Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[083]

 

 

 

Korani Kwenye Biblia, Torati na Agano

 

(Toleo La Edition 3.0 20040828-20041122-20110503)

 

Kitabu cha Koran kina ujumbe muhimu sana kuhusu Biblia au Maandiko Matakatifu na Torati na Agano. Kitabu hiki cha Korani kinauthibitisha au kunga mkono ujmbe wa Biblia na Torati na Ushuhuda na Agano la Mungu. Hakuna mtu anayedai kuwa yeye ni Mwislam anaweza kuwa wa imani hiyo pasipo kukubaliana na Maandiko Matakatifu na Torati ya Mungu kwenye ubatizo na uanachama au ushirika wa Kanisa la Mungu.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2004, 2011 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Korani Kwenye Biblia, Torati na Agano


 


Kumbuka: Muhammadi ni jina la kanisa.

Ahmedi anatajwa kama Roho Mtakatifu.

Jina la mtume lilikuwa Kasimu (aliyeitwa hatimaye Muhammadi)

*************

Tumeona kuwa Kristo alikuwa mlengwa muhimu kwenye Korani akijulikana kama Nyota ya Alfajiri. Torati na Sheria za Mungu ilitolewa kwa Mababa wa imani na kwa nabii Musa na kwa Kristo, kama tunavyoona kwenye Sura zake. Zile zinaofanya Madaraja ya nyadhifa. Kwenye hizi Sura, kwenye Sura ya 61:5-6, Musa na Kristo kwa wazi sana wanaonyeshwa kuwa ni kama manabii wawili wakuu sana wa Mungu. Kwanza kabisa, Musa aliaminiwa kwa kupewa Torati ya Mungu na watu hawakumsikiliza. Kristo alitumwa ili athibitishe yote yaliyofunuliwa mbele yake kwenye Torati na kumtaja au kumrejea yeye anayestahili kusifiwa, Ahmedi, ambaye maana yake ni: “Mwenye Kusifiwa au Mwenye Kustahili Sifa”. Huyu alikuwa ni mfariji wa Agano Jipya, Roho Mtakatifu, lakini maandiko ya Hadithi yanadai kuwa lilikuwa ni jina la Nabii wa Uarabuni. Mtu atauona utazamo hu ukielezwa kwenye tafsiri nyingi za Korani na jina la Ahmedi maranyingi imetafsiriwa. Hata hivyo, Sura ya 5 inamtaja Roho Mtakatifu kuwa ni kama uweza wa Mungu kwenye maelezo ya 5:110, ambaye alikuwa ndiye chombo au chimbuko ambalo alikuwa ameelekezwa pia.

 

Kristo ni mlengwa akiwa kama chanzo au kiini au chanzo cha Ufunuo na uelewa wake. Kwa yeye aliwafunulia Torati au Taurati, na Injili au Injeeli. Nyingi ya vifungu hivi vya maandiko zimeachwa bila kutafsiriwa au kutafsiriwa vibaya au bila umakini, na sio kufanya uelewa kirahisi, lakini kuhakikisha kuwa Waislamu hawaelewi na hivyo hivyo wasiongoke kikamilifu. Hakuna tofauti kati ya Ukristo wa sasa na Maimamu. Lengo lao ni kuihakikishia migawanyo na nguvu za kisiasa. Kwa kuwachanganya hawamhakiishii mtu yeyote aelewe na ni bure. Wanazishika sheria za Mungu na Injili, na huku bado ni hakika kuhusu kazi hizi zinazowapinga wanazuoni wa Hadithi wazipinge na wakatae kuzitii. Korani inatamngaza Kristo kuwa ni kama Mhukumu na ni kwa Torati ya Mungu aliyonayo ndipo ataitumia Kuhukumu.

 

[5.43] Na huwaje wakufanye wewe hakimu nao wanayo Taurati yenye hukumu za Mwenyezi Mungu? Kisha baada ya hayo wanageuka. Na hao si wenye kuamini.

 

Manabii wote na waamzi wa watu wa Mungu walikuwa walinzi wan eno lililofunuliwa la Mngu, na walinena sawasawa na sheria na ushuhuda wa Mungu (sawa na Isaya 8:20).

 

[5.44] Hakika Sisi tuliteremsha Taurati yenye uwongofu na nuru, ambayo kwayo Manabii walio nyenyekea kiislamu, na wachamngu, na wanazuoni, waliwahukumu Mayahudi; kwani walikabidhiwa kukihifadhi Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Nao wakawa ni mashahidi juu yake. Basi msiwaogope watu, bali niogopeni Mimi. Wala msibadilishe Aya zangu kwa thamani chache. Na wasio hukumu kwa aliyo teremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio makafiri.

 

Ndivyo ilivyo pia kwenye Injili ya Ufalme wa Mungu ilifunuliwa na Kristo iliongezwa kwenye Torati ya Mungu, ambayo ndiyo imeelezewa. Huu ni msingi wenye mashiko wa Korani yenyewe.

 

[5.46] Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na nuru na inayo sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa wachamungu. (dhdi ya uovu).

 

[5.66] Na lau kuwa wangeli ishika Taurati na Injili na yote waliyo teremshiwa kutokana na Mola wao Mlezi, basi hapana shaka wangeli kula vya juu yao na vya chini ya miguu yao. Wapo watu miongoni mwao walio sawa, lakini wengi wao wanayo yafanya ni mabaya mno.

 

Hakuna yeyote anayeweza kuwa na imani bali ni Kanisa la Mngu, ambavyo ni Uislamu wa Mungu, hadi wanapofuata Torati na Ushuhuda.

 

[5.68] Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Hamna lenu jambo mpaka muishike Taurati na Injili na yote mlio teremshiwa kutokana na Mola wenu Mlezi. Na hakika ulio teremshiwa wewe kutokana na Mola wako Mlezi yatawazidishia wengi katika wao uasi na ukafiri. Basi usiwasikitikie watu makafiri.

 

Tabia ya Torati na Ushuhuda kwa kweli ilimlazimisha muasi kupinga yaliyo kwenye maandiko, na kwa kweli kuongeza kwenye hali ya kutomiliki na kutoamini kama tunavyoona imani na itikadi kongwe za Kiyahudi, Ukristo na Uislamu. Hakuna mtu anayeweza kuwa na imani ya Kiislamu pasipo kuwa na Roho Mtakatifu.

 

[5.110] Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!

 

Roho Mtakatifu anaweza kupatikana tu kwa njia ya ubatizo, ambaye Korani inamtaja moja kwa moja kuwa ni wa Mungu.

 

Korani na Ubatizo wa Allah

 

Sura ya Ng’ombe

[2.138] (Pokea) Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu..


Korani Tukufu, iliyotafsiriwa na M.H. Shakir na kuchpishwa na Tahrike Tarsile Qur'an, Inc., mwaka 1983.

 

Tafsiri nyingine nyingi zimeorodheshwa hapo chini.

 

Pickthal: (Tunachukua vyetu) Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu..

Darabadi: Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu.

Mohammed Asad: [Sema: “O Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu.

Yusufali: (Dini yetu ni) t Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu?

 

Ufafanuzi: Sibghah ص ب غ: maana ya msingi yanaonyesha kidokezo cha kupaka rangi au rangi yenyewe; ni wazi kabisa kwamba Waarabu na Wakristo wamechanganya rangi kwenye maji ya ubatizo, wakimaanisha mtu aliyebatizwa aliyepata rangi mpya maishani mwake. Yusuf Ali.

 

Neno “Sibghatun” linamaana kutia rangi au rangi yenyewe, rangi (nauni). Kwa hiyo, maneno yaliyotoholewa kutoka kwenye neno asili humaanisha: kupaka rangi, kutia rangi, kubatiza, kutia ndani, kuzamisha, kupaka rangi, kuchukua tabia, mtindo, tabia asili, gombo la sheria, dini.

 

Kwenye Aya ya 138 ya Sura ya Al-Baqaraah ya Korani, tabia za Allah na Kitabu chake cha Torati inaitwa Sibghaha ya Allah.

 

Neno صِبْغَةَ limetoholewa kutoka kwenye Aya hii (aya) ikidaiwa kabisa kuwa ni kama kitu muhimu kwa Wakristo kwamba “ubatizo” wa maji hauathiri badiliko lolote kwa mtu.


Ni hili neno la
Tahkalluq bi Akhlaq Allaah, ambalo limetoholewa kuwa la tabia za Allah (za Mungu), na kanuni pana na mhimu za imani, zinazoonyesha matokeo yanayoonekana ya mabadiliko ya kweli na halisi moyoni na ya kitabia. Ni kwa njia hii ya “ubatizo”, ambao kimsingi mabadiliko mema yafanywayo na Roho Mtakatifu, ambayo yanawezesha au kufanya kuzaliwa kupya kutendeke. Kwa mujibu wa matumizi ya lugha ya Kiarabu wakati mwingine inapokuwa inakusudiwa kabisa kumtaka au kumlazimu mwanadamu kufanya kitu fulani vebu inarukwa, kama ilivyo kwenye 2:138 na ni kitu chenyewe tu ndicho kimetajwa. Kwa hiyo, kwenye tafsiri ya Aya hii (aya) ni lazima mtu aongeze vebu kama hiyo kama Khudhu yaani kudhania, au kuasili (Shahid Bin Waheed)

 

Kutokana na fafanuzi zilizo hapo juu tunaweza kuona kwamba wengine wanaelewa mabadiliko ya kitabia yatokanayo na uongofu. Matokeo ya ubatizo ni kutoka kwenye matokeo ya kila mara ya Roho wa Mungu.

 

Kutokana na andiko lililoko hapo chini, kilamtu anapaswa kuona kwamba ubatizo ni sehemu ya imani ya kweli iliyotolewa na kupewa mtu mara moja tu na ni ambayo bado inatakiwa kutunzwa na mwamini.

 

[2.136] Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.

 

Kwa hiyo, kuna imani iliyotolewa mara moja tu na imani hii walipewa mababa wa zamani wa imani. Hakuna muumini anayepaswa kuepuka au kuacha kufanya kitu kinachohitajika kufanywa ili kutimiliza matakwa ya imani.

 

[2.137] Basi wakiamini kama mnavyo amini nyinyi, itakuwa kweli wameongoka. Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani tu. Na Mwenyezi Mungu atakutosheni kukukingeni na shari yao, na Yeye ndiye Msikizi, Mjuzi.

 

Korani inaagiza kuwa muumini atubu na kusilimu. Yeyote anayefundisha kinyume na mafundisho hayo basi sio mwamini. Mafundisho ya Hadithi za kisasa yanafundisha kusilimu sio kitendo cha muhimu, na wanatumia maandiko kuonyesha kuwa Allah anasilimisha kuliko usilimishaji wowote unaofanywa wa kimwili unaohitajika, fundisho ambalo ni kinyume kabisa na nia au lengo la Korani na Biblia. Ubatizo ni sharti la mhimu kwa mteule ili aweze kuupata ufufuo wa kwanza wa wafu. Wale wanaofundisha kinyume na hivyo, hawataweza kuuingia Ufalme wa Mungu na kwenye Bustani ya Ufufuo wa Kwanza wa Wafu wenyewe, na wanawazuilia wote wanaowasikiliza kutofanya hivyo.

 

[2.138] (Pokea) Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu.

 

[2.139] Sema: Mnahojiana nasi juu ya Mwenyezi Mungu, naye ni Mola wetu Mlezi na Mola wenu Mlezi, na sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu? Nasi tunamsafia Yeye tu.

 

[2.140] Au mnasema kuwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zao walikuwa Mayahudi au Wakristo? Sema: Je, nyinyi mnajua zaidi au Mwenyezi Mungu? Na ni nani mwenye kudhulumu zaidi kuliko yule aliye ficha ushahidi alio nao utokao kwa Mwenyezi Mungu? Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na hayo myafanyayo. M.H. Shakir

 

Hadithi za Kiislamu zinasisitiza ushuhuda huu kuhusu usilimishaji wa Allah, ambao hi dhambi zilizotendwa zamani, mwongofu mpya la washika maagano wanapaswa kuupokea.

 

Hakuna mtu anayeweza kuongoa na kusilimisha vizuri kuliko Allah, hivyo jinyenyekeze kwake.

 

Dini ile inayoitwa “Uislamu” watu wake hawaisomi Torati na Ushuhuda kama vilivyoelekeza, uelewa kuhusu mambo muhimu yahusuyo ubatizo au kusilimu na umuhimu wake ulepotea. Na hata wanadai kwamba Biblia ilikuwepo na kwamba hadi ulipofika mwaka 632 BK wa kuanza huduma ya Mtume na imani yake, ndipo ilipotea. Wanafanya hivyo ili kwamba waidharau Biblia na ili waiharibu imani. Mtume anawaita waalimu hawa wa uwongo kuwa ni ngamia au punda waliobebeshwa vitabu vya dhahabu. Wanazibeba kila siku na kwa bidii kubwa lakini hawaelewi chochote kwa yaliyoandikwa ndani yake.

 

Biblia iliyosomwa na Mtume mwaka 632 bado ipo hadi siku hizi, na hakuna hata yodi moja au neno lolote dogo lililoondolewa kutoka kwenye Torati. Maneno ya Eloah au Allah hayarudi nyuma bure, au bila matokeo, kama tulivyoambiwa.

 

Kitendo cha kusilimisha cha Allah ni sakramenti ambayo iko bado na umhimu wake muhimu kwa imani na hali ya kujitoa, na ni jambo ambalo Waislamu wanalipuzia.

 

Korani inaonyesha kuwa Torati na Ushuhuda ni muhimu na ni lazima zifuatwe.

 

Torati na Injili

 

[2.63] Na tulipo chukua ahadi yenu, na tukaunyanyua mlima juu yenu (tukakwambieni): Shikeni kwa nguvu haya tuliyo kupeni, na yakumbukeni yaliyomo ndani yake ili mpate kujilinda. (dhidi ya uovu).

 

Torati inaendelea kufundisha kuhusu sheria kuhusu vyakula pia. Kile Biblia inachofundisha na kuamru kuwa ni sheria, kinakuwa ni sheria pia kwa Waislamu pia. Sheria zilizoandikwa za Torati ni sheria pekee kwenye jamo hili. Sheria za baadae za Wayahudi za Kashrut hazipaswi kufuatwa.


[2.168] Enyi watu! Kuleni vilivyomo katika ardhi, halali na vizuri, wala msifuate nyayo za Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu aliye dhaahiri.


[3.93] Kila chakula kilikuwa halali kwa Wana wa Israili isipo kuwa alicho jizuilia Israili mwenyewe kabla haijateremshwa Taurati. Sema: Leteni Taurati muisome ikiwa nyinyi ni wasema kweli.

 

Mafundisho haya hapa yanaonesha kuwa baadhi ya mafundisho ya uwongo kwa kweli yalitokea au kuanzishwa huko Misri, na sio yalitoka Babeli kama ilivyodhaniwa hapo kabla. Haya yanaweza kuwa na misingi yake fulani, kama mapokeo ambayo sio yaliyo kwenye msisitizo wa kibiblia ya watu wa jamii ya Lemba wa Afrika Kaskazini, ambao kinasaba ni wa uzao wa Wayahudi waliojiengua kutoka Yudea kipindi cha utumwa wa Warumi.

 

[5.5] Leo mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri. Na chakula cha walio pewa Kitabu ni halali kwenu, na chakula chenu ni halali kwao. Na pia wanawake wema miongoni mwa Waumini, na wanawake wema miongoni mwa walio pewa Kitabu kabla yenu, mtakapo wapa mahari yao, mkafunga nao ndoa, bila ya kufanya uhasharati wala kuwaweka kinyumba. Na anaye kataa kuamini bila shaka a'mali yake imepotea, naye katika Akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara.

 

[5.88] Na kuleni katika alivyo kuruzukuni Mwenyezi Mungu, halali na vizuri. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye mnamuamini.

 

Kwenye Sura ya 5 tunaona sheria za vyakula zikisisitizwa mara kadhaa.

 

Sheria za vyakula zinasisitizwa kwenye Korani na kuchukuliwa kama wajibu kwa Mungu.

 

[5.96] Nyinyi mmehalalishiwa kuvua vinyama vya baharini na kuvila, kwa faida yenu na kwa wasafiri. Na mmeharimishiwa mawindo ya wanyama wa bara maadamu mmeharimia Hija. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye mtakusanywa kwake.

 

Korani Sura ya 5:96 inaweka mwingiliano mgeni, kwa kile kilichooza cha samaki na kula samaki aliye safi wakati kwamba kwenye shughuli za hija, haifanyiki kwa sababu ya tofauti iliyopo kutokana na hali ya bahari. Hata hivyo, sio vibaya kufanya mawindo au kucheza wakati wa hija. Hakuna sababu inayotolewa kwa makatazo kwenye Korani, lakini inaonekana kutuama au kuweka msingi wake kwenye torati iliyo kwenye Kumbukumbu la Torati 14:22-27, ambapo panahitaji maongeo ya nchi yatolewe zaka na yachukuliwe kwenye misafara ya hija au mahali palipochaguliwa kufanywa kambi ya sikukuu ikimaanisha kuwa sheria haijashikwa bado. Kama njia ilikuwa ni mbali sana ndipo maongeo hayo yaliamriwa yabadilishwe kuwa fedha na zachukuliwe hadi huko na vyakula na sadaka zilitakiwa zinunuliwe kutokana na fedha zinazotokana na zaka. Kwa hiyo, kitendo cha kuwinda wakati wa hija au sikukuu kulionyesha kwamba zaka haikuwa imekusanywa kiasi cha kutosha na hakukuwa na umakini. Mchezo uliowakusanya kwa njia hii haukuwa sehemu ya sadaka halisi na za kweli za Israeli au za Waislamu au za Mungu.

 

Makatazo yaliyo kwenye maandiko ya Biblia yanakubalika pia na kuhusu mambo yahusuyo vita, lakini kile kilicho safi na kilicho najisi vilibakia hivyohivyo.

 

Zaka pia inajiri au inahusiana na vitu vilivyotekwa kutoka kwenye vita kama Ibrahimu alivyoonyesha wakati alipomtolea zaka yake Melkizedeki. Lawi, akiwa bado nyongani mwake, alimtole pia huyu Melkizedeki, ambavyo ilionyesha kuwa Melkizedeki kuwa ni kama kuhani mkuu sana, akiwa ni urithi wa Lawi pia. Ndivyo ilivyo pia, kwa Ishmaeli na Esau, na wana wa Ketura, walimtolea zaka zao Melkizedeki, pia wakiwa kwenye nyonga za Ibrahimu, kukimaanisha kwamba wao pamoja na watoto wao wote walikuwa wanamtii Kristo, na kuhani mkuu sana wa Kanisa la Mungu.

 

Neno mtume-nabii lililotumika kwenye Sura ya 7:157 mara nyingi limetafsiriwa kama Mjumbe, mtume kama kifungu kinachorudiwa ili kuficha maana yenye mwingiliano wa ndani kati ya Korani na Biblia.

 

Ummi kwenye Sura hii limerudiwa kama mtu aliyekuwa wala hawezi kusoma wala kuandika (kama inavyosema Pickthall). Hata hivyo, andiko linasema “kwa yeye walikuta aliwa ameandikwa chini na wao kwenye Torati na kwenye Injili”.

[7.157] Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii, asiye soma wala kuandika, wanaye mkuta kaandikwa kwao katika Taurati na Injili, anaye waamrisha mema na anawakanya maovu, na anawahalalishia vizuri, na ana waharimishia viovu, na anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyo kuwa juu yao. Basi wale walio muamini yeye, na wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyo teremshwa pamoja naye - hao ndio wenye kufanikiwa.

 

Wazo linaloaminika, ni lile la mjumbe wa Kanisa la Mungu, anayehubiri maana ya kweli ya Biblia na Torati ya Mungu, akiweka wazi tofauti iliyopo zilizopelekea kuonekana kuwa safi na najisi.

 

[8.69] Basi kuleni katika mlivyo teka, ni halali na vizuri, na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.

 

Maelekezo ya imani kwenye kweli ni kuifuata Biblia, ambacho ndani yake kuna Vitabu vinavyothibitisha kuwa ilikuwa imeandika kabla yao. Kwa hiyo Korani ni lazima ikubalianenacho na itimize yale yaliyoandikwa kwenye Injili iliyoitangulia na Torati, vinginevyo haitaweza kueleweka vema kwa kuisoma yenyewe tu peke yake. Hakuna nabii anayeweza kupingana na sheria au torati na kile kilichofunuliwa kabla yake kwenye maandiko na ushuhuda. Hakuna nabii au mtume anayefanya hivyo. Ujumbe wa kila nabii ni ufafanuzi tu wa kile kilichopita kabla yake, na ufunuo wa Mungu wa kuhusu kile kinachokwenda kutokea na kupita zake.

 

[5.48] Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu [Koran] hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu [Maandiko Matakatifu\] na kuyalinda. Basi hukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao ukaacha Haki iliyo kujia. Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka ange kufanyeni nyote umma mmoja, lakini ni kukujaribuni kwa aliyo kupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo yenu nyote, na atakuja kuwaambieni yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.

 

Paulo anaeleza kuwa migawanyiko au mafundisho ya kizushi vimeruhusiwa kuwepo miongoni mwetu ili kuwaonyesha dhahiri wale waliokubaliwa na Mngu. Andiko hili ni rejea ya maelezo ya Mtume Paulo, na migawanyiko inayotokana na makosa ya imani kwa imani kwa kushindwa kufuata Sheria na Ushuhuda.

 

Andiko lililo kwenye Sura ya 3:50 linaeleza kuwa ushuhuda wa Kristo unathibisha kuwa hii ilikuwa ni kabla yake kwenye Torati.

 

Jambo lililokatazwa lilikuwa ni kuongeza kwa kipindi cha ukuhani wa Melkizedeki hadi kwenye kipindi cha Kanisa, ambapo hapo mwanzoni sana, katika Israeli, ni kabila la Lawi tu ndilo waliruhusiwa au kupewa huduma hii. Haimaanishi chochote kuhusu sheria ya vyakula.

 

[3.50] Na ninasadikisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na ili nikuhalalishieni baadhi ya yale mlio harimishiwa, na nimekujieni na Ishara kutokana na Mola Mlezi wenu. Kwa hivyo mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

 

Hata hivyo, anaelezea kuhusu sheria za vyakula kwenye Sura ya 3:93, ambapo panaamriwa kwamba sheria ya biblia ya vyakula zinatofautiana kutokana na mapokeo au desturi za Wayahudi, ambapo ni uamuzi wa mtu binafsi, ikiwa kama ni matokeo ya maamuzi ya Waisraeli, ni sawa na ilivyokuwa kipindi cha kabla ya kufunuliwa Torati. Kwa hiyo, kutokana na Korani, Israeli inajlikana kuwa waliama huko Misri kuchukua baadhi ya makatazo au miiko ambayo haikuwepo kwenye Torati. Imani ya Kiyahudi ina makatazo au miiko inayoonekana kama inafanana na imani za siri, na mapokeo ya Wayahudi yanatuama kwenye mfano huo wa imani za Siri na za Kimafumbo, na hayapo kwenye maagizo ya torati ya Mungu iliyotolewa huko Sinai.

 

[3.93] Kila chakula kilikuwa halali kwa Wana wa Israili isipo kuwa alicho jizuilia Israili mwenyewe kabla haijateremshwa Taurati. Sema: Leteni Taurati muisome ikiwa nyinyi ni wasema kweli.

 

Kwenye sura ya 5:43 tunaona kwamba Sheria ya Mungu ni msingi wa hukumu yote na mwamini ndiye mtu Yule anayezifuata na kuzishika sheria na amri za Mungu na ushuhuda wake.

 

[5.43] Na huwaje wakufanye wewe hakimu nao wanayo Taurati yenye hukumu za Mwenyezi Mungu? Kisha baada ya hayo wanageuka. Na hao si wenye kuamini.

 

Korani inashikilia kuwa manabii wanahukumiwa kwa Sheria au Torati ya Mungu.

 

[5.44] Hakika Sisi tuliteremsha Taurati yenye uwongofu na nuru, ambayo kwayo Manabii walio nyenyekea kiislamu, na wachamngu, na wanazuoni, waliwahukumu Mayahudi; kwani walikabidhiwa kukihifadhi Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Nao wakawa ni mashahidi juu yake. Basi msiwaogope watu, bali niogopeni Mimi. Wala msibadilishe Aya zangu kwa thamani chache. Na wasio hukumu kwa aliyo teremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio makafiri.

 

Kwa hiyo, mtu asiyeamini au kafiri ni Yule asiyejiheshimu mwenyewe, na kujitathmini kwa yale yaliyofunuliwa kwenye Sheria na Ushuhua.

 

[5.46] Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na nuru na inayo sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa wachamngu. (dhidi ya uoavu).

 

Kristo alitumwa kwenye nyayo za manabii na kuthibitisha kuwa kile kilichokuwa kabla yake kilikuwa ni Torati. Hivyo basi, Korani inaungana na Injili na Agano Jipya kwenye maandiko ya Agano la Kale na Torati ya Mungu. Korani imeelekezwa moja kwa moja na kwa wazi kuwalenga Wakristo Waamini Utatu na wanaokataa kuitii na umuhimu wa Torati na sheria za Mungu.

 

[5.66] Na lau kuwa wangeli ishika Taurati na Injili na yote waliyo teremshiwa kutokana na Mola wao Mlezi, basi hapana shaka wangeli kula vya juu yao na vya chini ya miguu yao. Wapo watu miongoni mwao walio sawa, lakini wengi wao wanayo yafanya ni mabaya mno.

 

Mwongozo uliopo hapa ni kwenye Sura 5:66 ni kwa kushindwa kwa imani kuishika pamoja na Torati na Injili. Walishindwa kuichukua kutoka juu yao, yaani, kutokana na maongozi ya Mungu na kutoka chini ya miguuni mwao, yaani, kutoka miongoni mwa wale wanaodai kuwa ni Wakristo; kuna sehem muhimu na stahiki ya imani inayoishika na kuwa kwenye kiwango sawa na kile cha imani asilia iliyotolewa mara moja tu na iliyofuatwa na Kristo na Mitume. Hilo ni Kanisa la kweli la Mungu.

 

Kisha Korani inaendelea mbele kuwatangazia wale wanaodai kuifuata imani hivi:

 

[5.68] Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Hamna lenu jambo mpaka muishike Taurati na Injili na yote mlio teremshiwa kutokana na Mola wenu Mlezi. Na hakika ulio teremshiwa wewe kutokana na Mola wako Mlezi yatawazidishia wengi katika wao uasi na ukafiri. Basi usiwasikitikie watu makafiri.

 

Hapa Korani inasisitiza kwamba yeyote anayedai kuwa na imani ni lazima aishike Sheria na Ushuhuda. Lakini ni Sheria hii hii na Ushuhuda ambayo imekuwa kikwazo na kupingwa na wale wanaodai kuwa ni watu wa imani, au wanaotaka kuiingiza na kuitendea kazi kwenye matendo ya kipagani, kama walivyofanya waamini Utatu. Wengi wanakulia kwenye mazingira ya kutoamini kwa kuwa wanapinga na kuyazuia maelekezo ya Sheria na Ushuhuda. Hii ililengwa hapo mwanzoni kabisa kwa Wakristo wa uwongo, bali sasa inahusika na Hadithi za Kiislamu pia, kwa hilo hawazifuati Amri na Ushuhuda kama zilivyoelekezwa na Korani kabisa. Zaidi sana, ni kwamba sheria na Ushuhuda hazipo kwa ajili ya Taureti (Torati) peke yake na kwa ajili ya Injeeli au Injili tu, ambazo zinaonekana kuwa kama majina ya kijeneriki. Kitabu cha Hekima kinaendana sambamba na Torati na Injili kwenye maandiko yafuatayo ya Sura ya 5:110:

 

[5.110] Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!

 

Kumbuka pia 7:157 hapo juu, inayoelekeza kuifuata Sheria au Torati na Ushuhuda. Korani inaifungamanisha imani kwa wafuasi wa Eloah, Mungu wa Pekee na wa Kweli. Mungu huyu wa Pekee na wa Kweli, Eloah. Huyu Nguvu au Lah, amewanunua waumini wote kwa madhumuni kamili yaliyokusudiwa ya kuwapa uzima wa milele kwenye Ufufuo wa Wafu, ambao unatajwa na kufananisha na Bustani ya Paradiso. Tunaja kwamba kuna Bustani mbili za Paradiso, ni hizi zinawakilisha aina mbili za ufufuo wa (soma jarida la Kristo na Korani (Na. 163)).

 

[9.111] Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu - wanauwa na wanauwawa. Hii ni ahadi aliyo jilazimisha kwa Haki katika Taurati na Injili na Qur'ani. Na nani atimizae ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa biashara yenu mliyo fanya naye. Na huko ndiko kufuzu kukubwa,

 

Jina lililoko hapa ni la Muhammedi, lakini tunaongea habari za Kanisa hapa na sio kuhusu Nabii. Sura ya Al Hujarat inachukua jina lake kutoka kweye aya ya 4, Ahadi ya Kipekee ya Binafsi ambapo hali isiyo na umakini inawakumba waaminio.

 

Sura hii inaeleza kwa wazi kabisa kwenye Kanisa na jina la “Muhammedi” linalenga kwenye bodi au kundi zaidi kuliko kumkusudia mtu. Ndipo watafsiri waliongeza jina Muhammedi kwa sehem nyingine mbalimbali. Limewekwa mahali ambapo hapahusiki kwenye maandiko asilia au limeongezwa kwenye maandiko ya zamani sana. Kutumika kwa jina au neno Muhammedi mara nyingi kunajitokeza kuwa ni neno la kijenerikali au la jumla na linataja kikundi, ambacho kinaweza kuwa ni Kanisa la Mungu tu, peke yake.

 

[48.29] Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye wana nguvu mbele ya makafiri, na wanahurumiana wao kwa wao. Utawaona wakiinama na kusujudu wakitafuta fadhila na radhi za Mwenyezi Mungu. Alama zao zi katika nyuso zao, kwa athari ya kusujudu. Huu ndio mfano wao katika Taurati. Na mfano wao katika Injili ni kama mmea ulio toa chipukizi lake, kisha ukalitia nguvu, ukawa mnene, ukasimama sawa juu ya ubuwa wake, ukawafurahisha wakulima, ili kuwakasirisha kwa ajili yao makafiri. Mwenyezi Mungu amewaahidi walio amini na wakatenda mema katika wao msamaha na ujira mkubwa.

 

Alama ya usoni mara nyingi inaonekana miongoni mwa wale wanadai kuwa wenye kuamini ikiwa kama alama ya hisia au unyenyekevu wao. Wameweza kufanya hivyo kwa kujisugua sana ardhini vipaji vya nyuso zao kwenye mazingira ya kusujudu na maombi, ambayo wanafanya hivyo kwa kurudia rudia kama wanavyofanya wapagani wasioamini.

 

Kwenye Sura ya 61:6 tunaona kwamba Kristo anatajwa kuwa ni mjumbe au mtume wa Mwenezi Mungu. Habari njema ya Ahmedi ilikuwa ya kwamba “Mfariji” alikuwa analetwa Kanisani. Roho Mtakatifu akatokea akiwa na nguvu au uweza wa Mungu akiwa kama mjumbe au mfariji wa Kanisa siku ya Pentekoste ya mwaka wa 30 BK, lakini nguvu zake zilikataliwa au uweza wake ulidhihakiwa na wengi. Andiko hili linaloshabihiana na la Matendo Sura ya 2. Hadit imepotosha kwa makusudi nia iliyokusudiwa ieleweke kimaandiko.

 

[61.6] Na Isa bin Mariamu alipo sema: Enyi Wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu, ninaye thibitisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na mwenye kubashiria kuja Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad! Lakini alipo waletea hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio dhaahiri!

 

Itikadi ya kiimani imeelezwa kuwa ni kufanyika kuwa safi kwa kila mmoja miongoni mwa wateule kabla ya kufa kwao. Kristo mwenyewe anachukuliwa kuwa ni shahidi wa wale wote wanaodai kuwa wenye imani, na huku wakiwa hawalitii neno la Mngu.

 

[4.159] Na hawi katika Watu wa Kitabu ila hakika atamuamini yeye kabla ya kufa kwake. Naye Siku ya Kiyama atakuwa shahidi juu yao.

 

Walioitwa kwenye Kanisa la Mungu ndio wanaoonekana kuwa ni wenye imani linapoitwa, na kuletwa kwenye uelewa halisi na sahihi kabla ya kufa kwao.

 

Korani na Agano

 

Agano la Mungu limefungamanishwa kwene Korani na imani. Kwa hiyo, hakuna amtu anayeweza kuwa na imani na akakana au kulikataa Agano, au akataka kuenenda kinyume nalo.

 

[2.27] Wanao vunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo amrisha Mwenyezi Mungu kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye khasara.

 

Agano la Mngu linajulikana kuwa limewekwa na Wana wa Israeli pamoja na Mungu.

 

[2.40] Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni neema yangu niliyo kuneemesheni, na timizeni ahadi yangu, na Mimi nitatimiza ahadi yenu, na niogopeni Mimi tu.

 

Agano la Mungu lilifanywa kwa kupitia manabii. Manabii wale wanaonena sawasawa na Sheria na Ushuhuda ni lazima wasaidiwe. Wanalithibitisha kwa kulifanya imara Agano na kwa hiyo nabii ni shahidi dhidi yao.

 

[3.81] Na pale Mwenyezi Mungu alipo chukua ahadi kwa Manabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikima, kisha akakujieni Mtume mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juu yenu mumuamini na mumsaidie. Akasema: Je, mmekiri na mmekubali kushika agizo langu juu ya hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema: Basi shuhudieni, na Mimi ni pamoja nanyi katika kushuhudia.

 

Agano la Mungu linaunganisha kundi linalolisika. Hilo ni Kanisa la Mungu, ambalo ni Al Islam au Wanyenyekevu Waliojitoa kwa Mungu.

 

[3.103] Na shikamaneni kwa Kamba ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu: vile mlivyo kuwa nyinyi kwa nyinyi maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; kwa neema yake mkawa ndugu. Na mlikuwa ukingoni mwa shimo la Moto, naye akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi Mungu anakubainishieni Ishara zake ili mpate kuongoka.

 

Waaminio wamekombolewa kutoka mautini na kupewa fursa adhim ya wokovu. Agano hilo lilifanywa na Waisraeli na kisha na Kanisa, lakini wengi walilikiuka na kuliacha Agano hili la Mungu kwa fedha au mali tena na kufanyika kuwa Kanisa la uwongo kwenye mabaraza ya yaliyokaa vikao vyao katika Karne ya Nne, wakijichukulia wenye imani za kuabudu sanamu kwa kujipa mamlaka au uweza wa muda mfupi.

 

[3.187] Na pale Mwenyezi Mungu alipo fungamana na walio pewa Kitabu kuwa: Lazima mtawabainishia watu, wala hamtokificha, walikitupa nyuma ya migongo yao, na wakanunua kwacho thamani duni. Basi ni kiovu hicho walicho nunua.

 

Kwa hiyo, ujumbe wa Uislamu uliwalenga Wakristo waamini Utatu ikiwataka wairudie imani waliyopewa mara moja tu.

 

[5.15] Enyi Watu wa Kitabu! Amekwisha kujieni Mtume wetu anaye kufichulieni mengi mliyo kuwa mkiyaficha katika Kitabu, na anaye samehe mengi. Bila shaka imekujieni kutoka kwa Mwenyezi Mungu nuru na Kitabu kinacho bainisha.

 

Korani imesema waziwazi kabisa kuwa ni kitabu cha ufafanuzi na kuithibitisha Torati na Ushuhuda ambao ulikuwa ni Maandiko Matakatifu, na inahubiri yale isiyowahi kuyatenda kwenye bodi ya maandiko. Kwa hiyo karibu watafsiri wengi wa siku hizi wa Uislam kwa wanazuoni wa Hadithi hawako sahihi, na wao wenyewe wanajikuta wako nje ya uwanja wa imani, kwa sababu hawayashiki, au kunena sawasawa na ilivyo, Torati na Ushuhuda (Isaya 8:20).


[5.48] Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu [Koran] hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu [Maandiko Matakatifu\] na kuyalinda. Basi hukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao ukaacha Haki iliyo kujia. Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka ange kufanyeni nyote umma mmoja, lakini ni kukujaribuni kwa aliyo kupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo yenu nyote, na atakuja kuwaambieni yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.

q