Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[127B]
Makosa ya Kitafsiri ya Wabinitariani na Watrinitariani Kuhusu Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu
(Toleo La 1.0 20090213-20090213)
Baadhi ya watetezi
wa Ubinitarian na Utrinitarian wanayatumia vibaya maandiko ya zamani ya Kanisa wakidai
kwamba Kanisa la Kwanza lilikuwa ama ni la Kibinitarian au la Kitrinitarian.
Mitazamo kama hiyo inajulikana na imethibitika kuwa siyo sahihi na taasisi
husika za wanazuoni waliobobea kielimu lakini bado watetezi hawa
wanang’ang’ania kusisitiza kwa kutumia mafundisho bandia ya yasiyo na mashiko
wala uhalisia.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hatimiliki ã 2009, 2017
Wade Cox)
(Tr.
2009; rev. 2017)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Makosa ya Kitafsiri ya Wabinitariani na Watrinitariani
Kuhusu Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu
Baadhi ya watetezi
wa imani za Uungu wa Miungu wawili, maarufu kama Ubinitarian na ya waamini
Utatu, yaani Utrinitarian wanayatumia vibaya maandiko ya zamani ya Kanisa wakidai
kwamba Kanisa la Kwanza lilikuwa ama ni la Kibinitarian au la Kitrinitarian.
Mitazamo kama hiyo inajulikana na imethibitika kuwa siyo sahihi na taasisi
husika za wanazuoni waliobobea kielimu lakini bado watetezi hawa
wanang’ang’ania kusisitiza kwa kutumia mafundisho bandia ya yasiyo na mashiko
wala uhalisia.
Sababu ni kwamba
mitazamo ya Kibinitarian na Kitrinitarian umejikita kwenye maazimio ya mabaraza
ya kutunga imani ya kidini ya karne ya nne kwa uwepo wao. Ukristo wa Kirumi wa
Kiothodoksi unajiachia kwa raha na starehe kwenye kujua hivyo, lakini Uprotestanti
hauamini hivyo. La muhimu zaidi ni kwamba Herbet Armstrong alianzisha mtazamo
uliofunika na wa uwongo na mpotofu kuhusu Kristo, ambao uliibuka kutoka kwenye imani
ya Utatu au Utrinitariani ukimtambulisha Eloah kwenye kozi za Mafunzo na
mafundisho ya Bibilia kwa namna ambayo kwa kweli ilikuwa ni imani ya Kiditheist.
Katika juhudi za makusudi za kuepuka kuwakwaza na kugongana na uzushi wa Waditheist,
waabudu sabanu hawa walifanya makosa ya kutelezea kwenye Ubinitarian na kwa
hiyo ndipo walilazimika kuegemea kwenye usomi bandia wa Kitrinitarian ili kutetea
hoja zao.
Kwenye jarida la Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127), kulionyeshwa ni msimamo upi wa zamani na
uliodumu kwa kipindi cha zaidi ya karne mbili za mwanzoni na jinsi
ulivyobadilika na kuwa wa Kimodalist na hatimaye Ubinitarian tangu mwanzoni mwa
karne ya nne na kutoka kwenye Baraza la Mtaguso wa Nikea, na hatimaye la Kiutatu
kutokana na kutambulisha na kutangazwa rasmi kwenye Baraza la Mtaguso Mkuu wa Constantinople
mnamo mwaka 381 na kuthibitishwa kwenye Baraza la Mtaguso Mkuu wa Kalkedon
baada ya mwaka 451.
Matumizi ya
kwanza ya neno “Trias” hayakuwepo
hadi mwaka 180BK katika kazi ya Theophilus wa Anthiokia, kama ilivyorejelewa
kwenye jarida nambari 127.
Msimamo wa Kanisa
la Roma kuanzia katikati ya karne ya pili ulichukuliwa kutoka kwa Justin Martyr,
na ule wa Smirna ilichukuliwa kutoka kwa Irenaeus huko Lyon, ulioandikwa kwenye
mwishoni mwa karne ya pili yapata kama mwaka 195, na pia kutoka kwa Hippolytus.
Maandiko ya Polycarp ni machache sana kushughulikia mafundisho kwa ujumla bali
yale ya wanafunzi wawili waliofundishwa huko Smirna yanapotosha. Tunapo kunukuu
kutoka Sehemu ya 1 katika Namba 127, tunaona msimamo wa Jastin kuwa ni:
“Justin
Mwalimu
wetu katika masuala haya ni Yesu Kristo, ambaye pia alizaliwa kwa ajili hii, na
kusulubiwa chini ya Pontio Pilato wa Uyahudi, wakati wa Tiberio Kaisari; na
kuwa tunamuabudu, tukifahamu kuwa ni mwana wa Mungu wa kweli, na kumimshikia
katika nafasi ya pili, na roho mtakatifu kuwa katika nafasi ya tatu,
tutahakikisha kwani wakaushtumu uwazimu wetu kuweko hapa, eti kuwa tunaipeana
nafasi ya pili kwa mtu aliyesulubiwa kutoka kwa Mungu asiyebadilika na aishiye
milele, muumbaji wetu sote, kwa kuwa hawafahamu maajibu yaliyoko humo, ambamo
kwamo, tunavyokueleteza wazi, tunaomba usadiki (Apol I, xiii).
Na mamlaka ya kwanza baada ya Mungu Baba na Bwana wa wote ni Neno [8@(@H au logos],
ambaye pia ni Mwana. (Apol., I,
xxxii).
Kwa hiyo ni makosa kuelewa kwamba Roho na mamlaka ya Mungu, kuwa ni kama
kitu kinginecho mbali ya Neno [8@(@H
au logos], ambaye pia ni mzaliwa wa kwanza
wa Mungu. (Apol., I, xxxiii).
Kwahiyo, Justin anadhania Logos kuwa ni
kama taswira ya Mungu ambaye ni uwingi wa mjumuiko wa wengi ili kulipa mashiko
wazo hili la Roho kwa ujumla na hasahasa la Kristo. Hata hivyo anasema:
Wote,
yeye (Mungu) na Mwana (ambaye alishuka kutoka kwake na kutufunza mambo haya, na
mwenyeji wa malaika wote wazuri ambaye waliumbwa kama yeye, na wanafuata), na
roho wa unabii, kuwafahamu ki sababu na ki kweli na kakiri bila kibari kwa
yeyote anuiaye kufunza kama nasi tulivyofunzwa.
Kwahiyo, malaika alichukuliwa pia kuwa
wana namna ya sura na mfano wa Mungu. Kutokana na Sura za 13, 16 na 61 za
kitabu chake, Justin hakutetea ibada za kuwaabudu Malaika (soma pia sura ya 3 kwenye kamusi ya ANF,
Vol. 1, p. 164). Neno kuabudu limetoholewa
kutoka kwenye neno lililo kwenye Ufunuo 3:9 lililotuama kwenye maana ya proskuneo, linaloitwa BD@F6L<ZFTF4< au proskunesoosin
(Marshall), linalomaanisha atapiga magoti
mbele ya wateule wa Kanisa la Filadelfia. Kwa hiyo, neno hili halimanishi
kuwaabudu malaika au Kristo bali ni kuonyesha heshima na unyenyekevu kwa
kusujudu kifudifudi kimwili; kwa maneno mengine, ni kuonyesha heshima. Kwa
hiyo, viumbe vilivyotajwa hapa vitapewa heshima yao stahiki ikia ni kama sehemu
ya Malaika wanyenyekevu na watiifu wa Mungu. Malaika wanaotajwa kwenye kitabu
hiki cha Ufunuo wa Yohana kua walijizuia kufanya hivyo bali zaidi tu ni kwamba
walimwabudu Mungu (Ufunuo 22:9). Hivyo basi, wateule humwabudu Mungu peke yake.
Justin anaelezea juu ya kutoa heshima stahiki tu na siyo kuwaabudu. Ahadi
waliyopewa Kanisa la Filadelfia ilitokana na sababu za kwamba Wayahudi ambao
walidai kuwa ni Wayahudi, bali walikuwa ni sinagogi la Shetani, walikuwa
wameanzisha michakato ya dini za Kisirisiri za Merkabah zinazoendesha imani
yake kimafumbo au za wapanda Magari ya Farasi wa Mungu, na za matulizo au uheri
wa malaika kwa madaraja saba, (soma kitabu cha Mysticism). Kosa na upotovu huu ulienea hadi kwenye Kanisa la
Wakolosai kwa sehemu. Ibada ya Kanisa la Mungu inatakiwa imlenge Mungu na haipaswi
imlenge hata Kristo, zaidi ya kumpa tu heshima yake anayostahili kama kiongozi
na bwana. Lakini la muhimu sana ni kwamba Justin anaujumuisha mwili akijumuisha
Malaika watiifu. Hii kwa hiyo ni uwiano wa karibu kwenye mafundisho ya biblia
ya Roho kuwa anaweza anapopewa nafasi kama mtendaji kuwakumbatia wateule
wanaokwenda kufanyika kuwa theoi,
kama Kristo alivyo mmoja wa theoi
mdogo na msaidizi kwa theos wake
ambaye ni Mungu Baba. Kimsingi sana, yeye hata hivyo ni wa pili kwenye daraja
la juu sana la theos, akiwa ni kama
kuhani mkuu.
Yaonekana sana kabisa kwamba Justin ndiye aliyekuwa wa
kuanzisha ibada ya jumapili (Taz bacc anatinoman views” kuhusiana na sabato
kuwa adhabu kali; matazamo wake haukuungwa mkono na wakristo katika kipindi
hicho na Nacchiocchi ana shikilia kuwa wakristo hawa jawahi kubadili uongo kama
hao, (P. 225) kukiri kuwa Mungu anaiazisha tohara na sabato katika msingi wa
uovu wa Wayahudi tu kama alama ya utambulisho dhidi ya mataifa na sisi wakristo
ili wao tu ndio waweze kutoabika (Dial 16:1; 21:1 tazama pia Bacchiocchi Ibid).
kwamtia Mungu kosa la utovu wa nidahamu kwa binadamu na kinyume cha sheria za
toba za uongofu. Licha ya kosa hili, mtazamo wake kwa uongozi wa Mungu bado ya
walakini wa ubadala. Hata
hivyo anabuni mvuto wa hisia ambao unaenda sambamba na hii “Antinomianist
approach”. Kama tulivyoona, Justin, hata hivyo, alizipiga mafundisho ya Roho
kuendelea kuishi baada ya kufa nay ale ya kwenda mbinguni kuwa siyo ya
Kikristo, falsafa ambazo zinachipua kutoka katika dini potofu za kisirisiri
(Dial. LXXX).
Irenæus alikuwa ni mwanafunzi kutoka Smirna
aliyefundishwa na Polycarp, mwanafunzi wa Yohana, na kwa ukaribu sana tunapata
teolojia asilia yenyewe.
Irenæus amamwambia Mungu
Kwa
kuwa aliamrisha, na wakaumbwa, alizungumza na wakatengenezwa. Alimwamrisha
nani? Neno bila shaka na nani, anasema mbingu ziliumbwa na nguvu za pumzi ya
kunywa chake (Zab 33:6). (Adu haer, iii, viii, 3).
Irenæus alishikilia kuwa:
imehakikishwa
vyema kuwa si manabdii bali ni tume wapeana jina kuwa Mungu mwenine au kumwita
Bwana, bali Mungu wa kweli na wa pekee….. ila vitu vilivyobaniwa ni tofauti
naye aliyevibini, na vilivyo yeye mwenyewe hakuumbwa, hana mwanzo wala mwisho;
na anachukilia kitu. Yeye ni safi kwake mwenyewe, na zaidi anawapa uwepo
wengine wote, ila vitu vilivyoptengenezwa naye (Ibid).
Irenaeus
alikizidisha kiwango cha kuwa Mungu (theos an Elohim) hadi kwenye “Logos|” kitu
baki kutoka katika vitu vingine vilivyofanywa (ibid). alikuwa tayari
ameshafanya nafasi ya Mungu nay a mwana na wana wote wa Mungu kutoka kwenye
Kitabu III, Sura ya vi.
Kwa
hivyo si Bwana wala roho mtakatifu wala mitume wamewahi kumpa jina Mungu, bila
shaka, yeye ambaye hakuwa Mungu, labda ikiwa alikuwa Bwana wake wa kimwili, ila
Mungu Baba atawalaye kute vote, na mwanawe aliyepeanwa naye Mungu juu ya viumbe
vyote, kama isemavyo taarifa ijuatayoi. Neno la Bwana kwa Bwana wangu, ukae
mkono wangu kuume hata niwafanyapo adui zako kuwa chini ya miguu yako (Zab
110:1). Hapa, maandiko yanawalakisha maongoze ya Baba kwa mwana, aliyepewa
urithi ya ulimwengu, na adui zake wote kulengeshwa kwake.
Irenaeus
akaendelea kusema kusema roho mtakatifu aliwataja aliyezungumza na Abrahamu
kabla ya kutekofwa kwa Sodoma na alipokea nguvu (Kutoka kwa Mungu) kuwahukumu
wa Sodoma kwa uovu wao. Tazama kufungu kifuatacho.
inasema
ukweli huo huo; “kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele fimbo ya
ufalme wako ni fimbo ya achili, umependa haki, umeichuka dhaluma, kwa hiyo
Mungu, Mungu wako amekupaka mafuta (Zab 45:6), kwa kuwa roho anaambalisha wote
kwa jina Mungu (Theus an Elohim) wote, aliyepakwa mafuta na yule aliyeyapaka
mafuta, ambaye ni Baba na tena, Mungu anasimama katika kusanyiko la katikati ya
Mungu, anahukumu (Zab 45:6), yeye hapa yamaanisha Mungu, mwana na wale
waliopewa uwezo kuwa wana; lakini hili ndilo kanisa ambalo ndiyo sinagogi ya
Mungu ambalo Mungu mwana mwenyewe amekusanya, na anawaambia Mungu, Mungu Bwana
amenena, ametiita nchi toka maawio ya jua hadi machweo yake……. (Zab 50:1)
katika kifungu hiki, Mungu ni nani? Anawaambia Mungu mwana alisema, watu
wasionitaka wanamliza habari zangu (Isa 65:1) lakini aaongea juu ya Miungu
wapi? Ni Miungu wa wale awasemeao ‘mimi ninasema ndiyi Miungu na wana wa aliye
juu’ (Zab 82:6). Kwa hao, Bila shaka , wale ambayo wamepokea amani wa “ Kupokewa,
ambayo tuko Abba Baba” (Warumi 8:15) ( Agaisnst Heresies, Bk.iii, ch.vi, ANF,
Vol. I,pp. 418-419).’’
Kanisa lilielewa
barabara matumizi ya maneno ya Zaburi na kwa matumizi neno ‘Mungu’ likihusishwa
na Kristo ilikuwa ni kwa dhana ya kiumbe msaidizi tu. Zaburi hizi mbili zilizotajwa
hapa zimechambuliwa kwa kina kwenye majarida ya Zaburi 45 (Na. 177) na Zaburi 110 (Na. 178).
Tunapoendelea
kutoka kwenye Nambari 127 tunaona kwamba:
“Hapana shaka kuwa
Irenasus ilikuwa na mtazamo wa ushirikiano wa utawala wa Mungu na akaendelea
neno ‘Mungu’ kujumuisha mwana na wale waliopewa uwezo kuwa wana. Anaonekana
kuashiria kuwa wana. Ananena kuwa kuashiria kuwa Kristo akawakusanya wateule,
bali sisi twajua kuwa ni Mungu ndiye ampaye Kristo wateule (Yohana 17:11-12,
Waebwania 2:13; 9:15) matumizi ya neno hili kwa wateule wa kimwili huenda
yasisiwe sawa tukiuzingatia mtazamo wa irenaeuos hapa. Wenyeji wazalendo pia
wamehusishwa katika baraza tukitumia uelewavu wa Ufunuo 4 na 5- hivyo wenyeji
wazalendo ndio “Ecclesia” wa Mungu. Hapana shaka kuwa maneno “Elohim” au
“Theoi” yalimaanishwa kuenea hadi kanisani na kuwa ulikuwa ni uelewevu ya
kanisa la karne ya kwanza kutoka kwa Yohana na Polycarp, walionifunza
irenaeous, na kuingia katika karne ya pili na karne zilifuata.”
Kihistoria hili
limekuwa likifahamika kama baraza la Elohim ambao ni wana wa Mungu.Ni dhahiri sana kwamba Ireneaus aliacha kidogo kunukuu yale
yaliyonenwa kwa wazi sana alikuwa ametiwa mafuta ya furaha kuliko ndugu zake,
ambapo inaashiria kwamba alikuwa wa aina moja na chimbuko moja na Malaika. Alikuwa
kwa vyovyote vile, anasisitiza hali ya wateule wa kimwili na hakujihusisha na
andiko la pamoja na Malaika. Tutakwenda kulizungumzia na kulijadili hilo
baadae.
Tunaoma kuwa
Kanisa la sehemu zote mbili, yaani la Roma na Ufaranza ya katika karne ya pili
yalikuwa na mtazamo wa ubadala au wa ushirikishi kwa Kristo. Kanisa lilielewa
fika kutokana na maandishi ya Agano Jipya, na hasahasa ya Waebrania, kwamba
Zaburi 45 na 110 zilimrejelea Kristo. Ilieleweka pia kuwa Mungu kama Baba wote,
alikuwa ni Mungu wa Yesu Kristo. Alikuwa anajieneza mwenyewe kama Eloah au
Mungu wa Pekee wa Kweli ili afanyike kuwa Ha Elohim akiwa ni kiini cha kiumbe
anayeenea wa Elohim au wana wa Mungu.
Mchanganyiko wa
nadharia au mawazo ya Wayunani na “Wanostiki” yaliingizwa kwenye waraka wa Clemant
wa Alexandria kuanzia mwaka 127 kama hivi:
Clement wa Alexandria anasema
kwa namna hiyohiyo:-
Kwa
kuwa mwana ndiye nguvu ya Mungu, na kuwa ndiye neno la kale zaidi la Baba,
kabla ya kufanywa chochote na Bwana yake. Hivyo anaitwa mwalimu wa waumbile
yake. Sasa nguvu za Bwana lina marejeleo katika mwezi, na mwana ni nguvu za
Baba (“Strom.”, VII,ii,P.G., IX, 410).
Hata hivyo
Clement alielewa kuwa hatima ya wateule ni kuwa miungu. Alipoongea kuhusu
‘gnosis’ alishikilia kuwa ingepatikana na mwanadamu katika kanisa kwake kwenye
nchi au duniani:
Hafika upeo baada ya mauti ya kimwili, nafasi ya (gnoostikis) ilihusiwapo kuenda mahali pake rasmi, ambapo, baada ya kuwa Mungu, itafarijika, katika mapumziko yasio na mwisho. (S.R.C Lilla Clement of Alexander, a study in Christian platonisan and grosticison, Oxford 1971, P 142).
Hivyo tunaona hapa mchanganyiko wa ‘gnosis’
ya kigiriki na tamaduni za kale kuwa tutakuwa ‘theoi’ Elhim. Hapakuwa maoni
kuwa Kristo wala theoi wengine kuwa sawasawa na tutakatifu wa hali ya juu.”
Mtazamo huu ni a muhimu kwa jinsi yanavyotumiwa vibaya maandiko ya zamani yanayotuama kwenye utendeaji kazi wa neno elohim au theoi.
Katika maandishi yake dhidi ya Neotus. Hippolytus, mshirika wa Iraneous ambaye alikujakuwa askofu katika mji wa bandari wa Roma na aliyewakemea maaskofu wa karne ya tatu wa Kirumi na kanisa kwa ajili ya ukengeufu wao, alikuwa wazi hata kwa ukweli kwamba hakuwa na usawa wala kujilinganisha na Mungu mwenyewe.
Sasa ina sehemu gani maana ya “kuwepo
tangu mwanzoni” kwani ni je, hivi hawa Wabinitarian, Waditheist na Watrinitarian
kweli hawaelewi?
Kujilinganisha
na Umilele Ulio Sawa
A. Sifa au Sharti la …..1 La chimbuko au kiini cha usawa na uwiano 1622.2. Sawa nay a zamani 1700 3. Ikiwepo kwa wakati huo huo mmoja na 1704.4. Kwa kudura ya kudumu 1742…..
B.
Sb 1. Ya umri huo huo au kusimama 1656 2. Mtu au
kitu kinachomilikiwa kwa kipindi hichohicho.
Wakati Mababa wa
‘Ante Nicene’ walipotafsiri maana ya andiko ilikuwa wazi na hakuna mwanazuoni
aliyedai kuwa andiko hilo lilikuwa na maana nyingine zaidi. Si Kristo wala
kuimbe mwingine yeyote aliyekuwepo tangu mwanzo au aliyekuwepo huko mwanzoni
kabisa na Mungu. Hakua! Alikuwa Mmoja, peke yake. Vinukuu zenye msisitizo zimeongezwa
“Hippolytus anasema na la muhimu
na maana sana ni:
Kwa
kuwa sasa Neotus anahakikisha kwamba mwana na Baba walikuwa sawa, hakuna
asiyejua. Ila amamtoa maelezo ‘wakati Baba hakuwa amezaliwa, alikuwa
ameshahakikiwa kwa haki kuwa Baba; na kuendeleza vizuri kulipoupendeza, kwa
alikuwa wa pekee yeye mwenyewe akawa mwanawe, kulingana na kipindi cha
‘visiccitude’ (Hippolytus anarudia wazo hili katika utupisho wa kitabu chake X)
(Con. Neot,
n, 14, “The refutation of all Heresies Bk ix. Ch, v, ANT, Vol, v, pp 127-128);
Wakwanza na wa pekee
(Mungu mmoja), muumba na Bwana wa wote hakuwa na chochote “coeval” ndani
yake……… ila alikuwa mmoja na pekee yake. Kwa zoezi la mapenzi yake, aliviumba
vitu ambavyo havikuwepo mwanzoni yapokuwa alimwa viwepo kwani anafahamu yake
fika na chochote ambacho kinakaribia kutendeka, ufahamu wa kimbele pia anao
(Hippolytus, ibid, x, xxviii, p 150).
Kwa hivyo huyu Mungu
mwenzake yote, kwa uakizi mwanzo alileta ‘logos’ si neno kwa kufanywa na sauti
bali kama uswazisho wa ulimwengu, uliofanywa na kupewa makao akilini. Yeye
mwenye alichumbuka kutoka katika vitu vilivyo; kwa kuwa Baba mwenye alikuwa
ndiye uwepo, na kuzaliwa ndiko kulisababisha vingine kuwapo. Logos ilikuwa
ndani ya Baba mwenyewe, kushikilia mapenzi ya mwelekezi wake na si kuwa na
ufahamu duni wa akili ya Baba.
Sambamba na uwezo wake
kutoka kwa mwelekezi wale, na kuwa yeye ndiye mwanambee wa mwelakazi hiyo. Na
hivyo ndivyo ilivyokuwa, kuwa Baba aliponuru kuwekko ulimwengu, logos, mmoja
baada ya mwingien wakaukamilisha uumbaji hivyo kumfarahosha Mungu.
(Hyppolytus idid, x,
xxix).
Kristo, anamaanisha, hekima na uweza wa Mungu Baba vimeijenga nyumba yake... (kwa mujibu wa kitabu cha Fragment on Proverb [Dondoo kwenye Mithali] 9:1, ANF, Vol. V, p. 175)
Ni kupitia kwa mwandishi huyu ndipo tunaona kwamba mwendelezo wa kwanza wa makosa na upotoshaji yalianza kufundishwa kwamba Kristo alikuwa ni matokeo pekee wa Baba na kwamba viumbe wengine wote walipko mbinguni na jeshi lote la Malaika wameumbwa na Mwana na kwamba msishirikiane kwenye asili na tabia ya kimungu, kama afanyavyo Mwana. Sasa huu ndiyo msingi wa makosa au upotoshaji ambayo kwayo ndipo mafundisho ya Utatu yalianzia kujengwa na kuibuka. Elohim ni kama alivyoonyeshwa kutoka kwenye kiini na mafundisho ya msingi ya Kibiblia, wapo wengi wakiwa ni Jeshi la Malaika ambao kwamba Manakondoo ndiye Kuhani Mkuu, lakini yeye bado ni mmoja wao akiwa kama mshirika mwenzao au ndugu yao, ingawaje mfumo wote mzima wa kimadaraja ulianzishwa na yeye au kutokana na yeye na kwa ajili yake (Wakolosai 1:15).
Hivyohivyo, watakatifu nao walifanyika kuwa
wenza wa Kristo kutokana na Waebrania 3:14 na, hivyo kuwa ndugu na Malaika (Ufunuo
12:10) na warithi pamoja na Kristo (Warumi 8:17). Mbingu, na vitu vyote ambavyo
vimetajwa kuwa viliumbwa na Mwana, ni vya tabia ya kiroho na kimwili. Kuna
makusudio ya rejea kenye Yohana 1:3 kuhusu uumbaji na kwenye 1Wakorintho 8:6 kuhusu
ulimwengu (J BV<J" or ta panta) na wanadamu. Wakolosai 1:15-17 hasahasa
inaelezea na kuonyesha uumbaji wa vitu vyote, vinavyoonekana na visivyoonekana.
Uumbaji wa viti vya enzi vya ufalme au
ubwana au vya watawala au vya wenye mamlaka, kwa kupitia yeye na kwake, usemi
ambao hauwezi kuwa unarejelea Baraza la Elohim. Uumbaji wa Kristo wa ubwana
hauhusiani na haya. (6LD4`J0J,H au
kuriotetes) na siyo wa vitu.
Ni kutokana na mafundisho potofu nay a kizushi ya Noetus ndipo tunawaona waamini miungu mingi yaani Wabinitariani/Watrinitarini wakimuomba mungu Attis/Adonis/Osirus wakiindi na ibada na miungu yao kwenye imani ya Kikristo.
Hippolytus alijaribu kutofutisha kati ya Kristo na Malaika au elohim wengine lakini alikuwa bayana sana kwamba Mungu na Kristo hawakuwa na usawa wa umilele wala wa kiuungu. Maelezo haya yalikuwa ni kuelezea au kuifafanua dhana ya prototokos kama ilivyotumiwa na Kristo. Kristo alikuwa ni kiumbile wa Baba kupitia kwa Roho Mtakatifu. Bibilia inasema wazi sana kwamba waa wote wa Mungu walitokana na Baba na wote wanachimbuko moja.
Wana wa Mungu
walikuwa ni bararaza la Elohim. Kila mmoja aliyeujua ukweli huu kutoka kwa
manabii hadi kwa mitume na wazee wa imani. Mwanateolojia wa Kijesuit aitwaye
Leopold Sabourin S.J alilifafanua wazo hili kwenye kitabu chake cha The Psalms Their Origin and Meaning, [Zaburi, Chimbuko Lake na Maana Zake] their
Mungu Soc. Of St. Paul NY, 1974. (Imprimatur J.P.
O’Brien Vicar General NY. Nihil Obstat Donald A. Panella, Censor Librorum, and
Imprimi Protest by R.A.F. MacKenzie SJ, Rector, Pontifical Biblical Institute).
Ni suala la kufuata ukweli tu kwamba wanazuoni wa Kitrinitarian wenyewe wanakubalia kwamba mungu wa Utatu aliingiza kwa weledi mkubwa kwenye mawazo na nadharia ya Maandiko ya Wayunitarian. Mchakato huu umeelezewa na kufafanuliwa kwa kina kwenye kurasa za Nyongeza za jarida la Matamko ya Msingi wa Imani ya Kikristo (Na. A1). Wakiongozwa na wanateolojia wa Kanisa Katoliki la Roma kama vile C.M LaCugna na wengine wanaeleza jinsi mchakato ulivyotokea na ananukuliwa kwenye kurasa za Nyongezaa.
Si kwamba ni kana kwamba hatujui jinsi mchakato wenyewe ni ulivyo. Yeyote ambaye ameisoma Bibilia na kujisomea habari au Rekodi za “makasisi au mapadre” za kwenye Mabaraza Saba ya Mitaguso atafahamu ni kwa nini au kwa namna gani ilitokea. Kanisa Katoliki la Roma linadai tu kwamba walikuwa na haki ya kufanya hivyo. Na ni kwa jinsi hiyohiyo wanadai kuwa wanahaki ya kuibadili Sabato na maadhimisho ya Mwandamo wa Mwezi Mpya na Sikukuu takatifu. Kanisa halikukubaliana kamwe kabisa na madai hayo.
Kwenye mtihani mwingine wa hivi karibuni wa makosa na upotoshaji wa kiteolojia yaliyofanyika kwenye Makanisa ya Mungu na mahali pengine, soma pia kwenye jarida la Imani za Kibinitarian na Kitrinitarian (Na. 76).
Ni kwa vipi basi Wabinitarian na Watrinitarian wahalalishe madai yao kuhusu usawa wa umilele na usawa wa kiuungu wa Mungu na Kristo wakati ambapo rekodi zilizoandikwa ziko wazi sana?
Jawabu ni kuwa wanakosea kuwakilisha maandiko ya mababa wa zamani na matumizi yao ya neno “Mungu”.
Wanaliongeza zaidi jina hili kwa kumrejelea Kristo ndani ya dhana ya uwakilishi wake mdogo iliyo kwenye Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-8 wakijaribu kuyayskinisha makosa yao ya kimaandiko na kuwapotosha wale ambao hawajaelimika na walio na ufahamu mdogo kwenye histroria ya jambo lenyewei.
Katika neno “Mungu” tunayaona maana ya Kitetoniki ya kale kuwa ni: Kile kilichohitajika au kile kimachoabudiwa kwa njia ya sadaka.
Mungu: II Kwa maana ya Kikristo na Kimonetheism.
Mtu Mmoja Astahiliye Heshima ya Kuabudiwa: Muumbaji na ni ndiye Mtawala wa
Ulimwengu.
Ni sahihi kuwa
neno elohim lilitumika kwa Kristo (na
wengine) ambao pia walikuwa na elohim ambaye alikuwa ni Mungu wa Kristo.
Neno hili
latumika na kueleweka kwenye Kiaebrania na kwenye Kiyunani na liliandikwa
kwenye Agano Jipya kwa namna hiyo kama kuonyesha tofauti hizi za Kiebrania. Inafuatia
na usiku wa siku ambayo huwezi kuilinganisha na kuilingalisha umilele sawa na
Mungu wako mwenyewe isipokuwa ni sanamu. Daudi alimwita Bwana ingawaje alikuwa
ni wa uzao wake mwenyewe, na ni kwa kuwa alikuwa amekuwepo akiishi kwenye
kipindi kirefu cha kabla ya kuzaiwa kwake rasmi kimwili (soma jaridaa la Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na.
243). Hata hivyo, Kristo hakuwa na umilele sawa na Mungu. Hakuweza kamwe kuelewa
kuwa ana usawa woote au umilele sawa na Mungu kwenye Biblia ama kwenye Agano la
Kale wala Jipya na hii ni dhana ya kubuni tu kudai kwamba inasema au inaashiria
kumaanisha hivyo. Kila mwanateolojia mkubwa na mashuhuri msomi wa Biblia
wanakubaliana kuwa Biblia inashabihiana na mrengo wa Kiyunitarian, wakiwemo
Calvin na Harnack, na manateolojia Brunner anakiri na kukubaliana na ukweli
huo.
Hivyo basi, ni
maandishi yapi ambayo waandishi hawa wanayategemea kuyajengea hoja ya madai yao?
Andiko ambalo
wanalitumia wengi ni kazi mbovu au kitabu cha upotoshaji kilichotungwa au
kuandikwa na Clement ambaye anafiatiwa na kina Linus na Cletus wa Roma. Tatizo
ni kwamba hata hatujui kabisa kwamba Waraka wa Kwanza wa uliojulikana kuwa ni
wa Clement ndiyo uliorejelewa kwanza Eusebius (Historia ya Mhubiri iii, 16). Haukuja
kujulikana hadi ulipogunduliwa kwenye Gombo au Codex A manamo mwaka 1628. Unajumuisha
hadithi za kubuni au za uwongo zilizokubaliwa na waandishi. Unashughulika na uchochrzi.
Kile kinachojulikana kama kuitwa Waraka wa Pili ujulikanao kama uandishi wa kiubandia
au wa kiupotoshaji ulioandikwa na waandishi wengi waliofuatia baadae
aliyejulikana Clementi akisaidia misimamo iliyofuatia baadae. Mtu yeyote
aliyewahi kusoma vitabu vya Clement vya ANF ataujua ukweli wa mambo haya. (Tazama
kitabu hiki cha ANF, Vol. 1, pp. 2-3). Kwanza kabisa Clement hakuwa wa
mrengo wa Kibinitarian. Kwa kweli ni mfumo wa Kiyunitarian.
Watu kama vile Holmes,
na madanganyo wanaotaka kukubaliananayo, wanashikilia madai ya uwongo na ya
kipuuzi kwamba ule unaoitwa kuwa ni Waraka wa Pili wa Clement ndiyo “mahubiri
na ujumbe kamili wa kizamani zaidi wa Kikristo uliodumu kwa muda mrefu” (kwa
mujibu wa kitabu cha Holmes M.W., The Apostolic Fathers: Greek Texts and
English Translations [Makasisi Mitume: Maandiko ya Kiyunani na Tafsiri ya
Kiingereza], 2nd ed. Baker Books, Grand Rapids, 2004, p. 102).
Hakuna mwanazuoni
wa kidini angaliyeweaa kutekwa na mafundisho hayo yasiyo na mashiko.
Wabinitarian wanamnukuu Holmes licha ya kujua kwamba anarejelea kwenye uandishi
wa uwongo wa kubumbabumba. Kwa kweli, haitokani na mafundisho yalivyokuwa
kwenye karne ya kwanza na mapema karne ya pili ingawaje wengine hujaribu
kuyafanya yaonekane kuwa yalianza zama ya mapema kabla ya ‘Justina Martyr’. Mahala
Wengi wanaiweka kipindi cha kabla ya Justin na wanajaribu kuiweka iwe kabla ya
Athenagorus.
Waraka huu bandia
ndiyo hatimaye ulinukuliwa ukituama kwenye maandiko nyaraka nyingine za kubumba
ili kujipenyeza polepole na kwa hila Ubinitariani. Matumizi ya neno “Mungu”
kulikopenyezwa kama kuuthibitisha Ubinitariani uliotokana na azimio linalojulikana
Ante-Nicene.
Maneno yanayohusiana
na Mungu na Kristo ni sawa sawa tu na maandiko kama yalivyotumika kwenye Zaburi
45:6-7 na Waebrania 1:8-9. Kwa mfano matumizi ya maneno kutoka kwenye andiko
kwamba:
Wapendwa, yatupasa tumfikirie Yesu Kristo, kuwa ni kama Mungu, kama “Mhukumu wa waliohai na waliokufa (kwa mujibu wa Maandiko ya Wakristo wa Kale (liitwalo kama 2Clement), 1:1. Holmes M.W. The Apostolic Fathers: Greek Texts and English Translations, 2nd ed. Baker Books, Grand Rapids, 2004, p. 107).
Kwa huyo ndugu wapendwa, kama tukiyatenda mapenzi ya Mungu Baba yetu…(Kwa mujibu wa Mahubiri ya Zamani ya Kikristo (2 Clement), 14:1. Holmes M.W. The Apostolic Fathers: Greek Texts and English Translations, 2nd ed. Baker Books, Grand Rapids, 2004, p.121).
Kukinukuu kifungu hiki ni kama kuliunga mkono Kanisa la Kwanza kuwa ni kama lilikuwa la mrengo wa Kibinitarian ni kuwapotosha wanazuoni waseme maneno kidogo.
Robert M. Grant anaandika kwenye kitabu chake (cha The
Anchor Bible Dictionary [Nanga ya Kamusi ya Biblia], v. 1, p. 1061) kwamba:
Waraka wa zamani wa Wakristo uliotafsiriwa sambamba na 1 Clemet katika Gombo la kibiblia la Waalexandia (mwishoni mwa karne ya 4) na baadaye kwenye Gombo la Yerusalemu (mwaka 1056) ambalo linajumuisha Didache ya pamoja na kwenye toleo la Kisyria. Halikuwa limeandikwa na mwaadishi (au waandishi) wa 1 Clement na, kwa kweli, siyo waraka bali mahubiri yenye kiasi, toba na hukumu. Mahubiri haya yanaanza kwa ufupi sana kwamba: “Ndugu zangu, ni lazima tuwaze juu ya Yesu Kristo na kuhusu Mungu, ni kama mhukumu wa wafu na walio hai. Hatupaswi tuwazie kidogo kuhusu wokovu.” Mhubiri anatuambia kuhusu “ndugu zake wa kiume na wa kike” kwamba anawasomea “maombi” maalumu ya kimaandishi au “anawasihi” (Gk enteuxis) “watilie maana kwenye kile kilichoandikwa,” yaani, kwenye maandiko matakatifu ambayo ameyarudiarudia mara kwa mara (pamoja na nukuu kutoka kwenye “maneno ya kinabii,” vinginevyo haieleweki, na ni kitu kilicho kama Injili ya kiapokrifa ya Wamisri). Yeye mwenyewe anarejelea kwenye “vitabu” (yaani Agano la Kale) na mitume” kama mamlaka zake (14:2).
Kwa hiyo, ule unaojulikana kama 2Clement, ulikutikana kipindi cha milenia baada ya hapo, nan i wazi kabisa kwamba inaweka tofauti kati ya Mungu na Kristo na inampa Kristo mamlaka ya kuhukumu ambavyo ni ndivyo ilivyonenwa kwenye biblia. Hili silo andiko la Kibinitarian na linakadiriwa kuandikwa yapata kama miaka ya 130-160 BK katika kipindi cha mapema zaidi na huebda baadae (160-170). Ni hakika sana kwamba haiwezi kuweka msukumo zaidi kwenye usemi wa wazi au maneno ya waandishi wengine wa huko Roma na Lyon na huko Ostia Attica.
Andiko hilo laweza kupatikana na kusomwa kwenye tovuti ya http://www.earlychristianwritings.com/2clement.html
Maombi yamefanywa kwa Polycarp huko Smirna. Teolojia hii ilifundishwa na kina Irenaeus na Hippolytus na ni dhahiri kuwa walikuwa Wayunitarian.
Waraka wa Polycarp ulikuwa pia ni wa Kiyunitarian kabisa.
Kwenye sura ya
XII, ambayo ni ya kuwasihi kutokana na rehema mbalimbali anasema:
Basi Mungu na
Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na Yesu Kristo mwenyewe ambaye ni Mwana wa
Mungu, na Kuhani wetu Mkuu wa milele, awainue na kuwajenga kiimani na kwenye kweli,
na kwa upole wote, uvumilivu, subirá, luchukuliana mizigo na usafi au utakaso;
na awajalie mema yake mengi na nafasi baina ya watakatifu, na kwetu sisi pamoja
nanyi, na kwa yeyote aliye chini ya mbingu, atakayemwamini Bwana wetu, na
kumwamini Baba yake, aliyemfufua kutoka kwa wafu (sawa na Wagalatia 1:1 sawa na
ANF, Vol. 1, pp. 35-36).
Ni jinsi gani mtu
anaweza kuyapinga maandishi ya Polycarp kuwa ni ya Kibinitarian, hususan maandiko
yasiyopigwa na yaliyosemwa kuwa ni teolojia ya wanafunzi wake zilikuwa ni dhahiri
sana ni Uyunitarian? Waraka huo uliandikwa kwa Kiyunani lakini ulihifadhiwa
ukiwa umeandikwa kwa lugha ya Kilatini.
Sura za 10-13 zimebakizwa
tu kwenye toleo la Kilatini. Sura ya 13 iliunganishwa kama kukaririshwa. Tafsiri
iliyofanywa na Roberts na Donaldson inafuatiwa na ya Kilatibi katika kuzilinda
sura tatu zote za mwishoni. Lightfoot ni Mtrinitarian na aliliruka kuandika neno
“Mwana wa” kabla ya neno Mungu kwenye sura ya 12 na iliendelezwa kwa matumizi
ya neno “Mungu” pamoja na Bwana na Mungu kabla ya maneno “Yesu Kristo” kwenye
andiko lililotafsiriwa “dominum nostrum
et deum Iesum Christum.” Bado tungali hatujui ni lini andiko hili
la Kilatini liliandikwa. Lightfoot analitafsiri anndiko hili kama hivi:-
Sasa, Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na Huhani Mkuu Mwenyewe wa milele, [Mwana wa] Mungu, Yesu Kristo, na awainue na kuwjenga kwenye imani na katika kweli, na katika upole na kwa weledi wote wa kujiepusha na hasira na kwa kuchukuliana na kwa uvumilivu wote na kwa kudumu kwenye subirá na usafi au utakatifu; na awajalie sana fursa katikati ya watakatifu wake, na kwetu sisi pamoja nanyi, na kwa yeyote aliye chini ya mbingu, atakayemwamini Bwana na Mungu, Yesu Kristo na kwa Baba yake (Lightfoot. J, B, tr. The Epistle of Polycarp to the Philippians, in Apostolic Fathers (12:6, 7)).
Na hata hivyo, inakubalika sana na pasi shaka kwamba deum linaambata na matumizi ya neno theos kwenye Yohana na pia maneno yaliyo kwenye maandshi ya Justin, Iraneous na Hippolytus ambayo yanamrejelea Kristo kama theos na deum katika marejea ya Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-9. Kwa kweli huku sio kuunga mkono wala kuuthibitisha Ubinitarian. Hiyo ni teolojia kamilifu na ya kihistoria ni teolojia ya Uyunitarian Mdogo kama ilivyoonyeshwa na wanafunzi wa Polycarp ambao walifundishwa huko Smirna na inaiashiria kwenye teolojia yake.
Neno “mwana wa
Mungu” limetumiwa na Yesu Kristo. Polycarp aliyafuata mafundisho ya Yohana na
yalikuwa ya tofauti nay a Roma kwenye Malumbano na Hoja za Wakworodesiman (soma
kwenye jarida la Malumbano ya Wakwortodesiman (Na. 277)).
Kwenye Waraka wa
Polycarp kwa Wafilipi, Polycarp anamtaja au kumrejelea Ignatius na inaonekana
kwa wazi kuwa alikuwa anajua kuhusu Kuuawa kwake kwa ajili ya kuisimamia imani.
Ingatius alidaiwa
pia kwamba alikuwa ni Mbinitarian na watetea dini wa Kitrinitarian. Tatizo
alilokuwanalo Ingatius liko wazi sana na ni rahisi.
Kuna maandiko
muhimu kumi na matano yanayomwelezea Iganatius ambayo ni:
Moja ni kwa Bikira
Maria, la pili ni kwa mtume Yohana, moja ni kwa Maria wa Coassobellae, moja ni
kwa Tersians, moja kwa Waantiokia, moja kwa Shujaa shemasi wa Antiokia, moja
kwa Wafilipi, moja kwa Waefeso, moja kwa Magnesians, moja kwa Trallians, moja
kwa Warumi, moja kwa Wafiladelfia, moja kwa Wasyrneous, na mmoja kwa Polycarp.
Kati ya hizi, nyaraka
nane za kwanza ni za ulimwenguni kote zilizojulikana kuwa zimeghushiwa kwenye
zama zilizofuatia baadae na zinaishiria teolojia ile. Huenda ziliandikwa kwa
lengo la kuanzisha mlolongo wa upotoshaji au makosa au uzushi uliofuatia baadaye.
Saba nyingine zinazofuatia zingali zinaonyesha shaka nazo.
Kuna Nyaraka saba
ambazo zilidhihitishwa na Eusebeius (Hist iii, 36). Ni hakika maandiko haya
kuna maandiko mawili ya Kiyunani, moja ni toleo fupi na lignine ni refu. Linakubalika
kote ulimwenguni na wanazuoni ambapo nyingine ni andiko au nakala potofu
iliyotumika ili kuanzisha teolojia iliyofuatia baadae.
Inafikirikiwa
kuwa nakala fupi yaonekana kabisa kuwa inafanana na ile ya asilia. Hata hivyo,
hakuna mwenye uhakika wa kama ni halisi na yawezekana zote zikawa potofu. Kwa
hakika, mnamo 1666, uainisho uliowahi kusomwa zaidi na ambao uliwezesha zote
mbili ziliharibiwa au kupotoshwa au potofu ziliandikwa na Daillé (au Dalaeus). Askofu
Pearson aliandika ya kutisha mnamo mwaka 1672 kuutetea ule waraka mfupi na huo
uliokubalika umekubalika hadi sasa na wamini Utatu au Watrinitarian.
Kama tutazichukulia
kuwa zila nyaraka saba ni toleo fupi ni halisi, ambazo ni pasi shaka,
itatulazimu kuzilinganisha na maneno yaliyo kwenye Zaburi 45:6-7 na Waebrania
1:8-9 na kama ilivyelezwa kwenye zile zinazojulikana kama nyarakia halisi za
Justin na Ireanaeus na Hippolytus.
Tukichunguza ule
waraka mfupi, tunaona teolojia ileile ya ubadala ikiibuka. Kuubuka kuwa andiko
hili linamtaja Mungu na Mungu wetu – elohim mdogo na Ha Elohim au Mungu wa
kwenye maandiko .
Kwa kuwa Mungu wetu Yesu Kristo ilichukuliwa mimba
na Maria kulingana na ratiba na mpango wa Mungu.wa uzao wa Daud,,ni hakika,
lakini pia wa Roho Mtakatifu. Alizaliwa na kubatizwa ili kwamba kwa
kujinyenyekesha kwake aweze kuyatakasa maji (Igatius, Waraka kwa Waefeso 18,2
(ANF, Vol.1, p.57).
Maandishi yaliyo
kwenye sura ya 19 yamekuwa yakichukuliwa kama ni Mungu mwenyewe amekuwa
anajidhihirisha kwa umbo la kibinadamu kwa kuurejesha au kuufanya upya uzima wa
milele (ANF ibid.).
Haya ni makosa ya
kiteolojia ya Watrinitarian waliofuatia baadae na ni uwanja, kama ilivyoelezewa
na wanateolojia waliowatangulia kitambo kama vile akina Daille kuyapitia na kuyachambua
maandiko yote. Na wengine kama akina Holmes walirekebisha nukuu zisemazo “Mungu
alijitokeza kwa umbo la kibiudamu” na Wabinitarian wanamchukulia au kumnukuu Holmes. Andiko refu linasema “Mungu akiwa
anajishihirisha kama mwanadamu, na mwanadamu ameonyesha nguvu au uweza kama
Mungu.”
……Mungu
alijitokeza kwa umbo la kibinadamu ili kuleta upya wa uzima wa milele
(Ignatius. Epistle to the Ephesians, 19,3. As per
Holmes: The Apostolic Fathers: Greek Texts and English Translations [Waraka kwa
Waefeso, 19:3. Kama Holmes: Mapadri Mitume: Maandiko ya Kiyunani Kama
Yalivyotafsiriwa kwa Kiingereza]. Baker Books, Grand Rapids (MI), 2004, p.
149).
Waraka ule mrefu hautakuwa na maana iwapo kama utaonekana ama kuchukuliwa yeye ni Mungu wa Pekee na wa Kweli aliyejidhihirisha mwenyewe, ambapo ni wazi sana hakufanya hivyo. Ni kwa namna hii ya kujikanganya kwa maandiko ndiko kulikopelekea kwa watu waombe kuyakataa yote mawili
Ungatius anapingwa kwa kusaidia lakini kazi hii ya uandishi kwa hakika ni ya wa mrengo wa udogo iwapo tukilitendea kazi andiko la Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-9 katika matumizi yake ya ubadala.
Mjumuisho umetumika katika kuyaonyesha maneno Mungu Baba na Yesu Kristo Mungu wetu ambavyo ndivyo walivyokuwa wanasema waamini Umbadala wa Kiyunitarian pamoja na maneno aliyokuwa anayatamka au kuyanena Daudi kwenye Zaburi 45:6ff.
Kutajwa kwa Smyrnaeans kwenye Waraka kwa Wasmyrnaeaus hakulazimu kufanya madai ya Waraka kwa Waefeso bali Sura ya 1 inaanzia na maneno: “Namtukuza Mungu, hata Yesu Kristo, ambaye amewapeni hekima kama hiyo”. lakini inaendelea mbele zaidi kuwaeleza waamini mbadala nafasi ya Kristo kama ni Mwana wa Mungu kulingana na mapenzi na nguvu za Mungu (ANF, Vol.1, p.86).
Msimamo huo ni wa wazi kabisa wa waamini Ubadala wa Uyunitarian wa Kibiblia. Kutumiwa kwa maneno theos na elohim kwenye mundo wa kibiblia kunaeleweka na madai ya uwongo kwa hiyo yameshurutishwa kwamba Wayunitarian hawalitaji kabisa jina Mungu kwa Mwana wa Mungu wakati Shetani anaweza kuitwa kuwa ni mungu wa dunia hii (2Wakoritho 4:4) na Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-9 zinatumia jina elohim na theos kwao wote na kumfanya mmoja kuwa ni Mungu wa mwingine na kumtambulisha Yesu Kristo kama ni Mungu mdogo.
Chuo au Shule ya Waalexandrian na Umodalism
Karibia mwaka wa 177 tunaanza kuona Shule
au Mrengo wa Alaxzandria vikiibuka. Ilianza kwa maandishi ya Athenagoras ambaye
alianzisha kimsingi mkubwa wa kifilosofia kwenye Ukristo kwa kuanzisha itikadi
ya Kimodalism. Alifanya kosa kubwa sana la kiteolojia na aleta au kusababisha kuwe
na tofauti kwenye uelewa kuhusu uhusiano ulivyo baina ya Kristo na wana wengine
wa Mungu wa Majeshi. Alikuwa ni Muathenian na mwanafilisofia na ujumbe wake kwa
Mfalme Marcus Aurelius na kwa mwanawe Commodus kulianzisha kazi uandishi wa kitabu
kijulikanacho kama: Mwito kwa Wakristo yaani
Plea for the Christian. Aliwataja wao kama ni “Washindi na
walioziteka Armenia na Samartia, na zaidi ya wanafilisofia wote.” Hivyo anaweka
msingi mkuu wa kuibuka kwa Filosafia ya Kiyunani na kuingia kwenye Ukristo na
kumtayarishia njia Clement wa Alexandria ambaye makosa yake yamejadiliwa katika
Sehemu ya 1 ya 127.
Akaanza maombi
yake kwa mfalme Commodus kwa kuanzia na madai ya uwongo dhidi yao na kwa kuukanusha
Uatheism. Katika sura ya IV
anaweka madai ya kuwa kuna Mungu Mmoja tu. Anadai kuwa Mafundisho ya Kikristo
ni ya imani juu ya Mungu mmoja, yaani ya kimonotheist.
“Lakini kwa kuwa mafundisho
yetu yanamtambua Mungu mmoja, muumbaji wa ulimwengu huu, ambaye yeye mwenyewe hakuumbwa
(kwa kuwa hilo halitakuja kutokea, bali kile kisicho hivyo) bali aliumba vitu
vyote kwa huyo Logos, ambaye ametoka kwake, tunafanyiwa mambo pasi kufikirika
kwa namna mbili zote, huheshimu kuwa sisi sote tumedhalilishwa na kuteswa
kwacho (soma ANF, Vol. II, p. 131).
Hivyo anaanza
tatizo tata la akidai Mungu Mmjoa, wa Kweli ambaye hakuumbwa na Logos ambaye
aliumbwa kutokana na yeye mwenyewe akiwa kama matokeo ya mapenzi yake.
Na ndipo anaanza
kuwajadili au kuwauliza wanafalsafa na misimamo yao kama ilivyo kwa Mungu.
Madai yanafanywa
kwamba kuna Mungu Mmoja wa Kweli aliyekuwepo na asiyewahi kuumbwa na Logos
aliumbwa na yeye.
Tuliona kwamba
Neotus alishutumiwa na watetea dini wa mwanzoni kwa kutangaza kwake kuwa Mungu
alitokau na yeye mwenyewe na akafanyika kuwa mwanawaake mwenyewe. Jambo hili lilianzisha
makosa hayohayo ambalo linapekea Umodalism na hatimaye kwenye Ubinitarian na
kisha Utrinitarian.
Katika sura ya VII
anaitaja dhana ya psuche au nafsi” ambayo ni nadharia ya Socrates na
iliendelezwa kwenye Uplatoni (soma jarida la Mafundisho ya Kisocrati ya Nafsi (Na. B6)).
Makosa haya yalianza
kuweka msingi wa mafundisho ya kizushi ya Umodalisti ambayo yaliibua mlipuko
kamili kwenye sura ya X wakati alipodhaniwa kutangaza, na Watrinitarian katika
Kichwa cha Somo cha Sura, ambayo wao na siye aliyeandika, kwamba Mungu mmoja anaabudiliwa
na Wakristo kama Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.
“Huyu Mungu
mmoja hakuumbwa na wa milele, hauonekani, hapitiki, hashauriwi au kuelekezwa,
hana viwango wala kikomo, na ambaye hawezi kuelezeka kwa kumuelewa tu kwa
kifikra na ambaye haonekani kwa kumulikwa kwa nuru na kwa urembo, na roho, na
nguvu isiyoeleweka na yeye ambaye ulimwengu umeumbwa kwa njia Logos, na kuiweka
kwenye utaratibu au mzunguko wake na kuufanya uwe – nimekwisha onyesha vya kutosha
kabisa. [iwapo kama nikisema “Huyu Logos”], kwa kuwa tunamtambua pia Mwana wa
Mungu. Wala mtu yeyote asidhani kuwa ni upuuzi kwamba Mungu anaweza kuwa na
Mwana… Yeye ni zao la kwanza la Baba, sio kwa kama siyo kwa kuweza kuletwa
kwenye ukweli (kwa kuwa tangu mwanzo, Mungu, ambaye ana mawazo ya umilele
(neous), alikuwa na Logos ndani yake mwenyewe, akiwa tangu tofauti ya milele
pamoja na Logos (logoikos); lakini kwa kadiri alivyokuja na kujitokeza kuwa
anatia nguvu ya kila kitu kilichopo, ambavyo vinalala kama tabia pasipo monekano
wake, na kwenye dunia isiyofanya kazi shirikishi kubwa kubwa zikiwa zimewekwa bile
bila vikuumbusho, vipisi vikubwa kuchanganywa na wepesi. Roho ya Unabii
inakubaliana pia na maneno yetu.
“Bwana”
inasema, amenifanya mwanzo wa njia ya kuielekea kazi zake (Mithali 8:22) Roho Mtakatifu
mwenywe pia, ambaye anatenda kazi ndani ya manabii ambao tunawaamini kuwa anatokana
na Mungu na anatoa maelekezo yake, na anayokea kwake, na anarudi tena kama
mwanaga wa jua. Ni nani basi yeye ambaye hajihusishi kusikiliza wanadamu wanaomnena
Mungu Baba, Mungu mwana na Roho Mtakatifu, na anayetangaza mambo yote mawili,
yaani nguvu kwenye umoja na tofauti zao kwenye utaratibu, uitwao
Atheists?
Wala mafundisho yetu ambayo kwamba yanahusiana na
tabia ya kimungu vikijumuishwa na vipengele hivi; lakini tunatambua pia kwamba
kundi kubwa la malaika na watumishi, ambaye Mungu aliye Muumbaji wa ulimwengu
aligawanya na kuweka vipendele kadhaa kwa Logos huyu, kujikubali wenyewe na
kupangwa kwenye nafasi kadhaa mbalimbali na Logos wake, ili kujihimilisha wenyewe
kuhusu mambo haya ,zna mbingu, na dunia, na vitu vilivyomo ndani yake, na taratibu
nzuri sana za hao wote.”
Makosa aliyoyafanya yaliengemea kwenye midani ya filosofia za Kiyunani. Yalikuwa ni:
1) Kuwepo kwa nafsi isiyoweza kufa
2) Kushindwa ka huyu msaidizi kupatanisha kwa njia ya sadaka ya toba na upatanisho
3) Miungu na wanadamu hawawasiani. Kuna philia tu na eros, wenye mapenzi ya kidugu na kierotiki. Neno Agape ni la Kiebrania liliklotoholewa kutoka kwenye Kiyunani kutoka kwenye Wimbo Uliobora kwenye LXX.
Kwa hiyo Kristo ilimlazimu awe ni sehemu ya Mungu na si aliyo sawa kama walivyo wana wengine wa Mungu na tena ilimpasa kabisa akubali nafasi zao kwenye mfumo wa Mungu. Huu haukuwa ni utaratibu ambao ulikuwa na hata kwenye Kabrasha R ambalo linaunda kile kilichojulikana hapo mwanzoni kuwa creed au ukiri wa imani ya kanisa la Roma katika karne ya pili (Tazama jarida la Chimbuko la Mafundisho ya Imani ya Kikristo (Na. 88)).
Kabrasha R na
maandishi ya Tertullian ni ya Kiyunitarian. Yamejuluishwa kwenye jarida Namba 88
hapo juu. Wanaelezea ka kina imani ya Kanisa ilivyokuwa hadi mwishoni mwa karne
ya pili.
Ni kutokana na imani
ya Alexandiria ambapo tunaona marejeleo ya kwanza yakiibuka mnamo mwaka 180 kwa
kuingizwa kwa neno Trias huko Antiokia.
Athenagoras
aliweka mgawanyiko wa kifilosofia kati ya Kristo na wana wengine wa Mungu na
kuanzisha upinzani au mchuano mkali na wa kikatili kwenye uingizaji wa ibada za
Kibinitarian iliyokutikana kwa waumini waaminifu na watiifu wa vikundi vya dini
potofu ya Attis, Adonis na Osirus, na kutoka kwenye dini za Kimafumbo na za
Siri ambazo zilianzishwa huko Nicada mnamo mwaka 325. Ni kama aina ya
mafundisho ya Kizushi ya Noetian yailiyoshutumiwa na wanafunzi waliofundishwa wa Kismirna.
Kanoni za Nicaea ziliharibiwa na kuchukuliwa kama mafundisho ya kizushi na kwamba
imani hiyo iliondolewa tangu mwaka wa 327 kwa kuwarejeshwa upya Wayunitarian
Wasaidizi ambao kimakosa waliitwa Waarian
au Waeusabians na Watrinitarian wa
siku zilizofuatia. Kurejeshwa kwa Ubinitarian na kuupa mwanya Utrinitarian
kulitokana na kuchaguliwa kwa Theodosius kuwa mfalme wa upande wa Mashariki na
Gratian na usaidizi wake kwa Waathanasians mnamo mwaka 451 kutokana na Baeaza
la Mtaguso wa Kalkedoni.
Makosa ambayo
yaliendeleza mafundisho ya baadae ya kizushi kuhusu Asili ya Mungu yaliegemea
kwenye wazo la kwamba kulikuwa na Mwana mmoja tu wa Mungu aitwaye Yesu Kristo,
aliyekuwa kwa namna fulani wa tofauti na Jeshi la Malaika wengine ingawaje
Biblia inasema, wawili wote kwenye Malaki na kwenye Kiebrania, kwamba sisi sote
tuna Baba mmoja na kwamba uumbaji ni wachimbuko moja. Bibilia inaonyesha kwamba
dhana hiyo ni ya uwongo mkubwa sana.
Kitabu cha Ayubu kimerudia
mara kadhaa kutaja uwingi mkubwa wa wana wote wa Mungu pamoja na viongozi wao
ambao ni Nyota wa Alfajiri ambao walikuwa ni wengi, na wanasemwa wazi sana kwamba
Shetani alikuwa mmoja wao. (Ayubu 1:6, 2:1, 38:4-7).
Kitabu cha Mwanzo
kinatumia neno elohim kwa viumbe wengi
na pia inatumia neno Yahova kwenye takriban
viumbe wanne hivi kwa mpigo. (Tazama mada iliyojadiliwa kwenye jarida la Malaika wa YHVH (Na. 024) na kwenye jarida la Ibrahimu na Sodoma (Na. 091)).
Hivyo tuonaona mafundisho
haya ya kizushi yakiibuka kutoka kwenye mgawanyiko wa Kanisa. Roma ilitaka kuukumbatia
upagani na kwa hivyo maaskofu hapo waliyakumbatia na kuyafundisha mafundisho ya
ibada za mungu Attis huko Roma na za dini za Kisirisiri. Anicetus aliihamishia na
kuiingiza ibada na tamaduni za Easter huko Roma mwaka 155 BK, ambayo nusura
isababishe mgawanyiko wa Kanisa kwa kubishana na Polycarp. Victo aliiwekea
mkazo na msisitizo mwaka 192, dhidi ya Polyrates na kusababisha mgawanyiko wa Kanisa.
Sulala hili imejadiliwa kwa kina kwenye jarida la (Mabishano ya Wakurtodesiman (Na. 277)).
Waungao mkono
Utatu wanawataka Wakuartadesi,am kumuunga mkono na kushirikiana na Ireneous
ambaye alikuwa askofu wa Wasardi na ambaye alikuwa ameuawa. Kudai kwamba
alikuwa ni askofu wa Smirna na, kwa hiyo, inaashiria mafundisho ya Smirna ni ya
uwongo. Pia anarejelea kwenye masalia ya maandiko yake kuwa alikuwa kama ni askofu
wa Attica na Ittica. Nyaraka hizi ni zile zisizofanana kwenye utunzi na
uandishi wake asilia. Polycarp kwenye waraka wake kwa Victor mnamo mwaka 194 (ka
mujibu wa kitabu cha Eusebius, Hist. Eccl. V xxxiv) anamtaja yeye kuwa ni
Mkuartodesiman. Karibia maandiko haya yote yamepotea; hata hivyo, orodha ya
nyingi zake imetunzwa na Eusabius pamoja na madondoo (ibid IV, xiii, xxvi).
Jitabu cha Ensaikolopedia ya Kikatoliki kinaelezea asili mbili za Kristo kwake (C.
E., Vol. X, p. 166) kikidai kwamba Labrynth wa Hippolytus kama ushahidi.
Waraka uliyohifadhiwa
ni Maombi ya Msamaha kwenye Imani ya Kikristo aliyopewa Marcus Aurelius (mnamo
mwaka 170) inawezekana kabisa kwamba Athenagorus aliandika waraka wake wa
kuomba msamaha yapata miaka saba baada ya huu ili kudai mabadiliko ya kimfumo
kwenye Ubinitarian kwenye mawazo na moyoni mwa Mfalme na mwanae.
Ombi hili la
msamaha LISICHANGANYWE na lile ombi la msamaha la Wasyria lililonena na Melito
na linalodaiwa kuwa lilitolewa mbele ya Kaisari Antoninus. Ni ombi la msamaha
kwa Wasyria uliotolwa na Melito. Ulichapishwa na kutangazwa huko Kisyria na kwa
Kiingereza na Cureton, kutoka kwenye Jumba la Makumbusho la MS (C.E. Ibid)
Lightfoot anasemekana kuwa alionea mashaka kwa hakika kabisa wa kile kilichojulikana
kuwa kilitajwa kwenye tangazo la kiserikali la Antoninuso (tazama pia ANF, Vol.
Viii, p, 750 n. 6 na fn. 11). Waraka unaodhaniwa kuwa unamlenga Antoninus kwa
kweli unasomeka Atoninus (ANF, ibid., p. 756, fn. 1). Kipengele cha (1) hata
hivyo kinahusika na kumwabudu Baba:
“Ila kwa wana wema, waambeni hivi: Yupo Mungu, Baba wa wote ambaye hakufanyika
kuwa kiumbe au kuumbwa na hakufanywa, na ambaye kwamba viumbe vyote humtii.
Naye ndiye pia aliyeitengeneza nuru na vyote ving’aravyo ili kuzifanya kazi
zake ziweze kuonana; na anajiamuru kwa uweza kwa kazi zake zote. Kwa kuwa
haijaruhusiwa kwa kiumbe yeyote kukubali kubadilika na kuona. Ni yeyé asiyeweza
kubadilika. Lakini ni kama yeyé na uelewa na umakini wa maneno yake, na
wanakubali kwenye agano ambalo halibadiliki, ‘wanamuona’ Mungu – kwa vile
inavyoonekana kuwa inafaa kumuona yeyé….” (ibid p. 755).
Maandishi haya yanaonekana
kuwa ni ya teolojia ya Uyunitarian wa kibiblia kabisa. Melito amekuwa akitafsiriwa
vibaya na waandishi waliofuatia baadae kwa ombi lake linalodaiwa kuwa ni
mitazamo yake. Origen anamtaja yeyé kama ni mtu wa mrengo wa bua kama: Anthropomorphy,
lakini AA MacEarlean anashikilia kuamini kuwa masalia ya vitu vya Kisyria
yanaonyesha kinyume chake. Vitabu vinne vya Wasyria mara nyingi vimemtaja na
kumsifia Melito lakini mara nyingine pia vimemtaja Alexander wa Alezandria. Kwa
maneno mengine, ni kwamba hawafai ni ipi iliyo halisi na ni ipi isiyo halisi. Maandishi
mengi yaliyotapakaa yamekuwa yakimtaja na kumsifia yeye, na baadhi yake chimbuko
lake ni Zama za Kati (idib pp 166-167).
Usomaji wa karibu
wa dondoo kubwa za maandiko yake unaonyesha ni ya Uyunitarian wa mrengo wa
Kisubordinati. Dondoo zingine za Kisyria zinamtaja yeye kama ni askofu wa Wasardi
(II) ni askofu wa kawaida (IV) askofu wa Attica (V) na kisha ni askofu wa
Ittica (VI). Hakujawahi kuwa na maelezo ya kutosha ya mambo haya (soma ANF Vol
viii, pp 757-758 kwenye maandishi). Yaonekana kuwa ni vigumu sana kwamba alijiita
mwenyewe ni askofu kenye maeneo matatu tofautitofauti kwenye kabrasha moja, ambalo
laweza kuwa kabisa kuwa ni maandishi ya waandishi tofauti tofauti mbalimbali au
huenda ni waandishi waliofuatia baadae.
Malumbano yake yaliyoelezewa
ni kuhusu msalaba (III) ni hata yananguvu zaidi kuliko yale ya teolojia ya
Attis. “Alijiundia mwili yeye mwenyewe akitaka afanane na sisi…….na bado akabakia
kuwa kama Baba; akiendelea kuishi duniani na huku akiijaza mbingu; akiijitokeza
kama mtoto mchanga lakini akiwa hajaiacha asili ya umilele ya asili yake; akiwa
amewekezwa mwili na lakini bado akiwa hajaathiriwa na mazingira
yasiyochangamana na hali halisi ya Uungu wake; akiwa maskini mwenye kuheshimika
lakini akiwa bado hajapoteza utajiri wake; akihitaji akiba kwa uwingi wake
kwakuwa yeye ni kama Mungu …..
Alisimama mbele ya
Pilato huku kwa wakati huohuo akiwa ameketi pamoja na Baba yake..”
Maelezo yake
yanapingana na maelekezo ya Injili zote na maneno ya Kristo, hususan kuhusu mti
wa kunyongea, nay a Agano Jipya kwa wote wawili, yaano Mitume Paulo na Yohana.
Inakanganya maelezo yaliyo kwenye kipengele (II) na pia ikimtaja yeye.
Dondoo moja linamtaja
Melito kuwa kwa kweli anasema: “Yeye aliyetuzaa sisi duniani alizaliwa mtini.
Bwana aliridhia awe na mwili wenye kusikia uchungu na wa kuwa mtupu - Mungu akamtia
kifoni, Mfalme wa Israeli akachinjwa.” (VI. ANF, Vol. VIII, p. 758). Andiko
hili ni rejea ya dhana ya Maandiko Matakatifu kwenye Zaburi 45 na 110 na Waebrania.
Inatoka kwa Melito, askofu wa Ittica. Tunaweza kuwa tunashughulika na Melito
mwingine.
Dondoo zilizofuatia
zilihifidhiwa na Eusebius (kwenye kitabu cha Hist Eccl l c) kwenye ujumbe wake
kwa Marcus Aurelis Antoninus. Dondoo iliyochukuliwa kutoka kenye kitabu cha
Historia ya Mambo ya Kale ya Waalexandria kinasema “Sisi hatupo miongoni mwao
wale wanaoyasujudia na kuyaabudu mawe bali tunamwabudu Mungu peke yake,
aliyekuwepo kabla ya watu wote na na aliye zaidi ya yote, na zaidi sna, sisi
tunamwabudu Kristo ambaye ni anayeonekana kama ni kweli Mungu Neno, aliyekuwapo
tangu jadi”. Hatahivyo, huyu na wengine wamesemekana kuwa ni matokeo ya Alexandria
na yakajulikana baadae kama ni mafundisho ya Waalexandria yaliyopelekea yale ya
Nicaea.
Kutokana na
maandishi haya Wabinitarian wanapinga kuwa Kristo alikuwa na umilele sawa na
bado wengine walitambua dondoo za Melito zinaonyesha kifungu hiki ili kuonyesha
uumbaji wa kimwili kwa kuwa wote wanamtambua na kumjua Mungu wa Pekee na wa
Kweli ambaye ni Baba. Maandiko haya yanapinga kuwa Mungu Baba ni Mungu mmoja,
wapekee na wa kweli na muumba wa vyote. Kifungu IX “Ufunguo” inaorodhesha njia
zote kwamba Kristo amehifadhiwa na akawa anaelezewa kwenye Maandiko Matakatifu.
Uaelewa wa maandiko ya Danieli 7, 9, 13, 22 ulikosewa (sawa pia na ANS idid pp 160-162).
Hata hivyo ni wazi kuwa maandishi yote yanaonyesha kuwa Kristo alikuwa ni kiumbe
aliyekuwepo wakati wa Agano la Kale aliyewatokea Mababu wa imani, na kwa Musa
na kwa Manabii. Neno “vidole vya Bwana” ambalo kwacho sheria au ammri ziliandikwa
ndani yake zilieleweka kama neno la Kristo ni kama lilivyokuwa neno “vidole vya
Bwana” (Zaburi 8:3). Hivyo Kristo alionekana kama “Uwepo wa Bwana” na ni kiuumbe
aliyetajwa katika Bibilia kama “Malaika wa Bwana” yule aliyewatokea Mababu wa
imani na aliyeuonyesha uweza au nguvu za Roho Mtakatifu kwenye Agano Jipya.
Kuna marejeleo ya moja kwa moja kwenye Zaburi 45 kwenye maandiko yanayomwonyesha
Kristo kama msaidizi wa Mungu wa Israeli.
Hivyo hebu turudi
nyuma kwenye haiba yake ya usaidizi ya Zaburi na Waebrania. Ibada kumwabudu
Kristo inapingwa pia kwenye andiko hili. Hata hivyo, ni ukweli unaojulikana
kuwa Makanisa ya Mungu hayakuwa kabisa yakimuomba wala kumwabudu Kristo kwenye
imani na taratibu zao kwa kipindi chote cha miaka 2000 na bado ndivyo yalivyo
hata Makanisa mengine ya Mungu yenye imani thabiti. Neno proskuneo linamaanisha pia wateule kwenye Ufunuo 3:9. Neno “Mungu Neno”
ni “theou logou” linatumia mfumo huo huo kama tunaouona kwenye Yohana 1:18 la
monogenes theos au aliyezaliwa pekee na Mungu (Tazama kwenye jarida la Kwenye Maneno: Monogenese Theos Kwenye Maandiko Matakatifu na Mapokeo (B4)).
Bila shaka kabisa
kwamba Melito alikuwa Mkuartodesiman na sehemu ya Shule ya Wasardi. Hakutokea Smirna
ingawaje pasi shaka kabisa aliwajua wao kwa ukaribu sana. Polycrates anasema
kuwa yeye alikuwa ni Mkurtodesiman. Mafundisho ya Shule ya Smirna kiusahihi
yanajiambua maandiko ya Irenaeus na Hippolytus. Mgawanyiko uliosababishwa na Hippolytus
kuhusu Kristo kutoka kwa Malaika, na huku yakiwa ni makosa, hakufanyi kwa namna
yoyote kupunguza mtazamo wa Kisabinasheni ya Kiyunitarian ya Shule ni kama
tuonavyo hapo juu. Maandiko yalijitokeza kwenye Mabishano ya Wakuartodesiman na
kiwango au mtazamo wa Kanisa kuhusu mafundisho ya kizushi kuhusu Easter
Hivyo sio bahati
mbaya Mafundisho ya Kibinitarian ya wanaomuabudu Attis yaliibuka kuda mfupi
baada ya kuingia kwa Dini ya Easter mwaka 155 kutoka Roma, na yaliingizwa mara
tu kabla ya mgawanyiko wa Makanisa ya Mungu na ya Kanisa la Roma mwaka 192-4
Easter ni jina la mungumke Ishtar liliaminiwa kutumiwa pia kwa majina mengine mbalimbali.
Walifundisha na kuaminishwa kuwa mungu Attis aliuawa siku ya Ijumaa na alifufuliwa
na mungumke siku ya Jumapili. Huo ndio mkururu wa matukio ya ibada za Easter. Haina
uhusiano wowote na Kristo, wala na maadhimisho ya Pasaka.
Tangu mwishoni
mwa karne ya pili tunshuhudia kwamba elimu au teolojia kuhusu Asili ya Mungu ikianza
kuzorota.
Tumewazungumzia wanateolojia
hawa katika Sehemu ya 1 Clement, huko Alendandria, aliendelea mbele na mitazamo
ya Athenagoras ikilindwa na kuhifadhiwa. Makosa ya Athenagoras yalikuwa ni kule
kuiendeleza kikamilifu itikadi ya Kimodalism ya Alexandria.
Waandishi kama
vile Tertullian waliendeleza nadharia kuhusu Asili ya Mungu, ambayo ilielezewa
katika Sehemu ya I. Aliendelea na ujumbe au fundisho la Shule ya Alexandria na
aliiendeleza nadharia ya kwamba Roho Mtakatifu alitokana Baba kwa kupitia Mwana.
Hivyo tunaweza kupinga Ubinitarian wa kweli ulioanzishwa na Tertullian kwa
kuwajumuisha viumbe hawa wawili kuwa Mungu mmoja. Tertullian aliandika kwa
msisitizo mkubwa sana na mitazamo yake inaonyesha kujiepusha na Umontana kwenye
uandishi wa nyaraka zake. Ni yeyé ndiye anayeendeleza malumbano ya kwamba Kristo
alikuwepo hata kabla ya mwanzo wa uumbaji kwa kuwa yeyé ndiye alikuwa “stadi wa
uumbaji” wa Baba na hivyo ni busi kwamba awe alikuwepo kabla ya mwanzo wa
uumbaji. Hata hivyo, kwa vile kizazi cha Kristo akiwa kama prototokos ni mwanzo
wa uumbaji na hoja zake zinakosa mashiko. Anamfanya Kristo kuwa ni utambulisho
wa Mungu. Hoja kama hizi ziko wazi kwenye kazi yote ya uumbaji na inaishinda
imani ya Kibinitarian.
Kama
tulivyojionea katika Sehemu ya I Tertullian alishikilia msimamo wake kwamba kabla
ya vitu vyote kuumbwa Mungu alikuwa peke yake.
“Kwa kuwa kabla ya
kuwepo kwa vitu vyote Mungu alikuwa peke yake – akiwa ndani yake mwenyewe na
kwa ajili yake yeye mwenyewe ulimwenguni, na kwenye anga na kwa vitu vyote.
Zaidi ya yote ni kwamba, alikuwa peke yake kwa kuwa hakukuwa na kitu chochote
nje yake bali ni yeye tu peke yake.
(Adv. Prax. V).
Alishikilia
kuliamini pia andiko hili la kwamba ni Mungu peke yake aliyekuwepo tangu mwanzo
kwenye uwepo wake wa milele. Kwa hiyo makosa ya kwamba Kristo akiwa kama “stadi
wa kazi” kama sehemu ya umilele ya Mungu, dhana hiyo ilianzisha kwa nia ya
kuyashinda malengo ya Uplatoni Mambo leo.
Katika Sehemu ya
I tulichangaza pia maandishi ya Origien ili kuanzisha msimamo wake.
Utrinitarian unajaribu kumjumuisha kweeye Ubinitarian na ni kutokana na makosa
ya kiutafsiri kwenye maandiko yake. Origin alikuwa mrithi wa kiti cha Clement
kwenye Shule ya Alexandria. Aliamini kwamba Mwana wa Mungu ni “mwana wa Muumba
wa ulimwengu (concles VIII, xiv).
Hatahivyo, yeye
aliushuhudia uumbaji wa ulimwengu sambamba na msitari Neo – Platonis na katika
Sehemu ya I aliielezea nadharia yake ya kujumuika na kuwa pamoja tangu umilele.
Hata hivyo, aliamini kwamba Baba, kiteolojia ni wa kwanza kwa Mwana na Mwana
alikuwa ni tunda la Baba. Utangamano huu haukuwa Umodalism kamili lakini fursa
imewekwa kwa ajili ya kuendelea majadiliano kati ya Roma na Alexandria kupitia Umodalism
na Ubinitarian wa Nicaea mnamo 325.
Kwa kufanya kwao
hivyo waliendelea kuingiza na kufundisha mafundisho ya kipagani kutoka kwenye
dini za Kisirisiri za kipagani.
Origen anapendelewa
na ni chaguo la Watrinitarian kwa kuwa kazi yake inakubalika na wao kwenye
mtazamo wao kuliko Mafundisho ya Wayunitarian wanaoamini kuwa Kristo ni Msaidizi
tu mafundisho yaliyokuja hatimaye kupewa jina bandia la Uarian, Ueusebiani na,
baada ya Mtaguso wa Nicaea, wengine kama vile Uariani nusu.
Mafundisho haya
na tafsiri zake potofu yameainishwa kwa kina kwenye majarida yafuatayo:
Uriani na Nusu Uarian (Na. 167)
Usosiniani, Uariani na Uyunitariani (Na. 185)
Vita Vya Wayunitarian na Watrinitarian (Na. 268)
Ubinitariani na Utrinitariani (Na. 076)
Kushamiri Kwa Mtindo wa Uplatoni Mamboleo (Na. 17)
Makuhani wa Attis
walikuwa wanalalamika katika karne ya nne kuwa Makanisa ya Kikristo yameyaiba mafundisho
yao yote na mafundisho yenyewe ni pamoja nay ale mapotofu ya Ubinitarian yaliyokuwa
yakifundisha karibia maeneo yote ya dola hiyo, isipokuwa Uingereza tu peke yake
kukiwemo kuboresha viwango vya maadhimisho ya Easter huko Nicaea. Yapasa
ukumbukwe kwamba Ubinitarian wa Nicaea uliotangawa mwaka 325 ulitupiliwa mbali
pamoja na maaskofu wake ilipofikia mwaka 327 na kanoni zake ziliteketezwa
zikichukuliwa maka upotoshaji. Baadaye ziliandikwa au kutungwa tena huko
Costantinople mnamo mwaka 381. Dola ya Kirumi na mara nyingine hata wafalme
wenye mrengo wa Uyunitarian unaoamini kuwa Kristo ni Msaidizi tu ambao kimakosa
waliitwa Wasrians au Waeusebians na Waathanasians wa Binitarian bandia.
Alexandria ilipewa jukumu juu ya kupangilia kalenda kuhusiana na Easter kuanzia
mwaka 325 na kuhidadhi mfumo na taratibu zote za Easter huko. Uingereza
iliendelea kuwa ya mrengo wa Kuartodesiman hadi mwaka 664. Makanisa ya Mungu
hayakushikilia kabisa wala kuamini Ubinitarian huu mpotobu hadi kufikia karne
ya 20 na mara nyingi walikuwa wakishutumiwa kuwa ni Waarian. Katika baadhi ya
karne fulani fulani mtu yeyote aliyehitilafiana na asikubaliane na mafundisho
ya Kanisa la Roma alitangazwa kuwa ni Mmanichean Ndumila Kuwili pasi kujali
wanachokuwa wanakiamini. Mtu alitakiwa awe ni Mtrinitarian anayeishika Ester na
mwabudu Jumapili na aliyetangazwa kuwa dunia ina umbo la meza na mtu aliye
mhafidhina kwenye mafundisho na imani hiyoi.
Watu wengi, kwa
kweli sasa hawajui historia ya suala hili. Halijali jambo hili katika matawi fulani
fulani kwa kuwa somo lenyewe linawaletea mgawanyiko wanaouona kuwa hauna maana
wala umuhimu kuhusu jambo hili linalotokana na Wahafidhina wa Kiyunitarian
kuliko kukataa tu uwepo wa Kristo gapa duniani kipindi cha kabla ya kuzaliwa
kwake rasmi hadi kwa Waditheist, Wabinitarian na Watrinitarian.
Tatizo halisi
hivi leo, kati ya makundi haya, lilitokana uelewa potofu wa kiteolojia kuhusiana
na mundo na utofauti uliopo kati ya Uyunitarian wa Kibiblia na Uyunitarian wa
Wanamatengenezo Wahafidhina ambao unapinga dhana ya Kristo kuwepo kwake hapa
duniani katika kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi hapa duniani (soma
jarida la Uwepo waUwepo wa Yesu Kristo Duniani Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwakwe
Rasmi (Na. 243)). Uyunitarian wa Kihafidhina
haukuwepo na wala kujulikana kwenye makanisa ya kwanzoni. Ni teolojia ya Wana
Matengenezo ndiyo iliyoanza kufundisha hivyo.
Ni kwa sababu
zote zaidi ya ile Sehemu ya I, na sehemu hii, kwamba Uyunitarian wa Kibiblia
unaoamini Kristo ni Msaidizi ndio mtazamo asilia. Madai kama yale ya Larry
Hurtado, kwenye hitimisho lake kwenye ukurasa wa 114 wa kitabu chake cha One
God One Lord: Early Christian Devotion and Ancient Jewish Monotheism [Mungu
Mmoja na Bwana Mmoja: Msimamo wa Wakristo wa Kwanza na Imani ya Mungu Mmoja ya
Wayahudi], kwamba msimamo wa Wakristo wa kwanza ulikuwa ni wa mwonekano wa
Kibinitarian hayapo sahihi. Mtazamo wake ulitokana na kutoelewa vizuri
Uyunitarian wa Kibiblia. Mwendelezo wa kidogokidogo umekuwa umeondolewa kwenye
vitabu vingi vilivyoandikwa.
Uandishi wa Lavvy
Hurtado umetokea kuungwa mkono kwa miaka kadhaa iliyopita. Yuko sahihi kwa hilo
baada ya Malumbano ya Kuartodesiman, ndani ya Ukatoliki, yaliyoibua na
kuendeleza imani ya Kibinitarian lakini halikuwa ni fundisho la Kanisa la Kwanza
na wala halijawahi kuwa fundisho la Washika Sabato wa kweli. Kuibuka kwake
kulitokana na teolojia ya Wayunitarian waamini Usaidizi wa Kristo hadi kwenye mgawanyiko
uliofuatia wa Malaika kulikopelekea kiasi cha kwamba sasa Kristo ainuliwe juu
zaidi kuliko wana wengine wa Mungu na kumfanya awe tofauti nao wakati msimamo
wa biblia hauungi mkono kabisa wazo kama hilo. Msimamo wa biblia ni kwamba
wateule watakujafanyika pia kuwa elohim pamoja na Mungu akiwa kama kiumbe aliyeenea
na kujizidisha (soma jarida la Wateule Kama Elohim (Na. 001)).
Ubinitarian na
muundo unaojulikana sana wa Utrinitarian una makosa kwa kuwa unapingana na Jopo
lote la Malaika, kwa namna mbili zote, yaani kiroho na kimwili, ili kufamyika
kuwa Elohim.
Maandishi ya wanateolojia
wa kanisa hayakutoa ushahidi wa kuushuhudia Ubinitarian hadi wakati imani ya
Eastern na harakati zake vilipochukua nafasi na kuingizwa huko Roma na mafundisho
ya Attis yalianza kuingizwa na kukubalika huko. Licha ya kwamba Ubinitarian
haukuwa umeonekani kabisa kwenye maandiko ya kanisa hadi yapata mwaka 177 BK na
sio kabla ya 155 BK. Hayakuwa kabisa mafundisho ya Wakuatodesimam.
Msimamo wa
Bibilia, ni wa namna zote mbiili kama ilivyoeleweka kwenye imani ya Kiyahudi
pamoja na Kanisa la Kwanza, ni kwamba ule wa Mungu Aliye Juu sana (Elyon) akiwa
na Mungu mdogo wa Israeli ambaye kupitia kwake anatenda kazi zake. Waebrania
wanafanya tofauti nyingi kati ya viumbe hawa na neno “wana wa Mungu” linasambaa hadi kwa Jopo la Malaika. Wayahudi wanaielewa
vyema tofauti hii na tunapolisoma jina la Mungu Mmoja wa Kweli Yahova (SHD
3069) wanalisoma elohim na wanapilisoma
Yahova kwa maana ya Mungu msaidizi wa Israeli (SHD 3068) wanasoma adonai. Wamelibadili jina hilohilo la Yahova
na kuwa Adonai kwenye sehemu 134 kwenye maandiko ya Agano la Kale. Tunarekodi au
tarifa za mabadiliko haya. Mambo haya yameandikwa na kuainishwa kwa kina kwenye
majarida mengi sana.
Ni suala la
mashiko halisi kwamba kila tendo la kuwazaa wana wa Mungu kwa Mungu, kumtumia
Roho Mtakatifu, ni tendo la uumbaji wa Kiroho. Kristo ndiye Stadi wa Uumbaji wa
Mungu (Tazama majarida ya Satadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na.
229) na lile
la Jinsi Mungu Alivyofanyika Kuwa Familia (Na. 187)).
Makanisa ya Mungu
yanayozishika Sabato yamedumu kuwa ya mrengo wa Kiyunitarian kwa enzi na enzi
zilizopita na yamekuwa yakiteswa na Watrinitarian kwa ajili ya kuamini kwao
hivyo. Amekuwa wakiitwa kimakosa majina ya Waarian na Waeusebian au majina mengine
mengi ili kupotosha kuendelea kwa mafundisho yao. Hakutoka rekodi ya wao kuwa
Wabinitarian hadi ilipofika karne ya 20 (tazama jarida la Utendaji Kazi wa Amri ya Nne Kwenye Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato
(Na. 170)).
Ubinitarian halikadhalika,
teolojia ya Kitrinitarian, hawaelewi au kuutambua Uyunitarian wa mrengo wa
kuamini kuwa Kristo ni msaidizi katika teolojia ya Bibilia na kutokana na Kanisa
la Kwanza. Wanatafuta pia kuanza kusema kwamba Ubinitarian ulikuwa ni teolojia
iliyoanzishwa na kufundishwa na imani iliyoibuka katika karne ya ishirini chini
ya H. W. Armstrong wakati haikuwa hivyo. Wanatafuta kukwepa kukosolewa kwa
Utrinitarian kuliko kuelewa tu kuwa haikuwa sahihi na teolojia ilikuwa ikiwayawaya
tu kutoka kwenye ile iliyo sahihi ya Uyunitarian unaoamini Usaidizi wa Kristo
hadi kwenye Uditheism. Ni azi kabisa kwamba wamemuita kwenye kundi la mchungaji
wa vinyago au sanamu wa kwenye unabii.
Teolojia ya
Makanisa ya Mungu katika karne ya ishirini ilikuwa ni ya Uyunitarian unaoamini Usaidizi
wa Kristo kwenye Kanisa la Mungu (La Siku ya Saba) au linajulikana kama Church
of God (Seventh Day) kwenye Mkutano Mkuu wa Halmashauri ya Kanisa huko Caldwell
nchini Marekani na waliishika kalenda sahihi inayoanzia kipindi cha mpito cha
kutoonekana mwezi, ni kama yalivyofanya makanisa yaliyokuwepo kabla yao. Walishambuliwa
kuwa ni Waarian, wakati hawakuwa hivyo, wakipewa maana na tafsiri ya
Utrinitarian, lakini hiyo ilimaanisha kidogo. Upotoe wa Ubinitarian uliingia kwa
kupitia kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Kanisa huko Denver nchini Marekani
na hatimaye ulitangazwa rasmi na wao mnamo mwaka 1995 kama sehemu ya kuidunisha
na kuipuuza teolojia ya Makanisa ya Mungu iliyokubalika na kuanza kufundishwa
kwenye makanisa ya lililokuwa likijulikana kama Kanisa la Mungu Ulimwenguni
kote (WCG)
na kwenye Uadventisti kabla yake. Uadventist ulishuka kiwango chake tangu mwaka
1931 baada ya kifo cha Uriah Smith. Ulikuwa ni wa mrengo wa Kiyunitarian hadi mwaka
1931 na hadi kufikia mwaka 1978, Kanisa la Waadventist Wasabato lilitangaza
rasmi kuwa limeachana na kuamini Mungu mmoja na badala yake limejiunga rasmi na
wamini Utatu na kuwa rasmi la Kitrinitarian.
Imani na uongozi wa
Kanisa hili la WCG haikutangaza au kubainisha kuwa Kristo alitokana na Mungu,
kama ni sehemu yake mwenyewe kama alivyokuwa amependekeza Athenagoras hapo juu
na waabudu Attis waliamini. Kwamba imani ya kanisa la WCG, katika miaka
iliyofuatia lilifundisha kuwa Kristo alikuwa ni Mungu ambaye alisimama katika umilele
wote pamoja na Mungu wa Kweli. Walifundisha kwa kuyatumia vibaya maandiko ya Mika
na Isaya, kuwa alikuwa mwezi wa milele. Hoja hizo kwa kweli ndizo zilitiwa nguvu
na kuwezeshwa na Waprotestanti waamini Utatu (soma majarida ya Mika 5:2-3 (Na. 121) na lile la Isaya 9:6 (Na. 224)). Pia wanatangaza kuwa Mungu na Kristo walikuwa na mjadala na mmoja akakubali
kuja hapa chini ili kuwa mwana wa mwingine. Matazamo huu mpotofu wa Kiditheist
ulifundishwa kwenye kipindi chote cha miaka iliyofuatia ya H. W. Armstrong na mwanzoni
mwa uongozi wa J. Tkach Sur. Mnano mwaka 1991, ilichapishwa kwenye jarida rasmi
lililokuwa linamilikiwa na kanisa hili la WCG, la The Good News [Habari Njema], na ikafundishwa kwenye mahubiri
ingawaje sura ya 8 ya jarida lililojulikana kama Kozi Ndefu ya Biblia lilimtaja
kuwa ni Mungu Mmoja wa Kweli, Eloah, aliwaumba elohim, fundisho ambalo ni la dhana
ya Uyunitarian wa kibiblia. Makanisa yaliyoibuka kutoka kwenye lililokuwa WCG yanajitahidi
kujiweka mbali na mafundisho ya kizushi ya Uditheist huku yakidhania kwamba
Ubinitarian unakubalika. Kwa hiyo ndipo wanatumia hoja za WaProtestanti Waamini
Utatu wasio na habari au walaghai ili kuunga mkono hoja na mitazamo yao.
Ni kama kilivyo
kifungu cha zamani: “Hebu niambie kile unachokitaka ili kuthibitisha nami
nitakuelekeza mahali utakapoupata ukweli” na siyo hati ya ufaulu wa masomo.
q