Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[034]
Roho ya Kufanywa Wana
(Toleo La 2.1 19940604-20000620)
Jarida
hili linahusika kuelezea dhana ya wokovu kwa kufanyika kuwa Mwana wa Mungu.
Fundisho la Kuzaliwa Mara ya Pili limechambuliwa na dhana yenyewe kama ilivyokuwa
kwenye Kanisa la kwanza na jinsi ilivyoendelezwa. Historia ya Agano la Kale
imechambuliwa na mchakato wa kukubalika na Baba unaonyeshwa. Mchakato wenyewe
unahitaji unyenyekevu kamili kwa Baba ambao unahitaji tendo la ukombozi.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1994, (ed. 1997), 2000 Christian
Churches of God)
(tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Utangulizi
Makanisa ya mwanzoni baadhi yetu tungeweza kufundishwa kwamba Mungu “anajiongeza
mwenyewe” kwa kupitia kwa mwanadamu. Ilifundishwa kwamba mchakato huu wa
“kuzaliana” ulichapishwa kupitia kwenye mlinganisho wa utungaji wa mimba na
uzazi au kuzaliwa. Kwa uwazi kabisa ilisemwa kwamba wakati mtu anapobatizwa na
kumpokea Roho wa Mungu, ndipo anakuwa “ametungwa mimba” akiwa kama kiumbe
muhimu wa Mungu. Mawazo ya mwanadamu na roho vilifananishwa kama kiluwiluwi au
yai ndani ya mwili wa mwanamke. Roho wa Mungu anafananishwa kama “seli takatifu
ambayo ni mbegu pia” inayoingia kwenye lile “yai” na, kwa hiyo kutunga mimba ya
kiumbe kipya cha kiroho.
Kanisa kwa upande mwingine lilifananishwa na mwili wa mwanamke, na hasahasa
tumbo lake. Kiumbe kipya anayefanyiwa mtungo wa mimba na Mungu kinatakiwa kiwe
kimeambatanishwa kiuimara kwenye “ukuta wa kupitishia mkojo” wa mama—na ndivyo
ilivyo kwamba Wakristo wanahitaji kushikamana kwa uimara wote na Kanisa na
kupata malisho kutoka kwenye maelekezo ya huduma na sharika zao
zinazofananishwa na mwili. Iwapo kama Mkristo ataachana na bodi ya Kanisa,
inaweza kuwa kama “utoaji mimba” wa kiroho na matokeo yake yatakuwa ni “kifo au
mauti ya kiroho” ya Mkristo Yule. Iliwapasa Wakristo wakulie kwenye mwili ambao
ni Kanisa, hadi kufikia ufufuo wa kwanza wa wafu wakiwa “wamezaliwa mara ya
pili” wakiwa kama viumbe kwenye ulimwengu war oho. Rejea za Agano Jipya kuhusu
“kuzaliwa mara ya pili” kwa kweli zilikuwa zinataja na kuuelezea mchakato,huu wa
“mwenendo wa kiroho na kuzaliwa kwenye ufufuo wa wafu".
Yote kwa yote ulikuwa ni mlinganisho wa wazi na ufafanuzi wa mchakato wa
uongofu wa Mkristo na mpango mzima na kusudi la Mungu.
Hata hivyo, ilikuwa ni ukweli wa mlinganisho usio wa kibiblia.biblia haisemi wala kuuelezewa mchakato wa wongofu
wa Mkristo na kukua kwa mambo ya kifikra wakati wa ubatizo na kuzaliwa kwenye
ufufuo wa wafu. Ilikuwa ni kwa ajili ya kutolielewa neno lililotumika kwenye
Kiingereza cha Zmani kuhusu neno uzawa
ambalo linaonekana kwenye tafsiri ya KJV, linalopelekea mlinganisho huu
mpotofu. Neno kuzaliwa halimaanishi mtungo wa mimba; bali linamaana ya kwa baba. Mlinganisho wa kibiblia wa kzaliwa mara ya pili ni kwamba tunakuwa
tumezaliwa upya au tumezliwa upya kwa njia ya wongofu na ubatizo. Tangu hapo
inatupasa kukua kimwili na kifikra kama Wakristo hadi tufikie kikamilifu tabia
ya Yesu Kristo.
Lakini sio tu kuwa ulikuwa ni mlingano huu usio wa kibilia, bali ililazimisha pia uelewa mpotofu wa vifungu
vingine vya Maandiko Matakatifu. Kwa mfano, kwenye Warumi 8:15 tunasoma:
Warumi 8:15 Kwa kuwa
hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa
wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
Ilisemekana kwamba neno lililotafsiriwa kuwa kufanywa wana kwenye kifungu hiki halimaanishi kufanywa wana kabisa, bali zaidi sana linamaanisha uwana – ambavyo kwamba Mungu anajiongeza
mwenyewe na kwamba sisi tunafanyika kuwa wana halisi, na sio kuwa ni wana wake kwa kuasiliwa. Msaada wa hilo umechukuliwa kutoka kwenye uwezekano wa tafsiri
mwenza kama vile ya RSV ambayo inasema hivi:
Warumi 8:15 Kwa kuwa
hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa
wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
Ni kweli, aya ya 23 ya sura hiyohiyo kwenye RSV haikunukuliwa! Inasomeka
hivi:
Warumi 8:23 Wala si
hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua
katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.
Kwa hiyo, kwenye tafsiri moja tuna neno kuasili,
na kwenye nyingine tunapata maana mbili zote za kuasili na kufanywa wana na
bado kuna nyingine (kama vile Moffatt) neno uwana linatumika kiutofauti kabisa. Je,
habari ya kweli hapa ni ipi? Je, ni kweli kwamba sisi ni wana wa kie na wa kiume
wa Mungu, au ni watoto tulioasiliwa tu? Je, Paulo anajua lolote kuhusu
“kuzaliwa mara ya pili” na ulinganisho wake? Je, tafsiri hii nyingine iliyo
kati ya hizi nyingine nyingi zinamakosa kwa kuwa watafsiri wake hawakujua
ukweli kuhusu makusudi ya Mungu kwa mwanadamu, au kwa kuwa walikuwa wanajaribu
kulificha? Kutumia usemi kwamba, "Ni
mtego kiasi gani?"
Msimamo wa Kisomi na uaminifu wa kutumia akili
Kwa kuhusianisha na jambo hili au dhana ya “kuzaliwa mara ya pili” kura
waliojulikana wakisema kama tukiliiodhoa mlinganisho wa dhana hii ya “kuzaliwa
mara ya pili” ya tutungwa mimba wakati wa ubatizo na kuzaliwa tena kwenye
ufufuo wa wafu, ndipo tunakuwa tunaiharibu kabisa dhana iliyoko kuhusu “Familia
ya Mungu”. Zaidi sana, ni kwamba kama hatutakubaliana kwamba Wakristo wata
“zaliwa mara ya pili” kama viumbe wa kiroho kwenye ufufuo wa wafu; kama
hatutakubali kuwa wongofu kwa hakika ni “kutungiwa mimba” kiroho na kwamba
maisha ya Mkristo ni sawa na "kipindi cha mtungo wa mimba" ndani ya mwili
au tumbo la mama (ambalo ni Kanisa), ndipo dhana yote ya Mungu kujiongeza
mwenyewe itakosa mashiko – na sambamba yake ni, ‘Familia ya Mungu".
Hata hivyo, mtindo huu we kufikiri na kujiuliza hauna maana. Mtu huyu amechukua
kile ambacho haya hivyo, ni mlinganisho,
na tafsiri iliyoaminika na kuwa na mashiko
katika karne ya ishirini kwenye vifungu fulani vya Biblia, na vkakubalina
na kutiliwa mkazo kuwa ni kweli. Kwa kweli, kuielewa Biblia kama ilivyokusudiwa
ieleweke, kwa kujumuisha desturi na mpangilio wa siku zilivyowekwa wakati
ilipoandikwa, na kumruhusu Roho Mtakatifu atuongoze kuielewa na kwa kuelewa
huko na kweli, wengine wanaamua badala ya kuyapa kipaumbele mawazo na tafsiri
ya wanadamu kuwa ni kama mwongozo mtakatifu usio na makosa kwa kile kilicho
kweli. Watajikita kushikilia mawazo yaliyopita na fafanuzi zake, licha ya
makosa yaliyomo ndani yake.
Kwenye Makanisa ya Kikristo ya Mungu, lengo letu ni kutafiti, kufundisha,
na kuitangaza kweli bila woga au kumpendele mtu yeyote. Tunajitahidi kuwa
waaminifu kiakili, na kuwa na uelewa wa kutosha kimafundisho kwenye utafiti wetu
na kuwa tayari kuukubali na kuupokea ukweli ulio kwenye Biblia, hata kama
“utaumiza” au kwma utaendana kinyume na mawazo ya zamani, na haijalishi ni kwa
kiasi gani “yalipendwa” na sisi. Petro na Paulo wanatuonya sisi kwa kusema hivi:
1Petro 4:10-11 kila
mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili
wema wa neema mbalimbali za Mungu. 11 Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu;
mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe
katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na
milele. Amina.
2Timotheo 2:15 Jitahidi
kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya
kutahayari, ukitumia kwa halali neno la
kweli.
Mungu anajiongeza mwenyewe
Kabla hatujasoma somo hili la kufanyika
kuwa wana tunapaswa kujua kwamba Mungu kwa kweli anajizidisha, au anajiongeza
mwenyewe, kwa maana ya kwamba anawaumba watu wakiwa ni viumbe wanaoongez na
ambao wanashiriki asili yake, kwa jinsi amnavyo tabia zake zimewekwa. Mungu kwa
kweli anajiongeza mwenyewe kwa wengi, wana wengi wakiume. Kristo alikuwa
mzaliwa wa kwanza wa wanawe na ni wa uzao
uliotokana na asili ya Mungu:
2Wakorintho 4:4 ambao
ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru
ya injili ya utukufu wake Kristo aliye
sura yake Mungu.
Wakolosai 1:12-15
mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu
katika nuru. 13 Naye alituokoa katika nguvu za giza,
akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; 14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa
dhambi; 15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana,
mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Waebrania 1:3 Yeye
kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote
kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa
kuume wa Ukuu huko juu;
Inafurahisha kuona kwamba kwenye Kiyunani neno lililotafsiriwa kujiongeza kikamilifu kiuzao hapo juu ni
tabia (SGD 5481) ambalo kutoka kwalo
ndipo tumepata neno la Kiingereza lenye maana ya mwenendo. Tafsiri ya Thayer ya Lexicon yenye mchanganyiko wa
Kiyunani na Kiingereza inatoa maana ifuatayo kuhusu hii:
1.
Kifaa kilichotumika kuchongea
au kuwekea umbo
2.
alama iliyowekwa kwenye
kifaa kile au kileondolewa mbali ya hiyo
a) alama au kitu kilichochosemwa kwenye (Walawi
13:28) au kilichowekwa juu yake, kuonyesha.
b) uonyesho halisi (kilicholengwa) cha mtu yeyote
au kitu, kilionyesha kufanana, ongezeko halisi la kiuzazi kwa kila chenye kutamanika,
yaani nukushi.
Kwa hiyo, Kristo alikuwa na tabia za Mungu au asili “iliyowekwa ndani yake”
kwenye uzaoi chake (uliotajwa hapo juu kama akishirikishwa
kwenye utukufu wa Mungu).
Inafurahisha sana pia kuona kwamba neno la Kiyuani lililotafsiriwa kama kuchukua sura na umbo na kuichukua hali kufanywa wana hapo juu ni
eikon kutoka kile tunachopata kwenye neno la Kiingereza icon. Lina
maana ya sura, umbo, kufanana; mfano wa
vitu vya mbinguni; nk. Imetumika katika kumuelezea Kaisari kwenye picha
zilizotumiwa kuandikwa kwenye sarafu za Warumi (Luka 20:24), wakristo walio na
sura na tabia za Adamu na Adamu wa Pili (1Wakorintho 15:49), sura na mafano wa
wanadamu na wanyama iliyoyumiwa kwenye ibada za sanamu (Warumi 1:23), na “Sura na
Mfano wa Mnyama” (Ufunuo 15:13). Kwenye kila tukio inaelezea kitu ambacho ni nakala ya kitu fulani kingine kinachotokana
na kitu asilia kwenye muonekano na au kazi na utendaji wake. Kristo ni mjumbe
wa Mungu kwa maana ya asili na tabia zake na mwenendo wake.
Kwa jinsi hiyohiyo, Wakristo wanabadilishwa kwenye nakala, kufanana, au sura
na tabia ya Kristo (na kwa hiyo kuwa na sura na mfano wa Mungu). Kwa hiyo,
Mungu anajiongeza mwenyewe moja kwa moja kwa maana ya asili yake na tabia yake
kwa wanadamu. Tumeumbwa kwa “sura na mfano wa Mungu” tayari kutokana na inavyosema
Mwanzo 1:26 na 1Wakorintho 11:7 na kutoka hapo tunakuwa tunakuwa na uwezo kama
Mungu wa kimawazo, kufikiri, na uwezo wa kufanya maamuzi na kujijengea tabia.
Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu,
kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama,
na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
1Wakorintho 11:7 Kwa
maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na
utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.
Lakini tumebadilishwa kutoka kwenye umbo hili lenye kuwa na mpaka wa
kiuwezo na kuwa na umbo lenye tabia kamilifu ya Mungu na asili yake.
2 Wakorintho 3:18 Lakini
sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika
kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama
vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.
Wakolosai 3:10 mkivaa
utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.
Huu ni mchakato ambao hautakamilika hadi ufufuo wa wafu.
1Wakorintho 15:49 Na
kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake
yeye aliye wa mbinguni.
Suala ni kwamba Mungu anajiongeza mwenyewe ndani ya wanadamu/ amekwisha
jiongeza tayari kwa wenyi – huenda kwa mamia na mabilioni ya watoto wa kiroho
ambao tunawaita kuwa malaika – na
ataukamilisha mchakato na wanadamu kwa kipindi chake alichokikusudia kwenye mpango
wake wa wokovu.
Warumi 8:29 Maana
wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa
Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
Waebrania 2:10-11 Kwa
kuwa ilimpasa yeye, ambaye kwa ajili yake na kwa njia yake vitu vyote
vimekuwapo, akileta wana wengi waufikilie utukufu, kumkamilisha kiongozi mkuu
wa wokovu wao kwa njia ya mateso. 11 Maana yeye
atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni
haya kuwaita ndugu zake;
Kile tunachokishughulikia wakati tunapotathimini somo hili la kufanwa wana sio tu kule kuwa I kaama
Mungu anajiongeza mwenyewe au sivyo, lakini zaidi tu ni ulinganisho utakaotusaidia kuelewa mambo fulani yaliyo kwenye
mpango wa Mungu wa wokovu.
Vifungu vya Maandiko
Neno hili kufanywa wana linaonekana
kwenye maandiko yafuatayo ya Biblia:
Warumi 8:15 Kwa kuwa
hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa
wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
Warumi 8:23 Wala si
hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua
katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.
Warumi 9:4 ambao ni
Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa
torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake;
Wagalatia 4:5 kusudi
awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa
wana.
Waefeso 1:5 Kwa kuwa
alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa
na uradhi wa mapenzi yake.
Neno lililotafsiriwa hapa kama kuasiliwa
linatoka kwenye lugha ya Kiebrania la huiothesia (SGD 5206). Lilikuwa
ni neno la viwango linalomaanisha kuasiliwa
katika karne ya kwanza. Ilionekana kuwa ni neno la jumla linalomaanisha kuchakuliwa kama mwana.
Kwa Kiingereza, neno kufanywa wana limechukuliwa
kutoka neno la Kilatini adoptare linalomaanisha
kuchagua. Kwa upande
mwingine, uwana linatokana na kutoka
kwenye neno lenye chimbuko la lugha mchanganyiko ya Kihindo na Ulaya (Indo-European)
linalomaanisha kuzaa. Tofauti iliyopo
kati ya maneno ni kwamba maana moja ya kuchaguliwa,
kuwa mwana na lingine ni kuwa
mwana kwa kuzaliwa. Kwa hiyo inapotokea kutafsiri kuwa huiothesia,
tafsiri sahihi zaidi ni kufanywa
mwana na sio uwana ni kwa sababu
kwenye desturi ya Warumi na Wayunani, dhana ya kuasiliwa lilitumika zaidi sana
zaidi ya vile inavyofanya katika siku zetu. Ilikuwa inamaanisha kufanyika mwana
au binti wa baba aliyemuasili kwa namna isiyotofaitshika
na kutokana na kuwa mwana au binti kwa kuzaliwa. Hii itafafanuliwa kwa
undani zaidi na kikamilifu kama tunavyoendelea.
Historia rejea ya Agano la Kale
Kitabu cha fasiri ya Biblia cha International Standard Bible
Encyclopedia (ISBE), kwenye makala yake kuhusu Kuasili mtoto [Adoption] (Vol. 1, p. 53) inasema
kwamba:
Desturi iliyoaminika
kwa Wayunani, Warumi, na watu wengine wa zama kale (wakiwemo Wahurrians; soma
jarida la ABRAHAM III); lakini haionekani kwenye Sheria au Torati ya Wayahudi.
Hakukuwa na posho maalumu inayojulikana bayana kwa shughuli hii ya
kumuasili mtoto kwenye vitabu vya Torati. Hata hivyo, kuna mifano kadhaa ya
kuasili watoto kwenye Agano la Kale:
Kinachofurahisha kuhuau mifano hii ni kwamba inatokea tu nje ya Palestina –
katika Misri na Uajemi, nmbako desturi ya kuasili watoto ilikuwa imeshamiri.
Kinachofurahisha zaidi pia ni kwamba kwenye Agano Jipya dhana hii inatokea
kwenye nyaraka za Paulo, na hasa hasa zile zilizoelekezwa kwenye makanisa
yaliyo nje ya Palestina. Ilionekana kwa hiyo kwamba zaidi ya kufanya mfano wa Agano
la Kale au historia, Paulo alikuwa anatilia maanani au kulinganisha na uelewa
wake wa ulimwengu wa Warumi ambako desturi hii ilikuwa inafanyika kwa kiasi
kikubwa na ilikuwa na maana. (Wayunani, kama ilivyoelezewa, pia walifanya pia,
lakini ilionekana kutoka kwenye waraka ambao ulikuwa na mfano wa Warumi
aliokuwanao mawazoni mwake.)
Kufanywa wana – kwa sasa na zama ijazo
Paulo aliandika kuhusu kufanywa wana huku kuwa kutafanyika kwa zama zote
mbili, yaani kwa mtazamo wa sasa na kwa zama ijayo. Kwenye Warumi 8:15 Paulo anasema
kwamba tumapokea tayari roho ya kufanywa
wana.
Warumi 8:15 Kwa kuwa
hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa
wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
Neno roho limeandikwa kwa herufi
kubwa kwene bilib ya KJV, lakini kwenye Kiyunani asilia kulikuwa hakuna jinsi ya
kutofautisha. Hii inaeleweka vyema kabisa kama “mmepewa roho (inayoshirikisha
mawazo, nia, jinsi ya kufikiri) ya kufanwa wana”. Inadbaniwa kuwa uwepo wa Roho
wa Mungu ambaye sisi tumefanywa kwaye au kuchaguliwa kuwa wana wa Mungu
mwenyewe, na tunaweza sasa kumuita asi kukosea na kwa jina la uhusiano wa
karibu kuwa ni Aba ambalo ni neno la
Kiaramu lenye maana ya Baba. Kuwa na
Roho wa Mungu kunabadilisha njia au namna yetu ya kufikiri. Inaonyesha pia
ni kama mmoja wa wana wa nyumbani mwa Mungu, na ni sehemu ya familia yake.
Waefeso 2:19 Basi
tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na
watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.
Wadhifa wetu mpya umehuhudiwa hivyo kwa Roho wa Mungu na roho zetu.
Warumi 8:16 Roho
mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
Kwakuwa Mungu ni Baba yetu, nasi ni watoto wake (kwa usemi wa kawaida),
basi tunakuwa pia ni warithi, tuurithio kila alichonacho.
Warumi 8:17 na kama
tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam,
tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
Lakini mchakato wetu wa kufanywa wana haujakamilika bado.
Warumi 8:23 Wala si
hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua
katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.
Ufafanuzi wa kile anachokimaanisha Paulo kwa hii umetolewa kuelekea
mwishoni mwa jarida hili.
Kufanywa wana huku kunafanywa na Baba
Biblia ya ISBE inasema kwamba:
Nia na msukumo wa
kufanywa wana huku kila mara kunatuama kwa baba anayetufanya kuwa wana, na ambaye
anafanya upungufu wa kizazi asili na kukidhi madai ya kufanyika hivyo na
kidini, na hamu na kufanya mamlaka makubwa ya kiubaba au kuendeleza familia
yake. (ibid.)
Mwenendo na msukumo wa kufanywa wana mara
zote unaendana na kitendo hiki cha kufanywa wana na baba. Nia ya baba
ilikuwa ni kusaidia kuliendeleza jina la familia, na kukithi mahitaji yake
binafsi na hamu ya kuonyesha athari au madhara kwa mtoto wake.
Tunaanza kuona hapa kwa nini Paulo
alitumia mlinganisho huu kushughulikia wito wa Mkristo na wongofu wake. Mungu
ndiye anayewezesha wito wetu. Lakini sisi hatuwezi kuliwezesha hilo. Hatuweze
tu kuamka siku moja na kuchagua kuwa Wakristo. Mungu ndiye anayepandikiza ndani
yetu ile hamu ya kufanya hivyo na hata ile shauku ya kuitafuta kweli. Sio kwa
ajili ya “wema” wetu, kwa kweli au kufikiri kwetu, kulikompelekea Mungu
atuchague sisi.
Waefeso 2:8-9 Kwa
maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi
zenu, ni kipawa cha Mungu; 9 wala si kwa matendo, mtu
awaye yote asije akajisifu.
Yohana 6:44 Hakuna
mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku
ya mwisho.
Yohana 6:65 Akasema,
Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa
amejaliwa na Baba yangu.
Zaidi sana ni kwamba, Mungu anafanya hivyo kutokana na shauku yake ya kuiongeza familia yake, na kutuonyesha sisi upendo wake na athari zake.
Waefeso 2:4-7 Lakini
Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; 5 hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu;
alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. 6
Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa
roho, katika Kristo Yesu; 7 ili katika zamani
zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa wema wake kwetu
sisi katika Kristo Yesu.
Mungu analiweka jina lake juu yetu.
Yohana 17:11 Wala
mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba
mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa
uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
Ufunuo 3:12 Yeye
ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka
humo tena kabisa, nami nitaandika juu
yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu
mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile
jipya.
Ufunuo 14:1 Kisha
nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu
mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji
vya nyuso zao.
Kama Mkristo, tunapoipokea roho ya kufanywa wana, tunaungana na familia ya
Mungu, tukiwa na sehemu ya baraka zake, na tunalikubali pando lake
.
Masharti muhimu makuu yanayotangulia kabla ya kufanyika
wana
Tendo la kuasiliwa kwenye imani na utaratibu wa Warumi, wakati wote
ulitanguliwa na masharti fulani muhimu yafuatayo:
Kitendo hiki cha kuasili watoto kilifanyika pia kama kigezo cha
kustahilisha uhalali wa kuzipa nchi au dola fulani fulani stahili na haki zao.
Mambo yote yaliwekwa juu ya uraia wa Warumi walioasiliwa ikiwa ni mchakato wa
makini sana na sio kitu kilichofanywa kijuujuu.
Tena tuweza kunona hapa la kujifunza sisi.
Majina yetu yametajwa mbinguni, mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, mara nyingi
sana tena na tena. Mungu hana kigeugeu au kubadilika kwa maana ya jinsi anavyowateua
na kuwachagua watu wake. Kwa hiyo, ni kama wale waliochaguliwa na kuchaguliwa,
hatupaswi pia sisi kufanya maamuzi kiranisi sana hivyo.
Waebrania 2:1 Kwa
hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa
Waebrania 2:1 Kwa
hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa. Vinginevyo
tutafanana na meli inayopita mandarini ikiwa na mavunjiko.
Kujinyenyekeza kikamilifu kwa Baba
Tendo la kumuasili mtoto kwenye familia ya Kirumi kilimaanisha kuwa na
unyenyekevu kamili kwa baba mpya. Biblia ya ISBE inaeleza kwamba Warumi
walikuwa na neno maalumu kuhusu jambo hili, lililojulikana kama patria
potestas, na lilimaanisha kunyenyekea
kikamilifu kwa baba mpya, kiasi cha kufanana baribu kama mtumwa na bwana
wake, kwa kipindi cha kadiri baba alivyokuwa hai anaishi.
Tendo la kuasiliwa na Mrumi kinatufundisha mambo makuu nay a muhimu mawili.
Tunapaswa kujinyenyekeza kikamilifu kwa Mungu kwa kila jambo.
Unyenyekevu huu na ushirika wa familia ya Mungu unapaswa kuendelea kwa
kadiri Mungu aishivyo na, kwa kuwa Mungu ni wa milele, tunajua kwamba sehemu
yetu tukiwa kama watu wa numbani mwake Mungu ni ya milele.
Mwanzishi wa Waebrania anaandika hivi:
Waebrania 12:7-10 Ni
kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana
yupi asiyerudiwa na babaye? 8 Basi kama mkiwa hamna
kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si
wana wa halali. 9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba
zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia
chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? 10 Maana ni
hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye
kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.
Sisi tunajinyenyekeza sasa kwa baba yetu kwa namna zote mbili za muadibisho,
na kwenye urithi, na kwa njia nyingine
yoyote kama tulivyofanyika kikamilifu kuwa ni wana na binti za Mungu ambavyo
ndivyo tulivyo. Mahali petu tukiwa kama watu wa nyumbani mwake Baba na familia
yake ni wa milele kwa kweli na ni hakika.
Zaburi 23:6 Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote
za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.
Kurehesha mahusiano yaliyopita
Desturi ya kuasili mtoto ya Kirumi ilihitaji mtu anayeasiliwa aseme wazi
kabisa na akiri kwamba anaukana uhusiano na haki zote za familia aliyokuwako
zamani huko nyuma, zikiwa ni pamoja na uhusiano wa kisiasa, na imani zote za
zamani za kidini na kila alichokuwa anakitumikia.
Wakati akifanya hivi, mtoto aliyeasiliwa anahamisha kile rasilimali
alizonazo kwa wakati huo na hata madeni na vingine atakazomudu kuzipata baadae
kwa wazazi wake hawa wapya. Neno maalumu la kisheria lililokuwa linatumika kuelezea
kitendo hiki, lilikuwa, per universitatem kuonyesha kwamba mchakato wote
wa kubadilishana umekamilika. Sasa, hii haiwezi kuonekana kuwa ni wazo jema, lakini
kulikuwa na motisha kwa mtoto aliyeasiliwa kwamba uhamishaji huu wa mali na
stahiki ulikuwa unahusisha pia na madeni
aliyokuwa anadaiwa, ili kwamba mtoto aliyeasiliwa aweze kuwa huru kutokana
na madeni yake ya zamani.
Tunaweza kuyatendea kazi mambo haya kwa sisi wenyewe kwa hatua sababu na
namna zifuatazo:
Mambo haya yameelezewa kwenye vifungu kadhaa vya maandiko.
1Petro 4:1-2 Basi
kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia
ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi. 2 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu,
bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
Warumi 12:1 Basi,
ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo
hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Waebrania 13:15-16 Basi,
kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la
midomo iliungamayo jina lake. 16 Lakini msisahau
kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.
Warumi 8:1 Sasa,
basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
Wakolosai 2:13-14 Na
ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili
wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote; 14 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa
hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea
msalabani;
Yaliyohitajika na ya muhimu kwa ukombozi
Tendo la kumuasili mtu lilihitaji kuwa na mtu aliyehiyari kuasiliwa na mtu
huyo anapaswa anunuliwe au akombolewe kutoka kwa wazazi wake asilia, na kwa
kweli, mchakato wa kumuasili haukukamilika hadi pale hawa wazazi wapya watakapokuwa
wameutimiza mchakato huu. Biblia ya ISBE inasema kwamba:
... kuasili
kikamilifu (adoptio) ulikuwa
ni mchakato ambao kwamba mtu alihamishwa kutoka kwenye mamlaka ya baba yake
halisi na kuhamishiwa kwa yule baba mpya aliyemuasili, na ilifanywa kwa mauzo ya
namna fulani yam toto huyo, na kitendo chake cha kujiachia au kujisalimisha
kutoka kwa baba yake wa asili na sasa kuwa kwa baba mpya aliyemuasili. (ibid.)
Paulo alielezea jambo hili la matendo ya Warumi kwenye waraka wake kwa
Wagalatia.
Wagalatia 4:4-5 Hata
ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na
mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, 5 kusudi
awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa
wana.
Mara tu ukombozi unapokuwa umefanyika, ndipo tendo la kuasili lilikuwa
limekamilika. Kwa kweli, kitendo cha kumuasili kilikuwa kimekamilika na kilikuwa ni kilele cha mchakato huu, na mabadiliko ya wazazi yalichukuliwa kuwa ni kweli kabisa, na kwamba mtoto
asliyeasiliwa alihudumiwa kwa muktada sawa na kama alikuwa ni mtoto asili na
mzaliwa wa kwenye familia hiyo. Mtu aliyeasiliwa, anapofikisha umri tarajiwa au
daraja tarajiwa la kimaisha, alichukua jina au daraja la kimaisha alilokuwanalo
baba yake mpya aliyemuasili, na kulikuwa hakuna mamlaka yeyote iliyoweza
kupunguza au kuyapuuzia mabadiliko haya.
Nasi kama Wakristo, tunampokea roho wa Baba yetu mpya, na kumuira kwa jina
la Baba. Alianza maisha mapya, akiwa
kama mtoto mpya wa Mungu, aliyezaliwa upya katika maisha ya kimakuzi na
kimaendeleo cchini ya matunzo na uangalizi wa Baba yetu.
Warumi 6:4 Basi tulizikwa
pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo
alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi
tuenende katika upya wa uzima.
1Petro 1:3 Ahimidiwe
Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa
mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo
katika wafu;
1Petro 1:23 Kwa kuwa
mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika;
kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.
1Petro 2:2 Kama
watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili
kwa hayo mpate kuukulia wokovu;
Waefeso 4:13-15 hata
na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu,
hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa
Kristo; 14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa
huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa
ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. 15 Lakini
tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye
aliye kichwa, Kristo.
Matendo ya siri; kudhihirika kwake baadae
Hatimaye, hili ni jambo linalopendeza sana la desturi ya matendo ya Warumi ya
kuasili watoto. Mchakato huu ulijumuisha na tendo la siri la kuasili, na ambalo hatimaye linafikia kwenye mdhihiriko wa wazi. Hii ndiyo aliyokuwa anafikiria
Paulo alipokuwa anaandika waraka wake huu:
Warumi 8:23 Wala si
hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua
katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu.
Wakati unakuja, unaotajwa kuwa ni wa ufufuo wa wafu, wakati wale wote
tuliowaasili wakiwa kama wana wa Mungu watatangazwa kwa wazi, nao watapokea utambulisho wa wazi. Lee dunia haitutambui
kabisa kuwa sisi ni watoto wa Mungu kama ulivyomtambua Kristo. Lakini wakati
unakuja wakati ukombozi wa miili yetu,
ambao ni wa kubadilishwa kwetu na kuwa viumbe wa kiroho tulio mfano wa Kristo,
na madai yetu ya kuwa ni wana kiume na wa kike wa Mungu watajulikana kwa wazi.
1Yohana 3:1-2 Tazameni,
ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo
tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado
tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa
maana tutamwona kama alivyo.
1Wakorintho 15:49-53
Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura
yake yeye aliye wa mbinguni. 50 Ndugu zangu, nisemayo
ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala
uharibifu kurithi kutokuharibika. 51 Angalieni,
nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, 52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda
ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu,
nasi tutabadilika. 53 Maana sharti huu uharibikao uvae
kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.
Wafilipi 3:20-21 Kwa
maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi,
Bwana Yesu Kristo; 21 atakayeubadili mwili wetu wa
unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo
aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.
Ufunuo 3:9 Tazama,
nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali
wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua
ya kuwa nimekupenda.
Wazo hili la kutangazwa au kudhihirika wazi kuwa ni wana wa kweli wa kiume
na wa kike wa Mungu kwenye ufufuo wa wafu uliotajwa kwenye vifungu vingi kadhaa
vya biblia vinavyohusisha uwana hu na ufufuo wa wafu, kwa matukio yote mawili,
yaani ufufuo wa Kristo na Wakristo.
Warumi 1:3-4 yaani,
habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili, 4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi
ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;
Luka 20:34-36 Yesu
akawaambia, Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa; 35 lakini,
wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kufufuka
katika wafu, hawaoi wala hawaolewi; 36 wala hawawezi
kufa tena; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kwa vile
walivyo wana wa ufufuo.
Hitimisho
Kwa hiyo sasa tunaweza kuelewa ni kwa nini Paulo alitumia mfano wa
kuasiliwa kwenye nyaraka zake. Ni kama mfano wa kimafundisho wa mifano ya
Kristo, iliwasaidia kuelewa Wakristo wa wakati ule waliokuwa wanazisoma nyakara
zake ujumbe na somo muhimu na la maana kuhusu kuingia kwenye familia ya Mungu
na kuhusu mpango wa Mungu wa wokovu. Mlinganisho huu hauna namna nyingine wa kupungua
kutoka kwenye ukweli wa kwamba kujiongeza mwenyewe kwa Mungu au kujiendeleza
kwake kupitia wanadamu. Zaidi ya kuwa inaongeza
kwenye uelewa wetu kuhusu Ubaba wa Mungu na uwana wa Wakristo.
Kwa neno la kisheria, huiothesia maana yeke ni mchakato wa kuasili mtoto, mchakato wa kumpeleka kwenye uwenyeji wa
nyumba mpya. Kwa maisha halisi,
inamaana ni hali ya kufanya ibada kamili, ambayo haina namna nyingine ya
tofauti na ile inayotokana na kuzaliwa. Uhusiano uiliopo kati ya mzazi na mtoto
ni sawa kabisa uwe imara kwa mambo yote mawili.
Paulo alikuwa anafundisha kwamba mtu ambaye hajafanyika kuwa mkazi wa
nyumbani mwa Mungu kwa sasa ni mtoto wa kweli na ni mrithi stahiki, na hakuna
namna ya kumtofautisha na Yesu Kristo. Paulo alitumia mlinganisho wa desturi ya
Warumi ya kuasili watoto ili kuyapa uzito madai yetu ya kuwa ni wana wa Mungu
kwa namna yoyote iwezekanayo, na
kwamba haki yetu ya kisheria ya kuurithi na kutawala ulimwengu tukiwa pamoja na
kiongozi na kaka yetu, Yesu Kristo.
q