Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[178]

 

 

 Zaburi 110

(Chapisho La 2.0 19970904-20000712-20070509)

Zaburi hiI fupi lakini ni ya muhimu sana. Sura hii ni moja kati ya sua 134 zinazipotoshwa na Wasoferim ambayo kwayo Yahova (au Yehova)aligeuzwa jina lake na kuitwa Adonai. Ilianza kwa kutambulisha kwamba hii ni Zaburi ya Daudi. Lakini aya haimtaji Daudi bali inamtaja Bwana wa Daudi. Na mtu huyo ni Masihi, na ndiye anayetajwa kama Yehova kwenye  Zaburi ya 110:5 na neno hili lilibadilishwa na kuwa Adonai kama tutakavyoona.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

Email: secretary@ccg.org

(Hati Miliki © 1996, 2000, 2007 Wade Cox)

(tr. 2014) 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org


Zaburi 110


Zaburi 110:1-7 Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako. 2 Bwana atainyosha toka Sayuni Fimbo ya nguvu zako. Uwe na enzi kati ya adui zako; 3 Watu wako wanajitoa kwa hiari, Siku ya uwezo wako; Kwa uzuri wa utakatifu, Tokea tumbo la asubuhi, Unao umande wa ujana wako. 4 Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki. 5 Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake. 6 Atahukumu kati ya mataifa, Ataijaza nchi mizoga; Ataseta kichwa katika nchi nyingi. 7 Atakunywa maji ya mto njiani; Kwa hiyo atakiinua kichwa chake.  

 

Zaburi hiI fupi lakini ni ya muhimu sana. Sura hii ni moja kati ya sua 134 zinazipotoshwa na Wasoferim ambayo kwayo Yahova (kimakosa kabisa alitajwa kwa jina la Yahwe au Yehova) andiko lililo kwenye sura ya 110:1 linatumia mtaji wa adoni, ukweli wa kwamba umetumika na Waunitariani wenye itikadi kali ili kuonyesha inaashiria kwamba neno Bwana kwa masuala ya kibinadamu mwenye umbo la mmiliki, bwana au bwana. Hata kamusi ya Strong inaorodhesha hii kwa hivi ndivyo ilivyo. Hatahivyo, mfananisho huu usio na mashiko ulikataliwa na Bullinger akionyesha kuwa ilivyomtaja waziwazi Adonai akiwa ndiye aliyeketi Mkono wa Kuume wa Mungu. Neno lililotumika kwenye Zaburi 110:5 asili yake lilikuwa linamtaja Yahova lakini lilibadishwa na kuwa Adonai kwa muundo uleule wa kiuandishi wa neno Adoni kama inavyoonekana kwenye Zaburi 110:1 na inamaanisha Adonai na inamtaja Yahova.

 

Zaburi hii inashughulikia kwa wazi viumbe wawili wa mbinguni ambao mmoja wao ni mdogo kwa mwingine na akiwa amekei kwenye mkono wa kuume wake. Huyu mdogo pia anaitwa Yahova (rejea kwenye jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24) [The Angel of YHVH (No. 24)]. Wasoferimu walibadilisha jina Adonai ili kuupa mashiko ukweli wa umbunguni wa Masihi kwa kumshirikisha na Yahova kuwa ni Mungu wa Pekee na wa Kweli. Inaanzia na utambulisho kwamba Zaburi hii ni ya Daudi. Wakati kwamba aya hiii haimtaji kabisa Daudi bali Bwana wa Daudi. Hivyo basi, mtu aliyekusudiwa hapa ni Masihi. Baraza la marabi wanalitumia andiko hili kwa ufafanuzi ujnaomtaja Ibrahimu wakihusianisha na kitendo chake cha kuonana na Melkizedeki kwenye aya ya 4 (tazama ufafanuzi wa Soncino kuhusu Zaburi hii  (kurasa za 371-372) na kumbukaa pia kitabu cha Kienrania cha MT kwenye aya zotte mbili). Hata hivyo, Ibrahimu alimpa zake Melikizedeki kwa hiyo tunalazimika kumtaja Masihi hapa na huduma yake ya kikuhani ambaye ni Ibrahimu ni mdogo kwake. Anatajwa kuwa ni Yahova (au wengine wanamuita Yehova) kwenye Zaburi 110:5 na hii ilibadiloishwa kuwa Adonai kama tutakavyoona huko mbele.

 

Zaburi 110:1 Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.

 

Hapa Yehova anamwambia kiumbe anayeitwa Bwana Wangu (Adoni) ambaye ndiye Bwana wa Daudi. Kiumbe huyu ni Adonai. Namna ya kiuandishi iliyotumika kumuelezea kiumbe huyu mtakatifu kwa Kiebrania kama kiumbe mwingine lakini mmoja akielezewa kwa kufananishwa na mwanadamu na mwingine akielezewa waziwazi kuwa ni Yahova kana kwamba hili  lilikuwa ni neno la asili. Kwa hiyo Waserafimu waliibadlisha andiko hili. Andiko hili limenukuliwa kutoka kwenye Mathayo 22:41-46, Matendo 2:34-35 na Waebrania 1:13.

 

Huyu Yehova anayetajwa hapa ni Yehova ne’um. Hizi kwa kweli ni semi au lugha za Kinabii zinazotumika kumtaja Yahova. Mara zoe zinatumika kwa usemi wa haraka na wa moja kwa moja kumjata Yehova na mara chache kwa nabii (kama kwenye Hesabu 24:3,15), au Daudi (katika 2Samweli 23:1) (tazama kwenye Companion Bible, fn. to v.1). Huyu Bwana Wangu anayetajwa hapa ni Bwana wa Daudi, yaani Masihi. Kwa hiyo, Nasihi alikuwa ni Bwana wa Daudi, wakati ambapo bado alikuwa kwenye mlolongo wa kizazi cha mababu zake. Mwishoni mwa Zaburi kwenye aya za 5-7 inaonyesha ulikuwa ni unabii na ulikuwa haujatimilika bado.

Mathayo 22:41-46 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo? 42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi. 43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema, 44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako? 45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe? 46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.

 

Kwa hiyo alikuwa amewekwa wakfu tayari tangu mwanzo, ili aweze kumuombea Daudi na huku akiwa wa uzao wake pia (tazama pia jarida la Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Kimwili (Na. 243) [The  Pre-Existence of Jesus Christ (No. 243)].

 

Andiko linalosema, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako. limenukuliwa mara saba kwenye Agano Jipya (Mathayo 22:44; Marko 12:36; Luka 20:42; Matendo 2:34; Waebrania 1:13; 10:13; 1Wakorintho 15:25). Kifungu hiki kinatokana na neno lenye maana sawa na kusema kuseta miguu shingoni mwa adui (kama kwenye Yoshua 10:24).

 

Inamaanisha kuwaseta maadui zake Masihi chini ya miguu yake. Kwenye Agano Jipya la Kiyunani limetumika neno tithemi linalomaanisha ni lazima atawaseta (tazama kwenye Companion Bible, ibid.). 1Wakorintho 15:25 inachukuliwa kuwa ni aya ya pekee kuelezea kipindi atakacho sio tu kwamba  atawaseta miguuni pake bali chini ya miguu yake kitakapofika kipindi cha utawala wake Kristo mwenyewe (Mathayo 25:31; Ufunuo 3:21) inatajwa kwenye andiko lile badala ya kusema katika kipindi atakachokuwa Baba yake kwenye Kiti chake cha Enzi,kama ilivyoonekana kuandikwa maeneo mengi (ibid.). Kitabu cha fafanuzi cha Soncino kinaepuka kuonyesha nia ya Masihi kwenye zaburi hii.

 

Zaburi 110:2 Bwana atainyosha toka Sayuni Fimbo ya nguvu zako. Uwe na enzi kati ya adui zako;

 

Neno fimbo ya nguvu ni usemi wa Kiebrania unaomaanisha kwa fimbo yako yenye uweza au fimbo ya kifalme yenye uweza mkubwa (tazama kitabu cha fafanuzi cha Soncino). Tunatakiwa kushughulikia fimbo kuu yenye uweza wa kufanya kazi zote inayofanya kazi mbili zote, yaani ya kikuhani nay a kifalme, na aliyopewa Masihi hapa akiwa ni mwana wa Daudi.

 

Sayuni inayotajwa hapa ni kitovu cha ufalme wa Masihi (sawa na Warumi 11:25-27). Andiko linalosema, utawale katikati ya maadui zako, likiwa limewekewa alama ya mkato au koma, linamaanisha kuwa ni neno linaloashiria amri kutoka kwa Mungu (Soncino).

 

Warumi 11:25-27 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili. 26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake. 27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.

 

Andiko hili linapaswa kulinganishwa na lile la Isaya 59:20 na Luka 21:24. Kuja kwa Masihi huko Sayuni na kwa wale watakaoacha maovu katika Yakobo. Kwa hiyo, kwa muda wake uliokusudiwa wa nyakati za mwisho za Mataifa, Masihi atakuja kuwakomboa Israeli na kuuanzisha mfumo na utawala wake kutoka Sayuni.

 

Zaburi 110:3 Watu wako wanajitoa kwa hiari, Siku ya uwezo wako; Kwa uzuri wa utakatifu, Tokea tumbo la asubuhi, Unao umande wa ujana wako.

 

Usemi unaosema watu wako watakuwa tayari siku hizo za mamlaka yako linamaanisha kwamba watajitoa kwa hiyari ya mioyo yao yote katika siku utakazokuwa mtawala. Watakuwa ni sadaka ya hiyari ya aina kama iliyoko kwenye Kutoka 35:29; 36:3; 1Nyakati 29:9,14,17; Ezra 3:5; 8:28. Hii ina chanzo kimoja na ile ya Waamuzi 5 (Soncino). Neno uweza wako linamaana alisia ya kusema jeshi lako. Kipindi hiki kwa usemi wa wazi ni wa kipindi cha jeshi la Bwana la Siku za Mwisho. Watu watatoa mifugo yao kwa kiwango chake halisi (cf. Soncino).

 

Maneno yasemayo uzuri  wa utakatifu yanaonekana kuonekana kwenye maeneo au sehemu za ndani (au juu) [fn. v. 3). Soncino inadai kwamba ayah ii inamaanisha kwa heshima ya utakatifu, sawa na Zaburi 29:2; 96:9. Heshima ya utukufu ni vazi la kikuhani (Soncino) – ambayo kwamba ile kanzu au vazi jeupe ya wateule. Jopo la marabi liligawanyika kimtazamo kwa kuihusianisha hii na Daudi. Lakini tafsiri za kina Kimchi na Hirsch zimetafsiri mkuu wa patakatifu wakilihusisha andiko hili na mji wa Yerusalemu.

 

Andiko hili linaielezea kama [kama umande] utokao tumboni kabla ya asubuhi nilokuzaa wewe [mwana] (sawa na Zaburi 2:7). Ilipaswa kusiwe na alama ya nukta baada ya neno asubuhi. Tunashughulikia wazo la mwana ambaye alikuwepo tangu mwanzo hata kabla ya kuzaliwa kwake duniani, na kuwekwa wakfu kabla ya asubuhi au hata kabla ya nyakati za umilele. Ana umande wa mwana (hapa anaonekana akiwa kijana) (tazama tafsiri ya Companion Bible).

 

Zaburi 110:4 Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki.

 

Hapa neno upanga linahusiana na lile lililo kwenye aya ya 1 kama Unabii au Fikra za Mungu. Hapa tunaona kwamba Masihi aliwekwa wakfu kuwa kuhani wa milele baada ya kufanyika hivyo Melkizedeki (soma Mwanzo 14:18; Waebrania 5:6,10; 6:20; 7:1-28). Marabi wanajaribu kuifananisha hii na Daudi kwa kujaribu kuiepusha na ukweli wa kwamba ni Masihi aliyekusudiwa na kitendo cha kuhamisha huduma ya kikuhani. Kuweka mashiko jambo hili kunachukuliwa na inavyosema 2Samweli 8:18 ambapo limetumika neno cohen linalomaanisha wana wa Daudi na ambalo linalenga viongozi wakuu—lakini neno cohen. Madhaifu ya Daudi ni mifano yenye kuonya (2Samweli 6:14) na alitoa sadaka za kuteketezwa na sadaka nyingine za amani (2Samweli 6:17). Hata hivyo, hii ilikuwa ni kazi ya Mfalme kama tunavyoona kwenye Ezekieli na pengine pengi na haihusiani na uanzishaji wa utaratibu mwingine wa kikuhani. Tunaona kwenye Agano Jipya kwamba utaratibu na kazi hii alipewa Masihi na kutoka kwa yeye likapewa Kanisa. Walawi walitafsiri jambo hili kimakosa. Tafsiri ya Companion Bible inatafsiri vibaya maana ya ukuhani hapa pia. Ulifunguliwa kwa Wamataifa wasio na uhusiano wa kinasaba na usio na mwanzo wala mwisho. Ukuhani wa Haruni uliendelea kwa kupia kizazi kimoja hadi kingine kwa kufuata nasaba ya kuzaliwa hadi kutoka Lawi. Masihi alikuwa ni wa ukoo wa Daudi na Daudi hakuwa wa ukoo wa kikuhani. Masihi alikuwa wa ukoo wa Lawi pia kupitia ukoo wa nyumba ya mama yake (tazama jarida la Kizazi cha Masihi (Na. 119) [Genealogy of the Messiah (No. 119)]. Alitabiriwa kuwa atatoka ukoo wa Lawi kupitia kwa Shimei, na kwa Daudi kupitia Nathan (soma Zekaria 12:12). Ukuhani wa Haruni ndio ulioenea kwenye mbadilishano huu ulijumuisha sio Yuda peke yao bali ni kwa Israeli na kwa Wamataifa. Mungu hatajutia wala kujilaumu kwa yule aliyemchagua (tazama pia jarida la Melkizedeki (Na. 128) [Melchisedek (No. 128)].

 

Zaburi 110:5 Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake.

 

Andiko hili lilibadilishwa na Wasoferimu kutoka kwenye jina Yahova (au Yehova (kutoka) mkono wako wa kuume na isomeke Adonai mkono wako wa kuume (soma machapisho ya Nyongeza au Appendix 32 hadi kwenye tafsiri ya Companion Bible kwenye orodha hiyo). Ubadilishaji huu ulifanywa kwa kuwa kulikuwa na jina lililoonekana wazi la Yahova (au Yehova) ambaye alikuwa ni mdogo kwa Yahova wa Majeshi ambaye ndiye alikuwa Bwana wa Daudi, Masihi, ambaye pia anatajwa kama Yahova lakini sio Yahovi (au Yehovi) ambaye ndiye Yahova wa Majeshi. Tofauti hii imefunikwa na neno au jina la Yehova (SHD 3068) na Yehovi (SHD 3069). SHD 3068 kila mara linakosewa kwa kuitwa Adonai na Yehovi (Yahovi) (SHD 3069) kila mara inalikita elohim inapokuwa inataja. Kwa namna hii Wayahudi walitafuta kulinda hadhi yenye ukweli kuhusu umoja wa Mungu kwa jina la Yahova wa Majeshi (soma kamusi ya Strong’s ili kupata ufafanuzi zaidi). Yahovi (Yehovi) kwa hiyo alikuwa ndiye Mungu wa Majeshi Aliye Juu sana. Yahova (Yehova) alikuwa ndiye elohim wa Israeli akiwa ni msaidizi wa mambo ya mbinguni. Kwa hiyo, Masihi atawashinda wafalme wote itakapofika siku yake iliyowekwa tayari kwa ajili yake (maarufu kama siku ya hasira ya Bwana Mungu) iwakayo.

 

Zaburi 110:6 Atahukumu kati ya mataifa, Ataijaza nchi mizoga; Ataseta kichwa katika nchi nyingi.

 

Masihi ndiye hakimu atakayeyahukumu mataifa (pamoja na Wamataifa). Hebu na awahukumu watu wote [maeneo yote] yatakuwa yemefurika mizoga mingi (tazama vitabu vya kina Kimchi, sawa na Soncino). Kwa hiyo, vifo vya wengi vimetabiriwa vitatokea. Neno la Kiebrania limetumika kuelezea miili ya waliokufa limemaanisha sawa na waliiohai walioandikwa kwenye (Mwanzo 47:18) na mili iliyokufa au maiti. Ibn Ezra anaelewa hivyo kwa mtazamo au uelewa wa kale, mataifa yatakuwa na nguvu za kiidadi. Wengine wanafikiri kuwa inataja au imanaanisha mizoga ya waliochinjwa au kuuawa. Hirsch anaelewa kuwa hii inawalenga wahanga walio kwenye mataifa waliokuwa wanawadhulumu. Mpango wa Wokovu unaonyesha kwamba itakuwa ya namna zote mbili (tazama hasa Ufunuo 20:1-15). Masihi atawaondoa viongozi wa mataifa. Kwa hiyo, maongozi ya mfumo wa dunia yataondolewa. Kichwa kimoja peke yake ambacho ni mfano wa Shetani na kuangamizwa kwa utawala na dini ya mnyama itakayokuwa chini ya imani na mafundisho ya nabii wa uwongo wa Siku za Mwisho (Ufunuo 19:11-21). Hii inaelezea pia uzao wa mwanamke ambaye ni Masihi (Mwanzo 3:15). “Mataifa mengi” yametajwa kama nchi kubwa.

 

Aya hii inayofuatia kwa kweli inaanza na neno la Kiebrania Mem au Kutoka. Hii inahusiana na aya ya 3 hapo juu.

 

Zaburi 110:7 Atakunywa maji ya mto njiani; Kwa hiyo atakiinua kichwa chake.

 

Usemi wa Naye atakunywa vijito akiwa njiani unahusianishwa kitendo cha kumuinua kichwa chake. Hii inamaanisha kuhamishwa kwa mamlaka. Kimchi anasema kwamba andiko hili kwenye haki ya umoja hapa huenda linaweza kuonesha katika uwingi pia(Soncino). Kichwa kilichoandikwa kwa umoja kilichoondolewa ni kile cha Shetani katika mataifa (pia soma Zaburi 98:22 kwa kifungu hiki kinamuonyesha kiongozi wa wanaume wanaopigana (sawa na Rashi, Soncino). Hapa ilimaanisha kiongozi wa waasi. Kwa jinsi hii, Shetani ni Mpingakristo, na mengine yoyote yanayoendelea kwenye mfumo wake ni itikadi zenye lengo la Mpingakristo. Kichwa kilichoinuliwa juu ni uongozi wa Mungu wa kweli kupitia Roho Mtakatifu. Masihi anakunywa roho hii. Kwa jinsi hii, anatimilika kwa hali zote kuwa na hali kamili ya Uungu au kuwa Theotetos. Huu ni uweza wa kimbinguni (soma kitabu cha Thayer’s). Kristo alijazwa na nguvu za mbinguni na alijazwa na Uungu. Aya ya 10 inatuonyesha kwamba hata sisi tumejazwa na Uungu wa Kristo au na hii Theotetos.

 

Hii inaonekana kwa ile dhana ya kuwepo kwake kabla ya kuzaliwa kwake kwa mipango ya Mungu kunakosemwa kwenye Ufunuo 7:9-15. Mwanadamu aliyekombolewa na Wazee au Baraza wako mbele za Mungu. Kwa ajili hii Mungu anatukuzwa. Wazee wanazitupa taji zao mbele za Mungu wakimaanisha kuwa wanaweka na kuuachilia mfumo wao wote kwa Mungu wa Pekee na wa Kweli na kwa hiyo wanakuwa ni wenye kuamini juu ya Mungu mmoja. Na wanapokuwa kwenye kiti hiki cha Enzi, kila mmoja anapangiwa ofisi yake na mamlaka yake na uweza wake.

 

Kwa jinsi hii ndiyo maana tunaviinua vichwa vyetu kwa kunywa kutoka kwenye vijito, ambavyo ni Roho Mtakatifu.

 

Metsudath David anasema kwamba ushindi utapatikana kikamilifu kama matokeo ya mwingilio kati wa Mungu (sawa na Soncino, fn. to v. 7). Huu ndyo mwisho wenyewe kamili hadi kufikia maasi na marejesho mapya yatakayofanywa na Masihi aliyeketi Mkono wa Kuume wa Mungu.

q