ndogo na Ethiopia hadi
India. Hii inaonekana kabisa kuwa alikuwa ni Askofu Mkuu wa Abyssinia, na
askofu Mueses alimfuatia hadi India na hadi huko China (soma jaridda la Migawanyiko Mikuu ya Makanisa Yanayozishika
Sabato (Na..122)).
Hakuna
shaka kuwa Antioch hakuwa mwamini Utatu wakati ule na Wasabato wa mrengo wa
Kiarian walikuwa wanaithibiti Asia Ndogo chini ya Wapaulician na Waarabu kwa
ujumla na pia Wanestorians. Hii iliendelea hadi na ilichangia kuibnuka kwa
Uislamu mwaka 622.
Swali la 9. Kwenye
maandiko kadhaa na tafsiri zinazojiri mambo ya dini ya Kiislamu tunaliona neno wasio waaminifu au makafiri likijitokeza (kwa Kiarabu al kafir). Walikuwa watu
gani hawa waliotajwa kuwa ni al kafir au wasioamini wakati wa Mohammad?
Jibu. Wasioamini kipindi kile
walikuwa ni watu wanaopinga na kuikataa imani kwa kuvunja Sheria na Ushuhuda.
Kwa kawaida walikuwa ni Wapagani au Watrinitariani waliojulikana rasmi kwa
mafundisho yao. Hata hivyo, Watrinitarian hawakuruhusiwa kumuoa au kuoana na
Waislamu ila waliruhusiwa kuoana na Wasaabato Wayunitarian.
Swali la 10. Kwenye
Sura ya 6:125, panasema kwamba Allah huwaongoza watu fulani waamini, na ten
anawahukumu wasioamini. Tunajua kuwa Allah ni mwenye haki kabisa, hivyo basi unaitafsirije
Sura hii?
Jibu. Sura hii inaelezea
kuhusu wito wa Mungu kama linavyosema Agano Jipya ambapo Mungu huwaita watu na
inafanya rejea kwenye Warui 8:29-30. Mungu huwaita wale
aliowaridhia na hufungua matiti yao kwenye imani. Wale ambao hajawaita huwaacha
kama walivyo. Hawa ni wale waliokataa kuamini na ni wale aliowakusudia kuwepo
kwenye Ufufuo wa Pili wa wafu kama tuonavyo kwene Agano Jipya ha hususan kwenye
waraka kwa Warumi na kwenye Ufunuo sura ya 20. Kila mmoja ameitwa kwa wakati
muafaka.
Swali la 11. Pia kuna ayats
(aya) zinazosema kuwaua "waovu". Je, aya hizi zina maana gani, na
inakuwa muhimu kuziweka kwenye mukutadha wa makosa kwa zilivyoandikwa?
Jibu. Maandiko ya Agano la
Kale yako wazi kuhusu hukumu zilizoelezewa na sheria au amri za Mungu na Korani
inakazia tu sheria hizi na hukumu zake ambazo kwa sehemu nyingi zimehusiswa na
hukumu ya kwenye Ufufuo wa Pili wa Wafu.
Swali la 12. Sura ya
5:69 haisemi “Wayahudi” bali inatumia vebu ya “Wale walioingia kwenye imani ya
Kiyahudi”. Je, inawaongelea waumini wa namna gani hapa?
Jibu. Hawa ni Waebionite na
Wanazarayo waliotajwa hapo juu.
Swali la 13. Ni kwa
nini Kur’ani inawatofautisha Wasabean ma Wakristo?
Jibu. Wasabaean walikuwa ni
Wakristo Washika Sabato ingawaje yaweza kuwa walitokana na kujipenyeza hadi Waabyssinian
mwaka 300-350. Kipindi hiki cha mwanzo wa Uislamu walikuwa wanaishi Kaskazini
mwa Uarabuni ingawaje chimbuko lao lawezakuwa upande wa Kaskazini na hususan (huenda
walikuwa huko hata kabla ya kipindi cha Sulemani) walikuwa wanaabudu mungu
Mwezi na sayari ya kwenye jua au mungu Shams na imani ya Nyota ya Asubuhi ya Astarte.
Waliondolewa upande wa Kaskazini na kizazi kingine cha kifalme. Mnamo mwaka 300 BK kundi kubwa la wahamiaji wa Abyssinian
lilikipindua kizazi cha kifalme cha Himyarite upande wa Kusini mwa Uarabuni, na
wakaanzisha au kuuzindua “Ufalme wa Saba, Raidan, Hadhramôt, na Yemen", ambao
baada ya mapatano na mahala pa nafasi ya kutosha pa utawala wa Wayahudi wa
asili ya Sabean na mateso makubwa ya kidini, ambayo yaliwalenga au kuwakusudia
jamii ya zamani ya Wakristo wa Abbysinian (yaani. Pereira, "Historia dos
Martyres de Nagran", Lisbon, 1899) ulianzishwa kwa kuingilia kati kwa Byzantine
mwaka 525. Baada ya msafara wa Viceroy Abraha huko Maka mwaka 570, Waajemi
walichukua udhibiti wake. Kusini mwa Arabia ikafanyika kuwa jimbo la Waajemi
hadi kipindi cha kuanza kwa dini ya Kiislamu.
Baada
ya kipindi hiki kulikuwa na aina tatu ya vikundi vya Wasabean. La kwanza
lilikuwa huko Iraq karibu na Basra waliokuwa pia wanaitwa Wanasorians au Wamandeans
au Wakristo wa Mtakatifu Yohana. Kulikuwa na kundi la Wanosriki waliotenda
matendo ya ubatizo wa kawaida wa kuzamisha majini, huenda kwa mtazamo wa kila
mwaka. Walikuwa wanaelewana na kufanana na Waislamu lakini huenda hawakuwa ni
kundi lililotajwa kwenye Korani (sawa na asemavyo Yusuf Ali n. 76).
Kundi
lingine la Wasabean bandia liliishi karibu na Harran na walisababisha mvuto
mnamo mwaka 820. Walikuwa na nywele ndefu na walivaa nguo za kipekee na huenda
walichukua jina hilo ili wapate faida kwa kuwa Wasabean walitajwa kwenye Korani
na kisha walidhaniwa kuwa walikuwa ni watu wa Kitabu (ibid).
Swali la 14. Ni kweli
kwamba Uislamu na Waislamu ni wenye misemo mipya kwamba watawa wa Kiristo au watawa
wakiume walioghushi msingi wa neno la Kiarabu la "mwislamu"?
Jibu. Neno la Kiarabu la Muislamu ni kisarufi tendaji cha aslama ambacho kwamba nauni tendaji yake
ni Uislamu. Kwa hyo inatokana na lugha
ya Kiarabu yenyewe. Inamaana ya Kustaafu au Kujisalimisha
kwa Mungu na linachukuliana na maana itokanayo na mtindo wake wa kishina.
Mkristo anadhihaki na kujiepusha
hazikuonekana hadi kwenye karne zilizofuatia za Kanisa la Kikristo hata kabla
ya kuanza kwa Uislamu wenyewe. Hivyo ni vigumu kuunda vikundi hivi vilivyopotoka
na kukengeuka.
7: Makhalifa Wanne Viongozi
Swali
la 1. Nimesikia kuwa kuna matawi mbalimbali ya Uislamu, na kama ni hivyo ni
yapi hayo basi?
Jibu.
Matawi
mawili makuu ya Uislamu ni ya Wasunni na Washi’a. Lakini pia kuwa Dini fubo ya
Kisiri ya Wasufi ambao wanaenea ulimwenguni kote. Matawi mengine makubwa ni
Wakarijite, Ahmadiya, na pia vuguvugu la Wakurani.
Maelezo ya kina ya makundi haya na meingine
yanayofanana nayo ni kama vile matawi yafuatayo:
Yanapatirana kwa sehemu tofauti tofauti kwenye:
http://en.wikipedia.org/wiki/Islamic_schools_and_branches
Pia kuna makundi mengine tofauti kama vile Wakurdi
ambao walikuwa wa kabila la Sala u Din au Saladin Mkuu, jemadari wa Kiislamu wa
wakati wa vita vya kidini vijulikanavyo kama Crusades. Pia Waalawi wa Syria ambao
ni tawi dogo lingine ila lenye uthibiti mwingine tofauti wa siasa zake na kundi
la maafisa. Mgongano kati wenye mrengo
wa uhafidhina wa Kiislamu na na wa Mahuru pia ni mkubwa sana.
Swali
la 2. Je, kila kundi la Waislamu hawa wanaamini nini?
Jibu. Maelezo ni
marefu sana kuyaelezea hapa, ila maelezo yanaweza kupatikana kwenye kamusi iitwayo
Kitabu cha Orodha ya Ufafanuzi wa Dini na
Maadili, au Encyclopedia of Religion
and Ethics (ERE) na tovuti mbalimbali za makala za Wikipedia kama zilizo
hapo juu.
Swali
la 3. Je, kuna mgongano wa kiimani kati ya matawi haya na Uislamu?
Jibu. Uislamu umefumbwa kwenye vikundi
mbalimbali vya kidini na vita vyake vya kila mara. Ndilo tatizo lililoko huko
Iraq na kwingineko kote pia.
Swali la 4. Je, unaweza kuelezea
tafadhali Khalifa ni nani? Na pia kwamba ofisi hii na mtu huyu (vyovyote
inavyoweza kuwa) ana kazi gani leo?
Jibu. Huduma ya Khalifa ilikuwa ni mtawala wa
Waislamu. Neno hili linatokana na neno la Kiarabu la Khalifah ambalo maana yake
ni mrithi. Wadhifa huu sasa unatumika kama Khalif. Kamusi ya The Oxford Universal Dictionary inasema
matamshi yenye “a” ndefu na mvuto ni
mbaya.
Ni cheo cha Kiislamu cha utawala wa kidunia na kidini kama mritht wa mtume
Kasim na kiongozi wa “Muhammad.” Mamlaka yake ni ya Ukhalifa.
Makhalifa wanne wa kwanza waliitwa Makhalifa Viongozi Wanne. Baada ya
kipindi kile Uislamu ulionekana kuwa unapungua nguvu yake ya kiteolojia chini
ya uongozi wa Ummayid na Abbasid. Kuna mfululizo wa majarida ya Uislamu kwenye
tovuti ya www.ccg.org na pia kwenye anguko la Yerusalemu
chini ya Omar kwenye jarida la Golgotha: Mahali pa Fuvu la Kichwa (Na.
217). Pia tazama kwenye Imani Fumbo za Siri Kweye Sura ya 5 Uislamuu (Na.
B7_5).
Swali la 5. Je, unaweza kufafanua tafadhali ni
niniJe, unaweza kufafanua tafadhali ni nini maana ya Imamu na mtu anafanyikaje
au alichaguliwaje kuwa Imamu?
Jibu. Kuna maana mbili na matumizi ya neno hili la Imamu. Cheo chenyewe
kinamaanisha kwenda mbele ya au kutangulia lilitumika kama kumweka
kuhani kwenye Msikiti wa Waislamu.
Pia
lilitumika kama jina la cheo walilopewa viongozi mbalimbali na watemi wa
Kiislamu wakiwemo na Makhalifa au wafalme wanaojitegemea. Somo la kawaida nida
na kukubalika kwa jamii ya Kiislamu ni muhimu na kunahitajika.
8: Paradiso
Swali la 1. Kwanini imani hii wanadai kuwa wanakwenda
moja kwa moja mbinguni wakiwa pamoja na wanawali wazuri 70 wakimtumikia mmoja
wao na kumhudumia mahitaji yake yote (licha ya kwampa kuna wengi ambao hawakubaliani nao kuwa inawezekana), kuna mashiko yoyote kwa Mungu na
kwenye Maandiko Matakatifu au kwenye Kur’ani?
Jibu. Jibu ni kwamba hakuna na wala hakuna
fundisho kama hilo kwenye imani au kwenye Kurani na hao wanaofundisha hivyo ni
waongo na watakabiliwa na hukumu ya manabii nay a wateule kwenye ufufuo wa pili
wa wafu.
Kwenye Sura ya 2, ya Ng’ombe, kwenye
aya za 111-113, Korani inasema hivi:
“Na walisema: Hataingia
Peponi ila aliyekuwa Yahudi au Mkristo. Hayo ni matamanio yao. Sema: Leteni
ushahidi wenu kama nyinyi ni wasema kweli. Sivyo hivyo! Yeyote anaye elekeza
uso wake kwa Mwenyezi Mungu naye ni mtenda mema, basi ana malipo yake kwa Mola
wake Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika. Na Mayahudi
husema: Wakristo hawana lao jambo. Na Wakristo husema: Mayahudi hawana lao
jambo. Na ilhali wote wanasoma Kitabu hicho hicho (Biblia). Na kadhaalika
walisema wale wasio jua kitu mfano wa kauli yao hii. Basi Mwenyezi Mungu
atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyo kuwa wakikhitilafiana..”
Kwa hiyo, Korani iko wazi kwamba
Ufufuo wa wafu utakuwapo na utawahusu wote
wenye mwili na sio Wakristo au Wayahudi peke yao, au kwa wale wanaoitwa
“Waislamu” peke yao.”
Biblia na
Korani vinasema tu kwamba ufufuo wa wafu utafanyika kwa watu kuwa kwenye
Bustani ya Paradiso, kama inavyoitwa kwenye Korani, na kwenye hukumu. Hakuna
anayekwenda mbinguni au motoni baada ya kufa. Hakuna kitu kama hicho cha
mbinguni na motoni kwenye Biblia wala kwenye Kur’ani (soma majarida ya Roho (Na. 92) na pia Ufufuo wa Wafu Na. 143)).
Swali la 2. Linatoka
wapi basi wazo hili la watu kudhani kwamba tutaungana pamoja na hata kwa namna
fulani inakubalika kuwa watakuwepo mahali fulani mbinguni ambako watapewa
wanawali wazuri, warembo na weledi wa kuwahudumia kila mahitaji yao?
Jibu. Kwa kweli, wale wanaodhani kuwa ni wafia-dini na mashahidi wa imani na
kwamba watakwenda moja kwa moja mbinguni na kupewa wanawali warembo na weledi
70 wanaosubiria kuhudumia huko mbinguni hawakuyapata mafundisho hayo kutoka
kwenye Korani, kwa kuwa haisemi kitu kama hicho kabisa.
Kama
unasema wewe ni Mkristo, au Myahudi, au Muislamu, na huujui ukweli kuhusu
Ufufuo wa wafu, na Utawala wa Masihi, basi huitendei haki Torati na Ushuhuda wa
Manabii na imani ya Yesu Kristo na hakuna nuru ndani yako (Isaya 8:20). Korani na
Biblia hazitofautiani kwenye fundisho hili. Na wala hazitofautiani kwa kuwa Korani
na Biblia hazitofautiani. vinginevyo basi, Korani ingekuwa ni maandiko ya
uwongo ya nabii wa uwongo.
Kristo alisema
kwamba malaika mbinguni hawaoi wala kuolewa. Kristo alisema: “Kwa
maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika
walioko mbinguni.” (Marko
12:25).
Swali la 3. Agano Jipya linatuambia kuhusu Mbingu
ya tatu ambako ndiko iliko Paradiso, na Korani inaonyesha Mbingu ya saba. Je
mtume aliipata wapi mbingu hii?
Jibu. Majina haya
yanafanana kimuktadha. Neno lililo kwenye Agano Jipya linataja uchambuzi wa
kimadaraja wa msingi wa Kimazingira, Kisola na mfumo wa Kigalaktia ya Dunia na
muundo wa kimbingu wa Kiti cha Enzi cha Mungu kwa “pande za Kaskazini”.
Madaraja haya saba ya Korani mi mwendelezo wa haya yanayofanya tofauti kati ya
mwenendo wa Hali ya hewa, kwa upande wa ndani na wa nje ya anga, mfumo wa Jua
au Sola, kundi la Vitu vilivyoko Angani na kadhalika.
9: Sharia
Swali la 1. Ni kwa msingi na sababu zipi hii Sharia ilianzishwa? Chanzo chake kilitokana
na maagizo ya Korani au ni kwenye hizi Hadithi, au mahali pengine?
Jibu. Sharia zinatokana
na Hadithi na hazina misingi kwenye Biblia wala kwenye Korani. Ni mafundisho ya
kizushi tu haya.
Swali la 2. Je,
Uislamu unaruhusu ndoa za matala? Watu wengi wanaitumia aya ya 3 ya kwenye Sura
ya 4 kudai kwamba unaruhusu, lakini hivyo ndivyo hasa andiko hili linavyosema?
Jibu. Ndoa za wake wengi au matala ziko mbali na nadharia, lakini kama zipo leo
kwenye jamii zetu kunahitaji utaratibu au sheria. Na ndiyo maana Mohammad aliruhusu
kwa kulinganisha na sheria za Mungu alizopewa nabii Musa (soma jarida la Ndoa za Matala
Kwenye Biblia na Kwenye Korani (Na. 293).
Swali la 3. Je, kuna vifungu vyovyote kwenye Kur’an
vinavyofundisha utoaji wa zaka, na kama ndiyo, hii haionyeshi kuwa wale
walioiandika Kur’an kwa kweli walitoa zaka?
Jibu. Mungu alisema
kwa kupitia nabii Malaki kwamba utoaji wa Zaka ni ishara ya toba ya mwanadamu na ni jaribio
la kumrudia Mungu (Malaki 3:6-18). Kumbuka
kuwa Zaka ni msingi wa ishara wa kumrudia Mungu, kwa mujibu wa Sura
hizi za 2:43,83; 4:162; 5:12,55; 9:11; 19:31,55; 21:73; 27:3; 98:5 nk. Kwa hiyo
basi mtume ameungana na fundisho la Kanisa kuhusu kutoa na kutunza zaka.
Mafundisho sahihi kuhusu utoaji wa zaka yameelezwa kwenye jarida la Utoaji wa Zaka (Na.
161).
Swali la
4. Waislamu wanadai kuwa unywaji wa pombe uekatazwa kwene Kur'an? Je, ni unywaji au ulevi ndio uliokatazwa?
Jibu.
Mlevi
hatauingia Ufalme wa Mungu kwa sababu ya kukosa kwake kujitawala. Kiasi
kinatakiwa – na sio kujinima kunywa (tazama ilivyoandikwa kwenye. Sura za 16:67; 2:219; 10:91 na kwenye jarida la Mvinyo Kwenye Biblia [188]). Kunywa kileo kwa kiasi ni vizuri na
hakuna kosa. Kama una matatizo na kileo, basi jifunze kujitawala.
10: Kalenda
ya Kiislamu
Swali la 1. Waislamu huifuata kalenda ya mwandamo wa
mwezi, lakini mbona hahesabu miezi kutoka wakati wa mpito wa mwezi kutoonekana
badala ya siku ya kuandama mwezi mchanga?
Jibu. Fuqaim, inayodaiwa na Kinana kwenye kipindi cha kabla ya nyakati za Hadithi waliwajibika
kwenye mambo ya kalenda huko Ishmaeli kama Walawi na Isakari walivyofanya
katika Israeli. Mwanzoni mwa Uislamu, wana wa Israeli na wa Ishmaeli waliadhimisha
pamoja siku takatifu kwa siku moja na zinazofanana. Kalenda iliamriwa kisahihi
kwa kipindi cha miaka na miaka kilichofuata, kwa kipindi cha millennia, hadi
fundisho la kutukuza mwezi mchanga lilipoingizwa kutoka kwenye upagani na imani
za Kibabeloni. Waarabu waliifuata imani halisi hadi kwene nakati za mtume.
Mara tu baada ya kufa kwake mtume, mafundisho yake
yaligeuzwa na kuposhwa na
kalenda ilipotoshwa pia. Chini na baada ya kipindi cha Khalifa Omar II
(717-720) kile kilichojulikana kama Hadithi kilianza kuandikwa. Vivyohivyo
kutoka baada ya kufa kwake Kasim mwaka 632 maneno yasiyokubalika na “wa
Muhammad” waliachana na kukataa kuyaandika au kutungwa kwa sababu nzuri.
Hadithi zimeivunja kalenda ya Kiislamu kutokana na tafsiri ya Sura na kwa karne
kadhaa imani hii potofu iliuharibu na kuupotosha Uislamu na kupotosha aina zote
za uhusiano au mapatano fananishi ya imani zote kuu tatu.
Uislamu umefanya upotoshaji au ubatilishaji mkubwa wa
Kalenda ya Mungu kwa kuyatumia vibaya maneno ya unabii na kuiweka vingine kalenda
kutoka majira yake hadi mavuno yaliyoelezwa kwenye Biblia. Kwa hiyo, mpango wa
wokovu umepotoshwa na kufanywa kupuuzwa na Waarabu wanaodai kuwa wanamfuata
Mungu na imani ya Kiislamu kama ilivyofunuliwa kwa Ibrahimu, Musa, Haruni,
manabii, Kristo na Kanisa, ambalo ndilo Muhammad wa kweli wa kwenye
mandiko.
Swali la 2. Kwenye imani za
Kikristo na Kiyahudi kuna miezi mitakatifu. Je Uislamu una miezi yake wenyewe
mitakatifu?
Jibu. Miezi Minne Mitakatifu ya Kiislamu ni Rajab, Sha’aban,
Ramadhan na Muharram. Mwanzoni ilikuwa ni mine hiihii sawa tu na ile iliyo
kwenye dini ya Kiyahudi na kwenye Biblia na ya Waisraeli wa Zamani. Miezi Minne
Mitakatifu ya Imani ni Abibu, Iyari na Siwani ikiwa kama miezi mitatu ya
kwanza, na Ethanimu au Tishri ukiwa ni mwezi wa Saba kwa mujibu wa Biblia na
ndiyo ilikuwepo kwenye Korani pia, lakini haikupewa majina yake, kwa hiyo
Hadithi zikaiondolea maana na umuhimu wake pia. Hizi Hadithi hazina uhusiano
wowote na Uislamu, ni kama Talmud zisivyo na uhusiano wowote na imani ya
Kiyahudi.
Kalenda ya
Kanisa la Mungu huko Uarabuni liliharibiwa na hizi Hadithi na Waarabu wapagani
baada ya kufa kwa Makhalifa Viongozi Waanzilishi na Mwezi Mchanga havikuingizwa
kwenye Uislamu na kanuni zake kwa kipindi cha takriban miaka elfu moja baada ya
uanzishwaji wa imani kule.
Tunajua kwa ukweli kwamba mtume na kanisa walifunga
saumu kwa mujibu wa Mwandamo wa Mwezi Mpya kama ilivyokubalika na Kalenda ya
Hekalu na tunajua kuwa kipindi cha mpito cha mwezi mwingine Kuandama kilichukuliwa
kama Mwandamo wa Mwezi Mpya kwa mujibu sawa na maelekezo ya huko Maka
iliyofanywa baada ya kuanzishwa kwa Uislamu (soma jarida la Jinsi Zinavyofanana Kalenda ya Kiebrania na ya Kiislamu (Na. 053)).
Swali la 3. Je, Korani
inatetea maadhimisho ya siku ya 7 ya Sabato?
Jibu. Waislamu wa zamani
au wa mwanzoni chini ya Waarabu waliichukulia wiki kwa kuilinganisha na hesabu
za Wayahudi na Wakristo. Majina ya wiki yalitokana na majina ya Wayahudi na
Wakristo wa Kwanza kama vile al Jumaah, ambayo maana yake ni mkutano au kusanyiko la
ibada, na siku inayofuatia au siku ya saba ya juma iliitwa as- Sabt, yaani Sabato, ambayo kwayo,
ibada zilifanyika kuuabudu Mungu tangu siku za manabii na Kasim mwenyewe
alifanya maombi mara mbili msikitini na kuacha au kusimamisha shughuli zote za
biashara. Siku ilianzia baada ya jua kuzama hadi kuzama tena wakati ambapo hata
rangi huwezi kuitofautisha kuweza kuingiza uzi kwenye sindano. Jambo hili
halijabadilika kabisa tangu siku hizi za zamani na inakubalika na imani zote za
Kiyahudi za zamani.
Wakati Waislamu wanapitwa kwenye maombi au sala za
Ijumaa, wanafanya haraka kwenda kumkumbuka Allah na wanaacha kufanya biashara (soma
Sura ya 62 Juma’ah (Makutano)). Hii inaonyesha ukwel wa kwamba
kwene majira ya alasiri ya Ijumaa shughuli zote za biashara zilisimama na watu
walijiandaa kwa Sabato. Udanyanyifu mkubwa wa Waislamu waliofuata baadae
waliielekeza sala hii majira ya alasiri ya siku ya sita peke yake, na
wakaachana na Sabatoa wakaachana na Sabato. Ukristo mamboleo ulipokuja nao,
uliiruka Sabato hii ya siku ya saba na wakaifanya siku ya kwanza ya juma
(ijulikanayo kama Jumapili) kuwa ndiyo Sabato yao, kitendo alichokifanya Zoroaster
huko Uajemi tangu karne ya tisa KK.
Sabato iliwekwa kwa ajili ya maendeleo ya kiroho kwa kupitia
kitendo cha kiitii amri ya Mungu na kwa njia ya kutafakari, kusali, kusikia, na
kusima vitabu vitakatifu na kuabudu. Kitendi cha kushindwa kuinenyekeza kwa
Mungu na kuzikataa Baraka zilizofunuliwa za Sabato ni sawa na kujiita tumbili.
Ambavyo ni kujifanya mwenyewe kuwa hufai na hustahili na huna adabu wala utii
kama mchezo na usiye na uelewa wowote wa mambo ya kiroho.
Muhammad aliamuru
kuzishika Sabato na alisema kuwa yeyote asiyeishika anafanana na nyani. Ni sawa
tu kama Wakristo na Mitume, wote walio umma wa Al Islam tangu Adamu hadi Kristo
waliishika Sabato. Bali wale waliouamini uwongo waliiacha na walibadilisha siku
ya kuabudu iliyoamriwa na kuiweka Jumapili. Hawakuishia hapo tu, bali pia waliitukuza
Easter kwa kuuabudu Mungumke wa zamani aliyewasababisha Israeli na Waarabu na
wana wa Ketura wajikwae na kumchukiza Mungu wao. Kwa jinsi hiyohiyo, maombi ya
siku ya Jumaa yakapangiwa yafanyike siku ya Ijumaa na Sabato ikasahauliwa
kwenye Uislamu.soma jarida Sala ya Ijuma'aa ni Maandalizi ya Sabato (Na. 285).
Kudhania
kwamba Ishmaeli alikuwa na kalenda yake ya tofauti na ya wa Israeli na baadae
ya Wayahudi na Wakristo ni kupotoka kukubwa. Wiki imepangiliwa kwa kuiangalia
Sabato na ilibakia na iliendelea kudumu hivyo., ikiwa imesisitizwa hata na
Manabii kuwa itunzwe na kuheshimiwa (soma jarida la Sabato
Ndani ya Kur'an (Na. 274)).
Swali la 4. Kwa nini basi Waislamu wa sasa hawaishiki
Sabato?
Jibu. Uislamu uliharibiwa na kupotoshwa na ushawishi
wa dini za kale za asili au jadi ya kimashariki na wapagani waliuharibu kabisa.
Dini hizi za jadi na za Kimafumbo zilianzisha Hadithi ili kuipotosha kabisa
Kur’an kama Wayahudi walivyoanzisha Talmud ili kuipotosha na kuitokomeza
Torati. Hata nembo au alama ya Waislamu wa Sasa ya mwezi mchanga wenye nyota ndestroy
the Torah. Evi nembo au alama ya dini ya mungumke aitwae Istar au Easter. Hakuna
hata moja kati ya dini hizi kubwa inayofuata maagizo ya Torati, Manabii au
Kanisa.
11: Ibrahimu
Swali la 1. Dini ya
Ibrahimu ilikuwa ipi? Je, alikuwa
Myahudi, Mkristo au Mwislamu?
Jibu. Kuna dini moja tu na imani moja
na mtindo mmoja wa kuabudu kutoka kwa Mababa wa zamani hadi kwa Musa na Kristo
na Kasim na wazee wa “Muhammad”
na hadi kufikia kwenye zama za Kanisa la Mungu hadi kipindi hiki.
Unyenyekevu na Torati ya Mungu vilitolewa na
akapewa Ibrahimu na Isaka, nabii wa haki na kwa njia ya mstari wake
(Sura ya 37:83-113). Kizazi cha Ibrahimu kilipaswa wawe na kazi kubwa katika
siku zijazo ulimwenguni na kwa kupitia wao, ulimwengu ungepata sifa kubwa.
Swali la 2. Ni nani
basi “mtoto wa pekee” wa Ibrahimu? Waislamu wanasema kuwa ni Ishmaeli, mwanae
wa kwanza na sio Isaka.
Jibu. Kutoelewana kuliko kwenye Korani kuhusu sadaka aliyotolewa Isaka
kueelezewa vizuri kwenye jarida la Mwanzo 22, Imani za Kiyahudi, Uislamu na Sadaka ya
Isaka (Na. 244). Ni Isaka ndiye aliyetajwa kuwa ni dhabihu iliyokusudiwa na sio Ishmaeli
kama inavyofundichwa kwenye Hadithi. Dhaana iliyopo kuhusu kifungu kihusucho utaratibu
wa ibada kinasababisha mkanganyo huu usiwe sawia, hata hivyo, haisemi kuwa ni Ishmaeli
moja kwa moja kwene maandiko ila zaidi tu ni mafundisho ya Hadithi tu
Swali la 3. Je,
ni kweli kwamba Ibrahimu alikuwa ni baba wa Waabudu Mungu mmoja yaani wa Monotheism?
Jibu. Hapana. Adamu ndiye aliuwa
Baba wa Umonotheism na mababa wote wa imani na manabii walikuwa Wamonotheists.
Swali la 4. Kur’an
inasema kuwa Ibrahimu alikuwa rafiki wa Allah. Kwa nini ilikuwa hivyo?
Jibu. Sababu zake zote zinapatikana kwene
Maandiko Matakatifu na ufafanuzi wake unaonyesha moja kwa moja kwenye maandiko
yaliyoko kwene Maandiko Matakatifu. Sababu zake pia zimeelezwa kwenye maandiko
yaliyo kwenye jarida la Kwanini Ibrahimu Aliitwa “Rafiki wa Mungu"? (Na. 35).
Swali la 5. Yapi ni Maandiko Matakatifu ya Ibrahimu?
Jibu. Kwa kweli ni Dini ya Ibrahimu
na sio Maandiko Matakatifu. Ibrahimu aliruzukiwa imani na akaitwa kutoka Uru ya
Wakaldayo. Ni kwa sifa yake hii njema ndipo aliwapa uzao wake.
Swali la 6. Kwa mujbu Sura
ya 2:130, je, Ibrahimu alikuwa ni mmoja wa wateule?
Jibu. Sura hii na aya yake
vinathibitisha kuwa aliitwa na Mungu na kupewa imani na ilikuwa kwa hii imani
yake ndipo aliwapa uzao wake. Hii ilikuwa ni imani ya Mnyenyekevu au Al Islam kwa
Kiarabu. Aya ya 130 inasema atakuwa kama mtamba kama mmoja wa Wenyehaki na
watakatifu, hivyo basi alikuwa ni mmoja wa wateule. Maandiko ya Kiebrania ya
kitabu cha Mwanzo yanasema kwamba Wamataifa walimjua kama mfalme wao elohim na
hivyo, ni mwana wa Mungu. Tafsiri ya Kiingereza haitafsiri hii kiusahihi sana.
Swali la 7. Ni jinsi gani ambayo Ibrahimu amekuwa ni mfano wa kuigwa, kwa mujibu wa Sura ya 60:4?
Jibu. Kwa mujibu wa aya hii,
Ibrahimu na walw alionao ni mfano wa imani na tofauti iliyopo kati ya imani na
kutokuwa na uadilifu, isipokuwa ule alioufanya Ibrahimu, wakati alipowaombea
wasamehewe.
Swali la 8. Je, neno
la Kiarabu la hanif linamaana
gani?
Jibu. Hanif ni mtu anayeenenda kikamilifu kwenye imani ya Mungu mmoja ya
nabii Ibrahamu. Kwa maneno mengine, ni Kanisa la Mungu na manabii na mababa wa
imani ni Hanif wa “Muhammad,” ambaye ni mwili wa Kristo.
Kumbuka kuwa wengi wa hawa Hanifs walikuwa ni
Wakristo marafiki au hata wapinzani wa Uislamu. Umuhimu uliendelezwa na mtu
mwenyewe kwenye Imani ya Ibrahimu. Ulipokuwa unaangula Uislamu baada ya kufa
kwa hawa Makhalifa Wanne Waanzilishi, baadhi ya hawa Hanif walilazimika kupinga
vile uislamu ulivyokuwa unaelekea kuwa. Wengine walijulikana kama Wakristo
washika Sabato na wengine ni kama wapinzani tu wa Uislamu. http://en.wikipedia.org/wiki/Hanif
12: Unabii wa Kur’an
Swali la 1. Kur’an
inasemaje kuhusu unabii au kuhusu manabii?
Jibu. Korani ina mengi
ya kusema kuhusu manabii kwenye Sura za 2:61, 91, 136, 177, 213; 3:21, 80nk.
Uvuvio wake umeelezewa kwenye 4:163 na 6:86nk. Kuna adui
kila pamoja (6:113). Mungu amefanya agano na kila mmoja wao (33:7). Nyingi ya nabii
zilizo kwenye Kurani ni marudio tu wa maelezo yahusuyo mpango wa Wokovu kwene
Maandiko Matakatifu hasahasa kuhusu Bustani ya Paradiso (sawa na Sura za 2; 7;
13; 15; 18; 19; 22; 25; 36; 37; 38; 43; 44; 47; 52; 55; 56 na 76). Kwakuwa
Maimamu hawasomi Maandiko Matakatifu wanakosa kujua kipindi kilichokusudiwa
kati ya kile cha Bustani za Kwanza na Ufufuo wa Pili wa Wafu.
13: Waarabu
Swali la 1. Unweza kuelezea kahudhui ya imani ya Waarabu
kabla ya kuibuka kwa Uislamu katikati ya Waarabu?
Jibu. Waarabu walikuwa na
imani mchanganyiko ambazo zilikuwa nusunusu kati ya Ukristo, Upagani na dini ya
Kiyahudi. Ukristo ndio ilikuwa aina mpya uliotokana na Usabato wa mrengo wa
Kiyunitari, ambao kwao Kasimu alikuwa mmoja wapo wa Watrinitariani na pia wa
mrengo wa Nestorianism. Imani ya kipagani kwa kweli ilikuwa ni ya waabudu mungu
Mwezi aliyeitwa Sin na Shams au Shamas mshirika wake wa kike na mungu Juan a
Nyota ya Asubuhi yaani Istar, au Easter, Mungumke ambaye imani ya Kiyahudi ya
Uarabuni walikuwa wanamuabudu mapema sana hata kabla ya kukengeushwa na Imani
fumbo za Kitalmudi.
14. Taqiyya
Swali la 1. Waislamu wanafundisha kuwa si vibaya
kusema uwongo kuwadangana wengine ili kuwavuta kwenye imani au ili kujipatia
faida. Wazo hili limetokea wapi na limetokana na nini?
Jibu. Tendo hili linaitwa Taqiyya. Linatokana na kuitafsiri vibaya au kuipotosha
Korani kwenye Sura ya 3:28 na 16:106.
Waumini wasiwafanye
makafiri kuwa wapenzi wao badala ya Waumini. Na anaye fanya hivyo, basi
hatakuwa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Ila ikiwa kwa ajili ya kujilinda na
shari zao. Na Mwenyezi Mungu anakuhadharisheni naye. Na marejeo ni kwa Mwenyezi
Mungu. (sawa na alivyoandika Yussuf Ali na 373).
Waislamu
hata wanadanganyana wenyewe kwa wenyewe kwa masuala la mitazamo yao na uhusiano.
Kwenye maeneo mengine ni vigumu kujua wepi ni Sunni na wepi ni Shia ni wengi (hasahasa
Shia) wanajivunia tabaka lao na wanajitambulisha kama Sunni wawapo kwa wa Sunni
au Shia wanakothibiti maeneo na fundisho hili la Taqiyya.
Mtazamo huu
ni tofauti kabisa na yasemavyo Maandiko Matakatifu na Korani. Mtazamo ni upotoshaji wa Korani na ni
uvunjifu wa moja kwa moja Amri ya Tisa ya Mungu. Sura ya 16:106 inawalaumu walio
kwenye mateso au vitisho (sawa na Yussuf Ali n. 2145 re ‘Ammar bin Yasir). http://en.wikipedia.org/wiki/Taqiyya
q