Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[229]

 

 

Mwanzo wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega

(Toleo La 1.0 19971217-19971217)

 

Malumbano na hoja za Wakristo wa siku hizi kuhusu Kristo yana mambo mengi yanayotokana na falsafa za Kiyunani na imani na matendo yaliyokuwa kwenye dini za kale yanayoenenda kinyume kabisa na mafundisho ya Biblia. Baadhi ya maandiko ya aya za biblia za Kiingereza yamepotoshwa kitafsiri ili kutimiza malengo na mwelekeo wa mwenendo wa kiimani na jinsi ya kuyachukulia maneno kwa kuwa yanakusudiwa yaendane na mwelekeo wa imani na teolojia ya waamini Utatu. Maana wanayoyachukulia neno la Mwanzo, Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, chimbuko na mwisho wake. Yamefafanuliwa kwa kina ikitiliwa maanani kujumuisha maandiko mengine kadha wa kadha.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki © 1997  Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org


Mwanzo wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega

 


Kwenye majarida mbalimbali yanayohusu Mungu na Masihi, tumeshughulika na mambo mawili ya kwanza ya dhana iliyopo kuhusu Uungu, kwa wale wanaoitwa Mungu Baba, na Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu. Muhtasari wake unapatikana kwenye ya kwanza ya jarida letu la Matamko ya Msingi wa Imani ambapo Mungu Baba anaonekana wazi sana kuwa ndiye Mungu wa pekee na wa kweli, na kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu na kwamba kwa kujua na kuelewa hivyo ni sharti muhimu katika kuupata uzima wa milele (Yohana 17:3).

 

Mungu Baba

Muweza wa Mambbo yote na Muumbaji wa Ulimwengu huu ni Mungu. Yeye ni Mwenye Uweza na guvu zote, Muumbaji na ndiye Aliyezifanya au Kuziumba Mbingu, nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake (Mwa. 1.1; Neh. 9:6; Zab. 124:8; Isa. 40:26,28; 44:24; Mdo. 14:15; 17:24,25; Ufu. 14:7). Yeye peke yake ndiye hawezi kufa wala kupatwa na madhara yoyote (1Tim. 6:16). Yeye ndiye Mungu wetu na Baba yetu, na ndiye Mungu na Baba wa Yesu Kristo (Yn. 20:17). Yeye ndiye Mungu Mkuu na Aliye Juu Sana (Mwa. 14:18; Hes. 24:16; Kum. 32:8; Mk. 5:7) na ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli (Yn. 17:3; 1Yoh. 5:20).

 

Yesu Mwana wa Mungu

Yesu ni mzaliwa wa kwanza (prototokos) kati ya viumbe vyote (Kol. 1:15) ambaye ni mwanzo (arche) wa kuumba kwa Mungu (Ufu 3:14). Yeye ni mzaliwa wa pekee (monogene) Mwana wa Mungu (Mt. 3:17; Yn. 1:18; 1Yoh. 4:9), aliyetungwa mimba yake kwa uweza wa Roho Mtakatifu na akazaliwa na bikira, Mariamu ambaye anaitwa kimakosa Maria au Mary kwa Kiingereza (Lk. 1:26-35). Yeye ni Kristo au Masihi (Mt. 16:16; Yn. 1:41), aliyetumwa kutoka kwa Mungu ili awe Mwokozi na Mkombozi wetu (Mt. 14:33; Yn. 8:42; Efe. 1:7; Tit. 2:14).

 

Maelezo yaliyo kwenye Ufunuo 3:14 kwamba Kristo ni mwanzo wa kuumba kwa Mungu yana maana kubwa sana. Hatuelewi kwa ujumla leo kwa nini Yesu  Kristo alimwambia Yohana awaambie Kanisa la Walaodikia, akikazia kuwa, “mwambie malaika wa kanisa lililoko Laodikia kuwa mimi ni mwanzo wa kuumba kwa Mungu”. Sasa, sababu iliyofanyika hivyo ilikuwa ni kwa sababu, kwenye kanisa la Walaodikia, malumbano yaliibuka kwa namna zote mbili, yaani kanisani na kwa zama zile kwamba Kristo hakuwa mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Malumbano haya yalituama karibu kwenye suala la umilele na uwepo wa Mungu kwenye mambo yote.

 

Neno mwanzo maana yake ni kuanza. Neno lililo kwenye Ufunuo 3:14 linaonekana kuhusiana na mjadala wa kifalsafa ambao ulishika kasi sana huko Mashariki ya Kati kutoka kwa Philo kwa kupitia Imani ya Kiplatoni ya zama za Kati. Hoja ilituama kwenye suala la theori kuhusu chanzo au mwanzo wa dunia. Yakupasa kuelewa kuhusu hoja hizi kwa kuwa maana yake inaelekea kwenye Vuguvugu la Mkakati wa Zama Mpya. Utaelewa au kujua pia kuhusu Kufuru ya mkakati huu wa Vuguvugu la Zama Mpya. Na pia utajua kuwa ni unabii wa Yesu Kristo kwamba hoja hizi zingeweza kuibuka kwenye kanisa katika siku za mwisho na kwamba kanisa la Walaodikia lingetiwa unajisi na vuguvugu hili na kuondolewa sehemu yake kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu. Mwanazuoni wa kiteolojia Clement wa Alexandria aliyachukulia malumbano haya kama ni mtindo au aina ya Ukostiki (Nostis au Gnosis maana yake ni ujuzi au maarifa wakati kwamba Unostiki au Gnosticism ulikuwa ni mchakato ambao kwamba mwangaza uliowezeshwa na kutolewa). Kuna viwango viwili vilivyopo; vya kukubalika na Unostiki. Makuhani kwa kweli walifanyika kuwa na asili ya Unostiki. Walidaiwa kuwa wana maarifa ya siri na hii haki ilipewa kiwango cha chini cha ujuzi au maarifa. Haya kiutendaji yalifanyika kuwa mafundisho ya Wanikolai ambapo makuhani walioelimishwa au kusomeshwa waliaminiwa kuwa walikuwa na maarifa na uelewa ambao hii haki hawakuwanayo, au hawakumudu kuwanayo kiasi cha kuwafanya wakubalike kujumuishwa kwenye imani za kisirisiri na za fumbo zilizohusiana nayo. Kristo alisema kwamba anayachukia mafundisho ya Wanikolai na mafundisho ya Balaamu ya kufundisha kwa ajira. Mafundisho ya Balaamu yanaendana mkono kwa mkono na mafundisho ya Wanikolai na mafundisho haya, na kwa kweli, ni ya Mpingakristo moja kwa moja. Yanahuia au kuzuia nafasi ya Roho Mtakatifu kukua ndani ya mtu. Yatupasa kujua uhusiano na utendaji kazi wake katika Roho Mtakatifu. Mafundisho haya yamefafanuliwa vizuri kwenye majarida ya Wanikolai (Na. 202) na pia lile la Mafundisho ya Balaamu na Unabii wa Balaamu (Na. 204).

 

Clement alimfuatia mwandishi wa Kiyahudi aliwate Philo kwenye kuutafsiri mwanzo uliotajwa kwenye kitabu cha Mwanzo kwa kutuama kwenye tofauti iliyopo kati ya Uplatoniki kati ya mguso hisia na uashawishi wa kiakili ya dunia ya wenye akili. Maneno ya kiraslimali na yasiyo ya kiraslimali kimsingi yaliendelezwa sambamba na mistari ya Kiplatoniki. Kwa hiyo, alikuwa akibishana pia na upande wa Uplatoniki ambao pia ulichukuliwa kuwa ni ulimwengu wenye kuvutia kama nakala yenye mashiko. Salvatore Lilla (kwenye kitabu chake cha Clement of Alexandria [Clement wa Alexandria], Sura ya III, Oxford University Press, 1971, p. 192) analiona hili na kwenye ukurasa wa 230 anasema:

Fundisho lililohusika la Clement, kama Philo na Uplatoni wa Kati, yaonekana kuamini kwenye dhana ya kuwepo kwa kiumbe siku za kabla ya kuzaliwa rasmi na kuichukulia hii kubadilisha aina yoyote na kiwango chochote (sawa na ilivyo kwenye Sura ya III, ukurasa wa 226).

 

Makubaliano yalikuwa ni sehemu tu kwa kama alivyokataa Clement mtazamo wa nadharia hii ya Kiplatoni kwa mujibu wa jambo ambalo kwamba mtu anaweza kuwa archai – uwingi wa mwanzo chimbuko au chanzo cha dunia. Clement alisema kuwa isingeweza kuwa; lakini wao walisema ilikuwa hivyo, na jambo hilo ni halisi. Clement anatetea kwamba Mungu ndiye mwanzo pekee na wa kweli na mwanzo mwingine wowote mwingine unafuatiwa kutoka kwa Mungu. Sasa Kristo alikuwa anasema kwamba yeye alikuwa ndiye mwanzo wa uumbaji wa Mungu kwa kuwa aliumbwa kuwa mwakilishi kutoka kwa Mungu. Huo ndio msimamo wa biblia, na ndiyo maana Yesu Kristo alisema hivyo. Clement aliamini baadae, kwamba Mungu ndiye mwanzo pekee wa uumbaji, jambo ambalo ni kweli kutokana na Ufunuo 4, ambapo vitu vyote vimeumbwa kwa mapenzi ya Mungu. Lakini Waplatoni walikuwa wanasema kuwa yeye mwenyewe tu ndiye alikuwa ndiye mwanzo. Clement aliamini uwepo wake mapema ya mwanzo wa dunia. Kwa maneno mengine, yeye alikuwa na uwepo au uzima wa ndani kwa ndani yake mwenyewe kabla ya kuumbwa kwa dunia. Hii ni sawa tu na suala la kipigo kikubwa. Kwa hiyo nadharia ya kipigo kikubwa sio kitu kipya. Haya ni mafundisho ya Kiplatoniki. Clement alitetea lawama ya kwamba Wastoniki, Plato, na Aristotle walichukulia uwepo huu wa mwanzoni kuwa ni kama moja ya kanuni za kwanza. Aliliweka sawa jambo hilo ili lielezewe na wanafalsafa hawa kama kiasilia kulikuwa tupu na hakukuwa na ubora wowote na kukafafanuliwa na Plato kama ni mimi anayekuja kuwepo na kuishi kwa kukubalika (upodoche) (soma pia Timaeus 49e-50a, 50b-c), na kuwa umbo tupu (Tim. esp. 50d-e), vigumu kujua (51b1), maana iliyo pana zaidi kwa maana ya kutokuwa halali au kiuharamu (alikosea: Lilla) kufikiria kwa kutoaminika kirahisi (52b2). Clement anaonekana kukubaliana nao kabisa (Lilla, p. 193). Kwa hiyo huko tuna makanisa yanayoanza kutunga na kuingiza dhana hizi, wakiachana kabisa na isemavyo biblia na wakielekea kwenye Uplatoniki. Huu ni mwanzo wa kufikiria Uttinitariani na Uplatoniki wake, safi na rahisi. Philo (wanafalsafa wa Kiyahudi akiandika kwenye kipindi cha kabla ya Kristo) na Plutarch kwa kinyume chake kabisa alimchukulia huyu aliyekuwako huko nyuma kuwa ni kama bado ni ousia (Lilla, p. 230). Lilla anasema kwamba Plutarch pamoja na Waplatoni wengine wa zama Kati kama vile akina Albinus, Apuleis na watunzi wa kitabu cha tatu wa huko Diogenes Laertius na wa Hippolytus walimchukulia kiumbe huyu kuwa ni kama wa milele na aliye tupu kwa kila kiwango na asiye na umbo (ibid., Ch. III, pp. 193,195-6). Kwa hiyo, walikuwa wanasema kabisa kwamba ni juu yake na yupo, lakini hana umbo waka muonekano, bali ananing’inia tu mahali apajuapo mwenyewe. Tuna muundo huu (umilele) unaobeba ujazo wa tabia ya Mungu. Una umilele kwa haki yake. Kutokana na mchakato huo wa kimawazo ndipo kumetokea imani ya Uanimisti ya Kibabeloni na kwa zaidi tu kwamba ni mwanzo wa mchakato wa wazo au dhana hiyo. Kuhusiana na jambo akiwa kama mimi zaidi Clement anakubaliana na imani ya Upythagoreanism mamboleo, pamoja na Plotinus, na huenda pia na Ammonius Saccas (Lilla, Ch. III, pp. 195-196 and fn. 1, p. 226).

 

Kiumbe anayejadiliwa kuwa ni kama hana umbo na wa milele au ameumbwa bila umbo. Hicho ndicho kiini na maana ya mabishano haya. Umilele usio na umbo wa kiumbe huyu unamfanya awe kuwa ousia au mshirika na Mungu, kwa hiyo Mungu ndiye aliyefanyika kuwa mwili na ambaye ni washirika na Mungu walikuwa ni washirika wa kimsingi. Sasa tunakwenda mbali na zaidi ya hapo makanisani mwetu.

 

Ndipo swali liliibuka: Dunia iliumbwa au haikuumbwa? Kwa maneno mengine, je, ilikuwa na uzima yenyewe au iliumbwa? Hii inaondoa malumbano ya huko nyuma sasa ya nadharia ya viumbe kugeukageuka yaani evolusheni na uumbaji. Kristo alikuwa anasema kwamba haikuwa hivyo; na kwamba yeye alikuwa ndiye chanzo. Alikuwa ndiye chombo kilichotumiwa kwenye uumbaji wa Mungu na kwamba jambo hilo (ulimwengu) wenyewe haukuwa ni chanzo na Mungu sio kwamba hayupo kwenye jambo, hayuko kwenye miamba, kwenye jiwe, na kwenye nyasi. Kusema kwamba Mungu yupo kwenye jambo, kwa maana ya kuharibu au kuangamiza na kuua na kwamba Mungu mwenyewe anamaovu yake kwa ndani yake, dhana hiyo ni ya makufuru makubwa. Hivyo tunafikia kwenye hatua ambapo Shetani alichukuliwa kuwa muovu tangu mwanzoni mwa kuumbwa kwake na kwa kweli ni mshirika anayeandamana na uovu akimchukiza Mungu.

 

Ni sawa tu kabisa, kwamba malaika ni washiriki wa Mungu, kama viumbe wapeleka ujumbe wake. Mtu anaweza sasa kuona uovu mkubwa wa kufuru inayojitokeza. Watu wamepigwa upofu kwenye tatizo hili. kwa kiasi kikubwa ni kwa sababu wanayafuata mafundisho na sera za serikali ambazo hazina lolote la kulinganisha na imani ya kibiblia. Na ndiyo maana Mungu na Kristo wake wanayachukia sana mafundisho ya Wanikolai. Yanawapofusha watu wasiisikie wala kuona kweli. Wamepotoshwa kwa mafundisho ya Waplatoni. Wateule wanapaswa kutahadharishwa na kujiepusha na makosa ya kimafundisho.

 

Ujumbe kwa Walaodikia umeweka wazi sana kwa kiasi fulani kutokana na mjadala huu. Mjadala wa kifalsafa ulituama karibu kwenye utoshelezi wa kwamba muumbaji mwenyewe ni ousia au mshirika wake yeye na kwamba Mungu alikuwa yupo kwenye suala zima lolote. Kwa hiyo Mungu alikuwa kwenye ubao au kuni na jiwe. Hii ni dhana au wazo la msingi nyuma ya imani ya Kianimism pamoja na ile iliyokutikana huko Babeli, ya Ushamanism na Nadharia zote za Uhuru na Ukombozi zinazoeneza imani ya Kibudha na imani iliyoshika dau huko Japani ya Ushintoism. Sasa kitabu cha Sir Wallace Budge kuhusu Babeli (alichimba kwa kina kuhusu jambo hili) kimekuwa karibu kwa kipindi kirefu. Tumekijua kwa zaidi ya miaka mia kuwa dini ya Babeli ipo. Dini ya Kibabeli ilikuwa ya kianimistiki nah ii ndiyo hasa dini yenyewe iliyoyasukuma karibu Makanisa mengi ya leo.

 

Clement, kama alivyokuwa Philo na Waplatoni wa pande za Mashariki ya Kati – Plutarch na Atticus – walionyesha wazi sana kupendelea kizazi. Clement, akimfuatia Philo, alitetea kwamba uumbaji haukuwa umefanyika kwa wakati, kwakuwa wakati wenyewe unategemea moja kwa moja na mwelekeo wa ulimwengu (Lilla, p. 230). Hii kimsingi makosa (kwa kuwa sababu zilimetolewa hapo mwanzoni na kwenye majarida mengine) na zilichukuliwa na Augustine kwenye kitabu chake cha Mji wa Mungu. Kurudia kipengele cha Wakati na Hali ya Kutokufa kutoka kwenye jarida la Uzima wa Milele (Na. 133):

Wazo au dhana ya wakati inajitokeza tu wakati kunakuwa na uhusiano kati ya vitu. Kwa mfano, siku inatokea kwa mzunguko au mwenendo wa dunia kwenye mhimili wake ikihusishwa na jua. Mwaka unaotokana na mzunguko wa jua unajulikana kama mageuzi mamoja ya dunia karibu na Jua. Kuna miaka kadhaa inayohusishwa kwenye mwenendo au mzunguko wa mhimili, yaani Jua/Upande/Kigalaktiki. Ulimwengu una jinsi ya kujiongeza au kujitanua ambayo inahusiana na mwenendo wa mbali na kituo cha msingi.

 

Kituo cha msingi kiliamuliwa na Penrose kuwa ni kama kipimo cha nguvu cha kumi na hadi kwa kumi hadi kwa 123 [cha nishati]. Hivyo, kutokana na nguvu zake zote za asili za namba hii yapasa kuwa na sababu ya mwanzo wake, na sio nyingine kwa ulimwengu. Mienendo yake yote imeelezewa kwene dhana ya wakati ambao unahusiana na mfumo wa mzunguko wa dunia.

 

Licha ya utaratibu wa upimaji inaweza tu wakati ule ilianza kwa kuhusiana na idadi ya kitu kimoja au zaidi kwa kila kimoja kwa kingine. Hivyo basi kipindi kingeanzia tu kwa uwepo wavitu viwili au zaidi. Mungu alikuwepo hata kabla ya kuanza kwa muda. Kizazi cha elohim kwa kweli ndicho kilikuwa ndiyo mwanzo wa wakati. Mwanzo wa kuumba kwa Mungu (Ufu. 3:14). Wakolosai 1:15 inasema kwamba Kristo alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza na wa pekee wa Uumbaji.

 

Kwahiyo Bwana Mungu ni Alfa, kwa maana zote mbili na yupo anaishi, na ndiye mwisho wa mambo ya matendo yale. Yeye pia ni Omega:

Ufunuo 1:8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.

(yaan wakati anapofanyika kuwa yote katika yote na ndani ya yote (Efe. 1:23)).

 

Wazo la wakati lilianza kwa uwepo wa Yesu Kristo. Kwa kuwa wakati Yesu Kristo alipoumbwa (na elohim walipoumbwa) ndipo wakati ulianza kwa kuwa kulikuwa na uhusiano kati ya viumbe. Ni Mungu peke yake ndiye aliishi milele pasi kufa wala kupatwa na madhara. Licha ya masuala ya upimaji, kuna vitu viwili vinavyofanya kuwepo na muda au wakati. Kristo ndipo anafanyika kuwa uumbaji wa Mungu kutokana na kuzaliwa kwake. Viumbe wote wametokana na Mungu. Kwa hiyo, Mungu ndiye wa Mwanzo au Alfa kwa namna au maana mbili zote na kwa kuwepo na ni wa mwisho kwenye utendaji. Hivyo, yeye pia ni Omega kutokana na Ufunuo 1:8. Hivyo Kristo alilionya kanisa la Walaodikia na tunapaswa kujua kuhusu maonyo waliyoonywa Walaodikia.

 

Alfa na Omega jinsi alivyoendelea hadi kwa Yesu Kristo

Majina cheo ya Alfa na Omega na majina mengine yaliyotumiwa hasahasa kwenye kitabu cha Ufunuo yanajibu hamu ya kifilosofia ya Kiyunani pamoja na kuelezea ukweli wa uwakilishi wa elohim kwa wateule kupitia kwa Yesu Kristo.

 

Ufunuo 1:11 kwenye tafsiri ya KJV inataja cheo hiki cha Alfa na Omega ikimtaja na kumhusisha Yesu Kristo. Jina hili la kicheo halipo kwenye tafsiri ya RSV na nakala za maandiko ya kale (kama inavyosema Companion Bible angalia kwenye andiko hilo). Inaonekana tu kwenye tafsiri ya Receptus na pia kwenye KJV.

 

Umuhimu wa nyongeza hii kwenye matumizi yake ili kuonyesha mtiririko ya kile kinachotokea kwenye utendaji kazi wa jina cheo hili toka Mungu hadi kwa Kristo kwenye mtiririko wa unabii wa Ufunuo.

 

Hivyo, andiko halisi linalosomwa zaidi au lisilosomwa sana kama ilivyo tafsiri ya RSV:

Ufunuo 1:11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.

 

Andiko hili linatokana na tafsiri ya KJV:

Ufunuo 1:11  ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.

Uingizaji huu wa andiko umefanywa maalumu na kwa makusudi ili kuunga mkono au kutetea imani ya Utatu au Utrinitarian na kupuuzia maana iliyokusudiwa na sehemu nyingine iliyobakia ya Ufunuo kwenye suala hili.

 

Ufunuo 1:8 inafafanua rejea hii kuwa inamhusu Mungu ambaye Ufunuo 1:6 inasema kuwa ni Mungu na Baba wa Kristo.

Ufunuo 1:8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.

 

Tunaona tena KJV ikiitumia tafsiri ya Receptus kuwakilisha maneno ho theos au Mungu na ikitumia kurios peke yake au Bwana. Kwa hiyo andiko hili linabeba tofauti kubwa sana na lengo la kupotosha na kudanganya kwa maandiko yote mawili yanayomtaja Kristo wakati Alfa na Omega yanatofauti inayomaanisha Bwana Mungu na Baba wa Kristo na hayamaanishi Kristo kabisa tangu mwanzo. Hii ina mengi ya kufanya na teolojia kama ilivyoendelezwa kutokana na msukumo wa wanafalsafa wa Kiyunani na waamini Utatu kama tuonavyo hapa. Lilikuwa ni jaribio la makusudi la kuipotosha asili ya kweli na nafasi aliyonayo Kristo kwenye uhusiano wake na Mungu wake na kumuinua yeye kwa kutumia imani na mfumo potofu wa Kiutatu.

 

Ufunuo 1:8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.

 

Aya za Ufunuo 1:17 na 2:8 havina maneno haya ya Alfa na Omega. Zinatumia maneno protos na eschatos ambayo yanaashiria wazo linguine linalotofautiana na maana ya Alfa na Omega.

Ufunuo 1:17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

 

Ufunuo 2:8 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika; Haya ndiyo aneneyo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai.

 

Maneno ya protos na eschatos yanabeba dhana iliyopo kwenye Ufunuo 3:14 ambapo Kristo anatajwa kuwa ni mwanzo au chanzo cha kuumba kwa Mungu akiwa ni prototokos au mzaliwa wa kwanza kama mtoto wa kiroho. Hatimaye alifanyika kuwa ni mzaliwa wa pekee wa Mungu aliyenenwa kwenye Yohana 1:18 (akiwa kama theos au elohim au monogene theos).

 

Utandaji huu umeongezweka. Atakaporudi Masihi hapa duniani na kwenye mchakato wa mwisho kwenye tukio la kushuka kwa Mji wa Mungu, tunamuona Masihi akiwa ni Alfa na Omega. Majinacheo haya hayakutumika kumuita yeye kimsingi, ambavyo ni nia na mkakati ulio nyuma ya tafsiri potofu na za uwongo.

 

Kwenye Ufunuo 22:13-16 tunaona majina mawili yakitokana na Masihi kuwa alifanyika kuwa nuru na nyota ya asubuhi.

Ufunuo 22:13-16 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. 14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya. 16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung'aa ya asubuhi.

 

Amepewa majina haya ya kivyeo kama mtu aliyepewa uweza kutoka kwa Mungu. Akiwa kama protos wa uumbaji anafanika kuwa mmoja na huyu Alfa. Akiwa kama eschatos wa uumbaji, anafanyika kuwa mmoja na Omega kama Mungu alivyo yote katika yote na ndani ya yote (Efe. 4:6).

 

Ufunuo 21:6 inaonyesha kiwango wakati tukio hili linapotokea. Kristo anafanyika kuwa Alfa na Omega na mwanzo na telos. Alianza kama mwanzo au wa kwanza kwenye uumbaji wa Mungu kwa mujibu wa Ufunuo 3:14. Hapa tuna wa kwanza aliye kama mwanzo na telos kama mwisho. Neno linalotokea ni la uwingi wa ujumla na lisilo la kijinsia la gegonan (sawa na ilivyo kwenye Ufunuo 16 na 17 na kwenye kamusi ya Marshall's Interlinear RSV). Imetafsiriwa kama imefanyika. Hata hivyo, ina maana sahihi, na Marshall anaitafsiri kama ni, imekwisha kuwa.

Ufunuo 21:6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.  

 

Imekwisha kuwa imetafsiriwa kuwa kama ilikwisha fanyika ili kulipa mashiko wazo la kwamba mchakato huu wa Mungu kufanyika kuwa yote katika yote na ndani ya yote uanzie kwa Kristo ambayo hakuwa hivyo hapo mwanzoni.

 

Kwa hiyo tunashughulika na wazo endelevu la utendaji wa Masihi na wateule. "Tazama, nayafanya yote kuwa mapya".

 

Mungu anafanyika kuwa yote katika yote. Hivyo basi, Mungu ni Omega au matokeo ya mwisho ya uumbaji wake mwenyewe. watafsiri wa Kitrinitarian walioitafsiri bilbia ya KJV kwa makusudi kabisa wameuficha ukweli huu na dhana yake nzima kwa wasomaji wake.

 

Kristo akiwa kama wa Kwanza kwenye mrengo wa Kitrinitarian

Malumbano nahoja zilizotajwa hapo juu zinachukuliwa kuwa ndiyo msimamo na kiini cha ujumbe lililopelekewa Kanisa la Walaodikia. Kwa hiyo, hoja hizi yapasa ziwe chimbuko au chanzo cha msingi wa makosa kwenye kanisa lile – au kosa kwa kueneza. Unabii unasema kwamba makosa yapo. Ni makosa la msingi la kanisa la Walaodikia na sababu ambayo Mungu anasema atalitapika kanisa la Laodikia kutoka kinwani mwake.

 

Kristo anasema kwamba yeye alikuwa ni mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Clement alimchukulia Mungu kuwa ni kama ni mwanzo pekee wa kweli akizuia wazo la kwamba Kristo awe ni mwanzo wa utendaji kazi wa Mungu. Hivyo ndivyo ilivyojiri. Watrinitarian hawapendi Kristo awe kwenye wajibu ule kwa kuwa Kristo ndiye aliye kwenye nafasi ile kwa kuwa ndipo Kristo alikuwa ndiye kazi ya Mungu zaidi ya Mungu mwenyewe kama ilivyo imani ya Wabinitarian.

 

Usipokuwa ni muumini wa imani ya Kibinitarian hutaweza kujenga wazo la Utrinitarian – na mbegu ya Utatu inarithiwa kwenye imani ya Ubinitarian. Hivyo basi, Ubinitarian una chembe ya mbegu ya maangamizi wake wenyewe. Kinachoendana mkono kwa mkono nayo ni mafundisho potofu kuhusu Uhai wa nafsi. Clement hata hivyo, alikuwa ni mwanateolojia ambaye alikuwa, kwa azima yoyote ile na malengo yote, ni Mnostiki. Aliamini fundisho hili la uhai wa nafsi na kwamba roho zinapaa kwa viwango au madaraja saba na kwamba zinakuwa zimetoka na hazishikamani tena na hali ya kuwa kwenye mwili na kuwa kwenye nosis (Lilla, p. 182). Hivyo, wateule walichukuliwa kuwa wanapitia kwenye mchakato huu wa kujiwezesha au kujimudu. Kanisa lolote, linapokuwa la Kitriitarian, litajikita kuyakumbatia mafundisho haya ya Roho kuwa hai. Hatimaye kabisa, itabidi kuwe na imani ya ulimwengu inayoamini fundisho hili la roho kuendelea kuishi. Mshuko wa ngazi au madaraja saba anaouongelea Clement ni imani ya Ushamanism kabisa. Inatokana na imani ya dini za Kibabeli na ikatoka na kuendelea hadi kwenye Steppes za Urusi kwa tukio la utawanyiko wa watu kulikotokea baada ya gharika kuu. Ilianzisha imani za Kishamanism wakati waumini wake walioishika wanakwenda kutoka kiwango kimoja hadi ya pili kwa kupitia hatua saba kwa ujumla. Zinaweza kuwa ni nyingi kiasi cha tisa hadi kumi na tatu. Kuna roho ya kimizimu au ya kipepo inayotawala (au mungu kama wanavyoita wenewe) kila moja yah atua hizo saba hadi utakapo panda hadi kufikia usawa wa juu zaidi.

 

Hiki ndicho alichokuwa anashauri Clement na ndivyo ilivyo kwa maana hasa ya mipando na dini za siri za Kiplatoniki ilivyo. Na kiki ndicho wanateolojia wa Kikapadokia walichokuwa wanadhania. Walikuwa wanaunga mkono mipando ya imani za siri ya madaraja saba. Miungu waliyoipana na iliyowajilia haikuwa ni huyu Mungu wa kweli. Waliokuwa ni wakimapepo. Na ndiyo imani hiyohiyo inayoendelea kwenye imani ya kibudha leo. Kwenye sherehe za kusimikwa au kuwekwa wakfu mtu za Kibudha za hapo kale kulikuwa na koni yenye ujazo sawia ndani yake, pamoja na yai kwenye levo moja; zote hizi zikiashiria maana ya kuwaita maroho au mizimu washuke kwa kupitia ngazi hizi ili wawaendee waumini wao. Yeyote Yule kwenye imani ya Kibudha analazimika kuwa anaaimi imani ya Kishamanism. Wanawaita mizimu waje wao na wawapagae. Utaratibu wote wa kupandisha mizimu unafanyizwa na nguvu za mapepo na kwa kuwaita au kuwapandisha hao mizimu. Ni roho nyingine na tofauti kabisa na Roho Mtakatifu. Na ndiyo maana ni muhimu kuelewa au kujua kabla hatujamsoma Roho Mtakatifu.

 

Tofauti ya vitu kati ya Wakristo, Waplatoni na Wanostiki kuhusu dhana ya uumbaji inahusu mianzo ni kwamba Wanostiki waliamini kwamba waanzilishi au archontes walikuwa kwa ujumla wao ni nguvu ovu waliokuwa chini ya uhakimu wa Jaldabaoth wa umbo duni au dhaifu la udongo wa duniani (soma kitabu kiitwacho Apochryphon of John 41:12-14 na gombo liitwalo codex II Krause-Labib, II. 4-5, p. 139; Lilla, p. 183 and fn. 5). Tofauti ya utendaji kazi umekuwa kwenye karne mbili za kwanza. Utambulisho wa neno au Logos ilifanywa kama mshirika wa pili wa Mungu. Clement analiona logos kama ni mshirika wa Mungu, na sio wa kwanza pamoja na hekima takatifu, wa kwanza kati ya viumbe walioumbwa na Mungu na mshauri wake (Lilla, p. 208). Mshauri wa Mungu alikuwa ni hekima kutokana na Mithali 8:22. Hii inatokana na hali ya kutoyajua majukumu ya Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alikuwa ni nguvu ya kwanza ya Mungu aliyoitumia Mungu wakati wa uumbaji. Roho Mtakatifu hakuja baada ya Kristo. Kimsingi anatoka kwa Mungu, akiwa ni nguvu au uweza wake. Ni kifaa ambacho kwacho Kristo na Malaika wote wanafungamanishwa na kuwa na ushirika na Mungu. Hoja hii ni ya muhimu sana, hivyo basi hebu isome ili kuielewa hoja za watu hawa.

 

Kwa hiyo, mjadala uliotuama karibu na falsafa unaotafuta kushindana na Maandiko Matakatifu ili kwamba viumbe wote walioumbwa walikuwa ni washirika au ousia wa Mungu. Washirika na ousia hawakuwa na majina sawa ya kuadibiwa. Ushirika huu unatokana na neno la Kistoiki; ousia ni neno la Kiplatoniki. Yote yanamaana na asili moja tu. Waamini Utatu wanatumia washirika kama wanaotokana na ousia moja. Kwa hiyo wanatumia majina mawili kumaanisha Mungu kuwa ni kama anajumuisha washirika watatu. Ni muhimu jukua kuwa watu hawa wanasema wakati wanapoyatumia maneno haya (soma jarida la Matumizi ya Neno Washirika (Na. 230) kwa ufafanuzi kamili wa maneno haya). Malaika ndio wanachukuliwa kuwa ni washirika wa Mungu kama walivyo mapepo pia. Hivyo Shetani angekuwa muovu kutoka mwanzo wa kuumbwa kwake kama ilivyoendelezwa hivi karibuni na wanazuoni kwenye Makanisa ya Mungu. Tumejionea tayari jinsi hilo lisivyo sahihi. Biblia inasema wazi sana kwamba Shetani alikuwa mkamilifu kutoka wakati alipoumbwa (Eze. 28:15).

 

Dhana iliyopo ni kwamba: Kama ni Mungu tu yupo ndani ya viumbe vyote ni washirika tu wa Mungu, kwa hiyo Shetani ndiye atakuwa mshirika ambaye hana uhalisia zaidi ya kuwa tu ni mwelekezaji wa mawazo ya Mungu. Ni sawa tu na ilivyo kuwa malaika pia ni wanaakisi taswira ya Mungu na hawana uhalisia wa uwepo wao zaidi ya kuwa ni washirika tu. Uwongo huu umeenea hadi kwenye uwepo wa kimaumbo kwa kupitia mwendelezo wa falsafa za Uplatoni mamboleo. Umeenea mbali zaidi ya Utrinitariani wa kihafidhina hadi kwenye Teolojia Mchakato iliyoendelezwa kutoka kwenye Uplatoni mamboleo. Umekuwa ni msingi wa mfumo wa ibada za nyakati za mwisho.

 

Utaratibu huu wa Teolojia Mchakato ulioendelezwa na Waplatoni mamboleo inaounda Utrinitarian utakuwa ndiyo mfumo, utakaoijumuisha imani ya Kibudha na dini hizi zote nyingine na kuijumisha kwenye imani na mfumo wa siku za mwisho. Inakubalika kwenye Teolojia Huria ya Washinto nay a Wahindu. Ni itikadi jumuishi na ni chombo cha uharibifu au cha kuliangamizia Kanisa Katoliki, na sio cha kulikengeushia. Ni chombo ambacho atakitumia Mnyama kumgeuka Mwanamke Kahaba na kumwangamiza. Kwa kweli sisi tunatazamia kuona dini ya nyakati za mwisho ikianzishwa. Dini hii inajipenyeza pia ili ianze hata kwenye Makanisa ya Mungu. Ni kutoka kwenye imani au mfumo huu ambapo yule Mtu wa Kuasi ataibukia. Imani hii na mfumo wake, utafanikiwa kuwadanganya yamkini hata walio wateule ikiwezekana.

 

Dhana na imani hii ni ya udanyanyifu na uwongo mtupu na imeingia kwenye Makanisa ya Mungu katia siku hizi za mwisho kama alivyosema Kristo. Kristo alitoa ufafanuzi kuonyesha kwamba alikuwa ni mwanzo au wa kwanza kwenye uumbaji wa Mungu. Clement alikuwa sahihi kusema kwamba Mungu alikuwa mwanzo halisi kwa maana kwamba aliumba kutokana na utashi wake na kwa mapenzi yake vitu vyote viliumbwa (Ufu. 4:11). Kwa hiyo, Mungu ndiye muumba ila Kristo alikuwa ni chombo tu cha kuumbia na alikuwa ni mwanzo (soma tena hapo juu).

 

Wazo la kwamba hekima mtakatifu wa kimungu ndiye mshauri wa Mungu na wa kwanza kati ya viumbe walioumbwa na Mungu ni, kwa mujibu wa Lilla, kwa tabia ya falsafa ya Wayahudi wenye asili ya  Alexandria ya siku za kabla ya Philo. Kwa hiyo Wayahudi wa Alexandria walielewa kwamba hekima alikuwa ndiye wa kwanza kati ya viumbe wote wa Mungu. Kwa hiyo anatangulia kutoka kwa Mungu, na Neno wa Mungu na kisha akaishi na kujumuika pamoja na Mungu, kwa hekima akiwa kama Roho Mtakatifu. Yeye ni yule Sophia aliyenenwa kwenye Mhubiri 1:4 na ni kiumbe wa kwanza kuumbwa aliyenenwa kwenye Mithali 8:22. Kitabu cha Hekima ya Sulemani 9:9 inaonyesha kuwa anamsaidia Mungu kwenye uumbaji. Kitabu cha Mwanzo kinamtaja kuwa ni Roho ya Mungu kwenye Mwanzo 1:2. Waandishi waliokuwa kipindi cha kabla ya Kristo walifafanua kimakosa kitu hiki ambacho ni uweza wa Mungu kuwa ni kiumbe na kosa hili limeendelea hadi siku hizi kama dhana kwamba Roho Mtakatifu ni nafsi au mtu. Huu ndiyo mwanzo wa upotofu r.

 

Kimsingi, Roho ni mwanzo wa uumbaji wa kwanza ya Mungu, kwa kuwa uzao wa Kristo na wa elohim wngine walifanya hii iwe na mashiko muhimu kwa hizi kuwa mahali pa kitendea kazi tu kwa uadilifu wake kwa Mungu ili kwamba kuweze kuwa na mwonekano halisi wa imani ya Mungu mmoja kama muunganiko mzima. Mungu ni kiini cha viumbe wote. Viumbe wote pamoja na Malaika ni mali yake na wanaungana naye kwa njia ya Roho Mtakatifu. Ni kwa kupitia huyo Roho ndipo asili ya Mungu na tabia zake zinawaambukia viumbe wote, wote wawili, yaani Kristo na wateule wengine waliobakia, na hatimaye wanadamu wote. Yeye ni kitendea kazi tu na usipoelewa mtiririko huo kwa kweli huwezi kuelewa kinachotokea kwa Roho Mtakatifu.. Inatokea kwa kuwa sheria ya Mungu inatokana na uwepo wa wema wa tabia ya Mungu. Kwa hiyo, hawezi kuwa wa Kibinitarian kwa kuwa ana kiini au asili halisi ya wema, na wema huo ni Mungu. Kristo alisema kwamba ni Mungu tu ndiye aliye mwema; kwanini unaniita mwema, ni Mungu tu ndiye aliye mwema kwa sababu ya ukweli wa asili yake ya kijadi ya wema usio na kifani. Hatuwezi kuwa na mfumo au imani ya kiditheist. system. Ukifikiri kwa kina, na kwa mashiko, kunatuambia kuwa hawezi kuwa hivyo. Torati au sheria ya Mungu inatokana na tabia ya Mungu inayosimama milele, kama alivyo Mungu mwenyewe habadiliki, akiwa ni mwema kabisa akiwa kama kiini cha wema wote.

q