Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[128]

 

 

 

 

Melkizedeki

(Toleo La 2.0 19950729-19980907-20110618)

 

Utambulisho wa kiumbe anayejulikana kuwa ni Melikzedeki kila mara limekuwa ni tatizo kwa wanafunzi wengi wa Biblia. Jarida hili linaangalia mapokeo au desturi za kikuhani pamoja na kuonyesha tambulisho tarajiwa na sababu iliyo nyuma ya harakati za mtu huyu. Maana ya ukuhani wa Melkizedeki unaweza kueleweka vyema kutokana na jarida hili.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

 (Hatimiliki © 1995, 1998, 2011 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Melkizedeki


Utambulisho wa kiumbe anayejulikana kama Melkizedeki limekuwa ni somo linalochukuliwa kama la kukanganya kwa zaidi ya miaka kadhaa sasa. Wengine wameulinganisha utambulisho wa Masihi kwa Melkizedeki; wengine wamemjumuisha yeye na mababa wa zamani wa imani. Kutenganisha uwezekano wa utambulisho huu yatupasa kutathimini maandiko yanayofanana na kushabihiana na mtiririko wa kihistoria uliopo ambao aliishi kwao. Matokeo muhimu ya uwiano ya kuja na kuzaliwa kwa Masihi pia ni jambo linalohitaji kutiliwa maanani, iwapo kama, kwa mfano, mtu atafananisha na utambulisho wa Masihi. Kwa maneno mengine, kama mtu atang’ng’ania kusema kwamba Melkizedeki ni Yesu Kristo, inapasa ipimwe dhidi ya maandiko yanayofanana na madhara kwa wokovu wa mwanadamu kwa tukio kama hilo la ukuwili. Kipindi hiki kilikuwa pia ndani ya kipindi zama cha mababa wa imani walioishi baada ya gharika kuu ya ulimwengu wote. Hakuna shaka maana nyingine yapasa itoholewe kutoka kwenye vipaumbele.

 

Kipindi zama cha baada ya gharika kilishuhudia ulimwengu ukiwa na lugha na usemi mmoja na ukiwa chini ya kuhani mmoja. Mtazamo wa Kiyahudi ulikuwa kwamba kuhani huyu alihudumu huko Salemu chini ya Melkizedeki. Alama au utambulisho wa Melkizedeki umekuwa ni utata. Melkizedeki, kwa mujibu wa Midrash, alionyeshwa na Shemu (Rashi: soma kitabu cha Soncino).

Kwa hiyo aliitwa hivyo kwa kuwa alikuwa mfalme (melech) wa mahali palipokuwa mashuhuri kwa utakatifu wake (tsedek) [kwa mujibu wa Abraham ibn Ezra] N[achmanides] sawasawa kabisa: Alitawala mahali ambapo siku moja lilijengwa Hekalu ndani mwake ambamo kulikuwa na Maskani ya Takatifu ambayo iliitwa tsedek. Midrash inadondoa neno hili kuwa linamaanisha Yerusalemu kwa ujumla, kama  ilivyoandikwa, Haki na Utakatifu ulikuwa ndani yake (Isaya 1:21) (kwa mujibu wa kitabu cha Ufafanuzi cha Soncino hadi Mwanzo 14:18).

 

Melkizedeki alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana. Nachmanides anadumu kuamini kwamba ilikuwa ni:

Abrahamu tu ndiye aliyejua kwamba hiki ndicho kilichompelekea yeye ampe zaka yake. Aliye juu Sana maana yake ni aliye juu ya miungu yote  (N) (Soncino).

Rashi anasema na kuamini kwamba mkate na divai alizotoa Melkizedeki na kumpa Ibrahimu vilikuwa ni viburudisho kutokana na uchovu wa mapiganoni akawaacha huru wafungwa. Kw hiyo alionyesha kwamba alimzaa Ibrahimu na asione uchungu kwa kumtoa mwanae achinjwe (viz. Cherdorlaomer, etc.) (soma kitabu cha Soncino). Mtu huyu ni wa muhimu pasi kujali mstari wa uzao wa waliohusika. Ni muhimu sana kupewa heshima ya moja kwa moja ya uzao ya walipatwa na madhira. Maana ya mkate na divai aliyopewa Ibrahimu kulihusiana moja kwa moja kwa maana ya Mkate na Divai ambayo ilikuwa adilifu kwenye Mkate na Divai iliyoanzishwa na Masihi kwenye Meza ya Bwana. Tukio hili liliangalia mbele kwenye mfano wa kuwepo kwa Roho Mtakatifu kama ilivyokuwa inahudumu kwenye ukuhani mpya wa mfano wa Melkizedeki kama ulivyoanziashwa na Masihi.

 

Ukweli wa kwamba Melkizedeki aliweka taswira ya tukio hili hailazimu kumaanishi kuwa yeye ni Masihi. Kwa kweli, kama angekuwa hivyo, kuna sababu zote za matatizo kwenye dhana ya sadaka isiyo na doa au dhambi ya Masihi. Je, yeye alizaliwa? Alikuwa ni wa jinsia ipi, ni mwanaume? Na kama ni hivyo, je, alikuwa ndiye yule aliyezaliwa na mwanamke bikira? Kwa hakika hakuwa ni wa mstari wa uzao wa Daudi. Na kama alikua ni malaika, hiyo itakuwa ina maanisha nini na utaala wa Salemu kwa wakati ule? Je, ulikuwa ni ukuhani wa namna gani ule? Kwa nini ukuhani wa malaika haukuandikwa mahali popote? Ni nini matumizi aliyokuwanayo malaika kwa zaka za vita? Na kama hakufa, basi tutasemaje kuhusu maandiko ya Yohana kuhusu fundisho la Mpingakristo? Matatizo ya msingi yalielezewa kuhusu uhusiani wa Masihi na Melkizedeki ni ulivyo mkubwa.

 

Somo au fundisho kuhusu Melkizedeki mara nyingi halieleweki sana, hasa ni kwakuwa mtiririko na maana za hadithi yenyewe haieleweki sana. Kanisa la Mungu, kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu mbili, haikuwashikilia mtazamo usioeleweka kwenye somo au fundisho, na ushauri kuhusu suala la hayakuonekana kuwa kama ni suala la kimafundisho, au ni kitu muhimu kwa wokovu. Kwa hakika, hadi kwenye hatua zisizovumilika ya Kanisa kwenye Krne hii, suala halijawahi kuonekana kama kuhalalisha uthibitisho na uimara wa kimafundisho. Itasaidia kutathimini historia ya kuijenga historia.

Mwanzo 11:1-32 1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja. 2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko. 3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa. 4 Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote. 5 Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu. 6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. 7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao. 8 Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji. 9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote.

Hapa tunaona kutawanyika kwa watu kutokana na mfumo uliokua umewekwa huko Babeli, chini ya serikali iloyoanzishwa na Nimrodi huko na Akkadi, Ereki na Kalne. Kutoka huko aliujenga Ninawi, Rehobothi na Kala (Wanzo 10:10-11). Kuhani wa Mungu hatahivyo, alikuwa Shemu, akiwa ni mwana wa Nuhu. Nuhu aliishi miaka 350 baada ya gharika kuu (Mwanzo 9:28) na alifariki akiwa na umri wa miaka 950 (Mwanzo 9:29). Shemu alikuwa ni kiini au mtumainiwa aliyewekwa kuhudumu kipindi cha baada ya gharika kuu.

 

10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu; Shemu alikuwa mtu wa miaka mia akamzaa Arfaksadi miaka miwili baada ya gharika.11 Shemu akaishi baada ya kumzaa Arfaksadi miaka mia tano, akazaa wana, waume na wake. 12 Arfaksadi akaishi miaka thelathini na mitano, akamzaa Sela. 13 Arfaksadi akaishi baada ya kumzaa Sela miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake. 14 Sela akaishi miaka thelathini, akamzaa Eberi. 15 Sela akaishi baada ya kumzaa Eberi miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake. 16 Eberi akaishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi. 17 Eberi akaishi baada ya kumzaa Pelegi miaka mia nne na thelathini, akazaa wana, waume na wake. 18 Pelegi akaishi miaka thelathini, akamzaa Reu. 19 Pelegi akaishi baada ya kumzaa Reu miaka mia mbili na kenda, akazaa wana, waume na wake. 20 Reu akaishi miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi. 21 Reu akaishi baada ya kumzaa Serugi miaka mia mbili na saba, akazaa wana, waume na wake. 22 Serugi akaishi miaka thelathini, akamzaa Nahori. 23 Serugi akaishi baada ya kumzaa Nahori miaka mia mbili, akazaa wana, waume na wake. 24 Nahori akaishi miaka ishirini na kenda, akamzaa Tera. 25 Nahori akaishi baada ya kumzaa Tera miaka mia na kumi na kenda, akazaa wana, waume na wake. 26 Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani. 27 Na hivi ndivyo vizazi vya Tera. Tera akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani. Harani akamzaa Lutu. 28 Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika Uru wa Wakaldayo. 29 Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori aliitwa Milka, binti Harani, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska. 30 Na Sarai alikuwa tasa, hakuwa na mtoto. 31 Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko. 32 Siku za Tera zilikuwa miaka mia mbili na mitano; Tera akafa katika Harani

Kuna idadi kadhaa ya vipengele vya muhimu vinavyoibuka kwenye andiko lililoko kwenye Mwanzo 11. Cha kwanza kinahusiana na umri wa Shemu na wengine. Kutoka kwenye maandiko tunaanzisha tarehe au vipindi vya baada ya gharika kuu, tarehe za kuzaliwa na kufa kwao. Miaka yenyewe ni ya kipindi chenye urefu mkubwa sana. Zama hizi maalumu hazikubaliki kuwa ni vipindi vya wazi sana kwa nyakati za sasa. Kwa kweli, kudhania kwamba nyakati maalumu hizi ni za kweli ni za kukaribisha kebehi. Hata hivyo, waamini kuona kwa macho yao hawawezi kuwanayo wakati wote kwa namna zote mbili. Kama Biblia ni ya kweli kihalisia na Melkizedeki alikuwepo ndipo vipindi hivi maalumu na vya aina yake navyo ni vya kweli pia na Shemu ndiye mlengwa au masimamizi. Hadithi za mataifa yanayoizunguka Kanaani huko Mashariki ya Kati ambayo yalionyesha taswira pia hadithi zihusuzo kuanzishwa kwa miji. Tabia hizi zilipaswa pia zionyeshwe mwelekeo kwenye hadithi za mataifa, huenda kwa majina mengine. Yapasa ikumbukwe kwamba majina yalikuwa na maana na majina waliyopewa mababa wa imani wa zamani ambayo sio lazima sana yafanane na yale waliyojulikana kwayo kwenye nchi zingine. Kwa mfano, Nuhu alijulikana kwenye Zama Maalumu ya Gilgamesh kama Uta-Napishtim (aliitwa kuwa wa mbali sana) (soma kitabu cha Budge, cha: Babylonian Life and History [Maisha ya Wababeloni na Historia];, 2nd edn., London, 1925, pp. 92ff.).

 

Kuna miingiliano mikubwa sana zilizoko kwenye hadithi au ngano za Kimisri kuhusiana na hadithi au habari ya Shemu kwenye nafasi yake kama muangamizaji wa dini potofu na kikengeufu ya Wamisri. Mambo haya yote yanakanganya sana kwa kazi hii na inapasa yashughulikiwe na mahali penginepo. Hadithi au ngani wa Kimisri ambazo zinamwonyesha Shemu ni hadithi ya Typhon, kaka yake Osiris, ambaye aliiamuru serikali ya Misri na kujaribu kuanzisha mtindo wa Kimisri kuwa ni kitu cha kuigwa na kutawala ulimwenguni kote. Typhon anaonyeshwa kwa mwonekano wa kama mtenda maovu aliyepangilia mbinu chafu na hila kwa washirika sabini na wawili. Pamoja nao, alimkinga au kumlinda Osiris kwenye kifua kwa udanganyifu na kumtupia kwenye mto Nile. Maana yake hapa ni kwamba tarakimu hii ya sabini na mbili inahusiana na Baraza la Utawala la Mungu.

 

Baraza la Sanhedrin lilikuwa la jumla ya watu sabini na mbili; hata hivyo, mara zote lilikuwa na wastani wa watu sabini na mbili kwa ujumla na baadae walijumuisha na Nasi. Masihi aliwatuma wale sabini baada ya kuwachagua na kuwateua (Luka 10:1). Walirudi na furaha, wakisema kwamba hata mapepo wanatutii (Luka 10:17). Mamlaka yalihamishiwa hapa kwenye Kanisa. Kwa matukio yote mawili, kwenye andiko hili limeorosheshwa kwenye makusi ya Marshall’s Interlinear kutoka kwenye maandiko ya Nestles kama hebdomekonta [duo] au sabini [na mbili]. Kwa hiyo, idadi hii ya sabini ilijulikana kuwa iliendana na nyongeza ya wawili, na kufanya jumla ya watu sabini na mbili. Hili kwa kweli ni Baraz la Elohim. Kwa hiyo, ngano au hadithi ya Osiris na Isis inamuweka Typhon kuwa ni kichwa cha Baraza hili lakini akiwa muovu kama adui wa Misri. (soma kitabu cha Bullfinch’s Mythology, Avenel Books, New York, 1979, pp. 293ff.). kwahiyo Typhon aliweza kusemekana kuwa anashikilia mahala la Kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana akiwa ni kichwa cha Baraza. Alionekana pia kufanana na Melkizedeki. Shemu anaonekana pia kwenye kundi hili. Hata hivyo, ng’ombe dume Apis anahusianishwa pia na Osiris, aliyeaminiwa na kuchukuliwa pia kuwa ni udhihirisho wa roho ya Osiris, na kujihamisha yenyewe hadi kwa kila mrithi Apis. Kwahiyo umaarufu umefungamanishwa kwenye hadithi au ngano za dume la ng’ombe linalichinjwa na ambayo ni dini potofu za kisirisiri. Wote wawili, yani Shemu ambaye ni kama mrithi wa Nuhu na wa dunia mpya, na Masihi, wana uhusiano unaofanana kwenye hadithi hizi. Kwa hiyo, Melkizedeki angeweza kuonekana akiwa ni kama anahusiana na wote wawili, Shemu na Masihi. Imani ya kiyahudi ilimuona yeye kama Shemu kwa sababu ya muonekano wa moja kwa moja. Waessene yawezekana, na kwa kweli, walifanya, kumchukulia kimfano yeye kama Masihi na Mikaeli.

 

Shemu aliishi baada ya gharika kuu kwa miaka 502 na maisha yake yana maashirio ya utawala kwa mataifa. Tumeandika jedwali kama ifuatavyo:


 

 

Mababa

Umri wa kumzaa motto

Kuzaliwa

Kufa kwake kwenye miaka ya kabla ya gharika kuu

Shemu

100

 

Gharika + 502

Arfaksadi

35

Gharika +   2

Gharika + 440

Shalaki

30

Gharika + 37

Gharika + 470

Eberi

34

Gharika + 67

Gharika + 531

Pelegi

30

Gharika+101

Gharika + 340

Reu

32

Gharika+131

Gharika + 370

Serugi

30

Gharika+163

Gharika + 393

Nahori

29

Gharika+193

Gharika + 341

Tera

70

Gharika+222

Gharika + 427

Harani

Nahori

Abramu

 

Gharika +  ?

Gharika +  ?

Gharika+352

Kabla ya Gharika + 296.


 

Mgawanyo wa mataifa ulitokea wakati Ibrahimu alipokuwa na umri wa miaka 48, alipokufa Pelegi miaka 340 baada ya gharika kuu (kwa mujibu wa kitabu cha Seder Olam Rabbah, Ch. 1).

 

Abramu (Ibrahimu) aliondoka Harani baada ya kifo cha Tera kipindi cha baada ya Gharika + 427 (mwaka 1921 KK kwa MT). alikuwa na umri wa miaka sabini na tano (Mwanzo 12:4). Hatuna uhakika kama mababu walikuwa wangali hai bado wakati alipokufa Tera na uingiaji wa Abramu huko Kanaani walikuwa Shemu, Arfaksadi, Shalaki na Eberi. Shemu alikuwa ni mkubwa wa kuzaliwa. Kwenye Mwanzo 9:26, Yahova (au Yehova) anatajwa kuwa ni Mungu wa Shemu, na Yafeti aliyeishi hemani mwake. Shemu ndiye anayebarikiwa hapa ingawa Yafeti ndiye mkubwa (Mwanzo 10:22). Kwa hiyo, Shem ndiye kuhani wa Mungu Akiye Juu Sana kipindi cha Ibrahimu. Mgawanyo wa wengine haujulikani, lakini Shemu aliwazaa Arfaksadi na Elamu na (ambao walijiengua baadae na kujitokeza kuwa Waashuru). Ufalme wa zamani wa Elamu, wakati ulipoungana na falme zingine, vikaunda chimbuko la dola ya Waashuru.

 

 

Kuhamahama kwa makabila kunaashiria kwamba mgawanyo wa mataifa kwenye miji na maeneo kunapunguza uwezekano wa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana huko Salemu kuwa ni huyu Shemu, au Arfaksadi, aliyepewa yanayojulikana kuwa ni makazi ya wana wengine. Arfaksadi alifariki kwenye mwaaka baada ya Gharika wa + 440 (1908 KK kwa hesabu ya miaka ya MT) kwa hiyo ni kama tu kwamba mababu walikuwa wangalipo bado na mkubwa ni yule aliye wa tofauti nao au aitwaye Mfalme Wangu Mtakatifu, ingawaje Salaki au

 

 

Eberi wana uezekano huo bado. Shemu ameitwa ni baba wa wana wote wa Eberi (Mwanzo 10:21). Hivyo inawezekana kwamba neno Waebrania lilienea mbali na Waisraeli hadi kwa watu wengine waliohusiana nao. Hili ni fundisho kwa haki yake yenyewe.

 

Baraka za Ibrahimu alizopewa na Melkizedeki kwenye Mwanzo 14:20 zinaelezwa (na Rashi) kuwa zilikuwa ni Baraka za kwanza kupewa Ibrahimu kwa kitendo hiki cha kupigana vita, na kisha Mungu kwa mumsaidia kwake yeye. Ukweli wa kwamba Ibrahimu alitoa zaka yake vyote alivyokuwanavyo unaonyesha kwamba uzao wake wangetoa zaka kwa makuhani (kwa mujibu wa Nachmanides). Zaka ilikusudiwa kuwa ni kama sadaka ya shukurani kwa Mungu, na kuhani pekee aliyestahili kuzipokea ni Melkizedeki. Tafsiri ya kimapokeo ya Kiyahudi, kwa hiyo, ilikuwa ni kwamba Melkizedeki alikuwa ni Shemu na kwamba huduma ya kikuhani ya baada ya gharika iliwekewa makao yake makuu huko Yerusalemu.

 

Melkizedeki kama Masihi

Madai ya kwamba Masihi alikuwa ni Melkizedeki yanapotosha usahihi wa kilichokusudiwa na maandiko ynayotanabaisha mstari wa vizazi. Kulikuwa na mtazamo halisi wakati wa Kristo kwenye baadhi ya madhehebu ya Kiyahudi, kama tunavyoambiwa kutoka kwenye Gomgo zilizogunduliwa kwenye Bahari ya Chumvi maarufu kama the Dead Sea Scrolls, kwamba huyu Melkizedeki alikuwa ndiye Masihi. Mtazamo huu pia ulijumuishwa na dhana ya kwamba Masihi alikuwa pia ni Malaika Mkuu Mikaeli. Mtazamo wa kwamba Melkizedeki alikuwa Masihi yaonekana kuwa umetuama kwenye ukweli wa kwamba Masihi alipasa aje kutenda mambo mawili. Hii inaweza kuwa imeelezewa na idadi kubwa ya unabii, lakini la msingi zaidi ni huduma ya kuhani mkuu katiku ya Upatanisho, ambapo kulikuwa na ukuwili wa kimavazi, ukiwakilisha huduma za kikuhani nay a kusamehe dhambi na maovu yote kutoka kwenye mavazi ya hariri, na kubadilishwa kwa kuhani mkuu na kuwa wa huduma ya kifalme hapo mwishoni, kukimaanisha pia mfalme Masihi. Kwa hiyo ujio wa kwanza ulikuwa ni wa kikuhani na wa pili ulikuwa wa mfalme Masihi. Yuda ilikuwa chini ya kongwa la Warumi na walimhitaji mkombozi. Hivyo huenda wengine waliona kuwa ndani ya Melkizedeki kuna huduma ya kuhani. Masihi alitabiriwa kuhani baada ya aina ya Melkizedeki kutoka kwenye Zaburi 110:4.

Zaburi 110:1-7  Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako. 2 Bwana atainyosha toka Sayuni Fimbo ya nguvu zako. Uwe na enzi kati ya adui zako; 3 Watu wako wanajitoa kwa hiari, Siku ya uwezo wako; Kwa uzuri wa utakatifu, Tokea tumbo la asubuhi, Unao umande wa ujana wako. 4 Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki. 5 Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake. 6 Atahukumu kati ya mataifa, Ataijaza nchi mizoga; Ataseta kichwa katika nchi nyingi. 7 Atakunywa maji ya mto njiani; Kwa hiyo atakiinua kichwa chake.

 

Kutoka kwenye aya ya 1 ya Zaburi tunajua kwamba ni Masihi anayetajwa. Kuchaguliwa kwake hapa ni kwa kuwa kuhani milele baada ya kuwa wa mfano wa Melkizedeki. Haikusema kwamba Masihi ni Melkizedeki.

 

Kutokana na gombo za Dead Sea Scrolls (DSS) (Damascus Rule [Sheria za Damascus] VII hususan pia kwenye maganjo yaliyopatikana pangoni [esp. also the fragment from cave IV]) tunajua kwamba Masihi alikuwa na marejeo mawili; Masihi wa Haruni (au Masihi kuhani) na Masihi wa Israeli (au Masihi mfalme). Gombo hizi za DSS jamii iliamini kwamba walikuwa ni Masihi mmoja (tazama kenye kitabu cha Vermes, The Dead Sea Scrolls in English, p. 49 kwa kuyajadili maandiko haya).

 

Gombo hili la DSS limetoa mkururu wa madondoo kumi na tano kutoka kwenye pango la XI juu ya Melkizedeki. Yalichapishwa mwaka 1965 na A.S. van der Woude. Maandiko yenyewe yapo kwenye aina ya kazi ya wachimbuzi ya madrashi ambayo kwamba utangazaki wa uhuru kuwatangazia mateka katika siku za mwisho (Isaya 61:1):

 

… inaeleweka kama kuwa sehemu marejesho ya jumla ya raslimali kwenye mwaka wa Jubile [Mambo ya Walai 25:13], iliyoonekana kwenye Biblia [Kumbukumbu la Torati 15:2] kama msamaha wa madeni. Mkombozi wa kutoka mbinguni ni Melkizedeki. Anayetambulika kama malaika mkuu Mikaeli, yeye ni kichwa au kiongozi wa ‘wana wa Mbinguni’ au ‘miungu wa Haki’ ns inatajwa kama elohim na el. Maneno haya ya Kiebrania kwa kawaida humaanisha ‘Mungu’, lakini kwa maana halisi maalumu mapokeo ya Kiyahudi pia yanamwelezea elohim kama kimsingi sana anachukuliwa kama ‘mwamuzi’. Hapa Melikizedeki anaonekana kama anasimamia Hukumu ya mwisho na kuhukumiwa kwa mshirika wa mapepo, Beliali/Shetani, Mkuu wa Giza, mahali pengine pia anaitwa Melkiresha’ [soma pia kitabu cha Vermes, ibid., pp. 253,260]. Tukio kuu la ukombozi linatarajiwa kutokea katika siku ya Upatanisho mwishoni mwa mzunguko wa Yubile ya kumi. Maandiko haya asilia yanaonyesha mwanga wa muhimu siyo kwenye umbo la Melikizedeki tu alivyoandikwa habari zake kwenye Waraka kwa Waebrania sura ya vii, bali pia kwenye mwendelezo wa dhana ya Masihi kwenye Agano Jipya kwenye Ukristo wa kwanza. (Kuhusu umasihi na huduma zake soma kwenye kitabu cha G. Vermes, cha Jesus the Jew [Yesu Myahudi], London, 1973, pp. 129-59, 250-56)... Mwaka huo wa Yubile [kila mmoja wenu]mtairudia kila mtu milki yake.  [Walawi 25:13]; na hivyohivyo, Na jinsi ya maachilio ni hii, kila mkopeshaji na akiache alichomkopesha mwenziwe, wala asimlipize mwenziwe wala nduguye; kwa kuwa imepigwa mbiu ya maachilio ya Bwana [umetangazwa]. [Kumbukumbu la Torati 15:2]. [Na utatangazwa kwenye] mwishoni mwa siku kuhusu watumwa kama [Alivyosema, Kuwatangazia uhuru waliofungwa [Isaya 61:1]. Tafsiri yake ni kwamba Yeye mwenywe] atawaunganisha kwa Wana wa Mbinguni na kwenye urithi wa Melkizedeki; [kwa kuwa atapiga] [kura] zao akijumuisha mahala pa Melkizedeki, atakayewarudisha wao huko na atawatangazia wao uhuru, na kuwasamehe [makosa yao] waliyoyatenda kwa maovu yao yote (Vermes, ibid., p. 266).

Na kwa hiyo inaonekana kwamba Melkizedeki alikuwa anachukuliwa kuwa ni Malaika Mkuu Mikaeli na kwamba alikuwa ni Masihi pia ambaye amepewa mamlaka ya kuhukumu. Hii imetuamanishwa kwenye andiko la Zekaria 3:1-10, linaloonyesha pia upinzani wa Shetani kwenye mchakato huu. Mtu huyu pia alijulikana, kutoka kwa hii, kuwa ni Elohimu anayewahukumu watakatifu wake Mungu, kama ilivyoandikwa kwenye Zaburi pale iliposema kwamba:

ELOHIM [Mungu] asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu. [Zaburi 82:1]. Na ilikuwa kuhusu yeye ambaye alisema, (Kusanyiko la mataifa na likuzunguke, Na juu yake uketi utawale. ELI (Bwana) atawaamua mataifa, [Zaburi 7:7-8]. Pia kwa pale aliposema, [Hata lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya?. Selah [Zaburi 82:2], tafsiri yake kuhusu Shetani na roho za kura yake [yeye] alieasi kwa kuziachiliambali sheria za Mungu kuzifanya…Na Melkizedeki atalipa kisasi kwa kisasi cha hukumu ya Mungu…na [atawatoa kutoka kwenye mikono] ya Shetani na kutoka kenye mikono ya [roho za] [kura] yake. Na ‘miungu yote [ya Haki’] watakuja kumpa msaada [ili] kushuhudia [kuangamia] kwa Shetani....(kutoka kwenye kitabu cha Vermes, p. 267).

 

Isaya 52:7 inatumia neno elohim kwa maana ya ujio wa Masihi huko Sayuni (soma Waebrania 12:22-23).

 

Inaonekana kutoka kwenye maandiko ya Vermes kwamba hakukuwa na shaka kwamba maandiko yanayotajwa yalikuwa ya Masihi. Hakukuwa na shaka pia kwamba Shetani alipewa kazi ya nguvu kwenye hukumu. Neno uwingi wake linatumika kuonyesha mgawanyo wa kazi za nguvu takatifu, kwa mujibu wa mchakato wa uliopatikana Hekaluni, wa majukumu yote na vipindi vya kazi kwa kura au kwa uwingi. Baraza la miungu kwa hiyo wanaonekana kuwa ni kama wateule na Malaika watiifu ambao wamekwishapewa uweza. Kuonekana kwa Melkizedeki kuwa ni kama Masihi ndiko kulikoonekana ni kama kuwa na nguvu na mashiko sana kulikopelekea kuishawishi Jumuia inayoamini yaliyo kwenye Gombo la Bahari ya Chumvi wakati wa Kristo, na uhusiano unaokutikana kwenye Kitabu cha Waebrania. Uwiano wa kwenye Kitabu cha Waebrania hata hivyo, inachukuliwa kutoka kwenye andiko la Waebrania 7:6-8.

Waebrania 7:6-8 Bali yeye, ambaye uzazi wake haukuhesabiwa kuwa umetoka kwa hao, alitwaa sehemu ya kumi kwa Ibrahimu, akambariki yeye aliye na ile ahadi. 7 Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa. 8 Na hapa wanadamu wapatikanao na kufa hutwaa sehemu ya kumi; bali huko yeye ashuhudiwaye kwamba yu hai.

 

Andiko hili linaonyesha kwamba mtu huyu alitajwa kama ni mtu asiyekuwa na mstari wake wa uzao. Haijadaiwa kwamba hakuwa na uzao.

 

Tofauti imefanywa kwenye andiko hili, hata hivyo, kwamba zaka zilipokelewa na mtu mwenye damu na mwili. Hapa inadaiwa kwamba zilipokelewa na mtu ambaye ilishuhudiwa kwamba anaishi, huu ni msingi wa uhusiano wa andiko hili na Masihi. Hata hivyo, Waebrania 7:11 inasema wazi kabisa kwamba Masihi alikuja kama kuhani mwingine.

 

Dhana ya kuishi inaweza kutokana na Roho Mtakatifu aliyewapa uzima mababu hawa, kama alivyofanya kwa watu wa nyumbani mwake Daudi. Kwa hiyo, andiko lililo kwenye Waebrania 7:8 linaweza kuonyesha kuwa linataja nafasi ya Roho Mtakatifu kwa Melkizedeki kama ni mmoja wa wateule. Sio lazima kwamba andiko hili liwe linamhusu Masihi.

Waebrania 7:11 Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?

 

Kwa hiyo, kubadilishwa kwa ukuhani kulihusiana pia na kubadilika kwa sheria. Hivyo, Melkizedeki alikuwa ni wa aina yake ambaye alianzishwa tena kwa Masihi na kwa mteule.

 

Ukuhani wa Melkizedeki ni sehemu ya ahadi ya Mungu.

Waebrania 6:17-20 Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati; 18 ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu; 19 tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia, 20 alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki

 

Hapa Masihi alifanyika kuwa kuhani wa milele baada ya aina ya Melkizedeki. Hakuonyeshwa kama kuhani. Yeye ni Kuhani Mkuu milele baada ya hapo. Kwa hiyo, Melkizedeki alianzisha utaratibu. Jesu alikwenda akiwa kama mtangulizi kwa niaba yetu. Kwa maneno mengine, yatupasa sisi pia kuwa makuhani wa aina hiyo.

 

Waebrania 7 inaonyesha uhusiano wa Melkizedeki na ukuhani.

Waebrania 7:1-28 Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki; 2 ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;

.

Andiko hili linaelezea kwamba jina Melkizedeki linamaana zote mbili, yaani mfalme wa Salemu, au mfalme wa amani. Uelewa wa Kiebrania kwa mujibu wa watu wote wawili, Milik na Vermes ni kwamba neno Melkizedeki maana yake ni Mfalme Wangu ni wa Haki (au Utakatifu) na ni mfalme wa Jeshi la nuru. Jina la Shetani ni Melkiresha’ maana yake ni Mfalme Wangu  ni Udhaifu (soma utunzi wa J.T. Milik, wa Jarida la Masomo ya Kiyahudi [Journal of Jewish Studies], 1972, pp. 126-135 na pia utunzi wa Vermes, op. cit., pp. 252-253). Hakuna shaka kwamba tunaelezea kuhusu vita vya Shetani dhidi ya Masihi vitakavyotikea katika nyakati za mwisho kwa mtazamo wa Gombo la Bahari ya Chumvi au DSS.

hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.

 

Anaaminika kuwa hakuna na baba wala mama na asiye na wazazi (apatoor, ametoor, agenealogetos). Hana wala mwanzo, wala mwisho wa siku zake wala misho wa maisha yake, lakini anafanana na Mwana wa Mungu na anaendelea kuwa kuhani milele. Mtazamo wa kimasihi wa andiko hili unaonekana kutuama kwenye mawazo ya kubuni kwamba hakuwa na uzao na kwamba alikuwa ni wa milele. Na kwamba basi alikuwa ni Masihi. Andiko linasema kwamba alifafana na Mwana wa Mungu. Halisemi kwamba alikuwa ni Mwana wa Mungu. Neno lililotumika ni aphomoioo: kufanana kwa ukaribu zaidi, au kufanya ifanane au kufananisha. Kwa hiyo, alifanywa kuwa kama Mwana wa Mungu. Lengo ni sawa tu na kuwepo wa kiumbe huyu, akiwa ni mmoja wa mababu muhimu na mashuhuri wa imani, alithibitika kuwa ni kama Mwana wa Mungu, kwa kuwa wote alikuwa ni wateule, katika roho, na akafanyika kuwa kuhani wa aina ambayo ilichukua nafasi ya Haruni hata ingawaje ukuhani ule wa Haruni ulikuwa haujawepo bado. Andiko linasomeka kwamba alibakia kuwa kuhani wa milele {tazama kamusi iitwayo Marshall’s Interlinear). Neno kuhani aliyeendelea kuhudumu milele limetafsiriwa kimakosa ili kumaanisha uzima tele au uzima endelevu. Hili sio tatizo zaidi ya kuwa tu kwa maana hiyohiyo ni kama wateule wanavyitwa waliolala mauti.

 

Maana ya maandiko haya yameainishwa hapo chini, kwa kuhusianisha na sharia zinazotumika kwenye huduma ya kikuhani.

Basi, angalieni jinsi mtu huyo alivyokuwa mkuu, ambaye Ibrahimu, baba yetu mkuu, alimpa sehemu ya kumi ya nyara. 5 Na katika wana wa Lawi nao, wale waupatao ukuhani, wana amri kutwaa sehemu ya kumi kwa watu wao, yaani, ndugu zao, kwa agizo la sheria, ijapokuwa wametoka katika viuno vya Ibrahimu. 6 Bali yeye, ambaye uzazi wake haukuhesabiwa kuwa umetoka kwa hao, alitwaa sehemu ya kumi kwa Ibrahimu, akambariki yeye aliye na ile ahadi.

 

Andiko hili linasema pia kwamba mtu huyu pasi kuhesabia wazazi kutoka kwao (soma kamusi ya Marshall’s Interlinear) alipokea zaka kutoka kwa Ibrahimu. Hayasemi kwamba hakuwa na wazazi.

 

 Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa. 8 Na hapa wanadamu wapatikanao na kufa hutwaa sehemu ya kumi; bali huko yeye ashuhudiwaye kwamba yu hai.

 

Andiko hili ni andiko muhimu sana kutokana na madai kwamba Melkizedeki hakuwa mwanadamu. Ni madai kama hayohayo yamefanywa na wateule. Hawafi bali wanalala mautini (1Wakorintho 15:6,18).

 

Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi; 10 kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye. 11

 

Kitendo cha kumpa zaka kuhani kilikuwa kinaonyesha kwamba sharia zilizo kwenye torati ya Mungu zilikuwepo na zilikuwa zinaendelea, na kwamba hazikuanzishwa na Musa na makuhani Walawi.

 

Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?  

 

Hapa Masihi anaonyesha wazi sana kuwa ni kama kuhani mwingine wa mfano wa Melkizedeki. Hakuna undani wala uhusiano wowote hapa unaoonyesha kwamba Melkizedeki alikuwa ni kiumbe huyu huyu. Wakayi hili likiwa ni kama lenyewe ndipo kunakuwa na shaka kisodo kwamba mwandishi wa waraka kwa Waebrania basi ungekanganya mwelekeo hasilia. Alichukuwa anajaribu kukifanya ni kusisitiza uhisiano uliopo kati ya Masihi na Melkizedeki, kwa kuwa inaonekana kuwa ni suala muhimu kwamba matarajio ya madgehebu ya dini ya Kiyahudi yaliyokuwepo katika karne ya kwanza yaliwategemea wote wawili, yaani kwamba Mikaeli ni ana haiba zote mbili, yaani kwamba ni Masihi na Melkizedeki. Waraka kwa Waebrania ulifungamanisha uhusiano ndani ili kuonyesha kwamba unabii ulikuwa umetimia kwa Masihi, kuwa ni kama kiumbe aliye wa mfano wa Melkizedeki, na mtangulizi wa huduma ya kikuhani wa wateule wa aina hiyo. Utaratibu au mfano wake ulikuwa ni kwamba hakuzaliwa na wala hakuna na wazazi kwa kuwa wateule walipaswa kuchaguliwa kutoka kwenye makabila yote ya Israeli na hatimaye kutoka kwa Wamataifa, ambao wenyewe amejiunga kwenye makabila hayo wakihudumu kama makuhani. Kwa hiyo, mstari wote mzima wa wateule ulikuwa usio na mama, wala baba, wala uzao kwenye ukuhani. Kigezo cha kuchaguliwa hakikutegemea na mambo kama hayo.

 

 Maana ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike. 13 Maana yeye aliyenenwa hayo alikuwa mshirika wa kabila nyingine, ambayo hapana mtu wa kabila hiyo aliyeihudumia madhabahu. 14 Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lo lote juu yake katika mambo ya ukuhani.

 

Kupanuliwa wigo kwa huduma hii ya kikuhani zaidi ya Walawi umeelezewa na kufafanuliwa wazi sana kwenye andiko hili. Andiko linaelea mbele kwa kumfananisha Masihi na Melkizedeki.

Tena hayo tusemayo ni dhahiri sana zaidi, ikiwa ametokea kuhani mwingine mithili ya Melkizedeki; 16 asiyekuwa kuhani kwa sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili, bali kwa nguvu za uzima usio na ukomo; 17 maana ameshuhudiwa kwamba, Wewe u kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki. 18 Maana, kuna kubatiliwa kwa ile amri iliyotangulia, kwa sababu ya udhaifu wake, na kutokufaa kwake; 19 (kwa maana ile sheria haikukamilisha neno); na pamoja na hayo kuliingizwa matumaini yaliyo mazuri zaidi, ambayo kwa hayo twamkaribia Mungu.

 

Nia ya kuondoa au kufutilia mbali wazazi kama lengo la andiko limefanywa liwe kitu rahisi tu hapa. Huduma ya kikuhani imetokana siyo tu na heshima ya kimwili bali pia ni kwa nguvu ya maisha au uhai usioweza kupatwa na madhara (soma Warumi 1:4). Hivyo basi Roho Mtakatifu alimpa uweza na mamlaka kwa Melkizedeki kama alivyofanya Ibrahimu na mababu wengine wote wa imani, pamoja na Daudi, Waamuzi na Manabii na kuendelea hadi kwa mitume na wateule. Umuhimu wa andiko hili siyo kwenye ukweli kwamba Melkizedeki angekuwa ndiye Masihi, lakini, zaidi ni kwamba ni muhimu sana kama hakuwa hivyo.

 

Na kwa kuwa haikuwa pasipo kiapo, 21 (maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia, Bwana amea pa wala hataghairi, Wewe u kuhani wa milele;) 22 basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi

 

Ni ushuhuda wa Mungu kwamba wateule waliitwaa ofisi. Masihi alipewa ofisi kwa kuahidiwa na Mungu kwa kiapo.

 

Ukuhani wa Kilawi uzifikia kikomo kwa kifo ndipo aliacha kuendelea kuhudumu. Watakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Alio kwenye utaratibu wa Melkizedeki watakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu. Wale wateule wanaufufuo mwema (Waebrania 11:35).

Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae; 24 bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.

 

Mwendelezo wa milele unatokana kwa kupitia kifo hadi ufufuko wa wafu. Ukuhani haujaondolewa kutoka kwa wateule, ni kama ulivyokuwa haujaondolewa kutoka kwa Masihi na kwa mababu wa zamani wa imani.

Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee. 26 Maana ilitupasa sisi tuwe na kuhani mkuu wa namna hii aliye mtakatifu, asiyekuwa na uovu, asiyekuwa na waa lo lote, aliyetengwa na wakosaji, aliyekuwa juu kuliko mbingu; 27 ambaye hana haja kila siku, mfano wa wale makuhani wakuu wengine, kwanza kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za hao watu; maana yeye alifanya hivi mara moja, alipojitoa nafsi yake. 28 Maana torati yawaweka wanadamu walio na unyonge kuwa makuhani wakuu; bali hilo neno la kiapo kilichokuja baada ya torati limemweka Mwana, aliyekamilika hata milele.  

 

Hivyo Masihi alikuwa ni utimilifu au upeo kwenye utaratibu huu mpya wa kikuhani unaoenea hadi kwa wale waliokuwa wamechaguliwa na Mungu, waliomchagua Masihi na kumfanya awe mkamilifu milele.

 

Tumeona kwamba baadhi ya madhehebu ya Kiyahudi yanamchukulia Masihi kuwa ni kama Mikaeli (kutokana na Danieli 12:1). Dhana au nadharia zilizotuama kwenye ukweli wa kwamba ni Mikaeli imedumu kuaminiwa ma Waisraeli, na Taifa la Israeli alipewa Yahova na Mwenyezi Mungu wakati alipoyagawanya mataifa sawasawa na wana wa Mungu (sawa na ilivyo kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8 tafsiri za RSV, the LXX na ya DSS). Jina Melkizedeki lina maana yake, nayo ni: Mfalme Wangu ni Mtakatifu au Mfalme Wangu ni Mwenye Haki (maneno haya haki na utakatifu yanaendana sawasawa) (soma kitabu cha Vermes, cha Dead Sea Scrolls in English [Gombo za Bahari ya Chumvi, toleo la Kiingereza], ukurasa wa 253). Iliadhaniwa pia kwamba Melkizedeki lilikuwa ni jina la kiongozi wa Jeshi la Nuru, ambaye tumeona kuwa ni kazi ya Masihi (kitabu cha Vermes, ukurasa wa 260).

 

Mawazo hayoyote yanafanyika kutokana na maandiko yaliyoharibiwa ya Agano la Amramu. Hivyo ingeweza kuendelea kuaminiwa kwa dhana hii ya umuhimu wa ujumuisha wa Melkizedeki-Masihi kwa Waessene. Hata hivyo, Melkizedeki hadi Masihi wakati kuna tatizo kubwa kuhusu dhana ya kuzaliwa kwake hapa duniani kulikuwa kwa mabadiliko ya kimaumbile ya kutoka aina moja ya kiumbe na kuja kwenye aina nyingine na la sadaka. Sasa tutautazama uhusiano uliopo kati ya sheria na ukuhani.

 

Cheo hiki kinaonekana kuwa ni kama cheo cha kiurithi cha mfalme wa Yerusalemu (au Urusalaim). Mamia ya miaka baada ya Ibrahimu tunakudana na mfalme mwingine akiwa na cheo kama hichohicho, Bwana wa Utakatifu au Bwana Wangu ni Mtakatifu, kipindi cha kuingia kwao Israeli na kuikalia Kanaani wakiongozwa na Yoshua. Ndipo kwenye Yoshua 10:1 tunakutana na Adonisedeki, ambaye ni mwingine tofauti na Melkizedeki, akitawala Yerusalemu. Jina lake la kicheo kwa mwonekano wake wa tofauti, kwa hiyo ni la kurithi na linamuashiria Masihi kwa ubora wa utawala wake kutoka Yerusalemu, na huenda alionekana kwa jinsi hii na Daudi pia. Kwa namna hii pia wateule ni makuhani wa aina ya Melkizedeki, kwa kuwa wanatawala pamojanaye kutoka Yerusalemu wakiwa ni elohimu (sawa na Zekaria 12:8; Ufunuo 7:1-17).

 

Dhana ya Wakristo ya kwamba Melkizedeki ni Masihi inatokana na kutokuelewa kwao andiko la Waebrania 7:3. Neno la kwamba hana baba, mama na wazazi (apator nk.) linakusudia kuonyesha umuhimu wa kumjumuisha kwenye uzao wa Haruni (Nehemia 7:64) kwa huduma ya ukuhani wa Kilawi.

 

Neno lisemalo mwanzo wa siku na mwisho wa maisha linamaana umuhimu wa kuanza kuhudumu au kufanya kazi akiwa na umri wa miaka thelathini na kuacha kufanya kazi akiwa na umri wa miaka hamsini (Hesabu 4:47). Kuhani Mkuu alirithi huduma ya kuhani wakati anapokufa mtangulizi wake. Melkizedeki hakuwa na ulazima huo. Waraka kwa Waebrania unanukuliwa kwenye tafsiri ya kamusi ya Marshall’s Interlinear kwamba alikuwa mwanadamu (Waebrania 7:4). Aliumbwa umbo sawa kama Mwana wa Mungu (Waebrania 7:3) lakini hakuwa kabisa Mwana wa Mungu, aliyekuwa ni kuhani mwingine (Waebrania 7:11). Kwa hiyo wateule wote wanaweza kushiriki kwenye huduma ya kikuhani, wakiwa wamefanyika kama Mwana wa Mungu, pasi kujalisha na uzao wanaotokea, wakiendelea hata milele. Ni kama alivyokuwa Melkizedeki, nasi tunaweza pia kukisia. Waessene walilipotosha andiko kwa maslahi ya kimalipo kama walivyo wahafidhina wa siku hizi. Suala la Wapaulicians ambao pia waliamini kuwa mtazamo huu waliitwa Wamelkizedekiani, lakini walimfanya awe ni tofauti na Masihi kama mwombezi kutoka mbinguni (soma pia jarida la Migawanyo Mikuu ya Makanisa ya Washika Sabato (Na. 122)). Yaonekana kuwa kitabu cha Waebrania kiliandikwa kwa lengo la kusahihisha makosa lakini kwa chenyewe kimejikuta kikirekebishwa kimakosa pia. Midrash anaamini kuwa alikuwa Shemu (Rashi) akiwa mfalme (melek) wa mahala pa haki (tsedek) (kwa mujibu wa Abraham ibn Ezra & Nachmanides). Mahali hapo palikuwa ndipo ambapo hekalu lilijengwa kwa Maskani Takatifu, ambapo Midrash panapachukulia kuwa ni Yerusalemu kwa vyovyote kutokana na andiko lisemalo Haki imewekwa kwake (Isaya 1:21) (ibn Ezra & Nachmanides, soma pia Soncino, linganisha na Mwanzo 14:18).

 

La muhimu zaidi, dhana ya kwamba Baraza la Elohimu lilikuwa sahihi na halipingiki kama litakuwa limeeleweka vyema kwa maandiko ya Agano la Kale yanayomtaja elohim. Mfumo saidizi wa Elohimu umeeleweka kwa upande mmoja, lakini umekosa kueleweka vyema kawa kuahusianisha na Mikaeli na Melkizedeki.

 

Ufunuo 4 & 5 inaonyesha kwamba kundi hili limehesabu viumbe wapatao thelathini wakiwemo makerubi wa nne. Vipande thelathini vya fedha vilihitajika ili kumsaliti Kristo (Mathayo 27:3,9 sawa na Zekaria 11:12-13) kwa kuwa ilikuwa ni uovu dhidi ya mhimili wote wa Uungu. Viongozi wanalaumiwa kwa kusimamia maombi ya watakatifu (Ufunuo 5:8) na Kristo ndiye Kuhani wao Mkuu. Alikuwa ni mshiriki wa baraza la Viongozi aliyeonekana kuwa anastahili kukifungua kitabu cha mpango wa Mungu ili awaokoe au kuwapata watu waliosamehewa makosa yao na kuwafanya wawe ufalme na ukuhani wa Mungu wetu – yaani Mungu wa Baraza hilo na Kristo (Ufunuo 5:9-10).

 

Sadaka ya msamaha wa wanadamu ni sehemu ya marejesho mapya ya nyakati za mwisho, ambayo yatafanyika wakati wa ujio wa pili wa Masihi akiwa Mfalme wa Israeli; ujio wake wa kwanza ulijulikana kama Masihi wa Haruni. Ujio huu wa kwanza wa Masihi ulikuwa ni wa ongoleo la dhambi na wa uanzishaji wa ukuhani wa Melkizedeki. Marejesho ya nyakati za mwisho yaliejulikana kuwa ni upanuzi wa wigo elohim kama ilvyoonyeshwa kwenye Zekaria 12:8. Kwenye marejesho ya nyakati za Mwisho, wakati atakapokuja Masihi huko Sayuni kama ilivyokuwa ikielezewa na kueleweka kwenye Waebrania 12:22-23, mkururu wa matukio yanayohusiana na kuulinda Yerusalemu na kuimarishwa kwa wakazi wake walio kwenye mji huo kwa ajili ya utawala wa Milenia. Tena tazama kwamba Zekaria inaendelea mbele kwa kusema:

Na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu (elomih), kama Malaika wa Bwana [Yehova] mbele yao. (msisitizo umewekwa ili kusisitiza).

Maana yake hapa yalikuwa kwamba Zekaria alipewa neema ya kuelewa kwamba Malaika wa YHVH alikuwa elohim, na kwamba watu wa nyumbani mwa Daudi (ambaye alikuwa amekwisha kufa kitambo) waliungana na wale ambao hatimaye watakuwa elohim, wakiwa kama ni sehemu ya watu wa nyumbani mwa Daudi.

 

Zekaria aliandika mwishoni mwa kipindi cha Biblia, kikiwa ni moja ya vitabu vya mwisho kuandikwa (inadhaniwa ni kama mwaka wa. 410-403 KK, Nyongeza ya 77 ya tafsiri ya Companion Bible inasema hivyo). Uelewa ma mkururu huu kwa hiyo haukupotoshwa kwa kipindi chote kirefu cha ukusanyaji wa maandiko haya.

 

Hitimisho la kwamba ni Melkizedeki haliwakilishi kwa ujumla mtazamo wa Kanisa la Mungu kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu mbili. Imekuwa ikiaminika hivyo na vikundi vingine na baadhi ya madhehebu au dini za Kiyahudi. Inaonekana kuwa Masihi hakuwa Melkizedeki, bali kwamba kuendelea kwa uzima wa milele kwa Melkizedeki kwa kupitia kwenye huduma yake kwa Roho Mtakatifu kumekuwa hakueleweki. Ukeli wa jambo lenyewe sio wa mihimu kwenye imani, wala kiini cha fundisho hili sio muhimu kwa mtu kukubalika kwenye ushirika. Mahala pa muhimu kwenye majukumu ya Masihi huenda kunadhoofisha hoja ya kuingizwa kwa wateule kwenye huduma hii ya kikuhani wakiwa kama elohim tu kuliko kulienekeza jambo lenyewe. Uhusiano wake kwa hakika unatuama kwenye utunzi wa fundisho kwa kutumia andiko lililo kwenye aya moja tu peke yake.

q