Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021E]

 

 

 

Ufafanuzi Wa Kitabu Cha Yona

 

(Toleo La 1.0 20140928-20140929)

 

Ishara ya Yona ilikuwa ndiyo ishara pekee lililopewa Kanisa. Kwa hiyo ina umuhimu mkubwa sana kwenye uelewa wa Imani.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2015)

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi Wa Kitabu Cha Yona



Utangulizi  

Yona mwana wa Amitai ni mtu anajulikana kwa umahiri wake. Ametajwa kwenye 2Wafalme 14:25. Alikuwa ni mtu anayetokea huko Gath-hefa ambao ni mji wa mpakani wa huko Zabuloni (soma Yoshua 19:13). Huenda unatajwa kwa pamoja na Khirbet ezZurra’ ambako ni eneo kubwa lililo maili tatu Kaskazini Mashariki mwa Nazarethi, ambao ulikuwa katika Galilaya. Maneno ya Mafarisayo kwenye Yohana 7:32 kwa hiyo yalikuwa ni uwongo. Kristo alikuja akitokea kwenye eneo la Nazarethi katia Galilaya, kama alivyokuwa Yona. Ilikaliwa katika Zama za Mawe awamu ya I na II yapata mwaka 1200-600 KK na kwa hiyo kwenye kipindi cha Yona na labla ya hapo kwenye kipindi cha Mwishoni mwa zama ya Shaba tangu mwaka 1550 KK na kwenda mbele. Yona alikuwa nabii aliyetabiri wakati wa Yeroboamu II mfalme wa Israeli (yapata mwaka 793-775 KK) na miaka ya mwanzoni ya Uzia (mwaka 775-757 KK). Imejiri kipindi kifupi kwa upande wa kaskazini na masalia ya kijiji cha Meshedi ambayo ni uwanja wa kidesturi wa Kaburi la mahali alipolala Yona.

 

Unabii huu kama Ishara ya Yona ulikuwa ni ishara pekee lililopewa Kanisa na Mungu na kwa hiyo ni muhimu kwenye uelewa wa harakati na kifo cha Kristo na pia wa unabii uliotolewa kupitia nabii Danieli kwa kuwa imejumuishwa na kufungamanishwa kwenye unabii wa Majuma Sabini ya Mwaka kwenye Danieli 9:25, na kuanguka kwa Hekalu mwaka 70 BK mwishoni mwa majuma 70 ya miaka. Uhusiano ule umeelezwa kwenye jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 013).

 

Imejumuishwa pia na siku za mwisho na kuingia kwa kanisa wakati wa Kurudi kwa Masihi kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Kristo amemuweka kwenye kiwango cha namna moja cha uwepo wa wazi na Malkia wa Sheba na kutangaza ishara kwa yeye aliye wa pekee aliyepewa kanisa (soma Mathayo 12:40). Wafafanuzi walio wengi hawajui ishara na kwa hiyo wanajaribu kuonyesha umuhim. Kama maneno Kristo aliyoyasema yale aliyopewa na Mungu, wakosoaji wanaoyakataa mafundisho ya Kristo wanatuama kwenye uvunio wa Mungu.

 

Kristo alipaswa afe kabisa kwa muda wa siku tatu usiku na siku tatu nyingine mchana na awe kaburini kama Yona alipokuwa ndani ya samaki na kwa hiyo wote walipaswa kuwa wamekufa na wafufuke toka kwa wafu. Kipindi cha siku tatu usiku na tatu nyingine mchana hufanya kipindi kipana cha sehemu ya Siku na kutowezekana haiendani kabisa na ile inayoitwa kuwa Ijumaa wa Mateso na Ufufuko wa Jumapili. Dhana ya kufufuka kwa mungu Attia iliyoingia kwenye imani ya Kikristo kwa imani ya madhimisho ya Easter au dini ya mungumke Cybele au Easter na kuna kutowezekana (soma pia jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235)).

 

Luka 11:30 inaonyesha kwamba Yona alikuwa Ishara ya watu wa Ninawi, kama Kristo alivyokuwa kwenye ufufuko wake.

 

Wayahudi wa siku za Kristo walikasirishwa na toba ya wanafunzi chini ya Kristo kama Yona alivyokuwa kwa toba ya watu wa Ninawi.

 

Mungu alisema kwamba angeyaweka maneno yake kinywani mwake yeye aliyemtuma na mara saba Kristo alijaribiwa kwenye ukweli huo kwenye Injili ya Yohana (Yohana 7:16; 8:28, 46- 47; 12:49; 14:10, 24; 17:8).

 

Yona alikuwa ameamriwa aende akawafariji Israeli (2Wafalme 14:25,26) na Ashuru ilikuwa kwenye magumu makubwa kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi na sita na katika kipindi hiki, ilimpasa Yona agundue kwamba Ashuru inaelekea kwenye toba ili waweze kuwa fimbo ya kuwarekebisha Israeli. Kinachoonekana kuwa ni mtazamo uliodhahiri ni kwamba Yahova alikuwa ni mkweli katika Neno lake na kwamba kama alifanya tangazo kuwatangazia watu wa Ninawi na kuutaka mji utubu, ulipelekea kuanguka kwa kishindo kwa Israeli, ambalo kwa kweli lilifanya. Kukimbia kwake kwa hiyo haukutokana na woga wao bali ni kuwalinda watu wake na kuikubali hukumu ya Mungu.

 

Utaratibu na mfumo wa kitabu upo kwenye migawanyo miwili ya minne:

  1. 1:1 Neno la Yahova
  2. 1:2 Huduma ya Nabii huko Ninawi
  3. 1:3 Kutotii kwa Yona
  4. 1:4-2:10 Matokeo mabaya na Kifo na Kufufuka kwa Yona.
  5. 3:1 Neno la Yahova
  6. 3:2 Huduma ya Ninawi
  7. 3:3,4 Utii wa Yona
  8. 3:4-4:11 Mapatilizo na Kurekebishwa kwa Yona.
  9.  

Sasa tutaenda kwenye sura nne na kutazama nia yake na msingi.

 

Sura ya 1 inahusika na mahubiri na maelekezo ya Yona na matendo yake yaliyofuatia. Bilashaka kabisa kwamba Yona alielekezwa na Mungu na kujua kwamba Mungu ndiye aliyemuelekeza yeye.

 

Yona Sura ya 1

1 Basi neno la Bwana lilimjia Yona, mwana wa Amitai, kusema,

 

Usemi huu au kama maneno unapatikana mara saba kwenye kitabu cha Yona, sura na aya hizi 1:1; 2:10; 3:1,3; 4:4,9, 10.

 

2 Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, ukapige kelele juu yake; kwa maana uovu wao umepanda juu mbele zangu.

 

Na kwa hiyo inakuwa dhahiri kwa Yona kwamba Yahova alikuwa anakaribia kuwsahughulikia watu wa Ninawi. Kwa hiyo mgongano huu wa mawazo kwa watu wake uliojitokeza ungeweza kuwafanya watubu. Ninawi (kwa mujibu wa Mwanzo 10:11,12) ulikuwa ni mji mkuu wa Dola ya Ashuru upande wa kushoto mwa Mto Tigri ulioitwa hapo mwanzoni Nina kwa jina la mungumke waliyemdhania kuwa ni mlinzi wa mji huo. Ulikuwa na chimbuko la Kibabeloni kutokana na koloni kutokana na Nina Kusini mwa Babeli. Khamurabi kutoka kwenye kipindi cha zamani sana cha mwanzoni aliuita mji huu Ni-nu-a.

 

Bullinger anakinukuu kitabu cha ufafanuzi kiitwacho Encyc. Brittanica (11th Cambridge edition) kama ilivyoanza uchimbuzi ambao ulidhihirisha maandiko ya Nabi Yunus (nabii Yona) akiwa kaburini hakuweza kutathiminiwa.

 

Aliamriwa apige kelele kuuonja mji huu (kwa Kiebrania Kara’) na kwa hiyo kufanya tangazo la jumla.

 

Ninawi ulijulikana kutokana na imani yake wenyewe ulioshamishwa kwao kwa uovu wake na ukatili wake (soma pia Nahumu 2:8-13). (Kiebrania kina neno la uwingi la ra’a’.)

 

3 Lakini Yona akaondoka akimbilie Tarshishi, apate kujiepusha na uso wa Bwana; akatelemka hata Yafa, akaona merikebu inayokwenda Tarshishi; basi, akatoa nauli, akapanda merikebuni, aende pamoja nao Tarshishi, ajiepushe na uso wa Bwana.

 

Yona alijua kuwa Ashuru ilikuwa ni upanga wa adhabu au mapatilizo ya Mungu dhidi ya Israeli na kwa hiyo hakuwa kwenye ugomvi usiovumilika kwamba kama Ashuru haikuachwa salama kupitia toba na Rehema ya Mungu kwa Israeli ilikwa budi iokolewe. Inaonekana kuwa inawezekana sana kuwa ni sababu ya mapenzi yake na kukimbia kwake (soma pia sura na aya za 4:1-3). Alikwenda Yopa ambayo sasa inajulikana kama (soma Yoshua 19:46; 2Nyamati 2:16; Matendo 9:36) na akapanda meli kwenda Tarshishi. Na ndipo alikimbia na kwa kadiri alivyoweza wakati ule ambako ni Tarshishi (soma 1Wafalme 10:22) ambao uko upande wa kusini mwa Hispania na ulikuwa ni kitovu cha kibiashara ya Mwingiliano katika Mediterranean kama tunavyojua vizuri sana na hadhari kuu leo. Ni nai ajuaye mahali ambapo kwa hakika alikuwa anakusudia kwenda. Kwa hakika walikuwa wanafanya biashara huko Kusini mwa Amerika kabla ya wakati ule. Meli (kwa Kiebrania ‘aniyah) ilikuwa ya ukubwa wowote wa meli za wafanya biashara na sio neno hilohilo kama ilivyo kwenye aya ya 5.


4 Lakini Bwana alituma upepo mkuu baharini, ikawa tufani kubwa baharini, hata merikebu ikawa karibu na kuvunjika.

 

(Upepo ulikuwa ni burudisho kubwa ya kiroho.)

 

Neno lililotumika kuwaita Mabaharia kwenye aya ya andiko hili kwa Kiebrania huitwa mallachor salts. Ndipo manahodha walijulikana kama chumvi na kama ilivyokuwa kawaida kwa Kiingereza.

 

5 Basi wale mabaharia wakaogopa, kila mtu akamwomba mungu wake; nao wakatupa baharini shehena iliyokuwa merikebuni, ili kuupunguza uzito wake. Lakini Yona alikuwa ameshuka hata pande za ndani za merikebu; akajilaza, akapata usingizi.

 

Kila aloiyelia kwenye maombi (Kiebrania Ze’ah (sio kama ilivyo kwenye aya za 2,14)) kwa mungu huyu. Na walitupa shehena (yaani shehena kwa Kiebrania Keli, au kuipa mashiko au kusaidia) baharini.

 

Neno lililotumika kumuelezea mahodha hapa ni mkuu wa kamba ambaye ni nahodha, neno la kwa Kifoenikiani lililotumika kumuita nahodha (kwa Kiebrania Rab hachobel). Kwa majadiliano kwa kutokea kwa neno nahodha tazama kitabu cha Bullinger fn 6 Comp. Bible p. 1248).

 

6 Basi nahodha akamwendea, akamwambia, Una nini, Ewe ulalaye usingizi? Amka, ukamwombe Mungu wako; labda Mungu huyo atatukumbuka, tusipotee.  

 

Hapa neno hili ni Elohimu lenye niherufi eth linamaanisha Mungu wa kweli pia kwenye mwonekano wa pili. Kwa hiyo nahodha alichukuliwa kuwa ni mungu wa Yona au Yunus kuwa ndiye Mungu wa kweli.

 

Muundo au utaratibu wa andiko la sura na aya zake kama hivi: 1:7-12 inaonyesha kujitoa mhanga kama sadaka kwa Yona.

Aya ya 7 inaonyesha upigwaji wa kura na Yona anachukuliwa.

Aya ya 8 inaonyesha udadisi wa kuuliza sababu

Aya ya 9 inaonyesha ukiri wake

Aya ya 10-11 inaonesha hofu yao na kuchanganikiwa kwao.

Aya ya 12 inaonyesha maamuzi ya Yona yanayotokana na matendo ya Mungu.


7 Wakasemezana kila mtu na mwenzake, Haya, na mpige kura, mpate kujua mabaya haya yametupata kwa sababu ya nani. Basi wakapiga kura, nayo kura ikamwangukia Yona. 8 Ndipo wakamwambia, Tafadhali utuambie, wewe ambaye mabaya haya yametupata kwa sababu yako; kazi yako ni kazi gani? Nawe umetoka wapi? Nchi yako ni nchi ipi? Nawe u mtu wa kabila gani?

 

Kumbuka kuwa wanaomba utaifa wake lakini anasema anasema tu kuwa Namcha Bwana Mungu. Hakutangaza kwamba alikuwa ni nabii bali walikuwa wameghadhibika kwamba alikuwa amewajulisha sana wao kwa hatari kama ile kama alivyowahi kuwaambia kwamba alikuwa amemkimbia Mungu.

 

9 Akawaambia, Mimi ni Mwebrania; nami namcha Bwana, Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi kavu. 10 Ndipo watu wale wakaogopa mno, wakamwambia, Ni jambo gani hili ulilolitenda! Kwa maana watu wale walijua ya kuwa amekimbia, ajiepushe na uso wa Bwana, kwa sababu alikuwa amewajulisha.

 

Kisha watu wanatafuta ulinzi wake kama kwa namna atakavyoweza kutoroka au kuliepuka tatizo lile ambalo yeye mwenewe amelisababisha. Hatimaye anaelewa ukubwa wake wa jinsi lilivyo tisha na anasema “Niondoeni mimi” akiona mapatilizo na suluhisho.

 

11 Basi wakamwambia, Tukutende nini, ili bahari itulie? Kwa maana bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. 12 Naye akawaambia, Nikamateni, mnitupe baharini; basi bahari itatulia; kwa maana najua ya kuwa ni kwa ajili yangu tufani hii imewapata.

 

Licha ya ushauri huu, watu wale bado walijaribu kumuokoa na kwa hilo hawakumcha Mungu wake.

 

13 Lakini wale watu wakavuta makasia kwa nguvu, ili wapate kurudi pwani, wasiweze; kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia sana. 14 Basi wakamlilia Bwana, wakasema, Twakuomba, Ee Bwana, twakuomba, tusiangamie kwa ajili ya uhai wa mtu huyu, wala usitupatilize kwa ajili ya damu isiyo na hatia; kwa maana wewe, Bwana, umefanya kama ulivyopenda.

 

Hatimaye walimuomba Mungu kwa hofu kwa sababu walijua kuwa alikuwa ni mtu asiye na makosa na kwamba amekimbia tu kutoka mbali kwa woga. Hawakujua uasi wake. Walilazimika kukubaliana naye na wakamtupa kwenye kilindi cha maji. Bahari ikaacha kuchafuka na jambo hilo liliwafanya wamuogope Mungu hata zaidi na kisha walitoa sadaka kwa Mungu wa Waebrania.


15 Basi wakamkamata Yona, wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka. 16 Ndipo wale watu wakamwogopa Bwana mno, wakamtolea Bwana sadaka, na kuweka nadhiri. 17 Bwana akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona, naye Yona akawa ndani ya tumbo la samaki yule muda wa siku tatu, mchana na usiku.

 

Mungu alijua kile ambacho Yona alichokifanya na kile kingalichofanyika baada ya hapo na akamuandaa samaki mkubwa ammeze Yona.

 

Yona Sura ya 2

1 Ndipo Yona akamwomba Bwana, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki, 2 Akasema, Nalimlilia Bwana kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu naliomba, Nawe ukasikia sauti yangu. 3 Maana ulinitupa vilindini, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu. 4 Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako; Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu. 5 Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu; Vilindi vilinizunguka; Mwani ulikizinga kichwa changu; 6 Nalishuka hata pande za chini za milima; Hiyo nchi na mapingo yake yalinifunga hata milele; Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni, Ee Bwana, Mungu wangu, 7 Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nalimkumbuka Bwana; Maombi yangu yakakuwasilia, Katika hekalu lako takatifu. 8 Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo Hujitenga na rehema zao wenyewe; 9 Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa Bwana. 10 Bwana akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.

 

Neno nyangumi halijaandikwa popote na huyu alikuwa ni samaki mkubwa na Yona asingeweza kustahimili ndani ya yule samaki kwa muda wa siku tatu za mchana na tatu za usiku. Aliomba na hatimaye alikufa kama Kristo alivyoomba na hatimaye akafa. Alifufuka kutoka tumboni mwa samaki kama Kristo alivyofufuka kutoka kaburini mwishoni mwa siku tatu za mchana na tatu usiku na Yona alitapikwa nje kwenye nchi kavu pale ambapo Mngu alitaka awe.

 

Yona Sura ya 3

Hapa tunaona amri ya pili kwa Yona na mara hii anatii. Mlolongo wa matukio ya nyakati ni muhimu kwenye huduma au misheni hii ya Kristo.

 

1 Neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili, kusema, 2 Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa; ukaihubiri habari nitakayokuamuru. 3 Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu.

 

Ni mfululizo huu wa matukio ndipo Ninawi kwa mwendo wa siku tatu kuingia ndani, Yona anaingia mjini siku moja na kisha akahubiri kwa siku mbili akitangaza kwamba zimebaki siku arobaini tu za wao kutubu au vinginevyo wataangamia.

 

4 Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa. 5 Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo. 6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu. 7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng'ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji; 8 bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake. 9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe?

 

Ndipo mji wote ukatubu. Hili ndilo Yona aliloiogopa sana. Tukio hili lilifanya taswira ya huduma ya Kristo. Mwandamano wa matukio ulikuwa hivi:

Siku ya 1=Mwaka wa 1. Huduma ya Yohana Mbatizaji

Iliyoanza mwaka 27 BK na Kristo alikuja kubatizwa na kuchagua wanafunzi wake.

Siku ya 2 na ya 3 = mwaka wa 2 na wa 3. Kristo anafundisha kuanzia baada ya Pasaka ya mwaka 28 BK wakati Yohana Mbatizaji alipokuwa amefungwa hadi Kristo alipouawa wakati wa Pasaka ya mwaka 30 BK na kufufuka na kunena na kanisa alipofufuka.

 

10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.

 

Wale waliotubu ambao walikuwa ni watu wote wa Ninawi walinusuriwa na Mungu. Walipewa siku arobaini na walitubu kwa haraka. Yuda wamepewa miaka arobaini na hawakutubu na waliangamizwa na kutawanyishwa tangu mwaka 70 BK.

 

Jambo hili lilimkasirisha Yona na aliudhika sana kuona kuwa Mungu amewasamehe watu walewale ambao wangefanyika kuwa kifaa cha kuiangamiza Israeli upande wa Kaskazini na kuwaondoa waende mbali kupita Araxes.

 

Mungu hakujuta kwa kuwa yeye Anajua kila kitu na anatuliza katika maafa au adhabu na mapatilizo. Anasema alikuwa anakaribia kuwaletea maafa au kufanya hivyo.

 

Yona Sura ya 4

Hapa tunaona kuwa Yona yupo kwenye majadiliano na Yahova wa Israeli kwa niaba ya Mungu wa Pekee wa Kweli. Anamkumbusha Mungu kuhusu yale aliyoyasema kumwambia yeye alipokuwa bado yuko huko Israeli na sababu iliyomfanya yeye akimbilie Tarshishi.

 

1 Lakini jambo hili lilimchukiza Yona sana, naye akakasirika. 2 Akamwomba Bwana, akasema, Nakuomba, Ee Bwana; sivyo hivyo nilivyosema, hapo nilipokuwa katika nchi yangu? Hii ndiyo sababu nalifanya haraka kukimbilia Tarshishi; kwa maana nalijua ya kuwa wewe u Mungu mwenye neema, umejaa huruma, si mwepesi wa hasira, u mwingi wa rehema, nawe waghairi mabaya. 3 Basi, sasa, Ee Bwana, nakuomba, uniondolee uhai wangu; maana ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.

 

Yona alija kutokana na vitabu vya Torati (Kutoka 34:6; Hesabu 14:18-19); Daudi alijua (Zaburi 86:5); Hosea alijua (Hosea 11:8-9); Yoeli alijua (Yoeli 2:13) na Mika alijua (Mika 7:18).

 

Angeweza kufa kuliko kuishi. Hakuwa na furaha kuona kuwa hakuwa nabii aliyefanikiwa. Kwa kuwa anaiokoa Ninawi aliipenda Israeli lakini imani yake kwa Mungu ilipasa iwe kubwa zaidi.


4 Naye Bwana akasema, Je! Unatenda vema kukasirika?

 

Kisha Mungu akamkemea kwa kuona kwake mambo kama mtoto mdogo. Hata hivyo, alikanganywa akiwa kama nabii kwa watu wake.

 

5 Ndipo Yona akatoka mjini, akaketi upande wa mashariki wa mji, akajifanyia kibanda huko, akakaa chini yake uvulini, hata aone mji ule utakuwaje.

 

Hakuwapa tumaini kwamba Ninawi ingerudia kutenda dhambi na kuangamia. Hatimaye akaketi kwenye mretemu aone kitakachotokea na kuipata Ninawi. Hatimaye Mungu akamlinda alipokuwa akingojea na kutumia hilo kama mfano kwa Yona.

 

6 Na Bwana Mungu aliweka tayari mtango, akaufanya ukue juu ya Yona, ili uwe kivuli juu ya kichwa chake, na kumponya katika hali yake mbaya. Basi Yona akafurahi sana kwa sababu ya ule mtango. 7 Lakini siku ya pili kulipopambazuka, Mungu akaweka tayari buu, nalo likautafuna ule mtango, ukakatika. 8 Basi ikawa, jua lilipopanda juu, Mungu akaweka tayari upepo wa mashariki, wenye hari nyingi; jua likampiga Yona kichwani, hata akazimia, naye akajitakia kufa, akasema, Ni afadhali nife mimi kuliko kuishi. 9 Mungu akamwambia Yona, Je! Unatenda vema kukasirika kwa ajili ya mtango? Naye akasema, Ndiyo, natenda vema kukasirika hata kufa. 10 Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja; 11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana?

 

Upepo huu ulikuwa kama ruach kama roho. Kwa hiyo, mfano wa mmea na Ninawi ulitumika kuonesha rehema za Mungu. Angepaswa kwa hiyo kuwa angejua kwamba kama Israeli wangelitubu wasingeweza kuchukuliwa utumwani ng’ambo ya nchi yao.

 

Kama tulivyoona kutoka kwenye jarida la Kuanguka Kwa Misri (Na. 036), mnamo mwaka 732 KK Mwashuru Tiglath Pileser III aliitwa Dameski na kuifana Israeli na Yuda kuwa ni nchi za kukusanya kodi. Mwaka 729 KK Tiglath Pileser III aliungana na Babeli na ShalmaneserV (tangu kwama 724-721 KK) aliitwaa Israeli mwaka 722 KK. Mrithi wake Sargon II aliyafukuza makabila kumi.

 

Mwaka 710 KK Wacimeriani waliishambulia msafara wa Wacaucasi kutoka kwenye kingo za urusi. Waliuangamiza Urartu na ufalme wa Frigia huko Anatolia. Mwaka 705 KK Sargon II aliuawa alipokuwa akipigana na Wacimeriani. Mwaka 701 KK jeshi la Sennikarebu liliondoka pasi kutegemewa kutoka kwenye kampani ya kuwaadhibu katika Yuda. Mwaka 720 KK Sargon II alianzisha mji mkuu wa dola ya Ashuru huko Dur Sharrukinor Ngome ya Sargon. Mwaka 701 KK Sennikarebu aliondoka huko Fort Sargon na kuifanya Ninawi mji mkuu tena. Kwa hiyo kuna kinachoonekana kuwa ni kutafakari kupya kuhusu unabii kuhusu Ninawi.

 

Shahidi wa Yona alikuwa na miaka arobaini tangu kutawala kwa Yeroboamu II (mwaka 793-775) hadi Uzia (mwaka 775-753) na tawala za pamoja na jumla kilikuwa ni kipindi cha miaka arobaini pamoja na kipindi cha matazamio cha ziada kutoka mwaka wa tatu wa utawala wa Uzia takriban mwaka 772-732 hadi hadhi ya Utozaji kodi ulipokuwa wa Waashuru, Israeli walikwenda utumwani kwa Waashuru kwa kipindi cha kutoka mwaka 722 KK ambacho kilikuwa ni wastani wa miaka 40 na kisha miaka 50 au yubile moja tangu unabii wa Yona kwa Israeli. Yona alipaswa ajfunze kutoka hudum yake ya Ninawi na kuwaonya Israeli kuhusu kile Mungu alichowafanyia na kile kilichopasa kuwatokea Israeli lakini hawakusikiliza kama Yuda walipoacha kusikiliza wakati wa kipindi chote cha miaka arobaini walichopewa watubu (soma pia jarida la Mchanganuo wa Ratiba ya Nyakati (Na. 272)).

 

Kama Yuda wangetubu wasingeweza kuangamizwa pamoja na Hekalu mwaka 70 BK na Yuda wakatawanyishwa.

 

Yuda walipewa miaka 40 kamili kwa hesabu za mwaka mmoja kwa siku moja kulinganishwa na iliyopewa Ninawi. Ninawi ilitubu lakini Yuda hawakutubu. Walimuua Kristo mnamo siku ya 14 Abibu Mwaka 30 BK na Yerusalemu ukazingirwa na majeshi na kuhusuriwa siku ya 1 Abibu 70 BK na Hekalu likateketezwa huko Yerusalemu na Hekalu la Heliopolis huko Misri lilifungwa siku ya 1 Abibu 71 BK.

 

Katika kila tukio Mungu aliwapa Israeli na Yuda miaka 40 ya kutubu ambayo ni kiwango cha wastani na hawakutubu. Tangu Kristo na kanisa lilipoanzishwa, Mungu ameipa dunia yubile 40 tangu mwaka 27 BK hadi 2027 ya kutubu na hawajatubu na hawatatubu na dunia itaenda utumwani chini ya Masihi na Hukumu kwenye Milenia wakati wa Mapumziko ya Sabato ya Mungu chini ya Kristo.

 

                                                            q