Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[298]

 

 

 

Vita Vya Warumi na Kunguka kwa Hekalu

(Toleo La 1.0 20060902-20060902)

 

Nabii Danieli alionyeshwa maono akionyeshwa kipindi cha Majuma Sabini ya Miaka. Matukio ya juma la mwisho la miaka yalikuwa ni maafa kwa Yuda na kwa Waedomu. Unabii huu unaweza kueleweka tu kuwa unauhusiano na Hekalu. Wakristo wengi wameutafsiri kimakosa sana unabii huu wa Danieli 9:25-27 kwa faida zao wenyewe utakaowafikisha kwenye mwisho mbaya. Vita vitakavyopiganwa na Warumi na mwenendo wa Yuda kwa kipindi hiki vimesababisha hali ya kutawanyika kwao Yuda hadi siku za mwisho.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

 

(Haki Miliki © 2006 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 

 


Vita Vya Warumi na Kuanguka kwa Hekalu

 


Utangulizi

Nabii Danieli anakitaja kipindi kijulikanacho kama cha Majuma Sabini ya Miaka ambacho kinahesabiwa kuanzia kipindi cha kutolewa amri ya kujengwa kwa Hekalu huko Yerusalemu hadi kile cha maangamizo yake mwaka 70BK. Historia hii imeelezewa kirefu kwenye jarida letu la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)].

 

Danieli 9:25-27 inasema: 24Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana. 25Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuweko majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu. 26Baada ya majuma sitini na mawili Mpakwa mafuta atakatiliwa mbali wala hatabakia na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa. 27Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamuriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.


Tunajua kwamba mtiwa mafuta wa kwanza alikuwa ni Nehemia, aliyeteuliwa na mfalme aende na kuwa liwali wa Yuda, na ndiye aliyefanya kazi ya kusimamia ujenzi wa kuta na kulikarabati na kulirembesha kwa mapambo Hekalu, kazi aliyoifanya akiwa na Ezra mwandishi. Hiki kilikuwa ni kipindi cha utawala wa Artashasta II. Ezra alikufa mwaka 323KK, ni mwaka huohuo ndio aliokufa Mfalme Iskanda Mkuu, na kazi ya kuyapitia na kuhakiki maandiko ilihitimishwa na kufungwa mwaka 321.

 

Mwishoni mwa kipindi cha pili cha majuma sitini na mawili ya miaka kilishuhudia tukio la kuuawa kwa mtiwa mafuta mwingine naye alikuwa ni Yakobo (James) aliyekuwa ni Askofu wa Yerusalemu na ndugu wa Yesu Kristo. Baada ya kuuawa kwake Yakobo huko Yerusalemu, Kanisa liliachwa kwenye uongozi wa Simon (Simon mwana wa Yose) aliyekuwa ni binamu wa Yesu Kristo na mwana wa Mariamu na Klopa. Mariamu huyu alikuwa ni dada wa Mariamu mama wa Yesu Kristo. Na huyu Klopa alikuwa askofu wa Yerusalemu, kipindi kinachodhaniwa kuwa ni cha kati ya utawala wa Yakobo nduguyake Kristo (takriban mwaka 64BK) na inadhaniwa kuwa huyu Simon mwana wa Klopa na binamu ya Kristo (soma kitabu cha Hippolytus sehemu ya Nyongeza ya jarida la Kuanza Kwa Kanisa la Kikristo Nchini Uingereza (Na. 266) [Origin of the Christian Church in Britain (No. 266)].

 

Simon alichukua usimamizi wa Kanisa (baada ya kifo cha Klopa) na walikimbilia mahala paitwapo Pella, wakiyatii maonyo yaliyotolewa kwenye unabii wa nabii Danieli. Kanisa lilikuwa kwenye hali ya shida na uhitaji mkubwa, na kwa kweli lilisaidiwa na makanisa yaliyokuwa Asia Ndogo.

 

Maandiko yaliyo kwenye kitabu cha Danieli yanasema kwamba mfalme anayekuja atafanya agano thabiti na wengi kwa kipindi cha juma moja, na kwa kipindi cha nusu juma ataikomesha dhabihu na sadaka. Anaendela kwa kusema kuwa kwenye kipindi hiki cha chukizo la uharibifu, atakuja mtu atakayefanya uharibifu hadi kutakapotolewa amri itakayotangazwa na mharibifu huyu. Sentensi ya mwisho inaelezea kipindi muhimu ambacho hakihusiani na kipindi hiki cha Majuma Sabini ya Miaka ila inakiongelea kipindi ambacho mfumo huu unaoelezewa utakapokuwa umekomeshwa.

 

Kipindi hiki cha juma la miaka kinachoelezewa hapa ni cha kuanzia mwaka 62 hadi 69BK na mwaka wa mwisho ulikuwa ni ule wa 70BK.

 

Kilele chake kilikuwa ni mwishoni mwa miaka 490 ya Majuma Sabini ya Miaka kabla ya Pasaka ya mwaka 70BK, imeelezwa kwamba mnamo siku ya 1 mwezi wa Abibu, Jeshi la Warumi liliuzingira mji wa Yerusalemu. Huu ulikuwa ni Mwaka Mpya. Pia ulikuwa ni kipindi kamili cha mwisho wa “Miaka Arobaini ya Toba” walichopewa Yuda tangu Pasaka ya mwaka 30BK.


Juma la mwisho la miaka lilikuwa ni miaka saba inayoendelea hadi leo. Katika kipindi kile Kanisa lilikimbilia huko Pella kwenye kipindi cha manzo wa juma, baada ya kifo cha Yakobo (na huenda ni yule mwana wa Klopa). Katikati ya juma lile (au kipindi cha Sabato), mlolongo wote wa matatizo ulitokea katika Yudea. Matukio mawili ya Wayahudi yaliuzingira Mji wa Daudi na Mlima uliojengwa Hekalu na kuanzisha harakati za vita vya wenyewe kwa wenyewe kutoka kwenye ngome zao. Mwanahitoria Josephus anayaelezea maafa haya pia. Anasema kuwa matendo mabaya waliyowafanyia Warumi yalikuwa ni afadhali kuliko yale waliyoyasababisha wao wenyewe.


Kwenye kitabu chake Emile Schürer (kinachoitwa Historia ya Watu wa Jamii ya Kiyahudi Kwenye Kipindi Cha Yesu Kristo, (History of the Jewish People in the Age of Jesus Christ),  Matoleo ya. 1–3, ya T &T Clark, Rev. ed. Mwaka 1987) yanatoa historia hii kwa kirefu sana na jarida hili linatuama kwenye maelezo ya Schürer na Josephus.

 

Liwali wa Yudea kipindi kile alikuwa ni Gessius Florus (miaka ya 64-66BK). Alikuwa ni mtu muhimu na wa kuaminika sana na maliwali wa Kirumi, na Josephus anashindwa kuwa na maneno ya kumelezea jinsi alivyokuwa na uwezo mkubwa wa kimaongozi. Albinus alijulikana kuwa ni “mtu mwema na mpenda haki” na alifananishwa naye. Albinus alikuwa anayashughulikia matendo maovu kwa siri, bali Florus alikuwa anayaanika na kuyashughulikia hadharani pasipo uficho, na hakuridhia matendo ya wizi kwa mtu yeyote, bali “aliiteka miji yote na kuteketeza jamii zote zilizofanya hivyo. Lakini kadri wezi na majambazi walipommshirikisha mambo yao machafu na yeye waliyafanya mambo yao pasipo kizuizi” (Schürer, Toleo la 1, ukurasa 470, akinukuu kitabu cha Josephus, kiitwacho Vita vya Wayahudi [Wars of the Jews] (B. J.). ii. 14, 2; na Antiq, xx 11, 1). Schürer anaielezea hali kuwa ilikuwa mbaya sana kwa kiasi kisichovumulika na kulihitajika chembe moja tu kuweza kusababisha mlipuko ambao ungeshinikizwa na nguvu za asilia.

 

Kwa hiyo, Florus aliridhia sana na kupendezwa na tabia hii ya kuwapora watu, lakini kwenye kipindi cha katikati ya juma la miaka Florus alipora vitu vya thamani vilivyokuwa kwenye hazina ya Hekalu la Yerusalemu vya talenti kumi na saba. Jambo hili lilichokoza hali ya jazma na vurugu. Baadhi ya wale waliochanganikiwa na kuchukizwa na hali hii walipata wazo la kutembeza vikapu na kuchangisha misaada ya kumpa Florus waliomdhihaki kuwa maskini, na ndipo Florus alichukizwa na kuamua kuwaadhibu kwa ajili ya dhihaka waliyomfanyia. Idadi kubwa ya wananchi wakiwemo mashujaa wanaotoka kwenye koo za daraja la juu la Kirumi wenye uzawa asilia wa Kiyahudi walitiwa mbaroni kwenye rabsha hii na wakapigwa mijeledi na kusulibiwa. Inaaminika kuwa Malkia Berenice alikuweko Yerusalemu kipindi haya yanatokea na hakuchukua hatua yoyote ya kukomesha hali hii, jambo ambalo angeweza kabisa kumkataza liwali wake na wanajeshi wake wasifanye hivyo. Tukio hili lilifanyika siku ya 16 ya mwezi Artemi au Iyari, mwaka 66 BK.

 

Tarehe hii ni ya muhimu sana kwa kila msomaji wa Biblia. Siku ya 16 mwezi wa Iyyari (au Iyari) ni siku ya 16 ya mwezi wa Pili na ni siku baada ya kuadhimishwa kwa Pasaka ya Pili ya waliokosa kuitunza ile ya Kwanza, na ni fursa ya mwisho ya kufanya toba nay a ulinzi wa Pasaka kwa mwaka ule. Pasaka inaadhimishwa kwa kula Ushirika wa Meza ya Bwana au Mlo wa Pasaka siku ya 14 ya mwezi wa Abibu au hadi mwezi wa Iyyari yanapofanzika maadhimosho ya Pasaka ya Pili inayofanywa nje ya malango ya kila mtu inayoendelea hadi asubuhi ya siku ya 15 ya mwezi huo, ambayo ni baada ya usiku wa Pasaka, siku ya 15 ya mwezi wa Iyyari, ambapo wapendatoba waaminifu wanaruhusiwa kurudi kwenye hema zao kufanya ukumbusho wa Siku Takatifu ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Na kufuatiwa na siku ya 16 jioni ya siku hii (Kum. 16:5-7). Mungu alikiweka kipindi hiki cha Pasaka ya Pili kwa ajili ya toba na kisha kuwafungulia mbwa wa vita.


na siku inayofuatia, Florus aliwaamuru wananchi wawasalimie askari wa vikosi viwili au wanajeshi wanapopita jiani wanaporudi nyumbani wakitokea Kaisaria. Wanajeshi hawa walisalimiwa, ila waliwadharau wananchi hawa waliolazimishwa kwa amri ya Florus. Ndipo wamanchi wakaanza kupiga makelele na kukashifu Florus kitendo kilichowafanya wanajeshi waanze kuwaua hovyo raia hawa wakaingia mjini ambako kulitokea mapigano ya mitaani mjini ambako watu wengi sana waliuawa kinyama na wanajeshi hawa. Lakini raia hawa walifanikiwa kuudhibiti Mlima Uliojengwa Hekalu na kukata mawasiliano kutoka kwenye ngome ya Antonia. Ndipo Florus akaondoa makazi yake kutoka Kaisaria akakiacha kikosi cha wanajeshi mjini Yerusalemu na kuwaachia viongozi wa mji wajibu wa kuongoza na kutoa amri.

 

Historia ya walikotokea Agripa na Bernike na kipindi cha kudumu kwa Vita

 

Agrippa II alilelewa na kusomeshwa huko Roma. Klaudio alimpa kiti cha ufalme cha mpwawake Herode wa Chalcis huko Lebanon takriban mwaka 50BK, na kumpa pia madaraka ya kumteua Kuhani Mkuu wa Kuhudumu Hekaluni kama mjomba wake alivyoridhia na kumwamuru kufanya. Inadhaniwa kuwa huenda aliishi mjini Roma lakini hakwenda Lebanon hadi baada ya mwaka 52BK, kwa mujibu wa mwandishi Schürer (kitabu chake hikihiki, ukurasa 472). Mwaka 53BK, alipokuwa anarudi akiwa ameshindwa vita na kuurudisha ufalme mdogo wa Chalcis, alipewa cheo kikubwa cha kiutawala cha liwali Philip na kuwa juu ya Batanea, Trachonitis, na Gaulanitis, liwali wa Lysanius (Abila) ambaye pia ni liwali wa jimbo la Varus. Baada ya kifo cha Klaudio (mwaka 54), Nero aliupanua ufalme wake na kuuzidisha kwa kulichukua jimbo hili, ambalo lilikuwa ni muhimu sana kama sehemu ya jimbo la Galilaya na Peraea, na kuliita kuwa ni jimbo la Tiberio na Tarichea pamoja na majimbo mengine yaliyowazunguka, na mji wa Julio pamoja na vijiji vyake vinavyowazunguka ambavyo idadi yake ni kumi na nne (kitabu hichohicho ukurasa wa 472-3).

 

Katika kipindi cha maaasi, Agripa alikuwa Alexandria na aliharakisha kurudi Yerusalemu. Dada yake ambaye aliishi kipindi baada ya kifo cha mume wake (ambaye alikuwa ni mjomba wa Chalcis), alikuwa ni mwanamke aliyeshukiwa kusababisha kifo hiki na alikuwa ameachwa na kuhofiwa na watu na alikuwa ni mama wa wa sehemu mbili. Kisha aliolewa na Mfalme Polemon wa Cilicia aliyempa sharti kwamba atahiriwe govi ya mwili wake, lakini ghafla sana akarudi kwa kaka yake. Na alikuwwko mjini Yerusalemu kipindi hiki cha maasi, ikiwa ni matokeo ya nadhiri ya Kinazarayo kwa mambo yote (anasema Schürer, kwenye ukurasa wa 474-5).

 

Agripa na Berenike walikuwa na hamu sana ya kumuona na kumsikiliza Mtume Paulo (Matendo 25:22). Inaonyesha kwamba kipindi kinachotajwa kwenye Matendo 26:28, kwa mujibu wa mwandishi Schürer anadhani kwamba walikuwa wameachana na ushabiki wa uhusiano thabiti wa mambo ya kidini wenye maswali yasiyo na maana. Maana yake ni kwamba Yakobo alikuwa ameishauawa huko Yerusalemu na alikuwa ni Shahidi wa Ufalme wa Mungu. Tunahisi kuwa Agripa aliwahi kumsikia Paulo kwa masikio yake. Yakobo aliuawa mnamo mwaka 62BK ambao pia ni mwisho wa kipindi cha majuma 69 ya miaka. Mtume Paulo aliuawa kwa kukatwa kichwa mjini Roma mwaka 66BK. Kwa hiyo, baada ya kuuawa kwa Mashahidi hawa wawili wa Mungu ambao wote hawa waliuawa kwenye miji ya Yerusalemu na Roma, ndipo Mungu alianza kuushughulikia mfumo huu.

 

Kisha Agripa alikwenda Misri kutoa heshima kwa Wakuu wake wa kazi waliokuwa huko Misri ambao ni Tiberius Iulius Alexander. Kisha Agripa alirudi haraka ambako yeye mwenyewe na dada yake walifanya juhudi zao zote ilivyowezekana ili kuzuia machafuko haya na uasi visitokee. Walisimama upande wa kupenda amani na tangu hapo na kuendelea wakasimama kidete kwenye upande wa Warumi, na matokeo yake walipoteza idadi kubwa ya miji. Yeye na wanajeshi wake walikuwa wanaelekea kufanya kama aliyofanya Cestius Gallus aliyesababisha maafa makuu na ya ghafla dhidi ya Yerusalemu. Hatimaye aliweza kuurudisha tena sehemu za majimbo yake zilizokuwa zimeporwa mwaka 67BK baada ya Warumi kuyarejesha majimbo yao yote ya pande za kaskazini ya Palestine.

 

Nero alifariki tarehe 9 Juni 68BK. (Kama tujuavyo kwamba Mitume hawa wote wawili yaani Paulo na Petro waliuawa vifo vya ushahidi siku za utawala wa Nero). Ndipo Tito na Agripa walikwenda kutoa heshima yao kwa Mfalme mpya Galba, lakini walipokuwa njiani wakienda huko, walipokea habari kuwa Galba ameuawa tarehe 15 Januari 69BK.

 

Ndipo Tito alirudi kwa baba yake Vespasian, na Agripa akaenda Roma. Baada ya Verspasian kuchaguliwa kuwa mfalme na Kundi la watu waliotoka Misri na Syria mwezi Julai 69BK ndpo alirudi akatoe heshima kwa amri aliyopewa na Bernike aliyekuwa akisaidia sana upande wa Flavian. Tangu hapo na kuendelea, Agripa alikuwa kwenye mrengo endelevu wa kumsaidia Tito mtu ambaye Verspasian alimwamini sana kwa shughuli ya kupanga na kupigana vita. Baada ya kuanguka kwa Yerusalemu, Tito alisaidia sana shughuli za kimichezo kwenye mji mkuu wa Agripa, Kaisaria ya Filipi. Mji mkuu wa Agripa ndio ulikuwa kitovu cha mambo yote ya burudani cha Warumi kwenye maeneo mteremko yenye wakazi wengi Wayahudi.

 

Baada ya vita, mipaka ya nchi yake iliongezwa, na mwandishi Josephus aliandika kuwa Maeneo haya ni ya pande za Kaskazini mwa Lebanon, ambako ni kaskazini mashariki ya Tripoli, kote kulikuwa ni eneo la utawala wa Agripa (B. J. vii, 5, 1, tazama ukurasa wa 37 wa kitabu cha Schürer, Toleo la 1, ukurasa 478). Josephus hakuielezea kuwepo kwenye Vita hivi (B.J. iii, 3, 5), inadhaniwa kuwa huenda ilikuwa haijatolewa bado kwake, na Schürer anaendelea tu na mtazamo huu (kitabu hichohicho, ukurasa wa 478).

 

Baada ya vita mwaka 75BK, Agripa na Bernike walifika Roma ambao Bernike alizirudia kazi zake alizokuwa amezianza alipokuwa na Tito katika Palestina. Malkia wa Kiyahudi aliishi na Tito katika Palestina wakati kwamba Agripa walipata upendeleo kwenye cheo cha uhakimu. Ilitarajiwa kuwa wangeoana lakini jinsi walivyoipokea hali hii huko Roma ilikuwa ni kinyume kabisa kiasi kwamba Tito alilazimishwa amfukuze na kumrudisha alikotoka.

 

Mwaka wa Yubile ulikuwa ni 77BK. Kuteketezwa kwa mji wa Yerusalemu kulimalizika mwaka 70BK na Warumi walichukua mamlaka na udhibiti wote kwenye kipindi hiki cha Sabato ya Saba ya mwaka 76BK, kabla ya Yubile ya mwaka 77BK.

 

Baada ya kifo cha Vespasian, Bernike alirudi Roma tarehe 23 Juni 79BK, lakini Tito akiwa kama mfalme alimdharau na hakumtilia maanani kabisa. Mwandishi Schürer anadhani kuwa hatimaye alirudi tena Palestina, lakini ni mambo machache sana yanayojulikana kumhusu yeye na maisha yake tangu kipindi hiki.

 

Utawala wa Agripa wa ile dola yake iliyopanuliwa ulidumu hadi ukaishia mwaka 86BK, wakati aliponyang’anywa makoloni yaliyokuwa huko Uyahudini. Josephus anaelezea kisa hiki kwenye kitabu chake kiitwacho Antiquities (xvii, 2, 2 (28)), akisema kwamba hatimaye haawakuwa na sehemu yoyote kwenye dola hii. Anaonekana kuwa alitawala hadi kipindi cha utawala wa Domitian. Schürer anadhani kwamba alikufa katika miaka ya 92/93BK, na kwamba Photius sio mtu wa kutegemeka tena ilipofika miaka hii ya 100BK (soma ukurasa wake wa 481). Akiwa hata hana mototo mmoja, ufalme wake haukuishikamana na majimbo ya Syria alipokufa.

 

Vita hivi vya Warumi viliishia polepole tangu mwaka 66BK hadi 74BK, lakini nabii zilizotolewa zinahusiana na kuteketezwa kwa Hekalu na kuondolewa kwa mfumo wa kibinadamu, jambo ambalo liishia mwaka 70BK.

 

Maandalizi ya Vita

 

Agripa aliyanya matumizi ya mara kwa mara haki ili kuwateua na kuaweka Makuhani Wakuu, na aliwaweka na kuwateua Makuhani Wakuu hadi kilipofika kipindi cha maasi ya mwaka 66BK.

 

Katika kurudi kwao kutoka Alexandria kwa uasi wa mwaka 66BK, Agripa aliwakusanya watu mahali paitwapo Xystus, ambapo palikuwa ni uwanja wa wazi mbele ya Ikulu ya Hasmonaeans alipokuwa akiishi. Alijaribu kuwashawishi watu ili arejeshe amri na wamtii Florus aliyekuwa amechukiwa sana na watu, lakini lile lilikuwa ni pigo la mwisho. Watu walimkataa na kumbeza na kumtweza na alirudi kwenye ufalme wake.

 

Ndipo waasi walipoiteka na kuikalia Masada, ambao no ngome mashuhuri ili karibu na Bahari ya Chumvi upande wa kusini (inayoitwa sasa Bahari ya Mfu).

 

Kiwango cha uasi kilikuwa ni kukubwa sana na kisichoweza kuzuilika.

 

Katika uchochezi alioufanya Elieza mwana wa Anania Kuhani Mkuu, sadaka ya daima iliyokuwa inatolewa kilasiku na mfalme ilisimamishwa na hakuna tena sadaka kutoka kwa Mmataifa iliyoruhusiwa kuletwa. Hii ilikuwa ni rejea ya maombi yaliyofanywa na Sulemani alipomuomba Mungu wakati wa uzinduzi wa Hekalu, na kwa kufanya hivyo kulikuwa kunamaanisha tangazo la kuvunja mkataba wa muafaka walioufanya kati yao, yaani Israeli na Mungu kuhusu Wamataifa. Jambo hili limeelezewa vema kwenye jarida la Amri za Wafalme: Sehemu ya II: Sulemani na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C) [Rule of the Kings: Part III: Solomon and the Key of David (No. 282C)] na iliwapasa kufikia mwenye tamati ya mbali.

 

Tendo la kuisimamisha na kuikataa sadaka ya mfalme lilikuwa na maana ya kufanya tangazo la wazi na la makusudi kwa mfalme la kusudio lao la kuasi dhidi ya utawala wa Kirumi. Juhudi zote zilizofanywa za kuwashawishi kutofanya hivyo viongozi wao, kuhani mkuu na Mafarisayo zilishindikana.


Baraza la amani lililojumuisha Makuhani wa vyeo vya juu, Mafarisayo maarufu na Wahasmonia (Hasmoneans), yaani watu wanaohusiana na kuingia bila kizuizi kwenye Nyumba ya Herode, pia walishindwa kuinusuru hali hii. Walikimbilia kufanya juhudi za kuwalazimisha na kumsihi Mfalme Agripa ili awasaidie. Akatuma kikosi cha askari 3,000 kilichoongozwa na makamanda wawili, yaani Dario na Philippus, na kwa msaada wao walifanikiwa kushinda na kudhibiti Mji wa Juu wakati Waasi walishinda na kuchhukua udhibiti wa sehemu ya Kilima cha Hekalu na sehemu ya Chini ya Mji. Hatahivyo, majeshi ya mfalme walilazimishwa kuhamia kwenye Mji wa Juu, na kwa kujilipiza kisasi waasi waliyachoma moto majumba ya kifahari ya Kuhani Mkuu Anania, Agripa na Bernike. Siku chache baadae, mwezi wa Lous au Abu sawa na katikati ya miezi ya Julai/Agosti. Waasi waliikamata ngome ya Antonia na kuanza kuizingira sehemu ya juu ya jumba la Herode mahali ambapo majeshi ya kulinda amani yalikuwa yamekimbilia.

 

Uwezekano wa kuwazuia haukuwepo na wanajeshi wa Agripa walipewa hifadhi. Watu wa jamii ya daraja la juu wa Kirumi walikimbilia kujificha kwenye maeneo matatu yaliyokuws ns ngome zenye minara kwenye Ikulu ya Herode (kw mujibu wa Hippicus, Phasael na Mariamne). Majumba ya kifahari yaliyobakia yalichomwa moto mnamo siku ya 6 ya mwezi Gorpiaeus  (Eluli). Siku iliyofuatia Kuhani Mkuu Anania alikamatwa kutoka mafichoni pake na akauawa. Kikosi cha wanajeshi wa Kirumi chenye minara mitatu kililazimika kusalimu amri. Wanajeshi waliahidiwa kulindwa na kuwa salama. Hatahivyo, waliposhusha chini mikono yao, waliuawa kinyama hadi mtu wa mwisho (kwa mujibu wa kitabu cha Schürer, kurasa za 486-487).

 

Hivyobasi, Yerusalemu ukawa umeshinda. Kwenye miji mingineya Yudea na Galilaya vita ya umwagaji mkubwa wa damu iliendelea. Huku Wayahudi wakishinda kwa kuwauwa Wamataifa na pale Wamataifa walipopata ushindi waliwauwa kwa kuwachinja Wayahudi. Josephus anasema kuwa madhara ya maasi yalitokea Yerusalemu yalienea mbali hadi kufika maeneo ya mbali huko Alexandria (kwa mujibu wa kitabu cha B.J. ii, 18, 1-8 (457-98); soma pia kitabu cha Schürer, ukurasa wa 487).

 

Kujibu Mapigo

 

Baada ya kipindi kirefu cha kuelewa kilichoe; ezewa kuwa ni cha maandalizi, Cestius Gallus, liwali wa Syria, alipelekwa Yudea ili akakomeshe maasi.

 

Akarnda na askari wa Kikosi cha 12 na wanejeshi wanaume wapatao elfu mbili kutoka kwenye vikosi vingine, na vikosi vingine sita na vikosi vine vya askari wapanda farasi pamoja na idadi kubwa ya wanajeshi wa akiba walipelekwa kwa agizo la wafalme rafiki akiwepo Agripa.

 

Majeshi yalioongozwa na Gallus yaliondoka Alexandria kwa kupitia njia ya Ptolemai, Kaisaria, Antipatri, na Lydda. Walifika huko Lydda wakati wa Sikukuu ya Vibanda, mwezi wa Tishri. Walienda mbele hadi Yerusalemu kwa kupitia Beth Horon, na walifika Gibeon, umbali wa viwanja hamsini kutoka Yerusalemu (kwa mujibu wa vitabu hivyohivyo hapo juu).

 

Wayahudi waliishambulia kambi ya Beth Horon na Warumi walikuwa kwenye hatari kubwa lakini hatimaye mambo yakawageukia Wayahudi.

 

Kisha Gallus akahamia eneo la karibu na Yerusalemu na kuweka kambi yake kwenye Mlima Scopus, ulio na umbali wa takriban viwanja saba kutoka Yerusalemu, siku ya 26 mwezi wa Tishri. Siku nne baadae, yaani siku ya 30 mwezi Tishri (Hyperberetaeus), aliiteka na kuvidhibiti viunga vya upande wa kaskazini mwa Bezetha bila kukutana na upinzani wowote, na wakauchoma kwa moto.

 

Hatimaye akajaribu kuushambulia Mlima wa Hekalu bali akashindwa na akaamua kuuachia na kuondoa majeshi yake. Josephus haelezei ni kwa nini alifanya hivyo. Huenda ni kwa sababu hikuwa amejiandaa vema na alikuwa chini ya viwango vya kufaa kufanya mashambulizi na kuuzingira.

 

Kisha alipumzika kwenye bonde lililoko karibu na Beth Horon, ambako Wayahudi walikwenda na kumzingira kabisa na kumshambulia kwa mashambulizi mabaya sana na kuwaondoa wanajeshi wake. Kwa kuwaepusha wanajeshi wake wanaotegemeka zaidi na kuwapeleka Antiokia, akalazimika kuviacha vifaa vyake vya vita nyuma ili vitumiwe baadae na Wayahudi.

 

Maandalizi ya mashambilizi makuu zaidi ya Warumi

 

Washindi walirudi Yerusalemu siku ya 8 ya mwezi wa Dius, au Marcheshvan au Buli.

 

Baraza la usuluishi la wapenda amani sasa walisalimu amri kabisa na kuamua kujiunga na waasi. Mbinu za kimaandalizi zilianza zilizolenga kuwafanyia mashambulizi ya kujibu mapigo ya Warumi. Kundi maarufu Hekaluni lilimchagua Joseph ben Gorion na Kuhani Mkuu Ananus kuamuru mkakati wa kuulinda mji wa Yerusalemu.

 

Yesu bin Safia na Elieza bin Anania (wote wawili wanatoka kwenye ukoo wa Kuhani Mkuu) walienda Idumea kuamuru na kuusimamia mkakati wa kuulinda. Karibu kila moja miongoni mwa maeneo haya kumi na moja au maeneo ambayo kwayo Yudea ilikuwa imegawanywa ilimpokea kamanda wake. Yosufu bin Mathias, mwanahistoria wa siku za mbele, alitumwa kwenye kamandi ya Galilaya.

 

Hii ilikuwa ni komandi ngumu, kwa kuwa Warumi wakishambulia bilashaka watafika hadi huko kwanza wakiwa na kikosi kamili cha majeshi ya Kirumi dhidi ya raia hawa wasiopata mafunzo maalumu. Kamandi hii iliashiria kuwa na umaarufu fulani kwa Josephus kwenye jamii bora na ya kikabaila ya Yudea. Na ingawa hakufundishwa hili, aliikubali na kuianza kazi hii kwa moyo wa ujasiri na furaha.

 

Aliweka utaratibu wa kiserikali huko Galilaya pamoja na muundo wa baraza la kidini maarufu kama Sanhedrin lenye idadi ya watu sabini ili washughulikie baadhi ya mambo muhimu ya kisheria na kushughulika kuanya maamuzi makubwa makubwa.

 

Baraza la watu saba liliundwa kila kwenye mji ili washughulikie kusuluhisha mambo au kuamua penye mabishano.

 

Alipaswa kubomoa Jumba la Kifahari la Tiberio, lakini waasi walikuwa wameshafanikiwa tayari kufanya hivyo. Aliizungushia kuta na kuijengea ngome moji yote mikubwa ya Galilaya kwa kuiwekea ulinzi zaidi na kuihakikishia usalama wake. Miji hiyo ilikuwa ni Jotapata, Tarichea, Tiberias, Sepphoris, Gischala, Mlima Tabor, na Gamala ulioko Gaulanitis na sehemu nyingine ndogondogo. Aliwaita watu 100,000 wanaume na kuwafundisha mitindo asilia ya Kirumi.

 

Umahiri wa Josephus na umakini wake wa kuandaa vita ulipigwa kumbo na kupingwa na John wa Gischala, ambaye alikuwa ni mpinzani wa Warumi mkubwa sana katika Galilaya.

 

Josephus hakuwa amejiandaa vizuri kufanya upinzani na katika mji wa Tarichea, ambako Josephus aliweka makao yake kulikuwa na machafuko makubwa sana baada ya kugundulika kuwa Josephas anadaiwa kuwa ni mateka kutoka kwenye kundi la vijana wa kijiji cha Dabaritta, ambako alichukuliwa kutoka huko kwa afisa mmoja wa Agripa.

 

Hali ya uchungu wa kisasi na kutomwamini tena Josephus vilionekana kuwa dhahiri. Maisha ya Josephus yalitishiwa na kwa kutumia tu mbinu za kijanja na unyenyekevu vilimsaidia kuepukana na hatari. Hatimaye, akiwa huko Tiberias alilazimika kuwakimbiza na kuwafukuza wauaji waliotumwa wakamuue na mtu aitwaye John wa Gischala.

 

Hatimaye, Gischala aliitangua ahadi ya kukutana aliyoifanya Josephus, na jeshi la askari 2,500 likiongozwa na makamanda maarufu wanne walitumwa waende Galilaya kwa lengo hili. Hivyo basi, Josephus akafanikiwa kuitangua marufuku iliyowekwa na wajumbe wanne waliitwa tena. Walipokataa kuja ndipo alikamatwa na kurudishwa nyumbani.

 

Wakazi na wenyeji wa Tiberias waliokuwa wanaendelea kuasi, walinyamazishwa kwa lazima. Mji ukaasi siku chache baadae mkakati ulifanywa na Agripa na Warumi ambao ulikomeshwa baadae kwa kutumia mbuinu chafu na hila. Kwa mujibu wa Josephus, mji huu ulikuwa na wakazi waliokuwa ni watu wenye damu mchanganyiko na baadhi yao waliuunga mkono uasi huku wengine wakimsaidia Agripa na Warumi (B. J. ii, 21, 8-10 na Vita 32-34; 66-68).

 

Mji wa Yerusalemu ulikitumia kipindi hiki cha kusimamisha mapigani kwa kuwafundisha vijana matumizi ya silaha na kutengeneza silaha kuzisambaza na kuwafundisha jinsi ya kuvizia na kuteka. Katika kipindi cha Pasaka ya mwaka 67BK mji ulikumbwa na maafa makubwa kwa mara ya pili kwa mashmabulizi makubwa kuliko yale ya kwanza.

 

Mashambulizi Mkuu ya Warumi ya Mwaka 67BK

 

Nero alikuwa huko Akaya wakati habari za kushindwa vita kwa Cestius Gallus zilipomfikia. Akaihamisha komandi ya kukandamiza na kukomesha uasi wa Wayahudi kwa Vespasian aliyekuwa na uzoefu na kazi hii. Baada ya kushindwa kwake vita, Gallus alikufa kipindi kifupi tu baadae.

 

Mchakato huu ulianza kipindi cha kampeni cha majira ya baridi.

 

Vespasian na majeshi yake wakaenda huko Antiokia na kuweka kambi la askari wake huko na akamtuma mtoto wake Tito aende Alexandria akamletee wanajeshi wa Kikosi cha 15 waliokuweko huko.

 

Mara tu mwishoni mwa majira haya ya baridi, alienda Ptolemais mahali alipokwenda kumngojea Tito, lakini kabla Tito hajawasili, wajumbe wa amani kutoka Sepphoris ya Galilaya na kuomba askari wa Kirumi waje kulinda amani ya mji. Ndipo Vespasian alifanya haraka kwenda na kikosi cha askari 6,000 kilichokuwa kinaongozwa na Placidus ili kikaulinde mji wa Sepphoris. Na pasipo hata kupiga mbiu ya kuhadharisha watu, Warumi waliuchukua mji huu muhimu sana na ulikuwa umezungushiwa ngome kubwa na imara  katika Galilaya.

 

Kipindi alipofika Tito, alikuta wanajeshi wa komandi ya Vespesian wameigawanya kwenye makundi matatu yanayojitegemea kama ifuatavyo: Komandi ya 5, 10, na 15; vikosi vilivyokuwa na divisheni ishirini na tatu za nyongeza vikosi sita vya wapanda farasi na askari wengine wa ziada walioongezwa na Mfalme Agripa, pamoja na Antiochus wa Commagene, Soaemus wa Emesa, na Malchis II wa Nabataea, ambao jumla yao walikuwa ni jesgi la wanaume 60,000.

 

Vespasian akaondoka kutoka Ptolemais na kuweka kambi yake kwenye mpaka na Galilaya.

 

Wanajeshi wa Kiyahudi yakiongozwa na Josephus waliweka kambi yao huko Garis, umbali wa stadia 20 kutoka Sepphoris wakawangojea Warumi huko (kwa mujibu wa jarida la Vita 71 (395)).

 

Hari ya kushinda vita iliwaishia wanajeshi wa Kiyahudi hata kabla wanajeshi wa Kirumi hawajajitokeza, na wakatawanyika. Upande wa nyanda za chini wa Galilaya ukaangukia mikononi mwa Warumi pasipo hata kutumia upanga hata mmoja.

 

Josephus alilazimika kwenda kupumzika huko Tiberias. Na sasa Vespasian akaifanya kazi iliyokuwa rahisi sana ya kuziteka ngome zote hatua kwa.

 

Josephus akatuma ujumbe akiwaasa wakazi wa Yerusalemu watafute kama kuna mtu miongoni mwao aliye na haiba na uwezo wa kupigana na Warumi. Lakini rai yake ilichelewa.

 

Sehemu kubwa ya wanajeshi wa Josephus walikuwa huko Jotapata. Josephus akasema kwamba Warumi watajenga barabara itakayotumiwa na askari wapanda farasi watakapokuja, jambo ambalo walilifanya kweli kuanzia siku ya 17 hadi 21 mwezi wa Iyari. Inaaminika kuwa Josephus alifika huko siku ya 21 mwezi wa Artemesius (Iyari) mwaka 67BK. (Muda huu ulikuwa ni mwishoni mwa maadhimisho ya Pasaka ya Pili ambayo ingefuatiwa pia na Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu). Vespasian alifika kwenye mji huu jioni ya siku iliyofuatia. Jesephua anasema kuwa mzingiro huu ulidumu kwa kipindi cha siku 47 (B.J. iii, 7, 33 na 8, 9 na yaliishia siku ya 1 Panemus (B.J. iii, 7, 36).

 

Josephus anasema wazi kabisa kwamba mji ulitekwa siku ya 1 Panemus. Pia anasema wazi tu kuwa kipindi cha kuzingirwa kwake mji huu kilidumu kwa siku 47. Anaeleza pia kwamba kazi ya ujenzi wa barabara ilichukua siku nne kabla ya kuwasili kwake siku ya 21 mwezi wa Iyari. Kwa hiyo, vikosi zaidi vya Warumi vya kuja kuulinda mji na kuuzingira viliwasili siku ya 14 mwezi wa Iyari au katika kipindi cha maadhimisho ya Pasaka ya Pili. Mara tu baada ya barabara kujengwa, mkakati wa kuuzingira mji ulipaswa uenndelezwe na usonge mbele na watu wa Vespasian. Sababu ya kufanya maadhimisho ya Pili ya Pasaka mwezi wa Iyari kwa operesheni zote mbili kuu ilikuwa ni kuwafanya wasiwapoteze wanafunzi wa Biblia. Mungu anaruhu hali hii itokee ili ashughulike na watu wa Yuda.

 

Mji wa Jotapata ilitekwa na kutwaliwa siku ya Mwandamo wa Mwezi wa Nne (Tamuzi) mwaka 67BK. Ulikuwa ni mji uliozungushiwa kuta mande zote katika Israeli tangu kipindi cha Yoshua (kama miji ya Mishnah, Arak. 9:6).

 

Mashambulizi ya kwanza yalilipuka huko. Kisha Warumi wakaanza kufanya utaratibu wa kuuzingira. Josephus anaelezea uzingiraji huu kwa undani kwenye kitabu chake cha Vita vya Wayahudi (Wars of the Jews)

 

Hatimaye, licha ya kutumia mbinu za kijanja na hata uwongo na hila za kutuma watu wakiwa wamevaa ngozi za wanyama wanapikwenda kuchukua mahitaji yao saa za usiku, na kutumia mafuta ya oili chafu iliyochemshwa ya moto na uwatu wakivitumia kama vifaa vya kutimiza kwenye mkakati wao wa kuwazingira na kuweka utelezi kwenya madaraja na kuwapa askari zana za kujikinga au ngao, na kuweka mashujaa wa kuwazuia, havisaidia bali hatimaye mji ulianguka. Wataalamu wa kutafuta na kufukua miili walioshughulika kwenye uzingiraji huu walimuona hata Vespasian mwenyewe akiwa amejeruhiwa. Mji ulisalitiwa na hali ya uhitaji na maafa yaliyogundulika kuletwa na wakazi asilia waliokula njama na Warumi.  Walinzi waliochuku zamu zao asubuhi walikaa macho hadi asubuhi na hawakulala. Ndipo Tito akiwa na jeshi dogo akaingia mjini humo kwa werevu na mbinu kipindi cha mabadilishano ya zamu ya asubuhi na wakawaua walinzi na mji ukashindwa kuwazuia washambuliaji waliokuwa wanashambulia kutoka nje.

 

Wanaume wengi waliuawa na kufichwa kwenye mapango. Waliuawa kwa kuchinjwa na Warumi au walijiua wenyewe. Kwenye vitabu vyake Josephus anasema kuwa yeye alinusurika kwa kile kinachosemekana kwamba alipigiwa kura kwa kudhaniwa alikuwa ni mtu wa mwisho miongoni mwa wale waliojiua wenyewe waliokutwa mle pangoni, na kudhaniwa kuwa huyu aliamua kujisalimisha. Alifanya mambo yakr kana kwamba alikuwa nabii na ilithibishwa kwamba yeye ndiye aliyetabiri hapo kabla kipindi ambacho mzingiro ule utachukua. Josephus alitabiri kwamba Vespasian ndiye akatayerithi kiti cha ufalme, na kwamba yeye atayetawala kwa huruma nyingi.

 

Warumi walifanya maangamizi makubwa mno kiasi kwamba waliwaua wanaume wote na kuwaacha mateka wachache tu na waliwaacha hai watoto wakiume wachache na mama zao wakiwa kama watumwa. Waliuangamiza mji wote na kuusafisha kabisa. Josephus aliachwa hai ili ayachukue na kuyaandika matukio haya. Mji huu uligunduliwa tena mwaka 1847 na E. G. Schultz kuwa ulikuwa huko Jefat upande wa kaskazini mwa Sepphoris.

 

Tarehe 4 Panemus, Vespasian alienda Kaisaria akipitia njia ya Ptolemais na kuwaruhusu wanajeshi wake wapumzike wakati huu anapokwenda Agripa iliyoko Kaisaria Filipi. Walikuwa na kipindi kirefu cha kusherehekea kilichodumu kwa muda wa siku ishirini. Kisha Tito akaamuru kikosi cha wamajeshi kutoka Kaisaria Maritima na wakaelekea huko Tiberias. Mji huu ukasalimu amri na ukatawaliwa kwa huruma kwa heshima ya Agripa.

 

Kisha wakauelekea mji mwingine wa Tarichea. Kwa nguvu na kujiamini kwingi, Tito aliuchukua mji huu mwanzoni mwa mwezi wa Gorpiaeus au Eluli.

 

Kwa hiyo, Miandamo ya Mwezi na maadhimisho ya Pasaka ya Pili yanamaana sana na ni matukio yanayokumbukwa kwenye vita hivi. Mungu anawaonya Yuda lakini hawataki kusikia.

 

Hadi kipindi hiki tunaona kuwa ni Galilaya na Gischala tu na Mlima Tabori (Itabyrion) ndizo zilkuwa zimebakia hadi kipindi hiki zikiwa na maboma na kuzungushiwa kuta imara na muhimu za Gamala iliyoko Gaulanitis.

 

Hatimaye Warumi waliushambulia Gamala baada ya mji ule, na mwanzoni walionekana kufanikiwa na wakaingia mjini. Hata hivyo, mashambulizi ya kujilipiza yalikuwa yamepangwa na yakawalenga Warumi kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba walikimbia na kuondoka wakiwa wamepata hasara kubwa sana, na ilimgharimu Vespasian kuyatumia mamlaka yake yote ili kumudu kurudisha utulivu na hari kwa askari wake (kitabu hikihiki cha Schürer, ukurasa 495).

 

Mnamo siku ya 23 mwezi Tishri (Hyperberetaeus), ndipo hatimaye mji wa Gamala ulianguka. Na Mlima Tabori pia ulitekwa na kikosi cha askari kikapelekwa huko kipindi hiki cha kuuzingira mji huu wa Gamala. 

 

Tito akatumwa kwenda Gischala akiwa na kikosi cha askari wa deraya 1,000. Mji ukasalimu amri kwa Tito siku ya pili yake. Yohana na Uzelote wake wakalikimbia na kujiepusha usiku wake na wakakimbilia Yerusalemu.

 

Vespasian akawachukua wanajeshi wake na kuwapeleka kwenye jumba la mapumziko ya majira ya baridi. Yeye mwenyewe pamoja na Vikosi vyake Kombania ya 5 na 15 waliweka kambi yao huko Kaisaria. Kikosi cha 10 kiliweka kambi yake huko Scythopolis.

 

Kwa hiyo, majira ya baridi ya mwaka 67BK, pande zote za kaskazini mwa Palestina ulikuwa mikononi mwa Warumi.

 

Vita Vya Wenyewe Kwa Wenyewe Vya Mwaka 67BK

 

Viongozi wa waasi ndio walioanza kuonekana kuwa ni viongozi wanaoyumba yaani kuwa mguu mmoja ndani na mwingine nje au waliokuwa ni sehemu ya wale wanaotafuta muafaka. Wale wenye msimamo mkali wa kutetea na kujivunia utaifa walitwao Wazawa au Wazelote (Zealots) wakaanza kuwalaumu kwa kusababisha maafa makubwa vile na kusalimu amri mwanzoni kabisa mwa vita. Wakalaumiwa kwa kutoiongoza vita kwa kwa umakini na umahiri wa kutosha. Mawazo haya na lawama zote hizi zilionekana kuwa ni za kweli na za msingi.

 

Kisha Wazelote hawa wakaanza kuchukua hatamu za uongozi na kuhitilafiana na viongozi wao wa siku za nyuma. Hawakupenda kuonyesha utii tena kwa moyo wao wote kwa viongozi wao hawa na hatimaye vita kuu vya umwagaji damu mkuu vya wenyewe kwa wenyewe vilifuatia na kupiganwa kuanzia majira ya baridi ya mwaka 67-68BK.

 

John wa Gischala ndiye alikuwa kiongozi wa watu hawa wa mrengo wa Kizelote. Alinusurika na kuponyoka na kukimbia na wanajeski wake hadi Yerusalemu kwenye kipindi cha mwanzoni mwa mwezi Novemba. Aliwakusanya vijana na kuwajenga moyo wa vita na kuwashirikisha matendo makuu anayokwenda kuyafanya. Manajeshi na wapenda vita wa mrengo huu wa Kizelote waliokuwa wamekimbilia pande za kaskazini wakamiminika mjini Yerusalemu pamoja na wale wa kujitolea waliotoka kila mahali. Mara, Wazelote hawa wakaudhibiti mji wa Yerusalemu.

 

Mkakati wao wa kwanza ulikuwa ni kuwaondoa wale wote wanaodhaniwa au kuonekana kuwa wanawapenda au kuwapendelea au kujikomba kwa Warumi. Idadi kuwa ya watu maarufu akiwemo Antipas kutoka kwenye jamii ya Nyumba ya Herode walichukuliwa kuwa ni watu wa aina hii na waliuawa gerezani.

 

Kuhani Mkuu mwingine alichaguliwa kwa kupigiwa kura kama alivyopigiwa aliyepita na wote hawa wakiwa wanatokea kwenye jamii ya daraja la juu miongoni mwao. Jambo hili liliwafadhaisha sana na kuwashusha hadhi na pigo kwa Mafarisayo, na hatimaye kulishuhudiwa mfumo mpya wa marabi wa zama mpya za Hekalu uliotokana na Mafarisayo.

 

Kuhani Mkuu aliyechaguliwa Phannias, kutoka Apthia (pia alijulikana kama Phanni, Phanasus, Pinhas). Josephus anamwelezea kwamba sio tu kwamba alikuwa na uelewa mkubwa tu wa shughuli na wajibu wa Kuhani Mkuu, bali alikuwa pia mtu wa watu na hili ndilo lilikuwa jambo la maana na muhimu (B. J. iv, 3, 6-8).

 

Viongozi walioshikilia madaraka ya Yerusalemu, yaani Gorion ben Joseph, Simon ben Gamaliel Farisayo, na Makuhani Wakuu wawili, yaani Ananus ben Ananus na Jesus ben Gamaliel walijaribu kujiondoa na kujitenga mbali na baraza la Wazelote kwa nguvu. Na kwa kuwa walikuwa wachache walilazimishwa kuingia kwenye uwa wa ndani wa Hekalu na kwa kuwa hakuna mtu aliyetaka kuleta ghasia kwenye malango matakatifu wakafungiwa ndani.

 

Wazelote hawa wakatuma ujumbe kwa wapenda vita wa jamii ya Idumeans. Hawa ni wana wa Esau waliokuwa wamepigwa na kushindwa vita na John Hyrcanus na wakaongoka na kuingia dini ya kiyahudi kipindi cha karne mbili na nusu zilizopia. Asilimia kubwa ya wakazi wa Yudea walikuwa ni hawa wa jamii ya Idumaean, na walikuwa ni Wakulima na Wafugaji (Na ni Hasmonaeans) wao wenyewe.

 

Hawa Idumeans wakaja wakitokea kwenye kuta za Yerusalemu bali hawakuruhusiwa waingie ndani. Kulipofika majira ya usiku, vurugu kubwa ilitokea iliyotumiwa kama sababu ya Wazelote na kufungua malango na wanajeshi waliojiandaa na kujipanga vizuri waliingia kwa ghafla na kuanza kupora na kuua watu humo mjini. Hali ya udhibiti ilikuwa dhaifu kuweza kuwazuia na zama ya utawala wa kigaidi ikaanza. Wazolete hawa wakaelekeza mauaji haya kwenye mwanzo wa kuwashughulikia wale waliokuwa ni masalio na vibaraka wa Warumi. Ndipo Makuhani Wakkuu kina Ananus na Jesus wakauawa pia.

 

Walifikia pia kwenye kiwango cha kulazimisha kuweko kwa majaribio ya kawaida ya kuhalalisha na kuwapa heshima wauaji hawa, lakini mahakama ilitoa hukumu ya kuwafutia mashitaka washitakiwa akina Zacharias ben Baruch, na ndipo Wazelote hawa wakamuua kwa madai kwamba “sisi tuna kura zako pia” (kitabu cha Schürer, ukurasa wa 497-498).

 

Hawa Idumeans kwa sasa wakagundua kuwa kile kinachoitwa hali tete ya kiusalama ilikuwa ni kisingizio tu cha kuanzisha sheria zinzokusudia kuwabana wananchi. Hatimaye wakaamua mujiondoa.

 

Wazelote wakaendelea na utawala wao wa kiimla na kigaidi na usiojizuia. Wakamuua Gorion na sehemu ya waliojiuliza wafenye nini sasa, na viongozi hawa walikuwa wanawatishia kuwa hakukuwa nakizuizi tena. John wa Gischala akawa ni mtu mwenye kuogofya na tishio mjini Yerusalemu.

 

Jinsi Kanisa la Pella Lilivyolindwa

 

Kanisa lilikuwa limeshaonywa kuhusu maafa haya kupitia unabii wa Danieli. Kabla ya kuzuka kwa vita, na baada ya kifo cha James, chini ya Simon ndugu yake Kristo lilikimbilia mahali paitwapo Pella kipindi kirefu kabla ya Pasaka ya mwaka 66BK.

 

Eusebius ananukuu aliyoyaandika Josephus (kwenye kitabu chake cha HE III, V-VI) akielezea kwa undani matukio ya kutisha waliyofanyiwa watu mjini. Kanisa likalindwa na mambo ya kutisha ya Wazelote na kipindi cha kutisha cha njaa ambacho kiliharibu mji na muundo wake wa kihari.

 

Ndipo majenerali wa vita wa Kirumi wakaona umuhimu kwamba mji wa Yerusalemu ulipaswa kushambuliwa haraka sana. Kwa ajili ya mapigano yaliyokuwa yakiendelea humo mjini wakaona kwamba jambo hilo lifanywe kwa tahadhari na uangalifu mkubwa.

 

Vespasian aliona kuwa vi vema na busara kuuacha mji uendelee hadi kiasi kibaya na mambo yao ya uadui na chuki zilizomo, na kuuacha ufikie kwenye hali mbaya mno wenyewe.

 

Mungu ameupa mji wa Yerusalemu miaka 40 ya kutubu kwa mujibu wa unabii wa Ishara ya Nabii Yona, na walikuwa wanakwenda kupata kila siku ya nyingine nyingi zilizoazimiwa kwao (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)].

 

Wangeweza kutubu na Mungu angewasamehe na kuwaokoa, hadi kwenye kipindi cha mwisho.

 

Badala yake, Vespasian alielekeza mawazo yake huko Peraea, mahali ambako ndiko ulikokuwako mji wa Pella. Eneo hili lilikuwa ni la Wamataifa ila walikuwa ni wanaowachukia Warumi na walikuwa na mambo mengi wanayopingana nayo kinyume na walivyokuwa watu wa mji wa Gadara.

 

Gadara ulikuwa umeomba msaada wa wanajeshi wa Kirumi waje kuwalinda dhidi ya cheche zilizokuwa zinajionyesha za uchokozi.

 

Vespasian alipeleka jeshi huko kutoka Kaisaria hata kabla ya majira ya baridi kufika. Alifika huko tarehe 4 Dystrus, au mwezi wa Adari wa mwaka 68BK na kuuchukua mji. Hatimaye alirudi Kaisaria. Vespasian akaacha kikosi cha kiasi cha wanajeshi 3,000 vijana na wenye hari ya kazi na askari wapanda farasi 500 wakiongozwa na Placidus, na hivyo kuhitimisha hali kuuitiisha mji wa Peraea pamoja na Machaerus. Hali hii ilikuwa na madhara katika kuhakikishia kwamba Kanisa limeachwa na amani na kuona kwamba hakuna mtihani mbaya unaotokea huko Yudea, Galilaya na Idumea.

 

Wakati majira ya baridi yakiwa yamekamilika na kuendelea, Vespasian aliondoka tena kutoka Kaisaria. Lengo lake lilikuwa ni kuweka utii wan chi nzima ili kwamba Yerusalemu uwe ni sehemu ya mwisho na itakapoangamizwa vipingamizi vyote viendane nao.

 

Akautwa na kuukalia mji wa Antipatris, na kuiteka miji ya Lydda na Jamnia. Akapeleka Kikosi cha wanajeshi Kombania ya 5 likaweka kambi yake nje ya mji wa Emmaeus. Kisha akaushambulia ghafla mji wa Idumaea. Akiwa anarudi na kuelekea upande wa kaskazini, akiwa njiani akipitia Emmaeus, alienda hadi akafika Samaria hadi Neapolis (Shekemu) akipitia Korea. Alifika Korea siku ya 2 mwezi Sivan (Daisius) na kisha akaelekea Yeriko. Alipeleka jeshi ili kuulinda mji wa Yeriko na Adida. Aliuharibu kabisa mji wa Gerasa na kikosi cha jeshi lake la akiba kililochoongozwa na Lucius Annius.

 

Kipindi hiki Yudea ulikuwa umeshatiishwa na kuacha jeuri kabisa. Sasa Vespasian aliweza kurudisha mawazo yake kwenye suala la Yerusalemu (kama anavyosema Schürer, kitabu chake, ukurasa 498-499). Kisha akarudi nyuma huko Kaisaria na kuanza maandalizi, lakini kifo cha Nero kilichotokea tarehe 9 Juni 68BK kulimlazimisha afanye marudio yote ya mipango yake. Dola yake yote ingekumbwa na ghasia na ndipo alilazimika kuelekeza mawazo yake huko. Kwa njia hii, Mungu alihitimisha lengo lake la kuwalazimisha Yuda wajitathmini katika kipindi hiki kizima cha miaka arobaini ya toba.

 

Vespasian alisubiri kupewa taarifa, na kwenye kipindi cha majira ya baridi ya mwaka 68/9BK alipokea taarifa kwamba Galba ametangazwa kuwa mfalme. Akampeleka motto wake Tito aende Roma aende kumpa heshima na pongezi mfalme huyu mpya na kungojea amri yake. Kwa hiyo, ni Tito peke yake ndiye aliyewahi kufika maeneo yote hadi huko Korintho wakati alipoarifiwa kuwa Galba ameshambuliwa mnamo tahere 15 Januari 69BK.

 

Ndipo Tito alirejea kwa baba yake huko Kaisaria. Vespasian aliendelea kuvuta subira.

 

Tamalaki ya Pili ya Yudea

 

Jinsi matukio yalivyokuwa yalimlazimisha Vespasian aamue kuondoka na kwenda Yudea wakati Simon Bar-Giora (mwana wa mwongofu) ambaye alikuwa na mwenendo na tabia sawa na zile za ho John wa Gischala – aliyekuwa ni Mzelote asiyeweza kuchukuliana na wengine-na ambaye ameanza kukusanya kikosi cha wafuasi ili kukomesha mapigano. Kwa hiyo, yeye na wafuasi wake wakaanza kuenea pande za kusini mwa Palestina, akifanya uporaji na kuiba popote walipokwenda.

 

Basi wakauangamiza mji ule kama nzige wanavyovamia na kuteketeza majani. Baada ya kufanya shambulio la ghafla la aina yake huko Hebron, wakatoa onyo kwa kuwaburuza mateka wao (Schürer, ukurasa wa 499 na kama alivyoandika B. J. iv, 9, 3-8).

 

Hatimaye, Vespasian akalazimika kuuhusuru. Mnamo tarehe 5 Daisius, au Siwani mwaka 69BK, baada ya kipindi cha mwaka mmoja kamili wa mapumziko, akaja tena kutoka Kaisaria. Akayadhibiti majimbo ya ya Gophna na Acrabata na miji ya Betheli na Efraim. Akauendele na kuukaribia mji wa Yerusalemu wakati ndugu yake Cerealis akiushinda na kuuteka na kuuteketeza kabisa mji wa Hebron, baada ya kukabiliana na upinzani wa kimapigano. Pamoja na hali ya kujiona kwake mji wa Yerusalemu, na ngome kuu tatu zilizoizingira miji ya Herodium, Masada na Machaerus, maeneo yote ya Palestine yalikuwa yametekwa na kusalimu amri kwa Warumi (kitabu hikihiki, kurasa za 499-500).

 

Watu Wawili Hatari na Tishio Wa Yerusalemu

 

Mji wa Yerusalemu ulikuwa umechoshwa sana na matendo ya John wa Gischala, na Simon Bar-Giora wakiwa wakatafuta jinsi watakavyoweza kujiondoa kwa John. Kwahiyo, hata kabla Vespasian hajaliteka na kulitiisha eneo la kusini, Simon alirudi Yerusalemu na alialikwa Yerusalemu kwa wito wa Kuhani Mkuu, Mathias. Akaingia Yerusalemu mwazi wa Xanthicus, au Nisan ya mwaka 69BK.

 

Badala ya kuwekwa huru na kuokolewa na matisho na mateso ya John, wakajikuta wakiwa na watu tishio wawili sasa ambao wote hawa walimuona kila mtu mwenye hela kuwa ni adui wao mkubwa.

 

Dola Iliyogawanyika 

 

Mungu atafanya kitu kwa lengo la kuupa Yerusalemu kipindi kamili cha kutubu na kuwapa Yuda fursa ya kubakia.

 

Wakati Vespasian alipokuwa anarudi Kaisaria, habari zikamfikia kuwa jimbo la Magharibi limemtangaza Vitellius kuwa mfalme. Jimbo la Mashariki likaamua kuwa ni vema wawe na Vespasian kuliko kuwa na mtu mwenye uchu na mlafi Vitellius.

 

Tarehe 1 Julai 69BK, Vespasian alitangazwa kuwa ni mfalme wa Misri. Siku chache bade Majimbo ya Palestina na Syrian yakafuatia. Kabla ya katikati ya Julai alitawazwa rasmi kuwa mfalme wa pande zote za Mashariki.

 

Ndipo Vespasian aliona ni mhimu kwanza aanze kwa kukusanya nguvu zake na kuachana na habari ya uasi wa Wayahudi hadi baadae. Muda ulipaswa uendane kwa mujibu sawa na makusudi ya Mungu na kalenda yake.

 

Vespasian alipokea wajumbe akiwa huko Berytus na kisha akaelekea Antiokia. Na akiwa huko alimtuma Mucianus aende kwa njia ya bara hadi Roma pamoja na jeshi na baadae akaelekea Alexandria. Wakati akiwa huko alipokea habari kwamba mji wa Roma umeshambuliwa na kushindwa na kwamba Vitellius ameuawa tarehe 20 Disemba 69BK.

 

Akakaa mjini Alexandria hadi mwanzo wa majira ya joto ya mwaka 70BK, lakini amamtuma Tito na jeshi lake kwenda Palestina kwenye kukomesha vita ya Wayahudi.

 

Yerusalemu na Watu Tishio

 

Kwenye kipindi kibaya cha mwaka hali ya mambo ilikwenda vibaya sana kwa kweli mjini Yerusalemu, kama.

 

Na badala ya kuwa na makundi mawili tu Tishio na ya wataabishaji, wakajikuta sasa wana makundi matatu. Kukawa na kundi la Elieza, ambaye alikuwa ni mototo wa Simon lililotokana na kujiengua kutoka kwenye kundi la John Mzelote. Mji ukawa sasa umegawanyika makundi matatu. Simon alidhibiti upande wa Juu wa Mji na sehemu kubwa ya pande za Chini za Mji. John akadhibiti Milima wa Hekalu, na Elieza akadhibiti sehemu ya uwa wa Hekalu. Watu hawa watatu walikuwa na mizozo endelevu na mji mzima ukawa ni uwanja wa vita usiokoma.

 

Badala ya kuruhusu hali ya kila mmoja aweze kuingia kwenye utaratibu wa mgao wa chakula kwa ghara ma ya wengine, wakachoma moto kwenye maghala yasiyojulikana ya nafaka ya Yerusalemu na kuufanya mji uwe kwenye kipindi cha baa la njaa. Wakahakikisha kwamba mji uwe kwenye kipindi cha nja kali jambo litakalowafanya washindwe kustahimili kipindi watakapouzingira Warumi, na kuwafanya wachanginikiwe na kuwa na usuni utakaowafanya kushindwa kustahimili mapigano.

 

Walistahili kila mmoja wao kupatwa na maafa haya ya makali ya upangawa, na kipindi hiki upanga ulikuwa umekaribia sana kuwashukia kwa mwonekano wa mapigo ya kibinadamu yaliyoongozwa na Tito na jeshi lake.

 

Kuteketezwa Na Kanguka kwa Yerusalemu

 

Jeshi hili lililoongozwa na Tito liliundwa kwa mkusanyiko wa kombania nne. Mbali na kombania za Vespasian za Vikosi namba 5, 10 na 15, yeye alikuwa na kingine cha 12, ambacho kilitokana na kikosi kilichokuwa huko Syria chini ya Cestius ambaye alianza mkakati wa uzingiraji wa kwanza.

 

Makamanda wa Vikosi vya Vespasian walikuwa ni:

Sextus Vettulenus Cerealis Kombania ya 5

A. Larcius Lepidus Sulpicianus Kombania ya 10

M. Tittius Frugi Kombania ya 15

Kamanda wa Kombania ya 12 hajulikani.

 

Liwaliwa wa zama ni wa Yudea, Tiberius Iulius Alexander, alimsaidia Tito.

 

Alitoa amri kwa makamanda wa majeshi haya wakutanenaye mjini Yerusalemu huku yeye mwenyewe na kamati yake kuu wakaondoka na kwenya Kaisasria. Kikosi cha 5 kikaenda Emmaus na cha 10 kikaelekea njia ya Yeriko. Huku akiwa na kikosi kizima cha jeshi cha washirika wake kilichoongezewa, na ambacho kilitiwa nguvu, Tito alikuwa na jumla ya jeshi la wanaume 2,000 waliotoka Misri na 3,000 waliochukuliwa kutoka kwenye jeshi la vikosi vya Frati.

 

Schürer anasema kwamba Tito alifika kwenye kuta za Yerusalemu siku chache kabla ya Pasaka ya mwaka 70BK (kwenye kitabu chake ukurasa 502); na vyanzo vingine vinasema alifika siku ya 1 mwezi wa Abibu mwaka 70BK. Hii ilikuwa ni kwa kufuata mpangilio wa kipindi uliokusudiwa. Haina maana yoyote na wala haibadilishi maana yake halisi hata kama ilifanyika siku ya 1 au 13 Abibu. Pasaka ilikuwa ni hukumu ya Mungu.

 

Tito ameenda mbele akitumia jeshi la askari wapanda farasi 600 na alikuja kukiwa na pigo kuu sana na upinzani uliofanywa na Wayahudi na kwa kweli ni ushujaa wake tu ndio ulimsaidia kujiokoa kutoka mikononi mwao.

 

Ushujaa wa kishabiki wa Wayahudi uliheshimiwa sana na Warumi. Kikosi cha 10 kikafika na kuweka kambi yake kwenye Mlima wa Mizeituni. Kwenye mchakato huu kilishambuliwa na watetezi hawa wa mji na ilikuwa ni karibu sana kitekwe na kushindwa kabisa. Mwingilio wa binafsi wa Tito ndio ulionekana kusaidia na kuzaa matunda kiasi cha kuweza kuwashambulia na kuwarudisha njuma.

 

Mapigano ya ndani kwa ndani yaliendelea kupamba moto mjini. Chini ya Warumi hawa, mauaji makubwa sana yalifanyika kwenye malango ya mji huu, na mauaji mwengine yalitokea kwenye kipindi cha Pasaka ya mwaka 70BK huko Yerusalemu. Wafuasi Eleaza walifungua malango ya Hekalu ili kuwaruhusu waingie wale wanaokuja kuabudu kwenye Pasaka. Wafuasi wa John wa Gischala wakaitumia fursa hii kwa kuingiza wanajeshi na wakawaua wafuasi wa Eleaza na kuchukua udhibiti wote wa eneo la Mlima wa Hekalu. Jambo hili likaendelea kuleta mgawanyiko kwenye makundi haya mawili na kuweka makundi mawili hasimu kati ya John na Simon.

 

Mwandishi Schürer anatoa maelezo kuhusu kilichotokea humu mjini kwenye kitabu chake cha 1 kwenye ukurasa wa 503 na anatumi pia nukuu za Josephus (B. J. ukurasa wa 4) akisema yafuatayo:

Ili kujua mkakati wa kuuzingira mji, jambo ambalo linakwenda kufanyika sasa, ni muhimu kuwa na wazo la jumla la kujieneza mjini. [B. J. ukurasa wa 4] Mji wa Yerusalemu uko katikati ya vilima viwili, kirefu kimoja kwa upande wa magharibi na kingine upande wa mashariki, unatenganishwa na maporomoko yanayotitisha maji kutoka upande wa kaskazini kuelekea kusini yanayoitwa Tyropoeon. Kwenye kilima kilicho upande wa magharibi ndiko kunakoitwa mji wa juu, kwenye kilima kidogo cha magharibi, na ndiko kunakoitwa mji wa chini. Sehemu nyingine inayobakia inaitwa ‘Acra’ kwa kuwa ndipo hapa ngome ya Yerusalemu ilijengwa na Antioko Epifani (Antiochus Epiphanes) na ndipo alipokuwa amesimama hapo zamani. [kitabu cha Schürer kurasa za 154-5]  Kaskazini mwa Acra ndiko kuna eneo lililojengwa Hekalu, mahali ambapo palipanuliwa na Herod Mkuu. Sambamba na eneo hili la Hekalu kwa upande wa kaskazini kulikuwa na ngome ya Antonia. Eneo lilipo Hekalu lilikuwa limezungukwa pande zake zote nne kwa kuta imara na kwa hiyo lilizingirwa na ngome ndogo usiku mzima. Upande wa juu na wa chini wa miji hii uliunganishwa na ukuta wa kawaida ambao uliunganisha ukuta wa magharibi wa sehemu ya Hekalu, na kisha kuelekea upande wa upande wa magharibi, ukipitia kwenye mji iliyo pande za juu na za chini kwenye pango kubwa la kusini, na hatimaye kufikia mwisho wake kwenye kona ya upande wa kusini mashariki ya kiwanja cha Hekalu. Zaidi ni kwamba sehemu ya juu ya mji ilipaswa itngwe na eneo la upande wa chini ya mji kwa ukuta uneotokea upande wa kaskazini na kuelekea kusini ukipitia Tyropoeon. Kipindi Tito alipokuwa anadhibiti eneo la chini ya mji, aliwaelekeza wanajeshi wake waufanyie madhara ukuta ulio sehemu ya juu mwa mji. Upande wa magharibi, kusini na mashariki, ukuta wa nje kulikuwa na gema au maporomoko, ni upande wa kaskazini tu ndiko kulikuwa na uwanja ulioonekana kuwa ni sawia na usio na milima wala mabonde. Hapa palikuwa na ukuta wa pili uliofanya handaki la upande wa kaskazini na kuunganisha viunga au mitaa ya zamani, na kisha, mrremko wa upande wa kaskazini, na ukuta wa tatu ulianzishwa na Agrippa I na alimalizia tu kipindi cha maasi na machafuko ulipoonekana kuwa ni muhimu. Ukuta huu wa tatu uliambatanishwa na kile lichokuwa kinaitwa Mji Mpya au kiunga cha mji kilichoitwa Bezetha.93 [Msomaji watakumbuka kuwa mji wa Bezetha ilichomwa moto na Warumi hapo nyuma kwenye tendo la kwanza la Cestius. Soma kitabu cha Schürer ukurasa wa 488] Kama hali ya uwanda wa mji yenyewe ilivyohitaji, Tito aliyaelekeza mashambulizi yake dhidi ya upande wa kaskazini, na dhidi ya eneo lote la theluthi moja, au ni kuaema kuwa kutoka kwenye matuo ya washambuliaji, kwenye ukuta wa kwanza ni kwa jinsi hiyo tu ndipo hawa wanajeshi waovu walipoanza kazi yao ya kushambulia wakianzia maeneo makuu matatu, na ndipo mashambulizi ya ndani yalipoisha na pande zote mbili yaani upande wa John wa Gischala na Simon Bar-Giora, waliyaunganisha majeshi yao pamoja. Kwenye jaribio lao moja la mashambulizi walipigana kwa mafanikio na ni kwa ajili ya kuingilia kwake Tito binafsi (ambaye yeye mwenyewe aliwaua maadui kumi na wawili) na machine zilipona na kuokolewa. [B. J. v 6, 2-5] Baada ya kazi ya siku kumi na tano, mmoja kati ya mafahali wake wa vita alibomoa shimo la ukuta na Warumi wakalibomoa, na katika siku ya 7 Artemisius (Iyari, yaani kati ya Aprili/Mei) wakamudu kuudhibiti ukuta wa kwanza. [soma kitabu chake Josephus B. J. v,7,2] ”

 

Siku tano baada ya kutekwa kwa ukuta wa kwanza, ukuta wa pili uliangushwa kwa nyundo kubwa na Warumi. Tito aliingia na wanajeshi maalumu walioteuliwa lakini akazuiwa na kurudishwa nyuma na Wayahudi

 

Siku nne baadae aliuchukua tena na wakati huu akauchukua moja kwa moja. Tunaona tena jinsi siku hizi za 12 na 16 za mwezi wa Iyari zlivyomuhimu wake kwenye maagimisho ya Pasaka ya Pili.

 

Hatua ya pili ya Tito ilkuwa ni kuzijenga ngome mbili ili kujilinda dhidi ya watu wa mjini na nyingine mbili za kujilinda dhidi ya Antonia.

 

Kila kikosi kimoja miongoni mwa vikosi hivi walipewa kazi ya kujenga ngome moja. Simon Bar-Giora alikuwa ndiye amiri wa Mji wa Juu na John wa Gischala alikuwa ni amiri wa Antonia (B. J. v 9,2).

 

Kisha Warumi walimpa Josephus kazi ya kuwaasa watu wanaoishi ndani ya mji huu wiajtsalimishe, kazi ambayo haikuzaa matunda yoyote, maana hawakumsikiliza.

 

Hatimaye chakula kikaisha mjini na masikini waliojaribu kutoka kwenda kujitafutia huko nje ya mji walikamatwa na kuteswa mbele ya macho ya watu waliokuweko mjini. Na wakati mwingine walikatwa viongo vyao na kurudishwa kwa nguvu mjini (B. J. v 10, 2-5).

 

Warumi walimaliza ujenzi wa ngome zao siku ya 29 Iyari mwaka 70BK.

 

Wayahudi wakiwa chini ya John na Simon, waliendelea kukaidi hadi ujenzi wa ngome hizi ulipoisha kabla hawajakomeshwa na mji kuangamizwa.

 

John alichimba barabara ya chini kwa chini kwenye ngome hizi hadi Antonia na kisha akaichoma moto minara kwa wakati wake muafaka. Matokeo yake barabara hii ya chini kwa chini ilianguka na ngome zikaangukia kwenye wimbi la mwako wa moto na ukateketea. Siku mbili baada ya Simon Bar-Giora kushambuliwa na kuteketezwa, pia ngome za Mji wa Juu ukateketezwa (B. J. v 11, 4-6).

 

Kisha Tito akauzungushia mji kwa ukuta imara na wakudumu wa mawe kabla hajaanza kujenga ngome mpya. Alifanya hivyo kuwa ni mbinu ya kuutenga mji huu ubaki upweke ili usiweze kupata mahitaji yake toka nje na kisha ukumbwe na baa la njaa na hatimaye ujisalimishe. Na kilikuwa ni kipindi cha kushangaza cha aina yake kilichodumu kwa siku tatu na jeshi lililoulinda mfululizo likizuia asiwepo hata mmoja wa kutoroka. (B. J. v 12, 1-32)

 

Hali mbaya ya njaa iliyoukumba nji huu ni jambo ambalo Mungu aliwahi kuwaambia hapo kabla (Law. 26:29; Kum. 28:29; Yer. 19:9; Eze. 5:10) na kama ilivyonukuliwa kwenye historia (2Fal. 6:28-29; Omb. 2:20; 4:10; Bar. 2:3). Maria wa Beth-Ezob ndiye aliyeandikwa kuwa ni miongoni mwa waliokula watoto wao (B. J. vi 3, 4; Euseb. HE iii, 6; & Jerome ad Joel 1:9 ff (CCL lxxvi, p. 170; cf. Schürer fn. 102, p. 504).

 

Mafuta matakatifu ya mzeituni yaliyokuwa kwenye “Chumba cha Myumba ya Mafuta” kilichokuwa upande wa kusini magharibi mwa sehemu iliyokuwa inajulikana kama Uwa wa Wanawake hatimaye ukatumika kwa kufanyia mambo ya kufuru na machukizo. Josephus alilishutumu sana tendo hili lakini lilikuwa ni jambo linaloeleweka (B. J. v 13, 6).

 

Na kwa kipindi cha takriban siku ishirini, ngome ilikuliwa imeisha kujengwa na kipindi hiki nyingine nne zilikuwa zimeshajengwa dhidi ya mji wa Antonia. Wakati huu, mbao zililetwa kutoka umbali wa stadia 90 (mwendo wa saa 4.5) hadi kuleta kwenye kiwanja wa ujenzi iliyokuwa wazi.

 

John wa Gischala akalijaribu kuwashambulia siku ya 1 mwezi Panemus au siku ya Mwandamo wa Mwezi Tammuz au Wanne  lakini akashindwa, hali iliyosababishwa na ukosefu wa ujasiri na mori wa vita kutokana na mauaji yaliyotokea na Warumi kuwa na ujasiri na nguvu kubwa na morari wa vita (B. J. vi 1, 1-3).

 

Wayahudi wakaondoka na mafuriko ya maangamizi kaanza. Ilipoanza haikuonyesha mafanikio lakini hatimaye ukuta ulianguka kwa namna yake wenyewe na kufanyika kuwa umeanguka sana. Hatahivyo, John wa Gischala alikuwa ameshausimamisha ukuta wa pili tayari nyuma ya eneo ulilokuwa umenguka na kufanya iwe ni vgumu sana kuuongeza.

 

Mnamo siku ya 3 Panemus (Tammuz) Tito aliwaamumrisha wanajeshi wake wauchukulie hatua, na askari wa Kisyria aitwaye Sabinus na washiriki wenzake kumi na moja waliuangusha fell (B. J. vi, 1, 3-6). Siku ya 5 mwezi Panemus, kiasi cha takriban askari ishirini au thelathini walupima ukuta majira ya usiku na kuwaua asakari wa kikosi cha kwanza cha kulinda doria. Ndipo Tito akaendelea mbele kwa haraka mbele yao na kuwasumia mbali Wyahudi na kuwarudisha kwenye eneo lilikokuwa Hekalu.

 

Jweshi la Warumi lilirudishwa nyuma pia tena lakini waliiteka Antonia na wakafanya uwezekano wa kuuangusha chini (B. J. vi 1, 7-8).

 

Wayahudi walizewa kuudhibiti shughuli zite za utoaji wa sadaka za kila siku za asubuhi na za jioni ingawje walizikomesha zile sadaka za Wamataifa ilipofika mwaka 66BK, kipindi yalipoanza maasi.

 

Na ilipofika siku ya 17 ya mwezi wa Nne au wa Panemus au wa Tammuz, kukawa hakuna wanaume wa kutosha kuendelea na shughuli ya utoaji sadaka na wakaingia kwenye mkumbo uliowapata wa janga la ukosefu wa chakula uliosababisha baa kuu la njaa, jambo lililopelekea utaratibu wa kutoa sadaka usimame. Licha ya juhudi zilizofanywa za kuirudisha hali hii kwenye maasi ya Bar Kochba, haikuwezekana kuirudisha hali hii kwa mafanikio yake.

.

Mungu akaondoa na kukomesha utoaji wa sadaka na akaliondoa Hekalu lililokuwa linaonekana kwa macho, na kumfanya Masihi kuwa ndiye Hekalu, yaani Kanisa. Na ule utaratibu wa kutoa dhabihu ya wanyama wa kuchinjwa utarejeshwa tena mjini Yerusalemu baada ya kurudi kwake Masihi na kuurejeshamarejesho mapya mji wa Yerusalemu na kipindi ambacho Hekalu litarejeshwa upya kwa mujibu wa sawa na unabii wa Ufunguo wa Daudi (pia soma jarida la (Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria (Na. 297) [Commentary on Zechariah (No. 297)].

 

Josephus akatakiwa afanye juhudi ya kuwasihi tena ili wasalimu amri, lakini juhudi yake haikuzaa matunda tena hata mara hii.

 

Mashambulizi zaidi ya kulishambulia Hekalu saa za usiku yalishindwa na Tito hakuwa na namna nyingine bali kuamua kufanya mashambulizi makubwa ya sehemu zote. 

 

Hekalu lilikuwa limejengwa vizuri na lilizungushiwa na ngome imara, ambayo ilikuwa ni ya mraba na yenye nguzo zilizojengwa kwenye kuta nene. Uwa wa ndani pia ulizungushiwa na kuta nene, na kufanya safu ya pili ya ulinzi baada ya kuta za nje zikianguka.

 

Tito alianza kwa kujenga ngome nne kwenye kuta za nje. Wakati huu vifaa vya ujenzi vililetwa mbali kiasi cha urefu wa stadia 100 kutoka Yerusalemu.

 

Wayahudi hawakuwa wavivu wa kufanya kazi. Waliazimu kuzungushia safu ya nguzo kwenye ukuta wa upande wa magharibi kwa kutumia vifaa mchanganyiko vya ujenzi na vyenye kuweza kuwaka kiurahisi na wakaifanya ionekane kama imeachwa na kufukarika. Warumi wakapanda kwenye nguzo zile. Walipokwisha panda tayari hadi kileleni, Wayahudi wakaiwasha moto kuichoma. Warumi walishindwa kabisa kujiepusha na wakafa kwa mwali wa moto

 (B. J. vi 3, 1-2).

 

Ngome hizi ziliisha mnamo siku ya 8 Abu au mwezi Lous. Wanajeshi wakaletwa na kusonga mbele na kazi ya kuuzingira ikaanza tena. Kuta zilikuwa hafifu sana na Tito akalazimika kuyachoma moto malango ili apate nafasi ya kuingia kwenye Ua wa Nje. Mtu anaweza kujiuliza ni kwa nini hakujaribu kufanya hivyo pale mwanzoni.

 

Hadi kufikia siku ya 9 Abu, malango yote yalikuwa yameteketezwa kabisa. Josephus anadhania kwamba baada ya hapo Tito aliunda baraza la Vita ambalo lilishauri kuwa waliache Hekalu peke yake (B. J. vi 4, 3).

 

Siku ya 10 Abu Wayahudi wakafanya mashambilizi mawili ya kujipizia yaliyotokea kwenye Ua wa Ndani wa Hekalu iliyokuwa kama ngome yao.

 

Wakiwa wanajilinda kwa kujihami na mashambulizi haya ya pili, mwanajeshi mmoja wa Kirumi ambaye alikuwa kwenye mahangaiko makubwa akarusha kizinga cha moto kupitia kwenye safu ya nguzo ambacho kilienda hadi kwenye Helaku na kuanza kuwaka

 

Josephus anadai kwamba baada ya Tito kufahamishwa habari hii kwa haraka alimuamuru kamanda wake aende haraka na wanajeshi wake ili wakajaribu kuuzima mto huo na kuliokoa Hekalu. Alipotoa amri hii muhimu na inayohitaji kutekelezwa maarufu kama “mêlée” amri yake ilipuuzwa na moto ukazidi kuwaka na kuteketeza.

 

Anaelezwa kuwa alitoa amri kadhaa ili kuliokoa Hekalu, lakini inaelezwa kwamba askari wake waliokuwa wamekasirika na kuchoshwa na vita sio tu kwamba walipuuzia tu amri zake bali inaelezwa kuwa waliendelea kutupa makombora kadhaa ya moto ndani yake. Inaelezwa kuwa Tito alikuwa ameingia ndani na kuliangalia kabla halijateketezwa (B. J. vi 4, 6-7).

 

Josephus anaitaja tarehe ya kuteketezwa kwa Hekalu hili kuwa ni siku ya 10 Abu (B. J. vi 4, 5). Hata hivyo, kwa mujibu wa mapokeo ya marabi, siku hii ya kuteketezwa kwa Hekalu inatajwa kuwa ilianzia jioni ya siku ya 9 Abu (m Taan. 4:6), yssni msjira ya jioni (b Taan. 29a) na ilikuwa ni mwishoni mwa maadhimisho ya siku takatifu ya Sabato.

 

Lakini ukweli ni kwamba, inawezekana sana kuwa huenda hapa Josephus anajaribu kumuosha Tito kwa kitendo chake cha kishenzi na kisicho na huruma wala hofu. Mwanahistoria mwingine maarufu, Sulpicius Severus (kwenye kitabu chake kiitwacho Nyakati [Chron], ii 30, 6-7) anatoa mtazamo wezekano na mwandishi mwingine Orosius (vii 9, 5-6) pia anaelezea juu ya maangamizi haya kuwa ni ya Tito, wakati mwandishi mwingine Schürer anasema kwamba W. Weber ndiye mwenye mtazamo huo.

 

Schürer anasema kwamba Valeton anaukosoa mtazamo huu mpotofu wa Josephus kwa kushindwa kwake kuchukua na kuyaandika vizuri matukio ya vile baraza la Vita.lilivyoamua kulichukua na kulikalia Hekalu na jinsi walivyolichukua kwa nguvu na walivyoliteketeza kwa makusudi kama walicyoweza. Mwanahistoria mwingine Valeton anadai kwamba tendo hili lilitokana na maelekezo na amri aliyoitoa Vespasian lakini baraza hili lingeweza kabisa kuubatilisha uamuzi huo na kuupinga. 

 

Askari wa miguu wa Kirumi waliletwa ndani ya Hekalu na kutweka bendera yao wakilikabili Lango la upande wa Mashariki. Na askari hawa wakatoa sadaka mbele yao. Josephus anasema kwamba Tito alitangazwa kuwa ndiye Mhusika Mkuu na Aliyewezesha mambo yote haya baada ya kumaliza kutoa sadaka yao kuu.

 

Vyumba vilivyokuwa kwenye kuta za Hekalu vilikuwa vikitumiwa na makuhani nao walikuwepo bado. Walilazimishwa washuke chini kutoka mafichoni walikojificha wakiwa na kiu kali na hatimaye waliuawa wote.

 

Tito akawaambia Wayahudi waliomshambulia kwa maneno wakimlaumu kwa kujaribu kumlazimisha mambo kwa kuamuru mashambulizi na kuuteketeza mji wa Yerusalemu. Warumi walichoma moto maeneo yote muhimu na pia mji wa Acra, hadi kwenye jumba la halmashauri na mji wa Ophlas. 

 

Watu kutuka jamii ya daraja la juu walimsihi tena na akaruhusu baadhi yao wachukuliwe na kupelekwa Roma kwa ajili ya usalama wao (B. J. vi. 6, 1-3).

 

Josephus aliandika taarifa za unyama mkubwa waliofaunya waasi wa Kiyahudi kwenye mji huu kwa wakati ule.            Wazelote walikimbilia kwenye Mji wa Juu. Hatimaye mji ulifanyiwa matendo ya unyang’anyi na uporaji na uharibifu ulifanyika kwenye Mji wa Juu na Warumi walichukizwa wakiamini kuwa matendo yale ya unyang’anyi na uporaji yalikuwa yamepangwa na kukusudiwa.

 

Wazelote walitumia udhaifu wa Warumi ili kuwapiga, wakatuama kwenye maeneo ya kujificha na wakafanya mauaji ya kumchinja kila mtu aliyejaribu kutoroka na kwenda kwa Warumi. Hakukuwa na mahala mjini kote ambapo hapakuchafuliwa na mtapakao wa maiti ya wale waliokufa kwa njaa au kwa kuchinjwa. Walijaribu kujificha kwenye mahandaki mjini na waliyachoma maeneo mengi kwa moto kwa kiasi kibaya mno kuliko hata walivyofanya Warumi wenyewe. Watu waliokimbi nje ya nyumba zao ili kujiepusha na moto waliuawa na Wazelote hawa pasi na huruma. Walikula vyakula vilivyotekwa kwa mwagiko wa damu na unyang’anyi. Josephus anasema kwamba anaamini kuwa iwapo kama wasingewateketeza, basi wangeila niili ya wafu yenyewe (B. J. vi  7, 1-3).

 

Mnamo siku ya 20 mwezi Abu, Tito alitoa amri ya kuzingira kingo na kuzitenganisha na maeneo ya Juu ya Mji ya Mlima Sayuni.

 

Vikosi vine vya wanajeshi vilikwenda na kuweka kambi zao upande wa Mashariki mwa mji mkabala na Jumba la Ikulu ya Kifalme. Mabaki ya wanajeshi hawa pamoja na maboma yaliyotoka Xystus hadi kwenye daraja na mnara ambao Simon aliujenga na kuuimarisha ili ajilinde dhidi ya John.

 

Mpango wa kujaribu kuudhoofisha uliofanywa na Idumeans ulikubaliwa na Tito, lakini Simon aliuzuia na watu wane walipokuwa wakirudi na waliuawa na viongozi wakatiwa jela. Hata hivyo, matendo ya uteketezaji na maafa vilizidi kupamba moto.

 

Waliwaacha kwenye mateso na familia zao. Kima cha kuwanunua watumwa kilipungua chini bei yake kwa kuwa walipungua thamani yao kwa kuwa watu waliotekwa nyara walikuwa wengi na wanunuzi walikuwa ni wachache. Kuhani aliyeitwa jina lake Jesua (Yesu) mwana Thebuthus alipata ulinzi wake kutoka kwa Kaisari, na kwa Phineas mtunza hazina aliyekuwa anafanya kazi ya utunza hazina wa fedha na vitu vya Hekaluni vikiwemo vinara vya dhahabu pamoja na mavazi ya kikuhani ya rangi ya zambarau na nyekundu kwa ajili ya kujifunika na vilikuwa ni vitu vya gharama. Hata hivyo, walipewa msamaha kama walivyofanyiwa na wale waliowaacha upweke (B. J. vi 8, 1-3). Dhahabu iliyochukiliwa kwa kuporwa ilikuwa nyingi sana kiasi kwamba iliathiri bei ya dhahabu kwenye masoko ya Syria baada ya mzingiro huu.

 

Kingo za kuzungusha kwenye mji huu ziliisha kujengwa siku ya Saba ya mwezi wa Eluli au mwezi wa Gorpieus, kwa siku kumi na nane. Watu wengi walikuwa wametoroka na kujificha. Hata wale wababe waliowasumbua sana watu pamoja na jeshi lao walishindwa na kudhoofika na woga, na waliiacha minara ambayo ilikuwa ni imara sana na migumu kushindwa na wazingiraji.

 

Josephus aliamini kuwa ilikuwa ni Mungu mwenyewe tu ndiye aliwaondoa kwenye minara ile baada ya walivyoondoka toka mjini. Walifanya haraka kukimbia ili wajiponye kwenye bonde lililokuwa huko Siloam. Waliwashambulia ili kujilipiza kisasi kwa Warumi ila walikuwa ni dhaifu na walichoshwa na kukatishwa tama na walinzi.

 

Kisha Warumi wakaenda mjini na kuanza kuwaua na kuchoma moto kila mahali na kila waliyemuona humo mjini. Mawindo yao hayakuwafaa kwa kuwa vyumba vya juu vya nyumba vilikuwa vimejaa miili ya watu waliokufa kwa njaa. Mji ulikuwa unawake moto kama ulivyokuwa siku ya 8 mwezi Eluli na ukawa ndiyo kwanza umechukuliwa na kudhibitiwa na Warumi (B. J. vi, 8, 4-5).

 

Watu walionusurika walikuwa ama wameuawa, au walipelekwa migodini au walihifadhiwa kwa kuvalishwa kombati za wanamgambo.

 

Machimbo haya yalikuwa nchini Misri na kwa hiyo, ile ahadi ya Mungu kuwa atawarudisha tena Misri kwa kosa lao la kulivunja agano lake ikatimia. Watu wenye sura nzuri sana na watanashati na wenge nguvu kuliko, walichaguliwa ili kusherekea kushindwa kwa John wa Gischala na alikuwa ametolewa kutoka kwenye pango alimokuwa amejificha kwa ajili ya njaa na akafungwa kifungo cha maisha gerezani. Simon Bar-Goria, akakamatwa kipindi fulani baadae, na akahifadhiwa kuwa ishara ya ushindi wao.

 

Na kama tulivyojionea wenyewe yoka mwanzo, ni minara mitatu tu ya majumba ya Herode (ambayo ni Hippicus, Phasael na Mariamne) na upande mmoja tu wa ukuta ndizo zilikuwa zimebakia zimesimama.

 

Tito alisherehekea tukio hili kwa kuwagawia zawadi wanajeshi wake, na kutoa sadaka na kwa kufanya sherehe kubwa za nderemo.

 

Mtiririko wa matukio ya Vita tangu Mwaka 71 hadi 74BK

 

Tito akakiacha Kikosi cha 10 kwa walinzi wa mji wa Yerusalemu.

 

Akaondoka na wanajeshi wealiobakia hadi Kaisaria Maritima, ambako mateka na wafungwa waliwekwa kwenye gereza salama.

 

Tito akaenda Kaisaria Filipi, kumuona Agripa, ambako baadhi ya wafungwa walilazimishwa kupigana na wanyama wa porini, au kuchukua sehemu yao kwenye michezo ya kupigana na wanyama. Kisha akarudi Maritima na kusherehekea maadhimisho ya kuzaliwa kwa ndugu yake Domitian (tarehe 24 Octoba) kwa michezo mingine mingi mnamo tarehe 17 Novemba huko Berytus alisherehekea kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa baba yake Vespasian kwa mtindo ule ule kama alivyofanya huko nyuma.

 

Wafungwa wa Kiyahudi walilazimishwa wauane kwenye sherehe hii iliyofanyika kwenye mji wote wa Antiokia. Kisha wakaondoka na kuelekea Zeugma iliyoko Frati na kurudi Antiokia. Kisha wakarudi kutoka Misri na kuviacha vikosi vyao vya wanajeshi huko Alexandria (Schürer, Toleo la  I, p. 509).

 

Wafungwa maarufu wapatao mia saba wakiwemo Simon na John walihifadhiwa kwa ajili ya kuwatumia kwenye shughuli za sherehe. Na ingawaje waliweza kushunda mara kadhaa, lakini Vespasian, Domitian na Tito waliweza kuwashinda kwa pamoja mnamo mwaka 71BK. Kwa kufuatia destuiri za wahenga wa hapo zamani, baada ya sherehe hii ilibidi Simon alichukuliwe kutoka gerezani na akauawe.

 

Miongoni mwa tunu zilizotolewa kuwapa mashujaa waliosababisha kushunda kwa vita ile vilikuwa ni tunu mbili za dhahabu zilizotolew kutoka Hekaluni na ndizo zilikuwa ndiyo zawadi kuu kupewa mashjaa hawa (na zilitolewa mbele ya macho ya Wayahudi wenyewe wakishuhudia). Navyo vilikuwa ni Meza ya Mikate ya Wunyesho na vichala Saba vya vinara vya dhahabu (B.J. vii 5,5).

 

Vespasian akaviweka vinara hivi kwenye Hekalu la Mungu-mke wa Amani (Pax) aliyokuwa ameijenga na ambayo hatimaye ilichomwa moto na kuangushwa chini na Wanajeshi watiifu (Herodian i 14, 2, sawa na anavyosema Schürer, ukurasa wa 510, pia ukurasa wa 132).

 

Schürer anaamini kwamba Geiseric aliwachukua na kuwapeleka Afrika baada ya kipindi ambacho Vandals waliuteka na kuuchukua mji wa Roma mwaka 455BK, na hatimaye wakasafirishwa hadi Constantinople na Belisarius baada ya kuanguka kwa dola ya Vandal mwaka 534BK (sawa na vinavyosema vyanzo vingine).

 

Kusalimu amri kwa sehemu zilizobakia za Palestina

 

Palestina ilikuwa haijasalimu amri yote bado ingawa mji wa Yerusalemu na upande wake wa kaskazini ulikuwa umeteketezwa kabisa.

 

Ngome za Herodium, Machaerus na iliyokuwa sasa ni mashuhuri ya Masada zilikuwa hadi sasa kwenye udhibiti wa waasi.

 

Lucilius Bassus, liwali wa Palestina, alikuwa amepewa kazi ya kuwapunguza waasi hawa.

 

Josephus anaonyesha kwamba mkakati wa kuwazingira na kuwashinda uliobuniwa na Herodium ilikuwa umekamilika bila matatizo makubwa (B. J. vii 6, 1). Machaerus ilichukua kipindi kirefu lakini hatimaye nayo ilisalimu amri pia kabla ya shambulizi la mwisho halijatokea. Machaerus ulikuwa upande wa kusini ya mpaka wa Peraea ikifuaatiwa na jimbo la Nabataean. Ilikuwa ni siku ya sherehe ya kupeana zawadi ya Khirbet el Mukawer. Mwanzoni kabisa ulilindwa kwa ngome ya Alexander Jannaeus, ambayo iliaharibiwa na kuangushwa na Gabinus (kitabu cha Antiq., xiv 5, 4). Hatimaye ikajengewa ngome tena na Herode Mkuu (B. J. vii 6, 2 sawa na asemavyo Schürer 1, ukurasa wa 511, na. 135, re Pliny NH v 16 na umuhimu wake).

 

Kijana aliyejulikana kwa jina la Eleaza alijitathmini na kutaka kuulinda lakini alikamatwa. Warumi walimtisha na hatimaye walimsulibisha mbele ya lango la ngome na hatimaye watu waliokuwa ndani ya ngome hiyo wakaamua kujisalimisha. Hili lilikuwa ni tendo geni kuwahi kutokea, lakini ngome ikabakia ukiwa ikiwa imekimbiwa na wakazi wake hadi Masada iliyokuwa upende wa kusini iliyokuwa ngome pekee iliyobakia ya waasi na kuonekana kuwa ungekuwa ni uamuzi wa busara (B. J. vii 6, 1-4).

 

Lucilius Bassus alikufa kwenye kampeni hii na kazi yake akapewa mrithi wake Flavius Silva ili aendelee na mkakati wa kuupunguza Masada.

 

Huu Masada (ambao maana yake ni ngome ya mlimani) ulipunguzwa baada ya kampeni ya siku nyingi. Kazi ya kuuzingira ya mwaka 73BK inaonekana hadi sasa (hadi sasa kuna sahani zinazoonekana). Ingeweza kukabiliwa tu kwa kutumia mwelekeo wa upande mmoja tu (pia tazama kitabu cha Strabo xvi 2, 44 na Schürer kilikile., ukurawa 137).

 

Masada umekuwa ukishikiliwa tangu mwanzoni kabisa mwa Vita hii kwenye zama za Sicarii aliyekuwa chini ya Eleaza mwana wa Yairo, aliyekuwa ni wa uzao wa Yuda Mgalilayan, aliyeijenga ngome hii.

 

Upande unaoelekea Bahari ya Chumvi una maporomoko na hauwezi kusogelewa na wazingiraji. Ni mahali pamoja tu kwenye maporomoko ambapo watu hawa waliokuja kuuteketeza mji wangeweza kuteketezwa, na wahanga wakuuhami mji walikuwa wametegemea tayari wanategemea kuvunjika na kusimamishwa kwa lundo la kuni na dunia ambalo lilikuwa sawa kama na mnyumbuliko ambao maporomoko yalikuwa ni makubwa sana dhidi yake (kwa kujibu wa kitabu cha Schürer).

 

Warumi walifanikiwa kukipunguza kizuizi hiki kwa moto.

 

Ndipo Eleaza akaona kuwa bilashaka Warumi wangeweza kuwashinda. Akawashauri kwa maneno kuwa kikosi kizima cha ulinzi wa mji kiwaue watu wa nyumbani wao wenyewe na kasha wajiue wenyewe (kitabu cha B. J. vii, 8, 6).

 

Walitii na kufanya hivyo, na Warumi wakaingia kenye ngome ya mlimani ya watu waliokufa na wakakuta wanamgambo wao wote wake kwa waume na watoto wamekufa. Waliacha aswira ya mauaji ya kuchinja kusiko na huruma walikokufanya.

 

Josephus anaelezea kuwa mauaji haya makuu ya kujitoa mhanga yaliyofanywa kwa kujichinja huko Masada yalitokea siku ya 15 mwezi Xanthicus, au Abibu, mwaka 74BK. Na kuifanya, Siku ya Kwanza ya Mapumziko Matakatifu ya Pasaka kuwa ni siku ambayo wanamgambo wao wote walifanya uamuzi huu wa kujiua.

 

Maana ya jambo hili lilikuwa dhahiri na kamili. Baada ya Malaika wa Kifo kupita mbali na Yuda kwenye Pasaka hii siku ya 15 Nisan, ikawakuta wao wameisha mkataa Kristo na Dhabihu yake. Watu walipewa miaka arobaini ya kufanya toba. Lakini hawakufanya hivyo na kipindi cha nusu ya mwisho ya majuma ya mwisho ya miaka yalishuhudia kuanza kwa vita. Siku ya 10 Abu, Hekalu liliteketezwa. Kwenye kipindi cha Pasaka ya mwaka 74BK, uwezo wao wa kuzuia na kushindana waliokuwanao watu wa Yudea ulikoma na kwisha kabisa na taifa zima likawa kwenye mtafaruku na mtawanyiko.

 

Jambo lisilosameheka ni kwamba mataifa yaliyokuwa karibu yake yalikichukulia kipindi hiki cha maasi kuwa ni kizuri kwao na cha kuwafanyia mambo ya ukatili Wayahudi na kisha wakaanza kuwaua kwa kuwachinja Wayahudi kila mahali. Katika mji wa Damascus, wananchi wa Syria walianza kuwachinja Wayahudi, lakini hakukuwa na hata mji mmoja miongoni mwa miji ya Syria ambao haukumuua mkazi wa Kiyahudi. Mji wa Damascus peke yake ulifanya maangamizi ya Wayahudi wanaokadiriwa kufikia elfu kumi na nane, wakiwemo wanaume, wanawake na watoto. Nchini Misri waliuawa Wayahudi zaidi ya elfu sitini (B. J. vii, 8, 7).

 

Wayahudi walikuwa wanateswa kwa moto na kubanwa kwenye vitu asili yachuma hadi kufa. Baaadhi yao walitolewa waliwe na wanyama wakali wa porini lakini waliokolewa kimiujiza, ni wachache wao tu ndio waliliwa, na walipopona walipelekwa tena kwa wanyama hawa kwa mara ya pili huku wakijiburudisha kwa vile wanavyoraruliwa na wanyama hawa na wao wakiona jambo hilo nikama burudani tu kwa umati uliokusanyika kuja kushuhudia (kitabu hikihiki cha B. J.). kwa jinsi hii walikuwa wamedhalilishwa sana. Mungu ana maana kamilifu kuihusu hali hii, na nabii Zekaria ameielezea kwenye unabii wake kwao (soma jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria (Na. 297) [Commentary on Zechariah (No. 297)].

 

Baada ya kuanguka kwa Masada kulikuwako bado mahali pa kutokea dhabihu ambapo palikuwa panaendelea kufanya kazi napo palikuwa ni huko Leontopolis. Vespasian aliamuru pafungwe mwaka 71BK lakini ubishani na mapigano vilitokea bado mnamo mwaka 74BK na mapigano yakatokea mara tatu huko Alexandria na Cyrene pia. Schürer anamnukuu Josephus (B. J. vii 10, 1-3) kwa kusema kuwa hadi tete nay a ghasia ilyotokea huko Alexandria ilipelekea kufungwa kwa Hekalu la Leontopolis, ambalo lilikuwa limejengwa na Kuhani Mkuu Onias IV yapata mwaka 160BK, ili kuutimiza unabii uliotolewa na nabii Isaya 19:18-23. Josephus anasema kwamba Hekalu hili lilikuwa limeendelea kufanya kazi kwa kipindi cha takriban miaka mia tatu na arobaini (B. J. vii, 10, 4). Anasema kwamba Lupus, liwali wa Alexandria, alikwenda kulitembelea kwa amri ya Kaisari na akaondoa baadhi ya misaada na kulifunga. Kwa mujibu wa Josephua, kipindi cha kudumu kwa Hekalu kilikuwa ni kuanzia ujenzi wake hadi kufikia mwisho wake miaka ya 270-272KK. Kipindi hiki ni kabla ya zama ya Onias IV. Kwa hiyo, ni lazima kuamini kwamba kuna ushahidi wa kuweko na chanzo kingine cha uwepo wa Hekalu hili uliokuweko siku kabla ya Onias IV alipokwenda kule, au kama vinginevyo basi na tuamini ya kuwa Josephus alikuwa na makosa makubwa kwenye uandishi wake.

 

Kisha Sicarii akakimbilia Alexandria na hakutosheka na kule kulelewa kwake kwenye ardhi ya Palestina akaasi, akashawishi na kuhamasisha uasi huko Alexandria na akamwua kiongozi wa Wayahudi aliyekuwa anawapinga. Sababu ya kukataa kwao likuwa ni kwamba walilazimishwa kumwita kaisari kuwa ni Bwana wakati wakijua na kuamini kwamba ni Mungu peke yake ndiye aliye Bwana. Watu wa Alexandria wakawageukia kama walivyofans turned on them, as did the Thebans turn on thoseya watu wa Thebes na wakawatoa ili wateswe. Josephus anaelezea jinsi walivyokuwa wakakamavu na wajasiri watu wazima na watoto wao ambao waliwashangaza sana watu kwa jinsi walivyovumilia mateso na wasigeuke na kukiri kuwa Kaisari ni Bwana (B. J. vii 10, 1).

 

Sicarii, akiwa na mtu aitwaye Jonathan, pia aliwachochea waasi waliokuwa huko Cyrene miongoni mwa watu maskini na wajinga. Catallus, liwali wa mji wa Pentapolis ulioko Libya akasikia jinsi masikni hawa walivyohamasika na kuwa wanaenda msituni wakiwa upande wa Jonathan ili wakajionee ishara na maajabu aliyowaahidi. Catallus akapeleka wanajeshi, wa aina mbili, yaani wapanda farasi na watembea kwa miguu na akakutana nao njiani. Wakawachinja watu wengi sana.miongoni mwao walikuwa ni askari wa kiraia wasiokuwa na mafunzo ya kijeshi.. Jonathan mwenyewe akatoroka bali alikamatwa baada ya msako mkali. Hatimaye aliwalaumu wayahudi matajiri kuwa walikuwa nyuma ya jambo hili na kwa hiyo Catallus aliweza kuwapokonya idadi kubwaya wafuasi wa Kiyahudi. Akawa anamshutumu kwa kwa uwongo Sicarii aliyekuwa ni Myahudi mwenye mali nyingi na watu elfu tatu miongoni mwao walikufa na mali zao zikaongezewa kwenye hazina ya Kaisari. Ili kujiepusha na adhabu kwa maovu haya, ndipo akawashawishi kina Jonathan na Sicarii wakubali kutoa ushahidi wa uwongo dhidi ya Hayahudi matajiri walioko kote kuwili yaani wa Alexandria na wale wa Roma, kufanya mateso yaongezeke kwa Wayahudi wote wanaokaa kwenye miji mashuhuri ya ukanda wa Mediterranean (B. J. vii, 11, 2-3).

 

Kisha Catallus akaenda Roma kuwachukua Jonathan na wafuasi wake pamoja na mateka wao wote. Alitaraji kukabili mashitaka lakini Vespasian akatoa ombi maalumu la kuondoa mashitaka ya Wayahudi walioshitakiwa na Catallus na Jonathan. Kisha Jonathan akateswa na kuumizwa akiwa hai. Vespasian hakumuadhibu Catallus, bali Catallus alipatwa ugonjwa na kufa kwa hali ya kushangaza sana kipindi kifupi tu baadae, kwa kusumbuliwa na maradhi ya mwili na akili. Utumbo wake yalikuwa yameharibika na kutokeza nje na hatimaye akafa (B. J. vii, 11, 3-4). Josephus alishikilia kuamini kuwa huu ulikuwa ni mfano wa mapigo kutoka mbinguni kwa watu waovu.

 

Kwa hiyo, Viya vya Wayahudi iliishia kwa maangamizi ya watu wa Yuda, na nchi ikasambaratika. Kila jaribio lililofanywa kulirejesha upya taifa hili na kulijenga Hekalu lile lilishindwa na kuishia patupu. Kania liliteswa pia lakini tangia kipindi hiki limeendelea kudumu likiwa jangwani kwa kipindi cha miaka elfu mbili. 

 

Lakini marejesho mapya na wongofu wa watu wa Yuda unakuja na kipindi hiki cha Siku za Mwisho tutajionea marejesho ya mfumo wa Masihi huko Yerusalemu.

q