Makanisa ya Kikristo ya
Mungu
[281]
Raheli na
Torati
(Toleo La 1.0 19981211-19990625)
Historia ya Raheli imejaa mambo mengi ya kushangaza
yanayoonekana pengine
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
1998, 1999 Christian Churches of God; ed. Wade Cox)
(tr. 2012)
Masomo
yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote
kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Raheli na Torati
Historia ya Raheli imejaa mambo mengi ya kushangaza yanayoonekana pengine kama maigizo, na ni mojawapo ya uthibitisho kwamba Amri ya Kumi ilipewa mkazo wake hata kabla ya kipindi cha kutolewa kwake huko Sinai. Hapa tunashughulika na idadi kadhaa ya mambo yaliyotendeka na uhusiano wake ulio sambamba na habari ambayo kwa kawaida inaepusha mtazamo. Hii ni somo linalotu sura iliyo kwenye Biblia ni mgodi wa dhahabu wenye tutuonyesha mambo ya kushangaza na yenye thamani kuu kimasomo au kimafudisho.
Ingawaje hadithi ya Raheli ni mojawapo ya zile zinazopendwa sana na watoto, bali watu wazina nao wanapaswa kujisomea hadithi kila mara, na wafanye kwa kumaanisha kujifunza kit una wasisome kwa mtindo wa kujisomea hadithi tu kikawaida.
Baada ya Yakobo kumwibia haki ya uzaliwawake ndugu yake Esau, kwa kumdanganya baba yake Isaka, mahali wapokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani hapakuwa salama tena kwa yeye kuendelea kuishi na ndipo Yakobo alilazimika kukimbilia sehemu nyingine ili kujiponya nafsi yake.
Mwanzo 27:41 Esau akamchukia Yakobo kwa ajili ya ule mbaraka babaye aliombarikia. Esau akasema moyoni mwake, Siku za kumlilia baba yangu zinakaribia, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.
Hapa kunaona mawazo aliyokuwanayo Esau kwa Yakobo kuwa yalikuwa sawa tu na vile alivyokuwa akiwaza ndugu yake, ni sawa na Kaini alivyokuwa akimuwazia ndugu yake Abeli. Rebeka akasikia maneno ambayo mtoto wake mkubwa Esau aliyoyatamka akimnuia mdogo wake. Ndipo akamuita Yakobo na kumuonya akimbie kabla mambo hayajawa makubwa na hajachelewa. Akamshauri aondoke na aende nchi ya mbali ya Harani, mahali alipokulia yeye na aliamini kuwa huko kungekuwa mahali salama kwake. Pia aliamini kuwa hatimaye hasira za Esau zingetulia na kisha angeweza kurejea baada ya kitambo hapo mbeleni baada ya siku nyingi kupita.
Mwanzo 27:42-44 Rebeka akaarifiwa maneno ya Esau, mwanawe mkubwa. Akapeleka mtu kumwita Yakobo, mwanawe mdogo, akamwambia, Tazama, katika habari zako Esau, ndugu yako, anajifariji moyo wake, maana anakusudia kukuua. 43 Na sasa, mwanangu, sikia sauti yangu, uondoke, ukimbilie kwa Labani, ndugu yangu huko Harani; 44 ukae kwake siku chache, hata ghadhabu ya ndugu yako igeuke;
Woga aliokuwanao Rebeka wa kutokea
uwezekano wa kuwakosa wanawe wote wawili kwa tendo lile lililotokea ulikuwa sio
wa kawaida. Kitendo cha kuuawa Yakobo na Esau
kingefuatiwa na kuuawa kwa Esau na wenye kulipiza damu aliyoimwaga ya ndugu
yake,
Mwanzo 4:10
Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu
yako inanililia kutoka katika ardhi.
Mwanzo 4:13-14 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki. 14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.
Tunaona mkazo umewekwa na kuwa muhimu hapa kwa kuwa kulikuwa na malipizo ya damu kwa mtu anayeua, hasa kwa anayemuua ndugu yake. Hapa kunaonekana wazi kwamba amri ya sita ilikuwepo tangu siku za Adamu.
Amri hii ilirudiwa na Nuhu:
Mwanzo 9:5b-6 … kwa mkono wa ndugu ya mtu nitataka uhai wa mwanadamu. 6 Atakayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu, maana kwa mfano wake Mungu alimfanya mwanadamu.
Hapa tunajioea wazi mkazo ulivyowekwa kwenye amri ya sita na maana au sababu zake. Pale Sinai ilisisitizwa na kurudiwa kwa maneno machache:
Kutoka 20:13 Usiue
Rebeka alimwendea Isaka na kumuomba amruhusu Yakobo aondoke na kwenda zake mbali na uso wa Esau, na akamkabili kwa namna ya werevu wa hali ya juu sana, akijifanya kumtaka mawazo yake Isaka juu ya hali ile.
Mwanzo 27:46
Rebeka akamwambia Isaka, Rohoni mwangu sina raha
kwa sababu ya hao binti za Hethi. Kama Yakobo akitwaa mke katika binti za
Hethi, kama hawa binti za nchi, maisha yangu yatanifaidia nini?
Esau aliwaoa binti za Kanaani na hawakupata kibali au idhini na kupendwa wazazi wake.
Mwanzo 26:34-35 Esau alipokuwa mwenye miaka arobaini, akamwoa Yudithi, binti Beeri, Mhiti, na Basemathi, binti Eloni, Mhiti. 35 Roho zao Isaka na Rebeka zikajaa uchungu kwa ajili yao.
Ilikuwa pia ni kinyume na mapenzi ya Mungu kuwaoa binti za Kannani na kuwafanya wakeze, au kumtoa binti na kuwapa Wakanaani ili aolewe nao, na kulikuwa na sababu za msingi kutofanya kwao hivyo.
Kumbukumbu la Torati 7:1-4 Bwana, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki,
atakapoyang'oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na
Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na
Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe; 2 wakati Bwana, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe
utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala
kuwahurumia; wala usioane nao; 3 binti yako usimpe mwanawe mume, wala usimtwalie mwanao mume binti yake.
4 Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate
kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye
atakuangamiza upesi.
Baada ya Esau
kugundua kwamba ndugu yake Yakobo ameondolewa aende mbali, na
tena akiwa amebarikiwa, na akatafute mwanamke asiye wa Kikanaani, ndipo alijarubu
kujifariji kwa kuweka
Mwanzo 28:6-9 Esau akaona ya kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padan-aramu, ili ajitwalie mke huko, na katika kumbariki akamwagiza, akasema, Usitwae mke wa binti za Kanaani, 7 na ya kuwa Yakobo amewatii babaye na mamaye, akaenda Padan-aramu. 8 Esau akaona ya kuwa binti za Kanaani hawakumpendeza Isaka, baba yake. 9 Basi Esau akaenda kwa Ishmaeli akamtwaa Mahalathi, binti Ishmaeli mwana wa Ibrahimu, ndugu wa Nebayothi, kuwa mkewe pamoja na wakeze aliokuwa nao.
Makabila lililotokana na Ishimaeli, mwana wa Ibrahimu, ni watu wanaofanananao tu na hawako kwenye nasaba ya dam una Wakanaani.
Isaka alimpeleka Yakobo huko Padan-aramu ili kufanya mwanawe akajitwalie mke kwa binti za Labani:
Mwanzo 28:1-2 Basi Isaka akamwita Yakobo, akambariki, akamwagiza akamwambia, Usitwae mke wa binti za Kanaani. 2 Ondoka, uende Padan-aramu, mpaka nyumba ya Bethueli baba ya mama yako, ukajitwalie huko mke katika binti za Labani, ndugu wa mama yako.
Isaka alimpa Yakobo amri ya kumuoa mmoja tu kati ya binti zake Labani. Isaka alikuwa ni mume wa mke mmoja tu, na alimshauri mwana wake afanye vivyohivyo. Lakini kulingana na mazingira yalivyokuwa Yakobo alishindwa kutii agizo hili la baba yake.
Jambo la muhimu
hapa hata hivyo ni kwamba, Isaka alimsababishia pia
manawe Yakobo kutenda dhambi. Baada ya kugundua madhara ya dhambi hii, Yakobo
alishindwa kukataa ushauri wa baba yake kuhusu jambo
hili. Dhambi yenyewe ilikuwa ni tendo la kwenda
kujipatia mke na kuoa ndugu wa karibu ndani ya familia
Mwanzo 28:2 Ondoka, uende Padan-aramu, mpaka nyumba ya Bethueli baba ya mama yako, ukajitwalie huko mke katika binti za Labani, ndugu wa mama yako.
Pale Sinai amri hii ilitiliwa mkazo na kufafanuliwa kwa kina zaidi:
Mambo ya Walawi 18:4-5 Mtazifanya hukumu zangu, nanyi mtazishika amri zangu, ili mwenende katika hizo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 5 Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana
Kwa kujua kile ambacho kinamwezesha mtu kuishi kwacho, ndipo sheria hii iliwekwa kwa haraka na mara moja kwa upesi:
Mambo ya Walawi 18:6 Mtu ye yote aliye wa
kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu;
mimi ndimi Bwana
Hili ni jambo lililo wazi, na lilikuwa likitenda kazi kwa siku
zile za Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu. 12 Naye kweli ni ndugu yangu, binti wa baba yangu ila siye mwana wa mama yangu, ndipo akawa mke wangu. (Mwanzo 20:11-12)
Kwenye aya kadhaa chache, tunajionea zaidi kwamba inawezekana kabisa kwamba hali ya ugumba inaweza kuwa hukumu kwa ajili ya dhambi iliyotendwa.
Mwanzo 20:17-18 Ibrahimu akamwomba Mungu, Mungu akamponya Abimeleki, na mkewe, na wajakazi wake, nao wakazaa wana. 18 Maana Bwana alikuwa ameyafunga matumbo ya watu wa nyumbani mwa Abimeleki, wasizae, kwa ajili ya Sara mkewe Ibrahimu.
Udugu kama iliokuwepo kwenye ndoa
kati ya Ibwahimu na Sara haukuruhusiwa, na umetajwa kinaga ubaga na bayana:
Mambo ya Walawi 18:11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa
na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wako
Kwa ajili ya adhabu ya kwenye ndoa kwa
ajili ya uhusiano huu wa damu uliokuwepo kati ya Abrahamu na Sara, basi
walikosa kuzaa mwana na akawa tasa:
Mwanzo 16:1 Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri.
Mungu aliwaahidi Ibrahimu na Sara
mtoto. Kipindi kikapita na Sara akapoteza imani yake
kabusa.
Mwanzo 18:10-14 Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. 11 Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. 12 Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? 13 Bwana akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? 14 Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.
Tunaona
hapa kwamba ingawa ilikuwa ni vigumu sana kwa mwanadamu, lakini haikuwa vigumu
kabisa kwa Mungu, na kwa uweza uaio wa kawaida kwa miujiza, aliwaondolea ule
utasa..
Mwanzo 21:1-3 Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema. 2 Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu.
Halikuwa
jambo jambo lisolo la kawaida kwa Isaka kumtuma
mwanawe Yakobo aende Padan-aramu ili akajitwalie
mke huko. Baba yake alimpa mtumishi wake agizo kwa
kumuapia kwamba akamtafutie mwanamke sahihi kwa ajili ya mwanawe Isaka.
Mwanzo 24:1-4 Basi Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na Bwana alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote. 2 Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao; 4 bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke.
… na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke. Hapa
tunamwona Abrahamu akiangukia kwenye chimo lile lile
Mwanzo 24:15 Ikawa, kabla hajaisha kunena, tazama, Rebeka anatokea, binti wa Bethueli mwana wa Milka, mkewe Nahori, ndugu wa Ibrahimu, naye ana mtungi begani pake
Mwanzo 24:50-51 Ndipo Labani na Bethueli
wakajibu wakasema, Neno hili limetoka kwa Bwana, wala sisi hatuwezi kukuambia
neno jema wala baya. 51 Tazama, huyo Rebeka
yuko mbele yako, umchukue, ukaende zako awe mke wa mwana wa bwana wako, kama
alivyosema Bwana.
Mwanzo 24:67 Isaka akamwingiza Rebeka katika hema
ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake.
Ndoa hii iliandaliwa na mtumishi wa Abraham. Na bado huko mwanzoni ndoa hii
ilikuwa ya utasa,
Kutoka 20:5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,…
Tendo la kuufunua
utupu wa mababa (Kufanya matendo maovu
yaliyofanywa na mababa huko nyuma) [visiting
of the iniquity of the fathers] sio
t uni kuivunja amri ya pili, bali inatenda kazi pia kwenye Torati yote,
Yakobo 2:10 Maana mtu awaye yote
atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
Hata hivyo, kwenye hali
Mwanzo 25:19-21 Na hivi ndivyo vizazi vya Isaka, mwana wa Ibrahimu. Ibrahimu alimzaa Isaka. 20 Isaka akawa mwenye miaka arobaini alipomtwaa Rebeka binti Bethueli, Mshami, wa Padan-aramu, ndugu wa Labani, Mshami, kuwa mke wake. 21 Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.
Ndoa
kati ya Isaka na Rebeka ilikuwa ni ya utasa, bila
mtoto katika kipindi cha miaka ishirini ya kwanza. Tunaona tena hapa kwamba
ililazimu Mungu aingilie kati kimiujiza kwa Rebeka, ni
Tunaona
hali waliyokuwanayo wake za Yakobo.
Mwanzo 28:5 Basi Isaka akampeleka Yakobo, naye akaenda Padan-aramu, kwa Labani, mwana wa Bethueli, Mshami, ndugu wa Rebeka, mama
Mwanzo 29:1-10 Kisha Yakobo akashika njia yake, akafika nchi ya wana wa mashariki. 2 Naye akaangalia, na tazama, kiko kisima
kondeni, na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu nacho, kwa sababu katika
kisima kile hunywesha makundi; na palikuwa na jiwe kubwa juu ya kinywa cha
kisima. 3 Makundi
yote hukusanyika huko, watu wakafingirisha hilo jiwe katika kinywa cha kisima
wakawanywesha kondoo, na kulirudisha jiwe juu ya kinywa cha kisima mahali pake.
4 Yakobo
akawauliza, Ndugu zangu, watu wa wapi ninyi? Wakasema, Tu wa Harani sisi. 5 Akawauliza,
Je! Mnamjua Labani, mwana wa Nahori? Wakasema, Tunamjua. 6 Akawauliza, Je!
Hajambo? Wakasema, Hajambo; tazama, Raheli binti yake anakuja na kondoo. 7 Akasema,
Tazama, ukali mchana bado, wala sio wakati wa kukusanya wanyama; wanywesheni
kondoo, mwende kuwalisha. 8 Wakasema, Hatuwezi,
hata yakusanyike makundi yote, watu wakafingirishe jiwe katika kinywa cha
kisima, ndipo tunapowanywesha kondoo. 9 Hata alipokuwa akisema
nao, Raheli akaja na kondoo za baba yake, maana aliwachunga. 10 Ikawa Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa
mamaye, na kondoo za Labani, ndugu wa mamaye, Yakobo akakaribia, na
kulifingirisha lile jiwe litoke katika kinywa cha kisima, akawanywesha kondoo
za Labani, ndugu wa mamaye.
Yakobo
alifurahishwa
Mwanzo 29:11 Yakobo akambusu Raheli, akainua sauti yake akalia
Jw, ni kwa nini Yakobo alilia kwa sauti kuu? Je, hii ilitokana na uppendo aliokuwanao kwa yule binti, au ilisababishwa na
mawazo yake kwamba kuoa mtu aliye wa jamaa yake wa karibu kungeleta kizuizi
kumpata binti huyu aliyempenda
Mwanzo 29:12 Yakobo akamwarifu Raheli ya kuwa yeye ni ndugu wa babaye, na ya kuwa ni mwana wa Rebeka. Basi akapiga mbio akampasha babaye habari.
Uhusiano wa kindugu kwenye familia ni wa muhimu
Mwanzo 29:13-16 Ikawa Labani aliposikia habari
za Yakobo, mwana wa nduguye, akaenda mbio amlaki, akamkumbatia, akambusu,
akamleta nyumbani kwake. Naye akamwambia Labani maneno hayo yote. 14 Labani akamwambia, Ndiwe kweli mfupa wangu na nyama
yangu. Naye akakaa kwake muda wa mwezi mmoja. 15 Labani
akamwambia Yakobo, Kwa sababu wewe ni ndugu yangu, basi, je! Unitumikie bure?
Niambie mshahara wako utakuwa nini? 16 Labani alikuwa na
binti wawili, jina la mkubwa ni Lea, na jina la mdogo ni Raheli.
Maandiko haya yanaotoa dokezo kwamba Labani anamtafutia kwa bidii kitu chema huyu ndugu wa jamaayake wa karibu. Tabia na hulka za Labani, hatahivyo zilikuwa ni uchoyo (Mwanzo 24:29-30, 53) na Yakobo alikuja pia kugundua kwenye miaka iliyofutia baadae.
Mwanzo 29:17 Naye Lea macho yake yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo, na mzuri uso.
Hapa tunajionea ulinganifu kati ya
Lea na Raheli, ni kwamba Lea alikuwa haoni vizuri kwa
kuwa macho yake yalikuwa dhaifu. Tafsiri ya Mfalme Yakobo (KJV) inalielezea
jambo hili kwa namna nyingine.
Mwanzo 29:17 Naye Lea macho yake yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo, na mzuri uso.
Hapa inaelezea kwamba macho ya Lea yalikuwa ni ya makengeza. Hii inaonekana tena kuwa ni hitilafu, na ilikuwa ni kinyume kabisa na jinsi alivyoonekana Raheli. Jamieson, Fausset, anatoa maelezo mengine kwa kusema:
Ni kwamba, macho yalikuwa ni ya kibluu nyepesi-yaliyodhaniwa kuwa na chongo au kilema
(Jamieson, Fausset, Brown Commentary Old Testament Vol. 1, 1991, Ages, Albany OR)
Na kwa kuwa macho ni mvuto wa moyo, basi ni kitu muhimu
Na hili ndilo lililomtokea Sara, mke wa Ibrahim, wakati alipokuwa na umri wa takriban miaka 65.
Mwanzo 12:10-15 Basi
kulikuwa njaa katika nchi ile; Abramu akashuka Misri, akae huko kwa muda maana njaa ilikuwa nzito katika nchi. 11 Ikawa alipokuwa karibu kuingia Misri,
akamwambia Sarai mkewe, Tazama, najua ya kuwa u mwanamke mzuri wa uso; 12 basi itakuwa, Wamisri watakapokuona watasema,
Huyu ni mkewe; kisha wataniua mimi na wewe watakuacha hai. 13 Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe
heri kwangu kwa ajili yako, na nafsi yangu iishi kwa ajili yako. 14 Basi ikawa Abramu alipofika Misri, Wamisri
wakamwona huyo mwanamke ya kwamba yeye ni mzuri sana. 15 Wakuu wa Farao wakamwona, nao wakamsifu kwa Farao;
basi yule mwanamke akachukuliwa nyumbani mwa Farao.
Ni mtindo huo huo wa kuongopa ulijitokeza ambao ulisababishwa na woga kwa Isaka ba Rebeka.
Mwanzo 26:6-9 Isaka akakaa katika Gerari. 7 Watu wa mahali hapo
wakamwuliza habari za mkewe. Akasema, Ni ndugu yangu huyu maana aliogopa
kusema, Ni mke wangu, watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa
maana alikuwa mzuri wa uso. 8 Ikawa alipokuwa
amekaa huko siku nyingi, Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, akachungulia
dirishani, akamwona Isaka anacheza-cheza na Rebeka mkewe. 9 Abimeleki
akamwita Isaka, akasema, Yakini huyu ni mkeo, mbona ulisema, Ni ndugu yangu
huyu? Isaka akamwambia, Kwa sababu nalisema, Nisife kwa ajili yake.
Labani alikwenda kufanya matano na Yakobo kwa ajili ya mshahara wake, na kwa ajili ya uroho, akamuuza binti yake Raheli kwa Yakobo. Yakobo akaukubali mshahara huu na kuuona ulistahili kwa kipindi cha miaka saba ya utumishi wake wa kuchunga mifugo.
Mwanzo 29:18-20 Yakobo akampenda Raheli akasema, Nitakutumikia miaka saba
kwa kumpata Raheli, binti yako mdogo. 19 Labani
akasema, Afadhali nikupe wewe kuliko mtu mwingine; kaa kwangu. 20 Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli. Ikawa machoni pake kama siku chache tu kwa
vile alivyompenda.
Yakobo alikuwa
anampenda
Mwanzo 29:21 Yakobo akamwambia Labani, Nipe mke wangu, maana siku zangu zimetimia; niingie kwake.
Tunaona hapa kwamba kicha ya upendo wake uliokuwa unawake kwa kipindi cha zaidi ya miaka saba, Yakobo hakumtaka Raheli afanyenaye tendo la ngono hata kidogo. Alikuwa ni bikira bado, jaambo ambalo kwa kawaida za ulimwenguni tunaoishi siku hizi ni jambo lisilotarajiwa wala kufikirika kubakia kuwa hiyyo. Hapa kuna mfano tunaouona na ambao unatakiwa kufuatwa au kuigwa.
Licha ya tumaini la haki na uaminifu aliokuwanao na taraja la kumpata mke kwa siku zake za usoni, bali kile kilichofanyika kilikuwa ni kinyume kabisa na Sheria za Mungu na ilikuwa ni uvunjaji wa imini. Dadayake Lea kwa hila na udanganifu uliopagwa kwa makusudi kabisa akampiku Raheli na kuchukua mahala pake kwenye ndoa. Inaonekana kabisa kwamba Labani alikubaliana na binti yake Lea wamdanganye Yakobo na kumuamuru Raheli asijitambulishe na abakie kimya au aende mbali kabisa na asiwe karibu napo.
Kwa kukosa
kwake uaminifu Lea pamoja na udhaifu wake alijikuta
akiingia kwenye jaribu hili la udanganyifu, tendo ambalo lilimuathiri mdogo wake
na mume wake kwa kipindi chote kizima kilichobakia cha maisha
Mwanzo 29:22-26 Labani akakusanya watu wote wa mahali pale, akafanya karamu. 23 Ikawa wakati wa jioni akamtwaa Lea, binti yake, akamletea Yakobo, naye akaingia kwake. 24 Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake. 25 Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda? 26 Sikukutumikia kwa Raheli? Mbona umenidanganya? Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa;
Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea: Ni lazima tu kulikuweko mawazo na mazingira yenye uchungu mkubwa wakati Yakobo alipomtazama na kuyaona macho dhaifuya bluu ama ya makengeza ya Lea, badala ya kuyaona yale meusi ya Raheli. Kwa kuwa walikuwa ni ndugu inawezekana walikuwa na umbo linalofanana. Kwa hiyo Yakobo hakuweza kugundua tofauti yoyote pale gizani. alikoseshwa na kutapeliwa na Labani. Hata hivyo, tapeli huyu Labani alimweleza sababu ya kumfanyia vile, na kumruhusu aanze tena kwa huyu mwingine ambaye alikuwa ni kwa ajili yake, ambaye alifanya ushauri wa maana na akampa Raheli kwa mara ya pili kwa sharti la Yakobo amtumikie tena kwa kipindi kingine cha miaka saba cha mshahara wake.
Mwanzo 29:26-28 Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya
mkubwa; 27 timiza siku zake saba, nasi tutakupa huyu
naye kwa utumishi utakaonitumikia, miaka saba mingine. 28 Yakobo akafanya hivi, akatimiza siku zake
saba. Naye akampa Raheli binti yake kuwa mkewe.
Akatimiza siku zake saba. kilikuwa ni kipindi cha kawaida cha fungate au sherehe ya ndoa. Ndoa hii ya Lea ilikuwa ni ya kinyume na maagizo ya Torati.
Mambo ya Walawi 18:6 Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana.
Kisha baada ya juma moja kupita, alimuoa Raheli. Ni sawa tu na ile ya kwanza, ndoa hii aliyoifunga na Raheli ilikuwa ni kinyume na maagizo ya Torati na dhambi iliendelea kufanyika:
Mambo ya Walawi 18:18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai
Mwanzo 29:29-30 Labani akampa binti yake Raheli mjakazi wake Bilha, awe mjakazi wake. 30 Akaingia kwa Raheli naye, akampenda Raheli kuliko Lea, akatumika kwa ajili yake miaka saba mingine.
Kuna jambo lingine linaloelekezwa na Torati ambalo lilikuwa limevunjwa, ambalo ni kwamba hairuhusiwi mtu kuoa tena kwenye kipindi cha ndani ya mwaka mmoja wa ndoa (Kumbukumbu la Torati 20:7). Tatizo sio kwa inavyotokea vita tu, bali ni kulinda umilkaji na uzao. Ilivunjwa mara ya kwanza kwa tendo la kumuibia haki yake Raheli. Na ikavunjwa kwa tukio la pili kwa kuzima na kuyakiuka matarajio ya Lea. Hata hivyo, ilisemekana na wengi kuwa aliyasababisha haya yeye mwenyewe.
Hali hii ya utata kwenye ndoa ilisababisha na mgongano na upotevu wa mshikamano kati ya Yakobo na wake zake, na kati ya wake zake wenyewe. Hii ilihitaji achukue hatua muhimu katika kuweka mtengamano na maelewano ya kifamilia kwa kipindi kingine kilichofuatia. Mahusiano yalikuwa ni ya matatizo zaidi, kipindi ambacho wakezake wote walipokuwa hawazai, jambo lililosababishwa na kufanya ndoa hizi za ndugu wa karibu ambazo zimeharimishwa.
Mwanzo 29:31 Bwana akaona ya kwamba Lea hakupendwa, naye akafungua tumbo lake; bali Raheli alikuwa hazai.
Mungu akaingilia kati utasa wa Lea, kwakuwa Yakobo hakumpenda. Alikuwa hajaingilia kati bado utasa wa Raheli. Licha ya ukweli kwamba Lea alimzalia watoto Yakobo, bali alikuwa hampendi tu bado na kidogokidogo Lea akaanza kupoteza imani kwamba Yakobo ataweza kuja kumpenda, na hatimaye akamshukuru BWANA, Mungu.
Mwanzo 29:32-35 Lea akapata mimba akazaa mwana, akampa jina lake, Reubeni, maana alisema, Kwa kuwa Bwana ameona teso langu; sasa mume wangu atanipenda. 33 Akapata mimba tena akazaa mwana, akasema, Kwa kuwa Bwana amesikia ya kwamba mimi sikupendwa, amenipa na huyu; akamwita jina lake Simeoni. 34 Akapata mimba tena, akazaa mwana, akasema, Basi wakati huu mume wangu ataungana nami, kwa sababu nimemzalia wana watatu. Kwa hiyo akamwita jina lake Lawi. 35 Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu Bwana; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa.
Sasa kwa mara ya kwanza tabia za Raheli zikafunuliwa. Hazikuonekana
kuwa zilikuwa njema kabisa, na hatimaye zilifanana tu
na zile za baba yake Labani kwa mambo mengi aliyoyafanya. Alikujakuwa ni mwanamke mwenye wivu na uchungu
Mwanzo 30:1 Naye Raheli alipoona ya kuwa hamzalii Yakobo mwana, Raheli alimwonea ndugu yake wivu. Akamwambia Yakobo, Nipe wana; kama sivyo, nitakufa mimi.
Ingawa Yakobo
alijua vema kuwa Raheli alikuwa tasa kwa ajili ya ukaribu wake wa kindugu kati yao,
na kwamba BWANA anaweza kuwahurumia na kuingilia kati kwa niaba yao, hakufuata
mfano wa imani ndogo ambayo kwayo baba yake Isaka aliifuata kipindi cha
majaribu ya utasa wa Rebeka. Hakumuombea, bali
alikasirishwa na hali ile. Hii ilionekana kwa Raheli ambaye
aliamua kufanya tendo lilelile alilolifanya Sara la kumpa Ibrahimu suria wake
Hajiri awe mkewe ili amzalie wana. Raheli akamtoa mtumwa wake Bilha na kumpa Yakobo kkwa lengo lilelile la kumzalia wana.
Mwanzo 30:2-13 Yakobo akamghadhibikia Raheli, akasema, Je! Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia uzao wa mimba? 3 Akasema, Yuko mjakazi wangu, Bilha, uingie kwake ili kwamba azae juu ya magoti yangu, nami nipate uzao kwa yeye. 4 Basi akampa Bilha mjakazi wake kuwa mkewe. Yakobo akaingia kwake. 5 Naye Bilha akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana. 6 Raheli akasema, Mungu amenipa haki yangu, naye amesikia sauti yangu, akanipa mwana. Kwa hiyo akamwita jina lake Dani. 7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili. 8 Raheli akasema, Kwa mashindano makuu nimeshindana na ndugu yangu, nikashinda. Akamwita jina lake Naftali. 9 Lea alipoona ya kuwa ameacha kuzaa, alimtwaa Zilpa, mjakazi wake, akampa Yakobo kuwa mkewe. 10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana. 11 Lea akasema, Bahati njema! Akamwita jina lake Gadi. 12 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili. 13 Lea akasema, Ni heri mimi, maana wanawake wataniita heri. Akamwita jina lake Asheri.
Mazingira yote haya hayawezi kuonyesha kuwepo kwa uhusiano wa kawaida wa kifamilia na ulio imara. Hatimaye Yakobo alifanyika kuwa mwanasesere wa wanawake wanne na kwa watoto wake.
Kilichofuatia
baada ya hapo ni mfululizo wa matukio ya kusikitisha
yakutumia mbinu za kumvutia mwanaume hadi kuanza kutumia matunda yaliyojulikana
1Samweli 15:23 Kwani
kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni
2Nyakati 33:6 Tena akawapitisha wanawe motoni katika bonde la mwana wa Hinomu; akatazama bao, akabashiri, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.
Hizi Tunguja (Tunguja
za mvuto au dawa ya mvuto wa kimapenzi kama
ijulikanavyo kwa Kimombo Mandragora officinarum L.) chanzo chake hasa yanatoka
pande za mashariki mwa Mediterranean na Magharibi ya
Mwanzo 30:14-16 Reubeni akaenda siku za mavuno ya ngano akaona tunguja kondeni, akazileta kwa Lea mamaye. Ndipo Raheli akamwambia Lea, Nipe mimi
baadhi ya tunguja za mwanao. 15 Naye akamwambia, Je!
Ni jambo dogo kuninyang'anya mume wangu; hata wataka kuzitwaa tunguja za
mwanangu pia? Raheli akamwambia, Kwa hiyo atalala kwako usiku huu kwa tunguja
za mwanao. 16 Yakobo akaja kutoka kondeni jioni, Lea
akatoka kumlaki, akasema, Lazima uje kwangu, kwa sababu nimekuajiri, kwa
tunguja za mwanangu; akalala kwake usiku ule.
Yakobo alikuwa amezidiwa
akili na wake zake na aliuzwa kwa Raheli kwa kupewa
tunguja ambazo zilimvuta hadi akubali kulala naye Lea, siku ile. Maandiko
hayatuambii
1Samweli 15:23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni
Lakini binti hawa wa Labani inaonekana walikuwa na ushawishi fulani kwenye mambo haya yaliyo sawa na ibada za sanamu, kwa jinsi tunavyowaona wakitumia tunguja na mboga kwa ajili ya kurutubisha au uzazi. Hata hivyo, tunguja hizi hazikumsaidia Raheli lea akaendelea kumzali Yakobo watoto wengine
Mwanzo 30:17-18 Mungu akamsikia Lea, naye akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana wa tano. 18 Lea akasema, Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nimempa mume wangu mjakazi wangu. Akamwita jina lake Isakari.
Baraka ya mwisho ya Yakobo kwa mwanae Isakari iliashiria mazingira ya kuzaliwa kwake na hatima yake itakavyokuwa:
Mwanzo 49:14-15 Isakari ni punda hodari,
Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo; 15 Akaona mahali pa
raha, kuwa pema, Na nchi, ya kuwa ni nzuri, Akainama bega
Soma tena kwenye wavuti ya: www.members.xoom.com, 1998, Bewitching
herbs, Mandrake
Baada ya kuzaliwa kwake Isakari, Lea alimzaa Zabulon na Dina
Mwanzo 30:19-21 Lea akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa
sita. 20 Lea akasema, Mungu amenipa mahari njema,
sasa mume wangu atakaa nami, kwa kuwa nimemzalia wana sita. Akamwita jina lake
Zabuloni. 21 Baadaye akazaa binti, akamwita jina lake
Dina.
Raheli alijifunza njia ngumu na akamwangalia Mungu akihitaji msaada wake.
Mwanzo 30:22-24 Mungu akamkumbuka Raheli; Mungu akamsikia, akamfungua tumbo. 23 Akapata mimba, akazaa mwana, akasema, Mungu ameondoa aibu yangu. 24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Bwana aniongeze mwana mwingine.
Baada ya miaka
hiyo yote ya kujaribu kupita njia zilizo kinyume na
mapenzi ya Mungu, ndipo Raheli akautafuta msada wa Mungu, na akajipa moyo kwa
kutoangalia makosa na maovu yake. Raheli akampa Mungu utukufu kwa hili, na akamuomba haraka ampe mwana mwingine. Na baada
ya miaka kadhaa (yapata
Yakobo aliichukulia
ile
Mwanzo 30:25-26 Ikawa Raheli alipomzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, Nipe ruhusa niende kwetu, na kwenye nchi yangu. 26 Nipe wake zangu na watoto wangu, niliokutumikia, niende zangu, maana umejua utumishi wangu niliokutumikia.
Labani mroho hakulipenda wazo hili la kumpoteza mchungaji mzuri wa mifugo yake na mtu mwadilifu na shujaa, na akajaribu kuzinunua huduma za Yakobo tena kwa kukiongeza kipindi kingine cha utumishi wake kwake. Mara hii Yakobo alimzidi maarifa.
Mwanzo
30:27-43 inasema: Labani akamwambia, Iwapo nimeona fadhili machoni pako,
kaa, maana nimetambua ya kwamba Bwana amenibariki kwa
ajili yako. 28 Akasema, Sema mshahara wako utakao, nami
nitatoa. 29 Akamwambia, Umejua jinsi
nilivyokutumikia, na jinsi wanyama wako walivyokuwa kwangu. 30 Maana
mali yako ilikuwa haba kabla sijaja, nayo imezidi kuwa nyingi, Bwana
akakubariki kila nilikokwenda. Basi sasa, nitaangalia lini mambo ya nyumba
yangu mwenyewe? 31 Akamwuliza, Nikupe nini? Yakobo akasema,
Usinipe kitu; ukinifanyia neno hili, nitalisha wanyama wako tena na kuwalinda. 32 Nitapita katika wanyama wako wote leo, na kutoa huko
kila mnyama aliye na madoadoa na marakaraka, na kila mnyama mweusi katika hao
kondoo, na aliye na marakaraka na madoadoa katika mbuzi; nao watakuwa mshahara
wangu. 33 Na haki yangu itanishuhudia katika siku
zijazo, utakapokuja kwa habari ya mshahara wangu ulioko kwako. Kila asiye
madoadoa au marakaraka katika mbuzi, au asiye mweusi katika kondoo, akionekana
kwangu, itahesabiwa kuwa ameibiwa. 34 Labani akasema,
Tazama, na iwe hivi kama usemavyo. 35 Basi akatoa siku ile
mbuzi waume walio na milia na madoadoa, na mbuzi wake walio na madoadoa na
marakaraka, kila aliye na doa jeupe, na kondoo wote waliokuwa weusi, akawatia
mikononi mwa wanawe. 36 Akajitenga na Yakobo
mwendo wa siku tatu; naye Yakobo akachunga wanyama wa Labani waliosalia. 37 Yakobo akatwaa fito za mlubna mbichi, na mlozi, na
mwaramoni, akazibambua maganda, mistari myeupe ionekane ndani ya hizo fito. 38 Akazisimamisha fito hizo alizozibambua katika mabirika
ya kunyweshea maji, pale walipokuja wanyama wanywe; wakachukua mimba walipokuja
kunywa. 39 Wanyama wakapata mimba mbele ya hizo
fito, wakazaa wanyama walio na milia, na madoadoa, na marakaraka. 40 Na Yakobo akawatenga wana-kondoo, akazielekeza nyuso za
makundi zielekee wale waliokuwa na milia, na kila aliyekuwa mweusi katika
wanyama wa Labani. Akaweka kando wanyama wake mwenyewe, wala hakuwachanganya
pamoja na wanyama wa Labani. 41 Ikawa kila
walipopata mimba wanyama wenye nguvu, Yakobo akaziweka zile fito mbele ya macho
ya hao wanyama katika mabirika ili kwamba wachukue mimba kati ya zile fito, 42 lakini wanyama walipodhoofika hakuziweka zile fito. Basi
wale dhaifu walikuwa wa Labani, na wenye nguvu walikuwa wa Yakobo. 43 Kwa hiyo mtu huyo akazidi mno, akawa na wanyama wengi,
na vijakazi, na watumwa, na ngamia, na punda.
Kwa ongezeko
hili la haraka la mshahara ndani ya miaka sita, kwa
gharama za Labani, na ndipo alibadili mtazamo wake kinyume na Yakobo kwa kuwa
haikuwa
Mwanzo 31:1-2 Basi Yakobo akasikia maneno ya wana wa Labani,
wakisema, Yakobo amechukua
Ndipo Yakobo alipoambiwa na BWANA ajiandae kurejea nyumbani kwake. Ndipo Yakobo akawaita wake zake Lea na Raheli na kuwaeleza sababu inayomfanya aondoke na kurudi kwao.
Mwanzo 31:3-13 Bwana akamwambia Yakobo, Urudi mpaka nchi ya baba zako na kwa jamaa zako, nami nitakuwa pamoja nawe. 4 Yakobo akatuma watu, akawaita Raheli na Lea waje nyikani
kwenye wanyama wake. Akawaambia, 5 Naona uso wa baba
yenu, kwamba hanitazami vema kama jana na juzi. Lakini Mungu wa baba yangu
amekuwa pamoja nami. 6 Nanyi mmejua ya
kwamba kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu. 7 Na baba yenu amenidanganya, akabadili
mshahara wangu mara kumi; lakini Mungu hakumwacha kunidhuru. 8 Aliposema, Walio na madoadoa watakuwa mshahara wako,
wanyama wote wakazaa madoadoa. Aliposema, Walio na milia watakuwa mshahara
wako, ndipo wanyama wote wakazaa wenye milia. 9 Hivi
Mungu akamnyang'anya mali yake baba yenu, na kunipa mimi. 10 Ikawa,
wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika
ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na
madoadoa, na marakaraka. 11 Na malaika wa Mungu
akaniambia katika ndoto, Yakobo! Nikasema, Mimi hapa. 12 Akasema,
Inua, basi, macho yako, ukaone; mabeberu wote wanaopanda wanyama wana milia, na
madoadoa, na marakaraka; maana nimeona yote aliyokutendea Labani. 13 Mimi ni Mungu wa Betheli, huko ulikotia mafuta nguzo, na
kuniwekea nadhiri. Sasa ondoka, toka katika nchi hii, urudi mpaka nchi ile
uliyozaliwa.
Tatizo la Raheli
na Lea lilikuwa wazi
Kumbukumbu la Torati 5:16 Waheshimu baba
yako na mama yako;
Mwanzo 31:14-16 Raheli na Lea wakajibu, wakamwambia, Je! Imetubakia sehemu au urithi katika nyumba ya baba yetu? 15 Hakutufanya kama wageni, maana ametuuza, naye amekula fedha zetu kabisa? 16 Maana mali yote ambayo Mungu amemnyang'anya baba yetu, mali hiyo ndiyo yetu na ya wana wetu. Basi yo yote Mungu aliyokuambia, uyafanye.
Akiwa ameweka sawa mambo ya wake zake, na kufanikisha kuweka ushirikiano mzuri nao, Yakobo alijiandaa na kuondoka zake na kila alichokuwanacho, pasipo kumuarifu Labani.
Mwanzo 31:17-19a Ndipo Yakobo akaondoka, akapandisha wanawe na wakeze juu ya ngamia. 18 Akachukua wanyama wake wote, na mali yake yote aliyokuwa ameyapata, na wanyama aliowapata katika Padan-aramu, ili afike kwa Isaka babaye katika nchi ya Kanaani. 19 Basi Labani alikuwa amekwenda kuwakata manyoya kondoo zake, …
Ndipo mambo yalipojileta penyewe:
Mwanzo 31:19b … na Raheli akaviiba vinyago vya babaye.
Raheli aliiba miungu ya nyumbani mwao, sanamu—na kwa lugha ya Kiebrania., Teraphim. Hii inaonyesha kwamba vinyago vya Babeli na ibada zake vilikuwa bado vinatumika na kuabudiwa kwenye familia ya Labani. Na kwa kufanya kwao hivi, basi Raheli hakuwa mwaminifu sio kwenye amri hizi za Mungu tu, bali pia kwa wenzake wote.
Kumbukumbu la Torati 5:7 Usiwe na miungu mingine ila mimi
Yeye na wenzake wote mara hiyo waliivunja amri ya pili kwa kuwa na miungu ya kuchonga:
Kumbukumbu la Torati 5:8-10 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, au kilicho chini duniani, au kilicho majini chini ya nchi. 9 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao; hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 10 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu
Raheli,
Kumbukumbu la Torati 5:11 Usilitaje bure Jina la Bwana, Mungu wako; maana Bwana hatamhesabia kuwa
hana hatia, mtu alitajaye jina
Raheli na Lea waliivunja amri ya kwanza. Huenda hata sisi tunaweza kufikiri,
Kutoka 20:8-10 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
Isaya 56:1-8 Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatende haki; kwa
maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. 2 Heri
afanyaye haya, na mwanadamu ayashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje,
auzuiaye mkono wake usifanye uovu wo wote. 3 Wala
mgeni, aambatanaye na Bwana, asiseme hivi, Hakika yake Bwana atanitenga na watu
wake; wala towashi asiseme, Mimi ni mti mkavu. 4 Kwa
maana Bwana awaambia hivi matowashi, wanaozishika sabato zangu, na kuyachagua
mambo yanipendezayo, na kulishika sana agano langu; 5 Nitawapa
hawa nyumbani mwangu, na ndani ya kuta zangu, kumbukumbu na jina, lililo jema kuliko
kuwa na wana na binti; nitawapa jina lidumulo milele, lisilokatiliwa mbali. 6 Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa
watumishi wake; kila aishikaye sabato
asiivunje, na kulishika sana agano
langu; 7 Nitawaleta hao nao hata mlima wangu
mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na
dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote. 8 Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli
asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya hao walio wake
waliokusanywa.
Raheli aliiba miungu iliyokuwa kwenye nyumba ya baba yake.
Kwa ajili ya hasira, alishindwa kumheshimu baba yake wa
hapa duniani kwa kuwa myoni mwake alimuona ni
Kumbukumbu la Torati 5:16 Waheshimu baba yako na
mama yako;
Raheli,
Kumbukumbu la Torati 5:17 Usiue
Raheli aliivunja
pia amri ya saba. Na
Ezekieli 23:36-38 Tena Bwana akaniambia, Mwanadamu, utawahukumu Ohola na
Oholiba? Basi uwahubiri machukizo yao. 37 Maana
wamezini, na damu imo mikononi mwao, nao
wamezini na vinyago vyao; tena wana wao walionizalia wamewapitisha katika
moto ili waliwe nao. 38 Tena wamenitenda
haya; wamepatia unajisi mahali pangu patakatifu, siku ile ile, nao wamezitangua sabato zangu.
Kumbukumbu la Torati 5:18 Wala usizini.
Ni wazi kabisa kwamba Raheli aliivunja amri ya nane kwa kuiiba ile miungu.
Kumbukumbu la Torati 5:19 Wala usiibe
Raheli hakumwambia
Yakobo kwamba alikuwa amefanya hivyo,
Kumbukumbu la Torati 5:20 Wala usimshuhudie jirani yako uongo
Na ndivyo pia Lea alitoa ushahidi wa
uwongo kwenye jambo
Kumbukumbu la Torati 5:21 Wala usimtamani mke wa jirani yako; wala usiitamani nyumba ya jirani yako, wala shamba lake, wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala kitu cho chote alicho nacho jirani yako
Tumeona kwamba kwa wizi na udanganyifu wa Raheli na Lea hatimaye walifikia kwenye hatia ya kuzivunja amri zote Kumi za Mungu. Yakobo pia hakuwa mbali na tendo hili la wizi.
Mwanzo 31:20 Yakobo akamhadaa Labani, Mshami, kwa kuwa hakumwambia ya kwamba anakimbia.
Inajulikana
Mwanzo 31:22-31 Hata siku ya tatu Labani akaambiwa ya kwamba Yakobo amekimbia, 23 akatwaa ndugu zake pamoja naye, akamfuata mwendo wa siku saba. Akampata katika mlima wa Gileadi. 24 Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari. 25 Labani akamfikia Yakobo, na Yakobo alikuwa amepiga hema zake katika mlima, na Labani na ndugu zake wakapiga hema zao katika mlima wa Gileadi. 26 Labani akamwambia Yakobo, Umefanya nini? Umenihadaa, ukawachukua binti zangu kama mateka waliotwaliwa kwa upanga. 27 Mbona umekimbia kwa siri ukanihadaa, wala hukuniambia, nipate kuagana nawe uende zako kwa furaha, na nyimbo, na ngoma, na kinubi? 28 Wala hukuniacha niwabusu wanangu, na binti zangu; basi umetenda upumbavu. 29 Ninao uwezo mkononi mwangu wa kukufanyia madhara; lakini Mungu wa baba yako usiku huu ameniambia, akisema, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari. 30 Basi sasa, umetoka kwa sababu umetamani sana nyumba ya baba yako. Mbona basi umeiiba miungu yangu? 31 Yakobo akajibu, akamwambia Labani, Kwa sababu naliogopa, nikasema, Usije ukaninyang'anya binti zako kwa
Hapa tunaona uweza
wa Mungu wa Isaka kwa Labani, na akayatii maneno
aliyoyasema. Lakini licha ya yote haya bado alidai kurusi kwenye ibada na tumaini
Mwanzo 31:32 Awaye yote utakayemwona kuwa nayo miungu yako, yeye asiishi.
Mbele ya ndugu zetu ukitambue kilicho chako kwangu, ukakichukue. Maana Yakobo
hakujua ya kwamba Raheli ameiiba.
Bila kujua
Yakobo akamlaumu mkewe kipenzi
Mwanzo 31:33-35 Labani akaingia katika hema ya Yakobo, na hema ya Lea, na hema ya vijakazi wawili, wala hakuiona. Akatoka katika hema ya Lea, akaingia katika hema ya Raheli. 34 Basi Raheli alikuwa amevitwaa vile vinyago ameviweka katika matandiko ya ngamia, na kuvikalia. Labani akapapasa hema yote wala hakuviona. 35 Naye Raheli akamwambia babaye, Bwana wangu asikasirike kwa sababu siwezi kuinuka mbele yako, maana nimeshikwa na mambo ya kike. Akatafuta, wala hakuviona vile vinyago.
Baada ya Labani kushindwa kuviona hivyo vinyago, ilikuwa ni nafuu kubwa kwa Yakobo, na alijisikia kupata nguvu kuu sana kwa jambo hilo na akasema maneno makuu sana kwa Labani.
Mwanzo 31:36-43 Yakobo akakasirika, akagombana na Labani. Yakobo akajibu, akamwambia Labani, N'nini hatia yangu? Nayo ni nini dhambi yangu, hata ukanifuatia namna hii? 37 Umepapasa-papasa vyombo vyangu vyote; ni kitu gani ulichokiona cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya ndugu zangu, na ndugu zako, wakaamue kati yetu. 38 Miaka hii ishirini nimekaa kwako; kondoo zako wala mbuzi zako wake hawakuharibu mimba wala waume katika wanyama wako sikuwala. 39 Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea, mimi mwenyewe nimetwaa hasara yake, wewe umekidai katika mkono wangu, ikiwa kilichukuliwa mchana, au ikiwa kilichukuliwa usiku. 40 Hii ilikuwa hali yangu; mchana jua likanipata, na baridi usiku, usingizi ukanitoka machoni mwangu. 41 Miaka hii ishirini nimekaa nyumbani mwako; nilikutumikia miaka kumi na minne kwa binti zako wawili, na miaka sita kwa wanyama wako, nawe umebadili mshahara wangu mara kumi. 42 Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu. 43 Labani akajibu, akamwambia Yakobo, Hao binti ni binti zangu, na wana ni wanangu, na wanyama ni wanyama wangu, na yote uyaonayo ni yangu; nami naweza kuwatendea nini leo binti zangu na wana wao waliowalea?
Sasa Labani akagundua
kwamba amepoteza sababu na akajaribu kuuokoa uso wake kwa
weledi mkubwa
Mwanzo 31:43-55 Labani akajibu, akamwambia Yakobo, Hao binti ni binti zangu, na wana ni wanangu, na wanyama ni wanyama wangu, na yote uyaonayo ni yangu; nami naweza kuwatendea nini leo binti zangu na wana wao waliowalea? 44 Haya! Na tufanye agano, mimi na wewe, liwe kwa ushahidi kati ya mimi na wewe. 45 Yakobo akatwaa jiwe akalisimamisha kama nguzo. 46 Yakobo akawaambia ndugu zake, Kusanyeni mawe. Wakatwaa mawe, wakafanya chungu, nao wakala huko karibu na ile chungu. 47 Labani aliiita Yegarsahadutha, lakini Yakobo aliiita Galedi. 48 Labani akasema, Chungu hii ni shahidi kati ya mimi na wewe hivi leo. Kwa hiyo likaitwa jina lake Galedi, 49 na Mispa, maana alisema, Mungu avizie kati ya mimi na wewe, wakati tusipoonana. 50 Ukiwatesa binti zangu, na ukitwaa wake zaidi ya binti zangu, wala hapana mtu pamoja nasi, tazama, Mungu ni shahidi kati ya mimi na wewe. 51 Labani akamwambia Yakobo, Tazama chungu hii utazame na nguzo niliyoitia kati ya mimi na wewe. 52 Chungu hii na iwe shahidi, na nguzo hii na iwe shahidi, ya kuwa mimi sitapita chungu hii kuja kwako, wala wewe hutapita chungu hii na nguzo hii uje kwangu, kwa madhara. 53 Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba yao, ahukumu kati yetu. 54 Yakobo akachinja sadaka katika mlima, akawaita ndugu zake waje wale chakula, nao wakala chakula, wakakaa usiku kucha mlimani. 55 Labani akaondoka asubuhi na mapema, akawabusu wanawe na binti zake, akawabariki; kisha Labani akaenda zake, akarudi kwao.
Tunaacha matukio mfululizo ya Yakobo na Esau, Penieli na Dina, hadi kwenye mtangamano wa kila mahali na mwendelezo wa historia ya Yakobo alipokuwa huko Betheli ambako Yakobo aliviondoa vinyago vyote kutoka kwenye nyumba yote.
Mwanzo 35:1-3 Mungu akamwambia Yakobo, Ondoka, panda uende Betheli, ukakae huko; ukamfanyie Mungu madhabahu huko; yeye aliyekutokea ulipomkimbia Esau, ndugu yako. 2 Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, Ondoeni miungu migeni iliyoko kwenu, mjisafishe mkabadili nguo zenu. 3 Bwana akamwambia Yakobo, Urudi mpaka nchi ya baba zako na kwa jamaa zako, nami nitakuwa pamoja nawe.
Kipindi kinachofuatia
ni lazima kiwe ni cha mshtuko mkubwa
Mwanzo 35:4 Nao wakampa Yakobo miungu migeni yote iliyokuwa mikononi mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu.
Sababu ya kweli ya kuichukua miungu ile migeni inaweza kuwa kwamba malighafi iliyotumika kutengeneza vinyago vile haikuwa ni udongo wa kawaida wa mfinyanzi, bali kwa kweli ilitengenezwa kwa vitu vya dhahabu na fedha (sawa na Waamuzi 18:14). Tunaweza kudhania jambo hili pia kwa majibu waliyokuwa wakijibizana kina Lea na Raheli, binti za Labani na mawazo aliyokuwanayo Labani kwa Yakobo kama tulivyojionea hapo juu. Kulikuwa na hali halisi ya uchungu kwenye upande wa wana wa Labani na mjukuu wake kwa matendo aliyowatendea, na wote walijisikia kudanganywa. Kwa matendo haya aliwasababishia wote wazivunje amri. Labani ndiye aliyeanza kufanya udanganyifu na wizi na binti yake wa kwanza, Lea, aliyekubali kufanya kitendo kisicho cha haki. Kwa makusudi kabisa yeye aliingia kwenye tendo la uvunjifu wa amri na kumdanganya mume wake na mdogo wake, ambaye ndiye alikuwa wa kwanza kujaribu na kumdanganya mume wake na haki ya uzaliwa ya mtoto wake. Kwa vyovyote, hii ilimjumuisha baba yake. Wizi huu haukuheshimiwa na Mungu, ambaye mwishowe aliihamisha haki hii ya uzaliwa kwa wana wa Raheli kupitia kwa Yusufu. Reuben mzaliwa wa kwanza alimvunjia heshima baba yake, kwa kulala na Bilha suria wa baba yake (Mwanzo 35:22), na alisaidia kufanya madhara ya kuhamisha kwake. Jambo hili lilikuwa na madhara ya mbali ya urithi na haki ya uzaliwa wa kwanza ya makabila, na lilihukumiwa sawasawa.
Janga hili la kuzivunja Sheria, linahusika pia na uvunjaji wa majukumu yaliyo chini ya Sheria na maelekezo ya Torati, ambayo inahusisha pia na uvunjifu wa wajibu ulio chini ya Sheria ambayo inabidi ifuatwe na kwenye Agano Jipya, itokanayo na hali ya kutolitendea kazi au kulidharau Agano la kale. Nasaha iliyoko ni kwamba “msiwachokoze watoto wenu,” (Eph. 6:4; Col. 3:21).
Kupitia kwa Mikali, Daudi pia alipaswa ahusishwe na utumiaji wa kinyago nyumbani mwake. Hata hivyo, vilifanya kazi yake kwa kuyaokoa maisha yake (1Samweli 19:13). Kwa kujifunza maana ya miungu migeni na vikuku vya masikioni, basi jisomee majarida ya: Chanzo zha Uvaaji wa Ndewe Masikioni & Vito vya Dhahabu Siku za Kale (Na. 197) na Ndama wa Dhahabu (Na. 222) [The Origin of the Wearing of Earrings & Jewellery in Ancient Times (No. 197) and The Golden Calf (No. 222)].
Mwanzo 35:5-15 Wakashika njia, hofu ya Mungu ikaishika miji iliyowazunguka, wala
hawakuwafuata wana wa Yakobo. 6 Basi
Yakobo akafika Luzu, ulio katika nchi ya Kanaani, ndio Betheli, yeye na watu
wote waliokuwa pamoja naye. 7 Akajenga huko
madhabahu, akapaita mahali pale, El-Betheli; kwa sababu huko Mungu alimtokea,
hapo alipomkimbia ndugu yake. 8 Akafa Debora mlezi wa
Rebeka, akazikwa chini ya Betheli, chini ya mwaloni; na jina lake likaitwa Alon-bakuthi.
9 Mungu akamtokea Yakobo tena, aliporudi kutoka Padan-aramu
akambariki. 10 Mungu akamwambia, Jina lako ni Yakobo;
hutaitwa tena Yakobo, lakini Israeli litakuwa jina lako. Akamwita jina lake,
Israeli. 11 Mungu akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi,
uzidi ukaongezeke. Taifa na kundi la mataifa watatoka kwako, na wafalme
watatoka viunoni mwako. 12 Na nchi hii
niliyowapa Ibrahimu na Isaka nitakupa wewe, na uzao wako baada yako nitawapa
nchi hiyo. 13 Mungu akakwea juu kutoka kwake mahali
hapo aliposema naye. 14 Yakobo akasimamisha
nguzo mahali aliposema naye, nguzo ya mawe, akamimina juu yake sadaka ya
kinywaji, akamimina mafuta juu yake. 15 Yakobo akapaita
mahali pale, Mungu aliposema naye, Betheli.
Sasa tuko kwenye kilele cha mambo yote. Yakobo kwa mara nyingine tena anatamka hukumu ya kifo kwa Raheli,
pasipo kujua, na ilibakiwa
Bali hakuwa na la kufanya kwa kuitoa aina ile ya kiapo aliyoifanya bila
kuzingatia sheria na kanuni
Mwanzo 35:16-20 Wakasafiri kutoka Betheli, hata ukabaki mwendo wa kitambo tu kufika Efrathi, Raheli akashikwa na utungu wa kuzaa, na utungu wake ulikuwa mzito. 17 Ikawa alipokuwa anashikwa sana na utungu, mzalisha akamwambia, Usiogope, maana sasa utamzaa mwanamume mwingine. 18 Ikawa hapo katika kutoa roho yake, maana alikufa, akamwita jina lake Benoni, lakini babaye alimwita Benyamini. 19 Akafa Raheli, akazikwa katika njia ya Efrathi, ndio Bethlehemu. 20 Yakobo akasimamisha nguzo juu ya kaburi lake, ndiyo nguzo ya kaburi la Raheli hata leo.
Ni ukatili kiasi gani ulionekana kwa Raheli kufa akiwa anajifungua mtoto. Hata hivyo tunaweza kujenga hoja kwamba ilisababishwa na mazingira halisi ya maisha yake, kwa vile alivyoshindwa kujikabidhi kikamilifu kwa Mungu.
Mazingira
yanaweza kuwa yalimpelekea kwenye hali hii, kwa ajili
ya kiapo alichokifanya Yakobo bila kufikiria vizuri, na alichokifanya pasipo
sababu yoyete ya msingi. Inaweza kuchukuliwa kama
funzo la maafa mabaya
Ilikuwa ni kutokana na utakaso huu alioamuru Yakobo ambao ulikuwa ni neema iokoayo ya familia yake na fundisho kuu tunalojifunza kwenye andiko hili. Ni kwa kujitakasa tu na kumrudia Mungu ndipo tunawezakuwa ni sehemu taifa la Mungu, yaani Israeli. (soma pia jarida la Utarakaso na Tohara (Na. 251) [Purification and Circumcision (No. 251)]. Baada ya Yakobo kuiakasa familia yake, ambayo ilikuwa ni kiini au chanzo cha taifa la Israeli, huko Betheli, alibadilika na familia yake ilisamehewa na walichukuliwa kwenye wajibu au majukumu ya El-Betheli au El wa Nyumba ya El, ambaye ni Kuhani Mkuu au El Shaddai (sawa na Mwanzo 35:11).
Akaitwa jina
jipya la Israeli au utatawala
Licha ya baraka hizi, wakiwa njiani
wakitokea Betheli na kabla hawajafika Efrati, Raheli alikufa baada ya kumzaa
mwanae wa pili. Akamuita mtoto wake Benoni (SHD 1126) ambalo maana yake ni mwana au mtoto wa huzuni yangu. Katika
mtoto wake huyu wa mwisho wa Yakobo, ambaye sasa ni Israeli,
safari
Ilikuwa ni kutoka kwenye mchakato huu wa kutoka Betheli, ambapo
maana yake ni Nyumba ya Mungu, ambapo tunaona makusudio ya habari hii. Israeli na watu wote wa nyumbani mwake walitakaswa kwa uingilio
alioufanya Kuhani Mkuu au El Bethel. Kwenye uzaliwa wa
mtoto na kufa kwa mwanamke tunapata wazo la ahadi ya haki ya uzaliwa wa kwanza
kwa Kanisa na ua uwana wa ahadi. Kupitia kwenye jina lile la wana wa huzuni kunabadilika
na kuwa wana wa ahadi. Walipokuwa
njiani kuelekea Efrath alikufa
na akazikwa karibu na Bethlehemu mahali ambako
alijionyesha mfano kwa wana wa ahadi na kwa mwana wa Yuda ambaye ni Masihi.
Alikuja alitokea Bethelehemu ya Epratha,
uliye mdogo ssana katika majumbe wa Yuda. Wana wa Lea waliungana na wana wa Raheli, kwa kuwa fimbo ya
kifalme itatoka katika Yuda na haki ya uzaliwa wa kwanza wa itatoka kwa Yusufu.
Wana wa ahadi wanapaswa kuwa ni wale wote walio kwenye
koo za Israeli na wa mataifa yote ya dunia wanapaswa waungane nao kwa utakaso
Tunaweza
kujifunza somo muhimu
§ Unapaswa kuwa mwangalifu kilamara unapoweka nadhiri au kula kiapo au unapokuwa unaomba. Mara nyingi kiapo au nadhiri itatiizwa sawasawa na jinsi ulivyoiweka, hata hivyo, kuwa inatokea tofauti kwenye mazingira tofauti na vile ilivyotarajiwa.
§
Kwa kuivunja amri moja tu, basi Torati yote
itakuwa imevunjwa kwa mapatilizo makubwa
§
Kuishika amri ya kwanza kwa
mahali pa kwanza,
§
Kila kinachoonekana
§ Unapaswa kila mara kuwa makini na maagizo ya Torati.
§ Fundisho kuu ni kwamba hatujahesabiwa haki kwa jinsi tujionavyo kwa macho yet una tunahukumiwa kwa matendo yetu.
§ Tunatengwa na kukosa haki yetu kwa ajili ya dhambi, lakini pia hatuhesabiwi haki kwa Sheria.
§ Tunaokolewa kwa Neema.
§ Mungu ametuahidi kupitia kwa mababa zetu wa imani kwamba hatutashindwa.
§ Tunazishika amri za Mungu kwa kumpenda yeye na kwa kuwa alijifunua kwetu sisi yeye mwenyewe kama alivyofanya, kupitia kwa El Betheli na Masihi, kwa wote wawili, yaani kwa mababa wa imani na kwa Kanisa.
Ufunuo 14:12 Hapa ndipo penye subira ya
watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.
Jitahidi kuyajua yale yaliyotokea kwa habari kugundulika kwa familia ya makabila ya Israeli na mazingira yale ambayo yaliathiri kuendelea kuwepo kwayo, hata katika maisha ya Raheli na kuwepo kwa wana wa Israeli kwenye haki ya uzaliwa wao. Raheli aliruhusiwa afe ili kwamba sisi tuwe na mfano wa imani na ahadi kwa Israeli ya Masihi na ya Kanisa.
Waebrania 11:6 Lakini
pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu
amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale
wamtafutao.
q