Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[192]

 

 

Siku ya Bwana

Na

Siku za Mwisho

 

(Toleo La 2.0 19970208-20070824)

 

Maneno haya yanayosema kwamba Siku ya Bwana na Siku za Mwisho au Nyakati za Mwishoni mara nyingi yanachanganya na yanatafsiriwa kimakosa kwa ujumla. Kwenye Maandishi na Majarida mbalimbali ya Kikristo. Hapa tunafafanua maneno haya kwa mtazamo na maana ya kibiblia na kuona jinsi maandiko kadhaa zinazoelezea kuhusu dhana hii ya Siku ya Bwana tutaona kuwa haina maana ya Siku ya Bwana inayopigiwa upatu na kutafsiriwa kuwa ni siku ya Jumapili inayotumiwa kwa ibada za Wakristo wa mrengo huu wa Jumapili. Badala yake tutaiona kuwa ni kipindi cha fadhaa na kamsa ambacho kitafuatia Kurudi kwa Masihi na kuweka kipindi maalumu cha uingiliaji wa kimbinguni kwenye mambo ya mwanadamu. Pia tutajionea maana ya neno Siku za Mwisho au Nyakati za Mwisho Siku Iliyo Kuu ya Mwisho zinazojiri na kipindi chote cha Zama ya Masihi ambacho kimeelezewa vema sana kwenye unabii hadi kwenye kusudi lake kuu na mwisho wake.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

(Hati Miliki © 1997, 2007  Wade Cox)

 (Tr. 2013)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Siku ya Bwana na Siku za Mwisho



Mojawapo ya maneno yanayokosewa kueleweka maana yake kwenye Biblia ni usemi wa Siku ya Bwana, likifuatiwa kwa karibu na maneno mengine ya Siku za Meisho au Nyakati za Mwisho.

 

Dini kongwe za Kikristo yanajaribu kuichanganya Siku ya Bwana na Siku ya kumfanyia ibada Bwana na wanalitumia neno hili katika kuipa mashiko siku ya Jumapili kuwa ni ya kumfanyia ibada. Baadhi ya watunza Sabato wanalielewa neno hili kimakosa na wanalifanya utendaji kazi wake kuwa ni wa siku moja fulani tu na maalumu.

 

Siku za Mwisho

Maneno haya, Siku za Mwisho au Nyakati za Mwisho maranyingi yamechukuliwa kuwa yanahusiana na kipindi cha wakati fulani mahala fulani kilichokuwa mwishoni mwa karne ya ishirini au hata siku za mbele yake. Hata hivyo, hii sio maana iliyokusudiwa na Biblia kuhusu maneno haya.

 

Kusudi la kuandika jarida hili ni kuelezea na kufafanua maana ya maneno haya na kisha kuelezea vipindi husika vinavyojiri maneno haya.

 

Kuna awamu tatu za uumbaji wa viumbe. Awamu ya kwanza ilikuwa ni ya Adamu hadi Nuhu ambacho kiliishia kwenye kipindi cha Ibrahimu. Awamu ya pili kilikuwa ni cha Ibrahimu na Israeli ambacho kimeishia kwa Masihi. Awamu ya mwisho ni ya zama ya Masihi. Awamu hii inadumu kwa kipindi kilichokusudiwa kuwa ni cha miaka elfu mbili. Awamu hizi tatu zinadumu kwa jumla ya Yubile arobaini kwa wastani—na kufanya vipindi vitatu vyenye jumla ya miaka elfu mbili kila kimoja. Vipindi hivi vitatu

 

vilifanywa kwa mifano katika siku za nabii Musa kikiwa ni kipindi cha miaka arobaini mara tatu katika maisha yake. (tazama majarida ya Musa na Miungu ya Misri (Na. 105) na Pentekoste ya Sinai (Na. 115) [Moses and the Gods of Egypt (No. 105) and Pentecost at Sinai (No. 115)]. Musa alikuwa ni mfano wa Masihi, na maisha yake yaliwakilisha majukumu ya Masihi katika uumbaji.

 

Unabii wa Biblia unatuambia kwamba Siku za Mwisho au Nyakati za Mwisho zilianza kutoka kwenye huduma ya Masihi, na zilianzisha kipindi au zama za Masihi ambacho ndicho kilichoshuhudia adhimisho la kwanza la Pentekoste ya zama zake tuionayo kwenye Matendo 2:14-36.

 

Matendo 2:14-36  Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu. 15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana; 16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli, 17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto. 18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri. 19 Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi. 20 Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri. 21 Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa. 22 Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; 23 mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; 24 ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. 25 Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike. 26 Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi wangu ukafurahi; Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.27 Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu; Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu. 28 Umenijuvisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako. 29 Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo. 30 Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi; 31 yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu. 32 Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake. 33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia. 34 Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume. 35 Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako. 36 Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

 

Kwenye andiko hili, Mtume Petro alinukuu nabii Yoeli na pia alijuza kwamba mchakato ulikuwe kwamba, kabla ya kuja Siku ya Bwana, Mungu angefanya kitu kilichotabiriwa kupitio nabii Yoeli. Mungu alimfanya Yehoshua kuwa Bwana na Masihi, au Kristo, kwa kumfufua kutoka kwa wafu na kupaa kwake mbinguni.

 

Siku hii ya Bwana inatkuwa ni ya kamsa na maafa na sio siku ya kuabudu. Ni mwisho na kikomo cha zama ya Masihi. Maandiko haya yamenukuliwa kutoka kwenye 2:28-31.

Yoeli 2:28-31  Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; 29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu. 30 Nami nitaonyesha mambo ya ajabu katika mbingu na katika dunia, damu, na moto, na minara ya moshi. 31 Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo.

 

Andiko lililo kwenye Matendo ya Mitume linaendelea kwa kuinukuu Zaburi 16:8-11.

Zaburi 16:8-11 Nimemweka Bwana mbele yangu daima, Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa. 9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahi, Nao utukufu wangu unashangilia, Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini. 10 Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu. 11 Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele.

 

Kwa hiyo, zama za Masihi ilichukuliwa kuwa ni kipindi kilichojulikana kama Siku za Mwisho na ambacho kilianzia kwenye tukio la Pentekoste, kama ilivyoelezwa na Mtume Petro.

 

Siku hizi za Mwisho zilitajwa kwanza kwenye Mwanzo 49:1. Ahadi hii ya Yakobo ilikuwa itimilike kwa Israeli katika Siku za Mwisho sawasawa na makabila yao. Kwa hiyo ahadi ya uzaliwa wa kwanza iliyo kwenye Mwanzo 49 ambayo ni zama za Masihi.

Mwanzo 49:1-2  Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho. 2 Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu.


Tafsiri ya Biblia ya Revised Standard Version (RSV) inaiweka siku hii kama siku zijazo, bali maana yake ni Siku za Mwisho, kama ilivyotafsriwa hapa.

 

Nukuu-andishi kwenye Matendo 2:17 ilivyofanywa kwenye tafsiri ya New Oxford Annotated RSV inasema kwamba kipawa cha Roho Mtakatifu kwa wote wenye mwili, na sio ni kwa wateule mmoja mmoja, ni ishara ya zama za Masihi. Maana halisi ni kwamba Wamataifa walikubaliwa kuwa makuhani wa wateule pasi kujali nasaba zao.

 

Kitabu cha Waebrania kiliandikwa katika Siku za Mwisho.

Waebrania 1:1-2 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.  

 

Kwa hiyo ni jambo lisilo na shaka kuamini kwamba Biblia inataja kwamba Siku za Mwisho zilianzia tangia kuzaliwa na kufufuka kwake Masihi. Mtume Petro alijua Siku hizi za Mwisho kuwa zilianzia tangu kipindi hiki sawa na tunavyojjonea kwenye 1Petro 1:20, akiita kama utimilifu wa nyakati na mchakato wake ni mwendelezo uliofichika (1Petro 1:5).

 

Mtume Yohana alisema kwamba ilikuwa ni nyakati za mwisho au siku ya mwisho.

1Yohana 2:18  Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho.

 

Neno hili limeandikwa kama eschate õra (tazama kamusi ya Marshall’s Greek-English Interlinear). Hakuna makala kwenye kifungu hiki; kwa hiyo, makala nyingine zinapaswa zitathiniwe na kuonyesha kuwa “saa la mwisho”. Kwa hiyo Siku za Mwisho zilionekana kama ni mgawanyo wa nyakati. Matukio na kazi za Mpinga au Wapingakristo zitafanyika ndani ya kipindi cha migawanyo hii.

 

Nyakati zenyewe zinaonekana kuwa zitakuwa za hatari na za kutisha sana.

2Timotheo 3:1  Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

 

Mtume Yakobo, aliyekuwa ndugu yake Kristo, anaonysha kwamba hii itakuwa ni mabadiliko kamili kuipata dunia iliyopo leo na mfumo wake na taratibu zake za kiuchumi katika Siku hizi za Mwisho, na ambayo inaelekea hadi kupelekea kwenye kipindi cha kurudi kwake Masihi na anguko la mfumo ulioko leo (Yakobo 5:3-11).

Yakobo 5:3-11 Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. 4 Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. 5 Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. 6 Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi. 7 Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho. 8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia. 9 Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango. 10 Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu. 11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.

 

Kupinduliwa na anguko la utawala na mifumo iliyoko duniani leo kutafanya na mfumo mwingine ulio tofauti na mfumo wa kiuchumi uliozoeleka wa kimashirika ya leo na utakaomilikiwa na kutawaliwa na Mungu mwingine—atakayetoa Sheria, na ndiye yeye huyu aliyempa nabii Musa kwa mkono wa Kristo alipokuwa kama malaika hajazaliwa katika mwili.

 

Yuda 18 inarudia maneno ya kwenye 2Petro 3:3, akilionya Kanisa.

 

Usemi Siku ya Mwisho ndio neno la mwisho linalohitimisha kipindi hiki kinachoitwa cha Siku za Mwisho au Nyakati za Mwisho. Kutokana na mtume Yohana. Kristo anaonyesha kuwa hiki ni kipindi nyakati kinachojiri kwenye tukio la ufufuko wa wafu.

Yohana 6:39-44 Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho. 40 Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. 41 Basi Wayahudi wakamnung'unikia, kwa sababu alisema, Mimi ni chakula kilichoshuka kutoka mbinguni. 42 Wakasema, Je! Huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?43 Basi Yesu akajibu, akawaambia, Msinung'unike ninyi kwa ninyi. 44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.

 

Kwa hiyo, Siku ya Mwisho inayotajwa hapa ni ile ya Ufufuko wa Wafu ambacho ni cha Ufufuo wa watakatifu. Hata hivyo, kipindi hiki chote sio ni cha mchakato cha Ujio wake na kuwa hakina uhusiano wowote na Ufufuo wa Kwanza wa wafu.

 

Ufufuko wa wote wenye mwili pia unaitwa ufufuo wa Siku ya Mwisho.

 

Yohana 11:24-27 Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho. 25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo? 27 Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.

 

Hapa Kristo alikuwa anasema kwamba Lazaro alikuwa anapewa ufufuo katika Kristo mbali na ule ulikuwa unatarajiwa na Yuda. Watu waliomkataa Kristo bado watahukumiwa ifikapo Siku ya Mwisho.

Yohana 12:48 Yeye anikataaye mimi, siyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.

 

 Kwa hiyo, Siku ya Mwisho inajiri kipindi cote cha ufufuo, ambacho ni cha miaka efu (Ufunuo 20:4-14) kujumlisha miaka mia moja mingine (Isaya 65:20).

 

Ufunuo 20:4-14  Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu. 7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; 8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. 9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. 10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele. 11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

 

Kwa hiyo miaka mingine mia ya Ufufuo wa Pili inatokea.

Isaya 65:20 Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.  

 

Kipindi hiki cha miaka hii mia moja ni sehemu ya mchakato wa hukumu ya mwisho. Siku ya Mkutano wa makini ni sikukuu yenye umuhimu mkubwa sana. Hiki ni kipindi tofauti na kile cha Milenia, bali ni sehemu bado ya Siku ya Bwana.

 

Usemi usemao Siku za Misho au Nyakati za Mwisho unaelelezea pia mcakato mzima wa utawala wa millennia wa Masihi.

Mika 4:1-2 Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi. 2 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, na nyumbani kwa Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana litatoka Yerusalemu.

 

Kipindi hiki kinaonekana wazi sana kuwa kitakuwa kwenye ufufuko wa wote wenye mwili. Neno linalotumika hapa ni Nyakati za Mwisho, lakini kwenye tafsiri ya KJV inasomeka kuwa Siku ya Mwisho na aya yenyewe inamaanisha kuwa ni mwishoni mwa siku zote (ukitazama Biblia ya Companion Bible utaona hivyo, sawa na hivyo, pia kwenye Mwanzo 49:1 (aya hiyohiyo moja); Hesabu 24:14; Isaya 2:2 nk., Ezekieli 38:8,16; Hosea 3:5).

Hosea 3:5 baada ya hayo wana wa Israeli watarejea, na kumtafuta Bwana, Mungu wao, na Daudi, mfalme wao; nao watamwendea Bwana na wema wake kwa kicho siku za mwisho.   

 

Wakati Israeli watakapokaa salama katika Siku au Nyakati za Mwisho, majirani wao wa kaskazini yaaani Gogu na Magogu wataletwa ili kupigana na Israeli. Hii ndiyo maana inaitwa Nyakati za Mwisho, na tunaona kwenye Ufunuo kwamba itatokea mwishoni mwa millennia pamoja na kipindi chote cha mwanzoni (sawa na Ezekieli 38:1-23).

Ezekieli 38:1-23 inasema: Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee Gogu, wa nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake, 3 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Gogu, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali; 4 nami nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa, pamoja na jeshi lako lote, farasi na hao wapandao farasi, wote wamevaa silaha za namna zote, jeshi kubwa sana, wenye ngao na kigao, wote wakishika upanga; 5 Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo; 6 Gomeri, na vikosi vyake vyote; nyumba ya Togarma, pande za mwisho za kaskazini, na vikosi vyake vyote; naam, watu wengi pamoja nawe. 7 Ujiweke tayari, naam, jiweke tayari, wewe na majeshi yako yote waliokukusanyikia, nawe uwe jemadari wao. 8 Na baada ya siku nyingi utajiliwa; katika miaka ya mwisho, utaingia nchi iliyorudishiwa hali yake ya kwanza, baada ya kupigwa kwa upanga, iliyokusanywa toka kabila nyingi za watu, juu ya milima ya Israeli, iliyokuwa ukiwa wa daima; lakini imetolewa katika kabila za watu, nao watakaa salama salimini wote pia. 9 Nawe utapaa juu, utakuja kama tufani, utakuwa kama wingu kuifunika nchi, wewe, na vikosi vyako vyote, na kabila nyingi za watu pamoja nawe. 10 Bwana MUNGU asema hivi; Itakuwa katika siku hiyo, mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utakusudia kusudi baya; 11 nawe utasema, Nitapanda juu niiendee nchi yenye vijiji visivyo na maboma; nitawaendea watu wanaostarehe, wanaokaa salama, wote wakikaa pasipo kuta, ambao hawana makomeo wala malango; 12 ili kuteka mateka, na kuwinda mawindo; uugeuze mkono wako juu ya mahali palipoharibika, ambapo sasa panakaliwa na watu, na juu ya watu waliokusanyika toka mataifa, waliopata ng'ombe na mali, wakaao katikati ya dunia. 13 Sheba, na Dedani, na wafanya biashara wa Tarshishi, pamoja na wana-simba wake wote, watakuambia, Je! Umekuja kuteka mateka? Umekusanya jeshi lako, ili kuwinda mawindo? Kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua ng'ombe na mali, kuteka mateka mengi sana? 14 Basi, mwanadamu, tabiri, umwambie Gogu, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile watu wangu, Israeli, watakapokaa salama, hutapata habari? 15 Nawe utakuja kutoka mahali pako, kutoka pande za mwisho za kaskazini, wewe, na watu wa kabila nyingi pamoja nawe, wote wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, na jeshi kuu; 16 nawe utapanda juu uwajilie watu wangu, Israeli, kama wingu kuifunika nchi; itakuwa katika siku za mwisho, nitakuleta upigane na nchi yangu, ili mataifa wanijue, nitakapotakaswa kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao. 17 Bwana MUNGU asema hivi; Je! Wewe ndiwe niliyemnena zamani za kale, kwa vinywa vya watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri siku zile kwa muda wa miaka mingi, ya kwamba nitakuleta upigane nao? 18 Itakuwa katika siku hiyo, Gogu atakapokuja kupigana na nchi ya Israeli, asema Bwana MUNGU, ghadhabu yangu itapanda katika mianzi ya pua yangu. 19 Kwa maana katika wivu wangu, na katika moto wa ghadhabu yangu, nimenena, Hakika katika siku ile kutakuwako tetemeko kubwa katika nchi ya Israeli; 20 hata samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama wa kondeni, na vitu vyote vitambaavyo juu ya nchi, na wanadamu wote walio juu ya uso wa nchi, watatetemeka mbele ya uso wangu; nayo milima itatupwa chini, na magenge yataanguka, na kila ukuta utaanguka chini. 21 Nami nitaita upanga, uje juu yake katika milima yangu yote, asema Bwana MUNGU; nao upanga wa kila mtu utakuwa juu ya ndugu yake. 22 Nami nitamhukumu kwa tauni, na kwa damu; nami nitanyesha mvua ifurikayo, na mvua ya mawe makubwa sana, na moto na kiberiti juu yake, na vikosi vyake, na watu wa kabila nyingi walio pamoja naye. 23 Nami nitajitukuza, na kujitakasa, na kujidhihirisha, mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.  

 

Kutoka kwenye aya hii tunona kwa wazi kwamba miaka ya mwisho inahusika na mchakato huu unaoitwa siku moja.

 

Tunaona kutoka na mwenendo huu kwamba Mungu alianza kufanya kazi na Israeli na Yuda wakati alipowapeleka kwanza huko utumwani. Kipindi chote cha Masihi kinahusiana na muingilio kati wa Mungu kwenye mambo na shughuli za wanadamu. Mungu akaiteua Yerusalemu kuwa ni kituo au kitovu cha ibada kwa nyakati zote mbili, yaani kipindi cha Hekalu lake la nyakati za mwisho na kwa kile cha marejesho mapya cha Masihi ambacho kwamba Mungu ataifanya upya dunia kwa kufanya kazi na wanadamu kwenye kipindi chote cha millennia.

 

Yohana Mbatizaji na Masihi walikuwa ni mashahidi wawili huko Yerusalemu na Yuda watakuwa kwenye mwanzo wa kipindi cha zama za Masihi. Kwa hiyo Kanisa lilisimama kama shahidi dhidi yao kwa kipindi chote cha miaka arobaini ya Ishara ya Yona. Mtume Yakobo aliuawa shahidi mwaka 63 BK na Kanisa likakimbilia huko Pella tangu kipindi hiki. Mnamo siku ya 1 Nisan 70 BK, Yerusalemu ulizingirwa na jeshi la Warumi. Kwa hiyo ukahusuriwa kwa maangamizo yaliyopangiliwa kwa makini kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja hadi kufikia Siku ya Upatanisho ya mwaka 70 BK.

 

Mchakato huu umeelezewa na kuandikwa kwenye kitabu cha nabii Ezekieli tangia sura ya 4 na kuendelea. Ulijikuta ukizingirwa na Wababelonia kama maonyo, lakini maonyo yaliyotolewa kwa unabii na Ezekieli hayajawahi kutimilika hadi ilipofikia mzingiro wa mwisho.

 

Mchato huu uliendelea kwa kipindi cha miaka elfu mbili nab ado unaendelea.

 

Kwanza kabisa Ezekieli aliwataja wateule tangia kwenye sura ya 5:1-4.

Ezekieli 5:1-4 Nawe, mwanadamu, ujipatie upanga mkali, kama wembe wa kinyozi ujipatie, ukaupitishe juu ya kichwa chako na ndevu zako; kisha ujipatie mizani ya kupimia, ukazigawanye nywele hizo. 2 Theluthi ya hizo utaiteketeza katikati ya mji, siku za mazingiwa zitakapotimia; nawe utatwaa theluthi, na kuipiga kwa upanga pande zote; nawe utatawanya theluthi ichukuliwe na upepo, nami nitafuta upanga nyuma yake. 3 Nawe twaa nywele chache katika hizo, na kuzifunga katika upindo wa mavazi yako. 4 Nawe utatwaa tena baadhi ya hizo, na kuzitupa katikati ya moto, na kuziteketeza katika moto huo; kutoka nywele hizo moto utakuja na kuingia katika nyumba yote ya Israeli.

 

Wateule ni masalio yaliyounguzwa na moto, na kati yao utakuja moto utakaoiunguza nyumba yote ya Israeli katika Nyakati za Mwisho.

 

Ndipo Mungu ataanza kufanya kazi pamoja na taifa lenyewe la kimwili akiongoza kutoka Yerusalemu.

Ezekieli 5:5-12 Bwana MUNGU asema hivi; Huu ndio Yerusalemu; nimeuweka kati ya mataifa, na nchi zauzunguka pande zote. 6 Nao umeasi hukumu zangu, kwa kutenda mabaya kuliko mataifa hayo, nao umeasi sheria kuliko nchi hizo ziuzungukazo; maana wamezikataa hukumu zangu, wala hawakuenda katika sheria zangu. 7 Basi, kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi mmefanya ghasia kuliko mataifa wawazungukao ninyi, wala hamkuenda katika sheria zangu, wala hamkuzishika hukumu zangu, wala hamkutenda kama kawaida za mataifa wawazungukao; 8 basi, Bwana MUNGU asema hivi; Angalia, mimi, naam, mimi, ni juu yako; nami nitafanya hukumu kati yako machoni pa mataifa. 9 Nami nitakutenda nisiyoyatenda zamani, wala sitafanya tena mambo kama hayo, kwa sababu ya machukizo yako yote. 10 Kwa sababu hiyo baba za watu watawala wana wao kati yako, nao wana watawala baba zao; nami nitafanya hukumu ndani yako, na hao wote waliosalia kwako nitawatawanya kwa pepo zote. 11 Kwa sababu hiyo, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika kwa kuwa umepatia unajisi patakatifu pangu, kwa matendo yako yote niyachukiayo, na kwa machukizo yako yote, kwa sababu hiyo mimi nami nitakupunguza; wala jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma. 12 Theluthi yenu mtakufa kwa tauni, na kwa njaa watakomeshwa ndani yako; na theluthi yenu wataanguka kwa upanga pande zako zote; na theluthi yenu nitawatawanya kwa pepo zote, kisha nitafuta upanga nyuma yao.

 

Yerusalemu uliingiliwa na walioushinda mara 24 kwa mujibu wa historia yake, na watu wake waliwekwa kwenye mazingiwa na kutekwa. Vitisho vya waliowazingira Yuda vinaonekana hapa. Utawanyiko wa wakazi wake uliosababishwa na mzingiro wa tatu ambao waliokoka kwa kufuatwa na upanga. Hii ina maana fulani katika Nyumba ya Mungu. Kwa kipindi cha karne kadhaa, wateule wamekuwa wakijaribiwa kwa moto usiokoma. Mungu aliendelea kuuonya mji wa Yerusalemu tangu kwenye Ezekieli 5:13-17.

 

Hatua ya pili katika kuliadhibu taifa la Israeli ni kwenye kipindi ambacho Israeli ilikuabwa na na hali iliyolisababishia kuwa kama taifa lililoparaganyika au milima. Wakajitia unajisi kwa kuabudu sanamu na miungu ya uwongo, na miji yao ilifanyika kuwa maganjo kwa ajili ya kuabudu kwao miungu ya uwongo.

Ezekieli 6:1-7 Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, uelekeze uso wako uitazame milima ya Israeli, ukaitabirie, 3 ukisema, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana MUNGU; Bwana MUNGU aiambia hivi milima na vilima, na vijito na mabonde; Tazama, mimi, naam, mimi, nitaleta upanga juu yenu, nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, 4 Na madhabahu zenu zitakuwa ukiwa, na sanamu zenu za jua zitavunjika; nami nitawatupa wana wenu waliouawa mbele ya vinyago vyenu. 5 Nami nitaiweka mizoga ya wana wa Israeli mbele ya vinyago vyao; nami nitaitawanya mifupa yenu pande zote za madhabahu zenu. 6 Kila mahali mkaapo miji itaharibika, na mahali palipoinuka patakuwa ukiwa; ili madhabahu zenu ziharibiwe, na kufanywa ukiwa, na vinyago vyenu vivunjwe, na kukoma, na sanamu zenu za jua zikatwe, na kuangushwa, na kazi zenu zifutwe kabisa. 7 Na hao waliouawa wataanguka katikati yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana 

 

Taifa la Israeli lilipaswa lipelekwe utumwani na kutokomelea huko wakati lilipoangukia kwenye kwenye mkazo wake wa kuabudu na wajibu wake kwa Mungu. Baadhi yao hata hivyo waliachwa na kunusurika hai wakiwa kama masalia watakaomrudia Mungu.

Ezekieli 6:8-10 Lakini nitasaza mabaki; maana mtakuwa na baadhi ya watu watakaoukimbia upanga kati ya mataifa, mtakapokuwa mmetawanyika katika nchi za watu. 9 Na hao wa kwenu watakaookoka watanikumbuka kati ya mataifa, watakakochukuliwa mateka, jinsi nilivyoiponda mioyo yao ya kikahaba, iliyoniacha, na macho yao, yaendayo kufanya uasherati na vinyago vyao; nao watajichukia nafsi zao machoni pao wenyewe, kwa sababu ya mabaya yao yote, waliyoyatenda kwa machukizo yao yote. 10 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; sikusema bure kama nitawatenda mabaya hayo.  

 

Wakati wenyeji hawa wa Yerusalemu walipopelekwa utumwani kwenye hatua yao ya mwisho mwaka 70 BK, ilionekana haikuchuma ubani kwa vinyago. Walipelekwa utumwani kwa kuwa iliziasi na kuzibadili Sheria za Mungu kwa mapokeo yao. Bali walikuwa bado wanaendelea kwa uaminifu sana kumuabudu Mungu huyuhuyu wa kweli, ila walikuwa wameziasi na kuigeuza Torati yake kwa kuyatukuza mapokeo ambayo yaliwapelekea wenyewe kuangukia imani na dini za Kibabeloni. Walikuwa bado wanaziadhimisha Sikukuu na Siku zote Takatifu bali walikuwa wanayageuza maana yake na ibada na walikuwa wameanza kuitumia Kalenda iliyoanzishwa kwa mujibu wa mapokeo yao.

 

Baada ya kumshuhudia Masihi, ndipo Yuda walianza kulitesa Kanisa kiasi cha kuwaua wateule wake. Yakobo, ndugu yake Yesu, alikumbwa na maafa kama hayahaya kama Masihi, na ndivyo walivyowafanyia Mitume wote isipokuwa Yohana. Kutopka kipindi hiki, Mungu alianza kuwaletea maangamizi kwenye itikadi na imani ya Yuda katika Yerusalemu. Ugumu huu wa mioyo wa Yuda utaishia na kufikia kikomo chake itimiapo miaka elfu mbili. Mwishoni wataongoka. Hata hivyo watakuwa wamebobea kwenye mapokeo yao kwa kipindi chote kizima. Kwakweli, walikuwa wameyashinikiza mapokeo haya kiasi kwamba inaonekana kuwa ni vigumu kushika imani ya kale asilia kwa kuyashika mapokeo yao na mfumo wao wa kalenda. Muundo mzima wa Wayahudi walioko Ulaya ulikuwa karibu ukomeshwe kabisa kwenye mauaji ya Kimbari maarufu kama Holocaust yaliyofanyika kwenye Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Vita vya karne ya ishirini ilikuwa na maonyo kwa wote wawili, yaani Israeli na Yuda, ila hawakuweza kabisa kuyajali wala kuyatilia maanani maonyo haya. Tunapaswa kukumbuka kwamba Mungu alisema kwamba: Hakuna laana inayokuja pasipo sababu (Mithali 26:2).

 

Kuja kwake kutafanyiza marejesho mapya ya mfumo mzima wa kiibada na imani ya kweli ya Torati ya Mungu. Mapokeo yote pamoja na imani na mafundisho yote ya uwongo ya wote wawili, yaani Wayahudi na dini potofu za kale za Ukristo wa uwongo vitafutiliwa mbali kipindi hiki. Masihi alisema kuwa maandiko hayawezi kutanguka (Yohana 10:35), na manabii wamesema kwamba utaratibu wote wa utunzaji wa Sabato, kukiwepo na Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu, vitaanzishwa kutoka mjini Yerusalemu.

 

Kipindi cha kuanzia Ujio wa Masihi akiwa kama Mfalme-Masihi wa Israeli hadi ufufuo wa wote wa wafu utakapotokea na kuirudisha Siku ya Mwisho, ambayo ni Mwisho wa Siku zote ambayo pia ni Siku ya Bwana.

 

Siku ya Bwana

Neno sahihi na halisi la kwanza la Siku ya Bwana lipo kwenye Isaya 2:12.

Isaya 2:12 Kwa maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.

 

“Yatashushwa chini linamaanisha kubadilisha sheria iliyopo leo hapa duniani kama tunavyoona kwenye Ufunuo na Yakobo 5 (hapo juu).

 

Hii ni ya kwanza kati ya maonekano ishirini ya neno hili kwenye Biblia. Kutoka kwenye matumizi haya tunaona kwamba inaonyesha mwingiliano wa mambo ya hapa sayarini, ambayo ni Ujio wa Masihi na kuyatiisha mataifa. Hili litafanyika kwa kuongeza muda. Tumejionea kutoka hapo juu kwamba neno lipo kwenye kipindi cha muunganiko na neno Siku ya Mwisho, ambacho kinadumu kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu moja.

 

Mtume Petro anatuambia jambo hili anapoongelea kuhusu uvumilivu wa Mungu na suala la muda machoni pa Mungu.

2Petro 3:8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

 

Kwenye matukio kumi na sita neno hili limeandikwa yom Yahovah au siku ya Yahova (Isaya 13:6,9; Ezekieli 13:5; Yoeli 1:15; 2:1,11; 3:14 (sawa na Waebrania 4:14); Amosi 5:18,20; Obadia 15; Sefania 1:7,14 (mara mbili); Malaki 4:5).

Isaya 13:6-9 Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu. 7 Kwa sababu hiyo mikono yote italegea, na moyo wa kila mtu utayeyuka. 8 Nao watafadhaika; watashikwa na utungu na maumivu; watakuwa na utungu kama mwanamke aliye karibu na kuzaa; watakodoleana macho; nyuso zao zitakuwa ni nyuso za moto. 9 Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.   

 

Kipindi hiki pia kitakuwa na vita.

Ezekieli 13:5 Hamkupanda kwenda mahali palipobomolewa, wala hamkuitengenezea nyumba ya Israeli boma, wapate kusimama vitani katika siku ya Bwana.

 

Yoeli 1:15 Ole wake siku hii! Kwa maana siku ya Bwana inakaribia, nayo itakuja kama uangamivu utokao kwake aliye Mwenyezi.

 

 Siku hii ya Bwana ni ya mapigano ya mwanzo wa kipindi cha mwanzo wa millennia kilichotabiriwa na kwenye Yoeli 2:1-11.

Yoeli 2:1-11 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu; Wenyeji wote wa nchi na watetemeke; Kwa maana siku ya Bwana inakuja. Kwa sababu inakaribia; 2 siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza kuu. Kama mapambazuko yakitandazwa juu ya milima, hao ni wakuu, tena wenye nguvu, mfano wao haukuwako kamwe, wala hautakuwako baada ya hao, hata katika miaka ya vizazi vingi. 3 Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na bustani ya Adeni mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao. 4 Kuonekana kwao ni kama kuonekana kwa farasi; na kama wapanda farasi ndivyo wanavyopiga mbio. 5 Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto ilapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita. 6 Mbele yao watu wanahangaika; nyuso zote zimegeuka kuwa nyeupe kwa hofu. 7 Hupiga mbio kama mashujaa; huupanda ukuta kama watu wa vita; nao huendelea mbele kila mmoja katika njia zake, wala hawapotoshi safu zao. 8 Wala hapana mmoja amsukumaye mwenzake; huendelea mbele kila mmoja katika njia yake; hujifanyizia njia kwa nguvu kati ya silaha, wala hawaachi kuifuata njia yao. 9 Huurukia mji; hupiga mbio juu ya ukuta; hupanda na kuingia ndani ya nyumba; huingia madirishani kama aingiavyo mwivi. 10 Nchi inatetemeka mbele yao; mbingu zinatetemeka; jua na mwezi hutiwa giza, na nyota huacha kuangaza; 11 naye Bwana anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya Bwana ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili?

 

Kwa hiyo, vita ya Siku ya Bwana itakuwa ni kubwa sana mwanzoni mwake na hakutakuwepo na kitu chochote kama hiki kwa vizazi vingi.

 

Hii inajumuisha kipindi cha mchakato huu haiepushi na kuwa mbali na kipindi kingine cha mbele, kama tunavyojionea kwenye maandiko.

 

Inapendeza kuona aina vita na uwezo wa majeshi yakizuia uwezekano wa watu kujeruhiwa. Hii ni aina ya vita inayopiganwa na silaha na mashine ambayo hatujawahi kabisa kuviona hapo kabla au hata kuziwazia kwenye fikra za mavumbuzi ya kisayansi inayoghushiwa kwenye sinema. Mungu anaruhusu utisho huu kuwaangukia wanadamu kwa ajili ya uovu wao.

 

Hukumu ya itikadi ya Mungu kwa namna mbili. Ya kwanza ni hukumu ya kimwili na itakayowatiisha mataifa ili kuanzisha utaratibu wake. Hii inahusisha tu kuukomesha na kuuangamiza mfumo na utawala wa mataifa.

 

Yoeli 3:9-21 Tangazeni haya kati ya mataifa; takaseni vita; waamsheni mashujaa; watu wa vita na wakaribie; na wapande juu. 10 Yafueni majembe yenu yawe panga, na miundu yenu iwe mikuki; aliye dhaifu na aseme, Mimi ni hodari. 11 Fanyeni haraka, mje, enyi mataifa yote, wa pande zote, jikusanyeni pamoja; na huko watelemshe mashujaa wako wote, Ee Bwana. 12 Mataifa na wajihimize, wakapande juu katika bonde la Yehoshafau; maana huko ndiko nitakakoketi niwahukumu mataifa yote yaliyo pande zote. 13 Haya! Utieni mundu, maana mavuno yameiva; njoni, kanyageni; kwa maana shinikizo limejaa, mapipa nayo yanafurika; kwani uovu wao ni mwingi sana. 14 Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno! Kwa maana siku ya Bwana i karibu, katika bonde la kukata maneno. 15 Jua na mwezi vimetiwa giza, na nyota zimeacha kuangaza. 16 Naye Bwana atanguruma toka Sayuni, atatoa sauti yake toka Yerusalemu; na mbingu na nchi zitatetemeka; lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, na ngome ya wana wa Israeli. 17 Hivyo ndivyo mtakavyojua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, nikaaye Sayuni, mlima wangu mtakatifu; ndipo Yerusalemu utakapokuwa mtakatifu, wala wageni hawatapita tena ndani yake kamwe. 18 Tena itakuwa siku ile, ya kwamba milima itadondoza divai tamu, na vilima vitatiririka maziwa, na vijito vyote vya Yuda vitatoa maji tele; na chemchemi itatokea katika nyumba ya Bwana, na kulinywesha bonde la Shitimu. 19 Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya dhuluma waliowatenda wana wa Yuda; kwa sababu wamemwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao. 20 Bali Yuda atadumu milele, na Yerusalemu tangu kizazi hata kizazi. 21 Nami nitaitakasa damu yao ambayo sijaitakasa; kwa maana Bwana ndiye akaaye Sayuni.

 

Kitendo cha kuyatiisha mataifa kitashuhudia pia uanzishwaji wa Yuda na Yerusalemu katika Siku za Mwisho. Ila siku hizi sio jambo muhimu sana cha kuangalia kwenye matarajio pekee.

Amosi 5:18-27 Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru. 19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma. 20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga. 21 Mimi nazichukia sikukuu zenu, nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini. 22 Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka zenu za amani, na za wanyama walionona. 23 Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu. 24 Lakini hukumu na itelemke kama maji, na haki kama maji makuu. 25 Je! Mliniletea dhabihu na sadaka jangwani muda wa miaka arobaini, enyi nyumba ya Israeli? 26 Naam, mtamchukua Sikuthi, mfalme wenu, na Kiuni, sanamu zenu, nyota ya mungu wenu, mliojifanyizia wenyewe. 27 Kwa sababu hiyo nitawahamisha, hali ya kufungwa, mwende mbali kupita Dameski, asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.

[Matendo 7:43 inasema mbali na Babeli amhavyo ni zaidi ya Damascus na inammanisha mfumo wa kidini pia. Roho Mtakatifu amelichukua andiko la aya hii.]

 

Siku ya Bwana inayotajwa hapa ilikuwa ni kwa Waisraeli kwanza, kisha kwa Yuda na hatimaye kwa mataifa. Kwa hiyo, neno hili lilitumika kama mlolongo au mfuatano wa matukio ya Mungu kwa kipindi kizima chote cha utumwa wa Israeli na kutiishwa kwa mataifa. Tunajionea kutokana nah ii kukamilika kwa Mpango kama mara moja kwenye kurasa za historia, ikihusiana na mlolongo wa matukio ya unabii wa Siku za Mwisho.

 

Upangiwaji wa mataifa kwenye ahadi zaa milki zao za uzaliwa wa kwanza (kama tuonavyo hapo juu) kunaonekana kuwa kutaitangulia hukumu ya Mungu kwa Israeli. Kitashuhudia Baraka kuu, hawakuzitunza Sikukuu zake na katika utakatifu na haki yake. Hukumu na Haki ni neno moja kwenye lugha ya Kiebrania la: tsedek.

 

Tunaona kwamba hii inatenda kazi kwa wamataifa, kutokana na Obadia 15-17.

Obadia 15-17 Kwa maana hiyo siku ya Bwana i karibu juu ya mataifa yote; kama ulivyotenda, ndivyo utakavyotendwa; malipo yako yatakurudia juu ya kichwa chako mwenyewe. 16 Kwa maana kama vile mlivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote watakavyokunywa daima; naam, watakunywa na kubabaika, nao watakuwa kana kwamba hawakuwa kamwe. 17 Bali katika mlima Sayuni watakuwako wenye kuokoka, nao utakuwa mtakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki milki zao.

 

Mchakato huu ni wa taratibu kwa watu wote. Vita vya karne ya ishirini ni sehemu ya nchakato huu unaokusudia au kulenga kuvunja nguvu za watakatifu. Ni mara tu baada ya nguvu za watakatifu zitakapokomeshwa, ndipo ule mwisho utakapokuja (Danieli 12:7). Mchakato huu umeanza kuanzia Vita Kuu ya Pili ya Dunia na unaendelea. Kipindi kinachojulikana kama cha Utimilifu wa Mataifa kiliishia mwaka 1996-1997 (tazama jarida la Kuanguka Kwa Misri (Na. 36); Unabii wa Mikono ya Farao Iliyovunjika [The Fall of Egypt (No. 36) The Prophecy of Pharaoh’s Broken Arms)].

 

Sefania 1:7-18 Nyamaza kimya mbele za Bwana MUNGU; Kwa maana siku ya Bwana i karibu; Kwa kuwa Bwana ameweka tayari dhabihu, Amewatakasa wageni wake. 8 Na itakuwa, katika siku ile ya dhabihu ya Bwana, nitawaadhibu wakuu, na wana wa mfalme, na watu wote waliovaa mavazi ya kigeni. 9 Na katika siku ile nitawaadhibu hao wote warukao juu ya kizingiti, waijazao nyumba ya bwana wao udhalimu na udanganyifu. 10 Na katika siku ile, asema Bwana kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani. 11 Haya! Lieni, ninyi mkaao katika Makteshi, maana wafanya biashara wote wameangamia; hao wote waliokuwa na mizigo ya fedha wamekatiliwa mbali. 12 Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya sira zao; wasemao katika mioyo yao, Bwana hatatenda mema, wala hatatenda mabaya. 13 Na huko utajiri wao utakuwa mateka, na nyumba zao zitakuwa ukiwa; naam, watajenga nyumba, lakini hawatakaa ndani yake; nao watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake. 14 Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko! 15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu, 16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana. 17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi. 18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha.

 

Neno Maktesh maana yake ni chokaa au tukuza au soketi. Inadaiwa kuwa ni jimbo au wilaya iliyo karibu na mji wa Yerusalemu, ila mtazamo huu unawezakutokana na matumizi yake hapa. Huenda linawamaanisha wakazi wa mji. Kama haita maanisha mahala maalumu. Kuharibiwa kwa utaratibu kijamii unaofanywa na masuala ya kijeshi na kiviwanda ndiyo inayomaanishwa. Na hii inahusisha kipindi kirefu na kilicho zaidi ya karne ya ishirini.

 

Kwahiyo, Yuda wanatajwa hapa kama walengwa wa maangamizo ya majeshi yaliyowazunguka ya mataifa, kama vile ya Ashuru, na kunatajwa kuangamizwa kwa mji wa Ninawi. Mchakato huu wa kuondolewa na kuangamizwa kwa Yuda ulifanywa na Wababelonia, waliochukua nafasi ya kutawala ya Waashuru. Kwa hiyo, hii Siku ya hasira ya Bwana, iliyotajwa kwenye Sefania 2:1-14, inahusisha kipindi cha uharibifu na maangamizo ya Waashuru na kinaendelea hadi kwenye kipindi chote cha utawanyiko, na hadi kipindi cha marejesho mapya yatakayofanywa kwa lugha kamilifu na katika marejesho mapya ya Israeli (Sefania 3:6-20).

 

Maana Nyingine

Kwenye vifungu vine imeelezewa kwa kutumia neno lamed na maana ya siku inayojulikana na Yahova (Isaya 2:12 (angalia hapo juu); Ezekieli 30:3; Zekaria 14:1,17).

 

Kuangamia kwa Misri na kusini kulionekana kuwa kama ni sehemu ya Siku ya Bwana au Siku inayojulikana na Yahova.

Ezekieli 30:3-7 Kwa maana siku ile i karibu, siku ile ya Bwana i karibu, siku ya mawingu; itakuwa wakati wa mataifa. 4 Na upanga utakuja juu ya Misri, na dhiki itakuwa katika Kushi, watakapoanguka watu waliouawa katika Misri, nao watauondoa wingi wa watu wake, na misingi yake itabomolewa. 5 Kushi, na Putu, na Ludi, na watu wote waliochanganyika, na Kubu, na wana wa nchi ya agano, wataanguka kwa upanga pamoja nao. 6 Bwana asema hivi; Nao pia wanaoitegemeza Misri wataanguka, na kiburi cha uwezo wake kitashuka; toka Migdoli hata Sewene, wataanguka ndani yake kwa upanga, asema Bwana MUNGU. 7 Nao watakuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake itakuwamo kati ya miji iliyoharibika.

 

Kwenye andiko hili, maangamizo ya Misri yanaanza na Nebukadneza wa Babeli (Ezekieli 30:10). Kwa hiyo. Siku inayotajwa hapa sio ile iliyo kwenye Ufunuo bali ni ya kamsa inayoonyesha mfano unaoendana.

 

Aina hii ya siku inayojulikana na Bwana, inaonekana pia kwenye Zekaria 14:1-21. Hata hivyo, kwenye andiko hili tunaona kwamba Masihi anahusishwa na watakatifu (Zekaria 14:1-5) na kwa kweli ni kipindi cha mwingiliano.

Zekaria 14:1-5 Tazama, siku moja ya Bwana inakuja, ambayo mateka yatagawanyika kati yako.2 Kwa maana nitawakusanya mataifa yote walete vita juu ya Yerusalemu; na huo mji utapigwa, nazo nyumba zitatekwa, nao wanawake watatendwa jeuri; na nusu ya watu wa mji watatoka kwenda utumwani; ila mabaki ya watu wa mji hawatakatiliwa mbali. 3 Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita. 4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini. 5 Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu; kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli; naam, mtakimbia, kama vile mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku za Uzia, mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye.

 

Usemi na dhana ya kusema siku moja inavyoonekana kutoka kwenye andiko hili.

Zekaria 14:6-16 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba nuru yake haitakuwa na mwangaza na kiwi; 7 lakini itakuwa siku moja, iliyojulikana na Bwana; si mchana, wala si usiku; lakini itakuwa, ya kwamba wakati wa jioni kutakuwako nuru. 8 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba maji yaliyo hai yatatoka katika Yerusalemu; nusu yake itakwenda upande wa bahari ya mashariki, na nusu yake upande wa bahari ya magharibi; wakati wa hari na wakati wa baridi itakuwa hivi. 9 Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja. 10 Nchi yote itageuzwa kuwa kama Araba, toka Geba mpaka Rimoni upande wa kusini wa Yerusalemu; naye atainuliwa juu, atakaa mahali pake mwenyewe, toka lango la Benyamini mpaka mahali pa lango la kwanza, mpaka lango la pembeni; tena toka mnara wa Hananeli mpaka mashinikizo ya mfalme. 11 Na watu watakaa ndani yake, wala hakutakuwako laana tena; lakini Yerusalemu utakaa salama. 12 Na hii ndiyo tauni, ambayo Bwana atawapiga watu wote waliofanya vita juu ya Yerusalemu; nyama ya mwili wao itaharibika, wasimamapo juu ya miguu yao, na macho yao yataharibika ndani ya vichwa vyao, na ndimi zao zitaharibika vinywani mwao. 13 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba mashaka makubwa yatokayo kwa Bwana yatakuwa kati yao; na kila mmoja wao atakamata mkono wa jirani yake, na mkono wake utainuliwa ili kushindana na mkono wa jirani yake. 14 Yuda naye atafanya vita juu ya Yerusalemu; na huo utajiri wa mataifa wa pande zote utakusanyika, dhahabu, na fedha, na mavazi; vitu vingi sana. 15 Na hivyo ndivyo itakavyokuwa tauni ya farasi, na nyumbu, na ngamia, na punda, na ya hao wanyama wote watakaokuwamo matuoni mle, kama tauni hiyo. 16 Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda.

 

Aya ya 17 inaonyesha kuwa mataifa hayo ambayo hayatawapeleks watu wake kushika sikukuu huko Yerusalemu, vyua haitanyesha kwao kwa wakati muafaka. Ni kusema kwamba dunia itakuwa inazishika kwa kuziadhimisha Sikukuu za Mungu kipindi hiki cha utawala wa millennia au vinginevyo watakumbwa na baa la njaa hadi watakapotubu au vinginevyo watakufa.

 

Usemi huu wa siku moja ni wa kimfano tu, kwa kuwa itachukua kipindi cha miaka saba kuyaleta na kuyatiisha mataifa hadi yayatii mamlaka ya Yerusalemu. Tunajionea somo hili au mchakato huu kutokana na anguko la mataifa kwa namna mbili zote na habari ya Yeriko (tazama jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142) na pia kutokana na vita vilivyoandikwa kwenye Ufunuo, kwenye majarida ya  Mihuri Saba (Na. 140), Baragumu Saba (Na. 141) na Miaka Thelathini ya Mwisho ya Dhiki ya Mwisho (Na. 219) [The Fall of Jericho (No. 142), The Seven Seals (No. 140); The Seven Trumpets (No. 141) and The Last Thirty Years: the Final Struggle (No. 219)].

 

Kwa hiyo inahusika na Ufufuo wa Kwanza kutoka hapo na kuendelea. Hii siku inaonekana itakuwa kwenye kipindi cha utawala wa millennia, na mataifa yote watajua umuhimu na kulazimika kuitunza Sikukuu ya Vibanda kila mwaka, vinginevyo mvua haitanyesha kwao kwa majira yake muafaka (Zekaria 14:13-21).

 

Sehemu nyingine kwenye Biblia neno hili limejumuisha na maneno mengine kama vile hasira au kisasi.

 

Neno Siku ya Bwana limetokea mara nne kwenye Agano Jipya (1Wathesalonike 5:2; 2Wathesalonike 2:2; 2Petro 3:10 na Ufunuo 1:10).

 

1Wathesalonike 5:1-4 Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. 2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. 4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

Maana yake hapa ni kwamba dunia inafikiri kwamba imeendeleza ama kuanzisha utawala wa amani na mtangamano pasipo Torati ya Mungu, lakini hiki ni kipindi ambacho mifumo hii yote itakuwa imekomeshwa na kuangamizwa.

 

Neno lililotumika kwenye 2Wathesaloniake 2:2 ni siku ya Kristo kwenye KJV, bali neno halisi ni siku ya Bwana (kuriou; sawa na ilivyo kwenye Marshall’s Greek-English Interlinear). Siku hii ya Bwana ni siku iliyokuwa kwenye unabii wa Agano la Kale uliotajwa hapo juu. Neno Siku ya Kristo limetumika kwenye Wafilipi 1:10. Mtume Paulo anasema kwamba hii ni Siku ya Kristo (Wafilipi 2:16) na kwamba ataifurahia, na kwamba hatakimbia mbio za bure.  Kwa hiyo, Siku ya Kristo ni namna nyingine ya kuelezea mchakato wa matukio yatakayoanza kutokea taiga Ujio wake hadi Ufufuo wa wafuwote. Mtume Paulo anaingojea siku hii na tukio hili kwa hamu kubwa, kwa kweli, hakujua kitu zaidi hadi ifike siku hii.

 

Mtume Petro anaonyesha kuwa Siku ya Bwana inahusika kipindi chote cha kuanzia kuja kwake hadi kile cha hukumu na hadi cha kuangamia kwa Dunia yote kwa moto na kuanzishwa kwa makao mapywa kwenye Mji wa Mungu. Maandiko haya hayapingani; bali yanawaonysha wasomaji wenye bidii wa Biblia mpangilio na Nyakati zilizo kwenye Mpango wa Mungu.

2Petro 3:10-16 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? 13 Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. 14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake. 15 Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; 16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.

 

Mungu alimpa Kristo unabii wa mwisho wa Ufunuo, ambao alifunuliwa na Mungu. Kristo, alikuwa nao hadi kipindi kile, akautendea kazi kwa imani na aliendelea kuwa mwaminifu na mtiifu hadi kifo chake kwa imani. Hatimaye Kristo akamfunulia mtume Yohana ili uweze kuandikwa vema na kiuaminifu. Mambo mengine bado yamefichwa hayajafunuliwa hadi kwenye kipindi chake cha mwisho ambapo yatafunuliwa kwa manabii wa Mungu. Na ni kwa sababu hii ya kunukuu Ufunuo wa Mungu ndipo Yohana alisalia kuwa hai, kama Kristo alivyoonyesha (Yohana 21:22-23). Ufunuo ni ufafanuzi wa unabii wa Mathayo 24 (hususan aya ya 22). Ila siku hizo zitafupishwa inamaanisha uharibifu au maangamizi, bali sio mchakato wote mzima.

 

Ufunuo 1:1 Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohana;

Yohana alichukuliwa katika Roho katika Siku ya Bwana ili aione hatima yake na mchakato wa maangamizo ya mataifa kwa kipindi hiki. Yohana aliyaona matukio yatakayokuwa yakiendelea kwenye kipindi chote kizima. Kipindi hiki kilikuwa ni cha miaka elfu moja na mia moja cha Siku ya Bwana.

 

Siku Iliyokuu nay a Mwisho ni Sikukuu yenye umuhumu wake kwa kuwa inatoa taswira ashirio la kipindi hiki cha mwisho cha miaka mia moja cha mchakato wa Ufufuo wa Pili wa wafu.

 

Andiko lililo kwenye Ufunuo 1:10 limasema Siku ya Bwana nadala ya Siku Iliyowekwa na Bwana na waabudu siku ya Jumapili wanavyojaribu kuitafutia namna ya kuihalalisha kwa kutumia Biblia kwa matendo yao, itikadi ambayo ukweli uliopo imetokana na ibada za kale za waabudu Jua. Wanatafuta kwa mbinu kutokana na maneno haya kwamba Yohana alipewa maono haya siku ya Jumapili, ambayo kwamba ndiyo aliyoiita kuwa ni Siku ya Bwana. Huu ni uwongo mkubwa kabisa. Tendo la kuabudu siku ya Jumapili na kufanya makutaniko ya ibada halikuwa likifanyika hapo mwanzoni hadi ilipofikia katikakati ya karne ya pili—na hatimaye ilifanyika huko Roma peke yake. Iliibuka kutoka na waliokuwa wanaipinga imani ya Kisemitiki na ilitumika kama namna ya kulilinda Kanisa huko Roma lakini haikuweza kuchukua mahala pa Sabato hata kama hivyo (tazama kiyabu cha Justin Martyr (Martyr-Mfiadini), kiitwacho Dialogue with Trypho; cf. Bacchiocchi, From Sabbath to Sunday, pp. 231ff.).

Ufunuo 1:10-11 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu, 11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.

 

Maandiko ya Kiyunani yametumia neno kuriake emera au siku ya kifalme (tazama kitbu cha Marshall’s Interlinear). Inaelezea mchakato wote mzima au mfululizo wa mambo na matukio yaliyoandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo yatakayojiri kwenye kipindi cha utawala wa miaka elfu moja. Haimaanishi kabisa na siku ya Jumapili; wala na mchakato unaohusiana na Ujio wa Bwana siku ya kupigwa kwa Baragumu ya mwisho, kama mlolongo wa mambo yaliyo kwenye kitabu cha Ufunuo ilivyelekezwa kwa kina sana. Mchakato mzima unaonekana kuwa ni Siku ya Bwana. Ufufuo wa wafu utakuwa wa awamu mbili na utachukua kipindi cha miaka elfu, kama inavyosema na kuonekana kwenye Ufunuo 20 ambako imeelezwa kwa wazi sana. Mchakato uneoonyesha ,chakato endelevu wa Siku ya Bwana hadi kufikia kwenye utiishaji wa mataifa ya dunia. Kwa kweli, Kristo pia anauelezea awamu hii iliyoelezwa pia kwenye Ufunuo ambayo inaendelea kwa kipindi cha miaka elfu moja akiifananjsha na saa oja kwenye Yohana 5:25-29.

Yohana 5:25-29 Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai. 26 Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake. 27 Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. 28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. 29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.

 

Biblia ya KJV inasema kuwa ufufuo wa hukumu na, neno lililotumika la kiyunani ni kriseõs na lina maana ya hukumu na, kwa hiyo usahihi (tazama kitabu cha Marshall’s Interlinear na Bibliai ya RSV). Tafsiri hii kwenye  Biblia ya KJV imetolewa ili kuunga mkono imani ya Utatu au Utrinitariani ya mafundisho kuhusu roho, ambayo ni ya uwongo (tazama jarida la Roho (Na. 92) [The Soul (No. 92)].

 

Kipindi mtambuka cha Siku za Meisho na cha Siku ya Kumuadhimisha Bwana kinatuama jumla ya zaidi ya miaka efu tatu. Usemi huu wa saa moja linaweka neno linguine la nusu saa lililotumika kwenye Ufunuo 8:1 kwa mihuri saba zaidi kuliko kitu kingine chochote. Nusu saa ni kipindi moja ya arobaini na nane ya siku moja. Hesabu hii ni kipindi cha mtambuka wa miaka iliyo kwenye Yubile inayotangulia kabla ya miaka ya mwisho ya Sabato na Yubile ya miaka. Hesabu hii ya arobaini na nane ni mavuno ya tatu. Nusu saa iliyo kwenye maelezo haya inamaana ya moja ya arobaini na nane au mwaka wa hamsini ya miaka elfu moja; ambayo kwamba, ni miaka ishirini kwa kudumu kwake. Kutokana na jinsi alivyotumia Kristo kuhusu saa, kingeweza pia kuendelea zaidi.

 

Tatizo halisi lililoko hapa ni kwamba tofauti ya maneno itategemea na mgawanyo wa vipindi vinavyohusiana na zama za mwanadamu na uhusiano wake na sayari au dunia.

 

Maneno haya yanasisitiza uingiliaji wa Mungu kupitia Masihi.

 

Kwa hiyo, tofauti hii imeendelezwa na Biblia kwamba zama za leo ni siku za mwanadamu, ambayo kwamba wanadamu wanajaribu kumuondoa Mungu kutoka kwenye uumbaji (1Wakorintho 4:3).

1Wakorintho 4:3 Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.

 

Siku ya Bwana ni kiondi cha haki na hukumu ya Bwana, na hiki kinachukua kipindi cha zaidi ya miaka elfu moja cha kukamika au kuhitimishwa kwa zama za Dunia.

 

q