Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[073]

 

 

 

Samsoni na Waamuzi

(Toleo La 2 19941022-20031011)

 

Matendo na maovu ya Israeli waliyoyafanya wakiwa kipindi cha uongozi wa Waamuzi kulipelekea hatimaye kuinuka kwa Samsoni akiwa kama Mwamuzi wa Israeli akitokea kabila la Dani. Habari hii imeelezewa kwa kina kwa mtazamo wa kiroho, ukionyesha mlolongo wa matukio kama unavyochukuliwa na kufananishwa na maendeleo ya Roho Mtakatifu kwa kila mtu kwa maelekezo ya Yesu Kristo na pia kwenye Kanisa kama kundi. Hadithi hii ina mafundisho mazuri nay a kushangaz kwa siku zetu za sasa kwenye uelewa wa matendo na kazi za Masihi na kwa Kanisa.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1994, 1998, 1999, 2003 WadeCox)

(tr. 2015)

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Samsoni na Waamuzi



Waamuzi

Bwana aliwaingiza kwenye nchi ya ahadi Israeli wakiwa chini ya uongozi wa Yoshua (wokovu)\mwana wa Nuni (uvumilivu). Israeli walimtumikia Bwana siku zote za Yoshua na siku za wazee wa Israeli (mabaki ya wale Sabini) ambao waliishi na kuhudumu baada ya Yoshua, aliyefariki akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi (Waamuzi 2:7-8). Vizazi vyote walikusanyika na mababa zao, yaani, walifariki (Waamuzi 2:10). Wana wa Israeli walifanya maovu baada ya hayo na wakamtumikia Baalimu au Mabwana wengine (Waamuzi 2:11). Na hii ikafanyika kuwa ni tabia yao Israeli kwa kanuni na sheria zao. Kuna maovu sita yaliyoorodheshwa na kuandikwa kwenye Waamuzi 3:7,12; 4:1; 6:1; 10:6; 13:1. Kuwatumikia huku miungu mingine, wakiwemo Baali na Ashtorethi, kulimkasirisha sana Bwana na kumchukiza na akawatoa mikononi mwa waangamizi na mikononi mwa maadui zao ili wasiweze kuwashinda (Waamuzi 2:12-14). Wakati wowote walipokwenda vitani mkono wa Bwana ulikuwa kinyume chao (Waamuzi 2:15). Walipelekwa utumwani na Mungu akawainulia Waamuzi wa kuwaokoa (Waamuzi 2:16).

Waamuzi 2:17-23 Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo. 18 Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua. 19 Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi. 20 Basi hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akasema, Kwa kuwa taifa hili wamelihalifu agano langu nililowaamuru baba zao, wala hawakuisikiliza sauti yangu; 21 mimi nami tokea sasa sitalifukuza taifa mojawapo la hayo aliyoyaacha Yoshua alipokufa; 22 ili kwa njia ya hayo nipate kuwajaribu Israeli, kwamba wataishika njia ya Bwana kwenda katika njia hiyo, au sivyo. 23 Basi Bwana akawaacha mataifa yale, wala hakuwafukuza kwa upesi, wala hakuwatia katika mikono ya Yoshua.

 

Israeli waliachwa na kutawanyishwa kwenye mataifa mbalimbali yaliyobakia yakiwakalia ili kwamba Israeli wajaribiwe kwa kupitia mataifa hayo (Waamuzi 3:1-4).

Waamuzi 3:1-11 Basi haya ndiyo mataifa ambao Bwana aliwaacha, ili awajaribu Israeli kwa hao, yaani, awajaribu hao wote ambao hawakuvijua vita vyote vya Kanaani; 2 ili kwamba vizazi vya wana wa Israeli wapate kujua ili kuwafundisha vita, hasa wao ambao hawakujua vita kabla ya wakati ule; 3 aliwaacha wakuu watano wa Wafilisti, na Wakanaani wote, na Wasidoni, na Wahivi waliokaa katika kilima cha Lebanoni, toka mlima wa Baal-hermoni mpaka kuingia Hamathi. 4 Naye aliwaacha ili awajaribu Israeli kwa hao, apate kujua kwamba watasikiliza amri za Bwana, alizowaamuru baba zao, kwa mkono wa Musa. 5 Basi wana wa Israeli wakaketi kati ya Wakanaani; hao Wahiti, na hao Waamori, na hao Waperizi, na hao Wahivi na hao Wayebusi; 6 wakawaoa binti zao, na binti zao wenyewe wakawaoza wana wao waume, na kuitumikia miungu yao. 7 Wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakamsahau Bwana, Mungu wao, nao wakawatumikia Mabaali na Maashtorethi. 8 Kwa hiyo hasira za Bwana ziliwaka juu ya Israeli, naye akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia; na wana wa Israeli wakamtumikia huyo Kushan-rishathaimu muda wa miaka minane. 9 Kisha wana wa Israeli walipomlingana Bwana, Bwana akawainulia wana wa Israeli mwokozi, aliyewaokoa, yaani, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu. 10 Roho ya Bwana ikamjilia juu yake, naye akawa mwamuzi wa Israeli; akatoka kwenenda vitani, naye Bwana akamtia huyo Kushan-rishathaimu, mfalme wa Mesopotamia, mkononi mwake; na mkono wake ukamshinda Kushan-rishathaimu. 11 Nayo nchi ikawa na amani muda wa miaka arobaini. Kisha Othnieli, mwana wa Kenazi, akafa.

 

Kila wakati mwamuzi aliyechaguliwa na kuwekwa na Bwana alipokufa, watu waligeuka na kufanya maovu na kuandama ibada za sanamu. Hawa Waamuzi walikuwa na Roho Mtakatifu, aliyejulikana kama Roho wa Bwana. Mfano wa jinsi hilo lilivyofanyika umeonyeshwa kwenye hadithi ya Samsoni, ambao utaelezewa kwa kina hapo chini.

 

Baada ya Othnieli (maana yake ni jeshi la Mungu) ambaye alikuwa ni mwana wa Kenazi, ndugu wa Kalebu, kufa walitenda dhambi tena.

Waamuzi 3:12-15 Basi wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu tena mbele za Bwana; naye Bwana akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu juu ya Israeli, kwa sababu walikuwa wameyafanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana. 13 Huyo Egloni akakutanisha kwake wana wa Amoni na Amaleki; akaenda na kuwapiga Israeli, nao wakauchukua huo mji wa mitende. 14 Wana wa Israeli walimtumikia Egloni mfalme wa Moabu muda wa miaka kumi na minane. 15 Lakini wana wa Israeli walipomlilia Bwana, Bwana akawainulia mwokozi, Ehudi, mwana wa Gera, Mbenyamini, mtu aliyekuwa mwenye shoto; nao wana wa Israeli walimpelekea Egloni mfalme wa Moabu tunu mkononi mwa huyo Ehudi.

 

Zawadi ambayo walimtumia Egloni, mfalme wa Moabu, ilikuwa ya namna ya sime iliyosimikwa kwa Ehudi, mwana wa Gera, kwenye paja la kuume ya Mbenyami (Waamuzi 3:16).

 

Wabenyamini waliachwa wamepewa, jambo lililodaiwa kuwa ni upewaji dhaifu kuliko zote. Mfano ni kwamba Mungu huathiri mpango wa ukombozi kwa kupitia vitu dhaifu sana. Kutoka kwa vitu vidhaifu sana anawezesha kuwepo na uweza. Hii imeathiri mara saba kwenye mfano kielelezo wa Waamuzi 1Wakorintho 1:27; 2Wakorintho 12:9. Nazo ni:

·      Mkono wa kushoto (Waamuzi 3:21);

·      Fimbo ya kuswagia ng’ombe (Waamuzi 3:31);

·      Mwanamke (Waamuzi 4:4);

·      Msumari au kucha (Waamuzi 4:21);

·      Kipande cha jiwe la jiwe la kusagia (Waamuzi 9:53);

·      Wasimika hema na tarumbeta (Waamuzi 7:20); na

·      Mfupa wa taya la punda (Waamuzi 15:16).

 

Bullinger (soma tafsiri ya Companion Bible, kwen.ye Waamuzi 3:21) anashikilia kuamini kwamba mlolongo huu wa matukio uliendelea kwenye nyakati zilizofuata kwenye harakati za Luther (mtoto wake mdogo), Calvin (mwana wa mtengeneza mapipa), Zwingle (mtoto wa mchungaji, Melancthon (mtoto wa armoureri) na John Knox (mtoto wa halisi wa mwenyeji). Kwa hiyo watano hawa walionekana kama walifana idadi ya watu saba. Hitimisho ni huenda ni zaidi kwa kufikia kuliko wale aliowaona Bullinger.

 

Ehudi alitoroka baada ya kumuua Egloni na akawahutubia Israeli kutoka kwenye milima ya Efraimu.

Waamuzi 3:27-30 Ikawa, hapo alipofika akapiga tarumbeta katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu, ndipo wana wa Israeli wakatelemka pamoja naye kutoka huko milimani, naye akawatangulia. 28 Akawaambia, Niandameni mimi; kwa kuwa Bwana amewatia adui zenu, Wamoabi, mikononi mwenu. Basi wakatelemka na kumfuata, wakavishika vivuko vya Yordani kinyume cha Wamoabi, wala hawakumwacha mtu kuvuka. 29 Wakati huo wakapiga katika Wamoabi watu waume wapata kama elfu kumi, ambao wote walikuwa wanene, na wote mashujaa; hakupona hata mtu mmoja. 30 Basi Moabu alishindwa siku hiyo chini ya mikono ya Israeli. Nayo nchi ikawa na amani muda wa miaka themanini 

 

Kwa hiyo vizazi viwili vilipita. Baada ya Ehudi alifkuwepo au kufuatiwa na Shamgari, mwana wa Anathi, aliyewaua Wafilisti mia sita kwa taya au mfupa wa punda (Waamuzi 3:31). Wakati Ehudi alipofariki, baada ya Shamgari, watu walifanya maovu tena machoni pa Bwana na aliwaokoa kutoka kwenye mikono ya Wakanaani chini ya Yabini wa Hazori, ambaye ndiye alikuwa mkuu wa majeshi wa Sisera na waliwatesa Israeli kwa mateso makubwa sana kwa kipindi cha miaka ishirini (Waamuzi 4:1-3).

 

Debora, nabii mke wa Efraimu, aliyeishi katikati ya Rama na Beth-eli aliwaamua Israeli wakati ule. Kwa maongozi ya Mungu, alimuelekeza Baraka awakusanye watu wa makabila ya Naftali na Zabuloni ili wakawaokoe Israeli.

 

Kimsingi, hapo mwanzoni Israeli walisalitiwa kibiashara na Heberi (maana yake ni jamii au jumuia au ushirika na pia ni mhamasishaji), Wakeni, ambao ni wana wa Hobabu, babu yake Musa. Alijitenga mbali na Wakeni na aliweka hema ya kambi lake kwenye nchi tambarare ya Zaanaimu (maana yake ni yaliyozolewa na kuondolewa) karibu na Kedeshi (Naftali) (Waamuzi 4:11-12). Kulikuwa na amani kati ya watu wa Heberi, Wakeni, na Yabini, mfalme wa Hazori (Waamuzi 4:17). Sisera akakimbia na kuelekea kwenye hema za Heberi. Mke wa Heberi Yaeli alitoka nje kwenda kukutana na Sisera na, baada ya kumpa ulinzi, alimuua kwa haraka kwa kumshindilia msumari kwenye hekalu lake hadi chini sakafuni (Waamuzi 4:21-22).

 

Kwa hiyo, Mungu aliwanyenyekesha Wakanaani, na kuwafanikisha Israeli. Wimbo wa Debora unaonyesha kwamba, Malaika wa mbinguni walihusika kupigana vita hivi (Waamuzi 5:20). Vita tunavyopigana kwenye mchakato huu sio vita vya kutumia silaha zinazoonekana, bali vinajumuisha uweza wa Malaika wa mbinguni.

 

Ardhi ilipumzika kwa kipindi cha miaka arobaini (au kizazi kingine) na kisha walianguka kwa kurudia tena kuabudu sanamu na Mungu akawafanya wawe mateka kwenye mikono ya Wamidiani kwa miaka saba. Israeli waliishi mapangoni na kwenye miamba ya milima. Wamidiani na Waamaleki na wana wa mashariki walikuja wakiwashukia Israeli na kuharibu mazao na kuwaacha Israeli wakiwa hawana chakula wala mifugo (Waamuzi 6:1-5). Israeli wakamlilia Bwana na waakatumiwa Gideoni wa kabila la Manase. Hadithi ya Gideoni (maana ya jina lake ni kuuangusha mti au kukata na kuangusha chini na, kwa hiyo ni, mwangushaji au mtu shujaa) au Yerubaali (maana yake ni Baali atashindana) (Waamuzi 6:1 hadi 8:28) inaelezewa na kufundishwa kwenye jarida la Jeshi la Gideoni na Siku za Mwisho (Na. 22). Kiini cha hadithi hii kinahusika na kufanya taswira ya siku za mwisho na kwenye hadithi ya kuondoa ibada za sanamu na vita iliyojitokeza kila mara iliyofuatia, kutokana na ukweli wa kwamba Baali anashindana katika siku za mwisho. Maana yake kwa wateule na ukengeufu wa siku za mwisho kunahitajika masomo au mafundisho.

 

Gideoni alikuwa na wana sabini, ambao waliweka taswira ya baraza la wazee. Mara tu baada ya kufa kwake Gideoni, Israeli walitenda dhambi tena kwa kufanya ukahaba na muingu migeni. Jambo hili lilijitokeza kila wakati ambapo mwamuzi alipokuwa anakufa. Israeli waliuacha ujumbe wa Mungu na kugeukia ibada za sanamu, hadi pale walipomlilia Mungu na akawainulia mwamuzi mwingine. Kila wakati mwamuzi alitoka kwenye kabila linguine na alikuwa na mamlaka ya kitofauti na yale ya mwamuzi aliyemtangulia. Haikuwahi kutokea kwamba mtoto wa mwamuzi amrithi huduma hii hata kwa sababu iliyoonenaka kuwa ni njjema, au kwa kuamriwa na Mungu.

 

Abimeleki, mwana wa Yerubaali, au Gideoni aloyemzaa na mjakazi wake (Waamuzi 9:18) alifanywa kuwa mfalme wa Shekemu, kwa watu wa nyumba ya mama yake. Abimeleki akawatawala Israeli kwa miaka mitatu (Waamuzi 9:22). Utawala wa Abimeleki ni taswira ya jaribio la kwanza la kutwaa kwa nguvu au kunyang’anya mamlaka baraza la kidini la Sanhedrin hadi kwenye kipindi cha ufalme. Abimeleki alimuua kaka yake mwenyewe, wa sabini, ili ajitwalie utawala. Abimeleki aliuawa na mwanamke aliyempiga kwa kipande cha jiwe la kusagia kutoka kwenye mnara wa Tebesi. Ilivunja fuvu la kichwa chake na akamuomba mbeba silaha wake amuue ili asisimangwe na watu kuwa aliuawa na mwanamke (Waamuzi 9:53-54). Kwa jinsi hiyohiyo, huu ni mfano kwa Malaika ambapo Shetani, ambaye anafanya vita ya sabini Malaika watakatifu, ameshindwa na mwanamke ambaye ni Kanisa lake Mungu.

 

Baada ya Abimeleki, mwenye kuwashindia Israeli, alikuwa ni Tolasoni wa Pua wa kabila la Isakari. Aliishi huko Shamiri kwenye Mlima wa Efraimu na aliwaamua Israeli kwa miaka ishirini na tatu (Waamuzi 10:1-2). Baada ya Tola alifuatiwa na Yairi, Mgileadi, aliyewaamua Israeli kwa miaka ishirini na miwili (Waamuzi 10:3). Alikuwa na wana thelathini ambao waliendesha magari ya farasi.

 

Mlolongo wa mambo tunaouona ni kwamba Wokovu kwa njia ya Uvumilivu umerithiwa kutoka na hukumu ya Malaika. Kulikuwa na jumla ya waamuzi kumi na wawili katika Israeli baada ya Yoshua hadi kufikia zama za kuanzishwa utawala wa wafalme. Yoshua alikuwa ni Kiongozi wa Vita wa Israeli chini ya Musa. Aliwaongoza Israeli kuwaingiza Palestina na kufanikiwa kuiteka ardhi hii. Baada ya yeye Waamuzi wa Israeli wanaonekana kama mwanzo wa utawala.

 

Hawa ndio waliohudumu kuwa waamuzi:

·      Othenieli, mwana wa Kenazi, mpwae Kalebu;

·      Ehudi wa kabila la Benyamini;

·      Shamgari, mwana wa Anathi;

[Baada ya Ehudi kufariki watu walitolewa kwenye mateso ya Yabini mfalme wa Kanaani. Kwa jinsi hii Shamgari alikuwa sio mwamuzi wa moja kwa moja kama tunavyoona kwenye Waamuzi 3:31-4:4].

·      Debora nabii mke, mke wa Lapidothi wa Efraimu (alimtumia Baraka wa Naftali alikuwa kiongozi wa vita) (Waamuzi 4:4-7);

·      Gideoni alikuwa wa kabila la Manase;

[Abimeleki mnyang’anyaji, mwana wa Gideoni kwa mwanamke Mshekemu, alijifanya kuwa mfalme wa uwongo. Hii ndiyo mana ya kuitwa mnyang’anyi. Hakuwa mmoja wa wale waamuzi kumi na wawili ila alikuwa mfalme bandia na wa uwongo.]

·      Tola, mwana wa Pua wa kabila la Isakari, aliwaamua miaka ishirini na tatu (Waamuzi 10:1-2);

·      Yairi wa Gileadi (Gadi na Manase), aliwaamua kwa miaka ishirini na miwili (Waamuzi 10:3-5);

·      Yepta Mgileadi, mwana wa mwanamke kahaba (Waamuzi11:1), aliwaamua miaka sita (Waamuzi 12:7).

 

Yefta alihamasishwa na wana wa Gileadi, ndugu zake kutoka kwa mke wa Kigileadi. Makiri, mwana wa Manase, alikuwa ni baba wa Gileadi (Yoshua 17:1). Kwahiyo, mwamuzi wa Israeli hapa alikuwa ni mtoto wa haramu wa mwanamke kahaba wa Gileadi. Wakati Wagileadi walipoingia kwenye matatizo, wazee walimjia na kuomba msaada wake na kumfanya awe kiongozi wao (Waamuzi 11:9-11). Yefta aliwashinda na kuwatiisha Waamoni. Alikuwa ni Yefta huyuhuyu ndiye aliyejipiz kiapo kilichomletea madhara binti yake kwamba atamtoa sadaka kwa Bwana. Tafsiri ya Biblia iitwayo Companion Bible inaenda mbali kwa kudhani kwamba kama sadaka yake ilivyokuwa isiyo sahihi, andiko linamtaja binti huyu kuwa alikuwa ni bikira. Andiko lililo kwene Waamuzi 11:34-40 haiashirii hivyo na tafsiri ya Soncino inaichukulia sadaka hii kuwa ni kama kitu kisicho na maana yoyote kwa kweli. Kwa mjibu wa Talmud (Taan. 4a) na vyanzo vingine kadhaa vya marabi, ikiwemo Targum, vinamchukulia kuwa alikuwa ni sadaka ya kutosha kabisa kwa kweli. Kimchi alielezea kuhusu andiko lisemalo Sitoweza kurudi nyma kwamba kisheria kiapo hiki kilitanguka na kingeweza kutanguliwa. Kwa mujibu wa Soncino:

Kile kijulikanacho kama Midrash Rabbah (Mwisho wa huduma ya Kilawi) inahusiana kwamba angeweza kwenda kwa Finehasi au Kuhani Mkuu angeenda kwake na ndipo kiapo chake kngetanguliwa. Kila mmoja alisimama kwa uadilifu wake na kuwangojea wengine wachukue hatua, na kati ya hawa wawili walipatilizwa. Wote wawili waliadhibiwa, Utukufu au Uwepo wa Mungu ukaondoka kwa Finehasi na ukoma ukampata Yefta.

 

Fundisho la kujifunza hapa ni kwamba hakuna mtu anayefungwa katika Israeli kwa kiapo ambacho kinavunja sheria ya Mungu. Kosa la kuhani la kutochuku hatua na watu binafsi kuikana au kuiacha imani ni kuondoka kwa Roho Mtakatifu kwa kila mtu binafsi mhusika. Wingu lijulikanalo kama Shekina litakuwa kwa wale wanaoonyesha kuzaa matunda. Malumbano ya kwamba mtu aliyejikita kwenye mashirika au vikundi, vinavyoenda kinyume na maagizo ya Biblia, kwa kudhani kwamba kuna mtu aliyepewa mamlaka ya Mungu kupitia Roho Mtakatifu ni ya uwongo kabisa. La muhimu sana zaidi, ni kwamba mtu anayeshindwa kuenenda hivyo atakufa. Ugonjwa wa ukoma ni mbaya sana, ambao unaonyesha mfano wa kuharibika au kuangamia kwa mwili wa kiroho. Malumbano ya hivi karibuni kuhusiana na kutii na kujinyenyekeza kwenye makanisa yaliyokengeuka, au kufuata utaratibu wa shirikisho, ni kitendo kibaya sana na kudhuru, kwa wote wawili, makuhani wanaojua na kuelewa vyema kabisa na walio kwenye mafundisho hayo ya, na watu wanaojidanganya wenyewe kwa kufuata ushauri kama huo. Makund yote mawili, yaani ya makuhani na wazee watakufa.

 

Yefta pia alipitia kwenye vita ya ndani kwa sababu ya makosa yake. Waefraimu wote walikusanyika kinyume chake na watu 42,000 wa Efraimu waliuawa kwenye maeneo ya kingo za Yordani kwa kuwa walishindwa kulitamka sawasawa neno Shibolethi bali zaidi sana tu wao walilitamka Sibolethi (Waamuzi 12:1-6). Shibolethi maana yake kijito kinachofuatia, ambacho ni kidogo, na pia ni tawi au ni kama kichala cha mahindi.

 

Maana ya makosa hasiyoelezwa yanaonyesha huenda kwamba taswira inayowatambulisha wateule inatolewa na kuna hasara kubwa katika Efraimu kulikotokana na makosa yao ya kutochukua hatua. Munbu anawachukulia hatua kuwatetea na ana umuhimu na ubora kwao. Wagileadi wanakuwa wakimbizi katikati au ndani ya Wamanase (Waamuzi 12:4-5) lakini watapewa uweza katikati yao wakiwa kama jeshi la Israeli. Tunajua kwamba Wamanase, Wareubeni na Wagadi walipokea urithi wao ng’ambo ya Yordani, na Wamanase walipewa urithi wa ziada katika Israeli. Mfano wa jambo hiili nii kwamba Manase, Reubeni na Gadi walipokea urithi nje ya Israeli. Makabila ya Gadi na Manase yote mawili yaliishi katika nchi iliyojulikana kama Gileadi, upande wa mashariki mwa Yordani.

Waamuzi waliofuatia ni:

·      Ibzani wa Bethlehemu, aliyewaamua miaka saba. Alikuwa na wana thelathini na mabinti thelathini kutoka nje kwa wanawe (Waamuzi 12:8-10). Hii ni taswira ya baraza la ndani.

·      Eloni wa Zebuloni, aliwaamua miaka kumi (Waamuzi 12:11).

·      Abdoni, mwana wa Hilleli Mpirathi wa Efraimu, aliwaamua kwa miaka minane. Alikuwa na wana arobaini na wapwaze thelathini walioendesha magari ya farasi sabini (Waamuzi 12:13-14). Hii ni taswira ya baraza lote kamili la waliorejeshwa sabini.

 

Baada ya hii, wana wa Israeli walitenda dhambi na Bwana akawatia mikononi mwa Wafilisti kwa kipindi cha miaka arobaini, kama alivyofanya huko nyuma na Wamoabi (Waamuzi 13:1). Wakati wa kipindi hiki, Samsoni alikuwa mwamuzi. Waamuzi wawili wa mwisho wameendelea hadi kwenye 1Samweli ambao ni Eli na Samweli na ndio walikuwa ni waamuzi wa mwisho wa Israeli. Samweli alikuwa nabii na mwamuzi katika Israeli, ambaye alimtia mafuta Sauli awe mfalme na kutimika chini yake au kipindi chake, lakini kwa hakika hakuhesabiwa au kujumuishwa miongoni mwa wale waamuzi kumi na wawili. Baada ya kufariki Eli ndipo mfumo wa utawala wa kifalme ulianza.

 

Samsoni

Waamuzi 13:1-25 Wana wa Israeli wakafanya tena yaliyo mabaya mbele za macho ya Bwana, Bwana akawatia katika mikono ya Wafilisti, muda wa miaka arobaini. 2 Palikuwa na mtu mmoja wa Sora, wa jamaa ya Wadani; jina lake akiitwa Manoa; na mkewe alikuwa tasa, hakuzaa watoto. 3 Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, wewe sasa u tasa, huzai; lakini utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume. 4 Basi sasa, jihadhari, nakuomba, usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi; 5 kwani tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume; na wembe usipite juu ya kichwa chake; maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni; naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya Wafilisti. 6 Ndipo yule mwanamke akaenda akamwambia mume wake, akisema, Mtu wa Mungu alinijia, na uso wake ulikuwa kama uso wa malaika wa Mungu, wa kutisha sana; nami sikumwuliza, Umetoka wapi? Wala hakuniambia jina lake; 7 lakini aliniambia, Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume; basi sasa, usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi. Maana mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni, hata siku ya kufa kwake.

 

Ukombozi wa Israeli ulifanywa na Malaika wa Yahova. Malaika huyu anaelezewa kuwa ni Kristo (soma majarida ya Mteule Kama Elohim (Na. 1) ; Uwepo wa Zama ya Kabla ya Kuzaliwa Kimwili Yesu Kristo (Na. 243) na Maila wa YHVH (Na. 24)). Samsoni aliteuliwa na kutengwa mahsusi tangu kuzliwa kwake kuwa ni mtakatifu kwa Bwana. Hii inatokana na dhana ya kukusudiwa na kujulikana kwa wateule kulikofanywa tangu kuwekwa kwa misingi ya dunia. Urithi wa Dani ulikuwa ni kuwahukumu watu wake kama mojawapo ya makabila ya Israeli (Mwanzo 49:16) na Samsoni alikuwa ni wa kwanza na mfano mkubwa wa jambo hili. Hata hivyo, unabii huu haukuhitimishwa tni wa kwanza na tni wa kwanza na kwa Samsoni. Kulikuwako pia mji wa Dani kaskazini mwa Palestina wakati wa Ibrahimu (Mwanzo 14:14), ambao ni tofauti na huyu mtoto wa Lea aliyeitwa Dani na walio kwenye kabila lake la Dani. Eneo hili la kale lilikuwa kaskazini mwa Gileadi. Waamuzi 18:30 inaelezea ibada za sanamu za wenyeji wa Dani. Kujumuishwa kwa Dani na Ufraimu kwenye Ufunuo 7:4 kama kabila la Yusufu, ni jambo linaloonekana wakati mwingine kama hukumu kwa kabila la kwanza lililoingia kwenye ibada za sanamu (soma pia Kumbukumbu la Torati 29:18-21; Mambo ya Walawi 24:10-16; 1Wafalme 12:30; 2Wafalme 10:29). Ni ili kuwawezesha kabila la Lawi waingie wakiwa jumla ya watu144,000 kama makuhani.

 

Kufanywa kwa mwamuzi kuwa ni Mnazarayo au Mnadhiri toka kuzaliwa kwake, ni alama pia ya mteule. Nadhiri za Mnazarayo zilikuwa zinadumu, na hazikuwa muhimu sana kama za Masihi ambaye yeye mwenyewe hakuwa Mnadhiri. Kutokana na kumbukumbu za Biblia, hakuna mahali panapoonyesha kuwa huduma ya Kristo ilimlazimu aweke kiapo cha kuwa Mnadhiri. Elimu ya Samsoni pia ilikuwa chini ya maelekezo na maongozi.

Aamuzi 13:8-18 Ndipo huyo Manoa akamwomba Bwana, akisema, Ee Bwana, nakuomba, yule mtu wa Mungu uliyemtuma na aje kwetu mara ya pili, atufundishe hayo yatupasayo kumfanyia huyo mtoto atakayezaliwa. 9 Mungu akasikiza sauti ya Manoa; naye malaika wa Mungu akamwendea yule mwanamke tena alipokuwa anaketi shambani; lakini mumewe, Manoa, hakuwapo pamoja naye. 10 Basi huyo mwanamke akaenda haraka, akapiga mbio, na kumwambia mumewe, akisema, Tazama, huyo mtu amenitokea, huyo aliyenijilia siku ile. 11 Basi Manoa akainuka, akamwandama mkewe, na kumfikilia mtu huyo, akamwuliza, Je! Wewe ndiwe mtu yule aliyenena na huyu mwanamke? Akasema, Naam, ni mimi. 12 Manoa akasema, Basi sasa hayo maneno yako yatakapotimia, je! Huyo mtoto atakuwa wa namna gani, na kazi yake itakuwa ni nini? 13 Malaika wa Mungu akamwambia Manoa, Katika hayo yote niliyomwambia huyo mwanamke na ajihadhari. 14 Asile kitu cho chote kitokacho katika mzabibu, wala asinywe divai, wala mvinyo, wala asile kitu cho chote kilicho najisi; hayo yote niliyomwamuru na ayatunze. 15 Kisha Manoa akamwambia huyo malaika wa Bwana, Nakuomba, tukuzuie, ili tupate kuandaa mwana-mbuzi kwa ajili yako. 16 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Manoa, Ujapokuwa wanizuia, sitakula katika mkate wako; na kwamba wataka kufanya tayari sadaka ya kuteketezwa, inakupasa kumsongezea Bwana. Kwa kuwa Manoa hakujua ya kwamba yeye ni malaika wa Bwana. 17 Manoa akamwambia huyo malaika wa Bwana, Jina lako ni nani, ili kwamba hapo hayo maneno yako yatakapotimia nipate kukutukuza? 18 Huyo malaika wa Bwana akamwambia, Kwani wewe kuniuliza jina langu, kwa kuwa jina hilo ni la ajabu?

 

Neno kustaajabisha (limetafsiriwa kamairi kwenye tafsiri ya KJV likonyesha kubadilisha maana halisi ya uhusiano) ni jina la Masihi kwenye Isaya 9:6.

 

Waamuzi 13:19-25 Basi Manoa akamtwaa yule mwana-mbuzi, pamoja na sadaka ya unga, akamtolea Bwana hapo juu ya mwamba; huyo malaika akatenda la ajabu; Manoa na mkewe wakaangalia. 20 Kwa maana, ikawa, mara huo mwali wa moto ulipopaa juu mbinguni kutoka pale madhabahuni, huyo malaika wa Bwana akapaa katika mwali wa moto wa madhabahu; nao Manoa na mkewe wakaangalia; wakainama kifudifudi. 21 Lakini malaika wa Bwana hakumtokea Manoa tena, wala mkewe. Ndipo Manoa alipojua ya kwamba ndiye malaika wa Bwana. 22 Manoa akamwambia mkewe, Hakika yetu tutakufa sisi, kwa sababu tumemwona Mungu. 23 Lakini mkewe akamwambia, Kama Bwana angetaka kutuua hangepokea sadaka ya kuteketezwa, wala sadaka ya unga, mikononi mwetu, wala hangetuonyesha mambo hayo yote, wala hangetuambia mambo kama hayo wakati huu. 24 Basi yule mwanamke akamzaa mtoto mwanamume akamwita jina lake Samsoni, mtoto huyu akakua, Bwana akambarikia. 25 Roho ya Bwana ikaanza kumtaharakisha katika Mahane-dani, katikati ya Sora na Eshtaoli.

 

Jina Samsoni maana yake ni nuru au mwanga wa jua na kwa kupitia nuru ya ulimwengu, Israeli wanapewa haki yao. Roho wa Bwana ndiye silaha ambayo Samsoni alipewa nguvu zake kwaye. Nywele za Samsoni ndizo zilizoonekana kama ishara ya nje ya nguvu zake au zilikuwa pia ni ishara ya kimwili aliyopewa ikiwa kama ahirio la uwepo wa Roho Mtakatifu.

 

Kabila la Dani waliweka hema zao huko Mahane-Dani au kwenye kambi ya Dani ambako ni Kiriyathi-yearimu katika Yuda/ kutoka hapo walikwenda na kuingia Efraimu na kuziondoa sanamu au terafimandi kutoka kwenye nyumba ya Mika na kuanzisha uwekaji wa Laishandi kwenye sanamu ya kuchongwa ya Mika katika nyumba ya Mungu katika wakati wote ambacho ilikuwa huko Shilo na Yonathani mwana wa Gershomu mwana wa Manase, Mlawi, na wanawe walikuwa ni makuhani hapo (Waamuzi 18:12-13, 30-31).

 

Mfano wa kwanza tulionao wa Samsoni ni pale anapoomba aoe mwanamke wa Kifilisti na kuwaomba wazazi wake wampe binti huyo. Mipango ya kuoa iliandaliwa na wazazi na hasahasa baba (Wanzo 21:21; 24:4; 34:8 Kutoka 21:9; soma kitabu cha Soncino, Daath Mikra). Mipango ya kuoa iliandaliwa na baba ni taswira ya kutolewa kwa wateule kwenye arusi na Kristo. Kwa mujibu wa kitabu cha Soncino, marabi waliamini na kufundisha kwamba kabla ya kuolewa mwanamke anaweza kuwa mwongofu aliyetoka kwenye umataifa kama ilivyokuwa haimithiliki kwamba Mnadhiri anaweza kuishi na mwanamke mmataifa asiye Muisraeli (Kimchion 12:4, Metsudath David). Ukweli ni kwamba wateule wote walikuwa ni Wamataifa walioitwa na wakatoka kutoka kwenye imani za kimataifa na kuandaliwa kwenye arusi kupitia kwa Roho Mtakatifu na Masihi mwamuzi aliyeonekana kimfano hapa kama Mwamzi au wa Dani ambaye ni mwamuzi wa Israeli kama kabila hapa na kuwa mwamuzi wa waamuzi wa kimwili.

Waamuzi 14:1-4 Samsoni akatelemkia Timna, akaona mwanamke huko Timna, mmojawapo wa binti za Wafilisti. 2 Kisha akapanda, akawaambia baba yake na mama yake, akasema, Nimemwona mwanamke huko Timna, mmojawapo wa binti za Wafilisti; basi mnipatie, nimwoe. 3 Ndipo baba yake na mama yake wakamwambia, Je! Hapana mwanamke hata mmoja katika ndugu zako, au katika jamaa zangu zote, hata uende kumwoa mwanamke kwa hawa Wafilisti wasiotahiriwa? Samsoni akamwambia baba yake; Mnipatie huyo, kwa maana ananipendeza sana. 4 Lakini baba yake na mama yake hawakujua ya kuwa jambo hili ni la Bwana; maana alitaka kisa juu ya Wafilisti. Basi wakati ule Wafilisti walikuwa wakiwatawala Israeli.

 

Hapa tuna usemi maalumu unaoonyesha kuwa alikuwa Malaika wa Yahova (aitwaye Yahwe au Yehova) ndiye aliyekuwa anamtumia Samsoni kwa kujifungamanisha na hatimaye kuwapiga Wafilisti. Watu hawa wanawakilisha Wamataifa ambao walipewa mamlaka ya kuwatawala Israeli kwa utumwa wa Wababeloni, hadi pale nyakati za Mataifa zilipohitimika. Akiwa kama Malaika wa Bwana aliwaokoa Israeli kutoka mikononi mwa Wafilisti kwa kupitia Samsoni, na ndivyo hivyo atawakomboa Israeli katika siku za mwisho kwa kupitia utaratibu wa hukumu ya watu waliochanganika kati ya Wadani na Waefraimu (Yeremia 4:15) na mashahidi (Ufunuo 11:1-2) ambao watatangulia ujio wake akiwa kama mfalme Masihi (sawa na majarida ya Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44) na Mashahidi (wakiwemo Mashahidi Wawili) (Na. 135)).

 

Waamuzi 14:5-11 Ndipo Samsoni na baba yake na mama yake wakatelemkia Timna, wakafika mashamba ya mizabibu huko Timna; na tazama, mwana-simba akamngurumia. 6 Roho ya Bwana ikamjilia kwa nguvu, naye akampasua kana kwamba anampasua mwana-mbuzi, wala hakuwa na kitu cho chote mkononi mwake; lakini hakuwaambia baba yake na mama yake aliyoyafanya. 7 Basi akatelemka na kuzungumza na huyo mwanamke; naye akampendeza Samsoni sana. 8 Kisha baadaye akarudi ili kumtwaa, naye akageuka kando kuuangalia mzoga wa huyo simba; na tazama, nyuki wengi walikuwamo ndani ya mzoga wa simba, na asali. 9 Akatwaa asali mikononi mwake akaenda mbele, huku akila alipokuwa akienenda, akawafikilia babaye na mamaye, akawapa, nao wakala; lakini hakuwaambia ya kuwa ameitwaa hiyo asali katika mzoga wa simba. 10 Basi babaye akamtelemkia huyo mwanamke; Samsoni naye akafanya karamu huko; kwa kuwa vijana ndivyo walivyokuwa wakifanya. 11 Basi ikawa hapo walipomwona, wakamletea wenziwe thelathini, wawe pamoja naye.

 

Washirika thelathini ndio tena dondoo kwenye baraza la ndani la Malaika. Kitendo cha kuchukua asali kutoka mwenye mwili wa simba kinawakilisha usafishaji na chakula, ambao ni wa kitu kisichosafi na kilichonajisi chenyewe. Kitendawili kilifanywa kwenye siku saba za sikukuu. Kafiri au kefhiri huyu au simba kitoto cha simba mkamilifu na kubwa (kutoka guri, hadi kefiri, hadi ariyehi hadi labi na kisha laishi) anakuwa mkali zaidi kuliko anapozeeka. Desturi ya kuwa na sherehe za arusi kwa kipindi cha siku saba inaandikwa na kuonyeshwa kwenye Mwanzo 29:27, kuwa ni kama ilitendeka hata katika siku za Mababa waliotangulia nyuma yao huko Mesopotamia. Wayahudi wanaendelea kufanya hivyo hata leo, kwa sababu ya maelekezo ya mafundisho na imani za marabi (soma Soncino, p. 271). Sikukuu inayowakilisha taswira ya arusi ya Mwanakondoo inaadhimishwa mwezi wa saba uitwao wa Ethanimu au Tishri.

 

Waamuzi 14:12-14 Samsoni akawaambia, Mimi nitawategea ninyi kitendawili; kama mwaweza kunionyesha katika hizo siku saba za karamu, na kukitambua, ndipo hapo nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavao mengine thelathini; 13 lakini msipoweza kunionyesha ndipo hapo ninyi mtanipa mimi mavazi thelathini ya kitani na mavao mengine thelathini. Basi wakamwambia, Haya, tega kitendawili chako, ili tupate kukisikia. 14 Naye akawaambia, Katika huyo mwenye kula kikatoka chakula, Katika huyo mwenye nguvu ukatoka utamu.

 

Kuna mlolongo wa mambo yanayoonyesha uwezekano kwenye andiko hili. Mavazi yavaliwayo na wahudumu wa baraza la katikati yameandaliwa kwa ajili ya kumuwakilisha elohimu. Simba mfu ni wazo au dhana ya mrejeo wa mmeguko mpya na hari ya kupenda vita waliyonayo Malaika walioasi. Uangamivu wake utasababisha kwenye mavazi mapya na kuondolewa kwa machungu ya uasi. Mwamuzi ni mtumishi wa siri za Mungu. Wateule wamepewa uwezo wa kuzijua siri hizo pia, kama wakiwa tayari na ni muhimu au lazima kuudhihirisha mpango wa wokovu. Wamataifa wanatamani kuzijua siri hizi na wanabakia kwenye mtafaruku wanaposhindwa kuzielewa au kuthibiti mchakato. Na ndiyo maana wanatafuta na kufanya kila liwezekanalo kumwangamiza bibi arusi wanapokuwa wamekanganyika.

 

Waamuzi 14:15-20 Ikawa kwa siku ya saba, wakamwambia mkewe Samsoni, Mbembeleze mumeo, ili atuonyeshe hicho kitendawili, tusije tukakuteketeza moto wewe na nyumba ya baba yako; je! Mmetuita ili mpate kuichukua mali yetu? Je! Sivyo? 16 Basi mkewe Samsoni akalia mbele yake, akasema, Wewe wanichukia tu, wala hunipendi; wewe umewategea kitendawili hao wana wa watu wangu, nawe hukuniambia mimi. Naye akamwambia, Angalia, sikumwambia baba yangu wala mama yangu, nami nikuambie wewe? 17 Naye akalia mbele yake hizo siku saba, wakati ulioendelea karamu yao; basi ikawa siku ya saba akamwambia, kwa sababu alikuwa akimsisitiza sana; naye akawaambia wale wana wa watu wake hicho kitendawili. 18 Nao watu wa mji wakamwambia siku ya saba kabla ya jua kuchwa,Ni kitu gani kilicho tamu kuliko asali? Ni kitu gani kilicho na nguvu kuliko simba? Naye akawaambia, kwamba hamkulima na mtamba wangu,Hamngekitambua kitendawili changu. 19 Roho ya Bwana ikamjilia juu yake kwa nguvu, naye akatelemkia Ashkeloni, akapiga watu waume thelathini katika watu hao, na kuzitwaa nyara zao, na kuwapa hao waliokitambua kitendawili mavao hayo. Hasira zake zikamwaka, naye akakwea kwenda nyumbani kwa baba yake. 20 Lakini huyo mke wa Samsoni aliozwa mwenzake, ambaye alikuwa amemtendea kama rafikiye.

 

Mtamba ni taifa la Israeli, limewakilishwa pia na dume la ng’ombe la Efraimu. Mtamba mwekundu huwatakasa makuhani (soma jarida la Masihi na Mtamba wa Ng’ombe Mwekundu (Na. 216)). Mtamba aliyefundishwa wa Hosea 10:11 anafananishwa pia na Misri kwenye Yeremia 46:20. Efraimu na Yuda watawekwa kwenye kongwa sawasawa na unabii ulio kwenye Hosea 10:11. Israeli walijifunga kwa kuweka agano na Mungu walipokuwa jangwani, lakini walilivunja na kumgeukia mungu wa urutubisho aliyeitwa Baali walipofika Kanaani. Ndiyo maana andiko hili linaelezea juu ya kulima kwa kutumia mtamba wa ng’ombe wa Mwamuzi. Kwa sababu hii Israeli amefanywa kuwa tasa kwa mujibu wa Hosea 9:11 nk.

 

Kujipatia siri kwa njia ya uwongo na ulaghai, kwa lazima, kunajumuisha na maangamizo ya watu wake mtu mwenyewe. Mavazi ya watu thelathini yanahusiana na karama au kipawa cha Mungu ambacho hakiwezi kupatikana kwa njia ya ulaghai.

 

Mke ambaye alikuwa sio mwaminifu, alikuwa amepanga sawasawa na maagizo ya sheria zilizoanzishwa na Malaika walioasi, kwa kuchukua nafasi ya torati ya Mungu. Maandiko ya kisheria yanayowekewa maswali ni yale yajulikanayo kama Sheria za Hamurabi seksheni za 159, 163 na 164. Mpangilio wa mwanamke kulifanyika kwa mujibu sawa na sheria hizi zinavyosema, ambazo zimewekwa kwa nia ya kuchukua pahala pa zile za Mungu na ambazo zilikuwa zimeangamiza na kuwadhuru watu kwenye sehemu ya kwanza. Kwa hiyo, desturi ya kuingilia kati kwa Wamataifa na wito wa wateule. Hii ilifanya matokeo kupoteza kwa mahali pa mke wa kwanza wa Samsoni, kama tunavyoona kwenye andiko lililo kwenye aya inayofuatia.

Waamuzi 15:1-2 Lakini ikawa baadaye, wakati wa mavuno ya ngano Samsoni akaenda kumtazama mkewe, akamchukulia mwana-mbuzi; akasema, Nitaingia chumbani kwa mke wangu. Lakini baba yake mwanamke hakumwacha kuingia. 2 Baba yake akasema, Hakika mimi nalidhani ya kuwa umemchukia kabisa; basi nalimpa rafiki yako. Je! Ndugu yake mdogo mzuri kuliko yeye? Tafadhali, mtwae huyo badala yake.

 

Hii inasanyiza jambo kwa awamu inayofuatia ya harakati za hukumu. Ndoa ya Wamataifa inaendelea. Hapa tuna mfano wa kwanza wa matumizi ya Roho Mtakatifu. Hili ni pendo la kwanza la mlolongo huu wa matukio. Huu ni mwaka wa Waefeso na mzunguko – unaofanyiza mwaka wa kwanza wa kipindi cha miaka saba na mzunguko wa kwanza wa mizunguko saba ya Yubile. Awamu na hatua za mwonekano wa uthihirisho wa Roho Mtakatifu kwa Samsoni, hufuatia hatua za mfano wa mti kama ulivyotolewa na Kristo kwenye Luka 13:8.

Luka 13:6-9 Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate. 7 Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu? 8 Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; 9 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.

 

Mchakato huu hu0ndelea kwa miaka mitatu. Kisha wa nne mi mmoja wa urutubisho na kulazimishwa kukua. Wa tano ni mmoja ya wa neema na wa sita ni mmoja wa majaribu. Wa saba ni ule wa mapumziko ya Sabato. Kwa hiyo sheria ililazimishwa na mchakato unaanza tena kwa kiwango cha juu sana. Mchakato wa mwaka wa saba unaweza kushuhudia kuondolewa au kuzimishwa kwa waonyesha nia, ambao kwa hiyo wameitwa lakini hawajachaguliwa. Kupungua kwa upendo wa kwanza kunafuatia pia kama hatari iliyotofauti wa mchakato huu wa mwanzo. Mchakato huu umeonekana pia kama hatua saba za Kanisa, kwa kupitia makanisa saba ya Mungu yaliyo kwenye Ufunuo 2 na 3.

Waamuzi 15:3-8 Samsoni akasema, Safari hii nitakuwa sina hatia katika habari za hawa Wafilisti, hapo nitakapowadhuru. 4 Samsoni akaenda akakamata mbweha mia tatu; kisha akatwaa vienge vya moto akawafunga mbweha mkia kwa mkia, akatia kienge kati ya kila mikia miwili. 5 Alipokwisha kuviwasha moto vile vienge, akawaachia mbweha kati ya ngano ya Wafilisti, akayateketeza matita, na ngano, hata na mashamba ya mizeituni. 6 Ndipo Wafilisti wakasema, Ni nani aliyetenda hivi? Wakasema, Ni huyo Samsoni, mkwewe yule Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake. Wafilisti wakaenda wakamteketeza yeye na baba yake kwa moto. 7 Samsoni akawaambia, Ikiwa ninyi mnafanya mambo kama hayo, hakika nitajilipiza kisasi juu yenu, na baadaye nitakoma. 8 Akawapiga upeo, mapigo makuu sana, kisha akatelemka akakaa katika ufa wa jabali la Etamu.

 

Hapa, tunakutana na hadithi hiyohiyo ya Gideoni, ambapo mienge inatumika katika kuwaangamiza Wamataifa. Mbeha mia tat uni sawasawa na wanaume wa vita mia tatu wenye silaha za kuchomea maadui kwenye hadithi ya Gideoni. Hapa huyu ni Roho Mtakatifu kwa mikono ya Kristo akimtumia mwamuzi wa Dani kuwaanzaa wao. Kutajwa kwa bustani za mzeituni kunahusu matumizi ya neno litumikalo kwa ajili ya ukuhani. Dini na imani potofu za Wamataifa yamejumuishwa na neno la Mungu, mikononi mwa mteule. Na ndiyo sababu mke wa Mwamuzi aliteswa na walichomwa moto hadi kufa, kama walivyokuwa wale waliokuwa kwenye mstari wao wa kiuzawa, kwa ajili ya makabila yaliyofichika ambayo kwayo idadi ya wale 144,000 wanachukuliwa au kutokana nayo.

 

Kwa sababu hii Wamataifa ndipo waliishambulia Yuda.

Waamuzi 15:9-13 Basi Wafilisti wakapanda wakapiga kambi yao katika Yuda, wakajieneza katika Lehi. 10 Watu wa Yuda wakasema, Mbona mmekuja kupigana nasi? Wakasema, Tumepanda ili kumfunga Samsoni, kumtenda yeye kama alivyotutenda sisi. 11 Ndipo watu elfu tatu wa Yuda wakatelemka hata ule ufa wa jabali la Etamu, wakamwambia Samsoni, Je! Hujui ya kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hii, basi, uliyotutenda? Akawaambia, Kadiri ile walivyonitenda mimi, ndivyo nilivyowatenda wao. 12 Wakamwambia, Tumeshuka ili kukufunga, tupate kukutia katika mikono ya Wafilisti. Samsoni akawaambia, Niapieni ya kwamba ninyi wenyewe hamtaniangukia. 13 Wakamwambia, wakisema, Vema, lakini tutakufunga sana, na kukutia katika mikono yao; lakini hakika hatutakuua. Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya, wakamchukua kutoka huko jabalini.

 

Kwenye mfano huu mwamuzi wa Israeli alitokana na Yuda, kwa kuwa walishambuliwa na Wamataifa, kwa nia ya kulitokomeza kabila ambalo kwalo walitokea ama kuchipukia. Masihi aliruhusu afungwe mkatale na kumtoa ili auawe. Hata hivyo, alirejeshwa kwa kufanywa upya na kurudishiwa uweza au nguvu zake tena kwa uweza wa Roho Mtakatifu, kama atakavyokuwa katika siku za mwisho atakaporudi akiwa ni mfalme.

Waamzi 15:14-17 Alipofika Lehi, Wafilisti wakapiga kelele walipokutana naye; ndipo roho ya Bwana ikamjia kwa nguvu, na zile kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa kama kitani iliyoteketezwa kwa moto, na vile vifungo vyake vikaanguka mikononi mwake. 15 Naye akaona mfupa mbichi wa taya ya punda, akautwaa, akapiga watu elfu kwa mfupa huo; 16 Samsoni akasema, Kwa taya ya punda chungu juu ya chungu, Kwa taya ya punda nimepiga watu elfu. 17 Ikawa, alipokuwa amekwisha kunena akautupa ule mfupa wa taya mkononi mwake; na mahali pale pakaitwa Ramath-lehi.

 

Hivyo basi, ingawa jambo hili wokovu ulifanyika. Ulinzi wa wateule unafuatiwa na wokovu ule.

Waamuzi 15:18-20 Kisha akaona kiu sana, akamwita Bwana akasema, Wewe umetupa wokovu huu kwa mkono wa mtumishi wako; na sasa nitakufa kwa kiu, na kuanguka katika mikono ya watu wasiotahiriwa. 19 Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi leo. 20 Naye akawa mwamuzi wa Israeli: katika siku za Wafilisti muda wa miaka ishirini.

 

Hapa, tunaona mchakato wa hukumu ukianzishwa. Hukumu hii ya miaka ishirini uliofuatiwa na mfuatano huu wa matukio. Ndipo anguko la Wamataifa limeonyeshwa pia, kwa kupitia watu mia tatu pamoja na Gideoni. Mchakato huu unaweza kuchukuliwa kama taswira ya mambo hadi siku za mwisho. Kwa hiyo mchakato huu ni endelevu kutokana na mlingano uliorudiwa. Mfano linganifu wa kuugawanya mwamba kwa kipigo huko Lehiisi pia ni alidurufu harakati za Masihi, kukifanya iwezekane kuwepo kwa mito ya maji yaliyo hai kutoka kwenye mwamba ambao ni Mungu.

 

Hadithi ya Samsoni na Delila inajulikana sana lakini haieleweki vizuri. Anguko la Samsoni lilitokea mwishoni mwa kipindi chake akiwa kama Mwamuzi wa Israeli, ambapo kinadhararia angeweza kuwa na nguvu zaidi kwa njia ya kukua katika Roho Mtakatifu. Mwaka wake wa ishirini kwa kweli ulikuwa ni mwaka wa tatu wa majaribu kwenye mfumo wa Jubile. Mchakato ulianzia kwenye mwaka wa kumi na tisa. Hadithi hii hata hivyo, inachukua mzungujko kamili kuendeleza. Kwenye awamu ya kwanza alitupwa kwenye ibada ya sanamu ya kiuhusiano na mpagani. Uhusiano huu ulianza kwa mwongozo na maelekezo ya Roho Mtakatifu, kama ilivyokuwa hapo kwanza. Lengo hasa lilikuwa ni kuuleta nyumba yote ya nyumba ya Wamataifa. Huu kwa kweli ni mchakato kamili kama utakavyoonekana mwishoni mwa Yubile ishirini za Milenia, wakati Shetani atakapokuwa amefunguliwa tena na mataifa yatakapomilikiwa tena na Malaika waasi, na wakianzisha tena dini potofu na za uwongo. Uwakilishi wake unajiri pia na Kanisa katika siku za mwisho kama utakavyokuwa chini ya kahaba.

Waamuzi 16:1-3 Samsoni akaenda Gaza, akaona huko mwanamke kahaba, akaingia kwake. 2 Watu wa Gaza wakaambiwa, ya kwamba, huyo Samsoni amekuja huku. Wakamzingira, wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji, wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, Na tungoje mpaka mapambazuko, ndipo tutamwua. 3 Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji, na miimo yake miwili, akaing'oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.

Hapa, Roho Mtakatifu yuko pamoja naye. Samsoni anaanza kujiamini kwa nguvu zake ambazo amepewa. Wamataifa walichukizwa na nguvu ambazo zilikuwa zilimfanya amudu kuwa kwenye kiwango cha Roho Mtakatifu. Mwonekano wa Samasoni tangu kuzaliwa kwake ulijulikana kama mfano kwamba Kanisa linaweza kufanya kazi vizuri likiwa na mchanganyiko au na mtu binafsi watakatifu.

Waamuzi 16:4-12 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila. 5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja. 6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe. 7 Samsoni akamwambia, Wakinifunga kwa kamba mbichi saba ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. 8 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamletea kamba mbichi saba zisizokauka, naye akamfunga nazo. 9 Na yule mwanamke alikuwa na watu katika chumba cha ndani, wakimwotea. Basi akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Ndipo akazikata zile kamba kama vile uzi wa pamba ukatwavyo ukiguswa na moto. Basi hiyo asili ya nguvu zake haikujulikana. 10 Delila akamwambia Samsoni, Tazama, umenidhihaki, na kuniambia uongo; sasa tafadhali, niambie, waweza kufungwa kwa kitu gani? 11 Akamwambia Wakinifunga tu kwa kamba mpya ambazo mtu hakufanya kazi nazo, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. 12 Basi Delila akatwaa kamba mpya akamfunga nazo, akamwambia, Wafilisti wanakujia, Samsoni. Na wale wenye kuotea walikuwa katika chumba cha ndani. Naye akazikata, akazitupa kutoka mikononi mwake kama uzi.

 

Mchakato umeendelea kutoka kwenye vigingi vya shungi hadi kamba. Jaribu linakuwa gumu zaidi kadiri linavyoendelea mbele. Saba ni tarakimu ta ukamilifu. Kuna mizunguko saba ya Yubile ambayo kwayo mchakato huu unarudiwa.

Waamuzi 16:13-14 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. 14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung'oa ule msumari, na ule mtande.

 

Hapa mchakato unakaribia kwa ukaribu na ukweli. Majaribu matatu ambayo aliyapitia yalikuwa chini ya ulinzi wa Mungu. Samsoni alikuwa anaanza kujiamini, na kudhani kwamba nguvu alizokuwanazo zilikuw ni zake yeye mwenyewe, na sio za Yule Malaika wa Bwana, ambaye ndiye Masihi, aliyemuwezesha Roho Mtakatifu aliyekuwa ndani yake. Mchakato huu wa majaribu ulidumu kwa kipindi cha miaka mine ya kukua na kuhitimika. Mwaka wa kwanza wa ndoa kwa mujibu wa torati humzuia mtu kwenda vitani.

 

Mwaka wa tano wa neema unamuandaa mtu kwa ajili ya mwaka wa sita wa majaribu. Ata hivyo, mchakato wa majaribu huanza katika Mwaka wa Neema na huishia kwa mavuno maradufu ya mwaka wa sita wa mavuno. Kwenye Mwaka wa Neema ishara za kushindwa kwetu kuamini zinatolewa ama kuonyeshwa dhahiri na Mungu anautumia mwaka huu ili kuanzisha mchakato wa kuwapitisha watu kwenye kipindi hiki kigumu nauthibitisho au kuwahesabia haki kila mmoja wao. Kila mwaka mchakato huu huanza na kuelekea kwenye majira ya Pasaka, na Mlo wa Meza ya Bwana, Uoshanaji wa miguu na, na Sakramenti ya Pasaka ambayo kwayo dhambi zetu zimesamehewa kwa mwaka mwingine. Hatahivyo, Mwaka wa Tano wa mzunguko ni wa muhimu sana kwa namna yake na watu wengi wanajaribiwa kiimani katika mwaka huu. Zile dhambi zilizoachwa kutiliwa maanani hadi sasa zinaletwa mbele machoni na kwenye matukio mengi, watu wengi mmoja mmoja wanaondolewa kabisa kutoka Kanisa la Mungu kwa ajili ya dhambi zisizotubiwa na kubwa.

 

Mungu atawashughulikia pia watu kwa mtazamo kwamba ni muhimu kwenye mzunguko wa miaka ya Sabato na kwamba hapendi kuwaacha bila kuwarudi kwa ajili ya mzunguko unaofuatia. Vishinda saba vya ufungaji nywele wa Samsoni vinafanya taswira ya mizunguko saba na Malaika wa Makanisa saba wayasimamiao ambao ni Kristo.

Waamuzi 16:15-20 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi. 16 Ikawa, kwa vile alivyomsumbua kwa maneno yake kila siku, na kumwudhi, roho yake ikadhikika hata kufa. 17 Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu. 18 Delila alipoona ya kuwa amemwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akatuma mtu akawaita wakuu wa Wafilisti, akisema, Njoni huku mara hii tu, maana ameniambia yote aliyo nayo moyoni mwake. Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea wakachukua ile fedha mikononi mwao. 19 Naye akamlaza usingizi magotini pake. Kisha akamwita mtu akavinyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake; akaanza kumsumbua, nguvu zake zikamtoka. 20 Kisha akasema, Samsoni, Wafilisti wanakujia. Akaamka katika usingizi wake, akasema, Nitakwenda nje kama siku nyingine, na kujinyosha. Lakini hakujua ya kuwa Bwana amemwacha.

 

Kifungu hiki cha mwisho ni cha muhimu sana kukitilia maanani. Hakujua kuwa Bwana alikuwa amemwacha inaashiria kwamba umuhimu wa kujali masharti ya kiroho chetu sisi wenyewe unapungua kwa kiasi kikubwa sana kwa wateule. Bwana alimuacha Samsoni kwa njia ya kumfanya Samsoni awe na mawazo ya kujiamini kupita kiasi, lakini ni kwa njia ya Roho Mtakatifu tu ndipo Samsoni angeweza kuwashinda Wamataifa. Siri ya nguvu zake ilitunza na kubakia kuwa siri hadi siku ya mwisho alipoitoboa mwenyewe. Inafunuliwa ili kumjaribu huyu teule na kuwahukumu Wamataifa na ili kuivunja na kuiharibu imani yao na dini yao iwe si kitu. Wamataifa walichukua uweza na kumshinda mwamuzi wa Israeli na, ndio akaondokwa na uweza au nguvu za Roho Mtakatifu. Walimng’oa macho yake na ha kuweza kuona tena, kama walivyofanywa Yuda na watu wengi wa mataifa hilo, hadi pale watu wapatao 144,000 walichukuliwa na watu wengi walijaribiwa kwenye adha ya dhiki kuu. Uweza na utawala wa Mnyama utaendeleza jambo hili.

Waamuzi 16:21-31 Wafilisti wakamkamata, wakamng'oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza. 22 Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake. 23 Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu. 24 Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu. 25 Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, Mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili. 26 Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, Niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea. 27 Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza. 28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili. 29 Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto. 30 Samsoni akasema; Na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. Basi wale watu aliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati wa uhai wake. 31 Ndipo ndugu zake, na watu wote wa nyumba ya baba yake wakatelemka, wakamtwaa wakamchukua, wakamzika kati ya Sora na Eshtaoli, katika kiwanja cha kuzikia cha Manoa baba yake. Naye alikuwa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini.

 

Uweza wa Mungu wenyezi ulionekana kwenye mchakato huu wa marejesho mapya ya Roho Mtakatifu, ambao ulionekana kwa kupitia nywele zake. Ndipo kupitia kwa mtu kipofu ambaye hapo zamani alikuwa anaona, ndipo dola au utawala wa dunia utaangushwa chini. Na ndiyo mana kwamba kipindi au zama ya mwisho ya Kanisa, Walaodikia ambao ni wenye mashaka, na maskini, vipofu na wa uchi. Inataniwa na Wamataifa kwa kuwa limechukuliwa utumwani kwa ajili ya tama zake na ulafi ua uroho wake. Ndipo kutokana na ukengeufu wake mdogo na mfumo wake dhaifu, bado kutakuwa na wateule wachache ambao watamshinda na kumpondaponda na kumwangusha chini MUNGU wa Wafilisti na kuvunja nguvu zao, ili kwamba ufalme mpya uweze kuanzishwa. Vinyago na ibada za sanamu kwenye nyumba ya Mungu za huko Shilo, chini ya makuhani wake wakengeufu, vitaondolewa na mahala ake patachukuliwa na Hekalu Jipya la Masihi la huko Yerusalemu.

 

Yubile na mizunguko ya miaka saba katika nyakati za mwisho

Tunaona uhusiano ulipo kati ya mizunguko ya miaka saba kwenye maisha ya Samsoni, kama unavyotenda kazi kwa kila mmoja chini ya Yesu Kristo na kama Kanisa lililo chini ya maongozi ya Kristo na Roho Mtakatifu. Kila mtu anaenenda kwa mzunguko wa maendeleo kwa kipindi chake cha miaka hamsini cha maisha yake, kama ilivyoelezewa na kulinganishwa na Yubile. Kwa hiyo, mtu ni Yule aliyefikia utu uzima akiwa na umri wa miaka ishirini na anaendelea hadi miaka sabini au Yubile kamili.

 

Kanisa limeamriwa kutilia maanani hilo kama lilivyoanzishwa likiwa kama mwili chini ya Yesu Kristo. Mwili huu umewekewa utaratibu kwa mujibu wa mlolongo na utaratibu wa Yubile arobaini jangwani. Tunajua wakati utaratibu wa Yubile umo na umeandikwa kwenye maandiko ya Biblia (soma majarida ya Maana ya Maono ya Ezekieli (Na. 108); Usomaji wa Torati Ulivyofanywa na Ezra na Nehemia (Na. 250)). Miaka saba ya mzunguko ni hii 1998, 2005, 2012, 2019, 2026 pamoja na Yubile ya mwaka 2027/28 na mwaka wa kwanza wa mzunguko ujao utakaokuwa ni mwaka mtakatifu wa 2028/29.

 

Na kwa hiyo unafuatiwa na miaka ya mateso na dhiki kwa Kanisa kuanza na pamoja na mwaka wa tano na wa sita ya mzunguko na miaka mingine ya Sabato na ya Mapumziko nay a Usomaji wa Torati. Kwa hiyo, kila Kanisa linajaribiwa na kuchekechwa na kila taifa linajaribiwa kwa msingi wa mzunguko wa miaka ya Sabato. Kwa hiyo, miaka ya 1996/97/98,2003/04/05, 2010/11/12,2017/18/19 na 2024/25/26 ilikuwa au inaendelea kuwa ni miaka ya kujaribiwa na kuchekechwa kwa Kanisa na kwa mataifa. Kwa utaratibu wa usomaji wa torati kwa kipindi cha zaidi ya miaka mingine thelathini, kila mzunguko utashuhudia kukaziwa kwa hukumu na matokeo mabaya au mateso kwa Kanisa na kwa taifa, na muongezeko mkubwa wa mateso na dhiki kuu hadi dunia itakapokuwa imeangamia kabisa mwaka 2025. Katika mwaka huo, mataifa yote yatapaswa yawe chini ya hukumu ya Masihi na kuletwa kwenye mamlaka kamili ya Masihi. Mwaka wa kwanza wa Yubile ya kwanza utakuwa mwaka 2028/29. Masihi atatawala dunia kwa kutumia mtindo wa agizo jipya la ulimwenguni kote kutoka Yerusalemu, kwa amri na torati ya Mungu tangu itakapofanywa upya na marejesho.

 

Joka ataangukia usoni na Sinagogi la Shetani litaonekana wazi likiabudu machoni pa wateule. Wateule watafanyika kuwa nguzo kwenye Hekalu la Mungu na hawataondoka kabisa kutoka hapo. Watakuwa na jina la Mungu na jina la Mji wa Mungu na jina jipya la Kristo. Shika sana ulichonacho asije mtu akaitwa taji yako (soma Ufunuo 3:8-13).

 

Hadithi ya Samsoni kwenye hekalu ya Joka ni awamu ya mwisho ya hadithi ya Samsoni, wakati alipoondolewa kwa ubatili wake mwenyewe, alishinda na kujitiisha Hekaluni. Hadithi hii kwa kweli ni habari ya kanisa la Walaodikia katika siku za mwisho. Inaonesha taswira kurejea kwa wale walio kwenye madaraja ya vyeo vyake wanaofanya matengenezo kwa msaada wa Roho Mtakatifu, na kuuangusha mfumo na imani ya Mnyama. Marejesho yale yanatokea katika siku za mwisho wakati Kanisa litakaposhindwa na wale walio wateule wake (kama asemavyo Danieli) kuwa watashindwa na nguvu za Mnyama na dini yake. Hata hivyo, kanisa linafanya marejesho ya imani ya kweli na kutoka kwenye harakati hizo Kristo atakuja kuwaokoa wale wanaomsubiri kwa hamu kubwa. Hili Hekalu la Joka ni imani na dini potofu ya huu ulimwengu, na kwamba mfumo na imani yote itaangushwa chini na kuangamizwa.

 

Vishinda saba vya nywele za Samsoni vinawakilisha roho saba za Mungu na nyakati saba za makanisa, kwenye mchakato wake wa maendeleo, yakielekea kwenye hatua ya yeye kuwa maskini, mwenye mashaka, kipofu na uchi, akakamatwa na Wafilisti (mungu wa dunia hii), akashindwa na kuletwa ndani akafanyika kama kichekesho na acheze mbele yao kwenye Hekalu la Dagoni (Waamuzi 16:25). Ni mwisho ule, kiwango cha chini zaidi cha Kanisa nipo Kanisa litapata nguvu za Roho Mtakatifu, na kumuangusha chini na kumwangamiza mungu wa dunia hii na dini yake yote na imani yake ambayo inafanya juhudi ya kulikomesha au kuliangamiza.

q