Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[244]

 

 

Mwanzo 22, Imani ya Kiyahudi, Uislamu na Sadaka ya Isaka

(Toleo La 3.0 19980407-20000425-20110504)

 

Andiko la jarida hili linaelezea mabishano yaliyopo kuhusiana na sadaka iliyotolewa ya Isaka yaliyoendelezwa na Rabi E. Ben-Yehuda na pia imefanyiwa tathminiwa kwa kujibu sawa na ilivyoandikwa kwenye Biblia na Qur’an au Koran.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1998, 2000 Thomas McElwain, ed. Wade Cox)

(rev. 2011)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mwanzo 22, Imani ya Kiyahudi, Uislamu na Sadaka ya Isaka



Kwenye Taasisi ya Watafiti wa Ukristo wa Kiyahudi, Toleo la 1, la Novemba 1986, Rabi E. Ben-Yehuda alichapisha jarida lene kichwa cha habari Sadaka ya Isaka [The Sacrifice of Isaac].

 

Mwandishi ametoa dhumuni moja tu lililoelezewa kwa kuelezea jambo hili.akisema. “Mjibu au miitikio yote ya Kiyahudi yametokana kipindi kifupi kabla ya Wakristo kudai kwamba upotovu au makosa makubwa ya kitoaji dhabihu wa Yesu Kristo pale msalabani umeifanya kuonyesha umuhimu wa dhahiri kwa Wayahudi wote kukubaliana na jukumu hili la Masihi pamoja na hadhi yake ya kimbinguni. Ubatilishaji uliofuatia unajaribu kuonyesha kuwa Wayahudi walikuwa na nasibu kwenye historia yao muda mrefu kabla ya kuanza kuhesabu kipindi ch Mateso ambayo yalikuwa na matokeo sawa kwa mtazamo wa Wayahudi” (ukurasa 1). Ushawishi pekee ulioelezewa ni “kuja kwenye kuling’ang’ania au kulishikilia” jambo hili.

 

Kitendo cha kuondoka ni wazo la kwamba kuna udhaifu kwenye imani ya kiyahudi iwapo kama kusingekuwa na utoaji wa dhambihu kwa ajili ya dhambi ambayo kwayo Mungu huitumia kuwarehemia watu. “Kwa kuwa sadaka haitolewi tena kwenye imani ya Kiyahudi, ni wapi utakapotarajia tena kukutana na rehema za Mungu?” (ukurasa wa 2). Marabi wamekuta msingi uliachwa na kupungua wa neema mahali alipokuwa amefungiwa Isaka. “Kwenye liturjia, tunaelezea tena na tena kuhusu “kufungwa kamba kwa Isaka” kama sababu ya Mungu ili kusamehe kwa mara moja dhambi za wana waliotokana na uzao wa Isaka” (ukurasa wa 2).

 

Baada ya kujitambulisha kwao, rabi wlikuta ushahidi ufuatao wa kwmba Isaka alitolewa sadaka kweli kama ilivyoelezwa kwenye Mwanzo 22, na kisha hatimaye alifufuka kutoka kwa wafu. Inaleta mwaswali kwamba Mungu mwenye sifa ya kujua kila jambo lililopita, lililoko na lijalo angehitaji “kumjaribu” Ibrahimu. Alama aminika za N-S badala ya N-S-H ni neno lililotumika kwa kweli. Kwa hiyo tafsiri iliyotumiwa ya “kujaribu” ni kutolielewa andiko. Ingepaswa zaidi iwe “tangazo” au “mfano” badala ya “kujaribu” (ukurasa wa 2). Kwa nini kitendi hiki cha kufungwa tu kwa Isaka kiwe ni tukio lililoleta gumzo kubwa duniani kama liturjia ya kiyahudi inavyoonyesha? (ukurasa wa 2).

 

“Kitabu cha fafanuzi n fasiri cha Kiyahudi kinasema ‘Mungu mwenyewe aliiamuru iwepo hii sadaka ya Isaka – lakini kama Ibrahimu angemruhusu mataika yeyote ashindane na Muumba wake?’” “Ufafanuzi unaelezea kwamba, ‘malaika alisema akmwambia Ibrahimu na Ibrahimu akkataa kusimama, alisem kuwa Mungu amemuamuru, na ni yeye tu ndiye anayeweza kunizuia mimi” (ukurasa wa 2). Amri iliyotolewa ya kutomdhuru au kumchinja Isaka ilimaanisha kwamba alipaswa kutolewa sadaka yote mzima na pasipo kuumizwa (ukurasa wa 3). Maneno haya yanaweza kutafsiriwa kama ‘kondoo mwingine’ au ‘kondoo atafutwaye’ (ukurasa wa 3). Tahat bno linamaana ya chini ya mwanae kuliko maana ya mwanae (ukurasa wa 3). “Kitu hiki” na “hukumuachilia mtoto wako” kwenye Mwanzo 22:15-17 linaashiria kuwa Isaka alitolewa sadaka (ukurasa wa 3). Andiko linaarifu kwamba wote wawili, yaani Isaka walipanda kwenda, lakini ni Ibrahimu peke yake ndiye aliyerejea (ukurasa wa 3). Abraham alikwenda moja kwa moja huko Be’rsheba. Mwanzo 23:2 linaripoti kuwa Sara alifariki huko Kirjath-arba. Kwa hiyo Ibrahimu hakuonana uso kwa uso na Sara baada ya sadaka hii ya Isaka, na Sara alifariki kwa huzuni baada ya kusikia kuwa Isaka alikuwa amefariki (ukurasa wa 3).

 

Mwanzo 23:2 inaripoti kuwa Ibrahimu “alikuja” kuomboleza kifo cha Sara, lakini hakuna taarifa iliyofanywa kuhusu Isaka (ukurasa wa 3). Mwanzo 24 inaeleza kuhusu alivyompatia mke “Isaka”, ambavyo kwamba, Ibrahimu alikiinua kizazi kwenye jina la Isaka. Hakuna msisitizo kuhusu Isaka, lakini Rebeka anaulizwa kama angeafiki. Rebeka alistushwa kumkuta Isaka akiwa hai kwa hiyo alijiinamisha kwenye ngamia wake na kujifunika uso wake (ukurasa wa 3). Isaka akaja kutoka kwenye njia inayoelekea kisimani lahay roi’, kisima cha Uhai cha Yeye anionaye, ambalo ni jina la yeye kuwa amefufuka (ukurasa wa 4). Utajaji kuhusu ufufuko kwenye maombi ya Kiyahudi yaliyo katika siku hizi (ukurasa wa 4). Isaka alifarijiwa baada ya kifo cha mama yake kwa kumuoa kwake Rebeka miaka mitatu baada ya tukio hili, akionyesha kwamba alikuwa amejifunza tu jambo hili wakati alipofufuka (ukurasa wa 4). Matendo ya Kiyahudi ya Kidush Hashem yanatuama kwenye kifo na ufufuko wa Isaka (ukurasa wa 4).

 

Kila moja kati ya malumbano haya yamefafanuliwa kwa utaratibu.

 

Inashangaza na ni jambo la kujiuliza kwamba Mungu mwenye sifa za kujua kila kitu ahitaji “kumjaribu” Ibrahimu. Inadaiwa na wenye imani kali kuwa kwa kweli lilitumika neno N-S badala ya N-S-H. kwa hiyo, tafsiri ya neno “kujaribu” ni matokeo ya kutolielewa andiko. Ingekuwa kwa zaidi mna tu ya jinsi ya ”bango” au “mfano”, badala ya “jaribu” (ukurasa wa 2).

 

Viambishi hivi N-S-H imetumika takribam mara 36 kwenye Maandiko Matakatifu ya Kiebrania karibu wakati wote kwa namna iyiyo wazi inayomaanisha “kutia majaribuni”. Mifano yake ipo kama kwenye Kutoka 15:25; 1Samweli 17:39 na 1Wafalme 10:1. Mwanzo 22:1 haionekani kuondoka kwenye matumizi haya ya wazi. Hata hivyo, kama neno jaribu kwa kweli likiwa linamaanisha kuwa Mungu “alifanya mfano” wa Ibrahimu, zaidi ya kuwa “alimtia majaribuni”, matokeo yake hayawezi kuwa ni kama alionekana kabisa kuwa ni mtoto wa kambo tafsiri yoyote ijulikanayo ya kutolewa sadaka kwa Isaka. Haiashirii kuwa Isaka kwa hiyo alitolewa sadaka kwa kweli zaidi ya kuwa alifungwa tu madhabahuni.

 

Kwanini kitendo hiki cha kufungwa tu kwa Isaka kiwe ni tukio linalotiliwa umuhimu mkubwa kama liturjia ya Kiyahudi inavyotaka? (ukurasa wa 2).

 

Kama kuna maelezo endelevu kwenye ufungaji kamba wa Isaka kwenye machapisho ya Kiyahudi, hii haisaidii kwa kuzipa mashiko nukuu znisemazo there is a continual reference to the binding of Isakwamba uzoefu wa Isaka ulikuwa na maana kubwa kwenye imani ya Kiyahudi. Haifuatii kwamba Isaka kwamba kwa hakika Isaka alitolewa sadaka. Na hata hivyo haifuatiwi kuwa imani ya kwamba Isaka alitolewa sadaka haikuenea kabisa kwenye imani ya Kiyahudi. Maelezo ya kiliturjia yalinukuu maneno “kufungwa kamba”, na sio sadaka yenyewe. Na kwa hiyo inaeleza mambo yaliyo kinyume na mtazamo wa rabi huyu.

 

“Kitabu cha fafanuzi cha Wayahudi kinasema ‘Mungu mwenyewe ndiye aliamuru kutolewa sadaka kwa Isaka – lakini je, Ibrahimu angemruhusu malaika kupingana na Muumba wake?” “Kitabu hiki cha fafanuzi kinaendelea kufafanua, ‘malaika alimwambia Ibrahimu na Ibrahimu alikataa kusimamisha mchakato, akisema kuwa Mungu ameniamuru, ni yeye tu ndiye mwenye uwezo wa kunisimamisha mimi nisifanye hivi.’” (ukurasa wa 2).

 

Malumbano yametuam kwenye mgongano kati ya jumbe za Mungu, Elohim kwenye Mwanzo 22:1-2 na ule wa malaika wa Bwana ulio kwenye Mwanzo 22:11-12. Kinachoonekana ni kwamba Ibrahimu alipokea hayo yote kama amri mbili zinazopingana, zikitokea kutoka kwenye vyanzo viwili tofauti, na akaamua kumtii Mungu na Elohim wake kama ndiye mwenye mamlaka kuu zaidi kuliko malaika wa Bwana.

 

Tatizo lililopo kwene tafsiri hii ni kwamba hakuna kitangulizi kingine kwenye Maandiko Matakatifu ya Kiyahudi kuonesha kwamba malaika huyu wa Bwana alipingana na Mungu. Kwa kweli, malaika wa Bwana alikuwa ni mwakilishi wa karibu wa YHVH ambaye wakati mwingine hunena akiwa kama nafsi ya kwanza, Mimi YHVH, kama ilivyo kwenye Mwanzo 18 ambapo viumbe watakatifu hawakuw wanaitwa malaika kabisa, ila ni wanadamu na YHVH, waliokuwa wanatenda mambo na kuenenda kama wanadamu. Shauri hili lingeweza kufanyika, ni kama kwenye Mwanzo 18 na Mwanzo 22:12, ambako YHVH alinena maneno kumuelezea kama malaika wa Bwana (YHVH). Kwenye Mwanzo 19 watu hawahawa wanaendelea kuitwa malaika.

 

Mwanzo 22:12 inaweka makubaliano kati ya Mungu, Elohim na mlaika wa Bwana. Inasema kwa kuwa najua kwamba unamtii na mumcha sana Mungu. Kiidadi, andiko hili halisaidii kuonyesha mgongano kati ya Mungu na malaika wa Bwana (soma majarida ya Malaika wa YHVH (Na. 24); Wateule Kamas Elohim (Na. 1) na Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Kimwili (Na. 243)).

 

Amri iliyotolewa kuwa asimdhuru Isaka ilimaanisha kwamba alitakiwa atolewe sadaka akiwa mzima na asiumizwe (ukurasa wa 3).

 

Hoja hizi zinakubaliana na makubaliano yaliyopo kati ya malaika wa Bwana na Mungu. Maneno ya malaika kwa tafsiri hii hayakatazi kutolewa sadaka kwa Isaka, lakini zaidi ni kwamba yanakataza asimuumize Isaka anapomtoa sadaka. Umuhimu wa maneno kwa hiyo yangekuwa kwamba Isaka alitakiwa awe kwenye hali kamilifu wakati anapotolewa sadaka.

 

Kwa kuwa hoja hii inapingana na hoja ya tatu, tafsiri moja au nyingine yapasa ichaguliwe. Zote mbili hazikubaliki. Kama tutakubali uwezekano wote wa aina mbili wa nusu ya kwaza ya aya ya 12, nusu ya pili inayofuatia itaweka sawa kile ambacho hakipo. Kutokana na hoja ya nne, maana ya andiko yangeweza kusomeka hivi: “Usimchinje Isaka, kwa kuwa sadaka inatakiwa isiwe na waa: kwa hiyo sasa najua ya kuwa unamcha na kumtii sana Mungu, kwa kuwa hukumzuia mwana wako wa pekee, mwana wako wa pekee uliyempata kutoka kwangu.” Hakuna muunganiko wenye mashiko kati ya aya ya kwanza na nusu ya pili ya ayah ii. Kwa mujibu wa tafsiri za kimapokeo, maana au nia ya ayah ii ingesomeka hivi: “Usimdhuru Isaka au kumtoa sadaka kwenye mashindano: kwakuwa sasa naona kuwa unamcha na kumtii Mungu, kwa kuwa hukumzuilia mwana wako, mwanao wa pekee kunitolea mimi.” Kwenye jambo hili, andiko linaambatana au linaendana. Nusu ya kwanza inaingilia utoaji wa sadaka, na nusu ya pili inaashiria kwamba jaribio limeisha, kwa kuwa Ibrahimu hakumkatazia mwanae (sawa na jarida la Malaika na Sadaka ya Ibrahimu (Na. 71)).

 

Maneno yanaweza kutafsiriwa kama “kondoo mume mwingine” (ukurasa wa 3). Ishirio ni kwamba kondoo mume ni sadaka ya nyongeza kwenye sadaka ya Isaka, kwa kuwa ni “nyingine” au “baada”. Biblia ya KJV inatafsiri “nyuma yake” pamoja na matamshi ya maandiko mlalo, kuonyesha kuwa imeongezewa. Tafsiri hii ya KJV imeliacha neno lote, ikisema “pale kichakani alimuona kondoo mume aliyenasa kwenye pembe zake.”

 

Kwa mtazamo huu rabi yuko sahihi. Uelewa mwngi wa mashiko ya kiliturjia ya maneno haya ni kondoo mume mwingine; ni sahihi pia kwamba Isaka ni mtu pekee ambaye ngekuwa ni kondoo mume wa kwanza, kwa kuwa ilikwisha wekwa wazi kwamba hakuna mnyama mwingine aliyetolewa kwenye Mwanzo 22:7. Haifuati, hata hivyo, kwamba Isaka kwa hiyo alitoewa sadaka. Inafuatia tu kuwa alikuwa ni kondoo mume ndiye aliyetakiwa kutolewa sadaka. Kondoo aliyekamatwa kichakani alikuwa ni sadaka nyingine.

 

Neno Tahat bno maana yake ni “chini” ya mwanae kuliko kuwa “badala ya” mwanae (ukurasa wa 3).

 

Ni kweli kwamba neno tahat maana yake ni chini. Limetumika kama hivyo kwenye Mwanzo 1:7. Hata hivyo, neno hili linamaanisha pia badala ya, kama lilivyotumika kweye Mwanzo 2:21 “Bkisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,”. Ingekuwa hakuna maana kutafsiri chini kwa maelezo haya. Neno limetumika badala ya kwenye Mwanzo 4:25; 30:15; Mambo ya Walawi 14:42; 2Samweli 19:14. Imetumika kama chini kwenye Mwanzo 7:19; Kutoka 32:19; na inawezekana sana kwenye 1Nyakati 29:34. Limetumika kwa maana ya kwa ajili yake kwenye Kutoka 21:26. Limetumika kwa matumizi ya kwenye Zaburi 66:17. Limetumika wakati kwamba kwenye Isaya 60:15. Hatimaye kabisa, limejumuisha na sehemu nyingine nyingi kwa matumizi mengine kwenye kitabi cha Yeremia. Tofauti kubwa ya maana ya neno, na ukweli kwamba limetumika kwa maana haya ya chini kwenye uchache wa matukio ya kibiblia, inaelezewa kinyume na mtazamo na fikra ya rabi. Hatimaye, dhana ya “chini” haina mashiko yoyote kabisa. Kama kondoo huyu alitolewa sadaka chini ya Isaka, basi angewekwaje pale, kwa karidi kwamba Isaka alikuwa alikuwa amekwisha fungwa kamba tayari pale madhabahuni? Na kama huyu kondoo alikuwa ametolewa dhabihu chini ya Isaka, ndipo itaonekana kuwa huyu kondoo sio wa mbadala/mwingine/wa pili, bali ni wa kwanza. Tafsiri ya kwamba ni badala yake ni tafsiri pekee ambayo inafanya kuwe na mitizamo inayopingana.

 

“Kitu hiki” na “hukumzuia mwanao” kwenye Mwanzo 22:15-17 vinaashiria kwamba Isaka alitolewa sadaka (ukurasa wa 3).

 

Rabi anaelezea maelezo yaliyo kwenye Mwanzo 22:16 hukumzuilia mwanao kuonyesha kuwa Isaka alitolewa sadaka. Maelezo hayohayo yasemayo, loo chasakhtaa eth binkhaa, yanakutikana kwenye Mwanzo 22:12. Kwenye Mwanzo 22:12 Ibrahimu ni wazi kabisa kwamba alikuwa hajamtoa sadaka Isaka, na lakini alikuwa amekwishatimiza tayari kila kilichotakiwa asikizuilie. Kwa kuwa maelezo haya kwa wazi kabisa hayaelezi kuwa alichukua sadaka ya kuteketezwa kwenye Mwanzo 22:12, basi hakuwa sababu kudhania kuwa inaelezea kuwa ilichukuliwa na kuletwa sadaka ya kuteketezwa kwenye Mwanzo 22:16.

 

Andiko linaripoti tu kwamba wote wawili, Ibrahimu na Isaka walikwenda kwenye Mwanzo 22:8, lakini ni kwamba Ibrahimu tu ndiye alitudi nyumbani kwenye Mwanzo 22:19 (ukurasa wa 3).

 

Ripoti ya rabi kuhusu andiko ni ya hakika. Ukweli, hta hivyo, ni kwamba, wote wawili wametajwa kwenye safari yao ya kurudi nyumbani, haimaanishi kuwa Isaka hakurudi. Kwenye Mwanzo 12:14 inasema kuwa Abramu alipanda kwenda Misri. Haisemi kuwa Sarai alikwenda pamoja naye. Kwa kweli, aya zinazotangulia zinaonyesha kuwa Abramu aliogopa kumchukua mke wake kwendanaye Misri.  Kwa kutumia utaratibu wa rabi huyu wa kutafsiri, tungeweza kuona kutokana  na hili kwamba kwenye wakati wake wa mwisho waliamua kuwa asiende, badala ya kuongopa kuhusu uhusiano wao. Lakini licha ya ukweli kwamba andiko hili linasema tu kuwa Abramu alikwenda Misri, lo, na sasa tazama, aya hiyohiyo inaendelea kwa kusema “Wamisri wakamuona kuwa mwanamke uule alikuwa ni mzuri sana”. Kama isingekuwa ile aya ya kumi na saba, ambako jina la Sara limetajwa, tungehitimisha hat kwa kwa kutumia mtindo wa rabi wa kutafsiri, kwamba Abramu alikuwa na mke mwingine wa kujishikizia aliyekwenda nye Misri.

 

Mwanzo 22:19 inahitimisha kwamba walikwenda pamoj hadi Beer Sheba. Ingawaje wavulana wanatajwa pia, tuna haki zaidi ya kuhitimisha kwamba Isaka alifuatana nao kama tunavyohitimisha kwamba Sarai alishukia kwenda huko Misri kwenye Mwadzo 12.

 

Ibrahimu alikwenda moja kwa moja hadi Be’re Sheva. Mwanzo 23:2 inatuambia kuwa Sara alifariki akiwa huko Kirjath-arba. Kwa hiyo Ibrahimu asingeweza kumuona Sara baada ya kumtoa dhabihu Isaka, na alikufa kwa huzuni na kihoro aliposikia kuwa Isaka ameuliwa (ukurasa wa 3).

 

Rabi huyu anadhani kuwa Ibrahimu alikwenda Beer Sheba badala ya kurudi kwa Sana. Lakini Mwanzo 21:33, ni aya mbili tu kabla ya ile amri ngumu iliyotolewa ya kumtoa sadaka Isaka, aliyombiwa Ibrahimu alipokuwa bado yungali aliishi huko Beer Sheba. Ingawa andiko halisemi hivyo, isingeweza kwa kiasi kikubwa kudhania kuwa mke wake Sara alikuwa anaishi kule na yeye. Mwanzo 21:34 inaashiria kuwa Ibrahimu aliishi huko Beer Sheba kwa kipindi kirefu. neno hili ‘siku nyingi’ halina mkanunisho kama ulivyo kwenye lugha ya Kiingereza la majuma machache tu. Ni sawasawa na maelezo yasemavyo kwenye Zaburi 23:6, ilitafsiri kwa ilivyo kwenye zote mbili, yaani biblia za KJV na NIV kama milele. Kuna kikomo kwenye maelekezo yaliyo kwenye Mwanzo 22:1, kwa hiyo inawezekana kudhania kwamba Ibrahimu alikuwa anaishi kwenye kipindi cha sehemu zilizojulikan. Lakini ukweli kuwa Mwanzo 22:19 inasema kuwa alikwenda Beer Sheba inadhaniwa kwa kiwasi kikubwa alianza nje kutoka pale, na kwamba Sara alikuwa anamngojea pale, isipokuwa kwa kweli alikuwa anamngojea akiwa na vijana wa kiume. Andiko halimtaji tu Sara kabisa, na udadisi na mtazamo wa rabi huyu, kama tutakavyojione, kuwa ingemaanisha kabisa kuwa alikuwa amekwisha kufa, na kufufuka na kuf tena kwenye Mwanzo 23.

 

Njia bora ya kulielewa andiko ni kudhania kwamba Ibrahimu na Sara walikuwa wanaishi huko Beer Sheba kwa karibu kipindi cha kufungwa kwa Mwanzo 22:19. Kuna kikomo kingine kwenye maelezo ya Mwanzo 22:20, ambapo panaendelea hadi mwanzoni mwa Mwanzo 23. Kwa hiyo, hakuna sababu ya kimaandiko ya kudhania kuwa Ibrahimu alikuwa anamkwepa Sara.

 

Mwanzo 23:2 inaripoti kuwa Ibrahimu “alikuja” kumuombolezea Sara, lakini hakuna kitu kinachoelezea kuhusu Isaka (ukurasa wa 3).

 

Rabi huyu anadhani kwamba Isaka inawezekana kabisa alikuwa amekwisha kufa kwa kuwa haelezewi kaisa kuwa alikuwepo kwenye mazishi ya mama yake Sara. Tena hitimisho kama hilo kutokana na kile ambacho andiko halisemi hakithibitiki, kama tulivyokwisha kujionea tayari. Ni wazi kwamba Sara alishuka kwenda Misri, ingawaje andiko linasema tu kuwa ni Ibrahimu ndiye aliyeshuka kwenda huko. Ni wazi sana kwamba Sara alikuwa yungali hai bado kipindi hiki kilichoelezewa kwenye Mwanzo 22, ingawaje halisemi kuwa alikuwepo kwenye shughuli hii muhimu iliyo kwenye kifungu hiki cha kutolewa sadaka kwa mwanawe Isaaka. Ni wazi pia kwamba kutoka kwene andiko kwamba Isaka alikuwa yu mzima wakati alipofariki mama yake. Alikuwa angali hai bado kwenye Mwanzo 22:12 na Mwanzo 24:6.

 

Mwanzo 24 inaelezea kuhusu alivyopewa mke “Isaka”, ili kwamba Ibrahimu ajipatie uzao kutokana na jina la Isaka. Hakukuwa na la kumuuliza Isaka, ila Rebeka aliulizwa kama anakubaliana. Rebeka alishangazwa kukuta kuwa Isaka alikuwa mzima, ndipo alijiinamisha juu ya ngamia wake na kujifunika uso wake (ukurasa wa 3).

 

Wazo la kwanza la huyu rabi ni kwamba Ibrahimu alimuokoa Isaka, ambaye alikuwa amekufa, kwa kuipanda tena mbegu kwa kumpa Isaka mke. Hoja hii imekosa mashiko kwa ukweli kwamba kwenye Mwanzo 24:6 Ibrahimu anaamuru watumishi wake wasimchukue mtoto wake na kumrudisha kwenye nchi ya uzaliwa wake. Maana ya tendo hili iko wazi sana kwamba Isaka alikuwa mzima na kwamba Yule mke alikuwa ni kwa ajili yake mwenyewe kabisa.

 

Sababu y pili ya huyu rabi ni kwamba kwakuwa haoinyeshi kuwa Isaka alishauriwa au kushirikishwa, wakati mawazo na ushauri wa Rebeka unaonekana ulifanyika kwa karibu sana. Kwa hiyo anaamini kuwa Isaka alikuwa amekwisha kufa. Hata hivyo, hakuna sababu ya kuelezea kuhusu ushirikishwaji wa Isaka, kwa kadiri tunavyoona ni salama zaidi kudhania kuwa akipofikia umri wa utu uzima wa miaka arobaini alikuwa yu tayari sana kuoa. Ushirikishwaji wake unatakiwa uelezwe tu kwa mambo yaliyo kinyume. Kuulizwa kiukaribu kwa mawazo na ushauri wa Rebeka hakupingani na kitendo cha maandalizi ya ndoa au kwa utaratibu wa viwango vya ufungaji ndoa wa eneo la Mashariki ya Kati. Kudhania kuwa ni kinyume ni tabia tu ya ubaguzi wa Kimagharibi.

 

Sababu ya tatu ya huyu rabi ni kuwa kitendo cha  Rebeka cha kuinamia kwenye ngamia na kujifunika shela kinaashiria mshangao wake kumuona Isaka amefufuka. Mwanzo 24:64 inasema kuwa alishuka kutoka mgongoni mwa ngamia. Shina la neno hili ni N-P-L ambalo kwa kweli ni lilitumika kwa kawaida likimaanisha kushuka chini kutoka mlimani au kutoka kwenye gari, hata hivyo. Limetumika sana kama hivyo kwenye 2Wafalme 5:21 pamoja na kwenye Mwanzo 24:64. Tafsiri ya huyu rabi huenda rni wa maana ya kiliturjia ambao sio wa lazima. Kitendo cha mwanamke kushuka kutoka mgongoni mwa ngamia, ambapo ni juu sana kuliko mgongo wa farasi, kungelazimu zaidi sana kuliko kumsaidia tu kumvua shela yake. Kwenye maeneo ya nchi za Mashariki ya Kati leo bado kuna utamaduni huu wa mwanamke kushuka kutoka kutoka mlimani juu kama atakutana na mwanaume anamjongelea akija kwake barabarani. Hakuna mashiko yoyote kuamini kuwa Rebeka alifanya hivyo kwa ajili ya kushangaa. Katika nchi ile, tabia yake ile ilikuwa ni ya kawaida, ambayo inaelezea au kuonyesha kinyume sana na matokeo ya msituko au mshangao.

 

Isaka alitokea kwenye njia ya kisima cha lahay roi’, kisima ch Uzima way eye anionaye, ambalo ni neno linaloashiria kuwa alikuwa amefufuka (ukurasa wa 4).

 

Rabi alitafsiri kitendo cha Isaka kuja akitokea kwenye njia ile ya kisima cha lahay roi’ kama ushahidi wa kuwa yeye alikuwa amefufuka. Hata hivyo, maneno haya hayana maana hii ya kiulinganisho kwenye maandiko haya. Yanaelezea kuwa ni kisima tu cha kawaida cha maji ambacho kiliipewa jina hilo na Hajiri kwenye Mwanzo 16:13-14. Maana isemayo Mungu aonaye imetokana na matatizo aliyokutananayo Hajiri, na sio Isaka. Halina maana ndogo kwa kumaanisha kufufuka kwa Isaka.

 

Kutajwa kwa ufufuo kwene maombi ya Wayahudi bado kunaendelea hadi sasa (ukurasa wa 4).

 

Rabi huyu anahitimisha kuwa kutajwa kwake kwenye maombi ya Wayahudi wakimuombapo Mungu awafufue wafu, kwa kuwa yalikuwa yanafundishwa hata leo, kwa namna yoyote inavyomaanisha kutokana na hiyo, kwa kuwa hakuna kitenzi kiashiriacho tendo kufanyika kila siku kwenye lugha ya Kiebrania, kunamaanisha kuwa Mungu bado yupo hata sasa akiwafufua wafu. Kwa kuwa Mungu bado yupo hata sasa akiwa ni mfufuaji wa wafu, basi angeweza pia kumfufua Isaka. Kama tunakubaliana na hoja za rabi, kwamba Mungu tayari yupo hata sasa akiwa ni mfufua watu kutoka kwa wafu, basi haiashirii kuwa Isaka ni miongoni mwa hao waliofufuliwa. Kuna jinsi inavyotejwa kwenye biblia kwa watu wengine waliowahi kufufuliwa kwa wafu, kama lile tukio la mtoto wa mjane wakati wa Eliya (1Wafalme 17:17 nk.), na mtoto wa mwanamke Mshunami wakati wa Elisha (2Wafalme 4:8ff.).

 

Ingawa maombi ya Wayahudi yanaashiria kitu fulani muhimu kwene maisha ya Wayahudi, ambalo ndilo lilikwa kusudi la mafundisho ya rabi sehemu ya kwanza, hawawezi kutoa ushahidi wa kwamba andiko hili la Mwanzo linaripoti au haliripoti kwa kweli dhana hii ya kufufuka kwake au kama haisaidii. Isaka alifarijika baada ya kifo cha mama yake kutokana na kuoa kwake mwanamke huyu Rebeka miaka mitatu baada ya tukio, ikionyesha kuwa alikuwa amejifunza kwa uhakika jambi hili wakati akiwa amefufuka (uurasa wa 4).

 

Haifuati. Inawezekana kabisa kwamba yawezekana kuwa Isaka alimuombolezea mama yake kwa kipindi cha takriban miaka mitatu, kwa kiasi kwamba ndoa yake ilimfariji sana. Hakuna ushahidi wa kifo cha Isaka na kufufuka kwake hapa.

 

Imani ya Wayahudi ya Kidush Hashem yanatokana na kifo na kufufuka kwa Isaka (ukurasa wa 4).

 

Ingawa imani kwenye kifo na kufufuka kwa Isaka inaweza kuwa na athari ya ushawishi kwa baadhi ya Wayahudi ili kuwafanya wawe waaminifu kwenye imani yao ya kuifia dini, imani ile ni ya muhimu sana kwenye uaminifu kama huo. Uamifu kama huo sio ushahidi ama kwenye imani ya kifo.na ufufuo wa Isaka au kwa ukweli wa tukio lenyewe.

 

Kwa hoja hii inawezekana kufanya tathmini ya jumla ya somo. Tatizo la kwanza ni nia ya rabi na hoja zake. Nia yake inakuwa imepotoshwa, kwa hiyo matokeo yake hayawezi kusaidia ila imekuwa imepotoshwa. Nia sahihi pekee kwa kujisomea andiko ni kujitafuti ukweli, ukweli wa kile kilichomaanishwa hapo mwanzoni na maandiko na jinsi inavyoweza kusaidia kwenye imani ya mtu binafsi na uzoefu wake. Rabi huyu hapendi kutafuta ukweli, lakini kwa maneno yake mwenyewe, anapendezwa na hamu ya kupata utenzi wa Wakristo kwenye imani ya \Kiyahudi. Anataka kukuta mbadala wa bandia wa kifo cha Yesu mtini kama njia ya neema ya mbinguni. Kwa nia hii moyoni, anakomelea kwenye sadaka ya Isaka.

 

Hoja yake imebakia bila kuonekana. Hoja ni kwamba kumuamini mtu aliyeuawa shahidi au kufufuka kutafanya kwa yenyewe tu isiwekane kwa Mungu kusamehe dhambi. Ingawa hoja hii inakubalika na imani za Kikristo, mwanazuoni wa Kiyahudi anawajibu wa kuonyesha uwepo wake. Rabi hafanyi juhusi yoyote ya kufnya hivyo. Anakubaliana tu na mtazamo huu wa Wakristo na kuanzia kutoka hapa. Huu ni mwendelezo au mtiririko uliomaanisha sana wa kimethodolojia.

 

Kuna aina kadhaa za udhaifu kwenye hoja hizi za rabi. Kwanza kabisa, kuna makosa yakimkanganyiko. Ni kana kwamba utendaji wa kompyuta imepokonya watafiti wa msingi wa uwezo wake wa kutofautisha lugha mbalimbali. Kuchagua maana moja y neno na kuitenda mbele ya baraza kunaanzisha utendaji kazi wa juujuu wa kiufundi na ukosefu wa uadilifu wa kitathimini ambao ungeweza kutofikirika mbele ya kizazi cha watafsiri wa mambo ya kiufundi. Methodolojia kama hiyo inakutikana kwenye njia ya rabi ya jinsi anavyolitumia maneno ya tahat (badala ya) na tippol (alishuka chini). Matumizi ya maneno haya ni makosa mkubwa ya kitafsiri.

 

Kuna matatizo mengine ya kilugha pia. Tafsiri ya kialama haikubaliki wakati andiko likiwa wazi na maana isiyohitaji kutafsiriwa vingine. Rabi anafanya makosa haya katika kushughulikia vyema naelezo au usemi walahay roi’. Kosa linguine la kilugha ni kutoa maelezo yaleyale kwenye dhana yenye maana tofauti, isipokuwa ile dhana inayohitajika na muhimu. Rabi alifanya hivyo kwa maelezo kwamba hukumzuilia mwanao, yanayojitokeza mara mbili kwenye kifungu kinachojadiliwa. Hatimaye, rabi anaelezea mjadala wa kilugha ambao haufanani na nasaha kama walivyokuwa navyo, kama kwenye utendaji kazi wa huduma ya kirabi N-S-H.

 

Kuna makosa ya kimashiko pia. Rabi anatoa tafsiri inayopimgana ya maana iliyo kwenye Mwanzo 22:12 kama ushahidi kwa tafsiri hiyohiyo ya sadaka ya Isaka. Hii haiwezekani kabisa na inadhoofisha sana hoja yake. Rabi anafanya hitimisho lisilo na mashiko na kueleweka kutoka na vitu vilivyoachwa bila kuezewa vizuri kwenye maandiko: kwamba Isaka hakurudi pamoja na Ibrahimu baada ya utoaji ule wa sadaka, kwamba Isaka hakuhudhuria mazishi ya mama yake, na kwamba Isaka hakuhusishwa kwenye mipango ya ndoa yake. Hoja zilizotuama kwenye kitu kisichoeleweka hayawezi kustahili zaidi ya kuwa hakuna. Mwishoni kabisa, rabi anafanya makosa kimashiko kwa kufana hitimisho kutoka kwenye maelezo yaliyo kwenye andiko. Anafanya hitimisho la kuw Sara alikuwa huko Kiriath-arba wakati Ibrahimu alipokuwa huko Beer-Sheba kwa msingi wa ukweli kwamba alifariki huko. Data zilizo kwenye andiko hazitoshelezi kufanya hitimisho lile.

 

Rabi anafanya hitimisho kutumia makosa ya kidesturi na kwa mawazo ya kisaikolojia. Anakosea kwa kufanya udadisi au upelelezi kuhusu hisia ya mwanamke aliyependa wala kutamani mambo ya kuolewa au ndoa iliyoandaliwa. Anakosea kwa kudhania kuwa Isaka hakumuombolezea mama yake kwa kipindi stahiki cha miaka mitatu.

 

Kuna yapata dosari kubwa kwenye mafundisho ya rabi. La kwanza ni linalotokana na kutegemea tofauti iliyopo kati ya Elohimu, Mungu na malaika wa Bwana. Hakuna kinachotangulia kati yake kutok kwenye Maandiko Matakatifu, la pili halihitajiki, na inaleta mambo yenye matatizo ya kiteolojia ambayo kwayo rabi anayajua na kuyataja. Wazo la mgongano uliopo kati ya Elohimu Mungu na malaika wa Bwana haikubaliki kabisa kama msingi wa andiko la biblia.

 

Kosa kubwa la pili dosari au makosa makubwa ni kushindwa kwa rabi kuyatilia maanani maandiko haya, ambayo yanapinga kwa wazi kabisa juu ya kufa n kufufuka kwa Isaka. Miongoni mwa hayo kwenye Mwanzo 24:6, panaposema kuwa Isaka alikuwa hai wakati ule kiasi kwamba kwa mujibu wa dhana alikuwa hajafufuka bado.

 

Somo hili linakanganya pia kutokana na kushindwa kwake kuyatilia maanani maandiko yaliyo kwenye kifungu, ambayo kwa kweli yanaleta au kusababisha matatizo. Mahali panapoonekana wazi kuhusu jamho hili ni kwenye Mwanzo 22:2 na Mwanzo 22:16, ambapo Isaka anaitwa kuwa ni mwana wa pekee wa Ibrahimu. Hakukuwa na wakati wowote mwingine ambao Isaka aliitwa kuwa ni mwana pekee wa Ibrahimu. Hili ni kosa mojawapo la kihistoria ambalo linahitaji kutilia maanani sana, na twaweza kumshukuru Rabi Ben-Yehuda kwa kuanzisha mjadala huu.

 

Sehemu kubwa ya masomo haya yatatathimini au kufafanua maandiko ya biblia, lakini kwa nia ya kufafanua kile kinachoonekana kutoendelea ndani yake. Wazo la msingi ni kwamba tafsiri ya Masoretic Text ya Biblia ya Kiebrania, hasa kama ilivyo kwenye Mwanzo 22 imehusika, imeimarika na inajitosheleza sana kikamilifu kwa kuwiana yenyewe kwa yenyewe.

 

Kwenye Mwanzo 22:2 (na kwenye Mwanzo 22:16), Isaka anaitwa mtoto wa pekee wa Ibrahimu. Hii haijitoshelezi na ripoti iliyo kwenye Maandiko ya Masoretic katik Mwanzo 16:15 ambapo inasema kuwa Hajiri alimzalia Abramu mtoto wakiume aitwaye Ishimaeli. Kwenye Mwanzo 17:17-19, ni dhahiri sana kwamba Ishimaeli alikuwa yupo na mzima kabla ya kuzaliwa kw Isaka. Mwanzo 21:2-3 inatumbia kuhusu kuzaliwa kwa Isaka baada ya kutahiriwa kwa Ishimaeli akiwa na umri wa miaka kumi na tatu (Mwanzo 17:25). Mwisho kabisa, Mwanzo 25:9 inasema kuwa Ishimaeli alikuwepo na alikuwa mzima bada ya tukio lililo kwenye Mwanzo 22. Isaka kwa hiyo hakuwepo kwa mujibu wa andiko lisemalo mwana wa pekee Ibrahimu wakati wa tukio hili kwenye Mwanzo 22 au kipindi kingine chochote kilichopita kwao.

 

Kuna matatizo mengine kwenye habari iliyo sambamba na kilichoandikwa kwenye andiko hili. Imani ya Kiyahudi kwa ujumla inaitafsiri habari hii kuwa ni kama ufunuo kwa Ibrahimu tu kwakuwa Mungu haukubali wala kuipokea sadka ya mwanadamu. Wakristo wanaitafrisi hadithi hii kiujumla wakisisitiza somo la utiifu. Kwahiyo Wakristo wanakabiliwa na mgano wa kiteolojia kuhusu amri hii ya kumtoa sadaka mtoto huyu kama sadaka ya kuteketezwa. Amri kama hii inapingana na amri iliyo kwenye Kutoka 20:13, Usiue. Ingawa wanateolojia wanaweza kuleta ufumbuzi wa jambo hili kwa kiasi fulani kwenye mawazo yao na mitizamo yao wenyewe, Wakristo wengi wanaachwa kwenye mshngao au njia panda. Hawawezi kuelewa jinsi Mungu anavyoweza kumuamuru mtu yeyote kwa kwli amuue mtoto wake mwenyewe.

 

Kama tutaielewa hadithi hii kama ilivyo kwa ujumla – kwamba ni kweli kuwa Mungu alimuamuru Ibrahimu amuue mwanae wa pekee – kisha kuna matatizo fulani ya kimaelezo kwenye hadithi hii kama yanavyoonekana kwenye Biblia. Mazungumzo yaliyo kwenye Mwanzo 22:7-8 hayakithi haja kwenye sababu ya ya tukio ambalo kwamba Ibrahimu alikusudia kbisa kumuua Isaka. Isaka akauliza ni wapi alipo mwanakondoo, kana kwamba mwanakondoo ndiye anayekwenda kutolew sadaka na sio Isaka. Zaidi ya yote, hkuna ushahidi unaofuatia wa kwamba Ibrahimu alimuarifu Isaka baadae kuhusu hali halisi ya jinsi sadaka itakavyokuwa, halafu Isak akahiyari na kujua kuwa ni mshiriki wakati wote huu.

 

Kile ambacho Biblia inakielezea ni tukio ambalo kwalo baba anamchukua mwanae, akaenda mahala pasipojulikana wakiwa kama kikundi cha wanaume watupu lililoachwa kwenye zamu, akijitenga mwenyewe mbali na mwanae, akitoa sadaka ya dhihaka au mfano ya mwanae, kisha akamtoa mnyam sadaka kama sadaka ya kuteketezwa, na akarudi nyumbani peke yake bila mtoto.

 

Kipindi hiki chote ch mchakato huu, Isaka bado anaitwa mwana wa pekee. Na haitwi mahala pengine popote kwenye miito yote ya kitabu cha Mwanzo. Ukweli huu unaendana na tukio hili. Tukio hili linajumuisha matendo ya utoaji wa sadaka na mfuatano wa maelezo au maswali na majibu. Kifungu hiki kinajionyesha chenyewe kama kipo, licha ya hitilafu au tofauti ya baadhi ya hotuba au semi. Andiko linapuuzia matatizo ya kiteolojia ya majiribu kutoka juu mbinguni na sadaka ya mwanadamu, kana kwamba hii siyo jambo la muhimu.

 

Kwa jinsi hii tunakuwa tumezipunguza au kupingana na taarifa za biblia. Ni muhimu kuangalia ufafanuzi wa mambo yaliyo nje ya andiko lenyewe. Kuna ukweli kadhaa wa kuuangalia. Ikiwezekana, kutaweza kukuta mifano ya sadaka ya mzaha ya vijana na baba zao au mamlaka nyingine zilizofuatia na sadaka iliyochuua mbadala ya mnyma. Matukio haya ya utoaji wa sadaka yalijumuisha mlolongo wa hotuba au semi, ambayo yangepuuzia au kukataza hali yenyewe halisi.

 

Mwaka 1909, A. van Gennep alitambulisha kwa wazi aina hii ya jambo kwenye kitabu chake cha Les rites de passage. Sheria au kanuni za kifungu cha namna hii inafanyika kwa vijana wa umri fulani, ingawa kuna kanuni kama hizohizo kwenye baadhi ya jamii zinazowahusu wasichana pia. Sheria hizi mara zote zimehusiana na jinsi ya kutoa hotuba au semi kwenye kile kinachoitwa kuwa ni mfumo shinikizo. Kuna igizo la kumuua kijana, kutimilizia sadaka ya mnyama badala yake, na mfano wa kufufuka wa kijana. Mara nyingi ni kipindi cha kujitenga kutoka kwenye jinsia tofauti. Mwishoni mwa sheria hii, kijna anakuwa amepita umri wa utoto na kuingia umri wa utu uzima, na anaweza kuoa au kubeba majukumu mengine ya kiutu uzima au mwenendo wa utu uzima, au anakuwa amepita kutoka kwenye umri mmoja hadi mwingine kwenye maisha yake ya utu uzima.

 

Ingawa lirutjia au sheria za kidini za kanuni au sheria za kifungu kwa kawaida inaonekana kuwa ni jamii isiyojua mabo ya uandishi, kuna mifano ya maandiko yenye miundo shinikivu kwenye maandiko mbalimbali ya madara ya kidini ya ulimwengu. Moja ya hizi ni sehemu ya kwanza ya Kathopanishad, moja ya Vedic Upanishads inayojulikana sana kwenye Maandiko muhimu kwenye daraja za Kihindu. Kuna mwendelezo fulani kwa muundo shinikizo kwenye maandiko ya dini za kale kutoka ulimwenguni kote, na hakuna sababu yoyote kabisa ya kwa nini tusiweze kuukuta mmoja kwenye Biblia. Ni wazi kuwa hadithi ya kutolewa sadaka kwa Isaka inakuwa na mambo yote muhimu ya namna hiyo sheria na kanuni ya utoaji dhabihu.

 

Kama hadithi inaelezea kanuni au sheria ya kifungu cha liturjia, hotuba itafanywa kuwa ni hotuba inayohusiana na taratibu zake. Kwa kweli zilitolewa kama zilitokea kwa kipindi chake maalumu na kwa mahala maalumu na mtu maalumu aliyehusishwa, ila yawapasa wajue kuwa zikitokea kwa mumhusu kila kijana wa kiume kwenye utamaduni uliotolewa wakati ilipohitajika jinsi iliyo muafaka.

 

Sheria na kanuni hizi zinaanzia na mchocheo wa Mungu, aliyemuita Ibrahimu kwenye Mwanzo 22:1. Jibu la Mungu kwenye aya ya 2 ni pia limefundishwa kwenye vifungu vya tafsiri ya kiibada. Hii inafafanua na kuelezea sababu ya kwa nini hapa Isaka amexkuwa kila mara anaitwa mtoto wa pekee. Ni sehemu ya taratibu za kiibada. Inawezekana kuwa wakfu ni inatajwa kwa mzaliwa wa kwanza wa kila mwanamke. Kitendo cha kumuweka alama mzaliwa wa kwanza ni jambo endelevu kwa sehemu nyingi za Biblia. Kitendo cha kumuweka wakfu mzaliwa wa kwanza wa kila mwanamke kumeelezewa kwa mara ya kwanza kwenye Kutoka 13 na kwenye vifungu vingine vilivyofuatia. Maelezo haya yangechukuliwa kwa ujumla kuwa ya kweli, na yangeishia tu kwenye hali ya ndoa ya matala, kama ilivyo kwa habari ya Ibrahimu. Bado hata katika hali hii ya ndoa ya matala, maneno hayahaya ya kiutaratibu wa kiibada yangeweza kutumika kwenye tukio la utoaji wa sadaka, kwa kadiri kwamba liturjia ya kimapokeo au maneno muafaka kwa ajili ya sadaka yangeweza kutumika wakati wote

 

Tabia na pambanuzi za kawida za kanuni za vifungu vinavyoshabihiana kwenye hadithi iliyo kwenye kitabu cha Mwanzo kama hii. Makundi yote ya wanaume yaondoke kwa ajili ya safari ngumu na ndefu ya siku tatu (Mwanzo 22:3,4). Wale ambao hawashiriki kikamilifu wanaachwa wasubiri na kulinda (Mwanzo 22:5). Sheria nyingi za vifungu zinajumuisha vikorokoro au zana kama hizi za kuni ya kutumia kwenye ibada hii ya kutolea sadaka, moto, na zana au silaha (Mwanzo 22:6). Kanuni nyingi za vifungu zinajumuisha maandiko yaliyowekewa kiwango cha hotuba na majibu kati ya mtu aliyechukua cheo cha mwingine na uimaririsho (Mwanzo 22:7,8). Sheria nyingi za vifungu zinajumuisha maandalizi ya dhabihu na sadaka kivuli iliyokusudiwa ambayo kwayo yeye amefungwa kamba au kufungiwa kwenye kifungo cha gizani (Mwanzo 22:9-10). Sheria nyingi za vifungu hujumuisha sadaka mbadala ambayo inakutikana kwenye mlolongo wa maelezo au hotuba, iliyofanyika kuwa ni mbadala wa kilichodhamiriwa na dhabihu (Mwanzo 22:11-13). Sheria nyingi za vifungu hujumuisha na kutaja majina ya maeneo au itendo cha kutaja yaliyokusudiwa au mara chache sana, kupewa cheo (Mwanzo 22:14). Nyingi ya hizi sheria zinazowekwa au kuingizwa zinaishia na kuwabariki au kuzibariki juhudi, kuelekezea utu uzima au wadhifa na heshima stahiki (Mwanzo 22:15-18). Sheria nyingine za vifungu huishia na kumtafuta kijana anayetafuta nyumba na njia zake mwenyewe, kuonyesha faida yake ya wadhifa wake mpya kabisa (Mwanzo 22:19).

 

Andiko lililo kwenye Mwanzo 22 limetathiminiwa kutoka kwenye mtazamo wa muundo uliorasimishwa kama sheria ya kifungu. Hakuna isiyokuwepo au kudumu miongoni mwa dhana na wazo hili la kitafsiri ambapo kunapatikana kwenye maandiko ya biblia.

 

Tafsiri nyingine ya andiko hili kama kanuni ya andiko inafanya namna ya kuendelea kwa kiwango chu kutoimarika mbele kwa Mwanzo 22. Tofauti au mkinzano wa hotuba, pamoja na kuendelea kufifia mng’aro au mvuto wa kumuita Isaka kuwa ni mwana pekee wa Ibrahimu, kunaonekana kuwa yanaendelea kuendelevu wote kabisa na sheria ya kifungu. Amrisho lenye kukinzana la kiteolojia imepeleke utoaji wa sadaka au dhabihu ya mwanadamu kutokomea. Jaribu la Mungu limepunguzwa kwa umhimu wa kumkomboa mzaliwa wa kwanza wa kila mwanamke, au kuelezea kwamba Ibrahimu ni mfano kwa vizazi vijavyo.

 

Swali laweza kujitokeza kama tunayo haki kulitafsiri andiko kuwa mfumo shirikishi kwa kuwa hakuna hakuna kitu kutoka kwenye maandiko kinachosema kuwa ni hivyo. Mtu anaweza moja kubwa dhidi ya tafsiri nyingine. Kulitafsiri andiko vinginevyo kunaweza kutuacha na matatizo yaliyotajwa hapo juu, baadhi yake yakiwa ni ya muhimu na baadhi yake yamefifia sana kimawazi. Tunahesabia haki kwa kuyakubali maelezo yatolewayo kwa sababu nyingi zaidi kuliko zile zilizopo na yaliyoenezwa sana kila mahali ulimwenguni kote na kwa karne nyingi katika Australia, Asia, Afrika na Amerika. Ukweli ni kwamba miundo elekevu inaonekana kwenye maandiko mengine ya kidini, kama vile Kathopanishad, ingawa mashauri fulani hayatusukomi au kutushurutisha kuikubali hii kuhusiana na maandiko ya kibiblia. Tunakuwa salama kwa kukubali tafsiri mahiri kwa kuwa ukombozi wa mzaliwa wa kwanza kumeamriwa kwenye Kutoka 13, na ilivyoelezewa na kuwa alidangantika kwa mara nyingi. Chochote kilichoamriwa na kuwa kuhadaika kunatakiwa pia kuwa matendo.  Ni dhahiri pia kuwa ilielezewa kwenye Mwanzo 22.

 

Yapasa ielezwe kuwa andiko hili, kutolew Sadaka kwa Isaka, kulikuwa kuna maana kubwa sana kwenye uzoefu wa mambo ya kidini. Dhana ya kimakosa kuwa Mungu anaweza kumuamuru mtu ajishughulishe na utoaji wa sadaka ya mwanadamu kumefungua mlango wa kukosolewa kwa dini kwa nyingine zote kwa upande mmoja, na mambo menyine makuu ya matendo yasiyo imara kwa meingine/ kwenye dini ya Kiyhudi, inaonekana kuwa nia na lengo la hadithi hii ni kwamba Mungu alimfundisha Ibrahimu kwa njia pana kwamba yeye hakuwa anaipokea sadaka ya binadamu. Ilikuwa njia ya kimatendo kwa kuwa matendo ya kutoa sadaka za wanadamu huko Kanaani kwa namna nyingine yangewashawishi na kuwavutia kwa namna fulani Ibrahimu na uzao wake.

 

Ukristo umejionea maalidi ya hadithi kuwa ni kwamba utii wa Ibrahimu ni mfano kwa wote kuufuata’ imani zote mbili, yaani Wakristo na Wayahudi wameitumia hadithi hii kama ni silaha ya kuikosoa imani ya Kiislamu. Kor’ani ([37]:103-106) [inadaiwa kuwa ed.] inaelezea tukio hilohilo kwa Ishimaeli badala ya Isaka. Wanazuoni wa Kiislamu wameona kutajwa kwa “mtoto wa pekee” kwenye Mwanzo 22:2 kama masalia ya andiko la kweli linalomtaja Ishmaeli, ambaye alikuwa mtoto wa pekee wa Ibwahimu kwa maisha halisi. Mwanazuoni na mtafsiri kama huyu angeshauri kuwa andiko lilikuwa limegeuzwa na Wayahudi na kumuelezea Isaka badala yake.

 

Kwenye mambo au matukio yanayopigiwa chapuo, ukweli ungekuwa ni tofauti. Wote wawili, yaani Ishimaeli na Isaka, wote wawili wakiwa ni wazaliwa wa kwanza kutoka tumboni mwa mama zao, walipaswa kukombolewa. Dr McElwain anahitimisha andiko kwa kutoa fafanuzi. Ukombozi wa lazima, wa kutoa kikombozi cha sadaka mbadala vilifanyika kwa wote wawili. Mwishoni, maandiko ya biblia yanaenda pamoja, na Biblia na Korani zote mbili ziko sahihi. Kila moja inakubali na kukiri na sisi sote tunakabiliwa na kuishi pamoja kwa amani. Je, tunaweza kuinuka kwa jaziba kwenye changamoto ile?

 

Hata hivyo kuna kosa kubwa katika kudhani au kwenye dhana kuhusu imani ya Kiislamu kuhusu Ishimaeli. Andiko kwenye Korani Sura ya 37:103-106 haionekani kumtaja Ishimaeli kabisa.

 

Dhana hii inabakia kwenye ukweli kwamba andiko lililo kwenye Sura ya 37:112 ndipo inaendelea mbele kuelezea kuzaliwa kwa Isaka. Ndipo wazo linapofanywa kwamba andiko hili linamtaja Ishimaeli na kisha Isaka. Ukweli ni kwamba andiko hili linaiezea baraka ya Isaka kama nabii wa haki kuanzia hata kabla kuzaliwa kwake. Andiko hili linakutja kuzaliwa kwa Isaka na baraka zake na huduma yake ya kinabii, au wadhifa wake akiwa kama nabii, miongoni mwa mwa manabii wa Biblia (pamoja na Nuhu (37:79-82, Ibrahimu (37:83 na kuendelea), Isaka (37:112 na kuendele.), Musa na Haruni (37:120 na kuendelea), Eliya (37:130 na kuendelea), na Yona (37:139 na kuendelea)). alitangaziwa Ibrahimu kabla ya kuzaliwa kwake. Ukweli wa mambo ni kwamba Sura ya 37 haina lolote la kufanya wala kuhusiano wowote na Ishimaeli na ni marudio ya hadithi ya Mwanzo 22:2 na 25:5-6, 9, 11, 12. Ina,fanya Isaka kuwa ni kama nabii, kama mmoja wa wale walio kwenye vyeo akipewa hata jina la Sura hii. Sura hii inashughulika na kukemea ibada potofu na miungu wa dunia hii ambalo kwa hakika ndiyo maana halisi kabisa ya hadithi hii ya kutolewa sadaka kwa Isaka. Agano lililofanywa na Ibrahimu ilikuwa ni ishara iliyotolewa badala ya sadaka ya mwanadamu kama ilivyokuwa inatolewa kwenye imani na ibada za Moleki na kwenye imani na ibada za Baali-Ishta. Ilikuwa ni kawaida tu huko Uarabuni na ulimwenguni kote kwa ujumla hadi kipindi cha kumuabudu Ndama wa Dhahabu ilipokomeshwa na imani ya Ukristo (soma jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222)). Kuhusishwa kwa Ishimaeli ni jambo lililofanywa kwa fikra tu kwamba watajwe wote kwenye kuzaliwa kwao kwenye Sura ya 37:101, 112 inawataja watoto wawili ambao ni Ishimaeli na Isaka na Ishimaeli hatajwi kwa jina. Wazo hili ndilo ambaalo lililotolewa na kudai kuwa mgongano kati ya Korani na andiko la kitabu cha Mwanzo. Kutokana na hili upungufu wa uvuvio inaodaiwa kuwepo kwenye Maandiko Matakatifu na kwenye Sheria za Mungu zilizo kwenye Torati kwa Waislamu wa siku hizi wanayoyatumia ili kuhalalisha mambo yasiyo na uhusiano na Maandiko Matakatifu na Torati ya Mungu. Hebu na tutathimini andiko lote zima kuwahusu Ibrahimu na Isaka:

99: Na akasema: Hakika mimi[Ibrahimu]  nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

100. Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

101. Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

102. Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye [Ibrahimu], alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.

103. Basi wote wawili walipo jisalimisha, (kwa Allah) na akamlaza juu ya kipaji.

104.Tulimwita: Ewe Ibrahim!

105. Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.

106. Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.

107. Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu

108. Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.

109. Iwe salama kwa Ibrahim!

110. Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema

111. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.

112. Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.

113. Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi. (Tafsiri ya Kiswahili)

Kisha andiko linaendelea kwenye kifungu cha maandiko na mstari wa orodha ya manabii hadi kufikia Ibrahimu na Isaka, wakitajwa majina yao kuwa ni Musa na Haruni (37:114). Ishimaeli hatajwi wala mstari wa uzao wake Ishimaeli na taifa la Kiarabu. Kama Ishimaeli akihusishwa basi ni kwa nasibu kwa lengo la kumuelezea Sara na ni lazima iwe kwa kifupi hata haiwezekani kudai kanuni ya kifungu.

 

Tafsiri iliyofanywa na Arberry (iitwayo Korani Ilitafsiri [Koran Interpreted], Oxford, 1964) anatumia maneno kisha ili kuashiria ukitambo wa muda kuendeleza malumbano haya kwamba wote wawili, yaani Ishimaeli na Isaka wameelezewa kwenye mchakato, lakini hii ni leseni ya mtafsiri ambayo haikuchukuliwa na Pickthall. Sale (Warne and Co., pp. 336-337) yaonekana kubeba dhana au wazo kuhusu ukuwili wa matangazo na kwa hiyo ndipo watoto wawili walitajwa kwenye tafsiri yake ingawaje hakuna sababu kwa namn yoyote ile ya kufanya hivyo kutoka kwenye maneno ya tafsiri. Kwa kweli kinyume chake ndicho kinachoonekana. Tafsiri ya Dawood inafuatia andiko kama anavyofanya Pickthall na inafanya uandishi mwingine tena jambo lililopo kuhusu Isaka kwenye sura ya 37:112.

 

Abdullah Yusuf Ali anaanzisha malumbano makubwa kwenye kitabu chake cha fafanuzi (kiitwacho The Qur’an, Text, Translation and Commentary [Korani, Andiko, Tafsiri na Ufafanuzi], Tahrike Tarsile Qur’an Inc, 1987 print, p. 1205) kwamba kwa miaka kumi na minne Ishimaeli alikuwa ni mtoto pekee wa Ibrahimu. Anashikilia kuwa hoja yake ilikuja kutupiliwa mbali baadae na imani za Kiyahudi na Kikristo ambao walimkweza Yule kijana mdogo wa familia, aitwaye Isaka. Hata hivyo, tunajua pasi shaka kutokana na watalaamu wa elimu kale na uchimbuzi wa siku hizi na maandiko ya kale kwamba ni maana ya kweli na maandiko ya Maandiko Matakatifu ya kale ya wakati wa Kristo na yalikuwa ni maandiko yanayoeleweka hata wakati wa Qasim (aliyeitwa Muhammad), na ni maandiko asilia ya Biblia.

 

Hata hivyo, sisi tunajua pia kwamba wakati wa tukio hili Ishimaeli na mama yake Hajiri walikuwa wamekwishatoka na kuondoka zao, kutokana na mgongano uliokuwepo na chuki kati ya Hajiri na Sara. Kwa hiyo Ibrahimu aliachwa na Isaka aliwa ni mtoto wake wa pekee na hii ndiyo iliyomaanishwa na fungu hili la Biblia.

 

Andiko lililo kwenye Qur’an (Korani) halipingani kwa namna yoyote na maandiko ya Biblia kwenye kitabu cha Mwanzo na ni ushahidi mwingine zaidi kwamba tafsiri ya Marabi wa Kiyahudi inayomuona Isaka kuwa ndiye aliyetolewa sadaka inakosea kabisa. Pia, uelewa sahihi kama ulivyofunuliwa kwenye Sura kama ilivyoeleweka na Mtume ni sawa na ilivyo kwenye maandiko ya Biblia. Na kwa kweli inapasa kuwa hivyo. Hata hivyo, iwapo kama inadaiwa kuwa Ishimaeli anahusika, kutokana na kukarabatiwa kwa maanndiko, ndipo kanuni ya ya muafaka wa kifungu itaondoa mgongano na inasisitiza umuhimu wa kuondolewa kwa mifumo na imani za zama kale kutoka katikati mwa watu wa Mungu wawe Waarabu au Waisraeli, iwe kimwili ama kiroho.

 

Agano la Mungu ni la lazima na muhimu kwa ajili ya imani na kwa wana wa Ibrahimu kwenye kila ushawishi wa kidini

.

 

q