Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[050]

 

 

 

Maana ya Arusi ya Kana ya Galilaya

(Toleo La 1.0 20030411-20030411) 

 

Kwenye Injili fupi ya Yohana tuna hadithi moja iliyoandikwa inayoonyesha jinsi maji yalivyogeuzwa kuwa divai kwenye arusi ya Kana ya Galilaya. Tutaona kwamba hakuna sio tukio moja tu peke yake bali ni mawili ambayo yameelezewa kufanyika hivyo. Tukio la pili ni agano ambalo Ibrahimu na uzao wake waliloingia walifuate na kumti yeye Mungu wa Pekee na wa Kweli.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2003 Peter Donis, ed. Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Maana ya Arusi ya Kana ya Galilaya


 


Arusi iliyofantika na kuandikwa (Injili ya Yohana) ina maana katika kuashiria wito wa kuitwa taifa la kimwili la Israeli, sadaka ya Masihi, na kuwakusanya watu ambao waliwezesha kufanyika mwili au kundi la Kanisa.

 

Arusi hii iliyoandikwa inaashiria mfano wa ukombozi wa mwanadamu. Inaonyesha kwamba Kristo ndiye msingi wa mpango wa wokovu. Arusi hii ni taswira ya ya agano la Mungu linaloendelea. Tunaona jinsi linavyoendelea bado na limetolewa Kanisani, watumishi wake, yeye Mungu Aliye Juu Sana. Mvinyo uliotolewa kwanza na ukaisha ulioandikwa ni taswira ya dhabihu ya mnyama iliyokuwa inafikia kikomo, na mvinyo mpya uliotolewa ni ishara ya agano jipya ambalo Kanisa linakwenda kujumuisha nalo.

 

Hadithi inaanzia kwenye Yohana 2:1 kama hivi.

Yohana 2:1-10 Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. 2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. 3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia. 5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni. 6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. 7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu. 8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka. 9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, 10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.

 

Tunaangalia kwenye kila aya moja moja, kwa mpangilio wa ufafanuzi, tukianzia aya ya kwanza ya Yohana sura ya 2. 

Yohana 2:1 Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya;

 

Kuna mifano mingi kwenye Biblia inayotaja matukio yaliyotokea katika siku ya tatu. Mojawapo na linalojulikana sana ni lile la Ufufuko wa Kristo kutoka kwa wafu siku ya tatu. Tungeweza kufundisha somo la ukombozi, wokovu au uhai, vinavyohusiana na matukio yaliyotukia siku ya tatu.

 

Mkusanyiko uliokuja kwenye arusi hii ulitokea siku ya tatu. Shughuli za Arusi na ndoa siku za kale mara nyingi zilichukua siku nyingi sana na hapa tunaona mfano uliotumika mara nyingi kwenye mpangilio wa mzunguko wa mwaka wa saba, ambao vitu vingi vilianzia kwenye mwaka wa tatu ulio kwenye mzunguko mtakatifu. Kuna  mlingano mkubwa zaidi unaofanana na Israeli wa zamani, ambao walikuwa wakikusanyika pamoja na kufika kwenye jangwa la Sinai katika mwaezi wa tatu baada ya kuondoka Misri na kuingia kwenye agano na Mungu (Kutoka 19:1). Matukio yalilo kwenye Kutoka sura ya 19 yanafanana na hili la arusi liiyohudhuriwa na Kristo na wanafunzi wake. Makutano waliambiwa wazifue nguo zao, jambo ambalo linafanana na vazi la mhusika wa arusi na kanzu nyeupe la kuushinda ulimwengu huu (Ufunuo 6:11; 3:5) kuuvaa unyenyekevu (1Petro 5:5).

 

Mkutano uliambiwa kuwa tayari siku ya tatu (Kutoka 19:11,15). Kwa kuwa ilikuwa ni siku hii ndipo Mungu, kwa kupitia Malaika wake, ambaye alikuwa ni Kristo, alijitokeza machoni mwa watu wote (Kutoka 19:11) kuingiza kwenye agano.

 

Kutoka 19:10  Bwana akamwambia Musa, Enenda kwa watu hawa, ukawatakase leo na kesho, wakazifue nguo zao, wawe tayari kwa siku ya tatu; maana siku ya tatu Bwana atashuka katika mlima wa Sinai machoni pa watu hawa wote.

 

Ndivyo ilivyo pia, kwamba Kristo alishirikiana na wanafunzi wake, alikuja arusini, ambako agano kati ya bibi arusi (ambaye ni sawa na Kanisa) na bwana arusi (anayefananishwa na Kristo) lilifanyika. Kristo alipasa kujidhihirisha mwenyewe kwa kupitia ishara yake ya kwanza kwa watumishi, ikiwaashiria wale walioitwa.

 

Tunaweza kuhitimisha pia kwamba hii siku ya tatu iliyotajwa inamwambatano wa maana kwenye hadithi ya Yoshua 9:1-27. Kwa jambo hili, wenyeji wa Gibeoni, wajulikanao kama Wahiti, walijua kwamba Bwana Mungu alikuwa pamoja na Yoshua. Walijua kwamba wasipojitoa wenyewe kwenye mikono ya Yoshua wasingeweza kuishi. Utoaji wao “viriba vikukuu na vyenye ngozi iliyopasuka na kushonwa tena” kuliweka taswira ya hali yao ya kiroho wakati walipolikaribia kundi la Israeli likiwa chini ya Yoshua.

 

Katika siku ya tatu Yoshua alifika kwenye miji yao. Tunaona la kujifunza likiendelea. Yoshua mwana wa Nuni (maana yake ni Wokovuthe unapatikana kwa kuvumilia) linaonekana kufanana na la Kristo (soma jarida la Yoshua, Masihi, Mwana wa Mungu (Na. 134)). Wale waliokuwa ni wamataifa walipewa fursa ya kupandikizwa kwenye mwili au kundi la Israeli/ Yoshua aliwauliza, “Ninyi ni kina nani na mnatoka wapi?” Wahiti walimjibu kwa udanganyifu. Walimjongelea Yoshua, na ingawa walikuwa ni majirani, walisema, “Sisi watumishi wako twatoka nchi iliyo mbali sana”. Jambo hili lilionyesha au kuashiria hali ya kiroho waliyokuwanayo.

 

Matukio haya yanakumbushia wakati Yesu alipokuwa na wanafunzi wawili zaidi, yaani Filipo na Nathanieli (Yohana 1:43, 47), katika siku ya tatu baaya ya kubatizwa kwake na Yohana Mbatizaji, Yesu alimuona Nathanieli anakuja kwake. Kristo alisema, “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.”, sio kama Wahiti waliomjia Yoshua kiudanganyifu. Kristo alimjua Nathanieli kuwa ni mtu wa aina gani mara tu alipomfikia na kule alikotoka. Hii imeonekana kwa ukweli kwamba Masihi ajimuona Nathanieli alipokuwa ameketi chini ya mti wa mtini (Yohana 1:48). Alikuwa na tunda la roho. (Rejea kwenye jarida la Kuulaani Mtini (Na. 90)). Nathanieli alimjia Masihi bila hila wala udanganyifu wowote, nia yake ilikuwa ni kuutafuta ukweli kwa moyo wake wote. Hili linapasa kuwa ndilo lengo letu pia. Hakuna jinsi ya kumdanganya wala kumpumbaza Mungu.

 

Mji wa Galilaya unatumika na kutajwa kwa namna hii, kwamba unaweza kufanana na sisi, kama mtu mmoja mmoja au kama bodi ya kanisa. Galilaya inaweza kuwa na maana zaidi kama ni sehemu mojawapo ya Israeli. Kusifiwa kwake kwa mema kunaweza kutuelezea sisi kama mtu mmoja mmoja na kanisa. Tunaweza kuichukulia Galilaya ili kumaanisha hilo:

 

Kristo alikuja kama nuru ing’aayo huko Galilaya ya Wamataifa, wale ambao waliwahi kuishi gizani (Isaya 9:1). Kristo alikuja kuwaponya hata wenye magonjwa na waliosumbuka ma maumivu miongoni mwetu (Mathayo 4:23). Tulimkaribisha Kristo mioyoni mwetu (Yohana 4:45) na anatutumia sisi kuwafikia wengine (Yohana 4:3,4). Tumekuwa tukipewa roho ili kuyafundisha mataifa yote (Matendo 2:7).wale wanaotusikia watajua kuwa sisi ni wake, katika Kristo kwa kuwa tunaongea kwa lafudhi ya kipekee (Mathayo 26:73; Marko 14:70), ambayo ni tofauti na wengine. Dunia hii haikanushiki kuwa inatutupa sisi nje, kwa kuwa sisi tunazishika amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo (Mathayo 26:69). Kristo anaonekana ndani yetu, baada ya ufufuko wake (Mathayo 26:32) sasa, Kristo huyu anaishi ndani yetu, sisi ni Kanisa linalomfuata yeye na ni kumtumikia yeye. Ili tuwe tumekuja pamoja naye kwenye Yerusalemu ya Kiroho (Marko 15:41), mama wa sisi sote (Wagaatia 4:26).    

 

Mawazo haya yameakisiwa kwa wanafunzi wake Kristo. Wanafunzi wote wa Masihi walikuwa ni Wagalilaya, na isipokuwa mmoja wao—Yuda Iskarioti (Mathayo 4:18; Yohana 1:43–44; Matendo 1:11; 2:7). Rejea kwenye vitabu vya hawa wafuatao Youngblood, R. F. (1995). Nelson's new illustrated Bible dictionary. Rev. ed. ya: Nelson's illustrated Bible dictionary; Includes index. Nashville: T. Nelson.

 

“na mama yake Yesu alikuwepo”

Maria (ambalo limetafsiriwa kimakosa, kwa kweli ni Mariamu) alikuwa inayonekana kabisa kuwa alikuwa na uhusiano wa karibu na wa kidamu wa upande wa bwana arusi. Kwa hiyo, hawakuhitaji kualikwa. Wajbu wake wa kwanza ulipasa kuwa ni kusaidia kuandaa shughuli ya arusi, kwa kupangilia shughuli na kazi zote za upande wa bwana arusi. Aliwajibika pia kuwaelekeza watumishi mambo ya kufanya.

 

Injili ya Yohana haitaji kabisa mama wa Yesu kuwa ni Maria. Hii ni kuonyesha tofauti, kama tutakavyoona baadae. Kama tujuavyo, mwanamke anawakilisha haiba ya kanisa au taifa (Ufunuo 12:4-6). Kwenye jambo hili, twaweza kutafsiri kuwa mama yake Yesu analiwakilisha taifa la kimwili la Israeli ya kale na ukuhani wa Walawi kwa kupitia uzao wa Ibrahimu.

 

Kuonekana kwake kama yuko hapo tayari, kunaonyesha jambo la kwamba anafanya taswira ya ukuhani wa Kilawi ambao walikuwa wanashiriki kwenye Agano na Mungu. Tunapaswa kutilia maanani pia ukweli wa kwamba mama wa Kristo alikuwa kwa sehemu ni Mlawi. Kwa kuhitaji msaada kunaweza kuashiria kwa jambo hili utaratibu wa kutoa sadaka ambao kwamba makuhani walihudumu kaka kitu cha kwanza kwenye agano.

 

Aya ya 2: Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

 

Ili kuwa sehemu ya wanaoshiriki sherehe za arusi, inabidi mtu aalikwe. Ni Mungu ndiye anayefanya uchaguzi. Kristo hahusiki na mchakato huu wa kukaribisha ndipo kusema kuwa Mungu ndiye anayemchagua mtu na kumpa Kristo (Yohana 6:39).

 

Kristo alikuja ili kufanya mfano wa bwana arusi wa Kanisa (Mathayo 9:15; Marko 2:20). Wanafunzi waki watano waliokuja pamoja naye wanaweza kuyawakilisha makanisa matano ya kwenye Ufunuo ambayo yanamfanya bwana arusi ayafanye yaweze kuingia kwenye ufalme (pamoja na kila mmoja anayefanyaiwezesha kwa kupitia tangu kwa Makanisa ya Walaodikia na Wasardi). Kwa kina zaidi kuhusu somo hili, soma jarida la Davudi na Goliathi (Na. 126).

                            

Wakati tunapolitazama hili kama agano kwenye mchakato, tunaona kwamba mwaliko wa Kristo unakuwa wa makusudi ya namna mbili. Mwaliko wake ulitumwa maelfu ya miaka huko nyuma kupitia Ibrahimu (Mwanzo 12:3, 22:18). Tazama pia jarida la Agano la Mungu (Na. 152).

 

Mwanzo 26:4 Nitazidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, nami nitawapa uzao wako nchi hizi zote, na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia. Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu.

 

Ili kuupokea mwaliko inahitaji kufanya kitu fulani kwa upande wetu. Ibrahimu aliupata mwaliko wake wa kuingia kwenye agano na Mungu, kwa kuzishika amri na maagizo yote ya Mungu, miongozo yake na sheria zake. Alizichukulia sheria za Mungu kuwa ni kitu cha thamani kinachotakiwa kutamaniwa. Tunapaswa nasi pia kufanya hivyohivyo, kama tunaukubali mwaliko huu. Yatupasa pia kulitii neno la Mungu na amri zake, kama tutamkubali Roho Mtakatifu na kuingia kwenye sherehe ya arusi. Mfano wa wanawali wapumbavu watano na werevu watano unaonyesha kwamba wale walio na mafuta bado kwenye taa zao zikiwaka, waliweza kuingia kwenye karamu ya arusi. Kwa mwonekano wan je, wote walionekana kufanana. Bali walikuwa ni wale waliolithamini neno la Mungu na kuwa na Roho Mtakatifu, ambao waliweza kuingia wakati bwana arusi aliporejea.

 

Mithali 21:20 Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

 

Watu wote, wa mataifa yote walihakikishiwa kuupata wokovu kwa kupitia Kristo.

 

Wagalatia 3:8 Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.

 

Mungu, baba yetu alituchagua sisi kabla ya kuwekwa misingi ya dunia na ametuweka kwenye mwili wa.

 

Waefeso 1:4 kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.

 

Yatupasa tujue kwamba baada ya ubatizo Mkristo aliyeongoka anaambiwa awe mtakatifu na asiwe na dawaa kwa wenzake na katka kumpenda kwake Mungu kwa utakatifu (Walawi 19:2). Sheria zake zinatokana na asili yake au jinsi alivyo yeye mwenyewe, kama tunavyoona; Sheria yake ni takatifu (Warumi 7:12). Sheria zake zinadhihirisha upendo, kwakuwi pendo (1Yohana 4:16). Kwahiyo yatupasa kufikia kwenye hi=atima hiyohiyo kama Ibrahimu, na Sulemani, walivyofanya, ambavyo ni kumcha Mungu na kuzishika amri zake (Kutoka 12:13).

           

Tumepewa mwaliko mkuu (Isaya 55:1-13) pasipo kulipa gharama yoyote (Ufunuo 22:17) wa kuwa wana wa Mungu (soma jarida la Roho ya Kufanyika Wana (Na. 34)). Filipo kwa mfano alipewa mwaliko wa kumfuata Kristo (Yohana 1:43). Ni mwaliko wa kuubeba msalaba (Marko 10:21). Ni wito wa kufanika sadaka iliyohai (Warumi 12:1). Wengi wameipuuzia fursa hii (Luka 14:15-24). Lakini hatujachelewa bado (Yoeli 2:12-13); kwa wale wanaoukubali mwaliko watabarikiwa (Mathayo 25:34).

 

Aya ya 3: Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.

 

Hii ni kuonesha kwamba sadaka zote za wanyama walizozitoa makuhani zingekoma na zilimlenga Kristo. Tungedhania kuwa ule mvinyo ulioisha wakati sherehe hii ya arusi ingali ikiendele bado ilikuwa ni tawira ya mchakato wa ukombozi ambao ulitafutwa kwa kupitis sadaka za wanyama zilizotumiwa na Makuhani Walawi. Uandaaji wa arusi unapunguza nguvu utaratibu na mchakato wa ukombozi wa mwanadamu. Utaratibu wa kutoa dhabihu ulikuwa ni budi ufikie mwisho au ukome ili kuuwezesha utaratibu mpya uchukue mkondo wake. Damu wa mafahali ya ng’ombe na ndama ilipasa imilike katika Kristo, ambaye afipangiwa afe mara moja na kwa ajili ya wote (Waebrania 7:27, 9:24-28, 10:10,12,14; 1Petro 3:18). Mungu alifungua njia ya wokovu kwa kupitia Kristo. Hii ndiyo sababu mama yake Yesu alimwendea. Inatupasa kujua na kuzingatia dhana ya kwamba Mariamu hapa ni mfano wa taifa lililo chini ya ukuhani wa kimwili. Namna ambayo Mariamu alimaanisha nia na wajibu wake kwa mvinyo, inaonyesha na kumaanisha ukweli kwamba makuhani walijua kwamba sadaka ya damu ya ilitakiwa na ilikuwa muhimu.

 

Hebu na tusahau sasa habari za wageni waliohudhuria arusi na kunywa mvinyo. Neno yayin (SHD 3196) linatokana na shina la neno lisilotumika la yayan  kuchachusha au kughoshiwa. Ilikuwa ni mvinyo huu kama mvinyo ulioghoshiwa na kwa hiyo, inaweza kumaanisha pia kama kulevya. Kuna mwingine ambazo zinamaanisha mvinyo huu ili usiweze kunywewa, na kule kutajwa kwake mvinyo huu kwenye Biblia unatajwa juisi ya zabibu zisizochacha. Mtazamo huu unachukuliwa kimakosa kwenye uelewa wake wa Maandiko Matakatifu. (Rejea kwenye jarida la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188)).

 

Kwene Maandiko Matakatifu mvinyo kwa kawaida unafananishwa na habari njema na zene furaha. Wakati Mariamu aliposema, “Wameishiwa na mvinyo”, anaweza kuwa alikuwa anamaanisha ukweli wa kwamba hawakuweza kuwa na furaha ya kipawa cha Roho Mtakatifu (1Wathesalonike 1:6). Hata wanafunzi wa Kristo walipata ugumu kuelea kile Masihi alichokuwa anajaribu kuwafundisha. Walikuwa wanaanza tu kwa kweli kuelewa neno la Mungu wakati Roho Mtakatifu alipowashukia siku ya Pentekoste.

 

Mariamu alikuwa na imini kubwa kwa mwanawe. Kungekuwa na idadi ya watu pale ambao wangemwonea mashaka Kristo ukweli wa kwamba mimba yake ilitungwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Huenda mama yake angempasa akaguliwe ili kumthibitisha mbele y wote waliokuwepo. Mafarisayo kwa mfano uliofuatia, walipokuwa wanaitetea haki yao, walitangaza walimpazia sauti zao kwa nguvu wakimwambia Yesu, “Sisi sio watoto wa zinaa,” (Yohana 8:41), ikiashiria vile alivyokuwa Kristo. Inayewekana kuwa huenda Mariamu alidhaniwa kuw wa namna hii kwenye fursa ya kueneza uvumi wa namna yoyote aliyeweza kuwa amezungukwa.

 

Aya ya 4: Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.

 

Kristo anaelekeza majibu yake kwa mama yake. Kristo anatumia neno ‘mama’ akimaanisha kimfano kulitaja taifa la kimwili ya Israeli na akionyesha ukuhani wa kimwili.

 

Wagalatia 4:4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,

 

Tunaweza kudhani kwamba Kristo alikuwa anawaambia makuhani kwamba hawajui anachokwenda kukifanya na kukianzisha kwenye agano lilolopo sasa na kwamba utaratibu wa utoaji wa dhabihu walionao unakwenda kukamilika katika yeye. Kristo anaonyesha tofauti kati ya utaratibu wa kimwili wa kidini wa siku zile na kile alichokuwa anakwenda kukihitisha ambacho ni kuzaliwa tena kwa mwili wa kiroho (Yohana 3:5).

 

Ndiyo, kipindi cha kutolewa kwa dhabihu ya Kristo ulikuwa umekaribia. Lakini mchakato wote mzima unaoendelea yapasa uwe sawasawa,na mapenzi ya Mungu. Hatuwezi kubadili ni nani, ni wakati gani, au jinsi ya yule,tunayemwabudu ambaye ni Mungu wa Pekee wa Kweli.

 

Ukristo mamboleo uliopo sasa umepotoka kwa kutoelewa kile ambacho upande wa pili wa agano hilihili inachohitaji na kwa ajili hii wanajikwaa (Waebrania 10:1-31). (Rejea kwenye jarida la Tofauti Kwenye Torati (Na. 96)). Kusudi la Kristo limeshindwa kueleweka na mashirika mengi ya kidini. Ili kuelewa vizuri zaidi jambo hili rejea majarida ya: Lengo la Uumbaji na Sadaka ya Kristo (Na. 160) na Kazi ya Mwasihi (Na. 226).

 

Aya ya 5:  Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

 

Maneno haya ya mama yake Yesu yanahusiana na maneno yaliyonenwa na Musa kuwaambia Israeli wa kimwili kuhusu Masihi.

 

Kumbukumbu la Torati 18:15 Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.

 

Mama yake aliyewakilisha Israeli ya kale, alielewa kwamba amri zilipaswa kushikwa (Kumbukumbu la Torati 26:17-19). Sheria ya utoaji dhabihu ilikuwa inakubalika kwenye sheria zote (Kutoka 20 to 34). Sheria ya utoaji dhabihu ilimlenga \masihi na ilitimilika kwa yeye. Sheria hii haikuondolewa kwa tendo hili. Mfuatano wa matukio ya utaratibu huu wa ibada haukubadilishwa. Mfano shirio wake ulikuwa na maana nyingine tu (soma jarida la Agano la Mungu (Na. 152)). Kristo alisema:

 

Mathayo 5:17-19 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. 19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.

 

Tumeamriwa kuendelea kwenye sheria kamilifu na yenye uhuru (Yakobo 1:25).

 

Haya ni maneno ya mwisho yaliyoandikwa ya mama yake Yesu Kristo. Tunaona kwamba walikuwa ni hawa wenyewe tu ndio walioambiwa wamtii Kristo. Hakuwaelekeza watumishi wamwendee mtu mwingine yeyote. Kwa kuwa ni kwa huyo Kristo tunaokolewa (Matendo 15:11). Tunaona kwamba Kristo anamsikiliza mama yake kulitenda jambo hili. Hii inapotosha pia ukweli kwamba mwitikio wa maonyo ya unabii umekuwa ukichukuliwa kuoka kwa makuhani wa kimwili wa Israeli ya zamani na limepewa Kanisa, watumishi wa Mungu. Zipo kwenye uangalizi wa Kanisa sasa Maonyo ya Mungu (Na. 184)).

 

Tungedhania kwamba fundisho hili lingeweza kuonekana kuwa limechukuliwa na wakati Kristo alipomuweka mama yake chini ya uangalizi wa Yule “mwanafunzi aliyempenda””.

 

Yatupasa kuwa makini kwamba neno mwanafunzi aliyempenda kwa maana kubwa kwamba aliwapenda wale aliopewa na Mungu. Aliutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake (Yohana 15:13). Mwanafunzi aliyempenda laweza kuwa hi neno la mfano lililotumika kulielezea Kanisa

 

Yohana 19:26 Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake

 

Tunapoliangalia andiko hili kwa mwangaza wa yeye ambaye watu hawa wawili wanaweza kujifunza kutoka kwake, tunaona kuwa Kristo alikuwa anaonyesha kuwa Makuhani Walawi ambao Kanisa limeanzisha ulikuwa ni wa mwana wake. Alikuwa ni kwa huyu mwanae kwamba urithi unakuwa. Kristo analiambia pia Kanisa kuwa linapaswa kulijua na kuliheshimu agano walilopewa na kulishika Israeli wa zamani. Tutakwenda kuiona hii imewekwa kwenye taratibu za kikanuni kwenye amri ya tano isemayo Mheshimu Baba yako na Mama yako (Kutoka 20:12). Tangu kifo cha Kristo, Kanisa linawajibika kushika maagizo yaliyo kwenye Agano, pamoja na sheria zote na kanuni zake Mungu.

 

Katika siku moja, kama Maandiko Matakatifu yalivyonena kabla, kuna dhabihu moja ambayo itakuja kuikomesha na kuundoa utaratibu wa utoaji dhabihu wa Walawi (Malaki 2:3), kwa hiyo utaratibu mpya wa makuhani, ulio mfano wa ukuhani wa Melkizedeki utaanzishwa. Ilikuwa ni kwa sababu hii ndio maana alipoambiwa kuwa mama yake na ndugu zake wapo nje wanahitaji kuongea naye kwa mazingira aliyokuwanayo ya kuongea na Mafarisayo aliwanyooshea kidole wanafunzi wake na kusema: “Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!.” Alisema kuwa mama yake na ndugu zake walikuwa ni wale waliokuwa wanayatenda mapenzi ya Baba yake aliye mbinguni (Mathayo 12:46-50).

 

Wale wanaosadikika kuwa ni wafuasi wa Kristo leo na huku wakizipuuzia amri na sheria za Mungu wapo kwenye kundi la waivunjao amri ya tano isemayo; mheshimu Mama yako na Baba yako. Kwa kutozingatia na kuzikubali amri za Mungu na sheria zake mioyoni mwao, basi walikuwa wanasema moja kwa moja kwamba walikuwa hawamchukui mama yake Kristo majumbani mwao. Wangekuwa wamelikataa kulishika na agizo la Kristo la kuwataka wamchukue na kumtunza huyo mama yake, kwa kuwa wangeona kuwa sheria za Agano la Kale hazina ulazima wowote tena, na kwamba hazihitajiki kuzishika tena. Kwa hiyo wangeivunja sheria kwa kutompenda na kumheshimu mama yake Kristo na kumuona kama wa kwao.

 

Kumbuka kuwa Mariamu alikuwa na watoto wake wengine wa kiume aliyewazaamwenyewe ambao angeweza kuondoka na kwenda kuishi nao. Lakini wakati tunapomtathimini kila mmoja kwa kuchukulia mfano sehemu mbili la Agano la Mungu, tunaona kwamba walipasa kuwekwa wawiliwawili na kuishi pamoja. Agano la kwanza halikuwa limeondolewa na kukoma, bali liliendelea hadi kwenye hili la pili.

 

Mama yake Kristo hakumuomba msaada kila mtu pale arusini. Hamuombi kila mtu kumwendea na kumpa mkono. Ni wale tu waliokuwa pale wamehudhuria ndio walichaguliwa kwa kazi ile. Wale wanaomtii Mungu na Mwanae Yesu Kristo walioelezwa kwenye Maandiko Matakatifu kuwa ni watumishi. (2Nyakati 24:9; Tito 1:1; Yuda 1:1; Yakobo 1:1; 2Petro 1:1). Kwa kuwa hilo ndilo lengo letu, kutumika na si kutumikiwa.

 

1Wakorintho 4:1 Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.

 

Anawatumia watu dhaifu na wanyonge wa dunia hii ili kuwaaibisha wenye nguvu (1Wakorintho 1:27).

 

Sisi, Kanisa, tunsaendea kumwabudu na kumii Mungu wa Pekee na wa Kweli, Eloa, kuzishika Sabato zake, Miandamo ya Mwezi Mpya, Sikukuu zake na Siku zake nyingine takatifu  (soma jarida la Siku Takatifu za Mungu (Na. 97)). Hatujapewa mamlaka ya kuzivunja au kuziondoa sheria za Mungu na kumuweka Eloa, Mwenyezi Mungu kwenye muundo wa Uungu wa kiutatu (soma majarida ya Mungu Tunayemwabudu (Na. 2) na Amri Iliyokuu ya Kwanza (Na. 252)).

 

Aya ya 6: Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.

 

Mapokeo ya Kiyahudi yalihitaji kufanyika kwa uoshaji wa namna mbalimbali wa kukamilisha maagizo na taratibu za kidini. Wayahudi walisisitiza sana kuosha mikono yao kabla kula chakula, katikati yam lo na baada ya kumaliza kula. Aina hii ya utakaso iliendelea sio kwa kuosha mikono yake mtu peke yake, bali pia ni kwa mtu kuosha vikombe vyake na sahani zake (Marko 7:3, 4).

 

Vyungu vyenye maji vilitumika kwa kuhifadhia maji. Watu wamefananishwa na vyombo kama hivi  kwenye Biblia (Isaya 66:20).  Vyungu hivi sita vya kuhifadhia maji vinaweza kuwa vinawakilisha mwanadamu, kwa kuwa sita inaaminika kuwa ni tarakimu mwanadamu. Vikiwa vimetokana na moto vingefananishwa na ukweli kwamba kwa kuyaamini na kubobea kwenye mapokeo yaliyotungwa na wanadamu, mioyo yetu ilifanyika kuwa migumu kama jiwe.

 

Kristo analiendeleza wazo hili wakati alipowakataa Mafarisayo. Kristo alifundisha kwamba yatupasa tusafishe kwanza kile kilicho “ndani ya kikombe” na ndipo hata kile kilicho nje kitakapokuwa kisafi pia (Mathayo 23:26). Kikombe kilitumika kwa kuwa kilikuwa ni chombo kinachoweza kushikilia maji na kwa hiyo ni mfano wa kifaa au chombo.

 

Nabii Ezekieli aliongelea juu ya kubadilishwa kwa vyombo hivi kutoka kwenye moyo wa jiwe, na kufanyika kuwa ni vyombo vilivyojazwa Roho wa Mungu, vikiwa na hamu ya kweli nay a kumaanisha ya kukaa kwenye neno la Mungu.

 

Ezekieli 36:25-27 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote. 26 Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.27 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.

 

Ezekieli anaongelea usafi wa kunyunyiziwa na Roho Mtakatifu. Tutapewa moyo mpya na kwa hiyo tutazitii sheria za Mungu. Sheria za Mngu ambazo zilikuwa zimeandikwa kwenye mbao za mawe, zitaandikwa kwenye vibao vya mwili mioyoni (2Wakorintho 3:3).

 

Yatupasa kusafisha mioyo yetu ya uovu na kutakasa mioyo yetu.

 

Yakobo 4:8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

 

Vyombo hivi vya utakaso bado vinatumika hata leo. Yatupasa tuweze kuona kwamba sisi vyombo vya Mungu Aliye Juu Sana. Na kama tunazishika sikukuu za dini za kipagani, zilizoanzishwa na wanadamu, kama vile sikukuu za Kristmas na Easter, ndipo kwa kweli tunakuwa kama Mafarisayo. Tunachotakiwa kufanya ni kujisafisha sisi wenyewe kwa nje, kwa muonekano peke yake, tukishuhudiwa na wote kuwa tunazishika sheria zake ‘tukiziacha amri za Mungu na kuyashikilia kufuata mapokeo ya’ (Marko 7:8).

 

Yatupasa kutilia maanani zaidi kutakasa mioyo yetu kwa kuzitii sheria za Mungu kwenye kweli yote. 

 

1Petro 1:22 Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo.

 

Yatupasa tujiulize wenyewe swali hili, “Je, sisi bado tunajiosha kwa nje na tukiwa hatuzishiki amri za Mungu? Je, bado tunaziadhimisha sikukuu zilizoamriwa na siku nyingine zote za ibada kwa ajili ya mapokeo yaliyoanzishwa na wanadamu, na hasahasa yakiwa chini ya mwavuli wa Mungu au dini? Je, tunamtii Mungu kikweli? Je, tunao upendo wa dhati kwa wapendwa wenzetu wa imani moja? Je, mioyo yetu iko safi?”

 

Dunia hii ipo ili kutuonda sisi mbali kabisa na Mungu. Yatupasa tufikirie juu ya toba yetu kuzitubia dhambi tulizozifanya kwa kuzishika sikukuu za kipagani na kuamua kubazitwa kabisa ili kuziosha na kuziondolea mbali dhambi tulizozitenda huko nyuma (Matendo 22:16). Wale waliobatizwa yawapasa kuendelea kujitakasa mioyo yao kwa kumtii Mungu na sheria zake. Tukimkaribia Mungu naye atatukaribia sisi (Yakobo 4:8).

 

Aya ya 7: Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.

 

Sasa ni Kristo peke yake anayewaambia wanafunzi wake, kwa kuwa wanaliwakilisha Kanisa. Anatuamuru sisi kuijaza mitungi ya maji. Twaweza kudhania kwamba Kristo anatuambia sisi kuwajaza watu walio kwenye mataifa kwa maji ambavyo tunaweza kuchukulia tendo sawa na neno la Mungu. Kwa hiyo mitungi ya maji tuliyoijaza ili kuwaosha mataifa mikono na vikombe vilivyojazwa maji ili kuashiria kuoshwa kwa mataifa kwa njia ya neno la Mungu (Waefeso 5:26).

 

Waebrania 10:22 na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamiri mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi.

 

Ni wajibu wetu kuihubiri injili kwa mataifa yote, ambayo ni ishara ya kuvijaza vile vyombo hadi juu. Hakuna taifa au watu walioachwa nje ya wale wasionufaika na sadaka au dhabihu ya Kristo isipokuwa ni Wanefili peke yao (soma jarida la Wanefili (Na. 154)).

 

Wote tunakazi ya kufanya, na yatupasa kuifanya kwa uaminifu mkubwa. tll have a job to do, and we una Mungu muaminifu, ambaye kila wakati yupo hapa. Tunaongozwa hatua kwa hatua. Miujiza isingeweza kutokea kama watumishi wake wasingetii, au kufanya walichoambiwa kukifanya. Wanaweza kuwa hawakuyaamini yatakayotokea, au waliendelea kuwa na mashaka mioyoni mwao. Sisi ni muujiza unaoendelea, hivyo ni kusema, Tumejazwa na Roho wa Mungu. Mara tu tukiacha kumwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, na tukaacha kumwamini mwanae, ni wakati ambao muujiza wetu unaacha kutokea.

 

Aya ya 8: Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.

 

Kristo aliyageuza maji kuwa divai. Sasa tunajua kwamba Kristo ni divai na sisi tulio watu wake, ni matawi (Yohana 15:1-11). Kuwa mawazo fulani kwenye aya hizi yanahusiana na sherehe hii ya arusi. Kristo aliyageuza maji yaliyokuwa kwenye vyungu na kuwa divai. Tunaona kutokana na aya za hapo juu kwamba Kristo ndye mvinyo wa kweli. Kila tawi ndani yake linapasa lizae matunda. Kwenye Yohana 15:3 tunasoma kwamba tumekuwa safi kwa neno. Tumeambiwa kuwa ndani ya Kristo. Sisi tulio matawi “Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.” (aya ya 4). Kwa jinsi hiyohiyo, watumishi hawakuweza kuwa na mvinyo bila kuwa ndani ya Kristo.

 

Na karidi arusi ilipokuwa inakaribia, ikiashiria taswira ya zama hizi zetu, ni sehemu ndogo tu walikuwa wanaondoka kwa Mshereheshaji. Bwana Mungu ni “Bwana wetu” (Yeremia 3:14). Watumishi wanawakilisha wale wene ushuhuda na imani ya Yesu Kristo. Watumishi waliambiwa kuwa sasa wanaweza kuchota kwenye vyungu vya maji. Hii inaonyesha mbele kwenye uhai wa Kristo uliotolewa na damu yake ilimwagika kwa ondoleo la dhambi.

 

Warumi 6:22 Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele.

 

Tumepewa fursa ya kuchota mvinyo. Sisi kama watumishi tumepewa fursa ya kuja kwenye ushirikiano mwema na Mungu na Mwana wake. Hatupaswi kuikataa fursa hii, bali na tuitumie na tuende mbele za Mungu tukiwa kama watumishi wa Kristo (Wagalatia 1:10; Wakolosai 4:12; Warumi.1:1) ambaye yeye mwenyewe anamtumikia Mungu (Wafilipi. 2:5-8).

 

Aya ya 9: Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,

 

Mungu ameiandaa arusi na amemwandaa bibi arusi. Anautumia mfano huu ili kulinganisha na wokovu wa mwanadamu. Kikombe kinachotumika kuchotea maji kinafananishwa na mwanadamu, anayeonekana kumuwakilisha Kristo aliye limbuko la malimbuko yote na kinaweza pia kufananishwa na wale wanaounda mkusanyiko au mwili wa wateule. Hawa ni wale waliochukuliwa kutoka hapa ulimwenguni, kutokana na dhabihu ya Kristo, na wamemwagwa kama sadaka ya kinywaji kwa Mungu Aliye Juu Sana.

 

Twaweza kujifunza somo kutokana nah ii. Roho wa Mungu hapaswi kuachwa kwenye vyombo. Alilazimu kuletwa mbele za Mungu, afungiwe kama ilivyokuwa. Tunapaswa kujitoa kwa Mungu, kama sadaka zilizohai. Tumekirimiwa vipawa kwa kupitia Roho Mtakatifu ambazo hazifai zipotezwe tu kirahizi (Mathayo 25:14-30).

 

Mungu anaujua mwisho tangu mwanzo wake (Isaya 46:10; Ufunuo 1:8). Twaweza kujionea hapa kuwa Mungu, Baba yetu hana upendeleo. Kila amchaye na kuishi sawasawa na neno lake anakubalika machoni pake.

 

Watumishi walijua ulikotoka mvinyo. Kama watumishi hawa ni sisi tunaojua, ndipo yatupasa wote tujue kuwa tu sehemu ya mwili wa Yesu Kristo, na kwamba tumeokolewa kwa kupitia uingiliaji kati wa Yesu Kristo na karama ya Roho Mtakatifu. Tumepewa kujua kwamba kuna miujiza iliyohusika na kwamba Roho wa Bwana ndiye mwili ule. Huyo ni Roho wa Bwana, Roho wa kweli, aliyemtia mhuri Kristo na ndiye anayetutia mhuri na sisi sote pia, na ndiye anayetuwezesha sisi kuwa ni sehemu ya mwili huo. Tunafanyika kuwa sehemu ya Mungu, kama Kristo alivyofanyika kuwa sehemu ya Mungu. Tunaishi ndani ya Kristo, na Kristo na Mungu Baba wanaishi ndani ya kila mmoja wao. Sote tunauhusiano unaoingiliana. (Rejea kwenye jarida la Maana ya Mkate na Divai (Na. 100)).

 

Aya ya 10: akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.

 

Mungu, Baba yetu anafanya tofauti kati yake yeye mwenyewe na jinsi wanavyowaza wanadamu na jinsi wanavyotenda. Baba yetu wa mbinguni anafikiri, anatenda na anatilia maanani kwa kiwango kikubwa sana kiasi kwamba hakuna hata mmoja wetu angaliyeweza kudhani kabisa. Uelewa wa Mungu ni mkubwa sana na mawazo yake yapo juu sana (Zaburi 147:5). Baba yetu wa mbinguni hakosei na anajua kila jambo (Ayubu 37:16).

 

Kitendo cha kuwapa mvinyo bora zaidi baadae kwenye sherehe hii ya arusi kunahusishwa kwenye Maandiko Matakatifu. Mungu alishasema hapo mwanzoni kuhusu utukufu wa hekalu utakavyokuwa katika siku za mwisho.

 

Hagai 2:9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi.

 

Arusi iliyo kwenye injili ya Yohana inaenda sambamba na agano ambalo Mungu aliliweka na Ibrahimu na sasa linaendelea na Kanisa la Mungu.wyatupasa sasa kuitakasa mioyo yetu ya jiwe na kuwa na mioyo ambayo ameiandika sheria zake.

 

Sisi sasa ni washirika wa mwili wa Kristo. Kama utasoma kile anachokisema Kristo kwenye Yohana 15:1-11 tunaona kwamba aya hizi zinahusiana na matukio ya kwenye arusi ya Galilaya na kwenye Kanisa linaloshiriki agano na Mungu. 

Yohana 15:1-11 Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. 2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa. 3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. 4 Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu. 5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. 6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea. 7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. 8 Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu. 9 Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu. 10 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. 11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.

 

Matendo au harakati za Yesu Kristo katika kuja na kuzaliwa kwake katika mwili hazikulihalifu au kutangua agano aliloliweka Mungu na Waisraeli. Kristo alilifanya upya agano hilo na kufanya au kuweka utaratibu mpya na wa hali ya juu wa mwingiliano uliopo na wanadamu kwa njia ya Roho Mtakatifu. Sisi kwa kulishika agano la Mungu, tunajifanya wenyewe kuwa tayari ni mabibi arusi kwa ajili ya arusi ya mwanakondoo (Ufunuo 19:7).

q