Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[299E]

 

 

 

Mtu wa Kuasi, na Ukengeufu

 

(Toleo La 1.0 20101030-20101030)

 

Kuja kwa Mwana wa Uharibifu kwenye Kanisa la Mungu katika Siku za Mwisho kuna maana kubwa sana na kuujua utambulisho wake ni jambo la muhimu sana kwa Kanisa ambalo ni Mwili wa Kristo.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hakimiliki © 2010 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki..

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Mtu wa Kuasi, na Ukengeufu


Jina hili la Mtu wa Kuasi au Mwana wa Uharibifu linatokana na maandiko ya Mtume Paulo kwenye Waraka wake wa Pili kwa Wathesalonike ambao aliwaandikia rasmi ili kuwaonya kwa tukio hili kuwaeleza jinsi litakapotokea na kipindi chake na mambo yatakayotokea kabla ya kutokea kwa Ukengeufu huu na Kurudi kwake Kristo.

 

Aliwaandikia Wathesalonike akitumia maneno ya “Katika jina la Mungu, Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo. Kwa hiyo andiko hili halipaswi kutafsiriwa vibaya kana kwamba linatutia moyo kuamini imani ya miungu miwili kama wanavyolichukulia watu wa imani hiyo

 

2Wathesalonike 1:1-12

1Paulo, Silvano na Timotheo, Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo: 2Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.

 

Kanisa la Thesalonike lilikuwa na msingi imara wa kiimani na lilikuwa linaendelea vizuri katika kumpenda Bwana na inaonekana kuwa watu wenye mafundisho yanayopinga ulazima wa Amri na Sheria za Mungu maarufu kama Waantinomia walifaulu kuwapata baadhi yao na walianza kueneza mafundisho haya mapotofu ya hawa Waantinomia. Hadi hapo kanisani kwao na ndipo Paulo alipochukua hatua hii ya kuwaandikia waraka huu akikusudia kuwaimarisha imani yao na pia kuwafariji na mateso waliyokuwa wakiyapitia


3Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu sikuzote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka. 4Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili. 5Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mtastahili Ufalme wa Mungu, ambao ninyi mnateswa kwa ajili Yake. 6Mungu ni mwenye haki: Yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi 7na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu. 8Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.

 

Walikuwa wanaadhiwa kwa ajili ya kuzifuata na kutii sheria na amri za Mungu na hawa Waantinomia walilishambulia kanisa wakisingizia kuwa tendo lao la kuzitii zmri hizi ndicho chanzo cha malumbano na mapambano yao yanayowafikisha kwenye hali hii ya kuhitilafiana.

 

Aliwaambia kuwa wameahidiwa mapumziko mema atakaporudi Kristo na atawapatiliza kuwahukumu wale wote waliokuwa wakilitesa kanisa. Hukumu watakayopewa watu hao ni maangamizo ya milele na hawatakuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu. Mtu yeyote anayejaribu kuzidharau sheria na amri za Mungu na kuyafuata mafundisho haya ya Waantinomia anapaswa kujua kuwa hukumu yao ni hii:


9Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza Wake, 10siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu. 11Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili kwamba Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito Wake na kwamba kwa uwezo Wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu. 12Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani Yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.

 

Chanzo au sababu za Waantinomia kulitesa Kanisa la Mungu vimeelezewasana kwenye jarida la Jinsi Waantinomia Wanavyozipinga Sheria Na Amri za Mungu (Na. 164D) (Antinomian Attacks on the Law of God (No.  164D)] kwenye tovuti ya: http://www.ccg.org/english/s/p164d.html.

 

Kipindi Hadi Kuja Kwa Masihi

Kisha Paulo anaendelea mbele hadi kuelezea ukweli ulivyo wa jinsi Kurudi Tena kwa Masihi kutakavyokuwa. Akaema kwamba kutalazimika kwanza kuwepo kwa uasi mkuu na ukengeufu utakaloliandama Kanisa na vuguvugu la kuzipinga Sheria ambazo pia ni Amri za Mungu na kwamba hayo yatatokea kabla ya kuja kwa ile Siku yenyewe ya Bwana. Unaweza kujionea na kusoma habari hii kwenye jarida la Siku ya Bwana Na Siku za Mwisho (Na. 192) [The Day of the Lord and the Last Days (No. 192)] kwenye tovuti ya: http://www.ccg.org/english/s/p192.html.

 

2Wathesalonike 2:1-17

1Ndugu, kuhusu kuja Kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele Zake, tunawasihi, 2msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.

Kwa hiyo, kulikuwa hakuna sababu ya kuweko waraka mwingine wowote au neno vya kusema kuwa Bwana ameisharudi.

 

3Mtu ye yote na asiwadanganye kwa namna yo yote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa. 4Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.

Maasi Makuu lazima yaje kwanza ambayo ni maasi dhidi ya amri na sheria za Mungu, maasi yatakayoanzishwa na kuendelezwa na huyu mwana wa ukengeufu ambaye anafunuliwa kwa sasa. Neno hili “ukengeufu” kwa lugha ya Kiyunani linaitwa “Apostasia” au Ukengeufu Mkuu ambao maana yake ni kuondokana au kuachana kabisa na chembe yoyote ya ukweli wa Kiimani. Na imani hii waliyoachana nayo wao ni ile ya kuzitii sheria na amri za Mungu. Ndiyo! Mwana huyu wa ukengeufu ndiye huyu Mwana wa uharibifu, jambo ambalo ni tendo la kuziasi Sheria za Mungu (1Yohana 3:4). Dhambi maana yake ni uasi, neno ambalo kwa Kiyunani linaitwa anomias ambalo maana yake ni mtu aishie bila kutiisheria. Wale wote wayafuatayo mafundisho haya yanayosema kuwa sheria za Mungu hazina kazi kwetu leo na zilikoma wako kwenye kundi hili la waanomia, yaani ni watu wanaoishi bila kutii sheria au waantinomia ambayo maana yake ni wapinga sheria. Ni walewale na ni kitu kile kile. Wamekuwa ni wapinzani na wenye kulidharau Kanisa la kweli la Mungu kutoka siku za nyuma karne ya kwanza. Tumewaona wakiendelea na kuzidi kuongezeka miaka hadi miaka. Ukengeufu huu umetokana na Waingereza wa mrengo huu wa Kiantinomia na dini yao ya kumwabudu mungu Attis au Adonias, au Osiris au Mithras au Baali na alijulikana na kuabudiwa kwa kutumia majina ya namna mbalimbali lakini ni yeye huyu ndiye aliyekuwa akiabudiwa. Ikafikia mahala pa kwamba hata Makanisa ya Mungu katika mataifa ya magharibi yamepotoka na kujiingiza kwenye imani ya Miungu miwili au mitatu, yaani Ubinitaria au Utrinitaria ambayo ni imani ya hawa Waantinomia na kwa kuamini kwao hivyo wamejiondolea stahili yao ya kuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu lakini wanadhani kuwa wako sahihi kwa kuamini kwao hivyo.

 

Kwenye zama mpya ya vuguvugu hili la nguvu za upotevu na Ukengeufu kulianza na harakati potofu za kile kilichoitwa Mageuzi na Matengenezo ya makanisa, harakati zilizoendelea hata kwenye Makanisa ya Mungu yaliyokuwa yanateswa na Mfumo wa dini ya Kirumi. Wakafanyika kuwa ni wapinga mfumo ule lakini wakigeuka na kushiriki kikamilifu kulifanyia ubaya na kulitesa Kanisa la Mungu hali waliyoendelea nayo kwa karne kadhaa sasa.

 

Makanisa haya yaliendelea kasi yake zaidi hasa wakiulinganisha mfumo wao na ule wa Makanisa ya Mungu yalivyokuwa kipindi cha zama ya Wasardi baada ya kipindi hiki cha Matengenezo. Mfumo wa kwanza ulishuhudia makanisa yakiangukia kwenye Ukengeufu pia. Hawa walikuwa ni Wanafunzi walojaribu kuisoma Biblia na kuyachunguza maandiko ambao hatimaye walikujajiita kuwa ni Mashahidi wa Yehova. Watu hawa walitangaza kuwa sheria za Mungu zimekoma na kupita wakati wake na kupinga kabisa umuhimu wa kuzitunza Sabato na kuwa ni siku ya Kuabudu na wakajiondoa kabisa kushirikiana na Makanisa ya Mungu ni hali kama hiyohiyo ndiyo ililikumba Kanisa la Mungu (La Sabato ya Siku ya Saba) [Church of God (Seventh Day)]. Wakati kanisa la Waadventista wa Kisabato (SDA) walipojiengua kwenye Kanisa hili la [COG (SD)] na kuachana na sheria nyingine za Mungu na wakashikilia utunzaji wa Sabato ya juma tu na kuacha kuzizingatia amri nyingine zilizoorodheshwa kwenye Amri ya Nne na hatimaye wakajiunga na mafundisho ya Utatu kwa uoande wa Magharibi mwaka 1978 na kasha wakatokomea na kuingia zaidi barani Afrika 2003-5.

 

Hata Herbert Armstrong akiwa na kanisa lake la RCG/WCG alianza kwa kufuata mfumo huu wa Ukengeufu na kulipotosha Kanisa la Mungu kwa kiasi kikubwa sana wakati alipoifuata Kalenda potofu ya Hillel yenye kufuata mtazamo na mzunguko wa Kibabeloni na wenye mahirisho wa zama za kabla ya ujenzi wa Hekalu. Akafundisha mafundisho yenye mwelekeo wa Kiditheism, yaani imani inayoamini uungu wa miungu miwili na hatimaye imani hii ya Kiditheism ilizaa mafundisho ya kuamini Miungu Miwili yaani Ubinitaria na akayakumbatia na kuyaridhia pia mafundisho ya Utatu yaani Utrinitaria. Hatimaye akawa ni Mcuungaji mwabudu sanamu na akalipeleka Kanisa la Mungu kwenye ukengeufu wa hali ya juu sana kiasi cha kufikia kutangaza kuwa Sheria na Amri za Mungu hazihitajiki tena na sio muhimu na akaikubali na kuiridhia imani ya Utatu kuwa ni imani rasmi ya kanisa na kurithia vile isemavyo kwamba Mungu ni wa utatu maka wasemavyo wakengufu wote wengine.

 

Kufikia kwenye kiwango hiki cha kufundisha ukengeufu huu ndipo alikufa majuma 40 baadae, kwa siku na saa ileile aliyokuwa anafundisha hivyo kwa mujibu wa wale walio fuatilia siku na saa aliyokuwa akihubiri ujumbe huu na alivyokufa kwa maumivu makali. Makanisa yakaanza kuwa na mfumo wa makanisa ya Wasardi na Walaodikia na yameliharibu Kanisa la Mungu uoende wa Magharibi.

 

Hadi leo makanisa yanafundisha mafundisho haya Mapotofu ya imani hii ya Kibinitaria na Kitrinitaria na yanaifuata Kalenda potofu ya Hillel na wendine hata wameshindwa kujua ni kalenda gani waifuate kwenye mambo fulanifulani. Ukengeufu huu utaendelea tangu sasa hadi kipindi kile cha mashahidi na hatimaye kurudi kwa Masihi. Ni makanisa haya mawili tu miongoni yale saba ndiyo yatashuhudia watu wachache watakaoingia kwenye ule Ufufuo wa Kwanza. Hebu na tujionee aya hizi hapa chini na tujionee jinsi zinavyoelezea jinsi mfumo wa dini ya uwongo ya Mwanamke Kahaba na watoto wake makahaba watakavyoshirikiana na kuwa kitu kimoja katika siku za.

 

Paulo anaelezea jinsi ile siri ya kuasi ilivyokuwa imekwishaanza kufanya kazi katika siku zake. 

 

2Wathesalonike 2 inaendelea kusema:

5Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya? 6Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili kwamba apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia. 7Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa. 8Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa Chake na kumwangamiza kabisa kwa ufunuo wa kuja Kwake. 9Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo 10na kila aina ya udanganyifu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.

 

Kumbuka kuwa siri hii ilikuwa imefichwa lakini hatimaye iliruhusiwa ifunuliwe. Nguvu za imani hii ya Waantinomia inatoka kwa Shetani mwenyewe. Ujio wa mwisho wa huyu Mtu wa kuasi na Mwana wa Ukengeufu pia utawezeshwa na nguvu za Shetani na imani hii inaweza kujulikana kwa urahisi kwa tabia na mafundisho yake ya kuzikataa Sheria na Amri za Mungu.  Imani na mfumo huu vitaendelea miongoni mwa Wakristo na kama itawezekana utawapoteza yamkini hata wateule (Mathayo 24:24; Marko 13:22). Kuna sababu zitakazopelekea Makanisa ya Mungu yabughudhiwe na kutekwa na ukengeufu huu na ndipo Makanisa ya Mungu yatajikuta yameangukia kwenye ukengeufu huu. Watazikana nguvu za Mungu na ukweli kuhusu Mungu na kuamua kuwa wana Utatu au Mabinitaria na ndipo wote watakapokuwa ni Waantinomia.

 

Nguvu za Upotevu

Je, itawezaje kuwa rahisi kwa Makanisa ya Mungu na Ulimwengu wote wa Kikristo kuingia kwenye mtego huu wa kudanganywa? Na itawezekanaje kwa wana Yuda waende sambamba na uongo huu wa Waantinomia? Na je, itawezekanaje basi imani hii ya wana Utatu kuchanganika na ile ya Yuda au ya Kiyahudi? Jibu ni hili:


11Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo 12na hivyo wote wahukumiwe ambao hawakuamini ule ukweli bali wamefurahia uovu.

 

Dhambi ni ile tendo la kuziasi Amri na Sheria za Mungu. Haki na Utauwa ni ni kitu kimoja, yaani ni utii kwa amri za Mungu. Hali ya kukosa kutenda haki ni dhambi na zinajulikana kwa kigezo cha kupima kwenye Amri za Mungu.

 
13Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho na kwa kuiamini katika kweli. 14Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili kwamba mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo. 15Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.

Kwa hiyo, kwa kupitia Roho wake Mungu aliwachagua wale ambao aliwakusudia tangu mwanzo na kwamba kamwe hawatapotezwa na Ukengeufu huu wa hawa wa Antinomia

 

16Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema Yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, 17awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.

 

Kwa hiyo, hi kwa ajili tu ya faraja ya milele ambayo Mungu ametupatia kwa neema yake tu kwa Bwana wetu Yesu Kristo ambayo inatufariji mioyo yetu na kutuwezesha kufanya kila tendo jema na neno, ambayo ni matendo ya wateule kwa kuzifuata na kuzishika Sheria na Amri za Mungu na Ushuhuda wa Yesu Kristo.

 

Kisha anamalizia waraka wake kwa kunapaswa kukaza mwendo na kuendelea mbele na kushinda ili tuokolewe na watu waovu ambao hawajapewa imani hii ambayo wamepewa watakatifu mara moja tu.

 

2Wathesalonike 3:1-18 insema:

1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili kwamba Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwa upande wenu. 2Ombeni pia ili kwamba tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si kila mmoja ana imani. 3Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu. 4Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza. 5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.

 

Kwa hiyo, sisi tuko kwenye maongozi ya kanisa yanayotuwezesha Kumpenda Mungu na kusimama imara kwa Kristo.

 

Kumbuka pia kwamba uzembe ulikuwa ni sababu kuu katika kuwaathiri watu wasio imara kwenye imani. Mtume Paulo anasema:

 

6Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa. 7Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi, 8wala hatukula chakula cha mtu ye yote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu ye yote miongoni mwenu. 9Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, lakini ili kusudi tujifanye sisi wenyewe kuwa kielelezo.” 10Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri ili kwamba: ‘‘Mtu ye yote asiyetaka kufanya kazi, wala asile.’’ 11Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine. 12Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwaonya katika Jina la Bwana Yesu Kristo wafanye kazi kwa utulivu na kujipatia mahitaji ya maisha yao wao wenyewe.

 

Watu hawa walikuwa pia walitokana na ndugu wale waliopata nasaha kuwa wasiogope na kuacha kutenda mema. Kusema kweli, watu hawa wanaoendekeza uvivu ni tatizo na ni mzigo kwa wapendwa wengine.


13Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.

Taratibu za kanisa ni vema ziheshimiwe na wale wasiozitii wanapaswa kukemewa na kuonywa.

 

14Ikiwa mtu ye yote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili kwamba apate kuona aibu. 15Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu. 16Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote. 17Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo. 18Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.

 

Tunajua kuwa andiko hili liko wazi na kwamba kiini cha maneno ya andiko hili kipo kwenye sura ya 2 kama ifuatavyo.

 

Ni jambo lililowazi sana kuwa kuanza kazi kwa huyu Mtu wa Kuasi au Ukengeufu vitaanza kabla ya kurudi kwa Kristo na fundisho hili lilikuwepo kwenye kanisa la Mitume kipindi kile ambacho mitume walikuwepo. Ilimlazimu Mtume Paulo ashughulikie kuyakemea mafundisho yale ya uwongo na tunaweza kuhutimisha jambo hili na kujua lile alilokuwa akifundisha Mtume Paulo katika kukemea mafundisho yale ya uwongo. Jambo hili limeelezewa kwenye jarida la Mafundiko ya Uwongo Kwenye Kanisa la Mitume (Na. 089) [Heresy in the Apostolic Church (No. 089)] kwenye tovuti ya: http://www.ccg.org/english/s/p089.html.

 

Alama au Mhuri utakaopigwa Kanisa na hawa Waantinomia katika Siku za Mwisho ulielezwa na Kristo. Aliutaja kuwa ni haya mafundisho na imani ya Kiantinomia.

 

Mathayo 24:9-10 insema:

9“Ndipo mtasalitiwa, ili mteswe na kuuawa, nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa ajili yangu. 10Wakati huo, wengi wataacha imani yao, nao watasalitiana kila mmoja na mwenzake na kuchu  kiana.

Mathayo 24:11-12 inasema:
11Watatokea manabii wengi wa uongo, nao watawadanganya watu wengi. 12Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo wa watu wengi utapoa,

Tunapitia kwenye mateso na tunapaswa kusaidiana ili tusimame imara kwenye imani. Mkakati wa Ukengeufu unaendelea kushika kasi kwenye siku hizi za mwisho ukiwatumia wahubiri maarufu wa Kiantinomia. Na matokeo yake, upendo wa Mungu unazidi kupoa kwa wengi, hata kwa hawa wahubiri wa ueongo wenyewe. Hawana upendo halisi wa Kristo wanaodai kuwa nao.

 

Na kama tulivyosema hapo juu. Kristo alituonya sana kuhusu matatizo yanayolikumba Kanisa la Mungu leo.


Mathayo 24:24 inasema:
24Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo na kufanya ishara kubwa na miujiza mingi ili kuwapotosha, hata ikiwezekana wale wateule hasa.

Kwenye kipindi cha miongo kadhaa iliyopita Makanisa ya Mungu yalidanganyika hasa yale yaliyokuwa kwenye ukanda wa magharibi ya dunia kiasi kwamba hawa Waantinomia na wahubiri wa uwongo walijitokeza na kutapakaa miongoni mwao. Historia ya mafundisho yetu iko wazi na inaeleweka na wateule wote na hawawezi kudanganyika lakini wale walio katika nchi za Magharibi wamepotoshwa na kudanganyika vibaya sana na wataipoteza fursa yao kwenye ufalme wa Mungu wasotubu.

 

Uwongo wa Mwisho

Nguvu za Upotevu zinaendelea kutenda kazi katika siku hizi za mwisho, kwa uweza wote wa ishara na maajabu.

 

Sababu hizi ndizo zitakazopelekea Wakristo na mambo mengine yatakayosababisha hata Wayahusi wenyewe huenda wakadanganyika na kuacha kusimama imara kama alivyofanya Nabii Nuhu.

 

Ukengeufu huu umeishaanza kutenda kazi yake tayari na umekubalika kwenye mfumo wa kipapa ili kuweka dhana potofu ya kwamba Sabato ionekane kuwa ni sheria inayowahusu Wayahudi peke yao na kwamba haiwahusu Wakristo na pia kwamba Wayahudi watailazimisha kalenda ya Hillel na taratibu zake. Tendo la kuitunza Sabato za kweli, Miandamo ya Mwezi, na Sikukuu Takatifu zalizoamriwa na Kanisa la Mungu vitapigwa marufuku na kuzuiwa kabisa visifanyike. Wakati huo Wakristo watatambulika kwa kutii kwao amri ya kuabudu siku ya Jumapili na kwa kuzishika taratibu zake wakati kwamba Waislamu watakaosalia watapangiwa kuabudu siku ya Ijumaa ambayo ni jioni ya maandalizi ya ibada ambayo huitwa kimakosa Juma’ah ambayo ni kama Sabato ya Waislamu, wakati sio kweli kabisa na wala sio Sabato bali ni siku tu ya kufanya maandalio ya Sabato (soma jarida la Sabato Kwenye Qura’an (Na.274) [The Sabbath in Qur’an (No. 274)] kwenye tovuti ya:

 http://www.ccg.org/english/s/p274.html na la Siku Ya Juma’ah: Na Maandalio ya Sabato (Na. 285) [The Juma’ah: Preparing for the Sabbath (No. 285)] kwenye tovuti ya: http://www.ccg.org/english/s/p285.html.

 

Kwa hiyo, kwa kanuni zilizowekwa zinazojifanya kuonekana kama zinashabihiana na kuwezekana kuzitunza kwa mujibu wa sheria na amri za Mungu lakini zinazipinga nyingi zake na na kuizuia au kuinyima nafasi Sabato ya Mitume wa Kiyahudi, na ndipo nguvu kubwa ya upotevu itawaingia wengi na huyu Mtu wa Kuasi atajiimarisha kwa kusaidiwa na mafundisho potofu ya hawa Waantinomia na kusaidiwa na Wakristo Waliokengeuka na Wayahudi Waliokengeuka na kuasi.

 

Amri za Mungu

Amri aliyotoa Kristo ni kuvumilia hadi mwisho kwa uvumilivu wote na watatambulika kwa kuvumilia kwao utakaotokana na kuzitunza kwao amri za Mungu na imani ya ushuhuda wa Yesu Kristo. Walichoahidiwa ni kuwa na amri ya kuula mti wa uzima na kuingia kwenye Mji wa Mungu.


Mathayo 24:13 inasema:
13Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ndiye atakayeokoka.

Ufunuo 14:12 inasema:
12Hapa ndipo penye subira na uvumilivu wa watakatifu, yaani, wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu kuwa waaminifu kwa Yesu.

Ufunuo 22:14 inasema:
14“Wamebarikiwa wale wafuao nguo zao, ili wapate haki ya kuuendea huo mti wa uzima na kuuingia huo mji kwa kupitia kwenye malango yake.


Amri ya Mungu inaendelea tangu mwanzo wake na ni asili yake na inatoa maana na kuelezea upenda wake ambao Masihi aliuonyesha kwetu. Mungu ni upendo. Na sio uchaguzi kati ya Amri za Mungu na upendo wa Wakristo. Ni kama Aaantinomia walivyojaribu kuzitenganisha Amri za Mungu kutoka kwenye Neema yake, lakini hawawezi kutenganisha Upendo wa Mungu wakaweka mbali na Amri zake. Amri za Mungu, Neema yake, na Upendo wake, vyote hivi hufanya kazi pamoja kwa nia njema itokanayo na uumbaji wake.


Mathayo 19:17 inasema:
17Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mimi mwema? Hakuna aliye mwema ila Mmoja tu, ndiye Mungu: Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”

 

Mtu wa Kuasi Kwa Mujibu wa Zaburi

Zaburi 9-15 ni sehemu iliyo kwenye kundi la Zaburi inayojiri kumwelezea “Mtu wa Dunia.”  Inafuatiwa na Zaburi 8 inayoishia na wazo-dhana ya kumtaja Mwana wa Wuasi: Aliyerudiwa.

 

Kitabu cha kwanza cha Zaburi hufananishwa na kitabu cha Mwanzo, 1-41.

Zaburi 1-8 inahusu Mwana na Mwana wa Adamu;

Zaburi 9-15 inahusu Mtu wa Dunia (Mpingakristo 10:18);

Zaburi 16-41 inahusu Mwanadamu Yesu Kristo.

Zaburi 9 inahusu Mtu wa Kuasi (Kwa Ujumla).

Zaburi 10 inahusu Mtu wa Dunia (Kwa ujumla wake).

 

Bullinger anaandika maoni yake kuihusu Zaburi hii ya 9 na 10 (ambayo kwa mujibu wa nakala ya Sptuagint ni sura moja tu). Ni zaburi yenye mshabihiano usio wa kawaida. Barua saba zimerukwa miongoni mwa mbili hizi. Alfabeti imevunjika na inaonekana visivyo kawaida kusomeka “kuhusiana na kipindi cha taabu na mateso.” Ni dhiki kuu inayoongelewa hapa. Somo moja limeenea kote.

 

Kipindi cha Mateso na Dhiki kimeelezwa katika sura na aya ya 9:9 kama kilivyotajwa kwenye Mathayo 24, Yeremia 30 na Zaburi 10:1 na inaonekana kwamba mwana huyu wa uharibifu atakuwa na sehemu yake pia katika kipindi hiki. Zaburi ya 9 na 10 zimewekwa kwa kanuni ya kiuandishi wa pamoja, na kila beti ya pili huanza kwa herufi iliyoimgizwa ya pekee ya alfabeti ya Kiebrania, mazingira yanayosaidia kuhesabia upungufu utokanao na kile kinachoonekana kuwa ni mwendelezo sanifu. Hata hivyo jambo hili linahitaji kulifanyia juhudi ya makusudi ya kulisoma ili kulijua jinsi lilivyo na kujua uhusiano wwke ulivyo na huyu mtu wa kuasi. Inaonekana kwamba mfumo wake umeungamanishwa pamoja kwenye mlolongo wote ulio kwenye taratibu za kishetani na ndipo huyu Mtu wa Kuasi atakapopewa uweza na Mpingakristo.

 

Zaburi 9:3-10 inaelezea jinsi uovu utakavyokomeshwa. Mlolongo wake utakuwa ni kukomeshwa kwake, hukumu na kusomewa kwake tena hukumu, na kukombolewa tena.

 

Mtu huyu wa Kuasi ameandikwa kwenye Zaburi ya 9:5, 16 na 10:2, 4, 13, 15 na kwa mujibu wa neno la Kiebrania lililoko kwenye kitabu cha fafanuzi cha SHD 7563 linaitwa “rasha” ambalo maana yake ni uovu au uhalifu kama inavyoweza pia kumaanisha ifuatavyo:

 

a) mwenye hatia, mwenye hatia ya uhalifu (mwalifu)

 

b) mwovu (mwenye kumchukia Mungu)

 

c) uovu, hatia ya dhambi (kumtenda Mungu au Mwanadamu) kwa mujibu wa kitabu cha fasihi namba 7561 neno linaonyesha kuwa mwovu, kufanya matendo maovu

 

a) kupenda ugomvi (Qal)

 

1) kuwa mwovu, kufanya matendo maovu

 

2) kukutwa na hatia, kulaumiwa

 

b) kujikunyata kwa aibu (Hiphil)

 

1) kuhukumiwa kwa hatia iliyofanyika (kwenye mahusiano ya kijamii)

 

2) kushitakiwa kama mkosaji (kwenye mahusiano ya kimaadili kwenye jamii)

 

3) kutenda maovu kinyume na maadili ya kidini)

 

Kwa maneno mengine ni kwamba, kuziasi amri na sheria za Mungu ni kufuata ikikadi za Mpingakristo na tendo hili amelielezea sana mwandishi Bullinger kwenye kitabu chake (amelinganisha kutokana na Biblia, kitabu hiki cha zaburi sura ya 9:5).

 

Unaposoma kitabu chake, utaona kwamba amemtaja huyu mtu wa kuasi akilinganisha na aya za zaburi sura ya 9:6, 15. Ni muhimu sana kujua kuwa aya ya 15 inaelezea jinsi wamataifa watakavyozama kwenye shimo walilojichimbia wenyewe. Kwenye aya ya 16 mtu huyu aitwaye mwana wa kuasi atakuwa ni miongoni mwa watakaozama kwenye shimo hili walilojichimbiaa. Maneno yanayotamkwa kama Haggaion na Selah yameongezwa kwenye aya hizi, ambayo maana yake ni kuandaa matokeo yanayoashiria kuipa uweza hii Shelah ilazimishe na kuendeleza. Maelezo ya wingi yaliyo kwenye aya ya 16 yanafuatiwa na maneno yenye kuashiria umoja yanayomtaja huyu mtu wa kuasi kwenye aya ya 17 ambavyo kwamba mtu huyu wa kuasi atakuwa pamoja na wafuasi wake wengi ambao watatokana na kunaswa kwenye mtego ambao ni shimo walilowachimbia wateule ambalo litawapelekea kuhukumiwa hatimaye.  

 

Kwa mujibu wa lugha ya Kiebrania, Zaburi 9:9 na 10:1 inasomeka ukitaja hii kama “Kipindi cha Taabu” au “Wanaoteswa” ililitumia neno Kitu kilichoharibuwa kwenye sura na aya ya 9:9 na 10:18.

 

Zaburi 10:15 inasema Vunja mkono wa mtu mwovu na mbaya, mwite atoe hesabu ya maovu yake ambayo yasingejulikana. na inahusiana pia na Wachungaji wanaovitumikia Vinyago waliotajwa kwenye Zekaria 11:17.

 

Wale ambao hawajamsahau Mungu na wamebakia wanyenyekevu wanakumbukwa.

 

Zaburi 11 ni Maombi yenyemwonekano sawia na Zaburi 9 na 10.

 

Zaburi 12 inahusu Ubatili wa Mwanadamu.

Aya hii inafananisha pia na maneno ya udanganyifu wa mwanadamu na ule wa mtu wa kuasi aliyeko hapa duniani dhidi ya wateule waliosafi wazishiko amri za Mungu ambazo ni kamilifu.

 

Zaburi 12:6 inasema kuwa maneno ya Bwana ni maneno safi kama ilivyo fedha iliyojaribiwa kwa kupitishwa kwenye tanuu la moto hapa duniani likatakaswa mar asaba. Utaratibu wa tarakimu ya saba kiroho unamaanisha utakaso wa kiroho na pia unaashiria ujumbe wa Mungu kupitia malaika saba wa makanisa saba na wa baragumu saba.

 

Zaburi 13 ni maombi yenyekufanana tena na Zaburi 9 na 10. Aya za 1-4 ni maombi, aya za 5-6 ni sifa kwa Mungu.

 

Zaburi 14 inahusu Ukengeufu wa Mwanadamu na Zaburi 15 inahusu Ukamilifu wa Mwanadamu.

 

Huu ni mfano mwingine wa huyu Mtu wa Kuasi au Mtu wa Ukengeufu; ambaye pia ni Mpingakristo na mfumo wake wa Kiantinomia na mtu mkamilifu atakayeshinda na na kujivunia kwa kujigamba kwa ajili ya mfumo ule wa ukengeufu au wa Kiantinomia. 

 

Mkakati wa Waantinomia unaotokana na Imani ya watu wa imani ya Wakanamungu maarufu kama Waatheist na kuelekea kwenye mtazamo wa Ukristo wa uwongo au imani bandia.

 

Zaburi 14 inasema Mpumbavu anasema moyoni mwake, ‘‘Hakuna Mungu.’’ Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa, hakuna atendaye mema. Neno maovu limetumiwa hapa likimmanisha hali ya watu kujiharibu kwa kuzivunja amri za Mungu, na kwamba hakuna mtu aliyesafi, hakuna hata mmoja. (imeongezwa kutoka kwenye sura ya LXX). 

 

Je, wanaofanya maovu wote hawajui kuwa wanafanya hivyo, au ni kweli kwamba hawajau kabisa kwamba wanakosea au hawazijui kabisa amri za Mungu?

 

Aya ya 6 inamaanisha kwamba watu hawa wamelidharau na kulipuuzia mashauri ya wale waliodhumuliwa ambao waliwadhulumu na kuwatesa. Kwa maneno mengine ni kwamba waliyapuuzia mashauri ya wateule na kuzidharau Amri za Mungu na kujiharibu wao wenyewe kwa kuwatesa wateule. 

 

Zaburi 14 inashughulika na hukumu ya walio kwenye kizazi cha wabezaji na waovu. Mjinga anayetajwa hapa sio wale wenye tabia za kupuuzia mambo tu au wasiojua mambo, bali ni wale ambao wamejiingiza kwenye atendo maovu kwa kiasi kikubwa mno na kupotoka matendo yao kimaadili (linganisha na 2Samweli 13:13; Mithali 10:23). Tangazo la kuwa Hakuna Mungu (lisemavyo kwenye Zaburi 10:4) si tangazo lisemwavyo kwa wazi na Wakanamungu hawa walioko leo, ila wanakataa kuwa Mungu atakuja kuaadhibu watu kwa mujibu wa amrizake (linganisha na Zaburi 10:11 na 94:7 na waweza pia kujisomea maandiko kutoka kwenye Biblia ya RSV iitwayo Oxford Annotated RSV. )

 

Andiko hili linatuonyesha kuwa Mungu anawarudisha waliopelekwa utumwani walio wake na kutoka uzao wa Israeli na Yuda ambao kwa pamoja watafurahia kuwa pamoja na kwa umoja.

 

Zaburi hii inaonekana kufanana na Zaburi ya 53 iliyolitaja neno Elohim mara tatu na Yehova mara nne hapa na jina la Elohimu limetajwa mara saba kwenye Zaburi 53) dika three Elohim and four Yahovah here) and   seven x   Elohim are used in ps. 53). Zaburi 53 ipo kwenye kitabu cha Kutoka na inamtaja pia Yakobo na Israeli. 

 

Zaburi 15 inaunda andiko lililotumika kwenye hotuba ya Mlimani (Mathayo sura 5 hadi 7). Inauhusiano na tangazo la Ufalme wa Mungu na sio Kanisa la Mungu. Bali ni ufalme wa Mlima Sayuni.

 

Mtu mkamilifu huzitii zmri za Mungu na hatazidharau.

 

Mambo yanayofuatia kutoka kwenye Zaburi 16 hadi 41 zinamtaja Yesu Kristo. Zaburi 16 inaelezea jinsi atakavyopokea sadaka zake. 

 

Huyu Mtu wa Kuasi ni Mpingakristo ambaye anajulikana wazi, na mfumo wake inajulikana, na dalili zao ni itikadi yao ya kuzikataa amri za Mungu na wameyaeneza mafundisho yao na kuwaharibu Wakristo na kudhoofisha maundisho ya kweli kwa kipindi cha karne nyingi sana hadi sasa. Lakini mwisho wao umefika. Hawa Waantinomia watakatiliwa mbali na kufutiliwa mbali na Masihi hapo atakapokuja.          

 

q