Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[014]

 

 

 

Zaburi 8

Toleo La 1.0 20000907-20000907)

Zaburi 8 ni sura muhimu kwenye maandiko ya kinabii na inatumika kumhusisha Masihi na ni ya mhimu sana katika kuielewa Asili ya Mungu, Malaika wa Mbinguni na uhusiano wao na Masihi na Mwanadamu kwa ujumla.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2000 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Zaburi 8


 


Kwenye Yohana 5:18 tunaliona andiko zuri saa.

 

Yohana 5:18 Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu, bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu. Basi Yesu akajibu, akawaambia, Amin, amin, nawaambia,

 

Maneno aliyoayasema Kristo kuwaambia viongozi wa Wayahudi wa siku zile, yanaonysha kuwa walielewa kuwa Elohim aliyetajwa kwenye Agano la Kale na aliyempa Torati nabii Musa, alikuwa ni Malaika Mkuu, ambaye alikuwa pia ni mmoja wa wana wa Mungu.


Walilielewa pia andiko la Zaburi 45:6-7: lisemalo "Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako" kuwa linamlenga Masihi, ambaye alikuja na kuwa Mwana wa Mungu. Hii hatimaye imetokana na andiko la Kiebrania, pia kwenye Waebrania 1:8-9, ambaye anachukuliwa kuwa ni elohim mdogo au Kristo.


Mithali 30:4-5 inauliza swali ni kama lilivyo jina la Mungu na lililo jina la mwana wake, na kisha inalipa jina Mungu wa Pekee wa Kweli kwa umoja kwenye aya ya 5; imwitayo, Eloa.


kwa Kikaldayo, huyu alikuwa ni Elahh. Uwingi wake ulikuwa Elohim na Elahhin kwa Kikaldayo. Toleo hili la kimashariki la lugha, ambalo kikiujakuwa Kiaramu cha Kimashariki na hatimaye likawa la Kiarabu, ndiyo sababu inayowafanya Waarabu kulitamka jina la Mungu Allah'; na herufi mbili za h zinafanyika kuwa kama kivutio au kitu cha hamu.


Mahali ambapo lugha ya Kiyunani inatumia neno 'aggelos’ lilitafsiriwa kama malaika kwa Kiingereza, lilitumika kama wana wa Mungu, au elohim, kwa Kiebrania. Tafsiri ya Kiyunani ya Septuagint (LXX) na kwenye Agano Jipya pia.

 

Jambo hili limejtokeza nje kwa uzuri sana kwenye Zaburi 8 na matumizi yake kwenye maandiko ya Kiebrania na kwenye tafsiri ya LXX.

 

Zaburi 8:1-9 Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; 2 Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi. 3 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha; 4 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? 5 Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima; 6 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. 7 Kondoo, na ng'ombe wote pia; Naam, na wanyama wa kondeni; 8 Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini. 9 Wewe, MUNGU, Bwana wetu, Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!


Zaburi 8:2a imenukuliwa kwenye Mathayo 21:16. Jina au neno babes huenda ni rejea kwa kipindi chake cha ujana na huenda pia lililo kwenye 1Samweli 17:14,33, 42,55,56. Andiko linaelezea maadui kuwa ni washitaki wake maadui na neno mlipiza kisasi hapa ni mtu wa kisasi.


Zaburi 8:4,5,6 imenukuliwa pia kwenye Waebrania 2:6-8 kama "Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? 5 Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima; 6 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake."

 

Andiko hili hapa kwenye aya ya 4 linamtaja mtu mwenye kuweza kufa ‘enosh na ‘adam kwa Kiebrania.

 

Tunaona kwenye Waebrania 2:9 kwamba ilikuwa inamaanisha mateso ya kifo ambayo tulifanyika kwayo daraja la chini kuliko walivyokuwa wadogo kidogo. Bullinger alichukulia usomaji wa “kwa kiasi fulani” kwa kuliona hivyo andiko hilo. Kwa hiyo linafanana na la Wafilipi 2:5-8.

 

Wafilipi 2:5-9 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

 

Kwa hiyo, hakujaribu kujifanya kuwa sawa na Mungu au kuasi ila alifanyika kuwa mwanadamu na akajinyenekeza hadi mauti. Alifanyika kuwa Mwana wa Mungu mwenye uweza kwa kufufuka kwake toka kwa wafu (Warumi 1:4), kama tuonavyo kwenye (Wafilipi 2:9):

 

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

 

Sasa, nano hili linaitwa malaika kwenye Zaburi 8 na hata kwenye Kiebrania, kama tunavyoona kwenye Kiebrania elohim na linamaanisha miungu. Lilitafsiriwa kama ‘aggelos (kwa wajumbe) kwenye tafsiri ya Septuagint, na pia kutokana hilo kwenye maandiko ya Kiyunani na kwenye Kiebrania, na linarudia kwa namna hiyohiyo kwene tafslri za Vulgate, Kisyria na Kiarabu. Lilitafsiriwa kama malaika kwenye tafsiri ya Kiingereza. Sababu yake iliyodaiwa kwa maana hiyo ni kwamba liliwapendeza watafsiri wa Kiebrania cha kiasilia ili kuwataja wajumbe kwa kuwa ilikuwa inahusisha uwingi wa wana wa Mungu kama elohim, zaidi kuliko Eloah. Waamini Utatu wamefuata hii kwa kumfanya kama “malaika” na kuliruka neno lisemalo “kwa maana ya muda mfupi” na pia kwa maana iliyo kwenye Kisyria na Kiarabu. Sababu inayoonekana kuwa kwamba hakuna mmoja wao aliye tayetaka kujua kuwa hawa elohim walikuwa ni viumbe waliobeba majukumu ya ziada nay a zaidi.


Hata hivyo, andiko hili linaonyesha wazi kwamba etohim aliye kwene Kiebrania asilia, na Bullinger anaandika hilo kwenye mandiko yake kwenye kifungu au aya iliyo kwenye tafsiri iitwayo Companion Bible. Makuhani walijua kwamba mwana wa mtu alikuwa ni elohim aliyefanyika kuwa Mwana wa Mungu akijulikana kwa Kiyunani kama monogenes theos au mwana wa pekee wa Mungu kwenye Yohana 1:18 (sawa na ilivyo kwenye tafsiri ya Kiyunani na Kiingereza iitwayo Marshall's Greek English Interlinear RSV). Maandiko yaliyo kwenye tafsiri ya Companion Bible kwenye maandiko yanayofafanua mambo haya.

 
Wanamhusisha yeye kuwa anajifanya kuwa sawa na elohim, na kama hili halikuotajwa kwenye lugha ya Kiyunani, lakini ya Kiaramu, tunapata andiko hili kama elohi ambalo linafanana na kama malaika.


wana wa Mungu wote walikuwa elohim kama yanavyoonyesha maandko ya Agano la Kale kwa jinsi walivyotumika. Elohim hawa walijulikana kama 'aggelos, au wajumbe, na walitafsiriwa kuwa malaika kwenye lugha ya Kiingereza na kwenye maandiko mengine. Hata hivyo, makuhani wa Hekalu hawakujizuia na mapokeo ya kipagani ya Warumi kwa kipindi cha karne kadhaa kwa kipindi hiki, na kwa hiyo walijulikana kuwa wanaonyyesha dalili za wazi kabisa.

 

Neno wana wa mtu (sio kisarufi) lililotumika kwenye Zaburi 8, limetumika mara tatu kabla ya andiko hili kwenye Hesabu 23:19; Ayubu 25:6; na 35:8. Ni mara 111 kwa umoja kwene Agano la Kale na mara 39 kwenye uwingi. Pengine ilipojitokeza ni kwenye Zaburi (Zaburi 49:2; 144:3) ni nino linguine tofauti. Hapa kwenye Zaburi 8:4 jina hili la kicheo linamaanisha utawala au mamlaka ya kidunia, na linaiumika kwa maana hiyo kwene maandiko ya Kiebrania likimaanisha kuwa ni Masihi.

 

Andiko lililo kwenye Zaburi 8:6 linataja mamlaka aliyopewa mtu wa kwanza, Adamu, na ambayo yaliangukia kwenye anguko lake. Utawala, au mamlaka na marejesho ndilo lengo la wokovu ambao tunapasa kuutilia maanani sana na kuutunza kwa umakini wote. Idadi yake kwenye aya za 7 na 8 ni vitu sita, ambayo ni tarakimu ya kibinadamu.

 

Waebrania 2:1-18 Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa. 2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki, 3 sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia; 4 Mungu naye akishuhudu pamoja nao kwa ishara na ajabu na nguvu za namna nyingi, na kwa magawanyo ya Roho Mtakatifu, kama alivyopenda mwenyewe. 5 Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena, ila mtu mmoja ameshuhudia hivi mahali fulani, akisema, 6 Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie? 7 Umemfanya mdogo punde kuliko malaika, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; 8 Umeweka vitu vyote chini ya nyayo zake. Kwa maana katika kuweka vitu vyote chini yake hakusaza kitu kisichowekwa chini yake. Lakini sasa bado hatujaona vitu vyote kutiwa chini yake. 9 ila twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu.

 

Kwa hiyo, alifanyika kuwa mtu na akafa ili kutupatanisha na Mungu.

 

10 Kwa kuwa ilimpasa yeye, ambaye kwa ajili yake na kwa njia yake vitu vyote vimekuwapo, akileta wana wengi waufikilie utukufu, kumkamilisha kiongozi mkuu wa wokovu wao kwa njia ya mateso. 11 Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake; 12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa. 13 Na tena, Nitakuwa nimemtumaini yeye. Na tena, Tazama,mimi nipo hapa na watoto niliopewa na Mungu.

 

Anayatangaza majina yetu kwenye makusanyiko ya elohim, na haoni haya kutuita sisi ndugu zake.

 

14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, 15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa. 16 Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu. 17 Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye suluhu kwa dhambi za watu wake. 18 Na kwa kuwa mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wao wanaojaribiwa.

 

Sababu ya kwamba Mungu hafananishi na elohim waitwao malaika hapa, bali pia kwamba wana walio wa uzao wa Ibrahimu, ni wale waliochaguliwa ili kutufanya sisi kuwa makuhani, na inahusiana na kutufana sisi kuwa hivyo kwa kupitia kwa Kristo.

 

Hapa tunaliona andiko kwenye Waebrania liitajalo sheria iliyotolewa na malaika. Mtu au kiumbe huyu aliyeitoa Torati na kumpa nabii Musa alikuwa Kristo, na alijulikana hivyi na Kanisa la Kwanza kuwa ni Kristo.

 

Kwa hiyo hatua yenyewe ilikuwa ni ya kuutunza wokovu mkuu kuliko ilivyowezekana chini ya Sheria bila Roho Mtakatifu.

 

Ndipo hivyo kwamba \Krisuo alikuja kuutangaza wokovu huu mkuu. Mitume ambao walimshuhudia kwa macho yao waliutangaza hivyo. Ulikuwa umeshuhudiwa kwa uweza wa Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu kwa ishara na maajabu kwa kile tunachokiita leo kuwa miujiza.

 

Kwenye andiko hili tunauona sasa ukweli, kwamba mamlaka au uweza wa kuutiisha ulimwengu ujao hayakuwa yamepewa elohim kama malaika. Bali yalitolewa na akapewa Kristo kama Mwana wa Mtu, na kwa wanadamu, ili tuweze kuonyesha uwezo wetu wa kuuingia wokovu chini ya Kristo.

Hakuna mtu yeyote awezaye kwenda kwa Baba isipokuwa Kristo.

 

Ilimpasa Kristo afanyike mwanadamu, na kuonyesha utii wake na kutostahili kutuongoza sisi kupitia mauti. Kwa kuwa kwa sisi, kuipata kwetu haki ya kuwa warithi pamoha naye, kulilazimu kuwe na kifo kwanza cha mtu anayeweza kuitoa faida au hali ile, aliyopewa na muumbaji kama mamlaka makubwa zaidi.

 

Tutawahukumu malaika (1Wakorintho 6:3). Mapepo watahukumiwa na sisi katika ukamilifu wa dahari. Ndipo nao watapatanishwa kwa kupitia Kristo.

 

Hiki ndicho walichukuwa wanakitarajia kujiepusha kwa mapatano na kuyapatanisha Mapepo kwa kila mtu kwa njia ya dini potofu za siri. Kama ingelikuwa hivyo basi wangelibakia mbinguni bila kuhukumiwa.

 

Pia ni kwa mtazmo huu kwamba yeye aliyejitoa sadaka, na wale waliotakaswa wana upya wa asili. Hivyo, ilimpasa afanyike kuwa mwanadamu kutoka kwenye hali yake ya elohim na afe, ili kufanya kuwe na utakaso wa wote wawill, yaani mwanadamu na elohim, au mwanadamu na malaika, ili wapatanishwe na Eloah, ambaye anafanyika kuwa kiini cha wote na ndani ya yote na katika yote (Waefeso4:6).

q