Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[282D]
Utawala wa Wafalme
Sehemu ya IIIB:
Mtu Kama Hekalu la Mungu
(Toleo La 1.0 20120326-20120326)
Kwenye Sehemu ya III (A) tuliona Ufunguo wa Daudi na nafasi
ya Sulemani kwenye Hekalu la Mungu
na nafasi yake katika ujio
wa Masihi. Kwenye sehemu hii tutaona
HeKalu la Kiroho la Mungu ndani ya mwanadamu na jinsi
linavyohusiana na mfumo wa nasaba
damu ujulikanao kama DNA wa wanadamu
na uhusiano wa vitabu vya
Biblia katika kuelezea mpango wa Wokovu
na Hekalu la Mungu likiwa kama
uumbaji wa mwanadamu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
2012 Wade Cox)
(Tr.
2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna
malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu
fupi zaweza kuwekwa toka kokote
ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila
kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu
ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Utawala wa
Wafalme Sehemu ya IIIB: Mtu Kama Hekalu la Mungu
Kwenye jarida la Utawala wa Wafalme Sehemu ya III; Sulemani na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C) hekalu na Ufunguo wa Daudi vimeelezewa na kufafanuliwa lakini muundo wa Hekalu ama utaratibu wake kama Nguvu za Kiroho ndani ya Mwanadamu haikuelezewa na hata haikuelezewa kuhusu jukumu la Biblia kama neno la Mungu haikuelezewa pia. Jarida hili linachukua Sehemu ya III katika kuelezea kuhusu Hekalu la Kiroho na linafafanua kuhusu Biblia na uhusiano wake na Hekalu.
Biblia imetengenezwa kwa mjumuisho wa vitabu 66 vilivyogawanywa kwa sehemu mbili kuu zinazojulikana kama Agano la Kale na Agano Jipya ingawa hapo mwanzoni ilichapishwa kwenye tafsisiri ya KJV katika migawanyo sita ambazo ni tarakimu ya kibinadamu.
Muundo wa Biblia ni:
Agano la Kale
Mgawanyo wa Agano la Kale unajumuisha vitabu 12 kutoka kitabu cha Mwanzo
hadi 2Wafalme, kisha vitabu vingine 14 na 1 na 2Mambo ya Nyakati. Idadi hii ina maana
yake katika kufanya migawanyo miwili ya saba inayokamilisha idadi na kufanya
jumla ya 14.
Marejesho ya utaratibu wa maongozi
ya Torati yalikuwa yamekwisha kamilika kwenye kitabu cha
15 na cha 16 vilivyoandikwa na Ezra na Nehemia. Utaratibu wa ukamilishaji wa Hekalu ulikuwa kwenye kitabu cha
22 kinachoishia kwenye Wimbo Uliobora. Alfabeti za Kiebrania ziko
22 zinazomaanisha hitimisho.
Kitabu cha 23 kilikuwa cha nabii Isaya. Kwenye Isaya 53:4-5 tumepewa utaratibu na maana
ya Masihi ambaye ndiye alikuwa Mwanzilishi
wa Hekalu la Kiroho na Kuhani wake Mkuu. Lilikuwa ni andiko hili ambalo Towashi
wa Kihabeshi alikuwa akilisoma na likafafanuliwa maana yake na
Filipo na kisha akabatizwa na akapewa
uweza wa kumpokea Roho Mtakatifu. Hatimaye
Filipo akatwaliwa na kutoweka machoni pake kimiujiza.
Tarakimu au nambari hii
inafikia kuonysha maana ya mwanadamu kwenye Nyanja za uumbaji. Ni kitabu cha 23 kwenye Biblia na kinauhusiano wa kitarakimu na
ya Kromosomu kwenye mwili wa mwanadamu
na inafanya mrejesho wa DNA ya mfumo wa Mwanadamu
ambayo kwayo mwanadamu aliumbwa kwayo ili aweze
kumpokea Roho Mtakatifu kwa
kupitia dhabihu aliyojioa Kristo na inajumuisha vipengele 46 za mateso ya Kristo ambazo ni idadi ya pea za mfumo wa
DNA ya Mwanadamu na inawakilishwa kwa Nguzo za Hekalu la Mungu
kama tutakavyojionea hapo chini.
Agano hili la Kale linaendelea kwa kutukumbusha Manabii Wakuu pamoja na Yeremia na Maombolezo na
pia vitabu vya Ezekieli na Danieli ambali waliongelea sana kuhusu muundo wa
Uumbaji na ukamilishaji wa sehemu au awamu
ya Kwanza hadi kwenye Ufufuo wa
wafu wa Kwanza
ambapo ni Naos au Patakatifu pa Patakatifu.
Hivyo ni vitabu 27 hadi kufikia mahali
hapa. Awamu inayofuatia kwenye Manabii Wadogo 12 wanaoshughulika na mwisho wa awamu
ya Kwanza na ujenzi wa Hekalu la Milenia litakalotumika kipindi cha Masihi. Kwa hiyo, Agano la Kale linahitimika kwa jumla ya vitabu
39 vya kazi iliyovuviwa vyote.
Agano Jipya
Agano Jipya ni mjumuisho wa Injili
Nne na Kitabu
cha Matendo ambazo ni vitabu vitano vinavyotangulia hadi kufikia siku
watu walipompokea Roho
Mtakatifu wa Neema kwenye kitabu cha Matendo
ya Mitume, na kuanzishwa ramsi kwa Kanisa la Mungu kama Hekalu la Mungu.
Kisha kuna nyaraka nyingine za Makanisa Saba zinazohitimisha idadi ya vitabu vinane zinazoonyesha mwingiliano wa kimahusiano na Makanisa Saba ya Mungu.
Nyaraka za Wakorintho na
Wathesalonike kama kazi mbili zinafanya
kuwa na jumla ya vitabu tisa. Waraka wa 1Wakorintho ni kitabu cha 46 ambacho kinatueleza sisi kuwa sisi tu Naos au Hekalu la Mungu. Tarakimu ya 46 ni kipimo cha Nguzo za
Hekalu la Mungu na pia ni tarakimu
ya pea kwenye vijino vya DNA na inaonyesha
ukweli wa kuumbwa kwa mwanadamu
akiwa na kipimo nasaba kamili
cha mfumo wa DNA kama Hekalu
la Mungu na inatuonyesha kusudi la uumbaji wa wanadamu
wote. Nguzo mbili zinaonyesha aina mbili za DNA na kipomo
X na Y cha nasaba ya ute au
kromosomu: X kwenye kipima nasaba cha
mtDNA cha mwanamke na Y cha
mfumo YDNA ya mwanaume.
Sehemu au mgawanyo wa
mwisho ni ule wa Vitabu Kumi na Viwili vya
mfuatano wa nyaraka walizoandikiwa watu binafsi tangu
nyaraka za I na II za Timotheo, Tito,
Filemoni, Waebrania, Yakobo,
I na II Petro, I, II na III
Yohana, Yuda ambazo zinafanya
kuwa na jumla ya vitabu 65. Yuda alikuwa ni Ndugu yake Kristo na ndiye aliyeelezea
juu ya Imani Iliyotolewa Mara Moja tu ambayo
ndiyo makusudi au malengo ya maandiko
yaliyovuviwa na ndiyo iliyofanya waraka wa kumi
na mbili wa watu binafsi.
Kumi na mbili ni tarakimu ya ukamilifu.
Kitabu cha Ufunuo ni cha
27 kwenye Agano Jipya na ni
cha 66 cha vitabu vya maandiko
yaliyovuviwa zikimaanisha ukamilifu wa uumbaji
wa mwanadamu. Kumi na Tatu ni tarakimu inayomaanisha au kuashiria Uasi na kitabu hiki
cha Ufunuo ni cha nne katika
vitabu alivyoviandika Mtume Yohana, ambapo wakara wa IYohana
unaanza kwa kuionyesha Nuru na ushirikiano wa mwanadamu na Mungu
na Kristo ambaye alikuwa ni mtetezi kwa Baba wa watenda
dhambi wote. Sura ya 2 inaelezea umuhimu wa kuzishika amri
za Mungu na kwa mtu
kama huyo upendo wa Mungu unakamilika
na dhambi za ulimwengu zinashindwa
kwa uweza wa Roho Mtakatifu ambaye ni mwalimu wa watu
wote. Sura ya 3 inaonyesha kwamba kwa kupitia
ushindi huo sasa tunakuwa wana
wa Mungu na ulimwengu hautujui.
Kwenye kifungu cha sura ya 3:4 tunaambiwa kwamba dhambi ni kile kitendo cha
kuzivunja amri na hatutaweza kujiepusha
na dhambi hadi pale tutakapozishika sheria na amri
hizi. Mtume Yohana anaelezea kwenye nyaraka zake akutuandaa
sisi kwa ajili ya Siku za Mwisho. Ufunuo ambao ni kitabu cha Kumi na Tatu kwenye mlolongo huu na ni kitabu
cha mwisho kina idad ya Uasi huu.
Ufunuo ni ujumbe ulioandikwa kwa ajili ya Makanisa Saba ya Asia. Kinatuonyesha
kuwa sisi tumefanyika kuwa wafalme na makuhani
kwa Mungu wetu. Kinamtaja kuwa ni Alfa na Omega, Bwana aliyeelezewa kwenye maandiko (soma jarida la Ustadi wa Kazi ya Uumbaji
wa Mungu kama Alfa na Omega (Na. 229) [Arche of the Creation of God as Alpha and Omega (No. 229)]. Sura za 2 na 3 zinashughulikia matatizo yaliyojitokeza kwenye Makanisa Saba, yakwa kama kielelezo cha tangu wakati
huo hadi kuja kwa Masihi. Tangu sura ya 4 tunakiona kiti cha Enzi cha Mungu
na roho saba za Mungu ambazo
ni miongoni mwa makanisa saba. Vitabu vya Mihuri Saba ndipo sasa vinafunguliwa na Mwanakondoo anaonekana kuwa ndiye anayestahili kuzifungua Siri za Mungu, na
athari mbaya za Dini ya Uwongo zinafunuliwa kutoka kwenye ile Mihuri
Saba hadi kwenye Mhuri wa Tano na
Ujio wa Masihi kuja kuwaokoa wanadamu
kutoka kwenye yenyewe na kuanza kwa Utawala au
Ufalme wa Mungu kupitia kwa
Roho Mtakatifu chini ya Masihi
nao unaelezewa kwa kina. Uasi unaotokana na uangamivu mkubwa
na kuangamia kwa wale waliokuwa
kwenye uasi na Ufunuo 12:17 na 14:12 inatuonyesha kwamba wateule wa Mungu ni wale
wanaozishika Amri au Sheria
za Mungu na Ushuhuda au
Imani ya Yesu Kristo. Imani potofu ya dini ya uwongo ya mfumo wa Kibabeli
ya siri na ambayo ndiyo unatawala
dunia pamoja na uharibifu wake
imeelezewa kwenye sura za 18 na 19 tunaziona,
kutoka kwenye uangamivu wake, mwendelezo na kuziabudu
mbingu kwenye Ufalme wa Mungu na
Karamu ya Arusi ya Mwanakondoo,
ikifanywa na wateule wakiwa wametengwa mbali na kutokuwa na
sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza
wa wafu. Kwenye Sura ya 20 mwandamano wa matukio ya ufufuo
wa Kwanza na wa Pili nay
a Kiti cha Enzi, Kikubwa
Cheupe cha Hukumu vinaelezewa na mwandamano wa matukio
haya unaishia kwenye Sura za 21 na 22 kwa
kuonyeshwa Mji wa Mungu na
madhumuni au malengo ya uumbaji wa kila kilichoko
duniani yanafunuliwa kwenye fumbo au
Siri za Mungu. Mchakato wote mkamilifu unafunuliwa kwenye Sura ya 22 kwa Roho Mtakatifu kutufanya sisi sote kuwa ni wana wa Mungu pamoja
na Malaika wa Mbinguni na uumbaji wa
vitu vyote vya kimwili unaishia
kwa vitabu hivi 66 na nia
yake yote ikiwa imeelezewa. Mlolongo unaofuatia haujaelezewa bado kama unavyokwenda kuwa kwenye uumbaji na Viumbe wa
Kiroho jinsi utakavyokuwa na kuenea ukiwa kama
ni mchakato wa Saba kwenye sehemu nyingine
kumi na mbili
ambazo hazijaandikwa bado ukiwa kama
mambo ya mwisho ya Ufunguo wa Daudi kwenye Hekalu la Kiroho la kwenye Mji wa Mungu.
Sasa tutarejea kwenye Sehemu ya III (A) ili kutathmini sehemu ya Hekalu la Sulemani.
“Daudi alimuamuru Sulemani katika mwaka wa Kwanza
wa Yubile ya 61. Maandalizi yalianza ili kwamba Hekalu
liweze kujengwa kwa ajili yha
Usomaji wa Torati uliotarajiwa kufanywa kwenye Yubile ile.
Iligharimu muda wa miaka takriban ishirini kukamilisha ujenzi wa Nyumba ya Bwana na nyumba ya Mfalme
na nyumba nyingine zilizojiri (tazama hapo chini).
Ukamilishaji wake hii yote ulifanyika
katika mwaka wa 25 wa yubile
ya 61.
Hekalu lilianza mnamo mwaka wa Arobaini wa utawala wake
Sulemani, ambao ni mwaka wa 968 KK.
Ujenzi wote na kuikamilisha
Nyumba ya Mungu kwa kumalizia majengo mengine yaliyohitajika kulikamilika mnamo Mwezi wa Saba ulioitwa mwezi wa Ethanimu, au wa Tishri, na
Sikukuu iliadhimishwa kwa siku 14.”
Maskani yenyewe asilia na utoaji wa
sheria vilifanyika kwa zaidi ya miezi
sita na Musa alikuwa na kazi kubwa
ya kupanda mlimani na kushuka mara sita na aliimaliza kazi
yake yote mnamo mwishoni mwa mwezi wa
Eluli ili kwamba mwezi wa
Ethanimu utakaswe na kubakia kuwa Mtakatifu tangu Siku
ya Upigaji wa Baragumu. Mwezi wa Siwani uliwakilisha mwanzo wa utoaji wa
sheria na ilikuwa imekamilika katika mwezi wa
Eluli. Idi ya Ukumbusho wa kuzipiga Baragumu ilikuwa ni taswira ya Ujio wa Masihi katika Mwezi wa Saba ili kuja kuanzisha
Milenia ya Saba tangu Uumbaji
(soma pia jarida la Upangaji
Mlimani wa Musa (Na. 070)
[The Ascents of Moses (No. 070)].
Hekalu la Kwanza hata hivyo
lilikuwa halijaisha bado hadi kufikia
Sikukuu ya Vibanda.
Kuendelea kutoka Sehemu ya III (A)
“Ni kama tuonavyo hapo
chini, ujenzi halisi wa je jengo
lenyewe ulichukua miaka saba na miezi
saba na ulikamilika katika mwezi Nane wa mwaka wa
Kumi na moja wa utawala wa Sulemani. Kwa hiyo ukamilishaji wake haukuwa kipindi
muafaka kwa maadhimisho ya Sikukuu ya Vibanda ya mwaka ule. Kwa hiyo, kuna maana nyingine kwa ajili ya kipindi
hiki. Hekalu lilifuatia baada ya Idi ya Pasaka, katika mwezi wa Pili wa
mwaka wa Nne wa Sulemani na liliisha mwezi
wa Nane wa Buli, au wa Heshavan
(katikati ya Octoba/Novemba ya mwaka wa 487 tangu kipindi
cha Kutoka kwao utumwani, ukiwa ni mwaka 961 KK).”
Mwandamano huu wa kipindi
maalumu unaunda pia sehemu ya ufunguo
wa Daudi. Vipindi maalumu vilivyotajwa kwa kuvitenganisha pia vina maana yake kwa ajili
ya kipindi cha Siku za Mwisho cha
tangu kurudi kwa Masihi na kuanzisha
Hekalu la Kiroho, na hitimisho la mwisho la utawala wa kimwili
na utaratibu wa Hekalu huko
Yerusalemu.”
Kwa hiyo, Ufungua wa
Daudi ni sehemu pia ya mlolongo wa kipindi
na taswira ya Ujenzi wa Hekalu la kimwili na la Kiroho
linaloelekea kwenye wongofu wa watu
wa Mataifa na kuona jinsi
watakavyopata nafasi sawia au kukubalika
kwenye Hekalu ambalo ni
Kanisa la Mungu.
“Katiika mwaka wa
28 na wa yubile, Torati ilisomwa kwenye Nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Kipindi chote kizima cha ujenzi kilijiri
miaka 21 ya Utakaso wa Hekalu, na
mwaka wa Sabato ulikuwa tayari. Mwaka wa 29 ulipelekea kwenye Yubile na
ambao taifa lilikuwa limetakasika kwa kipindi kile chote pia. Kwa hiyo ilikuwa
ni miaka elfu tatu hadi kuanzishwa
kwa utawala wa millennia wa
Yesu Kristo katika Yubile ya 120 ya tangu uumbaji kutoka
ilipofungwa Bustani ya Edeni ambao
ni aawa na mwaka 2027BK.
Yubile 60 ziliyosuatia ziliweka taswira ya ujenzi wa taratibu wa
kimwili wa Kanisa na wa utawala
wa serikali ya Mungu. Ni wazi kwamba Mungu anajishughulisha kipekee kwenye utaratibu wa Yubile
na anavitumia vipindi vya Yubile
kwa mgawanyo wa kitarakimu wa
10, 20 na 40.
Kutoka kwenye maandiko ya Agano la Kale
ni wazi sana kwamba Masihi alipaswa kuinuliwa kwenye Yubile ya mwaka 27BK na huduma
yake ianze rasmi mwaka 28BK. Ilimpasa afe ili
awaokoe wenye dhambi. Ni sawa tu na ilivyo wazi
kabisa kwamba ilimpasa kufanya Upatanisho na kisha
arusi tena akiwa kama Mfalme Masihi. Kipindi hiki maalumu kilipasa
kichukue miaka elfu sita ya uumbaji wa Mungu na kuishia
na Yubile ya 120 mnamo mwaka 2027.
Tangu wakati ule, kipindi
cha Utawala wa Masihi kingeanza
tangu mwaka 2028 hadi mwaka 3027, kipindi kijulikanacho kama ni mapumziko ya Sabato ya Masihi. Baada ya kipindi hicho kitafuatiwa
na cha Hukumu
itakayofuatiwa na Ufufuo wa Pili wa wafu au
wa Wote waliokufa
Mautini.
Maandiko yanasomeka yakisema hivi:
1Wafalme 6:1-38 Ikawa katika mwaka wa mia nne na themanini baada ya kutoka wana wa Israeli katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa kutawala kwake Sulemani juu ya Israeli, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa pili, akaanza kuijenga nyumba ya Bwana. 2 Nayo nyumba hiyo mfalme Sulemani aliyomjengea Bwana, urefu wake ulikuwa mikono sitini, na upana wake ishirini, na kwenda juu kwake mikono thelathini. 3 Na ukumbi mbele ya hekalu la nyumba, urefu wake ulikuwa mikono ishirini, kadiri ya upana wa nyumba; na upana wake mikono kumi mbele ya nyumba. 4 Akaifanyia nyumba madirisha ya miangaza yenye kimia. 5 Nao ukuta wa nyumba akauzungushia vyumba, kushikamana na kuta za nyumba kote kote, za hekalu na za chumba cha ndani; akafanya vyumba vya mbavuni pande zote. 6 Chumba cha chini kilikuwa mikono mitano upana wake, na chumba cha katikati kilikuwa mikono sita upana wake, na chumba cha tatu kilikuwa mikono saba upana wake; kwa kuwa upande wa nje akaupunguza ukuta wa nyumba pande zote, ili boriti zisishikamane kutani mwa nyumba. 7 Na nyumba ilipokuwa ikijengwa, ikajengwa kwa mawe yaliokwisha kuchongwa chimboni; wala nyundo, wala shoka, wala chombo cha chuma cho chote, sauti yake haikusikiwa ilipokuwa ikijengwa nyumba. 8 Mlango wa vyumba vya chini ulikuwapo upande wa kuume wa nyumba; mtu hupanda madaraja ya kuzunguka mpaka vyumba vya katikati, na kutoka vile vya katikati mpaka vile vya tatu. 9 Basi ndivyo alivyoijenga nyumba, akaimaliza; akaifunika nyumba kwa boriti na mbao za mwerezi. 10 Akavijenga vyumba mbavuni mwa nyumba yote, kwenda juu kwake kila kimoja kilikuwa mikono mitano; vikaitegemea nyumba kwa boriti za mwerezi.
Mawe ya kujengea Hekalu yalikuwa yanachongwa au kuandaliwa sehemu
nyingine mbali na uwanja linapojengewa
na yaliletwa kwenye eneo la ujenzi. Na ndivyo
ilivyo kwamba mawe yaliyohai yamekwisha tengenezwa tayari kutoka maeneo
yaliyo mbali na Yerusalemu na
yanaletwa huko ili kuanzishwa kwa Hekalu la Kiroho wakati atakaporejea Kristo. Yako alisia na makamioifu
na hayahitaji kuchongwa tena yajapo kwenye uwanja wa
ujenzi, kisha yajengewe na takataka
zikiwa zimejichanganya pamoja nayo.
Kwahiyo kuna aina mbili za ujenzi ; moja ni kwenye uanzishaji wa haya Mawe yaliyo
Hai; na mwingine ni ule wa utaratibu
wa maongozi ya kimwili wa chini
ya maongozi ya Torati kutoka Yerusalemu.”
Mambo mawili tofauti ya utaratibu au muundo
yalikuwa ni wa kimasharti ya mtu kuwa mtiifu kwenye neno
la Mungu ambalo lenyewe tu kama lilivyo lilitaswirisha uumbaji na lengo
la uumbaji huo kwa mionekano ya namna mbili, ya vitabu 66 vya neno
la Mungu ambalo ndilo lengo ambalo
Kristo alikuja kwa muonekano wa namna
mbili, mmoja kama Malaika wa Uwepo wake au Memra
na mwingine ni kama Mwana wa Adamu akiwa ni Neno au Logos anayeonekana kimwili. Tunaendelea mbele kwenye Sehemu ya III (A).
“Kwenye ukenzi wa
Hekalu neno la Mungu ndipo alipewa Sulemani, aweke agano imara kwa Israeli kulikuwa ni lazima katika kuonyesha
kwake utii.
11 Neno la Bwana likamjia Sulemani, kusema, 12 Katika habari ya nyumba hii unayoijenga, kama ukienda katika sheria zangu, na kuzifanya hukumu zangu, na kuzishika amri zangu zote na kwenda katika hizo; ndipo nitakapolithibitisha neno langu kwako, nililomwambia Daudi baba yako. 13 Nami nitakaa katikati ya wana wa Israeli, wala sitawaacha watu wangu Israeli. 14 Basi Sulemani akaijenga hiyo nyumba akaimaliza. 15 Akazijenga kuta za nyumba ndani kwa mbao za mwerezi; toka sakafu ya nyumba hata boriti za juu, akazifunika ndani kwa mti; akafunika sakafu ya nyumba kwa mbao za mberoshi. 16 Akajenga mikono ishirini pande za nyuma za nyumba toka chini hata juu kwa mbao za mwerezi; naam, ndani akaijengea chumba cha ndani, yaani, patakatifu pa patakatifu. 17 Nayo nyumba, ndiyo hekalu la mbele, ilikuwa mikono arobaini. 18 Na ndani ya nyumba, mlikuwa na mwerezi ulionakishiwa maboga na maua yaliyofunuka wazi; mlikuwa na mwerezi mahali pote; wala mawe hayakuonekana. 19 Akaweka tayari chumba cha ndani katikati ya nyumba ndani, ili atie humo sanduku la agano la Bwana. 20 Na ndani yake chumba hicho cha ndani mlikuwa na nafasi, mikono ishirini urefu, na mikono ishirini upana, na mikono ishirini kwenda juu kwake; akaifunika na dhahabu safi. Akaifunika madhabahu nayo kwa mwerezi. 21 Hivyo Sulemani akaifunika nyumba ndani kwa dhahabu safi. Akaitenga kwa mikufu ya dhahabu mbele ya chumba cha ndani; akapafunika na dhahabu. 22 Akaifunika nyumba yote kwa dhahabu, hata ilipokwisha nyumba yote; tena madhabahu yote iliyokuwa ya chumba cha ndani akaifunika kwa dhahabu. 23 Akafanya ndani ya chumba cha ndani makerubi mawili ya mzeituni, kwenda juu mikono kumi. 24 Na bawa moja la kerubi lilikuwa mikono mitano urefu wake, na bawa la pili la kerubi mikono mitano; mikono kumi toka mwisho wa bawa moja hata mwisho wa bawa la pili. 25 Na kerubi la pili lilikuwa mikono kumi; makerubi yote mawili walikuwa ya cheo kimoja na namna moja. 26 Kwenda juu kwake kerubi moja kulikuwa mikono kumi, na kerubi la pili vivyo. 27 Akayaweka hayo makerubi katika nyumba ya ndani; na mabawa ya makerubi yakanyoshwa, bawa la moja likafika ukutani huko, na bawa la kerubi la pili likafika ukutani huko; mabawa yao yakagusana katikati ya nyumba. 28 Akayafunika makerubi kwa dhahabu. 29 Akazinakshi kuta zote za nyumba kwa nakshi za makerubi, na mitende, na maua yaliyofunuka wazi, pande za ndani na nje. 30 Na sakafu ya nyumba akaifunika na dhahabu ndani na nje. 31 Akayafanyia maingilio ya chumba cha ndani milango ya mzeituni; kizingiti na miimo ilikuwa ya pande tano. 32 Hivyo akafanya milango miwili ya mzeituni; akanakshi juu yake nakshi za makerubi, na mitende, na maua yaliyofunuka wazi, akaifunika kwa dhahabu; akatia dhahabu juu ya makerubi, na juu ya mitende. 33 Ndivyo alivyoyafanyia maingilio ya hekalu miimo ya mzeituni, yenye pande nne; 34 na milango miwili ya mberoshi; mbao mbili za mlango mmoja zilikuwa za kukunjana, na mbao mbili za mlango wa pili za kukunjana. 35 Akanakshi juu yake makerubi, na mitende, na maua yaliyofunuka wazi; akazifunika kwa dhahabu iliyonyoshwa juu ya machoro. 36 Akaijengea behewa ya ndani safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi. 37 Katika mwaka wa nne nyumba ya Bwana ilitiwa msingi, katika mwezi wa Zivu. 38 Hata katika mwaka wa kumi na mmoja, katika mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, nyumba ikaisha, mambo yake yote, na sharti zake zote. Basi muda wa miaka saba alikuwa katika kuijenga.
Hii ni hatua ya kwanza ya mafuatano ya Ufunguo wa Daudi na inahusiana na
utaratibu wa kwanza, ambao ni Nyumba ya Mungu iliyojengwa kwa Mawe Yaliyohai,
na mlolongo ule unahusiana na kurudi kwa
Masihi na hitimisho lake kwa Mataifa.”
“Nyumba ya Sulemani ilijengwa kwa kipindi cha
miaka kumi na mitatu; kisha
akajenga nyumba kutokana na miti
iliyotoka kwenye Misitu ya Lebanoni pia. Hekalu ndilo
lilikuwa juhudi yak kubwa alipoiweka na hadi kukamilika
kwake lilijengwa kwa jumla ya miaka
ishirini. Na pia alimchukua binti wa Farao
na kumuweka nyumbani mwake mwenyewe kama mke
wake.
Mlolongo huu wa matukio
kama tunavyouona, ulichukua miaka saba na miezi saba kwa
Nyumba ya Mungu na kisha miaka
mingine mitatu kwa ajili ya Nyumba
ya Mfalme, Ukumbi wa kutolea Hukumu,
na Nyumba ya Misitu ya Lebanoni.
1Wafalme 7:1-51 Naye Sulemani alikuwa katika kuijenga nyumba yake mwenyewe miaka kumi na mitatu, akaimaliza nyumba yake yote. 2 Kwa kuwa aliijenga nyumba ya mwitu wa Lebanoni; mikono mia urefu wake, na mikono hamsini upana wake, na mikono thelathini kwenda juu kwake, juu ya safu nne za nguzo za mwerezi, na mihimili ya mwerezi juu ya nguzo. 3 Ikafunikwa juu kwa mwerezi juu ya mihimili arobaini na mitano, iliyokuwa juu ya nguzo; kumi na mitano kwa safu. 4 Na madirisha yalikuwako safu tatu, mwangaza kuelekea mwangaza katika madaraja matatu. 5 Na milango yote na miimo ilikuwa ya mraba, ilivyoangaziwa; na mwangaza kuelekea mwangaza katika madaraja matatu. 6 Akaifanya baraza ya nguzo; mikono hamsini urefu wake, na mikono thelathini upana wake; na ukumbi mbele yake; na nguzo na mihimili minene mbele yake. 7 Akaifanya baraza ya kiti cha enzi, ili ahukumu ndani yake, ndiyo baraza ya hukumu; nayo ikafunikwa mwerezi tangu sakafu mpaka dari. 8 Nayo nyumba yake atakayokalia, katika behewa nyingine iliyokuwa ndani kupita baraza, ilikuwa ya kazi kama hiyo. Tena akamjengea nyumba binti Farao, (ambaye Sulemani alikuwa amemwoa), mfano wa ile baraza. 9 Hizi zote zilikuwa za mawe ya thamani, mawe ya kuchongwa, sawasawa na cheo, yaliyokatwa kwa misumeno, ndani na nje, tangu msingi hata mawe ya juu, na nje vile vile hata behewa kuu. 10 Nao msingi ulikuwa wa mawe ya thamani, mawe makubwa, mawe mikono kumi, na mawe ya mikono minane. 11 Na juu kulikuwa na mawe ya thamani, mawe ya kuchongwa, sawasawa na cheo, na mierezi. 12 Na behewa kubwa pande zote ilikuwa na safu tatu za mawe ya kuchongwa, na safu moja ya mihimili ya mierezi; mfano wa behewa ya ndani ya nyumba ya Bwana, na ukumbi wa nyumba.
Hiramu alimsaidia kwenye ujenzi huu. Huyu Hiramu alikuwa nusu Muisraeli. Baba yake
alikuwa ni mtu wa Tiro na mama yake alikuwa ni mjane kutoka kabila la Naftali.
Kwa hiyo yalikuwa ni mataifa rafiki na yanayoshirikiana pia na washirika wa
kuaminika wa Israeli na leo ni kama tunavyojionea kwenye maandiko yaliyotajwa
hapa chini.
13
Mfalme Sulemani
akatuma watu kumleta Huramu kutoka Tiro. 14 Naye
alikuwa mwana wa mwanamke mjane wa kabila ya Naftali, na babaye alikuwa mtu wa
Tiro, mfua shaba; naye alikuwa mwingi wa hekima na akili, mstadi wa kufanya
kazi zote za shaba. Akamfikilia mfalme Sulemani, akamfanyia kazi yake yote. 15 Kwa maana alizifanyiza zile nguzo mbili za shaba, mikono
kumi na minane kwenda juu kwake kila moja; na uzi wa mikono kumi na miwili
kuizunguka nguzo hii au hii. 16 Akafanya taji mbili za
shaba iliyoyeyushwa za kuwekwa juu ya vichwa vya nguzo; kwenda juu kwake taji
moja mikono mitano, na mikono mitano kwenda juu kwake taji ya pili. 17 Kulikuwa na nyavu kama kazi ya kusuka, na masongo ya
mikufu, kwa taji zilizokuwako juu ya vichwa vya nguzo; saba kwa taji moja, na
saba kwa taji ya pili 18 Hivyo akazifanya nguzo; na
kulikuwa na safu mbili za kuzunguka juu ya wavu mmoja, zifunike taji
zilizokuwako juu ya vichwa vya nguzo; akafanya vivyo hivyo kwa taji ya pili. 19 Na taji zilizokuwa juu ya nguzo ukumbini zilikuwa za kazi
ya mayungi, mikono minne. 20 Kulikuwako tena taji juu
ya nguzo mbili, karibu na uvimbe uliokuwako kando ya wavu; na makomamanga
yalikuwa mia mbili, safu safu pande zote juu ya taji ya pili. 21 Akazisimamisha nguzo ukumbini pa hekalu; akaisimamisha
nguzo ya kuume, akaiita jina lake Yakini; akaisimamisha nguzo ya kushoto
,akaiita jina lake Boazi. 22 Na juu ya nguzo kulikuwa
na kazi ya mayungi; hivyo mambo ya nguzo yakatimia. 23 Tena
akaifanya bahari ya kusubu, mikono kumi toka ukingo hata ukingo, ikaviringana,
na mikono mitano ilikuwa kwenda juu kwake; na uzi wa mikono thelathini
kuizunguka kabisa. 24 Na chini ya ukingo wake kulikuwa
na maboga yaliyoizunguka, kwa mikono kumi, yakiizunguka bahari; kulikuwa na
safu mbili za hayo maboga, yakafanywa kalibuni hapo bahari ilipofanywa. 25 Ikakaa juu ya ng'ombe kumi na wawili, watatu wakitazama
kaskazini, na watatu wakitazama magharibi, na watatu wakitazama kusini, na
watatu wakitazama mashariki; na bahari iliwekwa juu yao, na pande zao za nyuma
zote zilikuwa ndani. 26 Na unene wake ulikuwa nyanda
nne; na ukingo wake ukafanywa kama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi; huingia
bathi elfu mbili. 27 Akayafanya yale matako kumi ya
shaba; mikono minne urefu wa tako moja, na mikono minne upana wake, na mikono
mitatu kwenda juu kwake. 28 Na kazi ya matako ndiyo
hii; yalikuwa na papi; na papi zilikuwa katikati ya vipandio; 29 na juu ya papi zilizokuwa katikati ya vipandio kulikuwa
na simba, na ng'ombe, na makerubi; na juu ya vipandio kulikuwa na tako; na
chini ya simba na ng'ombe kulikuwa na masongo ya kazi ya kupembeza. 30 Kila tako lilikuwa na magurudumu manne ya shaba, na
vipini vya shaba; na miguu yake minne ilikuwa na mataruma; chini ya birika
yalikuwako mataruma ya kusubu, yenye masongo kila moja mbavuni. 31 Na kinywa chake ndani ya taji na juu yake kilikuwa mkono
mmoja; na kinywa chake kikaviringana kama kazi ya tako, mkono mmoja na nusu;
tena juu ya kinywa chake kulikuwa na nakshi, na papi zao zilikuwa za mraba,
wala hazikuviringana. 32 Na magurudumu manne yalikuwa
chini ya papi; na mikono ya magurudumu ndani ya tako; na kwenda juu kwake
gurudumu moja mkono mmoja na nusu. 33 Na kazi ya
magurudumu ilikuwa kama kazi ya gurudumu la gari; mikono yake, na maduara, na
matindi, na vipande vya ndani, vyote vilikuwa vya kusubu. 34 Kulikuwa
na mataruma manne katika pembe nne za tako moja; mataruma hayo ni kitu kimoja
na tako lenyewe. 35 Na juu ya tako kulikuwa na duara
nusu mkono kwenda juu kwake; na juu ya tako mashikio yake na papi zake vilikuwa
vya namna iyo hiyo. 36 Akachora juu ya mabamba ya
mashikio yake, na juu ya papi zake, makerubi, na simba, na mitende, moja moja
kama ilivyokuwa nafasi, na masongo pande zote. 37 Hivyo
akayafanya yale matako kumi; yote yalikuwa ya kalibu moja, na cheo kimoja, na
namna moja. 38 Akafanya birika kumi za shaba; birika
moja huingia bathi arobaini; na kila birika ilikuwa mikono minne; birika moja
juu ya tako moja, katika yale matako kumi. 39 Akayaweka
yale matako, matano upande wa kuume wa nyumba, na matano upande wa kushoto wa
nyumba; akaiweka ile bahari upande wa kuume wa nyumba upande wa mashariki,
kuelekea kusini. 40 Tena Huramu akazifanya birika, na
majembe, na mabakuli. Hivyo Huramu akazimaliza kazi zote alizomfanyia mfalme
Sulemani katika nyumba ya Bwana; 41 zile nguzo mbili,
na vimbe mbili za taji zilikuwa juu ya nguzo; na nyavu mbili za kuzifunika hizo
vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo; 42 na
makomamanga mia nne ya zile nyavu mbili; safu mbili za makomamanga kwa kila
wavu, kuzifunika hizo vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo; 43 na yale matako kumi, na birika kumi juu ya matako; 44 na ile bahari moja, na ng'ombe kumi na wawili chini ya
ile bahari; 45 na masufuria, na majembe, na mabakuli;
hata vyombo hivyo vyote, Huramu alivyomfanyia mfalme Sulemani, katika nyumba ya
Bwana, vyote vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa. 46 Katika
uwanda wa Yordani ndipo mfalme alipovisubu, katika udongo mzito kati ya Sukothi
na Sarethani. 47 Sulemani akaviacha vyombo vyote
visipimwe kwa kuwa vilikuwa vingi mno; wala uzito wa shaba haukujulikana. 48 Sulemani akavifanya vyombo vyote vilivyokuwamo nyumbani
mwa Bwana; madhabahu ya dhahabu, na ile meza iliyokuwa na mikate ya wonyesho
juu yake ilikuwa ya dhahabu; 49 na vinara vya taa,
vitano upande wa kuume, na vitano upande wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani,
vya dhahabu safi; na maua, na taa, na koleo ya dhahabu; 50 na
vikombe, na makasi, na mabakuli, na miiko, na vyetezo, vya dhahabu safi; na
bawaba za dhahabu, za milango ya nyumba ya ndani, yaani, patakatifu pa
patakatifu, na za milango ya nyumba, ndiyo hekalu. 51 Hivyo
ikamalizika kazi yote Sulemani mfalme aliyoifanya katika nyumba ya Bwana.
Sulemani akaviingiza vile vitu alivyovitakasa Daudi baba yake, yaani, fedha, na
dhahabu, na vyombo; akavitia ndani ya hazina za nyumba ya Bwana.
Majina ya nguzo za Hekalu yamechukuliwa kutoka kwenye majina ya Waisraeli wawili. Mmoja ni Yakini, wa kabila la Simeoni, wa uzao wa Wayakini. Wapili ni Boazi, alikuwa ni wa kabila la Yuda. Habari za Boazi zinafahamika sana. Alikujakuwa ni mume wa Ruthu na baba wa Obedi, baba yake Yese,baba yake Daudi na kisha hadi kufikia kwa Masihi (sona jarida la Ruthu (Na. 27)). His name Boaz (SHD 1162) is from an unused root of uncertain meaning and was only applied to this man, the ancestor of David. With different vowels it may relate to being strengthened.
Jina la Yakini (Yachin, SHD 3199) maana yake: Yeye ataanzisha, au Yah (au kiukamilifu wake Yaho[vah]) ataanzisha na atakuwa tayari zaidi kama inavyoonekana kama rejea ya maana ya jina la Mungu kama ndiye anayelengwa kunenwa kwamba Ndiye yeye atakayeanzisha.
Ingawaje hatuwezi kupuuzla ukweli kwamba Simeoni walikuwa watawanyike huku na huko katika Israeli, bali angeweza pia kujionea mzao wake Daudi, na kwamba Daudi aliitwa kwa majina yote mawili, yaani nguzo za mababu imara wa uzao wake akiwa kama mfano wa Imani.
Inaonekana vyema sana kwamba taswira ya majina huashiria jukumu la Mungu katika uanzishaji wa Hekalu la Kiroho la Mungu.
Wakati kwamba jina la Boazi halionyeshi
maana yake hasa kwa wazi,
na pia limeelezewa kwa kazi yake
ya ukombozi kwenye habari zilizo
kwnye kitabu cha Ruthu. Kwa
hiyo nguzo mbili zilizo kwenye
lango la Hekalu humaanisha: Yeye atiaye nguvu (Bullinger anasema: Katika
yeye ipo nguvu au uweza) na Yeye aanzishaye. Maana hizo zinaonyesha
kiini cha matendo ya ujenzi wa Hekalu la mwisho la Kiroho la Mungu.
Pia yana maana nyingine
tofauti maalumu na vipimo vyake
vimepewa kitofauti kabisa kwenye idadi
ya maandiko. Hii haikwanganyi
sana, lakini sana tu kuwa ni tofauti
tu kwa jinsi yalivyopimwa.”
Tutaona sasa jinsi uhusiano
wa hizi nguzo
ulivyo na jinsi tunavyotakiwa kutafsiri vipimo vyake.
“Kwenye 1Wafalme 7:15-16, nguzo mbili zimetajwa ili kupima vipimo
vya dhiraa 18 kwenda juu kwake
kwa nguzo moja, na ya pili ilikuwa
na mikono kumi na mbili
kwa mzunguko au duara. Zile kubwa zilikuwa na dhiraa 5.”
Kumbuka: dhiraa 18 huwakilisha misingi 18 ya muundo wa mfumo wa
kipimo cha nasaba damu cha
YDNA ya mwanadamu.
Idadi ya jumla ya dhiraa za nguzo zote na
zile kubwa ni 23 kwenda juu na
12 kwa kuzunguka au kwa duara.
Namba 12 inaonyesha hitimisho
na ukamilifu wa kimuundo wa
kazi ya Mungu pamoja na tarakimu
nyingine ya 22. Namba 23 ni Genomu
ya Mwanadamu kama tutakavyoona hapo chini.
Tunadhani kwamba nguzo hizi
mbili zote zipo kwenye mtindo wa
kisimetrikali na inashangaza sana kama inavyoonyesha kipimo cha urefu wa
kwenda juu na duara kwa
nguzo zote mbili. Yeremia
52:21-22 anatoa urefu wake kamili wa
nguzo hizo na zile kubwa. 2Wafalme 25:17 inasema nguzo hizi
zilikuwa 18 kwenda juu, pamoja na
dhiraa 3 kwa zile kubwa za
katikati. Kipimo hiki kwa uwezekano
wote kukiwepo na mapambo ya jani,
ambalo lilikuwa ni kazi ya ua kama
ilivyoelezwa kwenye maandiko (1Wafalme 7:22).
Andiko lililo kwenye 2Mambo ya Nyakati linatoa nguzo kipimo kilivyojumuishwa
cha dhiraa 35 na 5 kwa zile
kubwa za katikati. Kwa hiyo, nguzo hizi ni za
dhiraa 35 kwa 17.5 kila moja pamoja na nusu dhiraa
kwa kuunganisha, na viwiko au
egemezo za nguzo zilikuwa mikono 5.
Wafafanuzi wanaelezea tathmini yao kuwa tu ndiyo lengo la maandiko hayo. Tarakimu ya arobaini ni nambari ya toba, na nguzo, nguzo
zinazoashiria ukombozi wa Mungu na
uanzishaji wake kwa kipindi cha
toba kilichowekwa kwa kila mmoja. Nguzo hizi zinaashiria maendeleo ya mwanadamu kwa kuingilia kwake
Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu. Kipimo cha chokaa kilichotumiwa
kujengea kila nguzo kilikuwa ni 1 kwa 6 pamoja na
2/3, ambacho ni kipimo cha mwanadamu cha
mwili hadi kichwani, kwa karibu
1 hadi 7.”
Hata hivyo, vipimo hivi
vinahusiana pia na kipimo cha
muundo wa DNA cha Kromosomu 23 na jumla yake
ni 46 kwenye pea 23 ambayo
ni tarakimu ya pea za DNA. Dhiraa ni kipimo cha viumbe wote
wawili, yaani cha malaika na
kinaonyesha kusudi la mwisho la uumbaji kwenye Mji wa
Mungu ambako mwanadamu na Malaika watakuwa viwango na hali sawa.
“Zile kubwa za katikati
zinatofautiana kivipimo.
1Wafalme 7:20 inasema kwamba
kulikuwa na komamanga kwenye zile kubwa za
katikati zilikuwa mia mbili kwenye
mistari inayozunguka kuhusu sura hizi. Ile nguzo iliyosimamishwa upande wa kuume
ilimuwakilisha Yakini/Jachin na
ile ya upande wa kushoto ni Boazi.
Zaidi sana kwenye aya ya 42
inasema zilikuwa ni mia mbili ili
kuzionyesha kuwa ni mia mbili zilichukuliwa kwa kila kubwa
(soma pia 2Mambo ya Nyakati
4:13). Kwenye 2Mambo ya Nyakati
3:16 zimeitwa mia moja, ikimaanisha, zilikuwa mia moja kwenye kila mstari. Yeremia 52:23 inasema kwamba mistari hii ya Ruachi au kwenye mwelekeo wa upepo (yaani
imefunuliwa) kuwa zilikuwa
96.”
Mia mbili kwenye kila
zile kubwa sio hakika sana lakini zimepewa nguvu kwa kulinganishwa
na idadi ya Genomu za Mwanadamu
huenda inahusianishwa na DYS ndani ya YDNA zinazofanya uwezo wa kujikinga mara 400.
“2Mambo ya Nyakati pia inaendelea
kwa kusema kwamba ukumbi moja liliuwa na kipimo
cha ujazo cha 120, kikitumia me’ah (SHD 3967) na 'esriym (SHD 6242). 1Wafalme 6:2-3 inasema
Hekalu lilikuwa ni la dhiraa 60 urefu, na dhiraa ishirini
upana na dhiraa thelathini urefu wake kwenda
juu. Inasemekana pia kuwa kila ukumbi
mmoja ulikuwa wa mikono 20 urefu
wake, na sawasawa na mapana
ya nyumba, na mapana ya upande wa mbele ya nyumba
(yaani wa kuingilia kwenye ukumbi) lilikuwa na dhiraa 10. Ipo kimya kama kwenye
urefu wa kwenda juu wa
ukumbi, na watu wanadhani kwamba ulikuwa ni urefu uleule wa
kama mwili wa Hekalu lakini
maandiko yanasema ilikuwa ngi mara nne urefu wa
mwili wa Hekalu. Ukumbi wenye dhiraa 120 unaashiria urefu wa kipindi cha
uumbaji wa kimwili wa zama
hizi kilichopimwa kwa idadi ya Yubile.
Namba hii ilikonyesha pia kipindi cha
uhai na maisha
ya nabii Musa kama tunavyoona kwenye vitabu vya Torati
na pia kwenye
kipindi cha kwanza cha maisha ya mababa.
Kipindi cha uhai au maisha
ya Musa yaligawanyika katika
migawanyo mitatu ya miaka arobaini-arobaini na yalifanya taswira
ya awamu za Utawala wa Wafalme.
Tarakimu ya “thelathini” ni
kiini kikubwa iliyoashiria serikali ya ndani ya Mungu, na pia umri
unaofaa kufikia kipindi cha kabla
mtu hajawa kiongozi wa kundi
au kusanyiko la Mungu.
Ngazi sita za kuingilia zinaashiria
mizunguko sita ha kwanza ya maisha
ya mwanadamu. Ngazi ya saba
na ambayo ndiyo ilikuwa ni sehemu ya Hekalu lenyewe, iliashiria mzunguko wa Sabato ya mwisho ya Yubile uliowekwa na kupewa
wanadamu. Mtu anapaswa awe na
umri wa miaka
ishirini ndipo ahesabiwe kuwa ni mtu mzima na astahili
kwenda vitani. Inampasa mtu awe
na umri wa
miaka ishirini na tano kabla hajaruhusiwa
kufanya kazi na huduma za
Hekaluni, na hadi awe na
umri wa miaka
thelathini ndipo awe mzee kwenye
ushirika au kanisa la Mungu.
Mtu amewekewa au kupewa
Yubile moja akiwa mtu mzima ili
aweze kuendelea katika Roho Mtakatifu. Musa alipewa
Yubile mbili. Daudi alifariki akiwa na umri wa
miaka sabini ikimaanisha ashirio la kupungua kwa wakati
hadi kufikia Yubile moja. Alimuachia madaraka ya ufalme wake Sulemani kabla hajafa, kitendo kilichoashiria utaratibu kwenye mwendelezon wa mamlaka kwa
mtiwa Mafuta wa Bwana.
Patakatifu pa Patakatifu palikuwa
ni Naos, ambayo iliashiria
mwaka wa mwisho wa maisha
ya mwanadamu na wakati mtu alipoupata
umoja mkamilifu na Mungu. Ndipo
hii Naos iliwakilisha
hatua ya maendeleo ya mwanadamu wakati Mungu alipoingia kwa mwanadamu kwa kupitia
Roho Mtakatifuna kumuinua yeye kwa
elohm. Na hii ndiyo maana
Agano Jipya linatutaja sisi
kuwa ni Naos, “na ni Naos tulivyo sisi”
(1Wakorintho 3:17).
Zile Meza, na Mkate wa
wonyesho, na vinara kumi vya
taa vilisimama kwa ajili ya kuliendeleza
Kanisa la Mungu kwa kipindi chote lilichopewa Kanisa kwenye awamu zake
saba za maendeleo likiwa chini ya malaika saba wa makanisa saba.
Zile tatu nyingine ziliwakilisha
vinara ambazo zilikuwa ni Masihi na Mashahidi Wawili (soma jarida la Mashahidi (Wakiwemo Mashahidi Wawili) (Na. 135) [The Witnesses (including the Two Witnesses) (No. 135)].
Patakatifu pa Patakatifu palikuwa
na Sanduku la Agano na Torati ya Mungu,
ambapo Torati ya Mungu iliwekwa kwenye mioyo ya watu waliokujakuwa hatimaye kuwa ni Hekalu la Mungu.
Bahari iliyoyeyuka au kioo cha Hekalu
vilikuwa kubiti thelathini vilivyozunguka na hivyo Mungu
alifunua kiwango cha uweza wa
kimazingira yake (1:3) kwenye urefu wake
wa kiina na ubora. Ilikuwa
ni nje ya Nyumba ya Mungu, kama ilivyokuwa
madhabahu, ili kuashiria kwamba Kristo alikufa nje ya kambi akiwa kama
sadaka, mara moja tu na kwa ajili ya wote
ili sote tuweze kutakasika na kukombolewa
na Mungu.
Ukubwa wa Hekalu iliashiria
Mpango wa Wokovu na ukombozi wa
mwanadamu unaofanywa na Mungu. Mlolongo na mpangilio wa ujenzi wake uliendana na
ramani ile na ililiashiria kila kitu cha maendeleo yake. Ufunguo wa Daudi ni
kuelewa na kuzifundisha Siri za Mungu kwa mujibu sawa na mpangilio wa Yubile
ulivyopangiliwa na kulingana nayo, na kuweza kutabiri sawasawa na mafundisho
yenye uzima, na sawasawa na inavyosema Torati na Ushuhuda.”
Kulikuwa na idadi
kubwa ya mahekalu ambayo tutakwenda kuyaongelea habari zake hapo chini.
Ni baada tu ya
kukamilika Hekalu, ndipo Sanduku la Agano lililetwa na kuingizwa Hekaluni, ili
kwamba Mungu aonekane akiwa kama kiini chake. Lililetwa katika mwezi wa
Ethanimu, ambao unaashiria Ujio wa Masihi na Mfalme na Mtawala wa Ulimwengu
akiwa kama Nyota ya Asubuhi.
1Wafalme 8:1-66 Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni. 2 Wakakutana mbele ya mfalme Sulemani watu wote wa Israeli wakati wa sikukuu, katika mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba. 3 Wazee wote wa Israeli wakaja, nao makuhani wakajitwika sanduku. 4 Wakalipandisha sanduku la Bwana, na ile hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwa katika ile Hema; vitu hivyo makuhani na Walawi wakavipandisha. 5 Mfalme Sulemani, na mkutano wote wa Israeli waliokutanika kwake, walikuwako pamoja naye mbele ya sanduku, wakichinja sadaka kondoo na ng'ombe, wasioweza kuhesabiwa wala kufahamiwa idadi yao kwa kuwa wengi. 6 Makuhani wakalileta sanduku la agano la Bwana hata mahali pake, katika chumba cha ndani cha ile nyumba, patakatifu pa patakatifu, naam, chini ya mbawa za makerubi. 7 Kwa maana makerubi yalinyosha mbawa zao, juu ya mahali pa sanduku, makerubi yakalifunika lile sanduku na miti yake kwa juu. 8 Na ile miti kwa kuwa mirefu, ncha za miti zilionekana katika mahali patakatifu, mbele ya chumba cha ndani; lakini hazikuonekana nje; nayo iko kuko huko hata leo. 9 Hamkuwa na kitu ndani ya sanduku, ila zile mbao mbili za mawe ambazo Musa aliziweka ndani huko Horebu, Bwana alipofanya agano na wana wa Israeli, hapo walipotoka katika nchi ya Misri.
Kwa hiyo hizi
Meza ziliwekwa kwenye Sanduku la Agano ili kuonyesha ukweli wa kwamba Mungu
aliziweka Sheria zake mioyoni mwa watu wote na zingekuwa mahali pa katikati pa
makao yake kama Naos au Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu la Mungu. Na
hii ndiyo maana Sanduku hili la Agano lilipaswa liingizwe mioyoni mwa wateule
walio kwenye Makanisa ya Mungu.
10
Ikawa, makuhani
walipotoka katika patakatifu, nyumba ya Bwana ikajaa wingu; 11
hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya
wingu lile; kwa kuwa nyumba ya Bwana ilikuwa imejaa utukufu wa Bwana. 12 Ndipo Sulemani akanena,
Bwana alisema ya kwamba atakaa katika giza
nene. 13 Hakika nimekujengea
nyumba ya kukaa, iwe mahali pa
makao yako milele. 14 Mfalme
akageuza uso wake, akawabariki mkutano wote wa Israeli; na mkutano wote
wa Israeli wakasimama. 15 Akasema, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenena na Daudi baba yangu kwa kinywa chake
akalitimiza kwa mkono wake, akasema,
16 Tokea siku
ile nilipowatoa watu wangu Israeli katika Misri, sikuchagua mji wo wote
katika kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe hapo;
lakini nalimchagua Daudi awe juu ya watu
wangu Israeli. 17 Basi ilikuwa moyoni mwake Daudi, baba yangu, kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 18 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, Kwa
kuwa ilikuwa moyoni mwako kujenga nyumba
kwa jina langu, ulifanya vema kuwaza
hivi moyoni mwako. 19 Lakini wewe hutanijengea nyumba hiyo; ila
mwanao atakayetoka katika viuno vyako,
yeye ndiye atakayeijenga nyumba kwa jina langu. 20 Basi Bwana amelitimiza neno lile alilolinena; nami nimesimama mahali pa Daudi baba yangu, na kuketi
katika kiti cha enzi cha
Israeli, kama Bwana alivyoahidi,
nami nimeijenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 21 Na
humo sanduku hili nimelifanyizia mahali, ambalo ndani yake
mna maagano ya Bwana, aliyoyafanya na baba zetu, hapo alipowatoa
katika nchi ya Misri. 22 Sulemani akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana, machoni pa mkutano
wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake mbinguni. 23
Akasema Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama
wewe, mbinguni juu wala duniani
chini; ushikaye maagano na rehema
kwa watumishi wako, waendao mbele
zako kwa mioyo yao yote. 24 Umemtimizia mtumishi
wako, Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia; naam, ulinena kwa
kinywa chako, ukayatimiza kwa mkono wako, kama
ilivyo leo. 25 Na sasa, Ee
Bwana, Mungu wa Israeli, umfikilizie mtumishi wako, Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia, ukisema, Hutakosa kuwa na mtu wa
kuketi katika kiti cha enzi
cha Israeli machoni pangu, kama watoto
wako wakiangalia njia zao, ili
kuenenda mbele zangu kama wewe
ulivyoenenda. 26 Sasa, Ee Mungu wa
Israeli, nakusihi, ulithibitishe
neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu. 27 Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli
juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu;
sembuse nyumba hii niliyoijenga!
28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na
dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi
ya mtumwa wako, aombayo mbele zako
leo. 29 Macho yako yafumbuke na kuielekea
nyumba hii usiku na mchana,
mahali hapa ulipopataja, ukasema, Hapa ndipo litakapokuwapo jina langu; ili uyasikie
maombi ya mtumwa wako aombapo akikabili
mahali hapa. 30 Uisikie dua
ya mtumwa wako, na ya watu wako
Israeli, watakapoomba wakikabili
mahali hapa; naam, sikia huko
mbinguni, makao yako; nawe usikiapo,
samehe. 31 Ikiwa mtu amemkosa
mwenzake, na kupewa sharti ya kiapo aapishwe, naye akija na kuapa
hapa mbele ya madhabahu yako, katika nyumba hii;
32 basi, usikie
huko mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimpatiliza
mtu mbaya, kwa kuleta njia
yake juu ya kichwa chake; na
kumpa mwenye haki haki yake,
ukimjalia kwa kadiri ya haki yake. 33 Ikiwa
watu wako Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa
sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea
tena kwako, na kulikiri jina lako wakikuomba na kukusihi
katika nyumba hii; 34 basi,
usikie huko mbinguni, ukawaachilie watu wako Israeli dhambi yao, ukawarejeze tena katika nchi uliyowapa
baba zao. 35 Ikiwa mbingu zimefungwa,
hata hakuna mvua, kwa sababu
wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili
mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha
dhambi yao, wakati ule utakapowatesa; 36 basi, usikie
huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na
ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo
kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi
yako, uliyowapa watu wako iwe
urithi wao. 37 Ikiwa nchi imeingia
njaa, au tauni, au ukosefu
wa mvua, au ukungu, au
nzige, au panzi; ikiwa adui
wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba
wo wote, au uele wo
wote; 38 maombi
yo yote au dua yo yote ikifanywa
na mtu awaye
yote, au na watu wako
Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu maradhi ya moyo wake, na kuikunjua
mikono yake kuielekea nyumba hii; 39 basi,
usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa
kadiri ya njia zake; wewe ujuaye
moyo wake; (maana wewe peke yako
ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote); 40 ili
wakuche wewe siku zote watakazoishi katika nchi uliyowapa
baba zetu. 41 Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako
Israeli, atakapokuja kutoka
nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako; 42 (maana watasikia
habari za jina lako kuu, na
za mkono wako ulio hodari,
na za mkono
wako ulionyoshwa); atakapokuja na kuomba kuielekea nyumba hii; 43 basi, usikie huko
mbinguni, makao yako, ukatende kwa kadiri ya yote
atakayokuomba mgeni huyo; ili watu wote
wa dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha
wewe kama watu wako Israeli, nao wajue ya kuwa nyumba hii, niliyoijenga, imeitwa kwa jina lako. 44 Ikiwa
watu wako watoka kwenda kupigana
na adui zao,
kwa njia yo yote utakayowapeleka, wakikuomba, Bwana, kuuelekea mji huu uliouchagua,
na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako; 45
basi, uyasikie huko mbinguni maombi
yao na dua yao, ukaitetee haki yao. 46 Ikiwa wamekutenda
dhambi, (maana hakuna mtu asiyetenda
dhambi), hata ukawaghadhibikia, ukawatia katika mikono ya adui zao, wawachukue
mateka mpaka nchi ya adui zao,
iliyo mbali au iliyo karibu;
47 basi, wakijirudia
nafsi zao katika nchi ile
watakayochukuliwa mateka, wakitubu, na kukusihi
katika nchi ya hao waliowachukua mateka, wakisema, Tumekosa, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu; 48 watakaporejea kwako kwa mioyo
yao yote, na kwa nia zao
zote, katika nchi ya adui zao, waliowachukua
mateka, wakikuomba, kwa kuikabili nchi
yao, uliyowapa baba zao, na mji huu
uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga
kwa jina lako; 49 basi, uyasikie
maombi yao na dua yao, huko mbinguni,
makao yako, ukaitetee haki yao; 50 ukawasamehe watu
wako waliokutenda dhambi, na makosa
yao yote waliyokukosa; ukawape kuonewa huruma mbele yao waliowachukua mateka, ili wapate kuwahurumia.
51 Kwa kuwa ni watu wako, na urithi
wako, uliowatoa katika Misri, toka katikati ya tanuu ya chuma. 52 Macho yako na
yafumbuke, na kuielekea dua ya mtumwa wako, na
dua za watu
wako Israeli, ukawasikilize
kila wakati watakapokulilia. 53 Kwa maana uliwatenga na watu wote
wa dunia, wawe urithi wako,
kama ulivyonena kwa mdomo wa
Musa, mtumishi wako, hapo ulipowatoa baba zetu katika Misri, Ee Bwana MUNGU. 54 Hata ikawa, Sulemani alipokwisha kumwomba Bwana maombi hayo, na dua hiyo
yote, akasimama na kuondoka hapo
mbele ya madhabahu ya
Bwana, hapo alipokuwa amepiga magoti, na kuikunjua mikono
yake kuelekea mbinguni. 55 Akasimama,
na kuwabariki mkutano wote wa
Israeli kwa sauti kuu, akasema, 56
Na ahimidiwe Bwana, aliyewapa watu wake Israeli kustarehe, vile vile kama
yote aliyoyaahidi. Halikukosa kupatikana neno lo lote katika ahadi yake njema,
aliyoahidi kwa mkono wa Musa, mtumishi wake. 57
Bwana, Mungu wetu, na akae nasi,
kama alivyokaa na baba zetu; asituache,
wala asitutupe; 58 aielekeze mioyo
yetu kwake, ili tuende katika
njia zake zote, na kuzishika amri
zake, na sheria zake, na
hukumu zake, alizowaamuru baba zetu. 59 Na maneno
yangu haya, niliyoyaomba mbele za Bwana, na yawe karibu
na Bwana, Mungu wetu, mchana na
usiku, ili aitetee haki ya mtumishi wake, na haki ya watu
wake Israeli, kwa kadiri ya haja zao za kila
siku. 60 Watu
wote wa ulimwengu
wajue ya kuwa Bwana ndiye Mungu; hakuna mwingine.
61 Mioyo yenu
na iwe kamili
kwa Bwana, Mungu wetu, kuenenda katika sheria zake,
na kuzishika amri zake, kama
ilivyo leo. 62 Ndipo mfalme, na
Israeli wote pamoja naye, wakatoa sadaka mbele za Bwana. 63 Sulemani akatoa sadaka za amani,
alizomtolea Bwana, ng'ombe ishirini na mbili
elfu, na kondoo mia na
ishirini elfu. Ndivyo mfalme na
wana wa Israeli wote walivyoifanya wakfu nyumba ya Bwana. 64 Siku ile ile
mfalme akaitakasa behewa ya katikati iliyokuwa mbele ya nyumba ya Bwana; kwa kuwa hapo ndipo alipotoa
sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga,
na mafuta ya sadaka za amani;
kwa sababu ile madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo, haikutosha kuzipokea sadaka za kuteketezwa,
na sadaka za unga, na
mafuta ya sadaka za amani. 65 Basi,
wakati ule Sulemani akafanya sikukuu, na Israeli wote pamoja naye, kusanyiko kubwa sana, kutoka maingilio ya Hamathi mpaka kijito cha
Misri, mbele za Bwana, Mungu wetu, siku
saba na siku saba, yaani siku kumi
na nne. 66
Hata siku ya nane akaagana na watu,
nao wakambarikia mfalme, wakaenda hemani kwao, wakifurahi na kuchangamka moyoni kwa wema
wote Bwana aliomfanyia
Daudi mtumishi wake, na Israeli watu wake.
Agano Liliwekwa na
Sulemani
Malaika wa Mungu, msaidizi
au mjumbe wa Mungu wa
Israeli tunayemjua kama
Kristo (Zaburi 45:6-7; Waebrania
1:8,9) alimtokea Sulemani na
kuliweka Agano la Mungu kwa ajili yake
mwenyewe na kwa Taifa zima. Agano hili lilikuwa na
masharti. Waliambiwa kuwa wangeadhibiwa iwapo kama hawatalishika au wakiliasi.
1Wafalme 9:1-28 Ikawa Sulemani alipokwisha kuijenga nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme,
na mambo yote yaliyoingia moyoni mwake Sulemani, naye akataka kuyafanya, 2 basi,
Bwana akamtokea Sulemani mara ya pili
kama alivyomtokea huko Gibeoni. 3
Bwana akamwambia, Nimeyasikia
maombi yako na dua zako,
ulizotoa mbele zangu. Nimeitakasa nyumba hii uliyoijenga
ili niweke jina langu humo milele; tena macho yangu na moyo wangu
utakuwapo hapo siku zote; 4 na
wewe, ukienda mbele zangu kama
alivyokwenda Daudi, baba yako,
kwa ukamilifu wa moyo, na kwa
adili, kufanya hayo yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria
zangu na hukumu zangu, 5
ndipo nitakapokifanya
imara kiti cha ufalme wako
juu ya Israeli milele; kama nilivyomwahidia Daudi, baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kukaa
katika kiti cha enzi cha
Israeli. 6 Bali mkighairi, mkaacha kunifuata, ninyi na watoto
wenu, msizishike sheria zangu na
amri zangu, nilizoziweka mbele yenu, tena mkienda na kuitumikia miungu
mingine na kuiabudu, 7 basi
nitawakatilia Israeli mbali
na nchi hii
niliyowapa; na nyumba hii niliyoitakasa
kwa jina langu, nitaitupilia mbali na macho yangu, na Israeli watakuwa mithali na neno
la tusi katika mataifa yote. 8
Na ijapokuwa nyumba hii imetukuka
namna hii, lakini kila apitaye
atasituka na kuizomea; nao watasema,
Kwa nini Bwana ameitenda nchi
hii na nyumba
hii mambo haya? 9 Na watu watajibu,
Kwa sababu walimwacha
Bwana, Mungu wao, aliyewatoa
baba zao katika nchi ya Misri, wakashikamana na miungu mingine
na kuiabudu na kuitumikia, basi ndiyo sababu
Bwana ameleta mabaya haya yote juu yao. 10
Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo
Sulemani alizijenga zile nyumba mbili, nyumba
ya Bwana na nyumba yake mfalme, 11
(basi Hiramu, mfalme wa Tiro, alikuwa amemletea Sulemani mierezi na miberoshi,
na dhahabu, sawasawa na haja
zake zote), ndipo mfalme Sulemani akampa Hiramu miji ishirini ya nchi ya Galilaya. 12 Naye Hiramu akatoka
Tiro kuitazama hiyo miji Sulemani aliyompa; wala haikumpendeza. 13 Akasema, Miji gani hii uliyonipa,
ndugu yangu? Akaiita nchi ya Kabuli, hata leo. 14 Hiramu akamletea
mfalme talanta sitini za dhahabu.
15 Na hii
ndiyo sababu ya shokoa aliyoitoza mfalme Sulemani; ili kuijenga nyumba ya Bwana, na nyumba yake
mwenyewe, na Milo, na ukuta wa
Yerusalemu, na Hazori, na Megido, na Gezeri. 16 Farao, mfalme wa
Misri, alikuwa amepanda akautwaa Gezeri, na kuuteketeza kwa moto, akawaua Wakanaani waliokaa mjini, akampa zawadi binti
yake, mkewe Sulemani. 17 Naye Sulemani akaujenga Gezeri,
na Beth-horoni wa chini, 18 na Baalathi, na
Tamari ulio nyikani, katika nchi; 19
na miji yote ya hazina iliyokuwa yake Sulemani; na miji ya magari
yake, na miji ya watu wake
wapandao farasi, na kila alichopenda
kujenga Sulemani huko Yerusalemu, na katika Lebanoni, na katika nchi yote
ya mamlaka yake. 20 Kwa habari ya watu wote waliosalia,
Waamori, Wahiti, Waperizi,
Wahivi, na Wayebusi, wasiokuwa wa wana
wa Israeli; 21 watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana
wa Israeli hawakuweza kuwaharibu kabisa, katika hao Sulemani akawatumikisha
shokoa hata leo. 22 Lakini wa wana
wa Israeli Sulemani hakumtumikisha
mtu shokoa; ila ndio watu
wa vita, na wangoje wake, na
wakuu wake, na akida zake,
na wakuu, wa magari yake,
na wa wapanda
farasi wake. 23 Hao maakida
wakuu, waliokuwa juu ya kazi yake
Sulemani, walikuwa mia tano
na hamsini, waliowaamuru watu watendao kazi. 24
Lakini binti Farao akapanda
toka mji wa Daudi, mpaka hiyo nyumba yake
Sulemani, aliyomjengea; kisha,
aliijenga Milo. 25 Na mara tatu kila
mwaka Sulemani alikuwa akitoa sadaka za
kuteketezwa na sadaka za amani
juu ya madhabahu aliyomjengea Bwana akafukiza uvumba pamoja nazo
juu ya madhabahu iliyokuwako mbele za Bwana. Hivyo akaimaliza nyumba. 26 Tena, mfalme Sulemani akaunda merikebu huko Ezion-geberi, ulioko karibu na
Elothi, pwani ya Bahari ya Shamu, katika nchi
ya Edomu. 27 Naye Hiramu akatuma merikebuni watumishi wake, wanamaji wenye kuijua bahari,
pamoja na watumishi wake Sulemani.28 Wakafika Ofiri,
wakachukua toka huko dhahabu, talanta
mia nne na
ishirini, wakamletea mfalme Sulemani.
Kwa hiyo andiko lililo
kwenye Mambo ya Nyakati linahusu mambo yanayotakiwa kufanyika Hekalu na Agano lililowekwa na Taifa. Ni kama tunavyoona kwenye 2Mambo ya Nyakati 2:1-18. Kuanzia aya ya 4 tunaona kwamba Hekalu liliandaliwa
kwa utoaji wa sadaka ya kutekeezwa
na hii inawakilisha
maombi ya Watakatifu ya kila siku nay
a Sabato na Mwandamo wa Mwezi Mpya na sikukuu zote takatifu zilizoamriwa na Bwana kama amri ya milele.
4 Angalia, najenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wangu, ili kumfanyia wakfu, ya kufukizia mbele zake fukizo la manukato, na ya mkate wa wonyesho wa daima, na ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni, na za siku za sabato, na za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoagizwa za Bwana, Mungu wetu. Hili ni agizo la milele kwa Israeli. 5 Nayo nyumba nitakayoijenga ni kubwa; kwa sababu Mungu wetu ndiye mkuu juu ya miungu yote. 6 Lakini ni nani awezaye kumjengea nyumba, ikiwa mbingu hazimtoshi, wala mbingu za mbingu? Nami ni nani basi, hata nimjengee nyumba, isipokuwa kwa ajili ya kufukizia fukizo mbele zake?
Kisha Sulemani aliwaruhusu waimbaji au watunzi waende
na wakafanye hivyo na vitu
vingine pia (aya za 7-14).
Hiramu alipeleka
mwimbaji na mtunzi ambaye ni nusu Muisraeli. Baba yake alikuwa pia
Hiramu na mwimbaji na munzi
wa nyimbo alikuwa ni mtu wa baba yake.
Mtu Yule alikuwa ni kutoka kwa mwanamke
wa kabila la Dani, na ni mtu wa
Tiro ushiriki wa wanawake wa Israeli kwenye mwingiliano wa kindoa na
Wamataifa kwenye ujenzi wa Hekalu. Ukweli ule ulionyesha
kuelekea asili ya uzawa wa Israeli katika Siku za Mwisho na Wokovu
ule ulikuwa ni wa Wamataifa.”
Utaratibu wa kipimo cha
DNA kilijumuisha Israeli na
Wamataifa ili kwamba Ibrahimu afanyike kuwa
Baba wa Mataifa na Agano na Mungu na
Roho Mtakatifu ambaye ndiye
aliziandika Sheria zile ndani ya mioyo ya wanadamu na ili
iendelee kwa mfumo wote wa
mwanadamu na wokovu uliendelea hadi kwa Wamataifa.
15 Basi sasa hiyo ngano na shayiri, mafuta na mvinyo, aliyonena bwana wangu, na wapelekewe watumishi wake; 16 nasi tutakata miti katika Lebanoni, kadiri utakavyohitaji; na kukuletea tukiieleza baharini mpaka Yafa; nawe utaichukua Yerusalemu. 17 Ndipo Sulemani akawahesabu wageni wote waliokuwamo katika nchi ya Israeli, sawasawa na hesabu aliyowahesabu Daudi baba yake; wakatokea mia hamsini na tatu elfu, na mia sita. 18 Akaweka katika hao sabini elfu wawe wachukuzi wa mizigo, na themanini elfu wawe wachongaji milimani, na wasimamizi elfu tatu na mia sita, ili wawatie watu kazini.
Idadi yao watu hawa ilikuwa
ni 153,600 ambao ni wageni katika Israeli na walipangiwa kazi kwenye kazi hii
ya ujenzi wakiwa kama wakusanya changizo. Wanaume elfu sabini walikuwa
ni wachukuzi wa mizigo, 80,000 walikuwa wakata miti milimani
na 3,600 walikuwa wasimamizi au manyapara.
Kwa hiyo Wamataifa wote waliokuwa katika Israeli walihusishwa na kazi hii
ya ujenzi. Wakati wokovu ulipoenea na kuwafikia Wamataifa
ulimwenguni kote.
Mara tu baada ya vifaa vyote vya ujenzi
vilipokamilika na kuletwa, ndipo Sulemani alianza kulijega (2Mambo ya Nyakati 3:-1-17).
2Mambo ya Nyakati 3:1-17 Ndipo Sulemani akaanza kuijenga nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, juu ya mlima Moria, pale Bwana alipomtokea Daudi babaye alipotengeza mahali pale alipoagiza Daudi, katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.
Kwa hiyo eneo la Wayebusi
ambalo lilikuwa ni mahali pa kikuhani
pa Melikizedeki palifanywa kuwa ni mahali pa Hekalu na
kuwa ni pa imani ile.
2 Mambo ya Nyakati 3:2-17 inaelezea kuhusu ujenzi ule tuliouona
kwenye kitabu cha Wafalme lakini
kina mengi ya kuongelea kwa kina zaidi kama vile dhahabu
kuwa ni ya Parvaimu na dari yake ya afiri
na ya mawe ya thamani sana kwenye Nyumba Kubwa.
2 Akaanza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili
katika mwaka wa nne wa
kutawala kwake. 3 Basi hii ndiyo
misingi ya majengo ya nyumba ya Mungu aliyoiweka Sulemani. Urefu wake kwa mikono
ya cheo cha kwanza ulikuwa mikono sitini, na upana wake
mikono ishirini. 4 Na ukumbi
uliokuwa mbele yake, urefu wake
kadiri ya upana wa nyumba ulikuwa
mikono ishirini, na kwenda juu
kwake mia na ishirini; akaufunikiza
ndani kwa dhahabu safi. 5
Nayo nyumba kubwa akaifunika miti ya miberoshi, aliyoifunikiza kwa dhahabu safi, akaifanyizia
mitende na minyororo. 6 Akaipamba
nyumba kwa vito iwe na uzuri;
nayo dhahabu ilikuwa dhahabu ya Parvaimu. 7 Tena, akaifunikiza kwa dhahabu nyumba,
na boriti, na vizingiti, na
kuta zake, na milango yake;
akachora makerubi kutani. 8 Akaifanya
nyumba ya patakatifu pa patakatifu; urefu wake kadiri
ya upana wa nyumba, ulikuwa mikono ishirini, na upana wake
mikono ishirini; akaifunikiza kwa dhahabu safi, ya talanta mia sita. 9 Na uzani
wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu.
Akazifunikiza orofa zake za juu
kwa dhahabu. 10 Na ndani
ya nyumba ya patakatifu pa patakatifu akafanyiza
makerubi mawili ya kuchonga; wakayafunikiza kwa dhahabu. 11
Na mabawa ya makerubi hayo urefu wake ulikuwa mikono
ishirini; bawa moja mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na
bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la pili. 12 Na
bawa la kerubi la pili lilikuwa mikono
mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba;
na bawa la pili mikono mitano,
likishikana na bawa la kerubi la
kwanza. 13 Yakaenea mabawa ya makerubi hayo mikono ishirini; yakasimama juu ya miguu yao, na nyuso
zao ziliielekea nyumba. 14 Akalifanya
pazia la samawi na urujuani na
nyekundu, na kitani safi, akaifanyizia
makerubi. 15 Tena akafanya mbele ya nyumba nguzo mbili
za mikono thelathini na tano kwenda juu kwake,
na taji iliyokuwa
juu yake moja moja ilikuwa mikono
mitano. 16 Akafanya minyororo ndani ya chumba cha ndani, akaiweka juu ya vichwa vya
nguzo; akafanya makomamanga mia, akayaweka juu ya hiyo minyororo. 17 Akazisimamisha nguzo hizo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume, na
ya pili upande wa kushoto; akaliita
jina la ile ya kuume
Yakini, na jina la ile ya kushoto Boazi.
Ni kupitia wokovu wa Mungu ndipo tunaingia kwenye Hekalu la Mungu. Makerubi wanakilinda Kiti cha Enzi cha Mungu
na wanawakilisha Makerubi wa kundi
la Malaikana wanawakilisha
Makerubi wa kundi la
Malaika. Makerubi walioonekana
kwenye Hekalu aliloonyeshwa nabii Ezekieli wanaonyesha kwamba makerubi wengine wawili walioingizwa wa upande wao wa
mtende ambao ni Kristo, wanachukua nafasi ya mtu mwanaume na
kerubi mwenye umbo la kichwa cha samba cha malaika Muasi, aitwaye Shetani na Aeon mwenye kichwa cha samba. Hawa elohimu waliowekwa hapa ni Ibrahimu na Musa, ambao ni wawili pekee waliotajwa kuwa ni Elohim kwenye maandiko ya vitabu vya Mwanzo na Kutoka.
Wakati Ibrahimu na Musa wakiwa ni watu wawili tu pekee waliotajwa kuwa ni Elohim, kulikuwa
ni wawili waliomtokea Yesu,
ambao ni Musa na Eliya
(Mathayo 17:3). Kwa hiyo tunaweza
kudhania kwamba kunaweza kuwa na angao viumbe wane
waliohusika kwenye mlolongo huu, akiwemo
pia Henoko pamoja na hawa
wengine kina Ibrahimu, Musa na
Eliya na huenda hata na wawili
wengine ambao hawajajulikana bado.
Madhabahu ya shaba na
bahari ya kioo vilifuatiwa kujengwa. Habari zake zimeelezewa
pia kwenye 2Nyakati 4:1-22.
Kulisimamishwa kwa mistari miwili na maksai kumi
na mbili, kila watatu wao wakiangalia upande wa Kaskazini, Mashariki, Kusini na Magharibi.
Waliangalia wakiwa na waangalizi au
walinzi wao ndani yake. Bahari hii ilikuwa na maafu
3000. Unene wake ulikuwa ni wa sawa
na mkono mmoja tena kwa kipimo cha kazi
ya mwanadamu (aya ya 5).
Luva kumi za upande wa kulia
na tano za kushoto ziliwakilisha pia kazi ya mwanadamu,
wakati kwamba walisafishwa au kuitakasa sadaka kwa Bwana kiasi kwamba vitu vyote
vilivyotolewa sadaka kwa Mungu vilikuwa
vimeisha na kwa watu. Bahari yenyewe ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani
ya kunawia na shughuli hii ya kuwasafisha au kuwatakasa makuhani ilikuwa kwanza kwa Walawi lakini ilikuwa na ingepaswa kuwa ya Melikizedeki chini ya Masihi (kama ilivyo
kwenye Waebrania sura ya 1 hadi 8) na Kristo ni mwombezi aliyeitoa sadaka mara moja tu kwa watu wote (sura ya 9), na atawatokea wale
wanaomtafuta kwa mara ya pili pasipo kutenda
dhambi kwenye wokovu (Waebrania 9:28).
Imeandikwa kulikuwa na
vinara kumi vya taa vya
dhahabu, na tena vitano upande wa
kulia na vitano upande wa
kushoto vilivyowekwa kwenye meza kumi na pamoja navyo
mabeseni mia moja ya dhahabu (aya za
6-8).
Hekalu hili lilijengwa
pia nyua za makuhani na
Ua Mkubwa na milango ya ua. Kwa hiyo wateule walitengwa
mbali na Kuhani Mkuu na kuhani aliyesimama
katikati wanapokuwa kwenye kazi au
huduma zao muhimu (aya ya 9). Bahari iliwekwa upande wa kuume wa
mashariki mwishoni, ambako ndiko mfalme
anakoingilia akija helakuni.
Nguzo mbili za Hekalu zilitengenezwa na Wamataifa na
ziliwakilisha mfumo wa nasaba ya DNA za kipimo cha
Kibinadmu cha kubits 23 na 46 na pia cha
komamanga 400 kwenye shada za maua
mbili na mistari mkiwili katika kila shada
moja (aya za 12-13).
Vyombo vya shaba
vilichukuliwa kwenye uwanda Yordani na vilikuwa vingi vivivyopimika au kuhesabika kama sadaka za daima
za kila siku
ambayo ni Makutano Makuu ya
kanisa yalivyo hayana idadi (Ufunuo
7:9).
Vyombo vyote vilivyokuwa
kwenye Nyumba ya Mungu vilitengenezwa au vilikuwa vya
dhahabu kwa amri na maelekezo
ya mfalme, ambaye ndiye Sulemani, ambaye ni ishara ya Masihi ambaye ndiye mwenye
jumukumu kwa Kanisa la Mungu kupitia Roho Mtakatifu.
Vile vinara vya taa vilikuwa ni vya dhahabu safi
pia ambavyo walivitumia kuviwasha mbele za Bwana. Pia taa zote na vishikio
au koleo na beseni zote na mishumaa na
vijiko na vyetezo vyote hivi
vilikuwa vya dhahabu na kama
yalivyokuwa miaango yote ya kuingilia kwenye nyumba na
milango yote mingine midogomidogo, ya sehemu zote mbili, za ndani na
za Mahali Patakatifu au
Naos pia na milango ya nyumba za Hekalu (aya
za 21-22). Na idadi ya maandiko mengine yalioishia kwenye aya ya 22.
Mungu hakufifisha nuru na alikuwa na
mawazo makamilifu na mpangilio. Kwa hiyo, ndivyo tupaswavyo
kuwa hihi wateule tuwe watakatifu na kutakaswa kama
dhahabu na kuwa waelekevu au tunaofundishika.
2Mambo ya Nyakati 5:1 Hivyo ikaisha kazi yote Sulemani aliyoifanyia nyumba ya Bwana. Sulemani akaviingiza vitu alivyovitakasa baba yake Daudi; fedha, na dhahabu, na vyombo vyote, akavitia ndani ya hazina za nyumba ya Mungu.
Hivi vilikuwa ndiyo vifaa vilivyoelekezwa kwenye maandalizi, na ndizo hatimaye
zililetwa Hekaluni lilipokamilika. Kwa hiyo kulikuwa na vifaa
vilivyotumika kwenye ujenzi na kulikuwa
na vifaa vilivyotengwa maalumu kwa kutumiwa baada
ya awamu ya kwanza ya ujenzi
ilipokamilika.
2Mambo ya Nyakati 5:2 Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.
Wakati Hekalu lililokuwa tayari, ndipo Sanduku la Agano lililetwa Yerusalemu. Kwa hiyo, Sanduku hili
la Agano ni ishara ya Roho Mtakatifu kuwa ndani ya wateule, ambaye anafana makao yake huko
Yerusalemu baada ya Masihi kuikamilisha awamu ya kuu ya kwanza. Wokovu pia ni wa
watu wa Yuda na Yerusalemu kwenye
awamu ile, ni kama ulivyo kwa
Israeli wote.
Katika mwezi wa saba wanaume
wote wa Israeli walikusanyika mbele za mfalme wakati
wa sikukuu. Wazee wote wa
Israeli walikuja na Walawi walilibeba Sanduku la
Agano mabegani mwao na maskani ya mkusanyiko
wote hadi Hekaluni. Kwa hiyo vitu hivi vyote
vilikuwa Wakfu na Vitakatifu kwa
Bwana pamoja na wale wote waliojihudhurisha
kwenye kusanyiko hili lililofanyika kwenye Hekalu la Mungu mbele za
Israeli na walimtolea dhabihu Bwana Mungu. Kwa ajili hii, wateule wote
wa Israeli watapanda kwenda kwa Bwana huko Yerusalemu na kujihudhurisha mbele za Bwana na mbele ya Sanduku
la Agano ambalo ndilokituo au makao ya cha
Naos na ni makao ya Roho
Mtakatifu. Viliwekwa chini
ya kerubi d ambalo ni elohim wa Ufufu
wa Kwanza wa Wafu.
2Mambo ya Nyakati 5:3-14 Wakakutana watu wote wa Israeli mbele ya mfalme wakati wa sikukuu, katika mwezi wa saba. 4 Wakaja wazee wote wa Israeli, nao Walawi wakajitwika sanduku. 5 Wakalipandisha sanduku, na ile hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwamo Hemani, vitu hivyo makuhani Walawi wakavipandisha. 6 Mfalme Sulemani, na mkutano wote wa Israeli, waliokutanika kwake, walikuwako mbele ya sanduku, wakichinja dhabihu za kondoo na ng'ombe, wasiohesabika wala kujumlishwa kwa kuwa wengi. 7 Makuhani wakaliingiza sanduku la agano la Bwana mahali pake katika chumba cha ndani cha nyumba, patakatifu pa patakatifu, yaani, chini ya mabawa ya makerubi. 8 Kwa maana makerubi yalinyosha mabawa yao juu ya mahali pa sanduku, makerubi yakalifunika lile sanduku na miti yake kwa juu. 9 Na ile miti ilikuwa mirefu, hata ncha za miti zilionekana sandukuni mbele ya chumba cha ndani, lakini hazikuonekana nje; nayo iko kuko huko hata leo.
Sanduku la
Agano lilikuwa ishara ya mioyo ya wateule ambao walipaswa kumpokea Roho Mtakatifu na ambao walikujakuwa elohim au wana
wa Mungu. Mioyoni mwao ziliwekwa
sheria za Mungu.
10 Hamkuwa na kitu ndani ya sanduku, ila zile mbao mbili alizozitia Musa huko Horebu, Bwana alipofanya agano na wana wa Israeli, hapo walipotoka Misri.
Kwa hiyo maelezo kuhusu
Sanduku la Agano yamepunguzwa
ili kuzionyesha kuwa ni sheria za Mungu
tu zitakazokuwa mioyoni mwa wateule. Hatimaye
wateule walifanyika kuwa ni
makuhani wa Melikizedeki.
11
Ikawa makuhani walipokwisha kutoka katika patakatifu; (kwani makuhani wote waliokuwapo, walikuwa wamejitakasa, wala hawakuzishika zamu zao; 12 tena
Walawi waimbaji, wote pia, yaani
Asafu, na Hemani, na Yeduthuni, na
wana wao, na ndugu zao, hali
wamevaa kitani safi, wenye matoazi
na vinanda na vinubi, wamesimama
upande wa mashariki wa madhabahu,
na pamoja nao makuhani mia na
ishirini wakipiga panda;) 13 hata ikawa,
wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha
sauti moja ya kumsifu na kumshukuru Bwana nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na
vinanda, wakimsifu Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili
zake ni za milele; ndipo nyumba
ikajawa na wingu, naam, nyumba
ya Bwana, 14 hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya
huduma yao, kwa sababu ya lile wingu; kwa kuwa nyumba ya Mungu imejaa utukufu
wa Bwana.
Sanduku hili
la Agano haliteweza kuingizwa
mioyoni tena (soma jarida
la Sanduku la Agano (Na. 196)). Matokeo yake ni kwamba Roho Mtakatifu, ambayefundisha
Torati ya Mungu na kuwawezesha wateule kuielewa ataliweka tena Sanduku hili la kimwili la Agano na atawaongoa Yuda na Israeli katika Siku za Mwisho, lakini
ni pale tu baada ya kuwa sehemu—Kanisa
la Mungu–litakapokuwa limeanzishwa.
Yerusalemu ilichakuliwa
na Hekalu lilijengwa huko ili kupafanya kuwa ni mahali ambapo Mungu
atapachagua kufanya makao yake lakini
palikuwa ni kwa watu wote na
sio kwa ajili
ya Yuda na Israeli peke yao
na haikuwa ni urithi wa Yuda tangu mwanzo ila
lililetwa na Daudi kwa ajili ya Hekalu
na hatimaye ukafanyika kuwa ni mji wa Wayebusi kwa
Israeli kama ilivyokuwa ni lengo la siku za
Ibrahimu na Shemu akiwa kama Kuhani wa Melkizedeki (soma jarida la Melikizedeki (Na. 128).
2Mambo ya Nyakati
6:1-42 inafanya taswira ya maandiko yaliyo kwenye vitabu vya
Wafalme, na Sulemani aliwabariki makutano wa Israeli na kuonyesha
kuwa ndiye aliyechaguliwa miongoni mwa wana
wa Daudi kulikamilisha
Hekalu.
Ndipo
Sulemani akainuliwa na kuongezeka kama mwana wa Daudi na kwa hiyo
alimuwakilisha Masihi kama wana wa
Daujdi. Kisha akaomba akiwa
amesimama kwenye mimbari ya shaba kuwaombea Israeli wote. Andiko lililo kuanzia
aya ya 12 linasema kuwa mimbari hii ilikuwa
ni ya shaba na maombi yalifanyika kwenye uwa wa
hekalu. Lakini haya ndiyo yalikuwa ndiyo maombi yake kwa
Mungu ambayo ni fundisho kwa Wafalme.
2Mambo ya Nyakati 6:12-42 Akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana, machoni pa mkutano wote
wa Israeli, akainyosha mikono; 13 (maana
Sulemani alikuwa amefanya mimbari ya shaba, urefu wake mikono
mitano, na upana wake mikono
mitano, na kwenda juu kwake
mikono mitatu, na kuisimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake,
akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea mbinguni);
14 akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe,
mbinguni, wala duniani; ushikaye maagano na rehema
kwa watumishi wako, waendao mbele
zako kwa moyo wao wote; 15 uliyemtimizia
mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidi;
naam, ulinena kwa kinywa chako,
ukayatimiza kwa mkono wako, kama
ilivyo leo. 16 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, umfikilizie mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia,
ukisema, Hutakosa kuwa na mtu machoni
pangu, wa kuketi katika kiti
cha enzi cha Israeli; wakiwa tu watoto wako wataiangalia
njia yao, ili kuiendea torati yangu, kama wewe
ulivyokwenda mbele zangu. 17 Basi sasa,
Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia
mtumishi wako Daudi. 18 Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu
duniani? Tazama, mbingu na mbingu
za mbingu za mbingu hazikutoshi;
siuze nyumba hii niliyoijenga!
19 Walakini umwangalie mtumwa wako anayoyaomba, na kusihi, Ee
Bwana, Mungu wangu, usikie kilio na
maombi anayoyaomba mtumwa wako mbele
zako; 20 ili
macho yako yafumbuke kwa nyumba hii
mchana na usiku, mahali uliponena,
ndipo utakapoliweka jina lako; usikie maombi
atakayoomba mtumwa wako, akikabili mahali hapa. 21
Uyasikie atakayosihi
mtumwa wako, na watu wako
Israeli, watakapoomba wakikabili
mahali hapa; naam, usikie toka
makaoni mwako, toka mbinguni, nawe usikiapo, samehe. 22 Ikiwa
mtu amemkosea mwenzake, akitiwa kiapo, aapishwe, naye akija na kuapa
hapa mbele ya madhabahu yako nyumbani humu; 23
basi, usikie mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimlipiza mwovu, kumpatilizia njia yake kichwani;
ukamfanyie haki mwenye haki, ukimjalia
kwa kadiri ya haki yake. 24 Ikiwa watu wako
Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa
sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea
kwako, na kulikiri jina lako, wakikuomba na kukusihi
nyumbani humu; 25 basi usikie
huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watu wako Israeli, na kuwarejeza tena katika nchi uliyowapa
wao na baba zao. 26 Ikiwa mbingu
zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa
sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba
wakikabili mahali hapa, na kulikiri
jina lako, na kuiacha dhambi yao, uwatesapo; 27 basi
usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu
wako Israeli; uwafundishapo
njia njema iwapasayo waiendee; ukainyeshee mvua nchi yako, uliyowapa
watu wako iwe urithi. 28 Ikiwa nchi imeingia
njaa, au tauni, au ukosefu
wa mvua, au ukungu, au
nzige, au panzi; ikiwa adui
wamewahusuru katika nchi ya miji yao, au ukiwapo msiba
wo wote, au uele wo
wote; 29 yo yote atakayoyaomba na kusihi mtu
awaye yote, au watu wako
Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu pigo lake
mwenyewe, na msiba wake mwenyewe,
akiinyoshea mikono nyumba hii; 30 basi usikie huko
mbinguni, ukaapo, ukasamehe, ukampatilize kila mtu kwa
kadiri ya njia zake zote; wewe umjuaye moyo; (maana wewe peke yako
ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu); 31 ili wakuche
wewe, waziendee njia zako, siku
zote watakazoishi katika nchi uliyowapa baba zetu. 32 Hata na
mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu
wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo
mbali sana kwa ajili ya jina lako kuu, na mkono
wako ulio hodari, na mkono
wako ulionyoshwa; hao watakapokuja na kuomba wakiielekea nyumba hii; 33 basi usikie huko
mbinguni, toka makaoni mwako, ukatende yote atakayokuomba
huyo mgeni; ili watu wote wa
dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha wewe,
kama watu wako Israeli, tena wajue ya kuwa nyumba hii niliyoijenga
imeitwa kwa jina lako. 34 Ikiwa
watu wako wametoka kupigana na adui zao,
utakakowatuma ko kote, wakikuomba kuuelekea mji huu
uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga
kwa jina lako;35 basi uyasikie huko
mbinguni wayaombayo, na kusihi, ukaitetee
haki yao. 36 Wakikukosa, (maana hakuna mtu asiyekosa),
hata uwakasirikie, na kuwatia mikononi
mwa adui zao, wawahamishe, na kuwachukua mateka
mpaka nchi iliyo mbali au
iliyo karibu; 37 basi wakikumbuka
katika nchi walikohamishwa, na kutubu, na kukusihi
katika nchi ya uhamisho wao, wakisema, Tumekosa, tumetenda kwa ukaidi, tumefanya
maovu; 38 wakurudiapo kwa mioyo yao yote, na kwa nia
zao zote, katika nchi ya uhamisho wao, adui walikowahamisha, wakiomba na kuielekea
nchi uliyowapa baba zao, na mji
huu uliouchagua, na nyumba hii
niliyoijenga kwa jina lako; 39 basi
uyasikie toka mbinguni, toka makaoni mwako, wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao; ukawasamehe watu wako, waliokosa
juu yako. 40 Na sasa,
Ee Mungu wangu, macho yako yafumbuke, nakusihi, masikio yako yakasikilize
maombi yaombwayo mahali hapa. 41
Sasa, Ee Bwana, Mungu,
uondoke, uende kwenye raha yako,
wewe na sanduku
la nguvu zako; makuhani wako, Ee Bwana, Mungu, wavikwe wokovu, watakatifu wako na washangilie mema. 42 Ee Bwana, Mungu,
usiurudishe nyuma uso wa masihi wako,uzikumbuke fadhili za Daudi mtumishi wako.
Uponyaji ulombwa kwa wote
katika msamaha wa dhambi. Kwa hiyo wakfu wa
Nyumba hii ya Mungu ulikuwa ili
kwamba Wamataifa waweze kuokolewa pia, na ili
wamrudie na kumuomba Mungu chochote wakitakacho na wangepewa.
Baada ya Sulemani kumaliza maombi yake, moto ulishuka kutoka Mbinguni na kuiteketeza ile sadaka ya kuteketezwa ikiwa ni ishara kwa mba Mungu
alikuwa ametasikia na kuyakubali maombi
yao. Kwa hiyo Israeli walikijua
sana na walijihadhari sana kwa kile Mungu
alichokifana. Kwa hiyo, takriban miaka mia tano tangu kipindi cha Kutoka
kwao utumwani, Israeli waliweza kuziona tena ishara zikitolewa zinazoashiria uwepo wa Malaika wa Bwana katikati yao akiwa kama Yahova wa Israeli, ambaye ndiye Yesu Kristo (Zaburi 45:6-7; Waebrania 1:8-9).
2Mambo ya Nyakati 7:1-22 Basi Sulemani alipokwisha maombi hayo, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; utukufu wa Bwana ukaijaza nyumba. 2 Wala makuhani hawakuweza kuingia nyumbani mwa Bwana, kwa kuwa utukufu wa Bwana umeijaza nyumba ya Bwana. 3 Wakatazama wana wa Israeli wote, uliposhuka ule moto, utukufu wa Bwana ulipokuwapo juu ya nyumba; wakasujudu kifulifuli hata nchi sakafuni, wakaabudu, wakamshukuru Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele. 4 Ndipo mfalme na watu wote wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
Andiko hili linaonyesha kwamba Maskani na hatimaye Hekalu zote hizi zilijazwa na utukufu wa
Bwana. Moto ulioshuka kutoka
mbinguni na kuiteketeza dhabihu ilikuwa ni taswira ya Hekalu la Kiroho ambalo lingeweguswa na moto siku ya Pentekoste mwaka 30BK na wateule walianza
kuwa Hekalu la Kiroho lililojazwa
au lililotengenezwa kwa dhabihu ya wanadamu waliojitoa kwa Bwana Mungu na ambalo lingechukua
mahala pa lile Hekalu la Kimwili la Yerusalemu na ambalo
liliangushwa na kuharibiwa mwaka 70BK kama ilivyokuwa imetabiriwa kwenye Danieli 9:25 nk. Washirika wa
dhabihu hii walikuwa na maana
yake ya kiroho. Kila kitu kiliandaliwa tangu mwanzoni kama walivyokuwa wote zana na waimba
Zaburi.
5 Mfalme Sulemani akatoa sadaka ya ng'ombe ishirini na mbili elfu, na kondoo mia na ishirini elfu. Ndivyo mfalme na watu wote walivyoifanya wakfu nyumba ya Mungu. 6 Wakasimama makuhani sawasawa na malinzi yao; Walawi nao pamoja na vinanda vya Bwana, alivyovifanya Daudi mfalme, ili kumshukuru Bwana, kwa maana fadhili zake ni za milele, hapo aliposifu Daudi kwa mikono yao; nao makuhani wakapiga panda mbele yao; nao Israeli wote wakasimama. 7 Tena Sulemani akaitakasa behewa katikati, iliyokuwa mbele ya nyumba ya Bwana; kwa kuwa hapo ndipo alipotoa sadaka za kuteketezwa, na mafuta ya sadaka za amani; kwa sababu ile madhabahu ya shaba aliyoifanya Sulemani haikutosha kuzipokea sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga, na mafuta. 8 Basi, wakati ule Sulemani akafanya sikukuu, na Israeli wote pamoja naye, kusanyiko kubwa sana, toka maingilio ya Hamathi mpaka kijito cha Misri, muda wa siku saba. 9 Hata siku ya nane wakaita kusanyiko la makini; kwa maana walishika kuitakasa madhabahu siku saba, na sikukuu siku saba. 10 Akawaruhusu watu waende hemani kwao siku ya ishirini na tatu, ya mwezi wa saba, wakifurahi na kuchangamka mioyoni kwa wema wote Bwana aliomfanyia Daudi, na Sulemani, na Israeli watu wake. 11 Hivyo Sulemani akaimaliza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme; na yote yaliyomwingia Sulemani moyoni ayafanye nyumbani mwa Bwana, na nyumbani mwake mwenyewe, akayafanikisha.
Sikukuu ya Mwezi wa Saba iliadheimishwa
kwa siku kumi na nne,
siku saba zikiwa ni kwa ajili ya kuiweka
wakfu madhabahu, na siku saba nyingine
zikiwa ni kwa ajili ya maadhimisho ya Sikukuu ya Vibanda. Uwekaji wakfu ulikuwa
ni kuanzia siku ya 8 hadi ya 14 ya mwezi wa Ethanimu, na siku saba nyingine za Sikukuu zilikuwa
tangu siku ya 15 hadi 21 Ethanimu. Siku ya Mkutano wa Makini ilikuwa ya 22 Ethanimu, na siku ya 23 Ethanimu
walirejea majumbani au makaoni kwao.
Siku ya Kutaniko la Makini au
Iliyokuu ya Mwisho haikuhesabiwa kuwa ni ya Sikukuu kwenye hesabu hizi.
Siku Iyiyo Kuu ya Mwisho iliyo
kwenye nyakati za mwisho inafanya
taswira ya Hukumu itakayotolewa kwenye Kiti cha Enzi Kikubwa Cheupe na sio sehemu ya kipindi
cha utawala wa millennia. Ni siku ya Ufufuo wa Pili wa Wafu
na inahusiana na hukumu ya ulimwengu
na watu wake
wote. Kwenye mwandamano wa matukio
ya mwezi Tishri yaliyo taswira ya mwisho wa zama hizi
yanahusiana na Yubile ya mwaka 2027. Kisha marejesho yatakuwa yamekamilika na watu wanarudi kwenye
nchi au ardhi
zao katika Israeli na ulimwenguni kote kwingineko.
Matukio haya pia yanahusiana na mwisho wa
zama hizi. Siku ishirini na moja zilizotajwa kukamilisha kipindi cha mlolongo
huu na kufikia
kwenye mfumo wa kimillenia ulioelezewa
kwa kina kwenye jarida la Utakaso wa Mataifa
(Na. 77). Mchakato huu ni migawanyo mitatu yenye siku saba saba na marejesho
ya utawala mpya huko Yerusalemu. Kwa hiyo, awamu ya kwanza ya miaka saba ya kwanza ya Utakato itatupeleka hadi mwaka 2012, ambacho ni kipindi cha kuwajibika
kwa Kanisa. Mafundisho yake yanapaswa yawe sahihi na
yamekamilika ya yachapishwe
kwa mataifa yote kwa kipindi
hiki. Ufunguo wa Daudi limepewa Kanisa aminifu na adilifu
la Siku za Mwisho, linaloandika na kuchapisha au kutangaza
mafundisho asilia ya Kanisa
la Mungu yaliyotumika tangu karne ya Kwanza.
Hii inamaana ni mfumo wa kiimani wa
Waamini Mungu Mmoja na Wasiochanganya Imani na miungu Mingine
au Wayuniratiani wa Kimonotheisti pamoja na mafundisho
yasiyoghoshiwa, pamoja na fundisho kuhusu
Kalenda Takatifu amoja na Mwandamo wa Mwezi Mpya. Huu ndiyo Ufunguo wa
Daudi katika kuelezea wa mwandamano wa
matukio katika Siku za Mwisho kiunabii.
Kwenye awamu hii hapa,
kwenye mwandamano wa mambo ya Hekaluni, Utakaso wa Madhabahu
kwa kweli kwa kweli ni shughuli
ya pili iliyokuwa inafanyika siku saba za mwezi wa
Tishri, ikifuatiwa na siku ya Nane ya mwezi wa Tishri, au mwaka
2013 kwa hesabu za mwaka mmoja
kwa siku kuelekea kwenye Yubile ya mwaka 2027. Siku saba za mwisho za
mchakato wa kuwatiisha mataifa kutoka Yerusalemu chini ya Masihi tangu mwaka
2019 hadi 2026 (soma jarida
la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142)). Yubile ya mwaka 2027 inakamilisha mchakato na mwaka
2028 ni mwanzo wa utawala Mpya wa
Milenia. Mwaka huu wa 2028 Marejesho ya \utawala wa Milenia na kanuni
zake yatafanyika, na utaratibu wa
Hekalu na usimamizi wake na mambo yote ya kiuatawala huko Yerusalemu yatawekwa, kama nyumba za
Mfalme na Ukumbi wa kutolea
Hukumu. Kutoka huko ndipo hukumu
zitatolewa kwa watu wote ulimwenguni.
12 Bwana akamtokea Sulemani usiku, akamwambia, Nimesikia uliyoyaomba, na mahali hapa nimejichagulia kuwa nyumba ya dhabihu. 13 Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; 14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. 15 Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa. 16 Maana sasa nimeichagua nyumba hii na kuitakasa, ili kwamba jina langu lipate kuwako huko milele; yatakuwako na macho yangu, na moyo wangu daima. 17 Nawe, ukienda mbele yangu kama alivyokwenda Daudi baba yako, ufanye sawasawa na yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu; 18 ndipo nitakithibitisha kiti cha enzi cha ufalme wako, kama nilivyoagana na Daudi baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kutawala katika Israeli. 19 Lakini mkigeuka, na kuziacha sheria zangu na amri zangu nilizoweka mbele yenu, mkienda, na kuitumikia miungu mingine, na kuiabudu; 20 ndipo nitawang'oa katika nchi yangu niliyowapa; na nyumba hii niliyoitakasa kwa jina langu, nitaiondosha itoke mbele zangu, nami nitaifanya kuwa mithali na tukano katikati ya watu wote. 21 Na nyumba hii, iliyo juu, kila apitaye ataona ushangao, atasema, Mbona Bwana ameitendea hivi nchi hii, na nyumba hii? 22 Nao watajibu, Kwa sababu walimwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka nchi ya Misri, wakashikamana na miungu mingine, wakaiabudu, na kuitumikia; kwa hiyo ameyaleta mabaya haya yote juu yao.
Sulemani alikuwa ametahadharishwa vya kutosha kwa
kile kingalichotokea kama wangejiingiza kwenye ibada za
sanamu, lakini hatimaye yeye mwenyewe alijikwaa kwa hilo na akafanya hivyo.
2Mambo ya Nyakati 8:1- Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani aliijenga nyumba ya Bwana, na nyumba yake mwenyewe; 2 ndipo Sulemani akaijenga miji ile Hiramu aliyompa Sulemani, akawakalisha humo wana wa Israeli. 3 Naye Sulemani akaenda Hamath-zoba, akaushinda. 4 Akaujenga Tadmori wa nyikani, na miji yote ya hazina, aliyoijenga katika Hamathi. 5 Tena akaujenga Beth-horoni wa juu, na Beth-horoni wa chini, miji yenye boma, yenye kuta, na malango, na makomeo; 6 na Baalathi, na miji yote ya hazina Sulemani aliyokuwa nayo, na miji yote ya magari yake, na miji ya wapanda farasi wake, na ya anasa yote aliyopenda Sulemani kujenga humo Yerusalemu, na katika Lebanoni, na katika nchi yote ya mamlaka yake. 7 Basi kwa habari ya watu wote waliosalia wa Wahiti, na wa Waamori, na wa Waperizi, na wa Wahivi, na wa Wayebusi, wasiokuwa wa Israeli; 8 wa watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuwakomesha, katika hao Sulemani akawatumikisha shokoa hata leo. 9 Wala katika wana wa Israeli Sulemani hakuwafanya watumwa kazini mwake; lakini hao walikuwa watu wa vita, na wakuu wa majemadari wake, na maakida wa magari yake na wa wapanda farasi wake. 10 Na hao walikuwa maakida wakuu wa Sulemani, watu mia mbili na hamsini, waliotawala juu ya watu. 11 Sulemani akamleta binti Farao kutoka mji wa Daudi mpaka nyumba aliyomjengea; kwa kuwa alisema, Mke wangu hatakaa nyumbani mwa Daudi mfalme wa Israeli, kwa kuwa ni patakatifu, mahali palipofika sanduku la Bwana. 12 Ndipo Sulemani akamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, aliyoijenga mbele ya ukumbi, 13 kadiri ilivyohitajiwa huduma ya kila siku, akitoa sawasawa na amri ya Musa, siku za sabato, na za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoamriwa, mara tatu kila mwaka, yaani, sikukuu ya mikate isiyochachwa, na sikukuu ya majuma, na sikukuu ya vibanda.
Kumbuka kwamba binti Farao
hakuruhusiwa kuishi mahali ambapo Sanduku
la Agano liliwekwa kwenye nyumba ya Daudi. Kitendo hiki kingemsababishia kuingia kwenye ibada hizi za
sanamu za mataifa, jambo ambalo halikuruhusiwa kwenye Hekalu la Mungu au kwenye makao
ya Naos kama Watu walio kwenye Nyumba ya Daudi ambao walipaswa kuwa ni elohim.
Mwanamke huyu mwenyewe tu aliruhusiwa kujijengea madhabahu kwa ajili
ya mungu wake huko Kidroni na
wengine wengi.
Sulemani akaweka mkazo kwenye Torati ya Mungu na Kalenda na akazitunza Sabato na Miandamo ya Mwezi Mpya ma kuzisisitiza kuwa ni Siku Takatifu za Mapumziko na maadhimisho, pamoja na mkazo wa kuzishika Sikukuu; ambazo tunaziadhimisha mara tatu kila mwaka, sawasawa na vilivyo kwenye Kalenda Takatifu (soma jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156)). Utaratibu huu wa kalenda ulipaswa ushikwe hivyo tangu mwanzo hadi kuangamizwa kwa Hekalu mwaka 70 BK. Haya hivyo, mara ningi ilikuwa haishikwi, na Sikukuu na Usomaji wa Torati mara nyingi ulikuwa haufanywi kabisa kutokana na hali ya ukengeufu na ugumu wa mioyo au wavivu.
Utaratibu uliowekwa na Daudi ulianzishwa na kushikwa hadi na wafinyanzi waliotengeneza malango, na kilakitu kilikuwa na maana kwa ajili ya Hekalu lijalo la kipindi cha Yesu Kristo.
14 Akaziamuru, sawasawa na agizo la Daudi babaye, zamu za makuhani za kutumika, nao Walawi kwa kadiri ya malinzi yao, ili kusifu, na kuhudumu mbele ya makuhani, kama ilivyohitajiwa kila siku; tena mabawabu kwa zamu zao za kila mlango; maana ndivyo alivyoamuru Daudi mtu wa Mungu. 15 Wala hawakuyaacha maagizo ya mfalme aliyowaamuru makuhani na Walawi kwa neno lo lote, wala kwa habari ya hazina. 16 Basi ikatengenezwa kazi yote ya Sulemani hata siku ya kutiwa msingi wa nyumba ya Bwana, na hata ilipokwisha. Hivyo ikamalizika nyumba ya Bwana. 17 Ndipo Sulemani akaenda Esion-geberi, na Elothi, pwani ya nchi ya Edomu. 18 Naye Hiramu akamletea merikebu kwa mikono ya watumishi wake, na watumishi waliokuwa wana-maji; nao wakafika Ofiri pamoja na watumishi wa Sulemani, wakachukua kutoka huko talanta mia nne na hamsini za dhahabu, wakamletea mfalme Sulemani.
Kuna kazi nyingine mbili kamili pia kufanyika Hekaluni nje na Israeli huko Misri ambazo zilizofanyika wakati Hekalu la Yerusalemu lilikuwa halifanyi kazi zake kutokana na kuangamizwa kwake na Wababeloni na utumwa na pamoja kutokana na ujenzi wa Mahali pa Juu na Onias IV huko Gosheni huko Heliopolis wakati Kristo alipokwenda huko.
Mahekalu yalikuwa:
1. Hekalu la Sulemani liliangamizwa na Wababeloni;
2. Hekalu lililokarabatiwa kwa amri au agizo la Koreshi na Dario na II na Utoaji wa Amri wa Artashasta II (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13));
3. Hekalu lililojengwa na Herode ambalo ni miaka 46 tangu lilipojengwa hadi pale Kristo alipolitabiria kuwa litakuja kubomolewa na kwamba atalijenga tena kwa siku tatu (Yohana 2:19-20).
Mungu aliruhusu Hekalu hili lijengwe tena na Herode ili kuonyesha uhusiano uliopo kati ya ujio wa Masihi na uhusiano kati ya mwanadamu kama Hekalu na makusudio makamilifu ya uumbaji na kumpokea Roho Mtakatifu kama wana wa Mungu au elohim. Mwaka wa 70 BK baada ya juma la sabini la miaka lilihusuriwa au kubomolewa ili kwamba mwanadamu awe ni Hekalu pekee au Naos lililoachwa hadi kufikia kipindi cha kurudi kwa Masihi.
q