Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[113]

 

 

Mithali 30

 (Toleo La 1.0 20020810-20020810)

 

Dhumuni la jarida hili ni kuiainisha Mithali 30 kwa namna ya jinsi inavyomsisimua na kumpa hamasa msomaji ya kuzama na kufikiri kwa kina zaidi kutafakari kuhusu maisha yake. Imeandikwa kwa namna ambayo inatumainisha kumfanya msomaji aulize maswali ya kiudadisi na maana.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki ©  2002  Storm Cox, ed. Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mithali 30

 


Kwa mwanamke (au Kanisa) ambalo Mungu ametupatia Mithali hii ya 31, kwa mwanamume (au kuhani au kasisi) aliyetupa sisi Mithali 30. Mithali 30 ni mtazamo muhimu na wenye nguvu sana mawazoni mwa mwanadamu na mwelekeo au maelekezo anayopasa kuyachukua. Inaanza kwa kuionyesha toba na ubatizo.

 

Maneno ya Aguri

30 Maneno ya Aguri bin Yake; mausia mtu huyu aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.
2 Hakika nimekuwa kama mnyama, wala si mtu; Wala sina ufahamu wa mwanadamu;
3 Wala sikujifunza hekima; Wala sina maarifa ya kumjua Mtakatifu.
4 Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini?

Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake?

Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake?

Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi?

Jina lake ni nani?

Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua?

Safari ya maisha inaanza kwa kugundua kwamba maisha ya zamani au ya kale ni muhimu na hayana matokeo hasi. Tunajifanyia fujo na matatizo kwa dhambi. Kwa kumkataa Mungu na busara iliyo kwenye Maandiko Matakatifu, uamuzi tuyafanyayo na yasiyo na maana. Msukumo wa kijakamoyo wa maisha ya Misri yanatupelekea kutafuta mtindo wa maisha wa kimaisha. Kuishi bila Mungu hayatoi makusudio na kusiwe na hatima njema, kusiwe na sababu ya kuishi zaidi ya kuendeleza tu mtazamo wa shinikizo, kwa namna yoyote inayoonekana kuonekana. Kwa wengine, ni udhalilisho mkubwa; kwa wengine ni kwa njia ya ngono, na kisha kuna wale ambao kutokana na vita isiyoisha kujipatia faida.

 

Dunia inayoamkia kufanya kazi, husahau familia na marafiki; na inaelewa kidogo hitaji la upendo. Mashindano hushuhudia juhudi za kila mtu mmoja mmoja ya kutambuliwa. Upandishaji cheo unamaanisha utajiri zaidi, ongezeko bora la kiwango cha kuongezeka kima, na kufikia zaidi kwa bidhaa na huduma. Yampasa mke afanye kazi ili alipie bili. Watoto wanalelewa na wageni ili wazazi wamudu kuendesha gari zuri. Tunasema, anaishi kwenye nyumba ndogo, kwa hiyo hafanyi vizuri sana. Ana watoto wane, kwa hiyo inawezekana kuwa anafanya hivyo kwa shida na ugumu mwingi.

 

Anafanya kazi masaa 80 kwa juma na haioni kabisa familia yake, ni mfanya kazi mahiri kiasi hicho. Anavaa suti za gharama kubwa, ni lazima awe wa muhimu. Anakunywa sana pombe; ni lazima awe na jakamoyo. Anakopa hela ili awachukue watoto wake kuwapeleka mapumzikoni; kwa hiyo anatimiliza majukumu yake. Mke wake huvaa vito vya gharama kubwa, anampenda kwa kiasi gani basi. Anamajukumu ya kuwajibika kwayo, jaka moyo za kikazi zilimsababisha aende mbali kandoni. Anafanya kazi siku saba za juma, akiungua. Hata hivyo, familia yake ina mahitaji.

 

Anautumia muda wa bosi wake kwa kutandaza wavu; kazi hii ni ya muhimu sana. Anajihisi mzaa matunda kwa kiasi gani unadhani. Yampasa arudi nyumbani kwa familia yake kama usiku wa michezo.

 

Tunayafania kazi yale yaliyo ya muhimu maishani mwetu. Tunawezaje kupenda kila kitu bila kujua ni kwa nini? Yatupasa kufikiria; kwamba mimi ni mjinga sana kuwa mwanadamu. Yatupasa tatupasa tujiulize wenyewe; je, nimesahau kitu chochote kilicho muhimu maishani? Wazazi wangu walinilea wakinipenda – je, nimesahau hilo? Ni nani anaweza kunifundisha jinsi ilivyo? Kwa hakika najua.

 

Naona masumbufu ya dunia hii yananipotosha na kunirudisha nyuma. Naona kwamba utajiri unawadanganya watu. Naona kwamba hisia ya moyo ni tajiri kuliko miamba. Naona kuna ujinga kwenye dhambi. Naona Kristo ni mwalimu wangu. Najionea kuwa mhitaji yuko safi. Napenda kujifunza jinsi ya kuishi. Napenda niwafundishe wengine. Napenda wengine wajihisi kama ninavyojihisi mimi – kuwa niko huru. Napenda kufanya kazi na watu wanaohisi kama ninavyotenda na kujihusisha na mambo ya watu maskini na wajinga. Wakati wangu ni mzuri. Nazipenda sikukuu zangu na saumu zangu. Ni zangu na nazipenda. Nazihitaji pamoja na familia yangu yote.

 

Kwenye andiko hili tunajionea rejea inayolitaja jina la Mungu na ukweli wa uwepo wa Mwana wa Mungu.

 

5 Kila neno la Mungu limehakikishwa;

Yeye ni ngao yao wamwaminio.

Yeye ni Mungu wa Pekee na wa Kweli anayeniongoza na amemtuma mwana wake kuja kuniokoa mimi.

 

Mimi najiamini sana kwa kila nilifanyalo. Nimebatizwa na Kristo ni mwalimu wangu. Kuna jibu kwa maswali yangu yote kama nitautoa muda wangu kutembelea majarida haya na Maandiko Matakatifu na kujisomea. Najuma kwamba kufanya hivyo kila siku, kwa kuwa sheria au Torati inanionyesha kile inachotaka ninachohitajika kukifanya. Siwezi kupata madhara. Roho yangu inalindwa na kundi kubwa la malaika. Mungu ananiambia kuwa aliiumba dunia kwa muda wa siku sita. Ni kwa nini nisimwamini yeye? Mungu ananiambia kuwa alipumzika siku ya Sabato. Kwa nini nifikiri vyovyote vingine? Mungu ananiambia niwasaidie masikini kama afanyavyo yeye. Kwa nini basi nifanye vinginevyo tofauti? Mungu ananiambia kuwa Kristo atarudi tena. Kwa nini naamini vinginevyo tofauti? Mungu ananiambia kuwatembelea watu wangu na kutumia muda pamoja nao. Ni kwa nini nifanye kinyume chake. Mungu ameniambia nifunge saumu ili niwe karibu na yeye. Kwa nini basi nisimsikilize? Mungu ananiambia niende mahali pazuri nikaadhimishe sikukuu na kununua kila ninachokipenda, na kwenda kujifunza neno la Mungu pamoja na watu wangu na kwenda kula chakula kizuri. Ni kwa nini basi nisifanye hivyo? Ziwezi kushindwa kwa kuwa naamini. Roho ananifanya niamini.

 

6 Usiongeze neno katika maneno yake; Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.

Nimebatizwa na naijua kweli. Ufunuo anaoutoa Bwana unatosha. Je, nahitaji watu waniambie kwamba ni mimi ndiye niliyeviumba vitu hivi? Je, nahitaji watu waniambie kwamba ni mimi ninayeweza kukulinda wewe? Je, naweza mimi kukupa uzima wa milele? Je, naweza mimi kukupa mahali pako mbinguni? Je, naweza mimi kulijenga kanisa na kuwaondolea watu dhambi zao? Je, mimi naweza kukutawala wewe? Je, sisi hatuma Bwana wetu tayari na je, hatutajua tayari jinsi tunavyopasa kuishi? Je, hatujajua sisi tayari mambo ya kufanya kila siku? Je, hatujawa tumeshawishika tayari kwa mng’aro wa uumbaji na maajabu ya mwanadamu mwenzetu? Je, hatujashawishika tayari na kweli? Je, hatuoni kwamba kila Andiko Takatifu linafungamanishwa na kuwashikilia au kuwagusa watu wote pamoja? Je, hatuoni minyumbuliko na rangi ya dunia? je, tunawezaje kuthibitisha ukamilifu wake? Je, tunayakata na kuyaondoa masikio ya mtu na kuyarudishia tena kwa kuyashona au, kuikata miguu yetu ili kuifitisha kwenye shimo. Biblia imevuviwa na ni kweli. Imani yangu inatuama kwenye ukweli huo. Kama si hivyo, basi mimi ni sokwe. Mimi ni mnyama asiye na uhai. Naweza kuua na kubaka bila kujijua na pasipo kuwa hivyo. Biblia ndiyo inanifanya kuwa mwanadamu. Biblia inanifanya niwe wa hakika. Biblia inanitambulisha mimi kwa Mungu.

 

7 Mambo haya mawili nimekuomba;

Usininyime [matatu] kabla sijafa.
8 Uniondolee ubatili na uongo;

Usinipe umaskini wala utajiri;

Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.
9 Nisije nikashiba nikakukana,

Nikasema, Bwana ni nani?

Wala nisiwe maskini sana nikaiba,

 Na kulitaja bure jina la Mungu wangu

Ni kwa nini sifanyi kama anavyosema Mungu? Usimfiche kitu chochote mwanadamu. Kwa nini nahisi kama najilinda na kujitetea mwenyewe kwa kujidanganya? Ni nini anachoweza kukifanya mwanadamu ili anidhuru mimi? Je, kuna kitu chochote nilichokitenda kibaya sana? Ni kwa nini nisiwe mtu ninayethibiti hatima yangu; kujiamini na majivuno ya kujiona kuwa mimi ni kiumbe niliyeumbwa na Mungu? Mimi ni mtumishi mtendakazi wa kanisa, mume na baba, kaka na dada, mama na mke, mjomba, shangazi, binamu na rafiki. Je, nahitaji kuwa zaidi? Kwa nini napenda kuwa chini? Kwa nini tunadanganya? Maisha ni rahisi. Tunalala; tunaamka; tunakula; tunapenda na tunafanya kazi. Tunakunywa na tunacheka na kuwakumbuka watu wetu. Tunakwenda kanisani wakati tunapoweza. Tunajumuika; tunasoma; tunangojea kwa uvumilivu mwingi na tunaomba. Kwa nini kunakuwa na uhitaji wa ziada au kwanini tunahitaji zaidi na ni kwa nini kunahitajika kuukanganya ukweli ulio dhahiri na ulioko mbele yetu?

 

Kwa nini nataka mambo mengi sana? Kwa nini nahitaji kutiliwa maanani kwa namna hiyo? Wakati ninapokuwa nayo yote, sihitaji chochote. Je, ndipo hapo nakuwa simhitaji muumba na Mungu wangu? Ninafikaje hapo? Kama fedha zinaweza kupotosha, kwa nani kwa basi nijitaabishe na kujitoa mhanga? Kama hunipendi hadi niishi kwenye makazi au nyumba nzuri na kuendesha gari zuri na la gharama, unaweza ukanienda mimi kwa vyovyote vile? Utajiri na mali zangu zinategemea watu wengine. Iwapo kama tungemwelewa Mungu kwa kuwa wakamilifu, kwa nini basi atutake tufunge saumu? Kama tulimlipa mtu ili atupandie mazao, ni kwa kiasi gani basi tungeyaelewa masuala ya uumbaji? Ni kwa jinsi gani mtoto anaweza kuelewa uumbaji asipochezea na kutunza wanasesere? Watoto waishio mjini hawajawahi kumona ng’ombe kabisa.

 

Je, umekwishawahi kuuonja mkate uliouoka wewe mwenyewe? Inauma sana kuwa na njaa, lakini vyakula vingine havitoshelezi wala kushibisha kabisa. Nipe nyanya kutoka chunguni mwako; ladha yake haiwezi kufanana. Kwa nini nilazimike kuwa na gari wakati naweza kutembea kwa miguu yangu? Kwa jinsi hiyo ndivyo ninapowaona ndge. Ndiyo shauku na mpangilio wa jamii za kisasa zilizopo zinazotufanya sisi tudhoofike na tuwe na shauku.

 

10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake;

Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

Maka Mungu anasikia kila kitu tukisemacho, na anajua kila kitu tukifikiricho, ndipo tunapokuwa tunafikiri vibaya juu ya mtu mwingine ndipo tunamsengenya au kumsingizia mtumishi kwa bwana wake. Basi na tusichukulie fursa hiyo kwa wale walio watiifu na waadilifu kwene nafasi zao. Dunia inajali watu wake wote na watu wa mionekano na tabaka mbalimbali na wenye mawazo mbalimbali na viwango vya hekima na busara. Ninachotufanya tuwe bora, lakini uwezo wetu wa kusamehe kama Baba anavyotusamehe sisi. Ni ninii kinachokufanya wewe uwe mwenye hekima zaidi kuliko nilivyo mimi? Je, kila kitu wakati wote kinafanya kazi zake kikamilifu sana kwa jinsi tutarajiavyo? Naweza kupika chakula, lakini wewe unaweza kukarabati chungu kilichovunjika. Mwanamke anaweza kucheza vyema, lakini wewe mwanaume unaweza kuchora picha kubwa. Kwa hiyo, watu wengi wana muda na mimi, kwa niinini basi name nisiutenge muda wangu kwa kwa ajili ya wengine? Kwa nini namchukia ndugu yangu na kufanya uadui naye? Kwa nini namuumiza dada yangu? Kwa nini namsababishia Baba ajisikie maumivu kwa kuwadhuru-kuwaumiza watoto wake? Kwa nini nataka ulichonacho wewe wakati nikiwa tayari nimekwisha kuwa nayo zawadi kama hiyohiyo uliyonayo? Uwanaume wangu unategemea na uwezo wangu wa kufanya kazi na watu wengine. Nawahitaji watu wengine na wengine wananihitaji mimi pia. Kwa nini nimzuie mtu anayenisaidia wakati nahitaji sana msaada wake.

 

11 Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao.
12 Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao.
13 Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana.
14 Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.

Mimi ni nani nisiyekuwa na mama yangu na baba yangu na ni wao ni nani wasipokuwa na wazazi wao? Ni wao tu ndio walionileta mimi hapa duniani na ni Kristo tu ndiye anayeweza kunisafisha kwa kuniosha dhambi zangu. Ninawezaje kujishawishi mwenyewe kwa mazingira mengine yoyote? Unawezaje kunishawishi mimi kuwa unaweza kufanya kulifanya hilo badala yao? Unaweza kunipatia uhai nje ya familia na umilele nje ya uumbaji? Ni nani wewe hata unijaribu mimi kwa mawazo yaliyo kinyume na hivyo? Mimi sikuomba nizaliwe; wala sikuomba niwepo, na wala sikutuma maombi. Mama yangu na baba yangu walipendana na kuishi pamoja kwa maelekezo ya Mungu na ndivyo ilivyo hata kwa mimi pia. Familia ni mujumuisho wa baba na mwana na mama na mimi ni mtoto—inaweza kuwa ni ya namna nyingine yoyote ile? Simjui mwingine yeyote zaidi. Je, ni tofauti na mtu mwingine yeyote hapa duniani? Je, hatupo sisi sote sawa kwenye jambo hili? Je, sio kwamba watu weusi na weupe, Waasia na Wahindi wote wameumbwa kwa namna moja? Je, sio watoto wa wafalme na wa mamalkia wameumbwa kutokana na mpango mmoja huo huo kama watokanavyo watoto wanaozaliwa kwenye vichochoroni au makazi duni? Je, mahitaji yao hayafanani? Je, kazi na majukumu yao hayafanani? Je, thawabu zao hazifanani na na za sisi wengine wote? Wewe ni nani unayedhania kuwa mahitaji yako ni makubwa sana kuwaliko wengine na kwamba unastahili kuwa na umuhimu kwa kuwa una nembo fulani kwenye shati lako? Kama uhadhania hivyo, basi wewe husomi vitabu vilevile nivisomavyo mimi. Ni Mungu tu ndiye anayeweza kutulisha sisi. Ni Mungu tu ndiye anayeweza kutupatia sisi maji na ni Mungu tu ndiye anayeweza kutufundisha sisi kweli. Kwa nini uchukue kilicho kidogo alichonacho ili kuongeza kwenye lundo lako lisilo na kitu?

 

15 Mruba anao binti wawili,

Waliao, Nipe! Nipe!

Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe,

Naam, vinne visivyosema, Basi!
16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa;

Nchi isiyoshiba maji;

na moto usiosema, Basi!

Ni kwa nini tunajidanganya sana sisi wenyewe? Maisha yetu ni haki endelevu. Kwa nini tunapenda kile ambacho tulichomudu kujishawishi sisi wenyewe kuwa ni cha mhimu sana? Kristo alisema:

Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, 10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. 11 Utupe leo riziki yetu. 12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. 13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]”

 

Sikioni kitu kingine chochote kuhusu waosha vyombo au waosha sahani, vito vya thamani, magari, sikukuu, sofa za ngozi, watengeneza juisi, mashine za kutengeneza kahawa, mkandamizo au shinikizo, mashine zinazooka mkate, wasafisha mazingira kwa mashine za kiatomatiki ambazo hazihitaji kusukumwa huku na huko na vitu vingine cha kuchokesha zinazojiri mapema sana asubuhi. Sio dhambi kuwa na vitu hivi, lakini ni kujiuliza vina umuhimu gani kwenye maisha yetu? Tunahitaji kuishi kwa kiwango kipi? Je, kuta nzuri na zinang’arazo zinazojengwa, zinatufanya tuwe mbali na kutenganisha mbali na vile kunavyovihitaji kwa kweli? Je, ninafanya vya kutosha ili kujielewa sisi ni kina nani, au ninajaribu na kujitahidi kukupatia wewe vitu ninavyodhani kuwa unavyivihitaji? Sikihitaji hiki, nakihitaji, sijali hukusu ulichonacho, bali najali tu vile ulivyo. Watu walio kanisani ni matajiri sana ulimwenguni kwakuwa wapo kanisani. Sipendi kuwa tajiri sana na kama unanichukia kwakuwa mimi ni maskini, basi mimi ni tajiri zaidi kuliko wewe. Kama unanipenda, ndipo ninakuwa tajiri zaidi, na kadiri unavyonipenda ndipo ninapozidi kuwa mkuu zaidi.

 

17 Jicho la mtu amdhihakiye babaye,

Na kudharau kumtii mamaye;

Kunguru wa bondeni wataling'oa,

Na vifaranga vya tai watalila.
18 Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,

Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.
19 Mwendo wa tai katika hewa;

Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba;

Mwendo wa merikebu katikati ya bahari;

Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.

Uumbaji ni kitu kikubwa sana kuliko kingine chochote nilichowahi kukiona. Mawazo ya Mungu ni ukurasa ulio wazi. Tembea nje na soma kitabu. Hatujiulizi kabisa kama kuna Mungu, bali ni kwa nini hakuna mwingine? Ni wazi na dhahiri sana na ni kwa wazi sana. Ulimwengu hauwezi kuwepo kwa ujuzi au uelewa wa kisayansi bila kuwa na kuingiliwa kati. Ni mtu ytu yupi anayeweza kuuota mti? Ni mtu yupi anayeweza kumbuni ndege kwa kumchora asipokuwa ameonyeshwa yupoje? Malaika walilia kwa furaha baada ya kuumbwa ulimwengu huu. Ni nili ilikuwa mara yako ya mwisho ulipowahi kuulilia ulimwengu huu na waliomo ndani yake? Kama hujawahi kuulilia ndipo nakushauri uingie ndani na kuanza kufanya hivyo. Ni bustani yako. Umuumbwa kwa ajili yako. Ni zawadi kutoka kwa Mungu. Unashukuru kwa kiasi gani basi kila siku? Basi na uitunze bustani hii na uisafishe na pigania kuilinda. Kila siku fanya kitu kizuri ili kuiokoa. Walinde na kuwatunza wanyama na mimea yake iliyomo ndani yake. Usiiongezee ahadi ndani yake. Ikiwezekana tumia mtindo wa kutembea kwa migugu na usiendeshe gari.. tumia basi unaposafiri hata hivyo. Kama itatumika tena ndipo tumia tena. Kama ikivunjia, ndipo vunja na wewe. Kama itageuka na kuwa kitu kinginechochote, basin a uibadilishe na kuwa kitu kinginechochote. Usichague kwa kupiga kura – kasha ukamfanya mmoja wao kuwa ni uumbaji. Ni muhimu sana kuliko kulinda, barabara au hukumu ya kifo.

 

Kama unampenda Mungu unayapenda mawazo yake na utaziheshimu karama zake. Je, yanipasa kuelewa hilo? Kwa nini nahitaji kumwelewa mwanamke na ni kwa nini mwanamke anahitaji kumwelewa mwanaume? Je, huu si uwongo wa ajabu wa kisirisiri? Je, haifanyi iungo cha kuongeza kwenye rangi? Je, hamu haisababishi nguvu? Je, upendo sio safari? Kwa nini ni muhimu kuyapima na kuyachanganua mambo yote? Je, kuzijua siri zote, mambo yote kunanifanya kuwa mtu mzuri sana? Sio kule kujua kila kitu ndiko kunakotufanya tumpende Mungu. Bali kunatufanya tumheshimu Mungu zaidi. Kunatufanya tuuheshim uumbaji wake zaidi.

 

20 Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu;

Hula, akapangusa kinywa chake, Akasema, Sikufanya uovu.

21 Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka,

Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.
22 Mtumwa apatapo kuwa mfalme;

Mpumbavu ashibapo chakula;
23 Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo; Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.

Yatupasa tujue kwamba ni kwa kupitia kanisa tu tunaokolewa na kwa kupitia kanisa tu ndipo tunaweza kuvishinda vita dhidi ya uovu. Kanisa kongwe la kizamani, mwanamke kahaba wa kidini, linafunua kinywa chake na kusema “sijafanya ubaya wowote”. Tutafanyika kuwa wafalme. Kristo anatulisha chakula, kwa hiyo hatuwezi kudanganywa na tunafanyika kuwa watawala wa nyumba. Dunia haitabakia kama ilivyo wakati tunapolifikia lengo hili. Mume wetu atatupenda na wa mwisho atakuwa wa kwanza.

 

Ni nani anayependa dunia hii iliyopo isimame? Yatupasa tufanye kazi ili kuifanya ibadilike na kuitayarisha ili Kristo achukue hatamu. Kanisa ni kitu cha muhimu na muhimu kwa maisha yetu. Basi na usiende kuzini na mwanamke huyu kahaba wa kidini. Je, huoni kuwa ni vizuri sana ukalala kitandani kwako mwenyewe?

 

24 Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;

Lakini vina akili nyingi sana.
25 Chungu ni watu wasio na nguvu;

Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.
26 Wibari ni watu dhaifu;

Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.
27 Nzige hawana mfalme;

Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.
28 Mjusi hushika kwa mikono yake;

Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

Yeye asiyewatunza watu wa nyumbani mwake mwenewe ni mbaya kuliko asiye amini. Hatuhitaji kuwa imara sana, bali tunahitaji kuwa wene bidii na wenye akili na busara nyingi. Jipange kwa kujiandaa kwa ajili ya nyakati fupi. Je, mkulima hujaza pumba kwenye mazao mazuri kwa ajili ya ukame – au huwa anakwenda mapumzikoni? Je, tunazijenga nyumba zetu kwenye mchanga ulio kwenye ukanda wa fukwe za pwani ili zizoelewembali na mapigo ya mawimbi? Je, tunapenda mfalme wetu ajue kule tunakokwenda kupiga kwata? Je, Kristo anahitaji kuketi mezani kwako hata kabla hujapenda kwenda kanisani? Hata nzige, panzi wakubwa, wanajua kwamba ni nini kazi yao inayowapasa kuitenda. Je, tunataka Kristo atubebe mikononi mwake na kutufanya tuvinjari kwenye kasri yake? Enyi wanyama watambaao, hebu na awafanyie hivyo. Je, tunausikiliza unabii na kutii maonyo yake? Je, siyo Farao aliyejiandaa kwa baa la ukame? Tunajua kwa kuwa maneno ya Mungu yanathibitisha kweli yote. Acha chakula chako a chakula chako, jenga nyumba mahala pazuri, timiliza majukumu yako na mruhusu Kristo akubebe.

 

29 Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza,

Naam, wanne walio na mwendo mzuri.
30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote;

Wala hajiepushi na aliye yote;
31 Jimbi aendaye tambo; na beberu;

Na mfalme ambaye haasiki.

Wakati Kristo, mkono wake utakapokuwa nay eye kikamilifu sana. Wakati tunapoenenda kanisani na wote wakiwa na umoja na kutimiliza majukumu yao, basi Kristo anajivunia nao na hawazuii. Tunapigana na majeshi ya Shetani tukiwa pamoja na Kristo. Sisi tuko makini vitani. Kristo anatutaka tupigane naye huyo adui. Anatembea mbele kupitia kwa maadui na anashinda vita vyote wakati kanisa linaposonga mbele pamoja naye. Nguvu za kanisa haziwezi kupingwa; uweza wa kanisa hauwezi kupuuzwa. Sisi tu jeshi lake. Hatubebi mabunduki, wala hatutawaliwi au kuenenda kwa kanuni za namna moja maka hizo. Sisi tu kwenye jeshi la wanaojitolea, wadhaifu, tuliofanywa kuwa imara kwa malengo maalumu na mikakati maalumu.

 

32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza;

Au ikiwa umewaza mabaya;

Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.
33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi;

Na kupiga pua hutokeza damu;

kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.

[1]

Fikiri kile ukisemacho na fanya kabla hujatelekeza uamacho. Usitafute sifa na heshima kwene hii dunia unapokuwa hujaalikwa. Jiulize mwenyewe: ni kwa nini nilikukasirisha? Kwa nini ulikusudia kuniumiza? Je, iki? Kinapendeza? Hakiendani na upendo? Je, tunasema mambo yetu tukiwa na agenda za siri? Manabii wengi wa uwongo huja na kusema maneno yasiyo ya kweli na hata yasiyo na maana. Je, wewe ni mmoja wao? Je, unamtafuta roho akuongoze, au unaongozwa naye? Au unataka mamlaka ya kuwatawala wengine kwa ubatili? Kwa nini nafanya mambo yasiyo takiwa kufanywa hivyo wakati kila nilichonacho ni sahihi hapa?

 

Pendaneni kama Mungu na Kristo wanavyotupenda sisi.

 


[1] Kwa kujibu wa Tafsiri za Kiingereza za The Holy Bible: English Standard Version. 2001 (Pr 29:27-30:33). Good News Publishers: Wheaton

 

 

q