Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[135]

 

 

 

Mashahidi (Wakiwemo Hawa Mashahidi Wawili)

(Toleo La 5.0 19950923-20000708-20070906-20081228-20130121)

 

Jarida hili linahusu na utambulisho wa Mashahidi na wanabakia kuwa ni chanzo cha pekee cha utambulisho wa kibiblia. Uwezekano mkubwa wa aina mbili umejadiliwa pia pamoja na dhana yake kukijumuishwa na wakati unaoendea. Huenda hii ilipuuzia ufumbuzi usiiofikirika kwa namna yoyote ile kama ni muhimu nan i uezekano wenye hamasa. Majina mbalimbali yametumika kwa Mashahidi hawa Wawili watakaosimama kwenye Hekalu la Mlimani huko Yerusalemu katika Nyakati za Mwisho. Majina yao wanaitwa Mashahidi Wawili, Vinara Viwili vya Taa na Mishumaa Miwili Iwakayo. Pia wanaitwa kama Mizeituni Miwili au Vinara Viwili vya Dhahabu visimamavyo mbele za Mungu wa Dunia hii.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 1997, 2000, 2007, 2008, 2013 Wade Cox)

(re. 2017)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Mashahidi

Sehemu ya 1: Mashahidi Wawili

 


Mashahidi hawa ni vinara viwili vya taa wanaosimama mbele ya mungu wa Dunia hii. Wanaunda jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi sana la kiroho. Kila mmoja wao anashikilia vinara vya taa ni sawa kama yale kamanisa saba yalivyoshikilia kila moja kinara kimoja cha taa. Kwa hiyo wao ni silaha zenye uweza na nguvu sana za Mungu. Kwenye Sehemu hii ya 1 tutadadavua na kuonyesha uwezekano wa hawa ni akina nani na tutashughulika na dhana ya kipindi cha kuanzia mwaka wa 1996, ambao unahitimisha mwisho wa Nyakati za Wamataifa. Katika Sehemu ya 2 tutashughulika na jambo lingine kuhusu Mashahidi hawa linalochukua sehemu kubwa ya unabii wote.

 

Tutaanza na kuhesabia kipindi cha miaka thelathini ambayo hatimaye itaishitimisha Yubile hii na kuihitimisha kipindi cha miaka 2,000 cha Yubile ya arobaini ya Nyakati za Mwisho (soma jarida la Miaka Thelathini ya Mwiho: Pambano la Mwisho (Na. 219)). Mwaka wa 1996 ulikuwa ni wa maadhimisho ya 3,000 ya kuingia kwa Daudi mjini Yerusalemu. Haya yote yanauhusiano na hatua za maana na muhimu ambazo zinauka tangu mwaka wa 1996. Itakuwa ni miaka thelathini kamili hadi kufikia mwaka 2026 ili kufikiliza Milennia na zama za mapepo, na kuyaandaa mataifa yote kuyarejesha nyuma tena kwa ajili ya mwaka wa kuvuna mavuno maradufu, mwaka utakaoitangulia Yubilee ya mwaka 2027-28.

 

Mashahidi hawa Wawili wataanza huduma yao ndani ya kipindi hiki. Inaonekana kuwa inawezekana sana kuwa Mashahidi hawa Wawili wataanza kutoa unabii wao kwa kipindi chote kijacho cha miaka thelathini. Baadaye tutaainisha ni lini uwezekano wa kuanza huduma yao itaanza na ni mwandamano upi wa matukio utakaofuatana na kuzuka kwa vita mwisho na utakavyokuwa. Jarida hili linawahusu Mashahidi hawa Wawili.

 

Upimaji wa Hekalu umerejelewa ama kuelezewa kwenye Ufunuo 11:1-2.

 

Ufunuo 11:1-2 Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo. 2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili.

 

Mchakato huu wa kulipima Hekalu ni harakati rasmi zitakazofanyika katika Nyakati za Mwisho kukitanguliwa na harakati za Mashahidi Wawili, waliotajwa habari zao kwenye Ufunuo 11:3ff. hakuna mwanya wa wazi, na siyo kwa bahati mbaya kuona kwamba inaendelea mbele kwa haraka sana hadi kwenye suala hawa Mashahidi. Upimaji wa Hekalu ni harakati inayolitangulia tukio la ujio wa hawa Mashahidi. Sisi tu Hekalu la Mungu. Kwa hiyo upimaji wa Hekalu ni kuwaamusha wale walio ndani ya Hekalu la Mungu, na kuwachagua wale walioimara wanaobakia kuwa ni mawe yaliyohai ya Hekalu la Mungu. Wale wasiofaa – na kuna idadi kubwa sana ya watakaoonekana kuwa hawafai – watakaoondoleambali.

 

Upimaji wa Hekalu na mchakato wote mzima wa kuondolewa kwa wachungaji watatu kwa kipindi cha mwezi mmoja umeelezewa kwa kina – ni kama ulivyo mkururu wote wa mfano ashiria wa mchakato ulio kwenye Ezekieli 34, na maandiko kadhaa mbalimbali yanayohusika na dhana kama hizo kwenye jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137). Hata hivyo, jarida hili hasahasa linawahusu Mashahidi hawa Wawili na uwezekano wa kuwa ni kina nani hawa, na kuna idadi kadhaa ya fikra za uwezekano wao, kwa wanaweza kuwa ni kina nani watu hawa.

 

Ufunuo 11:3-4 Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia. 4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi

 

Kitu kimoja ambacho ni hakika ni kwamba; Mashahidi hawa Wawili hawafi wala hawawezi kuuawa hadi pale kazi yao itakapohitimika. Huduma au kazi yao hiyo itaanza na itafuatia mara moja ujio wa Masihi, na watafufuliwa.

 

Madai yaliyokwisha fanywa kuhusu Mashahidi hawa Wawili ni ya uwongo kabisa. Kuna watu ambao wamekwishawahi kuonekana kuwa ni kama wangekuwa Mashahidi hawa Wawili kwa nyakati mbalimbali. La msingi na linalotakiwa kujua tu ni kwamba Mashahidi hawa hawafi sasa na dunia itashangaa watakapokuwa hapa juu ya sayari hii. Mashahidi hawa hawatatoa nabii za uwongo. Hawatakuwa ni watu waliowahi kuhudumu na kujulikana kwenye kanisa lolote hapa duniani na wakahudumu kwenye karne ya ishirini na ambao kwa sasa wamekwishakufa.

 

Upimaji wa Hekalu utafanyika sambamba na mkururu wa matukio ya harakati mbalimbali, ambayo yatakitangulia kipindi cha siku 1,260, au cha miezi arobaini na miwili, au kipindi cha miaka mitatu na nusu. Wote watahudumu kwenye wakati mmoja, wakielezea matukio mbalimbali. Kwahiyo twaweza kudhania kwamba kumetajwa vipindi viwili, au ni kama tunashughulika na mizani mbili tofauti ya nyakati kwenye maandiko ya kitabu cha Ufunuo. Mzani wetu ni wakati, kwa msingi wa siku kuilinganisha na mwaka, na tunaipata miaka 1,260 kamili ya dhiki na mateso kwa hesabu ya mwaka mmoja sawa na siku moja, na kipimo kingine kinawakilisha kipindi halisi cha chini cha miaka mitatu na nusu. Sote tunajua na tunakumbuka kwamba kulikuwa na kipindi cha mateso ya watakatifu huko nyuma kilichodumu kwa kipindi cha miaka 1,260 tangu mwaka 590 BK hadi 1850 BK, kilichoshuhudia Kanisa likiteswa na kanisa lenye madaraja ya kivyeo lililopewa jina la Kanisa la Mwanamke Kahaba. Hii ndiyo imani inayotajwa kwenye Ufunuo 7:1-18.

 

Kipindi cha kuhudumu Mwashahidi hawa kimetengwa cha siku 1,260 watakapohudumu wakiwa wamevaa magunia. Kipindi hiki kinalingana na kipindi ambacho nyua zilizo nje ya Hekalu zitakapokuwa zimekanyagwa kwa miguu pamoja na Mji Mtakatifu, ambao ndio Yerusalemu.

 

Tungeweza kusema, na imekua ikisemwa, kwamba kipindi hiki cha miaka 1,260 kilichoishia mwaka 1850 kiliushuhudia mji wa Yerusalemu ukiwa umekanyagwa kwa miguu, na imani au mfumo mzima wote kwa kipindi kile chote kiliushuhudia Mji Mtakatifu nan chi yote ya Israeli ikikanyagwa kwa miguu. Tangu mwaka 590 hadi 1850 hakukuwa nan chi au jimbo la lililoshikamana lililotengwa kwa Waisraeli nan chi ilikuwa na mapigano mengi kati ya Wazungu wa Ulaya na Waislamu. Unabii ule haukushuhudia watu wowote wawili wakisimama kuhudumu huko Yerusalemu. Waadventista Wasabato wanatafsiri na kuweka hoja zao kwamba Mashahidi hawa Wawili si wengine bali ni Agano la Kale na Agano Jipya. Wanasema kwamba Maagano haya mawili yalichimbiwa/chini ya ardhi kwenye Mapinduzi ya Wafaransa na wakatangaza kuwa Biblia imekufa, na kwamba basi imani hivyo imekwisha mwishoni mwa Mapinduzi ya Ufaransa. Hata hivyo, huo haukua mwisho wa kipindi na hayakuchukuliwa na kwenda juu Mbinguni bado. Hakuna kilichotokea tangu mwaka 1850. Mapinduzi ya Ufaransa yalifanyika mwaka 1793 na siyo mwaka 1850 kabisa. Makanisa ya siku hizi, likiwemo vuguvugu la Waadventista, yanajaribu kudai kwamba mambo haya yamekwishapita tayari ili kukwepa mambo yanayofundishwa kwenye kitabu cha Ufunuo kwa kuwa kitabu cha Ufunuo ni nakala inayoogopesha sana. Makanisa mengine yametunga na kubuni fundisho walilolipa jina la ‘hahala salama pa makimbilio’.

 

Kipindi hili cha Mashahidi kinahusisha manabii wawili watakaosababisha mvua kutonyesha wakati wote wa kipindi cha kutoa unabii wao. (Sasa, ni budi ikumbukwe kwamba mvua imekuwa ikinyesha kwa kipindi chote cha miaka 1,260.) mashahidi hawa wanatabiri wakiwa wamevaa magunia kwa kipindi chote cha miaka mitatu na nusu.

 

Ufunuo 11:5-14 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa. 6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo. 7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua. 8 Na mizoga yao itakuwa katika njia ya mji ule mkuu, uitwao kwa jinsi ya roho Sodoma, na Misri, tena ni hapo Bwana wao aliposulibiwa.

 

Mji huo ni dhahirishahiri Yerusalemu. Waadventista wana tatizo hapa kwa kuwa mji wa Paris haukuwa ndiyo aliosulibiwa Kristo ndani yake.

 

9 Na watu wa hao jamaa na kabila na lugha na taifa waitazama mizoga yao siku tatu u nusu, wala hawaiachi mizoga yao kuwekwa kaburini.

 

Watu wa lugha mbalimbali na mataifa wanafanya kuwe na idadi kubwa sana ya watu. Ni dhahiri, inaweza kutendeka tu katika siku za wigo mkubwa wa mawasiliano na ya wengi, kama ulimwengu wote utakuwa uwanaona watu hawa wakiwa wamelala kwenye mitaa na wataacha hivyo hivyo bila kuzikwa. Hii huenda ni rejea kutoka kwenye mapokeo ya zamani kwamba mtu ambaye hajafa kihalali au kikawaida kwa sheria ya Kiyahudi asitangazwe au asichukuliwe kuwa amekufa hadi atakapoonekana kuwa bado amekufa kwa muda wa siku tatu mchana na usiku. Inawezekana pia kwamba tunaona kiunabii kipimo cha nyakati zikiwa nzito na zinazopungua, kila siku.

 

10 Nao wakaao juu ya nchi wafurahi juu yao na kushangilia. Nao watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa kuwa manabii hao wawili waliwatesa wao wakaao juu ya nchi.

 

Hii haijawahi kutokea bado huko nyuma. Kwa hiyo ni wazi sana kwamba ni tukio linalokuja huko mbele yetu.

11 Na baada ya siku hizo tatu u nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama.

 

Mashahidi hawa walifufuka baada ya kuthibitika kuwa amekufa kwa siku tatu na nusu.

 

12 Wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, Pandeni hata huku. Wakapanda mbinguni katika wingu, adui zao wakiwatazama. 13 Na katika saa ile palikuwa na tetemeko kuu la nchi, na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka; wanadamu elfu saba wakauawa katika tetemeko lile. Na waliosalia wakaingiwa na hofu, wakamtukuza Mungu wa mbingu. 14 Ole wa pili umekwisha pita, tazama ole wa tatu unakuja upesi 

 

Kuna idadi kadhaa ya mawazo na mapendekezo kuhusu andiko hili. La kwanza ni kwamba Mashahidi hawa hawawezi kuuawa hadi pale watakapohitimisha huduma na majukumu yao. Wanasimama mbele ya mungu wa Dunia hii, ambaye ni Shetani (2Wakorintho 4:4), na wapo pale ili kutoa ushuhuda au kuwahubiria watu mambo asiyoyataka yeye na yasiyotakiwa na imani na mfumo wa ulimwengu huu. Hakuna kinachoonekana kukemewa hadi pale kilipokemewa kwa kinywa cha hawa mashahidi wawili. Huo ndio mtazamo wa kibiblia. Ulimwengu hauwezi kukemewa hadi unapokuwakuwa inakemewa kwa vinywa vya mashahidi hawa wawili, na ndiyo maana wako wawili na ndiyo sababu wanasimama pamoja dhidi ya mungu wa Dunia hii. Ni hadi hapo mwishoni wa miaka 6,000 ya kudumu kwa mfumo wa ulimwengu huu ndipo Shetani na mapepo watahukumiwa kwa kupitia mfumo wake.

 

Wale wanaotafuta kuwaua Mashahidi hawa watauawa kwa namna hiyohiyo. Hiyo ndiyo kanuni ya kibiblia ya jinsi tunavyohukumu, na ndivyo tutakavyohukumiwa pia nasi; na hivyo ndivyo itakavyowatokea watu hawa. Mungu atawafanyia kwa jinsi hiyohiyo walivyowafanyia Mashahidi wake. Utaratibu wa kuwahukumu umeanzishwa Mashahidi hawa. Haya ni marejesho mapya yatakayoanzisha utaratibu wa kuhukumu, ambao utawezeshwa na kuakinizwa na Masihi atakaporudi. Hii ndiyo nguvu ya Eliya, aliyekuwa na uweza wa kuuagiza moto kutoka Mbinguni ushuke chini uwauwe makuhani waliokuwa wanaitumikia miungu ya uwongo (1Wafalme 18:1-46) na wale waliojipanga kumdhuru yeye (2Wafalme 1:10-15) au kwa kweli walioonyesha dharau au utovu wa nidhamu kwa watumishi waliochaguliwa na kutiwa mafuta au wajumbe wa Mungu wa kweli kama tunavyomuona na Elisha pia (2Wafalme 2:23-24). Elisha alikuwa na uweza kwenye maji pia (2Wafalme 2:19-22) na dhidi ya mvua. Mbingu ilifungwa kwa ajili ya dhambi za watu walishuhudiwa kwenye vinywa vya mashahidi wawili (1Wafalme 8:35; sawa na Mambo ya Walawi 26:19; Kumbukumbu la Torati 11:17). Nguvu hizi za Uliya zilikuwa na maana sana. Zilitumika kwa njia nyingi na zilikuwa na utendaji kazi wa namna mbalimbali.

 

1Wafalme 8:34-36 basi, usikie huko mbinguni, ukawaachilie watu wako Israeli dhambi yao, ukawarejeze tena katika nchi uliyowapa baba zao. 35 Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa; 36 basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao.

 

Tunajionea makundi mawili ya wateule, watumishi wa Mungu (gurudumu la ndani), na Isaeli, ambao ni gurudumu la nje la gari.

 

Mambo ya Walawi 26:19 Nami nitakivunja kiburi cha uwezo wenu; nami nitazifanya mbingu zenu kuwa kama chuma, na nchi yenu kuwa kama shaba

 

Hii ni hukumu inayotokana na dhambi. Mashahidi hawa wanazichukua dhambi za dunia nyuma kwenye kichwa chake.

 

Kumbukumbu la Torati 11:17 hasira za Bwana zikawaka juu yenu, naye akafunga mbingu kusiwe na mvua, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo Bwana.

 

Eliya alizifunga mbingu kwa neno lake.

 

1Wafalme 17:1 Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.

 

Ni wazi sana kwamba Eliya alijua kwamba alikuwa na uweza juu ya mvua hata kwa kiasi kwamba hata kama kulikuwa na umande au haukuwepo juu ya nchi, yeye alifunga tu. Ni muhimu kwamba tujue Eliya alikuwa ni mtu wa namna gani kwa kuwa kuna dalili na dondoo muhimu sana za kinabii kuhusu chimbiko la Eliya pia.

 

Eliya alikuwa ni Mgileadi. Gileadi ulikuwa ni ukoo au familia ya jimbo la Gadi (1Nyakati 3:14) ambao walikuwa ni wakazi wa Gileadi. Waliishi pande za mashariki mwa Yodani. Kumbuka kuwa kulikuwa na makabila matatu ambayo hayakwenda kwenye Nchi ya Ahadi na milki yao iko nje ya Israeli – na hiyo ni dalili na ishara kwa Nyakati za Mwisho. Milki ya milele imo katika Manase, Gadi na Reubeni. Tukichukulia umiliki nchi wa Israeli kwa kuelekea unabii (ambayo kwa kweli ni kuanzia kuanguka kwa Yeriko; soma jarida la Kuanguka Kwa Yeriko (Na. 142)), Gadi ni kabila kubwa nje ya Israeli katika Nyakati za Mwisho. Anapeleka majeshi katika Israeli sambamba na Reubeni na Manase ili kwenda kuchukua urithi. Gadi na Reubeni watayachukua maeneo mbalimbali. Reubeni, Simeoni na Gadi wapo upande wa kusini na moja lipo upande wa magharibi na urithi wao uko ulikuwa nje ya Israeli. Manase walikuwa upande wa magharibi. Kwa hiyo kuna makabila mawili upande wa kusini na moja upande wa magharibi katika Nyakati za Mwisho yanayokwenda Israeli. Makabila hayo yanaonekana kuchukua urithi wao kama sehemu ya makundi yaliyojiunga pamoja chini ya agano la haki ya uzaliwa wa kwanza waliyopewa Efraimu. Walikuwa ni wakazi tofauti katikati ya Waefraimu na Manase ambao ndio walipigana nayo chini ya Yefta (Waamuzi 11:4).

 

Jina Gileadi yawezekana kuwa lilichukuliwa kutokana na jina la nchi iliyo na makorongo, ikiwa inapakana na uwanda wenye rutuba wa Bashani. Eneo lake linasemekana kuwa linapakana na Amoni kwa upande wa kusini mwa Bonde la Yordani upande wa magharibi, sehemu za kusini na kaskazini mwa Yaboki na kwenye jangwa hadi upande wa mashariki, na pembezoni mwa Bashani, maili chache sana kusini mwa Yarmuki upande wa kaskazini, urithi au milki ya Gadi ilikuwa ni nchi iliyo na mawe na makorongo zaidi kuliko nchi ya Manase. Utithi wa makabila haya yote mawili ulikuwa ni nje ya Israeli ilichukuliwa kuwa ni ng’ambo ya Yordani. Kamusi ya The Interpreter’s Dictionary of the Bible inashikilia kusema kwamba Gileadi ni kabila lionekanako wazi kuwa sambamba na makabila ya Reubeni na Dani, na ni sawasawa na kabila la Gadi. Dhana iliyokuwepo huko nyuma ya pamoja na makabila ya Efraimu na Manase haina sehemu wala uhusiano na urithi wa Wareubeni na Wagadi na sehemu yao kwa Waefraimu, au umuhimu na maana ya urithi wao nje ya Israeli katika Nyakati za Mwisho kama ilivyoonyeshwa kwa kuvuka kwao mto ili kwenda uichukua nchi ya ahadi ya Israeli kwenye mfano wa kwanza wa nyakati za Yoshua. Huo ulikuwa ni unabii na pia ni ukweli wa kihistoria. Kwa maana ya kiupana zaidi walienea kwa undani zaidi pande za kaskazini huko Bashani na hata ng’ambo za mbali za Yamuki.

 

Kama ni matokeo ya mtafaruku huu, jimbo la Manase ni kitu kilichotajwa kama lineloendelea kuijieneza na kujishamirisha katika Gileadi. Hata hivyo, ni kawaida tu makabila haya ya Reubeni na Gadi peke yao ndiyo yaliyokuwa huko. Kwa hiyo Wareubeni na Wagadi walimiliki eneo moja. Inaonekana kwamba kulikuwa na ufalme wa kipeke yake uliokuwepo huko Gileadi ukiongozwa na mfalme Peka, mwana wa Remalia, tangu miaka miaka ishirini iliyowekwa au kuandikwa kwenye utawala wake kwenye 2Wafalme 15:27. Hii inaonekana kuwa ilitokea yapata kama mwaka 750 KK katika sehemu iliyobakia ya utawala wa Yeroboamu II. Alitawala huko hadi mwaka 735 KK. Alimuua mtangulizo wake akisaidiwa na Wagileadi (2Wafalme 15:25). Hatimaye alijaribu kuwaunganisha wote waliokuwa kwenye majimbo yote yaliyowazunguka ili wakapigane na Waashuru. Waashuru walimshinda na wakawachukua Israeli wengi wao wakiwa ni Wadileadi (2Wafalme 15:29), na tangu wakati huo wahakuwa tena sehemu ya ufalme huu. Hivyo walichukuliwa kwenda mbali utumwani kwa sababu ya upinzani waliouonyesha kwa Waashuru kabla Israeli wenyewe hawajachukuliwa kupelekwa kijumla utumwani. Gadi na Eeubeni na maeneo ya mashariki yenye uasili na ushawishi na Wamanase walichukuliwa na kupelekwa utumwani kabla Israeli hawajaenda kijumla utumwani.

 

Kwa hiyi, Eliya anaweza kuchukuliwa kuwa alikuwa alitokana na kabila hili la Gadi pia, akitpkea kwenye maeneo ya urithi wa Israeli ng’ambo ya Yordani. Tukio hili lina maana yake kwa Nyakati za Mwisho kama tukichukulia kwamba mfano au alama kurithi nje ya Israeli kuna maana yake kwa Mashahidi na mgawanyo wa makabila. Kama tunatarajia matukio ya Nyakati za Mwisho kwenye unabii, hayatatokea kwa Efraimu wala kwa Manase. Eliya alikuwa wa kabila la Gadi. Kutokana na uweza tunaouona aliopewa Eliya wa kuamuru kuwe na baa kubwa la ukame, kushusha moto uwaunguze watu na mambo mengine, tunaona kwamba Mashahidi nao watakuwa na nguvu na uweza wa Eliya kama ilivyonenwa na kuahidiwa kwenye Malaki 4:5-6.

 

Malaki 4:5-6 Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya. 6 Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.

 

Nguvu na ueza wa nabii huyu haupo tu kwenye masuala ya kutenda miujiza peke yake, bali pia ni kuhusiana na uezo wa kurejesha tena mahusiano ya kifamilia hapa Duniani ili ziweze kuokolewa. Yohana Mbatizaji alikuwa ni mtangulizi wa nabii huyu, lakini hakuwa ndiye nabii huyo.

 

Mathayo 11:12-14 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. 13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana. 14 Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja.

 

Hivyo Yohana alikuwa ndiye Eliya. Lakini kulikuwa na nabii mwingine ambaye alikuwa na roho ya nabii huyo pia (soma pia kwenye Marko 9:11-13).

 

Mathayo 17:10-12 Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza? 11 Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote, 12 ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.

 

Hata hivyo, Yohana Mbatizaji alikuwa ni Eliya kwa mujibu wa ushuhuda wake mwenyewe (Yohana 1:21). Kristo alisema kwamba alitimiliza kazi hiyo, lakini itatokea kwa uweza na nguvu nyingi katika nyakati za mwisho na Eliya mwingine.

 

Marejesho mapya ya mambo yote yatafanyika chini ya mfumo huo wa Nyakati za Mwisho (Mathayo 17:11). Mashahidi wana ngvu na uweza huo. Marejesho mapya ya mambo yote ikiwepo maadhimisho ya Yubile na Miandamo ya Mwezi Mpya pamoja na mfumo mwingine wote ya Ufalme wa Mungu, na uwezo wote wa kuelewa. Hakuna mwalimu wa ulimwengu huu aliyefanya mambo haya yote hadi sasa. Mambo haya yatatokea.

 

Kristo hakuanza huduma yake ya kufundisha hadi pale Yohana Mbatizaji alipofungwa gerezani. Wakati Yohana alipomalizia huduma yake, ndipo Kristo alioanza kufundisha. Mungu hakumpa Kristo fursa hadi Yohana alipomaliza. Na ndivyo ilivyo kwamba Masihi hatakuja hadi pale Mashahidi hawa watakapokamilisho huduma yao.

 

Kuna uwezekano wa aina mbili katika kushughulika na Mashahidi.

 

Uwezekano wa Kwanza

Uwezekano wa kwanza ni kamba maneno haya yanatafsiri ya moja kwa moja, na Eliya amehamishwa mbele kwenye nyakati za kuhitimisha kazi ya maandalizi ya Masihi, na ni mmoja wapo, au anayeyangulia, Mashahidi. Hivyo kuna uwezekano wa kwamba Eliya na mtu mwingine (ambaye hajajulikana bado) wanaweza kuletwa kwenye nyakati ambazo hazitaweza kuondolewa. Kuna watu wawili tu kwenye Biblia ambao hawakufa, na Biblia imeeka na kuainisha wazi kuhusu kutwaliwa kwao. Filipo alitwaliwa pia na Mungu kutokana na maono ya Mwithiopia lakini alitokea tena na akafa baadae (Matendo 8:39-40).

 

Kama Eliya ni mmoja wa Mashahidi, basi itamlazimu kuungana na mwingine atakapohudumu na kusimama huko Yerusalemu. Ndivyo inavyoonekana kuwezekana kabisa ndivyo yanavyosema Maandiko Matakatifu. Watu wawili peke yao waliowahi kutwaliwa kabla ya kufa kwao kwa mujibu wa biblia ni Eliya na Henoko. Kaka hivyo ni sahihi, ndipo unabii wa Yeremia 4:15 unawatangulia, kwa kuwa hakuna aliye wa mchanganyiko wa makabila mawili ya Dani na Efraimu kama alivyo nabii huyo. Henoko alikuwa wa kwanza kutwaliwa. Huduma yake ilikuwa ni kukishuhudia kizazi kilichokuwepo kabla ya Gharika Kuu. Mwingine alitwaliwa kwenye upande mwingine wa Gharika Kuu na mwingine kwenye upande mwingine wa Gharika Kuu, kwa kuwa hawa Mashahidi wanahitaji kueneza na kudhihirisha mwendelezo wa hila za utawala wa Kishetani na maangamizo yake. Dunia ilihukumiwa na kuangamizwa kwa haki na utakatifu wa Henoko. Sababu inayopelekea umuhimu wa Henoko ni kwamba uwepo wa watu wa kipindi cha kabla ya Gharika Kuu hususan Wanefili na kuangamizwa kwa Dunia hadi hapo na kwa njia ya Gharika Kuu. Kuangamizwa kwa ujumla kwa Dunia kutatokea au kutafanyika mwishoni mwa kipindi cha miaka 6,000. Kwa hiyo, tuna awamu moja ya maangamizo yalitofanywa na Gharika Kuu iliyohukumiwa dhidi ya Henoko.

 

Mwanzo 5:18-32 Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. 19 Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake. 20 Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. 21 Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. 22 Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake. 23 Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano. 24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa. 25 Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki. 26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake. 27 Siku zote za Methusela ni miaka mia kenda na sitini na kenda, akafa. 28 Lameki akaishi miaka mia na themanini na miwili, akazaa mwana. 29 Akamwita jina lake Nuhu, akinena, Huyu ndiye atakayetufariji kwa kazi yetu na kwa taabu ya mikono yetu katika nchi aliyoilaani Bwana. 30 Lameki akaishi baada ya kumzaa Nuhu miaka mia na tisini na mitano, akazaa wana, waume na wake. 31 Siku zote za Lameki ni miaka mia saba na sabini na saba, akafa. 32 Nuhu alikuwa mwenye miaka mia tano, Nuhu akawazaa Shemu, na Hamu, na Yafethi.

Dunia haikuwa imeangamizwa mpaka alipokufa Methusela. Mungu alituma Gharika Kuu katika mwaka wa kufa kwake. Akiwa ni mwana wa Henoko, Methusela alilelewa kwenye maisha ya haki na utakatifu na akajaaliwa aishi zaidi ya nyakati zake, na Dunia haikuangamizwa wakati mtoto wa Henoko na mjuu wake wakiwa wangali hai hapa duniani. Ilikuwa ni kwa kitukuu wa Henoko ambapo Bwana alipoweka mpango wa pili wa kuwaokoa walio kwenye mstari wa uzao wa Adamu. Henoko alikuwa ni baba yake Methusela. Hakuwepo, kwa kuwa Mungu alimtwaa; lakini hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu (Yohana 1:18). Halikadhalika Henocko hakuwa kiumbe mwenye mwili atakayefufuliwa kwenye ufufuo wa wafu. Kristo alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza wa waliokufa (Wakolosai 1:18). Kwa hiyo Henoko hakuwa ametwaliwa baada ya Yesu Kristo. Yesu Kristo ndiye kichwa au kiongozi na wa kwanza wa wana wa ufufuo. Alikuwa ni kiumbe wa kwanza kufufuka na mwanadamu wa kwanza kufanyika kuwa roho. Kwa hiyo, Henoko hakutwaliwa akiwa kama kiumbe wa kiroho. Kwa hiyo Henoko huenda ama alikufa au alihamishwa kwa nyakati mbalimbali. Jambo hili laweza kutokea tu kama muda utakuwepo kama nadharia na dhana isiyo na mashiko yake maalumu. Eliya alitwaliwa pia. Kwa kawaida anachukuliwa kuwa ni kama alikufa, kama walivyo watu weote mbali na Kristo. Ulimwengu wa kiroho hauwezi kubadilika kuwa wa kibinadamu hadi kwenye ufufuo wa wafu (soma majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Ufalme wa Milele wa Mungu (Na. 144)).

 

2Wafalme 2:1-17 Ikawa, hapo Bwana alipopenda kumpandisha Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya alitoka Gilgali pamoja na Elisha. 2 Eliya akamwambia Elisha, Tafadhali, kaa hapa; maana Bwana amenituma niende mpaka Betheli. 3 Elisha akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha, Basi wakashuka mpaka Betheli. Basi wana wa manabii, waliokuwako Betheli, wakatoka kuonana na Elisha, wakamwambia, Je! Unajua ya kuwa Bwana atamwondoa bwana wako leo, asiwe mkubwa wako? Akasema, Naam, najua; nyamazeni. 4 Eliya akamwambia, Tafadhali, kaa hapa, Elisha; maana Bwana amenituma niende mpaka Yeriko. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Nao wakafika Yeriko. 5 Basi wana wa manabii, waliokuwako Yeriko, wakamkaribia Elisha, wakamwambia, Je! Unajua ya kuwa Bwana atamwondoa bwana wako leo, asiwe mkubwa wako? Akajibu, Naam, najua, nyamazeni. 6 Eliya akamwambia, Tafadhali kaa hapa; maana Bwana amenituma niende mpaka Yordani. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Wakaendelea mbele wote wawili. 7 Basi watu hamsini wa wale wana wa manabii wakaenda wakasimama, kuwakabili kwa mbali; na hao wawili wakasimama karibu na Yordani. 8 Eliya akalitwaa vazi lake la juu, akalikunja, akayapiga maji, yakagawanyika huku na huku, na hao wawili wakavuka pakavu. 9 Hata ikawa, walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, Omba kwangu lo lote utakalo nikutendee, kabla sijaondolewa kwako. Elisha akasema, Nakuomba, sehemu maradufu ya roho yako na iwe juu yangu. 10 Akasema, Umeomba neno gumu; lakini, ukiniona nitakapoondolewa kwako, utalipata; la hukuniona, hulipati.

 

Huku sio kumpotosha na kumvunja moyo Elisha, kwa kuwa alipaswa kuamini kwa moyo wake wote kwamba alikuwa na mamlaka kamili ya Roho Mtakatifu, ili kuanzisha mambo ambayo alipaswa kukamilisha mambo aliyotakiwa kuyakamilisha. Hakuna nafasi ya kuonea mashaka kiimani ya kuyatendea kazi mamlaka ya Roho Mtakatifu. Kama Mashahidi walionea shaka kitu chochote kabisa, basi wasingeweza kutendea kazi mamlaka hayo ambayo walitakiwa kuyatendea kazi. Wanayatendea kazi mamlaka kwa imani kwa njia ya Roho Mtakatifu.

 

11 Ikawa, walipokuwa wakiendelea mbele na kuongea, tazama! Kukatokea gari la moto, na farasi wa moto, likawatenga wale wawili; naye Eliya akapanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli. 12 Naye Elisha akaona, akalia, Baba yangu, baba yangu, gari la Israeli na wapanda farasi wake! Asimwone tena kabisa; akashika mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili. 13 Kisha akaliokota lile vazi la Eliya lililomwangukia, akarudi, akasimama katika ukingo wa Yordani. 14 Akalitwaa lile vazi la Eliya lililomwangukia, akayapiga maji, akasema, Yuko wapi Bwana, Mungu wa Eliya? Naye alipoyapiga maji, yakagawanyika huku na huku, Elisha akavuka.

 

Elisha alifanya kilekile kabisa alichofanya Eliya. Alikuwa anayatendea kazi mamlaka yake katika Roho kwa mwelekeo mwingine, akionyesha kwamba alikuwa na uweza na mamlaka. Alikuwa anafanya hivyo mbele ya makuhani wa Israeli. Walikuwa wakitazama kutoka mbali na kutazamia kimsingi kushuhudia kuhamishiwa kwa nguvu za Mungu. Walitaka kuona kile kilichokuwa kinaendelea na Eliya na kungetokea nini kama Eliya akiondoka. Kilichotokea ni kwamba mamlaka na nguvu hizi zilihamishwa kutoka kwake na akapewa Elisha.

 

15 Na hao wana wa manabii, waliokuwako Yeriko wakimkabili, walipomwona, walisema, Roho ya Eliya inakaa juu ya Elisha. Wakaja kuonana naye, wakainama kifudifudi mbele yake. 16 Wakamwambia, Angalia, wako hapa pamoja nasi watumishi wako watu hamsini walio hodari; waende, twakuomba, wamtafute bwana wako; isiwe labda roho ya Bwana imemtwaa na kumtupa juu ya mlima mmoja, au katika bonde moja. Akasema, Msiwatume. 17 Wakamsisitiza hata akaona haya, akasema, Haya! Watumeni. Basi wakatuma watu hamsini; nao wakatafuta siku tatu, wasimwone.

 

Hii ni habari ya kwanza ambayo kimsingi tuliyonayo tunapokuwa na mkururu wa siku tatu tu baada ya kuondoka kwa Eliya.

 

Ina maana kwa kiwango cha juu sana kwamba hapa Roho ya Eliya kumwingia Elisha. Hivyo, roho ya Eliya iliaminika kuwa ilihama na inahamishika. Kwa hiyo kufumba kulikuwa dhana ya muhimu sana. Nguvu na ueza huu wa kiroho ndipo ilijulikana kuwa ni kama alitolewa na ili kwamba nguvu za Eliya iweze kujidhihirisha kwa watu wengine. Hii ina maana ya kwamba awe wa pili kwa Elisha. Eliya anachukuliwa na waandishi wengine kuwa iliamriwa ije baada ya kutwaliwa kwake. Hili ni jambo lingine kwa kuchora mchoro.

 

Nguvu hizi za Eliya zilihamishiwa pia kwa kufunika kwake. Manabii walimtafuta Eliya kwa siku tatu baada ya kutoweka kwake. Jambo hili lina maana yake. Kipindi cha baada ya kufa kwa Mashahidi kitakuwa pia cha siku tatu na nusu. Siku tatu zinahusiana na ishara ya Yona na zinapatikana kwa kanuni ya kulinganisha kwa kipimo cha mwaka sawa na siku moja pamoja na huduma ya Masihi. Mfano wa mwisho ni kwenye vifo vya hawa Mashahidi. Uwezekano wa kwanza kwa hiyo ni kwamba ni Eliya na Henoko walitwaliwa kwa wakati wote. Hiyo ingeonekana kama kichekesho, lakini kama tunawatafuta au tunapowaona Mashahidi kwenye Biblia tunaona kuwa wapo watu wawili na hawakufa, ambapo inaashiria na kuonyesha kwamba yawezekana kabisa kwamba walitwaliwa na kusafirishwa kwa wakati wote wakiwa kama Mashahdi Wawili. Usishangae tunapoliona gari la Eliya likiwashusha kina Eliya na Henoko mjini Yerusalemu. Huu ndiyo uwezekano uliopo. Kwa hakika ndiyo maelezo, au ufafanuzi ambayo vinginevyo hayapo na inayoondoa utofauti.

 

Mtazamo huu ulikuwa ni mtazamo asilia wa wakati wa Kristo na pia ni wa kanisa la kwanza. Mashahidi watarajiwa walikuwa ni Eliya na Henoko na kwamba inabakia hivyo hadi katika karne ya ishirini na yasiyo na maana wala mashiko ya Makanisa ya Kisabato na mengineyo.

 

Uwezekano wa Pili

Uwezekano wa pili ni kwamba Mashahidi wa Nyakati za Mwisho watautendea kazi uweza na nguvu zilezile za Eliya. Huo ndio mtazamo wa kimapokeo iliopo kwenye Makanisa ya Mungu ya Marekani. Mtazamo wa kwanza sio wa kimapokeo huko Marekani lakini ulikuwa ni mtazamo wa zamani wa mahali penginepo. Mtazamo wa siku hizi huko Marekani kusema kwamba walikuwa manabii wawili na wangali wanaishi hata sasa hapa duniani. Ni budi watakuwa wangali hai wakati huu, wakitabiri wakati wenyewe muafaka na kusisitiza ushikaji wa Torati. Ili kuandaliwa, watapaswa kuwa na umri wa miaka zaidi ya thelathini ili waanze kuhubiri – vinginevyo watakuwa wameihalifu Sheria ya Torati. Kwa hiyo, wanapaswa kuwa na umri wa zaidi ya miaka thelathini kabla hawajafundisha na miaka thelathini kuanzia mwaka 1996 hadi 2026, na ndipo wataanza kuhudumu kwa miaka mitatu kabla ya mwaka 2026. Muda mfupi sana ujao watakuwa hapa duniani mnamo mwaka 2023. Hiyo inamaanisha kwamba watapaswa wawepo hai sasa, na kwa muda mfupi sana, umri wa mwaka mmoja mwaka 1995.

 

Manabii hawa wawili yaonekana wanazitendea kazi nguvu hizi, wakiwa wanajulikana kama ni manabii wa Nyakati za Mwisho. Andiko linaonyesha kwamba hawa ni mizeituni miwili na vinara viwili vya taa wasimamao mbele ya mungu wa Dunia kwa hiyo wao wanakabiliana uso kwa uso na Shetani. Kumbuka kuwa Shetani alimkabili uso kwa uso Kristo hapo kwanza. Shetani alihukumiwa kwa kuhukumiwa kwa kumhukumu kwake Kristo. Hata hivyo, kwa aliji hiyo, Mashahidi hawa wanasimama mbele mungu wa Dunia hii na wanamkabili Shetani. Mfano kama huohuo unatumika kwenye Zekaria 4:3,11,14. Tunaona sehemu ya kwanza inahusiana na ujenzi wa Hekalu kwa kutumia roho saba za Mungu.

 

Zekaria 4:1-10 Na yule malaika aliyesema nami akanijia mara ya pili, akaniamsha, kama mtu aamshwavyo katika usingizi wake. 2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikasema, Nimeona, na tazama, kinara cha taa cha dhahabu tupu, nacho kina bakuli juu yake, na taa zake saba juu yake; tena iko mirija saba ya kuleta mafuta, kwa taa zote zilizo juu yake; 3 na mizeituni miwili karibu yake, mmoja upande wa kuume walile bakuli, na mmoja upande wake wa kushoto. 4 Nami nikajibu, nikamwambia yule malaika aliyesema nami, nikasema, Ee Bwana wangu, vitu hivi ni nini? 5 Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu. 6 Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi.

 

Hii ni aya moja wapo ya aya za muhimu sana kwenye Biblia: Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi. Hakuna kitakachotokea humu duniani kwa kushurutishwa au nguvu au uweza mkubwa au nia kuu ya vitu hivyo. Itakujatokea kwa kupitia Roho wa Mungu na ndiyo maana Mungu atafanya kazi katika Siku za Mwisho kwa kupitia watu hawa wawili watakaonena katika Roho wa Mungu.

 

7 Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie.

 

Ni nini maana ya kichwa cha jiwe kilichopo? It is Messiah.

 

8 Tena neno la Bwana likanijia, kusema, 9 Mikono yake Zerubabeli imeiweka misingi ya nyumba hii, na mikono yake ndiyo itakayoimaliza; nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu. 10 Maana ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli; naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote.   

 

Kinara cha taa kilikuwa ni kinara kimoja tu cha Maskani inayoonekana kwenye Kutoka 25:31 na kwenye Hekalu la Pili. 1Wamakabayo 1:21 na 4:49 inaonyesha kwamba kwenye Hekalu la pili walikuwa na kinara kimoja cha taa saba. Tunauona uwongo wa taa kwenye Duara la juu ya lango la Tito au Titus huko Roma. Wakati Hekalu lilipobomolewa na majeshi yakavichukulia mbali vyombo na mapambo ya dhamani ya Hekaluni, walichukua pia kinara cha taa kubwa cha Hekalu la pili. Kwa hiyo tukio hilo lilichorwa kwenye duara la zege la langoni likiashiria kuhusuriwa kwa Hekalu. Kwa hiyo, kulikuwa na kinara kimoja cha taa au kinara cha taa kwenye Maskani, na kwenye Hekalu la pili kulikuwa na kinara kikubwa kimoja kilichokuwa na taa saba.

 

Kwenye Hekalu la Sulemani kulikuwa na vinara kumi vya taa kama tunavyoona kwenye 1Wafalme 7:49 (sawa na Yeremia 52:19). Kuna dhana mbili zinazotofautiana zilizopo. Kwa hiyo kulikuwa na kinara kikubwa kimoja chenye taa saba pamoja na halafu taa kumi. Hawa Mashahidi wenyewe ni vinara viwili vya taa wanaosimama kwenye ama upande wa kinara kile kikubwa ambacho kilimwakilisha Masihi. Hiyo ndiyo maana yake. Masihi alikuwa ni kinara cha katikati cha taa, ya nane. Kutoka Masihi kulifuatia makanisa saba. Kwenye kamanisa haya saba ndipo tunakuta vinara viwili vya taa vya Mashahidi Wawili, vikiweka jumla ya idadi yake kuwa kumi kwa ujumla. Mfumo wa mara kumi ulikuwa ni kitu kilichoonekana kwenye Hekalu la Sulemani. Andiko la pili linaataja Mashahidi hawa, ambao ndio vinara kumi vya taa kwa upande wao wa kuume. Hekalu la Sulemani lilionyesha mkururu wa taa hivi kumi kama zikisimikwa kwenye ile ya kwanza ya zile saba. Kwa hiyo taa hizi kumi kwenye Hekalu la Sulemani zilimaanisha Masihi, makanisa saba na Mashahidi Wawili. Mashahidi hawa Wawili walipaswa kufanya kazi ya Makanisa ya Sardi na ya Laodikia, ambayo yote yameshindwa. Kwa hiyo Mungu anaonyesha kwamba Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi. (Zekaria 4:6).

 

Hekalu ni Kanisa la Mungu. Suala hili limerudiwa na Zekaria (sawa na Zekaria 4:11) kama kwamba amekuwa hajajibiwa bado kwenye mfano wa kwanza. Hii inaashiria harakati au mkururu wa mambo wa pili.

 

Zekaria 4:11-14 Ndipo nikajibu, nikamwambia, Ni nini mizeituni hii miwili iliyo upande wa kuume wa kinara cha taa kile na upande wake wa kushoto? 12 Nami nikajibu mara ya pili, nikamwuliza, Ni nini haya matawi mawili ya mizeituni, ambayo kwa njia ya ile mifereji miwili ya dhahabu hutoa mafuta yao? 13 Akanijibu, akasema, Hujui hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu. 14 Ndipo akasema, Hivi ni hao wana wawili wa mafuta, wasimamao karibu na Bwana wa dunia yote.

 

Nukuu inasema simama kwa Bwana wa dunia yote. Hawasimami kwa Bwana. Wanasimama kwa Mungu wa Mbinguni na wanasimama na Masihi anayechukua sehemu ya kuwa Bwana wa Dunia yote. Wanaongelea juu ya vinara vya taa na wanasi,a,a kwa Bwana wa Dunia yote, lakini wakiwa ni mashahidi wanasimama mbele ya mungu wa Dunia hii. Kwa hiyo wanasimama mbele na kumkabili Shetani, lakini wanasimama ama upande wa Yesu Kristo anayeichukua nafasi ya Shetani. Hili ni andiko lingine linaloonyesha kwamba Shetani, kama Nyota ya Asubuhi, amepewa nafasi na Yesu Kristo kama mungu wa Dunia hii.

 

Mwandamano huu wa matukio imeanza baada ya kipindi kijulikanacho kama Nyakati za Mataifa. Tunajua kwamba Hekalu liliangamizwa na mfumo au utaratibu wote ulichukuliwa utumwani Babeli. Harakati hizi zapasa ziishie kwenye Wakati wote wa Wamataifa na iliathiri imani zote mbili, yaani ya Kiyahudi na ya Kikristo. Na ndiyo maana kanisa la uwongo au kanisa la yule Kahaba linaitwa pia Babeli Mkuu na Mama wa Makahaba (Ufunuo 17:5). Unabii huu unakutikana kwenye Zekaria 5:1-11.

 

Agano la Kale laweza kujisimamia lenyewe. Agano Jipya ni ufafanuzi wa Agano la Kale, na siyo mbadala au ukiukaji wa Agano la Kale. Agano la Kale linajisimamia kama lilivyo kama tutalielewa. Hatuhitaji kuwa na Agano Jipya ili litusaidie kuuelewa Mpango wa Wokovu na matendo ya Yesu Kristo kwa nyakati zake kama tutalielewa vizuri Agano la Kale. Agano Jipya linahitajika kwa kuwa linalithibitisha Agano la Kale na Agano Jipya linafafanua na linathibitisha kile kinachomaanishwa na Agano la Kale. Tunaweza kukosea na Agano la Kale kama hatutalielewa vizuri. Kwa hiyo Agano Jipya linalithamanisha na kulithibisha kiusahihi na kiukamilifu zaidi maana ya nabii za Agano la Kale. Imani potofu na za uwongo zimelixhukua hilo na kukiweka kiambishi cha ni msingi Wake lenyewe. Kwa Kiebrania inaandikwa kwa umoja wa kike. Shinatri ni nchi ya Kibabeloni. Wanawake wawili wanaunda mifumo na imani mbili, yaweza kuwa ama ya kitaifa (kwa mujibu wa Companion Bible) au imani za kidini. Maana ya kina na ya ndani ni kwamba imani za Kiyahudi na Kikristo ziliharibiwa zote na imani ya Kibabeloni. Na hayo ndiyo maana yake halisi.

 

Zekaria 5:1-11 Basi, nikainua macho yangu tena, nikaona, na tazama, gombo la chuo lirukalo. 2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikajibu, Naona gombo la chuo lirukalo; na urefu wake ni dhiraa ishirini, na upana wake dhiraa kumi. 3 Ndipo akaniambia, Hii ndiyo laana itokayo kwenda juu ya uso wa nchi yote; maana kwa hiyo kila aibaye atatolewa kama ilivyo upande mmoja, na kwa hiyo kila aapaye atatolewa kama ilivyo upande wa pili. 4 Nitaituma itokee, asema Bwana wa majeshi, nayo itaingia katika nyumba ya mwivi, na katika nyumba yake yeye aapaye kwa uongo kwa jina langu; nayo itakaa katikati ya nyumba yake, na kuiteketeza, pamoja na boriti zake na mawe yake.

 

Hawa siyo tu kwamba ni farasi tu ambao watu waliishi nao; bali walikuwa ni farasi wa ibada. Utaratibu na imani ya kidini na Hekalu ziliharibiwa au kuangamizwa. Hata mawe ya Hekalu yaliangamizwa kwa kuwa walikuwa wanaapa kwa uwongo kwa jina la Mungu. Hii ndiyo imani ambayo iliyochukuliwa kwenye Hekalu na kwamba ndiyo iliondolewambali kipindi cha ushahuhuda wa Yesu Kristo. Hii ndiyo imani pia ambayo iliyochukuliwa na kuingiza kwenye imani ya Kikristo na kuuharibu au kuupotosha kabisa Ukristo pia. Ndoto na mitazamo hii – yote mbili za Hekalu la Kiyahuzi na Ukristo mkongwe zitaangamizwa. Hiyo ndiyo maana yake. Mwishoni mwake kila ndoto au mtazamo wa kila dini na majengo ya hapa duniani ya wanaodai kuwa ni Wakristo yatabomolewa na kuangushwa chini. Wengi wataangamizwa, wawe ni kama wana daraja za kiurithi ama sivyo.

 

5 Ndipo yule malaika aliyesema nami akatokea, akaniambia, Inua macho yako sasa, uone ni kitu gani kitokeacho. 6 Nikasema, Ni kitu gani? Akasema, Kitu hiki ni efa itokeayo. Tena akasema, Huu ndio uovu wao katika nchi hii yote; 7 na tazama, talanta ya risasi iliinuliwa; na tazama, mwanamke akaaye katikati ya hiyo efa. 8 Akasema, Huyu ni Uovu; akamtupa chini katikati ya ile efa; akalitupa lile jiwe la risasi juu ya mdomo wa ile efa. 9 Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu.

 

Talanta au kipaji cha kuongoza (kwa Kiebrania kikkar) ni karibu sana na kusema kuwa ni santuri ya mviringo ambayo inafanyika kuwa ni kifuniko cha efa. Upepo kwenye mbawa zake ilikuwa ruach ao roho. Hivyo yalipata nguvu kwa nguvu za kiroho. Mfumo na imani hii ya kidini imepewa nguvu na Duniani kote na imetajwa au kuelezewa na Mashahidi katika siku za mwisho. Mfumo na imanii hii imefikishwa mwishoni na ujumbe wa malaika kwa Injili ya Ufalme wa Milele wa Mungu. Mfumo na imani hii itaangamizwa kwa ujumbe huo.

 

10 Ndipo nikamwambia yule malaika aliyesema nami, Hawa wanaipeleka wapi efa hii? 11 Akaniambia, Wanakwenda kumjengea nyumba katika nchi ya Shinari; tena ikiisha kutengenezwa, atawekwa huko mahali pake mwenyewe

 

Mfumo na imani hii vililazimika vichukuliwe na kupelekwa utumwani Babeli, na imani ya Kibabeloni ilianzishwa kwa sababu ya muundo mbaya na mpotofu wa kidini wa Israeli.

 

Kipindi hiki kinaishia kwa nyakati saba au miaka 2,520. Ni kama tulivyoona kwenye jarida la Kuanguka kwa Misri (Na. 36): Unabii Kuhusu Mikono Iliyovunjika ya Farao, kipindi hiki kinaanzia tangu mwaka 605 hadi 525 KK na kuishia kwenye miaka ya 1914 hadi 1995/6 BK. Huu ndiyo mwisho wa Utimilifu wa Mataifa. Awamu ya mwisho ya miaka thelathini kwa hiyo ilianzia kwenye miaka ya 1996/7. Kipindi hiki ndicho kinapelekea ujio wa Masihi. Mashahidi ni sehemu ya muhimu sana ya harakati hiyo.

 

Dola ya Mnyama itaruhusiwa kuwaua baada ya watakapohitimisha kutoa huduma yao ya unabii. Mii yao itaachwa ikiwa imelala mitaani kwa muda wa siku tatu na nusu. Mashahidi hawa watafanya matendo kama yaleyale aliyoyatenda Musa huko Misri. Magonjwa ambayo Musa aliyaamuru yawapate Wamisri yaliwapata kwa kusababishwa na imani yao ya kiroho kama Mashahidi watakaposhughulikia imani ya Byakati za Mwisho.

 

Mchakato huu uliathiriwa na Eliya aliyeshuhudia dhidi ya dini na imani potofu za uwongo za dini iliyokuwepo huko Israeli. Kwa hiyo Mashahidi hawa watashuhudia dhidi ya dini ya uwongo, kwa pande mbili zote, yaani kwa Waisraeli na kwa mataifa. Mfululizo wa unabii wao na upeo au kiwango chake vitatolewa baadae. Watu hawa wawili watakaofanya kazi na matendo ya Musa na Eliya, wangali bado hawajachukua nafasi zao. Muda muafaka wa kutangulia ujio wa Masihi. Kipimo cha Hekalu utaanza au kutangulia kitendo hiki. Uwa wa Nje utakanyagwa kwa miguu wakati wa kipindi hiki cha huduma ya hawa Mashahidi (Ufunuo 11:2-3).

 


 

Sehemu ya 2

 

Kuna jambo linguine kuhusu hawa Mashahidi linalojiri kwa upana zaidi kwenye unabii na jaribio kuliko hawa manabii wakuu wawili watakaosimama mjini Yerusalemu katika Nyakati za Mwisho kwa siku 1,260 wakiwa wamevaa nguo za magunia. Jambo hli limeeleweka vibaya na mara nyingi limekanganywa na walivyo hawa wawili wenyewe.

 

 


Mashahidi wameorodheshwa kwenye Biblia. Ni kina nani haa na Biblia inawazungumziaje?

 

Kwenye Isaya 43, Mungu anampajina Yakobo na Israeli kama mashahidi wake.

Isaya 43:1-13 Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. 2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza. 3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako. 4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako. 5 Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi; 6 nitaiambia kaskazi, Toa; nayo kusi, Usizuie; waleteni wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia. 7 Kila mmoja aliyeitwa kwa jina langu, niliyemwumba kwa ajili ya utukufu wangu; mimi nimemwumba, naam, mimi nimemfanya. 8 Walete vipofu walio na macho, na viziwi walio na masikio. 9 Na wakusanyike mataifa yote, kabila zote wakutanike; ni nani miongoni mwao awezaye kuhubiri neno hili, na kutuonyesha mambo ya zamani? Na walete mashahidi wao, wapate kuhesabiwa kuwa na haki; au na wasikie, wakaseme, Ni kweli. 10 Ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. 11 Mimi, naam, mimi, ni Bwana, zaidi yangu mimi hapana mwokozi. 12 Nimetangaza habari, nimeokoa, nimeonyesha, na hapakuwa mungu wa kigeni kati yenu; kwa sababu hiyo ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, nami ni Mungu. 13 Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye kuizuia?

 

Kumbuka kwamba kwenye andiko hili tuna Yakobo na Israeli waliotajwa kama watu tofauti.

 

Kwenye kifungu hiki, tunaona kwamba Mungu ndiye aliyemuumba Israeli (sawa na ilivyo kwenye Isaya 44:2,21,24) na ni mkombozi (Isaya 41:14; 48:17; 49:7). Mungu anawaita kwa jina nao ni watu waliokaribu nan i mali halisi ya Mungu (sawa na isemavyo Isaya 45:3-4; Kutoka 19:5; 33:17).

 

Mungu huwalinda watu wake kwenye hatari zote (Zaburi 66:12). Hapa tumeona kwamba kusamehewa kwa Israeli kunajumuisha mataifa ya Afrika (Misri na Ethiopia) na Uarabuni (Sheba). Cyprus ilitarajiwa kuyashinda mataifa haya yote (kama usemavyo ufafanuzi wa Annotated Oxford Bible, kwenye Isaya 43:3c-7). Msamaha huu hapa kwa kweli ilihusiana na wokovu wa Wamataifa.

 

Kutokana na Isaya 43:8-13 tunaona mlingano ufuatao ukijitokeza:

·      Israeli anaweza kuongoka (aya ya 8);

·      Mataifa yanakwenda kukusanyika pamoja lakini hawataweza kuishinda miungu yao.

Kutokana na kipengele hiki, Mungu anatangaza kwamba hakuna na hatakuwepo mungu mwingine (sawa na Isaya 41:23-24; 48:5).

 

Kutokana na Isaya 43:14 hadi 44:5 tunaona unabii unaohusu Ukombozi na Marejesho mapya ya Israeli. Hapa tunamuona Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli wakiwekwa mrejeo sawa. Mkombozi ametajwa mara nyingi kwenye Isaya kuliko mahali pengine popote. Katika Mwanzo 48:15-16 tunaona kwamba Malaika wa Ukombozi alikuwa ni elohim wa Israeli (sawa pia na Isaya 43:1; 54:5; 59:20; Yeremia 50:34; sawa pia na Isaya 41:14; 47:4; 48:17 kwa neno hili ma Mtakatifu).

 

Kwenye Isaya 43:22 tunaona Yakobo na Israeli wakitajwa tena kwa kutofautishwa.

 

Isaya 43:22 Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli.

 

Mungu anafanya hivyo tena kwenye Isaya 43:28.

Isaya 43:28 Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa patakatifu, nami nitamfanya Yakobo kuwalaani, na Israeli kuwa tukano.

 

Kwenye Isaya 44:1 ananena tena kwa wote lakini wakati huu ni kama kwa mmoja.

 

Isaya 44:1-5 Lakini sikia sasa, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua; 2 Bwana, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua. 3 Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; 4 nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji. 5 Mmoja atasema, Mimi ni wa Bwana; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa Bwana, na kujiita kwa jina la Israeli.

 

Hivyo, wawili hawa wako tofauti lakini wako kwenye mfumo wa mtu mmoja. Pia tunaliona jina Yeshurun (SHD 3484) likijitokezwa kwenye uwili huu. Neno Yeshurun linatokana na shina la neno yashar (SHD 3474) lenye maana ya kuwa mkweli au kunena kinagaubaga. Ina maana ya kufanya jambo moja kwa moja au kunena kinagaubaga. Inapelekea dhana ya usawa na haki.

 

Tunaona hapa kwamba Mungu alimkomboa Israeli si kwamba alistahili lakini ni kwa ajili ya uhusiano wake wa Kiagano na taifa hili. Mungu ndiye mfalme wao na ufalme ule utakuwa umerejeshwa wakati yeye ajaye ambaye haki inakaa ndani yake nani mfalme wa haki.

 

Mungu anaonyesha hapa kwamba atawafanya Israeli kuwa ni kama mtu mnyofu. Kwa hiyo, Yeshurun itaunganishwa pamoja na Yakobo. Yakobo ni jina la baba yao alipoanza safari ya imani, na Israeli ni jina alilokuja kuitwa baadae. Jina hili lilikujakuwa pia ni jina la taifa la wana wa Yakobo. Kwa hiyo ukuwili unaonekana wazi kabisa.

 

Kiumbe anayenenwa hapa ni Yahova, Mfalme wa Israeli na Mkombozi wa Israeli. Yeye ndiye Yahova wa Majeshi. Hapa kuna watu wawili waliotajwa kwenye Zaburi 45:6-7. Kiumbe huyu hapa ni haElohim aliyetajwa mahali pengine kama Yahovi wakati neno Yahova wa Majeshi halikutumiwa na yeye.

 

Anawatangaza hapa tena kuwa wao ni mashahidi wake.

 

Isaya 44:6-8 Bwana, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, Bwana wa majeshi, asema hivi; Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu. 7 Naye ni nani kama mimi atakayeita, na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? Na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze. 8 Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.

 

Mungu huyu ndiye Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3) na zaidi yay eye hakuna elohim. Wengine wote ni wadogo kwake. Tafsiri ya RSV ina neno linaloishia na kifungu kisemacho: “Hakuna Mwamba? Simjui mwingine”. Hii inaonekana kuwa imefichwa kwa Watrinitaria wasijue kea sababu ya mfano wake.

 

Isaya 44:8  Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.

 

Kwa hiyo, Mwamba mmoja ulikanganya pia mawazo ya mrengo wa kibaba wa hoja za Petro zilizokuzwa na kuakinishwa na Kanisa Katoliki la Kirumi.

 

Dhana iliyoko hapa ni kwamba Mungu anasughulika na Yakobo na Israeli kama mashahidi wake kwa mataifa. Uwili unaotajwa hapa sio uwili wa Israeli na Yuda. Ni uwili wa kimwili na kiroho. Yakobo ni jina aliloitwa baba mchamungu ambaye alikujakuwa Israeli, jina ambalo maana yake ni kwamba atatawala akiwa Eli. Kwa hiyo maana yake ni kwamba taifa ni shuhuda mmoja na Kanisa ni shahidi mwingine. Kwa hiyo, ni Kanisa ndilo linalofanyika kuwa mwili au bodi ya Israeli na litatawala kama Mungu au elohim, kama Malaika au Mjumbe wa Yahova akiwaongoza (Zekaria 12:8).

 

Dhana ya Israeli kulinganishwa na Kanisa imeainishwa kwa kina kwenye majarida ya Mithali 31 (Na. 114); Agano la Mungu (Na. 152); Wimbo Uliobora (Na. 145); Ufafanuzi Kuhusu Esther (Na. 63) na Upimaji wa Hekalu (Na. 137).

 

Ni siri kubwa na nyeti sana ya Mungu na kweli ya Kanisa. Kwa hiyo, sio wote waliomo katika Israeli ni Waisraeli, na siyo wote walio wana wa Ibrahimu ni watoto wake au uzao wake.

 

Warumi 9:6-11 Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. Maana hawawi wote Waisraeli walio wa uzao wa Israeli. 7 Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa; 8 yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazao. 9 Kwa maana neno la ahadi ni hili, Panapo wakati huu nitakuja, na Sara atakuwa na mwana. 10 Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akiisha kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu, 11 (kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye),  

 

Hivyo Yakobo alikuwa Mwisraeli wa kimwili ambaye ahadi ya haki ya uzaliwa wa kwanza alipewa, na kupitia kake yeye makabila yalibarikiwa (Wanzo 49:1-33).

 

Lakini alikuwa ni baba wa kimwili wa taifa. Baba wa kiroho alikuwa Mbinguni na kwa hiyo, taifa lilifanyika kuwa la aina mbili; na Wamataifa ndipo waliitwa kwenye taifa la Israeli na siyo la Yakobo. Paulo anaonekana kuwa anafanya tofauti hiyo pia kwenye waraka wake wa 2Wakorintho 11:22 na anawataja Wayahudi na Waisraeli.

 

Yacobo alikuwa ni shahidi wa Mungu kwa muda mrefu hadi kuanza kwa Kanisa. Kanisa lilifanyika kuwa shahidi tangu kipindi cha Masihi na kuendelea. Mgawanyiko huu unashabihi kwenye kipindi cha ufalme miaka – 1,000 tangu kipindi cha Daudi hadi cha Masihi na miaka 2,000 tangu kile cha Masihi wa Haruni hadi Masihi wa Israeli (au Ujio wa kwanza na wa pili).

 

Kipindi hiki kilitajwa pia na jeshi Sauli, ambalo aliligawanya kwa 2,000 na 1,000 na akawaweka kwake mwenyewe chini ya usimamizi na uangalizi wa Yonathan. Hii iliashiria falme za kimwili na za kiroho ambazo kwanza ndizo Daudi alikuwa ni mfano wake daudi alionyesha kuelekea Masihi. Hakuna shaka kuhusu andiko hili na maana ya Warumi.

 

Waisraeli wa sasa ni Kanisa. Hivyo, ni kwenda mbali zaidi kulitendea kazi andiko hili kwenye Isaya hadi kwenye andiko lililo kwenye Ufunuo 11:1-14.

 

Ufunuo 11:1-14 Nikapewa mwanzi kama fimbo; na mmoja akaniambia, Inuka, ukalipime hekalu la Mungu, na madhabahu, na hao wasujuduo humo. 2 Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili. 3 Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia. 4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi. 5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa. 6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo. 7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua. 8 Na mizoga yao itakuwa katika njia ya mji ule mkuu, uitwao kwa jinsi ya roho Sodoma, na Misri, tena ni hapo Bwana wao aliposulibiwa. 9 Na watu wa hao jamaa na kabila na lugha na taifa waitazama mizoga yao siku tatu u nusu, wala hawaiachi mizoga yao kuwekwa kaburini. 10 Nao wakaao juu ya nchi wafurahi juu yao na kushangilia. Nao watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa kuwa manabii hao wawili waliwatesa wao wakaao juu ya nchi. 11 Na baada ya siku hizo tatu u nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama. 12 Wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, Pandeni hata huku. Wakapanda mbinguni katika wingu, adui zao wakiwatazama. 13 Na katika saa ile palikuwa na tetemeko kuu la nchi, na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka; wanadamu elfu saba wakauawa katika tetemeko lile. Na waliosalia wakaingiwa na hofu, wakamtukuza Mungu wa mbingu. 14 Ole wa pili umekwisha pita, tazama ole wa tatu unakuja upesi.   

 

Hapa tunaona kwamba manabii wawili wamekuwa wakitajwa kwa namna kwamba wametabiri kwa musa wa siku 1,260. Wamekuwa na uweza wa kuzifunga mbinguvu wakati wa kipindi chao hiki cha kutoa unabii na kuifanya mvua isinyeshe kabisa, na hawatauawa hadi watakapo hitimisha kutoa unabii wao. Baada ya kuuawa kwao, watalazwa mitaani kwa siku tatu na nusu na hatimaye watapaa juu mbinguni.

 

Mtu anaweza kusema kwamba kulikuwa na mambo au mitazamo miwili kuhusu unabii huu kwanye hilo kwamba siku 1,260 za mateso zilikuwa pia ni miaka 1,260 ya kudumu kwa ile iliyojulikana kama Dola Takatifu ya Kirumi, iliyodumu tangu mwaka 590 hadi 1850 BK wakati kweli ilipopigwa maufuku watu kuihubiri au kuifundisha. Baraza la mahakama ya kidini la mwisho lilifanya kazi tangu mwaka 1823 hadi 1846 na takriban watu 200,000 walihukumiwa kifo, au wafungwe maisha na picha au michoro, iliyopo kwenye Nchi ya Papa peke yake. Wengine wapatao 1,500,000 walewekwa kwenye kifungo cha uchunguzi wa kisiasa (kama kinavyosema kitabu cha Malachi Martin cha: The Decline and Fall of the Roman Church [Kudhoofika na Kuanguka kwa Kanisa la Kirumi], kurasa za 250-254).

 

Hapa tunafika kwenye kichekesho lakini chenye mashiko wa Mashahidi hawa Wawili kuwa ni taifa na Kanisa. Taifa na Kanisa ni mashahidi wanayoyashuhudia mataifa, lakini wote hawa hawatauawa katika Siku za Mwisho, na miili yao haitalala kwenye mitaa ya Yerusalemu kwa siku tatu na nusu.

 

Tunajua kutokana na Isaya kwamba kutakuwa na tukio kuu sana la Kutoka la mataifa kwenye Nchi ya Ahadi katika nyakati za mwisho ambapo kutafanyika tulio la kutoka la Misri lisikumbukwe tena.

 

Isaya 66:18-24 Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu. 19 Nami nitaweka ishara kati yao, nami nitawatuma hao waliookoka kwa mataifa, Tarshishi, na Puli, na Ludi, wavutao upinde, kwa Tubali na Yavani, visiwa vilivyo mbali; watu wasioisikia habari yangu, wala kuuona utukufu wangu; nao watahubiri utukufu wangu katika mataifa. 20 Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema Bwana; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka yao nyumbani kwa Bwana katika chombo safi. 21 Na baadhi ya hao nitawatwaa kuwa makuhani na Walawi, asema Bwana. 22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana. 24 Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.

 

Hivyo, taifa halitauawa na Waisraeli wataendelea kuwepo. Ni wazi sana kwamba watakuwa na kazi ya kufanya katika kipindi cha Milenia. Kwa hiyo, maneno yaliyoko kwenye Ufunuo 11 hayawezi kuwa yanalitaja taifa na uzao wa Yakobo.

 

Kwa hiyo kazi ya aina hizi mbili za makundi zinajulikana na ziko wazi. Kazi ya kwanza kama mashahidi halisi wa kimwili na kama mashahidi wa kiroho kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu mbili ya Kanisa kuwa jangwani. Taifa la Israeli lilikuwa pia ni watu ambao walipewa majukumu ambayo Kristo aliyasema wakati aliposema kuhusu wajibu kuwa umeondolewa kutoka Yuda na wamepewa wanaozaa matunda (Mathayo 21:43).

 

Mashahidi hawa kwa hiyo ni awamu ya mwisho kwenye mchakato huu na watauawa baada watakapokuwa wameifanya kazi yao. Hii imefanywa kwa sehemu na Masihi kwa kazi aliyoianzisha mzingi wake kwa siku tatu, mchana na siku tatu usiku kaburini na kisha akasubiri hadi asubuhi aenda mbinguni akiwa kama Mganda wa Kutikiswa.

 

Hivyohivyo ndivyo itatokea mwishoni. Ni kama walivyouawa Kristo na Yohana kwa kuwashuhuda kwao Yuda, ndivyo itakavyokuwa pia kwa Mashahidi hawa wa Nyakati za Mwisho watakavyouawa. Watu wa dunia yote watabadilishana au kupeana zawadi kwa kusherehekea kuuwawa kwao. Hii haiwezi na haitaweza kufanyika kuhusu taifa la Israeli na Kanisa. Na kama iliwahi kuwa hivyo, basi Maandiko yangekuwa yametanguka, lakini Maandiko hayawezi kutanguka. Mmoja ni mfano wa mwingine.

 

Kanisa linasimama kama shahidi anayeishuhudia dunia. Wengi wa wateule waliopo Kanisani wamekuwa wakiuawa kwa sababu za Kiimani kwa kipindi chote cha zaidi ya miaka 1,260. Hata hivyo, sio wote watakaouawa katika siku za mwisho. Na kwa jinsi hiyohiyo, ndivyo taifa nalo litadumu. Sababu ya kurudi kwa Masihi ni kwa faida ya wateule. Kama hatarudi wakati Mungu atakapokuwa anakifupisha kipindi hiki cha siku za mwisho, hakuna mwenye mwili atakayeachwa akiwa hai.

 

Mathayo 24:21-22 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. 22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.  

 

Siku hizo zitafupishwa kwa ajili ya wateule. Kama wateule wote wangekuwa Kanisani, na kuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu, hivyo basi lisingekuwa ni suala la ama siku hizo zingefupishwa au siyo. Bali atarudi ili kuwaokoa wale walio taifa litakaloingia kimwili kwenye Milenia na kutawala kama wafalme wa kimwili na makuhani ili kuufanya Mpango wa Mungu uhitimike.

 

Kwa hiyo hawatakufa na kulala mitaani. Ushuhuda ni mchakato endelevu, na mwishoni utawahusisha manabii wakuu na mashuhuri wawili pia na wakiwa wamepewa majukumu hayo na Kanisa na taifa kwa karne nyingi.

 

Kwa hiyo Kanisa na taifa vitafanya kazi kwa mambo yafuatayo:

·      Kutokana na ufalme wa kimwili huko Yerusalemu hadi kwenye ufalme wa Masihi na wa kiroho wa Kanisa pamoja na kuangamizwa kwa Hekalu la kimwili; na

·      Kutokana na miaka 1,260 ya kuanzia mwaka 590 hadi mwaka 1850 BK.

 

Kuna ushabihiano wa kimwonekano wa Mashahidi Wawili wa siku 1,260 za mwisho au miaka mitatu na nusu ya mapema sana kabla ya kurudi kwa Masihi.