Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[179]

 

 

Wimbo wa Musa

Kwenye Kutoka 15

(Toleo La 1.0 19981110-19981110)

 

Jarida hili la ufafanuzi linakwenda kushughulikia wimbo wa kwanza kati ya nyimbo mbili za nabii Musa zilizo kwenye gombo za Torati. Unahusu ukombozi wa Israeli. Wapili wake umo kwenye Kumbukumbu la Torati 32.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1998 CCG, Thomas McElwain, ed. Wade Cox)

(tr. 2014) 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Wimbo wa Musa Kwenye Kutoka 15  


Somo lifuatalo lina mambo mawili yote, yaani sio kawaida na ni ya kipekee sana. Mwandishi analiendea andiko akiwa na sehemu tu ya elimu ya kiuanazuoni, lakini akiwa hajaelewa kwa kina chanzo cha kiroho cha mlinganisho wake, lakini akiwa hajajikita kwenye vyanzo vya kimaandiko vya mlinganisho wake, na wala hakutathmini ukweli mwingi wa kihistoria na kitamaduni unaopelekea tafsiri yake. Anachagua kuyahifadhi baadhi ya maandiko yanayoashiria jambo hili. Mkazo mkubwa umewekwa kwenye majaribio ya kifilolojia yanayojumuisha mlinganisho wa maneno.

 

Kutoka 15:1 Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia Bwana wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia Bwana, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.

Wimbo wenyewe unaanza baada ya kupuliza. Unatumika tena ukiwa kama jibu la kiitikio kwenye sauti ya ridhimu ya kipulizio kwenye aya ya 21. Hii inaonyesha kuwa aya ya kwanza inabeba maana na kiini hasa cha wimbo wote unaosifia ushindi mtukufu wa Bwana. Wimbo wenyewe unahusu ukumbusho wa ukombozi wa watu wanaotoka utumwani Misri na mashambulizi ya Farao kwenye Bahari ya Shamu. Ingawa matukio mengi ya kukombelwa yanaelezewa kwenye Maandiko Matakatifu, bali hili moja linabakia kuwa ni kuu la kukumbukwa ambalo kwa kipindi cha karne nyingi kadhaa waumini wamekuwa wakilisemea. Wimbo huu wa ukombozi unaimbwa na wale ambao wamepata ushindi dhidi ya mnyama na sanamu yake kwenye Ufunuo 15:3, ambako unachukuliwa na kurudiwa Wimbo huu wa Musa ulioandikwa kwenye Kumbukumbu la Torati sura ya 32.

 

Kumbuka: Wimbo huu wa Musa umeandikwa kwenye maandiko ya vitabu vyote viwili, yaani kwenye Kutoka 15:1-19 na Kumbukumbu la Torati 32:1-43, na kote huko unasimama kama ushuhuda kwa Israeli ili kuwakumbusha kuzitii Sheria na Amri za Mungu na matendo yake.

 

Wimbo huu unaonyesha wazi kumsifu YHVH, jina amblo limetajwa mara mbili kwenye aya hii. Ushindi wenye utukufu mkuu namna hii unaweza uonekane kuwa si kitu sana siku hizi, lakini ni vema kukumbuka kwamba silaha za kivita za Wamisri ndizo zilikuwa zenye nguvu na za kisasa kuliko kwinginekokote duniani kwa wakati ule. Ujumbe ulioko hapa ni kwamba ushindi wa kijeshi wa Mungu uko juu sana, zaidi ya kiwango cha uwezo wa silaha zilitumiwa na watu na kwamba kwake hizo hazina lolote kabisa. Tendo la kuigawanya bahari linaweza kudhaniwa kuwa ni tukio linalotokana na natokea ya kimazingira yanayoweza kutokea wakati wa kupwa na kujaa kwa bahari mahali pale, na wapinjgaji wanaweza kuweka dhana wakisema kuwa bila shaka jambo kama hilo lingeweza tu kutokea mahala pale. Lakini tofauti iliyopo kati ya tukio la kiasili na la kimiujiza ni pan asana kulitathmini kiasi cha kuuzidi uellewa wa kibinadamu. Ni ukweli ulio wazi kabisa kuwa matengenezo ya umbile na vitu vilivyoko duniani ni mojawapo ya muujiza mkubwa unaotosha kushuhudia, na ni kitu kikubwa sana zaidi ya ule wa kuigawanya bahari. Bado watu wanashangaza kwa kutolichukulia jambo hili kuwa ni muujiza mkubwa kwenye mawazo yao. Yupende, tusipene, ukweli unabakia kuwa tukio hili ndilo oja ya matukio yaliyowahi kujitokeza mara moja tu pasi kujirudia, na kipindi chake kilikuwa cha muhimu sana ili kuwapa hitaji lao wana wa Israeli. Na kwa hakika kilikuwa ni cha muhimu sana ambacho kwacho uingiliaji wa Mungu ulifanywa na kuonekana kwa hawa Israeli wa kale kwenye Maandiko Matakatifu.

 

Kutoka 15:2 Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza. 

Aya hii inaumuhimu na utajiri mkubwa katika kumuelezea Mungu, tena haielezei kitu kingine chochote zaidi ya tabia na uweza mkubwa wa Mungu mwenyewe na jinsi alivyo. Zote zinahusianishwa na jinsi uhusiano wake ulivyo na mwanadamu. Kitendo cha kugundua kuwa Mungu ni nguvu ni cha kutambua kuwa kwa peke yangu siwezi kuifanya kitu chochote, lakini kwamba kila kilichofanyika ni mali ya Mungu. Hakuna uweza unaoweza kufantika zaidi ya ule wa Mungu. Kima cha utegemevu wa mwanadamu kwa Mungu na ukaribu wake kwa Mungu ni zaidi ya uwezo wa uelewa wa mwanadamu.

 

Mungu ndiye wimbo wangu, au kwa tafsiri nyingine Zaburi. Zaburi imeliiyata kuwa ni makao ya Mungu kwenye Zaburi (tazama Zaburi 22:3). Hapa inaonyesha kuwa Mungu ni Zaburi. Kama mtu kisema maneno kama hay oleo, basi watu wengi wangemuona kama anakufuru. Ukweli ni kwamba Mungu ni hatafuti wala kiupapasapapasa na chochote kile ambacho mwanadamu anakutananacho sio Mungu aishiye, bali ni makazi yake na namna ya ufunuo inatokana na kikomo cha upeo wa mwanadamu. Hakuna mtu aliyewahi kumuonja Mungu (Yohana 1:18; 1Timotheo 6:16). Anajidhihirisha mwenyewe kupitia Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, kwa ueuewa na uzoefu wa kibinadamu, Zaburi ambayo kwayo Mungu anadhihirishwa kwenye moyo wa mwanadamu ndiyo inayomwezesha mwanadamu kumjua Mungu. Zaburi ni Mungu. Makosa ya kihistoria yanayofanywa ili kulijua hilo yamesababisha dini ya Kiyahudi imeendelea sana zaidi ya dini ntingine za kale kama zile za Siddur au kitabu cha ibada kama kilivyo kitabu cha Zaburi, kikiendelea kwa toleo moja hadi linguine la vitabu vya nyimbo za kidini. Imani ya kikristo inaonekana kwenye mbali zaidi. Maandiko Matgakatifu ndiyo pekee yanayotuongoza kwenye ibada ya kweli pamoja na maombi bidii, ushuhuda na kusifu. Siyo Zaburi peke yake, bali pia baadhi ya Maandiko Matakatifu, kama vile kitabu cha Ufunuo, kimeandikwa wazi kwa nia ya kusifu na na kusikika kwenye ibada. Kama Maandiko Matakatifu yanajumuisha mguso wa Mungu, ndipo inaweza kushauriwa kuchukua mahala pa Zaburi kwenye vitabu vya nyimbo ili kuchukua mahala pa Mungu aliye kwenye Maandiko Matakatifu na hivyo kuwa ni ibada ya sanamu.

 

Mungtu anakuwa ndiye wokovu. Huu ni mchakato wenye hatua nne. Unaanza kwa kumtambua Mungu kuwa ndiye muweza na kwamba ndiye pekee anayepaswa kutegemewa na mwanadamu na kuwa na uhusiano naye wa karibu iwezekanavyo. Hatua ya pili ni kujua kwamba Maandiko Matakatifu ni Mungu mwenyewe, sawa na kama mwanadamu anavyomjua Mungu anapofunuliwa kwake kupitia Roho Mtakatifu. Hatua ya tatu ni wokovu kwa njia ya uwepo wa Roho Mtakatifu kama Mungu alivyo ndani yetu. Hatua ya nne ni kuutafsiri wokovu: Yeye ni Mungu.

 

Hapo ndipo hali ya kukombolewa inapokamilika. Ni kufanya makao ya Mungu, kwa hiyo tunapaswa kuimba Zaburi za ukombozi, sifa za Israeli ambao ndio watu wake. Mungu amechagua kuishi ndani ya wateule kama alivyoishi katikati ya Ishraeli. Na kwa hiyo wanakuwa ni Hekalu la Mungu. Uimbaji wa muziki uliovuviwa wa Biblia kwa Roho Mtakatifu kwenye ibada kunafanya sujenzi imara wa Hekalu la Mungu. Mahekalu ya wananadamu yanajengwa kwenye eneo fulani na kwa hiyo yanastahimili hali ya kumilikiwa na hatimaye uharibifu na udanganyifu. Hekalu la Mungu hujengwa kwa Wana wa Mungu waliozaliwa kwa Roho na wanaoabudu siku za Sabato, ambalo ni hekalu lililochaguliwa, jengo, lisiloweza kushikika na ambalo umbo lake linakuwa sawasawa kwenda juu kwake na upana wake kwa uwepo wa Roho Mtakatifu na linajumuisha uwepo wa Yeye Asiyeonekana. Hatimaye, hekalu la Mungu linajengwa kwa kuyasoma Maandiko Matakatifu, na sifa za Israeli, ambazo zinapatikana tena kwa umuhimu wake yanavyopatikana kwa kila mwenye sauti, macho, sikio, au akili. Nitamtukuza yeye kila mara, ni marudio yaliyo kile kwenye mawazo ya kwamba nitamjengea makao.

 

Mtume Paulo huenda alifikia kwenye ukweli usiotatiza wala kufungiwa kwenye kweli isiyofikirika uliokuwa kwenye maelekezo haya pale aliposema kwamba miili ya wateule walio katika Kristo ni hekalu la Mungu. Mtume Petro alienda moja kwa moja kwenye ukweli huu kwa kusema kwamba “Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu,...(2Petro 1:4).

Kutoka 15:3 Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.  

 

Kiebrania kwa kweli kinatumia neno iish au man kumtaja BWANA. Ingekuwa ni kupingana na Maandiko Matakatifu kwa kuyatatiza yenyewe kwa yenyewe katika kuelezea ubinadamu kwa Mungu kwa namna yeyote. Hesabu 23:19 inasema wazi kwamba: Maana iish Eel, Mungu si mwanadamu. Maelezo yake yangeweza kuwa yanahusiana kiufananisho na malaika wa BWANA, ila dhana iliyoo hapa inaonekana wazi kwamba ayah ii inamzungumzia Mungu mwenyewe. Kwa Kiebrania hairuhusiwi kutenganisha maneno mawili ya maelezo yaliyofanwa, nah ii iko miongoni mwa hizo. Kile kinachotakiwa kuelezea na kufafanua ni neno lote zima linalosema iish milhaamaa, au mtu wa vita. Namna hiyo, neno hili halielezei hali ya ubinadamu au ukosefu wake. Bali linaashiria shughuli za kijeshi. Kwenye jambo hili, shughuli za kujeshi ni mojawapo ya wokovu. Maelezo yake yana maana kwamba Mungu anaokoa.

 

Nusu ya mwisho ya aya inalifunua jina la Mungu. Ili kulijua jina la mtu au sifa zake njema au umaarufu wake (kwa Kiebrania neno hili linachukua maana zote mbili) linamaanisha kile anachoweza kukifanya mtu kwa matakwa yake mwenyewe. Mwanadamu anahitaji wokovu kwa kila kipindi, na kulijua jina la Mungu ni kujua pa kuelekea kumrudia, na kuwa na uwezekano wa kumrudia yeye.

 

Kutoka 15:4-10

Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.

Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.

Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana, mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui.

Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.

Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu, Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.

Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.

Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu.

 

Maelezo ya tukio lililotokea kwenye Bahari ya Shamu yanavutia na kupendeza na hata sauti yake ina nguvu kubwa. Jambo kuu linaloweka ugumu kwenye andiko hili maelezo va kielimu dini au kiampomofolojia ya Mungu. Jambo kama hilo linaweza kufafanuliwa na tabia ya maandiko ya kale ya Kiebrania ya kutumia maneno hayohayo kwa kukazia na kushangaa. Kwa mapokeo ya desturi za nje na ndani za kale yanaonyesha uwepo mkubwa wa dalili za kitamaduni au athropolojia na ugumu zaidi kuliko ilivyoshauriwa hapo mwanzoni kiasilia. Mfano elekezi upo mwanzoni kabisa mwa neno lililoandikwa kwenye kifungua hiki linalosema “mkono wako wa kuume.” Hata kama Mungu anamkono wa kuume au la, andiko hili haliashirii kwa namna yoyote ile. Usemi wa Kiebrania wa mkono wa kuume” unamaana ya “nguvu” au “uweza” kama unavyofanya mkono wa mwanadamu. Ili kuchagua kuwa huenda ni namna ya tafsiri, au ni kiuhalisia zaidi kuliko nyingine.

 

Mawazo yamezoea kushughulika na mifano ya tabia za Mungu inayoonekana kuwa ni vigumu kwenye maelezo ya elimu ya mila na desturi, lakini huu ni ubaguzi tu. Neno “mheshimiwa” lililo kwenye aya ya saba ndilo linaloweka ugumu hata kama msomaji aliliruka na kuliacha pasipo kujua ugumu wake. Neno g’oon linatokana na vebu inayomaanisha kukua kwa kurefuka. Kuelezea kwa kwa njia ya mfano kimo au urefu wa Mungu ni kumfanya Mungu kuwa ni eneo, jambo ambalo ni matatizo kwa kweli kama yalivyo masomo ya mila na desturi za watu au anthropomojia.

 

Jawabu kwa matatizo yote mawili ni rahisi kujua kwamba lugha ya mwanadamu haitoshi katika kuelezea ukuu na uweza wa Mungu. Kwa hiyo hatupaswi kuchukulia maelezo yake kama yanatosha kumuelezea Mungu. Kwa hiyo, kunasababu ya kumdhihirisha Mungu katika uhusiano wake na mwanadamu, na sio katika umuhimu wa asili yake. Na kwa nia hiyo ziko sahihi sana, kihalisia na kwa kushangaza.       

 

Kutoka 15:11-12

Ee Bwana, katika miungu ni nani aliye kama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu, Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?

Ulinyosha mkono wako wa kuume, Nchi ikawameza.

 

Kifungu hiki kinaanza kwa kuuliza swali: Nani aliye kama Mungu? Maelezo haya yanaonyesha cheo cha Malaika wa Bwana aliyeandikwa kwenye Danieli 12:1: akisema Na kwa kipindi hicho, Mikaeli atasimama... na kwenye Danieli 10:13,21. Kuna viumbe kumi na mmoja kwenye Biblia ambao pia wanaitwa kwa jina hili. Kusudi mkazo ulioko kwenye jina hili ni kukumbusha kuwa hakuna aliye kama Mungu kwa kuanzia usemi wa swali hili la kihamasa. Baadhi ya mambo ya kianthropomofia yanaonekana kuhusiana zaidi na Mungu kwenye Biblia kuliko ukweli wa kwamba inataja malaika wa BWANA ambaye anaonekana wazi kuwa ni mpeleka taarifa za ufunuo kwenye maandiko mengi yaliyopo (Mwanzo 16:7, 22:11 nk.) na huenda kwenye maandiko mengine mengi zaidi.

 

Kuna mawazo yanayotofautiana katika kutafsiri maneno ya Yesu yaliyo kwenye Yohana 8:58 (Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko) yanayosababisha kudai kuwa malaika huyu wa Bwana ndiye aliyetumwa duniani na kuzaliwa binadamu. Malaika wa Bwana ana mamlaka makubwa anapokuwa anayanena maneno ya Mungu moja kwa moja, katika nafsi ya kwanza, kana kwamba hakuwa na maisha hapo kabla ya kuzaliwa kwake duniani. Yesu anaonyesha jambo hili kwa kusema maneno yaliyo kwenye Yohana 5:30: “Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka. Hii ni namna fulani ya ushiriki wake kwenye asili ya kimbinguni 2Petro 1:4.

 

Maelezo au usemi miungu au Eeliim kwenye aya ya 11 yamewekewa maelezo yake kwenye jalada la chini ya ukurasa kwenye tafsiri ya KJV ikimaanisha wenye mamlaka. Hii kwa kweli inaonyesha kuwa ni kidokezo cha neno Eel kwenye Biblia, ambayo inatumika kwa namna mbalimbali sawa na neno Elohim. Limetumika kama uweza katika maeneo mengi kadhaa (Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Kumbukumbu la Torati 28:32; Nehemia 5:5; Mithali 3:27 nakadhalika). Na hata imetafsiriwa wema mkubwa Zaburi 80:10(11). Inamtaja kwa wazi mungu wa uwongo kwenye maandiko kadhaa, kama vile kwenye Waamuzi 9:46, na kwa sanamu za kuchonga ama kusubu kwenye maeneo mengine kama vile Isaya 44:10,15,17. Wakati mwingine ni neno la jumla kwa wote wawili yaani Mungu wa kweli na miungu ya uongo kama kwenye Kutoka 34:14. Ila mara nyingi inamtaja Mungu wa pekee na wa kweli kama ilivyo kwenye Mwanzo 14:18; 17:1; 21:33; 31:13; na 33:20, ambapo vyeo vyake vinaunganika nayo. Inatumika tu pale inapomtaja Mungu, ni ya kawaida sana kuonekana kwenye vitabu ninginevyo kama vya Ayubu, Zaburi, na Isaya (Ayubu 5:8; Zaburi 5:4(5); Isaya 5:16 et al.).

 

Lakini tuko hapa kukabiliana na matumizi maalumu ya neno lililo kwenye uwingi wenye mamlaka, ambao inaonekana kwamba kujumuisha kikundi cha miungu ya uwongo au mingineyo, wanaweza kuwa wanadamu wenye mamlaka au viumbe wengine wowote. Kutoka 15:11 ni andiko la kwanza linaloonekana kutaja kitu kingine zaidi kwa kutumia neno Eeliim. Mlinganisho na maandiko machache mengine yanaonyesha kuwa maelezo haya ni neno la kitaaluma kwenye kusanyiko linaloitwa kwa dhahiri la wana wa Mungu (Ayubu 1:6; 2:1 nk.), nyota za alfajiri (Ayubu 38:4), malaika (Isaya 1:9 nk.), na nyota za Mungu (Isaya 14:16). Zaburi 29:1: Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu;. Inavyosema hapa ni wana wa mwenyezi, maelezo yaliyopo kwa wazi hapa ni kitabu cha Ayubu. Zaburi 82:1: Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;… Maelezo yanaweza kuwa yalitafsiriwa vizuri kuwa kusanyiko kubwa au mkusantiko wa Mungu. Inaelezwa kwa wazi sana kuwa mkusanyiko huu sio wa namna nyingine ila ni wa wanadamu. Zaburi 89:6(7): Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na Bwana? Ni nani afananaye na Bwana miongoni mwa malaika? 7 Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu, Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka. Andiko hili linafanana sana na Kutoka 15:11. Ila inafafanua kwa karibu sana yule ambaye kwa hakika anahusika. Wenye nguvu hawa sio wale wanadamu wenye nguvu walio maarufu kwenye utawala wa Misri, bali ni viumbe walioko mbinguni. Aya hii inawahusisha pia wana wa mwenyezi walio kwenye Ayubu 29:1 katika dhana ya kusanyiko la mbinguni. Kwa hatua hii maelezo ya Zaburi kuhusu kuangukia mahali pa ufafanuzi wao kuhusu jukumu la Kutoka 15:11.

 

Tukiachana mbali na msisitizo ulio kwenye Zaburi, tunakutana na Isaya 14:13: Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. Iwe kwa namna nyingineyoyote au la, tunaitambua aya hii kama inamtaja Shetani, kwa kadiri mapokeo ya Kikristo yanavyojua na kuichukulia, kuna maeneo mawili yanayoonyesha wazi kuwa ni malaika wa mbinguni/ ya kwanza ni pale inaposema kuwa ni nyota za Mungu nay a pili ni pale inaposema kuwa mkusanyiko. Nyota za Mungu wanaweza pia kutafsiriwa kama nyota kuu, ambazo zinawatenga na kuwatofautisha na zile nyota zinazotoa nuru tunazoziona usiku wenye giza na usio na mawingu.

 

Danieli 11:36: “Naye mfalme atafanya kama apendavyo; naye atajitukuza na kujiadhimisha juu ya kila mungu, naye atanena maneno ya ajabu juu ya Mungu wa miungu, naye atafanikiwa mpaka ghadhabu itakapotimia; maana yaliyokusudiwa.” Maelezo yasemayo Mungu wa miungu yaliyopo hapa yanatamkwa pia kama Eel eeliim. Andiko linaonysha wazi kuwa Mungu ndiye anayetawala kwenye mkusanyiko wa eeliim.

 

Kutoka 15:12 inasema kwamba hawa wenyen mamlaka kuwa ni Wamisri/ inaonekana kuwa ni vyema sana kama tungelijua neno eeliim lililo kwenye aya ya 11 kuwa halimaanishi malaika waaminifu walioko kwenye baraza la mbinguni na wanadamu wanaoshirikiana nao, bali hata kwa wasio waaminifu na wenye dhambi wakiwemo wenye mamlaka wa Misri. Andiko linalofuatia kutoka kitabu cha Ezekieli linaonyesha kuwaelezea hawa mwenye mamlaka wa Misri wakiwa kwenye uangamivu wao pamoja na waasi wote waliokuwa kwenye baraza la mbinguni la malaika. Ezekieli 32:21: Walio hodari watasema naye, toka kati ya kuzimu pamoja nao wamsaidiao; wameshuka wamelala kimya, hata wasiotahiriwa, hali wameuawa kwa upanga. Neno eeliim limetafsiriwa hapa kama wenye nguvu (wengi).

 

Kutoka 15:13 Wewe kwa rehema zako umewaongoza watu uliowakomboa, Kwa uweza wako uliwaelekeza hata makao yako matakatifu.

 

Kifungu hiki kinabeba dhana ya wateule waliochaguliwa na Mungu. Wazo la kukombolewa au ukombozi kwenye Biblia lina misingi mikuu miwili. Wa kwanza ni ukombozi wa kila mzaliwa wa kwanza, ambalo ni kitendo cha kutambua ama kujua kwamba vitu vyote ni mali ya Mungu. Tendo hili limeelezewa vema sana kwenye maandiko kadhaa yaliyoko nyuma kabla ya andiko hili, ambayo ni Kutoka 13:2 na kadhalika., na inaonyesha mfano wa wazi kwenye Kutoka yenyewe, ambayo inachukua mahala pake kwenye andiko ambalo Mungu anamtaka mzaliwa wa kwanza wa Misri, na kupita juu kwenye nyumba zote walizopaka damu kwenye miimo ya milango yao (tazama Kutoka 12:12,13). Ukombozi mwingine mkuu kwenye Biblia ni ule anahusu kumuokoa mker wa ndugu aliye kufa wa ukoo wa lawi, wa ukoo wa lawi, ambaye alikuwa maarufu sana aliyeandikwa kwenye hadithi ya Ruthu. Wateule wanakuwa mali ya Mungu kwa mujibu wa kitabu hiki cha Kutoka, kwa namna ya mfano kama mzaliwa wa kwanza aliyekombolewa, au mke aliyekombolewa. Huu ni mwangukio mwingine wa usemi wa kinabii kwa Mungu kuwa ni kama Baba na bwana, na ni ibada ya sanamu kama ukahaba wa ndoa ya kiroho.

 

Swali linalofuatia ni kwamba huyu aliyekombolewa au mteule ni nani basi? Kuna mambo mawili ya kutimia maanani: moja inaheshima na nyingine ni shirikishi tu kwenye tendo la ukombozi wa Pasaka na Kutoka. Hiin ni barua halisia inayoonyesha maana muhimu ya historia. Ni watu halisia wasio na uzaliwa wa Israeli miongoni mwa waliokombolewa (Na kundi kubwa la watu waliochangamana mno wakakwea pamoja nao; Kutoka 12:38). Kwa ajili ya kuheshimu wito wa kupaka damu kwenye miimo ya milango yao, baadhi ya watu wasio hata wa nasaba ya Kiisraeli, kulikuwa na uwezekano mkubwa kuwa hata bkulikuwa na watu wengine waliokuwa na nasaba wa Kiisraeli hawakujumuishwa miongoni mwa wale waliokombolewa.

 

Hata hivyo, mambo yote mawili yana maana yake. Kwa ajili ya mtawanyiko wa Waisraeli, inawezekana kabisa kuwa hakuna mtu miongoni mwa walio hai leo anayetokana na uzao huu wa wale waliokombolewa wakati huu wa Kutoka kwao utumwani. Kama ukweli ungejulikana, basi wengi wangeshangaa sana kuona asilimia ya wazaliwa wanaoonekana leo kama ndio wenhyewe. Hata kwa Wayahudi walioko uhamishoni, siku zijazo wameijaza dunia, ili kufikia kiwango cha kwamba yale makabila kumi yaliyopotea yaweze kuikaribia kuijaza dunia. Hata hivyo, ushiriki wa mlo wa Pasaka na Kutoka kama vinavyotendeka kwa kiwango cha kidunia zaidi ni kitendo cha muhimu sana. Jinsi mtu anavyofanana na Wimbo huu wa Musa ni mwonekano wa muhimu kwake.

 

Kutoka 15:14-16

Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka, Wakaao Ufilisti utungu umewashika.

Ndipo majumbe wa Edomu wakashangaa, Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata, Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka.

Hofu na woga umewaangukia; Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe; Hata watakapovuka watu wako, Ee Bwana, Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.

 

Sehemu mbili za mwisho za utenzi huu mkuu zinaelezea makundi mawili yanayokabiliana: waliokombolewa na waoga walioshindwa vita. Maelezo ya kwanza hapa yanaelezea kwa kusisitiza jinsi waliopigwa walivyofikishwa kwenye hali ya kumcha Mungu kwa ushuhuda wa ukombozi wake uliotolewa na wale waliokombolewa kwenye Bahari ya Shamu. Hii inaenea zaidi ya Wamisri hadi kwa wale wanaompinga Mungu kwenye mataifa yote.

 

Kutoka 15:17-19

Utawaingiza, na kuwapanda katika mlima wa urithi wako, Mahali pale ulipojifanyia, Ee Bwana, ili upakae, Pale patakatifu ulipopaweka imara, Bwana, kwa mikono yako.

Bwana atatawala milele na milele.

Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, Bwana akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari.

 

Fungu hili la mwisho linarudia na kujenga umuhimu wa fundisho muhimun  za utenzi kwenye maelezo yake ya waliokombolewa. Kama vifungu vilivyotangulia yakienda zaidi ya Wamisri, basi hii inaenda zaidi vipindi katika kuangalia mbele kwenye ushindi wa dunia ya waliokombolewa. Wanapokea urithi wao na wanafanywa waishi kwenye Hekalu hilihili la Mungu, ambapo Bwana atatawala milele na milele.

q