Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[300]

 

 

 

Yubile Kuu ya Dhahabu

Na Milenia

 

(Toleo La 1.0 20060923-20060923)

 

Yubile Kuu ya Dhahabu au Yubile ya Hamsini tangu Kujengwa tena kwa Hekalu kulikofanywa na mfalme Dario mnamo mwaka 423KK kazi iliyosimamiwa na kina Ezra na Nehemia kwenye Yubile ya mwaka 374/3KK itakayoanzia siku ya 1 mwezi wa Abibu ya mwaka wa Kwanza wa Yubile ya 121 au mwaka 2028. yubile itaishia mwaka 2027BK. Yubile hii inamaanisha mwanzo wa Milenia ya Saba tangu kufungwa kwa Bustani na Edeni na mwisho wa enzi ya utawala wa Shetani. Kwa tarehe hii ya mwaka 2027 utawla wa Shetani utakatiliwa mbali na kukomeshwa kabisa na atafungwa kifungoni pamoja na Malaika wengine waovu kwenye kifungo kijulikanacho cha Tartarus kwa kipindi cha miaka elfu moja. Kipindi hiki kitatanguliwa na kile cha Ufunguo wa Daudi na cha kujengwa upya kwa Hekalu na utaratibu wake wa kimaongozi mjini Yerusalemu.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hakimiliki ©  2006 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki..

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Yubile Kuu ya Dhahabu na Milenia

 


Utangulizi

Dhana kuhusu Ufunguo wa Daudi inahusiana na Mrejesho ya mfumo wa Hekalu. Kuna mambo mengi muhimu kufanywa kuihusu dhana hii ya Ufunguo wa Daudi na ambayo yamejaribiwa na kuorodheshwa kwenye jarida letu la Kanuni za Wafalme Sehemu ya III: Sulemani na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C) [Rule of the Kings Part III: Solomon and the Key of David (No. 282C)[, na kususan kwenye maeneo yale ambayo yameongezewa baadae.

 

Hesabu ya siku zilizotajwa kwenye unabii wa Danieli 9:25-27 ni kitu muhimu sana kwenye tatizo hili. Mwaka ambao tangazo lile la kuwaachilia huru liliolewa ulikuwa ni katika kipindi cha utawala wa Dario II ambao ni mwaka 423 KK. Huu ulikuwa ni mwaka wa Kwanza wa Yubile, na Yubile iliishia kwa Marejeo ya Ezra na Nehemia mwishoni mwa juma la saba la miaka na ni mwaka wa Usomaji wa Torati. Jambo hili limeelezwa vizuri kwenye majarida ya Usomaji wa Torati Ulivyofanywa na Ezra na Nehemia (Na. 250) [Reading the Law with Ezra and Nehemiah (No. 250)] na lingine la Uchambuzi wa Ratiba ya Zama Mbalimbali (Na. 272) [Outline Timetable of the Age (No.  272)].

 

Hatua zilizopitia katika ujenzi wa Hekalu zimeonyeshwa kwenye jarida la Ishara za Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)].

 

Siku ya 1 ya mwezi wa Abibu, mwaka 423/2 hadi siku ya 30 Adari mwaka 2077 ni jumla ya Yubile 50, au ni jumla ya miaka 2500 tangu mwaka wa kwanza wa Yubile ya 50. th Jubilee. Kwa hiyo kuanza kwa Yubile mwaka 2028 na kuishia kwake mwaka 2077 kunaifanya iwe ni Yubile ya Hamsini au Yubile ya Dhahabu yangu kuanza kwake mkakati wa kulijenga Hekalu kulikofanywa katika mwaka wa pili wa Dario Mwajemi, kama alivyoelezea Ezra kwenye sura ya 4.

 

Nabii Hagai anauongelea pia mwaka huu na ujenzi wa Hekalu (tazama jarida la Ufafanuzi Kuhusu Unabii wa Hagai (Na. 21) [Commentary on Haggai (No. 21)].

 

Hini ni jambo la muhimu sana kulijua kuhusu Ufunguo wa Daudi.

 

Ishara ya nabii Yona na juma la sabini la miaka liliishia kwenye sehemu yake ya kwanza la kuhusuriwa au kuteketezwa kwa Hekalu kulikotokea mwaka 70BK wakati Warumi walipouzingira mji wa Yerusalemu na wakaliteketeza Hekalu. Hatimaye Vespasian akatoa amri kuamuru Hekalu lifungwe la Leontopolis, ambalo ndilo lilikuwa la mwisho lililokuwa linatolewa sadaka halisi za Wayahudi au Yuda ulimwenguni kote. Na kama vile Yona alivyotembea safari ya siku moja ndani ya mji wa Ninawi na kuhubiri kwa muda wa siku mbili, na ndivyo iliyotokea kwamba Yesu alibatizwa na Yohana Mbatizaji, na kufuatiwa na kifo cha Yohana kilichotokea baada ya Pasaka ya mwaka 28BK katika mwaka wa Kwanza wa Yubile, Kristo alihubiri kwa miaka miwili na kisha akauawa ili awakomboe wanadamu kutokana na dhambi zao.

 

Yuda (na Waedomu ambao walikuwa sasa wanasehemu kwenye ufalme wa Yuda) walipewa miaka arobaini ya kufanya toba, na Yuda hawakutubu. Kutoka siku ya 1 ya mwezi wa Abibu ya mwaka wa 70BK majeshi ya Warumi yaliuzunguka mji wa Yerusalemu, na kwenye kipinsi cha Pasaka ya mwaka huo wa 70BK, mkakati huu wa kuuzingira mji ulikamilika na maangamizi ya Yuda yalikamilika. Maangamizo haya pamoja na mtawanyiko wao yameelezewa kwenye jarida la Vita Vya Warumi na Kuteketezwa na Kuangushwa kwa Hekalu (Na. 298). [War with Rome and the Fall of the Temple (No. 298)]. 

 

Sehemu ya pili ya Ishara ya Yona ilikuwa ni kipindi cha Yubile Arobaini cha Kanisa kuwa Jangwani. Kipindi hiki kiliendelea tangu mwaka 28BK hadi mwaka 2027BK. Hiki ni kipindi cha Yubile ya 120 ambayo ni mwisho wa kipindi cha miaka elfu moja cha kutawala kwake Shetani tangu ilipofungwa bustani ya Edeni.  

 

Yubile hii ya 120 tangu mwaka 1978 hadi mwaka 2027 inapitia kwenye mlolongo wa matukio ya kushangaza na kusisimua. Yubile zilizopita kuanzaia mwaka wa 1928 hadi mwaka 1977 ilishuhudia Mauaji Makuu ya Kuwaangamiza Wayahudi na Vita Kuu ya II ya Dunia. Yubile iliyoitangulia kabla yake ya tangia mwaka 1877 hadi 1927, ilishuhudia Vita ya I ya Dunia na ndiyo ilikuwa ndiyo mwanzo wa kipindi cha mwanzo wa mchakato wa kufikia mwisho. Waweza kujisomea hayo kwenye jarida la Kuanguka kwa Misri: Unabii wa Mikono Iliovunjika ya Farao, (Na. 36) [The Fall of Egypt: the Prophecy of Pharaoh’s Broken Arms (No. 36)]. Mnamo mwaka 1916 ambao ni takriban miaka 2,520 tangu vita iitwayo ya Carchemish na ndiyo mwanzo wa utawala wa Nebukadneza, na ni miaka 80 ya kipindi hiki cha mwelekeo wa mwisho wa Utimilifu wa Mataifa kilichoanzia mwaka 1997. Mashambilizi ya Cambyses wa Misri yalifanyika mwaka 525KK na mwaka 1997 unafanyika kuwa ni Mzunguko wa Saba kwa mujibu wa kipindi cha mwisho cha mzunguko ule.

 

Mwaka 1948 tumejionea uanzishwaji tena wa taifa la Israeli na pia tumejionea vita ya kwanza ya Dunia. Mwaka 1967 tumeshuhudia mwanzo wa harakati za Kivita vya Mwisho ziliienga Israeli. Maana ya nyakati hizi na matukio yake ya machafuko yameelezewa kwenye majarida yafuatayo: Miaka Thelathini ya Mwisho: Pambano la Mwisho (Na. 219),[ The Last Thirty Years: the Final Struggle (No. 219)0; na zingine na Vita ya Hamon-Magogu (Na. 294) [War of Hamon-Gog (No. 294)]; na Maelezo-Fafanuzi ya Kitabu cha Zekaria (Na. 297) [Commentary on Zechariah (No. 297)]; na Vita Kuu ya III Ya Dunia: Sehemu ya 1 (Na. 299A) [World War III: Part 1 (No. 299A)] na Vita Kuu ya III ya Dunia Sehemu ya 2 (Na. 299B) [World War III: Part 2 (No. 299B)].

 

Vita vya siku za mwisho na ambavyo vitahusisha mgongano wa kuwagonganisha Israeli na Yuda ileshaanza mwaka wa 2001. Hii inajiri ili kuufanikisha mkakati wa kuanzisha Vita Kuu ya III ya Dunia, lakini mataifa nengi yanaonekana kuwa hayakulijua jambo hili kwa jinsi ilivyokuwa kwa wakati ule. Tarehe na mwanzo wa matukio vilitolewa tangu mwaka 1997 na waweza kujisomea kwenye jarida la Miaka Thelathini ya Mwisjo: Pambano la Mwisho, (Na. 219) [The Last Thirty Years: the Final Struggle (No. 219)] na hasa kama utapata na kusikiliza kwenye mkanda wetu wa kaseti. Jarida lile linaelezea mlolongo wa kipindi cha miaka thelathini ya mwisho ya zama hizi, ambayo imetajwa kuwa ni cha Manung’uniko cha wakati wa Musa. Kipindi hicho ni kile cha tangia mwaka 1997 hadi 2027.

 

Kipindi cha kuanzia mwaka wa 1967 hadi 1997 kilikuwa kilichofananishwa na kile kipindi cha Manung’uniko ya Haruni, kilichotokea katika siku za mwisho za miaka ile arobaini ya Waisraeli kuwa kwao jangwani. Kipindi kile kilihusu na ukuhani wa Mungu.

 

Kipindi cha kutoka mwaka 1987 hadi 2027 kinafanya na kukamilisha kipindi kinachoitwa cha Kupimwa kwa Hekalu. Tangu kipindi cha Upatanisho cha mwaka 1967 ilikuwa ni miaka arobaini cha mwisho cha neema kwa Makanisa. Kipindi cha mzunguko wa miaka 19 cha tangia mwaka 1967 hadi 1986 kilikuwa ni cha mwisho na ambacho kwamba mchungaji mwenye kuvitumikia sanamu alipewa utawala huru, na pia ndicho Mungu alianza kipindi chake cha hukumu kuifanya kwenye Nyumba ya Mungu, ambacho kinayahusisha Makanisa ya Mungu (soma majarida yafuatayo:Kupimwa Kwa Hekalu (Na. 137) [Measuring the Temple (No. 137)] na Mabashiri ya Uwongo (Na. 269) [False Prophecy (No. 269)].

 

Mlolongo huu wa ratiba uliwekwa kwa kulihusisha taifa lenyewe la kimwili la Israeli, sawa na kama Kanisa lilivyo kuwa ni taifa la kiroho la la Israeli. Wataletwa pamoja kipindi hiki na watautamalaki mji wa Yerusalemu kwenye kipindi cha kungojea Ujio wa Masihi.

 

Tengo la Kutakasa Mataifa lilianza mwaka 2006, ambao ulikuwa ni mwaka wa ishirini na moja wa kipindi-zama. Kilianza tangia siku ishirini na moja za kwanza za mwezi wa Abibu na Tishri (Ethanimu), ukihusisha miezi ya Kwanza na Saba (soma jarida la Kutakaswa kwa mataifa (Na. 77) [Sanctification of the Nations (No. 77)]. 

 

Mwaka 2012 ni kipindi kingine chenye umuhimu wake fulani kwa mujibu wa mambo yote mawili, yaani kwa ratiba ya kalenda ya kibiblia na pia kwa ratiba zilizo kwenye mfumo wa kalenda iliyo kwenye dinii za kipagani. Ni kipindi cha miaka arobaini sasa cha kuanzia pale Kanisa lilipopewa ujumbe wa maonyo kulitaka limrudie Mungu kwa kutubu kazi iliyoanza rasmi yangu mwaka 1972, na ni kipindi cha miaka arobaini kamili tangu watu wa Mungu walipochomwa na kuuawa kwenye Baraza la Mahakama yaKidini ya Uingereza (soma jarida la Miaka Arobaini ya Toba (Na. 290) [Forty Years for Repentance (No. 290)] na Mahakama ya Kidini ya Uingereza: Miongo Arobaini ya Toba (Na. 290B) [The Inquisition in Britain: Forty Decades for Repentance (290B)].

 

Kalenda ya dini ya Inca na Mayan zinaishia kwenye kipindi hiki cha miaka mitakatifu cha 2012 na 2013.

 

Kipindi cha kuanzia mwaka 1607 hadi 2007 ni cha miongo arobaini cha tangia kuanzishwa mkakati wa kuongeza watu wanaoongea lugha ya Kiingereza kwenye makoloni yao, mkakati ulianzia mwaka 1607 kwa uanzishwaji kwa mji maarufu wa Jamestown huko Marekani.

 

Mark Canada, ambaye ni profesa wa Chuo Kikuu kimoja kilichoko huko Karolina Kusini (North Carolina) kwenye mji wa Pembroke anaandika akisema:

Taifa la Marekani kwa kweli lilianzia na maeneo mawili tu tofauti na kwa malengo mawili tofauti. Mnamo mwaka 1607, watu takriban 100 na vijana walisafiri kwa njia ya bahari kutoka Uningereza wakatiananga mahali paitwapo leo Virginia na kuanzisha mji wa Jamestown. Wakivutiwa na kuhamasika na mafanikio ya wapelelezi na wagunduzi wa Kihispania ambao waliikuta dhahabu nyingi kwenye ukanda wa Amerika ya Kusini wasafiri hawa wenye moyo mkuu walitumaini kuwa watakuwa matajiri. Lakini badala ya kupata dhahabu walioitarajia, walikutana na mazingira hatari ambayo huenda yangeweza kuliangamiza kundi lao, lakini kwa msaada mkubwa wa Kapteni John Smith, ambaye alimudu kuwakusanya na kuwatiaahamasa malowezi ambao waliwaokoa wasife kwa njaa. Mnamo mwaka 1620, kundi la watu kutoka Uingereza, waume kwa wake walikuja Marekani wakiwa na shughuli za aina mbalimbali. Watu hawa walitumwa na Kanisa la Uingereza, ambao walidhani kuwa wangefanana kabisa na Kanisa la Kikatoliki, watu hawa waoenda Mafarakano wenye kujihesabia Haki zaidi walitafuta jinsi ya kuanzisha kanisa la Wenyeji asilia nchini Marekani. Mkakati huu uliongozwa na William Bradford, Wasafiri hawa walifika huko Massachusetts siku ijulikanayo kama siku ya kupeana zawadi kwa meli ijulikanayo wa jina la Mayflower.

Watu hawa hawakuwa Wenyeji asilia bali walikuwa ni Mababa Wasafiri. Walikuwa ni Wasabato waliojulikana kama Wtu wa rangi ya Kahawia (Brownists), baada ya kiongozi aliyekuwa pia ni mwalimu wa chuo maarufu cha Kanisa la St. Olave huko Surrey. Na ambao  walikimbilia Uholanzi kwa usalama wao miaka kadhaa kabla yake (soma jarida ya Uhusiano Kati ya Waholanzi na Mababa Wasafiri (Na. 264) [The Dutch Connection of the Pilgrim Fathers  (No. 264)]. Wenyeji hawa asilia waliowafuata hatimaye waliwageuka na kuwatesa walipokuwa wanakuja.

 

Profesa Canada anaendelea kwa kusema:

Miaka kumi baadae, John Winthrop aliyaongoza makundi mbalimbali ya Wenyeji hawa asilia na kwendanao maeneo mengine mengi, na ni kipindi hiki ndipo alikuwa na mpango wa kuweka mfano wa kanisa la kwao Uingereza. Na zaidi ya karne iliyofuatia au zaidi, Virginia na Kundi la Pwani ya Massachusetts waliungamanishwa pamoja na makoloni yao mengine, ikiwemo Pennsylvania, ukikaliwa kwa kiasi kikubwa na wafuasi wa imani kali ya kidini waitwao Quakers waliokimbia ili kujinusuru na mateso kutoka Uingereza, Connecticut, kilichoanzishwa na mtu aliyekimbiyeyakimbia mateso ya Wenyeji asilia wa Massachusetts; Maryland, ambao mfalme wa Uingereza alimpa Mkatoliki Mwingereza aitwaye Lord Baltimore; na Georgia, ambayo ilianzishwa na wadaiwa wa Uingereza. [Wasabato hawa walikimbilia kwenye Visiwa vya Rhode]. Kwenye miaka ya 1760, Uingereza pamoja na makoloni yake 13 yaliyoko Marekani walikuwa na mzozo wa kugombea makazi, utawala na kodi hasa ile inayotokana na Sheria ya Bunge ya Ushuru ya mwaka 1765. Hatimaye, mnamo mwaka 1775, mikwaruzano na mabishano yalitokea huko Lexington na Concord, Massachusetts. Mwaka 1776, Thomas Paine aliyakielezea kipindi hiki cha ukoloni kwenye jaarida lake liitwalo Maarifa ya Kawaida, na Thomas Jefferson alitoa tamko au Tangazo Maalumu la Uhuru. Zaidi ya kipindi cha miaka mingine mitano, Jemadari George Washington aliwaongoza Wamarekani kupambana na Waingereza. Na mnamo mwaka 1781, takriban askari 8,000 wa Kiingereza walisalimu amri huko Yorktown, Virginia waliwa na maumivu makubwa sana yaliyotokana na vita hivyo vilivyopelekea Waingereza kukubali kuyaachilia makoloni yake. Uingereza iliutambua rasmi uhuru wa Marekani kwenye Mkataba wa Paris ulioitishwa na Benjamin Franklin na wenzake wengine mwaka 1783. (kwa mujibu wa jarida la Colonial America 1607-1783, 1999): kwenye tovuti ya:

http://www.uncp.edu/home/canada/work/allam/16071783/history/history.htm

 

Australia ilianzishwa kwa kuwa Uingereza haikuweza tena kusafirisha nje watu waliopenda au waathiriwa kutoka kwenye jamii za wasiojiweza wa Marekani.

 

Watu wanaotoka kwenye jamii ya wanaoongea Kiingereza walipewa kazi ya kukusanya maeneo yenye makosa kwenye kuabudu yaliyoko kwenye mfumo wa Wanautatu, na ilianzishwa kwa kusudi hili kati ya idadi kubwa ya mataifa ili kuchukua urithi ulioahidiwa kwa Ibrahimu kwenye Agano lake na Mungu. Lakini wameshindwa kuifanya kazi.

 

Kipindi cha miaka ya 1607 hadi 2007 kinakamilisha miongo 40 iliyofuatia mchakato huu. Kipindi cha Taabu yake Yakobo kiko mwishoni mwa mchakato huu.

 

Mnamo mwaka 1619 watumwa kutoka Afrika walianza kuingia nchini Marekani. Mataifa yalikuwa yanaingizwa kwenye mfumo wa utumwa. Mwaka 2019 watoto wao, wakiwa na Kristo, watasaidia katika mwanzo wa utumwa utakaoyapata mataifa yote. Chini ya mamlaka ya Kristo, Kanisa lita “wachukua watumwa utumwani” na kuuweka huru ulimwengu wote mbali na mzingo za dhambi na dini ya.

 

Kuanzishwa kwa Kanisa la Sabato nchini Marekani mwaka 1620 kunaishia na kuanzishwa kwa mfumo wenye msingi wa kudumu katika mwaka wa 2020 kutoka Yerusalemu. Mwaka 2019/2020 utaanzisha utiifu wa mataifa yote watakaochungwa kwa Fimbo ya Chuma litakayopewa Kanisa na Masihi.

 

Hiki ni kipindi kilichotabiriwa na nabii Malaki kama ifuatavyo:

Malaki 4:1-6 ‘‘Hakika siku inakuja, itawaka kama tanuru. Wote wenye kiburi na kila mtenda mabaya watakuwa mabua makavu na siku ile inayokuja itawawasha moto,’’ asema BWANA Mwenye Nguvu. “Hakuna mzizi wala tawi litakalosalia kwao. 2Bali kwenu ninyi mnaoliheshimu jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake. Nanyi mtatoka nje na kurukaruka kama ndama aliyeachiwa kutoka zizini. 3Kisha ninyi mtawakanyaga waovu nao watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayofanya mambo haya,” asema BWANA Mwenye Nguvu. 4“Kumbukeni sheria ya mtumishi wangu Mose, amri na sheria nilizompa huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote. 5“Tazama, nitawapelekea nabii Elia kabla ya kuja siku ile iliyo kuu na ya kutisha ya BWANA. 6Ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, la sivyo nitakuja na kuipiga nchi kwa laana.’’

 

Dunia inaonywa lakini bado laotaki kusikia wala kujali.

 

Wateule ni wale wanaozishika Amri za Mungu na Ushuhuda na Imani ya Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12).

 

Nabii Eliya anayaonya mataifa kabla hawajatiishwa (tazama jarida la Mashahidi (Na. 133) [The Witnesses (No. 135)].

 

Kipindi cha kuanzia mwezi wa Abibu ya mwaka 2012 hadi Sikukuu ya Vibanda ya mwaka 2015 kinahitimisha jumla ya siku 1260 za kujaribiwa kwake dunia.

 

Tangia mwaka 1972 hadi 1975 Kanisa lilipewa siku 1260 za kushughulikia matatizo yake na kutafakari unabii, na jinsi lilishindwa kuifanya kazi yake kwa kutoa kwake unabii wa uwongo. Kipindi cha miaka ya 2012 hadi 2015 kinatimiliza mwisho wa miaka Arobaini ililopewa Kanisa ili kutubu.

 

Kipindi hiki dunia itakuwa kwenye uharibifu na maangamizo makubwa sana na itahitaji mbingu tu ziingilie kati kunusuru hali hii.

 

Mwaka 2019 tutamwona Masihi. Tangia mwaka wa 2019 hadi 2027 sayari hii itashushwa magotini na kuwa chini ya milki ya Masihi na itamtii. Mchakato huu umeelezwa kwenye majarida yafuatayo: Vita Kuu Ya II Ya Dunia: Sehemu ya 1 (Na. 299A) [World War III: Part 1 (No. 299A)]; Vita Kuu Ya III Ya Dunia: Sehemu ya 2 (Na. 299B) [World War III: Part 2 (No. 299B)] na Kuanguka Kwa Yeriko (Na. 142) [The Fall of Jericho (No. 142)]).

 

Tangu Siku ya Upatanisho ya mwaka 2027, dunia itakuwa kwenye kipindi cha urithi wa utawala wa Milenia kwa mataifa yote.

 

Tendo hili ndilo linalotangulia na kuanzishwa kwa kipindi cha Yubile ya Dhahabu, au Yubile ya Yubile nyingi.

 

Dunia Katika Mwaka 2027

Baada ya miaka ishirini na tano ya vita ni nini tunachokitarajia kutokea duniani? Au tunaweza kudhania tutakuwa na dunia ya namna gani?

 

Sayari hii itakuwa kwenye kwenye Kipindi cha Ajabu cha Joto Kali Sana la Milenia (maarufu kama MilWP). Hali itakavyokuwa ni zaidi ya ile iliyowahi kutokea kwenye Kipindi cha Joto cha Zama Kati (maarufu kama MWP).

 

Kina cha Bahari kitakuwa ni zaidi ya ile ya kwanza ya kina cha futi saba kilivyokuwa kwenye kipindi cha Zama Kati.

 

Kuangamia kwa hii sayari kutachukua kipindi cha zaidi ya miaka 25 na athari zake zitaendelea hadi kwenye Yubile ile.

 

Bahari zote zitakufa. Ardhi itaharibika na idadi ya watu itapungua kiasi cha asilimia kumi ya wakazi wake ikilinganishwa na ilivyokuwa mwaka 2007.

 

Mchakato mrefu wa kukarabati na kuirejesha upya utakuwa umeanza.

 

Hakutakuweko na mafundisho yajulikanayo leo kama Hadithi za Kiislamu, Marabi wa Kiyahudi, wala Ukristo wa imani ya Utatu. Wahubiri wao, maimamu, na marabi watakufa kwenye vita au watakuwa wameamini Imani ya kweli. Njinsi pekee bje ya vita hivi vya mwisho ni kupiga magoti yetu na kumlilia Mungu.

 

Mnamo mwaka 2026 na 2027 mataifa yatatuma wawakilishi wao mjini Yerusalemu kwa ajili ya mkutano muhimu sana kuliko yote katika historia ya dunia.

 

Wale wote ambao hawatakwenda huko ili kwenda Kuisoma Torati, mvua haitanyesha kwao kwa kipindi chote na watateseka kwa maafa ya tauni ya Wamisri. Umuhimu wa kuiheshimu na kuiamini Torati utarejeshwa na mshahara wa dhambi utakuwa ni kitu dhahiri utatolewa papo hapo.

 

Siku ya kumi ya mwezi wa Saba wa mwaka wa 49 wa Yubile ya 120, au siku ya Jumapili ya tarehe 20 Septemba, 2026, baada ya kipindi kirefu cha giza cha huko nyuma, mwaka wa Yubile utaanza.

 

Na ni kipindi hiki ndipo mataifa yatapangiliwa upya na kupewa urithi wake. Kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka wa Hamsini wa Yubile ya 120, Yubile hii itatangazwa, na katika siku ya 23 ya mwezi wa Saba, mara tu ikifuatiwa na Siku ya Mkutano wa Makiini mwishoni mwa Sikukuu ya Vibanda, marejesho ya ardhi yatafannyika. Watu wote watazirejea milki zao kwenye nchi zao.

 

Wataanza kulima na kupanda kwa mavuno ya kwanza kwenye mfumo wa milenia ya kwanza katika Pasaka ya mwaka 2028. Mavuno makuu ya ukanda wa Kusini mwa Dunia yatafanyia sawa kwa mujibu wa majira yake na hata mavuno yatakuwa hivyo hivyo. Ukanda wa Kaskazini mwa Dunia utakuwa.

 

Dunia itafanywa upya tangu mwaka 2028 hadi 2077. Katika kipindi hiki kutakuwa na mabadiliko ya mwonekano mzima wa kiwango cha ongezeko la watu duniani.

 

Tangia mwaka 2028 taratibu za Hekalu zitakuwa chini ya Ukuhani mpya wa Melkizedeki. Mahala pa ibada katika Yerusalemu utakuwa umeanzhishwa. Hili litakuwa ni Hekalu la Milenia na nadipo patakuwa ni mahali muhimu na pa pekee pa kufanyia ibada ulimwenguni kote.

 

Taratubu za Hekalu Jipya

Mataifa watapaswa kufikia hatua ya kutubu na kutakaswa. Mchakato huu utajiri miaka ishirini na moja hadi kwenye Yubile ya mwaka 2027. 

 

Hii itahusu taratibu zote za kikuhani wa kwenye sayari hii wakikusudia kumwelezea Mungu au Kristo.

 

Kitakachofuatia ni utakaso wa taratibu na mfumo wa Hekalu katika Yerusalemu chini ya kuhani mpya. Mchakato huu utahusisha utaratibu uleule ulio kwenye Ufunguo wa Daudi kama ulivyoelezewa siku za Daudi na Sulemani (tazama jarida la Utawala wa Wafalme Sehemu ya III: Sulemani na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C) [Rule of the Kings Part III: Solomon and the Key of David (No. 282C)]. Miaka arobaini tangu mwaka 1987 hadi 2027 inahusu maandalizi ya kuitiisha mataifa kama ilivyotokea kwenye kipindi  cha Daudi.

 

Kipindi cha pili cha miaka arobaini kwenye Yubile ya Dhahabu, cha tangu mwaka 2028 hadi 2068, kinahusu ujenzi wa Hekalu na matengenezo ya masuala ya uongozi mjini Yerusalemu tayari kwa ajili ya Usomaji wa Torati katika mwaka 2069, na katika mwaka 2076 na 2077 kwenye Yubile. Hekalu lenyewe litajengwa kabla ya ya kipindi hiki na hali hii ya kufanya upya na maongozi vitakoma katika siku hizo. Torati itasomwa katika kila mwaka wa Sabato katika kla siku ya Sabato katika kipindi chote cha miaka ishirini na moja cha kuanzia mwaka wa 2028, na kwenye miaka mingine ya 2034, 2041, na 2048 kwenye mchakato wa  utakaso (soma jarida la Kutakaswa Kwa Mataifa (Na. 77) [Sanctification of the Nations (No. 77)].  

 

Mwaka 2034 ni namna hiyohiyo kama ulivyo mwaka 2012 katika mchakato huu wa kutakaswa kwa mataifa. Sawa na inavyotakiwa kufanyika na kila mtu binafsi yake kwenye Kanisa la Mungu (soma jarida la Utakaso Kwa Ajili ya Dhambi Ndogo na Zilizofanywa Bila Kukusudia (Na. 291) [Sanctification of the Simple and Erroneous (No. 291)].

 

Tangu mwaka 2026 na kuendelea, Torati itasomwa kila Sabato na mwaka wake wa Sabato ulimwenguni kote sawa na ilivyoamriwa kwenye amri na sheria zake Mungu.

 

Hekalu litajengwa tena sawa na jinsi ilivyoagizwa kiroho na kimwonekano wake kwa jinsi ilivyoekelezwa na kuonekana kwenye unabii wa Ezekieli.

 

Kufanywa Upya Kwa Hii Dunia

Ni vigumu sana kukadiria jinsi uharibifu utakavyokuwa, na ni vigumu pia kukadiria au kupata taswira ya jinsi matengenezo yake mapya yatakavyokuwa.

 

Biblia inaeleza wazi sana kuhusu machafuko makubwa yatakavyokuwa yakiambatana na mauaji na maafa makuu yatakayoikumba dunia. Kristo amesema kuwa Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka (Yohana 10:34-35).

 

Lakini bado kuna vipindi kadhaa vya fursa walivyopewa wanadamu ili yatubie dhambi na makosa yao lakini hawataki kutubu. Mahala pengi hutoza faini kwa watu wanapokuwa wanavunja sheria. Matatizo haya yameelezewa vema kwenye jarida la Baragumu Saba (Na. 141) [The Seven Trumpets (No. 141)]. Matendo haya yanajiri kwenye kipindi kinachoitwa cha Vitasa Saba Vya Ghadhabu ya Mungu na hakuna hata kipindi kimojawapo miongoni mwake kinachoombwa kitokee.

 

Kipindi hiki cha Yubile ya Dhahabu ndipo dunia itafanywa upya, mito na maji yatafanywa upya pia, na dunia itakuwa ni mahali pa amani.

 

Kutakuweko na miti ya kupanda, maji ya kuyahifadhi na kuvunwa, na vyakula vitalimwa na wanyama wa kufuga watakuwepo.

 

Uponyaji ule ule utokao kwenye Mji wa Mungu utakaoanza tangu kurejeshwa huko Yerusalemu na Masihi, na ufufuo wa wateule

Ufunuo 22:2-4 inasema: 2kupitia katikati ya barabara kuu ya huo mji. Kwenye kila upande wa huo mto kulikuwa na mti wa uzima utoao matunda ya aina kumi na mbili, ukizaa matunda yake kila mwezi. Nayo majani ya mti huo ni kwa ajili ya uponyaji wa mataifa. 3Katika mji huo hakutakuwa tena na kitu cho chote kilicholaaniwa, bali kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo humo na watumishi wake watamtumikia, 4nao atamwona uso Wake na Jina lake litakuwa kwenye vipaji vya nyuso zao.

 

Kufanywa upya kwa sayari hii kumeelezewa kwenye kitabu cha nabii Ezekieli sura ya 47. Nuguvu za kimaandiko alizotumia Kristo alivyokuwa kwenye Hekalu la Mungu zitawaponya mataifa na nchi na bahari.

 

Ezekieli 47:1-23 inasema: 1Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa hekalu ulielekea mashariki.) Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa hekalu, kusini mwa madhabahu. 2Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini. 3Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000a kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu. 4Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni. 5Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu ye yote ambaye angeweza kuvuka. 6Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?’’ Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto. 7Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto. 8Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Arabab, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Baharic, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi. 9Po pote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako. 10Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuud. 11Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi. 12Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za huu mto. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.’’ 13“Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: ‘Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu. 14Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu. 15“Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo Hamathi hadi maingilio ya Sedadi. 16Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi,) hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani. 17Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasari Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini. 18“Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi Bahari ya Masharikie na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki. 19“Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba Kadeshi, kisha utaambaa na kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini. 20“Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi. 21“Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli. 22Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli. 23Katika kabila lo lote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema BWANA Mwenyezi.

 

Himaya watakazopewa kuzimiliki Israeli kipindi hiki cha Milenia zimeorodheshwa kama ifuatavyo.

Ezekieli 48:1-35 inasema: 1sehemu zao Kwenye mpaka wa kaskazini, Dani atakuwa na sehemu moja, mpaka huo utafuata barabara ya Hethloni hadi Lebo Hamathi, Hasari Enoni hata mpaka wa kaskazini wa ameski karibu na Hamathi utakuwa sehemu ya huo mpaka wake kuanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi. 2“Asheri atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Dani kuanzia mashariki hadi upande wa magharibi. 3“Naftali atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Asheri kuanzia mashariki hadi magharibi. 4“Manase atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Naftali kuanzia mashariki hadi magharibi 5“Efraimu atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Manase kuanzia mashariki hadi magharibi. 6“Reubeni atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Efraimu kuanzia mashariki hadi magharibi. 7“Yuda atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Reubeni kuanzia mashariki hadi magharibi. 8“Kupakana na nchi ya Yuda kuanzia mashariki mpaka magharibi itakuwa ndiyo sehemu utakayoitoa ili kuwa toleo maalum. Itakuwa na upana wa dhiraa 25,000a na urefu wake kuanzia mashariki mpaka magharibi utakuwa ule ule wa sehemu moja ya kabila, mahali patakatifu patakuwa katikati ya eneo hilo. 9“Hiyo sehemu maalum mtakayotoa kwa BWANA itakuwa na urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 10Hii itakuwa ni sehemu takatifu kwa ajili ya makuhani. Itakuwa na urefu wa dhiraa 25,000 upande wa kaskazini, upana wa dhiraa 10,000 upande wa magharibi, dhiraa 10,000 upande wa mashariki na urefu wa dhiraa 25,000 upande wa kusini. Katikati yake patakuwa mahali patakatifu pa BWANA. 11Hii itakuwa kwa ajili ya makuhani waliowekwa wakfu, Wasadoki, ambao walikuwa waaminifu katika kunitumikia nao hawakupotoka kama Walawi walivyofanya wakati Waisraeli walipopotoka. 12Itakuwa toleo maalum kwao kutoka katika sehemu takatifu ya nchi, yaani, sehemu takatifu sana, inayopakana na nch ya Walawi. 13“Kando ya nchi ya makuhani, Walawi watakuwa na mgao wa urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Urefu wake utakuwa jumla dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. 14Hawataruhusiwa kuuza wala kuibadilisha hata mojawapo. Hii ndiyo sehemu nzuri ya nchi kuliko nyingine zote, hivyo haitakuwa mikononi mwa watu wengine, kwa sababu ni takatifu kwa BWANA. 15“Eneo linalobaki lenye upana wa dhiraa 5,000c na urefu wa dhiraa 25,000, litakuwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya mji, kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na malisho. Mji utakuwa katikati yake 16nao utakuwa na vipimo hivi: upande wa kaskazini dhiraa 4,500 upande wa kusini dhiraa 4,500, upande wa mashariki dhiraa 4,500 na upande wa magharibi dhiraa 4,500. 17Sehemu ya malisho kwa ajili ya mji itakuwa na eneo la dhiraa 250 upande wa kaskazini, dhiraa 250 upande wa kusini, dhiraa 250 upande wa mashariki na dhiraa 250 upande wa magharibi. 18Eneo linalobaki, linalopakana na sehemu takatifu likiwa na urefu sawa nalo, litakuwa dhiraa 10,000 upande wa mashariki na dhiraa 10,000 upande wa magharibi. Mazao yake yatawapa watumishi wa mji chakula. 19Watumishi wa mji wanaolima shamba hili watatoka katika makabila yote ya Israeli. 20Eneo lote la hiyo sehemu litakuwa mraba, yaani, dhiraa 25,000 kila upande. Kama toleo maalum mtatenga sehemu takatifu, pamoja na milki ya mji. 21“Eneo linalobaki pande zote za eneo linalofanya sehemu takatifu na milki ya mji litakuwa mali ya mkuu atawalaye. Eneo hili litaenea upande wa mashariki kuanzia kwenye dhiraa 25,000 za sehemu takatifu hadi mpaka wa mashariki na kuelekea upande wa magharibi kuanzia kwenye dhiraa 25,000 hadi mpaka wa magharibi. Maeneo yote haya mawili yanayoenda sambamba na urefu wa shemu za makabila yatakuwa ya mkuu anayetawala, na sehemu ile takatifu pamoja na mahali patakatifu pa hekalu itakuwa katikati yake. 22Kwa hiyo milki ya Walawi na milki ya mji vitakuwa katikati ya eneo lile ambalo ni mali ya mkuu anayetawala. Eneo la mkuu anayetawala litakuwa kati ya mpaka wa Yuda na mpaka wa Benyamini. 23“Kuhusu makabila yaliyobaki: Benyamini atakuwa na sehemu moja, itakayoanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi. 24“Simeoni atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Benyamini kuanzia mashariki hadi magharibi. 25“Isakari atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Simeoni kuanzia mashariki hadi magharibi. 26“Zabuloni atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Isakari kuanzia mashariki hadi magharibi. 27“Gadi atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Zabuloni kuanzia mashariki hadi magharibi. 28“Mpaka wa kusini wa Gadi utapita kusini kuanzia Tamari hadi maji ya Meriba Kadeshi, kisha kupitia upande wa kijito cha Misri hadi Bahari Kuu 29“Hii ndiyo nchi mtakayogawanya kuwa urithi kwa makabila ya Israeli, nazo zitakuwa sehemu zao,” asema BWANA Mwenyezi. 30“Haya yatakuwa ndiyo malango ya mji ya kutokea: Kuanzia upande wa kaskazini, ambayo urefu wake ni dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu, 31malango hayo ya mji yatapewa majina ya makabila ya Israeli. Malango hayo matatu ya upande wa kaskazini moja litakuwa lango la Reubeni, lango la Yuda na lango la Lawi. 32“Upande wa mashariki, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Yosefu, lango la Benyamini na lango la Dani.

 

Kujumuishwa kwa kabila la Dani hapa kwenye milki ya wana wa Raheli kunaonyesha kwamba neno Yusufu linawajumuisha wale wa kabila la Efraim na Manase, lakini kwenye Ufunuo sura ya 7 kumeandikwa kwa kyaonyesha makabila ya Dani na Efraim kama kabila la Yusufu katika kuhitimisha idadi ya watu 144,000, na kabila la Manase linaonekana kuwa mbali na haya. Kabila la Dani limehesabiwa kuwa na lango lao kwenye mfumo huu wa milenia kwa kupewa haki yao ya kumiliki upande wa kusini. Lango hili la upande wa mashariki ndilo lililokuwa akilitumia Masihi.

33“Upande wa kusini, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Simeoni, lango la Isakari na lango la Zabuloni. 34“Upande wa magharibi, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Gadi, lango la Asheri na lango la Naftali. 35“Urefu wote kuzunguka utakuwa dhiraa 18,000. Jina la mji kuanzia wakati huo na kuendelea litakuwa: BWANA YUPO HAPA.’’

 

Jina la mji huu ni Yahova Shama. Matukio haya yana ufafanuzi wa kiroho (1Kor. 2:14) lakini yana maeneno yake maalumu kwa ajili ya maongozi ya sayari hii.

 

Kazi kubwa sana kupita zote itakuwa ni kuuelimisha ulimwengu uijue kweli na haki na ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu, itaishia miaka elfu moja hadi pale shetani atakapofunguliwa tena ili awadanganye wanadamu na kufanya vita mwishoni mwa kipindi hiki cha Milenia. Hadi kufikia kipindi kile Mji wa Bwana kwenye Nchi Takatifu utabakia kuwa ni kambi ya watakatifu na wa maongozi ya dunia na utakuwa ni kitovu cha dini ya dunia. Hatahivyo, utaitwa jina lake kuwa ni Yahova Shama au Yahoshama. Haitakuwa na maana ya Amani ya Mungu, bali neno hili liutamaanisha Makao ya Mungu.

 

Kwenye jarida linalofuata la Yubile ya Dhahabu na Milenia Sehemu ya II: Israeli na Mataifa Yanayoizunguka (Na. 300B) [The Golden Jubilee and the Millennium Part II: Israel and the Surrounding Nations (No. 300B)] tutajionea utaratibu wa utunzi au uundaji na maeneo ya mataifa yaliyoko huko Mashariki ya Kati kama ilivyo kwenye siku ya 23 ya mwazi wa Saba wa Yubile ya 120.

q