Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[126]

 

 

Daudi na Goliathi

(Toleo La 2.0 19950715-20000226)

 

Jarida hili linahusiana na hadithi ya Daudi na Goliathi na mwendelezo wa maana kusudiwa ya kiroho na kinabii ya harakati zinazohusiana na mazingirwa ya mgogoro huu. Kuelewa kiini na fundisho kuu la hadithi kwa ukaribu kunahusiana unaokusudia kwa ukaribu na ushindi wa Masihi dhidi ya utawala na imani za kidunia. Historia ya huko nyuma ya Wafilisti kuikalia Nchi Takatifu imetolewa pia. Kuanza kuikalia kwa Waisraeli kwenye nchi ya Kanaani kumeelezewa pia amoja na maelezo ya kina ya hadithi ya kuondolewa kwa Sanduku la Agano pia kumeelezewa ili kujenga vita na kuanzishwa kwa ufalme. Kuanzishwa kwa mstari wa uzao wa Daudi ni matokeo ya mwisho ya harakati hizi.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 2000 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki..

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Daudi na Goliathi

 


Watu wengi wanaijua hadithi ya Daudi na Goliath. Ni mojawapo kati ya hadithi kuu ya mara kwa mara na zinazoheshimika sana kwenye Biblia na mara nyingi inasimuliwa ili kufundisha jinsi mtu dhaifu, lakini aliye jasiri anavyoweza kumshinda mwenye nguvu, kwa masaada wa Mungu. Hata hivyo kuna mengi kwenye hadithi hii kuliko yale yaliyojitokeza tu kwanza. Kilichotendeka kwenye hadithi hii kinarudisha taswira nzima hadi nyuma mbali na hata kabla ya kipindi hiki ambacho Daudi aliingia uwanjani kupigana na Goliathi. Mkururu wote wa matukio uliwekwa kwa hisia yenye kumwamini Mungu kuwa ndiye aliyeko nyuma ya tukio lote zima, ambalo lilikuwa ni mfano na uwakilishi wa matendo au harakati za Masihi. Maana ya mambo yote yaliyo kwenye hadithi hii yote ya Daudi na Goliathi, na historia ya huko nyuma na hadithi yenyewe imeelezewa na kufafanuliwa kwa kina. Kuna maana yake nyuma ya kila kitu kimoja kilichosimuliwa na kufanyika kwenye historian a nyuma ya wahusika au wahusika wakuu au waprotogoni hawa wote, kwa kote kuwili, yaani kwa Waiasraeli na kwa Wafilisti.

 

Kuna fundisho maalumu lililowianishwa kwenye hadithi yote nzima ambayo ule mti unahusiana na ushindi wa Masihi kwa imani za ulimwengu. Giliathi wa Gahi alikuwa shujaa wa Wafilisti. Wafilisti walikuwa sio wenyeji wazawa wan chi ya Kanaani na hawakuendelea kuwa taifa lililo ndani ya nchi ya Kanaani. Mwishoni mwa karne ya kumi na tatu KK walikataliwa kuweka makazi yao kwenye kile kinachojulikana kuwa ni maeneo ya Aegean. Walikuwa wameondolewa kwa njia ya mikururu ya maafa na maangamizi makubwa yaliyouangamiza na kuupoteza ustaarabu wa Wahiti huko Uturuki, na pia nguvu au mamlaka ya Wamycenaens. Miji mikubwa ya Wakanaani iliangamizwa ia na Misri ilikupunguzwa au kupokonywa na kupunguzwa nguvu zake. Kipindi hiki kiliwekewa alama yake na utawala au mamlaka kwenye nchi hii na uaramia wa baharini.

 

Biblia inaelezea kwamba Wafilisti au Wafilistini, walikuja kwa barabara wakitokea Kafitori au Krete (Yeremia 47:4; Amosi 9:7; sawa na Kumbukumbu la Torati 2:23). Sehemu au pande za pwani kwa hiyo iliitwa Cretan Negeb au Negebu ya Wakerethi (1Samweli 30:14 soma kwenye Biblia ya RSV). Wakrete pia wana nasaba ya Wafilisti (Ezekieli 25:16; Sefania 2:5). Sura hizo zina uhusiano unaoendelea wa kinabii pia. Kwahiyo, hata hivyo, hakuna ushahidi wa kiakelojia wa Wafilisti kuikalia Krete. Kile tunachokijua ni kwenye Biblia inasema tu kwamba huko ndio walikotokea. Kwa hakika kabisa hawakukaa Krete kwa namna au maana yoyote. Hawakuacha ushahidi wa mambo mengi ya kiakiolojia. Ni wazi tu ulikuwa ni mpito endelevu. Kwakweli lilikuwa ni wimbi au kundi la pili la Wakaz wa Pwani mwa Bahari. Kuna kitabu kilichoandikwa na Velikovsky kinachoitwa Wakazi wa Maeneo ya Baharini, ambacho ni cha muhimu sana, na Velikovsky ameandika hoja nzuri sana kuhusu msalaba kwa wanazuoni kuhusu kipindi gani maalumu ulivyoanza na kuhusika. Kinachofanyika hapa ni kuvichukua vipindi maalumu vya wanazuoni kinachoendana sawa na wanahistoria wa kiakiolojia wa Kimisri hadi nyakati za Manetho, kwa nia ya kuepuka mngongano au mkanganyiko. Jina Wafilisti limetoholewa kutoka mtindo wa uandishi wa Kimisri la prst ambalo ndilo jina mmoja wa wakazi wa maeneo ya baharini. Neno la Kiebrania la pelishti ni kiambishi cha kisifa kulichotoholewa kutoka kwenye midhihirisho ya kieneo ya pelesheth. Chimbuko au mashina ya uandishi wa Kifilisti mbili zote zimeandikwa Pilisti au Palastu. Hakuna etymolojia ya Kisemitiki kwa jina hili na inaonekana kwamba ni ya mchanganyiko wa Kihindi na Kizungu, yaani Indo-European. Kwa hiyo, neno Wafilisti (Pisisti), au Palastu (Palestina), limetoholewa kutoka kwenye majina ya Wafilisti. Lakini watu walioko huko leo, Wafilisti, sio watu walewale kama Wafilisti au Wapalastu, ambao walikuwepo huko katika nyakati za Daudi. Waliuwa ni watu wa jamii ya mchanganyiko wa Wahidi na Wazungu ambao hapo mwanzon waliishi Misri na baadae kwenye maeneo ya pwani mwa bahari.

 

Wafilisti waliishi maeneo ya pwani ya bahari kwenye jimbo ambalo kwa sasa tunalijua kama Ukanda wa Gaza na kwenye maeneo ya bara ya Kanaani. Hapa walishirikiana na kundi lingine la watu wa makundi yaliyowasili hivi karibuni, ya Waisraeli. Chanzo cha migogoro na matatizo, ambayo ilifikilisha kufikia ukomo wa Zama za Shaba na mwanzo wa Zama ya Chuma, kumebakiwa kuwa ni mkanganyiko bado.

 

Dhana ya vita vya kikanda imebishwa na wale walio kwenye maafa ya asili. Kwa hiyo, wanazuoni wamekuwa wakijaribu kubisha kuwa au pengine ni vita vyao vya kikanda ndivyo vimesababisha vuguvugu au mwondoko huu, au huenda ni maafa ya kiasili. Velikovsky ni mtaalamu wa majanga na maafa ya asili. Anapinga kwamba mlipuko wa volcano ya Thera ulisababishwa na kuondoka au mwenendo wa watu hawa na kwa ajili ya kuwekwa tena kwa kipindi hii maalumu pia. Siri hii imeelezewa kwa kina zaidi kwa kukosekana kwa maandiko tangu kipindi hii, na hivyo kukapelekea kukiweka kipindi hii mwanzoni mwa Zama ya Chuma, kijulikanacho kama karne kuanzia ya kumi na mbili hadi ya kumi na moja KK, kijulikanacho pia kama Zama za Giza (usikichanganye na ile Zama ya Giza ya kipindi cha zama za kati kilichotokea yapata miaka ba kukipa muda kipindi hiki cano caused the moveme, iliyofuatia). Tulikuwanacho kabla ya kipindi cha zama kati, kile kilichokuwa kinajulikana kama Zama ya Giza kwenye karne ya kabla ya kuanguka kwa Dola ya Warumi huko Ulaya. Hivyo sivyo vipindi vya Zama ya Giza ambavyo watu hawa wanatajwa kwavyo. Wanaviita kuwa ni Zama za Giza za Mashariki ya Kati, karne ya kumi na moja kabla ya Kristo. Mwaka 1995 kazi ya uchimbuzi ilifanywa na Profesa Trude Dothan pamoja na Profesa Seymour Gitin wa Chuo Kikuu kilichojulikana kama the Albright Institute, kwenye maeneo hayo ya miji ya Wafilisti. Mji wa Ekron ulikuwa ni mji mdogo wa Wakanaani wa Dunams 50 na uliangamizwa mnamo mwaka 1200 KK na mahali pake palichukuliwa na mji uliozungushiwa vyema wa rudishwa tena kwa kuzungushiwa Dunams 200.

Kazi ya uchimbuzi imefanyika huko Ashidodi, Ekroni na Ashikeloni. Ashidodi na Ekroni inaonyesha jamii iliyopangilika vizuri ya wahamiaji wapya waliotokea kwenye historia ya kimijini iliyoanzisha miji mikubwa na iliyopangiliwa vizuri juu ya maganjo ya miji midogomidogo ya Wakanaani (kwa mujibu wa malaka ya Abraham Rabinovich, Jerusalem Post, art. Nothing But a Name, June 17 1995, p. 8).

 

Miji mingine miwili ya Wafilisti huko Pentapolis ni Gaza, ambao maganjo yake yako kwenye mji wa sasa, na Gati au Gathi, unaoaminiwa kuwa ni eneo la Tel es-Safi siyo mbali kutoka Ekroni. Adolphe Lods, aliyekuwa Profesa wa Kifaransa, anasema kwamba Wafilisti walikuwa ni wenyeji na wakazi wa maeneo ya bahari, na kwamba Rameses III alimrithisha kazi ya kuwasukumia kwenye mipaka ya Misri mwaka 1192 KK (Kwa mujibu wa kitabu cha Israel, Hooke kilichotafsiriwa na kina Routledge & Keegan Paul, London, 1962, p. 348), au huenda ni sahihi zaidi kama miaka minane ya Rameses III (takriban mwaka 1188 KK; kwenye kamusi ya Interpreter’s Dictionary of the Bible, Vol. 3, p. 791). Walizuia baadhi ya desturi zao. Silaha zao na zana zao kama zilivyoelezewa kwenye 1Samweli 17:5-7 zinafanana na za watu wa Asia Ndogo (ibid.).

 

Walitohoa desturi za Wakanaani pamoja na miungu yao walikuwa ni miungu halisi wa Kisemitiki: Dagoni, mungu wa mazao; Atargatis-Derketo, mungu-mke wa Ashikeloni, ni aina ya kushaniri kila mahali kwa Astarte Msemitiki (ibid., p. 349). Mengi yameandikwa kuhusu Dagon, kwamba ni kama alionyeshwa kwa umbo la samaki, lakini Dagon alikuwa ni mungu wa nafaka kwa mujibu wa Lods. Ndivyo ilivyokuwa pia, kwamba ibada za Astarte zilikuwepo huko chini ya Atargatis-Derketo. Astarte wa Wapalestina au wa Wafilisti anatajwa kwenye maelezo yaliyovumbuliwa huko Delos; Baal-Zebubu “mungu wa mainzi”, mungu wa Ekroni. Huyu ndiye alikuwa wa mungu wao mwenye umbo la mjumuiko wa miungu yote au muundo. Kimsingi, ilikuwa ni imani na muundo wa kisemitiki iliyotuama kwenye imani za Kibabeloni. Kwa hiyo, Wafilisti waliichukua dini na imani ya Kibabeloni. Miungu hii ilikuwa ya mrengo wa imani za Kibabeloni, na Wababeloni walikuwa ni Wasemitiki.

 

Maelezo ya kina kuhusu imani hii yameandikwa kwa kina kwenye jarida la Utakaso na Tohara (Na. 251).

Makuhani wa Attis ambao waliandamana katika karne ya nne kuwa wakristo wahiba  anane zao. Mipangilio ya ukristo wa kisasa wa jua ambayo watuma jina pasaka kwa rubundji wa mpangilio na kuutumiza Ahere na mfano ya miniyu na mungu mengine. Tertulian anasema Atargatis alikuwa miungu ya Syria. Kitabu cha Wamakabayo kinasema waliitu jua kuwa Hadard wamaanisha mwana wa kiume wa jua. Talmud analiita Taratha. Kule Armenia yeye ni Tharatha yeye ni kama miungu ya wasemetu Ishalar.Athtar au kwa upesi Anglo saxon Easter. Strabo na Hesychus pia wanamjua na Athara na malezo ya delos waaiita. Aphrodite (ERE ibid.) Askelon, Karnaim na Delos walimtumikia Astarte. Inavyojulikana kama Derketo kwa Askelon na miungu yake ya Chini Ilikuwa Samaki. Hiihuonekana kuwa mwanzo wa Mermaid. Lucian hawezii akamtambua roho ya wanasiria kule Hierapolis na muundo wa Askelon, kwa sababu roho huo kwa Heirapolis alikuwa na muundo kamili ya binadamu na akamwita. Hera, lakini akakubali unaweza kutambulishwa na Rheokuna kutiamini ambayo na chache kuwa moja na roho moja. Wanafunzi wa Atargatis na Astarte hawakula samaki, na maumbile yao ilitambulisha miungu hayo kama moja na roho sambamba. Roho ulitambulishwa miungu hayo kama moja na roho sambamba. Roho ulitambulishwa na eneo ambayo ulikuwa tofauti kwa mafikirio ya watu wa kawaida vile alivyokuwa. Ishtar kule Asssyria kule Nineveh na Arbela. Jina la kutumia ya Hierapolis ni Mabog na inamaanisha nyakati kule Aramaiz (cf. ERE, ibid.). Umoja wa maji na nyakati pia.

 

Kutokana na kitabu cha 2Wamakabayo 12:26 Yuda Mmakabayo aliliendea kinyume Hekalu la Atergatis la huko Karnion mwaka 164 KK na akawaua watu 25,000. Paton anahitimisha kwa maandiko yake yaliyo kwenye 1 Makabayo 5:43 kwamba imani na dini potofu ya Atargatis haikustawi tu huko Hieropolis na Askalon, bali huko Bashani pia. Tofauti zilizopo kati ya Damascus na Banias huko Kefr Hauwar zinaashiria dalili ya kwamba hekalu lilikuwepo huko na pia idadi ya utofauti za huko Delos, zinaweka tarehe za muda mfupi sana kabla ya kuanza kwa zama za Ukristo, ikimuonyesha yeye na Hadadi na pia kumuonyesha yeye kama Aphrodite (sawa na isemavyo ERE, vol. 2., p. 166). Kwa hiyo, yeye ni mwenzi wake Hadad, mungu jua au Baali. Ni kama alivyokuwa Rhea, alimfanyia Attis ambaye anaelezewa pia na yeye.

 

Paton pia anasema kuwa maandiko ya Ovid ya mwaka 17 BK inatuambuia vile vile Dereto miungu ya siria na Atargatus na uonyese maneno mapya kuwa alibadilishwa kuwa samaki kule Bamboyce, jina la ugiuku inayomaanisha Hierapolis maandiko ya Strabo yamwaka  24 BK Inasema.

 

Artargate (au Artagate kwenye baadhi ya MMS) Wasyria wanamwita Artara, lakini Ctesia wanaiita Derketo. Hapa Artagatus anatambuliwa na “Artar (Athtar, Astarte). Kwa njia hiyo ambapo anatambulika na Aphrodite kuluyana na marelezo ya Delo (ERE ibid).

 

Cornitus (mwaka 68 BK) anasema kwamba samaki na bata zilikuwa vitu safi kwake Atargatis miungu mke wa Wasyria. Hii imeaminiwa penye mfano ya samaki kule Ronia ilijitokeza katika karne ya kwanza. Wakristo hawangetengeneza mfano wa imani yao  kujaa kilichokuwa cha shetani kuabudiwe kule palestina kwa  karne nyingi na katika nyakati za Kristo. Pliny kwa mwaka 79 BK anasema kwamba Ceto anaabudiwa kule Yafa. Pliny na Strabo wanasema mabaki ya kiumbee cha ziwa ziwa kuhuekwa Joppa. Wote wawili, yaani Piny na Ceto wanaongelea kuhusu sanamu kubwa skeleton ya jitu au kiumbe wa baharini iliwekwa huko Yafa. Ceto huenda anachukuliwa kama mabadiliko ya Derceto na kusema lakini paton anasema hii haionekani (ERE ibid.). Pliny anaiona Atargatis kama Dereto na kusema kwamba ahabudiwe kule Hierapolis au Bambyce au Mabog. Plutarch anasema kulikuwa mahali pa maji ya kuweka samaki ilyoheshimiwa na kusema miungu huyo aliabudu hapo, Inatambuliwa na Aphrodite na Hera au miunguanayetengeneza kutokana na moshi ya hewa mbegu ya kila kitu (ERE ibid.). Dhibitisho sahihi ilitolewa na maandiko ya Lucian ca 200ce na mshahidi kiume yeye wa SiriaVile tumeandika katika angependeka kufahamu kama Hera LAKINI paton akasema hakuna ubabaishi tunakumana na Atargatis (ERE ibid.). Kwa hiyo miundo wa Atargatis, Ishtar au Astarte, Ashitaroth au Easter ni moja ya tabia ambazo zimekaliwa kwa biblia inavyohusu hivi mafikirio.Fikira ya ushafishaji inahusu mpango ya kutolewa kwa tabia ya huo nabudilaji. Inatuonya nyua kuhusu muundo wa Shahabu ya ndama chini ya majina kadha (sawa na ilivyo pia kwenye majarida ya Ndama wa Dhahabu (Na. 222)) na lile la (Utakaso na Tohara (Na. 251)).

Kwahivyo utakaso wa Attis na Easter bado uliendelea kule kule Siria hadi mwaka 200 CE.

(Imukuliwa tena kutoka kwenye jarida la W.E. Cox la Pinata (Na. 276)  Christian Churches of God, 1999.)

 

Viongozi waliitwa seren ambalo lilitumiwa tu kwenye lugha ya Kiebrania ikijumuishwa na lugha ya Wafilisti. Ni wazi na dhahiri sana kwamba neno la lugha yao wenyewe linashabihiana na neno la Kiyunani la turranos. Biblia ya Kisyria inalitaja neno hili truno na kwa lugha ya Targum ni turono (ibid.). miji mitano ilianzisha shirikisho. Kwa mfano, mwana mfalme wa Gathi wakati mwingine anafanywa kuwa mfalme lakini ni Mfalme wa Gathi peke yake, na sio wa Wafilisti wote. Hawakuwa na mfalme wan chi nzima. Kulikuwa na mabwana watano wa Wafilisti. Sehemu ya upande wa Dori ulimilikiwa na washirika wa Wafilisti, Wazekali, ambao ni kundi jingine la “wakazi wa maeneo ya bahari”. Hawakuwa ni wa kundi hilohilo moja. Wafilisti walifikia kupata umaarufu kimaajabu sana kwa uwashindi wa Waashuru chini ya Senikarebu mwaka 701 KK. Kwa kweli hawakufika kilele cha nguvu zao hadi hatimaye wapolishwa na Waashuru. Ilifanyika kuwa miji ya watu waliostawi ambayo ni mataifa pia ndani ya mfumo wa kiuchumi wa kifalme, kwa kuwa walikuwa ni watohoaji wakuu. Waliziainisha mila na desturi zao na waliziiga na kuzihusianisha kimila. Kwa namna hiyohiyo ndivyo dini za usiri za Kibabeloni ziliga na kutohoa. Hiyo ilikuwa ni kusababisha kabisa mauti au kifo chao, kwa kuwa hawakuwa na mfumo wala utaratibu maalumu wa kimila, ambao uliwafanya wawe ni watofauti. Watu hawa waliiga imani ya kidini ya Wababeloni na ndipo hatimaye walikithi vigezo kwenye mfumo wa kiuchumi wa Waashuru.

 

Hatimaye, waliangamizwa na Wababeli kwa kuwa walifanyika kuwa ni mji wenye mataifa yenye watu waliostawi ndani ya mfumo wa utawala wa Waashuru. Kwa hiyo hatimaye Wababeloni waliwaangamiza Waashuru, kwa kuwa walikuwa wameiga vitu vingi sana kutoka kwenye imani ya Waashuru. Walikuwa wamefanana sana na kujulikana na Waashuru. Walikuwa ni wa mwisho kusikilizwa kwenye orodha ya watumwa ambao ulishurutishwa au ksababishwa na dini. Ekroni iliangamizwa na Nebukadneza mwaka 603 KK. Orodha iliyokutikana kwenye matukio ya mafanikio ya Wababeloni yanaonyesha kutokea tangu karne ya tano KK huko Nippuri ukitaja matukio ya utumwa wa Is-qal-lu-nu (Ashkelon) na Hazatu (Gaza). Gitin anaonyesha kwamba rekodi hii inaonyesha kupotea na kutokomea kwa Wafilisti kutoka kwenye kurasa za historia (soma kitabu cha Rabinovich, ibid.). yuda, Lawi na sehemu ya makabila walirudi kutoka utumwani Babeli, Wafilisti hawakurudi. Ufafanaji wa kiutamaduni wao na Waashuru ulikuwa ni wa hali ya juu sana na kwamba hawangeweza kumudu kuishi kama utambulisho wa kimila, kwa mujibu wa Gitin. Hali yao ya kimaadili ilihusiana au kufanana na washiriki au marafiki wa Aegean wa huko Cyprus baada ya kuonyesha mpangilio kwene miji ya zamani kidogo iliyopelekwa kwenye maeneo mapya na kuanzisha mila au desturi tofauti iliyowasababisha wao wamudu kuishi. Kwa hiyo, ustaarabu wa Aegean, ndugu wa Wafilisti, walioishi huko Cyprus, waliweza kuondoka na kujongea kwenye maeneo mapya na walimudu kuishi kwa kuwa hatimaye walianzisha desturi na mila zao zilizotofauti. Na hii ndiyo sababu ya pekee iliyowafanya wamudu kudumisha. Mafunzo pekee tunayohitaji kujifunza kutoka kwa Wafilisti hata hivyo ni kuhusu wajibu wao kama nguvu ya upingaji dhidi ya Israeli ambayo ilisababisha kuwepo kwa kitisho cha nje kikubwa vya kutosha kuwalazimisha Israeli waungane kama taifa chini ya Sauli. Kushindwa kwa huko Ebeneza kulikuwa ni hamasa au changamoto. Hata hivyo, mchakato ulikuwa umekwisha kwa kipindi kilichoongezwa.

 

Kwa hiyo kile kilichotokea ni kile alichoamua Mungu ili kulianzisha taifa la Israeli kwenye Nchi ya Ahadi. Mlolongo wa maafa ulianza na Israeli wakaenda utumwani Misri. Adui aliamua kuwaweka watu wake mwenyewe wapate nafasi na fursa nzuri ya kuwazia Israeli wasiweze kuichukua na kuikalia nchi ya Kanaani au ya Israeli; kwa maneno mengine ni kwamba ili wasiweze kuimiza ahadi. Kwa hiyo watu wa asili ya maeneo ya pwani mwa bahari Wafilisti, ndipo wakawekwa katika Israeli wakijaribu kujikusanya na kuzuia kuingia na kutamalaki kwao Israeli kama taifa. Kama wangefanya hivyo, wangeweza kuihakikishia dini ya Kibabeloni kuwa ilikuwa bora na maana sana kuliko ile ya Waisraeli, na ndipo dini tuliyonayo sisi isingeweza kuwa na nafasi au kuingizwa na kuanzishwa humo. Dini ya Kibabeloni ingeweza kuichukua dini hii mapema sana. Na kwamba vita iyiyoko ya imani ya Kibabeloni dhidi ya imani ya kidini ya mchanganyiko wa Ukristo na dini ya Kiyahudi, ingali inakuja bado na vita hiyo inapigwa vita kati siku hizi za mwisho. Imani ya Kibabeloni ni imani ya dini iliyo kubwa sana hapa duniani kwa sasa. Wafilisti waliileta au kuiwakilisha dini ya Kibabeloni. Vita hivyo ni vile vinavyopiganwa ikihitimishwa sasa, katika nyakati hizi za mwisho.

 

Mateso na dhuluma walizofanyiwa Israeli na Wafilisti ilishuhudia makabila ya Dani na Yuda yakijisalimisha na kuwatumikia maadui wao waliowashambulia (soma Waamuzi 16:1-3). Hatimaye walienenda kinyume na makabila ya Ufraimu na Benyamini ambao waliyashinda. Katika Israeli, huenda kabila la Yusufu, ndiyo waliasi na Wafilisti wakawashambulia. Mungu amekuwa akitenda kazi na Waisraeli kwa kipindi hiki chote. Rehea nyuma kwenye majarida ya Samsoni na Waamuzi (Na. 73), na Jeshi la Gideoni na Nyakati za Mwisho (Na. 22), ambapo tutajionea jinsi Mungu alivyokuwa anashughuika na Israeli zaidi ya kipindi kile cha Wakanaani na Wafilisti. Kila mara walipoangukia kwenye dhambi Mungu aliwaacha ili wagawanike na kuvunjika, na kisha wakati walipokuwa wanageuka na kumrudia waliimarishwa na kujijenga tena. Kwa sababu hii, aliendelea kwa sababu za kimsingi sana dhidi ya Wafilisti ili kuwarejesha na kuwaimarisha tena Israeli kwa kipindi kilichokusudiwa. Aliweka mpango wa kumuinua kuhani mwaminifu (1Samweli 2:35) ambaye angefanya kila kitu sawasawa na mapenzi na nia ya Mungu. Kuhani huyu ndipo angeomba kwenye uwepo wake (NB).

1Samweli 2:35-36  Nami nitajiinulia kuhani mwaminifu, atakayefanya sawasawa na mambo yote niliyo nayo katika moyo wangu, na katika nia yangu; nami nitamjengea nyumba iliyo imara; naye atakwenda mbele ya masihi wangu milele.
36 Kisha itakuwa, ya kwamba kila mtu atakayesalia katika nyumba yako atakwenda kumsujudia, apate kipande kidogo cha fedha, na mkate mmoja; na kumwambia, Tafadhali unitie katika kazi mojawapo ya ukuhani, nipate kula kipande kidogo cha mkate.

 

1Samweli 3:1 Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri.

 

Kuna uhusiano na uhitajiko wa Kimasihi kwenye andiko hili. Linasema, kuna kuhani mwaminifu aliyeinuliwa, ambaye atakayefanya sawasawa na mambo yote yaliyo kwenye moyo wa Mungu, na katika nia yake. Atakwenda kumjengea nyumba iliyo imara; naye atakwenda mbele ya masihi wake milele. Sasa Samweli alikufa!

 

Kuna kuhani aliyeinuka atembee mbele za Mungu milele, mbele za mtiwa mafuta, na mtiwa mafuta huyo ni Masihi. Kwa hiyo kuna kuhani aliyeinuliwa atembee mbele za Masihi milele. 1Samweli 2:36 ni unabii kwa kuhani wa Israeli kwa kuwa ukuhani umetiwa unajisi na ulipaswa kuombea uwepo wake. Ni unabii mkuu na wenye nguvu sana!

 

Samweli aliawekwa kuwa ni nabii na Bwana basi maneno yake na yasiangukie chini.

1Samweli 3:19-21 Samweli akakua, naye Bwana alikuwa pamoja naye, wala hakuliacha neno lake lo lote lianguke chini. 20 Nao Waisraeli wote, toka Dani mpaka Beer-sheba, walitambua ya kwamba huyo Samweli amewekwa kuwa nabii wa Bwana.

 

Kisha Samweli aliwakusanya pamoja Israeli huko Shilo kwa kutegemea kile kilchojulikana kama mapenzi ya Mungu. Kumbuka kuwa, Yerusalemu ulikuwa sio makao makuu au mji mkuu na wala haukuwa huko Hebron. Maskani ya Mungu ilikuwa huko Shilo.

21 Naye Bwana akaonekana tena huko Shilo; kwa kuwa Bwana akajifunua kwa Samweli huko Shilo, kwa neno la Bwana.

 

1Samweli 4:1-11 [Ikawa siku zile Wafilisti walikusanyika ili kupigana na Israeli,] nao Waisraeli wakatoka juu ya Wafilisti kwenda vitani;wakatua karibu na Ebenezeri ,nao Wafilisti wakatua huko Afeki. 2 Nao Wafilisti wakajipanga juu ya Israeli; na walipopigana, Israeli wakapigwa mbele ya Wafilisti; wakauawa watu wa jeshi lao lililokuwa uwandani wapata watu elfu nne.

 

Hapa tunawaona Israeli wakimtii nabii wa Mungu lakini wakishindwa kwa upanga. Matokeo ya uadui huu yalitegemea kwenye uwepo wa kimwili wa Sanduku la Agano. Mungu alikuwa anawaimarisha Israeli na kuwaambia kuwa ‘hampo sahihi machoni pangu; hamjajiandaa’. Kwa hiyo anaweka masharti ambapo nakwenda kuwaunganisha na kuwaweka pamoja Israeli, kwa kuwa kila mtu wakati huu alikuwa anafanya kile alichokuwa anakiona kuwa ni chema machoni pake mwenyewe na walikuwa kwenye makundi tofauti mbalimbali. Walikuwa chini ya makabila na kulikuwa hakuna uongozi wa kati. Mungu alikuwa anakaribia kuwafanya wawe ni mhimili wa uongozi. Waliona kuwa wameshindwa, kwa hiyo hatimaye waliamua ‘ni jinsi gani tunaweza kushinda?’ ‘Najua kuwa Mungu ametuweka hapa, na tuende sasa tukalitwae Sabduku la Agano na kisha tukalitangulize hilo Sanduku mbele yetu tuendapo mapiganoni’. Kwa kuwa walikuwa na uwepo wa kimwili wa Sanduku hili la Agano walidhania kuwa hiyo inatosha. Hawakujua wala kushukuru kuwa lilikuwa ni alama tu ya sheria au torati ya Mungu, tabia na mapenzi yake. Ni kama walivyo Wayahudi wa leo hawayaoni malengo ya kiroho ya uhusiano na Mungu. Kuna makusudi ya kiroho kwa haya yote.

3 Hata watu walipofika kambini, wazee wa Israeli wakasema, Mbona Bwana ametupiga leo mbele ya Wafilisti? Twende tukalilete sanduku la agano la Bwana toka Shilo hata huku, lije kati yetu, na kutuokoa katika mikono ya adui zetu. 4 Basi wakatuma watu kwenda Shilo, nao wakalileta toka huko sanduku la agano la Bwana wa majeshi, akaaye juu ya makerubi; na Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwako huko pamoja na sanduku la agano la Mungu.

Kile anachokifanya Mungu hapa ni kwamba analichukua Sanduku la Agano kutoka kwenye Maskani na anasema: “Nakwenda kuweka uwepo wangu ujulikane matika Israeli”. Kwa wakati ule wana wa Eli (Hofni na Finehasi) walikuwa waovu. Ukuhani ulikuwa umepotoka na kukengeuka kabisa; wkatoto wake wakawa wanafanya ngono na wanawake hekaluni. Walidai na kupokea rushwa. Walipotosha hukumu kwa kupokea rushwa na Eli hakuwakemea. Samweli aliuona uovu kwenye huduma ya kikuhani chini ya Eli. Aliuona uovu wa Hofni na Finehasi na tutaona kwamba Samweli alifanya kitu hichohicho. Samweli alikuwa ni nabii wa Mungu lakini hakuzikemeadhambi au makosa waliyoyafanya watoto wake mwenyewe ambayo aliyaona yakifanywa wakati wa Eli yakitendwa na kina Finehasi na Hofni. Haya ni makosa yanayofanyika kila mara. Viongozi wa Makanisa ya wateule, kwa kweli wanaweza kuziona familia zao zilitenda maovu na mapotofu na warithi wao wanaweza kuyaona hayo nab ado wakawaacha watoto wao wayafanye hayohayo. Hivi ndivyo ilivyotokea kwa Eli, na hiki ndicho kilichotokea kwa Samweli. Kwa sababu ya hiyo, utawala ulichukuliwa wote kabisa na ukuhani. Utawala au uongozi wa Israeli ulichukuliwa kutoka wa waamuzi na kwenye ukuhani, na wakapewa wamonaki, mikononi mwa uongozi chini ya mfalme. Kwa hiyo Mungu aliwachukua kina Hofni na Finehasi pamoja na Sanduku la Agano kutoka Shilo, na kuwaweka kwenye nafasi ambayo waliuawa kwayo kwa kuwa walikuwa wamemtia unajisi na kumfanya asifae mchungaji wa Sanduku la Agano. Hii ilipuuwa na kutotiliwa maanani.

 

5 Na sanduku la agano la Bwana lilipoingia kambini, Israeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu, hata nchi ikavuma. 6 Nao Wafilisti waliposikia mshindo wa zile kelele, walisema, Maana yake nini mshindo wa kelele hizi kubwa katika kambi ya Waebrania? Wakatambua ya kuwa sanduku la Bwana limefika kambini. 7 Wafilisti wakaogopa, maana walisema, Mungu ameingia kambini. Wakasema, Ole wetu! Kwani halijawa jambo kama hili tangu hapo. 8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa na mkono wa miungu hawa walio hodari? Hawa ndio miungu waliowapiga Wamisri kwa mapigo ya kila namna jangwani. 9 Iweni hodari, na kufanya kiume enyi Wafilisti, msije mkawa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa watumwa wenu; fanyeni kiume, mkapigane nao. 10 Wafilisti wakapigana nao, Israeli wakapigwa, wakakimbia kila mtu hemani kwake; wakauawa watu wengi sana; maana katika Israeli walianguka watu thelathini elfu wenye kwenda vitani kwa miguu. 11 Hilo sanduku la Mungu Likatwaliwa; na Hofni na Finehasi, wale wana wawili wa Eli, wakauawa.\

 

Sanduku lilikua na madhara yaliyo kinyume. Wafilisti walipigana kwa nguvu zote kwakuwa walikuwa kwenye kitisho. Israeli elfu thelathini waliuawa wakiwemo watoto wa Eli. Mungu aliwauwa makuhani hawa na akalitoa Sanduku la Agano mikononi mwa Wafilisti. Jambo hili lilifanyika mahususi mikononi mwa mtiwa mafuta wake nabii. Kwa nini? Jibu lake lilikuwa ni kwamba Israeli walipoteza vigezo vya kuwafanya wastahili kusimama mbele za Mungu kwa utaratibu au vigezo zilivyokuwepo. Zaidi sana ni kwamba Mungu alikuwa bado ana kazi ya aliyotaka waifanye Israeli na isingeweza kufanywa kwa utaratibu ule ya upangiliaji au mpangilio. Kwa hiyo Mungu ilimlazimu kuwaacha n aka kufanya kwake hivyo ilimbidi kuwaangamiza makuhani pia. Alisababisha Hofni na Finehasi aende vitani, na aliwauliambali na kisha watu takriban 30,000 pamoja nao.

 

Kuondolewa kwa Sanduku la Mungu mikononi mwa Wafilisti kulibidi kuwaonyesha Wafilisti pia kwamba alikuwa wanaabudu vinyago au sanamu zisio na uweza. Sanamu ya Dagoni ilitengenezwa ikiwa inajionyesha jinsi ilivyokua imeliangukia Sanduku la Agano (1Samweli 5:3-5). Ilikuwa imeliangukia Sanduku la Agano na ilikatika kichwa chake na kuangukia kwa mwonekano wa kulisujudia sanduku kwa paji la uso ake. Kuna maana kutokana na kitendo hiki. Kitendo hiki cha kukatika na kuondolewa kichwa chake na mikono yake kutoka kwenye kiiliili kinahusiana na dhana ya kuwatia mhuri watu kwa mintaarafu ya imani ya mungu ao. Umetiwa mhuri kwenye paji la uso na mikononi kwa mawazo yako yahusuyo kwenye imani hii ya kidini na kwa kuwa ni kifaa au chomo cha kuchukua na kueneza imani ile kwa kazi yake na kwa matendo vya kijamii. Kwa hiyo, mpangilio wa kijamii na kiuchumi wa imani umeonyeshwa kitaswira na mikono, na dhamira ya kifikra au eshwa kitaswira kwa paji la uso. Na ndiyo maana, utiaji mhuri wa imani kwenye paji la uso na mikononi. Watu hawa walipigwa pia na maradhi ya majipu (1Samweli 5:6; 6:4). Maradhi haya ya mjipu yametajwa pia kwenye Kumbukumbu la Torati 28:27 kuwa ni moja wapo ya dalili za laana na tauni ya Misri. Tunajua kuwa haya ni haemoroids, au maganjo. Wafilisti walikua na aina zake nyingi yaliyoaua watu wake wakati walipokuwa na Sanduku la Agano na waliwapa majipu matano ya dhahabu na panya watano wa dhahabu, kila mmoja ni kwa kila bwana mmoja a mabwana wa Wafilisti, ni kama sadaka za kupigiwa kura kwa Sanduku lilipokuwa linarudi baada ya miezi saba (1Samweli 6:1-14). Walikuwanalo kwa kipindi cha miezi saba na halikuwawanyia kitu chochote ila ni mateso tu. Bwana aliapa ushuhuda ka njia ya kitendo hiki kwa pande mbili zote, yaani kwa Waisraeli na kwa Wafilisti.

 

Kwa kupitia dharura hii, Mungu aliianzisha serikali kuu na kiti cha enzi ambacho siku moja Masihi angekirithi. Alikuwa anaweka mfumo wa kurithi ajapo Masihi. Kwa hiyo matukio yanayozingira uanzishwaji wa mfumo a kifalme pia yanakwenda sambamba na makusudio yake.

 

Kwanza kabisa, ufalme ulinzishwa kwenye mstari wa uzao wa Sauli wa Benyamini. Benyamini lilikuwa ni kabila dogo zaidi kati ya makabila yote na kwa kweli lilikuwa karibu lifutiliwe mbali kwa kutokuwepo kwake kwenye matukio yaloyotangulia (Waamuzi 20 & 21). Mambo yaloiyosababisha Benyamini wafutiliwe mbali katika Israeli hayakuwa na maana yoyote. Soma Waamuzi 20 na 21 na utaona kwamba Benyamini walifutiliwa mbali, karibia kwa mtu (kulikuwa na idadi ya watu anaume 600 walioachwa katika Benyamini). Walipewa wanawake wa makabila mengine wawaoe, ili kwamba Benyamini wasiweze kufutiliwa mbali kabisa. Lakini dhambi iliyowapelekea wafutiliwe mbali inatokea ka msingi a kila siku wa watu wetu. Ni ka kiasi gani unaweza kudhani Mungu atahifadhi hasira yake dhidi ya makabila ya Israeli wakati hakuwa amemwachia ama kuwasamehe Benyamini kwa uovu wao mmoja tu?

 

Ufalme ulianzishwa na Mungu kwa kupitia nabii Samweli. Yapasa iulikane pia kwamba Samweli hakuwaadibisha watoto wake, ni kama alivyofanya Eli tu kwa kushindwa kuwakemea atoto wake kina Hofni na Finehasi aliokuwa pamoja naye. Wanasaikolojia wengine wangepinga kwamba Samweli alikuwa amelelewa na kukulia kwenye nyumba ya Eli, hekaluni, na hivyo alidhani kuwa namna ya kawaida ya kuwalea atoto wake. Hiyo ni kweli. Kama tutawaona wakilelewa kwa namna hiyo pasipo mfano mwingine wowote, basi tungezania kuwa hiyo ndiyo namna kufanya hilo. Samweli alijionea matokeo ya kina Hofni na Finehasi, lakini aliwalea watoto wake mwenyewe kwa nana hiyohiyo.

1Samweli 8:1-22 Hata Samweli alipokuwa mzee, aliwafanya wanawe wawe waamuzi juu ya Israeli. 2 Na jina la mwanawe mzaliwa wa kwanza aliitwa Yoeli; na jina la wa pili Abiya; walikuwa waamuzi katika Beer-sheba. 3 Ila wanawe hawakuenda katika njia zake, bali waliziacha, ili wapate faida; wakapokea rushwa, na kupotosha hukumu. 4 Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama; 5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote. 6 Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba Bwana. 7 Bwana akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao.

 

Wazo shirikishi: Hawakudhania kuwa Mungu angeingilia kati na kumuinua nabii mwingine ahusiane na wana. Walidhani kuwa waikuwa wanakwenda kupigwa na Yoeli na Abia wana wa Samweli. Hawakugundua kuwa Mungu alikuwa amewatoa kina Hofni na Finehasi watoke na kwenda kwenye uwanja wa vita au wa mapigano, wakati wakiwa hawana nia wala wazo la kwenda vitani, na kisha akawachinja huko. Hawakuwa na ujasiri, au imani, ya kuamini kuwa Mungu angewaondolea mbali kina Yoeli na Abia kama alivyowaondolea mbali kina Hofni na Finehasi. Walitaka kujiwekea Mfalme wao wenyewe na utakuta kwamba ndipo ufalme ulivyoanzishwa, lakini Mungu aliruhusu jambo hili kutokea kwa sababu mbalimbali. Mungu aliruhusu jambo hili kutokea ili kwamba ufalme uweze kuanzishwa, na kiti cha enzi kilianzishwa kwa ajili ya ujio wa Masihi.

8 Kwa kadiri ya matendo yote waliyonitenda tokea siku ile nilipowatoa katika Misri hata leo, kwa kuniacha mimi, na kwa kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokutenda wewe. 9 Basi sasa, isikilize sauti yao; walakini, uwaonye sana, na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki. 10 Naye Samweli akawaambia wale watu waliotaka mfalme maneno yote ya Bwana. 11 Akasema, Mfalme atakayewamiliki ninyi atakuwa na desturi hii; atatwaa wana wenu na kuwaweka kwake, kwa magari yake, na kuwa wapanda farasi wake; nao watapiga mbio mbele ya magari yake. 12 Naye atawaweka kwake kuwa maakida juu ya elfu, na maakida juu ya hamsini; na wengine atawaweka walime shamba lake, na kuvuna mavuno yake, na kufanyiza zana zake za vita, na vyombo vya magari yake. 13 Na binti zenu atawatwaa kuwa wafanyaji wa marhamu, na wapishi, na waokaji.

 

Wazo shirikishi: Wahatawatafuta farasi wako; hawataitafuta nchi yako; hawatakuwa wanapura nafaka zako; bali watakuwa wanaifanya kazi ya mfalme; watakuwa wanavuna mazao yake. Hawatakuwa wanatengeneza vitu dhaifu jikoni kwako; bali watazitengeneza jikoni kwa mfalme.

 

14 Atatwaa makonde yenu, na mashamba yenu ya mizabibu, na ya mizeituni, yale yaliyo mazuri sana, ili awape watumishi wake. 15 Naye atawatoza ushuru wa mbegu zenu na wa mizabibu yenu, awape maakida wake, na watumishi Wake.

 

Wazo shirikishi: Zaka yako haiendi hekaluni mwako sasa, bali inakwenda kwenye shughuli za kimaongozi za ofisi ya mfalme, na hatimaye ataitumia kwa malengo yake mwenyewe.

16 Atawatwaa watumishi wenu na wajakazi wenu, na ng'ombe zenu walio wazuri sana, na punda zenu, naye atawatia katika kazi zake mwenyewe. 17 Atawatoza fungu la kumi la makundi yenu; nanyi mtakuwa watumwa wake. 18 Nanyi mtalia siku ile kwa sababu ya mfalme wenu mliyejichagulia; Bwana asiwajibu siku ile. 19 Walakini hao watu wakakataa kuisikiliza sauti ya Samweli; wakasema, Sivyo hivyo; lakini tunataka kuwa na mfalme juu yetu; 20 ili sisi nasi tufanane na mataifa yote; tena ili mfalme wetu atuamue, tena atoke mbele yetu na kutupigia vita vyetu. \

 

Wazo shirikishi: Walimhitaji atokee mtu fulani kwao aliye kama Wafilisti; mtu fulani mkubwa na shujaa; mrefu kwa kimo na mabega yake zaidi ya wote, ambaye wangemkubali na kusema ‘wewe jitokeze na upiganenaye kwa pigo moja tu na kummaliza’, kwa kuwa nyakati hizo vita ilikuwa inaamuliwa na mtu mmoja tu mwenye nguvu. Ka hiyo, majeshi yaliwaacha mashujaa wapigane na kwa jinsi hivyo iliepusha watu wengi wasife. Walihitaji mfalme ambaye atawatangulia mbele mapiganoni kuwapigania na ndipo wangejua kile walichokuwa wanakifanya.

 

21 Samweli akayasikia maneno yote ya watu, akayanena masikioni mwa Bwana. 22 Bwana akamwambia Samweli, Isikilize sauti yao, ukawafanyie mfalme. Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, Enendeni kila mtu mjini kwake.

 

Kile anachokitenda Bwana hapa ni kwanza kabisa kuwekeza mioyoni mwa Israeli jinsi anavyofanya mfalme anayetokana na mfumo mbaya wa kiroho na jinsi alivyo. Anasema, ‘hivi ndivyo mfalme asiye na chembe yoyote ya maongozi ya Roho Mtakatifu atakavyofanya. Hiki ndicho mtakachokwenda kukabiliwa nacho’. Kwa namna hiyohiyo kwamba aliwaweka waamuzi na utaratibu uliokuwa chini ya manabii walioishi kabla ya wakati huo. Mchakato huu ulionyesha udhaifu wa mfumo wa wa kiserikali. Kwa hiyo aliuendeleza mfumo na utaratibu huo kwa kupitia Daudi na Masihi.

 

Ililazimu Israeli waende utumwani na wapate kutenganishwa na Yuda; kwa hiyo Masihi alitokea katika Yuda kipindi cha utawala au kongwa za Warumi katika karne ya kwanza ili kwamba Kanisa ndipo lianzishwe kama awamu ya mwisho. Kwa hiyo, kwanza kabisa alianzisha ufalme huu katika Benyamini na ufalme ungeweza kubakia katika Benyamini kwa kuwa sehemu ya Benyamini walibakia ndani ya Yuda. Waliuondoa kutoka Benyamini hadi Yuda.

 

Mungu alimpeleka Sauli kwa Samweli.

1Samweli 9:15-21 Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema, 16 Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe mtie mafuta ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia.

 

Walikuwa chini ya kongwa na walikuwa wanamlilia Bwana na ndiyo maana alitenda hivyo, kwa kuwa walikuwa wamemrudia Bwana.

17 Hata Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, Huyu ndiye niliyekuambia habari zake; huyu ndiye atakayewamiliki watu wangu. 18 Ndipo Sauli akamkaribia Samweli langoni, akasema, Tafadhali, uniambie, nyumba ya mwonaji iko wapi? 19 Samweli akamjibu Sauli, akasema, Mimi ndimi mwonaji; tangulia mbele yangu ukwee mpaka mahali pa juu, kwa maana mtakula pamoja nami leo; kisha, asubuhi nitakuacha uende zako, nami nitakuambia yote uliyo nayo moyoni mwako. 20 Na wale punda zako waliopotea siku hizi tatu, usijiudhi kwa ajili yao; maana wameonekana. Na yote yaliyotamanika katika Israeli amewekewa nani? Si wewe, na nyumba yote ya baba yako? 21 Basi Sauli akajibu, akasema, Je! Mimi si Mbenyamini, mtu wa kabila iliyo ndogo kuliko kabila zote za Israeli? Na jamaa yangu nayo si ndogo kuliko jamaa zote za kabila ya Benyamini? Kwa nini basi, kuniambia hivyo?

 

Mungu aliamua kumuinua mfalme kutoka kwenye ukoo mdogo na duni kuliko yote, wa kabila dogo kuliko yote katika Israeli. Sauli alitunukiwa na kutukuka ila hakujua ni kwa nini na alishangaa kwa nini alikuwa ameheshimiwa na kutunukiwa kiasi hicho.

1Samweli 10:1-12 Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake. 2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu? 3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai; 4 nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao. 5 Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri; 6 na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe utageuzwa kuwa mtu mwingine. 7 Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, fanya kama uonavyo vema; kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe. 8 Nawe utatelemka mbele yangu mpaka Gilgali; nami, angalia, nitakutelemkia huko, ili kutoa sadaka za kuteketezwa, na kuchinja sadaka za amani; siku saba utangoja, hata nitakapokujia, na kukuonyesha yatakayokupasa kuyafanya.

 

Kwa hiyo ilimazimu angojee kwa siku saba zaidi. Kuna maana ashiria ya mchakato huu wote wa ukaribisho kwenye andiko hili. Unatafuta dhabihu na mkate na kitu cha kumpa mfalme kwa mujibu saa na maagizo ya torati. Sasa Biblia inasema kwamba kila mtu atakayekuwa mtawala wa Israeli ni kutunza rekodi za maandiko yote yaliyo kwenye torati ili kwamba anapotawazwa kuwa mfalme asiipotoshe sharia. Kila mfalme yampasa awe na nakala yake ya torati ili imwandae kuwaongoza Israeli. Huu ni wajibu wa kila kiongozi wa watu – kujiandaa nafsi yake kwa kujisomea torati. Mkururu uliopo hapa ni kwamba Sauli alipewa mikate miwili na manabii. Jambo hili linaashiria kutolewa kwa torati na kutolewa kwa uweza wa kuielewa Biblia kwa Sauli akiwa kama mfalme. Roho ya torati au sheria, ndipo ikamshukia mfalme ili kukamilisha wajibu wake akiwa kama kiongozi. Hii ilikuwa ni kuonyesha kuwa chini ya utawala wa kifalme, uongozi na Roho Mtakatifu atawekwa juu ya mfalme, kama ilivyokuwa hatimaye kwa Daudi. Sasa ilimpasa angoje kwa siku saba, na siku hizi saba zilishuhudia vitisho vikubwa.

9 Ikawa, alipogeuka kumwacha Samweli, Mungu akambadilisha moyo; nazo ishara zile zote zikatukia siku ile ile. 10 Basi, walipofika Gibea, tazama, kikosi cha manabii wakakutana naye; kisha roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu, naye akatabiri kati yao. 11 Ikawa, wote waliomjua zamani walipoliona jambo hilo, kwamba, tazama, huyo anatabiri pamoja na manabii, ndipo watu wakasemezana, Ni nini hilo lililompata mwana wa Kishi? Je! Sauli pia yumo miongoni mwa manabii? 12 Naye akajibu mtu mmoja wa mahali hapo, akasema, Na baba yao n'nani? Kwa hiyo ikawa mithali, Je! Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?

 

Kile wanachokisema ni kwamba ‘Ni roho gani waliyenaye?’

 

Samweli aliwaita watu wakusanyike pamoja huko Mispa na akawaelezea maana ya kuwa na mfalme na majukumu yake kwa watu.

1Samweli 10:17-27 wana huko Mispa 18 akawaambia wana wa Israeli, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Naliwatoa Israeli kutoka Misri, nami naliwaokoa ninyi na mikono ya Wamisri, na ya falme zote zilizowaonea; 19 lakini leo mmemkataa Mungu wenu, naye ndiye awaponyaye katika misiba yenu yote na shida zenu; nanyi mmemwambia, Sivyo, lakini weka mfalme juu yetu. Basi, sasa, hudhurieni mbele za Bwana, kwa kabila zenu na kwa elfu zenu. 20 Basi Samweli akawaleta kabila zote za Israeli karibu; na kabila ya Benyamini ikatwaliwa. 21 Kisha akaileta kabila ya Benyamini karibu, kwa jamaa zao; jamaa ya Wamatri ikatwaliwa. Akaileta jamaa ya Wamatri karibu, mtu baada ya mtu; kisha Sauli, mwana wa Kishi, akatwaliwa; lakini walipomtafuta hakuonekana. 22 Basi wakazidi kumwuliza Bwana, Amebaki mtu asiyekuja huku bado? Naye Bwana akajibu, Tazama, amejificha penye mizigo. 23 Basi wakaenda mbio wakamleta kutoka huko; naye aliposimama kati ya watu, alikuwa mrefu kuliko watu wote, tangu mabega yake kwenda juu. 24 Samweli akawaambia watu wote, Mnamwona mtu huyu aliyechaguliwa na Bwana, ya kuwa hakuna mtu mfano wake katika watu wote. Ndipo watu wote wakapiga kelele, wakasema, Mfalme na aishi! 25 Kisha Samweli aliwaambia watu madaraka ya ufalme, akayaandika katika kitabu, akakiweka mbele za Bwana. Samweli akawaruhusu watu wote, waende kila mtu nyumbani kwake. 26 Sauli naye akaenda nyumbani kwake huko Gibea; na pamoja naye wakaenda kikosi cha watu, ambao Mungu alikuwa ameigusa mioyo yao. 27 Walakini wengine wasiofaa kitu wakasema, Huyu je! Atatuokoaje? Nao wakamdharau, wasimletee zawadi.

 

Ni wazi sana kabisa, kwenye andiko hili, walikuwa wanabahatisha kifikra za kama wanaopiga kura ili kuamua ni kwenye familia ipi ambayo mfalme huyu atatokea. Hawakumkuta Sauli, kwa hiyo Bwana aliwaambia mahali watakapomtafuta. Ni wazi sana kuwa aliogopa. Haukuwa ni mwanzo mzuri au wenye kutia moyo na bahati sana wakati mfalme anapokutwa amejificha, ingawaje alikwishaambiwa kuwa unakwenda kuwa mfalme.

 

Mungu alikuwa amewaandaa watu pamoja na Sauli. Hii imeonyeshwa kama ishara ya kuwagusa mioyo yao. Sauli alijaribu kujiepusha na majukumu yake hapo kwanza. Mungu alikua amewapa Israeli mfalme ambaye alionekana kuwa ni stahili au sahihi kwao na mwenye umbo lisilo la kawaida kwa mwonekano wan je, hata hivyo, Mungu alijua atakachokwenda kukifanya kutoka moyoni. Mrithi wake aliyechukua nafasi yake alikuwa ni wa tofauti naye sana. Hata hivyo, Mungu aliamfanya Sauli kuwa mfalme. Wakati Samweli alipikuwa mzee aliwaelezea Israeli majukumu yao wanayowajibika kumfanyia mfalme.

1Samweli 12:13-25  Basi sasa, mtazameni mfalme mliyemchagua na kumtaka; tazameni, Bwana ameweka mfalme juu yenu. 14 Kama mkimcha Bwana, na kumtumikia, na kuisikia sauti yake, msiiasi amri ya Bwana, tena kama ninyi, na mfalme anayewatawala, mkimfuata Bwana, Mungu wenu, vema! 15 Bali msipoisikia sauti ya Bwana, mkiiasi amri ya Bwana, ndipo mkono wa Bwana utakuwa juu yenu, kama ulivyokuwa juu ya baba zenu. 16 Na sasa simameni, mkalione jambo hili kubwa, Bwana atakalolitenda mbele ya macho yenu. 17 Leo je! Si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana, kwamba apeleke ngurumo na mvua; nanyi mtajua na kuona ya kuwa uovu wenu ni mwingi sana, mlioufanya machoni pa Bwana, kwa kujitakia mfalme. 18 Basi Samweli akamwomba Bwana, naye Bwana akapeleka ngurumo na mvua siku ile; nao watu wote wakamwogopa Bwana sana, na Samweli pia. 19 Watu wote wakamwambia Samweli, Utuombee sisi watumwa wako kwa Bwana, Mungu wako, tusije tukafa; maana tumeongeza dhambi zetu zote kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme. 20 Samweli akawaambia, Msiogope; ni kweli mmeutenda uovu huu wote; lakini msigeuke na kuacha kumfuata Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa mioyo yenu yote. 21 Wala msigeuke upande, maana, kufuata vitu vya ubatili, 22 visivyoweza kusaidia wala kuokoa, kwa kuwa havifai kitu. Maana Bwana hatawaacha watu wake kwa ajili ya jina lake kuu; kwa kuwa imempendeza Bwana kuwafanya ninyi kuwa watu wake mwenyewe. 23 Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka 24 Mcheni Bwana tu, mkamtumikie kwa kweli kwa mioyo yenu yote; maana, kumbukeni jinsi alivyowatendea mambo makuu. 25 Lakini kama mkiendelea kutenda mabaya, mtaangamia, ninyi na mfalme wenu pia.

 

Dhumuni la andiko hili ni kuwaonyesha watu kwamba wanawajibika kwa Mungu na kwamba kama mfalme ataviandama vinyago au sanamu na dini ya uwongo, ndipo hakutakuwa na namna nyingine ya kumfanya mtu yeyote ajitoe na kumfuata Mungu kikamilifu. Wawakuruhusiwa kumfuata kiongozi wa haiba au aina yoyote ambaye hamtafuti au kumfuata Mungu wao. Hilo ni wazi. Imeonyeshwa wazi hapa kwamba kama wanafanya maovu makubwa kihivyo, ndipo pande zote mbili, yaani, wao pamoja na mfalme wataangamizwa kama atakavyofanyiwa mfalme. Lakini kila mmoja ana wajibu wa moja kwa moja kwa Mungu na hilo ndilo lengo la andiko hili. Inaonyesha kwa wazi sana kwamba hakuna mtu aliyeondolewa kwenye wajibu huu kwa Mungu. Kwa mtu yeyote anayemsimamia au kumtunza yeye.

 

Sauli alikuwa amepewa majukumu maalumu na pia maelekezo kwa kupitia nabii. Uasi wake ulipelekea kuugharimu hata ufalme wake. Suala hili la kunpokonywa lilijumuishwa kwenye dhabihu aliyoitoa huko Mikimashi halieleweki vyema sana.

1Samweli 13:1-15 Sauli alikuwa na umri wa miaka kadha wa kadha hapo alipoanza kutawala;naye akatawala miaka kadha wa kadha juu ya Israeli. 2 Naye Sauli alijichagulia watu elfu tatu wa Israeli; ambao katika hao, elfu mbili walikuwa pamoja na Sauli katika Mikmashi, na katika mlima wa Betheli na elfu moja pamoja na Yonathani katika Gibea ya Benyamini; nao wale watu waliosalia akawaruhusu waende kila mtu hemani kwake. 3 Yonathani akaipiga hiyo ngome ya Wafilisti, iliyokuwako huko Gibea, nao Wafilisti wakapata habari. Naye Sauli akapiga tarumbeta katika nchi yote, huku akisema, Na wasikie Waebrania. 4 Waisraeli wote wakasikia habari ya kwamba Sauli ameipiga hiyo ngome ya Wafilisti, na ya kwamba Waisraeli wamepata kuwa makuruhi kwa Wafilisti. Basi hao watu wakakusanyika pamoja kumfuata Sauli huko Gilgali. 5 Nao Wafilisti wakakusanyana ili wapigane na Waisraeli, magari thelathini elfu, na wapanda farasi sita elfu, na watu kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi wao; wakapanda juu, wakapiga kambi yao katika Mikmashi, upande wa mashariki wa Beth-aveni. 6 Hata Waisraeli walipoona ya kuwa wa katika dhiki, (maana watu walifadhaishwa), ndipo hao watu wakajificha katika mapango, na katika vichaka, na katika miamba, na katika mashimo, na katika mabirika. 7 Hata baadhi ya Waebrania walivuka Yordani, wakaingia nchi ya Gadi na Gileadi; lakini Sauli alikuwa akaliko huko Gilgali, nao watu wote wakamfuata wakitetemeka.

 

Jeshi hili kubwa liliwatokea kinyume chao. Wafilisti waligundua kwamba walipaswa kushughulikia tishio hili, kwa kuwa Israeli walijiunga na kujikusanya chini ya mfalme na hilo lilikuwa na umuhimu mkubwa sana kwa maangamizo ya Wafilisti, kuliko hata walivyoamini Waisraeli hapo kwanza. Walikuwa ni kundi lililotawanyika la makabila hadi wakati huu. Wakiwa pamoja na mfalme walijipanga wenyewe kupigana na Wafilisti na mabwana wao.

8 Akangoja siku saba, kwa kadiri ya muhula uliowekwa na Samweli lakini Samweli hakuja Gilgali; na hao watu wakatawanyika mbali naye. 9 Sauli akasema, Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Akaitoa sadaka ya kuteketezwa. 10 Hata mara alipokwisha kuitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, kumbe! Samweli akatokea. Naye Sauli akatoka kwenda kumlaki na kumsalimu. 11 Samweli akasema, Umefanya nini? Naye Sauli akasema, Ni kwa sababu naliona ya kuwa watu wanatawanyika mbali nami, na wewe hukuja siku zile zilizonenwa; nao Wafilisti wamekusanyika pamoja huko Mikmashi; 12 basi nikasema, Wafilisti watanishukia sasa mpaka Gilgali, kabla sijaomba fadhili za Bwana; kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya kuteketezwa. 13 Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya Bwana, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana Bwana angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele. 14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amejitafutia mtu aupendezaye moyo wake, naye Bwana amemwamuru yeye kuwa mkuu juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika neno lile Bwana alilokuamuru. 15 Basi Samweli akaondoka, akapanda kutoka Gilgali mpaka Gibea ya Benyamini. Naye Sauli akawahesabu watu waliokuwapo pamoja naye, wapata kama mia sita.

 

Vita ilikuwa imepangwa na kukabiria. Samweli alikuwa amesema kwamba atakuja kwa wakati muafaka. Sauli alidhani kwamba alikuwa amechelewa kufika. Kwa hiyo, kwa kujua kinachotakiwa kufanywa, ndipo akaamua achukue jukumu lisilomhusu yasiyo yake ya nabii. Samweli alikuwa hajaacha bado jukumu la kuwaamua Israeli, kwa hiyo, majukumu yalikuwa hayajatolewa yote na kupewa mfalme. Samweli bado alikuwa anaifanya kazi na majukumu ya nabii. Kile kilichotokea kwa kweli ni kwamba Samweli alikuwa amechelewa. Sauli alikosea amekosea kuhesabu kipimo cha wakati. Huu ndiyo uhusiano wa nyakati za mwisho na ujio wa Masihi, wakati wanaposema ‘Bwana wangu amechelewa kuja kwake’. Inaonyesha pia umuhimu kuwa na dalili ya utii kwenye mamlaka ya kisheria ya Mungu kupitia nabii wake. Jinsi ya kuwajua manabii wa Mungu ni kuwapima kama wananena sawasawa na sharia au torati na ushuhuda (Isaya 8:20). Kama hawaneni sawasawa na sharia au torati na ushuhuda, hakuna nuru ndani yao, au kwao hakuna mapambazuko; hakuna nyota ya mchana; na wala hakuna nyota ya asubuhi. Ufalme wa Sauli uliondolewa kwa sababu hakumtii mtangulizi wake aliyemtia mafuta. Aliondolewa na Mungu alimuweka mwingine. Kwa suala hili ilifanywa kwa kupitia nabii yuleyule ambaye alikuwa hajafa bado.

 

Hadithi hii inaonyesha jinsi Sauli alivyotenda dhambi pia kwa kuyahesabu majeshi ya Mungu aliyehai. Daudi pia alitenda dhambi hii hii. Kwa sababu ya dhambi ya Daudi, watu 70,000 walikufa. Jambo hili linashabihiana pia na nyakati za mwisho. Kitendo cha kuhesabu siku hizi saba kinashabihiana na kipindi maalumu fulani. Sauli alianza kuhesabu siku ya mapema zaidi. Alihesabu sehemu ya siku. Kwa hiyo, alikuja kwenye siku ambayo Samweli alipasa awepo hapo na Samweli hakuwepo, kwakuwa alikuwa siku moja zaidi ya mapema yake. Alifika siku ya sita badala ya siku ya saba. Hiki ni kitu fulani ambacho watu yatupasa kukijua na kukitia akilini.

 

Mungu alipeleka maelekezo mengine kwa Sauli kwa kupitia Samweli kushabihiana na Waamaleki, maelekezo ambayo yalikuwa ni ya muhimu sana baadae na pia kama tutakavyoona pia kutoka kwenye Kitabu cha Esta.

1Samweli 15:1-23  Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana. 2 Bwana wa majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri. 3 Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda. 4 Ndipo Sauli akawaita watu, akawahesabu huko Telemu, askari waliopanda farasi mia mbili elfu, na watu wa Yuda kumi elfu. 5 Sauli akaufikilia mji wa Amaleki, akauvizia bondeni. 6 Sauli akawaambia Wakeni, Haya! Enendeni zenu, mkashuke ili kujitenga na Waamaleki, nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao; maana mliwatendea wana wa Israeli mema, walipopanda kutoka Misri. Basi hao Wakeni wakaondoka, wakajitenga na Waamaleki. 7 Sauli akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri, unaokabili Misri. 8 Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai, akawaangamiza hao watu wote kwa upanga. 9 Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo walio wazuri, na ng'ombe, na vinono, na wana-kondoo, na cho chote kilicho chema, wala hawakukubali kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa. 10 Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema, 11 Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha. 12 Samweli akaondoka asubuhi na mapema ili aonane na Sauli; Samweli akaambiwa ya kwamba, Sauli alifika Karmeli, na tazama, akajisimamishia ukumbusho, akageuka, akapita, akatelemkia Gilgali. 13 Samweli akamwendea Sauli; naye Sauli akamwambia, Ubarikiwe na Bwana, nimeitimiza amri ya Bwana. 14 Samweli akasema, Maana yake nini, basi, hiki kilio cha kondoo masikioni mwangu, na huu mlio wa ng'ombe ninaousikia? 15 Sauli akasema, Wamewaleta kutoka kwa Waamaleki; maana watu waliwaacha hai kondoo na ng'ombe walio wazuri, ili wawatoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, nao waliosalia tumewaangamiza kabisa. 16 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Ngoja, nami nitakuambia neno aliloniambia Bwana usiku huu. Naye akamwambia, Haya, sema. 17 Basi Samweli akasema, Ingawa ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa kuwa kichwa cha kabila za Israeli? Naye Bwana akakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli.18 Kisha Bwana akakutuma safarini, akasema, Enenda ukawaangamize kabisa wale Waamaleki wenye dhambi, upigane nao hata watakapoangamia. 19 Mbona, basi, hukuitii sauti ya Bwana, bali ukazirukia nyara ukafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana? 20 Sauli akamwambia Samweli, Hakika mimi nimeitii sauti ya Bwana, nami nimemleta Agagi, mfalme wa Waamaleki, tena nimewaangamiza Waamaleki kabisa. 21 Ila watu waliteka nyara, kondoo na ng'ombe walio wazuri, katika vitu vilivyowekwa wakfu, kusudi wavitoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, huko Gilgali. 22 Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu. 23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.  

 

Sababu yao fikirika ilikuwa ni kwamba kama walichukua kondoo hizi zote kutoka kwa Wamaleki wasingepaswa kuchukua asilimia kumi ya mifugo yao. Torati ilisema wazi sana kwamba mlichukua mateka au nyara zisizofaa na mlitoa zaka juu yake pia, na mliwapa watu. Lakini hakikuwa ndicho Mungu alichowaambia wakifanye. Wakuhitaji ng’ombe wala mifugo ya Waameleki. Hatujui ni nini hasa ilikuwa sababu yake ilikuwa nini. Huenda walikuwa ameathirika kwa magonjwa na huenda wangesababisha maambukizo ya magonjwa kwenye mifugo ya wana wa Israeli. Huenda wangekubalika tu kwa shughuli za utoaji dhabihu tu peke yake. Hatujui na hatujaambiwa lolote. Bali alipenda kila kitu kiangamizwe na alipenda Agagi wa Waamaleki auawe pia, ka kuwa Waagagi, wana wa Agagi, walikuwa hatimaye ndio kitisho cha kuwepo kwa jamii ya Wayahudi.

 

Fundisho lililoko hapa ni kwamba ufalme a wateule umetabiriwa kuwa ni waaminifu na watiifu. Kama unapenda uwe ni mmoja wa wafalme wa nyakati za mwisho, iwapo kama unapenda uwe mfalme na kuhani, basi yakupasa uwe mtii. Mfumo wote mzima unahitaji watu watiifu. Mungu hapendi kuonyesha kiburi; bali anawahitaji watiifu na anaataka watu watakaofanya kazi. Kiti cha enzi cha ufalme wa Israeli kilichukuliwa na Masihi kwa ajili ya utiifu wake (Wafilipi 2:6). Kristo hakujaribu wala kudai kuwa anausawa wowote na Mungu, bali alikuwa mtii hadi kufa. Wateule wamepewa sheria naushuhuda ili kuupima utiifu wao kwenye amri za Mungu, hadi kufa kwao, na wanauawa kwa ajili ya kuzishika kwao amri hizi za torati, hasa amri ya kwanza, ya pili na ya tatu, kabla ya amri ya nne.

 

Kitu cha muhimu hapa ni kwamba utii ambao Mungu aliuhitaji ni ule wenye matokeo ya muda mrefu. Watu waliambiwa kuwaangamiza hata watoto, hata watoto wachanga wa Waamaleki. Hawa wote walibidi kuuawa. Hili ni andiko la ajabu na lisilo la kawaida. Watu wangesema ‘ni kwa sababu gani Mungu alifanya hivyo?’ Amri yenyewe ilikuwa ni ya namna gani. Waamaleki angeweza kuwa tishio na kuwaangamiza Yuda katika siku za baadae. Mtu wa uzao wa Hagagi, Hamani, ndiye alikuwa adui mkubwa kwenye Kitabu cha Esta (soma jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Esta (Na. 63)). Tisho hili kwa usalama wa Israeli linahusiana pia na nyakati za Mwisho. Sehemu hii inataja kuhusu ufalme wa Masihi kama tunavyoona kutoka kwenye mwendelezo wa andiko hili.

1Samweli 15:24-29  Ndipo Sauli akamwambia Samweli, Nimefanya dhambi; maana nimeihalifu amri ya Bwana, pia na maneno yako; kwa sababu naliwaogopa wale watu, nikaitii sauti yao. 25 Basi sasa, nakuomba, unisamehe dhambi yangu; rudi pamoja nami, nipate kumwabudu Bwana. 26 Samweli akasema, Sitarudi pamoja nawe; kwa sababu umelikataa neno la Bwana, Bwana naye amekukataa wewe, usiwe mfalme wa Israeli. 27 Naye Samweli alipogeuka, aende zake, Sauli akaushika upindo wa vazi lake, nalo likararuka. 28 Basi Samweli akamwambia, Leo Bwana amekurarulia ufalme wa Israeli, naye amempa jirani yako, aliye mwema kuliko wewe. 29 Tena Yeye aliye Nguvu za Israeli hatanena uongo, wala hataona majuto; maana siye mwanadamu, hata ajute.

 

Ndivyo ilivyo, kwamba usimikaji na utiaji mafuta wa kiongozi wa watu wa Mungu utegemee na utii wake kwa Mungu. Kiongozi yeyote wa watu wa Mungu asiye mwaminifu na mtiifu kwenye torati ama sheria za Mungu, anapungua vigezo vya kufanya astahili kuwa na uhalali wa kutawala. Hili ndilo somo hasa linalotokana na andiko hili. Samweli alimuua Agagi kwa mikono yake mwenyewe na kisha alikata maasiliano yake na Sauli siku ya kufa kwake (1Samweli 15:35) lakini hakuacha kumuombolezea wala kuomba. Ndivyo itupasavyo hata sisi pia. Hatupaswi kuacha kuwaombolezea au kuaombea viongozi wa watu wetu hata kama watakuwa watenda dhambi.

 

Kisha Mungu akamwambia Samweli amtie mafuta Daudi. Ndipo na sisi tunakwenda kumsimika kwa kumweka mbadala mfalme.

1Samweli 16:1-7 Bwana akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe. 2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi Bwana akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea Bwana dhabihu. 3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako. 4 Samweli akafanya hayo aliyosema Bwana, akaenda Bethlehemu. Wakaja wazee wa mji kumlaki, wakitetemeka, nao wakasema, Je! Umekuja kwa amani? 5 Naye akasema, Naam, kwa amani; nimekuja kumtolea Bwana dhabihu; jitakaseni; njoni pamoja nami kwenye dhabihu. Akawatakasa Yese na wanawe, akawaita kwenye dhabihu. 6 Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake. 7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo.

 

Sauli alikuwa mrefu sana kiasi kwamba kichwa chake na mabega yake viliwazidi Israeli wote, lakini Sauli alikuwa muovu. Hivyo Mungu aliuona moyo na alijua kile kilichotakiwa kifanyike.

1Samweli 16:10-23 Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa. 11 Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku. 12 Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza. Bwana akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye. 13 Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama. 14 Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua. 15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua. 16 Basi bwana wetu na atuamuru sisi watumishi wake waliopo hapa mbele yako watafute mtu aliye stadi wa kupiga kinubi; basi itakuwa, roho ile mbaya kutoka kwa Mungu itakapokujilia, yeye atapiga kinubi kwa mkono wake, nawe utapona. 17 Basi Sauli akawaambia, Vema, nitafutieni mtu aliye stadi wa kupiga kinubi, mkaniletee. 18 Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, aliye stadi wa kupiga kinubi, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye Bwana yu pamoja naye. 19 Basi Sauli akampelekea Yese wajumbe, akasema, Nipelekee Daudi mwanao, aliye pamoja na kondoo. 20 Yese akatwaa punda, wa kuchukua mikate, na kiriba cha divai, na mwana-mbuzi, akampelekea Sauli kwa mkono wa Daudi mwanawe. 21 Basi Daudi akamwendea Sauli, akasimama mbele yake, naye akampenda sana; naye akapata kuwa mtu wa kumchukulia silaha zake. 22 Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, mwache Daudi asimame mbele yangu; maana ameona kibali machoni pangu. 23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha.

 

Daudi alikuwa na uweza au nguvu juu ya mapepo katika Roho Mtakatifu, na kwa jinsi hiyohiyo sisi tunayo nguvu pia dhidi ya mapepo kwa Roho Mtakatifu. Huu ndiyo ulikuwa ujumbe uliokusudiwa kwenye andiko hili.

 

Daudi alitiwa mafuta awe mrithi stahiki na akawekwa kwenye nyua za nyumba ya mfalme kwenye nafasi au daraja la chini sana ili kwamba aweze kujifunza mbinu za vita na za amani. Alikuwa amepewa Roho wa Bwana ili kwamba aweze kuyafanya mambo makuu zaidi. Na ndipo Daudi alifanywa kuwa kiongozi wa watu katika Israeli kwa mazingira yasiyo ya kawaida.

1Samweli 17:1-11 Wakati huo Wafilisti walikusanya majeshi yao kwa vita, nao wakakusanyika huko Soko, ulio mji wa Yuda, wakatua kati ya Soko na Azeka, katika Efes-damimu. 2 Naye Sauli na watu wa Israeli wakakusanyika, wakatua katika bonde la Ela, nao wakapanga vita juu ya hao Wafilisti. 3 Wafilisti wakasimama juu ya mlima upande huu, na Waisraeli wakasimama juu ya mlima upande huu, napo palikuwa na hilo bonde katikati. 4 Ndipo akatoka shujaa katika kambi ya Wafilisti, aliyeitwa Goliathi, wa Gathi, ambaye urefu wake ulikuwa mikono sita na shibiri moja. 5 Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani, tena amevaa darii ya shaba; na uzani wake ile darii ya shaba ulikuwa shekeli elfu tano za shaba. 6 Tena amevaa mabamba ya shaba miguuni mwake, naye alikuwa na mkuki wa shaba kati ya mabega; yake. 7 Na mti wa fumo lake ulikuwa kama mti wa mfumaji; na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma uzito wake; na mtu aliyemchukulia ngao yake akamtangulia. 8 Naye akasimama, akawapigia kelele majeshi ya Israeli akawaambia, Mbona mmetoka kupanga vita? Je! Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Jichagulieni mtu, akanishukie mimi. 9 Kama akiweza kupigana nami na kuniua, sisi tutakuwa watumwa wenu; nami nikimshinda yeye na kumwua, ninyi mtakuwa watumwa wetu, na kututumikia. 10 Yule Mfilisti akasema, Nayatukana leo majeshi ya Israeli; nipeni mtu tupigane. 11 Basi Sauli na Israeli wote waliposikia maneno hayo ya Mfilisti, wakafadhaika na kuogopa sana.

 

Mtu huyu alikuwa na urefu wa takriban futi kumi kenda juu kwake, mwenye silaha za kutisha. Ni vigumu sana kusimama mbele ya silaha zinazoendeleza aina ile ya mtindo wa nguvu wakati zinaporushwa na kulengwa wewe. Walitiwa hofu. Mfano ashiria wa Goliathi wa Gathi ni kama mfumo au aina ya sanamu ya nembo ya kidola ya dola ya Babeli paoja na warithi wake waliofuatia baadae walioonyeshwa kwenye sanamu ya Danieli Sura ya 2. Huu ni mfano mwingine wa mnyama menye nguvu mwenye kichwa kikubwa. Imani ile inahusu na mkururu wa dola nyingi na kuangamizwa na Masihi kwenye hatua zake za mwisho za dola ya wafalme kumi wa nyakati za mwisho, wakati wa lile jiwe ambalo ni Masihi litakapozipiga kwenye miguu yake. Hiyo ni Danieli sura ya 2. Kwenye tukio hili, Goliathi hapigwi miguuni. Bali anapigwa sawia katikati ya macho yake, ni sawia kwenye paji lake la uso, mahali ambapo mihuri ya imani inapigwa. Goliath anahusika na imani za kidini na kwamba kichwa kinabakia kuwa ni kitu cha msingi cha hadithi hii. Hadithi hii inaendelea hadi kwenye andiko la 1Samweli 17:12 kana kwamba Daudi hakuwahi kuwa pamoja na Sauli na kwa kweli hadithi yenyewe inaweza kushabihiana na mchakato usiohusiana. Una mkururu mmoja wakati unapoanzisha jinsi roho alipochukuliwa kutoka kwa Sauli na kupewa Daudi. Wakati Daudi alipompokea, alichukuliwa kutoka kwa Sauli na Sauli akateseka, na Daudi ndipo akafanyika kuwa mwenye nguvu nab ado alipewa jukumu la kuwa ni mchukua silaha wa Sauli. Alifanyika kuwa mtu wa mkono wa kuume wake. Mkururu huu unaendelea.

 

Daudi alikuja kwenye uwanja wa vita ili kutoa efa ya mahindi na mikate kumi kwa ndugu zake.

1Samweli 17:17-54 Ndipo Yese akamwambia Daudi mwanawe, Haya! Sasa uwachukulie ndugu zako efa ya bisi, na mikate hii kumi, ipeleke upesi kambini kwa ndugu zako; 18 ukampelekee akida wa elfu yao jibini hizi kumi, ukawaangalie, wa hali gani, kisha uniletee jawabu yao. 19 Basi Sauli, na watu wote wa Israeli, walikuwa katika bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti. 20 Daudi akaondoka asubuhi na mapema, akawaacha kondoo pamoja na mchungaji, akavitwaa vitu vile, akaenda, kama Yese alivyomwamuru; akafika penye magari, wakati lile jeshi walipokuwa wakitoka kwenda kupigana, wakipiga kelele za vita. 21 Nao Waisraeli na Wafilisti wakajipanga, jeshi hili likikabili jeshi hili. 22 Basi Daudi akaviacha vile vyombo vyake katika mkono wa mlinda vyombo, akalikimbilia jeshi, akafika, akawasalimu ndugu zake. 23 Hata alipokuwa akisema nao, kumbe! Yule shujaa alitokea, yule Mfilisti wa Gathi, jina lake Goliathi, akitoka katika jeshi la Wafilisti, akasema maneno yale yale; naye Daudi akayasikia. 24 Na watu wote wa Israeli walipomwona yule mtu wakakimbia, wakaogopa sana. 25 Watu wa Israeli wakasema, Je! Mmemwona mtu huyu aliyepanda huko? Hakika ametokea ili awatukane Israeli; basi, itakuwa, mtu yule atakayemwua, mfalme atamtajirisha kwa utajiri mwingi, naye atamwoza binti yake, na kuifanya mbari ya baba yake kuwa huru katika Israeli. 26 Daudi akaongea na watu waliosimama karibu, akisema, Je! Atafanyiwaje yeye atakayemwua Mfilisti huyo, na kuwaondolea Israeli aibu hii? Maana Mfilisti huyu asiyetahiriwa ni nani hata awatukane majeshi ya Mungu aliye hai? 27 Nao watu wakamjibu vivyo hivyo, wakisema, Ndivyo atakavyofanyiwa mtu yule atakayemwua. 28 Naye Eliabu, mkubwa wake, alisikia hapo alipoongea na watu; na hasira yake Eliabu ikawaka juu ya Daudi, akasema, Mbona wewe umeshuka hapa? Na kondoo wale wachache umemwachia nani kule nyikani? Mimi nakujua kiburi chako, na ubaya wa moyo wako; maana umeshuka ili upate kuvitazama vita. 29 Naye Daudi akamjibu, Je! Mimi nimekosa nini sasa? Je! Si neno kubwa hilo? 30 Naye akamgeukia ili kumwelekea mtu mwingine, akasema naye jinsi ile ile; na watu wakamjibu tena jinsi ile ile kama ya kwanza. 31 Na maneno hayo aliyosema Daudi yaliposikiwa, watu wakamweleza Sauli; naye akatuma mtu kwenda kumwita. 32 Daudi akamwambia Sauli, Asizimie moyo mtu ye yote kwa ajili ya huyu; mimi mtumishi wako nitakwenda kupigana na Mfilisti huyu.

 

Daudi alikuwa na akili sana na Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye na aliona madhara au kitisho cha huyu jitu alichokuwanacho kwenye hili jeshi. Walikuwa wanayeyuka mioyo yao kila siku kwa kuwa hakuna mtu aliyediriki kujitokeza kukabiliana naye. Hili ndilo lilikuwa tatizo na Daudi aliligundua na alijua kuwa yapasa awepo mtu wa kujitoa mhanga kukabiliana naye. Hili pia ndilo tatizo letu hata sisi, kwa kuwa hatuipigi vita imani; kwa kuwa hatulineni neno la Bwana kwa ujasiri mkubwa. Kwa kuwa sisi idadi yetu haichukui asilimia yoyote kwenye mamilioni, basi watu wetu hukata tama kwa sababu wao ni wachache mno idadi yao. Yatupasa kushuhudia imani yetu kwa ujasiri mwingi hata kama tupo wachache, kwa kuwa tunapigana na maadui wa Mungu aliyehai na wao hawapo hivyo. Haijalishi tu wachache kiasi gani, hatupasi kuyeyuka mioyo kwa kile tunachokifanya. Hili ndilo fundisho.

33 Sauli akamwambia Daudi, Huwezi wewe kumwendea Mfilisti huyu upigane naye; maana wewe u kijana tu; na huyu ni mtu wa vita tangu ujana wake. 34 Daudi akamwambia Sauli, Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na alipokuwa akija simba, au dubu, akamkamata mwana-kondoo wa lile kundi, 35 mimi hutoka nikamfuata, nikampiga, nikampokonya kinywani mwake; na akinirukia, humshika ndevu zake, nikampiga, nikamwua. 36 Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai.

 

Daudi alikuwa na kusudi na alilijua kusudi la Mungu. Alielewa kwa njia ya Roho Mtakatifu kwamba hakuna kitakachoyashinda majeshi ya Mungu aliyehai na hakuna kitakacho limudu hilo.

37 Daudi akasema, Bwana aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na Bwana atakuwa pamoja nawe. 38 Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii. 39 Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, Siwezi kwenda na vitu hivi, maana sikuvijaribu. Basi Daudi akavivua.

 

Masharti ya vita ni kujaribu kwa kupasha moto wa silaha zako kabla hujatoka. Daudi hakuwahi hata kuijaribu ngao yake. Alikuwa hajaivaa kabisa. Haiingii akilini kuona unakwenda kupigana na kitu ambacho hujawahi hata kukijaribu bado na wala hujakizoea. Usitoke na kwenda kupigana vita ukiwa na silaha usizozijua matumizi yake. Mungu ametupa sisi mavazi ya kujikinga na unaweza kujisomea kuhusu silaha hizo kwenye Agano Jipya. Silaha ya Bwana imejaribiwa na kuhakikishwa. Daudi aliziacha silaha alizokuwa amepewa na aliichukua fimbo yake mkononi mwake na akayachagua mawe laini matano kutoka kwenye kijito na kuyaweka kwenye mkoba wake wa kichungaji. Sasa jambo hili ni la muhimu sana. fuko wake silaha alizokuwa amepewa nazo gao Daudi hakuchagua kuyapiga majeshi ya Wafilisti, na mashujaa wa Kifilisti. Hakuchagua kupigana kwa silaha zilizokubalika na kuruhusiwa za ulimwengu huu. Imani ya Kibabeloni haikuwa inakwenda kushindwa kwa mfumo wa silaha zilizoruhusiwa na mfumo wa ulimwengu huu. Daudi alitumia kitu kingine na cha tofauti. Alichukua fimbo mkononi mwake pamoja na mawe laini matano, aliyoyachukua kutoka kijitoni. Maana yake ashirio iko wazi sana. Fimbo ya Daudi ni utawala wa Masihi na uweza uliowekwa ndani yake kwa njia ya Roho Mtakatifu. Mawe malaini tano ya kijitoni ni makanisa matano ya Mungu yanayoifanya hivyo katika siku za mwisho, yakiwa yamechaguliwa kwa kupitia maji yaliyohai ya Roho Mtakatifu. Mfuko wa kichungaji ni nguvu za ulinzi za Masihi. Mambo ya kuyafikiri pale ni yale mawe matano tu kwa kuwa makanisa mawili ya Mungu hayafanyi hivyo kwenye Ufalme. Makanisa ya Wasardi na Walaodikia yametupwa nje ya Ufalme.

40 Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti. 41 Huyo Mfilisti naye akamsogelea Daudi na kumkaribia; na mtu yule aliyemchukulia ngao yake akamtangulia. 42 Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri. 43 Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.

 

Mara tu alianza kunuizia miungu yake kinyume na Roho Mtakatifu kutoka kwa Mungu aliyehai, ambaye ka hakika sana kabisa ndiye mlengwa wa vita hivi.

44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni. 45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.

 

Sasa hii iko wazi sana; kwamba Mungu alimpeleka Daudi kwa makusudi na Daudi ananena kwa Roho Mtakatifu. Daudi anaongea na mtu anayetegemea nguvu zake mwenyewe za kimwili na silaha za kimwili. Silaha zetu zina nguvu ya kuziangusha ngome na hizi ndizo silaha za siku za mwisho. Hayo ndiyo mapigano au pambano la siku za mwisho.

46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli. 47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.

 

Huhu ni kijana asiye na silaha, anayeongea na jitu lenye urefu wa futi kumi kwenda juu na mwanajeshi aliyefunzwa vizuri, aliye na mbeba silaha wake, ambaye alijiandaa vizuri na mwenye uwezo wa kumuua Daudi mwenyewe. Ndipo alijitokeza nje dhidi ya watu hawa wawili. Mmoja wapo alikuwa ni jitu la urefu wa futi kumi na aliyepata mafunzo vizuri ya kijeshi.

 

Hapa tunaangalia idadi ya matatizo. La kwanza ni kwamba tunashughulika na aina ya silaha ya Daudi. Hakuwa amezoezwa kuvaa au kutumia silaha ya Sauli kwa kuwa silaha za vita vyetu hazipo sawa na zile za dunia hii. Masihi alikuwa hajafunuliwa bado kwao. Daudi alikuja kwa jina la majeshi ya Mungu aliyehai. Kuangamizwa kwa nguvu za mataifa ni sawa na kule kwa nyakati za mwisho. Neno Wafilistimu lililotoholewa kutoka kwenye neno Pereset au wakazi wa maeneo ya bahari linakuwa pia ni ndharia iliyohusiana au kufafa na Kitimu ya nyakati za mwisho. Wakitimu walikuwa ni maadui walioorodheshwa kwenye Magombo ya Bahari ya Chumvi, maarufu kama the Dead Sea Scrolls. Israeli kwenye karne ya kwanza waliwaona watu hawa kama wanaokuja wakitokea kwenye merikebu za baharini, yaani wakazi wa maeneo ya baharini. Majitu walikuwa wamehusiana na Wanefili ambao walikuwa ni matokeo au uzao wa malaika waasi (soma jarida la Wanefili (Na. 154)). Goliathi wa Gathi alikuwa jitu na Israeli kwenye karne ya kwanza walielewa kuwa hawa majitu kuwa ni uzao wa Wanefili. Waliwakilisha imani ya malaika waasi na mikakati yao. Imani iliyobuniwa na kutungwa ya mapepo. Hivyo, imani hiyo ingeweza kuwekwa kwa matendo ya mfalme mpya, Masihi. Mawe matano yaliyo ndani ya mfuko a kichungaji ni makanisa matano yaliyo na sehemu yake kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu. Makanisa ya Wasardi na Walaodikia hayatakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu kwa namna yoyote ile. Makanisa hayo yana watu mmoja mmoja binafsi tu kwenye kundi hilo. Kanisa la Sardi limekufa na la Walaodikia limetapikwa kutoka kwenye kinywa cha Mungu. Ni watu mmoja mmoja tu binafsi yao kwenye makanisa hayo ndiye anaweza kuuingia Ufalme wa Mungu.

 

Goliathi aliuawa kwa jiwe moja tu. Tunaona kwamba kutokana na mkururu wa Makanisa, ni hazima liwe ni la mwisho. Hata hivyo, ujumbe wa malaika wa kwanza ni mchakato endelevu, ambao unahitimisha au kukamilisha kwenye mamlaka ya nyakati za misho. Mayokeo yake ya mwisho ya mchakato huo ni kuangamizwa kwa dini ya uwongo ya Kibabeloni kama tunavyojionea kutoka kwenye mfululizo wa matukio ya ujumbe wa malaika (Ufunuo 14:6-12).

Ufunuo 14:6-12 Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, 7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji. 8 Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake. 9 Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, 10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo. 11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake. 12 Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.  

 

Moja kwa moja kutoka na ujumbe wa malaika wa kwanza kutapelekea kuanguka kwa Babeli kama jiwe kutoka kwenye kombeo ya mfalme wa Israeli.

 

Nia ya vita hii kati ya Daudi na Goliathi ilikuwa ni ili kwamba majeshi ya Mungu yaweze kujua kwamba Bwana haokoi kwa nguvu wala kwa uweza bali ni kwa roho wangu asema Bwana wa Majeshi (Zekaria 4:6).

 

Tena licha ya usemi huu, Daudi hatimaye aliyenda dhambi ya kuwahesabu Israeli (2Samweli 24:1 ff.; 1Nyakati 21:1 ff.). Dhambi hii ilisababisha vifo vya watu 70,000 katika Israeli. Dhambi ya kuwahesabu majeshi ya Bwana ni dhambi ya kwanza ya uongozi wa nyakati za mwisho. Siyo tu kwamba ni taifa ambalo limekaliwa kupita wastani wake na kikosi cha kijeshi. Makanisa ya Mungu katika nyakati za mwisho yametahesabu majeshi ya Mungu hadi mchakato mchakato ni kutokuwepo kwenye lugha ya watu wetu – kama tutarudi nyuma kwenye dhana au wazo la kuangamizwa kwa malaika. Hapa Daudi anamtegemea Mungu. Alimkabili Goliathi na akasema kwamba anakwenda kumwangamiza na kumuua Goliathi. Imani yake ni kubwa hapa na kwa kweli anakwenda kumwangamiza. Lakini hatimaye alipokuwa mzee alianza kutegemea kwenye idadi ya wanajeshi wake kama alivyosema Napoleon: Mungu yupo upande a bataliani kubwa; au alivyosema Stalin: Ni vikosi vingapi alivyonavyo Papa? Kitendo hiki cha kuyahesabu Makanisa ya Mungu katika nyakati za mwisho ni dhana moja ileile. Utamalakiji huu na uhesabuji, kwa tarakimu, kwa kile kinachoitwa ‘matunda’, ni machukizo machoni pa Mungu. Mchakato huu umepelekea kukaliwa au kujazwa tena na watu walioketi vitini na sio wanaofundisha, na sio kuwaweka watu kwenye mwili wa kanisa na sio kuwatayarisha kwa kazi zao. Matokeo yake watu hao wataondolewa sehemu yao kwenye Ufalme wa Mungu. Watu elfu sabini watakufa na kukabili ufufuo wa pili wa wafu kwa sababu ya kushindwa huko. Wakumbushao watakabili mchujo kama ngano. Mchakato huo na habari zake vimefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137). Ni habari ndefu na inayohusika.

48 Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti. 49 Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi.

 

Ni namna hiyohiyo kwamba mungu wa Wafilisti alianguka, na ndivyo alivyofanya hata shujaa wao. Mhuri wa Mungu upo katikati ya macho, na hili jiwe, ujumbe huu wa Mungu aliyehai, ulikuwa ni kuangamiza mfumo na imani pale walipotiwa mhuri, kwa jina la mungu wao. Na iliua shujaa wao na aliangukia paji lake la uso.

50 Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti, akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake.

 

Hiki ndicho kinachotokea katika nyakati za mwisho. Hatutahitaji upanga na tutayaangamiza majeshi ya mungu wa dunia hii. Tutawaangamiza mamilioni kwa mamilioni katika nyakati za mwisho na hakutakuwa na upanga mikononi mwetu.

51 Ndipo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia. 52 Nao watu wa Israeli na wa Yuda wakainuka, na kupiga kelele, nao wakawafuata Wafilisti mpaka ufikapo Gathi, na mpaka malango ya Ekroni. Nao majeruhi wa Wafilisti wakaanguka kando ya njia iendayo Shaarimu, mpaka Gathi, na mpaka Ekroni. 53 Kisha wana wa Israeli wakarudi kutoka katika kuwafukuza Wafilisti, wakateka nyara marago yao. 54 Naye Daudi akakitwaa kichwa chake yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu; lakini silaha zake akaziweka hemani mwake  

 

Kuna wazo la maana na muhimu sana hapa. Kichwa cha imani hii kiliondolewa kwa kutumia upanga wake mwenyewe. Kwa jinsi hiyohiyo Masihi atayashusha hadi chini kwenye bonde la kukata maneno, majeshi yote ya ulimwengu katika siku za mwisho, na atawaua kwa silaha zao wenyewe. Mataifa haya yote, moja baada ya jingine, yatashushwa chini. Majeshi yao yote yatashushwa chini na kuangamizwa.

 

Tazama, kichwa kimeletwa hadi Yerusalemu lakini silaha zake ziliwekwa kwenye hema la Daudi. Yerusalemu haukuwa bado mji wa Sauli. Na kwa kweli hata Sanduku la Agano lilikuwa huko Shilo na Daudi angeuweka huko Hebroni kabla ya vitu vyote viwili, yaani maskani na utawala wake havijahamishiwa vyote huko Yerusalemu. Wakati Daudi alipokileta kichwa cha Goliathi hadi Yerusalemu, alikuwa anatazama mbele kuelekea kwenye siku zijazo, kwenye ujio wa Masihi, wakati kichwa cha imani na dini ya Kibabeloni itakapoondolewa na mfumo wa kiutawala, mfumo na imani ya kidini vitakapopewa Masihi na kila kicha kitakapochukuliwa na kuletwa hadi Yerusalemu. Utawala wake ungetawala kutoka Yerusalemu. Silaha yake iliwekwa hemani kwake, kwa jinsi hiyohiyo nao mikuki yake na silaha zake ambazo zilikusanywa kutoka kwenye vita vya Armagedoni. Mambo haya yote yatachukuliwa na kukwamishwa. Ufafanuzi wake ni kwamba mambo haya yote yaliyokusanywa yatadumu katika Israeli kwa miaka saba. Kutakuwa na mali nyingi na za kutosha za kuzitumia nje ya majeshi, wakati watakaposhushwa chini, ili kuwaacha Israeli aendelee kwa kipindi chote cha Milenia.

 

Kwahiyo muundo unakuonyesha kwamba hii siyo historia tu, peke yake inayohusu kijana akiliua jitu kubwa na lenye vidole kumi kwenye mguu mmoja kwa jiwe la kwenye kombeo. Bali hii ni habari au hadithi ya Masihi. Ni hadithi ya ufalme uliowekwa na kusimamishwa imara mikononi mwa Mungu aliyehai na kwamba imani na taratibu hizi, na silaha ya dunia hii, na vifaa vya kivita ambazo Shetani amewafundisha watu wetu kuzitumia zitaondolewa. Zitakuwa silaha zao ambazo Shetani amewafundisha watu wetu wazitumie, ndizo kwa hakika zitauharibu kabisa mfumo huu, na kuwawka watu wetu chini ya Masihi huko ka watu wetu chini ya Masihi huko Yerusalemu. Uwekaji wa kiongozi huko Yerusalemu ulikusudia kuonyesha kwamba serikali na mfumo wote mzima wa Serikali au utawala na wakidini utakuwa huko Yerusalemu.

 

q