Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[089]

 

 

 

Mafundisho ya Kizushi Kwenye Kanisa la Mitume

 (Toleo La Edition 2.0 19950128-20000311)

Jarida hili linashughulikia sababu za kijipenyeza kwa mafundisho ya uzushi kwenye makanisa ya Wakolosai na Wagalatia. Kwa kweli   hii ni sehemu ya mlolongo wa majarida ya mafundisho ya Sheria ya Neema na inashugulika na nafasi ya Sheria au Torati kwa mujibu wa Mtume Paulo. Andiko linaendelea mbele kwa kuendeleza nafasi yake kwenye Makanisa yaliyosimamiwa na Mtume Yohana. Mafundisho ya Wanostiki yamechambuliwa pia. Nafasi ya kanisa la karne ya kwanza kuhusu Masihi ya Ujio wake mara mbili pia imechambuliwa kutokana na ushahidi wa Gombo zililogunduliwa kwenye Bahari ya Chumvi. Nafasi ya Paulo inaonekana kuwa imekosewa kiuandishi na waorthodoxi wa siku hizi. Jarida hili linashughulika na jarida linalofuatia la Tofauti Iliyo Kwenye Torati (Na. 96) na Mandiko ya Matendo ya Sheria-au MMT (Na. 104).

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1995, 2000 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mafundisho ya Kizushi Kwenye Kanisa la Mitume


 


Kumbuka: jarida hili yapasa lisomwe sambamba na kanda ya tepu.

 

Utangulizi

Vitabu vya Wakolosai na Wagalatia vinachukuliwa kuwa na idadi kadhaa ya mambo ya kimafundisho yasiyo sahihi kuhusu Agano Jipya. Miongoni mwa mambo mengine, ushindaniau mabishano ya sheria unaondolewa mbali ukituama kwenye kuubiri ni makosa. Mabishano makubwa kuhusu kosmolojia sahihi ya Agano Jipya yanahitaji kuendelezwa. Mafundisho ya Uzushi kwenye Kanisa la Mitume yangeweza kuunda sura ya kazi ile.

 

Historia ya Mambo Yaliyopita

Kanisa la Mitume lilikabiliwa na mlolongo wa matatizo wakati wa uchanga wake. Makanisa mengi miongoni mwa yale tuliyonayo kwenye rekodi ya Biblia yalianzishwa na au chini ya Mtume Paulo kwa kuwepo kwake. Matendo mengine kama vile wale watu wa Korintho walijiunga na matendo ya kawaida ya kimwili, ambayo yalikuwa yamepotoshwa au kudunishwa na hali ya halisi ya kiroho ya Kanisa. Matatizo mengine yalikuwa yamejikita sana na yaoonekana kuwa hayajamalizika kabisa na kueleweka. Hii inaonekana kuwa ilitokea kwa sababu ya kosmolojia iliokuwa imekubalika na Makanisa ya Agano Jipya hayakueleweka vyema na teolojia ya kipindi cha kabla ya mtaguso wa Nikea. Waraka kwa Wakolosai ni wa muhimu sana kwa ajili ya kuielewa kosmolojia ya Kanisa la Agano Jipya.

 

Andiko linguine la muhimu, lakini kwa upana mdogo, ni lile la Wagalatia. waraka kwa Waebrania ni andiko muhimu na la maana sana kuhusu uhusiano mtambuka uliopo kati ya Agano la Kale na Jipya na kosmolojia yake. Kwa kuyajua makosa ambayo kwayo makanisa haya yaliangukia tunaweza kuelewa vyema juu ya kosmolojia yake asilia. Wakati maandiko yanapotathiminiwa tunaweza kuona kiusahihi sana kuhusu jinsi makosa haya yalivyo, na kwa zaidi sana, tunaweza kujua jinsi yalivyotokea.

 

Wakolosai

Asili ya Andiko

Makosa na uzushi wa kimafundisho wa Wakolosai yalikuwepo--yaliandelea na kutoonekana kwa kipindi kirefu kwa msingi wa kukubalika kwa uelewa kuwa Wakolosai waliyachukua na kuyaendeleza au kuyakumbatia kutoka kwenye imani na mafundisho ya Wanostiki, ambayo hayakuweza kubuniwa au kutungwa vizuri na kikamilifu kutokana na maandiko.

 

Makosa haya yalidhaniwa kuwa yalihusika pia kuwa ni sehemu ya uhafidhina. Hii ilitokana na kutoelewa au kuelewa vibaya maneno yaliyotumiwa na Mtume Paulo kwenye maandiko au uandishi wake. Muono na mtazano wa Paulo kwenye andiko lenye dhana na lengo hilo ni la kificho na inahitaji kutathiminiwa na kuandikwa upya.

 

Wakolosai 2:8-10,16 inaeleza kuhusu dhana au nadharia ifuatayo:

·      mapokeo (B"DV(@F4<) [paragosin] (2:8);

·      ukamilifu (B8ZDT:") [plerõma] (1:9; 2:9,10);

·      filosofia (N48@F@N4") [philosophia] (2:8);

·      kula na kunywa ($DfF,4, B`F,4) [brõsei, posei] (2:16);

·      falme na mamlaka (•DP"4, ¦.@LG4"4) [archai, ezousiai] (2:15); na

·      mambo mengine ya duniani (FJ@4P,Ä" J@Ù 6`F:@L) [stoicheia tou kosmau] (2:8,20).

 

Maneno haya yanakutikana yakitumika pia kwenye imani ya Wanostiki wa Kiyahudi na kwa Wahelekini wa mrengo wa Kisynkretism. Kwa mujibu wa Bacchiocchi (kitabu chake cha From Sabbath to Sunday: A Historical Investigation into the Rise of Sunday Observance in Early Christianity, Appendix, pp. 343f. [Kutoka kwenye Sabato hadi Jumapili: Udadisi na Utafiti wa Kihistoria Kuhusu Kuinuka au Kuanza kwa Maadhimisho ya Jumapili kwa Wakristo wa Zamani]) anasema kuwa maneno haya ni

Yalitumika sawasawa na wafafanuzi katika kuelezea au kufafanua utohoaji wa maneno haya kytoka kwenye imani ya Kinostiki ya Wakolosai.

Bacchiocchi anaweka rejea maandiko ya Jacques Dupont, E. Percy, Lightfoot na Lyonnet na kuwafanya kuwa ni wanazuoni wa mfano waliouelezea uzushi kuwa ni mtindo wa Unostiki wa Kiyahudi. Kwa namna nyingine, Günther Bornkamm kwenye kitabu chake cha “The Heresy of Colossians” in Conflict at Colossae, [yaani “Mafundisho ya Kizushi ya Wakolosai” Yanavyopingana Kinyume na Wakolosai], p. 126 anasema kimtazamo wa ndani sana:

Bilashaka inaonekana kuwezekana kwangu hata hivyo, kwa upande mwingine. Mafundisho ya Wakolosai kuhusu vitu vinavyohusiana na imani za kizamani za kale na nadharia ya Kiteolojia ya Aeon-wa mashariki, ambayo yalikuwa yameenea sehemu zote na kuaminika kiutendaji na imani ya Waeleniki wa mrengo wa kisynkretism; sawa na alivyoandika na kuamini Ernst Lohmeyer, kwenye kitabu chake cha Der Brief an die Kolosser, 1930, pp. 3 f.; M. Dibelius, An die Kolosser, Epheser, An Philemon, 1953, excursus on 2:8, and 2:23. (Bacchiocchi, fn. to p. 343.)

 

Bacchiocchi anaendelea mbele kwenye pango kitita kwa kusema kuwa

Wengine wanatafsiri mafundisho haya ya kizushi ya Wakolosai kuwa kama usynkretism ya Kiheleniki na nasaba za Kiyahudi; soma kitabu cha Edward Lohse, cha A Commentary on the Epistles to the Colossian and to Philemon, yaani Ufafanuzi wa Waraka kwa Wakolosai na Filemoni 1971, pp. 115-116; Norbert Hugedé, Commentaire de l'Épître aux Colossiens, pp. 9, 143; W. Rordorf, Sunday, p. 136: 'Sisi kwa kweli tunashughulika na uwezekano wa mkondo wote mzima wa kisynkretistiki ambayo kwayo matirio za Wakristo wa Kiyahudi yamekuwa na mwingiliano kwa ndani zaidi na mafundisho ya walio wa jamii ya Kiheleniki na uthibitisho wa kimashariki'; sawa kama na asemavyo Handley C.G. Moule, kwenye kitabu chake cha Colossian Studies, 1898, aliyeelezea mafundisho ya kizushi kuwa ni kama ni 'mchanganyo wa mafundisho ya Kiyahudi na Unostiki, kwa rejea pana wa neno la baadae.'

 

Uelewa unaweza kuchambuliwa kutoka kwenye waraka na kosmolojia ya rejea za Agano Jipya hususan kwenye Ufunuo na kwa kusababishwa au kufanywa upya tena kwenye mlinganisho uliofanywa uliofanywa hapa kwenye sura ya 2, 3 na 4 [Alioufunua Mungu]. Mara tu kosmolojia ya biblia inapoeleweka, sababu ya asili ya tatizo huko Kolosai ilisahihishwa kwa namna iliyoonyeshwa kwamba Kanisa la huko Kolosai lilikuwa linakosea au linapotoka na kwamba upotoshwaji wao yalitokana na kutoelewa vizuri kwa sehemu ya kanisa kwa mtazamo mpana ambalo halikuwa ni kwa ajili yao wenyewe kuchukua jukumu la kukanusha au kuyapinga. Kwa hiyo tunakabiliwa na upotoshaji na makosa ya utenda kazi wake zaidi ya kuwa tu ni muigo mzima wa pamoja. Kutajwa kwa teolojia ya Aeon kulikofanywa na Bornkamm ni ishara au alama au nembo kubwa na muhimu kwenye mshangao. Teolojia inayojulikana kama ya aeon inadaiwa pia kuwa ni ya Kiebrania.

 

Bacchiocchi anayachukulia mafundisho ya kizushi ya Wakolosai kuwa yalianzishwa uzushi wa kiteolojia na kiutendaji. Anachukulia na kuona kwamba

Kiteolojia, ‘wanafilosofia’ wa Kikolosai (2:8) walikuwa wanashindana na Kristo kwa madai ya kibinadamu. Chanzo chake cha mamlaka, kwa mujibu wa Mtume Paulo ilikuwa ni mapokeo yaliyotengenezwa au kuratibiwa na - B"DV*@F4H [paradosis] (2:8) na lengo lake lilikuwa ni kushirikisha hekima ya kweli - F@N4" [sophia] (2:3,23), 'ujuzi- (<äF4H [gnosis] (2:2,3; 3:10) na- Fb<,F4H [sunesis] (1:9; 2:2). Ili kuupata ujuzi kama huu Wakristo waliaswa kuheshiku kwa kiasi kikubwa kanuni za kikosmikia (2:10,15) na kwenye mambo ya kilimwengu- J FJ@4P,Ã J@Ø P`F:@L [ta stoieea tou kosmou] (2:8,18,20).

 

Ni huhimu kutenganisha kabisa makosa ya kiteolojia nay ale ambayo Mtume Paulo aliyokuwa akiyasema kuliambia kanisa la Kolosai. Elohim, kama ilivyoonyeshwa na dhima ya kibiblia, ni Watakatifu wengi ambao kwamba Mwanakondoo ni Kuhani Mkuu, lakini yeye ni mmoja wao aliwa kama mwenzao au mshirika mwenzao wa dhati. Ufunuo 5 inaonyesha kuwa kuna majukumu yaliyotolewa kwenye Baraza la Elohim. Ufunuo 5:8 inasema wazi kwamba kila mmoja wao kati ya wazee ishirini na nne amepewa vinubi na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato ambayo ni maombi ya watakatifu. Ni wazi sana kwamba wazee hawa wana jukumu la kuwaweka sawa wateule. Ni wazi na dhahiri sana kwamba katika Kolosai urukaji wa msingi ulifanyika wakati kwamba kulikuwa na Elohim ambaye alikuwa amefanyiwa maombi moja kwa moja. Matendo ya zama kale ya kuwaomba wafu na mashetani yalishamiri kwa itikadi au imani zote mbili za Kishamanism na Kibabeloni. Muonekano au kujitokeza wa kimizimu iliyokutikana kwenye imani na hekalu la kimythilia huko Merkabah inaonekana kufanya msukumo wake kwenye maeneo ya Palestina kwenye karne hii ya kwanza. Jarida la Imani ya Ulaji wa Mbogamboga Tupu Kwenye Biblia (Na. 183) linaonyesha kuendelea kwa imani ya Kinostiki yenye mchanganyiko wa upaaji kwenye imani ya Kikristo. Ingeonekana kuwa matulizo ya imani ya kuwaomba malaika na anayepaa kwa kiasi fulani iliingia kwenye kanisa la Kolosai, huenda msingi wake ulituama kwenye sababu zilizotuama kwenye Ufunuo 5:8. Kitendo cha kuabudu sanamu kiligeuzwa na kubadilishwa na matulizo ya watakatifu na hatimaye ilijipenyeza kwenye imani za Ukristo Mkongwe. Hata hivyo, taratibu za utakaso za kiupaaji ilionekana kuwa na mafanikio yenye kikomo kikubwa zaidi. Mapokeo yal;oyotajwa na Mtume Paulo yanaonekana kutuama kwenye roho msingi za mwanzoni na zimeingiliana kwa undani na filosofia. Hiki ni kifungu kigumu sana kueleweka kinachojumuisha mikondo mitatu tofauti ya kinadharia – iliyojulikana kuwa ni mvuto au msukumo wa upande mmoja au mwingine zaidi wa wanafilosofia; yaliyotuama kwenye mapokeao ya wanadamu ambayo kwayo, mambo au desturi za Kiyahudi zimepata mashiko; na mwisho kabisa, utendaji au ushabihiano wa imani za kuomba roho za wafu. Bila shaka kabisa kwamba inahusiana na uheri wa viumbe duni kwa kuwa Mtume Paulo anaendelea kwenye Wakolosai 2:9-10 kumwelezea Kristo kuwa:

Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili. Na ninyi mmetimilika katika yeye aliye kichwa cha enzi yote na mamlaka.

 

Inapasa ijulikane kuwa neno utimilifu au ukamilifu wa kimungu limetoholewa kutoka kwenye neno 2, `J0J@H [theotetos]. Kama ilivyoonekana kutoka kwa Thayer (ukurasa wa 288) uungu unatofautiana na umbinguni kama kitu kinachotofautiana na ubora au mwonekano. Kwa hiyo, mungu au uungu unaotajwa hapa uliokuwa ndani ya mwili wa Kristo, ni roho wa Mungu. Ilikuwa ni kitu hiki muhimu inayotoka kwa Mungu ambayo inamwezesha Kristo kuwa mmoja na Mungu. Wakati Elohimu mwingine alipochukua roho hii, jambo ambalo Mtume Paulo anachoonekana kufanya ni kwamba Kristo ana mamlaka na ukamilifu wa ubora au kiwango cha kiuungu na kwamba aliwakilisha tabia za Baba. Hii inafanya kuonekana kwa vitu vingine visivyofanana kwenye uthibiti wa wateule. Kristo ni kiongozi au kichwa cha tawala na mamlaka zote (Wakolosai 2:10). Mungu ndiye mlengwa kwenye maombi. Kristo na wazee viongozi wanatenda kazi kwa uwakilishi tu. Kwa hiyo, suala lilikuwa ni yule anayetamalaki na kwenye mamlaka. Bacchiocchi (loc. cit.) anasema kuwa uhusiano uliopo wa ulimwengu (Wakolosai 2:8,18,20) kwamba:

Nyingi ya ufafanuzi wa fasili ya maandiko, zimetoholewa kwenve tafsiri ya stoicheia (hususan kwenye msingi wa kifungu kinachowiana kwenye Wagalatia 4:3,9; sawa na 3:19); vinavyowaonyesha wao kuwa ni malaika wapatanishi wa sheria (Matendo 7:53; Wagalatia 3:19; Waebrania 2:2) na miungu ubashiri wa kinyota wa kipagani ambao waliaminiwa na kuchukuliwa kuwa ni wadhibiti na kuhusika na hatima ya wanadamu. Ili kupata ulinzi kutokana na nguvu hizi za kikosmiki na falme, “wanafalsafa” wa Kikolosai walikuwa wanawasihi na kuwataka Wakristo kufanya mkakati potofu wa kuwafundisha watu mafundisho ya kizushi ya kuwapa heshima malaika na kuziamini nguvu na uweza wao (2:15,18,19,23) na kuzifuata taratibu za kidini na matendo ya kiascentiki (2:11,14,16.17,21,22). Kwa mchakato ule mtu alihakikishiwa kuingia kwa kwenda na kushiriki kwenye “utimilifu wa kimungu- (B8ZDT:")" [plerõma]" (2:9,10, cf. 1,19). Makosa au upotofu wa kiteolojia, ndipo kimsingi yalitokana na kuwaingiza malaika duni waombezi kwenye mbadala wa Kichwa Mwenyewe (2:9,10,18,19) (pp. 344-345).

 

Bacchiocchi anaendelea mbele kwa kusema hivi:

Matokeo yaliyo dhahiri ya nadharia hizi za kiteolojia yalikuwa ni msisitizo wa uascetiki wenyewe na itikadi kali ya mapokeo ya kidini. Hii inajumuisha na “kujivua mwili wa kibinadamu” (2:11) (inamaanisha wazi kabisa kuwa ni kutoka kwenye dunia); kuutendea mwili kitendo cha kujinyima (2:23); kukataza ama kutoonja au kutogusa vitu fulani fulani vya vyakula au vinjwaji (2:16,21), na kuadhimisha kiumakini siku takatifu na nyakati za sikukuu, miandamo ya mwezi na Sabato (2:16). Waktisto wanadhaniwa na kuaminika kuwa walifundishwa waamini kwamba kwa kujitoa kwao kutenda hivyo, hawakuwa wanajitoa imani yao kwa Kristo, bali zaidi tu ni kwamba walikuwa wanajongezea ulinzi na walikuwa wanajihakikishia kupata njia ya kuupata ukamilifu kamili (p. 345).

 

Dhana hii iliendelea ikahusisha kuonekana kuwa na dhamira ya kuvikana vitu vilivyofuatia na kupelekea kwa mtu anayemiliki kupitia kwa Kristo. Maombi yote yanapaswa yaelekezwe kwa Mungu Baba, kwa jina la Kristo. Ingawa kuna nguvu zinazomshawishi mwanadamu kuna Mwombezi au Mpatanishi mmoja tu kati ya Mungu na mwanadamu. Wala kunana mahala popote kwenye Biblia panapoonesha kuwa aliwahi kulengwa au kuombwa mtu mwingine yeyote ila Mungu peke yake ambaye ni Baba yetu pia. Kitendo cha kuwa tulizo la wazee kingeweza kuendeleza dhana ni ya kikosmolojia. Hata hivyo, kilichowazi ni kwamba baadhi ya mapokeo ya Mafarisayo walioshika sheria au torati yalijipenyeza kwenye Kanisa kwenye mchakato huu. Dhana ya kuamini roho za mwanzoni za ulimwenguni ilikanganya kwa kiasi kikubwa sana suala la hili (sawa na linavyosema jarida la Mandiko Kuhusu Matendo ya Sheria - au MMT (Na. 104)).

 

Tatizo la Sabao

Andiko la Isaya 1:14 kwa kawaida linatumika ili kuhalalisha ushikaji au kuadhimisha sikukuu za Wakaldayo za Easter na sikukuu ya Krismasi inayoadhimishwa mwezi wa Desemba katikati ya majira ya baridi, ambazo zimekatazwa na kupingana na sheria na mafundisho ya Biblia. Kwa kweli, kwenye tafsiri ya Mfalme Yakobo ambayo maarufu kama King James Version kwenye Matendo 12:4, andiko hili limepotoshwa kitafsiri kwa makusudi kabisa kwa kuandika Easter badala ya Pasaka. Kudhania au kufundisha kuwa Kristo aliliruhusu Kanisa kuzibadilisha sikukuu zilizopangiliwa kwa mujibu wa mpango wa wokovu kwa kuzigeuza kimbadala na sikukuu za kipagani wakati sikukuu hizi takatifu ziliwekwa na kuanzishwa kwa maelekezo kutoka kwa Mungu kunaonyesha kutokuwa jambo la kawaida na lisiloaminika wala kuingia akilini. Tertullian aliangukia kwenye kosa kama hili wakati alipompinga Marcion kuhusu Sabato. Haieleweki vizuri ni kwa kiasi gani Masihi alishiriki akiwa kama Elohimu au Malaika wa Yahova wa Agano la Kale, Tertullian alionysha kuwepo kwa watu waliotenganishwa na walidhaniwa wote kuwa ni Yahova wa Agano la Kale na Kristo kwenye Agano Jipya walioichukia Sabato. Tertullian alilimtumia andiko hili la Isaya kuwa ni kama la juu sana kwenye Agano la Kale na akahoji kuhusu Kristo kwa kusema kuwa:

Hata kama kiumbe huyu hatakuwa ni Yule Kristo wa Wayahudi, bado yeye [yaani Kristo wa Agano Jipya] alionekana kuchukizwa na siku hii takatifu sana kwa Wayahudi, alikuwa anadaiwa au kuonekana sana kuwa anamfuata Muumbaji, kwa kuwa ni kama Kristo [Masihi], kwenye mkakati huu wa kuichukia Sabato; kwa kuwa yeye alitambulishwa kwa mdomo wa nabii Isaya kwa kusema: 'Miandamo yenu ya Mwezi na Sikukuu zenu roho yangu inazichukia' (kitabu cha Bacchiocchi cha From Sabbath To Sunday: A Historical Investigation into the Rise of Sunday Observance in Early Christianity [Kutoka Sabato Hadi Jumapili; Utafiti wa Kihistoria ya Kuanza kwa Maadhimisho ya Jumapili Kwenye Ukristo wa Zamani], The Pontifical Gregorian University Press, Rome, 1977 akinukuu Kinyune cha Marcion 1,1, ANF, Vol. III, p. 271; (lakini mrejea wake ni kwenye mwanzo au chimbuko la uandishi wake peke yake)).

Maoni ya Bacchiocchi yalikuwa kwamba upingaji wa Tertullian kwenye Vitabu vyake vya I, II, III & V ulionyesha kinyume cha utofauti na kile alichofundisha Marcion, kwamba aina ya utunzaji wa Sabato uliofundishwa na Mungu wa Agano Jipya na ambaye ni Kristo ulionekana. Mafundisho yote mawili yalikuwa yanashabihiana. Yote mawili yalitokana na Mungu huyohuyo mmoja ambaye alikuwa ni Mungu wa migawanyiko yote miwili. Kwa kupinga kwake kuhusu ushabihiano wake, hata hivyo, alipotosha kwa kuona kuwa Sabato ni kama taasisi ambayo mara zote Mungu alikuwa ameipuuzia au kuidharau. (Bacchiocchi, ibid., p. 187, fn. 61)

 

Torati

Ni kwenye Kitabu cha V Sura ya IV ndiko Tertullian anajadili na kuibua wazo la kiumbe au mtu ambaye Warumi walimlinganisha na kiini cha mafunzo. Tertullian alimlinganisha mtu huyu na hata chimbuko la sheria au ya torati iliyodhaniwa kabisa kulingana au kufanana na kwamba torati ni sheria iliyotolewa ili kuwaelimisha wateule kiimani. Anataja au kufanya rejea kwenye dhana ya kwamba inayodhaniwa kutokana na Wagalatia, lakini hapa Paulo anaonekana kutaja au kuelezea kuwa ni mafundisho ya kizushi, huenda ni undani, unaohusiana na utulizaji wa nguvu au mamlaka za kiroho zinazoonekana kuwa ziliingia kwenye Kanisa la Galatia na kufanikiwa kuingia kwenye sikukuu za kibiblia na kisha kufanyika kuwa namna ya uhalali kwa kuambatana na sheria zaidi kuliko neema (Wagalatia 5:4). Tatizo hapa ni jinsi ya kuwakabili au kuwaendea Wakolosai. Tatizo la Wagalatia yanaonekana kufanana na imani ya Kinostiki ambalo limeanzisha mafundisho ya kizushi ya Wakolosai. Mafundisho ya kizushi yaliyokuwa huko Kolosai, kama tulivyojionea, yalihusu “mambo” na “mapokeo” na yanaonekana kuwa ni ya kuzipamba imani potofu ya kuamini nguvu au mamlaka za malaika au mapepo ambazo kupendeka kwake kulihusiana na maadhimisho au kutazama “nyakati au kanuni zake- *Î(:"J"" [dogmata].

 

Kama tulivyoona, imani hii potofu inaweza kuwa ilihusiana na kuanzishwa kwa imani au mwonekano wa kisiri-fumbo ya Hekaloth kwenye imani au dini ya Kiyahudi kwenye karne ya kwanza (soma kitabu cha Kaplan, cha Meditation and Kabbalah [Tafakari ya Kabbala], Samuel Weiser, Maine, 1989 ili kupata dondoo zaidi na za kina za imani au dini hii). Dhana ya kwamba utakaso unaweza kupatikana kwa kuadhimisha au kuangalia nyakati (na, kwa hiyo, ni kuwatumikia malaika) ilikuwa ni dhana ya kwamba “iligongomelezewa msalabani” na sio ile ya torati. Mabishano haya yaliendelea kuenea kwenye ukweli kwamba ndani ya Kristo, utimilifu wote wa Mungu uko katika mwili (2:9), na kwamba kwa hiyo aina zote za mamlaka yanayodumu yanamsaidia yeye ambaye ni kchwa cha tawala zote na mamlaka (2:10), na ni kwa kupitia kwa Kristo peke yake (ambaye hana hali kamilifu ya uungu bali pia kwa ukamilifu ukombozi na msamaha wa dhambi) (soma 1:14; 2:10-15; 3:1-5) ambayo kwayo, muumini anafikia ukamilifu wa maisha (2:10). Paulo, kinyume na utaratibu huu wa kawaida, hafanyi ionekane kuwa sheria ionekane hivyo, bali ni kwa njia ya ubatizo kama Bacchiocchi anavyokubaliana na Harold Weiss aanayepinga. Torati kama inavyoitwa (<`:@H [nomos]) iko nje ya isemavyo Wakolosai 2 kwenye mjadala wenye utata na hii ilihusiana na madai ya kwamba:

Mfundisho ya kizushi ya Wakolosai kwa kweli hayakutokana na itikadi kali ya kihafidhina ya Kiyahudi bali zaidi tu ni kwenye aina (syncretistic) isiyo ya kawaida ya kanuni za kiasetiki na kikalti (*Î(:"J" [dogmata]) unaodharau utimilifu wote wa ukombozi wa Kristo. (Bacchiocchi, ibid., p.347)

 

Hoja za Paulo kwa Wagalatia na Wakolosai yalieleweka vibaya na mara nyingi yalieleweka vibaya, hususan na wapinga Sheria au Nomia lakini hasahasa na wa Athanasians. Tertullian alikuwa ni wa kwanza kati ya waamini Utatu wa mwanzoni ambao waliuchukulia upungufu huu wa kiteolojia. Waamini Utatu hawakuyajua au kuyaelewa maana ya mabishano yaliyopamba moto kwenye kanisa la Wakolosai kwa kuwa hawakuielwa kosmolojia ya kwanza ya Ukristo. Mafundisho ya kizushi ya Wakolosai (nay ale ya Wavalentiniani) yalikuwa yanawezekana tu kwa kuwa Kanisa la Kwanza lilikumbatia mafundisho ya kikosmolojia (Ufunuo 4 et seq.) ambayo yalimwendeleza Elohimu kwa kumfanya kuwa ni mshirika wa tatu ambaye Wavalentiniani walimuita Aeons wakimlinganisha na mugu Aeon aliyekuwa anachongwa kwa kumuweka kichwa cha simbe. Jambo hili lilifanyika kila mahali pengine popote.

 

Wagalatia

Tertullian anadai kwamba kutokana na nukuu za Wagalatia na nyinginezozote penginepo zilikosea kwa kiasi kikubwa kwamba Mungu alizidharau Sabato na sikukuu nyingine ziolizoamriwa kwenye maandiko kwa kupinga kama ifuatavyo:

'Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka.' [Wagalatia 4:10] - Sabato, bado naamini, na ‘maandalizi yake' [tafsiri ya ANF inasema 'Coenas puras': huenda ni kama ilivyo kwenye B"D"F6,L"4 inayosema paraskeuai au maandalizi] ya kwenye Yohana xix. 31'; soma kifungu chinachoitaja 'Pasaka' kwa unyumbulisho wa jambo hili] na kifungu cha sikukuu, na ‘siku nyingine takatifu' [pia kwenye Yohana 19:31?]. kwa kuachana hata na hizi, sio hata chini ya mazingira ya tohara, iliyoamriwa kwa amri za Muumba, zilizonenwa na nabii Isaya, ‘mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada. Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia;’ [Isaya 1:13,14]; pia nabii Amosi, ‘Mimi nazichukia sikukuu zenu, nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini.’[Amosi 5:21]; pia na nabii Hosea, ' Tena nitaikomesha furaha yake yote, na sikukuu zake, na siku zake za mwandamo wa mwezi, na sabato zake, na makusanyiko yake yote yaliyoamriwa.' [Hosea 2:11]. Maelekezo ambayo aliyaweka mwenyewe unauliza kuwa kama aliyatengua? Ndiyo, zaidi ya kudhania tu vinginevyo. Sawa, na kama kuna mengine yanayopingana nayo, basi aliyasaidia kwa lengo la Muumba, kwa kuondoa hata kile ambacho alishawahi kukikemea. Bali hapa sio mahala pa kulijadili suala la kwamba ni kwa nini Muumba alizibatilisha sheria au torati yake mwenyewe. Inatosha tu kwa sisi kuthibitisha kuwa alikusudia kufanya mabatilisho kama hayo, ambayo kwamba yaweze kuimarika zaidi na kuonekana kuwa mtume hakuamua kufanya kitu chochote cha kuonekana kuwa alipingana na Muumba (Tertullian Against Marcion, Bk. V, Ch. IV, ANF, Vol. III, p. 436).

 

Tertullian anaonyesha kuwa Marcion anaweza kuonekana kwanza kuwa kama mzushi kwa kuitenganisha injili mbali na torati (soma kitabu cha Against Marcion, ibid., Ch. XXI, p.286). inavutia sana na kuweka maswali mengi, kujiuliza kwamba ni chimbuko hili la mafundisho ya kizushi ya wafuasi wa Marcion kuona kuwa ndiyo yanayoaminika na kujulikana ulimwenguniulimwenguni kote leo kwenye mafundisho yaliyookubaliwa na Wakristo ya kuondoa umuhimu wa maagizo ya torati kwa namna mbili zote, yaani kwa kufanya ibada siku hiyo na kuadhimisha sikukuu zake zilizoamriwa, na hasahasa kwa habari ya Sabato. Dhana yenyewe ni ya kifilosofia zaidi na haina mashiko kabisa na haina maana inayoonekana kuwa yalistahili yaenee kila mahali. Zaidi sana, vikwazo viliinuka kutoka kwa amtu aliyejulikana kama Lord Russell kwenye kile kilichojulikana kama sheria za kimungu au za mbinguni (zilizoitwa na kulikana hivyo, na kwamba hazikuwa zimetolewa kwa kuagizwa peke yake tu, bali ni budi kungekuwa na msingi mkubwa mwingine wa sauti) ambayo ilionekana kupingana na sababu au kiini cha sababu za kuamini na kuona mashiko ya msimamo wa Tertullian. Inadhihirika wazi sana kwa kusoma vitabu vyake kwamba haendani na mambo yenyewe ya kweli yaliyo nyuma ya maneno yaliyo kwenye vitabu vya manabii Isaya, Amosi na Hosea ambavyo sikukuu zimeetajwa na kuamriwa ziadhimishwe na makundi yote mawili, yaani ya Israeli na Yuda na wakilaumiwa kuwa wamezitia unajisi na kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kukosa kwao kutenda haki na utakatifu (Amosi 5:24) kwamba lilikuwa ndilo tatizo lao ni kama ilivyo dhahiri na hata ni haraka kuyasoma maandiko hayo. Kristo ni vivyo hivyo alibatilisha umuhimu wa kuidhimisha Sabato na Mafarisayo wanafiki.

 

Torati yapasa iendelee kutokana na misingi iliyo kwenye uasilia wa Mungu kuliko kufuata mambo yaliyo kwenye maneno na nadharia za kibinadamu peke yake kama anavyoeleza na kuonyesha Russell. Kwa bahati mbaya sana, uhusiano wa kimadaraja ya vyeo uliona kuwa ni humimu msimamo wa Russell na kukubaliana mtazamo wa Kinostiki na kuona kuwa ni sahihi sana hakika. Hata hivyo, Russell hakutafiti kikamilifu sana kosmolojia ya kweli zaidi ya kuonyesha (Kwa Nini Mimi Sio Mkristo) na kwamba suala la sheria za Mungu kwenye imani ya Utatu kwao ni upuuzi na hazina umuhimu kabisa. Suala la Sabato mara nyingi limeondolewa kutoka kwenye sheria ili kuzifanya amri zibakie tisa na sio kumi na zionekane kuwa sio amri muhimu, bali ni mapendekezo tu – kwa kuwa sheria au amri zenyewe zimekwisha koma umuhimu wake na zimeondolewa mbali. Hoja hhii inaonyesha kuwa Waprotestantii kutoshikamana au kukubaliana na asili au umuhimu wa amri hizi. Kitendo cha Waprotestanti cha kuikubali ibada ya siku ya Jumapili, ambayo kwa yenyewe tu chimbuko lake linatokana na mabaraza ya kihalmashauri ya kanisa la Waathanasiani, jammbo ambalo kimsingi ni upuuzi na haina mashiko. Kama kanisa lilipewa mamlaka ya kuibadili au kuitengua sheria yoyote ile, basi lingekuwa pia na mamlizwa kwenye torati na ndipo kanisa na imani ya Kiprotestanti ni waasi wasio na mamlaka. Hata hivyo, kile walichokiita Matengenezo yalishindwa kabisa na kuangukia kwenye hali iliyoonekana kuwa Matengenezo haya yalikuwa ni ya kurudi nyuma zaidi kwa kushikilia mafundisho ya kiteolojia ya Augustine na teolojia yake na teolojia hiyo sio sahihi kabisa kibiblia. Maandiko ya Augustine yametuama kwenye filosofia na haiungwi mkono kabisa na Biblia.

 

Paulo anachukuliwa kimakosa kuwa anaunga mokono matendo ya hawa wapinga sheria, wanaodai kuwa sheria zimeondolewa mbali umuhimu wake, kwa kutuama kwenye nadharia tu za upotofu wa tafsiri za nyaraka zake. Matatizo mengi ya Wagalatia yanatokana na kutoja vizuri maana aliyoikusudia Mtume Puulo. Alishambuliwa kwa kulaumiwa na pande zote mbili, yaani wahafdhina kwa upande mmoja na Wapinga torati kwa upande mwingine. Tatizo la Wagalatia halitokani tu na Wayahudi wahafidhina. Mapokeo ya kikaltiki yameelekezwa, kama tutakavyojionea, kwa nguvu za malaika waasi au mapepo wanaochukuliwa kuwa si theoi kwa sababu ya jinsi walivyo na asilia yao.

 

Kwa kweli Mtume Paulo alianzawaraka wake baada ya kusalimia na kujitambulisha  (Wagalayia 1:1-5), na kwa kuutetea utume wake (Wagalatia 1:6 hadi 2:21). Hatimaye akaendelea kuitetea injili yake (Wagalatia 3:1 hadi 4:31). Dokezo la kimaadili la injili ndipo pia linaonekana kwenye Wagalatia 5:1 hadi 6:10 na hitimisho linafanywa kwenye Wagalatia 6:11-18.

 

Tatizo lililokuwepo kwenye Kanisa la Galatia laweza kuonekana kuhaika au kunyumbulika vizuri kati ya nafasi hizi mbili zote. Hoja ya kwamba sheria zimekoma kutokana na kuzisoma nyaraka za Wagalatia na Wakolosai inatokana na mkakati wa kabisa wa Wapinga-sheria maarufu kama Waantinomia na hoja zao zinazoonekana kukataliwa na kupingwa sana na Mtume Paulo (na hata Yakobo na Yohana pia), kama ilivyo kwenye itikadi kali ya kihafidhina ya Mafarisayo wa Kiyahudi pia ilivyopingwa na kutokubalika (soma majarida ya Uhusiano kati ya Kuokolewa kwa Neema na Sheria (Na. 82); Imani na Matendo (Na. 86) na Maandiko ya Matendo ya Sheria au MMT (Na. 104)). Kukosekana kwa shukurani na uungaji mkono wa injili nyinginezo kumepingwa au kukanushwa na kamusi ya the Interpreter’s Dictionary of the Bible (Vol. 2, art. ‘Galatians’, pp. 338-343) kama kuashiria mshituko wa habari za upotoshaji na ushurutishaji wa kupigania irudishwe tena.

 

Hakuna mashaka kwamba Kanisa liliigeukia injili nyingine, ambayo haikuwa injili kabisa.

 

Mtume Paulo alifika Yerusalemu na kuwaona Petro na Yakobo (kwa maneno yake mwenyewe). Baada ya miaka Kumi na nne mingine alitembelea Yerusalemu tena ili kuweka msingi (pamoja na kina Yokobo, Petro na Yohana), injili yenye teolojia ya kisasa (kwa mujibu wa Interp. Dict., p. 341) hakumaanisha kuwa ni kama kuwa na uhuru mbali na sheria.

 

Kutokana na utembeleaji wa Paulo ilikuwa wazi kwamba ilimpasa kuhudumu kwa Wamataifa na kwa Wayahudi. Petro alikuwa ni mtume kwa Wayahudi kama inavyoonyesha Wagalatia. watu waliokuwa wahafidhina wasilobadilika kwenye Kanisa, kina Petro, Yakobo na wengineo, wanaonekana kuacha kushirikiana na Wamataifa Kanisani kama inavyoonyesha Wagalatia 2:11-14. Petro (Kefa) ametajwa hapa.

Wagalatia 2:11-14 Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu. 12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa. 13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao. 14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?

 

Hii inaonyesha uelewa wa Kanisa. Kufunguliwa kwa Kanisa kulikuwa ni kutoka kwenye mapokeo ya Mafarisayo na itikadi zao. Petro aliachana na mapokeo. Sehemu au upande wa Yerusalemu ulikuwa unaendelea kuyashika mapokeo. Kuwa huko Yerusalemu ilikuwa rahisi sana kuendelea kuyashika mapokeo kuliko kupingana nayo. Wamataifa kwa upande mwingine iliwalazimu kujipanga vilivyo ili kuyashika mapokeo, ambayo yalikuwa hayapo miongoni mwa sheria au torati iliyoagizwa. Zaidi sana, kuendeleza desturi kulizuia pia kwa sehemu kama vile utaratibu wa kutoa sadaka au dhabihu, ambao uliondolewa na kukomeshwa na Kristo.

 

Hoja ya kwamba sheria au torati imeondolewa mbali na kukomeshwa iliyotokana na dhama ya kwamba ilitimilizwa na Kristo inatokana na hali ya kutoelewa maana ya neno kutimilika.

 

Kutimilika maana yake (kwenye Kamusi ya Oxford Universal Dictionary) ni

1.    kupitiliza. Kujaza hadi juu, kuwezesha kujaa ...

2.    Kukithi haja au hamu - 1601.

3.    Kuhitimisha; kueneza au kutoa kilichopungua humo. Pia kutoa au kugawia sehemu ya (kitu); kufidia kwenye ...

4.    Kuchukua au kupeleka (unabii, ahadi, nk.); kutosheleza (hamu, shauku, maombi). Neno la asili la Kiebrania. M.E.

5.    Kutenda, kuondoa, fanya, tii au fuata M.E.; kujibu (kusudi au lengo), kwendana na (mazingira au masharti).

6.    Kufikia mwisho, kumaliza M.E.

 

Kwa hiyo inaweza kuonekana kuwa kuondolea mbali hakumaanishi na wala hakuwezi kumaanisha neno lililo kwenye tofauti nyingine yoyote ya maana ya Kiingereza. Zaidi tu, ni kwamba neno hili ni la Kiebrania. Kwa hiyo, maneno ya Kristo kwenye injili  yhanapasa yaeleweke kwenye tafsiri ya neno. Mathayo 5:17 kuna maneno aliyonena Kristo akisema:

Mathayo 5:17-20 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. 19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. 20 Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

 

Kristo hakuja kutangua torati wala manabii. Alisema hivyo. Alikuja kuzitimiliza (plerõsai). Amri za Mtume Paulo kwa Wagalatia yapasa ziwe zinamaanisha kwenye mtazamo huu. Iwapo kama hazijikanganyi zenyewe au kumkanganya Kristo, ni wazi kwamba Paulo kwa maana hii atakuwa anamkanganya Kristo na hivyo Wagalatia wangekuwa hawahamasiki. Paulo hawezi kushinda mdahalo dhidi ya Kristo. Zaidi sana, Biblia haiwezi kujikanganya yenyewe kimafundisho.

 

Amri hizi kwa hiyo sio tu kuwa zinatakiwa kushikwa tu bali hazitakiwi zichukuliwe kiwepesi. Maana ya kutimiliza yanaweza kuonekana pia kutoka kwenye maana mbalimbali iliyotafsiriwa kwenye maandiko ya Agano la Kale. Neno la kwanza ni mala (SHD 4390) kutia au kujaza hadi juu, kutimiliza uthibitisho, kutakatifuza au kuwa mwishoni dhana ya kuzungushiwa ukuta na pia kukusanyika pamoja au kuwa wote kikamilifu. Maana ya kinadharia haimaanishi kutenga mbali bali zaidi tu ni kufikia kiomo na kuwa kwenye uimara na kitu fulani na hivyo, ni sheria. Vifungu vya maandiko zilikuwa ni neno lililotumika kwenye Mwanzo 29:27, Kutoka 23:26, 1Wafalme 2:27, 2Nyakati 36:21 na Zaburi 20:4,5.

 

Neno la pili ni kalah (SHD 3615) kukomesha kwenye maana ya mpito. Kukoma, kumaliza, au kuangamia na kusafirisha, kuhitimiisha, kuandaa au kumeza, kwa hiyo inaweza kuwa kumeza au kuangamiza. Neno hili limetumika kwenye Kutoka 5:13 kwa maana ya kuhitimisha kila siku majukumu au kazi. Huu haimaanishi kuharibu au kukomesha. Haiwezi kuwa na maana ya ukomo, wa sheria na amri za Kristo mwenyewe. Neno la tatu linapatikana kwenye 1Nyakati 22:13: Kusudia kutimiliza amri na sheria. Neno lililotumika hapa ni ’asah (SHD 6213) kufanya au kutenda kwa maana pana zaidi. Kwa hiyo, neno hili linamaanisha kwendana na amri na sheria kwenye maana hii.

 

Neno lililotumika kutafsiri kile alichesema Kristo kwenye Mathayo 5:17 ni aina ya neno plerõ ambalo maana yake ni kufanya ujazo, ujazo moja kwa moja (kama wavu), kusawazisha (kutukuza) au kutia moyo kwa kung’arisha,, kushawishi, kutosheleza au kufanya kazi na kuwajibika ofisini. Kwa hiyo Kristo alieleweka wazi sana kuongeza kwenye torati mkakati wa kuifanya isitanguke wala kusiondolewe hata nukta moja ya maagizo ya torati kwa sababu zozote. Kudai kuwa Kristo alikuwa anafanya hivyo ni kupotosha uelewa kwa maneno yaliyotumika kwenye lugha zote, yaani: Kiyunani. Kiebrania na Kiaramu ambazo Kristo aliziongea, au kwenye Kiingereza ambacho hatimaye neno hilo lilitafsiriwa kwayo. Alitimiliza sheria au torati kwa kutuma au kumleta Roho Mtakatifu. Hiyo ndiyo maana halisi nay a kweli ya hoja za Paulo na za mitume wengine wote na manabii.

 

Jambo muhimu kwa Wagalatia ni andiko la Wagalatia 3:1-5.

Wagalatia 3:1-5 Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? 2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? 3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili? 4 Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli. 5 Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

 

Msimamo ni kwamba Roh ameletwa si kwa kuja kuzitenda sheria bali ni kwa imani. Dhana kuhusu uzima wa milele ni kwamba ndiyo iliyoondolewa kutoka kwenye msimamo anaoushikilia kila mmoja kwa kujikita kwenye mapenzi ya Mungu kwa kuyatendea kazi na kwa imani. Dhana hiyo ndipo imeendea kutoka kwa Ibrahimu ambaye ni baba wa imani.

Wagalatia 3:6-9 Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki. 7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu. 8 Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa. 9 Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

 

Mtazamo huo umendelea hadi wale wanaozitegemea kazi au matendo yao yatimilizwe kuliko dhabihu ya Yesu Kristo.

Wagalatia 3:10-14 Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye. 11 Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani. 12 Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo. 13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; 14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.

 

Kwa hiyo, upokeaji wa ahadi ni kwa kupitia imani. Sharti au stahili ya kupokea ahadi ni kwa njia ya utii. Ahadi ya kumpokea Roho Mtakatifu ilitabiriwa kutimilika kwa watiifu wote wanaozitii sheria na kuzishika amri za Mungu (Mathayo 19:17); soma pia majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117) na Uzima wa Milele (Na. 133).

 

Wayahudi walikuwa wanajaribu kuupata wokovu kwa matendo yao ya sheria na walikuwa wanapotosha kusudi la torati na kuihoji asili ya Mungu. Upotoshaji huu ulianza kujipenyeza kwa wateule.

 

Wagalatia 3:15-18 Ndugu zangu, nanena kwa jinsi ya kibinadamu. Lijapokuwa ni agano la mwanadamu, hata hivyo likiisha kuthibitika, hakuna mtu alibatilishaye, wala kuliongeza neno. 16 Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu na kwa mzao wake. Hasemi, Kwa wazao, kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo. 17 Nisemalo ni hili; agano lililothibitishwa kwanza na Mungu, torati iliyotokea miaka mia nne na thelathini baadaye hailitangui, hata kuibatilisha ile ahadi. 18 Kwa maana urithi ukiwa kwa sheria, hauwi tena kwa ahadi; lakini Mungu alimkirimia Ibrahimu kwa njia ya ahadi.

 

Inaweza kuonekana kwamba ahadi hii iliwekwa kwa Kristo na kwamba hakuna mtu anayeweza kuja kwa Mungu na kuokolewa isipokuwa ni kwa kupitia kwa Kristo. Wayahudi waliamini kwamba wanaweza ukwepaji wa umuhimu wa imani kwa kushikilia matendo peke yake. Lengo hapo ni kwamba kulikuwa na aina ya utakaso ulioingia kwenye Kanisa la Wagalatia, ambao ulikuwa unakutikana pia kwa Wanostiki na wa namna moja, lakini sio wa aina moja, kama ule uliokutikana kwa Wakolosai.

 

Paulo anaelezea maana na malengo ya torati.

Wagalatia 3:19-20 Torati ni nini basi? Iliingizwa kwa sababu ya makosa, hata aje huyo mzao aliyepewa ile ahadi; iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe. 20 Basi aliye mjumbe si mjumbe wa mmoja; bali Mungu ni mmoja.

 

Torati ilikuwepo hadi alipokuja Kristo kwa kuwa watu hawakuweza kuishi sawasawa na mapenzi ya Mungu ambaye kwake torati ilitoka na kuamriwa. Kristo hakufanya hivyo na kwa wale ambao walipewa Roho Mtakatifu kwa njia ya imani. Kwa hiyo sasa, Roho alikuwa ametolewa kwa manabii peke yao na waliirithi ahadi, lakini wengi walioitegemea matendo hawakeweza kutokea hadi Kristo na wateule wake. Maadui wa Mungu walibakia kwenye nafasi ya Roho Mtakatifu kwa malaika kwa njia ya mwombezi na mtetezi, anayetuwezesha sisi kuwa wamoja na Mungu kama Kristo alivyo mmoja na Mungu.

 

Torati haipingani na ahadi bali zaidi tu inaiweka wazi zaidi kwa umuhimu wake kwenye imani katika Kristo.

Wagalatia 3:21-22 Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? Hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, yakini haki ingalipatikana kwa sheria. 22 Lakini andiko limeyafunga yote chini ya nguvu ya dhambi, makusudi hao waaminio wapewe ile ahadi kwa imani ya Yesu Kristo.

 

Torati ilitenda kazi kama kuhitimisha hadi Kristo alipokuja kwa kuwa hatukuweza kuishi sawasawa na mapenzi na asili ya Mungu hadi tulipopewa Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu hakutolewa kwa kuombwa Kristo. Ni manabii tu na wale waliochaguliwa na Mungu kuuelewa mpango wa Mungu wa wokovu ndio walishirikishwa neema hii ya kumpokea Roho, kwa hiyo ni kwamba tangu wakati wa Kristo ilikuwa wazi kwa kundi kubwa la watu.

Wagalatia 3:23-29 Lakini kabla ya kuja ile imani tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa. 24 Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani. 25 Lakini, iwapo imani imekuja, hatupo tena chini ya kiongozi. 26 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. 27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. 28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. 29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

 

Katazo la Mungu alilolifanya kwa kanuni na taratibu zake lilikuwa ndilo kivuli ekee cha uhusiano wa kweli ambao wateule walikuwanao wakiwa pamoja na Mungu kupitia kwa Kristo. Tunaishiriki asili ya Mungu na kufanya kwa hiyari yetu wenyewe kwa mambo hayo, ambayo mwanzoni sana tulipasa kufanya kwa msukumo wa nje. Amri za Mungu zinaendelea sasa kwa wateule kwa kupitia Roho Mtakatifu. Wateule sasa ni uzao wa Ibrahimu ni kama Kristo alivyo kuwa ni uzao wa Ibrahimu na wakiwa ni warithi wa ahadi. Kwa njia hiyo tutakua hadi kwenye kimo cha Mwana wa Mungu kwa uweza kwa kupitia Roho Mtakatifu kwa kufufuliwa kwetu kutoka kwa wafu kama alivyofanya Kristo (Warumi 1:4).

 

Paulo anaendelea kwenye Wagalatia 4 kushughulikia dhana nyingine kwa pale anapoeleza roho muhimu ya kiroho. Kutoka juu, mstari huu haupo mtupu pasipo na umuhimu au maana.

Wagalatia 4:1-7 Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote; 2 bali yu chini ya mawakili na watunzaji, hata wakati uliokwisha kuamriwa na baba. 3 Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia. 4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, 5 kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. 6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba. 7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.

 

Wateule walitumikishwa na roho zitendazo nguvu za kidunia hadi alipokuja Kristo. Hivyo, hawa mapepo walitajwa kama roho zisumbuazo. Hivyo, dhana hii ilihusisha mawazo ya kipagani yaliyoendelea ambayo yalikuwa ni ya kawaida kwa wote wawili, yaani Wayunani na Warumi. Ni kama ilivyo sasa kuwa tunakabiliwa na aina fulani ya uenezwaji wa usynkretism ya Kihelleniki ambayo sio imani halisi ya Kiyahudi, bali angalau, inaweza tu kuwa ni mwanzo na utangulizi au mwanzilishi wa imani ya kimafumbo.

 

Anatajwa kwa wazi sana kabisa kwa Malaika walioasi kwenye Wagalatia 4:8ff. Dhana iko wazi wakati Paulo anaposema kuwa hapo mwanzoni sana tulipokuwa hatumjui Mungu tulikuwa kifungoni kwa wale ambao kwa asili walikuwa sio Theoi tukiyatenda mapenzi yao. Kifungu hiki kinaendelea kusema kuwa:

Wagalatia 4:8 Lakini wakati ule, kwa kuwa hamkumjua Mungu, mliwatumikia wao ambao kwa asili si miungu.

 

Kifungu kinaendelea kuchambuliwa kwenye Kamusi ya Marshall’s Interlinear kifungu kikubwa kwamba:

Lakini wakati ule, kwa kuwa hamkumjua Mungu, mliwatumikia wao ambao kwa asili si miungu.

Ni wazi kwamba kuwatumikia Malaika walioasi kunahusishwa na kwamba anawataja wao kama maroho yenye nguvu. Ni wazi sana kwamba Galatia iliwa inajaribu kufariji au kutuliza, kwa kuyashika mapokeo, maroho yatesayo, wakikosa kujua kwamba walikuwa pamoja na Malaika hawa waasi au mapepo. Walikuwa wanashirikiana nao Kanisani shughulii za utakaso ambazo zilikuwa ni ugonjwa ulionea kwenye imani ya Upythagoreani na ambazo zilikuwa zimejipenyeza huko Italia na kwa Warumi siku nyingi sana huko nyuma. Kwa hiyo, waongofu Wamataifa hawakuwa wakiendana na kanuni zilizopaswa kuzifuata kwenye uhalisia wa seria au torati na hawakujua mahali pake kwenye mambo ya imani. Tunaona jambo hilo kutoka kwenye aya za 9-11.

Wagalatia 4:9-11 Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? 10 Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka. 11 Nawachelea, isiwe labda nimejitaabisha bure kwa ajili yenu.

 

Uadhimishaji huu uliotajwa hapa unaweza kuonekana wazi kuwa umehamasisha kwa kiasi kikubwa makanisa kongwe ya kale kwa kipindi cha takriban miaka elfu mbili. Andiko hili haliiondoi Sabato na maadhimisho yake wala sikukuu zake.

 

Andiko la mtumwa na mtu huru linataja matumizi ya sheria au torati huko Yerusalemu.

Wagalatia 4:12-31 Ndugu zangu, nawasihi, iweni kama mimi, maana mimi ni kama ninyi. Hamkunidhulumu kwa lo lote. 13 Lakini mwajua ya kuwa naliwahubiri Injili mara ya kwanza kwa sababu ya udhaifu wa mwili; 14 na jaribu lililowapata katika mwili wangu hamkulidharau wala kulikataa, bali mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama Kristo Yesu. 15 Ku wapi, basi, kule kujiita heri? Maana nawashuhudu kwamba, kama ingaliwezekana, mngaling'oa macho yenu, mkanipa mimi. 16 Je! Nimekuwa adui wenu kwa sababu nawaambia yaliyo kweli? 17 Hao wana shauku nanyi, lakini si kwa njia nzuri, bali wanataka kuwafungia nje, ili kwamba ninyi mwaonee wao shauku. 18 Navyo ni vizuri kuonewa shauku katika neno jema sikuzote, wala si wakati nikiwapo mimi pamoja nanyi tu. 19 Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu; 20 laiti ningekuwapo pamoja nanyi sasa, na kuigeuza sauti yangu! Maana naona shaka kwa ajili yenu. 21 Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je! Hamwisikii sheria? 22 Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana. 23 Lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili, yule wa mwungwana kwa ahadi. 24 Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai, lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri. 25 Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto. 26 Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi. 27 Kwa maana imeandikwa, Furahi, wewe uliye tasa, usiyezaa; Paza sauti, ulie, wewe usiye na utungu; Maana watoto wake aliyeachwa pekee ni wengi Kuliko wa huyo aliye na mume. 28 Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi. 29 Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa. 30 Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa mwungwana. 31 Ndiposa, ndugu zangu, sisi si watoto wa mjakazi, bali tu watoto wa huyo aliye mwungwana.

 

Hatuzishiki sheria kwa kuwa tu watumwa wa sheria inazoendana sawa na mapenzi ya mwili, ambayo ni ulimwengu wa mapepo na wa mungu wa dunia hii. Tunamtumikia Mungu na ni sehemu ya Yerusalemu Mpya. Usemi wa Paulo aliowaambia wa kuwa kama alivyo yeye, unaonyesha kuwa haongelei tu ushikaji wa sikukuu kwa kuwa alizishika sikukuu na Sabato (kama tunavyojua kutoka kwenye Matendo na nyaraka zake) kama walivyofanya mitume wote. Na kama atakuwa anasema kuwa sikukuu hizi zimetanguliwa mbali, ndipo anamfanya Kristo kuwa ni muongo aliyenena na manabii na kusema kwamba Sabato na Miandamo ya Mwezi Mpya na sikukuu (Isaya 66:23) zinaendelea kuadhimishwa (Zekaria 14:16-19). Kama wateule watazipuuzia kwa kuacha kuadhimisha Siku hizi Takatifu na Sabato, basi itakuwa ni ugeugeu kwa kuwa Mungu atayahukumu mataifa kwa kutozishika siku hizi wakati wa utawala wa millennia. Mungu hana upendeleo na kwa hiyo anahitaji usawa wa viwango vya wanadamu.

 

Wateule wana kazi kubwa sana ya kuzitenda, kuendenda kwa imani. Kama mtu yeyote atasema kuwa sheria au torati imetanguliwa mbali, basi yeye ni mjinga tu, asiyeyajua Maandiko Matakatifu, ambayo hayawezi kutanguka, na asiyeijua asili ya Mungu. Zaidi sana hasa, watakuwa ni wajinga wa kutojua mambo ya kweli nay a muhimu mbali na vile walivyokuwa wenyeji wa Galatia na Kolosai. Kiwango cha makosa au upotoshaji kwenye makanisa hayo walianza kudai wenyewe kuwa ni Wanostiki kwenye hatua ya mwanzoni kabisa. Michakato ya kimawazo inabakia pia kwenye Teoljia ya Uhuru na, hususan kwenye imani ya Kibudha. Mawazo hayo yangali yanaendelea bado kwenye Teolojia Mchakato. Wanostiki waliachana na uwepo huo huo wa Mungu (jarida la Maandiko ya Matendo ya Sheria - au MMT (Na. 104) linafafanua vya kutosha jambo hili).

 

Mafundisho ya Kizushi Kwenye Kanisa la Yohana

Kila moja ya nyaraka tatu za Yohana ziliandikwa ili kushughulikia matatizo au chngamoto ya mafundisho na mamlaka ya injili kama ilivyokuwa imefundishwa kwao na Yohana.

 

Uzushi mkubwa sana kuliko yaonekana kuwa ulihusika na fundisho la Uungu na ulikuwa ni jaribio la kumuinua juu Kristo ili aonekane kuwa ni huyu Mungu Mmoja, wa Pekee wa Kweli. Mtume Yohana anaonyesha uhusiano huu kwenye andiko la Yohana 17:3 na tena alipokuwa anashughulikia mafundisho ya kizushi kwenye 1Yohana (hususan kwenye 1Yohana 5:20).

 

Upotoshaji ulikuwa wazi sana kutoka kwenye madai yake haya kuwa ni wateule (1Yohana 1:6) ndio waliohusika kujidai kuwa wao hawana dhambi (1Yohana 1:8). Suala lilikuwa ni uwezo wa kumjua Mungu, ambaye ni Ujuzi. Unostiki ulijumuisha nadharia au fundisho la kuwa sheria za Mungu au torati imetanguka au fundisho la kwamba amri za Mungu hazihitajiki kushikwa tena (1Yohana 2:4). Wajibu au fursa ya Roho Mtakatifu kuwa ndani ya wateule na kisha katika Mungu (1Yohana 2:6) alitegemea upendo wa wote wawili, yaani Mungu na ndugu wapendwa. Wateule hawapaswi kuwachukia ndugu zao (1Yohana 4:20).

 

Madai haya yanashabihiana kwa dhahiri. Maana kusudiwa ni kwamba upinzani ulioko ni:

… kumekuwa kukifanyika madai kwenye ujuzi kamili maalumu na upendo wa Mungu na kwa ushirika maalumu na mkubwa wa karibu na yeye ambao umewafanya wawe juu ya uwezekano wa kawaida wa kutenganisha kati ya wema na ubaya na kwa hiyo kuwa juu zaidi madai ya maadili na imani ya Kikristo. Ni huenda, zaidi sana, kwamba ujumbe muhimu wa waraka ni; “Mungu ni nuru na hakuna giza lolote ndani yake,” unaelekezwa dhidi ya teolojia inayoshikilia kudai kwamba Mungu alijidhihirisha mwenye kwa namna zote mbili, yaani nuru na giza (kwa mujibu wa Kamusi ya The Interpreter’s Dictionary of the Bible, Vol. 2, p. 947)

 

Aina au mtindo wa teolojia ya Kiyunani inashabihiana kwa karibu sana kuangukia kwenye mrengo huu ulikuwa ni aina ya itikadi za Kiplatoni au Upithagoreani. Hoja ya kwamba Mungu ni mambo yote na, hivyo, kiukweli kabisa haiwezi kuwa leo. Kimsingi, inaonekana kuwa ni kama Uanimism ulio kwenye dini ya Kibabeloni. Waalimu walikuwa pia wanakataa kuwa Yesu alikuwa ndiye Masihi (1Yohana 2:22). Kamusi ya The Interpreter’s Dictionary inaungana kwa kusema hivi:

Hatuwezi kuhitimisha hili kuwa hawa walikuwa ni Wayahudi au Wazayuni waliokuwa wanapinga Umasihi wake, lakini zaidi ni kwamba tu walikuwa Wakristo waliokuwa wanapinga fundisho la Inkaneshi au kwamba alikuwepo akiwa timamu hata kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake tumboni mwa mama yake. Kwa hiyo upotofu wao unaonekana kwa waziwazi kabisa na kudhihirika zaidi baadae kwenye waraka kama ukano kwamba “Yesu Kristo ametokana na mwili” (4:2) (ibid.).

 

Onyo juu ya kuzijaribu roho ili kuziona kama zina uhusiano na Mungu au sivyo, linafanya ionekane dhahiri tunashughulika na kukabiliwa na mwingiliano na maroho yasumbuayo na unenaji unaopingana na kuhesabiwa haki na Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu. Neno geni la chrism au unction ambalo limetumika mara mbili kwenye maandiko (kwenye 1Yohana 2:20,27) kuelezea karama za Roho ambazo kwazo kila Mkristo anashiriki limetumika kwenye kifungu hiki cha maandiko kwa sababu ya wafundisha uzushi hawa kwanza alilitumia ili kuelezea kile wanachokiamini kuwa ni kuwa ni utoaji au kujitoa kwa mshikamano wao wenyewe wa kiroho (Kamusi ya Interp. Dict., ibid.). hivyo, upako (Chrisma) wa Roho Mtakatifu ni kinyume na kutiwa upako wa maroho mengine haya yanayozidi kuendelea. Fundisho hili hapa limepewa jina ya kuwa ni la Mpingakristo, ambalo ni la yeye anayempinga Baba na Mwana pia. Ilionekana kuwa kilichokuwa kikipingwa ni kule kumfanya Kristo kuwa ni sehemu ya Baba kama kitu kimoja kama hakuwa amekufa kiujumla. Fundisho la kwamba Kristo ni Mungu kama moja ya mfumo unaomhusidha Roho kwa sasa limeenea na kushinda sana kwenye mawazo na imani za Ukristo wa dini kongwe. Hata hivyo, hoja zake yapasa zichukuliwe kwamba na utaratibu uliowekwa, na kwa utaratibu ulionenwa hapa, na wafundisha uzushi wa wakati wa Yohana.

 

Fundisho kuhusu Mungu kwenye maandiko ya Yohana liko wazi na laonyesha wazi kuwa ni la mrengo wa Kiyunitari na Kristo anaonekana wazi kuwa ni mwana wa Mungu wa Pekee wa Kweli (Yohana 17:3) aliyekufa kwa ajili ya wateule. Wamodalisti na ambao baadae walikuja kuwa Waaamini Utatu au Watrinitari wakijua hivyo sana, walikuwa na ugumu mkubwa sana kwenye maandiko haya ya Yohana (sawa na ilivyo kwenye majarida ya Mawazo Yaliyopo Kwenye Kati (Na. 74) na Imani ya Kibinitariani na Utrinitari (Na. 76)).

 

Kwenye 1JYohana anaelezea kifupi na kwa wazi sana kuhusu makosa au upotoshaji na hila zilizopelekea kufanya hivyo. Andiko linaonesha kusudi lake.

 

Wateule wamebatizwa kwenye mwili wa Kristo na sio kwenye kanisa lolote au kuwa mali dini yoyote. Maneno hayo yananenwa na karibu kila mteule wakati anapobatizwa. Kwa hiyo wateule ni wale waliofungamanishwa kwenye mwili wa Yesu Kristo wakimuabudu Mungu wa Pekee wa Kweli kama inavyosema Yohana 17:3. Kwa hiyo, wakati wateule wanapokusanyika kwenye maeneo ya makanisa, walikuwa wakikusanyika kwa msingi wa mshikamano wao kwenye kweli na kumuabudu Mungu wa Pekee wa Kweli na kumtumikia Mwana wake Yesu Kristo. Wakati kanisa lilipokabiliwa na fundisho lililojaribu kumfanya Kristo kuwa ni zaidi ya kuwa mwana wa Mungu na kumfanya kuwa ni sawa na Mungu na kumtenganisha na ubinadamu wake mbali na hali yake ya kimbinguni ndipo wateule walilazimika kujipanga au kujikusanya upya na kujitenga kutoka kwa hao walioanzisha mafundisho ya uwongo, ambayo yalipewa jina la wazi kabisa kuwa ni mafundisho ya Mpingakristo.

 

Msingi wa imani ni kweli na hakuna giza kwa wale wanaotembea kwene kweli.

1Yohana 1:1-10 Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima; 2 (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu); 3 hilo tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo. 4 Na haya twayaandika, ili furaha yetu itimizwe. 5 Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake. 6 Tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli; 7 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. 8 Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. 9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. 10 Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.

Kwa hiyo, ni lazima kwa wapendwa kutembea pamoja kwenye kweli.

 

1Yohana 2:1-6 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote. 3 Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake. 4 Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. 5 Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake. 6 Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda.

 

Kristo ni mtetezi kwa Baba. Wakili ananena kwa niaba ya mwingine. Wakili hawezi kuwa na kusema yeye mwenyewe tu.

 

1Yohana 2:7-11 Wapenzi, siwaandikii amri mpya, ila amri ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Na hiyo amri ya zamani ni neno lile mlilolisikia. 8 Tena nawaandikia amri mpya, neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu; kwa kuwa giza linapita na ile nuru ya kweli imekwisha kung'aa. 9 Yeye asemaye kwamba yumo nuruni, naye amchukia ndugu yake, yumo gizani hata sasa. 10 Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika nuru, wala ndani yake hamna kikwazo.

 

Upendo ni alama ya mteule. Mahali ambapo kundi linapenda ushirika wao, au viongozi wao, zaidi kuliko kupendana wao wenyewe kwa wenyewe na wanapofikia hata hali ya kutoijali kweli, kisha ndipo kundi hilo lina ishara ya kuwa imani potofu au kalti na wala halipo sehemu ya mwili wa Kristo. Mtume Yohana anaandika kuhusu neno la Mungu kukaa kwa wingi kwa wateule na kufanya hivyo, watamshinda muovu.

 

1Yohana 2:12-17 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba. 14 Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu. 15 Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. 16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

 

Agizo la kupendana wateule ni la Baba kabisa. Upendo wa wateule na umuhimu wa kupendana kila mmoja na mwezake unawezekana tu kwa kuwa na Roho Mtakatifu ndani ya kila mteule kutoka kwa Kristo na kuendelea. Kristo alijitoa mwenyewe kwa ulimwengu kwa njia ya pendo la Baba. Yohana 3:16 inasema kuwa Baba alimtoa Mwana.

Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

 

Hatuwezi kutoka kitu kisicho cha kwetu. Hakuna usawa kwenye karama za Mwana na Baba.

 

Zaidi sana, Kristo alitumwa na Baba kwa mapenzi na maelekezo kamili.

Yohana 4:34 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

 

Kwahiyo, kazi ni ya Baba na yapasa kufanywa na Roho Mtakatikatifu kwa ndani na ya mwanadamu na kwa kupitia kwa huyo mtu, kwanza kabisa ikiwa ni kwa Kristo na pili ni kwa mteule. Ni kwa jinsi gani basi mteule hapo zamani au hata sasa anaweza kubaki kwenye shirika linalofundisha kinyume na maagizo ya torati na ushuhuda na ikawa bado ni kazi ya Baba?

 

Mafundisho ya Mpingakristo hayahitimiki kwa kila mtu mmoja mmoja ni mafundisho, yanayotafuta kushusha hadhi au kudharau ukuu wa Mungu wa Pekee wa Kweli na ukamilifu au ukomo wa kifo na dhabihu ya Mwanae wa Pekee, Yesu Kristo. Kitendo cha kutoka kati ya wana wa dunia hii cha wateule ni cha kibiblia na kimafundisho na sio cha msingi wa ushirikiano tu peke yake.

 

1Yohana 2:18-29 Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. 19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu. 20 Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote. 21 Sikuwaandikia ninyi kwa sababu hamwijui iliyo kweli, bali kwa sababu mwaijua, tena kwamba hapana uongo wo wote utokao katika hiyo kweli. 22 Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. 23 Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia. 24 Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba. 25 Na hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele. 26 Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27 Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake. 28 Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake, ili kusudi, atakapofunuliwa, mwe na ujasiri, wala msiaibike mbele zake katika kuja kwake. 29 Kama mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendaye haki amezaliwa na yeye.

Hapa wazo la kutoka kati yao tulilonalo sisi limeendelea kufundishwa na Yohana. Hoja iliyoendelezwa Kanisani lililotajwa na Yohana lilionekana wazi sana hapa kuwa ni zaidi ya Uungu na uhusiano wa Baba na Mwana. Hoja ilikuwa ni linawasuta waamini Utatu. Ilijaribu kutenganisha ubinadamu wa Kristo kutoka kwenye hali yake ya kimbinguni. Kimsingi, ilijaribu kudai kuwa Kristo alikuwa na chembechembe ya ubinadamu iliyobakia imetenganishwa na ubinadamu wake na hakufa. Zaidi sana, ilibakia sehemu ya kitu tunachokijua leo kuwa Mungu. Kimsingi, yalijaribu kumfanya Kristo kuwa na sehemu yake na kuwa sawa na Mungu. Haya ni mafundisho ya Mpingakristo. Ilikuwa hivyo dhahiri na kuhusiana na imani ya Utrinitari ambavyo andiko la 1Yohana 4:1-2 lilibadilishwa ili kugeuza au kupotosha ukweli.

 

Wazo la kuwa sehemu ya mteule kwa mwenendo wa utakatifu. Kiini cha andiko la Yohana ni kwamba: atendaye haki yu na haki – naye atendaye dhambi ni wa ibilisi (diabolos). Kwa hiyo, haiwezekani kuunganishwa au kushirikiana na wale wasiohubiri ukweli. Amri za Mungu ni za muhimu. Dhambi maana yake ni uvunjifu wa amri za Mungu au hapa ni kitendo cha kuvunja sheria au kutojali kuhusu sheria. Amri ya kwanza inahusiana na kitendo cha kumuabudu na kumpenda Mungu. Sababu yake ni rahisi. Ni kwamba, tunawezaje kumwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli na huku tukiwa ni sehemu ya mfumo unaojaribu kumpinga Kristo kwa kujaribu kumlinganisha kuwa yu sawa na Mungu wa Pekee wa Kweli na kutenda dhambi hiyohiyo aliyoitenda Shetani? Kwa hiyo, inatupasa sisi kujitakasa kama Kristo alivyo mtakatifu.

1Yohana 3:1-10 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 3 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 4 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. 5 Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake. 6 Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua. 7 Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; 8 atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu. 10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

  

Kama hatutendi vyema ndipo tunakuwa si wa Mungu. Hatuwezi kuwa tunawapenda watu wetu, iwapo kama hatutawahubiria neno la Mungu kwa kweli isiyoghoshiwa.

 

1Yohana 3:11-24 Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi; 12 si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki. 13 Ndugu zangu, msistaajabu, ulimwengu ukiwachukia [mkolezo wa rangi ni msisitizo]. 14 Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti. 15 Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake. 16 Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. 17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli [imekolezwa rangi ili kusisitiza]. 19 Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake, 20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote. 21 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; 22 na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake. 23 Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri. 24 Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa.

Kwa hiyo Mungu yuko tofauti na halinganishwi wala hafanani na Mwana na tunasika amri zake tukitembea katika kweli. Wateule wanatakiwa kuzijaribu roho ili kuziona kama zinatoka kwa Mungu.

1Yohana 4:1-3 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. 2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. 3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.

 

Andiko na kifungu hiki kuhusu mafundisho ya Mpingakristo limebadilishwa na kupotoshwa kwa makusudi kwenye maandiko ya zamani. Maandiko yenewe sahihi na halisi yanaweza kuonekana kutoka kwenye maandiko ya vitabu vya Irenaeus (soma kitabu cha Ante-Nicene Fathers, Vol 1, fn. p. 443). Andiko hili linasomeka hivi:

Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo

Socrates wanahistoria anasema (VII, 32, p. 381) kwamba kifungu hiki kimepotoshwa na wale waliokusudia kuutenhanisha uwanadamu wa Yesu Kristo kutoka kwenye hali yake ya kimbinguni. Kwa hiyo, hoja ya kwamba sehemu ya Kristo ilibakia kuwa ni ya kimbinguni akiwa sehemu ni Mungu tofauti na ubinadamu wake na kufa kwake msalabani akikataa kabisa ufufuko na ni fundisho la Mpingakristo. Kwa hiyo, imani ya Utrinitariani inaangukia kabisa kwenye mafundisho ya Mpingakristo.

 

1Yohana 4:4-6 Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia. 5 Hao ni wa dunia; kwa hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia 6 Sisi twatokana na Mungu. Yeye amjuaye Mungu atusikia; yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu.

 

Hivyo roho wa kweli alikuwa anahitajika na bado anahitajina kutengana na roho wa upotevu. Jaribio hili ni kwa wateule kuonyesha yule aliye mteule na Yule aliyeitwa lakini hajachaguliwa bado.

1Yohana 4:7-21 Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. 8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. 9 Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye. 10 Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. 11 Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. 12 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. 13 Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake. 14 Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu. 15 Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu. 16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. 17 Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu. 18 Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina adhabu; na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo. 19 Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza. 20 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. 21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.

 

Wale walio na upendo mkamilifu hawahofii mtu yeyote, hebu na tuwaache na kujiepusha wale walio kwenye upotoe na kuikosa kweli. Umuhimu wa kuushinda ulimwengu umetajwa wazi kwenye 1Yohana 5:1-5.

1Yohana 5:1-5 1 Kila mtu aaminiye kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye. 2 Katika hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake. 3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito. 4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. 5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?. [msisitizo umeongezwa].

 

Tukimpenda Mungu basi na tushike amri zake. Kwa hilo tunajua kuwa tunawapenda watoto wa Mungu. Kuzaliwa na Mungu yatupasa kuushinda ulimwengu. Ili kuushinda ulimwengu yatupasa tuamini kwamba Masihi ni Mwana wa Mungu. Kwa hiyo, uhusiano wake uko wazi. Kitendo cha kugeuz ili kuyapotosha maandiko au vifungu vya biblia au kutafsiri kwa uwongo na upotoshaji kinyume na maana yake halisi na iliyo wazi ya maneno yanayoonekana hapo chini (hususan kwenye 1Yohana 5:7 inapolinganishwa na maandko ya uwongo yalivyo kwenye tafsiri ya Mfalme Yakobo ya KJV).

1Yohana 5:6-12 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. 7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli. 8 Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. 9 Kisha wako watatu washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe. 10 Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. 11 Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. 12 Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.

 

Kumbuka kuwa Mungu alitupa sisi uzima wa milele na uzima huu upo kwa Mwana wake. Kwa hiyo, Mwana anao uzima wa milele kutoka kwa Baba, ambao pia tumepewa sisi kwa namna hiyohiyo.

1Yohana 5:13-21 Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu. 14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. 15 Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba. 16 Mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi isiyo ya mauti, ataomba, na Mungu atampa uzima kwa ajili ya hao watendao dhambi isiyo ya mauti. Iko dhambi iliyo ya mauti. Sisemi ya kwamba ataomba kwa ajili ya hiyo. 17 Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti. 18 Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi. 19 Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu. 20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele. 21 Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.

Maandiko yaliyo kwenye 1Yohana yamefanya udanganyifu na upotoshaji kwa kipindi cha karne kadhaa sasa. Mkakati wa mwanzoni kabisa wa kughushi ulikuwa ni ugeuzaji au upotoshaji wa maandiko yanayoelezea vizuri kuhusu mafundisho ya Mpingakristo. 1Yohana 5:7 (tafsiri za Receptus na KJV) ilighushiwa kwa kugeuzwa mapema kwenye kipindi kilichojulikana kama cha Matengenezo. Ujanja na ulaghai wa pili zaidi wa utendaji ni kufanya ulaghai wa maana asili iliyokusudiwa kwenye maandiko, kama vile ugeuzi wa maana asilia iliyokusudiwa na maana ya wazi ya maneno yanayodaiwa kwao. Ulaghai kama huu yanapelekea aina ya hoja au mabishano yaendelee kwenye kitabu cha fasihi cha G.L. Haydock commentary to the Douay-Rheims Bible (1850 reprint of the 1819 version), kuhusu andiko hili la Yohana 17:3, yanayofanya rejea kwenye 1Yohana.

 

Aya ya 3. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Kwa maneno haya Waariani wanajifanya kwamba huyu Baba ndiye Mungu wa kweli. S. Aug. na wa-kukwepa wengine wanajibu kwamba maana na urekebishaji ni sehemu isemayo, ili wakujue wewe, na pia Yesu Kristo Mwanao, uliyemtuma kuwa ni Mungu wa Pekee wa Kweli. Tunaweza pia kuendelea kuwaona na kuungana na kina S. Chrys. Na wengineo ili kwamba Baba hapa anaitwa Mungu wa pekee wa kweli, pasipo kuwajuuisha Mwana na Roho Mtakatifu, ambaye ni yeye huyu Mungu wa pekee wa kweli na Baba, bali ni kutenganisha tu na miungu yaa uwongo ya Wamataifa. Hebu na Wasosiniani wajue na kukumbuke kuwa (1Yohana aya ya 20), Mwana wa Mungu, Kristo Yesu ndiye anayeitwa kwa haraka haraka Mungu wa Pekee wa Kweli, hata kwene mandiko ya Kiyunani, ambayo kwayo wanayategemea sana kujenge hoja zao.

 

Kumbuka pia matumizi ya nembo ya zisiyo sahihi na potofu za kukejeli au kudhalilisha, kama vile Waariani wanaotafuta kupotosha au kukataa uhalali wa imani ya kiyunitariani ya Biblia. Hakuna uwezekano kwamba huyu Mungu wa Pekee wa kweli kwenye Yohana 17:3 au 1Yohana 5:20 anayetajwa sio Yesu Kristo kabisa, kwa kusaidiwa au pasipo kusaidiwa na maandiko. Ukweli wa kwamba chapisho au tafsiri ya the Douay-Rheims ni tafsiri ya Vulgate ya Kilatini na, hivyo maandiko haya yametoholewa kutoka kwenye Kilatini hayakutajwa. Neno lililo kwenye maandiko asili hayataji Kristo bali yanamtaja tu Mungu wa Pekee wa Kweli ambaye Mwanae ni Kristo. Maana yake yanajulikana na yanaeleweka.

1Yohana 5:20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele

Yeye aliye wa kweli ni Mungu wa Pekee wa Kweli. Tunamjua yeye na tu ndani yake, yeye aliye wa kweli na mwanae Yesu Kristo. Tunamuabudu yeye aliye wa kweli, na sio mwana wake, Yesu Kristo.

 

Makosa na upotoshaji uliolikumba Kanisa la Mitume yaliendelea kutokana na mashambulizi yaliyokuwepo ya kuishambulia sheria au torati kwa ujumbe mzuri na wa heri wa Malaika, ambao kwa jinsi ulivyokuwa tu ulikuwa ni rahisi sana kuuhubiri na kuufundisha na kukomesha, hali hii ya kumuinua Kristo kwa kumlinganisha sawa na Mungu. Kila upotoshaji ulikusudiwa kulitenganisha Kanisa na mamlaka na amri za Mungu. Mara tu Uungu unapochanganwa na kweli kusahauliwa, wanaodai kuwa wafuasi wa Kristo wanapewa na kulimbikiziwa nguvu za upotevu ili wauamini uwongo (2Wathesalonike 2:11). Andiko hili linatoka kwene Isaya 66:1-4 ambapo Mungu anachagua upotevu au vitisho au shuruti za dini za uwongo, kutokana na neno ta’a’uwl (SHD 8586) maana yake ni kuchanganya au mchanganyo (kuwa ni kitu kilichopangiliwa) ambacho ni shuruti, na usahihi wake ni vitisho, ambavyo ni ubabe au upotevu. Hivyo, Paulo alikuwa ananukuu Mandiko Matakatifu yote mawili hapa na pia kwenye Warumi 1. Hivyo, vitisho vya dini za uwongo vinahusisha mateso na mikakati ya kikatili ya kuikomesha kweli. Na hii ndiyo sababu imani ya Kiyunitari imekuwa ikipitia vipindi vya mateso makali tkwa kipindi cha karne nyingi. Mara tu Uungu unapochanganywa na kuanzishwa kwa Utrinitari, ndipo upotofu unaanza na sheria au torati kushindwa.

 

Mashambulizi juu ya Uungu yameenda mbali zaidi ya hatua za majaribio rahisi kama ilivyojitokeza kwenye jaribio la kudai kuwa na usawa wa kicheo na wa umilele. Mbali na kuvifanya au kujitengenezea na kuviabudu vitu vilivyokufa au visivyo na uhai na kuviabudu, kwa mfano imani ya kumuomba Mariamu na kuwaabudu waliowapachika majina ya watakatifu na masalia ya miili au mifupa ya wafu malumbano yamekuwa yakiendelea na kupamba moto jambo linalokinza na kuishia kwenye uwepo huu huu wa Mungu akiwa kama ni nguvu inayoendelea. Hoja zenyewe zinatuama kwenye misingi ya imani za Uanimism wa Kibabeloni pamoja na machipukizi yake ya kimasgakiri ya mbali na ya karibu. Hoja hizi na malumbano haya vilikuwa ni vitu vya kawaida kwenye Unostiki na sasa yanaonekana au kujitokeza kwene Teolojia Endelevu, ambayo ni mrithi wa siku hizi wa nadharia ya Kinostiki.

 

Unostiki na Kutokuwepo Uwepo wa Mungu

Mungu anatajwa kuwa ni kama kiumbe. Kiumbe inatafsiriwa kwenye lugha ya Kiingereza kuwa ni uwepo, iwe rasimali au isiyo raslimali (Kamusi ya Universal Oxford Dictionary). Mapatilizo ya hatari sana ya mafundisho ya Ukristo wa baadae, ni kwamba Kristo ni Mungu kwa maana ya kwamba Mungu Baba ndiye Mungu, kimsingi umekuwa ni Uditheism. Utenganishaji wa mara kwa mara wa Roho Mtakatifu kama kitu chenye hisia na akili kilicho tofauti na mbali na Mungu Baba na Yesu Kristo kuendeleza Utritheism. Vitu vilivyowazi kwenye kuinuka umuhimu asilia wa Umoonotheism ulipelekea kwenye jaribio la kwenye karne ya tatu ili kuweza kuwa na utambulisho wa vitu hivi vitatu kwenye muundo mmoja. Mwendelezo huu na wa zaidi unatuama na kushikamana na imani ya mrengo wa waabudu miungu mingi. Kwa mfano, madai ya kwamba Mungu (au ktu na mtu mwingine yeyote anayedhaniwa kuishi kwa namna hiyo) wa ngozi ya mtu asiyeishi kwenye Teolojia ya Ukombozi kama inavyokutikana kwenye imani za Kibudha, Uhindu au dini ningine za ki-wahamiaji wa kuhamahama.

 

Kwenye itikadi ya imani ya Mungu Mmmoja au Umonotheism, nadharia kama hiyo kimsingi ni ya kipuuzi (kama ilivyo upuuzi, na kwa kweli ni kufuru) kwa Mkristo au mwamini Mungu Mmoja kuamini kwamba Mungu haishi. Kutoka juu, Mungu anatajwa kuwa ni kama kiumbe na kiumbe anatafsiriwa kuwa ni kama kiumbe anayeishi, ama kimwili au visivyo kimwili. Kwa hiyo, jaribio la kukitenganisha kitu au kiumbe, muundo wa kuabudu miungu mingi ulienea mbali hadi tangu kabla ya kuwepo kwake. Kutokana na imani ya wa Parmenidean ya Umonism, ya kwamba jinsi inavyoweza kufanya uwepo wake. Imani ya Baadae ya Umonism inadai kuwa hali ya kutanganisha kla mmoja peke yake ni imani ya kufikirika tu au ni dhana isiyo tekelezeka.

 

Tumeona kwamba msimamo wa kibiblia una Mungu mmoja tu mkuu na mwenyezi, Eloa, na Kristo na wana wa Mungu ni viumbe wadogo na wasaidizi. Kwenye Dola ya Kipagani ya Warumi, sheria au amri kama ilivyotolewa kwa Wayahudi ilipingwa vikali sana na wenye fikra wote waliofuatia baadae. Ukataaji au upuuziaji wa sheria kwa msingi endelevu na wanateolojia wanaopinga maazimio ya mtaguso wa Nikea ulipelekea kuwepo kwa msimamo wa kihafidhina wa wapinga Usemitiki wa vitabu na maandishi ya Athanasius na wanateolojia wa zama kale za kabla ya mtaguso wa Nikea. Sababu yake inadai kama ifua avyo.

 

Torati au sheria iliyotolewa na Mungu Baba haiipo imara kiasi cha mwanadamu kushindwa kuibadilisha kwa kusingizia hadhi yake ya kimamlaka ya kuwa msaidizi. Kwa hiyo, ndipo Kristo alipoinuliwa na kanisa kwa kiasi cha kumlinganisha na Mungu, kwa kanisa kudai kuwa limepewa mamlaka ya kuigeuza au kuyarekebisha maandiko ya Agano Jipya. Lakini mchakato huu ulikuwa ukifanyika taratibu sana na bila papara.

 

Catherine Mowry LaCugna na Karen Armstrong wote wawili walionyesha kwamba kwa sehemu kubwa kanisa lilikuwa msaidizi hadi kufikia karne ya nne na kwamba mafundisho ya umilele na usawa wa hawa wote wawili yalikuwa ni madai yao ya baadae. Lengo hapa ni kutilia maanani mafundisho asilia ya mwanzoni. Mchakato wa kuyaingiza mawazo haya ulianza kwa kushambulia uwepo wa Mungu kama ni mtu mmoja na kumuinua zaidi ya uwepo wake. Fundisho la kwamba Mungu hakunenwa kuwa yupo, likawa zaidi ya hali yake ilivyo, lililetwa na kupendekezwa kwanza na Basilides mwanazuoni na msomi wa Kinostik aliyekuwa anafundisha huko Alexandria wakati wa utawala wa Mfalme Hadrian. Itikadi na mafundisho yake yalishika kasi kwenye mwaka 125 BK lakini hakumudu kuupata umaarufu mkubwa (soma kitabu cha Schaff, History of The Christian Church, (Historia ya Kanisa la Kikristo), Vol. II, pp. 467-468). Uthibitisho wa kimapokeo kuhusu uwepo wa Mungu kama vile hoja za kiontolojia na kiontolojia hauwezi kuonyeshwa hapa kuwa ni michoro au alama muhimu. Hoja za kwamba Mungu yuko zaidi ya uwepo wake au hafungiki mahali pamoja kama kuwa hawezi kuwa kwenye umoja au peke yake ambaye anaitendea kazi ya stara au Ghiliba unafafanuliwa vya kutoksha kwenye Kitabu cha 2 kinachoshughulikia teolojia iliyopelekea kwenye mtguso wa Nikea na ule wa Constantinople na kuingizwa kwa imani ya Utatu au Utrinitari.

 

Kimsingi, madai kama haya ni ya ki Mmonistiki na, kwa inavyoonekana hapo juu ni kwamba hayana msingi wowote wa kibiblia. Hata hivyo, mafundisha ya namna hii yalielezewa tu baada ya miaka 400. Hatua za muhimu ni za muhimu kwa uelewa wowte wa mchakato ule na utaelezewa kwa msingi endelevu kwenye Kitabu cha 2. Kinachojiri kueleweka ni kwamba Ukristo wa siku hizi hauna uhusuano wowote na wala haufanani kwa lolote na Ukristo wa karne ya kwanza uliokuwa umejumuisha Wayahudi na Wakristo waliokuwa wa mrengo wa kuamini Mungu mmoja au Umonotheism hasahasa kwa jinsi ulivyoelezwa kwenye maandiko ya Agano Jipya. Shambulio lililofuatia kwenye teolojia ya Kiyahudi kuhusu ujio wa Masihi na mamlaka ya Maandiko Matakatifu lilianza kwa kukataa marejesho ya kipindi cha Milenia yanayofuatia ujio wake wa mara ya pili. Hoja yenyewe ilikuwa ya kawaida na ilijulikana sana katika karne ya ishirini kwa wanazuoni wasomi wa Kiathanasian.

 

Masihi Mwenye Ujio wa Aina Mbili

Kurudi au ujio wa Masihi utakuwa ni kwa ajili ya kuja kuansiaha Utawala au Ufalme wa Mungu wa millennia, ambao utaongozwa kwa mujibu wa maandiko ya Torati na sheria za Mungu kwenye utaratibu wa utawala wa kawaida wa kimwili. Ili kufanikisha mkakati huu wa kiutawala, ni muhimu kuwa Masihi ashike hatamu za utawala wa dunia kwa nguvu katika siku za mwisho. Vitabu vya kinabii vya Isaya, Ezekieli, Danieli, Zekaria na Ufunuo zimeeleza kwa wazi sana kuhusu kipindi hiki cha kuanza na kuendelaa kwa Ufalme huu. Hususan kitabu cha Ufunuo kimeelezea wazi kuwa kipindi hiki kitadumu kwa miaka elfu moja (Ufunuo 20:1-4). Wanazuoni wa siku hizi wanajaribu kupinga ukweli na uhalisia wa unabii kwa kudai kwamba maandiko haya yaliandikwa na Kanisa la karne ya kwanza lililokuwa linatuama kwenye msingi wa mafundisho ya kinadharia bahatishi tu (mfano wake waweza kuuona kwenye kitabu cha Bob Barnes (ANU) The Bulletin, 24-31 January 1995, art. ‘Apocalypse Sometime’, pp. 42-43). Kitabu cha the DSS kinaonyesha kwamba imani ya Kiyahudi ilitarajia Masihi wa ujio wa aina mbili (soma kitabu cha G. Vermes, cha The Dead Sea Scrolls in English [Nakala ya Kiingereza ya Gombo la Bahari ya Chumvi], hasahasa mahali pasemapo Messianic Anthology [Antholojia ya Masihi] na tafsiri ya sehemu ya kumi na tatu kutoka sehemu unayosema pango XI). Mstari wa uzao wa Masihi ulikuwa ni wa Nathani na Lawi (soma Zekaria 12:10; sawa na kwenye Luka 3). Antholojia ya Masihi inatilia maanani na iko makini sana na ahadi za Lawi zilizo kwenye Kumbukumbu la Torati 33:8-11 na 5:28-29. Maandiko yanamuonyesha nabii anayetajwa kwenye Kumbukumbu la Torati 18:18-19 na inamtaja au kumuonyesha Masihi kama inavyofanya Hesabu 24:15-17. Masihi Haruni na Masihi wa Israeli walikuwa ni mtu mmoja huyohuyo kwa Kanuni au Sheria za Kidameski (VII) na nyaraka nyingine zisizochapishwa wala kufundishwa za pangoni IV (Vermes, p. 49). Tafsiri ya Korani inamtaja Melkizedeki kuwa kama Elohim na El. Hii inatokana na dhana ya hukumu ya mwisho iliyotabiriwa kufanywa na Masihi Kuhani na ukuhani wake. Isaya 52:7 inatumia jina elohim ikimaanisha ujio wa Masihi akirudi huko Sayuni (soma Waebrania 12:22-23). Ilijulikana kuwa alikuwa anafahamika na malaika mkuu Mikaeli na alikuwa ni kiongozi au mkuu wa Wana wa Walioko Mbinguni au Mungu Mwenye Haki.

 

Kwa hiyo, dini za mrengo wa Kiyahudi zilifundisha,kuwa Masihi ni kama Mikaeli (aliye kwenye Danieli 12:1). Nadharia na fikra hizi zilikuwa ni makosa. Jina Melkizedeki lilikuwa na maana ya kuwa Mungu Wangu Ndiye Haki au Mfalme Wangu ni wa Haki (Haki na Utakatifu vinafanana maana zake) (kwa kujibu wa kitabu cha Vermes, cha Dead Sea Scrolls in English [Toleo la Kiingereza la Gombo la Bahari ya Chumvi], p. 253). Ilidhania pia kwamba Melkizedeki lilikuwa ni jina la kiongozi wa Jeshi au Nuru, ambao tuliyemuona, ni kazi ya Masihi (Vermes, p. 260).

 

Nadharia hizi za kifikra zimetokana na kuharibiwa kwa Agano la Amram. Ambacho kilibakia kwenye sheria na msisitizo wa Melkizedki-Masihi huko Essene. Kama Melkizedeki angelipokuwa Masihi ndipo kungekuwa na tatizo kubwa kuwezekana aje kuzaliwa hapa duniani na kujitoa dhabihu.

 

Fikra za Wakristo kudhani kwamba Melkizedeki ni Masihi zinatokana na kutoelewa maandiko yaliyo kwenye Waebrania 7:3. Maneno yasemayo hana baba, wala mama na wala hana mwana au zao (apator nk.) yanataja umuhimu wa kuandikwa rekodi yake kwenye mstari wa ukoo wa Haruni (Nehemia 7:64) kwa ukuhani wa Walawi.

 

Neno mwanzo wa siku na mwisho wa maisha lina maanisha umuhimu wa kuanza kazi akiwa na umri wa miaka thelathini (Hesabu 4:47). Kuhani Mkuu alirithi huduma yake tangu siku ya kufa kwa mtangulizi wake. Melkizedeki hakuwa na sharti kama hilo. Kitabu cha Waebrania kinaandika kuwa alikuwa mtu au mwanadamu (Waebrania 7:4). Aliumbwa kama Mwana wa Mungu (Waebrania 7:3) lakini hakuwa Mwana wa Mungu ambaye alikuwa Kuhani Mwingine (Waebrania 7:11). Hivyo basi, wateule wote wanaweza kushiriki kwenye huduma hii ya kikuhani, wakifanyika kuwa kama Mwana wa Mungu, pasi kujali uhusiano wao wa kinasaba wa uzao wala umri wao, wakiendelea milele. Ni kama Melkizedeki alivyokuwa nasi pia twaweza kuhudumu (soma jarida la Melkizedeki (Na. 128)). Waessene walipotosha andiko linalomwelezea Masihi ni kama wanavyofanya wahafidhina wa nyakati hizi. Inaonekana kuwa kitabu cha Waebrania kuwa kiliandikwa hivyo na kusahihisha kosa hili lakini chenewe kikiwa kimekosewa pia. Mwandishi Midrash anasema kuwa alikuwa Shemu (Rashi) akiwa mfalme (melek) wa mahali pa haki (tsedek) (kwa mujibu wa Abraham ibn Ezra & Nachmanides). Mahala hapa palikuwa ni pale ambapo Hekalu linapaswa kujengwa kwa ajili ya Uwepo wa Mungu au wa Kimbinguni, ambapo hii Midrash inapasa kuwa huko Yerusalemu kwa ujumla, kutokana na andiko linalosema haki itakuwa ndani yake (Isaya 1:21) (kwa mujibu wa ibn Ezra & Nachmanides, soma pia Soncino, fn. Hadi Mwanzo 14:18).

 

Lakini lililo muhimu sana ni wazo kuhusu Baraza la Elohim lilikuwa kamili na halikanushiki au kupingika kama ni maana iliyoeleweka vizuri kwenye maandiko ya Agano la Kale yanayomhusisha elohim. Mfumo au muundo wa usaidizi wa elohim unaeleweka kwa upande mmoja ila haueleweki kwenye uhusiano wake na Mikaeli na Melkizedeki. Ufunuo 4 na 5 inaonyesha kuwa kundi hili lilikuwa na idadi ya washiriki thelathini wakiwemo makerubi wanne. Kwa hiyo vipande thelathini vya fedha vilihitajika ili kumsaliti Kristo (Mathayo 27:3,9; sawa na Zekaria 11:12-13) kama ilivyokuwa chukizo dhidi ya Uungu wote au Baraza la ndani. Wazzee walipangiwa kusimamia maombi ya watakatifu (Ufunuo 5:8) na Kristo ndiye Kuhani wao Mkuu. Alikuwa ni mshirika mwezao aliyeonekana kustahili kufungua kitabu au gombo la mpango wa Mungu aliwaondolea dhambi wanadamu na kuwafana kuwa ufalme na makuhani wa Mungu wetu, yaani Mungu wa Baraza la Kristo (Ufunuo 5:9-10). Msamaha wa dhambi wa wanadamu ni sehemu ya marejesho au matengenezo yatakayotokea au kufanyika wakati wa kurudi kwake Masihi akiwa kama Mfalme wa Israeli, kwenye ujio wake wa kwanza anajulikana kama Masihi wa Haruni. Ujio huu wa kwanza wa Kimasihi ulikuwa ni upatanisho kwa ajili ya dhambi na kuanzisha ukuhani wa Melkzedeki.

 

Marejesho ya nyakati za mwisho yalijulikana kuwa ni mwendelezo wa elohim kama ulivyoonyeshwa kwenye Zekaria 12:8. Kwenye marejesho ya siku za mwisho wakati atakapokuja Masihi huko Sayuni, kama ilivyoeleweka kwenye Waebrania 12:22-23, mchakato wa matukio ya ujio wake yatahusisha mkakati wa kuulinda mji wa Yerusalemu na kuwaimarisha wakazi wake watakaokuwemo kwenye mji huo kwa utawala wa millennia. Lakini kumbuka kuwa Zekaria anaenda mbali sana kwa kusema:

Na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu (elohim), kama Malaika wa YHVH mbele yao. (msisitizo umewekwa).

Maana yake hapa yalikuwa kwamba Zekaria alipewa kujua kwamba Malaika wa YHVH alikuwa ni elohim na kwamba watu wa nyumbani wa Daudi (ambao walikuwa wamekwishakufa muda mrefu uliopita) walitakiwa kujumuika na wale ambao kwa wenyewe t uni elohim kama sehemu ya watu wa nyumba ya Daudi.

 

Zekaria aliandika mwishoni mwa kipindi cha Agano la Kale akiwa ni moja ya vitabu vya mwishoni kuandikwa (inadhaniwa kuwa ni takriban mwaka. 410-403 KK, Nyongeza 77 ya tafsiri ya Companion Bible inasema). Kuelewa mfululizo wa matukio ambayo hayajabadilishwa kwa kudumu kwa kipindi cha kuyaweka pamoja maandiko.

 

Hitimisho

Utokana na tafsiri ya DSS tunajua uelewa ulikuwa wa haraka wakati wa Kristo. Mafundisho mapotovu nay a kizushi ya Wakolosai yalijumuisha mhimili wa Baraza la Elohim. Huko Galatia walianza kuamini ushikaji wa mapokeo kwenye utimilifu au mkakati wa maroho machafu yatesayo na yadanganyayo watu wakikosa kujua kuwa walikuwa ni mapepo.

 

Nyaraka zilizoandikwa kwa makanisa yote mawili ya Kolosai na Galatia zinatumika ili kumfanya Kristo kuwa ni mwombezi pekee na kamili na anayetosheleza kati ya wateule na Mungu. Nyaraka hizi hazikuandika ili kuitangua torati. Kamwe Mtume Paulo hawezi na kumkanganya Kristo. Vivyohivyo Yohana alikanusha na kupinga toleo lililoenea zaidi kwa uzushi wa namna hiyohiyo bali, kipindi hiki, mtu anayetafuta kumuinua Kristo na huku akipinga kufa au kifo chake au dhabihu yake kamilifu aliyoitoa. Kujua kuhusu Uungu kukaanza kubadilishwa kwenye karne ya pili. Ushahidi wa kupotosha kosmolojia unaelezwa kwenye maandiko mengi. Hoja kuhusu makosa haya kuhusu Kristo kuwa Mungu alikutatanazo Mtume Yohana na ilisababisha kuanza kwa hila makanisani.

 


 

Nyongeza

 

Matumizi ya Neno Uzushi Kwenye Kanisa la Mitume

 


Neno uzushi linatumika kwene maandiko au nyaraka za mitume na limetafsiriwa kwa namna mbalimbali ili kuweka maana mbalimbali tofauti. Kwa mfano ni:

 

Matendo 5:17 inahusisha na vikundi vikubwa vya kidini au sehemu ya Masadukayo waliokuwa wanatumia airesis.

 

Matendo 15:5 inatumia neno aireseõs kutaja kundi la Mafarisayo. Kwa hiyo kazi kuu mbili za kiutendaji wa Wayahudi walioyataja mafundisho haya kuwa n uzushi. Kwa hiyo, hakuna uhusiano wa kikashifa.

 

Matendo 24:5 inatumia neno uzushi kwenye muundo wa kigrama aireseõs inapoelezea vikundi vya dini za Wanazarayo. Hivyo, kanisa la kwanza lilitajwa kuwa ni kama la wazushi.

 

Matendo 24:14 inatumia neno uzushi kwa muundo wa kigrama airesin inayomaanisha kuwa ni njia. Kanisa lilikuwa ni njia wanayoiita kikundi cha kidini (uzushi).

 

Matendo 26:5 inamnukuu Paulo kama kusema kwamba kwa mujibu wa sekti yenyewe kabisa ya dini ya Kiyahudi, aliishi kama Farisayo. Neno lililotumika ni airesin au uzushi. Tena hakuna kusudi la kufanya kashifa ya wazi.

 

Matendo 28:22 inataja kuwa aireseõs au uzushi ambayo imetafsiriwa kama kikundi cha kidini au sekti kwakuwa ni wazi sana kwamba kanisa linachukuliwa na mtazamo wa kiutofauti wa mawazo haukuwekwa sawa kwa namna sawa kama zilivyokuja kufanyiwa na Kanisa la baadae la Kiathanasian.

 

2Petro 2:1 inaiita mafundisho ya kizushi (aireseis) ya uharibifu ambayo yanatafsiriwa kuwa ni mawazo au nadharia yenye kuharibu na kuangamiz (RSV). Tafsiri ya KJV imetafsiri andiko hili kama ni mafundisho ya kizushi tu.

 

Wagalatia 5:20 inayaita migawaniko na aireseis imetafsiri sekti au sehemu ya maroho (RSV). Andiko hili hapa haliitaji tofauti yoyote ya kimtazamo au mawazo kuhusu mafundisho. Andiko hili linajiri matawi ya sheria au torati ambayo yalipasa yawe wazi kwa wale wenye Roho Mtakatifu. Kwa hiyo Paulo anatumia neno hili ili kufunika makosa ambavyo inatumika kwa kuwaelimisha wateule kama tunavyoona kwenye 1Wakorintho.

 

1Wakorintho 11:19 inaonyesha kuwa mafundisho haya ya kizushi (aireseis) yametafsiriwa sekti (RSV) kwenye makanisa yanaruhusiwa na ni ya muhimu. Tofauti kati ya mawazo makanisani inawafanya wateule kuichunguza na kuinisha au kuipima kweli na pia kuwaonyesha wale wateule wenye Roho Mtakatifu na kuipambanua kweli. Kwa hiyo, kitendo cha kuzima kwa shuruti mawazo stahiki (mahali yanapokuwa hayavunji sheria) ni kinyume kabisa na mafundisho yaliyo kwenye 1Wakorintho.

 

q