Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[144]

 

 

 

 

Ufalme wa Milele wa Mungu 


(Toleo la 3.0 19951124-20001021-200070718)

 

 

Masomo haya yanaghusia kwa kina lengo la mpango wa ukombozi pamoja na matokeo ya mwisho. Mji wa Mungu unaelezewa (Taz pia nakala hii Jiji la Mungu (nambari 180)) na umuhimu wa Kiroho ukitamblika. Harakati za Mungu kwa mfumo wa sayare hii huitaji mpangilio mpya wa muundo wa utawala wa ulimwengu.Hili limetatiminiwa 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati miliki  © 1995, 1999, 2000, 2007 Wade Cox)

 

 

(Toleo. 2012)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 

 

 

 

 



Ufalme wa Milele wa Mungu

 


Umuhimu haswa na kusudi la Ufalme wa Mungu ni kuleta hatima ya kila aina ya upotovu wa ulimwengu huu. Katika kuasisiwa kwa ufalme wa Mungu, dunia hii itarejeshwa pale ilipokuwa awali kabla ya uasi, lakini mara hii ubinadamu ukiwa mkamilifu zaidi.

 

Hawali, tumelighusia kwa kina swala la uasi wa Jeshi na jinsi ambavyo theluthi yao walivyoasi na kuangamiza sehemu mbalimbali za dunia, pia kuharibu mifumo ya ulimwengu, hali iliyohitaji kuundua upya. Tumo mwishoni mwa miaka elfu sita (60000) sasa ambapo uwezo wa shetani umezuiliwa. Kipindi kingine tutapitia ni kile cha miaka elfu moja (1000) kitakachoendelea hadi wakati wa ufufuo wa wafu. Katika ufufuo wa jumla,tutakumbana na kipengee cha ubinadamu kutokana na uumbaji baada ya kukumbana na kipengee cha Kiroho, na kufanya hii dhana  kufahamika  zaidi na, baadaye,tutakuwa na Uzima wa milele.

 

Tunavunja kila njia ya uwezo wa mapepo, kila mamlaka na utawala ambako yalikojengwa kwayo, na kila asasi ya serikali zilizoasisiwa katika ulimwengu. Ulimwengu si pahali pekee ambako kuna nguvu za mapepo. Ulimwengu uligawa katika vitengo vinne na kupewa nguvu chini ya baraza la Mungu (Elohim). Mapepo yalizuliwa duniani ili kuhukumiwa. Chini ya Baraza kuu lenye washirika sabini, kila mmoja alipewa mataifa ili Mungu aweze kukumbana nao.(kumbu 32:8-9).

 

Kulikuwa na mataifa sabini na washirika sabini wa Baraza la nche la Mungu (Elohimu). Waliwajibikia kuleta mataifa katika hukumu. Baraza kuu la Isiraeli wa zamani (Sandhedrin) ni kioo cha baraza la Mbinguni, na hicho kioo kilikuwa na takribani watu sabini, na kulikuwa na mataifa sabini yaliyowekwa chini ya watu hao. Kulingana na ufahamu kutona na nakala ya Kimasoreti Bibilia imebadilishwa li kuficha kiasi cha ukweli uo na nguvu hizo pia

 

Kuna maana tele katika kila mojawapo ya sentensi inayoghusia nguvu hizo, kwa mfano, katika taarifa ndogo yenye utata katika 1 wakor 15:24-28

1Wakor.15:24-28 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.

 

Dhana hii ni kuwa Yesu kristo ameharibu pingamizi sote zilizo kinyume na mapenzi ya Mungu na kukabidhi ufalme kwa Mungu.

 

25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

 

Kwa hivyo utawala wa Kristo ni kipindi cha masharti kinachoagizwa na Mungu ili kufunga nguvu za dunia na miliki pingamizi kwa Mungu. Kipindi hiki hakiamriwi vivi hivi tu, bali Mungu, katika ufahamu wa yote Alisema tutatawala kutimiza mwisho huu. Kipindi cha miaka elfu moja ni kipindi maalumu cha pumziko, ambacho ni mchakato wa kazi iendeleayo ya Ukuhani, kwa kuwa Ukuhani ulifanya kazi nyingi katika Pumuziko la sabato kuliko wakati mwingine wowote ule. Kulikuwa na wanyama wengi waliochinjwa, na Wakuhani walifanya kazi nyingi zaidi katika siku ya Sabato kuliko wakati wowote jumani. Mapumziko ya sabato si kupumzika kotokana na tendo, ni pumziko kutokana na ajira.  Tendo la Sabato linaenenda pamoja na mapenzi ya Mungu na kwa kumuabudu Yeye.

 

Kipindi cha miaka elfu moja si pumziko tu kulingana na ile dhana kuwa ni kukoma kuenda kazini.Ukuhani basi hufanya kazi zaidi. Hicho ni kipindi chao cha ajira. Sababu ya kuwekwa kwa dhabiu kwa njia hiyo ilikuwa kiashirio kuwa katika siku ya Sabato tufanye kazi zaidi. Katika kipindi cha miaka elfu moja ndipo kazi yetu itaanza.

 

Kipindi cha miaka elfu moja ni mchakato wa matendo ya mara kwa mara kila wakati wa Ukuhani ili kuandaa sayare kwa kumuabudu Mungu, na kufungwa kwanguvu za giza ili kila kitu kikabidhiwa kwake Mungu.

 

26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.

 

Taarifa hiyo inaashiria mwisho wa Maisha yote ya kimwili. Mauti yana maana tu kuhusiana na maisha haya tuanayona ya kimwili. Tukisha kufa akuna mauti tena. Ni dhana ambayo atuna. Kunaye mwingine aliye na hiyo dhana kutuusu. Tutakapofufuliwa na kuwa vyumbe vya Roho, hakuna atakayekuwa na dhana kuhusu kusita kwa vitendo vyetu. Tumekirimiwa uhai wa milele.Tumekirimiwa kutokufa kutoka kwa mungu ambaye hukirimu uhai wote. Hivyo sote tuko hai Kiroho. Kunao tukiu la mara kwa mara. Kimsingi, vitendo vya kimwili lazima vitasita ndipo mauti yakome kuwepo.Hii inatueleza kuwa hakutakuwa na uwepo wa kimwili.

 

27 Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo.

           

Mungu aliweka vitu vyote chini ya kristo.Ni wazi kuwa, ikiwa tutaweka kila kitu chini ya mtu fulani hatujiweki chini yake. Ikiwa tutagatua mamlaka kwa mtu mwingine basi hatutagatua mamlaka yayo hayo chini yao kwetu tena maana hili litafifisha dhana ya ugatuzi. Baadaye tunaona upotovu wa utatu. Paulo ni wazi hapa anaposema mungu aliweka vitu vyote chini ya kristo lakini akajitoa katika mfumo huo. Mungu hakumwinua kristo juu yake bali juu ya viumbe.

 

28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.

 

Ni bayana kuwa mwana ndiye aliye chini ya Baba, kwa hivyo, usawa haupo. Kristo hapa atakuwa chini ya mungu; hivyo basi mawazo ya utatu ni upotovu.

 

Neno kuwa mungu anaweza vyote kwa wote katika biblia (RSV)kwa kweli ina tokana na panta an pasini maana yote kwa yote.Tunaona katika waefeso 1 kuwa hili linafanyika ili Mungu afanyike vyote katika yote kupitia kwa Roho.Ni Roho Mtakatifu anaoruhusu mungu kuingia na kufanyika moja na Kristo, kama ilivyo nasi. Bila Roho Mtakatifu Kristo hangeweza kuwa umoja na mungu na mungu hangeweza kutimiza uwezo wake na mamlaka.

 

Kwa hivyo, Roho Mtakatifu ndiye njia kupitia kwayo yesu anatimiza nguvu na mamlaka.

 

Kristo hakuumba roho Mtakatifu, bali ni nguvu za Roho Mtakatifu zinazomwezesha Yesu Kristo na ndiyo maana Yeso kristo nasi tu warithi wa nguvu za Mungu.Hii pia ndiyo sababu utatu chini ya ukatoliki wa Rumi ni potovu.Utatu wa kimashariki hauneni hivyo.Utatu una nadharia nyingi.Utatu wa kiOthodoksi unasisitisa kuwa roho Mtakatifu hupatikana kutoka kwa baba tu bali si kutoka kwa Mwana.Utatu wa kimagharibi hunena kuwa roho mtakatifu hutokana kutoka kwa Baba na Mwana. Hii ndiyo iliyoshababisha kuwepo kwa uabudu wa miungu mwaka 1054CE .Uabudu huo wa miungu ulikuwa  sawa kuilingana nao. Wagiriki waliona kuwa utatu ni kitu ja ajabu kabisa. Roho Mtakatifu hutokana kwa baba na huwezesha wana wote wa mungu.

 

Tunaibua ubinadamu wote kuwa na uhusiano na mungu, ili kupata Roho Mtakatifu na kuwawezesha wao kuingia katika urekebisho na hukumu ili kuingia katika mchakato wa utakatifu. Mara tu nguvu za mapepo zinavunjwa, mapepo yanaletwa kwa urekebisho na Jeshi huamishwa katika nguvu chini ya Yesu kristo na chini yetu pia. Hali yote hurejeshwa chini ya mapenzi ya mungu.

 

Mapepo hayatakuwa nche ya mapenzi ya Mungu tena. Mfumo kamwe  hautafanya kazi nche ya mapenzi ya Mungu.Tumerejea chini ya mapenzi ya Mungu, kwa hivyo Mungu moja ni imara, Roho mtakatifu baadaye hurejea katika vyote; Baadaye kutakuwa na mfumo kamili chini ya mapenzi ya Mungu. Hakutakuwa na kuabudu miungu na ulimwengu wakati huu utakuwa na uhusiano tangamano.Hili litakapotukia tutakuwa katika hali ya kuukabidhi ufalme kwa mungu.

 

Mungu ataweza kuja duniani na kuhamisha  utawala wa ulimwengu hapa. Hatuwezi kutawala ulimwengu kwa utangamano ikiwa kuna uovu katika sayare. Fujo zapaswa kuondolewa kabla Mungu kuhamisha serikali yake huku. Kwa kuwa utawala wa sasa hautawaliwi kutoka kwa hii sayare. Wakati huo dunia yote itajaa utukufu wake (isaya 6:3), na Mungu pamoja na mwanakondoo watakuwa nuru ya huo mfumo (Ufunuo 21:23). Mchakato huu unaendelea kupitia kipindi cha miaka elfu moja mpaka ufufuo, na mwishoni mwa mchakato huu kutakuwa na uumbaji mpya.

 

Isaya 65:17-18 Maana, tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. 18 Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. (Biblia Takatifu BT)

 

Muundo wa mfumo wa utawala utakuwa kutoka Yerusalemu walakini kutakuwa na Mbingu mpya na dunia mpya. Hivi ni kusema, dunia hii, tunavyoijua, itaangamizwa. Dunia hii italemewa sana kufikia ile jioni ya siku ya Bwana, na hakutakuwa na samaki aliyehai katika ziwa; hakutakuwa na ziwa lilosalia, hakutakuwa na miti; kutapakia wanyama wachache walio hai na ndege watakuwa wakila mamilioni ya mizoga katika duniani. Hii inatuelezea kuwa lazima kuwe na matengenezo ili kutakazwa kwa moto. Katika uumbaji wa pili chini ya yelusalem, ziwa zitaondolewa.

 

Isaya 66:22-23 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana. (Biblia Takatifu BT)

 

Mbalamwezi mpya na Sabato sote ni siku za kuabudu.Hii inatueleza mambo kadhaa .Dhana ya mbalamwezi mpya na sabato itasalia katika siku kuu kama vipindi vya kuabudu vya lazima katika muundo wote. Bila shaka itakuwa kupitia kipindi cha miaka elfu moja. Lakini pia inaeleza juu ya mbingu mpya na nchi mpya. Kwa hivyo, vipindi vya kumuabudu Bwana vitaendelea kwa njia tofauti, walakini dhana za vipindi vya mbalamwezi na sabato zilizodhibitiwa zitasalia. Kama mtu atanena nasi kuwa: hakuna haja ya kuitunza sabato au hatupaswi kutunza mbalamwezi mpya mwelekeze kwa isaya 44 na Zakariah 14. Tutakuwa tumewaonyesha kuwa wanapaswa kufanya hayo. Ni wazi kuwa Masia ataendelea.

 

Kushuka kutoka Mbingu

ufunuo 3:12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.

 

Kristo ataandika jina la Mungu katika wateule. Hivyo basi,Mungu baba ni Mungu wa Kristo tunapojua kutoka Zaburi 45:4 na Waibrania  1:8. Kristo ameandika pajani mwake,”mfalme wa wafalme na bwana wa mabwana” na analo jina la Mungu wake. Watu watakapotuona watasema Mungu (Elohimu) na watebeba jina la Yahova (Yeova).Hii inaonekana kuwa dhana isiyokuwa ya kawaida. Watakapotuona watasema “naam”, Mtakatifu-Naam Mungu.Tutakuwa majaji wa mpangilio huo mpya.

 

Yesu kristo anasema wazi, kipindi hiki ambacho ni baada ya ufufuo wake kwamba, wale walio waminifu watafanyika kuwa nguzo za hekalu la Mungu. Kwa hivyo hekalu itakuwa mwiinuo wa kiroho bali si ile ya kuonekana. Mungu yuko ndani ya kila mmoja wetu na tunenapo watangundua kuwa nguvu za Mungu zanena kupitia kwetu. Hii ndiyo sababu watatuchukulia kuea kama Mungu (Elohimu).Tutakuwa kama Mungu, kwa kuwa tunanena kwa ajili ya Mungu. Tuenapo kwa niaba ya Mungu hatufanyi makosa, ikiwa tunao ucha Mungu ndani yetu kwa njia ambayo tutatekeleza mamlaka.

 

Nguzo hizi za hekalu ya Mungu ambazo ni kanisa la Kifiladefia, ni imara katika muundo wa hekalu. Muundo umejengwa katika msingi na msingi unauwekwa thabiti. ilivyo nguzo ni msingi wa imara ambazo husimamisha  hekalu. Hata kama ni wadogo mno na huwakilisha nguzo chache, Wafiladefia ni sehemu shupavu ya hekalu.Wanatawala jinsi ambavyo Wathiatira wanatawala mataifa kwa fimbo ya chuma. Wanatawala katika ufalme wa mungu kwa mihadi kwa Walaodekia. (Ufunuo 4:20-21)-

Wale walionusurika, lakini wachache watachukua nafasi zao. Wafiladefia watatekeleza nguzo zote za kizazi lakini wao ni miundo shupavu ya hekalu.Dhana ya “hakuna kuondoka nche tena” ina maana kuwa watakuwa wamekuwa hapo na hawataondolewa kama ilivyokuwa hapo hawali.

 

Yerusalem mpya ni Jiji takatifu ambalo linaloshushwa chini na hata kwa uumbaji na ambayo ni Mbingu mpya na dunia mpya.

 

Ufunuo 21:1-27 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

 

Uumbaji hautasalia jinsi uliyo sasa.Utaharibiwa Kwa moto pamoja na kila chembechembe za mastakimu ya binadanu zitaondolewa. Mungu hahitaji ziwa kuwepo kama viumbe vya kiroho hatuhitaji maji ili kuishi, maadam tutakuwa kupita uepo wa kimwili.

 

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

 

 Kuna dhana mbili za bi harusi. Moja ni kuwa kanisa ni Bi harusi; nyingine ni kuwa Yerusalem mpya ni Bi harusi. Kuna kuunganishwa kwa Jeshi la Mbingu na la duniani. Jiji la Mungu linashuka kutoka mbinguni na sisi tunaunda hekalu linaloketi katika mwa Jiji la Mungu. Jiji la Mungu ni mwinuo wa Kiroho, ambapo Jiji lote ni miinuo ya Kiroho. Malaika hujumuisha sehemu ya Jiji la mungu. Ikiwa tutaangazia upana wa jiji la mungu ni stadia  12,000 au kama maili 1500 Hii ndio kusema kuwa ni sehemu kubwa; hata hivyo, ukadirio huo wa upana ni wa kimfano tu. Hekalu la mungu haliwezi kusimama kama mawe moja juu ya lingine, Ni mahali ambapo mungu anaishi ndani mwetu, na sisi ndani ya mji wa mungu unaozingirwa na malaika ambao ndio mawe ya mji wa Mungu (Taz Mji Wa Mungu [180]). [The City of God (No. 180)]

 

Sisi sote ni mawe yaliyohai na vipimo ni kimfano kutuonyesha ukubwa wa mji huo na Jeshi la mbingu wataunda Jiji la Mungu. Tunapoupunguza kwa vipimo vya kawaida,vipimo hivyo havieleweki.Viko katika  hali ya kawaida ili tupate kuelewa kuwa kuna hatua sita ili  kufahamu sebuleni ya hekalu, kwamba unapopanda kupitia hatua sita za mpangilio wa sherehe za mwaka wa saba (Yubilii) hadi mwaka wa arobaini na mbili. Hatua ya mwisho, ambayo ni hekalu halisi,ni wakati tunapoingia hekaluni katika hatua ya mwisho na kuingia kwa patakatifu pa patakatifu katika siku ya kupatanishwa katika mwaka wa sherehe za Yubilii.

 

Wanajenga kitu kinachoonekana kutueleza jambo litakalotokea zaidi ya miaka hamsini ya uhai wa binadamu, ikiwa tuko chini ya mpangilio wa Mungu. Kwa hivyo, tukishaelewa vitu vinavyoonekana tunaelewa maana yake. Hivyo basi binadamu si atua sita moja juu ya nyingine.

 

Dhana inahusu atua sita za maisha yetu, moja juu ya nyingine, ili kututayarisha kwingia patakatifu pa patakatifu katika awamu ya mwisho ya mwito wetu. Wengine hawapewi miaka hamsini, wengine wameitwa wakiwa wamecheleewa, na hawapokei awamu nzima. Kwa hivyo tumeitwa wakati ambapo tutaingia katika hukumu pahali furani hapo katika hatua hiyo.Tunaingia ili kwamba kutakuwa na wakati wa kutoka tukiwa tumehitimu.Tunaweza itwa ndani bila ya kufanya hayo yote kwa sababu tunao sifa za kutosha kumwezesha mungu kufanya kazi katika awamu ya mwisho kutuweka sisi katika patakatifu pa patakatifu. Tunaweza kuwa namwaka mmoja tu au zaidi katika mwito. Huenda tukabatizwa na tukawa katika awamu yamwisho ya hekalu tuingie katika patakatifu pa patakatifu. Huu ndio mji wa Yelusalem.

 

Tukiwa tumewekwa ndani ya mji,mji unashuka kutoka mbinguni,na mji wote umeundua kwa Malaika walio hai.Tukiwa katikati ya mji kama serikari ya Mungu. Huo ndio ufahamu kamilifu wa Yerusalem mpya na sote zinajumuika pamoja, bila mvutano.

 

Hekalu, ambayo ni wateule imewekwa katikati ndani ya yerusalem mpya. Mungu na mwanakondoo ni nuru ya Hekalu na wanaangaza Mji. Roho inatiririka kama moto na mji wote unanyunyuziwa maji kutoka Hekaluni ambayo ni Mungu. Ule Roho Mtakatifu ni maji yanayotutuliza na kuunganisha mji. Katika ule mchakato wa mji wa mungu kushuka chini utapata Jeshi la binadamu wote pamoja baadaye kujengwa kuwa mji wa Mungu.

 

Sisi katika ufufuo wa kwanza tutakuwa kama Hekalu la Mungu katika ya Mji, Sababu Mji wote ni nyenzo za Hekalu ambamo Mungu Yupo, nasi ndio lile Hekalu. Hata hivyo, katika Mji wa Mungu, Mji wote ni Hekalu kwa kuwa wote wamewekwa wakfu kwa Mungu. Kunao tofauti baina ya Hekalu la Leo na Mji ule. Hii ndio tukio la mwisho la wakati huo wote. Hivyo tutaenda zaidi ya ule mchakato. Tumejiandaa wote kuolewa na Yesu Kristo ili atuelekeze katika mfumo ule atufanye sehemu ya muundo wa serikali.Tutakuwa Bi arusi wa Kristo na wana wa Mungu. Sasa, tutafanyikaje kuwa Bi arusi na wana wa Mungu? Tutaweza na tutakuwa, kwa sababu hizi ni dhana za kijazanda .Tumejiandaa wote hivi kwamba sote tukabidhiwe kwake Mungu.

 

Yesu Kristo ataunda sheria mpya na mamlaka, ili Yerusalemu mpya, Jeshi la Mbingu, wanajumuika nasi, wateule, kama Bi arusi wa Kristo na muundo mpya wa serikali utafanyika. Kutakuwa na maagizo mapya ya serikali Mbunguni. Kutakuwa na Baraza jipya la Mungu (Elohim) litakaloundua, Kutakuwa na Baraza jipya tangulizi la sabini (kwa kweli, sabini ongeza mbili; Taz Luka 10:1). Baraza jipya tangulizi la 120,300 na 500 litaundua na kutakuwa na maagizo yakayojumuisha hadi 144,000.

 

Wafalme na wakuhani watateuliwa na kupewa mamlaka na vyumbe vya Kiroho na sehemu ya majukumu. Kila idadi ya upako uliofanywa na Yesu Kristo tokea mitume 12 hadi 3 000 chini hadi 144,000 una umuhimu na uhusiano na serikali ya Mungu. Hakuna jambo la ghafla. Vyote vinauhusiana na kafara za karne zinazojumuisha kipindi baina ya kuja kwa Kristo na kurejea kwake.

 

Wateule wanaletwa Hekaluni kama Kafara Lake. Vitomeo hivyo basi hujenga muundo wa serikali na nguvu za Mungu. Hao 1000 wapya wamejumuisha katika 70, 120,300 na 500 wakiwa na misumaa kuleta jumlaa (Taz Ayubu 33:22-23)

 

Wateule wanatekeleza utawala vile vile ambvyo tawala za ulimwengu zinavyotekeleza uwezo wao. Kwa mfano mfumo wa kibabeli ulijaribu kutekeleza nguvu kupitia vyenzo 120. Waliita 127, lakini kulikuwa na makamanda wa kanda saba na vyenzo 120. Walijaribu kuiga Ufalme wa Mungu, kwa sababu ukweli hawa 120 ni hatua nyingine inayofuata baada ya ile ya sabini. Huyu alikuwa Shetani akijaribu kuiga umbo la kawaida la ufalme na serikali ya Mungu.  Hatimaye itakuwa 144,000, na hawa watakuwa watawala. Chini yao kutakuwa na halaiki na watatawala vipengee vyao muhimu, kama wale watakuwa wafalme na wakuhani duniani.

 

Halafu tutakuwa na kizazi chote cha binadamu katika mfumo huo. Kizazi cha binadamu kitaunganishwa na malaika nao watakuwa mji ambao utatawaliwa na hawa wafalme na makuhani - mabilioni yao.

 

Tutashiriki katika mambo yote haya na tutapewa majukumu ya moja kwa moja na tutapewa wajibu kama wafalme na wakuhani katika mfumo huo. Tutapewa umati chini ya ulinzi wetu katika mahali tofauti kwenye mfumo huo wa utawala. Sio tu kwa kipindi cha miaka elfu moja, na sio tu katika Jeshi la kibinadamu, bali tutashikamanishwa na Jeshi la heshima kuu la vikozi vya malaika; ambao ni ndugu setu.  Tutawaona kina Mikaeli, Gabirieli, Rafaeli na malaika wengine wote. Tutakumbana nao na tutakuwa sawa. Tutakuwa na uwezo wa kufikia historia ya binadamu na ufahamu wa binadamu, na siri za Mungu, ambazo tutazielewa.

 

Jeshi la Mbinguni wanasoma siri za Mbingu kupitia kwetu hivi sasa, wanatamani kuona siku za halafu ambapo tutapata ufahamu (1Petiro 1:12). Mungu hajafunua yote kwao au kwetu. Atakapofunua hili kwetu litafunuliwa kwao pia. Yeye uwaonyosha kupitia kwetu kuhusu siri zake ili waone hekima ya Mungu, sababu ni kupitia hili watatekeleza imani yao.Walakini wanapaswa kutelekeza imani yao ili waweze kuona mbali kuliko vile tunavyoona. Tunaona kupitia kioo cheusi vile Paulo anavyosema. Lakini hawajui ni nini hasa matokeo hatimaye na kuwa wamo vitani. Wanamtazama Mungu kwa baadhi ya siri vile zinavyofunuliwa kwetu katika Roho Mtakatifu na kupeanwa kanisani.

 

Katika nyakati za mwisho, mpango na siri za Mungu zitawekwa wazi, makanisa na vizazi vitaingia katika matokeo, na siri sote zitawekwa wasi. Jeremiah anavyosema, katika siku za Mwisho tutafahamu haya vizuri zaidi. Litawekwa wazi ili makuhani nao waelewe pale walikosea. Walakini Malaika wadumishe imani wakingoja siri zifunuliwe, si kupitia kwao, bali kupitia kwetu sisi. Hilo linahitaji unyenyekevu na shetani hangeweza kudumisha unyenyekevu. Mikaeli na Kristo wanaweza vilevile Gabriel anaweza. Ilikuwa wangoje na kusikiliza kwa msingi na vyumbe vidhaifu kutoa siri za Mungu, hivi kwamba wakati huo wataelewa hatua inayofuata katika uibuzi, Hii ndio unyenyekevu. Shetani hangeweza kufanya hivyo.

 

Tunachokitazama toka hapa ni kuwa Mungu anawanika wote katika mahali tofauti katika Ufalme. Yeye aliye wa kwanza atakuwa wa mwisho. Kuna watu wengi Sana wanaofikiria kuwa wao ni watakatifu na wamefikiria kuwa wao ni wa umuhimu katika Ufalme wa Mungu. Walifikiria kuwa wao walikuwa wapaao juu, walakini hawatakuwa wapaao Juu katika Ufalme. Fikira kama hizo zinatuweka chonjo Sisi sote. Msimamo huo hunena kuwa tunao kitu cha kutegemea Kiroho. Watu wanaofikiria kuwa wao ni moto, Kwa kweli wako taabani maana wanaibua haki za ubinafsi. Wao huanza kuwakejeli ndugu zao na hivyo huanza kuibua mafundisho ya Wanikolati. Mungu anachukia mafundisho hayo kwa sababu yanajaribu kutenganisha huduma na kweli na vinazaa dhana ya huduma kuwa kuu kuliko kweli, ambayo ni kinyume cha Bibila. Hivyo “yeye aliye wa kwanza atakuwa wa mwisho”, inatukumbusha kuwa tunao wajibu na tuwe tahadhari kwa kuwa huenda tukaanguka.

 

Wanawaka watatuaa nafasi muhimu katika hatamu na wajibu na mamlaka. Wengi watatawala juu ya wanaume (watangulizi) kwa idadi kubwa. Wanaume watadharauliwa na kukejeliwa kuonyeshwa vile walivyowatendea wanawake. Hili linapotokea, watapaswa kutubu, na wataonyeshwa ni kwa nini wako katika ufalme. Itakuwa bayana ni kwa nini wanawake watatuaa uongozi juu yao. Hii ni kwa sababu wao ni washupavu Kiroho na si mshangao kwamba wanawake wengi wanaaelewa ukweli huu. Kuna wanawake wengi washupavu kiroho katika kanisa katika nyakati hizi za mwisho. Katika Nyakati za mwisho. Kwa msingi wa kukadiria huenda tukapata kuwa kuna wanawake shubavu miongoni mwa wateule kuliko wanaume, hakika  walilazimika kuvumilia sana na wakapata uzoevu mwingi kutokana na ugumu. Wanao mtazamo havifu   kuhusu umuhimu wao.Tutakapopitia siku za Mwisho za mateso makuu, hili litakuwa hamana kubwa wala si kihitaji.

 

Kuna aina nyingi ya mambo yatakayojiri Katika ufalme.Wajibu wetu ni kuandaa wote waliokabidhiwa kanisa hili, ili kwamba tutawajibika katika ufalme wa milele wa Mungu katika yerusalem mpya.Hili ni kwa wote wake kwa waume. Hii ndio sababu wanawake wanapaswa kusoma na kutekeleza wajibu Katika kusambaza ujumbe kuhusu mamlaka ya kanisa. Hatuwezi kuwezeshwa kinguvu kwa kufanywa chini ya kutokuwa kimawazo.Hii ndiyo sababu mfumo wa karne hii lazima uharibiwe na mfumo mpya uundue. Inalazimu tujengane kiroho ili tuwe shupavu Katika imani ndio tupate kutumika Katika imani.

 

Kila mmoja anao njia awezaye kuchangia, aijalisi ni mnyonge, maskini, au bila kipawa chochote vile tunavyo jitazama. Kila mmoja anaweza kutambua hitaji Katika kanisa na anaweza timiza sehemu fulani ya mahitaji ili kupata kueneza ujumbe huu nje. Kadiri tunavyotoka nje kueneza ujumbe huu, ndivyo watu Wengi wanavyopokea nguvu na kufahamu maono ya ufalme. Haya ni maono ya uwezo mkuu na ni ya matumaini. Kunayo hali ya kutowazia ya kishetani ambayo inazuilia.Mafundisho ya Wanokali ni hoja muhimu Katika kuzuilia watu nyuma na kuzuia uwezo wao.Hatuna uwezo kamwe kama tutaingia kanisani na kuketi nyuma ya matabahu na kukariri mapokeo ya maombi yasiyokuwa na maana kama vile wasioamini wafanyavyo.    Haya si mamlaka na hata vifaa hatuna kufanyia chochote. Lazima tuwe na vifaa kufanya jambo ili kutimiza wajibu wetu.

 

 Kiroho tutaenda Katika ndoa ya Mwana Kondoo tukiwa na Mwenyeji wa kiroho.Zote tukiwa tumejianda kwa harusi chini ya Kristo Yesu,ili kwamba wote tukabidhiwe kwa Mungu.

 

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.

 

Kwa hivyo makao ya mungu yamo Katika binadamu. Si Mesia tu ambaye analeta mamlaka ya mungu; ni mungu pamoja na binadamu,ndani ya binadamu. Yeye tu anachukua masumbuko na uchungu. Shida zote ambazo zimemkumba binadamu na dhana yote kuhusu mauti na udhaifu wote unaondolewa. Hivi vitakuwa vimepita. Mambo haya hayatasumbua akili tena. Mungu atawezesha kila mmoja hivi kwamba hakutakuwa na kusononeka kwa akili.Kila mmoja atageuzwa kiakili, na kimwili.Watakuwa viumbe vya mbingu walakini kumbukumbu zao za kiroho na umbio wa kiroho, utakuwa imara. Hakutakuwa na ulemavu wa kimawazo wa fikira kutokana na kumbukumbu za yaliyopiota.

 

Mambo yote haya yatatukia atakapokuja Mungu hapa duniani. Yesu Kristo akija, Mungu bado hatakuwa isipokuwa kupitia kwa nguvu za roho mtakatifu. Mungu hawezi kuja mpaka pale yote yatakuwa yamedhibitiwa, Kwa kuwa mumgu ni mtakatifu na hawezi kutangamanana na uovu- na uasi ni uovu. Mungu anaweza kuifanya dunia hii kusita kuwepo ikiwa haitakuwa imefaulu uthibiti. Si mpango wa Mungu kuwa sayari hii iangamizwe ijapokuwa itangamizwa kama hatutafaulu kuthibiti, na halijatendeka, basi Mungu hatakuwa na lingine bali kuiharibu. Lakini hilo halitatukia.

 

5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli. 6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure. 7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

 

Twasema Mungu ni Alfa na Omega. Hakuna Mungu ila Yeye. Hakuna Mungu aliyekuwa kabla yake wala hakuna baada yake. Hakukuwa yeyote pamoja naye kabla ya Mwanzo wa uumbaji. Yeye pekee ndiye Mungu mmoja wa kweli, nukuu kutoka Yohana 17:3.

 

Tutafanyika wana wake Mungu katika nguvu baada ya ufufuo, kama vile Yesu katika nguvu zake Mungu alifanyika mwana kufuatia ufufuo wake kutoka mauti (kama tunavyofahamu kutoka warumi 1:4) Yeye ni Mwanzo na mwisho na alifanya Yesu Kristo kama Mwanzo na Mwisho wa uumbaji na tokeo la mwishowe. Hata hivyo, Mungu ndiyeMwanzo kwa kuwa Alimuumba Kristo aliumba washirika watakatifu wa mbingu (elohim) na Jeshi na vyote vile. Kwa mapenzi yake vyote vinaishi na viliumbwa. (Ufunuo 4:11)

 

Vile vile Yeye ni Omega kwa namna kuwa kupitia kwa Roho Mtakatifu atafanyika vyote ndani ya yote, na sisi sote tutafanyika vyote ndani ya yote, na sisi sote tutafanyika mungu (elohim) kama Malaika wa Yehova katika kichwani mwetu (Zak 12:8) Malaika ni Yesu Kristo katika Kichwa chetu, ambaye ni Mshirika mtakatifu(elohim) wa watu wetu. Tutapokea nguvu za Mungu kupitia Roho Mtakatifu. Sote tutaishi kama kitu kimoja kilichoundwa, kama Roho Mtakatifu alivyo nyenzo ya Mungu inayotuunganisha pamoja kama vile theruji inavyounganisha mawe, na kuyashikamanisha pamoja, Moja juu ya lingine. Hivyo ndivyo tutakuwa Mwinulia mmoja.

 

Kwa walio na kiu nitawanyweza kutoka kwa  chemichemi ya maji ya Uzima bila malipo (fungu :6) ni dhana ya Roho mtakatifu (Taz Roho Mtakatifu (Nam. 117)). [The Holy Spirit (No. 117)] Chemichemi hii inawajia watu wote walio katika Ufalme wa Mungu.

 

Neno Mwanangu (fungu 7) huonyesha kwamba tutakuwa kama Mwenyeji. Ayubu sura ya 1 na 38 huonyesha kuwa Mungu anao halaiki ya wanao tayari, walakini tutajumuishwa katika kundi hilo vumbuliwa la wana wake Mungu kama vile Malaika.na wakuu wa malaika.Yesu Kristo si pekee Mwana wa Mungu- wako wengi. Tutakuwa wana wake Mungu jinsi ambavyo Jeshi la mbinguni ni wana wake Mungu.

 

Ufunuo 21

8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.

 

 Hili ni kuwa ikiwa hatutaweza kushinda mambo haya katika ufufuo wa kwanza na wa pili, Kanisa limejaa watu wa aina hii ambao Mungu amewaita kutokana na mazingira kama hayo. Sote tumeitwa tuwe washindi ili tuwe mfano kwa watu wengine ambao wanahukumiwa kwa viwango hivyo. Mungu hafanyi mambo hayo kwa njia isiyo haki. Yeye huwaita watu na kuwapa nguvu ili kushinda na kudhihirisha kuwa kuna ushindi.

 

Funuo 21

 9 Akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na vile vitasa saba vilivyojaa yale mapigo saba ya mwisho, naye akanena nami, akisema, Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo. 10 Akanichukua katika Roho mpaka mlima mkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu; 11 wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri; 12 ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu, wenye milango kumi na miwili, na katika ile milango malaika kumi na wawili; na majina yameandikwa ambayo ni majina ya kabila kumi na mbili za Waisraeli. 13 Upande wa mashariki milango mitatu; na upande wa kaskazini milango mitatu; na upande wa kusini milango mitatu; na upande wa magharibi milango mitatu. 14 Na ukuta wa mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na katika ile misingi majina kumi na mawili ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

 

Kwa hivyo, milango kumi na mbili ni majina ya Makabila ya Isreal na mahakimu kwa makabila kumi na mbili ambao ndio misingi wa Jiji. Hatua kumi na mbili, Misingi kumi na mbili ni kwa ajili ya kila mmoja wa mitume. Wakiwa mahakimu, tunatambua kuwa hawajawekwa kusimama juu yao lakini chini yao ili kwamba wanaweza kusimama juu yao. Isreali Linasimamia Mitume kumi na wawili kama misingi, mmoja baada ya mwingine wa Mji wa Mungu. Hivyo basi hawa mitume si kama wanamataifa ambapo Bwana hutawala juu yao walakini ni kama yesu anayehudumu. Huu ndio wajibu wa uongozi wa roho mtakatifu. Ni nguzo ya ndani na si Nguzo tuu. Si hatua za uongozi. Ni msingi hivi kwamba kila moja kwa huduma yake atafanyika msingi na nguzo kwa wale anaowatumikia na huu ndio uongozi wetu. Hivyo ndivyo tunapaswa kufanya, kutoa Maisha yetu kwa ajili ya wengine.

 

Mitume kumi na wawili watapokea hatamu za Baraza ya ndani la Watakatifu wa mbingu (Elohim) katika matengenezo ya yerusalem mpya na Jeshi la mbinguni.

 

Vyeo vilivyounganishwa ni hivi kwamba kujaza pengo la Jeshi lililoanguka itatekelezwa kutoka kwa binadamu. Wanaunganishwa na maagizo mapya ya serikali uchukua nafasi katika mji. Mji huu ni mwinuo wa kiungu. sisi ni sehemu ya  mji uliyosalia ni wa Jeshi la mbinguni. Sisi Kama Hekalu la Mungu, hawa binadamu pia ni Mji wa Yerusalem Mpya. Sisi ni watakatifu wa watakatifu wa ndani, walakini wote hufanya mji huu. Wengine hawaelewi vipimo, wakisema itakuwa maeli 1,500 kwenda juu inayoonekana.

 

Watu wengi hupunguza ukali wa dhana hizi kuwa vitu vinavyoonekana eti kwamba wanaweza kumzuilia mungu kuwa kitu wanachoweza kupuuza. Haya ndiyo wale wa utatu wanataka kufanya hivyo kumfanya Mungu kuwa potovu. Wanamuweka Kristo kuwa usawa mpya, uhai milele mwenza ili kwamba Sheria za Mungu zinaweza kupuuzwa. Tunapozungumza kuhusu Roho Mtakatifu akihudumu na hayo na tuseme Mungu ndiye kila kitu kwa kila mtu badala ya yote ndani ya vyote, tutakuwa tunatazama vipimio vya umbo, tunapoteza kuona ufalme wa  Mungu. Hatuwezi kupata dhana hizi katika utatu. Hii ndiyo maana Utatu unafungia kila kitu tulivyo na tunachofanya na ndio dhana ya kipepo inayotenga kupunguza uwezo wetu wa mwisho.

 

Ufnuo 21

15 Na yeye aliyesema nami alikuwa na mwanzi wa dhahabu, apate kuupima huo mji, na milango yake, na ukuta wake. 16 Na ule mji ni wa mraba, na marefu yake sawasawa na mapana yake. Akaupima mji kwa ule mwanzi; ulikuwa kama maili elfu na mia tano; marefu yake na mapana yake na kwenda juu kwake ni sawasawa. 17 Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini na nne, kwa kipimo cha kibinadamu, maana yake, cha malaika.

 

Mtu na Malaika wako sawa, Ni kipimo cha kimalaika kinachozungumziwa. Ni kipimio cha kiungu

Ufunuo 21

18 Na majenzi ya ule ukuta wake yalikuwa ya yaspi, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi, mfano wa kioo safi. 19 Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi; 20 wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto.

 

Dhana za virembesho kumi na mbili zina umuhimu wa kiungu.

 

Ufunuo 21

22 Nami sikuona hekalu ndani yake; kwa maana Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake. 23 Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo.

 

Hatukuona Hekalu Kwa maana tulifanya Hekalu Kama Mwinuo wa Kiroho. Mji hauhitaji jua wala mwezi kwa kuwa nuru ya mwanakondoo ndiyo nuru yake. Wakati huo tutasita kuwa Hekalu bali tutakuwa mji wa Yerusalem mpya. Jiji lote watakua wana wa Mungu; hata hivyo, tulifanywa kuwa msingi. Pale Hekalu litakoma kuwa kielelezo na kufanyika kuwa sehemu ya mji, kwa sababu utawala wa wateule kama viongozi wa jiji lote hawatakuwa kando ya Jiji tena. Umekuwa mpana na Mungu na Kristo watakuwa Kivutio, U katikati wake Roho Mtakatifu wenye kufanya kazi ndani ya kila mmoja kote Jijini.

 

Hekalu limepanuliwa.Badili ya kuwa jumba lililo kando ndani ya mji, viongozi wa mji wote wao ni himana ya Roho wa Mungu. Hivyo, Hekalu, ikiwa ni hamana wa Roho, tena inapanishwa hili mji wote uwe hamana wa Roho.

 

Utawala wa kati, ambao ni sehemu ya Jiji, bado ni wana wa Mungu, ama ni kipengee muhimu kupitia kwacho Mungu anatawala uumbaji wake ambao haulingani na vile mataifa wanatawala mataifa yao. Si mfumo wenye vitengo ambapo kundi moja lahitaji kuliambia lingine kinachopaswa kutendwa.Ni uhusiano wa Kifamilia ambapo sote tunatawaliwa moja kwa moja na kristo na Mungu. Ni dhana ngumu sababu tunawazia mfumo wa daraja. Ni uhusiano wa moja kwa moja na Kristo na Mungu. Kichwa cha kila mtu ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu (1 Wakorinto 11:3)

 

Njiani kumetukia Pengo kwa jinsi ambavyo watu wanavyohusiana na mungu. Badala ya Hekalu, sasa tunao kupanishwa kwa Hekalu ambapo Roho anaenea Jijini kote.

 

Tunatoka kuwa hekalu kwenda hadi kuwa mji na tumeunganishwa kuwa umbo kubwa. Mungu anajaza pengo amefanyika vyote ndani ya yote.Hivyo, tunaishia Katika hali ya kivutio cha ndani kufunganisha mji wote Pamoja. Mungu ni mji ule kwa kuwa yeye yu ndani yetu kupitia kwa Roho mtakatifu.

 

kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo. 24 Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake. 25 Na milango yake haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku. 26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake. 27 Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.

 

Tunakumbana na njia ambayo mataifa yanaletwa Katika uwezo wa Kiroho, wakiokolewa na kuletwa Jijini. Bila shaka mataifa wanarithi ufalme wa mungu kupitia Yerusalem mpya. Malango ya mji ni lulu la hekima ya injili ya ufalme wa mungu vile unavyotawaliwa kupitia kwa mitume kumi na wawili. Hizi si lulu za kuonekana,bali Ujazanda ni wa kiroho kabisa.

 

Utawala

Ufunuo 22:1-5  Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung'aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo, 2 katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa. 3 Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia; 4 nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao. 5 Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele.

 

Mungu anapatanishwa nasi wateule ili kushiriki Katika utawala. Kristo ameketi chumbani mwa kiti cha enzi na tunashiriki katika hicho kiti.Tunashiriki hilo jukumu  katika mamlaka hayo. Ahadi kwa kanisa la kiladokia,kwa wale wanaoshinda Katika kanisa hilo ,tunapata katika Ufunuo 3.

 

Ufunuo 3:21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. (Biblia Takatifu BT)

 

Tunaketi Katika kiti cha enzi cha kristo vile Kristo anavyoketi Katika kiti cha enzi cha Mungu. Kwa hivyo mungu anafanyika yote na sote tunashiriki wadhifa huo wa utawala ambao ni mfumo shupavu. Mtazamo wa kuukabidhi kwa mungu haudunishi nguvu zetu bali huziongeza, vile utawala unazingatiwa hapa duniani kukiwa na Jeshi lote la Mbinguni. Tumeinuliwa Katika nguvu kwa kuondolewa kwa utawala na kuunganishwa kwa mifumo ya Kimalaika. Malaika wakuu watashikamanishwa pamoja na mitume ambao wao watafanyika wakuu wa malaika pia.

 

Tuna dhana ya 3 na ya 30. Ubadilisho wa yesu Kristo pamoja na musa na Elijah wakiwa mkabala pande zote inazaa kitengo cha ndani cha Baraza la Wtakatifu wa kimbingu (elohim). Hii ndiyo sababu katika kitabu cha kutoka 7 na 4 Mungu alimwambia Musa “Nitakufanya kuwa mungu (elohim).” Alimfanya kuwa mungu Kwa aroni, mungu kwa Firauni. Hakusema nitakufanya kuwa hakimu.Alisema “Nitakufanya kuwa mungu.” Jina lile lile linalotumiwa kwake na Baraza la miungu (Elohim). Hawa watu kiutawala wakawa viumbe shupavu.Hii ndio sababu kuna Makerubi wawili katika pande mbili za kiti cha Rehema Hekaluni.Hizi huwakilisha nguzo kwa Halmashauri ya utawala. Musa na Elija ni nguzo mbili kwa Halmashauri ya utawala na inapotelemka chini kidogo kwa kumi na wawili kupitia kwa mitume, kumi na wawili kupitia kwa maakimu na inaelekea hadi sabini.

 

Hii ni uwezo bayana si maneno matupu.Wako hapo kutupatia Mawazo kuhusu hatima ya watu wetu.Katika ufufuo wa wafu, wamepewa nguvu zao na mamlaka wakati ufalme utakabidhiwa kwa Mungu. Tunapopitia hayo, tunapokea wajibu wa kipindi cha miaka elfu moja (kimilenia) na tunatekeleza hayo.Baadaye tunapewa wajibu Katika ufufuo na tutayatekeleza. Baada ya hayo, tunapewa wajibu baada ya kupatanishwa hatimaye na Mwenyeji. Kuna hatua tatu za viumbe vya kiroho. Hayo yanapatikana Katika ulimwengu.

 

Utawala unajiri Kwa sababu kusudi la uhai uumbaji si kipindi cha miaka elfu moja (Milenia). Milenia si lengo na dhamira ya kuitwa kwetu. Ni gari tu la kurekibisha ubinadamu na kuhukumu wa jeshi walioanguka. Ni kipindi cha siku ya Bwana na “Siku”inachukua miaka elfu moja. Hii ndiyo sababu petro alisema siku moja Ni miaka elfu moja kwa Bwana (2petiro 3:8). Siku ya bwana Ni miaka elfu moja Katika kusudi na maazimio na inaishia Katika ufufuo wa wafu ambao huchukua miaka mia moja.

 

Siku ya bwana inahusisha kuasisiwa Kwa ufalme, utawala wa milenia, ufufuo wa wafu na kisha mapatanisho. Ni kipindi kimerefushwa cha miaka elfu moja ya utawala wa haki. Hali hii si kipindi tu bali ni kifaa cha kufundishia, Azima timilifu ya uzao wa binadamu kulingana na mwenyeji wa kimalaika haijatajwa. Hii tu ni kutawala nyota, kuna sehemu Katika Bibilia ambazo zinaghusia dhana kuhusu tunakoelekea Katika hatima yetu. Walakini hatima yetu ni kutawala nyota na kuumba tena umbo la utawala na kukabili hali mpya ulimwenguni. Tutapokea nguvu za uumbaji Kama vile Mungu alikuwa na uwezo wa kuumba, hivyo tutaumba. Kuna taarifa iliyofichwa Katika vitabu tano vya kwanza vya Biblia, ambayo haijaandikwa chini hapa vilevile Zaburi 8 na Daniel 2.

 

Zaburi 8:1-9

1 Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; 2 Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi. 3 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha; 4 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? 5 Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima;

 

Tunapokea uwezo Katika familia ya vyumbe watakatifu Kama wana wake Mungu, wakigawana nguvu za mungu.Hiyo Ni upungufu kidogo Na malaika (TKJV). Hata hivyo waibrenia husema, pungufu kidogo kuliko mungu (TZZ RSV) ambaye Ni mungu. LXX inatafsiri hawa kuwa malaika.Hivyo wanaona kuwa tunakabili malaika kama Mungu (Elohim).Waibrania wanaonekana kusema kuwa Mwana Wa Adam ana upungufu kidogo kuliko Mungu (Elohim) (Taz Bibilia ya Green’s Interlinear).

 

6 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. 7 Kondoo, na ng'ombe wote pia; Naam, na wanyama wa kondeni; 8 Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini. 9 Wewe, MUNGU, Bwana wetu, Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

(Biblia Takatifu (BT))

 

Dhana hii ni moja ya dunia- yote ikiwa kazi ya mikono ya Mungu- imewekwa chini ya binadamu.

 

Daniel 2:11 Ni neno la ajabu, hili analolitaka mfalme, wala hapana mwingine awezaye kumwonyesha mfalme neno hilo, ila miungu, wasio na kikao pamoja na wenye mwili.

 

Inaoonekana kuwa kazi hii; inazaa dhana kuwa tutatua mfumo ambao unapita uumbaji unaonekana.Hoja hi inapaswa kusoma zaidi ili kuibua dhana hii.

 

Daniel 2:44-45 Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele. 45 Na kama vile ulivyoona ya kuwa jiwe lilichongwa mlimani bila kazi ya mikono, na ya kuwa lilivunja-vunja kile chuma, na ile shaba na ule udongo, na ile fedha, na ile dhahabu; basi Mungu aliye mkuu amemjulisha mfalme mambo yatakayokuwa baadaye; na ndoto hii ni ya hakika, na tafsiri yake ni thabiti. (Biblia Takatifu BT)

 

Ni dhairi kuwa dhana ya kuvunjwa kwa ufalme inahusu pia umbo la utawala wa Jeshi la mbingu na kupangwa tena kwa umbo hilo. La muhimu, lina maana kuwa ni lazima kuwekwa mfumo mpya.Inapaswa kujumuisha nyota . Kupitia uumbaji, Mbingu mpya Na dunia mpya, Ina maana kuwa kutakuwa Na mbinu ya kudhibiti mfumo huo. Hatujaambiwa vizuri vile tutafanya.

 

Bibilia si wazi kile tutakachofanya Katika milenia isipokuwa tu kuwa tutakuwa Katika hatamu za utawala na mamlaka, kwa kuwa mambo haya yatatukia (marejeo kuhusiana na ulimwengu yapatikana Dan.7:27 na 12:3).

 

Daniel 7:27 Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii. (Biblia takatifu (BT)

 

Miliki zote chini ya mbingu zote huonyesha kuwa zinapita Dunia.Haijazingatia miliki zote Katika dunia: inaelezea juu ya miliki zote zilizo chini ya Mbingu.Hali ya kurejesha upya utawala inatupa, kwa kweli, uwezo wa uumbaji, mambo yaliyotendwa na Mungu (Elohim) hapa nasi tunatazama ili tuweze kutekeleza ipaswavyo uwezo wa ubunifu.Sababu ya kuruhusu tupitie haya yote duniani ni kutuandaa kwa wajibu baadaye ili tusije kuuharibu.

 

Hakuna sababu ya kutufanya kupitia hayo sasa ila tu kuandaliwa Kwa siku za baadaye. Sababu mojawapo huenda ikawa tutazame kipindi hiki nyuma Ili tusiasi tena.Uumbaji hautakumbukwa tena.Vitu vilivyo kuweko huku havirejeshui akilini tena Lakini si kwamba hatutakuwa na uasi tena kwa kuwa hatutazama nyuma. Kwa hivyo lazima kuwe na sababu sisi hupita hali hii ya utakazo. Lazima iwe ni kutekeleza uwezo juu ya dunia iliyonyooka baadaye. Hakuna sababu nyingine inayodhihirika kueleza ni kwa nini tutazaa mtawalio huu wa kuishi na urekebisho; kwa kuruhusu uovo huu kujiri, isipokuwa tu tunatakazwa kwa kazi Fulani katika siku za baadaye. Hi ni shule ya mafundisho ambayo tunafundishwa kwa kazi Fulani. Tunaweza kuona kupitia kioo cheusi kwa sasa. Tutakapomwona Mungu ana kwa ana tutaanza kuyaelewa yale tutakayofanya. Kazi yote hii imeelezwa katika ufunuo 22

 

Ufunuo 22:6-15 Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.

 

Kuna Malaika atakayetubiria nyakati za mwisho, mara tu kabla ya kuja kwa Mesia, ujumbe kuhusu yale ambayo ni lazima yajiri.Kusisimuliwa huku tunapewa katika siku za mwisho na Kristo yuaja karibuni.

 

7 Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki. 8 Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo. 9 Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu.

 

Mwabudu mungu. Ndiye wazo kuu la uabudu. Hali ya mwisho ni Uabudu wa Mungu

 

10 Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia. 11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

 

Maneno hayakutiwa muhuri katika kitabu hiki kwa kuwa saa hii karibu. Kitabu hiki hakikufungwa. Tunakusudiwa kukielewa.

 

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya. (Biblia Takatifu BT)

 

Dhana ya Mungu kuwa Alfa na Omega, akigatua wadhifa wake, vyeo vyake na Mamlaka yake kwa Kristo na kwa Jeshi. Uongo unawekwa pamoja na vitend viovu vya jinai. Hatuwezi kuepusha ukweli na kurithi ufalme wa mungu. Hii ndiyo sababu Mungu anawadhibu makuani na manabi wanaodanganya kwa sababu wako kwenye nafasi ambapo hawapaswi kufanya hivyo. Ni muhimu kimsingi. Ukweli ni muhimu kwa ukuhani na Unabii.

 

Ufunuo 22:16-20 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung'aa ya asubuhi. 17 Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.

 

Huyu ndiye Yesu kristo, ambaye anajitambua kuwa malaika aliyeuleta ujumbe.

 

18 Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki. 19 Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki. 20 Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu.

 

Amina Njoo Bwana Yesu (Biblia Takatifu (BT)).

 

q