Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[029]
Kondoo wa Mungu
(Toleo La 3.0
19940521-20000617-20071220)
Jarida hili
liliandikwa na mchungaji aliyekuwa anawafundisha kondoo na mbuzi kwa kutumia
filamu ya familia iliyopendwa na kusifiwa sana na iliyoshinda tuzo iliyojulinama
kwa jina la Babe. Anafundisha na kutathimini masomo au mafundisho
yanayohusiana na na dume la kondoo na ujumbe wa biblia kutoka uumbaji. Kazi na
jukumu la kondoo na mchungaji yameelezewa pia. Mwenendo wa kondoo na matarajio
ya mchungaji yameendelezwa. Tofauti iliyopo kati ya Wamisri na imani za kibilia
na mandondoo ya kiroho yanaonyeshwa.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1994 Storm Cox, ed. 2000, 2007 Wade
Cox)
(tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kondoo wa Mungu
Kutoka wakati
wake wa ujana mwandishi alikuwa anaelezea kuhusu maisha ya msimamizi au meneja
wa kondoo. Tangu ujana wake na kuendelea kwa kupitia chuo kikuu, na hatimaye
kazi zilizofuatia baadae akiwa kama mkufunzi wa wanyama (wa kondoo na mbuzi
kwenye sinema yake ya Babe), alishiriki
kwa karibu kwenye usimamizi na upandishaji wa madume ya kondoo kwa ujumla,
pamoja na shamba lingine la wanyama. Uzoefu wa kazi hii ulimfanya atafakari
utaratibu wa mbinu za wafugaji na wakulima za kibiblia, ambao walionekana kuwa
walikuwepo na waliishi kama wanaume nyakati za Agano la Kale. Uzoefu kama huu
ulimpelekea mwandishi kufikiri kuhusu maana ya waliowatumia kwa kiasi kikubwa
mfano elekezi wa kondoo na mchungaji, na kwenye jarida hili anajaribu kuhusisha
mambo yalivyo kwenye Kanisa la Mungu.
Katika siku ya tano
ya uumbaji, Mungu aliamuru kwamba nchi iwe na viumbe hai.
Mwanzo 1:24-26 Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo. 25 Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Neno la Kiebrania
kuhusu wanyama wa porini ni miqneh (SHD 4735), ambalo linamaanisha
pia milki, mali zilizonunuliwa au akiba. Neno hili linamaanisha pia kundi la mifugo na mifugo, ambalo hilo linahusisha kondoo, mbuzi, mifugo na wanyama wa
miguu minne wengine wote (wenye miguu mingine) wanyama ‘safi’. Walitengwa kama
wanyama ili watumike kwa kuliwa. Neno la Kiebrania la kondoo ni tso'n (SHD 6629), ambalo maana yake ni kondoo, mbuzi na ndama wa ng’ombe, kama
neno hili halitakuwa kaseb (SHD 3775;
Mwanzo 30:32,33,35; Walawi 1:10; 7:23; 22:19,27; Hesabu 18:17; Kumbukumbu la
Torati 14:4), ambalo litakuwa na maana ya moja kwa moja kuwa kondoo kama
tunavyowajua kondoo walivyo leo.
Raheli (7354) maana yake kusafiri na inamaana sawa na ole. Linaendana
kuwataja majike ya wanyama na linaendana na neno kebes (3532) kwa madume.
Neno la Kiebrania
kuhusu mifugo ni behemah (929), ambalo
maana yake ni wanyama wa miguu mine. Suala hapa sio lingine ila ni neno kaseb, ambalo linatumika kwenye aya nane
peke yake, maneno yanayotumika kwa ajili ya ng’ombe, mbuzi, pamoja na makund
mengine yote ya wanyama safi na wa miguu minne walio sawa. Ni hivyohivyo,
kwenye lugha ya Kiyunani, neno linalotuika kuita kondoo lililotumika kwenye
Agano Jipya lote ni probaton (SGD 4263), neno la Kiyunani lililo
sawa na neno la Kiebrania ni behemah, ambalo kama ilivyoelezwa, maana
yake ni mnyama aliyetengwa kwenye wanyama
wa miguu minne na pia linawahusu wanyama wote najisi.
Kuamua maeneo
maalumu kumetumika kwenye aya yoyote iliyotolewa ni uamuzi kwa niaba ya
mtafsiri, kutegemea na lengo la Maandiko Matakatifu.
Ng’ombe wote,
kondoo na mbuzi wanahusiana kimaumbile ya uzao, kuwa wote ni wa kundi la jamii
ya ki-bovidae. Tabia za wanyama wa
jamii hii ni kwamba wao huwa:
1. 1. Wanaocheua,
2. 2. Wana kwato zilizochanika katikati na,
3. 3. Wote wana pembe zenye mbugu.
Kila moja
inafikia masharti au vigezo vya kibiblia vya usafi (wa kimaandiko), kama
ulivyoelezwa kwenye Mambo ya Walawi 11 na Kumbukumbu la Torati 14, na kwa hiyo
wanaweza kuliwa.
Kata
tunavyosoma kwenye Mwanzo 1:26, mwanadamu alipangiwa na Mungu tangu uumbaji
awatawale wanyama. Kwa iyo, mtu anaweza kudhania kuwa ni sehemu ya wajibu wetu
kufanya hivyo kwa utaratibu sahihi. Kwa hiyo, kuwepo kwa mchungaji lilikuwa ni
jambo lililopangwa tangu mwanzo mwanzoni mwa kila jambo.
Neno la
Kiebrania kuhusu mchungaji ni ra'ah (SHD 7462) na linamaana au
kuelezwa maana yake kuwa ni:
... kuangalia au kuchunga kondoo, yaani kuwalisha; kuwaelekeza. Kuwapeleka malishoni (kuwashwa au mtini); kwa ujumla, kutawala kwa kuwa mfano, kushirikiana nao (kama marafiki):-* kuwaonya, kuwa mshirika, kushirikiana nao, kuwala, kula, kumtendea mbaya, lisha, kuwatumia kama marafiki, kufanya urafiki naye, kuwatunza (kondoo) (mtunza kondoo), mchngaji, + banda la kukatia manyoya, mchungaji, kustaajabisha, kupoteza.
Neno Ra'ah linatokana na neno ra', ambalo maana yake ni uadui,
mateso, mbaya, maafa na uovu. Ra'
maana yake ni kuharibu au kuangusha chini, ni kama neno ra'ah linayo linayo linayomaanisha kushikamana pamoja dhidi ya uadui. Neno ra'ah ni la kike na la kiume lake ni ra' (SHD 7451, kutoka kwenye 7489), na
hivyo ni kinyume cha kidokezo.
Kwenye
Kiyunani, neno hili ni poimen (pr.
poy-mane; SGD 4166), ambalo lina maana tu ya mchungaji wa mifugo au mchungaji
wa kiroho.
Kwa hiyo tunaona
kutoka kwenye Biblia historia ya mahala pa mchungaji na usimamizi wa mchngaji
na usimamizi wa wanyama walio safi ambao Mngu amewapa wanadamu na kuwaruhusu
kuwala. Wanyama safi ni zawadi kutoka kwa Mungu aliyotupa sisi kuwa ni chakula
chetu, ili tuishi juu ya Nchi au Dunia yake hii ndani ya mfumo na utaratibu
aliouweka kwa mafanikio yetu. Na ndiyo saababu sadaka ya Abeli aliyomtolea
Mungu ilimpendeza sana kuliko aliyoitoa Kaini machoni mwa Bwana, ni kama dhambi
inavyohitaji kufunikwa au kuondolewa kwa dhabihu ya damu, na ilikuwa ni taswira
ya damu ya Kristo (kama Mwanzo 4:3-5).
Katika nyakati za
Biblia, kama ilivyo leo, kazi kubwa ya kondoo ilikuwa ni kutoa au kuzlisha sufi
(Walawi 13:47-48; Ayubu 31:20), nyama (1Samweli 14:32), huficha (Kutoka 25:5; Waebrania
11:37), maziwa (Kumbukumbu la Torati 32:14; Isaya 7:21-22), na mazao mengi
mengineyo kama vile pembe kwa ajili kutengenezea vikapu na zana za muziki (1Samweli
16:1; Yoshua 6:4).
Katika siku za
zamani, sufu zilikuwa ni bidhaa ya thamani ilikuwa muhimu sana kibiashara.
Tunaona na kujua hivyo kutoka kwenye 2Wafalme 3:4 kwa Meshaki, Mfalme wa Moabu,
ilimpasa kumlipa Mfalme wa Israeli sufu kutoka kwenye mamia elfu ya kondoo zake
kila mwaka.
Kondoo
walichukuliwa pia kuwa ni utajiri wa mtu. Kwenye Biblia mtu alionekana kuwa
amebarikiwa kama alionekana kumiliki makumi au mamia elfu ya kondoo (Zaburi
144:13).
Kutoka kwene
Biblia, tunaweza kupata uelewa wa tabia na asili ya mnyama. Katika 2Samweli
12:3 tunaona kwamba kondoo walionekana kuwa ni viumbe wenye moyo wa kupenda. Kutoka
kwenye Isaya 53:7, Yeremia 11:19 na Yohana 10:34, kondoo wanatajwa kuwa ni
viumbe wapole na wasio na matata. Kwenye Mika 5:8 na Mathayo 10:16 kondoo
wanaonekana kuwa hawana ulinzi, na ni la muhimu sana, kwenye Hesabu 27:17,
Ezekieli 34:5 na Mathayo 9:36 na 26:31 tunaona kwamba kwa kweli walikuwa wanalindwa
wakati wote na waliapewa uangalizi.
Kwenye Agano la
Kale, wakati mchungaji na kundi lake wanapoelezewa au kutajwa, kwa kawaida ilikuwa
ni kwa maana ya kawaida. Kwenye Agano Jipya, hata hivyo ilikuwa inamaanisha kwa
lugha ya fumbo na mifano.
Kwenye kitabu cha
fasihi cha International Standard Bible Encyclopedia(ISBE) kwenye
ukurasa wake wa 464, kinainukuu Zaburi 95:7:
Na sisi tu watu wa
malisho yake [Mungu], Na kondoo za mkono wake.
Na kinaendelea kwa
kusema:
Maneno haya yaliyopangiliwa yanayotumia mifano ya kibiblia na yanayosisitiza kuelezea utegemezi wa wanadamu kwa Mungu kwa uwepo wao, kudumu kwao kwa nasibu, na mambo yao. Kitu chenyewe hutoa utambulisho wa kufurahisha kwa namna zote mbili, yaani kwa mahitaji ya mwanadamu kama kumbe na kwa utoshelevu wa Mungu akiwa kama muumbaji na mtoaji wa mahitaji ya watu wote. (ikifanya rejea kwenye 2Samweli 24:17, 1Nyakati 21:17, Zaburi 78:52, Ezekieli 34:31, Zekaria 11:4-17, 13:7 na Yohana 10:10-15).
Kutoka kwenye hii
tunaona mlingano uliopo kati ya mahusiano ya moja kwa moja na yakimfano uliopo
kati ya kondoo na watu wa Mungu.
Mishangao mingi
iliyopo kwa watu wengi, ni kwamba kondoo kwa kweli ni mnyama mwenye akili
nyingi. Kondoo wanafana mambo yao kimakosa na kwa kuchanganyikiwa kwenye wakati
yanapotokea machafuko na wanyama wengine, ni kama walivyo na uwezo mdogo wa
kimbinu kwa maeneo mengi ya nchi yaliyo mbali. Kutokana na hayo, kondoo
wanakuwa hawako salama na wanakuwa ni wanyama waoga. Katika siku zetu hizi,
mbinu za kiutawala au kusimamia makundi makubwa ya kutumia mbwa na pikipiki
peke yake, huongeza hali ya kutoogopa mioyoni mwa wanyama.
Siku za zamani,
usimamizi ulitumia mbinu tofauti kabisa. Mchungaji aliwaongoza kondoo mwenyewe akiwa ametangulia mbele yao. Kondoo walimsikia
sauti yake na kumfuata, salama mwene uwepo wake. Wakati kondoo wakiwa salama
watafanya yale yanayoonekana kama ndoto za mchana na watazishangaa sana, na kwa
dhahiri kile kinachotokea karibu yao. Mwanadamu anaweza kuwakamata kondoo hawa
kirahisi wakiwa kwenye majani au nyasi nyingi.
Kondoo wanaona,
wanasikia, wanafikiri na kujifunza, kama wanavyofanya wanyama wengine wote.
Kila mnyama anakiwango cha namna tofauti cha uelewa, kwa kiwango kikubwa kama
alichonacho mwanadamu. Kama mfundishaji wa kondoo, mwandishi anagundua kwamba
sio wanyama wote waliweza kuzipata baadhi ya tabia fulani walizotarajiwa kuwa
nazo. Kondoo wengine walichukua kuda mrefu kubadilika na kuchukuliana nazo.
Wengine walielewa na kuchukuliana nazo kwa haraka. Mara nyingi ilitegemea
uzoefu wao wa zamani na wanadamu na uzoefu uliopo kwenye mazingira ya mafunzoni.
Maranyingi
wanapokuwa na hamu zaidi ndipo mnyama aliyejitoa zaidi alivyoweza kujifunza na
hivyo kupokea thawabu au zawadi yake yam lo mtamu. Kwa ‘hiyo, heri wenye njaa
na kiu ya haki’.
Inapendeza sana
pia kujua kwamba kondoo aliyefunzwa anaporudishwa kwenye mazingira ya kundini,
kutokana na maendeleo yake, atafanyika kuwa kiongozi kundini na wengine
waliobakia watamfuata. Nasi ndipo tutafanyika kuwa ‘wavuvi wa watu’.
Iwapo kama kondoo
atatendewa vizuri na wanadamu, basi atakuwa na uwezo mkubwa sana wa kufikiri na
kuhisi mambo, na hivyo ataweza kuwa na kuwasiliana kirahisi. Kama kondoo
atakuwa ametendewa vibaya na kikatili na mwanadamu, ndipo atakuwa muoga na hatapenda
kuwasiliana. Hata baada ya kondoo kufundishwa kwa miezi mingi, bado anaweza
kukimbia na kutoroka iwapo kama mkufunzi atakuwa na moyo wa wasiwasi na
asipende kuwasiliana hata baada ya kutoroka kwake, kama mfundishaji alikuwa na
moyo wa wasiwasi na hajatulia au kama alisimama juu ya mnyama na kumkimbiza kwa
mwendo kasi sana. Tulifundishwa kuwa tumuendeshe tu mnama kwa kuelekea mbele na
kwa usawa wa macho, tukimpeleka kidogokidogo na kwa upole. Kama mfundishaji
akiwa na moyo mbaya na hajatulia ilikuwa ni vyema asimfundishe mnyama hadi atakapokuwa
na moyo mwema na uliotulizana. Ni rahisi kuahirisha wiki za kazi kwa kumpa
mnama uzoefu asi, hata kama mnyama aliogopa kwa bahati mbaya.
Kutokana na hili
tunaweza kuhitimisha kwamba kondoo ni wanyama makini, mwangalifu na mwenye
tahadhari. Wana uwezo usioweza kukadiriwa wa kukumbuka na kondoo aliye makini
zaidi atajifunza kwa masuala ya kazi au majukumu ya kama vile ya kusafiri kwa
kupitia kwenye njia zene vikwazo, kupelekwa kwenye alama, kurudi kwa kuamriwa
na pia kukwea kwene vizingiti.
Kondoo ni wanya
salama na hivyo hawawindi wanama wengine. Wanaridhika kwenye mazingira salama,
na hawana madhara na sio watukutu. Mahitaji yao ni rahisi na wanatoa sauti tu wanapokuwa
na njaa au wanapoiona au kuhisi hatari.
Kondoo
hushikamana na hukaa kwa kukaribiana ili kujilinda. Wakati kitu cha kusikitisha
kinapomtokea kondoo, kama vile ugonjwa au kuondolewa (yaani kutoka au
kuharibika mimba), ndipo kondoo mwingine jike watamtunza yule mtoto iwapo kama
ile hatari haitakapokuwa kubwa sana. Mara nyingi, kondoo mwenye mimba au mnene
kwa mafuta kuwa mengi anaweza kujiburuza kwa kutumia mgongo wake na hataweza
kurudi nyuma kwa miguu yake. Kwa hiyo anategemea matunzo ya mwanadamu ili
kumgeuza asimame kwa miguu yake. Ndege wadogo sana wanaweza kumuua kondoo iwapo
kama watampiga kwa nguvu au kumjeruhi. Kukimbia ni mbinu pekee ya kujilinda ya
kondoo. Ni mnyama mpole na mpenda amani kiasi hicho, na anayetegemea kwa ujumla
urafiki wake na mwanadamu.
Biblia inaelezea kuhusu
kondoo kwamba husikiliza na kuisikia sauti ya mchungaji (Yohana 10:3), na wachungaji
huwaita kondoo zao kwa majina (soma jarida la Anawaita kwa Majina: Somo la Zaburi 23 (Na. 18)). Hii inaonyesha jinsi wachungaji na watu
wote wanavyoweza kufanya, kwa kupitia utegemeano kati ya wanya wawili, unafanya
ongezeko la kimahusiano na aina zote za wanyama wa porini kama sehemu ya mbinu
zao za kiusimamizi. Na hii ndiyo sababu inayowafanya wanadamu wapende kufuga
wanyama wa kucheza nao sana.
Inapasa kukumbuka
kuonyesha kwamba Kansa lilitumiwa kwa mrengo wa kundi, na sio kwa muktada wa
wanyama wa kufuga, bali ni kama kundi ambalo ninatenda kazi zake vizuri kama
kundi lililoungana lote na kwa pamoja.
Mmoja anaweza
kwenda mbele, lakini kwa hakika tunaweza kuusifia mlingano wake na Wakristo na
kuiona sababu ufananishaji wa mchungaji wa kondoo ulitumika—kwa amani, bila
madhara, kwa muunganiko, na kwa tahadhari kwa kuwahudumia wachungaji.
Kujua tabia ya kondoo
kunaturuhusu na kutufanya tuunge mkono matendo na tabia na shughuli au wajibu
na umuhimu wa kazi za mchungaji kwa zaidi sana.
Ili kulijua hilo,
yatubidi kwanza kugundua au kuujua umuhimu wa majukumu yaliyowekwa kwenye
vichwa vya wachungaji. Kama tungekuwa na kiasi kidogo tu cha chakula cha
kujilisha sisi wenyewe na familia zetu kwa kipindi cha muda uliowekwa na pasipo
kile tunachoweza kushinda na njaa, ndipo kwa hakika tungetumia kila namna zote
zilizopo za kutetea namna zetu za akiba, na ingewezekana kwa mtu fulani kuvunja
nyumbani mwetu na kujaribu kuiba.
Haya makundi
yalikuwa ni damu ya kudumu ya familia za wachungaji. Makundi haya yalilisha na
kuwatunza watu wote, wakiwemo wajane, yatima na walemavu. Kama wanyama
watliibiwa au kufa ndipo hawakutoa vya kutosha kwa wote, na kwa hiyo kazi ya
kuwa mchungaji kwa kweli ilikuwa kubwa.
Hatua nyingine
nay a muhimu kuijua kabla hatujaendelea mbele ni nia au mtazamo wa kwamba
utaratibu wa kuchunga unahusishwa.
Mwanzo 46:34 34
Semeni, Watumwa wako tumekuwa wachunga wanyama tangu ujana wetu, na hata leo,
sisi, na baba zetu; mpate kukaa katika nchi ya Gosheni; maana kila mchunga
wanyama ni chukizo kwa Wamisri.
Desturi ya
Kiebrania ya kufuga kondoo ilichukiwa na mawazo ya Wamisri. Namna ya kifikra ya
Warumi ilieleweka nab ado inaeleweka kwenye Biblia yote likiwa ni wazo lenye
mchakato unaopingana na Mungu. Wamisri walikuwa matajiri wa taifa la
kibiashara. Walikuwa ni mabepari (kwa maneno mengine wenye kujilimbikizia
mali), walioutafuta utajiri na mali kwa mtindo wa vitu vya kimwili. Dhana hii
uliwapelekea kuwafanya Israeli watumwa. Walifanyika kuwa matajiri kutoka kwenye
kazi zao na kwa kuwadhuru wa mataifa mengine. Tumeona hilo kwenye vipindi vya
karibuni zaidi pamoja na kuwafanya Waafrika kuwa watumwa wa Wamarekani, miongoni
mwa mataifa mengine. Sababu iliyopelekea wachungaji wachukiwe ilikuwa ni kwa
kuwa, kwenye usimamizi wa makundi yao na familia na uongozi wao kwa ujumla,
walieleza kwa wazi mtindo wa kiuongozi wa kiutumishi wa kiserikali au uongozi.
Huu ni utaratibu kinyume kwa Wamisri, na kwa hiyo ni ushahidi kamili dhidi ya
utaratibu wao.
Mfundishaji wa wanyama
anafanya kazi kwa masaa mengi kwa kila siku ili kuona kwamba mahitaji ya
wanyama yanapatikana. Anafanyika kuwa mtumwa kwao, na ili kuweza kupata kutoka
kwao inalazimu kutoa muda mwingi na nguvu. Wachungaji, ili kuwawezesha watu wao
wale, inawapasa kufanya kazi kwa bidii na kujifanya watumwa kwenye makundi yao,
hata kama itamaanisha kufa (Yeremia 49:19; Amosi 3:12; tazama hapo chini).
Wachungaji
walikuwa ni watumishi tu wa watu wao,
ni kazi inayohitaji unyenekevu mkubwa, kinyume na majivuno na kiburi cha Wamisri.
Kutoka kwenye
Biblia tunajua kwama Yesu Kristo ndiye Mchungaji wetu, nasi tu kondoo wa kundi
lake. Hata hivyo, hata sisi tumekusudiwa kuwa wachungaji kama alivyo Kristo.
Hili limeelezewa kwenye Warumi 8:17, ambapo tunasoma hivi:
na kama tu watoto,
basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa
pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
Kutokana na hili
tunaweza kuhitimisha kwamba ni wajibu wetu kujifunza kuwa wachungaji kama Yesu
alivyo mchungaji. Mfano wa kulinganisha ilitumika rasmi ili kwamba watu – ambao
waliishi siku za nyuma kutoka kwenye historia ya umilikaji ardhi, kama tutakavyokuwa
sisi kwenye kipindi cha Milenia – tungeona kanuni na mchakato wa uongozi au utawala
wa kiroho kwenye mpangilio wa kawaida wakimwili ambao ulikuwa ni sehemu ya
uwepo wao wa kila siku. Leo, wengi wetu hatuna starehe au utulivu ule.
Ni nini kazi ya
mchungaji?
Kwa hali halisi
na ya kweli, matendo ya msingi ya msimamizi wa shamba kwa maana ya kutunza
konzoo zake linatuama kwenye makundi makuu mawili. Nayo ni:
1. 1.Lisha na
kuwanywesha maji, na
2. 2. Linda na ganga
Hii
ilikuwa, na bado inakuwa, shughuli ya wachungaji.
1. kulisha na kunywesha maji
kondoo
Ulishaji wa
kondoo ni wajibu mkubwa na wa muhimu wa mchungaji. Anapaswa kutiliwa maanani
aina ya chakula kilicho na faida na cha mana zaidi kwa mnyama na kinachotoa
faida ya virutubisho kwake.
Kazi
ilikuwa ni kuwanenepesha au kuwaandaa kondoo kwa kuliwa au kumtumia, kama
sadaka ya kukubaliwa kwa Bwana – kama tutatilia maanani mambo yaliyo kwenye
mrengo wa kibiblia. Huu ni msingi wa sababu iliyosababisha hasira ya Mungu kwenye
kitabu cha Malaki, ambako korban ya
Mungu inaaminika kudharauliwa; tena, ni wajibu wa wachungaji wenyewe kujikita
na kuandaa kile Mungu alichowapa kukisimamia. Biblia iko wazi kufundisha au
kuelezea jukumu la mchungaji. Mchungaji anatakiwa kutafuta malisho kwa ajili ya
kondoo zake (Ezekieli 34:2,9,13) na maji kwa kundi lake. Kondoo wanahitaji maji
yaliyotulia (Zaburi 23:3). Kondoo, akiwa ni mnyama mwenye hisia kali na makini,
hatakunywa tayari kutoka kwenye mito inayotiririsha maji kwa kasi. Mtu yeyote
aliyejaribu kupitisha au kuyavusha makundi makubwa kwenye mito anaweza kuwa ni
shuhuda wa jambo hili. Inaweza kuwa ndefu, kuchosha na wanachanganyikiwa mara
nyingi.
Wakati maji
yakiwa hayapo karibu na wao, ndoo ya ngozi au chombo cha kukatia mkate
lilitumika (Mwanzo 30:38; Kutoka 2:16). Hii ni kazi ngumu na inahitaji umakini
kama tutatilia maanani kwamba kila kondoo alihitaji kupewa maji angalau mara
tatu kwa siku, pamoja na masaada wa zaida wakati wa alasiri kwenye kilele cha
wakati wa joto la siku. Hii imeelezewa kwa ufasaha kwenye Mwanzo 29:2-10.
Shughuli na
utendaji mkuu ni kuwalisha kondoo zake. Tunajua hilo kutoka kwenye Yohana
21:15-17.
Yohana 21:15-17 Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. 16 Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. 17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.
Kristo alikuwa
anasisitiza kuhusu kuwalisha kondoo wake. Ilikuwa hapa kwamba huduma iliamriwa
ieneze neno la Kweli kama lilivyoelezewa kwenye Biblia. Kama wachungaji wema
walivyotakiwa kuwalisha kundi, ndivyo pia huduma inatakiwa kulieneza Kweli kama
malisho ya kondoo au kundi. Ni wajibu na kazi yetu kubwa kuieneza Injili ya
Kweli. Kama tutakuwa hatufundishi Ukweli kama Mungu anavyotutaka tufanye, basi
tutakuwa sawa na wezi. Kristo anatuambia jambo hilo kwenye Yohana 10:1.
Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang'anyi.
Yohana 10:10 inasema:
Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu;
Mwizi
anayeongelewa hapa anatudanganya na kutuibia taji yetu ili kwamba tusiungane na
Kristo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu, na ndipo tustahili sehemu yetu tukiwa
kama ni sehemu ya wteule.
2. Kuwalinda na kuwaganga kondoo
Kama
tulivyoelezea mapema, kazi ya wachungaji ilikuwa ni ya muhimu sana; uhai wa
watu wao ulikuwa vichwani mwao. Kwa hiyo, kuwalinda kondoo wao, ilikuwa ni sehemu
muhimu ya kazi hii.
Yeremia 49:19 Angalia, atapanda kama simba toka kiburi cha Yordani juu ya malisho yasiyonyauka; lakini nitamkimbiza ghafula ayaache; na yeye aliye mteule nitamweka juu yake; maana ni nani aliye kama mimi? Tena ni nani atakayeniandikia muda? Tena ni mchungaji yupi atakayesimama mbele zangu?
Maneno ya msingi hapa
ni samba, mchungaji na kusimama. Aya hii inamtumia mchungaji
kama mfano wa nguvu. Ni sawa na ilivyo kwenye Amosi 3:12 tunasoma hivi:
12 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa …
Uelewa wa jmla hapa
ni kwamba mwandishi anatilia maanani jukumu la mchungaji, akihusianisha na
kondoo zake, kuwa hivyo ndipo angewaburuza kondoo wake nje yam domo wa samba
kwa mikono yake mitupu kama ikihijika kuwa hivyo. Kwa kweli, usalama wa kondoo
ulichukuliwa zaidi sana kwa kumaanisha kama tungalivyoweza kudhania kwanza. Kwa
Daudi, tunajikusanyia tena habari ya mchungaji wake aliyedai kumuua mnyama wa porini
kwa mikono yake iliyokuwa tupu ili kuwaokoa kondoo wa Daudi. Licha ya ujumbe wa
moja kwa moja wa hadithi hii, dalili iliyoko kwenye kusudi hili ni ukubwa wa
wajibu wa kuwa mchungaji.
Kazi kubwa kuliko
zote ya muchungaji ni kulilinda kundi. Leo tunafaidika ya kitekinolojia kama
vile kuna zana za kuzungushia ukuta. Bunduki za kuwafukuzia au kuulia wanyama
wa porini, tochi za kumulikia wanyama nyakati za usiku na kwenye maeneo ya
dunia yenye watu wengi kuna mipaka iliyowekwa mwa mifumo iliyopangiliwa vizuri.
Hatahivyo, jukumu la kuliangalia kundi kwa kila siku kuwatazama wagonjwa na
wenye ulemavu unabakia kuwa ni muhimu kama ilivyo siku hizi na ni muhimu kuliko
ilivyowahi kuwa huko kabla. Kazi hii ilikuwa ni ngumu sana kwa hiyo, lakini
majukumu na wajibu yalijulikana. Bila mchungaji, kondoo wanakosa msaada. Hebu
na tusome Hesabu 27:17.
17
atakayetoka mbele yao,
na kuingia mbele yao; atakayewaongoza watokapo, na kuwaleta ndani; ili mkutano
wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji. …
Wazo hilohilo
limeelezewa kwenye 1Wafalme 22:17, 2Nyakati 18:16, Zekaria 10:2, Mathayo 9:36 na
Marko 6:34.
Kila usiku wachungaji
waliyapeleka makundi kwenye kile kinachoitwa zizi la kondoo (Mwanzo 31:39; 1Samweli 17:34). Hili zizi la kondoo
inaelezewa kuwa ni kama:
Ni mahali palipofungwa vizuri kwa kuzuia hatari na misukosuko ya usiku inayotokana na wanyama wakali, na wezi au majambazi. Wakati mwingine ukusanyaji wa pamoja ulitumiwa kwa idadi wachungaji kwa uwingi au makundi na uliangaliwa na mtu mmoja kwa usiku wote, kisha kila mchungaji huwaita kondoo wa kundi lake kunapopambazuka asubuhi (Yohana 10:14). Mazizi makubwa kama haya yanaingiliwa kwa kupitia malangoni (Yohana 10:2) na linawezakuwa ni eneo lililozungushiwa kwa kuta za mawe, zikionyesha juhudi iliyofananishwa na ile ya jingo la mji (Hesabu 32:16). (Kamusi mashuhuri iitwayo: The Interpreter’s Dictionary of the Bible, p. 316)
Mapango
yalikuwa yakitumiwa pia kama mazizi ya pamoja (Isaya 24:3). Ufunguzi wa mapango
kwa kawaida ulisimamiwa na mchungaji mwenyewe (Yohana 10:7,9).
Inafurahisha
kuona kwamba Daudi, mchungaji, alikuwa na ujuzi mkubwa sana wa kombeo. Uwezo
wake wa kumuua Goliathi kwa kutumia kombeo uliwaonyesha watu wake uwezo wake wa
kupambana akiwa mchungaji, kama kombeo na fimbo au au bakora zilikuwa ni zana
ambazo kwazo mchungaji alivitumia katika kuwalinda kondoo wake. Kwa hiyo, kwa
kuwa kwake imara na uhodari, alionyesha kujitoa kwake au umahiri wake kwenye
kazi yake kama mchungaji. Kwa hiyo, alistahili mara moja kuwaongoza Israeli. Hadithi
hii ipo kwenye Isaya 17:49.
Njia kuu
aliambayo mchungaji aliiweza kuitumia ili kulilinda kundi lake kwa usalama
zaidi ilikuwa ni kwa kupitia mafunzo. Najua kutokana na uzoefu wangu nikiwa
kama mkufunzi wa wanyama, kwamba baada ya kipindi fulani niliweza kuwaita kondoo
wangu waje upande wangu wakati walipoanza kuweza kupambanua na kuitambua sauti
yangu na kuijua kuwa ni sauti ya usalama nay a anayewapa chakula na maji.
Inachukua kuda kufikia kiwango hiki hata hivyo.
Wakati
tulipopewa kondoo kwa mara ya kwanza tuwafundishe, tulitumia kipindi cha saa
moja hadi mawili kwa siku, tukitumia muda huo kwa kutembea na kukaa pamoja na
mnyama, tukiongea wakati wote, ili kumhakikishia kuwa sisi tu watu wema kwake
na tukimzoeza atuzoee kwa maneno na sauti zetu. Yohana 10:4 inasema:
Naye awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake.
Hii inaashiria
mafunzo kama hayahaya na mbinu zake. Wakati wa kumfunga ukawasili.
Wakati
wowote ambapo mkulima anapowaingiza ndani kondoo wake kwenye mlowesho wa maji au
nyoa manyoya, huwahesabu mmoja mmoja ili kuhakikisha kuwa hakuna hata mmoja
aliyeachwa kwenye majani mengi. Tukio kama hilihili ndivyo lilivyokuwa
linatokea katika siku za Biblia. Kila usiku kama walivyokuwa wanaingia kwenye
zizi la kondoo walikuwa wanahesabiwa na vivyohivyo kila asubuhi walipoondoka.
Dhana hii imeenea sana (ISBE, Vol. 4,
p. 464) kwamba kila kundi lililohesabiwa lilikuwa na wastani wa mifugo 100 (Mathayo
18:12; Luka 15:4). Tofauti yoyote iliyojitokeza kwenye idadi ya mifugo ilihesabiwa
kuwa ni hasara ya wachungaji (Mwanzo 31:39; 1Samweli 25:15-21).
Yaonekana
kwamba mchungaji mwema hakuwa anakula yeyote kati ya wanyama wake mwenye,
haijalishi mazingira yako mabaya na magumu kiasi gani, lakini kwa ajili ya
wajibu wake kwa watu wake (Mwanzo 31:38-40; Ezekieli 34:7-16; Amosi 3:12). Mashitaka
ya Yakobo kwa Labani ni mfano tunaoweza kuufuata kwa kuwa kondoo hawakuwa wake
(Mwanzo 31:38-40). Ezekieli 34:7-16 inatuonyesha kuwa tusifanyen hivyo. Yohana
10:12 inatuonyesha kiwango cha kujitoa alichokuwanacho mchungaji kwa kondoo
zake.
Kwa suala
la kuwaganga, tunaweza kutegemea wataalamu wa tiba za Wanyama au ma bwana
Mifugo waliopo leo. Lakini haikuwa hivyo siku za nyuma. Mchungaji alipaswa
kushiriki wajibu wa ubwana Mifugo. Tunajua kutoka kwenye Isaya 1:6 na Yeremia
8:22 kwamba marihamu, mafuta ya mzeituni, au mafuta ya mnyama yalihitajika, kama
dawa, kwa kawaida wakati kondoo anaingia kwenye nchi yenye matatizo au kamsa
(Ezekieli 34:5; Mathayo 12:11; 1Wafalme 15:4).
Mwongozo
ulio wazi tulionao katika kuangalia usalama wa kondoo wa Mungu. Tunahukumiwa
kwa jinsi tunavyotendea kila mmoja na mwenziwe, kwa mukutada wa namna zote
mbili, yaani tukwa kama wachungaji na tukiwa kama kondoo. Hebu na tupendane
kama Mchungaji wetu alivyo tupenda na anavyoendelea kutupenda sisi wote.
q