Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[072]

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Wongofu na Kweli

(Toleo La  2.0 19941015-19980725-20090606)

 

Dhana ya uwongofu ukiwa kama mchakato wa kugeuka kutoka maovuni na upotofu inaonekana kuwa ni fundisho la muhimu na la msingi kwa Kristo.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1994, 1998, 2009 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Wongofu na Kweli



Dhana ya wongofu imechukuliwa kutoka kwenye ile ya kugeuka kutoka kwenye makosa, na kuisikiliza kweli, na kuelewa kutoka moyoni.

 

Isaya 6:10 Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.

 

Isaya 6:10 Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.

 

Dhana hii imenenwa tena na Kristo.

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.

 

Marko 4:12 ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa.

 

Kweli ile inayoendelea kutoka kwa Mungu ikiwa kama jambo muhimu ya kazi na matendo ya mwanadamu kwa kuzivunja sheria na matendo ya dhambi.

Zaburi 19:7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, Huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa Bwana ni amini, Humtia mjinga hekima.

 

Huu ni mwanzo wa dhana ambayo kwenye Agano Jipya ni msingi nay a muhimu kwa wokovu. La muhimu sana ni kwamba inahitaji matendo kwa mtu kuweka msingi wake kwenye kweli iliyofunuliwa ya Mungu. Mungu pia anaweka hilo wazi sana au kuwa dhahiri kwamba mchakato inathibitiwa. Watu walikuja kwa Mungu wakitegemea uwezo wao wa kufanya kwa mujibu wa kweli yake na kuifanya iwe lazima na muhimu kwa maisha yao.

 

Uhuhimu wa kweli hii umeendelezwa na Yakobo.

Yakobo 5:19-20 Ndugu zangu, ikiwa mtu wa kwenu amepotelea mbali na kweli, na mtu mwingine akamrejeza; 20 jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi.

 

Neno linalotumika kumaanisha wongofu kwenye lugha ya Kiyunani ni epistrepho(SGD 1994), ambalo maana yake ni kujirudi au kurudi tena. Neno hili linatumika kama neno kiini au chimbuko kwenye Matendo 15:3 linalohusu wongofu wa Mataifa ambao ni epistrophe (SGD 1995) lenye maana ya kurejea au kujirudi kwa maana ya mageuzi ya Wamataifa ing.

Matendo 15:3 Basi, wakisafirishwa na kanisa, wakapita kati ya nchi ya Foinike na Samaria, wakitangaza habari za kuongoka kwao Mataifa; wakawafurahisha ndugu sana.

 

Mchakato huu unatumika kwa neno la Kiebrania kwenye Isaya, ambalo ni shoob (SHD 7725). Hili ni shina la msingi lenye maana ya: kugeuka na kurudi nyuma. Kwa hiyo kweli ni lazima ipewe mara moja kwa mataifa yote ili kwamba waweze kurejea kwenye kweli.

 

Uanzishaji huu kwenye kweli ulitokea chini Nuhu na uanzishaji pya tena wa ulimwengu usio na uharibifu. Somo la msingi na la maana ni kwamba watu hawataki kuijua kweli au kuufanyia kazi au kulazimishwa kwenye kweli. Ndiyo maana dhana na watu ni kiunyume na hawahesabiki. Hakuna kitu kilichoelezewa kiusahihi kwenye mawazo ya mtu aliyeongoka. Mchakato wa kumshambulia mtu zaidi sana kuliko kutathimini kile kilichosemwa ni muhimu kwenye nia na mawazo ya mtu asiyeongoka.

 

Yuda 9 Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.

 

Namna hii ya fikra imefanyiwa mkazo kwene Makanisa ya Mungu na muhimu kwa mchakato ya kutawala nia na mawazo ya watu yaliyoendelezwa na dini za uwongo kwa kipindi kirefu.

 

Uwezo wa kuweka kikomo mbali na programu hii umesaidiwa na Mungu kwenye mchakato wa wito ambao unahusisha na shurutisho kwa msingi wenye mashiko wa ukweli, ni kama inavyodhihirika kwa mwongofu au kwenye moyo wa mwongofu. Moyo ule usiopenda kuelewa na kutenda sawasawa na kweli ya Mungu ni ya mtu asiyeongoka na asiyehitaji kuongoka. Mafundisho ya kweli ya Mungu na makosa ya uvunjaji wa sheria na amri za Mungu ni sehemu ya mchakato.

 

Zaburi 51:13 Nitawafundisha wakosaji njia zako, Na wenye dhambi watarejea kwako.

 

Zaburi 51:13 Nitawafundisha wakosaji njia zako, Na wenye dhambi watarejea kwako.

 

Mchakato wa wongofu ni wa muhimu, mchakato wa kurejesha vitu vyote kwa Mungu. Kumrudia Mungu ni mchakato wa kuwa sawa na mtoto mdogo.

 

Mathayo 18:3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

 

Neno “mwongofu” lililo hapa ni strepho (SGD 4762) ambalo maana yake ni: (kutiwa nguvu kwa) kutikiswa. Hivyo ina maana ya kuongoka kwa kugeuka nyuma.

 

Kuwa kama mtoto hakuna maana kubadilika hata uwezo wa kufikiri. Watoto wadogo wanajulikana kwa mambo mawili. La kwanza ni maswali ya kidadisi yasiyokoma. Swali la “Kwanini” linarudiwarudiwa sana kuulizwa watati wa utoto kuliko kipindi chochote kile kingine. Jambo la pili ni uwezo au kiwango cha kuamini au imani kwenye kweli za kile kilichopo kwenye wakati ule. Kwa hiyo, imani ni ufunuo wa Mungu kwenye Biblia sehemu kuhimu sana ya kuelewa. Hii haiwezi kutokea kwa kukubalika kusikoweza kuonewa mashaka kwa kile wanadamu wanachosema kuwa Biblia inasema, lakini, zaidi sana, kile ambacho kwa hakika inasema. Mchakato wa kuifundisha kweli unaenda kwenye tafsiri pia.

 

Mchakato wa wongofu unahitaji toba kama ilivyoelezwa huko mwanzoni.

Matendo 3:19 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

 

Wakati wa kuburudika ni mchakato wa kuwaita wateule na kisha marejesho na matengenezo mapya ya hii sayari. Kwa hiyo mchakato huu ni moja wapo ya kuielewa dhambi na ndipo imetolewa fursa ya kutubu. Wongofu ni mchakato ambao unahitaji mtu kujirudi kutoka kwenye makosa na dhambi. Hakuna mtu atakayebakia kwenye makosa na dhambini na akadai kuwa ameongoka. Nia ya kubadilika na kuishinda dhambi inawezeshwa na Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, haiwezekani kuuishinda ulimwengu pasipo uweza wa Roho Mtakatifu. Vita vilivyoko ni vita vya kiroho na mwanadamu hanabudi kuwa chini ya bwana mmoja au kwa yule mwingine. Wanadamu hawawezi kuuepuka mchakato huu; watapaswa ama wamtumikie Mungu au kutumikia Malaika muasi. Ili kumtumikia Mngu mtu atalazimika kuongozwa na kweli.

2Yohana 1-4 Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli; 2 kwa ajili ya hiyo kweli ikaayo ndani yetu, nayo itakuwa pamoja nasi hata milele. 3 Neema, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo. 4 Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba.

 

2Wathesalonike 2:10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa. 11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo; 12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu

 

Kama tutazifuata dhambi na uwongo, tutapewa nguvu zaidi za udanyanyifu. Inatupasa ama kuwa waangalifu na kuipenda kweli au tusifanye hivyo. Kama hatufanyi hivyo, basi tutapewa nguvu za kutenda dhambi zaidi na na kuendelea kutenda dhambi na makosa zaidi.

 

Kuipenda kweli ni alama ya mteule aliye na Roho ya kweli.

 

Yohana 14:17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.

 

Yohana 15:26 Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia.

 

Kwa hiyo kweli huendelea kutoka kwa Baba kupitia Roho Mtakatifu, na inapaswa iendane na haki na utakatifu.

Warumi 1:18 Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.

 

Iwapo kama mteule mmoja anaijua kweli na akawa haihubiri kwa watu – yaani anaificha kweli – hasira ya Mungu itamwagwa kutoka mbinguni kwa ajili yake. Hii ndiyo sababu wateule, kama watendakazi wazijuao siri za Mungu, wanahukumiwa kutokana nay ale wanayoyajua na kuyatenda. Mteule hawezi kubakia kimya au azinyamazie na kuvumilia dhambi. Inawapasa wanene na kutenda.

 

Viuno vya mteule ni kipimo kwa ajili ya kweli.

Waefeso 6:14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

 

Ukweli ni kwamba ni muhimu kuzijua silaha za Mungu. Pasipo kweli hatuwezi kufana lolote kwa kuwa tutaongozwa nayo na kuwaongoza wengine kwenye uwongo (soma jarida la Kweli (Na. 168)).

 

2Timotheo 2:15-25 Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli. 16 Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu, 17 na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto, 18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha. 19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu. 20 Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. 21 Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema. 22 Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi. 23 Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi. 24 Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; 25 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli;

 

Maagizo yaliyo kwenye 2Timotheo ni muongozo wetu sote. Ukweli ni malengo yetu na maazimio yetu. Kweli ni kile kitendo cha kuutafuta utakatifu.

Tito 1:1 Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo; kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu, na ujuzi wa kweli ile iletayo utauwa;

 

Kweli itakuwa ni alama ya marejesho mapya.

Isaya 65:16 Hata itakuwa yeye atakayejibariki duniani, atajibariki kwa Mungu wa kweli; naye atakayeapa duniani, ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za kwanza zimesahauliwa, na kwa kuwa zimefichwa machoni pangu.

 

Hakuna mtu anayeweza kuutoa uwezo wake wa kiakili na kumpa mwingine. Wanahukumiwa na kweli na jinsi wanavyokenenda katika kweli. Kwa hiyo hakuna Kanisa linaloweza kunena na kumuelekeza mtu kinyume na kweli ya Mungu. Kama fundisho lolote la mtu litakuwa kinyume na Maandiko Matakatifu, ndipo yeyote yeyote anayeyafuata mafundisho yale atatoa hesabu mbele za Mungu. Kwa hiyo, kuielewa Biblia na kumjua yeye Mungu wa Pekee wa Kweli na Mwanae, Masihi, ni muhimu kwa kuupata na kuhesabiwa kwenye uzima wa milele (Yohana 17:3). Kwa hiyo hakuna Kanisa la Waamini Utatu litakalokuwa kwenye ufufuo wa kwanza kwa kuwa wanapinga mafundisho kwa uwepo wao na kuendekeza uwongo kwa kimyakimya. Wanawajibika kwa Mungu na wameondolewa kwenye ufufuo wa pili ili kwamba maisha yao yaokolewe kwenye ufufuo wa pili, kama alivyokuwa yule mzinzi kwenye kanisa la Korintho.

1Wakorintho 5:4-5 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu; 5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.

 

Waebrania 10:26-27 Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; 27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.

Uasi wa makusudi dhidi ya kweli ndiyo dhambi ya makusudi inayotajwa hapa kwenye Waebrania. Kwa hiyo, ufufuo wa pili wa wafu ndiyo njia pekee ambayo kwayo watu hawa wanaweza kuokolewa kwayo. Kisha watahukumiwa na kuadibishwa mbali na uwongo na kwa Yule Malaika muasi, kwa kuwa hawakuweza kutofautisha kwa kuipambanua kweli na uwongo kwenye mazingira ambayo yanatupeleka hukumuni. Tunahukumiwa kwa uwezo tuliopewa wa kupambanua kati ya kweli na uwongo sasa na kuenenda kwa mujibu wa uelewa wetu ule. Kama hatutaenenda ndipo tutaingia hukumuni kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Kwa maneno mengine, tunaondolewa kutoka kwenye mchakato sasa na kutolewa kwa mungu wa dunia hii ili kwamba mjaribu na mfanya maudhi aweze kuokolewa katika siku za mwisho.

 

Ni kweli tu ndiyo inaweza kutuweka huru. wateule wanaijua na kweli inawaweka huru (Yohana 8:32). Kila mtu anapaswa kuenenda kwa uelewa. Inawapasa kutubu ili kwamba dhambi zao ziweze kufutwa (Matendo 3:19).

 

Mchakato wa kuwatenga wateule kwa mujibu wa kweli, ya muhimu, unapasa mgawanyo wa wateule.

1Yohana 2:17-27 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele. 18 Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. 19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu. 20 Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote. 21 Sikuwaandikia ninyi kwa sababu hamwijui iliyo kweli, bali kwa sababu mwaijua, tena kwamba hapana uongo wo wote utokao katika hiyo kweli. 22 Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. 23 Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia. 24 Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba. 25 Na hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele. 26 Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27 Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.

 

Mchakato wa kutoka nje kwa wateule haumaanishi kwamba wateule wanastahili kwenye utaratibu shirikishi—hawapo hivyo. Wateule wanatakiwa kujitenga wenyewe na wale wasioipenda kweli. Wale wasioongozwa na kweli hawaipendi kweli. Tunawajua wateule kwa kuwa wanaipenda kweli na hawachukuliwi na kuyumbishwa na uwongo. Wanauweka upendo wa kumpenda Mungu Mmoja Wapekee na wa Kweli na Mwanae, Masihi kwenye kipaumbele kuliko kitu kingine chochote. Watu hawa wataurithi Ufalme wa Mungu.

 

Wateule ni mfano kwa ulimwengu kwa kuipenda kwao kweli na kwa kupendana wao kwa wao.

Luka 22:31-32 Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano; 32 lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

 

Umuhimu uliopo hapa ni kutiana nguvu kula mtu na mwenziwe. Shetani anauwezo wa kumpepeta kila mteule kama Mungu ataruhusu hilo litokee. Kristo anaomba na kutuombea sisi dua. Petro aliokolewa kwa msaada wa Kristo. Hakuwa ameongoka hadi alipompokea Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste.

 

Matokeo ya mwisho ya mchakato ni kwamba walioongezwa katika Israeli watakombolewa na kuenea kwa wongofu ni kwa ulimwengu wote.

Isaya 1:27 Sayuni itakombolewa kwa hukumu, na waongofu wake kwa haki.

 

Tunawajibu kwa Mungu kuufanyia kazi wongofu wa watu wetu na wa ulimwengu. Tumeitwa kwa kusudi hili na kwa kazi hii. Kama watu wanavyotiwa nguvu na Roho Mtakatifu wamewekwa huru kuelekea kwenye lengo stahili. Wateule hawajitengi mmoja mmoja au kwa utaratibu wa ushirika wa amoja. Wateule huipima na kuitawanya kweli. Wanaiskia sauti ya mchungaji na kujuana kila mmoja. Watu wetu wamekabiliana, nab ado wanakabiliana na magumu makubwa kwa ajili ya kweli ya Mungu. Tutiane moyo kila mmoja wetu na kusaidiana katika kweli.

q