Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[080]

 

 

 

Hukumu ya Mapepo

(Toleo La 4.0 19941203-20060625-20100606)

 

Jarida hili linaelezea kuhusu kipindi cha mwishoni mwa utawala wa millennia wa Kristo wakati mapepo yatakapohukumiwa kwa makosa waliyowafanyia wateule kwenye kipindi cha mwisho wa Milenia. Mchakato wa hukumu unamambo fulani ya kushangaza yatakayohitimisha kwayo yanayohusu hukumu na adhabu watakayopewa mapepo kwa mtazamo wa kwamba mwingiliano holela wa asili na sifa au heshima ya Mungu.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 1994, 1999, 2006, 2010 Wade Cox)

 (Tr. 2013)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Hukumu ya Mapepo



Malaika wa Makanisa ya Mungu

Muundo wa ujenzi wa Hekalu unatuambia mengi kuhusu mtazamo wa kisayansi ya kiilimwengu au cosmolojia ya Kiebrania kuhusu ulinzi wa sayari na ambao umepelekea kuwapa wajibu malaika na hukumu. Kwa mfano, kwenye Ezekieli 41:18-19, wanaonekana makerubi kuwa wako wa aina mbili, kama vile mwenye kichwa cha mwanadamu na mwenye kichwa cha samba au Æon.

 

 Kwa hiyo maeneo mawili yanayodhibitiwa na viumbe hai wanaokizunguka Kiti cha Enzi cha Mungu, yamepewa wajibu mkubwa wa kusaidia maendeleo ya Israeli kwa mujibu wa nabii Ezekieli, walionekana kuwa ni mfumo wa kimalaika au kibinadamu, ambao kwamba Shetani alikuwa ndiye Yule kerubi wa kwanza mwenye mbawa zinazofunika na pia ni mfumo wa Æon, sehemu ya kile ninachoonekana kuwa aliuasi. Jambo hili limeongelewa sana kwenye kitabu kisemacho Tatizo la Uovu na Imani za Siri (The Problem of Evil and Mysticism). Huyu kerubi aliyefunika mbawa anaaminika kuwa Elohim bali wanajulikana pia kama Malaika. Malaika wa YHVH pia alijulikana kama Masihi (tazama majarida ya Malaika wa YHVH (Na. 24) na Mungu Tunayemwabudu (Na. 24) The Angel of YHVH (No. 24) and [The God We Worship (No. 2)]. Kitabu cha Ufunuo kinaonekana kumtaja Masihi kama Malaika pia. Kwenye Ufunuo 1:1 Malaika anatoa ujumbe au Ufunuo, ambao unatoka kwa Mungu akapewa Kristo.

 

Kwenye Ufunuo 1:10-20 inaonekana wazi kabisa kwamba Kristo ndiye anayetajwa kuwa ndiye anayeufafanua ule ujumbe. Ngazi za kimadaraka zinaonyesha kwamba Kristo ni Malaika au Kichwa cha Makanisa ya Mungu. Kila moja ya makanisa haya madogomadogo, ambayo idadi yake yako saba yaliwakilishwa na alama ya kinara cha taa, kinachowaka kwa kutegemea mafuta ya roho (Zekaria 4:2). Makanisa hayo saba ni: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia, na Laodikia. Yanasimamiwa na Malaika wadogo ambao waliandikiwa na kupewa zile nyaraka za Ufunuo 2 na 3. 1Timotheo 5:21 pia panaonekana kugusia kuwataja Malaika wa Makanisa ambayo Mtume Paulo anasema kuwa:

Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, na mbele za malaika wateule, uyatende hayo pasipo kuhukumu kwa haraka; usifanye neno lo lote kwa upendeleo.

 

Ni kweli kabisa kwamba Mtume Paulo hapa anawajumuisha maaika wema na watiifu kuwa ni sehemu ya wateule na kwamba ahadi inaendelea hadi kwenye muundo wa wote wawili yaani wanadamu na malaika.

 

Waandishi wa mambo ya kidini wanaamini kwamba kulikuwa na malaika msimamizi wa makanisa haya. Nao ni pamoja Origen (Hom. Aliye kwenye Luka 13:23), Gregory wa Nazianzus (Or. 42), Basil (Linganisha na Isaya 1:46), Gregory wa Elvira (Tract.16), Hyppolytus (De Antichr. 59), na Eusebius (Linanisha na Zaburi 47:50). Ili kujua kwa kina angalia pia kitabu cha Jean Danielou, cha Malaika na na Shughuli zao [The Angels and their Mission), (Westminster, Md, kilichochapishwa na Newman Press, 1953)] na kitabu kingine cha Wink, T, cha Uweza au The Powers, Vol. 2: na kingine cha ‘Unmasking The Powers’ (Fortress Press, Philadelphia, 1987 p. 192). Kwa bahati mbaya sana, teolojia ya kipatristiki hatimaye imekuwa na mwingiliano mkubwa na Mafundisho ya Dini za Siri ambazo kwenye kipondi cha Gregory wa Nazianzus, elimu ya cosmolojia ilienezwa ikijumuisha na mafundisho ya roho na mizimu, pamoja na mafundisho ya kwenye kwenye Yerusalemu ya Mbinguni (Or. 32 na pia Basil Ep. 2.238).

 

Imani ya kuwa na malaika mlinzi na wakuwaongoza wanadamu imeenea sana na inaingia akilini na kuaminika. Maelezo kamili ya mgawanyo wa uweza au mamlaka za malaika yametolewa kwenye kitabu cha Wink, cha The Powers, Vols. 1 na 2 (hususan Vol. 2); na cha Wagner et. al., Territorial Spirits (Sovereign World Limited, UK, 1991); na cha Dickason, cha Angels Elect and Evil (Moody Press, Chicago, 1975). Dhana ya kuwa dunia imegawanywa kwenye mamlaka yaliyo chini ya mamlaka za malaika ilienea na kuaminiwa sana sio kwa Waisraeli peke yao na Agano lao, bali hata na mataifa ya Wamataifa waliamini hivyo pia. Wink anasema hilo pia (n. 11 on ukurasa 196) kwamba:

Mfalme Julian (d. 363) akiwa kwenye umri mkubwa sana alisema akiamini kwamba wanadamu wote wana tabia mbalimbali, na lugha, na sheria au kanuni, zinazoendana na roho za wale waliowatangulia. ‘Iwapo kama kuna mungu wa taifa anaowatangulia, na chini yake kuna malaika na pepo na shujaa na kikundi fulani cha roho zilizoko pamoja zikiwa kama wasaidizi na wakala wa nguvu kuu zilizo nyuma yake, hawakufanya lolote la tofauti kwenye sheria na mataifa, sasa niambie, ni kigu gani zaidi kilichafanywa na hivi vyote? (Jarida la Kinyume au Dhidi ya Wagalilaya (Against the Galileans 143 B). watu jamii ya Demiurge 'wamewatenga watu kwa mlinganisho wa miungu mbalimbali, ambao kazi yao kubwa ni kuyaangalia mataifa na kuyalinda mataifa mbalimbali na miji yake. Kila mmoja wa miungu hii anatawala kwenye eneo lililomuangukia kimgawanyo na lillyosawa na asili yake ilivyo. Kila taifa inafanya mambo yake ama utamaduni wake sawa na jinsi linavyoongozwa na ungu anayelitawala’ (ibid., 115D).

 

Imani hii ya kuamini kuna Jeshi la mbunguni linalotulinda ni ya kale sana. Walinzi ('îyr) lilikuwa ni jina walilopewa Jeshi la malaika kutokana na imani ya kidini au walinzi wa Kikaldayo (Danieli 4:13,23), na pia alipewa mtu anayetoa amri ya kufanya mambo yaliyo kwenye taratibu za kisheria (Danieli 4:17; ila usichanganye na yaliyoandikwa kwenye Yeremia 4:16). Kristo anatajwa kuwa ni Kiumbe aliyewezesha uweza na mamlaka ya Viumbe hawa.

 

Malaika Mkuu Mikaeli anatajwa kuwa ni Malaika au Mfalme Mkuu (sar) asimamaye kwa upande wa Israeli (Danieli 12:1). Uelewa ulikuwa ni kwamba Israeli walikuwa wamechaguliwa na kusimama peke yao kati ya mataifa. Andiko lililoko kwenye Walawi 5:6 linasema (Malaika wa YHVH, ambaye baadhi ya makundi wamemtambilisha kama Mikaeli):

Mimi ni malaika anayeliombea mataifa la Israeli ili wasipigwe na kuangamizwa kabisa, na kila roho chafu inayoishambulia (APOT) (pia kumbuka alivyoandika Wink, ukurasa wa 197).

 

Muundo wote mzima wa kiroho wa dunia ulisimama kinyume na taifa hili teule, kadiri mungu (theos) wa dunia hii, Shetani Azazeli, na Jeshi lake lote lililoasi waliotupwa hapa duniani na wakiyamiliki na kuyaongoza mataifa, ambako waliruhusiwa wakae wakiwa chini ya Mwenyeji wao wa kwanza kuasi tangu uumbaji Adamu. Hii ndiyo maana ya iliyomaanisha lile neno mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Haikuwa na maana ya ujuzi tu bali ilimaanisha uwezo wa kaamua kufuata mwelekeo gani. Origen analijua hili. Origen aliamini kwamba malaika wa mataifa wangeweza kuongoka.

Ikiwa mwanadamu anaweza kuheshimu na kupita kutoka kwenye upotoe na kutoamini na kuwa mwamini, ni kwa nini basi tunasitasita kusema kilekile kuhusu Uweza? Kwa upande wangu, nathani kwamba imekuwa ikitokea wakati mwingine baadhi ya hawa wenye Mamlaka kuongoka Kristo alipokuja, na ndiyo maana baadhi ya miji na hata mamataifa yote walimkubali na kumwamini Kristo kwa utayari sana kuliko mengine (Wink, p. 197 sawa na ukilingan9isha na Yohana 18:59).

 

Origen anaamini kuwa Yule mtu wa Makedonia aliyemtokea Mtume Paulo kwenye maono akimuoma amsaidie kwenye Matendo 16:9 alikuwa ni Malaika wa Makedonia aliyekuwa anahusika na kuwajibika kuwapatia mahitaji yao yote mema ya kila namna (Hom. Kwenye Luka, 12). Na Origen anaamini hapa kama hivit:

Kabla ya kuzaliwa kwa Kristo malaika hawa walikuwa na maana ndogo kwa wale walioamriwa wawahudumie na mambo yao yalikuwa hayakubaliki na kufuatiliwa kwa mafanikio.

 

Daniélou ameandika kwa kina sana kwenye kitabu chake chenye kichwa cha somo (The Angels and Their Mission, (Malaika na Kazi Zao), Westminster, Md, Newman Press, 1953, pp. 15ff., 232: na chanzo kingine ni Les sources juives de la doctrine des anges des nationes chez Origène, Recherches de Science Religieuse 38 (1951, pp. 132-137).

 

Toba watakayoifanya Malaika hawa waasi ni kipindi kikuu sana kwenye swali la Uweza wa Mungu wa Kujua Kila Jambo. Mawazo ya Origen kuhusu tukio hili na nafasi ya hawa Malaika waasi kutubu na kuongoka yanachukuliwa kuwa yana maana iliyo sahihi katika mwendelezo wa falsafa ya Biblia. Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye kitabu kinachoitwa The Problem of Evil (Tatizo la Uovu). Mtazamo na kinachoelezwewa kwenye Biblia ni kwamba ni Shetani tu ndiye atakaye hukumiwa (1Wakorintho 6:3). Ishara ya anguko la Adamu hasajasa inaonekana kwenye Mwanzo 3:15 wakati nyoka alipowadanganya akijichanganya na mwanadamu, akijifanya kuwa sio miongoni mwa Malaika waasi na akamdanganya kwanza mwanamke na kumpotosha. Andiko hili linaendelea kueliezea tukio hili ikitumia nafsi ya umoja kwa wanamke (hapa inadhaniwa kwamba ilikuwa inamhusisha na kumtaja Masihi) kuwa ndiye kisigino cha wanadamu na kichwa cha huyu nyoka kita pondwa kwa miguu au kwato  na (SHD 7779) inafasiri maana yake kuwa kukiachanisha, au kukichoma kwa lugha ya mfano ni kukikomesha na kukishinda kabisa kwa:- kukivunja, kukiponda au kukifunika. Kisigino cha mwanadamu kinaumia na kichwa cha huyu joka kimepondwa. Lakini huyu mwanadamu hajaumia maumivu ya kudumu. Neno lililotumika halionyeshi dalili ya kukomesha au kumuondolea mbali mtu mmoja dhidi ya mwingine. Kwahiyo mgawanyo unaweza kusuluhishika na Malaika (pengine zaidi kuliko kwa Shetani) hata akitubu.

 

Hukumu ya Malaika

Kuhusu mhusika atakayewahukumu hawa Malaika umekuwa ni mjadala uliodumu kwa muda mrefu sana. Wakristo wa leo hawaelewi mlolongo sahihi wa hukumu ya hawa Malaika waasi, kwa sababu ya kutouelewa mchakato mzima wa kifo na ufufuo nay a uzima wa milele, wa wote wawili yaani wa wanadamu na wa Malaika. Wakristo wa leo wamejikuta wakiangukia kwenye makosa makubwa kutokana na kulitafsiri vibaya andiko la 1Wakorintho 6:2-3.

1Wakorintho 6:2-3  Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?

 

Je, ni malaika wapi wanaokwenda kuhukumiwa? Kwa mujibu wa andiko hili inadhaniwa kwamba Malaika watiifu wanaotajwa tu hapa na kwamba mapepo hawawezi kutubu. Hii sio kweli kabisa. Hukumu inaweza kuwahusu tu Malaika walioasi na hawawezi kuwa wale watiifu kwa Mungu.

 

Ni lini tunapowahukumu basi? Haiwezikuwa ni mwanzoni mwa kipindi cha Milenia kwa kuwa tutakuwa hatujafanya lolote na wanaweza kuhukumiwa tu kwa matendo yetu tukiwa kama wana wa Kiroho wa Mungu. Hii inamaana kwamba wanasehemu kwenye Ufufuo wa Pili wa wafu. Na hapa ndipo tutakapowahukumu. Kama watakuwa wamekwisha hukumiwa basi itakuwa ni kinyume chake.

 

Kwenye awamu ya kwanza ya Ukristo toba ilikuwa ni kitu cha lazima kufanywa. Tendo la kuangukia au kutupwa kwa Malaika kuzimuni lafaa lifafanuliwe kwa kuzingatia maelezo yafuatayo.

Isaya 14:1-32 inasema:  Maana Bwana atamhurumia Yakobo, atamchagua Israeli tena, naye atawaweka katika nchi yao wenyewe; na mgeni atajiunga nao, nao wataambatana na nyumba ya Yakobo. 2 Na hao mataifa watawatwaa na kuwaleta mpaka mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli watawamiliki, na kuwafanya watumishi na wajakazi katika nchi ya Bwana; nao watawachukua hali ya kufungwa watu wale waliowafunga wao, nao watawamiliki watu wale waliowaonea. 3 Tena itakuwa katika siku ile, ambayo Bwana atakupa raha baada ya huzuni yako, na baada ya taabu yako, na baada ya utumishi ule mgumu uliotumikishwa; 4 utatunga mithali hii juu ya mfalme wa Babeli, na kusema, Jinsi alivyokoma mwenye kuonea; Jinsi ulivyokoma mji ule wenye jeuri! 5 Bwana amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala. 6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu. 7 Dunia yote inastarehe na kutulia; Hata huanzilisha kuimba. 8 Naam, misunobari inakufurahia, Na mierezi ya Lebanoni, ikisema, Tokea wakati ulipolazwa chini wewe, Hapana mkata miti aliyetujia. 9 Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako, Ili kukulaki utakapokuja; Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako, Naam, walio wakuu wote wa dunia; Huwainua wafalme wote wa mataifa, Watoke katika viti vyao vya enzi. 10 Hao wote watajibu na kukuambia, Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi! 11 Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika. 12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. 16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao? 18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe; 19 Bali wewe umetupwa mbali na kaburi lako, Kama chipukizi lililochukiza kabisa; Kama vazi la wale waliouawa, Wale waliochomwa kwa upanga, Wale washukao mpaka misingi ya shimo; Kama mzoga uliokanyagwa chini ya miguu. 20 Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi, Kwa maana umeiharibu nchi yako, Umewaua watu wako; Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele. 21 Fanyeni tayari machinjo kwa watoto wake. Kwa sababu ya uovu wa baba zao; Wasije wakainuka na kuitamalaki nchi, Na kuujaza miji uso wa ulimwengu. 22 Nami nitainuka, nishindane nao; asema Bwana wa majeshi; na katika Babeli nitang'oa jina na mabaki, mwana na mjukuu; asema Bwana. 23 Tena nitaifanya hiyo nchi kuwa makao ya nungu, na maziwa ya maji; nami nitaifagilia mbali kwa ufagio wa uharibifu; asema Bwana wa majeshi.  

Maandiko yaliyotiwa wino mzito yanabeba ujumbe wa kupunguzwa kwa Shetani kwenye kima cha shimo. Ukweli ni kwamba alitupwa kaburini kwake (kaburini) kama tawi lisilotakiwa (aya ya 19, Biblia ya Interlinear Bible). Mzoga uliokanyagwa kwa miguu unaoelezwa hapa uliandikwa peger kwenye kamusi ya (SHD 6297), ambao unamaanisha mzoga mtepetevu uliooza, wa ama wa mwanaume au wa mnyama na kwa lugha ya fumbo inamaanisha ni aina ya kitu kilichutukuka sana cha ibada za sanamu. Kitu kiovu kinachotajwa hapa hakijajumuishwa kwenye mazishi yanayodaiwa kufanywa kwa sababu ya maovu.

Amefananishwa na mfalme wa Babeli (maana yake ni machafuko na dini za ulimwengu) lakini ni Lusifeli, Nyota ya Mchana ambaye anatajwa kama (kwenye aya ya 4). Na watu watamtazama na kusema; Je, huyu ndiye yule MTU aliyeitetemesha dunia (aya ya 16). Amekufa na hajalazwa kwenye kaburi lake.


Hakujumuishwa na wafalme wa dunia kwenye mazishi kwa sababu alikuwa ameiharibu dunia na kuwauwa watu (aya za 17-20). Hii inaweza kuwa ni vita tu ya mwishoni mwa Milenia wakati dini yote alitoianzisha na kuishamirisha itakuwa imekomeshwa sambasamba na “watoto” wake (aya ya 21). Andiko linaonyeha kuwa ni Bwana ndiye atakayeyakomesha mataifa na bwana atawajibu wajumbe wa mataifa na watu wake watafut mahali pa kukimbilia. Anaongelea kuhusu kushughulikia wenyedhambi siku ya hukumu.

 

24 Bwana wa majeshi ameapa, akisema, Hakika yangu kama vile vilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa; na kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyotokea; 25 kwamba nitamvunja huyo Mwashuri vipande vipande katika nchi yangu, na juu ya mlima wangu nitamkanyaga chini ya miguu yangu; ndipo nira yake iliyo juu yao itakapoondoka, na mzigo wake utatoka mabegani mwao. 26 Hilo ndilo kusudi lililokusudiwa duniani mwote, na huo ndio mkono ulionyoshwa juu ya mataifa yote. 27 Maana Bwana wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani itakayeugeuza nyuma? 28 Ufunuo huu ulikuja mwaka ule alipokufa mfalme Ahazi. 29 Usifurahi, Ee Ufilisti, pia wote, Kwa sababu fimbo ile iliyokupiga imevunjika; Maana katika shina la nyoka atatoka fira, na uzao wake ni joka la moto arukaye 30 Nao walio maskini kabisa watakula, Na wahitaji watajilaza salama; Nami nitatia shina lako kwa njaa, Na mabaki yako watauawa. 31 Piga yowe, Ee lango; lia, Ee mji; Ee Ufilisti, pia wote, umeyeyuka kabisa; Maana moshi unakuja toka kaskazini, Wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake. 32 Wajumbe wa taifa hilo waletewe jibu gani? Ya kuwa Bwana ameiweka misingi ya Sayuni, na ndani yake wale walioonewa katika watu wake wataona kimbilio.

 

Ili kushughulika na hukumu ya mapepo wanatakiwa wapunguziwe kwa wanadamu, waliokuwa amekufa na akawafufua na kuwapa miili wakawa hai hata kwenye Ufufuo wa Pili wa wafu. Hawa ndio watakaohukumiwa kwa hukumu ya Krisis au ya jumla ya wote na Roho Mtakatifu kwenye ubatizo. Dini na mifumo yao ya zamani na maroho zitatumika kuanzisha kumbukumbu za Ziwa la Moto.


Watapewa majina mapya na kufanywa upya kama wana wa Mungu kwa Roho Mtakatifu kama walivyokuwa huko mwanzoni kabla ya anguko lao. Mpango wa Mungu ni mkamilifu na haubadiliki.

 

Malaika waasi wote watatupwa hapa chini kwenye shimo. Baadhi ya mapepo hawa watatolewa nje ya shimo hili kwa kitambo ili wawadanganye wanadamu. Kujaribiwa huku kumelengwa wafanyiwe wateule.

 

Mapepo wanamtii Kristo na wateule tangu walipochaguliwa na kutumwa wale wanafunzi sabini (Luka 10:1,17-20).

Luka 10:17-20 Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. 19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu itakachowadhuru. 20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.

 

Kwa mujibu wa maandiko haya, anguko la Shetani limetajwa. Mapepo wana namna viwango mbalimbali vya kujisikia uhuru.

 

Mathayo 8:28-32  Naye alipofika ng'ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. 29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu? 30 Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha. 31 Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe. 32 Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini.

 Maandiko yaliyo kwenye Mathayo 8:28-32 na kwenye Marko 5:1-17 mara nyingi yanaonekana kama yanajichanganya, bali kwa kweli haya ni matukio mbalimbali tofauti. Moja linawahusisha watu wawili na linguine linamhusisha mtu mmoja. Idadi ya mapepo ni kubwa. Kwenye matukio yote mawili mapepo wanaamriwa waende wakawaliingie kundi la wanyama najisi na wanyama wanakufa. Kristo alifanikisha malengo mawili kwa kushughulika kwake na mapepo hapa. Aliwatumia mapepo kwa kuwakinga Israeli na wanyama najisi na kuwaondolea mapepo au roho chafu pia. Kwenye ukemeaji wake wa kwanza roho hawa wachafu walijua kuwa walikuwa na kipindi kifupi sana na walijua pia kwamba watakabiliwa na Kristo kwa jina la Mwenyezi Mungu kwa kipindi kile kilichowekwa. Na hapa kwenye Injili ya Marko tunaona kuwa ni mtu mmoja peke yake aliyekuwa amepagawa na jeshi la mapepo na wanamsihi Kristo asiwafukuze mbali na nchi ile. Kwa hiyo kulikuwa na namna nyingi mbalimbali himaya waliyokuwa wamepangiwa.

Marko 5:1-17 inasema: Wakafika ng'ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. 2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; 3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; 4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda. 5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe. 6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia; 7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese. 8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu. 9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi. 10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile. 11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha. 12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao. 13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini. 14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea. 15 Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa. 16 Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza ni mambo gani yaliyompata yule mwenye pepo, na habari za nguruwe. 17 Wakaanza kumsihi aondoke mipakani mwao.

 

Malaika walioelezwa kuwa wataingia shimoni kuzimuni ni wale wenye uweza waliopewa na Mnyama. Mashahidi wa nyakati za mwisho watapambana na nguvu za mapepo katika siku za mwisho.

Ufunuo 11:1-14 inasema: Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo. 2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili. 3 Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia. 4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi. 5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa. 6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo. 7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua. 8 Na mizoga yao itakuwa katika njia ya mji ule mkuu, uitwao kwa jinsi ya roho Sodoma, na Misri, tena ni hapo Bwana wao aliposulibiwa. 9 Na watu wa hao jamaa na kabila na lugha na taifa waitazama mizoga yao siku tatu u nusu, wala hawaiachi mizoga yao kuwekwa kaburini. 10 Nao wakaao juu ya nchi wafurahi juu yao na kushangilia. Nao watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa kuwa manabii hao wawili waliwatesa wao wakaao juu ya nchi. 11 Na baada ya siku hizo tatu u nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama. 12 Wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, Pandeni hata huku. Wakapanda mbinguni katika wingu, adui zao wakiwatazama. 13 Na katika saa ile palikuwa na tetemeko kuu la nchi, na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka; wanadamu elfu saba wakauawa katika tetemeko lile. Na waliosalia wakaingiwa na hofu, wakamtukuza Mungu wa mbingu. 14 Ole wa pili umekwisha pita, tazama ole wa tatu unakuja upesi.

 

Mchakato wa zama za Mataifa na kipindi cha maombolezo na ole cha miezi arobaini na miwili ni kipindi hikihiki ambacho malaika wenye nguvu wane wataachiliwa watoke kwenye shimo ili waue theluthi moja ya wanadamu. Malaika hawa waasi pia watakuwa na malaika juu yao huko kuzimu shimoni.

 

Ufunuo 9:1-18 inasema: Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. 2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni. 3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi. 4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao. 5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu. 6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia. 7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu. 8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba. 9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani. 10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao. 11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani analo jina lake Apolioni.

 

Malaika wane watasimama kwenye mto Frati, na wataachiliwa kwa kitambo kidogo katika siku za mwisho. Hii ni vita ya baragumu ya sita, itakayowaua theluthi ya wanadamu.

12 Ole wa kwanza umekwisha pita. Tazama, bado ziko ole mbili, zinakuja baadaye. 13 Malaika wa sita akapiga baragumu, nikasikia sauti moja iliyotoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyo mbele za Mungu, 14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati. 15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu. 16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao. 17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti. 18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao.

 

Mfumo huu wa kidini utakaowajumuisha malaika kwenye himaya moja dhidi ya Jeshi la Malaika ili kwamba uweza wao uzuiwe. Shetani hali kadhalika atakuwa ameingizwa na kuzuiwa kwenye ahimo hili.

 

Ufunuo 20:1-15 inasema:  Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. 2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; 3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.

 

Kitu muhimu cha kukijua hapa ni kwamba Shetani ametupwa kuzimuni kupisha utawala wa milenia wa watakatifu. Nguvu hizi kwa mataifa ilizuiwa ila nguvu ile itarudishwa tena siku au kipindi cha Milenia ili kushughulika na na mataifa. Tatizo kubwa sana kwa mataifa kipindi hiki cha utawala wa Milenia itakuwa ni kwamba watakuwa na hali ya kujiona wenye haki na watakatifu sana. Shetani ataachiliwa ili kuonyesha kwamba wanahaki na kama walikuwa hovyohovyo pasi na utaratibu bila Roho na walikuwa kwenye ushawishi wa kimaongozi na mwelekeo wa Malaika waasi.

 

Wateule watapewa uongozi wa hii dunia na Kristo na hapa ndipo watafanya kazi ya kuhukumu. Wengi wa wateule hawa wameuawa wakiwa mashahidi wa imani (Ufunuo 20:4).

 

4 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu. 7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; 8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. 9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. 10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.

 

Wafu waliosalia hawataishi hadi baada ya kipindi hiki cha miaka elfu kifike mwisho. Kwa hiyo, hukumu itafanywa na wateule peke yao waliokuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza. Hukumu ya mapepo na tendo la kumtupa Ibilisi (diabolos) kwenye Ziwa la Moto, pamoja na Mnyama na nabii wa uwongo ni andiko gumu kueleweka. Mfumo wa kidini wa unabii wa uwongo sambamba na ule wa mnyama vyote vitatupwa kwenye Ziwa la Moto pamoja na kifo, mauti na kuzimu baada ya Ufufuo wa Pili wa wafu. Mambo haya yatakuja kuondolewa mbali pamoja na wazo “dhana” au itikadi zake. Mambo haya yenyewe tu yanashughulikiwa sawa na mpango wa Mungu.

 

11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

 (imefafanuliwa kwenye jarida la Ufufuo wa Wafu (Na. 143) [The Resurrection of the Dead (No. 143)].

 

Azazeli mwenyewe ameikwisha hukumiwa tayari kama tunavyoona kwenye Yohana 16:10-13.

Yohana 16:10-13  kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena; 11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 12 Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa. 13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

 

Hukumu ya Shetani alikusudiwa hasa kwa kuwahukumu Malaika walioasi. Shetani alishahukumiwa kwa matendo yake akilinganishwa na Kristo. Malaika waasi wanahukumiwa kwa matendo yao wakilinganishwa na wateule. Kila ngazi inahukumiwa kwa kuilinganisha na ngazi yake stahiki kwenye mpangilio wa wateule wakiwa chini ya Kristo. Hukumu ya Malaika hawa inajumuisha pamoja na kuondolewa kwenye nafasi ya mamlaka ambayo waliaminiwa na kupewa. Hata hivyo wao hawana la kufanya zaidi ya kuonekana wakirekebishwa na mchakato wa uongozi adilifu na marekebisho.

 

Katika maongozi sahihi na maelekezo, mapepo wanaweza kutubu. Upingaji wa kwamba hawawezi na kwamba wamekusudiwa kudumu kwenye mateso ya milele ni ya Kishetani na yanayolenga kufuta mawazo sahihi ya tabia za Mungu za Rehema na huruma na yanalenga kumfanya Mungu aonekane kuwa sio muumbaji mkamilifu.

 

Kwa uweza wake wa Kuelewa Kila Jambo Mungu alijua kwamba Malaika na wanadamu watatenda dhambi. Ingekuwa kwamba aliweka utaratibu ili kuwafanya Malaika wote waokolewe, basi utaratibu mzima usingekuwa na maana yoyote. Dhambi za Shetani zilikuwa ni kwa ajili ya kujihesabia haki na kujiona bora. Akataka ampindue Mungu na kuchukua cheo chake. Kristo akateuliwa ili achukue mahala pake na alifanya lile ambalo Shetani alipaswa kulifanya huko mwanzoni. Mlolongo huu unaonekana kwenye Wafilipi 2:1-11.

Wafilipi 2:1-11 inasema: Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema, 2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. 3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. 4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. 5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. 9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; 10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; 11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

 

Tazama jinsi mlolongo ulivyo hapa:

1.      Kupewa uweza au karama za Roho kwa upendo, kukemea kwa huruma, esteule wanie mamoja.

2.      Kisifanyike kitu chochote kwa ubinafsi au kwa udanganyifu, bali ni kwa unyenyekevu, kuwaona wengine kuwa ni bora kuliko nafsi yako.

3.      Kila mmoja atangulize maslahi ya wengine.

4.      Hii ndiyo nia iliyokuwepo ndani ya Kristo ambaye ingawaje alikuwa yu namna (morphe) ya Mungu hakujaribu kujifananisha na Mungu. Hakujaribu kujifanya kuwa yu sawa na Mungu kama alivyojaribu kufanya Shetani hivyo. Badalayake, Kristo alifanyika kuwa ni mtumishi na kujinyenyekesha hadi mauti.

 

Mungu aliridhia kwamba Shetani alionyesha uongozi wake na utii lakini hakuwa mtiifu, Mungu alimuondolea mamlaka yake ya kuwa Nyota ya Asubuhi na akampa wadhifa huo Kristo (Ufunuo 2:28; 22:16). Nafasi hii anawashirikisha wateule.

 

Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti (1Yohana 5:17). Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi (1Yohana 3:9). Kwakuwa dhambi ni uasi. (1Yohana 3:4). Dhambi ilivyotawala katika mauti (Warumi 5:21). Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti (Warumi 6:23). Kristo alikufa ili awe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya dhambi mara moja kwa wote akiwa ni Kuhani Mkuu wa malaika na wateule (Waebrania 9:26; 13:11). Upatanisho huu haukuweza kuzuiwa na mwanadamu, na Kristo akiwa ni Kuhani Mkuu wa Malaika, ikiwa ni pamoja na mamlaka ya kimalaika. Ni sawasawa kabisa, hakutakuwa na upendeleo kwa yeyote, kwa kuwa hiyo ni dhambi (Yakobo 2:9). Kwa hiyo, kuwaacha malaika bila kutubu ni kuwapendelea kwa kuwa fursa hiyo imetolewa kwa wale walio ndani ya Jeshi la Malaika. Mungu hawezi kutenda dhambi na kwa hiyo Mungu hawczi kuwa na upendeleo kwa yeyote. Pia hawezi kumpendelea mtu atoapo hukumu (Mithali 24:23) na kwa kweli hana upendeleo (Matendo 10:34). Kwa hiyo Malaika watatubu na kuokolewa kwa dhabihu ya ondoleo la dhambi ya Kristo.

 

Toba ya Shetabi ndicho huenda kitu cha kukionea mashaka. Imani kuwa anaweza kutubu inatoa mashaka makubwa kwa kulinganisha na tabia zake zaidi kuliko tabia za Mungu. Hii haijaorodheshwa kwenye hii ya maandiko. Toba ya mapepo inachukuliwa kuwa ya namna ya kipekee aina yake na kwa kweli wengi wao wamekwisha tubu tayari. Hukumu aliyopewa Shetani ilikuwa ni kwamba aliondolewa kutoka kwenye mamlaka yake. Mapepo walioasi hawahukumiwa bado. Na wateule hawajaimaliza bado kazi au majukumu yao ili kuwafanya wawe wamepimwa kikamilifu dhidi ya matendo yao kama walinzi au waangalizi wa sayari hii.

 

Tunaweza kuifananisha toba ya Shetani na mfano wa Mwana Mpotevu (tazama jarida la Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199) [Lost Sheep and the Prodigal Son (No. 199)]; na pia kutoka kwenye ukweli wa kuwepo kwake Shetani kwenye ufufuo wa wafu akiwa na umbo la mwanadamu, ambalo tunaliona kwenye maandiko mengine yanayofuatia.

 

Jambo lililo wazi ni kwamba Shetani ametajwa kuwa ni ni mtu na anatokea shimoni kuzimuni kwenye Isaya 14. Uweza wake kama roho utaondolewa kutoka kwake kwenye kipidi cha mwishoni mwa utawala wa Milenia baada ya kugunduliwa kipindi cha mwisho. Kutoka kwenye Isaya 14 tunajionea kwamba mataifa yanaeleza kushangazwa kuona kuwa yeye ni mtu aliyeweza kuyaharibu mataifa. Mataifa wanamwambia Lusifeli kutokana na maandiko haya kwenye Isaya 14:10.

 

Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi! (tafsiri ya Interlinear Bible)

 

Andiko hili linaelezea mambo mawili. Hatimaye neno mtu linahudumia makusudio ya utambulisho kerubi lifunikalo ambavyo ndivyo alikuwa yeye, liitwalo la kaskazini au lenye kichwa cha mwanadamu. Pili tunajua kutoka na andiko hili kwamba Shetani atakwenda kuzimuni na kutaabika na mateso na maangamizo yatakayoendana na hali ya mwili alionao. Angalia tena andiko la Isaya 14:11-17.

Isaya 14:11-17 Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika. 12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. 16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?

 

Shetani ndiye aliyeondolewa kwenye mtandao wa nguvu za kiroho na nguvu zile ndizo zinazochoche moto kwenye Ziwa la Moto. Kwa hiyo nguvu zimewekwa kutumika kama kumbukumbu, moshi ambao utafumuka juu milele. Ukweli wa kwamba moshi utaendelea milele haumaanishi kuwa viumbe walioko ndani yake watateseka kwa kuunguzwa milele. Dhana hii sio ya kimungu na inapingana na tabia asilia za Mungu. Kuyatamani mateso ya mwingine ni wazo lililo kinyume na ni ukengeufu kwa mujibu wa mchakato huu. Njia ya kimungu imeelekezwa vema kwenye Injili zote. Mpende adui yako, Watendee mema wale wanaokuchukia. Watendee mema wale wanaokuchukia. Wahurumie wale wanaokutendea mabaya. Huruma za Mungu zadumu milele (Zaburi 136:24). Umilele huu hautakuja hadi hukumu itakapotimia. Mambo makuu yaliyo kwenye Torati ni hukumu na rehema. Hukumu inachukuliwa kuwa na maana ya marekebisho na kuadibisha. Marekebisho haya pamoja na fursa iliyopo ya kutubu imetolewa kwa Shetani sawa kama iliuvyotolewa kwa wengine wote.. yryr hapungukiwi na sifa ya kuwa ni kiumbe aliyeumbwa na Mungu na ndugu yetu zaidi ya walivyo Malaika wengine wote waasi. Shetani na Malaika wengine wote watafufuliwa na kusimama kwenye Kiti Kikubwa Chaenzi Cheupe cha Hukumu. Watachukuliwa na kuhukumiwa sawa na wanadamu wengine kwenye Ufufuo wa Pili wa wafu, pamoja na viumbe wengine wote ambao hawakuwepo kipindi cha Krsto wakiwa ni viumbe walio kwenye ulimwengu wa roho kipindi cha utawala wa millennia. Tunaona kwamba tukio hili linamjumuisha pia Shetani.

 

Andiko hili ni Andiko Takatifu, na Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka. Mapepo waliomba awahurumie (Mathayo 9:27) na huruma ile itaendelea kwao, ili kuwaonyesha malaika hawa kwamba umbaji wake wote ni mkamilifu. Ni mapenzi na makusudi ya Mungu kwamba yeyote mwenye mwili asipotee, bali wote wafikilie toba (2Petro 3:9). Katika mwanzo wa uumbaji Shetani na Malaika wote walikuwa ni sehemu ya waaminio. Keisto alisema kuwa yalikuwa ni mapenzi ya Mungu kwamba hata mmoja ya wadogo hawa asipotee (Mathayo 18:14). Kama mmoja wa wadogo walioko kundini akipotea hata kwa kiwango cha Nyota ya Asubuhi, Baba asingeweza kuonyesha kupitia uweza wake wa Kujua Kila  Kitu na uweza wake wa Kujua Kila Kitu na Uelewa wake mkuu kuliko kiumbe mwingine yeyote na pendo lake la agape? Je, ni lini Mungu aliwahi kukataa toba ya kiumbe wake? Je, angeweza kuikataa toba inayoombwa na mteule wake? Dhambi isiyosameheka ni ile ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Dhambi hii haimo miongoni mwa ile ya kuzikana nguvu za Roho Mtakatifu zenye kumwongoa kumbe yeyote na kumrejesha kwa Mungu. Mchakato huo unahusika na kuukana uweza na umoja wa Mungu kwa Malaika unaosababishwa na hali ya kujihesabia haki.

 

Kwa hiyo andiko lililoko kwenye Yeremia 10:11 linalosema kuwa Elahia (miungu) wata 'abad (imetafsiriwa kama kuangamia) ina maana ya ya kukosa jinsi ya kukimbia akiwa amevunjika kuliko kuchukuliwa kutoka kuwepo kwake. Fursa ya toba ipo kwa viumbe wote wa Mungu, kwa kuwa Mungu hana upendeleo (Warumi 2:11). Kama Shetani hawezi kutubu, basi Mungu atakuwa ni mwenye upendeleo. Bali hayuko hivyo na kwa hiyo hata Shetani anayo fursa ya kutubu. Mchakato wa toba yake utafanyika katika kipindi cha miaka mia moja ile ya Ufufuo wa Pili wa wafu kilichoko kwenye Ufunuo 20, ambacho kimetajwa pia kwenye Isaya 65:20. Kudai kwamba toba ya mapepo imekataliwa ni kupotosha ukweli kuhusu tabia ya Mungu na ni mchakato ule ule wa mawazo mapotofu ambayo yameiharibu sayari hii. Kristo ameushirikisha mchakato huu kwa wanadamu.

 

Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu

Ni fundisho kuu la Biblia kuwa Masihi alikufa ili awaokoe wenye dhambi.

 

Kifo chake kilichofanyika mara moja kilikusudia kuwaokoa wenye dhambi. Walipewa fursa ya kutubu na kuletwa hukumuni.

 

Biblia inasema pasi na kificho kuwa mapepo walimuomba Kristo awahurumie (kama tulivyoeleza hapo juu). Agano Jipya inaeleza pia kwamba Kristo aliwaendea mapepo waliofungwa kifungoni na akawahubiria baada ya kufufuka kwake.

 

Kama mapepo hayawezi kutubu basi kusingekuwa na haja ya Kristo kwenda kuwahubiria kama asingeweza kubadilisha chochote wala kufanya jambo la maana kwao ambayo ndiyo kusudi la kuhubiri.

 

Pia ni madai ya uwongo sana kwa baadhi wanaoamini kuwa kiumbe wa kiroho au pepo hawezi kufa.

 

Sababu ya 1. Iwapo kama mapepo waliweza kutebda dhambi na hawakutubu basi ni lazima wangekumbana na adhabu ya kifo na hakuna wokovu ungaliowezekana. Kwa hiyo viumbe hawa wangekuwa wamependelewa na Mungu, tabia ambayo Mungu hanayo kama tulivyoona na kujifunza hapo juu.

 

Sababu ya 2. Iwapo kama roho haiwezi kufa basi imani ya kwamba Kristo ambaye alikuwepo tangu zamani kabla ya kuzaliwa kwake kimwili asingeweza kufa. Bali Kristo alikufa na alifufuka kutoka kwa wafu.

 

Kwahiyo basi, kama Mungu alivyo na uweza wa Kufanya Kila Kitu pasi kushindwa, ndivyo ilivyo kuwa mapepo wanaweza kufa kwa namna sawa tu na alivyokufa Kristo ndivyo ilivyokuwa kumleta hapa chini duniani kwa wote wenye mwili na hatimaye kuzimuni na hatimaye akafa na kisha akafufuka ili kuwahukumu. 

 

Baada ya kufufuka kwake Kristo alikwenda kwa Roho Mtakatifu kuwahubiria roho walioko kifungoni, ambako ni kuzimuni. Roho hawa ni wale walioandikwa kwenye mwanzo 6:2,4 waliofanya dhambi ya uzinifu na binti za wanadamu na walihukumiwa na kufungiwa huko kwa sababu hii (soma pia notisi za ufafanuzi wa jambo hili kwenye Biblia ya The Companion Bible kwenye aya ya andiko hili hapa chini na kwenye jarida la Nyongeza ya 23).

 

1Petro 3:18-22  Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa, 19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; 20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji. 21 Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo. 22 Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.

 

Inafuata, kama usiku na mchana, ambao Kristo asingejisumbua kuwahubiri mapepo iwapo kama wasingeweza kutubu na kama wasingeweza kuokoka.

 

Mapepo hawa pia ni wale waliotajwa kwenye 2Petro 2:4 na Yuda 6.  

2Petro 2:4  Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu;

(Interlinear Bible)

 

Yuda 1:6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.

 

Biblia ya NIV imekosea kutafsiri andiko hili la 2Petro 2:4 na kutafsiri neno Tartarus kuwa ni jehanamu, ambavyo sivyo kabisa.

 

Wamefungwa huko hadi kipindi cha hukumu na tunajua kuwa itakuwa baada ya vita ya mwishoni mwa kipindi cha Milenia.


Malaika walioasi wametupwa kuzimuni au shimo refu lisilo na mwisho wa kina chake kipindi kirefu kilichopita wakingojea kuja kwa ukombozi wa Kristo siku ya hukumu.

 

Sasa, kama wamefungwa kwenye moto wa milele nasi wangekuwa wamekwisha hukumiwa tayari. Kwa hiyo Biblia kwenye maandiko haya yangekuwa hayana maana na yangekuwa hayajavuviwa. Neno liliikwenye andiko hili linaijata kuzimuni kama Tartarus, ambalo ni shimo kubwa lenye kina kirefu chini na lisilo na mwisho wake lakini linatumika kuwashikilia Malaika hawa waasi. 

 

Kristo alifikia vigezo stahiki vya kuwaokoa wanadamu na pia hata kwa hawa Malaika walioasi na mamlaka zote za mbinguni na duniani ambao ni wametiishwa kwake.

 

Hitimisho

Mapepo hawana uwezo na wako chini yetu na tutawahukumu kwenye Ufufuo wa Wafu. Kisha watapewa mwili wa kibinadamu kwa jinsi ileile ya kama wanadamu waliofufuka wa namna walivyoumbwa watakavyochuwa na kuwa na mwili wa kibinadamu tena kwenye Ufufuo wa Pili . kisha watabadilishwa wote ili wafanye toba na kuadibishwa wale ambao hawatatubu watakufa na kuchomwa kweny moto wa Jehanamu, ambalo ni shimo la takataka ambapo ni sehemu yao ya hukumu na kifo.

 

Iwapo kama tunashindwa kuhukumu kwa haki ndipo tutashindwa kuwapo pale kuwahukumu. Kuna pande mbili tu za Ufufuo wa Pili wa Wafu: wa wale wanaohukumiwa na wa wale wanaohukumu. Basi kama tutakuwa tumekwisha wahukumu tayari basi tujue kuwa tuna upendeleo na kuwa ni wahukumu tusiozingatia haki. Na hatustahili kuwa ni sehemu ya wale walio Nyumbani mwa Mungu kwa mtazamo na tabia aina hii.


Baba wasamehe kwa kuwa hawajui watendalo!

 

Ni kwa kupitia matendo yetu sasa ambavyo wanaweza kuhukumiwa. Tunaweka viwango kwa kaduri kwa jinsi watakavyohukumiwa na kwa jinsi tunavyotenda dhambi ndipo wanapohesabiwa haki. Na ndiyo maana Shetani anaitwa mshitaki wa watu wa Mungu.

 

Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? (Malaki 2:10)?

 

Je, angekuwa ni mkatili kiasi gani na aliyekosa wema na huruma akiruhusu mmoja ya watoto afe kwa ajili ya kulipa fidia ya mwingine? Lakini tunaamini kuwa Mungu bado hana upendeleo. Wote miongoni mwa watoto wake wamepewa fursa ya kutubu kweny kipindi hiki cha kuadibishwa na cha hukumu ya haki.

 

Kiumbe huyu Lusifeli ambaye alikuja kuwa Shetani ni roho. Anapaswa kuangamizwa na afe kabisa. Kwa hiyo anatakiwa afe kama mwanadamu na kama Kristo alivyokufa akiwa mwanadamu. Fundisho la kwamba roho haifi ni ya kishetani inayoendeleza fundisho la roho isiyoweza kufa na inayoishi milele, fundisho lililoimngizwa kwenye Makanisa ya Mungu na Armstrong na yameharibu fikra za wapendwa waaminio na kuwajaza mawazo ya chuki. Kama roho haiwezi kufa basi Kristo asingeweza kuwa mwokozi wetu.

 
Roho ile iliyoharibika na ni roho ya muovu, au ya kiibilisi au ya waabudu mashetani, ambayo ni ya unabii wa uwongo nay a Mnyama ambao watatupwa kwenye Ziwa la Moto kama walivyoelezewa habari zao kwa kina kwenye kitabu cha Ufunuo.


Kutoka kwenye kitabu cha nabii Ezekieli tunajua kwamba moto utashuka kutoka kwa Shetani na utamuangamiza yeye mwenyewe akiwa na umbo la mwanadamu.


Ziwa la Moto ni ukumbusho ambalo limefanyizwa kutoka kwa roho hii iliyochukuliwa kutoka kwenye kiumbe baada ya kutumiwa katika kumharibu katika mwili wake wenye mwonekano.


Yeye ni kiumbe, aliyeumbwa na wala hana tofauti na viumbe wengine hapa duniani waliowahi kufa na kuzikwa. Kwa hiyo yuko tayari kwa Ufufuo wa Pili wa wafu. Kiumbe huyu mdogo au ukumbusho wa viumbe amemrudi Mungu aliye muumba kama walivyo wenngine wote.


Mungu anapaswa kuwa kwenye uangalizi na uthibiti wa viumbe vyake. Kwa hiyo tunapaswa kuamua matokeo ili tuwe na uweza wote usioshindwa kitu chochote. 

 

q