Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[086]
Imani na Matendo
(Toleo La 2.0 19950701-20000327)
Jarida hili
linaonyesha uhusiano uliopo kati ya Imani na Matendo. Linaonyesha umuhimu wa
kuzitubia kazi zisizo na maana na mfu. Mwonekano wa imani unaonekana kuwa ulizingatiwa
sana na mitume, kuwa ni kwakupitia matendo ndopi imani inaonekana.
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki
© 1995,
2000 Wade Cox)
(tr.
2013)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Imani na Matendo
Ni kanuni ya
Ukristo kuamini kwamba mwenye haki ataishi kwa imani (Habakuki 2:4; Warumi
1:17; Waebrania 10:38). Dhana au mawazo yanayozoelekeka vichwani mwa watu siku
hizi ni kwamba imani ni muhimu na imeyazidi matendo na kwamba sheria za Mungu
au torati imekoma umuhimu wake. Na zaidi sana imedhaniwa kwamba kitendo cha
kuzishika sheria za Mungu ni sehemu ya matendo na kwamba matendo hayana umuhimu
katika wokovu wa mwanadamu. Mawazo haya yanatokana na kukosa uelewa uliopo kati
ya wokovu na neema na umuhimu wa sheria. Uhusiano huu umefafanuliwa sana kwenye
jarida la Uhusiano Uliopo
Kati ya Wokovu Unaopatikana kwa Neema na Torati (Na. 82) [The Relationship
Between Salvation by Grace and the Law (No. 82)].
Jarida hili
liafafanua uhusiano uliopo kati ya Imani na Matwndo.
Ni ukweli
usiopingika kwamba Kristo aliashiria kwamba sheria au torati imefanywa kwa
sehemu na kwamba mambo yaliyo mazito zaidi yahusuyo torati ni Haki na Rehema na Imani. Kristo alisema kwamba mambo haya yanapaswa yafanyike pasipo
kuyaacha na mengine (Mathayo 23:23).
Kwa hiyo suala
ni kwamba kulikuwa na mambo mazito zaidi. Yalikuwepo pia mambo maodgomadogo
yaliyohusiana na torati na ambayo yalitakiwa yafanyike pia. Kristo hakusema
kwamba haya yamemekoma na hayana umuhimu tena. Bali alisema kwamba: hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine
msiyaache. Kwa hiyo, yanatakiwa yafanywe yote, lakini mambo mazito zaidi yalichukua
umuhimu na yakachukua mahala pa kipaumbele cha mengine yaliyoonekana kuwa ni
madogo kwa mujibu wa sheria au torati. Kitendo cha kutoa zaka ya mnaanaa au
jira kutoka kwenye bustani yako, hakukupi haki yaw ewe kupuuzia kwenda
kuwatendea mambo mema majira zako. Ni jambo lililo kweli kwamba watu wengi
hudhani kwamba hawana hatia na ni watakatifu kwakuwa wanayafanya mambo fulani
madogomadogo katika kumtumikia Mungu. Lakini wanabakia wakiwa wanapuuzia
kuzifanya kazi nyingine za Mungu na zilizo muhimu na kubwa wasizifanye, au
wakizikimbia na kuziepa. Kristo anasema kwamba watu hawa, Waandishi na
Mafarisayo hawa walijua kikamilifu kile ambacho torati ilikuwa imeletwa kwacho
na umuhimu ambao kwawo torati ilitolewa kwetu, wanapokuwa wanatilia mkazo
kuhusu mambo hayo ambayo yalikuwa nje ya yale yaliyokuwa mambo muhimu ambayo
walitakiwa washughulike nayo. Hutakiwi kuyaacha tu pasipo kuyatenda, mambo
muhimu yahusuyo sheria au torati.
Kristo alituita
ili tufanye kazi. Hakutuita ili tukae chini tu na kuomba vyumbani mwetu.
Hutaweza kuuingia Ufalme wa Mungu kwa ajili ya kitendo chako cha kuomba dua tu
chumbani mwako, wakati ukiwa na uwezo wa kufanya mambo mengine. Kuna watu wengi
sana ambao hawaezi kutoka nje ya vyumba vyao na wanaomba kwa juhudi na huku
wakizifanya kazi za Bwana Mungu, kwa kuwa maombi ya mwenye haki yananguvu kuu
sana. Kuna mlolongo wa mambo mengi sana ambayo watu walitakiwa kuyafanya ambayo
wamepewa kwa kulinganishwa na uwezo wao na nia na umahiri wa kuyafanya. Watu
wengi wanaona ni vigumu kufanya hili na lile wakidhania kuwa kunasheria au
taratibu ambazo kwazo zinawafanya waishi.
Kutokana na
maelekezo ya Kristo yaliyo kweny Mathayo 23:23 yanaweza kuonekana kuwa imani ni
msingi wa torati zaidi kuliko uwekezaji wake.. kwa hiyo, Haki na rehema na
imani ni mambo makuu matatu yanayoitimiliza sheria au torati ambayo Kristo
alisema kuwa vinatakiwa vishikwe. Kwa kweli imani ni nyenzo muhimu ambayo kwayo
torati iliweza kutumika kwenye mazingira ya kiuadui na hatarishi. Pasaka
iliadhimishwa kwa imani, na sio mbadala wa imani. Wazo fikirika ni kwamba,
kabla torati haijatolewa kwa nabii Musa, Pasaka hii iliadhimishwa na Musa kwa
njia ya imani. Kwa hiyo, imani iliitangulia torati na ni sehemu ya
torati (Waebrania 11:28).
Hii ni muhimu
kwakuwa Waprotestant na wale wanaojiita Wakristo mamboleo wanakuja na wazo
kwamba torati ilikomeshwa na haina umuhimu tena na muhimu sasa imani na kuwa
ndivyo linavyofundisha Agano Jipya na kwamba liliondolea mbali umuhimu wa
matendo. Zaidi ya yote wanaamini kwamba imani katika Yesu Kristo ndicho kitu
pekee kinachohitajika na kwa njia ya imani katika Yesu Kristo wataokolewa. Hili
lina sehemu tu ya ukweli.
Andiko muhimu
ambalo ambalo maranyingi wanalitoa kujifariji hivyo ni Waebrania 6:1 kwa ajili
ya wito wake wa kuwataka watu wazitubie kazi zao mfu. Andiko hili linasomeka
hivi kwa mwonekano wake.
Waebrania 6:1-12 Kwa
sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo
ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na
uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa
mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya
milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia. 4 Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa
cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, 5 na
kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, 6 wakaanguka
baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa
wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa
dhahiri.
Andiko hili
linawahusu wale walio sehemu ya wateule, waliompokea Roho Mtakatifu na kisha
wakaanguka dhambini mbali na kweli ya Mungu. Haiwezekani kuwarejesha tena
kwenye ukweli. Wanakwenda kwenye ufufuo wa pili.
7 Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea
mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao
yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;
Ikiwa kama wewe
umehesabiwa (umeandaliwa) na kupewa Roho Mtakatifu, basi hiyo ni Baraka toka
kwa Mungu.
8 bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na
kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa. 9 Lakini,
wapenzi, ijapokuwa twanena hayo, katika habari zenu tumesadiki mambo yaliyo
mazuri zaidi, na yaliyo na wokovu.
10 Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na
pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu,
na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia. 11 Nasi twataka
sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini
hata mwisho; 12 ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi
wa hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu.
Hili ni jambo
lililo wazi sana. Hupaswi tena kuendelea kujifunza mafundisho ya awali.
Mafundisho ya awali ya Kristo ni toba ya kuzitubia kazi na matendo mafu na
yasiyo na maana, imani kwa Mungu na maelekezo juu ya umuhimu wa torati, ufufuko
wa wafu na hukumu ya milele. Haya ni sawa na maziwa. Bali sisi tunaenda mbele
na mbali zaidi kuyaangalia mambo makuu. Hii haina maana kuwa kazi au matendo
vimekufa na kwamba vinapaswa kuondolewa mbali kabisa kutoka kwenye umuhimu
wake.
Dhana iliyoko hapa
ni kututaka kuyatubia matendo maovu na yasiyo na maana. Hata hivyo, andiko hili
linawapeleka Wakristo hadi kwenye kiwango cha juu cha pande mbili za mafundisho
ya awali. Kwa hiyo kiwango cha ukuaji ni zaidi ya uelewa au hisia za kawaida za
kuzitubia kazi na matendo yasiyofaa. Kumbuka kuwa kinachosemwa hapa ni
kuzitubia kazi zisizofaa na sio kuyatubia matendo (sawa na Wagalatia 5:19-22).
Ni opotovu mkubwa wa kifasiri kuamini kwamba kazi zote zimekufa na hazifai.
Hiyo sio sahihi kabisa.
Hili ni kosa
kufikiri hivyo kuhusu jambo hili. Unapokuwa unampokea tu Roho Mtakatifu na
ukaweka bega lake kwenye gurudumu na ukahesabiwa kwenye jeshi la Mungu, basi
huruhusiwi kuendelea tena kuishi dhambini. Hili sio tu suala la kusema kwamba
"Nitaubeba msalaba wangu tena; na nitautua chini na kumzika baba yangu, au
nitamjaribu punda wangu; au nitafanya kitu fulani kingine na kisha nitaubeba
unapowezekana kufanya hivyo”. Hivyo sivyo imani hii inavyotakiwa kuwa.
Unapojiorodhesha kwa shughuli za kulima shamba hadi kufikia kuchwa kwa jua na
ukaitwa kwa wakati ule ule. Mfano wa wakulima walioajiriwa shambani
unatuonyesha kwamba wote walilipwa mshahara wa namna moja, ni swa kama ulivyo
wokovu wetu. Bali wote walifanya kazi na kulima hadi kuchwa kwa jua, hadi
mwisho wa siku. Ni jambo sawa na Yule anayeitwa amechelewa, bali wote walifanya
kazi pamoja tangu wakati walioitwa shambani. Ikiwa utaliacha shamba hutaweza
kulipwa ujira wako.
Matokeo ya
mwisho ya jambo hili yamo kwenye 1Wakorintho 5:5 – utolewe kwa adui na mshitaki
wako ili kwamba maisha yako yaokolewe siku ya mwisho. Hii ndiyo hukumu.
Unakwenda kwenye ufufuo wa pili. Mtu anahitaji kufanya toba kutokana na msimamo
wa kushikilia kuwa na Kristo na imani pekee iliyo kama dhana fikirika tu. Tuna
kazi ya kufanya na sote tunawajibika tuihitimisha kazi hii kwa kiwango
tunachoweza kukifikia. Baadhi yetu tumekirimiwa uwezo zaidi waliopewa wengine.
Baadhi yetu tuna uwezo na vipaji vya aina mbalimbali. Baadhi yetu tuko mahiri
na uwezo mkubwa katika maombi na kufunga saumu. Wengine wamekirimiwa vipawa vya
aina nyingine mbalimbali. Lakini sisi sote tumeitwa kufanya kazi tukiwa kama
washiriki wa mwili mmoja na kichwa chetu ni Yesu Kristo. Ni muhimu kukumbuka
kwamba kichwa cha kanisa ni Yesu Kristo na kufikiri vingine mbali ya hivi ni
uwongo.
Sura
iliyowaorodhesha mashujaa wa imani katika Waebrania 11 ni ya muhimu sana katika
kuonyesha jinsi imani ilivyokuwa inashikwa na jinsi watu walivyoiendeleza
imani. Hili sio wazo tu lililo kwenye Agano Jipya peke yake. Agano Jipya liko
wazi kabisa katika kuitilia mkazo imani kutoka kwenye ulimwengu halisia.
Webrania 11:1-39 inasema: Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni
bayana ya mambo yasiyoonekana. 2 Maana kwa hiyo
wazee wetu walishuhudiwa. 3 Kwa imani
twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu
vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri. 4 Kwa
imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo
alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo,
ijapokuwa amekufa, angali akinena. 5 Kwa imani
Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu
alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza
Mungu. 6 Lakini pasipo imani
haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba
yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao. 7 Kwa
imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado,
kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuokoa nyumba yake. Na hivyo
akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
Nuhu alionywa
juu ya mwisho wa zama aliyokuwa anaiishi na alianza kujenga safina. Ilimchukua
kipindi cha zaidi ya miaka mia na aliambulia kejeli na dhihaka kutoka kwa watu
wote waliokuwepo katika kipindi kile. Tumepewa kitabu cha Ufunuo baada ya
kuondoka kwake Yesu Kristo kikikusudia kutupa maonyo ya siku za mwisho.
Mwishoni mwa zama hizi tunazoishi kuna ishara za uhakika na kwa imani
tunatarajia kurudi kwa Masihi na pia kufikia kikomo cha zama hizi. Na ndivyo
ilivyokuwa kwa manabii walioishi zama za kabla ya kutolewa kwa Ufunuo, walitoa
maonyo kuhusu kuja kwa Masihi nay a mwisho wa dunia. Nasisi pia tumo kwenye
mzingiro huo huo wa wenye kutukejeli na kutudhihaki kwa ajili ya kuamini hivi.
Watu wengi zaidi na zaidi wanaojiita kuwa ni Wakristo wanasema kwamba Bwana
amechelewa kurudi. Na wengine wengi sana wataachana na imani na mafundisho
ya kurudi kwa Masihi na kuongeza tena na tena siku na tarehe. Kitu cha hatari
zaidi kinajitokeza hapa, na kile wanachoweza kukifanya kuwafanya watu waachane
na matumaini ya kurudi kwa Masihi. Kinachopiganiwa zaidi hapa ni kile
kinacholingana na juhudi za kuwasahaulisha watu kuhusu kurudi tumaini hili. Ni
hadi pale tu watakapo kabiliwa na uharibifu au maafa makubwa yatokanayo na
uharibifu na maangamizo, na ndipo watakapojirudi na kuanza kuomba kurudi kwa
Masihi. Ni watu wachache sana wanaomba ombi la Ufalme wako uje kwa sasa.
8 Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali
pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 9 Kwa
imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake,
akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile
ile. 10 Maana alikuwa akiutazamia mji wenye
misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu. 11 Kwa
imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimba; alipokuwa amepita
wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeahidi kuwa mwaminifu.
Mungu alimpa
Sara ahadi. Ingawaje alikuwa kwenye kipindi cha umri ulio zaidi na ule wa mtu
kuzaa mwana, bali yeye alizaa. Aliweza kumtimizia ahadi hii.
12 Na kwa ajili ya hayo wakazaliwa na mtu mmoja, naye
alikuwa kama mfu, watu wengi kama nyota za mbinguni wingi wao, na kama mchanga
ulio ufuoni, usioweza kuhesabika.
Ndipo uzao wa Ibrahimu
ulikuwa mwingi kama nyota za mbinguni. Walizidi kuenea hadi kufikilia Yuda.
13 Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi,
bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni,
na wasafiri juu ya nchi. 14 Maana hao
wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe. 15 Na kama
wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea. 16 Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora,
yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana
amewatengenezea mji.
Utafutaji huu
kwa kweli ni wa uzungukaji wa dunia, katika kumngija Mungu aushushe Yerusalemu
mpya hapa chini na kuipatanisha sayari yetu hii na watakatifu wake kutoka
mbinguni. Mafundisho na matumaini haya kwa sasa vimo kwenye mashambilizi
makubwa na jamii za ulimwengu huu—yaani ukweli wa kwamba Wakristo wajione kuwa
ni wapitaji na watumwa hapa ulimwenguni.
17 Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe
dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa
pekee; 18 naam, yeye
aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa,
Mungu alitoa
tamko hili, na kwamba Ibrahimu aliamriwa kabisa na wajumbe wa Mungu (Malaika wa
Mungu) kuahirisha mchkato ule.
19 akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka
kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano.
Kwa hiyo
Ibrahimu alikuwa na imani kubwa kiasi kwamba hata kama Mungu angemwambia amuue
mwana wake, alijua kwamba alikuwa na uwezo wa kumfufua tena na kuwaita wazao wa
dunia hii kupitia kwa Isaka. Alikuwa na ujasiri usio na shaka na imani kamilifu
kwamba hata kama Mungu angemuamuru amtoe mwana wake ili afe, ni kwamba angeweza
kumfufu tena mwana wake. Hili ni tendo la hatari sana katika kuitendea kazi
imani. Watu wengine hawana hata imani ya ile ndogo ya kuihatarisha kazi yao,
kwa juhudi ya kumtafuta au kumuishia Mungu wa kweli, achilia mbali kuwaambia
wawatoe watoto wao.
20 Kwa imani Isaka akawabariki Yakobo na Esau, hata katika
habari ya mambo yatakayokuwa baadaye. 21 Kwa
imani Yakobo, alipokuwa katika kufa, akambariki kila mmoja wa wana wa Yusufu,
akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.
Na hii ndiyo
maana aliwabarikia Efrraimu na Manase. Baraka hizi walipewa watu wetu kwa njia
ya imani, wakujua kwamba zitatimilika na zilitimilika. Baraka walizopewa wana
wa Yusufu zilitimilika miaka takriban elfu tatu (au zaidi) baada ya kifo cha
mababa yao. Hii inamaanisha kwamba ni zaid ya miaka elfu tatu tangia kifo cha
Yakobo, kabla Baraka kamili hawajaziona wakipewa hawa Efraimu na Manase. Hata
sasa hazijaonekana kikamilifu, kwa kuwa Masihi hajawapa Baraka kamili ambazo ni
za amani na za haki ya mzaliwa wa kwanza.
22 Kwa imani Yusufu, alipokuwa amekaribia mwisho wake,
alitaja habari za kutoka kwao wana wa Israeli, akaagiza kwa habari ya mifupa
yake.
Yusufu aliomba
wamchukue na kumrejesha hadi nchini Israeli ili wakamzike huko. Alijua kwamba
watu wake walikuwa utumwani kama watumwa tu huko Misri kama taifa, na tena
alimpa maelekezo mwanawe kwamba watarejea tena nchini Israeli na watamzika yeye
huko kipindi watakachotoka huko maarufu kama cha Kutoka. Haya yote yanatokana
na uelewa wa unabii na kuielewa imani. Haya ni matendo na kazi ya Roho
Mtakatifu ambaye ndiye aliyekuwa anatenda kazi miongoni mwa watu hawa,
akiwaambia yale yaliyokuwa yanakuja kutokea na kutimilika katika siku
zilizokuwa mbele yao. Mambo haya yote yako mbali sana kutimilika. Sura hii
inayoelezea imani ina maana nay a muhumu sana.
23 Kwa imani Musa, alipozaliwa, akafichwa miezi mitatu na
wazazi wake, kwa sababu waliona kwamba ni mtoto mzuri; wala hawakuiogopa amri
ya mfalme. 24 Kwa imani Musa
alipokuwa mtu mzima, akakataa kuitwa mwana wa binti Farao; 25 akaona
ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika
dhambi kwa kitambo; 26 akihesabu ya kuwa
kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa
aliyatazamia hayo malipo.
Huyu ni nabii
Musa ambaye anapitia mashutumu makubwa kwa ajili ya Masihi. Utawezaje
kumtenganisha Musa na matendo yake kumhusu Masihi, wakati Agano Jipya linaeleza
kwa wazi sana kwamba mateso na mashutumu aliyoyapitia Musa huko Misri yalikuwa
ni kwa ajili ya Masihi. Alifanya yote haya kwa niaba ya Yesu Kristo. Nili ni
fundisho la muhimu na lenye nguvu sana.
27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme;
maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana. 28 Kwa
imani akaifanya Pasaka, na kule kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza
wazaliwa wa kwanza asiwaguse wao. 29 Kwa imani
wakapita kati ya Bahari ya Shamu, kama katika nchi kavu; Wamisri walipojaribu
kufanya vivyo wakatoswa. 30 Kwa imani
kuta za Yeriko zikaanguka, zilipokwisha kuzungukwa siku saba. 31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba,
hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa
amani. 32 Nami niseme nini
tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni
na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; 33 ambao
kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi,
walifunga vinywa vya simba, 34 walizima nguvu
za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu,
walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni. 35 Wanawake
walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa,
wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora; 36 wengine
walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa
misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi
za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya; 38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa
nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika
mapango na katika mashimo ya nchi. 39 Na watu hao
wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi; 40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia
kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.
Mambo mawili na
ya muhimu kwenye andiko hili ni:
1. Imani ilikuwa ni kitu cha muhimu sana katika kuzitii sheria na kanuni za
Mungu; na
2. Licha ya kuwa walikuwa na imani kuu hivi, bali hawakuweza kuzifikilia na
kuzipata ahadi. Hivyo ni kwamba imani peke yake haimpi hakikisho mtu la wokovu.
Hicho ndicho
kigezo kikubwa cha matendo. Kuna mlolongo wenye masharti wa matendo
unaohitajika kuwanao wateule wote. Imeni ni kitu kimoja tu kuhitajika kwanza
ili kuupata wokovu. Vitu vingine ni toba na ubatizo kwa kupitia ndani ya mwili
na damu ya Yesu Kristo na kuanza kuzitunza amri za Mungu na kumpokea Roho
Mtakatifu kwa kuwekewa mikono na kuendelea kiimani katika roho. Masharti haya
yote yanaendana pamoja na ni ya muhimu. Imani yenyewe isipokuwa na matendo
imekufa. Wewe sio Mkristo kabisa kama utathani kwamba kwa imani peke yake
unaweza kuurithi Ufalme wa Mungu. Hutaweza kuurithi kwa namna hiyo peke yake.
Yakobo anasema
kwamba Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na
Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. (Yakobo 5:15)
Sababu ya kuandikwa kwa andiko hili kunahusiana na injili inayofundisha masuala
ya kiafya na ustawi na mafundisho yahusuyo magonjwa yatokanayo na maisha ya
dhambi ambayo pia yanahusiana na upotoshaji. Uponyaji
wa mtu binafsi yake kwa njia ya imani unajiri kwa mambo yote mawili, yaani
kimwili na kiroho na hivi ndivyo inavyotenda kazi. Hatuna shaka kabisa kuamini
kwamba magonjwa ni matokeo ya maadhi ya dhambi, lakini sio magonjwa yote
yanasababishwa moja kwa moja na dhambi alizozitenda mtu.
Huu ni ukweli
uliodhahiri. Dunia hii sasa imekuwa ni mahala pasipo na utulivu kwa kipindi cha
zaidi ya miaka elfu sita sasa ya utunzaji mbaya. Sio kweli kwamba unapokuwa
unaumwa basi umetenda dhambi. Na wala sio ishara ya kutokuwa na imani
tunapomshuhudia mtu akifa kwa ugonywa wa saratani.
Imani ni kitu
muhimu sana kwa ajili ya uponyaji, bali dhambi ni lile tendo la kuzivunja au
kuasi amri za Mungu (1Yohana 3:4). Kwa hiyo, imani inauhusino wa moja kwa moja
na sheria kwa ustawi wa kila mwanadamu (hususan ustawi wa kiroho). Kuna dhambi
nyingine zinazompelekea mtu kupatwa na hukumu ya kimwili. Kama ukichagua kuwa
mlevi basi unakabiliwa na adhabu ya kimwili kuibeba. Adhabu yenyewe ni ukweli
kwamba hutaweza kula vizuri na mfumo wako wa kimwili utadhoofika.
Uasi wa aina
yoyote ni dhambi (1Yohana 5:17). Haki na utakatifu ni mambo yaliyo sawa na
vinatokana na neno moja tu la Kiebrania (Zedek au Zadok). Kwa hiyo, maneno yote
haya; yaani haki na utauwa na imani yote yanahusiana kwenye torati yakisomeka
kama mwenye haki au mtauwa ataishi kwa imani (Habakuki 2:4 iliyonukuliwa kwenye
Warumi 1:17; Waebrania 10:38). Kwa hiyo imani ni ya muhimu ambayo kwayo wateule
watatembea katika utii au kumpendeza Mungu kwa kuzishika amri za Mungu. Hii
ndiyo muhimu ambayo kwayo mtu anatakiwa aendelee kuwa na imani, akiwa imara na
kujisimamia, na asiyumbe na kutoka nje ya tumaini la injili (Wakolosai 1:23).
Mtume Yakobo
analipanua suala la imani kwenye Yakobo sura ya 2. Chanzo cha tatizo
kinakutikana kusababishwa na hali ya kuwapendelea watu. Kitendo hiki cha kuwapendelea
watu fulani kimekuwa ni tatizo kubwa sana kwenye Makanisa ya Mungu kwa kipindi
cha karne kadhaa sasa. Mungu hana upendeleo (2Samweli 14:14) na ilikuwa
hivyohivyo kwa Kristo hakumpendelea mtu yeyote (Mathayo 22:16; Marko 12:14).
Yakobo aliliona tetizo hili na kuliandika kwenye waraka wake wa Yakobo 2:1 (kwa
sehemu akaandia kwa kutumia neno prosoopolempsiais linalomaanisha kuwaonyesha upendeleo au kuwaonea haya watu
tazama kwenye kamusi ya Marshall’s Interlinear) (sawa na ilivyoandikwa kwenye
jarida la Kuwapendelea Watu (Na221) [Respect of Persons
(No. 221)].
Yakobo
2:1-26 Ndugu zangu, imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe
nayo kwa kupendelea watu.
Kwa hiyo imani
ina namna nyingi mbalimbali (ni ya namna mbalimbali) au namna ambayo kwayo wewe
unaweza kuishikilia imani.
2 Maana akiingia katika sinagogi lenu mtu mwenye pete ya
dhahabu na mavazi mazuri; kisha akiingia na maskini, mwenye mavazi mabovu; 3 nanyi mkimstahi yule aliyevaa mavazi mazuri, na kumwambia,
Keti wewe hapa mahali pazuri; na kumwambia yule maskini, Simama wewe pale, au
keti miguuni pangu, 4 je! Hamkufanya hitilafu mioyoni
mwenu, mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu? 5 Ndugu
zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe
matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao? 6 Bali ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri
hawawaonei ninyi na kuwavuta mbele ya viti vya hukumu? 7 Hawalitukani
jina lile zuri mliloitwa? 8 Lakini mkiitimiza ile
sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako,
mwatenda vema. 9 Bali mkiwapendelea watu, mwafanya
dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji. 10 Maana
mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja,
amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema,
Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa
mvunja sheria. 12 Semeni ninyi, na kutenda kama watu
watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru. 13 Maana hukumu
haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.
Kwa maneno
mengine tunaweza kusema kwamba, kwa kadiri unavyohukumu wengine ndivyo na wewe
utakavyohukumiwa. Ukihukumu bila huruma na kama unakuwa mkali kwa wengine na
kama ukiwa ni mtu mwenye hasira ya karibukaribu na ikiwa unawachukulia hatua
kuwahukumu wengine kirahisirahisi, ndivyo vivyohivyo watu wale
watakavyokushughulikia wewe. Ndivyo hivyohivyo wale watu watakavyokukasirikia
na kuchukizwa na kukuchukulia hatua wewe na kukutendea wewe kwa mintaarafu
ileile uliyowatendea wengine. Mungu anautumia utaratibu huu ili kukurudi wewe
na kukurejesha kwake, anapokuwa anakushughulikia wewe.
Watu wanaosimama
kwenye kazi ya Mungu, au wanaojaribu kuyageuza mambo yaliyokusudiwa ya matendo
ambayo Mungu ameyafundisha, yafanyike hivyo. Anauwezo wa kuwaondoa watu na
anauwezo pia wa kuwaua. Kuna sababu za muhimu sana. Ni jambo la kutisha
kuangukia kwenye mikono ya Mungu aliyehai. Mambo yanayofanywa kwa Baraka au
pasipo na Baraka zake Mungu. Kama yanafanywa na Baraka zake Mungu na kama
unaifanya kazi ya Mungu, basi usijaribu kamwe kuiharibu kazi ya Mungu, kwa kuwa
unapigana na Mungu na atakushughulikia.
Uhusiano kati ya
imani na maingiliano yake na sheria vinaonekana kwenye maandiko haya (Yakobo
2:1-13). Cha umuhimu zaidi anachoonyesha hapa ni ubaya mkubwa uliopo kwenye
tabia hii ya kuwapendelea watu, kuwa inaonekana pia kwamba ni ukiukaji wa haki
na hivyo inakuwa ni dhambi au uovu. Hakutakiwi kuwepo na tabia hii ya
kuwapendelea watu kwenye Kanisa la Mungu.
Mtume Yakobo anakwenda mbali zaidi kwa kufananisha uhusiana uliopo kati
imani na matendo ambavyo anavielezea kwenye maandishi haya.
14 Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo
imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? 15
Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na
riziki, 16 na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu
kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa
nini? 17 Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa
nafsini mwake. 18 Lakini mtu atasema, Wewe unayo
imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami
nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu. 19 Wewe
waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na
kutetemeka. 20 Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu
usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai? 21 Je!
Baba yetu Ibrahimu hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka
mwanawe juu ya madhabahu? 22 Waona kwamba imani
ilitenda kazi pamoja na matendo yake, na ya kwamba imani ile ilikamilishwa kwa
njia ya matendo yale. 23 Maandiko yale yakatimizwa
yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye
aliitwa rafiki wa Mungu. 24 Mwaona kwamba mwanadamu
huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. 25 Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa
kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia
nyingine? 26 Maana kama vile mwili pasipo roho
umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.
Yakobo sura ya 2
inaungana mkono na Waebrania sura ya 11. Imani na matendo vinakwenda pamoja.
Tendo hilohilo ndilo linatakiwa kufanyika hata leo..moja ni lile la imani na
jingine ni la matendo. Matendo yenyewe yanatuama kwenye imani.
Kwa hiyo imani
iliendana na matendo hata kabla ya Musa na Ibrahimu na Ibrahimu alihesabiwa
haki kwa matendo yake. Imani ilionekana kwa matendo yake na imani inakamilika
kwa matendo. Imani pasipo matendo imekufa. Imuhimu wa sheria ni kwamba amri kuu
nay a kwanza inashikwa kwa njia ya imani na kwa kupitia matendo haitenganishwi.
Kuilinda kwa bidii amri ya kwanza miongoni mwa nne za kwanza, utaona kwamba
amri kuu ya kwanza inahusu kumpenda Mungu ndivyo inavyosisitiza.
Jambo la nne la
muhimu kulijua katika kumuabudu Mungu ni utunzaji wa Sabato na hili ni jambo la
muhimu sana. Hili ni jaribio linaloweka ufafanuzi wenye kutambuliwa kuwa
unamuabudu Mungu mmoja na wa kweli. Amri ya kuishika Sabato ni amri ya jaribio
miongoni mwa amri kuu na ya kwanza. Tunapaswa tukumbuke hivyo sisi sote. Na hii
ndiyo sababu watu wengi wanaipinga sana; na kwa nini waamini Utatu wanajikuta
kuwa ni vigumu sana kuishika amri hii.
Wakati kwamba
amri hii kuu na ya kwanza inaweza kushikwa kwa imani miongoni mwa hizi tatu za
kwanza, matendo ni ya muhimu katika kuishika amri hii ya nne. Zaidi sana kwamba
amri kuu ya pili inayosisitiza kumpenda jirani yako, inaonekana kwa njia ya
matendo tu na ndiyo maana imani bila matendo imekufa.
Neno lililorudiwarudiwa la Usifanye ni la kinyume au makatazo
kwenye amri hizi kumi, bali kuna mambo yanayoruhusiwa au kuagizwa yatendwe pia.
Amri ya tano na ya kumi ni amri zenye ahadi na zina mambo mazuri ndani yake.
Amri ya kwanza pia ni amri yenye ahadi ndani yake. Amri ya kumi inayosema Usitamani
inahusika na nia ya moyoau mawazo ya mtu. Unapaswa kuwa na mawazo chanya ili
uweze kuishika amri hii ya kumi, jambo litakalokusaidia hatimaye uweze kuishika
sheria nyingine ya kumpenda jirani yako. Mungu hana upendeleo (Matendo 10:34;
Warumi 2:11) na wala hampendelei mtu anapotoa hukumu zake (Mithali 24:23) kwa
liwa sio vizuri kufanya hivyo (Mithali 28:21) na kwa hiyo imani bila matendo
kutamzuia mtu yeyote kuuingia ufalme wa mbinguni. Kitu muhimu ili kuuingia
Ufalme wa Mungu uitii kwa njia ya imani katika Yesu Kristo, na sio kwa imani
katika Yesu Kristo tu pasipo kujali suala la utii.
Ikiwa una imani
katika Yesu Kristo, basi ziti amri zake sasa. Ikiwa unataka kuwa na Roho
Mtakatifu, basi zitii amri za Mungu sasa. Utii wa wateule unaonekana kwa
kuzitii amri za Mungu. Hebu mtii Mungu na kuzishika amri zake (Mhubiri 12:13).
Hata amri iliyondogo sana haipaswi upuuziwe ama ivunjwe (Mathayo 5:19). Ikiwa
tunataka kuingia uzimani, basi tunatakiwa kuzishika amri zake (Mathayo 19:17).
Mathayo 19:16-22 inaonyesha umuhimu na nia ya amri za Mungu.
Mathayo 19:16-22 16 Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu,
nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? 17 Akamwambia
Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia
katika uzima, zishike amri. 18 Akamwambia, Zipi? Yesu
akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, 19
Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi
yako. 20 Yule kijana akamwambia, Haya yote
nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? 21 Yesu
akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini,
nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. 22 Yule
kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na
mali nyingi.
Nia yake ni
kwamba tunapaswa kujitoa sadaka kwa kusaidiana na kwa matendo. Tukisema kwamba
tunampenda Mungu na huku tukiwa hatutendi jambo lolote, ndipo tutakuwa
hatuishiki imani na hatutaweza kabisa kuuingia Ufalme wa Mungu. Inatunapasa
kujitoa mhanga kwa ajili ya Ufalme wa Mungu na kumfuata Kristo. Kumbuka kuwa
maneno matupu na yasiyo na matendo hayana maana.
Waraka kwa
Waefeso unakazia kwenye fundisho lake kuu kuwa ni utii kwa Mungu na kuvumilia
mateso hapa duniani, na kile ambacho ulimwengu huu wa sasa unakita kuwa utawala
usiozingatia haki.
Waefeso 6:1-20 inasema: 1 Enyi watoto, watiini wazazi
wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. 2 Waheshimu
baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, 3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia. 4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni
katika adabu na maonyo ya Bwana. 5 Enyi watumwa,
watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa
unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo; 6 wala
si kwa utumwa wa macho tu kama wajipendekazao kwa wanadamu bali kama watumwa wa
Kristo, mkitenda yampendezayo Mungu kwa moyo; 7 kwa
nia njema kama kumtumikia Bwana wala si mwanadamu; 8 mkijua
ya kuwa kila neno jema alitendalo mtu atapewa lilo hilo na Bwana kwamba ni
mtumwa au kwamba ni huru. 9 Nanyi, akina bwana,
watendeeni wao yayo hayo, mkiacha kuwaogofya, huku mkijua ya kuwa yeye aliye
Bwana wao na wenu yuko mbinguni, wala kwake hakuna upendeleo. 10 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza
wa nguvu zake. 11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate
kuweza kuzipinga hila za Shetani. 12 Kwa maana
kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka,
juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa
roho. 13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu,
mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa
dirii ya haki kifuani,
Idadi hii ya
silaha inamaana sana. Zinahusu maandalizi ya kuzibeba zilaha za Bwana
zinazotokana na kweli. Ngao ya silaha hizi zote ni kweli. Haitakiwi kuwe na
uganganifu kwenye kile unachokifanya; wala kusiwe na hila na kusiweko na
kujidanganya mwenyewe.
15
na kufungiwa miguu
utayari tupatao kwa Injili ya amani; 16 zaidi ya yote mkiitwaa
ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule
mwovu.
Kazi kubwa
uliyotupiwa ni kutokubaliana na mashambulizi yahusuyo imani yako; imani ambayo
kwayo sisi tumefanyika kuwa ni sehemu ya mwili wa Yesu Kristo; ambayo kwayo
tunaifanya kazi ya Mungu, ambayo tunaongoizwa na Roho Mtakatifu na ambayo kwayo
sisi tunaunena ukweli na jinsi unavyotakikana kuwa. Haya yote yanaanzisha
mabishano. Njia pekee ambayo adui wetu anaipata kwako ni kutoka kwa watu walio
karibu nawe ambao kwao anaweza kuwatumia kukushutumu wewe. Atafanya hivyo kwa
kupitia kwa watu wanaojidhania kuwa wao ni watakatifu.
17
Tena ipokeeni chapeo
ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
Kofia ngumu ya
kichwani ya wokovu hulinda kichwa chako. Neema iokoayo ya Jesu Kristo inalinda
mawazo yako pia. Umepewa fursa ya toba, ambayo kupitia kwa kuielewa dhimbi
kunatupelekea hukumu. Kisha kwa ajili ya kujisikia kuhukumiwa moyoni ndipo
tunafikilia kutubu kwenye neema iokoayo ya Yesu Kristo. Ukamilifu wa dhabihu ya
Kristo ndiyo ngao ya wokovu.
Silaha
tunayoizungumzia ni neno la Mungu. Huu ndiyo upanga ukatao kuwili tulionao
mikononi mwetu. Na hii ndiyo maana tunaweza kuwashughulikia watu hawa ambao
wanaiyumia vibaya. Ni silaha zetu na sio zao, kwa kuwa yale wanayoyasema
hayawezi kustahimili, wakati yanapojaribiwa.
18
kwa sala zote na
maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu
katika kuwaombea watakatifu wote; 19 pia na kwa ajili
yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri
ile siri ya Injili; 20 ambayo kwa ajili yake mimi ni
mjumbe katika minyororo; hata nipate ujasiri katika huyo kunena jinsi
inipasavyo kunena.
Maombi haya
yanapaswa yaombwe na kila mmoja anayeliitia jina la Yesu Kristo, na kunenwa
katikati ya wateule wanaozihubiri siri za Injili.
Wazo
linaloshinikiziwa hapa ni kwamba malaika walioasi ndiyo msingi au sababu ya
vita tunayoendelea kupigana nayo. Mamlaka na nguvu hizi zimeanzisha mfumo usio
wa haki. Imani ndiyo moja ya kitu muhimu katika silaha za Mungu. Silaha kuu ni
upanga war oho ambao ndio neno la Mungu. Kwa hiyo, Biblia na hasa Maandiko
Matakatifu ya Agano la Kale yalikuwa ndiyo silaha kuu ya wateule. Umuhimu wa
kukesha ni kitu muhimu sana. Adui anatafuta fursa ya kuwapotosha wateule kwa
mafundisho ya uwongo yanayolenga kufutilia mbali umuhimu wa kuzishika sheria na
amri za Mungu na kuwadanganya wateule kama ikiwezekana. Ili kufanikisha hilo
wanajaribu kuzibadili amri za Mungu na mahala pake kufidia amri za wanadamu
(Mathayo 15:9; Marko 7:7). Tunamjua Mungu kwa kuzishika amri zake (1Yohana
2:3). Kama mtu yeyote atasema kuwa anamjua Mungu na huku akisema kuwa sio
muhimu kuzishika amri zake basi yeye ni mwongo na kweli haimo ndani yake
(1Yohana 2:4). Na yeye hayumo kabisa miongoni mwa wateule.
1Yohana 2:1-6 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili
kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba,
Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye
kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za
ulimwengu wote. 3 Na katika hili twajua
ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake. 4 Yeye
asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani
yake. 5 Lakini yeye
alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli.
Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake. 6 Yeye
asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama
yeye alivyoenenda.
Tunatembea kwenye mapito aliyoyapitia Kristo na tunazishika amri za Mungu na
kwa hiyo tunaonyesha upendo wetu kwa Mungu katika Kristo. Kwa kutembea kwenye
mapito aliyoyapitia Kristo ndipo upendo wetu kwa Mungu unakamilika.
Tusidanganyike
na mabishano yanayotafuta kuzipunguza amri kwa Usemitism. Waalimu kama hawa wa
uwongo wanafundisha mafundisho ya mapepo na mashetani. Na hakuna nuru kwao
(Isaya 8:20).
q