Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[096]

 

 

 

Mkanganyiko Kuhusu Sheria

Toleo La 3.0 19950318-19990614-20080128)

 

Jarida hili linatathmini tofauti iliyoko kati ya kanuni au sheria za kijamii na za utoaji wa dhabihu. Tofauti hii iweka sehemu ya msingi wa mambo yaliyotokee kwenye zama za uandishi wa kitabu cha Mwanzo. Jarida hili pia linafafanua kwa kina zaidi mambo kadhaa yanayohusiana na sheria za Mungu. Tofauti ya msingi iliyofanywa na Wanamatengenezo ileorodheshwa kama Msingi wa Imani tangia Waraka wa Pili wa Ukiri wa Imani wa Wahelvetiki kati ya Nyaraka Thelathini na tisa za Imani ya Kanisa la Uingereza za mwaka 1571 na nyingine za wana Matengenezo hadi kufikia za Wamethosti zilizojulikana kama Ukiri wa Imani ya Kidini ya mwaka 1784. Tangazo hili ni la muhimu kwa manufaa yao wenyewe.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1995, 1999, 2008 Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mkanganyiko Kuhusu Sheria



Baadhi ya mafundisho yaliyoko kwenye Ukristo wa leo ni kujaribu kudai kwamba Sheria au Toari imepitwa na wakati na haihitajiki tena, jambo linalotokana na kutozielewa vizuri nyaraka za Mtume Paulo zilizo kwenye Agano Jipya. Madai haya sio sahihi. Mafundisho haya yameanzishwa kutokana na kutokuelewa kile kilichoondolewa na kukomeshwa na dhabihu aliyoitoa Kristo na kugongolewa pale mtini au stauros, kunakoelezwa kwenye Wakolosai 2:14. Kristo alifuta mashitaka (cheirographon) kwenye mashitaka yaliyokuwa yanatukabili (au, yalikuwa yanatukabili tukiwa tumeshitakiwa; soma fasiri ya Biblia ya Marshall’s Interlinear, RSV) pamoja na madai yake. Iliondolewa mbali na kupigiliwa mtini au kwenye stauros.

 

Je, ni yapi haya mashitak yanayoelezewa hapa? Ni nini kilichoondolewa kwa dhabihu hii ya Kristo?

 

Kwa kweli haikuwa Torati ya Mungu iliyoondolewa. Tofauti iliyoelezwa na Mitume inaonyesha kuwa Amri zilizowekwa na MUngu zilikuwa muhimu nab ado zinaendelea (soma hapo chini). Cheirographon ni jalada au waraka uliotolewa kwa ajili ya kufutiwa mashitaka. Linatokana na neno la Kiyunani dogmasin, ni mfumo wa utaratibu ambao unatokana na Torati ya Musa (kutoka Waefeso 2:15). Uhusiano uliopo kati ya Mungu na Torati yake ni wa muhimu sana.


 

Mungu ni

 

 

Torati yake ni

 

 

Mtakatifu

(Ezr 9:15)

 

Takatifu

(Zaburi119:172)

 

Mkamilifu

(Mat. 5:48)

 

Kamilifu

(Zaburi 19:7)

 

Mtakatifu

(Law. 19:2)

 

Takatifu

(Warumi 7:12)

 

Mwema

(Zab. 34:8)

 

Njema

(Warumi 7:12)

 

Mkweli

(Kum. 32:4)

 

Truth

(Zaburi 119:142)

 

 


Mungu habadiliki. Na ndivyo ilivyo, kwamba Kristo ni yeye Yule, jana, leo na hata milele (Waebrania 13:8) kwakuwa ana ukamilifu wa asili ya kimbinguni (Wakolosai 1:19; 2:9). Torati ni ya muhimu katika kuyaonyesha mapenzi ya Mungu, ikitangulia au kuonyesha asili yake kamilifu, na iliyoandikwa kwenye mioyo ya wateule. Sheria za Mungu ni haki, ya kweli na njema (Nehemia 9:13). Wateule wametahiriwa mioyo yao kwa kuwa wanachukua hadhi ya umbinguni (2Petro 1:4), na kushindania ili kuwafanya wote waufikilie utimilifu (pleroma) wa Mungu (Waefeso 3:19), kama alivyokuwa Kristo. Watu wengine wote inawalazimu kuishika Torati ya Mungu. Wanahukumiwa kwa kutobadilisha baadika kwao (KJV); au kwa maneno mengine, kwa kuwa hawazishiki sheria (RSV, Zaburi 55:19). Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana.  (Zaburi 119:1). Torati inatimilika ndani ndani yetu sisi tunaoenenda sawasawa katika roho (Warumi 8:4). Sio wasikilizaji wa Sheria walio watakatifu, bali ni wale wanaozitenda na kuzitii (Warumi 2:13).

 

Uashikaji wa Amri za Mungu ni wa muhimu kwenye upendo na kumjua Mungu (1Yohana 2:3,4; 3:22; 5:3) na Kristo (Yohana 14:15,21), na kupokea maelekezo ya Roho Mtakatifu (Yohana 14:21; 1Jn. 3:24; Matendo 5:32), na Baraka za Mungu (Ufunuo 22:14). Kitendo cha kuvunja au kutozitilia maanani au mafundisho ya kuzipuuzia au kuzivunja Sheria ilikatazwa na Kristo (Mathayo 5:19).

Mathayo 5:19  Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.

 

Ukweli wa mambo ni kwamba alichokuwa anakiongelea Paulo kwenye maandiko ni kwamba sio tu aina mbili za sheria, bali pia kazi nyingine ya tatu iliyopotea kwa karne kadhaa. Aliyaita matendo haya ergon nomou, iliyotafsiraiwa kama Matendo ya Sheria, ambayo kwa kweli yalikuwa ni kundi lingine la maandiko lililopotea kwa kipindi cha takriban miaka elfu. Yalionekana yalipochimbuliwa na yanajulikana kama Gombo za Bahari ya Chumvi au the Dead Sea Scrolls na imeelezwa kwa kina kwenye jarida la Kazi za Maandiko ya Torati (Na. 104) [The Works of the Law Text - or MMT (No. 104)].

 

Paulo alifundisha kuwa kutahiriwa au kutotahiriwa kwao hakuna kinachoongezea chechote ila la muhimu ni ushikaji wa Sheria za Mungu [ndiko muhimu] (1Wakorintho 7:19). Ingekuwa vigumu sana ajichanganye mwenyewe tena kwa maandiko yake ya Wakolosai au Wagalatia (mfano Wagalatia 3:10). Kwa hiyo anaongelea mambo mawili ya sheria.

Sheria ile iliyokamilishwa na Kristo pale Kalvary, kwa hiyo alipaswa kuwa mojawapo ya aina ya vitu ambavyo havibadiliki lakini vinatimilika. Tofauti ya kawaida ni ile ya Sheria ya Maisha kwenye Jamii na Sheria za mambo ya Kidini. Sheria ya madili ya Jamii zilizoongelewa kwenye Amri Kumi za Mungu. Sheria hizi za Taratibu za Kidini zinajulikana kama Torati ya Musa. Tofauti itaonekana kuwa kama haitoshelezi. Andiko linaloelezea Matendo ya Sheria inaonesha kuwa jambo moja kubwa la kukosa uelewa kunakoiathiri itikadi ya waantinomia walio kwenye Ukristo wa leo. Tofauti imewekwa kwa wazi zaidi kutokana na mlinganisho ufuatao.


 

 

Torati ilikuwa

Sheria za Dhabihu au za Kidini zilikuwa

1. Imetolewa na Mungu kwa mkono wa Malaika pale Sinai (Kutoka 20: 1,22; Deut. 4:12;13; 5:22);

1. Zilinenwa na YHVH; zikaandikwa na Musa Musa (Kutoka 24:3,4,12); zilitolewa kama nyongeza ya zile Amri Kumi (Kutoka 24:12);

2. Ziliandikwa na Yahova (Kutoka 31:18; 32:16);

2. Ziliandikwa na Musa (Kutoka 24:4; Deut. 31:9);

3. Kwenye mawe (Kutoka 24:12; 31:18);

3. Kwenye kitabu (Kutoka 24:4,7; Kumb. 31:24);

4. Ilitolewa na Yahova na kupewa Musa (Kutoka 31:18)

4. Ilitolewa na Musa kwa Walawi (Kum. 31:25,26);

5. Iliwekwa na Musa kwenye Sanduku la Agano (Kum. 10:5);

5. Iliwekwa ndani ya sanduku la agano na Walawi (Kum 31:26) ambayo ilikuwa ni ushuhuda kwa Israeli.

Torati

Sheria za dhabihu au za Kidini

6. Ilihubiriwa pamoja na kanuni za kimaadili (Kut. 20:3-17);

6. Inahusiana na taratibu za mambo ya kiibada (kutoka kwenye matumizi yake yalivyoelekezwa kwenye vitabu vya Kutoka, Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati);

7. Inaidhihiridha dhambi (Warumi 7:7);

7. Inahusu utoaji wa sadaka za dhambi zilizofanywa (soma Mambo ya Walawi);

8. Inaonyesha kuwa uvunjifu wa sheria ni dhambi (1Yohana 3:4) na mshahara wa dhambi ni mauti (Warumi 6:23).

8. Hakuna dhambi kuzivunja kwa kuwa zimetanguka (Waefeso 2:15); kwahiyo, pasipo sheria hakuna dhambi au uovu utakaogundulika (Warumi 4:15).

9. Tunapaswa kuzishika sheria zote (Yakobo 2:10);

Tusiivunje hata yodi moja ya Torati (Mathayo 5:19)

9. Mitume hawakuamuru hivyo (hawakufundisha au kuamuru; diesteilametha) kuzishika sheria (Matendo 15:24);

10. Kwakuwa tutahukumiwa kwa mujibu wa torati (Yakobo. 2:12);

10. Hatupaswi kuhukumiwa kwa kuzishika (Wakolosai 2:16);

11. Mkristo anayeishika torati hii amebarikiwa kwa matendo yake (Yakobo 1:25);

11. Hatuhesabiwi haki kwa sheria bali ni kwa imani (Wagalatia 5:1-6);

12. Ni sheria kamilifu ya uhuru (Yakobo 1:25; sawa na Yakobo 2:12) kwa kuwa torati ni kamilifu (Zaburi 19:7);

12. Uhuru unatokana na imani na wala hatuhesabiwi haki kwa sheria (Wagalatia 5:1,3).

13. Torati hii ilianzishwa kwa imani katika Kristo

(Warumi 3:31); haikutanguka (Mathayo 5:17);

13. Kristo alikomesha migawanyiko ya sheria (Waefeso 2:15); madeni (Wakolosai 2:14); na muundo wenyewe (Wagalatia 3:19).

14. Kristo alikuja kuitimiliza sheria na kuzitukuza (Isaya 42:21);

14. Kristo alifziutiliambali hati zote za mashitaka yaliyokuwa dhidi yetu (Wakolosai 2:14).

15. Tunajua kwamba torati ni ya kiroho (Warumi 7:14 sawa na aya ya 7).

15. Hizi sheria ni za mambo ya amri za kimwili (Waebrania 7:16). Mungu aliwataabisha Israeli kwa kuwapa sheria ambazo wasingeweze kuishi kwazo kwa kuzihalifu kwao na kuzivunja (Ezek. 20:25). Sheria hizi hazikufanya jambo lolote kamilifu.

 

 


Muundo wa kimwili wa sheria ya utoaji dhabihu na alama au ishara zinazoonekana vilipaswa virudiwe kila mwaka hadi pale Kristo alipolipa mara moja tu na kwa wote kwa ajili ya dhambi zetu.

 

Sheria ya utoaji wa dhabihu zilipaswa kuondolewa kabisa ili ituwezeshe kuuimariha uhuiano wetu na Mungu kwa kiwango kikamilifu cha kimo cha kiroho. Ni kwa kupitia Krito tu na karama za Roho Mtakatifu jambo hili linaweza kufanyika, kama sisi wenyewe tulivyo kuwa ni sadaka iliyo hai za mfumo huu, tukiyatoa maisha yetu ili kutumikiana.

 

Maandiko ya Musa yanaelezea Amri Kuu mbili ambazo kwazo zinajumiuha mambo haya mawili. Torati yote na Manabii (sawa na majarida ya  Amri Kuu ya Kwanza (Na. 252) na  Amri Kuu ya Pili (Na. 257) [The First Great Commandment (No. 252) and The Second Great Commandment (No. 257)].

 

Kwa hiyo, kunamkanganyo wa heria na mkanganyo huu unazihusu wazi sheria za mambo ya kijamii. Sheria za Mungu za kijamii zinamfanya mtu wa kiroho awe mkamilifu kama zilivyoanzihwa, kuheshimika na kutukuzwa na Kristo kwa njia ya imani na kutoa uhuru. 

 

Ziliandikwa kwa chanda cha mkono wa Mungu na zinaitwa Sheria za Ufalme (Kutoka 31:18; Yakobo 2:8). Tunahukumiwa kwa sheria hizi, ambazo Kristo amezitukuza kwa kadiri zote. Kwa hiyo kufanya kinyume chake ni awasawa na kuzini. Sheria yote ni kuu na wala hakuna iliyo ndogo kwenye umuhimu wa kumfanya mtu awe mtakatifu. Manabii wamezitafiri sana sheria hii ya mambo ya kjamii kama zilivyoainishwa kwenye Amri Kuu Mbili ambazo zinazifafanua. Kwa hiyo, zile zinazoitwa ama kujulikana kama ‘sheria za mambo ya kidini’ ambazo kwa kweli zimegawanyika tena kwenye kundi la ‘sheria za dhabihu’ na fafanuzi za kiheria zinazotafsiri ‘sheria za kimaadili’. Kushindwa kuuelewa mkanganyo huu ni makoa makubwa ya Ukristo wa leo, yakirithi imani ya kiantinomia na Wanostiki. Ukristo huu mamboleo umefanya makosa ya kujaribu kuziondoa Sheria za Mungu kutokana na kukosea kuyaelewa maana ya nyataka za Mtume Paulo, na maana ya neno Ergon Nomou au Matendo ya Sheria. Kwa kufanya hitimiho hili na kuyakumbatia mafundisho yote ya Vitabu vya Musa au Torati kwa kile kinachoitwa sheria ya mambo ya kidini ndipo walizifananiha na taratibu za ibada za kipagani na ndipo walipojikuta wanaanzisha imani zi dini ya kuabudu Juan a Imani-siri. Ndipo Sabato ikabadilishwa na kuwa siku ya Jumapili na maadhimiho ya ikukuu ya Easter yakawekwa mahala pa maadhimisho ya Pasaka..

 

Kuzihika Amri za Mungu na Ushuhuda wa Yesu Kristo ni muhimu ili kuurithi ule mti wa uzima, kama tunavyoona kwenye Ufunuo 14:12 na 22:14. Sheria ya amri ilimeandikwa kwenye kanuni (Waefeo 2:15; Wakolosai 2:14) ilikuwa ni kivuli cha mambo mema yanayokuja (Waebrania 10:1), na iliondolewa kutokana na udhaifu wake na kutokuwa na tija kwake (Waebrania 7:18; 10:3). Ilitolewa kwa ajili ya maovu, yakianzihwa na malaika mikononi mwa mwombezi (Wagalatia 3:19). Kwa hiyo tunautarajia utaratibu wa kuondolewa dhambi kwa kupitia sheria ya dhabihu ambayo uiikuwa wa muhimu kutokana na kuendelea kwetu kwa kuhindwa kwendana na mfumo na makusudi ya Sheria. Kwa sababu hii, kumtahiri muumini mkubwa aliyebatizwa ilikuwa ni ishara ya kimwili wa utambulisho wa utaifa wa taifa ambalo lenyewe tu lilikuwa ni la kiroho, na ambalo lilikuwa na fungamano la kimwili la kitaifa. Kwa hiyo haukuwa na faida yoyote zaidi tu ya mambo ya kiroho ya kila mtu binafi yake (sawa na  jarida la Utakao na Tohara (Na. 251) [Purification and Circumcision (No. 251)].

 

Cha kuhangaza kingine ni kwamba, Torati ilitolewa huko Sinai. Sheria nyingine za Mungu za kijamii hazikutolewa Sinai. Ilikuwepo tangu uumbaji, tangu mwanzo wa kuwepo kwa Mungu. Dhali ilikuwepo hata kabla hata ya kutolewa Torati na kukabidhiwa Musa (Warumi 5:13), kwa hiyo, madhara ya kuzivunya Torati yalikuwa yamekwisha julikana tayari tangu Adamu, kwa hiyo dhambi haihesabiwi mahali passipo sheria. Wakati dhambi zilipozidi chini ya Sheria huko Sinai, ndipo neema iliongezeka (Warumi 5:15-21). Dhambi ni matendo yaliyo kinyume na asili na mapenzi ya Mungu (Zaburi 51:4).

 

Shetani alimtenda dhambi Mungu kwa kumdanganya Hawa atende kinyume na mapenzi ya Mungu na kwa hiyo aliwaibia wote wawili taji zao, yaani ya Adamu na ya Hawa na kuuharibu uhusiano wao mwema na Mungu. Shetani alivunya Amri ya Kwanza, ya Tano, ya Sita, ya Nane, ya Tisa, nay a Kumi  (Mwanzo 3:1-4; Isaya 14:13-14; Ezekieli 28:2-10). Shetani mara nyingi anafanya viwakilishi vya kimapepo, wanaojifanya kuwa vitu vya kuabudiwa na kulitia unajisi au kulikufuru jina la Mungu, na hivyo kuzivunja Amri za Pili na ya Tatu za Mungu.

 

Nyakati za Kristo, ilieleweka kuwa Shetani na mapepo waliacha makazi yao ya kwanza, na kuja kushiriki matendo ya uzinifu na binti za wanadamu na huko kulikuwa ni kuivunja Amri ya Saba (Mwanzo 6:4; 1Wakorintho 11:10; Yuda 6; tzama na kuisoma hasa tafsiri ya Biblia ya New English Bible kwa maelekezo zaidi ya hili andiko la Yuda 6; pia soma DSS, Genesis Apocryphon and 1Enoch). Kwa kipitia imani za dini za uwongo, Shetani na mapepo wameishambulia Amri ya Nne. Kwa hiyo, Torati inafanya mahusiano ya kweli kati ya viumbe wasio na mwili pamoja na wale wenye mwili. Kwa hiyo hawa ni wa kiroho wakati kwamba wanadamu ni wa kimwili. Waliouzwa kwenye utumwa wa dhambi (Warumi 7:7,14), wakiwa ni mapepo waliofukuzwa watoke mbele ya machoni pa Mungu. Mwongofu anaifurahia Sheria ya Mungu kutoka moyoni (Zaburi 119:1 ff.; Warumi 7:22). Wao sio hawadaiwi au sio watumwa wa mwili, bali wako Rohoni kama Wana wa Mungu (Warumi 8:9-17).

 

Mwanadamu aliasi kwa kuzivunja Amri za Kwanza, Pili, Nane na Kumi kwenye Bustani ya Edeni (Mwanzo 3:17) (pia soma jarida la Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni (Na. 246) na  Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemuj ya 2, Kizazi cha Adamu (Na. 248) [The Doctrine of Original Sin Part 1 The Garden of Eden (No. 246) and Doctrine of Original Sin Part 2 The Generations of Adam (No. 248)].

 

Kaini alitenda dhambi na kuvunja Amri ya Sita na Kumi kwa kumuua ndugu yake Abeli (Mwanzo 4:7-8). Kaini na Abeli wanamwakilisha Kristo na Shetani kwa Watakatifu. Sadaka ya mifugo ya Abeli ilikubalika zaidi na Mungu, ikiashiria dhabihu ya hiyari aliyojitoa kwayo Krito zaidi ya maongeo yaliyotolewa na Kaini yaliyotokana na mazao ya Ardhini. Maana ya sadaka hizi ni ya kiroho (soma jarida la Imani ya Uvijiteriani Kwenye Biblia (Na. 183) [Vegetarianism and the Bible (No. 183)].

 

Wanefili walitenda dhambi ya kuua watu na kufanya machafuko na machukizo kabla ya Gharika Kuu na Mungu akawahukumu na kuwaangamiza (Mwanzo 6:4-5, 11-13).

 

Henoko aliingia rahani mwa Bwana kwa kuwa alikuwa mwenye haki, na huyu anaiwakiliha imani ya Sabato (Mwanzo 5:22-24) (pia soma jarida la Mashahidi (Na. 135) [The Witnesses (No. 135)] kwa kujifunza zaidi kuhusu Henoko). Uumbaji umeendelea kuwa ihara ya Sabato na maadhimisho ya Siku Takatifu zilizoamriwa (Mwanzo 1:1-2:3). Kutokana na majira ya mavuno ndipo mwonekano wa Mpango wa Mungu unavyoonekana tangu uumbaji.

 

Hamu au Kanaani aliivunja Amri ya Tano kwa kumvunjia heshima Nuhu (Mwanzo 9:20-27). Kitabu cha ufafanuzi cha Wasoncino kinaonyesha kwamba kuna mgawanyiko wa kimaoni kati ya wenye mamlaka kuhusu kama huyu Hamu au Kanaani alikuwa na makosa ama la au kama uovu alioufanya ulihusiana na uhamisho au ni kitendo cha upotovu (Soncino: Rashi, Sforno).

 

Farao alitenda dhambi kwa kumchukua Sara afanyenaye uzinifu na kuivunja Amri ya Saba ingawa hakuwa anajua kama alikuwa anakosea kutokana na udanganyifu wa Ibrahimu, ambaye pia alitenda dhambi kwa kushuhudia uwongo, na ndipo aliivunja Amri ya Tisa. Pia aliivunja Amri ya Saba kwa kuwa alimpeleka mke wake akawe mtumwa ngono, ili akazini naye mfalme (Mwanzo 12:15-20). Uzao wake uliteseka kwa utumwa huko Misri kwa kipindi cha miaka mia nne (Mwanzo 15:13). Kwa hiyo, kuna kanuni mbili zinazoonekana kuwepo hapa.  Ya kwanza ni kwamba, hali ya kutozijua Amri za Mungu hakuwezi kuwa sababu ya kutoa udhuru. Ya pili ni kwamba wateule wanawajibika kutokana na kusamambisha mataifa wajikwae au kutenda dhambi, kwa kushindwa kwetu kuwaonya ili wayaache maovu yao (Ezekieli 33:1-6).

 

Abimeleki pia alijikuta akivunja Sheria za Mungu kutokana na uwongo alioufanya Abrahamu. Mara hii Mungu aliingiliakati (kuwaokoa Israeli), kwa kuwa Abimeleki hakuwahi kumuingilia Sara. Hata hivyo, alionywa kwamba angekufa kwa kuwa alikuwa anamchukua mke wa mtu mwingine (Mwanzo 20:3-4).

 

Wote wawili, yaani Farao na Abimeleki walikuwa wanajua sana kwamba walikuwa wamezivunja Sheria za Mungu Aliye Juu Sana. Kwa hiyo kitendo cha kuwapa Torati Israeli pale Sinai kilikuwa ni cha kutilia mkazo Torati hii (au maadili) ya Mungu, na kutoa maelekezo ya ziada ya kiutawala katika Israeli, na kuyaelekeza kumuashiria Kristo.

 

Ibrahim alisaidiwa na Mungu kwenye vita dhidi ya mataifa yaliyomfuatia ili kuishambulia miji ya uwandani kwa kuwa walikuwa wamezivunja Amri za Sita na Nane, ingwaje watendo yalijumuisha miji mingi miji hiyo ya Sodoma na Gomora kwenye maangamizo makubwa (Mwanzo 14:11-24). Kwa hiyo kwa Mungu hakuna upendeleo wala haangalii sura ya mtu (Kumbukumbu la Torati 1:17; 16:19; 2Samweli 14:14; 2Nyakati 19:7; Mithali 24:23; 28:21; Warumi 2:11; Waefeso 6:9; Wakolosai 3:25; Yakobo 2:1); (sawa na jarida la Kupendela Watu (Na. 221) [Respect of Persons (No. 221)].

 

Ayubu angetenda dhambi pia kwa kuivunja Amri ya Tatu kama angemlaani Mungu ili afe (Yakobo 1:22; 2:9-10). Yakobo anajulikana kuwa aliishika Torati kabla ya kutolewa kwake pale Sinai. Kwa hiyo, maana ya dhambi (Ayubu 2:10) pia iliitangulia Sinai.

 

Esau alishindwa kumheshimu baba yake kwa kumuuzia Yakobo haki yake ya uzaliwa wa kwanza, ambaye aliichukua na kuchukua mahala pake pia (Mwanzo 25:31-34), na hivyo aliivunja Amri ya Tano. Na kwa kuwa amri hii ya Tano ndiyo yenye ahadi, kupoteza kwa haki ya uzaliwa wa kwanza kulitokea kama adhabu au hukumu yake. Kwa hiyo, Mungu aliingilia kati ili kuilinda kanuni hii hata kama Yakobo alikuwa ameivunja Amri ya Kumina kama angeivunja pia Amri ya Tisa.

 

Musa alifanyika kuwa ni elohim kwa Farao (Kutoka 4:16; 7:1) kwa kuwa nchi ya Misri ilikuwa imezivunja Amri za Mungu.

 

Wale waliotenda dhambi kwa kuvunja maamrisho ya Torati ni wale waliokuwa hawako kwenye mwili wa washika Torati. Dhambi ilikuwepo hata kabla ya kutolewa kwa Torati pale Sinai, na kwamba pasipo Torati dhambi inakuwa imekufa (Warumi 7:8). Paulo anadokeza kusema kwamba kutojua kunatoa uhuru kwenye maneno yasemayo kwaba yeye alikuwa huru mbali na Torati lakini amri ilikuja ili dhambi ziweze kufunuliwa, na akafa (Warumi 7:9). Ni wazi kabisa, kanuni zote za ushikaji wa sheria za Torati zilikuwepo wakati anaandika andiko hili. Kwa kweli hakuna kilichotanguliwa katika kipindi hiki. Agano Jipya lilikuwa halijachukua bado mahala pa Agano la Kale kipindi ambacho Agano hili Jipya lilipokuwa linaandikwa.

Waebrania 8:13 Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka.

 

Lilikuwa limekwisha isha nguvu zake tayari au litatokomea hivi punde. Njia ya kupaendela Patakatifu pa Patakatifu ilikuwa haijakuwepo kabisa.

Waebrania 9:8 Roho Mtakatifu akionyesha neno hili, ya kwamba njia ya kupaingia patakatifu ilikuwa haijadhihirishwa bado, hapo hema ya kwanza ilipokuwa ingali ikisimama;

 

Njia iliweza tu kuwepo kwa kuangamizwa Helaku mwaka 70 BK, na kutawanyika kwa watu wa Yuda. Na hii ndiyo maana kamilifu ya Ishara ya Yona nay a unabii wa ‘juma la sabini la miaka’ lililoandikwa kwenye Danieli 9:25 (soja jarida la Ishara ya Yona na Hoistoria ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)], ambalo lilihusiana na ukomo wa Agano la Kale na kuanza kwa Agano Jipya. Kwa hiyo, Agano Jipya lilihusika na sheria ya utoaji dhabihu, ambayo iliweza kukomeshwa sambamba na tukio kuhusuriwa kwa Hekalu. Agano Jipya lilihusika na ukomeshaji wa sheria za kutoaji dhabihu za wanyama, na sio kuondolewa au kukomeshwa kwa Torati yote.

 

Mambo Mengine Zaidi Yaliyo Kwenye Torati ya Mungu

 Uhusiano uliokuwepo ni kwamba Amri Kumi zilikuwa ni sehemu pekee ya muundo mzima wa Torati ya Mungu, chini ya kichwa cha habari kisemacho sheria au kanuni ya kimaadili ambayo ilikuwepo kabla ya zama za Sinai, sio sahihi.

 

Amri Kumi za Mungu ni mhimili wa Torati kwenye Amri Kuu Mbili za Kwanza na ambazo zinatokana kwenye Sheria zao zote za Manabii.

 

Sheria za vyakula ilikuwepo mapema kabla ya Gharika Kuu. Utofauti uliokuwepo kati ya wanyama safi na najisi ulifahamika na Nuhu na alielekezwa na Mungu ili awaingize kwa utaratibu wake elekevu kwenye Safina (Mwanzo 7:2-3). Kwa hiyo, utoaji wa sheria ya vyakula ulifanywa kutoka kipindi cha uumbaji. Tofauti hii ilikuwepo na ilionekana tangu kipindi cha Adamu hadi cha Abeli (tazama hapo juu). Madai ya kwamba sheria hii ya vyakula ilikuwa kwa Wayahudi eke yao yanaonyesha ukosefu mkubwa wa uelewa juu ya misingi ya kanuni za kitabibu na au za kiafya na za kimazingira zinazohusiana na mambo ya vyakula na uhusiano wake na uumbaji au afya za viumbe(sawa na ukisoma jarida la Sheria ya Vyakula (Na. 15) [The Food Laws (No. 15)).

 

Sambamba na hiyo, fundisho la kwamba sheria ya utoaji zaka imefungamanishwa kwenye sheria za utoaji dhabihu zilizotolewa pale Sinai pia ni ya uwongo. Ibrahimu alitoa zaka yake kwa Melkizedeki wa Salemu kipindi cha takriban miaka mia nne kabla ya kutolewa kwa Torati mlimani Sinai (Mwanzo 14:18-20) (sawa na majarida ya Utani wa Zaka (Na161) [Tithing (No. 161)].

 

Kwa hiyo kuna mchakato endelevu kuhusu Torati, unaoendela zaidi ya kikomo cha maandiko haya ya Musa maarufu kama Torati na yanafunika mambo ya muhimu ya maisha ya kila siku ya Waisraeli nay a dunia. Masihi ataanzisha ufalme wake katika siku za mwisho, na kwahiyo ataanzisha na kusisitiza tena maadhimisho ya Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya (Isaya 66:20) na Sikukuu zake alizoziamru (Zekaria 14:16-19; pia tazama Ezekieli 45:1 hadi mwisho, na sura ya 46:1 hadi mwisho). Kwa hiyo, maandiko ya Mambo ya Walawi 23 yana umuhimu unaoendelea na mataifa yhatalazimishwa kuishika na kuiheshimu Torati.

 

Kristo ni yeye yule; jana, leo na hata milele (Waebrania 13:8), kwa hiyo hatazipindisha wala kuzibadili Siku Takatifu ambazo atawaambia watu kuziadhimisha. Ni sawa tu na mataifa wanatakiwa kuziadhimisha Sabato na nchi itapewa mapumziko kwa ajili ya kushindwa kuzitunza sheria hizi kimatendo. Kitakachotokea kati ya ushikaji wa Torati na mapatilizo yake yhatgakwenda kuonekana pia.

 

Kwa hiyo kuna mkanganyiko wa wazi kati ya Torati yha Mungu na sheria ile iliyotanguliwa na Kristo. Hii ilikuwa ni sheria ya utaji dhabihu iliyokuwa kwenye maagizo ya kidini tu. Sheria za utoaji dhabihu hazikuzihusisha Sabato zile zilizoelekezwa kwenye Torati. Bali zilielekeza kile kilichokuwa kinafanyika siku za Sabato kipindi cha kabla ya kuangushwa kwa Hekalu zikiwa kama taswira wa Masihi anayekuja na mwanzo wa mfumo mpya, ambayo ilikuwa inanenwa tu hapo kabla. Kwa hiyo, Sabato hazijatanguliwa bado kwa kifo cha Masihi. Sabato zimefanyika kuwa za muhimu sana kwa kuanzishwa kwa Kanisa, ambalo kwazo zinafasiriwa na kupewa umuhimu. Itikadi ya kuabudu siku ya Jumapili ilichukuliwa kutoka kwenye imani za kipagani na dini za kuabudu Jua na wala hazina uhusiano wowote na Ukristo (sawa na jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235) [The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].

 

Kuelewa mkanganyo uliopo kwenye Torati na kati ya Maandiko ya Musa na sheria za utoaji wa dhabihu ni ya siku nyingi sana na yanamaana. Wanamatengenezo waliweka wazi mambo yanayokanganya. Orodha ya matangazo mengi ya ikiri wa imani na tafiti hizi na yenye nguvu yanaonekana kwenye kanisa la Waadventista wa Sabato kwenye Kitabu kinachoitwa Maswali Kuhusu Fundisho (Review and Herald Publishing, 1957, pp. 131ff.). Yana mambo yafuatayo:

 

Mkutano wa pili cha Ukiri wa imani wa Helvetic (1566), wa kanisa liinaloitwa Reformed Church of Zurich, na mojawapo ya alama zenye nguvu za kila Bara (Philip Schaff, The Creeds of Christendom, Vol. 1, pp. 391, 394, 395), kwenye sura ya 12, “Au Sheria ya Mungu,” baada ya kuchanganya zile za “kawaida” na zile za “kiibada, kuhusu sheria za kimaadili, “Tunaamini katika mapenzi yote ya Mungu, na maelekezo yoyote yanayowezekana, kwa kila eneo la maisha haya, yametolewa kikamilifu kutoka kwenye sheria hii” (sio ile tunayoweza kuhesabiwa haki kwayo, bali ni ile tunayoweza kumrudia Kristo kwa imani). Aina na kiwango kinacotakiwa kukamilisha sheria ya mambo ya ibada vimekomeshwa. “Kivuli kilikoma wakati mwili ulipokuja,” lakini sheria za kimaadili kijamii hazipaswi kuachwa au kuondolewa, na mafundisho yote yanayopinga sheria yanapaswa kulaaniwa (soma kitabu cha Schaff, Vol. 3, pp. 854-856 (msisitizo umeongezwa)).

 

Makala Thelathini na tisa za Dini ya Kanisa la Uingereza (1571). Kifungu cha VII kinasema kwamba “sheria alizopewa Musa na Mungu” zilikuwa zinahusu “mambo ya ibada ya madhabahu” hazina kifungo, “hakuna muumini Mkristo awayeyote aliye huru asiyetakiwa kuzitii amri za Mungu, ambazo zinaitwa za maadili ya jamii.” (Schaff, vol. 3, pp. 491, 492) [spelingi za zamani zimetumika].

 

Toleo Jipya la Kiamerika lenye Vifungu Thelathini na tisa la Kanisa la Kiaskofu la Kiprotestanti (1801) linajulikana kwa kuendeleza kuamini hivyo. (Soma kitabu cha Schaff, vol. 3, p. 816.)

 

Makala ya Kiyahudi ya Kidinin (1615), inaaminika ilitungwa na Askofu Mkuu Ussher, baada ya kusema kwamba sheria ya mambo ya ibada imekoma, anasema: “Hakuna mtu aliyewekwa huru kutoka ushikaji wa Amri ambazo zinaitwa za Kimaadili ya jamii.” (Soma kitabu cha Schaff, vol. 3, pp. 526,541.)

 

Azimio la Ukiri wa Imani la Westminster (1647), baada ya kuonyesha tofauti kati ya sheria za kiibada na za mahusiano ya kijamii na utanguaji wa maandiko ya zamani nay a milele kwenye sura ya 19 inatangaza kwamba “sheria ya mahusiano ya jamii inawahusu watu wete,” na sio kwa kuhesabiwa haki, bali ni kanuni ya maisha, ili kuutambua uweza utendao kazi wa Kristo. Sheria hii inaendelea kuwa “kanuni kamilifu ya haki”. Na inaongeza “Wala hakuna mahali kwenye Maandiko ambapo Kristo amezitangua, bali mara zote amekazia sana sheria hii.” (Soma kitabu cha Schaff, vol. 3, pp. 640-644.)

 

Azimio la Savoy la Makusanyiko wa Makanisa (1658). Hakuna mabadiliko kama ilivyo kwenye sura ya 19, “Ya Sheria za Mungu,” kutokana na Azimio la Ukiri la Westminster. (Soma kitabu cha Schaff, vol. 3, p. 718).

 

Tamko la Ukiri la Wabaptist 1688 (Philadelfia), linatuama kwenye lile la London, 1677, ambalo halina mabadiliko na lile la Westminster kwenye sura ya 19, “La Sheria ya Mungu.” Linashughulika na mkanganyiko kati ya sheria za kijamii na za kiibada, na kusisitiza kwamba hakuna Mkristo aliye huru kutoka kwenye sheria hizi za kijamii. (Soma kitabu cha Schaff, vol. 3, p. 738.)

 

Makala ya Kidini ya Wameethodist (1784). Hizi makala ishirini na tano ziliandikwa na John Wesley kwa Wamethodist wa Marekani, ni za muhimu sana (sawa) na zile Malaka nyingine Thelathini na tisa za Kanisa la England, na zinatangaza: “Ingawa Sheria zilitolewa na Mungu na kumpa Musa, kama kanuni zenye mguso za kiibada na utakaso, hazimlazimishi Mkristo wala kwa mambo ya kijamii yaliyomo ambayo yanaumuhimu wowote kwenye mafungamano, tena, hata kama hakuna Mkristo kwa vyovyote vile aliyehuru kutokana na kuzitii Amri hizi zinazoitwa za mahusiano kwenye jamii.” (Soma jarida la Schaff, vol. 3, pp. 807,808.)

 

Kwa kujua maneno haya, Waadventista Wasabato wanaamini kuwa:

Imani hii imehusihwa na Waadventista Wasababo kwa kuzingatia  uhusiano wao na Vitabu vya Musa au Torati, na tofauti yake kati ya sheria ya kijamii na maadili na ile ya mambo ya ibada, zinaendelea kuwepo kwa uongozaji wa ukiri wa imani, makala za ukiri wa imani, na katekisimu ya historia ya Uprotestanti. Sababu iliyofanya Torati kuwa ilitanguka na kuishia kwenye kifo cha Kristo inahusiana kwa kiasi kikubwa. Kwa hakika haikufundishwa na mababa waanzilishi wa Uprotestanti kwa kuwa huo ni mgongano mkubwa na kamilifu wa imani yao (SDA Questions On Doctrine, pp. 131-134).

 

Ukweli ambao mtu anaweza kuukubaliana na hawa mababa waanzilishi wa Uprotestani unaweza kuchukuliwa kwa tahadhari kubwa sana, kwa kuwa walikuwa wamekosea kabisa kwa kuwa waliacha kurejea nyuma hadi kipindi cha Augustine wa Hippo kwenye harakati zao za Matengenezo. Kwa hiyo wanamatengenezo walishindwa kuyarejesha mafundisho asilia ya Kanisa.

 

Kosa la kuanzisha imani sahihi ya kuabudu kwa kufuata Kalenda ya Mungu (sawa na jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156) [God’s Calendar (No. 156))], na kisha walishindwa kuanzisha uhusiano sahihi na Sheria za Mungu na mkanganyiko wa Sheria.

 

Jambo moja na kosa walilolifanya lilikuwa ni kushindwa kwao kuyaonysha makosa yaliko kwenye imani ya Utatu, ambayo ilianzishwa kuanzia kwenye Miitaguso ya Constantinople (381 BK) na Chalcedon (451 BK). Kwa hiyo matengenezo yalishindwa na kwa hiyo walizuiwa kuanzisha maadhimisho ya Siku Takatifu kwa mpango wa kimbinguni na uingiliwaji kati.

 

Siku hizi Takatifu na Sabato ziliondolewa kwa makusudi. Hii ni ahadi ambayo Mungu mwenyewe aliitoa kwa kupitia manabii. Mungu alinena kupitia nabii Amosi na kuwafananisha Israeli katika Siku za Mwisho na kikapu cha matunda ya majira ya hari (Amosi 8:1 nk).

 

Hukumu kwa ajili ya kushindwa kumtii Mungu ni kwamba hizi Sabato na Sikukuu kugeuka kuwa maombolezo. Hii inafuatia njaa ya kukosa kulisikia neno la Yahova (Amosi 8:11-14). Kwa ajili ya kutojua ukweli kuhusu asili ya Mungu wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20), watu wanaadhibiwa (Hosea 8:5-9). Hata mashetani yanajua kwamba Mungu ni mmoja kwa kutetemeka (Yakobo 2:19). Mambo makuu kwenye Torati ya Mungu waliandikiwa Israeli kwakuwa waliyachukulia kama mageni kupitia uvunjifu wao wa Amri ya Kwanza ya Mungu na ueneaji au mlipuko wa dhambi kwenye ibada (Hosea 8:11-12; soma biblia ya the Interlinear Bible na pia jarida la Torati na Amri ya Kwanza (Na. 253) [Law and the First Commandment (No. 253)].

 

Sheria au umuhimu kati ya maadhimisho ya Sikukuu na utoaji dhabihu iliyoandikwa kwenye Kumbukumbu la Torati 12:8-14 iliondolewa pamoja na sheria ya utoaji dhabihu siku za Sabato za juma. Mtu hawezi kuiunganisha Kalenda Takatifu na Sikukuu na sheria ya utoaji dhabihu pasipo kuyatendea kazi mawazo mengine yote kwa mambo mengine yote ya Sheria. Muundo wote wa serikali ya Mungu umeondoa taratibu za utoaji dhabihu, pamoja na maadhimisho ya Siku Takatifu. Pasaka yenyewe ilianzishwa kabla ya kutolewa kwa Torati mlimani Sinai. Mchakato mzima wa  kuwaingiza wateule kwenye imani ya Kikristo umekuwa amehalifu na utaratibu wa Siku Takatifu tangia hapo hadi kwenye Ufufuo wa Pili wa Wafu. Haziwezi kutanguka hadi kufikia Siku Iliyokuu ya Mwisho au Siku ya Mkutano wa Makini. Kila Sikukuu inawakilisha mchakato unaoendelea wa Mpango wa Mungu ambao bado unafunuliwa. Zinamaanisha kuwa mchakato wa mavuno bado unaendelea na unafunuliwa (sawasawa na jarida la Sikukuu za Mungu Kama Zinavyohusiana na Uumbaji (Na. 227) [God’s Feasts as they relate to the Creation (No. 227)].

 

Torati ilkuwa ni kivuli cha mambo yajayo (Waebrania 10:1). Kivuli kinaonyesha jambo lililo la kweli’ hakiwezi kuondolewa au kutenganishwa nacho. Kivuli hiki kilifungamanishwa kikamilifu na dhabihu (Waebrania 10:1-10), na sio kwenye hizi Sikukuu. Makanisa ya Kikatoliki na hata ya Kiprotestanti badi yanajua kwamba Sikukuu za zamani zinatakiwa ziadhimishwe bado hata sasa. Wameichanganya Pasaka na sikukuu ya kipagani ya Easter na kuanza kuhesabu siku za kuelekea kwenye Pentekoste kimakosa tangia siku ya Easter, hata hivyo, hawaupingi umuhimu wake. Kwaajili ya makosa yao ya kiuelewa katika fundisho la Ufalme wa Mungu na kupiga kwao kuhusu kuwepo kwa kipindi cha utawala wa Millennia na Ufufuo wa Pili wa wafu, ndipo wanashindwa kuelewa mana ya Sikukuu hizi nyingine.

 

Mlo unaoliwa siku ya 14 Nisan, ambao hatimaye ulikujakuwa ni Ushirika wa Meza ya Bwana, uliunganishwa kwenye maadhimisho ya Pasaka na ililiwa nje ya miji, kama iliyoagizwa kwenye Kumbukumbu la Torati 16:6-7 (sawa na majarida ya Pasaka (Na. 98); Malumbano ya Wakotadesiman (Na. 277); Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 2131) [The Passover (No. 98); The QuartodecimanDisputes (No. 277); The Moon and the New Year (No. 213)]. Kwa hiyo, kipindi chote cha saa ishirini na nne cha siku ya 14 Nisan na jioni ya siku ya 15 Nisan, kinafanya jumla ya masaa 36, yaliyotumiwa kwa watu kuwa nje ya miji yao katika Israeli kwa Sikukuu moja tu. Mlo wa Meza ya Bwana ulifanyika na kuadhimishwa Kristo. Unaitangulia Pasaka, ukiadhimishwa usiku wa siku ya 14 Nisan. Dhabihu ya Pasaka ambayo ndiye alikuwa Kristo mwenyewe, ilifanyika au kutolewa siku ya 14 Nisan, na mlo wa Pasaka uliliwa siku ya 15. Jioni zote mbili zinapaswa kuadhimishwa, na ifanywe hivyo nje ya matuo na miji yetu. Kwa hiyo, adhimisho la Meza ya Bwana linatakiwa lifanyike mara moja tu kwa mwaka na likifungamanishwa na maadhimisho ya Pasaka na Mikate Isiyo na Chachu.

 

Biblia inatufundisha kwamba makwazo au unajisi kwenye Sikukuu yanasababishwa na wale walio kwenye Ushirika lakini wanaojitoa wenyewe kwa minajiri ya kufuata faida zinazotokana na makosa ya Balaam, kuangamia kwenye uasi wa Kora (Yuda 11-12). Kwa maneno mengine, wanafundisha kwa minajiri ya mashahara au watumishi wa mshahara na hawaoni shida kuzitia unajisi au kuzigeuza Sikukuu na kuielewa Torati na Ushuhuda. Hakuna nuru ndani yao (Isaya 8:20, KJV) au hakuna mapambazuko (RSV) kwao. Wamekufa mara mbili na wameng’olewa. Watu hawa hawana au hawaenendi kwa Roho na wanasababisha matengano katika Siku za Mwisho (Yuda 19). Uasi wa Kora ni mchakato unaoendelea dhidi ya neno la Mungu (sawa na jarida la Wanikolai (Na.v202) [The Nicolaitans (No. 202)].

 

Kristo anaweza kuwalinda wateule wasianguke na kuwawakilisha mbele za Mungu Mwokozi (Yuda 24-25; pia soma Marshall’s Interlinear, RSV). Hata hivyo, mgawanyiko kwenye Mwli wa Kristo umeruhusiwa uweze kuwadhihirisha wanaoishika kweli na waliokubalika na Mungu (1Wakorintho 11:19). Malumbano yasemayo kwamba aya ya Wagalatia 3:10 imeliondolea neno Sikukuu yanaonyesha kutoijua asili ya kipindi cha nyuma ya Sabato. Marejesho ya Sikukuu kwa adhabu ya kukosa chakula ni ya lazima na nyongeza ya mwanzoni mwa kipindi cha Milenia (Zekaria 14:16-19). Kristo habadili nia yake kwa kuwa anapenda ziadhimishwe.

 

Makanisa ya Mungu, linajumuisha Kanisa la Kristo na lile la Mitume (Mathayo 26:17-20; Luka 2:41,42; 22:15; Yohana 2:13,23; 5:1; 7:10; 10:22; Matendo 18:21(KJV); 19:21; 20:6,16; 24:11,17), yame zishika Sikukuu hizi kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu mbili ukiliondoa Kanisa moja kutoka karne ya kumi na tisa. masalio ya Makanisa ya Mungu Yayayozishika Sabato huko Ulaya na ambayo yameshindwa kuzishika Amri za Mungu au yaliyoangukia kwenye ukengeufu ndiyo hatimaye yalipoteza ushikaji wa Sikukuu hizi (soma majarida ya Kazi ya Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na. 170, Torati ya Mungu (Na. L1) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170), The Law Of God (No. L1)] na Mlolongo wa majarida yanayohusu Torati (Namba zote 252-263)).

 

Ni sawa kama Kristo na Mitume wake wengine wote na Wazee Waangalizi, Paulo pia alizishika Sikukuu hizi, kama tunavyoona kwenye Matendo ya Mitume. Kwa hiyo, kwa kweli hakudiriki kuzipotosha wala luzikomesha. Hekalu lilichaguliwa kuwa ni dhabihu (2Nyakati 7:12), baada ya Maskani ziliyokuweko huko Hebron na Shilo. Hata hivyo, maadhimisho ya Sikukuu hayakufungamanishwa na huduma za Hekaluni. Bwana aliuchagua mji wa Sayuni kuwa ni mahala pa kuweka miguu yake (Zaburi 132:13-14), lakini uchaguzi ule uliahirishwa kwa Kanisa kutangatanga jangwani hadi kurudi kwa Masihi. Kitendo hiki kilipimwa kwa kulinganishwa na kipindi cha miaka arobaini waliyokuwa chini ya nguzo ya moto na mawingi jangwani (sawa na jarida la Hesabu ya Nyakati za Zama (Na. 272) [Outline Timetable of the Age (No. 272)]. Ile ilikuwa ni ishara mahsusi ambayo Kristo aliweza kuionyesha kiini cha ibada kupitia wateule.

 

Chini ya Kanisa la Mitume, Kanisa lilishika Sikukuu kwa maeneo mbalimbali, ingawaje Mtume Paulo alitaka arudi mjini Yerusalemu kwenda kuadhimisha Sikukuu kama ilivyoonyeshwa kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume 18:21; 19:21 (soma tafsiri za KJV; The Interlinear Bible). Matendo 20:6 inaonyesha kwamba Paulo alizishika siku za Mikate Isiyo na Chachu akiwa Filipi akiwa amekawia kawia. Hatimaye alipenda awepo Yerusalemu siku ya Pentekoste (Matendo 20:16). Imani zote mbili, yaani Wayahudi na Wakristo walizishika Sikukuu kwenye nchi za utawanyiko walikokwenda. Sikukuu zilitangulia zama za Hekalu na ziliendelea hata baada ya kubomoshwa kwake. Ni dhabihu za wanyama tu ndizo zilitakiwa kutolewa Hekaluni. Hata hivyo, dhabihu zilionekana zikitolewa hahali penginepopote vipindi vyote viwili, yaani wakati Hekalu likiwepo na hata baada ya kubomolewa kwake kipindi chaa utumwa wa Babeli. Hekalu huko Elephantine liliaminika kufanya shughuli zake za utoaji dhabihu hadi kipindi cha ujenzi mpya wa Hekalu siku za utawala wa Dario II. Hatimaye Hekalu la Elephantine lilibomolrwa kwa kushambuliwa (soma kitabu cha Pritchard, The Ancient Near East, vol. I, pp. 278-282). Maandiko ya Kiaramu kwenye tafsiri ya Pritchard, ya Ginsberg, inaonyesha rekodi za maelekezo ya maadhimisho ya Pasaka kwenye dola iliyotajwa na nabii Ezra (soma jarida la Ishara ya Yona, Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)].

 

Michango kwa ajili ya majenzi mapya ya Hekalu imetajwa, sambamba na mazingira ya uharibifu wa Hekalu huko Elephantine katika mwaka wa 14 wa Dario II. Maliwali wa yuda pia alikuwa na sera ya kuwadhibiti makuhani huko Elephantine. Andiko linaonyesha kwamba dhabihu hazikukoma kamwe kipindi cha kuangamizwa kwake Yerusalemu, na Hekalu lilijengwa upya huko Yerusalemu wakati wa ujengaji mpya wa Hekalu huko. Dhabihu zilikoma kwa Agano Jipya na kwa maangamivu ya mwisho ya Hekalu huko Yerusalemu, lakini Sikukuu ziliendelea huko walikotawanyikia. Kanisa limeshika Sikukuu huku likiwa linapitia kipindi cha mateso kwa kipindci cha miaka elfu mbili.

 

Hekalu linguine lilijengwa pia huko Misri mahali panapoitwa Leontopolis, kwenye Nome ya Heliopolis, na Kuhani Mkuu Onias IV. Hekalu hili lilitabiriwa na Mungu kupitia nabii Isaya (Isaya 19:19). Lilifungwa kwa amri ya Vespasian mwaka 71 BK, baada ya kubomolewa kwa Hekalu la Yerusalemu, ingawaje liliendelea kutoalewa dhabihu tangu kujengwa kwake mwaka 160 KK.

 

Wateule watahukumiwa kwa kumjua kwao Mungu wa Pekee na wa Kweli. Kutokana na kumjua Mungu, ujuzi wa kuzijua Sheria unaendelea na unaingia akilini na mioyoni mwa kila mtu. Jambo hapa sio Sabato, au Sikukuu, au Torati, bali ni kuhusu ukweli kwamba Mungu Baba ni Mungu Mmoja na wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20), na kamba ni yeye peke yake ndiye asiyepatwa na madhara wala kufa (1Timotheo 6:16). Kama hatutaishikilia imani hii basi tutaondolewa kati ya wateule na tunaweza pia kupewa nguvu za upotevu ili tuuamini uwongo (2Wathesalonike 2:11). Marshall’s Interlinear inaitafsiri ayah ii kama mkakati wa makosa unaokusudia kuwafanya wauamini uwongo. Hawawezi kujisaidia wenyewe tena. Ni kwamba wameondolewa kutoka kwa wateule na uelewa wao umeondolewa pia. Hawawezi kuelewa ijapo kuwa walipenda kuyajua makosa.

 

Uelewa wote wa wateule umetegemea na uhusiano wao na Mungu wa Pekee na wa Kweli na kumjua kwao Mwana wake Yesu Kristo (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20). Uvunjaji wa Amri ya Kwanza ndio unaowafanya wafikiri kuwa Sikukuu zimeondolewa. Hawawezi kuzishika hata kama wale walio kwenye makosa wanapenda kuzishika. Mungu ataingilia kati kukatiza juhudi zo. Kwa wale wanaozishika Sheria au Torati, Sikukuu ni mkumbushiaji wa muhimu wa Mpango wa Mungu. Zaidi ya yote, marejesho ya lazima ya kipindi cha utawala wake yanaonyesha kwamba Sikukuu ni za lazima na kwa kweli ni Baraka kwa wafuasi.

 

Kitendi cha kuziondoa Amri hizi Kumi kutoka kwenye mambo muhimu ya Torati na mkanganyiko wao wa sheria za kimmandiko, kunatokana kiwango chao kikubwa cha kutojua mafundisho ya Kristo nay a Mitumem jambo ambalo hata wanamatengenezo wa Kiprotestant waliangukia kwenye makosa. Ni matokeo ya udhaifu wa kiroho, makosa kushindwa kwa Kanisa la Siku za Mwisho. Udhaifu huu imeonekana kwenye ahadi za Makanisa yaliyo kwenye Ufunuo sura za 2 na 3, ambapo Kanisa la Wasardi liliambiwa limekufa na Kanisa la Walaodikia liliambiwa litatapikiwa mbali. Hakuna hata mtu mmoja kwenye Makanisa haya atakayeuingia Ufalme wa Mungu. Bali ni wachache kati yao ndio watakuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu.

 

Uzao wa mwanamke, ambao ni Kanisa, ni wale wote wanaizishika Amri za Mungu na Ushuhuda au Imani ya Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12). Soma jarida la Upendo na Kanuni za Sheria (Na. 200) [Love and the Structure of the Law (No.200)].

q