Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[131]

 

 

 

 

Siri za Mungu

(Toleo La 1.1 19950819-19981214)

 

Ufunuo wa Mungu unajulikana na kueleweka kama ni Siri za Mungu na watumishi wake wateule. Mfano wa talanta na wa wanawali wenye busara na wapumbavu vimeainishwa pia. Viwango vya ufunuo wa Siri za Mungu vimeainishwa na kuekwa kwa mpangilio maalumu.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki ã 1995, 1998 Wade Cox)

(tr. 2017)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Siri za Mungu


Siri za Mungu zimehawanyika kwenye kile kinachoweza kuitwa kuwa ni viwango au hatua za ufunuo. Hatua ya kwanza imejuluishwa kwenye mafundisho ya msingi ya Uungu, uhusiano wa maisha ya Kikristo, na mambo ya kiunabii yanayoathiri uelewa wetu kuhusu Mpango wa Wokovu.

 

Roho Mtakatifu anatoa uwezo wa kuzilewa ziri za Mungu kwa wateule wake na kuwafabtwa wawe watumishi wanaozitumikia hizo Siri za Mungu.

 

1Wakorintho 4:1-5 Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. 2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu. 3 Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu. 4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana. 5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.

 

Tito 1:7 inawaonyesha wazee (the presbuterous au episkopon) kuwa ni watumishi wa Mungu.

Tito 1:7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mlevi wala mgomvi,asiwe mpenda mapato ya aibu.

 

Makatazo dhidi ya kujipendelea (kujipenda mwenyewe au authade) na ya kutojikweza (orgilon) au kunywa sana mvinyo au kulewa, mandindano au uchoyo wenye lengo au msingi wa kujinufaisha (aischrokerde) yanaonyesha kupendwa na mtu ambaye na kwa yeye ambaye siri hizi zimefunuliwa kwake. Tafsiri ya neno huperatas ambalo maana yake ni msimamo, au mtumishi, kama mtumishi wa Kristo kwenye tafsiri ya KJV yamepotoshwa, au yamekatazwa bila sababu za msingi, utendaji kazi wa mtumishi wa Siri za Mungu na kwenye ukasisi au ukuhani, ambayo siyo maana yake. Wateule wote wamepewa uwezo wa kuzielewa au kuzijua siri hizi kutegemea na uhusiano wao na Mungu katika Roho Mtakatifu. Na hata hivyo, haifai kabisa kuwa mtu asiyebagua kwenye kuelezea au kuzifafanua siri hizi.

 

Siri hizi wamepewa kwa wale waliojitoa na kujikabidhi kikamilifu kwa Mungu katika Yesu Kristo. Hakuna asiyelaumika kabla hajabatizwa. Hiyo haimaanishi kuwa ndicho kinachokusudiwa kwenye andiko la Tito 1:7. Nia na kusudi la kufunuliwa kwa Siri za Mungu ni moja ya kujitoa kusiko na ubinafsi kwenye kazi na wajibu huu.

 

Roho Mtakatifu anafanya kazi pamoja nasi kabla ya ubatizo na ndani yetu tangu tunapobatizwa (soma jarida la Toba na Ubatizo (Na. 52)). Hairuhusiwi kabisa kubatizwa na kisha usijitoe kuifanya kazi ya Mungu katika Yesu Kristo. Mkururu wenyewe umefanywa ni kama kuma ilivyoelezewa kwenye siri hizo, kufundishwa kwenye neno, na kisha kuandaliwa kulifundisha neno. Hicho ndicho alichokimaanisha Mtume Paulo wakati alipoelezea kuhusu maziwa na nyama.

1Wakorintho 3:1-23 Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. 2 Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, 3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? 4 Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu? 5 Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. 6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. 7 Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. 8 Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. 9 Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu. 10 Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. 11 Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. 12 Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. 13 Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. 14 Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. 15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto. 16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi. 18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. 19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao. 20 Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili. 21 Basi, mtu ye yote na asijisifie wanadamu. Kwa maana vyote ni vyenu; 22 kwamba ni Paulo, au Apolo, au Kefa; au dunia, au uzima, au mauti; au vile vilivyopo sasa,au vile vitakavyokuwapo; vyote ni vyenu; 23 nanyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu.

 

Andiko hili la kwenye 1Wakorintho 3 lilikuwa ni utangulizi kwenye mawazo yaliioelezewa kwenye sura ya 4. Kazi yaliyofanya Makanisa ya Mungu katika karne ya ishirini ni kinyume kabisa na kile alichokisema Mtume Paulo; kila moja linadai kuwa yanawafuata wanadamu. Na ndiyo maana kazi hizi zilielezewa kwenye moto wa ushuhuda wa uwongo na kuangamia kwa udhaifu wao wenyewe au dhambi zao. Mateso na majaribu tunayoyavumilia ni kujaribu imani yetu na msingi wetu kwa kuwa sisi tu hekalu la Mungu.

 

1Petro 2:1-5 Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. 2 Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu; 3 ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili. 4 Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima. 5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

 

Msimamo ambao unahitajika unatuweka mbali ma maovu, uladhai, wivu na kusingizia au kuteta. Yatupasa tufanye kazi kwa pamoja. Yatupasa tuwe kama watoto wachanga tukiyanywa maziwa safi ya kiroho ili kwamba tuukulie wokovu. Kristo alikuwa ni jiwe lililohai la kwanza lililochaguliwa na Mungu ambalo kwalo sisi tumeongezewa mmoja baada ya mwingine kwenye ujenzi wa nyumba ya Mungu.

 

Kwenye kila jiwe moja lililohai ambayo ni sisi, wengine wameongezwa. Ili ni budi tuwe wa kweli na imara kwa kuelimika na tusimame pasi kuyumbishwa. Mawe yaliyohai yamepewa pia manabii waliohai (Matendo 7:38) ambayo ni Maandiko Matakatifu, na tumaini lililohai (1Petro 1:3) ambayo ni imani (soma jarida la Manabii wa Mungu (Na. 184)).

 

Hatupaswi tubakie watoto wachanga tu kila wakati katika Kristo. Yatupasa tuendelee kukua kutoka kunywa maziwa na kula nyama.

Waebrania 5:5-14 Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. 6 kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani wa milele Kwa mfano wa Melkizedeki. 7 Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu; 8 na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; 9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii; 10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki. 11 Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia. 12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.

 

Tunaona kwamba Kristo hakujiinua mwenyewe kwa kuwa kuhani mkuu. Alichaguliwa na kupewa maagizo na Mungu ambaye ndiye Mungu wake pia (Waebrania 1:8-9). Na kwa kuwa Kristo alichaguliwa kuwa kuhani na ndivyo hata sisi tumechaguliwa kumfuata yeye kwenye ukuhani huo. Alifanywa mkamilifu kama tunavyotakiwa na sisi tuwe wakamilifu. Tunatakiwa tufanye kazi kwa imani. Tumeagizwa tufanye kazi kwa ajili ya okovu wa wanadamu kwa njia ya mahubiri na kulifundisha neno la Mungu. Lakini kuna bado miongoni mwetu sisi wanaoweza kufanya kazi, lakini wakiwa bado hawana uwezo na wakidumu kunywa maziwa. Udhaifu huu kwenye imani inatokana na makwazo au huzuni zisizotambulika au kwenye uovu na hasira. 1Wakorintho 13 inaonyesha kwamba upendo wapasa uwepo kwa wateule. Ni jambo lisiloruhusiwa kabisa kubatizwa na kisha kujitenga au kuioa kwenye huduma kwenye jeshi la Bwana. Hakuna mtu anayetia mkono wake kulima na kisha kurudi nyuma atakayefaa kuingia kwenye Ufalme wa Mungu (Luka 9:62).

 

Sio kwa bahati mbaya kwamba Mfano wa Wanawali Werevu na Wapumbavu unakafuatia mara tu baada ya Mfano wa Talanta kwenye Mathayo 25.

Mathayo 25:1-30 Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi. 2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara. 3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; 4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. 5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi. 6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki. 7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao. 8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. 9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie. 10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. 11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie. 12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi. 13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.

 

Mfano wa Wanawali Werevu na Wapumbavu unaelezea kwa namna moja kile kilichoelezewa kwenye Mfano wa Talanta lakini ni kwa mwelekeo mwingine. Jambo la kwanza kuhusu wanawali hawa linahusika na mwajibiko binafsi wa kila mtu kwa Mungu akiwa kama bibi arusi wa Kristo ili kuandaliana kila mmoja na mwingine katika Roho Mtakatifu. Ni mtu tu binafsi anaweza kufanya maandalizi hayo. Jambo la pili, na ambalo linahusiana kwenye Mfano wa Talanta linahusu kazi ya kuzaa matunda katika Roho Mtakatifu kwenye Ufalme wa Mungu. Jambo moja haliwezi kuendelea kuwepo pasipo kuwa na lile lingine. Maendeleo ya kiroho ya mtu pasipokuwa na mwingiliano wa pamoja na kazi kwenye imani ni kazi bure au haina maana.

 

14 Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake. 15 Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri. 16 Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano. 17 Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida. 18 Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake. 19 Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao. 20 Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida. 21 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. 22 Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida. 23 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. 24 Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya; 25 basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. 26 Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; 27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake. 28 Basi, mnyang'anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. 29 Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa. 30 Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

 

Talanta zinazoongelewa kwenye mfano huu hazimaanishi talanta au vipawa au uwezo wa mwanadamu tu, pekeyake. Bali zinamaanisha karama za Roho Mtakatifu na nafasi au fursa ya kiutendaji waliopewa wateule na Mungu ambao wanamtumikia kwao na kutimiliza kazi yake. Kila mmoja alipewa kipimo cha utajiri wa Ufalme wa Mungu. Kila moja imewekwa juu yake mwenyewe kazi au wajibu wa upimaki wa kipimo atakaporudi sawasawa na utajiri aliopewa. Wakati mtu anapopewa kiasi kidogo tu ilitegemewa kwamba kiasi hicho kingejumuishwa na nguvu na utajiri wa wale waliopewa dhamana pamoja na usimamiz au ulimzi wa utajiri ili kuwianisha na marejesho ya hesabu hizo. Kwa hiyo kila mtu ambaye yeye mwenyewe hawezi kutimiliza kazi ni lazima waziweke talanta zao kwenye bwawa la pamoja ili kwamba mkakati wa kuwianisha ifikiwe au utimilizwe kutokana kwa kila mshirika wa mwili wa Kristo. Kitendo cha kushindwa kutenda kazi kwenye wajibu wa kila mmoja ili kwamba kazi ifanyika kwa pamoja kunamfanya kila mtu kuhukumiwa na kukataliwa kwenye ufufuo wa pili wa wafu.

 

Wajibu wa wateule ni wa namna zote mbili, yaani wa kiroho na kimwili. Mambo ya kimwili ni ya kifedha. Kwa hiyo matendo ya wote au ya jumla ya Kanisa yamewekwa kwenye utumishi mzuri; hakuna mtu kwa hiyo atakayesimama peke yake na asiisaidie kazi. Kazi imeonekana imesimana imara kutokana na mafundisho yenye uzima kwenye Siri za Mungu na ibada zake.

 

Kutokana na utambulisho wa mafundisho na wajibu wetu bdipo tunaendelea kutoka utumiaji wa maziwa hadi ulaji wa nyama. Nyama ni kwa ajili ya wateule, ambayo inafuatia kutoka kwenye utumiaji wa maziwa waliyopewa kama watoto wachanga, ni nyama ile ile ambayo Kristo aliikomesha kwenye Yohana 4:34-38.

Yohana 4:34-38 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake. 35 Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. 36 Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja. 37 Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine. 38 Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.

 

Chakula cha Kristo au nyama vinavyoelezea hapa ilikuwa ni kazi ya Mungu. Kazi hii ilikuwa ni mavuno ambayo tunashiriki kwayo. Mpanzi na mvunaji wanafurahi pamoja. Kwa hiyo Kristo anavuna mahali asipopanda. Mungu kwa kupitia Roho Mtakatifu anafanya kazi kwa kupitia wateule wanaopanda mbegu kwa kazi ya wengine nasi tunavuna. Sisi tunapanga pia ili kwamba wengine wavune. Kwa hiyo tunashiriki sote kwa furaha tuliyopewa na Kristo. Hakuna kati yetu aliye wa Paulo wala wa Apolo. Ni kama alivyokuwa Paulo, sisi sote tu watumwa (doulos) wa Mungu (Tito 1:1).

 

Yatupasa tujitahidi iwezekanavyo kuiharakisha kazi ya Mungu kwa namna yake. Yatupasa tuzae matunda.

Tito 3:13-14 Zena, yule mwana-sheria, na Apolo, uwasafirishe kwa bidii, wasipungukiwe na cho chote. 14 Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda

 

Hapa tunaona kwamba Kanisa linaonekana kwamba wale waliosababisha mafarakano kwenye kazi kwa kuwafuata watu wanakemewa kwa kuambiwa kuwa wamemsaidia mteule mmoja na Paulo ambaye alichukuliwa kuwa ni wa kundi linguine. Kazi ya Mungu sio ya mtu yeyote ili kwamba hakuna yeyote mwenye mwili atakayejivuna wala kujitukuza (1Wakorintho 1:29). Basi kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu ya msingi wa kazi ya Mungu (1Wakorintho 3:10).

1Wakorintho 3:5-9 Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. 6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. 7 Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. 8 Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. 9 Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.

 

Kila mtu yapasa aangalie jinsi anavyojenga, ila kujenga ni lazima. Haijalishi ni wapi tunapofanya kazi, la msingi tu ni tunafanyaje hiyo kazi. Kwa kweli tusiwafuate watu. Wakumfuata ni Mungu kwenye mafundisho yenye uzima.

 

Siri za Mungu zinafunuliwa kwa hatua moja hadi nyingine.

 

Hatua ya kwanza inahusiana na kumjua Mungu, kuwa ni nani na yupoje. Kujue uwepo wa maovu na asili au tabia zake na madhara ya dhambi kunawaongoza kwenye shauku ya kufanya uamuzi wa kutubu na hatimaye kuelewa umuhimu wa kubatizwa na neema ya Mungu iokoayo. Mchakato huu umeingizwa kwenye misingi endelevu ya maisha ya mtu. Kuuelewa uhusiano uliopo kati ya Torati au sheria na dhambi, na wokovu na neema ni mchakato endelevu na wa kina zaidi. Kushindwa kuyaelewa au kuyajua masuala ya neema ni sababu ya msingi ya mtu au watu kujihesabia haki.

 

Hivyo Mpango wa Wokovu ni jambo muhimu na la msingi kuelewa kupitia kwenye vipindi vya Siku Takatifu. Mwendelezo wa kutoka Sabato za kila juma hadi kwenye Miandamo ya Mwezi Mpya unakamilisha mkururu uelewa. Hii ni kwenye awamu au hatua ya pili ya uelewa. Kuyaelewa mataifa yaliyohusishwa kwenye unabii pia ni sehemu ya awamu au hatua ya kwanza, ambayo inaendeleza kutokana na kuielewa Israeli ya kiroho. Uelewa wa kwanza na wa msingi katika kuelewa kile kinachojulikana kama Nyakati za Mataifa (soma jarida la Kuchanganua Ratiba ya Zama (Na. 272)). Hatua au awamu ya pili inaanzia na kuchanganua kile kinachojulikana kama Ujio wa Masihi na kuanzishwa kwa kipindi na utawala wa Milenia.

 

Mkururu wa matukio ya nyakati za mwisho na uanzishwaji wa utawala na mfumo wa milenia vinaeleweka sana kutokana na maadhimisho ya Siku Takatifu. Mkururu wa harakati ni jambo linguine tofauti.

 

Tungeurejelea mchakato huu kwa kutumia jedwali.

 

Hatua ya 1

Maziwa

1. Waioitwa kwenye maarifa ya kwanza nay a msingi ya Biblia:

a)      Dhana na nadharia ya kwanza nay a msingi ya Uungu. Baba ni Mungu.

b)      Kristo kama Masihi kwenye mzunguko wa kuzaliwa alikufa ili awaokoe wenyedhambi.

c)      Roho Mtakatifu ni uweza wa Mungu, ingawa sisi tunafanyika wamoja na Mungu.

 

2. Kuelewa historia ya Biblia na ya Israeli:

a)      Mababa wa imani.

b)      Wokovu wa kimwili wa Israeli kutoka Misri.

c)      Wokovu wa kiroho katika Masihi.

 

3. Asili na uhakika wa unabii kwa maagano yote mawili, yaani Agato la Kale na Agano Jipya:

a)      Mababa wa imani na Musa hadi Waamuzi.

b)      Wafalme hadi manabii wadogo.

c)      Unabii wa Agano Jipya tangu Kristo hadi Ufunuo.

 

4. Maisha ya Kikristo:

a)      Mtu mmoja mmoja binafsi.

b)      Familia.

c)      Kijamii.

 

5. Mambo ya kuyaendeleza kwenye Imani:

a)      Wajibu kwa Mungu kwenye mahusiano binafsi.

b)      Kulisaidia Kanisa kwenye kazi zake.

 

Misingi hii ni budi ilindwe kabla ya mwendezo halisi haujafanyika.

 

Hatua ya pili inaendeleza ile ya kwanza kwa viwango vya juu na kunaanzisha uelea wa kina zaidi wa maana ya manabii kwenye unabii na Mpango wa Wokovu.

 

Hatua ya kwanza ilipelekea kuelewa mkururu wa kihistoria. Hatua ya pili inapelekea kuelewa uwiano wa kiroho na kazi ya unabii Kanisani na utendaji au utimiligu wake. Kutokana na uelewa sahihi wa manabii kwenye hatua hii, nyakati za mataifa zinaweza kuelezewa na kuhamishwa kwa mamlaka kunaweza kuonekana kwenye unabii na kazi na wajibu wa watu na wa taifa kunaweza kuelezewa.

 

Nyakati za mwisho zinaweza kuwataswirishwa pamoja na mabadiliko na mchakato wa iliyofafanuliwa ya mwisho. Baadhi ya mambo haya yanaweza kuelezewa au kufafanuliwa kwa wasio na habari, na mengine yanaweza kuwa yasielezeke yakiwa bado. Kwa hiyo ni lazima kazi kimsingi igawanyike kwenye hatua kadhaa na mteule peke yake lazima aendelee hadi kwenye hatua ya pili. Kwa hiyo awamu ya kwanza imekutaswirishwa na kuunda msingi wa ujumbe kwa wasio washirika. Kuna mambo ambayo ni lazima yaongezwe kwenye bodi ya uandishi. Hata hivyo, kuna mambo fulani ambayo hayako sahihi kabisa kuwapatia wengine.

 

Kristo alilielezea jambo hili kwa namna mbili. Ya kwanza ni pale alipokuwa akiutoa mfano wa Siri za Mungu. Kutowapa na kuwaficha taarifa wengine na kuwapa walio kwenye ushirika kulifanywa kwa makusudi kabisa.

Mathayo 13:10-17 Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano? 11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa. 12 Kwa maana ye yote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini ye yote asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa. 13 Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa. 14 Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. 15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 16 Lakini, heri macho yenu, kwa kuwa yanaona; na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia. 17 Kwa maana, amin, nawaambia, Manabii wengi na wenye haki walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi, wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi, wasiyasikie.

 

Kwa hiyo kuelewa kunategemea pia na matumizi. Wale wasioweza kuona na kusikia watapoteza kile walichokuwanacho. Watasikia lakini hawataelewa kabisa. Siri za Ufalme wa Mbinguni zinsemwazo hapa ni sawa tu na neno musterion au ufunuo wa mambo ya siri za Mungu. Ujumbe wa mfano huu umerudiwa pia kwenye Marko 4:10-20.

Marko 4:10-20 Naye alipokuwa peke yake, wale watu waliomzunguka, na wale Thenashara, walimwuliza habari za ile mifano. 11 Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje yote hufanywa kwa mifano, 12 ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa. 13 Akawaambia, Hamjui mfano huu? Basi mifano yote mtaitambuaje? 14 Mpanzi huyo hulipanda neno. 15 Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja Shetani, akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao. 16 Kadhalika na hawa ndio wapandwao penye miamba, ambao kwamba wakiisha kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha; 17 ila hawana mizizi ndani yao, bali hudumu muda mchache; kisha ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara hujikwaa. 18 Na hawa ndio wale wapandwao penye miiba; ni watu walisikiao lile neno, 19 na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali, na tamaa za mambo mengine zikiingia, hulisonga lile neno, likawa halizai. 20 Na hawa ndio waliopandwa penye udongo ulio mzuri; ni watu walisikiao lile neno na kulipokea, na kuzaa matunda, mmoja thelathini, mmoja sitini, na mmoja mia.

 

Kristo alielezea madhumuni yake kwao wakati alipokuwa peke yao. Kuuelewa mfano huu kunategemea mmoja baada ta mwingine. Kila kitu kilicho kwenye Biblia kipo hapo kwa makusudi. Kila kitu lona maana makusudi yake. Kila kitu kina maana: kila tarakimu, kila jambo, kila mkururu.

 

Kristo alificha wasijue ili kwamba watu wasije wakaitwa kabla ya wakati na kisha wakaingia hukumuni. Neno la Mungu ni takatifu na ndilo limefichwa kwa wale wanaolitumia vibaya.

Mathayo 7:6  Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.

 

Majira yanakuja haraka wakati kuusema ukweli kutakuwa ni utaratibu wa siku ili kwamba jizazi hiki kibaya, kiovu na cha zinaa kitapokea wito wa toba. Kipimo cha wateule kinafuatia pia kwa wito au kuitwa kwa mkururu wa mwisho wa wale 144,000. Mkutano mkubwa umechukuliwa hapo pia kwenye mchakato wa mwisho. Wajibu umeorodheshwa hapa ni kama kuwa mwaminifu. Masumbuko ya dunia yanaonekana kama yanaingilia kati au yanatatiza uwezo a wale wanaolisikia neno na wasitende na wasifanye kazi na washirika wengine walio kwenye mwili wa Kristo. Kama wewe ukiwa mtu binafsi hushiriki kwenye mikusanyiko au  ibada za kila juma na wengine pale unapoweza na kufanya kazi ili kusaidia kazi basi hutaweza kuurithi Ufalme wa Mungu. Usidanganyike kwa kujitafutia udhuru kutokana na kushindwa kwako mwenyewe kuchukua hatua. Kama hutaweza kusaidia kazi basi huna sehemu nayo na kwa hiyo hutakuwa na sehemu kwenye Ufalme huo. Kama huisaidii kazi kwa fedha zako kama unavyotakiwa kuwa ndipo ujue kuwa unamuibia Mungu (Malaki 3:7-12).

Malaki 3:7-12 Tokea siku za baba zenu mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi, asema Bwana wa majeshi. Lakini ninyi mwasema, Turudi kwa namna gani? 8 Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu. 9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote. 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. 11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi. 12 Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema Bwana wa majeshi.

 

Hakuna kitu cha kutenganisha kwenye jambo hili. Kazi ya Mungu ni wajibu wa wote. Suala la kutoa zaka ni la jambo lingine na ambalo limeainishwa kwa kina kwenye jarida la Tutoaji wa Zaka (Na. 161)). Hata hivyo, sio suala la kuwa na shahada tu. Kuna malumbano makubwa kama ukweli wa mambo, kuhusiana na kusaidia kazi. Huu ni wajibu wa wote. Kila mteule anao wajibu kuutafuta ushirika wa wapendwa unaolihubiri neno la Mungu – kinagaubaga. Mara tu kazi hiyo inapoonekana ndipo inapasa isaidiwe na kuungwa mkono.

 

Kristo hakuacha kufanya kazi kwenye hatua yoyote kwa kipindi cha karne zote ishirini zilizopita. Anafanya kazi sasa. Kama hufanyi kazi kwa hamasa kubwa na kuusaidia mwili ule utakuwa kwenye fungu la watakaofufuliwa kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Hii ndiyo sababu ya kwamba kutakuwa na vilio na kusaga meno. Wengi watagundua na huku wakiwa wamechelewa sana kwamba walikosea njia kwa kutokuzitumia talanta walizopewa na Mungu. Usiruhusu hali hii ikukute hata wewe. Nenda! Ukauze ulichonacho na umfuate Kristo.

Mathayo 19:16-21 Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? 17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. 18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, 19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako. 20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? 21 Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.

 

Mungu atammwaga Roho na, katika hizi siku za mwisho, siri hizi zitafunuliwa ili kwamba Jeshi lote la Malaika walioko mbinguni waelewe hekima kubwa na iliyojificha ya Mungu.

1Petro 1:12 Wakafunuliwa ya kuwa si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Mambo hayo malaika wanatamani kuyachungulia.

 

Malaika hawa wanatamani sana kuichunguza hekima ya Mungu na kama sisi tunaujua au tunauelewa Mpango wa wokovu.

1Wakorintho 2:1-7 Basi, ndugu zangu, mimi nilipokuja kwenu, sikuja niwahubiri siri ya Mungu kwa ufasaha wa maneno, wala kwa hekima. 2 Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa. 3 Nami nalikuwako kwenu katika hali ya udhaifu na hofu na matetemeko mengi. 4 Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu, 5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu. 6 Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii, wanaobatilika; 7 bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

 

Kwa hiyo tunatukuzwa tunapokuwa tumechaguliwa, tumeitwa, tumehesabiwa haki na kisha kutukuzwa (Warumi 8:29-30).

 

Kitendo cha siri hizi kufunuliwa katika siku za mwisho kitaonyesha hekima ya Mungu kwa pande mbili zote, yaani mbinguni na Wateule wanadamu.

 

q