Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021B]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Yoeli

 

(Toleo La 1.0 20140903-20140903)

 

Nabii Yoeli anashughulika na kuwaandaa wateule hasahasa wale wa \Masihi na katika siku za mwisho. Huduma yake ina mambo muhimu yahusuyo utakaso wa kusanyiko la Israeli kama Hekalu la Mungu na inafuatiwa na maneno a matendo ya kusifia maandalizi ya maandiko ya nabii Ezekieli. Bullinger anakifananisha kitabu hiki na cha nabii Ezekieli katika mwaka wa tano wa Yehoyakini kuwa utumwani lakini hakikujulishwa tarehe wala mwaka wake. Marabi wengine wanakiweka kitabu hiki mahali pengine popote. Wataalamu wa kanuni za maandiko wanakiweka kitabu hiki katikati ya Hosea na Amosi.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Yoeli



Jina Yoeli maana yake ni “Bwana ni Mungu” na lina maana sawa na lile la Eliya.

 

Mapokeo yanahuasiana kati ya Hosea na Amosi kwenye Karne ya 8 KK, kwa hiyo amekubalina na utaratibu wa kikanuni wa maandiko. Kiteolojia kitabu chake kinahusiana na nabii Ezekieli na kinaonekana kuwa kinahusiana na mambo na matukio yanayolingana.

 

Kitabu cha Hosea kilikuwa kinashughulikia makosa na hatia ya Israeli. Kitabu cha Yoeli kimeegemea kwenye matukio ya dhiki yaliyowakumba Yuda kwa ajili ya mafundisho yao ya uzushi na makosa kwa wakati huo na katika siku za mwisho. Kinabeba mrejesho na kulitaja Helaku la Mungu katika Siku za Mwisho chini na huduma yake ambayo ni Kanisa la Mungu. Mfululizo huo kwenye utaratibu wa Kikanuni kwa vyovyote vile, hakuna sababu ya kudhania kuwa kiliandikwa na nabii Hosea. Kinahusiana na muundo wa kama;

  1. Mwito wa Kusikia
  2. Hukumu za walioteseka
  3. Mwito wa Kutubu
  4. Hukumu imeondolewa na Marejesho Mapya.

 

Tunaona kurejea kwa Yuda huko Sayuni na Mungu anayashughulikia mataifa. Haya yalikuwa ni maelekezo au maongozi kutoka mbinguni yaliyotoka kwa Mungu mwenyewe akampa nabii Yoeli kama tunavyoona tangu aya ya 1. Ni jinsi ileile ya jinsi Mungu alivyomtuma kwa Daudi kwenye Zaburi na maelekezo yake kama tunavyoona kwenye Matendo 1:16. Maandiko yote hayawezi kutanguka (Yohana 10:34-36). Inatokea na itaendelea hadi kwenye siku za mwisho na kwenye kipindi cha Milenia. Hekalu la Ezekieli la Milenia ambalo Yoeli anaendelea hadi kwenye Milenia na Marejesho ya Yuda na Zekaria yanaonyesha kile kinachokwenda kutokea mbele na kutoka Yerusalemu kwayo na kutoka kwenye marejesho ya Milenia.

 

Ni pasipo shaka kabisa msingi wa uhasama au uadui kamili ya Hadithi za Kiislamu ya Waarabu kwenye Biblia na mafundisho ya kizushi ya watu wa Palestina, Gaza na Lebanoni na Waarabu kwa ujumla katika Misri. Inaweza kuwa tayari na maandiko mengine ya manabii katika kuona sawasawa jinsi Yahova atakavyorejesha upya na kuwashughulikia Wamisri na wana wa Shemu pia.

 

Yoeli.1

1 Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli.

 

Kwamba Mungu sasa anatangaza kile anachokwenda kukifanya katika Siku za Mwisho na baada ya hapo kwa kupitia Yahova wa Israeli (Kristo) kama tunavyoona kutoka kwenye Zekaria 2:1-9. Anasema kwa watu wa kale wa Israeli wanaokumbuka, zaidi kuliko wazee rasmi wa baraza la Sanhedrin, na kwa wakazi wa nchi, wote wawili, yani vijana kwa wakubwa, wanaume kwa wanawake. Mungu anawapa changamoto na kuwaonyesha kuwa haijatokea wakati alipowaandikia, yaani huenda ilikuwa chini ya Wababeloni lakini kabla ya maangamizo.

 

2 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? 3 Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.

 

Kwa hiyo, unabii huu ulipaswa kutolewa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na ulikuwa ni kwa wakati cha mbali kwa siku za mbele.

 

4 Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu. 5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.

 

Maneno yasemayo Ninyi nyote mnywao divai ni sahihizaidi kama vebu inayoifanyiza nauni. Haimaanishi kwamba unywaji bali zaidi ni kwamba inamaanisha wale wanaoupenda mvinyo.

 

Unabii unasema na kutangaza maangamizo ya Israeli na Walevanti kwa sababu ya vita. Nzige walionyesha ia kuwa ni kama ishara ya majeshi ya Kaskazini kwenye Vita wakati kwamba hawa nzige hawakuja kiasili kutoka Kaskazini. Aina ne ya nzige walisemekana na Karaite mfafanuzi wa Jepheth b. Ali kwenye ishara ya mashambulizi manne ya Yuda ambayo yalikuwa kila mojawapo ni kubwa zaidi ya lililotangulia mwanzo na hii ni huenda ndiyo maana hasahasa kwa matumizi ya neno Ha Tsephoni linalomaanisha “atokaye Kaskazini” kwenye sura ya 2:20. Tafsiri ya Soncino inaonyesha na kuandika hivyo pia. Hesabu yaje ya tarehe, hata hivyo, inachukuliwa kuwa ni uwongo mtupu kama sehemu yake kwenye kanuni ya maandiko yalisaidia kutoka kwenye mtazamo wa waandishi wa wakati wa kina Ezra na Nehemia wakati ilipodhaniwa kuwa iliandikwa. Wanazuoni wa siku hizi wanaiweka hii kwenye siku za baadae, kama wanavyofanya kwenye nabii nyingine zote, kwenye mahali pa baada ya matukio yanapotokea. Hata hivyo, hawawezi kufana hivyo kama ilivyoelezewa na Masihi nah ii bila shaka iliandikwa vizuri kabla ya kufungwa kwa baraza lililoshughulikia Kanuni ya kuyatambua maandiko sahihi mwaka 323 KK.

 

Yuda ilishambuliwa na kushindwa na Wamisri na Wababelini na Waajemi pia wakawatawala lakini waliwaruhusu kulijenga Hekalu kipindi cha Dario II Mwajemi na utoaji wa kuwezesha ujenzi na aaliyetoa agizo hilo alikuwa ni Artashasta II kwa marejesho na matengenezo waliyoyafanya kina Ezra na Nehemia (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 013).

 

Maangamizo makubwa yaliyowakumba na kuwatawanya Yuda ilikuwa ni Vita yao na Warumi na maangamizo ya Hekalu ya mwaka 70 BK (soma jarida la Vita na Warumi na Kuanguka kwa Hekalu (Na. 298)). Waedomu walitokomezwa katika Karne ya Pili KK kama ilivyotabiriwa mapema na nabii Obadia. Esau alikatiliwa mbali kama taifa na kuangamizwa kwa kuondolewa kabisa kwenye Mlima wa Edomu. Walishindwa vita na kuangamizwa na John Hyrcanus chini ya Wamakabayo na alichukua vyote katika Yuda. Hawa walifanyika hatimaye kuwa ni jeshi kwa haki yao na wakatawala Yuda kama Waidumeans chini ya Herode baada ya vita ya Actium aliyewafanya wawe watu bora kutoka Roma. Alikuwa ni liwali wa mfalme wa Kirumi. Wanafikia sasa idadi ya takriban theluthi moja ya Wayahudi wote wa tabaka la Hg J. Wengine wote ni Waarabu.

 

6 Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu, Lenye nguvu, tena halina hesabu; Meno yake ni kama meno ya simba, Naye ana magego ya simba mkubwa.


Maangamizo yaliyosababishwa na Warumi yalikuwa ni makubwa hasahasa kitendo cha kuifanya nchi kuwa msitu na maganjo kwa kazi ya kuizingira iliyofanywa.


7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.

 

Marudio yaliyo kwenye aya za 8-12 ni mwito wa toba. Aya za 13-20 ni mwito wa toba.

8 Ombolea kama mwanamwali avaaye magunia Kwa ajili ya mume wa ujana wake.

 

Sadaka au dhabihu ya daima iliondolewa mbali mwaka 70 BK na sadaka ya nafaka na vinywaji ziliondolewa. Kisha Hekalu lenewe liliangushwa na kuharibiwa kukafuatia na baa kubwa la njaa iliyotokana na kuangamizwa kwa vinu vya kusagia kwa ajili ya vita kubwa ya Wayahudi wenyewe ndani ya mji. Ulikuwa ni unabii ambao walikuwa wanautimiliza wenyewe ndio ulikuwa unatimilika.


9 Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimekatiliwa mbali na nyumba ya Bwana; Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, wanaomboleza. 10 Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka. 11 Tahayarini, enyi wakulima; Pigeni yowe, enyi watunzaji wa mizabibu; Kwa ajili ya ngano na shayiri, Maana mavuno ya mashamba yamepotea. 12 Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu.

 

Kuharibiwa kwa ardhi ya watu wa Yuda na Wapalestina lilikuwa ni tukio la kimsingi linaloendelea hadi kufikia Karne ya Ishirini. Yuda ndio walikuwa walengwa na walitawanywa ulimwenguni kote. Taifa likaenda utumwani na kuwa kwenye mateso ya Warumi Wakatoliki tangu hapo hadi kufikia Vita Kuu ya II ya Manazi. Kukawa hakuna nah ado halipo hata sasa Hekalu katika Yuda. Hekalu pekee lililoko ni lile lililojengwa na Kristo mwaka 27-30 BK na ni Hekalu la Mawe Yaliyohai.

13 Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu.

 

Njia pekee nje ya utumwa huu  ilikuwa ni kwa huduma ya watu wa Mungu anayefanya kumuitaka au kumuomba Bwana. Ilipaswa ifanyike kwa mambo mawili. Jambo la kwanza lilikuwa ni mchakato wa Utakaso na wa pili ulikuwa ni tangazo la Kutaniko Takatifu kwenye Bodi ya Wateule na Kutaniko la Israeli. Mfululizo wa Kwanza wa utakaso ulikuwa chini ya Masihi tangu mwaka 27 BK hadi 30 BK wakati alipoanza mchakato wa Utakaso pamoja na mitume na akalisafisha Hekalu kabla ya kuingia kwake mjini Yerusalemu akiwa kama Mwanakondoo aliyetengwa mbali siku ya 10 ya mwezi Abibu. Tangu mwaka 30 KK kipindi cha Miaka 40 kwa ajili ya toba ya Yuda yalianza na kuishia mwaka 70 BK.

 

Mlolongo huu wa mambo unafanyika pia katika siku za mwisho kwa ajili ya kulitakasa Hekalu la Mungu, Hekalu ambalo ni sisi. Utakaso wa Hekalu umeagizwa na Torati na unapasa uanze kuanzia siku ya 1 Abibu na kuendelea hadi siku ya 7 Abibu sawasawa na maelekezo ya Mungu yaliyonenwa na nabii Ezekieli (Ezekieli 45:20). Utakatifu wa watu au makutaniko matakatifu yafanywa kwenye Sikukuu, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato za Bwana (Ezekieli 45:17) na inaanzia kutoka Siku ya Kwanza ya Mwezi wa Kwanza wa Abibu (Ezekieli 45:18). Hii inafanyika kwenye mchakato wa ujenzi hadi kwenye Pasaka ambayo inafanyika kwa mlo wa Meza ya Bwana siku ya 14 Abibu jioni. Inaandaliwa na kuadhimishwa kwa mahudhui ya kukumbuka dhabihu ya Kristo jioni inayofuatia kama Mwanakondoo wa Pasaka. Hata hivyo, utakaso unahitajika na Utakaso huu wa Kusanyiko ni lazima uambatane na mfungo wa saumu kama tunavyoona kwenye kitabu hiki cha Yoeli, na Ezekieli anatuambia kwamba wale ambao hawajui mema yoyote au wanaofanya makosa au wasioelewa mchakato wa Hekalu kama vile saumu Fupi nay a kuyatubia Makosa au dhambi zilizofanywa Kimakosa au pasipokujua, ni lazima wafunge saumu ili kwamba kusanyiko lote liwe limetakasika kwa ajili ya maadhimisho ya Pasaka.

 

Kwa maneno mengine, sisi tunaweza kuwa sehemu ya suluhisho au tunaweza kuwa ni sehemu ya tatizo. Sisi tu sehemu ya wateule wanaofunga saumu kwa ajili ya watu ambao hawajui lolote la maana au tunaweza kuwa sehemu ya watu ambao hawajui jema lolote. Hii ni amri ya moja kwa moja kwenye huduma ya Mungu katika Siku za Mwisho katika kuliandaa Hekalu la Mungu liwe tayari kwa maombi na kufunga saumu, Hekalu ambalo ndiyo sisi.

 

Kristo alistahili kuanzisha mfumo ambao uliweza kulitakasa kusanyiko kufanya hivyo. Kipindi hiki cha utakaso sio cha upambanuzi. Kanisa la Mungu lisilofanya havi halitakipata Kinara cha Taa cha Siku za Mwisho na Mungu ataiuinua sehemu nyingine ya Mwili wa Kristo au kanisa.

 

Mchakato wa utakaso katika kulijenga hadi Pasaka wakati wote inahusu mchakato wa kufunga saumu katika utakaso na wateule walifunga saumu mara nyingi kwenye mchakato huu na ni ndiyo maana uliitwa na kanisa kuwa ni mwezi wa kufunga saumu na ulikuwa ni mwezi wa majira ya baridi kama ilivyo Ramadan ya Waislamu hadi ulipogeuzwa na kubadilishwa kimakosa na maandiko wanayoyaita Hadithi.


14 Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa Bwana, Mungu wenu, Na kumlilia Bwana,

 

Mchakato wa utakaso umeonekana kutoka nyakati za kale zaidi za huko nyuma kama siku za Ayubu (Ayubu 1:5) ambaye aliwatakasa watu wa familia yake kutokana na makosa au dhambi zao. Dhahibu hazihitajiki tena, kwakuwa zimetimilizwa na Kristo lakini Utakaso kwa njia ya kufunga saumu bado unahitajika na wakati wote umekuwa ukihitajika.

 

Mchakato huu wa Utakaso unaonyesha na kuhitajika kufanywa na wateule mapema sana kabla ya Siku ya Bwana na unahitajika kufanywa na wote wa Nyumbani mwa Mungu. Kumbuka kwamba mchakato huu unatakiwa uanzie na Huduma ya utakaso na kuitisha saumu. Wanahitajika kushiriki mchakato huu kwa kuitisha kusanyiko takatifu. Sababu ya kufanya hivyo ilikuwa ni baada ya kuanguka kwa Wathiatira, Wasardi waliinuliwa baada ya zama za Matengenezo. Wasardi hawakuelezea tena Mwandamo wa miezi kama Wathiatira walivyoutunza. Hawakuadhimisha kipindi cha Utakaso na adhimisho ekee walilolifanya kwa umakini lilikuwa ni Ushirika wa Meza ya Bwana. Hawakuiadhimisha sikukuu ya Pasaka kwa kipindi chote kamili cha siku nane. Kundi la mwisho la imani ya Wasardi liliibuka kutoka kwenye Kanisa la Mungu (la Siku ya Saba) yaani, Church of God (Seventh Day) kundi lililoongozwa na Herbert Armstrong. Huduma yake iliharibiwa na imani ya ki Ditheism na waliichukua na kuiamini Kalenda ya Hilleli na kufanya isiwezekane kabisa kuziadhimisha Siku Takatifu kwenye siku zake sahihi kutokana na kile kinachojulikana kama mapokeo ya kuahirisha. Wakati mwingine wanashindwa kuziadhimisha hata kwenye miezi yake sahihi. Makundi yaha yote mawili, yaani makanisa ya mrengo huu na Wayahudi ni mara chache sana wanamudu kuzishika sikukuu hizi kiusahihi na kanisa la WCG na imani yake waliachana na kuadhimisha siku zote nane kamili za Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwaka 1965-1967. Kwa hiyo, ndipo walipokipoteza kinara chao cha taa na wakatawanyishwa. Kwa hiyo mkosa haya yapasa yaondolewe kutoka kwenye Makanisa ya Mungu mapema kabisa kabla ya kurudi kwa Masihi kama ilivyotabiriwa hapa na nabii Yoeli. Itahitaji kuhusisha ufungaji wa Saumu kama Utakaso na kuitisha Kusanyiko Takatifu la Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu.

 

15 Ole wake siku hii! Kwa maana siku ya Bwana inakaribia, nayo itakuja kama uangamivu utokao kwake aliye Mwenyezi.

 

Aya hii inatoa kipindi maalumu kamili kama inavyofanya na kuonyeshwa kwenye kitabu cha nabii Ezekieli. Kinafuatana pia na maafa katikati ya mataifa. Utakaso pekee unaowezekana na Yuda ni kwa kupitia Mwili wa Kristo unaowezesha mchakato huu katika Siku za Mwisho. Ujio wa \Mashahidi katika wakati ule watatoa mwito kwa Yuda na Israeli na ulimwengu wote utubu.


16 Je! Chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu? Naam, furaha na kicheko mbali na nyumba ya Mungu wetu? 17 Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka.

 

Maafa haya yatafuatiwa na ukame ambao utaathiri kwa kiasi kikubwa malisho ya nchi zetu.


18 Jinsi wanyama wanavyougua! Makundi ya ng'ombe yamefadhaika, kwa sababu hawana malisho; naam, makundi ya kondoo yamepata mateso. 19 Ee Bwana, nakulilia wewe; Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani, Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.


Andiko linahusisha na kutokea kwa baa la asili la ukame na baa la moto na maafa mngine kutokea ulimwenguni kote ambao utaathiri miti na wanyama wa porini. Mlolongo huu wa matukio utaendelea na kuzidi na utakuwa kwenye kipindi chote cha Mashahidi watakaohudumu huko Yerusalemu (soma jarida la Mashahidi pamoja na wale Mashahidi Wawili (Na. 135)).

 

Ni kipindi cha Baragumu la Tatu kwenye Ufunuo na kisha kinaendelea hadi kwenye Kitasa cha Nne cha Ghadhabu ya Mungu.


20 Naam, wanyama wa mashamba wanakutwetea wewe; Kwa maana vijito vya maji vimekauka, Na moto umeyateketeza malisho ya nyikani.

 

Hii inasababishwa na ongezeko la kiwango cha joto kitakachoamriwa kitokee na ghadhabu ya Mungu. Wale wanaoitwa kuwa ni wanasayansi wanalaumu hali hii kutokea kwenye harakati za wanadamu nah ii inasababisha hali ya joto. Kwa namna ya kinyume chake hii ni sahihi kwa kuwa uasi wa wanadamu umechoza Hasira ya Mungu iwaangukie. Ni kitu kinachoweka mzunguko lakini mzunguko huu Mungu amewatuma malaika zake waimwage hasira ya Mungu kwenye jua ili lizidishe hali ya joto kufanikisha mchakato huu (soma jarida la Mzunguko wa Kihistoria wa Mabadiliko ya Tabia Nchi (Na. 218B)).

 

Mabadiliko ya Tabia Nchi yanayofanywa na binadamu ni shutuma za Kishetani zilizohusisha wanadamu na mwenendo wake mbaya na utaelekea pabaya sana hadi pale atakapotubu.

 

Sura inayofuatia inahusu ujio wa Siku ya Bwana


Yoeli 2

1 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu; Wenyeji wote wa nchi na watetemeke; Kwa maana siku ya Bwana inakuja. Kwa sababu inakaribia; 2 siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza kuu. Kama mapambazuko yakitandazwa juu ya milima, hao ni wakuu, tena wenye nguvu, mfano wao haukuwako kamwe, wala hautakuwako baada ya hao, hata katika miaka ya vizazi vingi.

 

Vita vya Siku za Mwisho inaendelea kwenye majeshi yanayojumuishwa kwa mitandao na maroboti na vifaa au silaha zenye uharibifu au maangamizi makubwa. Tunajua kuwa majeshi ya Washami au Syria yanatumia silaha za sumu sasa na matumizi haya yanaongezea umuhimu wake kwenye Vita vya Baragumu la Tano na la Sita. Mataifa yenye silaha za Vita za Mfalme wa Kaskazini na Mnyama walikuja huko Mashariki ya Kati kutoka Afghanistan mwaka 2001 na Iraq mwaka 2003 na anauandaa mwaka 2014 arudi tena huko Iraq. Ndivyo pia nchi ya Urusi ilivvyoivamia Ukraine. Wanaleta maangamizo na uharibifu mkubwa. Ukosefu wa busara unaotokana na makosa ya kimaandiko ya Uislamu wene itikadi kali unaleta maafa kwenye mataifa yale yanayohusika kutokana na Malaika Wanne wanaoukausha mto Frati ambao wameamriwa kuua theluthi moja ya wanadamu.


3 Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na bustani ya Adeni mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao.

 

Roboti hizi na vifaa vya kiufundi vipo kwenye mchakato wa kutengenezwa kwa wingi sasa.

4 Kuonekana kwao ni kama kuonekana kwa farasi; na kama wapanda farasi ndivyo wanavyopiga mbio. 5 Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto ilapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita. 6 Mbele yao watu wanahangaika; nyuso zote zimegeuka kuwa nyeupe kwa hofu.

 

Ndvyo ilivyo pia kwamba askari wanasaidiwa na vifaa hivi. Lakini vitendea kazl na maroboti wanatumika kwa kiasi kikubwa sana siku hizi.


7 Hupiga mbio kama mashujaa; huupanda ukuta kama watu wa vita; nao huendelea mbele kila mmoja katika njia zake, wala hawapotoshi safu zao. 8 Wala hapana mmoja amsukumaye mwenzake; huendelea mbele kila mmoja katika njia yake; hujifanyizia njia kwa nguvu kati ya silaha, wala hawaachi kuifuata njia yao. 9 Huurukia mji; hupiga mbio juu ya ukuta; hupanda na kuingia ndani ya nyumba; huingia madirishani kama aingiavyo mwivi. 10 Nchi inatetemeka mbele yao; mbingu zinatetemeka; jua na mwezi hutiwa giza, na nyota huacha kuangaza;

 

Jeshi la Bwana linatumwa liende likafanye uharibifu utakaosababishwa na huyu mnyama.

11 naye Bwana anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya Bwana ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili?

 

Hata hivyo, Mungu anaruhusu na anautaka ulimwengu utubu kwa maombi na kufunga saumu.

12 Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea; 13 rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.

 

Anawataka watu watubu hata baada ya kurudi kwa Masihi akiliongoza Jeshi la Mungu wanadamu hawatatubu kama tunavyoona baada ya kila kufunguliwa Kitasa cha Hasira ya Mungu kilichoelezewa kwenye kitabu cha Ufunuo kuwa kitamiminwa juu yao lakini bado hawatatubu (soma jarida la Vita vya Siku za Mwisho na Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu (Na. 141B)).


14 N'nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu?

 

Kisha anaelezea umuhimu wake wa kuitisha Saumu ya Kujitakasa. Tunaweza tu kujitakasa kwa kufunga saumu. Dhana ya kwamba Kristo alifanya hivyo kwa ajili yetu ni upuuzi wa kifikra kama saumu hii haikuitishwa tu kwa kipindi cha miaka 2000 baada ya huduma yake lakini wakati atakaporudi tena kuja kutawala hapa duniani nab ado yupo aliyaongoza majeshi ya Mungu. Mchakato huu unahitajika ili kwamba ulimwengu wote ushiriki kwenye Kusanyiko Takatifu kwenye Kalenda ya Mungu (soma jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156)).


15 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu; 16 Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake. 17 Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, na walie Kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee Bwana, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, Hata mataifa watawale juu yao; Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao? 18 Hapo ndipo Bwana alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake 19 Bwana akajibu, akawaambia watu wake; Tazameni, nitawaletea nafaka, na divai, na mafuta, nanyi mtashiba kwa vitu hivyo; wala sitawafanya tena kuwa aibu kati ya mataifa;

 

Maandiko yaliyo kauanzia aya za 13-20 yanatumia maneno “Mungu wangu” na “Mungu wenu” kana kwamba Mungu wa makuhani alikuwa ni tofauti na Mungu wa manabii. Hivi ndivyo ilivyo kwenye siku za mwisho ambapo Mafundisho ya imani ya Kiyahudi pamoja na imani ya Ukristo Mkongwe wa zamani na kwenye Makanisa mengi ya Mungu yaliyopotoka ya iliyokuwa WCG na machipukizi yake.

 

Ni kwa toba ya watu wake ambayo Mungu anapunguza hasira kwenye vuguvugu au harakati hizi yenye madhumuni ya haraka ya kuwapelekea wao watubu na nyuma yao mataifa ya duniani.

 

Andiko linalofuatia linawataja walio upande wa kaskazini. Haya ni Majeshi ya Kaskazini yaliyoandikwa kwenye Ufunuo 9 na Danieli 11, ambao ni nzige walioandikwa kwenye sura ya 1:4. Nzige wa Waliotoroka hawatokei upande wa kaskazini bali ni majeshi ya Kaskazini ndiyo yanayofanya hivyo.

.
20 lakini jeshi lililotoka kaskazini nitaliondolea mbali nanyi, nami nitalifukuza mpaka nchi ya ukame na ukiwa; sehemu yake iliyo mbele itaingia katika bahari ya mashariki, na sehemu yake iliyo nyuma itaingia katika bahari ya magharibi; na uvundo wake utapanda juu, na harufu yake mbaya itapanda juu, kwa sababu ametenda mambo makubwa.

 

Bahari ya Kusini ni bahari ya Chumvi (ambayo pia inaitwa Bahari Mfu) (kama kwenye Ezekieli 47:18; Zekaria 14:8). Bahari yake kuu kabisa ni ile ya Mediterranean inayotia maji au kuungana na Bahari ya Atlantic. Neno “zuia au epusha” lililoandikwa kwenye Isaya 66:24. Hawa ni wale wagumu wa kutubu ambao hawatavishika Sabato na Miandamo ya Miezi ya Mungu na ndiyo maana maadui zao wapo kule. Huwezi kuwa sehemu ya wateule wa Mungu usipokuwa unazishika Sabato zake na Miandamo ya Miezi (Isaya 66:23) na Sikukuu zake (Zekaria 14:16-19). Na inakupasa uwe na sehemu kushiriki mchakato wa utakaso ukiwemo mfungo huu wa saumu.


21 Ee nchi, usiogope; furahi na kushangilia; kwa kuwa Bwana ametenda mambo makuu. 22 Msiogope, enyi wanyama wa kondeni; maana malisho ya jangwani yanatoa miche, na huo mti unazaa matunda yake, mtini na mzabibu inatoa nguvu zake.

 

Dhana na wazo lililoko hapa ni kwamba Yahova wa Israeli amejitukuza mwenyewe kwa kufanya mambo makuu; nchi itatengenezwa na kufanywa upya baada ya Vitasa hivi vya Hasira ya Mungu.


23 Furahini, basi, enyi wana wa Sayuni, mkamfurahie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya masika, kwa kipimo cha haki, naye huwanyeshea mvua, mvua ya masika, na mvua ya vuli, kama kwanza.

 

Andiko hili linamaana ya kipimo chake muafaka zaidi ya kumaanisha nyingi. Ipo kwa kipimo chake muafaka kinachofaa kutumika kupimia mazao au mavuno.


24 Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika kwa divai na mafuta. 25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu. 26 Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu;

 

Ili kwamba hatimaye Mungu aliwaleta na kuwaongoza kwenye toba. Ingawa kitend cha kuruhusu kuharibiwa kwa mazao yao, aliifanyia marejesho mapya nchi yao.

 

Kisha anatoa ahadi kwamba atakuwa katikati yao  Israeli. Hawatatiwa kwenye aibu au kuaibishwa tena. Huyu ni Yahova mdogo na msaidizi kwa Israeli aliyetajwa kwenye Zekaria 2:1-9 na Zaburi 45:6-7 ambaye ni Masihi (Waebrania 1:8-9). Ametumwa na Yahova wa Majeshi; Ha Elohim; Mungu.


Na watu wangu hawatatahayari kamwe. 27 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.

 

Andiko linalofuatia linakwenda nyuma kuelezea kinachofuatia baada ya unabii asilia kwa vizazi vinavyokuja. Hii ilirudiwa kama unabii kutoka kwenye aya za 28 hadi 32a na Mtume Petro siku ya Pentekoste wakati Roho Mtakatifu alipoletwa na kuwashukia wateule kwa kumpokea kwao Masihi kama Mganda wa Kutikiswa (Matendo 3:18-26). Kama taifa lingetubu kama ilivyoelekezwa na Petro matokeo yake yangekuwa ni tofauti kubwa sana. Maneno ya manabii yangetimilika na Roho Mtakatifu angeweza kushuka kwa taifa na utaratibu wa maandiko yanayofuatia yangeweza kutimilika pia katika Yuda. Ni kama ilivyokuwa kwamba hawakufanya hivyo na walipewa miaka arobaini ya kutubu kwa Ishara ya Yona na kisha wakazingirwa na Majeshi ya Warumi tangu siku ya 1 Abibu, mwaka 70 BK na Hekalu likamoboshwa na Yuda wakatawanyika (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi tena wa Hekalu (Na. 13)).

 

Marejesho na Matengenezo yaliyofanywa na kina Ezra na Nehemia na Nuru iliyowaka na kuenea kutoka kwa Masihi (Isaya 42:7; Mathayo 4:12-16; Luka 2:32). “Siku za Mwana wa Adamu” ndipo zilikuwepo (sawa na Luka 17:22). “Baada ya hapo” ni baada ya Marejesho yaliyoanzisha mwanzo wa Siku za Roho kama zinavyoonekana katika Siku ya Pentekoste wakati Yoeli 2:28-29 ilipoanza kutimilizwa. Hata hivyo, Kristo aliuawa na ni kama ilivyokuwa kwa Yohana Mbatizaji. Malaki 4:3 kwa hiyo aliona mbele mbaali kwenye ujio wa Eliya kaika Siku za mwisho.

 

Wanawake wamejumuishwa kwenye jambo hili la karama za kiroho za Mungu pia. Wito wao na karama zao ziko dhahiri kwa wateule pia (sawa na Hesabu 11:16,17,29).

28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; 29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.

 

30 Nami nitaonyesha mambo ya ajabu katika mbingu na katika dunia, damu, na moto, na minara ya moshi.

 

31 Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo. 32 Na itakuwa ya kwamba mtu awaye yote atakayeliita jina la Bwana ataponywa; kwa kuwa katika mlima Sayuni na katika Yerusalemu watakuwako watu watakaookoka, kama Bwana alivyosema; na katika mabaki, hao awaitao Bwana.

(maandiko yaliyokolezwa rangi yamerudiwa pia kwenye kitabu cha Matendo; kama ilivyo pia kwenye Isaya 46:13; 59:20; Obadia 17; Zekaria 14:1-5; Waumi 11:26).

 

Tangu mwaka 30 BK, Roho Mtakatifu alitolewa kwa watu wa madaraja yote ya watu wa Mungu, yaani kwa wazee, na kwa vijana. Kwa wote wanaotubu na kuti kwa njia ya ubatizo na kwa sheria za Mungu  pamoja na kuwa na imani ya kutosha. Mungu atanena na kuwasiliana kwa jia ya ufunuo kupitia ndoto na maono ambazo zilikuwa ni namna kuu mbili ya mafunuo ya kinabii zilizotolewa hapo zamani kwa watu wachache sana miongoni mwa wanadamu kwa makundi yote mawili, yaani makuhani na manabii.

 

Kristo aliufafanua mchakato huu kwenye aya ya 31 kuwa inafuatia mara moja baada ya dhiki kuu ya siku za mwisho na itafuatiwa na ujio wa Masihi ulioandikwa kwenye Mathayo 24:29; Marko 13:24; Luka 21:25 nk.

 

Baada ya kushindwa kwao kutubu Yuda mwaka wa 30 BK utaratibu wote ulijielekezea wenyewe dhidi ya utawanyiko wao Yuda kwa kipindi cha Yubile 40 jangwani kama walivyotumia miaka 40 jangwani naada ya tukio lao la Kutoka Misri. Ndivyo pia Kanisa la Mungu lilipotumwa kule hadi katika Siku za Mwisho.

 

Kisha Mungu alitangaza kile atakachowafanyia wao (yaani katika Siku) za Mwisho. Kipindi hiki kinajiri tangu siku ya 25 Kisleu mwaka 1917 kwa kipindi cha tangu mwaka 2027 na kuendelea (soma jarida la Maneno ya Unabii ya Mungu (Na. 184)).


Yoeli 3

1 Kwa maana, angalieni, siku zile, na wakati ule, nitakapowarudisha mateka wa Yuda na Yerusalemu, 2 nitakusanya mataifa yote, nami nitawaleta chini katika bonde la Yehoshafau, na huko nitawahukumu kwa ajili ya watu wangu, na kwa ajili ya urithi wangu, Israeli, ambao wamewatawanya kati ya mataifa, na kuigawanya nchi yangu. 3 Nao wamewapigia kura watu wangu; na mtoto mwanamume wamemtoa ili kupata kahaba, na mtoto mwanamke wamemwuza ili kupata divai, wapate kunywa.

 

Katika siku hizo inaelezea kipindi cha kupanua au kuweka kitambo cha unabii hadi kwenye hukumu ya mwisho ya mataifa wakati Masihi atakapokuja tena katika utukufu wake (Mathayo 25:31-46). Neno la kuelezea kuhusu marejesho ya bahati hizi kwa kuwarudisha tena watumwa kwa jinsi liliyotumika kwenye Kumbukumbu la Torati 30:3 (sawa pia na 42:10; Zaburi 126:1,4; Ezekieli 16:53nk; Amosi 9:14). Ni sawa tu na kama Kristo kuwachukua utumwani wafungwa au mateka. Hii ni idadi kubwa au kundi la mataifa ya Ufunuo 21:24. (Nitawakusanya [pia] sawa na Zekaria 14:2-4).

 

Mahali ambapo Yehoshafati (Yahova amehukumu) bado pamelindwa na kutunzwa kwa jina la kijiji cha Sh’afat huko Wadi Siti Miriam au Wadi Far’aun iliyoko kati ya Yerusalemu na Mlima wa Mizeituni. Hii itaenea hadi kwenye bonde wakati wa kuja kwake Masihi. Yahova ataingia Kuwahukumu (sawa na Isaya 66:16; Ezekieli 38:22).

 

Mambo ambayo mataifa waliwafanyia Yuda yataachwa vichwani mwao wakati wa hukumu kama tunavyoona kwenye Mathayo 25 na sio kwa kuwahesabia haki kutokana na imani yao na ndiyo maana sehemu ya pili inaelezea na kilichotokea kwa Watoro tangia kukomeshwa kwa nguvu za Wafilisti hadi walipojitoa na kuwapa mamlaka Waarabu na kujichanganya kwao kwenye makabila ya Waarabu. Ndiyo sababu ya makabila haya wanaitwa Wapalestina hadi leo. Waarabu na mataifa waliotawanyika katika Yuda na pia wale waliojichanganya kwa Wayunani na mataifa mengine watafanywa walipe

4 Naam, na ninyi ni kitu gani kwangu, enyi Tiro, na Sidoni, na nchi zote za Filisti? Je! Mtanirudishia malipo? Au mtanitenda neno lo lote? Upesi na kwa haraka nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe.

 

Tunaona kwamba katika kipindi hiki kama Yuda walivyochanganyika na Wapalestina na Wayunani na Warumi na kuuzwa nchi za ng’ambo, ndivyo pia wale waishio Gaza na Tiro na Sidoni na wa Lebanoni wote watakavyo tawanyika kwa Wasabeani au Waarabu wa Sheba wa upande wa Kusini Mashariki (kama ilivyo kwenye Ayubu 1:15; 6:19; Isaya 60:6), ilivyotokea kwa kipindi cha millennia mbili za mwisho na sasa wanapaswa kuhamishiwa tena kwa mwelekeo wa Ufalme wa Israeli utakaokuwa chini ya Kristo. Mungu atawaponya majeraha yao Israeli na Yuda na kuwatoa kwenye mataifa yote ambako waliuzwa kwayo (sawa na ilivyo kwenye Isaya 43:5,6 pamoja na 49:12; Yeremia 23:8).

5 Kwa kuwa mmetwaa fedha yangu na dhahabu yangu, nanyi mmevichukua vitu vyangu vyema vipendezavyo, na kuviingiza katika hekalu zenu; 6 tena watoto wa Yuda na watoto wa Yerusalemu mmewauzia Wayunani, mpate kuwahamisha mbali na mipaka yao; 7 tazameni, nitawaamsha wapatoke mahali mlipowauza, nami nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe. 8 Na mimi nitawauza wana wenu na binti zenu, na kuwatia katika mikono ya wana wa Yuda, nao watawauzia watu wa Sheba, taifa lililo mbali kabisa; kwa maana Bwana ndiye aliyesema neno hili.

 

Wakati huu Mungu aliyachochea mataifa na kuwaleta chini kwenye bonde la kukata maneno.

9 Tangazeni haya kati ya mataifa; takaseni vita; waamsheni mashujaa; watu wa vita na wakaribie; na wapande juu. 10 Yafueni majembe yenu yawe panga, na miundu yenu iwe mikuki; aliye dhaifu na aseme, Mimi ni hodari. 11 Fanyeni haraka, mje, enyi mataifa yote, wa pande zote, jikusanyeni pamoja; na huko watelemshe mashujaa wako wote, Ee Bwana.

 

Kumbuka kuwa mataifa yataletwa chini mahususi kukutana na Jeshi la Mbinguni. Mgongano unaonekana kwenye Danieli sura ya 12 mara moja na kwa haraka sana kufuatia vita vya Siku za Mwisho.


12 Mataifa na wajihimize, wakapande juu katika bonde la Yehoshafau; maana huko ndiko nitakakoketi niwahukumu mataifa yote yaliyo pande zote.

 

Mungu anayaleta mataifa kwa Yehoshafati ili kuyahukumu na kuyaangamiza majeshi yao na kisha kuyashughulikia mataifa yasiyo na majeshi yenye silaha.

 

13 Haya! Utieni mundu, maana mavuno yameiva; njoni, kanyageni; kwa maana shinikizo limejaa, mapipa nayo yanafurika; kwani uovu wao ni mwingi sana. 14 Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno! Kwa maana siku ya Bwana i karibu, katika bonde la kukata maneno.

 

Maadui wa Mungu wanafananishwa kwanza na “mavuno yaliyoiva” ambayo wakati wake wa kufyeka, kisha kwenye “kipimo/kilichojaa tele” zabibu ambazo ulikuwa wakati wa kuvuna au kupura. (sawa na Ufunuo 14:14-20, 19:15,18). Kwa hiyo Mungu atamtumia Kristo aende na kuuhukumu ulimwengu wote, akiwashurutisha watubu kwa kutumia Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu.


15 Jua na mwezi vimetiwa giza, na nyota zimeacha kuangaza. 16 Naye Bwana atanguruma toka Sayuni, atatoa sauti yake toka Yerusalemu; na mbingu na nchi zitatetemeka; (kama kwenye Yeremia 25:30; Ezekieli 38:18-22; Amosi 1:2; mgurumo = radi)

 

Hata hivyo, kumbuka kuwa wanaokimbilia kwa Watu Watakatifu ni kwa Kristo kwa uweza wa Mungu. “Mahali pa Salama” yuko mikononi mwa Mungu na sio mahala pengine popote panapodhaniwa na mwanadamu (soma jarida la Mahali Salama pa Kukimbilia (Na. 194)).

 

Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, na ngome ya wana wa Israeli. 17 Hivyo ndivyo mtakavyojua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, nikaaye Sayuni, mlima wangu mtakatifu; ndipo Yerusalemu utakapokuwa mtakatifu, wala wageni hawatapita tena ndani yake kamwe.

 

Nchi Takatifu inarejeshwa upya. Panapowataja wageni wakipita kwenye mambo ambapo watu watakwenda huko maalumu kwa malengo yaliyoelekezwa na Mungu kwenye unabii na chini ya maongozi lakini hawata tangatanga tu ndani yake kama mahali pa kutumia. Ni Mahali Patakatifu.

 

Kuna tukio kubwa la Kutoka kama lilivyotajwa kuwa litafanyika na nabii Isaya kwenye sura yake ya 65:17-25. Watu Watakatifu watarejeshwa kwenye nchi kutoka ulimwenguni kote.


18 Tena itakuwa siku ile, ya kwamba milima itadondoza divai tamu, na vilima vitatiririka maziwa, na vijito vyote vya Yuda vitatoa maji tele; na chemchemi itatokea katika nyumba ya Bwana, na kulinywesha bonde la Shitimu.

 

Katika siku za mwisho Waislamu wenye itikadi kali na mgawanyo wa Misri watasababisha dhiki kubwa kama inavyoonekana sasa na itapunguzwa kwa hali ya umakini kama walivyokuwa Waedomu kwenye eneo ambalo kwa sasa ni sehemu ya nchi ya Yordani. Masalia au mabaki ya Wafoinike.

19 Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya dhuluma waliowatenda wana wa Yuda; kwa sababu wamemwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.

 

Mtafaruku utaisha kati ya mataifa na hasahasa Misri italipa kama watakavyofanya Waedomu.

 

Haya sio matokeo ya mwisho kwa iapo kama Misri au Edomu kama taifa la Misri itarefanywa upya na Masihi baada ya Waashuru na Israeli wanaotoke upande wa kaskazini na kuifanya upya nchi kutoka kaskazini ya mbali mwa Iraq kutoka Frati hadi Mto wa Misri na bahari ya Mediterranean hadi kwenye Jangwa la Uarabuni linaloungana pia na nchi ya Yordani pamoja na Syria, Gaza na Lebanoni. Taifa la Misri linafanywa upya na kuwa kama mshirika wa Kusini ya washirika wake wa kibiashara wa mataifa matatu.


20 Bali Yuda atadumu milele, na Yerusalemu tangu kizazi hata kizazi. 21 Nami nitaitakasa damu yao ambayo sijaitakasa; kwa maana Bwana ndiye akaaye Sayuni.

           

Kwa hiyo wakosaji walio na hatia watahukumiwa (kama inavyosema Kutoka 34:7; Hesabu 14:8; Waebrania. Nakah haikutumika kusafishia. Tafsiri ya LXX nay a Wasyria zinaionyesha na kuitaja hii “kuunda baraza ka mahakama ya kidini” kama kwenye 2Wafalme 9:7 na Waebrania. Nakam ni kulipa kisasi kwanza  Nakah).

 

Yahova wa Israeli kama Masihi kisha anafanya makao yake katika Sayuni (Waebrania inasema Anakaribia kufanya makao yake huko Sayuni). Ndipo inaishia kama inavyofanya Ezekieli 48:35.

 

Kwa hiyo ulimwengu unaendelea kutoka Sayuni kama tunavyoona kwenye vitabu vya manabii Ezekieli na Zekaria (soma jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria (Na. 021K)).                                                         

q