Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[058]

 

 

 

Mwaswali Yaulizwayo Mara kwa Mara Kwenye Masomo ya Biblia ya Agano Jipya

(Toleo La 2.0 20000630-20011206-20091125)

 

 

Mwaswali Yaulizwayo Mara kwa Mara Kwenye kwenye maandiko ya Agano Jipya yameorodheshwa hapo chini, ndiyo haya.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 2000, 2001, 2009 Wade Cox)

 

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 



YALIYOMO KWA MUHUTASARI


 

Masihi…Mwana wa mtu-mtoto Pekee-Mwana wa Pekee, mwana aitwaye Yesu, Nabii wa Mungu-sadaka ya Dhambi-Imani kwa Kristo-Ubatizo wa Kristo-Njia pekee kwa Baba-Kuhani-Yoshua-Wengine walimuita Yesu-Barua ya Pilato-mwaka wa Kusulibiwa-Msalaba-Ufufuko-wa Kimwili au wa Kiroho-Mwili wa Yesu-Israeli walioolewa na Kristo-Dhabihu-Kundi dogo la wanafunzi-Yesu Mwokozi-Mafundisho-Asiyekula nyama-Neno la Yesu au la Mungu-Mkuu-Malaika wa Ufunuo-Yesu/Biblia.

Roho Mtakatifu…huyu Roho Mtakatifu-Mungu humtoa Roho Mtakatifu-Roho/Roho wake-Ufalme wa Mungu-Maji/miamba.

Mathayo…Mathayo 2:2;-2:13;-2:17-18;-6:5-15;-12:50;-17:21;-20:13;-28:19

Marko…Marko 5:21-43;-7:15;-10:18

Luka…Luka 12:36;-17:11;-19:12;-23:43

Yohana…Yohana/Mwanzo-Yohana 5:1-24;-5:18;-7:52;-Sura ya 10;-12:12-13;-19:31

Matendo…Hakuna neno amen-Matendo 1:15;-15:24-29;-15:28:29

Warumi…Warumi sura ya 1-Warumi 3:20;-10:4;-Sura ya 14;-16:16

1Wakorintho…1Wakorintho 5:5-6;-11:10-15

Wagalatia…Wagalatia 4:9-11;-4:10

Waefeso…Waefeso 3:15

Wafilipi…Wafilipi 2:10

Wakolosai…2:14;-2:16;-2:18;-4:3

2Wathesalonike…2Wathesalonike 2:3-4,6

1Timotheo…1Timotheo 4:1-3

Waebrania…Waebrania 7:3

Yakobo…Mwanzo wa Yakobo-Yakobo 1:17

1Yohana…1Yohana 5:7

Ufunuo…Mafunuo ya Mtakatifu Yohana-Ufunuo 1:4;-5:6;-2:17;-2:20;-2:28;-3:7;-3:12;-4:2-6;-5:12-17;-6:2;-6:4;-6:5;-6:8;-7:14;-8:10;-sura ya 9;-sura za 10;-13:18;-sura za 14;-17:5;-20:10;-20:15;-21:18;-21:1;-hali Ngumu ya Yakobo ya dunia-Kile knachotokea kwenye ufufuo wa Watoto wa kwanza wawajuao wazazi walio chini ya mamlaka ya mlo wa Arusi ya Yesu-Watakaohudhuria-Mji wa Mungu -

Kalenda…Wakati inapotimi saa la 3 la Ikwinoksi-Mwandamo wa Mwezi Mpya-Mwezi Mchanga-Kalenda ya uwongo-Mwaka wa Zaka-Ushahidi wa kipindi cha kiza cha mwezi-Mwandamo wa Mwezi Mpya wakati wa Kristo-kalenda ya Karaite-Tarehe lengwa-Pasaka: Usikuwa wa Kuuangaliwa sana-Hesabu ya Omeri-Mkate & Mvinyo-Kuoshana Miguu-Meza ya Bwana

Kanisa…Siku Takatifu za Wakristo-Ufalme wa Mungu-Mamlaka\ya Kubadili mafundisho-Masharti ya kuwa Mkristo-fursa ya Pili-Mteule-Mahali alipo Mungu-Ni S-Ni Sabato au Jumapili:Kuna ushahidi wowote katika kuishika na kuabudu siku ya Jumapili-kuna msaada wowote kwa upande asi wa Sabato-Wengi huabudu siku ya Jumapili-Ibadaa ya Kipagani ya Wapagani ya Jua-Dhana isemayo Kila siku ni Sabato-Kwa nini ni Jumapili sasa-Kanisa la Kwanza lilifanyaje-Mabaraza Manne ya Mitaguso-Mababa wa Kanisa na mpango wa Mungu kwetu -

Ibada za Kipagani: Easter-Utrinitari

Mpingakristo…Mpingakristo & Torati ya Musa-Mafundisho-Yesu akishukiwa kuwa mpingakristo.

 

 

************************************

 

MASWALI YAULIZWAYO MARA KWA MARA KWENYE AGANO JIPYA FAQ NEW TESTAMENT

 

Masihi

Ni nani Mwana wa adamu? Kwa nini aliitwa Mwana wa Adamu?

Jibu: Kulikuwa na wana wa Mungu wengi ambao Kristo alikuwa mmoja wao tu (Ayubu 1:6; 2:1; 38:4-7). Ni wale tu waliozaliwa wanadamu. Hii ndiyo maana lengwa ya neno monogenes theos au aliyezaliwa na mamlaka ya kiuungu ya Yohana 1:18 na Mithali 30:4-5.

 

Hii ndiyo dhana iliyoko nyuma ya andiko la Waebrania 1:8-9 iliyochukuliwa kutoka kwenye Zaburi 45:6-7. Kwenye Waebrania inazidi kwenda mbele kwa kuonyesha kwamba elohimu hakuwa tena kama sawa na malaika walioitwa wana wa Mungu. Bali alikuwa ni kuhani mkuu mpya kama mwana wa adamu.

 

Soma majarida ya Zaburi 8 (Na. 14); Uwepo wa Yesu Kristo wa Kabla ya Kuzaliwa Kwake (Na. 243); Jinsi Mungu Alivyofanyika kuwa Familia (Na. 187); na Kusudi la Uumbaji na Dhabihu ya Kristo (Na. 160).

 

Kwa nini Biblia inasema " Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, (monogene)"? Angewezaje basi kuwa wa pekee kama kusingekuwa na wana wengi wengine?

Jibu: Kuna wana wengi wa Mungu kama Maandiko Matakatifu yanavyosema. Hata hivyo, yeye alikuwa ni wa kwanza kuzaliwa. Wengine walikuwa ni wale walioumbwa wakiwa kama wana wa namna ya Kimalaika. Alikuwa ni Prototokos au Mwanzo wa Uumbaji wa Mungu na ni Stadi wa Uumbaji wa Mungu. Yeye pia ni Limbuko au Prototokos la waliokufa. Hata hivyo, yeye ni mzaliwa wa pekee wa Mungu au monogenes theos aliyetajwa kwenye Yohana 1:18.

 

Mambo haya yameelezwa kwa kina kwenye majarida ya Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229); na Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243).

 

Kwenye Zaburi 2:7, Matendo 13:33, na Waebrania 1:5 tunasoma: “Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa. na Yohana 1:14 “utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba.” Ni nini maana ya neno “mzaliwa wa pekee”? Wakati Kristo alipozaliwa na kwa nini hasa ameitwa Mwana mzaliwa “PEKEE” wakati malaika wakiwa pia ni wana wa Mungu? Je, usemi huu wa kuwa amefanyika kutokana na roho na kuwa mwanadamu mwenye roho?

Jibu: Ilitokeza kwa makusudi kabisa kwa Watrinitariani. Kuna majina mawili: moja ni la “Prototokos” lenye maana ya “mzaliwa wa kwanza” na linguine ni “monogenes” ambalo maana yake ni “mzaliwa wa pekee.” Jina linalofanana na Kristo kuwa ni kama mzaliwa wa kwanza na aliyezaliwa kwanza aliyefufuka kutoka kwa wafu ni “Prototokos.”

 

Anatajwa kuwa ni kama “mzaliwa wa kwanza wa Mungu” kwenye Yohana 1:18 kutokana na neno “Monogenes Theos.” Andiko hili lilibadilishwa kwenye Receptus ili lisomeke “mtoto pekee kuzaliwa” au “muunganiko wa monogenes” na kisha ikatafsiriwa kama “mwana mzaliwa wa pekee.” Hii ilifanyika ili kugeuza au kupotosha tofauti kati ya ukweli kwamba kulikuwa na wana wengine wengi wa Mungu wakiwa malaika, ambao kwamba Kristo ndiye “prototokos”, bali ni ndiye aliyezaliwa na kwa hiyo, alikuwa ni mzaliwa wa pekee “mungu” au “theos.”

Majina haya yamechambuliwa kwa kina kwenye majarida ya Mteule Kama Elohimu (Na.1) na Malaika wa YHVH (Na. 24); Ustadi wa Uumbaji wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229) na Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Duniani (Na. 243).

 

Kuna mahali popote kwenye Biblia ambapo Yesu anajiita Mwenyewe kuwa yeye ni Mungu?

Jibu: Anaitwa Mungu kwenye maandiko mengi ya Biblia. Hajitaji mwenyewe kuwa ni Mungu, bali maandiko yanafanya hivyo na inamtaja kuwa ni mungu mdogo. Kwa mfano, andiko lililo kwenye Zaburi 45:6-7 linaonyesha wazi sana kuwa ni Kristo ndiye aliyetiwa mafuta kuwa Mungu na Mungu wake kwa mafuta ya furaha awe juu ya washirika wake kwenye Waebrania 1:8-9. Uhusiano uliopo kati ya Malaika Mkuu wa Agano la Kale kama elohim ni jambo la muhimu sana kwenye Teolojia ya Biblia.

 

Muundo wa uhusiano huu umeelezwa kwa kina kwenye majarida yafuatayo: Mteule Kama Elohim (Na. 1); Malaika wa YHVH (Na. 24); na Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kweke Duniani (Na. 243). Tangazo la ukiri wa imani la Ulfilas, askofu wa Wagoths, limeainishwa kwenye jarida hili, pia linaainisha uhusiano huo. Jarida la Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127) litakuonyesha kwamba Kanisa la Mwanzo lilifundisha na kueleweka kuhusu jambo hili.

 

Je, Yesu alikuwa nabii?

Jibu: Musa alisema kwamba ndivyo alivyokuwa. Alisema kuwa Mungu atawainulia nabii kama alivyo yeye, Musa na kwamba iliwapasa wamsikilize yeye. Kwa hiyo, yeye alikuwa Kuhani, Mfalme na Nabii. Soma jarida la Yesu Kristo, Mfalme, Kuhani na Nabii (Na. 280). Maneno haya, kama yalivyoandikwa, yanaonyesha kuwa ni unabii, na yalotimilika kama alivyosema. Alinena kwa mujibu sawa na Torati na Ushuhuda (Isaya 8:20). Hiki ndicho kipimo cha nabii.

 

Mwanzo 4:7 inasomeka hivi: “Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni. Na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.” Tafsiri ya The Companion Bible inaonyesha dhambi – kama sadaka ya dhambi. Je, kinachoatajwa hapa kwa njia ya mfano na isiyo moja kwa moja kuwa Masihi kuwa ndiye sadaka hii ya dhambi iliyotajwa kwenye Zaburi 22 na mlango ulioandikwa kwenye Ufunuo 3:20 na damu ya kwenye miimo ya milango ya kwenye Kutoka 12:7?

Jibu: Ndiyo, ni andiko muhimu sana. Waaka kwa Waebrania unatilia mkazo kwa kusema “kweli” na pili “iwapo kama”. Bullinger anasema kwenye tafsiri ya the Companion Bible akitilia maanani andiko linalofana kuwe na uwezekano kamili na mtakatifu. Kwa Kiebrania ni “chat'a” na maana yake ni sadaka ya dhambi kama ilivyoongezwa kwenye Kutoka 30:10; Walawi 4:3; 6:25; 8:2; Zaburi 40:6 (sawa na 2Wakorintho 5:21; Waefeso 5:2).

 

Neno “lieth” ni la kiume na sadaka ya dhambi ni la kike. Kwa Kiebrania linasomeka: “kwenye lango la kuingilia [mwanaume] ipo, au sadaka ya dhambi.” Pia tazama kwenye Mwanzo 3:16 isemapo “tawala.” Masihi, kama tujuavyo ni sadaka ya dhambi. Tazama kwenye majarida ya: Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246); na Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya 2 Kizazi cha Adamu (Na. 248).

 

Wakristo wote wanaonekana kuamini kuwa wanahitajika kuwa na imani, lakini ni kuamini nini? Je, inamaana gani dhana hii ya kumwamini Kristo?

Jibu: Imani ni tumaini liendanalo na kumuamini Mungu na kuamini kuwa anaweza kuuleta wokovu wa kila mmoja, kwa mpango aliokusudia, ambao utafanya kazi kwa manufaa ya wata kazi kwa manufaa ya watu wote. Mungu ataufanyia kazi wokovu wa viumbe wake wote ili asiwepo mwene mwili yeyote atakayepotea.

 

Imani hii imeelezwa kwenye matendo ya Kanisa kwa kupitia historia yote tangu Adamu hadi sasa. Waebrania sura ya 11 inakupa orodha ya watu muhimu wanaojulikana kama mashujaa wa imani, na matarajio yao ya kila wakati na matendo yao. Wokovu haupatikani kwa kupitia imani iliyotajwa katika Kristo. Wokovu, kama watakatifu wa Kanisa, unapatikana kwa kuzishika Amri za Mungu na Ushuhuda au Imani katika Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12). Kristo mwenyewe alikuwa na imani kwa Mungu aliemuokoa.

 

Ni imani kwa Mungu ndiyo inayookoa kwa kupitia matendo ya Yesu Kristo aliyemtuma (Yohana 17:3). Wengi wamemuita yeye “Bwana, Bwana” na atawaambia “Tokeani kwangu, maana siwajui ninyi.” Kama unampenda Kristo, basi zishike amri.

 

Wakristo wamebatizwa kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, bali unadhani ni maneno gani aliyatumia Yohana Mbatizaji alipokuwa anambatiza Kristo?

Jibu: Ubatizo wa Yohana ulikuwa kwa ajili ya toba ya dhambi na kwa ajili ya maelekezo ya kuitayarisha njia kwa Yahova na kutengeneza mapito yanooke, kutokana Isaya 40:3 ambayo imenukuliwa kwenye Mathayo 3:3. Ubatizo wake haukufanwa kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu. Kristo alibatizwa ili ampokee Roho Mtakatifu, ambaye alimpokea, kama walivyompokea pia manabii wa zamani nyuma yake. Maneno yake yanaonekana kuwa: “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake;.”

 

Amri na maagizo yake kwa Kristo yalikuwa: “Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!(Yohana 1:29)) na alisema ninahitaji kubatizwa na wewe nawe waja kwangu.

 

Maneno yaloyo sehemu ya kwanza ndiyo yanayooekana kwanza kabisa kuwa kama yanatamkwa na yeye. Ambayo ni kwamba: “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba;.” Luka anaandika kuwa Kristo alikuwa anaomba pia huko (Luka 3:21). Mbingu zilifunguka na Roho Mtakatifu alishuka juu yake kama hua, na Mungu akasema, “Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.” Marko anamengi au machache ya kuandika kuhusiana na jambo hilohilo kama Mathayo. Hatujapewa maneno yenyewe halisi.

 

Je, ni kweli kuwa Yesu Kristo ndiye njia ya pekee ya kwenda kwa Baba?

Jibu: Kwenye Yohana 14:1-6 Kristo alisema kuwa yeye alikuwa ndiye njia pekee kwa Baba. Kuna vipingamizi vingi kwene tamko lake hili, lakini vipingamizi vyote vina msingi wa teolojia potofu nay a uwongo na kutoyaelewa maandiko ya Biblia.

 

Hoja ya kwanza: Mungu alinena na Musa na Mababa wa imani wa kale na manabii nab ado hawakumhitaji Kristo. Jibu ni kwamba hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu. Wamezaliwa tu katika Mungu, wakawa kifuani mwa Baba, aliyenena (Yohana 1:18). Kanisa la Kwanza lilifundisha kuwa Kristo ndiye alikuwa Malaika wa Agano la Kale aliyempa Torati nabii Musa na aliyenena kwa manabii. Justin Martyr anasema wazi kabisa kuhusu jambo hili kwenye kitabu chake cha “First Apology au Utetezi wa Imani wa Kwanza.” Pia soma jarida la Teolojia ya Mwanzo ya Uungu (Na. 127).

 

Mchakato wa ufufuo wa wafu unahakikisha kwamba hakuna atakayeweza uzima usioharibika au uzima wa milele isipokuwa ni kwa kusimama mbele za Kristo kwenye hukumu kama kiumbe aliyefufuka toka kwa wafu. Tazama majarida ya Roho (Na. 92); na Ufufuo wa Wafu (Na. 143). Na ndiyo maana mafundisho ya Roho Isiyokufa na Mbinguni na Motoni ni yasiyo ya kimungu na ni mafundisho yenye kukufuru.

 

Lilikuwa ni jaribio la kweli kwa Mkristo kwenye karne ya kwanza nay a pili. Yeyote aliyesema kuwa ni Mkristo na kwamba akifariki anakwenda mbinguni, hawakuwa wanamuamini. Walimhesabia kuwa hakuwa Mkristo. Kwa kupitia ufufuo wa miili wa wafu, kila goti sasa litapigwa kwa Kristo na hakuna mtu atakayekuja kwa Baba isipokuwa ni kwa kupitia yeye.

 

Mbali tu na Yesu Kristo kuwa Masihi au mwokozi wetu, yatupasa pia kumchukulia yeye kuwa kuhani, au huenda ni nabii au hata kuwa mfalme? Au basi yawezekasa kumuita kuwa alikuwa ni Mungu yeye mwenyewe?

Jibu: Ndiyo, yeye ni yote ya haya mambo yote. Yeye ni kuhani na ni kuhani mkuu wa mfano wa Melkizeeki. Yeye ni nabii, kama alivyosema Musa. Yeye ni Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana kwa kuruzukiwa na Baba.

 

Mungu wa Pekee wa Kweli pia alimchagua yeye kuwa ni mungu mdogo kwa kumtia mafuta ya furaha juu zaidi ya ndugu zake (Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-9). Hii ilionyeshwa pia kwenye Zekaria 12:8 wakati Malaika wa YHVH kichwani mwetu alikuwa ni elohim kama sisi wenyewe tutakavyokuwa elohim na Maandiko hayawezi kutanguka (Yohana 10:34-35). Tazama majarida ya: Mteule Kama Elohim (Na. 1); Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Duniani (Na. 243); Malaika wa YHVH (Na. 24).

 

Ni kwa nini kwamba neno la Kiyunani la Yoshua limetafsiriwa kwenye lugha ya Kiingereza kuwa Joshua isipokuwa wakati anapotajwa Yesu Kristo linatafsriwa kuwa Jesus ambaye ni Yesu? Kwani isingewezekana jina hilohilo lilivyo kwenye Kiyunani likatafsiriwa kama jina hilohilo moja kwenye lugha ya Kiingereza?

Jibu: Ndiyo, lilipaswa kutafsiriwa kwa namna moja hiyohiyo. Tofauti hii ilifanywa na Wayunani wenye mchanganyiko na Warumi alionuia kulitenganisha Agano la Kale na Agano Jipya ili wafanikishe azma yao ya kuziondoa Sheria au Torati ya Mungu. Habari hii imechambuliwa kwa kina kwenye jarida la Yoshua, Masihi, Mwana wa Mungu (Na. 134) (soma toleo la 2). Mabailiko yalifanywa pia kwenye majina ya familia yote ya Kristo kwenye Biblia pia. Soma jarida la Bikira Mariamu na Fa,ilia ya Yesu Kristo (Na. 232).

 

Wako wapi watu wengine wenye majina ya Yesu mbali na huyu Yesu wa Nazareti?

Jibu: Niyo, kwa kweli walikuwepo. Jina Iesous kwa kweli linatokana na uandishi wa Kiyunani wa jina Yoshua Yahoshua. Kulikuwa na namna mbalimbali ya kuliandika jina hili. Lilikuwa ni jina kuu na lenye heshima katika Israeli na kwa hiyo Yoshua lilikuwa jina linalijulikana sana katika Yuda pia

 

Kwa hiyo, Yesu halikuwa ni jina la Kristo. Bali hili ni jina lenye hisia ya Kiingereza la tafsiri ya Kiyunani. Josephus, na sasa Schurer, anayaandika majina mengine. Mfano ni kama Yesu, mwana wa Damnai; Yesu, mwana wa Gamaliel; Yesu, mwana wa Phiabi Kuhani Mkuu aliyemtiwa mafuta au kusimikwa na Herode; Yesu, mwana wa Sapphias, adui wa Tiberias kwenye uasi wa kwanza; Yesu, mwana wa See, Kuhani Mkuu aliyetiwa mafuta na kusimikwa na Archelaus; na Yesu, mpinzani wa Josephus (sawa na kisemavyo kitabu cha The History of the Jewish people in the age of Jesus Christ [Historia ya Wayahudi Wakati wa Yesu Kristo] (Vols. 1. 419, 431, 469, 489, 497; II, 180-181, 229, 232, 234).

 

Majina yaliyo kwenye Biblia za Kiingereza ni tafisiri ya Kiyunani na mara nyingi hayafanani na yalivyo kwenye Kiyunani, mbali na hata kuyafananisha na Kiebrania. Kwa mfano, jina James lilikuwa ni Yakob, Jude ni Yudah au Judah, Joses ni Yosef au Josef. Tazama pia majarida ya Bikira Mariamu na Familia ya Yesu Kristo (Na. 232) na Yoshua, Masihi, Mwana wa Mungu (Na. 134).

 

Inasemekana kuwa kuna waraka kutoka kwa Pilato aliomwandikia Mfalme Claudio unaoashiria kama alimtaja Yesu. Je, waraka huu bado upo? Na kama ni hivyo unasemaje kuhusu Yesu?

Jibu: Barua ya Pilato aliyomwandikia Claudio imejumuishwa au inapatikana kwenye Injili ya kiapokrifa ya Nicodemus iliyoko mwishoni mwa toleo la kwanza. Toleo la Kiyunani la barua hii linaonekana kuandikwa pia kwenye injili za kiapokrifa za Petro na Paulo. Utajionea matoleo kadhaa ya barua zilizoandikwa na kupelekewa wafalme Augustus, Claudius na hatimaye Tiberius kwenye kitabu cha the ANF vol viii, pp, 353, 454, 459 et seq.

 

Je, Kristo alisulibiwa kwenye mwaka ahirisho? Kama sivyo, nawezaje kuthibitisha hilo?

Jibu: Hapana, hakusulibiwa kwenye mwaka ahirisho na ni rahisi kuthibitisha. Kwanza kabisa, katika mwaka huu wa 30 BK siku ya 14 iliangukia siku ya Jumatano na ilikuwa ni namna hiyo isingejalisha ni utaratibu au mfumo gani ulitumika. Hata hivyo, sababu kubwa ni kwamba utaratibu wa kuahirisha haukuwa ukitumika wakati huo. Kimsingi, utaratibu wa Kuahirisha ulikuwa ni “barza maalumu” ulioingizwa baadae baada ya kipindi cha kuangamizwa kwa Hekalu mwaka 70 BK. Baraza la wazee lililojulikana kama Mishnah lililoundwa mwanzoni mwa karne ya tatu takriban zaidi ya mwaka 200 BK inaonyesha kuwa utaratibu huu wa uahirisho ulikuwa bado haujaanza hata kipindi hicho.

 

Utaratibu wa kuhesabu ndiyo unapelekea hali hii ya uahirisho na hata hivyo ilikuwa haujafanyika wala kuanza hadi ulipoletwa na kuingizwa na Marabi wawili wa Kibabeloni mwaka 344 na kisha ukabatilika na kuanzishwa rasmi chini ya Rabi Hilleli II mwaka 358. Hauikuwa umekamilika hadi kwenye karne ya kumi na moja. Kwa hiyo, Kristo alisulibiwa yapata zaidi ya miaka mia tatu kabla ya utaratibu huu wa uahirisho kuanza.

 

Kalenda ya sasa ya Kiyahudi haikuwa ikitumika kabisa kwenye shughuli za Hekaluni. Utajisomea na kujifunza zaidi kwenye majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156) na jarida la Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213) na pia Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho au Sikukuu? (Na. 195).

 

Ni kwanini basi kwamba kwenye maandiko ya Kiyunani neno msalaba halitumiki kabisa wakati yanapoelezea kuhusu pale aliposulibiwa Kristo? Neno la Kiyunani lililotumika ni “stauros,” ambalo halimaanishi msalaba, bali ni mti tu wa kawaida. Je, kwani alisulibiwa msalabani au kwenye mti?

Jibu: Neno hili msalaba halikutumika kabisa kwenye zama zote za Ukristo wa kwanza. Alama iliyokuwa karibu sana ilikuwa ni ya “kiutata.” Ilieleweka kwamba “stauros” ilikuwa ni mti. Mkakati wa kuufanya msalaba kuwa nembo ulifuatia baadae, na hatimaye wakajichongea sanamu juu yake baadae. Hakuna hata mojawapo ya mambo haya yaliyokuwa yanatumika na kuwekwa kwenye madhabahu za Kikristo za pande za Magharibi hadi millennia hii. Mwendelezo wa uhalalishaji wa nembo ya msalaba, habari zake zimechambuliwa kwa kina kwenye jarida la Msalabas: Chanzo Chake na Maana Yake (Na. 39). Makanisa mengi ya Mungu, hadi sasa, bado hayakubaliani kuweka alama yoyoyote ya msalaba kwenye ibada zao na hawauamini.

 

Je, unaweza kuelezea basi ni kwa jinsi gani huu msalaba ulionekana na ni kwa jinsi ipi Yesu alipigiliwa misumari juu yake?

Jibu: Neno lililotumiwa kuelezea “stauros” ambalo ni neno la Kiyunani ambalo linamaanisha “fimbo” na hasahasa ni “mti uliosimama kwenda juu” (sawa na inavyosema Thayers New Greek English Lexicon p. 586) na chanzo chake ni mti au mlingoti uliosimama wima, hususan uliosimikwa hivyo kwa kazi maalumu. Haya ndiyo matumizi yake kwa maandiko ya Kiyunani.

 

Wayunani na Warumi walikuwa na neno lao kuhusu kifo iki kwa kuongeza maana yake ya kusulibiwa mtini kutokana na lugha ya Kifoeniki (ibid). Neno “msalaba” linatokana na neno la Kirumi “crux.” Mwendelezo wa mkakati wa kuufanya msalaba kuwa nembo unaelezwa kwa kina kwenye jarida la Msalaba: Chanzo Chake na Maana Yake (Na. 39).

 

Kristo alisulibiwa kwenye hii “stauros” kwa kupigiliwa misumari mikononi na miguuni. Lengo lao lilikuwa ni kuufanya mwili uanguke chini kwa ajili ya uzito wake, ukishindwa kumudu kujishikilia wenyewe. Dhana ya msalaba ililetwa baadae ikifanywa kuwa ziada ya kuendeleza habari ya kifo. Kasi ya kifo cha Kristo na siku au tarehe vinaashiria kuwa hii “stauros” ilikuwa ndiyo mti wa kijadi wa Wafoenike na Wayunani, zaidi kuliko msalaba ulioingizwa baadae na kuendelezwa dhana yake. Historia yake, ya matumizi yake katika kipindi cha kabla ya zama za \Ukristo na siri au fmbo lake imeelezwa kwa kina kwenye jarida la Na. 39.

 

Biblia yangu ya NKJV inaema hivi: “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu...”(Mark 16:9). “Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu...” (Mat 28:1). Je, Yesu aliamka au kufufuka asubuhi ya siku ya Jumamosi au Jumapili asubuhi? Na kwa kuwa siku ya Mungu huanzia baada ya kuchwa jua, basi ikiwa kama alifufuka wakato wowote baada ya machweo ya siku ya Jumamosi basi ingekuwa imechukuliwa kuwa ni siku ya kwanza ya juma. Je, haikuwa hivyo?

Jibu: alitumia kushinda siku tatu mchana na usiku kaburini alifanya hivyo kuanzia siku inayoitwa leo Jumatano jioni wakati wa jua kuzama na alifufuka siku ya Jumamosi jioni majira ya jua kuzama.

 

Ilimpasa kuyatimiliza matukio matatu kwenye Pasaka yake. Ilimpasa afe au auawe kama Mwanakondoo kwa wakati wake muafaka wa kuuawa kondoo kwa kuchinjwa. Vinginevyo, basi asingekuweza kuwa kindoo wa Pasaka; bali angekuwa ni mtu mwingine tu aliyeuawa. Ilimpasa pia kuitimiliza Ishara ya nabii Yona, kwa kuwa hii ilikuwa ndiyo ishara pekee iliyopewa huduma yake. Hiyo ilikuwa muhimu kwa kuwahukumu Yuda kwa miaka mingine arobaini iliyofuatia, mwaka 70 BK.

 

Kitu cha pili alichopasa kukifanya kilikuwa ni kuhitimisha Sadaka ya Mganda wa Kutikisa. Alikuwa ni limbuko na hivyo alipaswa kukubaliwa na Mungu akiwa anafanya huduma yake kwa ajili hiyo. Kwa hiyo ilimlazimu kupaa juu kwa Mungu siku ya Kwanza ya Juma Asubuhi saa 3:00 asubuhi ili kuanzisha mchakato wa Kuhesabu Kipindi cha Mpito kuelekea Pentekoste ili mavuno yetu yaanze. Alikuwa ni Mavuno ya Shayiri na ilimpasa kukubaliwa ili kumuwezesha Roho Mtakatifu atolewe atakaporudi.

 

Fundisho la Easter la miungu migeni nay a uwongo lilianzishwa kwa makusudi mazima ya kutatiza au kuposha muujiza huu na uweza wa Mungu. Mungu wa Utatu aliingizwa au kubuniwa pia kwa kusudi hilihili. Na ndiyo maana imani ya Kiutatu haina maadhimisho ya Mganda wa Kutikiswa na unapinga upaaji wa siku ya Jumapili, wakauweka siku arobaini baadae kwa kuumujuisha kimakosa na ule upaaji wa mwisho. Ndiyo maana kwamba Shetani amefanikiwa kuwaleta ua kuwaweka Makristo wengi bandia—ili wafundishe watu kudharau utimilifu wa Sheria au Torati ya Mungu kwenye imani ya kweli ya maadhimisho ya sikukuu.

 

Na hii ndiyo sababu pia inayopelekea imani zilizo kwenye muungano wa Baali-Easter kuw na migogoro mikubwa na kupingana sana kwa kuitupilia mbali imani ya kweli na kalenda ya Mungu inayoendana kwa mujibu wa Amri za Mungu. Na hii ndiyo sababu pia ni muhimu sana.

 

Je, Kristo alikuwanao (wa kiroho au wa kimwili) alipofufuka?

Jibu: Maandiko ya Agano Jipya (hususan Yohana 20) yanaonyesha kuwa Kristo alifufuka kimwili, jioni iliyopita na alipaa juu kwa Baba wakati wa Mganda wa Kutikiswa, ambayo ilikuwa Jumapili asubuhi. Akarudi siku hiyohiyo na akamwambia Thomaso amsike. Anaonekana kuwa alikuwa amekwisha mudu kujibadilisha kutoka mwili wake wa kibinadamu na kuwa na wa kiroho. Tazama majarida ya Mganda wa Kutikiswa (Na. 106b) na Majira ya Kusulibiwa na ya Kufufuka (Na. 159). Nafasi yake kwenye Korani inaelezwa pia kwenye jarida la Kristo na Korani (Na. 163) kwenye tovuti ya www.ccg.org na www.logon.org ambako inapatikana pia kwa Kiarabu, Kirusi na lugha nyingi nyinginezo.

 

Kupewa huku kwa mwili wa Yesu hakuonekani kabisa, basi je, mwili wake wa kibinadamu utapaa mbinguni pamoja na roho yake? Nadhani kwamba ni roho yake tu ndiyo ilifufuka, na mwili ni kama gamba tu la kimwili lililovulika na kuachwa nyuma yake. Kama ni hivyo, kuna fursa yoyote ya kudhani kwamba mifupa au skeleton ya Yesu yawezekana upo mahali fulani popote, huenda ilifichwa na mmoja wa wanafunzi wake? Najua kuwa aliweza kuonekana siku kadhaa baadae, ila hii haikuwa ni kivuli tu, au alikuwa na mwili wa kibinadamu pia?

Jibu: Yesu alifufuka toka kwa wafu na mwili wake wa kibinadamu ulifufuka na kubadilika kama Mganda wa Kutikiswa wa juma majira ya saa tatu asubuhi, ambayo ni saa 9 asubuhi, na ambao ndio ulikuwa muda au kipindi ambacho ulikuwa unatolewa kila mara.

 

Kubadilika kwa mwili kunaaminika kulifanyika baada ya kufufuka toka kifoni. Nabii Ezekieli anaonyesha kuwa ilikuwa ni kimwili. Fundisho la roho kutokufa si la kibiblia kabisa. Jinsi ya kumgundua Mkristo wa uwongo kwenye karne ya 2 ilikuwa ni kwamba, kama atasema kwamba anapokufa atakwenda mbinguni, basi alihesabiwa kuwa sio Mkristo. Wanostiki aliingiza mafundisho haya ya watu kwenda mbinguni na motoni kwenye Ukristo tangu wakati huo.

 

Jambo hili limechambuliwa kwa kina kwenye majaria ya Roho (Na. 92) na Ufufuo wa Wafu (Na. 143). Watu wengi leo wanaodai kuwa Wakristo na wakiamini au kuhubiri mafundisho haya ya kwenda mbinguni na motoni hawajui wanachokiongea. Nyingi ya hizo zinatokana tu na mpagao wa kimsisimko wa kipagani, na mapokeo yao wapagani.

 

Dhehebu nililokuwa mshirika wao zamani lilikuwa likifundisha kuwa Israeli wa kale waliolewa na Kristo. Je, kuna Andiko Takatifu lolote linalounga mkono dhana hii?

Jibu: Yeye Aliye Juu Sana na Mwenyezi aliwakabidhi Israeli kwa Yahova awe urithi wake (Kumbukumbu la Torati 32:8) wakati alipoyagawa na kuyaanzisha mataifa sawasawa na wana wa Mungu. Jambo hili la andiko la Agano la Kale limepotoshwana baraza la Sopherim, baada ya kuanguka kwa Hekalu ili lisomeke “sawasawa na idadi ya wana wa Israeli.” Kwa hiyo, Yahova wa Majeshi Aliye Juu Sana aliwakabidhi Israeli kwa Yahova kama urithi wake. Tunamuona Yahova akihusishwa, akiwa kama msaidizi wa Yahova aliyefanyika kuwa elohimu wa Israeli.

 

Zaburi 45:6-7 inasema: “Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.” Kwa hiyo, Yahova au elohim wa Israeli ana Mungu. Tunajua kwamba huyu elohim wa Israeli ni Kristo, kwa mujibu wa Waebrania 1:8-9. Tunajua pia kutokana na andiko la Waebrania, kwamba malaika wengine ni washirika wazuri wa Kristo. Wao ni elohim pia kutokana na isemavyo Zaburi 8, ambayo kwenye tafsiriri ya Kiingereza, wanaonekana pia kuitwa “Malaika” ikifiatiwa na tafsiri ya  Septuagint. Kwenye Kiebrania pia ni “aggelos” na kwenye Kiyunani na inafuatia kwenye Kiingereza ikiandikwa “angels” kuliko kuitwa “miungu” (sawa na jarida la Zaburi 8 (Na. 14)).

 

Kiumbe huyu ndiye kwenye Agano la Kale aliyempa Torati Musa, na kumtokea kichakani, na ndiye aliyeshindana mieleka na mababa zetu wa imani, alikuwa ni Kristo kama elohim wa Israeli. Mungu Mmoja wa Kweli, Eloah aliyewatoa Israeli kwake kama wachumba wake na taifa zima lilikusudiwa kuwa ni wafalme na makuhani wa Mungu kupitia Kanisa. Wote kwenye Agano lote la Kale uhusiano na Yahova ulikuwa ni wa mume na mke. Ibada za sanamu zilichukuliwa kuwa ni uzinzi. Ndiyo maana Israeli walikwenda utumwani kama waliotalikiwa, na walipojirudi kutoka kwenye ibada zao za sanamu walifanywa upya. Taifa la Israeli liliendelea na likaenda utumwani. Yuda walitengwa na pia wakaandama ukahaba kwa kuzini na miungu wa uwongo (Yeremia 3:8-18).

 

Kwenye andiko la Yeremia Mungu anasema amewaoa Israeli na anasema kwamba atatuchukulia au kutupa, mji mmoja na familia mbili, na kutupeleka Sayuni. Atatawala kutoka Yerusalemu na Sanduku la Agano halitaletwa mioyoni tena. Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itatembea mkono kwa mkono na Nyuma ya Israeli kutoka upande wa Kaskazini hadi kwenye nchi waliyopewa baba zetu kuirithi. Kwenye Yeremia 3:14 Bwana anasema kuwa anafanya hivyo kwa kuwa amefanyika kuwa mume wetu.

 

Andiko lenyewe kwa kweli linasema hivi: “Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; maana mimi ni mume wenu;...”. Huyu ndiye Yahova, aliyetolewa kwa Israeli kama urithi wake, na tunayemjua kuwa kama Malaika Mkuu wa Agano la Kale aliyempa Torati Musa, na alikuwa ni mwamba wa roho jangwani ambao kwao, Israeli walikula na kunywa chakula cha kiroho (cha 1Wakorintho 10:4). Tunamjua mtu huyu kwenye Agano Jipya kuwa ni Yesu Kristo. Huu ulikuwa ni mtazamo wa Kanisa zima lote la Kikristo, likiwemo kanisa la Roma, kwa kipindi cha karne moja hadi mbili za kwanza (sawa na alivyosema Justin Martyr kwenye kitabu chake cha First Apology LXIII). Tazama majarida mengine ya: Teolojia ya Mwanzo ya Uungu (Na. 127); Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Duniani (Na. 243); Wateule Kama Elohim (Na. 1); Zaburi 8 (Na. 14); na Torati na Amri ya Tano (Na. 258).

 

Itakuwaje basi kuwe na sababu ya utoaji dhabihu kipindi cha Milenia kama kifo cha Kristo kilihitimisha dhabihu & kukomesha utoaji wa dhabihu siku hizi? (Zekaria 14:16-19; Ezekieli 46:3).

Jibu: Umwagaji wa damu umekoma na kuthibitiwa. Uanzishwaji wa utaratibu wa kuchinja wanyama wakati wa sikukuu huko Yerusalemu hauna mashaka yoyote kabisa. Sababu ya kufanya hivyo ni kuthibiti vifaa zana vya machinjioni na utakatifu wa mchakato wenyewe kwenye mpango wa Mungu. Imani ya kula mbogamboga peke yake na kutokula nyama ijulikanayo kama Uvujiteriani ni fundisho la mapepo na ndiyo maana vikundi vya watu hawa wasiokula nyama wanapenda kufundisha kuwa kipindi hiki cha millennia kitakuwa mbinguni kama wanavyofanya wafuasi wa Waadventista Wasabato wakiwa chini ya mafundisho ya nabii mke wa uwongo Ellen G White. Tazama na kulisoma jarida la Milenia na Unyakuo (Na. 95). Kristo alikuwa ni dhabihu kamilifu bali sheria na kanuni au utaratibu ya kusimamia sikukuu na ulaji wa nyama unazidi kawaida kwa kiasi fulani kwenye imani ya mrengo wa milenia ya kimwili.

 

Kwa nini wakati mwingine Kristo aliwagawa “makundi madogomadogo” wanafunzi watatu watatu? Nagundua kuwa kuna wakati ambapo wanafunzi walitumwa wakiwa na vikundi vya wawili wawili nk, lakini watatu hawa wanaonekana kuunganishwa pamoja kwa wakati wake muafaka.

Jibu: Utaratibu chini ya ufalme ulikuwa ni wa mfalme, akifuatiwa na watatu wengine na kisha thelathini. Mashujaa hawa watatu waliokuwa chini ya Daudi walikuwa chini ya Abishai, ndugu yake Yoabu na mwana wa Seruya (2Samweli 23:13, 18). Utaratibu au muundo huu unaonekana pia kwenye 2Nyakati 27:1. Jeshi la Israeli liligawanyika kwa vikosi 12 vya watu 24,000. Hawa walikuwa chini ya usimamizi wa watu kumi na mbili miongoni mwa thelathini. Hawa thelathini walikuwa ni baraza la ndani la wazee sabini.

 

Waliliwakilisha baraza la Elohim kwenye maskani ya mbinguni. Kwa hiyo, hawa watatu walikuwa ni mashujaa wa watu kumi na mbili na walikuwa ni makamanda wa jeshi zima la Israeli. Petro, Yohana na Yakobo wanawakilisha uwepo wa watu hawa watatu kwenye Jeshi la Israeli chini ya Masihi. Jeshi la askari 600 la Daudi (1Samweli 23:13) liligawanywa kwa vikosi vitatu vya askari 200 kila kimoja na lenye vikosi vidogovidogo kumi kumi. Kila kimoja kiliongozwa na mmoja wa wale thelathini. Kamanda wa wale thelathini hakuw mmoja wa wale watatu. Bullinger ameandika habari za watu hawa kwenye ura na aya za 27:1 na sura ya 11 na pia kwenye 2Samweli 23.

 

Kristo alikuwa na watatu pamoja na wale kumi na mbili, lakini kwa jambo hili, hawa watatu walikuwa ni sehemu ya kumi na mbili kwa kuwa hawa watatu kwenye kipindi cha milenia waliwakilishwa na mitume hawa waliokuja kipindi na zama nyingine. Na bado kwamba sehemu yao ilijulikana kama si ya muhimu kwenye mchakato na utendaji kazi wa huduma ya Kristo akiwa kama mfalme wa Israeli. Hawa watatu kwa kweli ni Ibrahimu, Musa na Eliya. Wote hawakuwepo hai kipindi hiki.

 

Kuna maandiko meingine mengi kwenye Biblia yanayosema kwamba Yesu Kristo ni Mwokozi wetu. Pia kuna maandiko mengi kuwa Mungu ni Mwokozi wetu. Tunaweza kudhani na kufikiri kutokana na andiko hili kwamba Mungu na Kristo ni mtu mmoja? Au huenda kwamba Mungu ana sehemu mbili au tatu za Utrinitariani au Ubinitariani tunaotakiwa kuuamini? Tafadhali, nisaidie kupata ufumbuzi wa fumbo hili. Je, Mwokozi wetu ni yupi hasa?

Jibu: Swali hili ni chanzo cha mkanganyiko uliowakumba waru wengi. Ndiyo, Biblia inasema kuwa Kristo ni Mwokozi wetu, na pia inasema kuwa Mungu ni Mwokozi wetu pia, na inatupa maandiko pia ambayo kwayo yanawataja watu wote wawili kwa uzito mmoja uliosawa. Ni kwa kutokana na maandiko mengi kwenye Biblia ambako maneno haya yanatumika na tunafikia kuelewa maana na utendaji kazi wa maneno haya.

 

Swali hili limejibiwa kwa kina kwenye jarida lenye kichwa cha maneno Mungu Mwokozi Wetu (Na. 198). Ni kama yalivyo majina yote ya vyeo vya Kristo, ni cheo alichopewa kama cheo alichoruzukiwa na Mungu. Kwa kutathmini kwa kina zaidi kuhusu kazi au huduma ya Masihi, kama tutaililia maanani kanuni hiyo basi tutaona mgongano wote ulioko kwenye mwonekano wake halisi. Majarida yanayosaidia kujua zaidi jambo hili ni haya hapa chini Kazi ya Masihi (Na. 226) na Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229).

 

Ni mtindo gani wa ufundishaji alioutumia Yesu ili kutimiliza unabii wa Zaburi? Wengine wanasema kuwa ni kwa Mifano. Nadhani aliutimiliza unabii kwa jinsi alivyoishi maisha yake na hadi kifo chake mtini na alivyofufuka. Je, nakosea?

Jibu: Waweza kufundisha kwa mifano pamoja na kwa kuelekeza. Biblia inasema kuwa alifundisha kwa mifano, na iltabiriwa kuwa atafundisha kwa mifano. Utaratibu alioufanya wa kufundisha kwa maelekezo ulikuwa sahihi pia. Kwa kweli, alifanya yote mawili, lakini mpango na jibu rahisi ni kwamba alifundisha kwa mifano, na hivyo ndivyo alivyofanya. Hakuna shaka kuhusu mfano wa maisha yake, kifo chake na kufufuka kwake vilikuwa ni mwonekano wa nguvu sana wa Mpango wa Mungu, jambo ambalo alikuja hapa kufundisha.

 

Kristo alisema kwa mifano ili wasiweze kuelewa kabla ya wakati wao na wasije wakageuka na kuokolewa: Zaburi 49:4; 78:2; Ezekieli 17:2; 20:49; 24:3; Mathayo 13:3-35; 21:45; 22:1 na kadhalika. Na ndiyo maana ni wachache sana wanaoielewa Biblia leo – kwakuwa walikuwa ni nyumba ya uasi.

 

Nimelitafuta jibu hili kwene Biblia na sijaliona. Utafiti wangu unaonekana kuwalenga kuonyesha kuwa watu wanaweza uwa walaji wa mbogamboga tu na wasiokula nyama kama watachagua kuwa hivyo. Hivi karibuni nilisikia kuwa  Kristo alikuwa mtu wa kundi hili la wasiokula nyama. Je, ni kweli?

Jibu: Yesu Kristo kwa kweli hakuna wa imani hii ya wasiokula nyma na wala mbogamboga. Yeye pamoja na mitume walimla Pasaka na walizishika sheria za ulaji wa vyakula na walisika maadhimisho ya sikukuu kama ilivyoamriwa na Mungu. Fundisho hili potofu la ulaji wa mbogamboga tu na kutokula nyama ni la uwongo, ambalo liliingia kwenye Ukristo kutoka kwenye Unostiki katika karne za mwanzoni na liliupotosha Ukristo tangu wakati huo kwa kiwango kukibwa na cha wastani.

 

Historia yote nzima ya fundisho hili imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Uvijitariani na Biblia (Na. 183). Likiwa ni fundisho la kizushi, kwa kawaida linaendelea mbali sambamba na fundisho linguine la kyjinyima anasa lihusulo kuwa na kiasi na unywaji wa juisi ya zabibu. Hii imeelezewa kwa kina pia kwenye jarida la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188). Fundisho la ulaji mbogamboga tupu au Uvijiteriani ni upotoshaji wa makusudi juu ya asili ya Mungu.

 

Ni imani yangu kabisa kuamini kuwa Mungu, Yesu na Roho Mtakatifu wako mbalimbali kila mmoja na mwenzake. Wakati Yesu alipokuwa pale mtini na akasema “Baba wasamehe kwa kuwa hawajui watendalo” hakuwa anamwambia Mungu? Iwapo kama unaambia watu kwamba wanasema kile kinachominiwa na dini potofu za uwongo au kalti. Wanaamini kuwa Mungu ni neno aliyekuwepo mwanzoni na kwamba ndiye huyu diye huyu Yesu na kwamba yeye ni (Mungu) aliyekuja duniani. Je, kuna majarida au maandiko matakatifu yanayothibitisha hilo?

Jibu: Kwenye karne mbili za kwanza za Kanisa, yeyote aliyesema kuwa Kristo alikuwa sawa na wa milele kama Mungu ambaye ni Baba, angetengwa na ushirka kwa kuchukuliwa kama mfundisha uzushi na angeondolewa mbali kutoka Kanisani. Tazama jarida la Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127). Imani ya Utrinitariani haikuwepo hadi mwaka 381 BK kwa maazimio ya mtaguso wa Constantinople.

 

Imani ya Kiinitarian ilianzishwa kwenye mtaguso wa Nicaea mwaka 325. Umodalism uliingizwa Kanisani kwenye karne ya tatu. Kwenye karne ya pili, kila mahali hata Wamontana, waliamini kuwa Kristo alikuwa ni Mwana wa Mungu na sio Mungu wa Pekee wa Kweli, na kwamba Roho Mtakatifu alikuwa ni nguvu au uweza tu wa Mungu. Kanisa huko Roma lilimwandikia mfalme wa Roma mnamo miaka ya 150-154 likisema kwamba Kristo alikuwa ndiye Yule Malaika wa Agano la Kale aliyempa Musa Torati (sawa na kitabu cha Justin Martyr: cha First Apology). Justin kwa niaba ya Kanisa la Roma alimwambia mfalme kuwa, kama wangeuja watu wanaodai kuwa wao ni Wakristo na wakasema kuwa kama watakufa watakwenda mbinguni, asiwaamini kabisa kwa kuwa hawakuwa Wakristo (kitabu chake cha Second Apology).

 

Walikuwa ni wafalme wa Kinostiki kabisa walioingia Kanisani na huk wakiwa na mafundisho yao ya uwongo. Lakini kinyeume na hali hiyo, siku hizi kama utaongea na Wabaptisti wa Kusini watakuambia: Hakika wanakwenda mbinguni na wakosefu wengine wote wanakwenda kuungua motoni milele.” Makanisa ya Kristo yatakupa dondoo za kina ya mahubiri ya jinsi unavyokwenda kuungua kwenye moto.” Kisha hao wote, Kanisa Katoliki la Roma kwa ujumla litakuambia kuwa ni uzushi mkubwa sana kutoamini Utatu, Fundisho kuhusu Roho na uwepo wa mbinguni na motoni na watachukuliwa na Maria kwenda mbinguni pia. Kama wangesema hivyo, basi maaskofu wa Roma wa kipindi cha mwishoni mwa karne ya kwanza vichwa vyao vingepasuka kwa mbio wangalizokuwanazo kukimbilia mlangoni ili kumkimbia mtu huyo.

 

Ukristo wa Makanisa Kongwe wa leo ni wa mchanganyiko wa imani za Kinostiki na Kipagani na ambao hauhusiani chochote na Ukristo wa kale wenyewe na wa ile Imani waliyopewa watakatifu mara moja tu. Ndiyo maana Kristo aliiliza swali kwamba “Nitakaporudi nitaikuta imani duniani?” kulia na kusaga meno kunawakumba watu waliohai leo wanaodhani kuwa wangekuwa huko ya Kristo leo, lakini wakijikuta wakikataliwa tu na wazee wake na manabii wake. Hawakuzishika sheria na Amri za Mungu wao wenyewe na waliwaua au kuwatesa wale walioamua kuzishika, wakati wowote walipofanya hivyo. Waalimu wa uwongo waliokufa, watabakia kuwa hivyo hadi kwenye Ufufuo wa Pili wa wafu. Wengi hawatashangaa kuhusu ni ufufuo gani watakaojikuta wenyewe wakiwemo. Wengine watashangaa sana. Kama unalijua hlo basi huenda Mungu anashughulika na wewe. Roho Mtakatifu atashughulika nawe kwa kukutia wenye kweli yote. Hebu mkabidhi njia zako Mungu, naye atakuongoza mawazo yako. Hakuna njia nyingine mbadala wake. Yakupasa kutenda sawasawa na ulivyopewa kuelewa, na utakapozidishiwa ufahamu zaidi. Yakupasa kumtafuta mmoja kati ya wazee wamtumikiao Mungu ili akuwekee mikono ili umpokee Roho Mtakatifu, kama umshabatizwa tayari ukiwa mtu mzima na sio kwenye dini yoyote ya imani kongwe hizi au kuwa mwanadini tu. Na ndipo yakupasa kuwa mtii kwenye ushikaji wa sheria na amri za Mungu. Usiwaruhusu vipofu hawa waendlee kukuongoza na ambao wanakuondolea fursa yako ya kuungia ufalme wa Mbinguni pia yasome majarida yafuatayo: Toba na Ubatizo (Na. 52); Msalaba: Chanzo Chake na Maana Yake (Na. 39); Torati ya Mungu (Na. L1); Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243).

 

Ni nini maana ya neno “stdi?”

Jibu: Neno “Stadi” (kwenye SHD 746) linamaanisha manzo au chanzo na kwa hiyo, ni mwanzo. Kwa mtazamo huu, linaweza pia kumaanisha “mwanzo” na wakati mwingine linatumika kwa kumaanisha “mtemi au kuu” akiwa wa kwanza katika kuwekwa kwenye utaratibu. Kwa hiyo linatumika kwa kumaanisha “utawala au sheria” kama ilivyo kwene Yohana 20:20 ambapo imetafsiriwa kama “nguvu.” Hii ni mara chache sana kama linavyotuiwa kwa kawaida kama “mwanzo,” nah ii ndiyo hasa kusudi lake. Matumzi ya “mtemi” au “mtawala” mara zote linamaanisha kuwa ni moja ya jozi kwa linavyojitokeza. Kwa hiyo, ni mamlaka au mfalme kwa jinsi ya kwamba mtu huyu ni wa kwanza kwenye jozi.

 

Inatumika mara 43 kwenye Agano Jipya ambako imetafsiriwa kama “mwanzo.” Matumizi ya neno “Stadi” ikimhusisha Kristo kuna maana maalumu ya kiteolojia, ambayo yamepingwa na waamini Utatu na imepelekea kwenye nyongeza ya kwenye tafsiri ya KJV kwenye Ufunuo 1, kusomeka Alfa na Omega. Jambo hili limechambuliwa kwa kina kwenye jarida la Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na: 229).

 

Tafsiri ya NIV inatajwa “stadi au mwanzo wa uumbaji” kwenye Ufunuo 3:14 kama “mtawala wa uumbaji wa Mungu” ili kupata dalili halisi ya matumizi ya neno hili kwene andiko hilo. Hata hivyo, tafsiri ya Thayers Greek English Lexicon pia inatoa ufafanuzi wa jambo hili na wakati wote kwenye muono huu inaonyesha kama ni mtu wa kwanza au kitu kwenye mwandamano wa matukio (pp. 76-77).

 

Ni nani basi huyu malaika aliye kwene Ufunuo anayesema: “Liambie Kanisa la Laodikia kuwa Mimi ni mwanzo wa uumbaji wa Mungu”?

Jibu: Mwanzo wa Uumbaji wa Mungu ni Yesu Kristo. Mazingira yameelezewa kwa kina kwenye majarida ya Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229) na Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasi Duniani (Na. 243).

 

Imekuwaje kwamba Yesu hakuandika kitabu chochote cha kwenye Biblia yeye mwenyewe? Nafikiri kwamba kitabu hicho kingekuwa bora zaidi kwenye Biblia yote.

Jibu: Kristo alinena kwa manabii, nao waliyanena aliyoyasema. Yeye ndiye aliyenena na Musa na kumpa Torati. Alinena na manabii wa Agano la Kale, na alinena kwa mitume wa kanisa la Agano Jipya, na aliwapa maelekezo na mifano, ambayo walinukuu na kuandika. Kwa hiyo, ndipo tuna Biblia ambayo ni kazi yenye uvuvio wa Mungu iliytolewa na Yesu Kristo aliyewapa manabii. Soma majarida ya Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243); na Biblia (Na. 164).

 

Roho Mtakatifu

Je, kwani Roho Mtakatifu ni mtu, au ni nguvu tu ya Mungu, au ni kitu kingine chochote?

Jibu: Roho Mtakatifu ni Nguvu au Uweza wa Mungu, iliyomwezesha Kristo naa Malaika wote kuwa wana wa Mungu. Suala la mwonekano wa kimwili wa Roho Mtakatifu lilijadiliwa sana kwenye Halmashauri Kuu ya Mtaguso wa Constantinople mwaka 381, ambapo walimtangaza rasmi kuwa ni nafsi ya tatu ya Uungu. Tatizo lililo kwenye lugha ya Kiingereza ni kuelewa kuwa yeye si nafsi ya kibinadamu, inatokana na utamaduni wa kutendanisha au kuipa jinsia kwenye kanuni ya lugha ya Kiingereza, jambo lisilo hivyo wala lazima kwenye lugha ya Kiyunani na hata kwenye lugha nyingine nyingi nyinginezo. Tazama majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117); Kuwa Sawa na Baba (Na. 81); Jinsia ya Roho Mtakatifu (Na. 155); na Mwendelezo wa Mtindo wa Uplatoni Mamboleo (Na. 17).

 

Je, unaamini kwamba kama ukiomba kwa Roho Mtakatifu, ndipo Mungu atakupa tu?

Jibu: Ndiyo, atakuzidishia mno na atakuleta kwenye ubatizo. Tatizo ni kwamba inakupasa kuwa mtii ili umpokee. Anatenda kazi pamoja nawe hadi ubatizwe na kisha anakaa ndani yako unapobatizwa, lakini kama ukiasi na kutotii ndipo huwezi kumpokea au kumpata. Mara tu unapofikia hatua ya kuelewa, utaweza kumtafuta na kumuomba mmoja wa wazee wa Kanisa na ubatizwe kwenye mwili wa Kristo ( na sio kwenye dini au dhehebu).

 

Kama hupendi kufanya hivyo, basi usiombe kufanyiwa hivyo, na hatabakia ndani yako. Tazama majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117) na Kuwa Sawa na Baba (Na. 81).

 

Je, kuna tofauti yoyote ya kibiblia kati ya nafsi na roho? Au ni kitu kimoja tu? Ni wapi basi kila kimoja kinakwenda baada ya kifo? Je, zinakwenda zote mbingun?

Jibu. Biblia inaongelea kuhusu nephesh (Kiebrania) na pneuma (Kiyunani). Wanyama wote wana hii nephesh. Nephesh ya mwanadamu imetajwa kuwa inamrudia Mungu aliyeitoa na mwili unangojea Ufufuo wa Wafu. Kwenye karne za kwanza kama mtuyeyote akisema kuwa yeye ni Mkristo na akasema kuwa wanapokufa au wakifa watakwenda mbinguni, ndipo ulijua kuwa walikuwa ni Wakristo wa jina tu lakini ni waumini wa imani potofu ya Kinostiki.

 

Justin Martyr alisema hivyo kwa Mfalme kwa niaba ya Kanisa huko Roma mwaka 150-4 BK. Tazama majarida ya Nafsi Hai (Na. 92) na Ufufuo wa Wafu (Na. 143).

 

Ni upi basi Ufalme wa Mungu? Unawezaje kuwa ndani yetu kama alivyosema Yesu?

Jibu. Ufalme wa Mungu u ndani yetu kama punje ya haradali. No Roho Mtakatifu tuliyepewa, na anayekua ili kwamba Mungu awe yote katika yote na ndani ya yote. Tunakuwa elohim kama Malaika wa Yahova vichwani mwetu.

 

Habari hii imeelezewa kwa kina kwenye majarida yafuatayo Ufalme wa Milele wa Mungu (Na. 144); na mengine ya Roho Mtakatifu (Na. 117); Kuwa Sawa na Baba (Na. 81); na Wateule Kama Elohim (Na. 1).

 

Kuna maeneo mengi kadhaa yanayotaja kuhusu maji na miamba, na maji yaliyotoka kwenye miamba, kwenye maandiko matakatifu. Ni nini maana ya haya yote?

Jibu: Miamba na maji ni ishara ya Roho Mtakatifu, anayetoka kwenye mwamba ambao ni Kristo, na ambaye ni mwamba usioweza kuchongwwa kwa mikono ya mwanadamu kutoka kwenye mlima wa Mwamba ambaye ni Mungu na ambaye juu yake Kristo atalijenga kanisa lake.

 

Kristo alikuwa ndiye mwamba uliokuwa katika Israeli jangwani na kutoka kwa huo, Israeli walikunywa maji. Kazi na huduma ya Kristo imeandikwa kwa kina kwenye majarida yafuatayo Kazi ya Masihi (Na. 226); Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243); Malaika wa YHVH (Na. 24); na Lengo la Uumbaji na Dhabihu ya Kristo (Na. 160).

 

Mathayo

Inaonekana kuwa watu huamini kwamba kulikuwa na nyota iliyokuwa ikiwaka na kung’aa upande wa mashariki wakari Kristo alipokuwa anazaliwa. Je, hivi ndivyo? Ni nini maana ya kuitaja nyota kwenye Mathayo 2 na maelezo mengine mengi ya kuzaliwa kwa Masihi?

Jibu: Andiko lililo kwenye Mathayo 2:2 inasema: maana tumeiona nyota yake upande wa “anatole” na huko ni “mashariki,” ila ni neno pia lililopewa Anatolia au Asia Ndogo. Inaweza kumaanisha kuwa ‘tuliiona nyota yake kutoka….’, yaani, wakati wakiwa upande wa mashariki au Anatolia. Kwa kweli, kuenda walikuwa upande wa kaskazini-mashariki mwa Yudea. Hesabu 24:15-19 inataja kuwa “Nyota” itatoka “kutoka kwa Yakobo,” ambaye ni Masihi.

 

Lengo lilikuwa ni kuifananisha hii kama nyota ya asubuhi Venus, ambayo ilikuwa ni alama au ishara ya utawala wa kisayari kama mleta nuru. Shetani ana cheo hiki ambacho kinamtaja pia Kristo kuwanacho atakaporudi. Ni kama anavyosema Bullinger, maswali yote yamefumbuliwa kama yatachukuliwa kama ni ya kimiujiza.

 

Inaonekana kuwa ni ngeni kwangu kwamba wakati Mfalme Herode alipojaribu kumuua Masihi angali bado mtoto mchanga (Mathayo 2:13), na Mfalme Herode Mwingine aliyekuwa na Yakobo, ndugu wa Yohana, alimuua (Matendo 12:1). Je, kuna kitu fulani ndani ya jina la Herode ambacho kina maana fulani ambavyo ndiyo sababu wanakuwa kinyume kabisa na Masihi na wafuasi wake?

Jibu: Chuki inarudi nyuma kwa namna kubwa. Herode alikuwa ni Idumean. Kwa maneno mengine alikuwa Muedomu. Kizazi chao chote cha utawala katika Yuda kilitokana na wongofu wa shuruti chini ya Hyrcanus na Wamakabayo. Walienea maeneo yote ya Midiani, lakini waliingia pia pande za kusini mwa Yudea kwa kuongoka kwao na wakaweka makazi maeneo ya Hebron. Eneo la mashariki mwa Yudea kwa hiyo lilikuwa ni la watu waliochanganika na Waedomu na Yuda, Lawi na Wasamaria.

 

Ndiyo maana Kristo alituhumiwa kuwa ni Msamaria na Mafarisayo – sio kwa sababu yeye alikuwa hivyo, bali kwa kuwa walikuwa na tahadhari kuhusu wakzi w eneo hilo wasiokuwa Israeli halisi waliokuwa chini ya utawala wa kizazi cha utawala cha Hasmonean tangu wakati wa Hyrcanus. Uchungu na kisasi unaelekea nyuma hadi kwenye zama za Esau na Yakobo. Haki ya uzaliwa wa kwanza ilikuja kwa kupitia Yusufu bali fimbo ya enzi ya ufalme ilikuja kupitia kwa Yuda, na Hasmoneans walijua sana kuwa hawakuwa kwenye mstari wa uzao wa kifalme wa Yuda. Familia ya Kristo ilikuwa ni ya uzao wa kifalme pia kama tunavyoona kwenye maandiko ya Agano Jipya na walikuwepon sana na wakiwa vizuri kama Desposyni walioliongoza au kulitawala kanisa. Kwa hiyo, Waherodi, na ambao baadae walijulikana kama askofu wa Kirumi, wote walijaribu kuwakomesha kwa sababu hizohizo. Tangu mwaka 318, askofu wa Roma alijaribu kuwaua na kukomesha imani yao kwa kipindi cha zaidi karne mbili, na hakkuweza kufanikiwa japo kidogo.

 

Kwenye Mathayo 2:17-18, Yeremia 31:15-20 kunanukuliwa kimakosa mno kama unabii ilitimia. Ni nini kilitokea kwa Herode ambaye hakuwa hata amekaribia kwenye unabii huo ulio kwenye Yeremia. Je, Mathayo alikuwa ni nabii wa uwongo?

Jibu: Hapana, watoto wa Raheli walikuwa na haki ya uzaliwa wa kwanza. Kwa jambo hili, iliwajumuisha makabila yote pamoja na Yuda. Mauaji ya Herode hayakufanyika kwa mtindo kama mauaji ya kuangamiza jamii nzima ya Wayahudi yajulikanayo kama Holocaust, bali wote walikuwa na ahadi moja hiyohiyo. Imeandikwa: “Manase atamlisha Efraimu na Efraimu watamlisha Manase na wote wawili watamlisha Yuda.” Sasa, Yuda ni mtoto wa Lea, na sio wa Raheli.

 

Umefafanua kuwa toba ya kweli inatikana na maombi na kufung; nimegundua kuwa Mungu maombi ya kupayukapayuka nay a kurudiarudia. Je, unaweza kuelezea njia bora ya maombi mazuri? (Mathayo 6:5-15)

Jibu: Mungu ameweka utaratibu wa kuomba kwenye Biblia. Kristo alitupatia madondoo ya jinsi ya kuomba kwenye Mathayo 6. Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba. Roho Mtakatifu atakupa jinsi ya kuomba na kutamka na kusihi.

 

Utaratibu wa kuomba na dondoo zake ni:

1) Baba yetu uliye mbinguni. Msifu yeye na mshukuru kwa kila jambo.

2) Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. Omba aje Masihi na kuanzishwa kwa utawala wa millennia na ufalme wa Mungu uje hapa duniani.

3) Utupe leo riziki yetu. Ombea mahitaji yetu ya kila siku na umshukuru kwa kutupatia.

4) Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. Hii inatukumbuksha kanuni ya sheria nay a msamaha wa dhambi na madeni ilivyo kwenye kanuni za Biblia.

5) Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. Utajaribiwa lakini hakuna jaribu ambalo hutapewa njia au mlango wa kutokea. Hata kwenye majaribu ya maishani mwetu tutatiwa nguvu kitabia.

 

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Hivyo, Maombi ya Bwana yanaweza kuonekana kuwa kama ni dondoo au kiashirio cha maombi ya watakatifu. Hayapo kwenye mpayukopayuko kwenye mpangilio wake. Tazama jarida la Tufundishe Kuomba (Na. 111).

 

Mathayo 12:50: “Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu.” Napenda kujua mawazo yako yalikuwa wapi kwa hili?

Jibu: Tukiweka msingi wetu kwenye andiko hili, tunachukua majukumu na wajibu wa kuwafundisha wengine kama washirika katika mwili wa Kristo kwa kiwango kingine cha juu sana. Kwa mfano, tunapokuwa kwenye majukumu au wajibu wa kuhakikisha kwamba masikini wanapaswa kusaidiwa wamudu kuhudhuria sikukuu, inafuatia kuwa inawapasa waishike sikukuu na wewe ili uwasaidie.

 

Yatupasa kufanya maamuzi haya kila siku. Kwa mfano, tunapokea maombi ya kuomba kusaidiwa kutoka kwa idadi kubwa ya Makanisa ya India, Afika na kwingineko. Wengine ni kutoka makanisa ya Kipentekoste na wengine ni kutoka kwa watu wetu wenyewe. Mara nyingi, wale wanaotokana na makusanyiko yetu wanapewa zaidi au wanawekewa kipaumbele kikubwa. Iwapo kama hatutafaletea madhara yoyote watu hawa, hatutaweza kuwasaidia kwa kuwapa vitu vyetu.

 

Akili za kuzaliwa nazo zinakuambia kuwa mtu anayeyafanya mapenzi ya baba yako wa mbinguni anastahili kupewa kipaumbele. Hili ni jaribio rahisi na lililosawa. Kama hawaneni wala kuenenda sawasawa na sheria na ushuhuda, hakuna nuru ndani yao (Isaya 8:20). Kama utaona tukio la mara moja linalohitaji msaada, ndipo unatoa msaada wako kama Msamaria Mwema. Inapojitokeza jambo linalostahili kusaidia sawasawa na hitaji ndipo itabidi uijali familia kwanza. Familia hiyo ni Kanisa. Tazama majarida ya Torati na Amri ya Tano (Na. 258) na Mlolongo wote wa majarida ya Torati likiwemo la Amri Iliyokuu ya Pili (Na. 257).

 

Nimekutana na maandio mengi yahusuyo ufungaji saumu kwenye Biblia, lakini sina uhakika yote haya yana maana gani. Je, unaweza kunifafanulia? (Mathayo 17:21)

Jibu. Andiko hili linaonyesha mapepo ya namna mbalimbali na aina hii ilihitaji maombi na kufunga saumu kwa wateule. Kwa hiyo, utaratibu wa kuabudu unaweza kuonekana kama mchezo au mzaha tu kama ukifanywa bila utii wa kuyatii tu mapepo.

 

Andiko hili linatokana na lugha ya Kisyria na maandiko mengine yameliruka. Bullinger ameandika vizuri sana kuhusu jambo hili na analinukuu andiko hili lililoachwa kuandikwa kwene ukurasa wa 21 kwenye tafsiri ya Companion Bible. Tazama pia kwenye jarida la Upatanisho (Na. 138).

 

Kwenye mfano wa Mathayo 20:13 tunasoma habari za mtu anayeitwa Rafiki aliyekata tamaa kutokana na wengine kulipwa ujira sawa na yeye ingawaje yeye alikuwa kazini kwa kuda mrefu zaidi ya wote. Kisha kwenye Mathayo 22 tunasoma habari za ‘mtu’ aliyeingia arusini bila kuvaa vazi la arusi. Kwenye aya ya 12 mtu huyu anaitwa pia ‘Rafiki’ na hatimaye kwenye aya ya 13 anafungwa na kutupwa nje gizani. Kisha kwenye Mathayo 26 tunasoma Kristo akimwita Yuda ‘Rafiki’. Swali langu ni kwamba je, Maandiko haya yanamaanisha kumtaja Shetani?

Jibu: Neno lililo kwenye Mathayo ni “hetairos” au ndugu, ambalo ni tofauti kabisa maana yake na neno “philos.” ‘Mtu’ aliyetajwa kwenye nje ya kundi, kwa namna hiyohiyo mtume Petro alikuwa ‘ndiye’ aliyetajwa kwenye Mathayo 19:27. Yeye hana vazi la arusi na haina maana yoyote kwa kuwa hawezi kujibu uachwaji huo. Kuna mlolongo wa makundi hapa. Yule aliyeficha hakuja. Hii inammaanisha Yuda. Anaweza pia kupunguza kwamba inaweza kuonekana kufunika watakatifu, na wote walikataa kuingia kwenye ufalme wa mileniamu.

 

Kitendo cha kulia na kusaga meno sio cha malaika walioasi. Wanajua walichokifanya na kilichobakia kwao sasa. Lakini bado wangali na fursa ya kuokoka, bali wakiwa kama viumbe wenye kuonekana, na kisha watabadilishwa kuwa viumbe wapya kwenye ufalme huo. Wao pia watapewa fursa ya kuzaliwa mara ya pili.

 

Wengi wa hawa watakaosaga meno watakuoja kutoka kwa wale wanaojiita wenyewe kuwa Wakristo lakini wakiwa hawazishiki amri zake Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12). Wanamwita “Bwana, Bwana” na huku wakiacha kutenda aliyoyatenda yeye au aliyoyaamuru, na wakiuhalalisha uasi wao kwa uwongo. Wapo wengi sana watu kama hawa na kwa kweli, wengi wao watakataliwa kwa kuwa mwenendo wao uliwaondoa kwenye atahiki ya kuuingia ufalme na hawajitawali kutokanao iwe kama wewe umebadilishwa na kuingizwa mjini Yerusalemu na Kristo au la, hakuna mjadala. Iwe kama umetii au la.

 

Wafu hawajui lolote, bali waliohai watasaga meno kwa kuwa wanakwenda kwenye dhiki kuu na hawatalindwa watoke katika saa ya kujaribiwa iliyoayari kuujaribu ulimwengu wote. Kwenye mfano wa tatu, Yuda alikuwa anawawakilisha Yuda iliyouza sehemu yao kwenye ufalme. Ndivyo pia alivyofana Shetani, na ndivyo adui anawakilishwa na atapasa kukabiliwa ufufuo wa pili wa wafu pia. Majarida haya ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Hukumu ya Mapepo (Na. 80); Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199); na Dondoo la Majira ya Nyakati (Na. 272) yanaonyesha mpango huu.

 

Je, Jina la Baba ni lipi na la Roho Mtakatifu kwenye Mathayo 28:19?

Jibu: Ni swali zuri. Biblia inajijibu yenyewe. Swali linatokana na Mithali 30:4: “Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua”. Limejibiwa kwenye aya inayofuatia: “Kila neno la Mungu limehakikishwa”. Jina la Mngu wa Pekee na wa Kweli ni “Eloah.” Ni Torati yake. Makuhani walimwabudu yeye na Hekalu lake. Alisababisha jina lake liwekwe huko Yerusalemu (sawa na Ezra 4:24-7:26).

 

Eloah ni jina linaloonyesha umoja na amejiongeza mwenyewe ili awe Elohim. Yeye ni “Ha Elohim” au “Mungu.” Huyu alikuwa “Elahh” kwa Wakaldayo na alijiongeza kuwa “Elahhin” kwa wana wa Mungu. Elahh ndiye hatimaye aliitwa “Allah’ ” kwa Kiarabu. Yeye ni Elyon au Mungu Aliye Juu sana. Yeye ndiye Yahovah wa Majeshi aliyewawatoa Israeli na kuwapa Yahovah kama mali na warithi wake maalumu (Kumbukumbu la Torati 32:8 RSV). Yeye ni Yahovih (SHD 3069) ambaye ni Mungu wa Yahovah (SHD 3068).

 

Mambo haya yameelezwa kwa kina kwenye majarida ya Majina ya Mungu (Na. 116); Malaika wa YHVH (Na. 24) na pia Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Hapa Duniani (Na. 243). Kuna matatizo makubwa sana kwenye teolojia ya Majina Matakatifu. Tazama jarida la Abracadabra: Maana ya Majina (Na. 240).

 

Marko

Unaweza kuniambia jinsi Yohana batizaji alivyokuwa anavaa vazi lililotengenezwa kwa singa ya ngamia na huku ngamia akiwa ni mnyama najisi na ambaye hatupaswi kugusa mizoga ya wanama najisi? Nadhani kuwa alikuwa anajivika mwili wake wote na sio nywele zisizokatwa peke yake. (Marko 1:6)

Jibu: Vazi lake halikuwa la ngozi bali ni la manyoya yaliyosokotwa ya ngamia. Hakuna katazo kufana hivyo. Katazo la kutogusa mizoga kwa kawaida linahusu vitu vilivyojifia vyenyewe kibudu. Kuna maandiko ya ziada kwene Campanion Bible kwenye Marko 1:6 kuhusu manoya ya ngamia.

 

Je, waweza kufafanua tafadhali maana iliyokusudiwa kwene Marko 5:21-43? Vitu ninavyovigundua ni mwanamke ugonjwa wa kutokwa damu kwa miaka 12 mwenye imani ya kugusa tu pindo la Kristo na akapona, na pia binti mwenye umri wa miaka 12 aliyekuwa hali ya kufa pamoja na baba, ofisa au mtumishi wa sinagogi, aliyekuwa na imani ya kwamba Kristo angewea kumpona. Ingawa aliambiwa kuwa mtoto wake alikuwa amekwisha fariki, Kristo akatangulia kwenye chumba cha mtoto na kumponya binti huyo na kumwambia apokee chakula. Ni vifungu vinavyovutia sana lakini maana yake ni nini?

Jibu: Maeleo ya maandiko yenewe ni haya.

Marko 5:21-43 Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng'ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari [Yairo akaja]. 22 Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake, 23 akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi. 24 Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa. 25 Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, 26 na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya 27 aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; 28 maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona. 29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule. 30 Mara Yesu, hali akifahamu nafsini mwake kwamba nguvu zimemtoka, akageuka kati ya mkutano, akasema, Ni nani aliyenigusa mavazi yangu? 31 Wanafunzi wake wakamwambia, Je! Wawaona makutano wanavyokusonga-songa, nawe wasema, Ni nani aliyenigusa? 32 Akatazama pande zote ili amwone yule aliyelitenda neno hilo. 33 Na yule mwanamke akaingiwa na hofu na kutetemeka, akijua lililompata, akaja akamwangukia, akamweleza kweli yote. 34 Akamwambia, Binti, imani yako imekuponya, enenda zako kwa amani, uwe mzima, usiwe na msiba wako tena. 35 Hata alipokuwa katika kunena, wakaja watu kutoka kwa yule mkuu wa sinagogi, wakisema, Binti yako amekwisha kufa; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu? 36 Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu. 37 Wala hakumruhusu mtu afuatane naye, ila Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye Yakobo. 38 Wakafika nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akaona ghasia, na watu wakilia, wakifanya maombolezo makuu. 39 Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu. 40 Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana. 41 Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka. 42 Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu. 43 Akawaonya sana, mtu asijue habari ile; akaamuru apewe chakula.

 

Kwenye Marko 7:15 Yesu alisema yafuatayo: “Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu.” Watu wengine huyatumia Maandiko haya kuonyesha kuwa hakuna chakula kilicho najisi na kwamba vitu vyote vinawea kuliwa. Kwani Yesu anasemaje hasa hapa?

Jibu: Mafarisayo walikuwa wanahusika na shuguli a kusimamia sheria na tarfatibu na taratibu a kutawadha aidi ya ilivyoagiwa kwenye Maandiko Matakatifu, na walikuwa wanawalaumu wanafuni. Lengo kamili la andiko hili lawea kuonekana kwenye jarida la Maandiko ya Mtendo ya Sheria - au MMT (Na. 104). Andiko hili lililopotea lilikutikana kwenye Gombo zilizochimbuliwa kwenye Bahari ya Chumvi, mashuhuri kama Dead Sea Scrolls kwenye karne hii. Mtume Paulo pia aliandika kupinga hali hii kwenye nyaraka zake kwa Wagalatia na Wakolosai. Luther hakuelewa kabisa alichokuwa anakisema na kumaanisha Mtume Paulo kwa sababu ya mtazamo wake wa kupinga Usemitiki.

 

Kristo alikuwa anasema kuwa Mafarisayo wanapaswa kuyaangalie au kuyatakari sana yale waliyokuwa wakiyasema, ambayo yalikuwa yanapotosha mahudhui ya sheria au torati zaidi kuliko vile walivyokuwa wakiogopa ambayo yaliingia vinywani wakati walipokuwa wanakula. Kristo na Mitume wakewote walishika Sheria ya Vyakula na Kanisa limekuwa likizishika kwa kipindi cha takriban miaka  2000. Tazama kwenye jarida la Sheria ya Vyakula (Na. 15).

 

Swali langu linatokana na Mark 10:18, linalosema: “Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.” Nilitaka kujua, kama Yesu alikuwa Bwana, basi ni kwa nini hakutaka kuitwa mwema, na ni yupi basi huyu Mungu mwingine anayemuita Mwema?

Jibu: Yohana 17:3 inajibu swali hili, kama inavyofanya Yohana 1:18 kwenye tafsiri ya Marshall’s Interlinear RSV na 1Timotheo 6:16. Yohana inasema: “ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.” Na tena “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”

 

Kwa hiyo, huyu Mungu wa pekee wa Kweli ndiye alimtuma Yesu Kristo. Ili kuujua ukweli huu na ili kuwajua wao ndiyo kuupata uzima wa milele. Yohana sura ya 1, inaelezea jinsi alivyotumwa Kristo, na huyu Mungu wa Pekee wa Kweli na kusudi lake. Yohana 1:18 inasema: “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua. Neno “monogenes theos” au “yeye aliyezaliwa na Mungu lilibadilishwa ili lisomeke “monogenes uios” au “mwana aliyezaliwa wa pekee” kwenye Receptus.

 

Pia Paul anafafanua kuwa hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu, au atakayeweza kumuona Mungu. Anaketi kwene makao yasiyofikika na yeye peke yake ndiye hawezi kufa (1Timotheo 6:16). Tazama kwene majarida ya Kwa Hali ya Kutokufa (Na. 165) na Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kwake Duniani (Na. 243). Kristo pia alifafanua kuwa hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu. Inamaana kwamba hakuna hata aliyewahi “hata kuisikia sauti yake wakati wowote wala kuliona umbo lake” (Yohana 5:37).

 

Kwa hiyo jinsi Kristo alivyo imeelezwa kwa kina kwenye Zaburi 45:6-7 na ambaye anajulikana kama Kristo kwenye Waebrania 1:8-9. Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,(ni kiti cha enzi cha) Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.” Kwa hiyo, mwana ni elohim. Anatajwa kwenye Zekariah 12:8 kama “Malaika wa Bwana” ambaye alikuwa ni kichwa cha numba ya Daudi, ambao ni wateule na ambao vilevile watakuwa elohim. Imeandikwa: “Mimi nimesema, Ndinyi miungu. Wana wa Alie Juu, ninyo wote pia, na maandiko hayawezi kutanguka” (sawa na Yohana 10:34-35).

 

Luka

Ni watu gani hawa wanaotajwa kwenye Biblia kuwa ni ndugu zake? Je, ni wale tu walio na imani sahihi na wanaozishika amri za Mungu, au ni wengine wote waliobatizwa kwa jina la Yesu lakini wakawa wanaabudu kwenye mapokeo ya wanadamu na sio kwa Mungu? Tunawezaje kuwafanyia vema wengine ambao hawajiiti wao wenyewe ndugu, bali ni wa dunia hii? (Luka 10:25-37)

Jibu: Swali aliloulizwa Kristo na Mwanasheria lilikuwa, “Jirani yangu ni nani” sawa na, “Ndugu yangu ni nani?” Ndipo Kristo akawapa mfano wa Msamaria Mwema ili kuonyesha kwamba dhana hii inawahusu watu wote. Torati au Sheria za Mungu zi mioyoni mwetu na kwa hiyo hakuna upendeleo unaowezekana. Tazama jarida la Kupendelea Watu (Na. 221) na Upendo na Utaratibu wa Torati (Na. 200). Tunatumwa na kupelekwa katikati ya mbwa mwitu. Wapende watu wote. Hata hivyo, wakati mwingine ni vizuri kumpenda mtu wa mbali.

 

Watu wengi duniani wanaamini kuhusu unyakuo wa kanisa. Mimi sipingi dhana hii, kwa kuwa name nimeipenda dhana hii, lakini siioni kwenye Biblia. Na ninapojitahidi kwa bidii kubwa kutafuta uthibitisho, ndipo kwenye Luka 12:36 najaribu kuona kama panafanana na fundisho hili lisemapo: “nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, ATAKAPORUDI KUTOKA ARUSINI, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.” Hii inaonekana kana kwamba alikuwa arusini, kashaa akarudi “kubisha hodi” kwa wale ambao hawakwenda arusini, kama ilivyo kwenye mfano wa wanawali 10. Je, ni wakati gani itakavyofanyika arusi hii na wa karamu ya arusi?

Jibu: Ndiyo, Luka 12:36 ni andiko linaloeleweka sana. 1Wathesalonike 4:17 ni andiko mashuhuri wanalolitumia waamini unyakuo. Andiko hili hata hivyo linaelezea kuhusu kuchukuliwa kwa wateule hadi mawinguni ili kumlaki Bwana atakaporudi hapa chini duniani na watakutanika nay eye huko Yerusalemu kama tuonavyo kwenye maandiko mengine mengi yanayohusiana na tukio hili. Jambo hili limefafanuliwa kwa kina kwene jarida la Tarumbeta (Na. 136). Dhana yote nzima kuhusu kunyakuliwa imetathiminiwa kwa kina kwenye jarida la Milenia na Unyakuo (Na. 95). Neno hili jinsi lilivyoandikwa kwenye injili ya Luka 12:36 ni “kurudi.”

 

Neno lililotumika ni “analuo.” Linajitokeza hapa peke yake na kwenye Wafilipi 1:23 kwenye Agano Jipya. Lilitumika kwenye tafsiri ya Septuagint (LXX) peke yake kwenye vitabu vya Apokrifa, na kilamara likimaanisha “kurudi tena.” Bullinger anasema kuwa lina mrengo wa “ana-kampti” (Waebrania 11:15). Mahali inapotajwa pengine ni kwenye vitabu vya Tobiti 2:9; Yudithi 13:1; 1Esdras 3:3; Hekima 2:1; 5:12; 16:14; Ecclesiasticus 3:15; 2Wamakabayo 8:25; 9:1; 12:7; 15:28. Nauni ya “analusis” kama “mwili kuyarudia mavubi”, kama kwenye Mwanzo 3:19, inaonekana mara moja tu kwenye 2Timotheo 4:6.

 

Utaratibu wa karamu ya arusi waonekana kuwa ulitabiriwa na walengwa wa kwanza ni waliokwisha kufa au kulala mauti katika Kristo ndio watakuwa wa kwanza kwenye utaratibu huu, na hatimaye waliohai watahusishwa kwenye awamu ya pili kwenda kumlaki hewani ili kuwa pamoja na Bwana milele. Biblia inasema kuwa wale watakaokutwa wakiwa hai hawatawatangulia (kuwazuia) wale waliokwisha kulala mauti. Bali watafufuliwa ili kuhudhuria kikamilifu karamu ya arusi kwanza. Hii ndiyo sababu na umuhimu wa kurudi kwake Masihi kwa wale wanaomngojea. kisha ndipo tutakapokuwa kwenye mchakato wa kuifanya upya dunia na kuitawala mwa kufuata mujibu wa Sheria za Mungu kwa kipindi cha miaka elfu cha Milenia. Tazama jarida la Uchambuzi wa Ratiba ya Nyakati (Na. 272).

 

Je, unaweza tafadhali kufafanua maana ya mfano wa wakoma 10 waliotakaswa na ni kwa nini ni Msamaria peke yake ndiye alirudi ili kushukuru na kumpa Mungu utukufu? Hadithi iliyoandikwa kwenye Luka 17:11.

Jibu: Andiko linasema kuwa Kristo alikuwa anapita katikati ya Samaria na Galilaya na wakoma kumi walimwendea wakasimama kwa mbali. Hii ilikuwa ni kwa mujibu wa sheria zilizoagizwa kwenye Mambo ya Walawi 13:45-46. Tafsiri ya Talmud hatimaye iliandika makadirio ya umbali huu kuwa ni takriban mita 100.

 

Makabila Kumi yalikuwa ni wa asili ya Samaria. Wasamaria walikuwa ni mchanganyiko wa Wakutheans na Wamedi waliochanganya damu zao na masalia wachache wa makabila kumi yaliyokuwa yamesalia katika Israeli baada ya kuhamishwa kwao utumwani na Mfalme Shalmaneser mwaka 722 KK.

 

Wayahudi waliwachukia na waliwapinga kwa kipindi cha karne kadhaa na kukataa kuyakubali mapokeo yao. Upande wa Kaskazini mwa Galilaya ulikuwa ni nchi iliyojitenga kabisa Yudea. Ulikuwa pia umejumuisha Wayahudi, Wasamaria na wengineo. Wayudea walikuwa ni mkusanyiko wa aina zote mbili, yaani Yuda na Lawi, na pia Waidumean au Waedomu walioongokea imani ya Kiyahudi chini ya Wamakabayo ambao Mfalme Herode alikuwa ni mmoja wao.

 

Mmoja wa hawa waliotakasika, Msamaria, alirudi kumpa Mungu utukufu kwa kutakasika kwake. Kristo akamuuliza, “Je, hamkutakaswa kumi? Wakowapi kenda wengine?” hii inaonyesha ukweli kwamba makabila mengi hayajamrudia yeye.

 

Mfano huu unatupeleka pia nyuma kwenye tukio lililo kwenye 2Wafalme 17:29-35 na kuondolewa kwa Israeli nchini mwao na nafasi yao kuchukuliwa na Wakutha na Waavi na Wahamathi. Jinsi Mungu alivyowapelekea simba ili wawaue hadi walipowaomba wapelekewe makuhani hadi Israeli ili wawaonyeshe na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Mungu. Lakini pamoja na hayo watu wa kila taifa wakajifanyia miungu yao wenyewe, wakaiweka katika nyumba za mahali pa juu, walipopafanya Wasamaria, kila taifa katika miji yao walimokaa. Watu wa Babeli wakafanya Sukoth-benothi kuwa mungu wao, watu wa Kutha wakafanya Nergali, watu wa Hamathi wakafanya Ashima, Waavi wakafanya Nibhazi na Tartaki; nao Wasefarvi wakawaunguza wana wao katika moto kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.

 

Kulikuwa na waume watano wa Kisamaria waliobudu na kulikuwa na miungu ya mataifa matano iliyoingizwa kutoka kwenye ufamle wa kaskazini na kutoka kwa Waisraeli waliotawanyika. Ndipo hatimaye walimwabudu Yahova pamoja na miungu wengine. Na hii ndiyo sababu iliyompelekea Kristo kumwambia yule mwanamke aliyekutananaye kisimani, ambaye alikuwa ameolewa na wanaume watano na yule aliyekuwanaye wakati ule sio wa kwake “Unaabudu usichokijua” (Yohana 4:18, 22).

 

Alitumiwa kama mfano na Mungu kwa maisha yake ya kikahaba na ndoa ya nchi za Kaskazini iliyofananishwa na wanaume watano, na wasiomjua Mungu wanaoishi dhambini kwenye amri au makatazo haramu katika Samaria. Mwanamke aliyekuwa kisimani ni mlinganisho wenyenguvu na pia ni fundisho kuhusu ndoa.

 

Tunaweza kulinganisha kifungu hik cha maandiko na Isaya 54:5; 23:17; Yeremia 22:20; Hosea. 2:10-12. Kutumia mfano wa wakoma kumi yalilenga kuhusianisha na makabila ya kaskazini nay a Wamataifa, na kuwaleta mataifa katika Israeli na kuwatakasa. Msamaria alikuwa ndiyo peke yake aliyerudi na kuja kushukuru kuonyesha kuwa ni sehemu ya hawa walioponywa ambao wametubu kihalisia na kumpa Mungu utukufu. Neno lililotumika kumtaja “mgeni” hapa ni “asiye mwenyeji.”

 

Hivyo, kuna mashahidi wawili pia kwa kila mataifa matano walioletwa upande wa kaskazini na walio kinyume na miungu mitano iliyoiletea madhara imani yao ya kiibada na inayowachukulia wao kuwa wako najisi na wakoma.

 

Rafiki yupo kwenye darasa la Biblia la Agano Jipya na aliuliza mahali ambapo mfano wa talanta ulikusudia, msikilizaji wake alikuwa nani na maana yake ilikuwa ni ipi. Je, unaweza kuniapa mtazamo wako kuhusu kifungu hiki? Je, unaielewaje maana yake Luka 19:12 na wa paundi 10?

Jibu: Mifano huu uliyofuatiwa unabii wa Mzabibu. Wanafunzi walimfuata Kristo kutoka Hekaluni hadi kwenye Mlima wa Mizeituni na wakamuuliza kwa siri awaambie ni lini mambo haya yote yatakapotokea. Ndipo akawapa mfano wa Mzeituni na kashaa akaendelea kuwapa mifano mingine. Maana ya andiko hili ni kwamba kila mmoja amepewa kiwango fulani cha nguvu za kiroho na uelewa, mwingine zaidi yaw engine. Kanisa linapaswa kuungana pamoja naa wengine wote wenye talanta au karama, bila kujali kwa wingi au uchache kiasi gani, bal wanatakiwa kuchangia ili kusaidia kazi ili kwamba iweze kukua.

 

Wale walo na msingi tu wa Roho hawasamehewi kufanya kazi. Wanatakiwa kujipambanua kama mwili na kuweka mali zao kwenye mahitaji ya wengine. Na kama hawatafanyahivyo basi Kristo atawakataa kuingia kwenye ufalme wake. Na ndiyo sababu hakuna yeyote kati yetu anayeweza kukaa nyumbani bila kujishughulisha na kitu chochote. Paundi zilizoelezwa kwenye mfano wa Injili ya Luka unamaana moja iliyochukuliwa kwa mujibu wa juhudi binafsi kwa niaba ya kazi. Utendaji wa kimakini na wa mafanikio ya kazi unaijara sawasawa na juhudi alizoonyesha mtu.

 

Wakati Kristo alipokuwa pale mtini akisulibiwa pamoja na wezi wawili, mmoja wao alimpokea Yesu. Na Yesu alimjiu kuwa ‘Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami Paradiso. (Luka 23:43). Je, Peponi au Paradiso ni “mahali pa kushikiliwa wafu” au ni mbinguni? Sielewi. Kwenye kitabu cha Mwanzo kuasema kuwa aliziumba “mbingu na nchi” mbingu nyingi na nchi moja. Tafadhali fafanua.

Jibu: Wakati Kristo alipokuwa pale mtini alimwambia mtu yule: “Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.” Ni sawa tu na kusema kwamba, “Nakuambia sasa hivi, utakuwa pamoja nami” nk. Imetafsiriwa vibaya na Wanostiki ili kuhalalisha mafundisho yao. Kristo alikuwa mautini kwa kipindi cha siku tatu mchana na usiku, kwa hiyo, kama alimaanisha hivyo, mtu yule angekuwa mbinguni pamoja naye siku ile, basi angekuwa ni mwongo na kumfanya asiwe Masihi. Maelezo kuhusu mchakato wa uumbaji ni mapana sana kwa dunia na hali yake asilia na kutoka kwenye mkazo wa huko nyuma.

 

Yohana

Natafuta mlinganisho kati ya kitabu cha Mwanzo na kitabu cha Yuhana. Nimekwisha fananisha tayari neno la Mungu na nuru na sijawa na kitu kingine chochote. Je, unaweza kunisaidia?

Jibu: Hili ni jambo linalopendeza. Injili ya Yohana iliandikwa baada ya injili nyingine zinazofanana, na inatosheleza mafungufu yaliyomo kwenye injili hizo ya kumtaja Kristo kwenye mfuatano wa matukio ya nyakati zake na kipindi kamili cha kuhudumu kwake. Yuhana anahusishwa, kama unavyoonekana kuashiria, kwa kudhihirisha nafasi na uwepo wa Kristo kipindi cha kabl ya kuzaliwa kwake rasmi duniani akihusiana kiukaribu na Mungu. Kanisa la Agano Jipya lilifanya kazi ya kufundisha kwa kipindi cha marne mbili kuwa Kristo alikuwa ndiye yule Malaika wa Agano la Kale aliyempa Torati nabii Musa. Hili lilikuwa ni jambo la muhimu ili kujua na kuelewa jukumu na wajibu wa Kristo na nafasi yake kwa Mungu, na mafundisho ya Agano la Kale kama yalivyotafsiriwa kwenye Agano Jipya. Mambo haya yamechambuliwa kwa kina kwenye majarida ya: Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243); Malaika wa YHVH (Na. 24); Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229); na Yoshua, Masihi, Mwana wa Mungu (Na. 134). Utakutana na idadi kubwa ya majarida kwenye tovuti yetu yanayoelezea asili ya Mungu na nafasi ya Kristo. Uhusiano wa Injili ya Yohana na vitabu vya Torati unaonekana wazi kwenye majarida.

 

Je, unaweza kunifafanulia kuhusu Yohana 5:1-24? Je, Yesu aliivunja Sabato au ni je, Mungu alimruhusu kufanya hivyo?

Jibu. Hapana, Yesu hakuivunja Sabato. Mafarisayo walisema kuwa alivunja. Kile alichotangua kilikuwa ni tafsiri yao ya uwongo ya naneno yaliyo kwenye Yeremia 17:21-22. Mafarisayo alikitumia kifungu hiki walifanya ubebaji wa kitu chochote kutoka sehemu moja ya wazi hadi nyingine, na kingine kutoka sehemu moja ya siri hadi nyingine, siku ya Sabato kuwa ni halali (soma Talmud Sabb. 6a).

 

Nabii Yeremia anaongelea kuhusu ubebaji wa mizigo kuingia Yerusalemu, au kutoka nyumbani, na kwenda kufanya kazi siku ya Sabato. Kuchua mkeka mmoja tu wa kulalia nyumbani kungekuwa ni uvunjaji mkubwa sana wa Sabato, lakini walikuwa wanataka kufanya ionekane hivyo. Hatimaye Baraza la Mishnah (mwaka 200) lilifafanua kwa kina kilichopasa kutolewa, kuhusu suala hili la vifaa vya kulalia, iwapo kama kwa mfano, Siku ya Upatanisho ikiangukia siku iliyofuatia baada ya Sabato, ambayo kwa wakati mwingine walifanya kabla ya mafundisho ya uahirisho hayajashika kasi. Kristo alishika Sheria, ila mara nyingi alikosoa kitendo cha kutafsiri vibaya au kimakosa sheria, kama ilivyo kwenye suala hili.

 

Yohana 5:18: Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu, bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu. Kwa nini Wayahudi walimwelewa Yesu kuwa alikuwa anasema kuwa alikuwa sawa na Baba, wakati inaonekana wazi sana kwamba alichokuwa anadai ya kuwa yeye ni Mwana wa Mungu? Wale wanaoamini Utatu wanalichukulia andiko hili kama ushahidi kwamba Mwana alikuwa na hadhi sawa ya kiuungu na Baba kama sehemu ya muungano wao wa Utatu.

Jibu: Kuelewa kuwa Elohim aliyetajwa kwenye Agano la Kale, ambaye ndiye alimpa Musa Torati, kuwa alikuwa Malaika Mkuu ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wana wa Mungu. Wanalielewa andiko la Zaburi 45:6-7: “Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.” kuwa ni kama linamtaja Masihi ambaye ndiye alikuwa Mwana wa Mungu.

 

Mithali 30:4-5 inauliza swali kama ilivyo kwenye jina la Mungu ni lipi na la Mwanae ni lipi pia, na kisha inalitaja jina lake Mungu wa Pekee wa Kweli kwa umoja wake kwenye aya ya 5, ilimuita kuwa ni Eloah. Kwa Kikaldayo, aliitwa “Elahh.” Uwingi wake ulikuwa ni “Elohim” na “Elahhin” kwa Kikaldayo. Toleo la kimashariki la lugha ambayo ilifanyika kuwa ni Kiaramu cha Kimashariki ambayo hatimaye kilikuja kufanyika kuwa ni Kiarabu, na ndiyo maana Waislamu wanasema kuwa jina la Mungu kuwa ni “Allah’”; likiwa na h mbili kuwa ni msisitizo.

 

Wakati Kiyunani kinapolitumia neon “aggelos” lililotafsiriwa kama “malaika” au “angel” kwa Kiingereza. Limetumika kuwataja “wana wa Mungu” au “elohim” kwenye Kiebrania. Limetumika hivyo pia kwenye tafsiri ya Kiyunani ya Septuagint (LXX) na pia kwenye Agano Jipya. Zaburi 8:4,5,6, iliyonakiliwa ikisema: “Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima; Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.”

 

Sasa neno hili ni, kama tunavyoliona kwenye Kiebrania, “elohim” ambalo maana yake ni “miungu.” Lilitafsiriwa kama “malaika” wengi kwenye tafsiri ya Septuagint na pia kutoka hapo hadi kwene maandiko ya Kiyunani kwenye Kiebrabia. Inabeba maana hiyohiyo kwenye tafsiri za Vulgate, Kisyria na Kiarabu kwa kuwa iliwapendeza waamini Utatu kuwa nayo hii kama “malaika” na kuruka maneno yasemayo “kwa kitambo kidogo.” Sababu iliuwa ni kwamba hakuna hata mmoja wao aliyependa kujua kuwa “elohim” walikuwa ni ongezeko tu la utaratibu wa viumbe.

 

Hata hivyo, andiko hili ni wazi kabisa linasema “elohim” kwenye Kiebrania asilia, na makuhani walijua kuwa mwana wa adamu alikuwa ni elohim aliyefanyika hatimaye kuwa ni Mwana wa Mungu akiwa ni “monogenes theos” au “mzaliwa pekee wa Mungu” aliyetajwa kwenye Yohana 1:18 (sawa na tafsiri ya Marshall’s Greek English Interlinear RSV). Maandiko yaliyo kwenye tafsiri ya Companion Bible kuhusu andiko hili yanafafanua kwa kina mambo haya.

 

Walikuwa wanamtaja yeye walimfanya kuwa sawa na elohim na, kwa kuwa hii haikuongelewa kwenye Kiyunani ila kwenye Kiaramu, tunapata andiko hili kuwa “elohi” kisha linaonekana kuwa ni “malaika.” Wana wa Mungu wote walikuwa ni elohim kama maandiko ya Agano la Kale yanavyoonyesha kwenye matumizi yake. Elohim hawa walijulikana kama “aggelos” {ang’-el-os} au “wajumbe” na walitafsiriwa kama malaika au “angel” kwa Kiingereza na kwenye maandiko mengine. Hata hivyo, makuhani wa Hekaluni hawakuyumbishwa na mapokeo ya kipagani ya Kirumi wakiigiza kujifanya kama Wakristo kwa karne chache za wakati huu, na kwa hiyo walijua maana yake kikamilifu na vizuri sana.

 

Kwenye Yohana 7:53 Mafarisayo wanamkemea Nikodemo wakisema: “Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii.” Usemi huu si sahihi, ikikumbukwa pia kwamba Yona alitokea Galilaya. Hata hivyo, Isaya 9:1 inasema: “...hatimaye yeye (Mungu) ataiondolea aibu na kudharauliwa Galilaya...” ambayo inafuatiwa na aya ya 6 inayosema “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, … Naye ataitwa jina lake … Mfalme wa amani.” Aliwezaje Isaya kupata uhakika wa wazi sana kiasi hiki? Je, Mafarisayo walifanya makosa ya kiuana zuoni, au walikuwa wanafanya makosa ya makusudi kuusema uweli, yaani waliamua kuongopa, ili kutumikia mwisho wao mbaya na usiofaa?

Jibu: Ndiyo, walikuwa wanaongopa ili kuzitumikia tama zao zisizokoma, kama mtazamo wa shughuli za kidini ulivyo hata leo, kuongopa ili kujipatia faida zao wenyewe. Ukristo wa imani za dini Kongwe ni vurimai ya ibada za kipagani, miungo ya uwongo na imani potofu kwa kuwa makasisi wake wanafundisha au kutumika kwa malipo au mshahara na wamejitungia au kijitengenezea imani zao za uwongo ili kukidhi au kuchanganya na mapokeo na imani za kipagani za watawala na Dola ya Warumi walizozipenda na kuziamini.

 

Yona na Hosea wote wawili walitokea Galilaya, Eliya alikuwa Mtishbi na Wagileadi walikuwa wanatoka mashariki, Bullinger anasema kuwa yeye na Elisha, na huenda hata Amos, wanaonekana kuwa walikuwa na uhusiano wa kinasaba na Galilaya.

 

Sababu hasa nay a kweli pia ilikuwa ni kwamba Wagalilaya walikuwa pia ni wana wa kweli wa Yuda, lakini wenyeji wa Yudea wengi walikuwa na idadi kubwa ya Waedomu. Hii huenda ndiyo sababu ya kwamba misingi halisi ya uliokuwa nyuma ya juhudi ya Mafarisayo ya kupotosha au kutafsiri vibaya Maandiko Matakatifu. Chini ya sheria, Galilaya ilichukuliwa kama ni sehemu nyingine iliyotengwa na nchi. Jambo mhimu na la kweli ni kwamba Yona alitokea Galilaya, na Ishara ya Yona ndiyo pekee iliyoitolwa ili kuithibitisha huduma ya Kristo na ambayo kwayo Yuda waliangamizwa kwayo. Soma kwene jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Tena wa Hekalu (Na. 13); na Uchambuzi wa Ratiba ya Nyakati (Na. 272).

 

Kwenye Yohana sura ya 10 Yesu Kristo anaongelea kuhusu Mchungaji Mwema na kuwajua kondoo wake, kuutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo zake hao, nk. Kisha aya ya 16 inaongelea kuhusu ‘kondoo wengine’, ambao sio wa zizi lake. (1) Kina nani hawa Kristo anaowaelezea kuwa ni kondoo wa ‘zizi hili’ na (2) kina nani hawa wanaotajwa kuwa ni ‘kondoo wengine?’

Jibu: Kondoo hawa ni wale wanaowafuata na kuwasikiliza wachungaji wa uwongo. Alisema pia kwamba wengi watamwita “Bwana, Bwana,” wa wasiyatende mapenzi yake. Atawaambia “Tokeni apa kwangu.” Hawa pia ni wale walioitwa lakini wasiwe wateule na kuingia kwenye zizi la wateule. Maelezo ya kitabu cha Ufunuo huonyesha kuwa kuna imani yaa dini za uwongo, ambazo zitaangamizwa katika siku za mwisho. Hivi ndivyo alivyoelezea na ufafanuzi alioufanya.

 

Dini za uwongo zilikuwa kazini katika kujaribu kuingiza imani potofu ya Baal-Easter mapema sana katika wakati wa Yohana, aliyeziandika kwa kina mafundisho na habari za Mpingakristo, mafun disho yanayotenganisha ubinadamu wa Kristo na hali ya uungu. Haya yalikuwa ni mafundisho ya imani ya waabudu mungu Attis, ambayo yalimuweka mungu Attis kwenye cheo cha namna zote mbili, yaani baba na mwana kuwa ni mungu mmoja huyohuyo.

 

Mafundisho haya na mtazamo huu ukaingizwa kwenye imani ya Kikristo kama Ubinitariani na hatimaye ukazaliwa Utrinitariani. Imani ya Unostiki ilipata nguvu na ushawishi mkubwa pamoja na kukubalika na kuingizwa kwa imani na mafundisho yao ya mbinguni na motoni, makatazo au kujinyima vinywaji, useja na ulaji wa mbogamboga tupu, yaani imani ya kutokula nyama. Soma majarida ya Uvijiteriani Kwene Biblia (Na. 183); na Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188).

 

Yohana 12:12-13 inaonyesha kuwa watu walibeba matawi a mitende na wakaenda kumlaki. Je, matawi ya mitende yana maana yoyote kiimani pamoja na miti yennewe ya mitende au kuna uhusiano na ile ya kwenye Kutoka 15:27, Hesabu 33:9 au ile ya kwenye mahekalu ya 1Wafalme 6:29,32,35, 2Nyakati 3:5, Ezekieli 40:16, 29, 32,35,41:18-20?

Jibu: Salamu iliyo kwenye andiko hili inatokana na Zaburi 118:25,26. Uingiaji wake Bwana Hekaluni na jinsi walivyomsifu kundi la watu kwa Kiaramu inamaaisha: “saidia sasa” (Hoshi' an-na). miti ya mitende ina maana yake kwa kuwa inafanana pia na ukweli wa Masihi. Kwenye hekalu aliloonyeshwa nabii Ezekieli utauona umewekwa katikati ya makerubi wawili, makerubi yenye vichwa vya binadamu na samba. Mti wa mzeituni unaashiria Malaika wa Uwepo na mti uliofanya maji ya Meriba yakubalike na Israeli.

 

Kama Yesu alisulibiwa siku ya Jumatano, ni nini basi kinachomaanisha kwenye Yohana 19:31?

Jibu: Siku hii ilikuwa ni ya 14 ya mwezi wa Abibu, ambayo ilikuwa ni Siku ya Maandalizi makubwa ya Pasaka ambayo mwanakondoo wake aliuawa alasiri wakati alipouawa Kristo. Na mwanakondoo huyo aliliwa usiku ule ule wa Siku ya Kwanza ya Miate Isiyotiwa Chachu. Kumbuka isemavyo Yohana 19:31:

“Basi Wayahudi, kwa sababu ni Maandalio, miili isikae juu ya misalaba [stauros] siku ya sabato, (maana sabato ile ilikuwa siku kubwa), walimwomba Pilato miguu yao ivunjwe, wakaondolewe. ”

 

Katika mwaka aliosulibiwa Kristo, ambao ni mwaka wa 30 BK, siku ya 14 Abibu iliangukia siku ya Jumatano. Kwa hiyo, Siku ya Takatifu ya Kwanza ya Mikate Isiyotiwa Chachu ya 15 Abibu iliangukia siku ya Alhamisi tangu join ya siku iliyotangulia (yaani usiku wa Jumatano). Kwa hiyo alishinda kaburini siku za Alhamisi, Ijumaa na siku ya Sabato. Alifufuka mwishoni mwa Sabato kukiwa ni siku tatu kamili za mchana na usiku kuwa kaburini, sawaswa na ulivyosema unabii.

 

Taarifa za mwanzoni zinasema walikuwa wanafundisha kuwa tukio hili la kusulibiwa lilifanyika siku ya Jumatano. Imani na maadhimisho ya Easter na Usulibiwaji wa Ijumaa vinatokana na imani potofu za miungu ya Attis na Adonis. Tazama majarida ya Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235); Mabishano ya Wakuartodeciman (Na. 277). Pia tazama jarida la Majira ya Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159). Itajibu maswali yako kuhusu nyakati na maandiko.

 

Matendo

Kwa nini baadhi ya vitabu kama cha Matendo haviishii na neno Amina na vitabu vingine vingi vinafanya hivyo?

Jibu: Neno hili “Amen” linatokna na lugha ya Kiebrania SHD 543 “'amina” maana yake ni “hakika.” Linapotumika kama kijivebu, linatumika kama “kweli” na kimsisitizo linamaanisha “uaminifu”. Kwa hiyo linamaanisha, “na iwe hivyo” au “ni kweli”. Neno “Amina” linatumika kwa kuwa ni agizo la moja kwa moja la Mungu chini ya sheria. Neno la Kiyunani SGD 281 amen ni tafsiri ya kiuandishi ya moja kwa moja kutoka kwenye lugha ya Kiebrania lenye maana hiyohiyo moja. Ilichukuliwa kutoka kwenye Kiingereza kwa karne nyingi lenye maana hiyohiyo. Kwa hiyo, watu wetu wanaendelea kulitumia hadi siku hizi kwa agizo walilopewa na Mungu pale Sinai. Makundi yote mawili, yaani wanawake na wanaume wanabudi kulitumia neno hili (sawa na Hesabu 5:22; Kumbukumbu la Torati 27:15-26). Ni msisitizo wa kuonyesha au kumaanisha ushindi au kukubaliana yaliyoombwa kwenye maombi na watu wote. Lilitamkwa hivyo kwenye kipindi chote cha marejesho mapya (Nehemia 5:13; 8:6). Linatokea kwenye Zaburi pia. Lilinenwa na manabii (Yeremia 28:6). Kristo aliagiza litumike kama sehemu ya Sala ya Bwana.

 

Limerukwa kwenye maandiko hayohayo kwa kuwa yalikuwa ni historia tu. Kwa wengine, lilitumika kama msisitizo wa kusema “na iwe hivyo” kwa kuwa Kanisa lilikuwa likishutumiwa lilikuwa kwenye anga la Mamlaka ya Mungu, wakati kwamba kitabu cha Matendo hakikuwa waraka uliohitaji kuonyesha ushindi au kutenda kutoka Kanisani. Kuna nadharia iliyozidishwa inayoendelewaa na baadhi ya Makanisa ya Marekani kuwa linauhusiano fulani na imani za kale za Wamisri na kwa namna fulani linatokana au limechukuliwa kwenye mitindi ya ibada za mungu Amun Ra. Huu ni uwongo wa wazi kabisa na waanzilishi wa uvumi huu au mafundisho haya wanajaribu tu kuishusha hadhi na kuipotosha sheria moja wapo iliyo kwenye Torati ya Mungu inayosisitiza kutamka neno hili, jambo ambalo Israeli na Kanisa wamekuwa wakilifanya kwa uaminifu mkubwa tangu pale Sinai hadi siku za leo.

 

Kwenye Pentekoste ya kwanza, baada ya kifo cha Measihi, wanafunzi 12 walikusanyika pamoja saa 3 asubuhi na wakampokea Roho Mtakatifu. Je, hii inaweza kuwa ni dalili ya wateule kuwa mahali pa kusaidia kusimamia sheria ya Mungu? Yawezekana kuwa kwamba wale makutano 120 wa kwenye Matendo 1:15 ni ishara au imanaanisha Yubile 120 iliyotimia kikamilifu, ambayo kwamba Shetani na malaika wake waasi watafungwa kwa kipindi cha miaka “1000” na Roho Mtakatifu wa Mungu atakuwepo ulimwenguni mwote wakati huu wa millennia na kufuatia?

Jibu: Ndiyo. Hili ni jambo lenye kupendeza sana. Tunajifunza kuona kwamba vipindi vitatu vya miaka arobaini arobaini vinafanya jumla ya miaka 120, ambavyo ni zama tatu na hivi vinaonekana kimuashirio kwenye maisha ya nabii Musa na vya Utawala wa Wafalme. Jaiida litatolewa hivi karibuni kuelezea kwa kina. Mtazamo wa kwamba hawa 120 walikuwa muhimu kama taswira ya kuhitimisha mavuno ya Mungu unavutia sana na huenda ni sahihi.

 

Matendo 15:24-29 inaonekana kusema kuwa wamataifa hawapaswi kuzishika sheria zote, bali wanapaswa tu kujiepusha na ulaji wa nyama zilizotolewa sadaka kwa sanamu na ulaji wa damu na uasherati? Wakati kwamba vitu vya “lazima vimekwisha orodheshewa?

 

Matendo 15:24-29 states: Kwa kuwa tumesikia ya kwamba watu waliotoka kwetu wamewasumbua kwa maneno yao, wakipotosha roho zenu, ambao sisi hatukuwaagiza; 25 sisi tumeona vema, hali tumepatana kwa moyo mmoja, kuwachagua watu na kuwapeleka kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, 26 watu waliohatirisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo. 27 Basi tumewatuma Yuda na Sila, watakaowaambia wenyewe maneno yayo hayo kwa vinywa vyao. 28 Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima, 29 yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu.

 

Jibu: Kwenye tafsiri, mtu hazuiwi wala kufungwa na chochote. Ndiyo, Agano Jipya linaonyesha wazi sana kuwa waliishika sheria ya vyakula, na waliishika Kalenda Takatifu, na waliishika Pasaka. Kwa kweli, Mabishano ya Waquortodeciman yalipelekea kufarakana kwa kanisa mwaka 192 na Makanisa ya Washika Sabato yamejitenga mbali kutoka kwenye Kanisa la Roma tangu wakati huo. Soma jarida la Mabishano ya Waquartodeciman (Na. 277).

 

Pia kuna makundi mengine yaliyotengwa mahali pengine ambayo hayajajuluishwa hapa. Kwa hiyo, andiko hili linapasa lishughulikiwe na mambo fulani yakinifu kwa malengo fulani kusudiwa. Hili limeongelewa kwa kina kwenye jarida la Sheria ya Vyakula (Na. 15) na Imani ya Kutokula Nyama ya Ulaji Mbogamboga Tupu na Biblia (Na. 183).

 

Andiko hili waliandikiwa watu waliokuwa kwenye mazingira ya numba ya wapagani, kama vile watumwa wa mabwana wapagani. Hii ilifanya mazingirfa kuwa ni vigumu sana kwa waongofu. Maandiko haya hatimaye yaliwahusu watu dhaifu aa imani wanaokula mbogamboga eke yake kwa tatizo kama hilohilo. Iwapo kama tutalitathimini andiko hili, na kulichukulia kama linavyosomeka kwamba hii ndiyo imayohitajika pekee kwenye imani, kisha ndipo amri mbili zikaorodheshwa na ni kipande saidizi cha sheria au kanuni kuhusu ulaji wa damu.

 

Amri ya sita hata haionekani kutajwa hapa, pamoja na ile ya pili moja kwa moja, nay a tatu, ya nne, ya hamsini na nane, ya tisa na kumi na sio vyovyote. Kwa hiyo, kwa tafsiri kama hiyo, si vibaya kuua, kudanganya, kuongopa, kuiba, kutamani, na kumkufuru Mungu. Hakuna anayeamini hivyo, na kuna aliyelitafsiri andiko hilo kwa namna hiyo au kwa mapokeo yoyote ya kidini, isipokuwa waantinomia siku hizi. Soma jarida la Sheria ya Mungu (Na. L1) na mwandamano wa majarid mengine ya Torati.

 

Naelewa kuwa inatupasa kuishika Torati au sheria za Mungu kutokana na maandiko mbalimbali kadhaa yaliyo kwenye Biblia. Nilikuwa nasoma kitabu cha Matendo na inasema hatulazimiki kutahiriwa au kuzishika sheria (Matendo 15:24).

Matendo 15:28-29: "Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima, 29 yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu.”

Naona mahali panapoonyesha kuwa walizishika Sabato, Siku Takatifu, Miandamo ya Mwezi Mpya, nk. Hii ni sehemu ya maagizo ya Torati. Je ayah ii inaongelea kuhusu sheria nyingine yoyote; je, ni inakosea au ni makosa ya kitafsiri; au kuna namna nyingine zaidi ya kuitafsiri kwamba ni kwa nini walisema kwamba Wamataifa hawalazimiki kufuata na kushika sheria?

Jibu: Andiko lililo kwenye Matendo 15:24 ni la kughushi na limeingizwa makusudi kwa nia ya kupotosha kwenye tafsiri ya Receptus likiwa na lengo la makusudi kabisa ya kupotosha mahudhui na umuhimu wa waaminifu wake wasiishike Torati ya Mungu. Tafsiri ya the Companion Bible KJV inamaelezo yanayoelezea vizuri maneno haya kwamba: “Kusema kwamba yawapasa mtahiriwe na kuzishika sheria” ambayo hayapo kwenye maandiko ya zamani, na yahapo kwenye tafsiri nyingine za Biblia na ikisomeka hivyo au ikituama kwenye maandiko ya zama kale.

 

Suala lililopo hapa kuhusu watu wa Mataifa kuingia kwenye imani ndani ya nyumba za wapagani na ambao walikuwa wanaonyeshwa kwenye imani hizo za kipagani. Utoaji wa moja kwa moja wa sadaka kwa sanamu uliepukwa, kama ilivyokuwa umeonekana mara nyingi kuwa ni matendo kutoa sadaka za wanyama zilizosongolewa au kibudu. Kinachotakiwa kuepukwa pia ni desturi ya uasherati au kufanya ngono, ambayo ilikuwa ni ya kawaida kufanyika kwenye ibada za Hekaluni ambako damu ilikuwa inaliwa pia. Kile kiitwacho “Utumbo wa Nguruwe” ni masalia ya siku hizi yatokanayo na matendo haya. Andiko hili linashughulika na matendo na halitenganishwi. Soma majarida ya Uvegetariani na Biblia (Na. 183) na Mafundisho ya Mapepo ya Siku za Mwisho (Na. 48).

 

Warumi

Yeyote anayeijua vyema Warumi sura ya 1 anajua kwamba Mtume Paulo anaendelea mbele zaidi kwa kulielezea tendo hili na analitaja kama tendo la ufiraji. Paulo anachagua kutumia neno ‘la kike’ kuelezea tabia takatifu ya kimbinguni. Mambo muhimu na ya juu kiasili yako kijozi, yaani mwanaume na mwanamke; mwanaume aliongozana na mwanamke, na mwanamke na mwanaume. Wakati mwanadamu anaposahau hili, walianza kuishi maisha ya jinsia moja, yaani mwanaume kwa mwanaume, na mwanamke kwa mwanamke. Kifungu kisemacho “Hekima ya Mungu iliyotajwa” (Luka 11:49) ni sahihi. Kwa imani ya Kiyahudi, neno Hekima lilikuwa la nasaba ya kike kwa Mungu. Neno lenyewe lilikuwa linaonyesha nasaba ya kike ya Mungu. Hekima ni kwa Mungu ambavyo Logos ni Mungu. Kwa mara nyingine tena tunaletwa kwenye mawasiliano na tabia asilia ya kike ya Mungu. Je, jambo hili linaashiria nini kwenye Ukristo?

Jibu: Dhana iliyopo ya Sophia, kuwa kama hekima, ni ya kike kwa kuwa Logos ni Bwana arusi, na Kanisa ni Bibi arusi. Hii imetokana pia na mgangano wa kijinsia wa Roho Mtakatifu (soma jarida la Jinsia ya Roho Mtakatifu (Na. 155)).

 

Mlingano huu mpya ulibidi uanguke chini tunaposema kuwa Kristo alipewa roho na kupaa juu kama Mwana wa Mungu kwa nguvu kwa Kufufuka kwake kutoka kwa wafu. Sio sahihi sana kumuweka roho wa Kristo kwenye jinsia ya kike kama ilivyo kwenye nasaba ya kiume kwa kanisa. Wanaume hawana ugumu wa kuelewa dhana ya ubwana arusi wa Kristo na wakuwa kwa wakati mmoja Mwana wa Mungu.

 

Tunajua dhana ya siri za Mungu kwenye Maandiko ya familia. Uandishi wa waraka wa Warumi umekusidiwa ili kuonyesha mwendelezo wa kupunguza watu wenye asili ya imani wakati ibada ya sanamu ikiwa imepuguzwa. Wakati mtu anapomchukua mungu wa uwongo, ndipo mtu huyo anaanza mwendelezo wa kupungua katika Roho Mtakatifu na kwa taifa. Ukweli unabakia kwenye ufisadi na ndipo hasira ya Mungu inawaangukia. Wanageukiana kwa tama zao za mwili.

 

Mtu hawezi kurikiria kuelezea vizuri kuhusu mwendelezo wa mzoroto au kuzorota na kupungua kwa Kanisa kwa kipindi cha zaidi ya miaka 2000. Baada ya kuingizwa kwa imani ya Mungu wa Utatu, kipindi cha karne ya pili, Kanisa lililoungana likafanyika kuwa ni shirika au kiungi kisichoongezeka klichobobea kwenye matendo ya kisodoma na ukengeufu; likiwaua wale wanaozishika amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo, likiyakumbatia mafundisho ya mapepo, na kuwaamuru wale wanaojizuia kuoa na kutokula nyama, ambazo zilitolewa ili zipokelewe kwa shukrani.

 

Matatizo mbalimbali yameelezewa kwenye majarida ya Uvegetariani na Biblia (Na. 183) na Wanikolai (Na. 202).

 

Ni nini “Matendo ya Sheria” (Warumi 3:20) anayoyataja Paulo kwenye maandiko yake?

Jibu: Matendo ya Sheria ni kitabu. Kilijulikana kama Miqsat Ma'ase ha Torah. Kwa Kiyunani, kilijulikana kama “ergon nomou” na kwa Kiingereza ndicho kinachoitwa “Works of the Law”, yaani Matendo ya Sheria.” Kitabu hiki kilipotezwa kwa makusudi miaka takriban 1900 iliyopita. Gombo mashuhuri la The Dead Sea Scrolls lina nakala yake. Nakala hii ilitafsiriwa na maprofesa Qimron na Strugnell. Waraka huu uliandikwa kwa maana yake kwenye fasiri za ufafanuzi za Agano Jipya. Jarida la Maandiko ya Matendo ya Sheria - au MMT (Na. 104). Maandiko asilia na tafsiri zake zinapatikana pia kwenye majarida na vitabu vya CCG.

 

Warumi 10:4 inassma: ‘Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.’

Je Torati iliishia kwa Kristo? Ni nini kilichogongomelewa mtini, maarufu kama msalabani? Na kama ni hivyo, ni kwa kitu gani gani basi tulichopatanishwa nacho sisi?

Jibu: Torati yote ilimhusu Kristo na mpango wa Mungu kwa kuwa sheria au torati ilianza kutokana na Asili au Tabia ya Mungu. Na ndiyo maana kwamba Kristo ndiye mwisho wa Sheria. Hakuitangua torati. Alichokigongomelea pale mtini kama inavyosema Wakolosai ni mashitaka ya deni au kwa lugha nyingine inaitwa Hati ya Mashitaka au Chierogriphon. Tuko huru kwa kuwa alilipa gharama ya madeni yetu kwa kila mmoja wetu na pia kwa kundi kama wateule.

 

Yeye ajitakasaye na wale wanaotakaswa wote wana asili moja kama inavyosema Waebrania. Tumepatana na Mungu kwa njia ya Kristo aliyestahili kuwa kiongozi wetu. Tazama jarida la Uhusiano Uliopo Kati ya Wokovu kwa Neema na Sheria (Na. 82). Mlolongo wa majarida ya Sheria ni muhimu ukasoma. Tazama pia kwene jarida la Sheria ya Mungu (Na. L1).

 

Unaweza kufafanua jambo alilokuwa anajaribu kulisema Mtume Paulo kwenye Warumi 14.

Jibu: Kwenye Jamii ya Warumi wengi waliokuwa waumini Kanisani walikuwa watumwa. Kwenye nyumba za Warumi walitenga milo au chakula kwa kulinganisha sawasawa na siku za utoaji dhabihu. Kwa hiyo, dhana ilikuwa ni kwamba mtu aliye kwenye milki ya nyumba ya wapagani alichukuliwa kama anakula nyama iliyotolewa sadaka kwa sanamu.

 

Samaki walikuwa watakatifu kwa Atargatis, au Dercato au Cato, na samaki alililiwa kwenye siku yake, na hivyo Ijumaa ilikuwa ni siku maalumu ya samaki. Kitendo hiki kinakutikana hata leo kwenye imani ya Wakatoliki Warumi. Wanapoulizwa wanasema kuwa walifanya uamuzi wa kusaidia kiwanda cha samaki, lakini ukweli ni kwamba ilianzia kwa samaki mtakatifu aliyejulikana kama mungu Atargatis. Pinata au kofia ya kiaskofu ilitokana na kumuenzi samaki huyu pia.

 

Nguva jike aliyopo ndani yake ni mbegu mpya za uzima au uhai na inatakiwa ivunjwe ili mbegu zitolewe: Ambayo ni sadaka ya damu ya mwanadamu. Mungu Attis, na makuhani wake matowashi, walishirikishwa na dini hii potofu ya Easter. Kanisa lilikuwa linashughulikia na ukweli ambao ndugu wapendwa hawakuujua kwamba ni wapi nyama hizo zilikokuwa zinatokea. Kwa hiyo, walikuwa wanahukumiana kila mmoja na mwenzake na wengine waliamua kula mbogamboga tupu, peke yake ili kujiepusha na uwezekano wa kula nama zilizotolewa sadaka kwa sanamu.

 

Mtume Paulo alikuwa anawaambia wajihadhari sana. Sanamu zenyewe hazikuwa ktu kwao, na kama mtu hakujua, ndipo wale waliokuwa na imani kuu mipngoni mwao walikula nyama bila kudhurika na chochote. Kwa jambo hili, kuua lilikuwa ni jambo sahihi na hivyo, damu haikuliwa. Kwa mujibu wa Bullinger, kipindi cha nabii Danieli, waliacha kula nyama kwa kuwa wanyama walikuwa hawakuchinjwa vyema (tazama tafsiri ya Companion Bible kwenye Daniel 1).

 

Kitendo cha kufuatilia siku kilifanyika kwa lengo la kuamua ni siku zipi ambazo pia ni aina gani ya nyama zinapaswa kutolewa sadaka. Halikuwa ni suala la kutozishika Sabato peke yake, kwa kuwa hilo lilikuwa wazi imeamriwa na kujulikana wakati ule. Kwenye suala hili, waliamua aina ya dhabihu kwa lengo la kuzila nyama zake. Jambo hili limeelezwa kwa kina kwenye jarida la Uvegetariani na Biblia (Na. 183).

 

Wakati mume anapomchukua au kumuoa mke, analazimika kumpa jina lake. Kwa hiyo inaweza kusemekana kwamba Kanisa likiwa kama bibi arusi wa Kristo yapasa liiwe kwa jina lake. Hivyo basi, mtu aliye kwenye Kanisa la Kristo anaweza kudai kuwa wao ni kanisa sahihi kwa kuwa wamelichukua jina hili kama lilivyo kwenye Warumi 16:16. Je, hii ni kweli na sahihi?

Jibu: Hapana. Hiyo si sahihi. Biblia inasema wazi kabisa kuhusu hilo kwamba Kanisa lina maneno machache. Na majina hayo ni kama yafuatavyo: “Kanisa la Mungu” (kwenye Wakorintho na kwingineko) kwa makanisa ya mahali pamoja, na “Makanisa ya Mungu” kwa jina la ujumla kwa mataifa yote. Pia waliitwa “Wakristo” na kama shirika waliitwa “Njia” au “Watu wa Njia Ile.” Warumi 16:16 inasema kwenye maandiko ya zamani kwamba “Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.” Hii kwa namna yoyote inapunguza uzito wa kusudi au lengo la Mungu la kuwa Kichwa cha Kanisa. Kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na Kichwa cha Kristo ni Mungu. Kristo ni mwili kwa maana ya kwamba yeye ni Kanisa, na hivi ndivyo ilivyotumika kwenye Warumi. Jambo hili limefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Muundo wa Makanisa ya Kikristo ya Mungu (Na. 68).

 

1Wakorintho

Je, kwani Paulo anaizungumzia Sikukuu ya Miate Isiyotiwa Chachu hapa?

IWakorintho 5:6-8 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima? 7 Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo; 8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli.

 

Na kama ni hivyo, hii inajumuisha pia kuishika Pasaka kama alivyosema pia kuwa Kristo alitolewa sadaka kama Pasaka wetu? Je, hii ndiyo sababu iliyopelekea Pasaka kutolewa kwa Waisraeli kwa kipaumbele cha kwanza ili dhabihu hii ikamilike katika Kristo?

Jibu: Ndiyo, alikuwa anaiongelea Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, ambayo ni sehemu ya sikukuu hii, inayofanyika mwanzoni mwa Siku 14 ya mwezi wa Abibu ambayo ni ya Maandalio. Pia alianzisha utaratibu wa kuadhimisha Mlo wa Meza ya Bwana kwenye mlo wa kwanza wa siku ya 14 Abibu kwenye karamu ya kwanza ijulikanayo kama Chagigah, ulioanzia siku ya Maandalio ya Pasaka jioni inayofuatia, ambayo ndiyo ilikuwa Pasaka ya Kristo.

 

Kama mtu haishiki Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu, basi halielewi lengo na dhumuni la kuondolewa kwa dhambi kupitia kwa dhabihu ya Kristo. Mtume Paulo mitume wengine na kanisa lote la kwanza walizishika sikukuu zote. Mkanganyo ulianzia mnamo mwaka 192 wakati askofu wa Roma alipojaribu kushurutisha kuingiza mafundisho ya kizushi ya maadhimisho ya Easter kitendo kilichopelekea kugawanyika kwa kanisa. Soma jarida la Malumbano na Hoja za Wakuartodeciman (Na. 277). Pia kuna majarida mengine ya Pasaka na Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu. Soma pia majarida ya Pasaka (Na. 98); Chachu ya Kale na Mpya (Na. 106a); na Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa (Na. 106b).

 

Wengine wamefikia kuhitimisha kwamba wanawake wanapaswa kujifunika ushungi vichwa vyao wanapokuwa wanamuomba Mungu Baba yetu. Nadhani hii ilikuwa ndiyo sababu kwa wanawake kuvaa nywele ndefu, ambazo ni kwa ajili ya kuwafunika na kuwalinda. Je, unaweza kunisaidia hili? Je, ni lazima wanawake wajifunike vichwa vyao wanapoomba?

Jibu: Mwanamke yampasa kufunika tu kichwa chake anapoomba, iwapo kama ana nywele fupi tu, kwa kuwa nywele zake ni utukufu wake. Yampasa kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mtiifu kwa mumewe kwa ajili ya Malaika (1Wakorintho 11:10-15).

 

Nywele zake ni kifuniko chake. Na ndiyo maana ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu. Mwanamke anapaswa awe na nywele ndefu ili kujifunika, kwa hiyo, urefu wa nywele za mwanamke wapasa uwe ni zaidi ya nywele za mwanaume. Ni mwanaume tu ndiye anaruhusiwa kukata nywele zake. Kama mwanamke akkata nywele zake, basi itamlazimu afunike kichwa chake. Ndiyo maana kwamba ni aibu kwa mwanamke kuwa na nywele fupi au zilizonyolewa kipara, kama tulivyoshuhudia, kwa mfano, yaliyotukia mwishoni mwa vita ya Ufaransa.

 

Wagalatia

Ni nini maana ya andiko lililo kwenye Wagalatia 4:9-11?

Jibu: Ni mafundisho ya kizushi yalijitokeza kwenye makanisa ya Galatia na Kolosai, na habari zake zimeelezwa kwa kina kwenye jarida la Mafundisho ya Kizushi Kwenye Kanisa la Mitume (Na. 89). Ilikuwa ni aina ya teolojia ya Kinostiki iliyokuwa inashughulika na mambo kadhaa fulani na kufanya mambo sawasawa na nyakati za mwanzo wa upagani. Waweza pia kusoka jarida la Uvegetariani na Biblia (Na. 183) na kwa mambo mengine soma jarida la Nafsi Hai (Na 92) ili kujua tatizo lilitokana na nini.

 

Waabudu Mashetatani na Wapigaramli au Wanajimu wanaoitumia kama kipimo cha kutabiri maafa, na kumuinua mtu juu kuliko Mungu na kumfanya kama ni mungu wa nadharia hii. Mafundisho ya Biblia yanakataza kufanya hivyo. Hatima yetu ni kufanyika kuwa wana wa Mungu, na tunangojea ufufuo wa kwanza wa wafu ili tufanyike kuwa wana wa Mungu wenye nguvu za Roho Mtakatifu, ili Mungu afanyike kuwa ni yote katika yote na ndani ya yote (Waefeso 4:6). Tazama majarida ya Nafsi Hai (Na. 92); na Ufufuo wa Wafu (Na. 143).

 

Ni siku, miezi, nyakati na miaka gani ambayo Wagalatia alikuwa wanaiadhimisha ambayo Mtume Paulo alikuwa anawaonya wasiiadhimishe?

Jibu: Wagalatia 4:10 haiwezi kusomwa na kueleweka pasipo kwanza kujua kilichojiri kwenye andiko lililotangulia ambalo ni Wagalatia 4:9 na aya nyinginezo. Desturi za kutenda dhambi au udhaifu na kuombaomba zilikuwa ni kawaida kwenye imani ya Wakostiki. Mafundisho ya kizushi ya Wakolosai yalitofautiana. Huko Galatia, walikuwa wanalinganisha mambo ya ulimwengu. Maandiko yaliyo kwenye Wagalatia hayana uhusiano wowote na mabishano au hoja zilizo kwenye Wakolosai 2:16 kuhusu ushikaji wa sikukuu na Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato.

 

Kwa maneno mengine, watu hawa walikuwa wanaamini elimu ya unajimu ili kujua la kufanya kwenye siku na nyakati za mwaka na zilituama kwenye ishara. Walikuwa wanarudi tena kuziamini ishara hizi. Hali hii iliwakumba waumini wa kanisa la Galatia. Pazia la Hekalu la Herode lilikuwa na ishara zilizoshonewa kwalo (kwa kujibu wa Josephus). Ushawishi wa imani ya Kinostiki kwenye Kanisa, umeelezewa kwenye majarida ya Uvegetariani na Biblia (Na. 183); Wanikolai (Na. 202); na majarida mengine mengi yanayoelezea Uungu, na pia jarida la Nafsi Hai (Na. 92).

 

Waefeso

Waefeso 3:15 inasema: "kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu." Kuna familia ngapi zilizoko Mbinguni? Unaweza kunijulisha na kunifafanulia?

Jibu: Mungu aliiweka familia tangu mwanzo na waliitwa wana wa Mungu (soma Ayubu 1:6 na 2:1) na hata Shetani alikuwa ni mwana wa Mungu na kerubi mwenye mabawa yafunikayo mtiwa mafuta.

 

Kwa kweli, Familia ni "ubaba". Huu ni mtazamo ambao kwao, Kristo anauitwa “Baba wa milele” kwenye Isaya 9:6. Soma jarida la Isaya 9:6 (Na. 224) kwa maelezo zaidi. Muundo wa Familia ya Mungu umeandikwa kwenye jarida la Jinsi Mungu Alivyofanyika Kuwa Familia (Na. 187). Jarida la Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229) itakuonyesha vyeo vya Kristo kutokana na matendo yaliyo kwenye mapenzi ya Mungu.

 

Wafilipi

Nimewasikia watu wakiitumia Wafilipi 2:10 “kuthibitisha” mtu anayepigamagoti “kanisani.” Je, andiko hili lina maana gani hasa?

Jibu: Wafilipi 2:10 ni ahadi inayohusiana na kumuinua Kristo kutokana na utii wake na kifo chake pale mtini. Hakupenda kujifanya kuwa sawa na Mungu bali alijifanya kuwa si kitu na akauchukua mwili na hali ya kibinadamu kama alivyoamriwa kufanya.

 

Kitendo cha kupiga magoti wakati wa kuomba maombi kilitokana na imani ya ibada za Baal-Easter, ambayo bado inafanyika. Kwa ajili hii, Mungu alijisazia watu wasiopiga goti kwa Baali. Katika siku za Eliya, kulikuwa na watu takriban 7000 wakati nabii Eliya alipokuwa anadhani kuwa yuko peke yake.

 

Andiko hili linaonyesha kuwa dini na imani yote ya ibada za Baali-Easter, ambayo inatuama kwenye imani hii ya unyenyekevu, italetwa kwa Kristo na kufanywa iwezekane kumjua yeye kuwa ni Bwana. Muundo wa uandishi umetuama kwenye neno “inama” kama “kampto” (Warumi 11:4 sawa na Isaya 45:23; Warumi 14:11).

 

Vitu vya kuinama kwa heshima: mbinguni (yaani jeshi la malaika, tazama Waefeso 3:10); vitu vya duniani (yaani vya kidunia kama kwenye 1Wakorintho 15:40); vitu vilivyo chini ya dunia (yaani wafu kwenye ufufuo wao, yaani aina zote mbili za Ufufuo (Ufunuo 20) sawa na Ufunuo 5:13 na malaika na mapepo (1Wakorintho 6:3 Luka 8:31; Ufunuo 9:11 na pia Zaburi 148.)

 

Badala ya kiumbe huyu kuongezewa unyenyekevu, kumeahidiwa kwamba yeyote atakayetenda hivyo na kutia uwezo wa Kishetani wa imani ya Baali-Easter ya waabudu jua na imani ya waabudu mungu mke, watafanyika watubie dhambi na matendo yao kwenye ufufuowa wafu.

 

Tazama majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Nafsi Hai (Na. 92); Hukumu ya Mapepo (Na. 80); na Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199). Suala la wajihi wa Kristo limeandikwa kwa kina kwenye majarida ya Sheria na Amri ya Kwanza (Na. 253);  Sheria na Amri ya Pili (Na.. 254); Sheria na Amri ya Tatu (Na. 255); na Amri Iliyokuu ya Kwanza (Na. 252). Tazama pia jarida la Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na. 243) na Stadi wa Uumbaji wa Mungu Kama Alfa na Omega (Na. 229).

 

Wakolosai

Nadhani kuwa Wakolosai 2.14 imeweka hatua ya somo kwenye aya zinazofuatia … akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani. Kwenye Wakolosai 2.13 Paulo anaongelea kuhusu ubatizo badala ya tohara. Kisha kwenye 1Wakorintho 5:7… ‘Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya’. Wakolosai 2.16 ‘Basi, mtu asiwahukumu ninyi….’ Haipasi watu kunihukumu na wala Kristo hakufanya hivyo. Kwa hiyo, hakuna mtu anayestahili kunihumu mimi kwa kile ninachokula au ninachokunywa, au kwa ajili ya Siku Takatifu ninazozichagua kuziadhimisha. Namaanisha kwa kweli, zile zinazomfanya mtu kama Mkristo hata hivyo?

Jibu: Kinachoelezewa kuwa kiligongomelewa pale mtini kwenye Wakolosai 2:14 klikuwa ni “cheirographon” au hati ya mashitaka unayopewa wakati unapokwenda mkahawani na kupewa bili ya chakula ulichokula. Aligongomelea hiyo bili ya madeni yetu tuliyokosa kwa mujibu wa sheria kwenye mti huu wa mateso, akatulipia kikamilifu madeni ya dhambi zetu mara moja kwa wakati wote.

 

Siku Takatifu hazikufutwa kama tunavyoona kwenye maisha ya imani ya Wanafunzi kwenye kitabu cha Matendo. Matendo 20:6 inaonyesha kuwa waliishika sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. baads that thy a Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu waliabiri kutoka Filipi. Kwa hiyo tunaona kwamba Paulo na Kanisa la Filipi walizishika Sikukuu. Wkolosai 2:16 inaonyesha kuwa Wakolosai walizishika pia. Matendo 20:7 inasema kuwa baada ya Sya Sabato au “mia ton Sabbaton” ambayo kwa maana nyingine ni “Sabato ya Kwanza kati ya nyingi nyinginezo” na Bullinger anasema hii kuwa ni Sabato kamili ya Kwanza ya Hesabu ya kuelekea idi ya majuma, na sio Jumapili. Kwa hiyo tunaona pia kuwa waliishika Pentekoste, ambayo tunathibitisha kuwa waliishika kutokana na inavyosema Matendo 2:1. Usemi wa kwamba Hata ilipotimia siku ya Pentekoste,” kunamaanisha kuwa walikuwa wanazishika Sabato iliyotangulia pia kama sehemu ya sikukuu hizi mbili. Tunajua kuwa waliishika Siku ya Upatanisho na Sikukuu zingine zote za Mwezi wa Saba, kutokana na andiko la Matendo 27:9, linaloonyesha ukweli kuhusu Siku ya Upatanisho.

 

Kwa hiyo, unasema, licha ya sisi kupewa Kalenda na Yesu Kristo, aliye mwombezi na mtetezi wetu kwa Mungu, na licha ya kwamba yeye pamoja na Kanisa la Agano Jipya kuwa lilishika; na licha ya Kanisa kuwa liliteswa kipindi chote cha historia kwa sababu ya kuzishika sikukuu hizi; bali wewe bado utaamua kutozishika idi hizo, na wala hutozishika Sheria za Mungu na wala hutawafundisha watu kuzishika. Kwa kweli, Kristo aliweka wazi kabisa kwa kinachotokea na kuwapata watu wanaofanya hivyo. Watahesabiwa kuwa si kitu kwenye ufalme wa Mungu.

 

Je, Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kwa kuwa hakuna namna au jinsi ya mimi kuzishika sheria, hivyo basi, iwapo kama namwamini yeye yanipasaje kuzishika sheria? Kwani hakuzishika kwa ajili yangu na kwa ajili ya mwingine yeyote amwaminiye?

Jibu: Hiyo ni ngano au hadithi ambayo waantinomia au wasiopenda kuzishika amri wangependa uamini hivyo. Hilo ni fumbo kubwa na hadithi dunia zinazosema kuwa sheria zimegongomelewa msalabani wanavyotumia kuitafsiri vibaya Wakolosai 2:14. Kilichogongomelewa pale mtini ni Chierographon, ambayo ilikuwa ni hati ya mashitaka chini ya sheria ambayo Kristo alitulipia na kwa njia ya neema tunaweza kuishi kwa Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu.

 

Hakuna nukta wala kijoti chochote cha torati kitakachoondoka hadi mbingu na nchi itapita. Bado iko na inadumu na itakuwa hivyo kwa kipindi kingine cha miaka mia elfu moja na moja na ishirini na saba angalau, kama tulijuavyo neno la Mungu.

 

Wateule na watakatifu ni “wale wazishikao amri za Mungu na ushuhuda (au imani) ya Wateule na watakatifu ni “wale wazishikao amri za Mungu na ushuhuda (au imani) ya Yesu Kristo" na ndiyo maana Yule joka anatukasirikia na anataka kutuangamiza (Ufunuo 12:17; 14:12). Mlolongo wa majarida yafundishayo Torati yatakuhekimisha zaidi. Soma jarida la Sheria za Mungu (Na. L1) na majarida mengine yote yanayofuatana nalo yaliyoandikwa na yanapatikana.

 

Wakolosai 2:16: inasema ‘Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika… Siku; lakini Mwili ni wa Kristo.’ Na Sabato zetu naongezea; ni vigumu sana kuyapuuzia mafundisho afundishayo mtu?

Jibu: Wakolosai 2:16 inaonyesha kuwa Kanisa lilikuwa linazishika Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Siku Takatifu. Usemi wake wa kwamba basi mtu na asiwahukumu unaonyesha kumaanisha kuwa unazishika basi. Kitabu cha Matendo kinaonyesha wazi kuwa Kanisa lote lilikuwa linazishika sikukuu na Sabato na hata Miandamo ya Mwezi Mpya. Tumekuwa tukzishika na kuadhimisha kwa kipindi cha zaidi ya miaka 1,971. Waliishika Pentekoste, hinginevyo wasingeweza kumpokea Roho Mtakatifu (Matendo 2:1). Injili imejaa maandiko yanayotaja ushikaji wa sikukuu uliofanywa na Kristo na mitume wake. Hakuna hata andiko moja linalosema kuwa waliacha kuzishika–hakuna hata moja. Mtume Paulo alizishika nah ii inaweza kutafsiriwa kutoka kwenye maandiko yake mwenyewe (Matendo 12:3; 20:6). 1Wakorintho 5:7-8 inaelezea jinsi tunavyotakiwa kuishika Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.

 

Kanisa lilishika na kuiadhimisha Siku ya Upatanisho (Matendo 27:9). Huwezi kuuelewa mpango wa Mungu pasipo kuzijua Siku Takatifu za Mungu. Kristo alikuwa ni Pasaka na Mganda wa Kutikiswa. Alituamuru tuadhimishe ushirika wa Meza ya Bwana jioni ya siku aliyosalitiwa, ambayo ni siku ya 14 Abibu.

 

Hakuna mahali popote hata pamoja panapotaja kuwa Sabatp ilibadilishwa, au panapoliambia Kanisa lisizishike Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa ikiwepo Wakolosai 2:16. Mtume Paulo anafanya masahihisho ya sadaka kwenye Siku ya Kwanza ya juma kwa kuwa ingeweza kufanywa siku ya Sabato. Hapa ndipo mahala pekee panapoonekana waliusanyika siku ya kwanza ya juma. Hata siku zenyewe zimeitwa kuwa “Siku ya Kwanza ya juma” kwa kweli inamaanisha “Sabato ya kwanza” kwa Kiyunani.

 

Tafadhali kinachosemwa kwenye Wakolosai 2:18 kuhusu kitendo cha kuwaabudu malaika?

Jibu: Neno “kuabudu” linamaanisha “dini” kwenye Matendo 26:5 na linajitokeza tu kwenye maeneo haya mawili tu. Ili kuelewa mafundisho ya kizushi yaliyokuwa huko Galatia na Kolosai, mtu anahitaji kujua au kuielewa dhana ya kidini kuhusu siku. Nadharia hizi zimeeleweshwa kwa kina kwenye jarida la Mafundisho ya Kizushi Kwenye Kanisa la Mitume (Na. 89). Upangiliaji wa utaratibu wa muda mrefu na mambo yanayoonekana kuwa ni sehemu yake. Maneno na maana zake yapo kwenye maandiko yanayotajwa. Mumbe hastahili kuabudiwa. Mtindo huu wa kuwaabudu malaika umeingia kwenye Ukristo kwa kupitia mtindo au mbinu nyingine na watu hawafikirii kuabudu kitu kingine zaidi kuliko ibada hizi za kuwaabudu malaika na watakatifu.

 

Je, unaweza kufafanua tafadhali kuhusu hii siri ya Kristo inayotajwa kwenye Wakolosai 4:3?

Jibu: Siri ya Kristo iliyotajwa hapa ni ukombozi kwa Wamataifa na kufanyika kuwa wana wa Mungu. Wale wasiokuwemo wanajumuisha moja kwa moja kwenye mchakato wa kununuliwa nje ya harakati za kanisa linalotenda kazi likitumikia siri za Kristo. Maandiko haya yanapatikana kwenye waraka kwa Wagalatia. wagalatia 3 inaonyesha kwamba kwa kupitia Ibrahimu mataifa yote yatabarikiwa na wamataifa wanahesabiwa haki kwa njia ya imani na Maandiko yanasema kwamba wale walio na imani ndiyo wana wa Ibrahimu (Wagalatia. 3:6-7).

 

Roho alimhubiria injili Ibrahimu akisema kwa yeye mataifa yote watabarikiwa (Wagalatia 3:8-9). Mtume Paulo anaichukulia “ergon nomou” au Miqsat Ma'ase ha Torah (MMT) (soma jarida la Maandiko ya Matendo ya Sheria - au MMT (Na. 104)). Anawakumbushia andiko hili Wagalatia kuhusu suala la laana ya torati. Hakuna anayehesabiwa haki kwa sheria, kama mwenyehaki anavyoishi kwa imani (Wagalatia 3: 11-12; Habakuki 2:4; sawa na Warumi 1:17; Waebrania 10:38).

 

Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti (Wagalatia 3:13; sawa na Kumukumbu la Torati 21:23). Hii ilifantika ili kwamba Baraka za Ibrahimu ziwafikie Wamataifa kwa njia ya Yesu Kristo na ili tumpokee Roho Mtakatifu kwa imani (Wagalatia 3:14).

 

Mtume Paulo anaiendeleza hoja hii ili kukabiliana na mafundisho ya kizushi huko Galatia na pia Kolosai. Soma jarida la Mafundisho ya Kizushi Kwenye Kanisa la Mitume (Na. 89). Kwenye Wagalatia 4:3 anaelezea kuhusu utumwa wetu tulionao kwa mambo ya dunia. Anashughulikia mafundisho ya kizushi yaliyojipenyeza huko Galatia. Anasema kuwa “Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.” (Wagalatia 4:4-6).

 

Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. (Wagalatia 4:7). Kwenye Waefeso 5:14 Paulo anaiainisha kwa kuifafanua Isaya 60:1-2 na anaongelea kuhusu nuru ilitolewa na Kristo kwa kuwaamsha wale waliokufa. Anatumia maneno hayohayo yaliyo kwenye Waefeso 5:16 kuhusu kuukomboa wakati kama tunavyoona kwenye Wagalatia 3:13 na Wakolosai 4:5. Akituonya tuenende kwa hekima kwa walio nje, na tukiukomboa wakati kwa kuwa ni nyakati za uovu.

 

Anaongelea pia kuhusu umuhimu wa kushukuru kwa kila jambo na kunyenyekeana na tukimcha Mungu. Kwa hiyo, siri ya Kristo ni ukombozi kwa Mataifa kama wana wa Ibrahimu kwa njia ya imani kwa Kanisa, na uwana wa Mungu kwa kupitia Kristo ambako ndiko kuvunjwa kwa laana ya torati lakni ni kuwezesha kuanzishwa kwa vitu vyote kwa imani.

 

Yatupasa tuenende kwa busara kwa njia ya imani tukishukuru kwa kila jambo na kunyenyekeana kwa imani tukimcha Mungu. Kwa namna hiyo, kwa njia ya siri za Kristo, tunafania kuwa wana wa Mungu aliyehai. Kwa kuwa imeandikwa: “Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu...” na maandiko hayawezi kutanguka (Zaburi 82:6; Yohaa. 10:34-35).

 

II Wathesalonike

Kutokana na hali ya mtawangiko wa Kanisa, unayaonaje Maandiko Matakatifu yaliyo kwenye IIWathessalonike 2:3-4, 6 kuhusu huyu mtu wa kuasi “aketiye juu ya Hekalu la Mungu?” kwenye aya ya 6 ni kitu gani hasa anachoambiwa kuwa “akijifanya yeye mwenyewe?”

Jibu: Ukengeufu Mkuu umekwishatokea kwa karne nyingi sana zilizopoita. Ulianzia huko Roma na ukaendelea kuenea kwenye Makanisa yote ya Kikristo tangia karne ya 4. Ukengeufu huu unaoendana na kuiasi kweli umezidi kuendelea na kudumu. Matokeo yake yakawa ni kutangazwa kwa amri ya kuwatesa watu wa Mungu waliokuwa wanajaribu kuitii Torati ya Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa.

 

Nyakaati za mwisho zimetolewa rasmi kwenye dini na imani ya uwongo, mfumo utakaopelekea kuwakomesheleambali Watakatifu wake Yeye Aliye juu. Ili kutimiliza hilo, karne iliyopita walimtangaza Papa kuwa ni Mwakilishi au Mbadala (Vicar) wa Kristo na Mungu hapa duniani. Yeye akiwa kama kiongozi wa dini na imani hii na mchakato huu unaomtoa huyu mtu wa kuasi na mwana wa uharibifu, tunatarajia kuwa ukengeufu ni budi uendelee na kuchukua mahali pake na kuwa ni mwisho wa zama ya Washika Sabato, ambapo watakomeshelewa mbali na kukomesha nguvu yao.

 

Hii imeshuhudiwa kufanyika kwenye miongo mitatu ya mwisho iliyopita kwa tukio lililojitokeza la Kanisa lote zima la Mungu na matawi yake madogomadogo kujikuta wanakuwa mawakala na watetezi wazuri wa imani zenye nasaba ya kipagani za Utatu na Ubinitariani zilizo kwenye mchako wa kumuabudu Mungu wa Utati. Ni Makanisa na vikundi vichache sana vilivyobakia vikiendelea kushikilia kwenye mafundisho asilia ya Kanisa lililoanzishwa na Mitume. Ni machache sana pia yanayoendelea kuzishika na kuzifundisha Sheria au Totati yake Mungu na kumfuata Kristo kwa kumchukulia kama Malaika Mkuu wa Agano la Kale aliyempa Torati nabii Musa, kama ilivyokuwa ikifundishwa kwenye Makanisa ya kipindi cha karne ya kwanza nay a pili.

 

Mtume Paulo anasema kwenye aya ya 7: “Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi”. Mungu anaiachia hali hii itokee “hata atakapoondolewa.” Kuna aliyekuwako wakati huo na aliruhusiwa aendelee hadi mwisho na “ili aondolewe?” Jibu lake laweza kuwa ni mmoja tu, ambaye ni mshitaki na adui Shetani. Siri ya kuasi ni mkakati mkuu wa imani hii na hivyo kwamba kwa njia ya Dini potofu za Imani Siri na fumbo, Shetani hutenda kazi ya ukengeufu na kuwadanganya ikiwezekana hata wateule.

 

Kwa hiyo, Shetani ndiye huyu anayeketi kwenye Hekalu la Mungu akijifanya yeye mwenyewe kuwa ni “Mungu,” na kina mtumishi anayemfuata na kufundisha mafundisho ya kuadhimisha sikukuu ya kipagani ya Easter ni “mtu wa kuasi” ambaye ni mwakilishi wa Shetani ulimwenguni akiwa ni sehemu ya imani ya waabudu Jua. Ni watu wachache tu ndiyo watakaomudu kubaki Kanisani katika siku za mwisho, wakimudu kufanya kazi na kueneza kwa kuyagawa machapisho mbalimbali yenye mafundisho yenye uzima na injili ya Ufalme wa Mungu.

 

Wakati wa mchakato huu, ndipo marejesho mapya yatafanyika na kuongoka kwa watu wa Yuda na wito wa watu waende Yerusalemu utaanza. Hadi wakati huo, itatupasa kujaribiwa kama kwenye moto. Soma majarida ya Kuitwa Kwa Watu Kwenda Yerusalemu (Na. 238); Ujumbe wa Ufunuo 14 (Na. 270). Kuna mambo mawili ambayo yanauathiri pia mchakato huu nayo yameainishwa kwenye majarida ya: Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44) na Jeshi la Gideoni na Siku za Mwisho (Na. 22).

 

1Timotheo

Andiko la 1Timotheo 4:1-3 linamaanisha nini linapoongelea kuhusu mafundisho ya mashetani?

Jibu: mafundisho ya Mashetani yalichukuliwa kama Unostiki wakati ule wa kanisa la kwanza. Walifundisha uasetiki au maisha ya kujienga na anasa na useja. Mafundisho haya yameaishwa kwenye majarida ya Uvegetariani na Biblia (Na. 183); Wanikolai (Na. 202); Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188); Nafsi Hai (Na. 92) na Mafundisho ya Mashetani ya Siku za Mwisho (Na. 48).

 

Waebrania

Napenda kuelewa vizuri zaidi maana ya andiko la Waebrania 7:3 lisemalo “hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake.” Mfalme huyu wa Salemu kwa hakika anaonekana Mfalme wangu wa Yerusalemu!

Jibu: Ukuhani wa Melkizedeki ni ukuhani mpya na wa tofauti kwenye Kanisa uliojiri baada ya ule wa Melkizedeki, uliohudumu tangu kipindi cha gharika kuu. Umefunuliwa kwa Wamataifa na hivyo kwamba wanawekwa wakati wanapoongoka na hivyo kuwafanya wawe washiriki/ “sanaa” na “ustadi” au “asiye na baba” wala “mama.” Hivyo basi, si mrengo wa uzao wa kiumeni wala wa kikeni.

 

Mwanzo wake wa siku na mwisho wa miaka ulikuwa unahitajika kwa kuhani. Sharti la kuingia Hekaluni na kuanza kuhudumu akiwa na umri wa miaka 25 na kuacha kuhudumu akiwa na umri wa miaka 50 ilikuwa ni sheria ya makuhani wa uzao wa Haruni, na kufundisha tangu umri wa miaka 30 na kuendelea hadi kipindi cha kushindwa kuendelea kuhudumu Hekaluni kwa kawaida kilikuwa ni umri wa miaka 65-70 au zaidi kidogo ya hapo. Hata hivyo, hakuna kuhani aliyehudumu Hekaluni baaba ya umri wa miaka 50.

 

Ukuhani wa Melkizedeki ni tofauti na, isitoshe unawaweza kuwajumuisha wana wa Haruni pamoja na Wamataifa. Ndiyo maana Ibrahimu alimwendea Melkizedeki huko Yerusalemu. Huu ulikuwa ni mji wa Wayebusi na ulikuwa ni wa Wamataifa. Kwa hiyo, Melkizedeki alikuwa na makuhani Wamataifa kwenye huduma yake. Tazama jarida la Melkizedeki (Na. 128) for more information.

 

Yakobo

Unaweza kunifafanulia tafadhali chanzo na maana ya waraka wa Yakobo.

Jibu: Mwandishi alikuwa yakobo, ndugu wa kimwili na Yesu Kristo na Mwenekiti wa Baraza la Mitume. Hoja na malumbano kuhusu uandishi kuondoa kwa Luther kwa Waraka (“wa”) ni kwa sababu ya ukali wa itikadi ya maadui wa Usemitiki na kutangazwa kwa Sheria au Torati kuwa ni Sheria Kamilifu ya Uhuru.

 

Wote hujaribu kuiondoa wanaposhikilia imani ya wapinga sheria za torati au uantinomia na wapinga Usemitiki. Fundisho hili linafuatilia kwa ukaribu sana sauti au mdundo wa kimafundisho wa Hotuba au Mafundisho ya Mlimani. Yakobo alikuwa ni ndugu yake Bwana (Wagalatia 1:19), na ni mmoja wa nguzo muhimu kama inavyosema Wagalatia 2:9. Alikuwa mwenyekiti na alitoa maamuzi kwenye Baraza ka Mitume (kama ilivyo kwenye Matendo 15:13,19).

 

Wayahudi walikuwa bado wanakusanyika kwa ibada zao kwenye masinagogi (2:2). “Maskini” (sawa na Yohana 12:8) walikuwa warithi wa ufalme (kama kwenye 2:5). Walithibitika kwa mujibu wa Torati na kumfanya Ibrahimu kama baba yao (2:8 ff., 21). Iuatiwa na Matendo 3:19-21, kuhusu ujio au “parousia” ya Bwana ambao ulikuwa imekaribia (5:7,8).

 

Umewalenga makabila kumi na mbili yaliyokuwa kwenye utawanyko. Unadhaniwa sana kuwa uliandikwa kutoka Yerusalemu si muda mrefu baada ya yaliyofanyika kwenye kitabu cha Matendo, na huenda hata kabla ya kipindi cha Matendo ya Mitume. Yawezekana sana kuwa ni mapema kabla ya kuuawa kwake mtume Yakobo mwaka 63 KK, ambako kumeainishwa kwenye jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Tena wa Hekalu (Na. 13).

 

Tunaweza kuona kwamba matokeo ya ujumbe huu yananguvu sana kuhusiana na mambo yahusuyo imani na matendo. Ni sawa tu na leo kama watu wanavyokuja kujikuta wakiangukia kwenye ulaghai wa Uantinomia wa Kiprotestant na kujikuta wamekamatwa na mapokeo ya Ukatoliki wa Kirumi, na kuanzia hapo tena kuangalia kwa kumaanisha Sheria za Mungu.

 

Yakobo 1:17: “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka..”

 

Ni kwa namna au jinsi gani inaposema kuwa wote wenye mwili wataokolewa kwenye Maandiko kadhaa tofauti tofauti yanasema kwamba wazinzi, wauaji na waabudu sanamu hawataurithi ufalme wa Mungu?

Jibu: Kwenye ufufuo wa pili wa wafu, watu wote watahukumiwa na watatubu. Hakutakuwa na kuoa wala kuolewa kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Watakatifu wafanyao hivyo kwenye ufufuo wa kwanza watakuwa hawajafanya hivyo, vinginevyo itawapasa watubu na kuacha kufanya hivyo.

 

Watu wote wengine watakuwa kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Huko watakuwa wamepewa kuelewa na kutubu au toba. Tazama majarida ya: Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Hukumu ya Mapepo (Na. 80).

 

1Yohana

Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. (1Yohana 5:7) andiko hili lina maana gani?  

Jibu: Unanukuu maandiko yaliyokosewa na yanayopotosha kwenye 1Yohana 5:7 kwenye Receptus yaliyoingizwa kwenye tafsiri ya KJV. Hayapo kwenye Biblia yoyote nyingine. Ni mwingizo wa andiko la 1Yohana ili kutafuta msaada mwingine wa kbiblia kuhalalisha fundisho la Utatu. Waprotestanti wanadai kuwa misingi ya “Sola Scriptura” au kuamini “Maandiko Peke yake” na hivyo ukosefu au kutokuwepo kwa Utatu kwenye Biblia kulipasa kuwe na hali ya unafuu kiuhalalisho na Biblia na mapokeo ya kimaandiko.

 

Kwenye teolojia ya Kanisa Katoliki ijulikanayo kama C. M. LaCugna (Mungu Kwa Ajili Yetu) inafafanua jinsi imani hii ya Utatu wa Mungu ilivyoingizwa kwenye teolojia ya kanisa tangu kwenye vikao vya Mabaraza ya Karne ya Nne huko Constantinople mwaka 381. Augustine ndipo alipoutafakari uhusiano kwa kiwango cha mwingiliano wa kimungu. Kanisa Katoliki la Roma linategemea maamuzi yanayotokana na vikao vya Mabaraza ya kanisa nah ii haihitaji kuingizwa mambo ya kughushi yaliyoingizwa kwenye Receptus ili kukithi haja ya kaulimbiu yao ya Sola Scriptura. Mchakato huu umeainishwa kwenye jarida la Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127).

 

Ufunuo

Najua kwamba kitabu cha Ufunuo alipewa Mtakatifu Yohana Ufunuo, lakini huyu alikuwa ni nani hasa kwa kweli?

Jibu: Kitabu cha Ufunuo ni Ufunuo hasa wa Mungu aliopewa Yesu Kristo. Yohana anasema kwamba aliuandika alipokuwa Patmo ukimbizini. Kristo alimpa alipoupokea kutoka kwa Mungu. Hili ni jambo la muhimu sana kuhusiana na suala la tabia ya Kujua kila jambo ya Mungu na utayari wa kujidhihirisha wa Mungu Baba yetu.

 

Inaonekana kuwa Yohana alikuwa ametupwa au kufungwa mwaka wa 96 wa kuinuka kwa mtawala au mfalme mpya. Eusebius anasema kuwa Yohana alirudi Efeso na kuishi hadi kipindi cha Trajan (H. E. III, 18.1; 20:9; 23:4). Appollonius anasema alimfufua mfu huko Efeso (Eusebius V, 18, 14).

 

Clement wa Alexandria anaeleza jinsi alivyomshuhudia na kumuongoa mnyang’anyi na kumleta kwa Kristo (Ni tajiri gani anayewezao ya kizushi Kuokolewa? 42). Irenaeus anaeleza jinsi alivyopingana na mafundisho ya kizushi ya Cerinthus (Her. III, 3, 4). Inasemekana kuwa alichukuliwa au kubebwa alipokuwa mzee, alirudia tena na tena kuwasihi watu akiwaambia kuwa: “Watoto wagodo pendaneni!”

 

Irenaeus alikuwa mwanafunzi wa moja kwa moja wa Polycarp na Papius, na walimpa taarifa za moja kwa moja akiwepo na kazi za Yohana huko Efeso na dini yake. Eusebius anasema kuwa Papius anasema kuwa yeye mwenyewe hakuwashuhudia mitume hawa kwa macho yake, bali alipata taarifa zao kutoka kwa marafiki zao (III, 39, 2). Kwa hiyo, Irenaeus alifundishwa na watu hawa pamoja na Polycarp akimpa habari za mkono wa kwanza za wanafunzi wengine. Hakuna mgongano kwenye taarifa hizi za Irenaeus.

 

Tertullian anasema kuwa Yohana alikwenda Roma na “alishindikana kuungua kwenye mafuta yaliyochemshwa moto na ndipo alihamishiwa Kisiwani.” (Patmo) (sawa na Kitabu cha Her, 36). Polycrates wa Efeso anasema kuwa Yohana alikuwa ni “kasisi alyekuwa anavaa joho lenye kimduara kama cha sahani” (Eusebius, Hist. V, 24, 3; cf. Interp. Dictionary of the Bible, John the Apostle, vol. 2, p. 954). Hii ilimfanya kuonekana kuwa Yohana ni mwana wa Lawi na ni Mkoheni.

 

Masalia yajulikanayo kama Muratorian Fragment (II, 9-23) yalisema kwamba Yohana alikuwa na mitume wengine waliobakia wakati Yohana alipopewa kuandika injili yake. Hii inamaanisha kwamba ilikuwa ni mapema sana kabla ya kuuawa kina Yakobo wa wenzake (yapata mwaka 63 BK) na huenda huko Palestina. Huenda ilikuwa hata kwenye Baraza la Mitume.

 

Desturi iliyotumiwa kujaribu kumuua Yohana inatikana na maandiko ya George Mdhambi (kwenye karne ya tisa) na nakala ya kwenye karne ya nane ya Historia ya Matukio ya kwenye karne ya tano yaliyoandikwa na Philip wa Side (Interp Dict. ibid). Hata hivyo, hii ni kinyume na jopo la mashahidi wengi wa zama za kwanza na Biblia inaashiria hakupasa kuuawa. Yohana aliandika vitabu vitano (Injili ya Yohana, Waaraka wa 1 hadi 3 wa Yohana na Ufunuo wa Yohana) kama zilivyo kwene mapokeo na desturi zilizokubaliwa.

 

Ignatius hamtaji yeye huko Efeso kama ilivyo kutokana na maandiko yake, kuna upotoshaji kiimani huko Roma kutoka kwenye teolojia ya kwanza ya mitume uliotuama na kumtafsiri vibaya Mtume Paulo. he Paulo. Hii ilikuwa ni kupotosha na hatimaye kuliharibu kabisa kanisa kwa ukengeufu.

 

Eusebius anashikilia kuamini kwamba Injili ya Yohana ni ya kwanza ingawaje zinaonekana kuwepo na zingine. Wanasema kuwa iliandikwa baada ya vitabu hivi vingine vitatu, na inasahihisha makosa ya kuruka ruka yaliyokuwa kwenye hizi tatu nyingine kuhusu miaka ya kwanza ya huduma ya Masihi. Ni Mathayo tu na Yohana ndio walikuw mitume wa mwanzoni.

 

Ni kwa nini basi asili ya kibinadamu INATAKA kuamini kuwa tunaongoza migogoro iliyoko ulimwenguni kote? Ni kwa nini kuna watu hapa duniani wanaonekana KUPENDA kuamini kuwa uovu utakuja kushindwa na kusababisha matatizo na jehanamu, kwa ujumla na kwa moja kwa moja? Kuna mtu alielezea ukweli kwamba kitabu cha Ufunuo kiliandikwa kwa lengo la kumpinga kisiasa ya Nero na ukweli huo unabaki kuwa ujuzi uliojikita mawazoni. Kwa nini wengine bado wanataka kuamini kuwa ni unabii?

Jibu: Wazo la kwamba kitabu cha Ufunuo kiliandikwa u wanaojaribu kuupotosha ujumbe ulio kwenye kitabu hiki cha Ufunuo. Kwa kweli sio sahihi kabisa kama wanavyodai wengine. Yohana mwenyewe anasema kuwa alikiandika wakati akipokuwa kifungoni kwenye Kisiwa cha Patmo. Alifungwa huko mnamo mwaka 95 BK na alirudi kipindi cha utawala mwingine wa mfalme mwingine Nerva mwaka 96 BK.

 

Kanisa Lote zima lilikubali kuhusu kuinuka kwa utawala huo kuwa ni kweli. Nero alikuwa akwishakufa kwa miongo kadhaa. Harakati zilizo kwenye Ufunuo zinaelezea kinagaubaga utawala wa Kristo na watakatifu wake utakaodumu kwa kipindi cha miaka elfu moja. Kudai kwamba huu si unabii ni utotofu tu.

 

Mtu anaweza kujiuliza kwamba huenda si kitabu chenye unabii uliovuviwa au la, kama walivyofanya wengine. Hata hivyo, kudai kuwa hiki sio kitabu cha unabii inamaana kwamba mtu kama huyo hajayaisoma maandiko au anajaribu tu kuyaondoa idadi kubwa ya mahudhui yaliyomo ndani yake. Historia ya mahali pake kwenye kanoni imeainishwa kwenye jarida la Biblia (Na. 164). Unabii wake mwingi umekwisha timilika na dondoo zake. Sehemu kubwa nyingine ya unabii wake haijatimia. Kwa kweli andiko hili linahusu mambo yatakavyokuwa atakaporudi Masihi na kwamba jambo hilo halijatimia bado. Madai ya kwamba kinachukuliwa kama unabii na watu wanaoonekana kutaka kuona migogoro ikienea ulimwenguni kote hayafai kabisa.

 

Uandishi wenyewe unaelezea dhamira isiyotafsirika ya ulimwengu kwa zaidi ya kipindi kizima cha kuangamia kwake kabisa. Kazi hii ni ya muhimu kiunabii ya Biblia na ambayo haijafunuliwa bado kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu mbili. Kunakaribia sana tutajionea jinsi kazi ilivyo ya kweli. Ni Ufunuo ambao Mungu alimpa Yesu Kristo ambaye naye aliamini kuwapa watumishi wake kupitia kwa Yohana. Hakuna kiongozi wa Kanisa la Mungu kwenye karne ya pili aliyekichukulia kitabu hiki kama ni cha habari za kihistoria tu, na hakuna kiongozi wa Kanisa hata aliyejaribu kudai kudhania hivyo. Na wala hakuna aliyediriki kudai kuwa kilikuwa ni waraka kwa Nero. Katika miaka kumi ya mateso ya Kanisa kati ya miaka ya 303 na 313 ilijulikana wazi sana kwamba waraka kwa Wasymirna ulikuwa na maana.

 

Mungu anasema: “Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.” Na hivyo ilivyoandikwa ndivyo itakavyokuwa.

 

Nimesoma kwenye Ufunuo kuhusu roho saba za Mungu. Kutokana na hizo nadhania kwamba pamoja na Mungu Mwenyezi, kwa sasa kunaweza kuwa na washirika sita wengine kwenye baraza la elohim wanaoweza kuwa na vyeo va chini zaidi ya Mwenyezi Mungu. Je, hii ni sahihi? (Ufunuo 1:4; 5:6)

Jibu: Roho saba za Mungu zimetajwa kwenye Ufunuo 1:4 na Ufunuo 5:6. Mtu anaweza kudhania kwamba kuna viumbe saba kutokana na isemavyo Ufunuo 1:4, lakini andio la kwenye 5:6 linaonyesha kuwa Mwanakondoo ana pembe saba na roho saba za Mungu. Kwa hiyo hizi ni alama au ishara za uweza na tabia ya Mungu.

 

Yapasa kuwe na misingi imara ya Roho Mtakatifu, inayofanya fursa ya kuonyesha uweza wa kujua kila jambo kwa mpokeaji, kwa kadiri anavyotenda kwenye Mapenzi ya Mungu kwa maongozi ya Roho Mtakatifu. Yapasaa kuwe na matendo ya Roho Mtakatifu kwenye mnyumbuisho wa kazi ya Mungu hadi kwa jeshi la elohim.

 

Unaweza kuelezea hii “mana iliyofichwa” ni nini na ni lini tutakapoyapokea majina mapya? (Ufunuo 2:17)

Jibu: Israeli walilishwa hii mana kwa kipindi cha miaka arobaini jangwani, ambayo iliitwa ni chakula cha malaika. Neno Mana maana yake ni “ni kitu gani hiki?” Neno hili lenyewe tu lilikuwa na maana yake fulani kama nieuwakilisho wa kitu fulani kilichokuwa hakijajulikana kwa Waisraeli wakati wa tukio lao la Kutoka.

 

“Mana liyofichwa” ilimaanisha Roho Mtakatifu, ambaye alikuwa ni kifaa muhimu ambaye kwaye tulifanyika kuwa wana wa Mungu na elohim. Walipewa wale wanaoshinda tu, peke yao. Tulipewa malipo ya awali kwa tulipobatizwa, na tunapokea uweza kamili wa Roho Mtakatifu kama wana wa Mungu wenye nguvu tutakapofufuka kwenye ufufuo wa wafu (Warumi1:4).

 

Kanisa lilipewa yubile arobaini kuwa kwenye jangwa la Kutoka. Lilikuwa ni jangwa la dhambi na walilishwa mana walipokuwa wanatangatanga jangwani.

 

Jiwe jeupe lenye jina jipya linaashiria mambo mawili. Mawe meupe yalitumiwa pia kwenye ujenzi wa Hekalu kutoka kwenye misingi wyake. Jina lililoandikwa kwenye jiwe linamaanisha uwenyewe kwenye Mji wa Mungu.

 

Hivyo basi misingi ya ujenzi ni wale walioshinda wanaotokea kwenye makanisa hayo saba. Watapokea uraia wao na watafanyika kuwa sehemu ya Hekalu la Mungu. Wataipokea mana kutokana na ubatizo wao na kisha kwa uweza kwa kufufuka kwao toka kwa wafu na wenyeji wao kamili kwenye Mji wa Mungu mwishoni mwa Ufufuo wa Pili wa wafu baada ya kazi zao kufanika kwa kipindi chote cha utawala wa milenia wa Kristo.

Soma majarida ya: Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Hukumu ya Mapepo (Na. 80); Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95); Mji wa Mungu (Na. 180); na Siku ya Bwana na Nyakati za Mwisho (Na. 192).

 

Je, jiwe jipya na jina jipya vina maana gani?

Jibu: Jiwe kama alama ya jina kwa maana ya wenyeji au uraia kwenye ulimwengu wa kale. Lilitumika kutia alama raia na liliashiria msimamo wao. Bullinger anasema kuwa jiwe jeupe lilikulikana siku za kale kama jiwe la “ushindi” (lisemwalo kwenye Ufunuo 2:17). Mwendelezo wa kutenganisha ulikuwa ni kwa kuweka chapa nyingi sana nyeusi dhini ya jina lililoorodheshwa. Alama nyingi sana nyeusi na zilimaanisha utumwa. Majina ya watu yote yana msingi wa miungu ya kipagani na ni vigumu kuyakwepa kwene jamii zetu. Wakati atakapokuja Masihi dunia itapewa lugha mpya na nzuri na wateule watakuwa na majina mapya. Hii itatimiliza unabii wa Isaya 62:2 na penginepo. Mawe mapya pia yanaunda sehemu ya utaratibu wa ujezi wa Hekalu la Mungu.

 

Ni nani huyu mwanamke Yezebeli aliyetajwa kwenye Ufunuo 2:20.

Jibu: Yezebeli alikuwa binti wa Ethbaali aliyekuwa mfalme wa Sidoni iliyokuwa chini ya dola ya Watiro. Ethbaali alikuwa ndiye aliyemuua mfalme na mkatili (Josephus A. Apion 1.18; A of J viii. 3. 1). Ethbaali alikuwa kuhani wa mungu Astarte au Easter, mungumke wa dini ya Wafoinike. Jina lake maana yake ya moja kwa moja ni “aliye pamoja na Baali.”

 

Yezebeli (‘Iyzebel’ maana ya kihamasa) alikuwa kuhani mke wa Baali-Easter. Kwa hiyo dhana ya “adhabu” hapa ni kumweka wakfu mungumke. Hakuwa vinginevyo bali ni adhibu yenye utaratibu wa hekaluni. Israeli walikuwa kwenye ushirikiano au ushirika na dini za Watiro na Wafoenike kutokana na urafiki wao na Daudi na Hiramu. Imani na dini hii ya Easter ilijipenyeza katika Israeli kutoka kwa Wafoenike, na ilifikia kilele chake chini ya Yezebeli ambapo Sheria na Torati ya Mungu ilipuuzwa kabisa. Watu walijikita kwenye imani ya mungu Easter na kumuabudu Baali na maashera. Manabii wa Mungu walitishwa kwa dharau.

 

Easter ni sehemu ya imani ya zamani za kale ya ibada za mungu Baali na haitofautiani na imani za Siri na fumbo. Tazama pia kwenye jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222). Wafoinike waliichukulia hii ulimwenguni kote kwenye taratibu zao za kibiashara.

 

Kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu, Biblia inamashiko, lakini uelewa wetu unakikomo, na mapenzi halisi yatatupeleka mbali. Kristo anatuita tuishi kwa imani na kumuamini yeye na kupendana. Hakutuamuru kabisa kuyafanya Maandiko yote Matakatifu kuwa sawa. Kwa kweli, aliwakemea watu waliokuwa wanadini sana wanaojifunza Maandiko Matakatifu ya siku zake ya kutokuwa sahihi kwenye tafsiri zao.

 

Kwa upande mwingine, Mungu aliivuvia Biblia, inajumuisha kweli yote. Wale wanaomwamini watapenda kulielewa Neno lake, na kuyafuata mafundisho yake ili wawe wazuri iwezekanavyo. Yatupasa tu kujua ukomo wa uwezo wetu, haitupasi, kwa namna yoyote ile, kutazama chini tukwaangalia wale wasioonekana kuyaelewa Maandiko Matakatifu pamoja na yale tunayoyadbania kuwa tunayafanya. Hebu na tuishi kwa imani na tuonyeshe pendo kila mmoja wetu.

 

Liana maana gani neno hili la kwamba "Nitampa nyota ya asubuhi"? (Kwenye Ufunuo 2:28)

Jibu: Nyota ndogo ya Asubuhi ni daraj la cheo. Kulikuwapo na nyota wengi wa Asubuhi waliokuwepo wakati wa uumbaji wa Dunia kama tuonavyo kwenye Ayubu 38:4-7. Jina la Lusifeli linahusiana na cheo hiki. Neno ndogo linachukuliwa kuwa la mungu wa ulimwengu hu. Siku hizi Shetani ni Lusifeli na Nyota ya Asubuhi.

 

Huyu mdogo anaweza kuchukuliwa kutoka kwake na akapewa Kristo atakaporudi. Yeye kama mteule atapewa cheo cha kutawala na Kristo. Kwa maneno mengine, wateule watashirikishwa kwenye Utawala wa Mungu hapa duniani kipindi cha Milenia na hata baad ya hapo. Jambo hili limeainishwa kwa kina kwenye majarida ya: Lusifa: Mpeleka Nuru na Nyota ya Asubuhi (Na. 223); na Utawala wa Mungu (Na. 174). Pia soma jarida la Jinsi Mungu Alivyofanyika kuwa Familia (Na. 187).

 

Ni kiumbe gani basi anayetajwa kwenye Ufunuo 3:7 kuhusu ufunguo wa Daudi? Je, inahusiana na Isaya 22:22?

Jibu: Ndiyo, uko sahihi. Ufunguo wa mwongozo wa ufalme wa Israeli ulifikia kilele chake chini ya Daudi na kufikia upeo wake kamili. Tendo lenyewe lilikuwa pia ni kuingia kwenye maskani lilijumuishwa kwenye mamlaka haya ya mfalme.

 

Sulemani, kwa mujibu wa mapokeo ya Kiyahudi, alikuwa na unfunguo wa Hekalu. Soma kwenye jarida la Wimbo Uliobora (Na. 145). Andiko lililo kwenye Isaya 22:22 linaonyesha kuwa uweza wote wa kifalme alipewa Masihi. Andiko lililo kwenye Ufunuo linaonyesha kuwa alikuwa na uweza huu na alitumia mamlaka yake kuliwezesha liwepo kanisa la Wafiladefia, kwenye Ufunuo, nguzo za Hekalu. Anawapa mlango uliofunguliwa wazi ili kuimaliza kazi kwenye siku au nyakati za mwisho. Andiko hili linaonyesha pia kuwa Wafiladefia ni Nguzo zinazolisimamisha Hekalu, tulimo sisi sote leo. Zimesimama kwenye mawe ya msingi ya Mitume na Yesu Kristo akiwa ni Jiwe Kuu la Pembeni lililo kwenye mwamba ambao ni Mungu. Tazama pia kwenye jarida la Mji wa Mungu (Na. 180).

 

Ina maana gani kwa kusema kwamba "Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu (Yesu) mwenyewe, lile jipya."? (Ufunuo 3:12)

Jibu: Andiko la Ufunuo 3:12 halisemi jina jipya la Mungu. Bali andiko linasema: "Nitaandika juu yake jina la Mungu wangu." Munbu ana majina, matumizi ya kila jina moja yanaendana na hali halisi ya kimamlaka. Akiwa Eloah, anaonyesha kuwa yeye ni wapekee na ni Mungu wa Kweli. Anapolitumia jina la Ha Elohim anaonesha kuwa ni muumbaji, yaani Mungu muumbaji, aliyeanza na elohim.

 

Kwa hiyo, wana wa Mungu wote ni alohim ai theoi. Yeye ni Yahova wa Majeshi na wote watumikao pamoja naye wanaliitia jina la Yahova. Na ndiyo maana kla mmoja wa malaika kwenye Agano la Kale wakati wote aliitwa Yahova. Yeye ni Yehovih au Elyon, Liye Juu Sana na “Anayesababisha Kuwepo kwake” wa Kutoka 3:14. Mji huu ni Yerusalemu Mpya, ulio juu na ni mama yetu sisi sote. Ushukao toka mbinguni kwa Mungu. Soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180).

 

Eloah hana jina jipya. Ni Kristi ndiye mwenye jina jip-ya. Sisi tu elohimu kama Malaika wa Yahova atutanguliaye (Zekaria 12:8). Sisi ni miungu (elohim na theoi) na Maandiko hayatanguki. Kristo amepewa jina jipya nasi tutakuwa na jina hilo jipya limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zetu na tutamtumikia Kristo na Mungu kwa uweza. Soma pia jarida la Uwepo wa Yesu Kristo Hata Kabla ya Kuzaliwa Kwake Hapa Duniani (Na. 243).

 

Ni nani huhu anayeketi kwenye kiti cha enzi cheupe na hiki ni kipindi gani? (Ufunuo 6:2)

Jibu: Kiti cha Enzi Kikubwa Cheupe kinaonekana kwenye Ufunuo 4:2-6. Utawala wa mwisho wa Milenia sasa utakuwa umefikia kikomo kwenye Ufufuo wa Pili wa Wafu ambapo Kristo atashirikiana utawala na mamlaka yake na Mungu naye atapewa mamlaka ya Kuukumu ulimwengu wote kwenye kipindi chote cha miaka 100. Hiki ni kipindi cha Ufufuo wa Pili wa Wafu, wa baada ya kupindi cha utawala wa Milenia wa Kristo na Watakatifu. Roho Mtakatifu ametumwa kutoka kwa Mungu na kwa uweza huo ndipo Ufufuo unafanyika na Hukumu ya watu itafanyika. Sayari nzima yote itatengamaa kipindi hiki.

 

Mwishoni mwa miaka 100, watakatifu watakuwa kwenye umoja na mwelekeo wa pamoja na kuwa kama Mji wa Mungu. Soma majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95) na Mji wa Mungu (Na. 180). Isaya 65:25 inasema: “‘Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng'ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema Bwana.”

 

Ufunuo 6:12-17 inasema:

Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu, na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi. Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake. Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima, wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo. Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?

 

Unadhani huu kuwa ni unabii? Inaweza hii kuwa ndiyo iliyosababisha au chanzo cha kundi la vilimia hapa duniani?

Jibu: Ndiyo, huu mhuri wa sita unaashiria mlolongo wa matukio ya ishara za mbinguni zilizosababishwa na muingiliano wa hali ya halisi ya hwa ulimwenguni, ina inawezekana kusababishwa na silaha zinazotoka kwenye vituo mbalimbali vya angani. Kile kinachokitangaza ni ujio wa Masihi. Wafalme wa duniani wanamashaka kwa kilichosemwa na manabii katika siku za mwisho kama ni kweli kwamba: Masihi amekuja na kwamba watakabiliwa na ghadhabu yake.

 

Mfano wa kondoo na mbuzi unakuambia unachopaswa kutegemea.kama walivyowahukumu watakatifu ndivyo watakavyohukumiwa na wao. Jambo hili limepembuliwa kwa kina kwene majarida ya Mihuri Saba (Na. 140); Baragumu Saba (Na. 141); Kuanguka Kwa Yeriko (Na. 142) na Baragumu (Na. 136).

 

Hawa farasi weupe na uta vinawakilisha nini?

Jibu: Ufunuo 6:2 inataja farasi mweupe na uta. Farasi mweupe anaonekana kuwa ni mmoja anayefanana na mwanakondoo lakini ni dini au imani au utawala unaoshinda ambao ni uta (toxon). Kiumbe huyu si Masihi na huyu farasi mweupe na anayempanda kwenye Ufunuo 19:11.

 

Huyu anayempanda ni taswira au anawakilisha dini ya uwongo inayotenda kazi kwa kibali na jina la huyu ampandaye lakini ni mwongo na washindaji walio sambamba na imani au dini ya uwongo. Kutokana na mpandaji huyu, kunatokea vita, na kisha magonjwa mabaya kama tauni na ukame, na hatimaye kufa kwa mpanda farasi mwingine. Huu ulikuwa ni mfumo au dini iliyokuwa imeandaliwa na kuwekwa wakati dini ya uwongo ilipowekwa hada duniani na Shetani nab ado inatawala hapa duniani. Soma majarida ya Upembuzi Kuhusu Ratiba ya Nyakati (Na. 272) na pia linguine la Mihuri Saba (Na. 140) na Baragumu Saba (Na. 141).

 

Huyu farasi mkali mwekundu mwenye upanga mkubwa vinawakilisha nini na vina umuhimu gani? (Ufunuo 6:4)

Jibu: Farasi Mwekundu anamaanisha vita. Huu ni mgogoro uliowahi kuipata dunia kama matokeo ya migawanyiko yake iliyosababishwa na dini ya uwongo. Upanga huu ni upanga wa vita na wenye kugawanya. Yakwanza inataingulia ya pili nay a pili inafuatiwa na ya tatu nayo inafuatiwa na ya nne. Tazama jarida la Mihuri Saba (Na. 140).

 

Je, huyu farasi mweusi anawakilisha nini na jozi ya mizani inamaana gani na vina maana gani? (Ufunuo 6:5)

Jibu: Farasi mweusi ni ukame, tauni na magonjwa. Mizani au uwiano vinamaanisha hukumu na uhaba wa vitu farasi wawili  na gharama au thamani ya wapanda farasi wa kwanza. Kipimo kimetolewa sawasawa na jinsi wanavyopimwa. Mafuta na mvinyo vinawakilisha watakatifu wenye Roho Mtakatifu waliotawanyika kwenye mataifa mbalimbali. Wanaweza kuuawa kama mashahidi wa imani lakini msingi muhimu wa kudumu na uadilifu wa kanisa vitalindwa na dunia yenyewe haitaweza kukumbwa na madhara hadi wale 144,000 watakapokuwa wamekwishatiwa mhuri na kundi kubwa likiwa limemalizika tayari.

 

Je, huyu farasi wa kijivujivu na jina la mauti vina maana gani? (Ufunuo 6:8)

Jibu: Farasi wa kijivu aliye kwenye Ufunuo 6:8 ni mauti na kuzimuni vinavyofuatiwa na machafuko yatakayojitokeza na kufanywa na Mpanda farasi aliyepita wa Dini ya Uwongo, Vita, na Magonjwa au Tauni isiyokoma na baa kuu la Njaa vilivyosababishwa na huyu Farasi Mweusi.

 

Haya mauti na vifo ni hukumu dhidi ya wakazi wa duniani wanaoifuata dini hii ya uwongo na wakaenda kwenye ufufuo wa pili na kisha kukabiliwa na mauti ya pili. Tazama majarida ya Mihuri Saba (Na. 140); Baragumu Saba (Na. 141); Ufufuo wa Wafu (Na. 143); na Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95).

 

Unaweza kunielewesha maana ya dhiki kuu itakayowakumba watakatifu iliyoandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo na watatoka wapi? (Ufunuo 7:14) Pia nilisikia ikisemwa kwamba kutakujakuwa na miaka 7 ya dhiki kuu katika siku za mwisho. Itatokea wapi?

Jibu: Biblia inataja aina tatu za dhiki kuu. Moja wapo ni ile ya siku 1,260 iliyotajwa kuwa ni ya mwanamke kuwa jangwani, ambapo joka atakuwa anamfuatilia na nchi itamsaidia na kummeza huyo joka. Hii ni miaka 1,260 au siku za kinabii za kudumu kwa iliyojiita kuwa Dola Takatifu ya Roma iliyodumu tangu mwaka 590 hadi 1850. Katika kipindi hiki, mamilioni ya Watakatifu wengi waliuawa na Kanisa la Ukristo unaoshadidia imani na maadhimisho ya Easter na washika Jumapili wa Ulaya. Tazama jarida la Kazi ya Amri ya Nne ya Mungu Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170).

 

Biblia pia inaitaja shiki kuu nyingine ya wakati wa kufunguliwa kwa Mmhuri wa Tano ambapo watakatifu waliambiwa wasubiri hadi itimie idadi ya ndugu zao waliouawa kama walivyouawa hao wenyewe. Mateso ya dhiki hii yameanza rasmi tangu kipindi cha Vita Kuu ya I ya Dunia na yaliendelea hadi kifo cha Stalin mwaka 1956. Watu wengi waliuawa na makanisa ya Kilutheri na Roma kwa kuwatumia Manazi wa Ulaya. Inakisiwa kuwa walikuwa takriban waumini milioni 18 miongoni mwao. Hatutaweza kuijua idadi kamili, ila waliuwa kwenye makambi ya mateso yapatayo takriban 15,000 na kwenye kambi za mauaji zilizoandaliwa sehemu zote za Ulaya.

 

Tuna tarifa rasmi ya idadi ya kambi hizi kuwa zilikuwa ni zaidi ya elfu kumi kumi na idadi tuliyonayo inaashiria kuwa ni zaidi ya kambi 15,000. Katika siku za mwisho, kutakuwa na Dhiki Kuu baada ya kurudi kwake Masihi atakayekuja kuliokoa Kanisa. Dhiki hii Kuu ya mwisho ni maafa yatakayofanywa na mwanadamu, ambayo yanaweza kuzuiwa au kuepushwa kwa njia ya toba. Habari hii imeelezewa kwa kina kwenye majarida ya Mihuri Saba (Na. 140); Baragumu Saba (Na. 141); pia na Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142).

 

Je, kuna uhusiano wowote ule kati ya Ufunuo 8:10 ambapo nyota inaitwa kuwa ni pakanga iliyosababisha 1/3 ya viumbe walioko majini kufa (kwa uchungu), na Kutoka 15:25, wakati Israeli walipofika Mara (ambayo maana yake ni uchungu pia) na maji ya huko yalikuwa machungu hadi ulipotiwa mti ndani yake yakawa matamu? Je, andiko hili la Ufunuo 8:10 livhukuliwe kwa tafsiri ya moja kwa moja kama lilivyo, au kama kimafumbo, au kama kinadharia tu inayoweza kutafsiriwa kwa namna zote mbili. Najua kwamba, mara nyingi, matukio ya kimwili yanapelekea utimilifu wa matukio au maana ya kiroho. Je, hiki ndicho tunachojionea hapa kuhusu maji machungu?

Jibu: Ni mtazamo wetu kwamba tafsiri na mtazamo huu ni sahihi. Maji ya huko Mara yalikuwa machungu. Mti ambao ulikuwa ni Kristo, ulitiwa ndani yake ili kuyafana yaondokane na uchungu. Huku ni kuzaliwa ambako ukweli wake ni kwamba Yesu Kristo anachukuliwa kitaswira kama mtende ulio katikati ya mtu mpya mwenye kichwa cha mwanadamu na Yule mwenye kichwa cha simba ambaye ni Kerubi wa kwenye Hekalu la Mungu lililo kwenye kitabu cha nabii Ezekieli.

 

Dunia itakujakuwa haifai na Kristo atarudi ili kuja kuikoa. Maji mapya yatakuwa yakitoka kwenye Mlima wa Hekalu na kuwafanya samaki na viumbe wengine waishio. Tazama jarida la Pentekoste ya Sinai (Na. 115).

 

Ole hizi ni za nini na ni lini hawa Mashahidi watakapo kuja?

Jibu: Ufunuo sura ya 9 inaelezea kuhusu Baragumu ya Tano nay a Sita, ambazo ni Ole ya Kwanza nay a Pili. Ole ya Pili inaendelea mbele kwenye kipindi chote kilicho kwenye Sura za 10 na 11.

 

Ufunuo sura ya 10 inaelezea kipindi cha mpito kati ya baragumu ya Sita nay a Saba. Huyu ni Malaika mwenye Gombo dogo au Injili. Huu ni ujumbe wa Baragumu ya Saba. Ni kwenye kipindi hiki ndipo siri za Mungu zitakamilika au zitafunuliwa kikamilifu. Tukio hili na kurejeshwa kwa maongozi ya Torati ni budi litawatangulia watakatifu. Baragumu ya Sita na vita vya Baragumu ya Tano nay a Sita zimepita. Ni kwa mwingiliano huu ndipo tunachukua awamu ya mwisho ya Kupimwa kwa Hekalu na ndipo siku 1260 za Mashahidi na kipindi chake cha miaka mitatu na nusu mitaani. Kitendo cha kuzirejesha Sheria za Mungu na Upimaji wa Hekalu vitafanyika pamoja sambamba (soma jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137).

 

Mwishoni mwa kipindi hiki ambacho Malaika wa Saba atapiga baragumu na ndipo ufufu wa wafu utafanyika. Baragumu la Saba kwenye vitasa Saba vya Ghadhabu ya Mungu. Kwenye Baragumu hii anaanza kutawala. Kristo hapa kwenye hatua hii kwenye wasaa maalumu wa Ufufuo wa wafu. Hii inaanzia kwenye mashahidi wawili. Mhuri ulifunguliwa wazi muda mrefu uliopita na unaendelea.

 

Kwenye Ufunuo 13:18, kunasema kwamba tarakimu ya Mnyama ni ya kibinadamu, na jumla yake ni 666. Nimejitahidi kusoma majarida na maandiko mbalimbali ya kanisa la SDA na yanasema kwamba tarakimu ya mtu huyu ni ya papa, ambayo ni Vicarius=112 Fil II=53 Dei=501 = 666. Unaichukuliaje tafsiri hii? Ulisema kwamba ni wa kidini, lakini kitabu cha Ufunuo hakisemi kuwa ni namba ya mwanadamu. Hii inafanya mashiko kwangu kujua kwamba huenda papa ni kiongozi wa dini na mfumo huu unaompinga Mungu.

Jibu: Kiongozi wa mfumo wa kidini wa ulimwengu, ulio kwenye mbobeo wa kuabudu jua na dini nyingThe head of tne za uwongo, ndiye mtu huyu. Dini yote na mfumo wake una nembo au alama yake. Wanaabudu siku ya jua, na ina fundisho la Mpinga Kristo. Inaamini mungu wa Utatu wa dini ya Baal-Easter na Ndama wa Dhahabu ilikuwa ndiyo dini yake ya mwanzoni. Soma majarida ya Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235); Ndama wa Dhahabu (Na. 222); Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246).

 

Hakuna watarajiwa wengi wenye heshima ya namna kuwili wa kuwa ni viongozi wa imani na dini hii. Ukweli kwamba wadhifa ay cheo unachokiongelea cha kipekee hadi kufikia tarakimu hii ya 666 tu unashinikiza tatizo au hitimii ule wa sheria za Mungu ulio kwenye mioyo na mikononi kwa matendo. Mambo haya yameainishwa kwenye jarida la lililo kwenye mlolongo wa majarida ya Torati au Sheria za Mungu (Na. L1).

 

Imani ya SDA inajaribu kuitafsiri alama hii ya kidini kwa kuifananisha na kitendo cha kuipinga Sabato na huku wakiipuuzia Kalenda yote ya Mungu, ambayo hawakuruhusiwa kuishika. Soma pia kwenye majarida ya Torati na Amri ya Nne (Na. 256). Pia soma jarida la Alama ya Mnyama (Na. 25).

 

Familia yangu na mimi tumefanya utafiti kuhusu hawa 144,000 waliotajwa kwenye kitabu hiki cha Ufunuo. Tumekuta vyanzo kadhaa vinavyofundisha kwamba hawa 144,000 watakuwa ni wale kipindi cha Kristo na hadi kwenye nyakati za mwisho, wakati vyanzo vingine vimesema kuwa hawa 144,000 ni wa kutoka wakati wa uumbaji hadi nyakati za mwisho. Je, unaweza kutoa maonre from the time yako kuhusu jambo hili? (Ufunuo sura ya 14)

Jibu: Mafundisho kuhusu watu hawa 144,000 limeainishwa kwenye jarida la Mavuno ya Mungu, Dhabihu ya Mwezi Mpya na Wale 144,000 (Na. 120). Hawa 144,000 wantokana na vipindi vya Mababa, Manabii, Waamuzi, Daudi na huenda Sulemani na viongozi wengine wakuu wa Israeli hadi karibu na mwanzo wa Agano Jipya. Kwa hiyo, Kanisa lilitumika kama chanzo cha kwanza kutoka kwa Kristo, na alama wazilizozitumia zimeelezewa kwa kina zote kwenye majarida. Hutaweza kuzijua kikamilifu hadi utakapolielewa jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156).

 

Tatakimu hii imejumuishwa na baraza au halmashauri ya Mungu, au Sanhedrin lene wajumbe 72, ambalo lilihamishiwa kanisani (Luka 10:1,17). Sabato Miandamo ya Mwezi Mpya, na Makusanyiko ya Mungu, yote yanajumuishaa wajumbe 72, na kwa zaidi ya miaka 2000 vinafanya kuwe na jumla ya watu 144,000. Kipindi kifupi na tata ni kile cha Shetani na cha Ujio wa Masihi kilichofanywa na Mababa pamoja na Manabii, na kufanya jumla ya hawa 144,000. Mkutano huu makubwa ni masalia ya kanisa, wanaoiwakilisha sadaka au dhabihu ya jioni. Dhabihu ya Asubuhi iliyo kwenye Hekalu la Ezekieli, inawakilisha kipindi na utawala wa milenia.

 

Tunavijuaje vigezo vya kukubaliwa kwa hawa 144,000?

Jibu: Ni Mungu tu ndiye anayewajua hawa ni kina nani na ndiye anayempa Kristo watu hawa, lakini hawajajulikana wala kutambulishwa na hata wenyewe hawajijui hadi kwenye kipindi cha marejesho mapya ma mwisho na ufufuo wa kwanza wa wafu. Dunia haitadhurika hadi atakapokuwa ametiwa mhuri mtu wa mwisho kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu kwenye mwili wa Kristo, kwa jina la Mungu.

 

Ni nani anayetajwa au kukusudiwa kwenye Biblia inapomtaja kwenye Ufunuo kinapotaja kuhusu Babeli Mkuu, Mama wa Makahaba na machukizo ya nchi? (Ufunuo 17:5) Nineshangazwa kila mara kuhusu aliyekuwa anakusudiwa kuongelewa hapa.

Jibu: Inaongelea kuhusu imani na mfumo wa dini kubwa uliojifunganisha kwenye mfumo wa dini ya Kibabeloni inayofungamana na waabudu mungu Sin ambaye ni mungu Mwezi na walio kwenye dini ya mungu Istar au Easter pia kama anavyojulikana kwenye kugha ya Kiingereza. Kwa Waisraeli wa zamani alijulikana kama mwenzi wa Ashtoreth na wa Baali na kwenye dini siri alijulikana kama Isis kwa Wamisri na Venus kwa Warumi.

 

Mungu mfu alikuwa ndiye mlengwa kwenye dini hii potofu kama ilivyokuwa kwene maadhimisho yake ya sikukuu ya Easter. Alikuwa pia ni mama wa mungumke na dini yake imeenea ulimwenguni kote. Na ndiyo maana anaitwa mama wa makahaba kwa kuwa ana dini yake inayoshughulika na kujitia unajisi yenyewe kwa kutumia nguvu za dola na za kisiasa na makuhani wake wanazini na wafalme wa dunia. Imani na dini hii imechambuliwa kwa kina kwenye majarida ya Ndama wa Dhahabu (Na. 222) na pia kwenye Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235).

 

Nina maswali  3: 1. Ufunuo 20:10 inasema: “Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”. Ni nani huyu anayetajwa hapa? 2. Je, Ufunuo 20:15 inamtaja mwanadamu pia? Unawezaje usionekane kwenye kitabu cha uzima? 3. Andiko la Ufunuo 21:8 lina maana gani?

Jibu: Soma majarida ya Hukumu ya Mapepo (Na. 80), Ufufuo wa Wafu (Na. 143); na pia Mji wa Mungu (Na. 180). Jibu la swali hilo linakutikana kwenye sehemu ya mwisho ya swali lako. Ufunuo 21:8 inasema kuwa, “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo Mauti ya Pili.”

 

Kwahiyo, ni mauti ya pili, na sio hukumu ya milele. Waovu na watenda dhambi wanatakiwa watubu na hukumu ya pili ya kurekebishwa inahusika na watu hawa. Kila atakayebakia kuwa mtenda dhambi atakufa na kuteketezwa kwa moto. Neno lililotumika kwenye Ufunuo 20:10 linamaanisha kuwa “watateswa,” (basanisthesontai) limetuama kwenye neno linalomaanisha “kuipinga kweli kwa uovu” na “kuondolewa mbali”. Na “kwenye ukamilifu wa dahari” inamaana ya “milele na milele.” Mnyama ni nadharia na mfumo wa utawala, na sio kiumbe binafsi.

 

Shetani ni roho. Ni “nabii mke wa uwongo au bandia” ni unabii wa uwongo na ni mfumo kwa ujumla, na sio ni nabii fulani binafsi wa uwongo. Ziwa la Moto ni “Puros” na “Theiou.” Huu sio moto wa kibiriti tuujuao. Puros ni kitu “kinachong’aa kama moto.” Neno “kibiriti” lililotumiwa hapa ni “Theiou.” Neno lwenyewe linaashiria “umbinguni.” Kwa hiyo, ni kama Ziwa kali na la hukumu (soma Thayers Lexicon). Tafsiri hii ya kiroho ni ukumbusho war oho ipotoayo au ya upotevu iliyoondolewa kwa uumbaji wa kimwili. Inamaanisha wanadamu wote. Wale ambao hawataonekana wameandikwa kwenye Kitabu cha Uzima ni Mnefili na Mrefaimu (Isaya 26:13). Soma jarida la Wanefili (Na. 154). Mauti ya pili ina nguvu kwa wale walio kwenye Ufufuo wa Pili. Kama mtu hatatubu ndipo atakumbwa na mauti hii. Ni kazi ya Kristo na wateule wake kuweka mikakati ya kuwaokoa ili wasife.

 

Magundua kwamba Ufunuo 21:1 inasema “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.” Je, kutakuwa na bahari kipindi cha milenia?

Jibu: Ndiyo, kutakuwa bado na bahari kipindi hiki cha Milenia. Marejesho haya mapya ya Masihi yanashuhudia kuwepo kwa mito itakayotokea kwenye Mlima wa Sayuni itakayoelekea kwenye bahari ya upande wa magharibi na hadi Araba na itatumiwa na samaki na kuokota au kuzoa chumvi kwenye kingo za Araba.

 

Andiko lililo kwenye Ufunuo linaelezea mazingira au hali inayoanzia mwishoni mwa Ufufuo wa Pili na ujio wa Mji wa Mungu. Soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180). Jarida la Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95) linashughulika na dhana potofu kuhusu Milenia na hali yake sahihi.

 

Kuna rejea nyingi sana zinazotaja “bahari” kwenye Maandiko Matakatifu; je, kuna ishara maalumu na muhimu ya kuitilia maanani ninapokuwa nasoma kuhusu bahari zilizotajwa hapo juu? Kuna dhana yoyote ya kwa nini isemwe kutokuwapo tena kwenye Ufunuo 21:1?

Jibu: Bahari ina maana zaidi ya mbili kwenye tafsiri ya Biblia. Maana ya kwanza ni ya moja kwa moja kama bahari tuionayo ya kimwili. Na maana ya pili ni ya kimfano na inamaanisha uwingi wa watu au mataifa meingi. Kwa hiyo lile neon la “wanyama kutoka baharini” wanamaanisha umati wa watu walio kama mfumo wa kimaongozi au serikali. Kwa hiyo, mnyama ni mfumo wa utawala wa kidemokrasia unaojiweka na kujihesabia haki wenyewe. Nyakati za mwisho, bahari hii itakuwa ya kiroho. Ka hiyo, umati utatoweka kwa maana ya kwamba utayeyuka na kuwa kitu kubadilikabadilika kama ulivyofanyika kuwa mji mmoja kama wana wa Mungu. Soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180).

 

Dunia itatakaswa kwa moto na bahari zilizopo zinaweza kuwa ama zimeondolewa au kufanywa upya kimuundo mwingine. Hiyo itatokea baada ya Ufufuo wa pili na hakutakuwa na mtu aishiye atakayebakia kama tujuavyo hivi sasa. Soma majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143).

 

Unamaana gani usemi huu “Wakati wa dhiki ya Yakobo?”

Jibu: Yakobo ni taifa la Israeli. “Wakati wa dhiki ya Yakobo” unamaanisha kuitaja hali ya taifa hili itakavyokuwa katika Siku za Mwisho. Mwishoni kabisa, karibu na ujio wa Masihi, taifa la Israeli litapita kwenye kipindi cha dhiki kuu itakayosababishwa na viongozi wake lenyewe pamoja na watu waovu watakaokujakuwa ndani yake. Taifa la Israel lililo kwenye hii Nchi ya Ahadi tuijuayo leo lina makabila mawili tu wanaoliunda, ambao ni kabila la Yuda na sehemu ya kabila la Lawi.

 

What does the Bible indicate the planet will be like at the beginning of the Millennium?

Jibu: Dunia inaonekana kuwa kwenye hali mbaya kwa sababu ya mwenendo wa watu wa nyakati hizi. Biblia inasema kwamba ulimwengu utakuwa karibu na kangamia kabisa. Mchakato unaendelea mbele kwa kupitia awamu mbalimbali tuzijuazo leo kama Mihuri Saba, na kufuatiwa na Baragumu Saba, Vitasa Saba vya Ghadhabu ya Mungu. Mihuri hii Saba ni Baragumu Saba, na hivi Vitasa Saba ni Baragumu ya Saba. Soma majarida mengine ya Mihuri Saba (Na. 140) na Baragumu Saba (Na. 141). Ulimwengu unaweza kutubu na kuachana na uwendawazimu wake, lakini hautaweza kutubu kihivyo. Wakati wa Baragumu hii ya Saba kutashuhudiwa theluthi ya miti yote na nyasi vikikauka, na theluthi ya maji yote duniani yatabadilika kuwa damu, theluthi moja ya bahari zote itakufa kiasi cha kusababisha samaki wote walio maeneo hayo kufa pia, na yapata zaidi ya theluthi moja ya wanadamu watauawa kwenye vita ya baragumu ya sita na ya sita. Lakini bado hawatatubu.

 

Masihi atakuja kusimamisha mauaji haya, lakini toba haitafanyika, na dunia itaendelea mbele kwa kuiangamiza miti yote na nasi zake zote, samaki wote wa baharini, karibu wanadamu wote, na wanyama watakufa pia. Kisha ndipo tutauunganisha ulimwengu uliokufa pamoja na kuanza tena kwa Sheria au Torati ya Mungu. Tutapaswa kuukomesha na kuanza kuzishika sheria au Torati ya Mungu sasa, lakini hatutaweza kufanya hivyo sasa. Tungeweza kuyalinda mazingira kwa kuzishika sheria za vyakula lakini hatutaweza kumudu kufanya hivyo kabisa. Soma jarida la Sheria ya Vyakula (Na. 15).

 

Tuna mfano wa kuufuata kutoka kwa Kristo na kwa Mitume na wa Kanisa la Kwanza. Hata hivyo, dunia iliwaua Mitume wote na watakatifu na wakaisimamisha dini na imani ya uwongo waliyoiita “Ukristo.” Umemuua kila mtu aliyejaribu kuzitii na kuishika Torati au amri za Mungu na Ushuhuda wa Yesu Kristo, wakiwaua kwa kutumia mkakati maalumu na uliopangiliwa vizuri tangu mwaka 590 BK. Wengi wa waliozishika Amri na Torati waliokuwa wasika Sabato wamekuwa wakiuawa kwenye karne hii zaidi, yawezekana hata kuliko hata wakati mwingine wowote wa kihistoria. Wamekuwa wakiuawa na “Wakristo wazuri wa imani ya Kikatoliki” na “Wakristo wengine wazuri wa imani ya Kiprotestanti” makundi haya yote mawili yakilitumia jina la Mungu wao wa Utatu, wanayemwabudu siku ya Jumapili, wakiwaua na kuwatesa wale wanaozifuata na kuzishika amri za Mungu wa kweli na imani au ushuhuda wa Kristo na Mitume. Haihitaji kuwa ya namna hiyo, lakini watu watafanya hivyo kuliko mumtii na mumcha Mungu.

 

Ufufuo

Tafadhali nifafanulie kitakachotokea wakati mtu atakapofufuka.

Jibu: Mchakato wote kamili umeainishwa kwenye jarida la Ufufuo wa Wafu (Na. 143). Tazama pia kwenye jarida la Nafsi Hai (Na. 92). Mchakato huu kama ulivyokuwa kwa Kristo alifufuka na kisha kubadilika kimwili. Alipaa kwenda mbinguni akiwa kama Mganda wa Kutikiswa siku ya Kwanza ya Juma asubuhi, akitolewa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu kama Mganda wa Kutikiswa. Aliingia Patakatifu pa Patakatifu na akarudi kwa uweza wa Roho Mtakatifu, aliowapulizia wanafunzi wake (sawa na ilivyo kwenye Yohana 20:22).

 

Ezekieli anaonyesha kuwa ufufuko ni wa miili. Wale wafu waliolala-wakiwa watakatifu-watafufuliwa kwenye Ufufuo wa Kwanza. Kisha ndipo na sisi tutakaobakia hai, wote tutabadilishwa na kwenda Yerusalemu kuwa pamoja na Masihi. Ndipo dhiki kuu itaanza. Majeshi ya mataifa yataletwa huko Armagedoni au kwenye bonde la Yezreeli. Watakuja kupigana na Masihi na yataangamizwa (soma jarida la Baragumu (Na. 136)).

 

Kisha dunia itaongozwa kutoka Yerusalemu kwa kipindi cha miaka 1000 (soma jarida la Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95). Mwishoni mwa miaka hii 1000, Shetani atafunguliwa tena na vita ya mwisho itatokea. Mataifa yatajikusanya na kuja tena Yerusalemu na kisha majeshi hayo yataangamizwa. Watu watakaobakia kuwa watiifu na wasiasi ni wale waliobadilishwa na kufufuka kwenye ufufuo wa kwanza.

 

Wale waliokuwepo na wengine wote waliowahi kuishi watafufuliwa kwa kipindi cha miaka 100. Ndipo dunia yote itapatana na Mungu na kuongoka. Kila pepo aliyeasi atafanyika kuwa mwanadamu kama alivyokuwa Kristo, na utambulisho wao wa hali ya zamani vitakoma. Watapewa pia fursa ya kutubia dhambi na makosa yao (soma jarida la Hukumu ya Mapepo (Na. 80)).

 

Kila mtu kwenye ufufuo wa pili atakabiliwa na madhara ya mauti ya pili kama hawatatubu. Walio kwenye Ufufuo wa Kwanza hautakumbwa na mauti haya ya pili, kwa kuwa muda wa kuhukumiwa kwao ni sasa. Hii ni dhana iliyo kwenye waraka wa Waebrania unaposema kuwa Ufufuko wa Kwanza ni ni wa heri na bora zaidi.

 

Mwishoni mwa Ufufuo wa Pili na Hukumu huenda ni takriban mwaka 3127, dunia itafanywa upya kwa moto. Mji wa Mungu utashuka kutoka mbinguni na ndpo Kristo atakabidhi mamlaka yote kwa Baba, na vitu vyote vitakuwa kwenye mamlaka ya Baba, naye atakuwa ni yote katika yote na ndani ya yote. Soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180).

 

Wakati wa ufufuo, je, watotoo watawajua au kuwakumbuka wazazi wao? Na watu wengine wataweza kujuana kipindi hiki kwa namna waliyojuana kabla ya wakati huu?

Jibu: Ndiyo, kwenye Ufufu wa Pili watu wote watafufuliwa na watapatanishwa wote. Viumbe wote pamoja na mimba zote zilizotungwa na ambazo ziliwahi kutungwa zinajlikana na ziko salama kwenye mawazo ya Mungu. Zitafufuliwa zote na watajulikana wote na kukumbukana.

 

Na hii ndiyo sababu kwamba watu wengi hawapendi kusikia jambo hili. Zaidi sana watu wanapenda kufundishwa uzushi wa kuwa wataishi motoni na kuunguzwa humo milele. Pia itakuwa vigumu sana kwetu kuhusika nao, kwa mfano, wanawake waliowashuhudia watoto wao wakiuawa kwa kupigwa risasi kwenye mauaji ya kuangamiza Wayahudi na Washika Sabato wa Ulaya yajulikanayo kama Holocaust, ndipo hawatakuwa na la kujitetea askari wa vikosi waliofanya hivyo.

 

Itakuwa ni rahisi zaidi kwa wao kutubu, kuliko kuwasamehe waliowakosea. Yote mawili ni muhimu kwa kuupata wokovu. Ndiyo maana kumefanywa uwongo mwingi wa namna mbalimbali kwenye dini za dunia. Kwa mfano, dhana au fundisho la kuzaliwa tena na tena kwa kubadilika badilika lilianzishwa ili kuwafanya watena na tena kwa kubadilika badilika lilianzishwa ili kuwafanya watu walichukulie fundisho la kweli la Ufufuo wa Pili kuwa ni kama aina tu nyingine ya mtindo huu wa kuzaliwa kwa kubadilika badilika waujuao itatupasa kushughulika kulielezea jambo hili pia.

 

Wanakwenda kuwa na makasisi wapotofu sana na wataabisaji kutokea watakaowafundisha aina nyingi ya ole na makatazo ya uwongo kwa ajili ya fedha na mamlaka. Tunapoyaona yaliyokwisha kufanywa huko nyuma kwa jina la dini, na hata kwenye karne hii, basi itawakumba watu wengi.

 

Nasoma mahali fulani kwamba kwenye Ufufuo wa Kwanza watu wataishi na kufa kama ilivyo sasa. Je, hii ina maana kwamba wakati atakaporudi Yesu, yeyote atakayekuwa anaishi hai kipindi hicho hataweza kufufuka? Je, watu wanaokufa kipindi hiki ch ufufuo wa kwanza watafufuliwa kwenye ufufuo wa pili?

Jibu: Ndiyo, watu wataendela kuishi, na sio kila mtu atafufuka wakati atakaporudi Kristo. Kwa kweli, watli, watu wengi hawatafufuliwa kwenye ule ufufuo wa kwanza. Ni watakatifu tu peke yao ndio watafufuliwa, waliozishika Amri za Mungu na Ushuhuda au Imani ya Yesu Kristoo (Ufunuo 12:17; 14:12) na aliopewa Kristo na Mungu watakuwa kwenye Ufufuo wa Kwanza.

 

Fufuo utakuwa wa makundi mawili. Kundi la kwanza ni la wale 144,000 na la pili ni la Mkutano Mkubwa kama linavyoonyeshwa kwenye Ufunuo 7. Watatawala duniani hapa pamoja na Kristo kwa kipindi cha miaka 1,000 kama alivyofanya Shetani pamoja na malaika zake kwa kipindi cha miaka 6,000 sasa. Mwishoni mwa kipindi hiki cha Milenia, Shetani atafunguliwa tena kwa muda mfupi ili awadanganye mataifa na ndipo vita ya mwisho itatokea. watu wataendelea kwa kiasi cha kuzidi au kupungua kiwango cha umri wao tukilinganisha na ilivyo sasa, lakini wote wataishi na kufuata maongozi ya amri na maongozi ya Torati ya Mungu. Kimeelezewa na manabii wa zamani kuwa ni kipindi cha Utawala wa Haki. Ufufuo wa Pili utahusu mfumo mzima wote wa Uumbaji na viumbe vyake vyote wakiwemo malaika waasi, na baada ya hapo tutaunganishwa wote na Mungu pamoja kwenye Mji wa Mungu. Soma majarida ya: Ainisho la Ratiba ya Matukio ya Nyakati (Na. 272); Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95); Baragumu (Na. 136); Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Nafsi Hai (Na. 92); na Hukumu ya Mapepo (Na. 80).

 

Je, naelewa vyema kuamini kwamba wale walio kwenye ufufuo wa kwanza watakuwa kweenye utawala wa Yesu na kila kitu kitakuwa kama kilivyo leo? Je, watajihisi kuhuzunishwa wakati mtu anapokufa, au zitakuwepo nyumba na makazi, watu kufunga ndoa, kazi na mishughuliko, shule na masomo, na dunia itakuwa inafagiliwa ili kuifanya iwe safi?

Jibu: Dunia itaendelea kudumu kwa kipindi cha miaka mingine 1000 baada ya kurudi kwake Kristo. Itakuwa kwenye hali ya kuharibika na itapasa kutengenezwa au kukarabatiwa upya. Dhumuni la Ufufuo wa Kwanza ni kufanya wawepo na kundi la viumbe wa kiroho watakao tawala na Kristo watakaozifanya kazi walizokusudiwa kuzifanya mapepo kama wasingeasi hapa duniani kwa kipindi hiki cha miaka 6000. Wakati huu mambo yote yatafanyika sawasawa na sheria ya Torati ya Mungu. Dunia bado itakuwa na viumbe wa kimwili kipindi hiki na kutakuwa na mpangilio wa kifamilia na watu wataenenda kwa mujibu wa maagizo ya Torati. Kutakuwa na tukio kubwa la Kutoka kwa wana wote wa Israeli wanaohitajika kuunganishwa ili kuhitimisha idadi katika Israeli, sawasawa na maelekezo ya Kristo, wakiwa kama makuhani na Walawi. Hii imeelezwa wazi kwenye Isaya 66.

 

Tukio hili la Kutoka litakuwa Kubwa kuliko lile la kwanza lililoandikwa kwenye kitabu cha Kutoka na litafanyika baada ya vita ya Armagedoni na kuangamizwa kwa majeshi ya ushirika wa mataifa. Kama mtu alichukuliwa kwenye Ufufuo wa Kwanza na akabatizwa, na mtoto akaachwa kwa kuwa hajafikisha umri unaostahili abatizwe, ndivyo sasa kwamba mzazi akiwa mtu wa ulimwengu wa roha atamuwezesha kufana hivyo kwa ajili ya matunzo ya mtoto kuliko hata angalivyoweza kumtendea wakati akiwa mwanadamu. Kwahiyo ndipo watafanyika kuwa elohim moja kwa moja. Watoto watakuwa wamebarikiwa sana kipindi hiki. Soma majarida ya: Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95); nad Ainisho la Ratiba ya Zama na Nyakati (Na. 272).

 

Karamu ya Arusi

Unaweza kunifafanulia kwa hakika ni nini maana ya karamu ya arusi ya mwanakondoo?

Jibu: Kwenye jarida la Baragumu (Na. 136) mambo mawili ya Siku ya Baragumu yameelezewa kwa kina. Sehemu ya kwanza ni ya Kurudi kwa Masihi nay a ili ni Karamu ya Arusi ya Mwanakondoo. Masihi baada ya mashahidi wawili watakapotoa ujumbe au watakapokuwa wamehubiri ujumbe wao na kuwezesha kurudisha kukubalika kwa maongozi ya Torati ulimwenguni. Watauawa na kisha watafufuka baada ya siku tatu na nusu.

 

Mhuri wa Sita wa Ishara kutoka Mbinguni zitakazotangulia Ujio wa Masihi. (soma jarida la Mihuri Saba (Na. 140).) Ni Baragumu Saba tunazoziona kwenye vita vya mwisho na Ujio wa Masihi. Soma jarida la Baragumu Saba (Na. 141).

 

Wakati atakapokuja Masihi, waliokufa katika Kristo ambao ni wale waliolala mautini watafufuliwa kwanza. Kisha wale walio hai ambao ni watakatifu watabadilishwa miili yao na kuvikwa miili ya kimbinguni au ya kiroho pamoja na wale waliokufa katika Kristo na ndipo watakwenda wote Yerusalemu ili kuwa na Kristo. Ataugawanya Mlima wa Mizeituni pande mbili na wateule pia watakuwa pamoja naye.

 

Karamu ya Mwanakondoo ni mojawapo ya mifano ya Wanawali Wenye Busara. Hawa ni wateule waliozishika amri za Mungu na ushuhuda au imani ya Yesu Kristo na watakuwa kwenye Ufufuo wa Kwanza. Soma pia kwenye jarida la Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Nafsi Hai (Na. 92) na Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95).

 

Kusaga meno kutakako yakumba Makanisa ya ulimwengu huu wanaomita Kristo “Bwana, Bwana” lakini wakiwa hawazishiki Amri za Mungu na Ushuhuda wa Krist. Hawa ni wale wanajaribu kwenda kwenye Karamu ya Arusi na kukuta walikuwa hawaruhusu wala kukifikia kigezo cha kiwango cha kiroho. Hawakuwa na mavazi meupe na hawakuwa viumbe walio katika ylimwengu wa kiroho. Hii ni hatua ya kukataliwa na kutupwa nje. Wanasaga meno kwa kuwa wanagundua kuwa waliyapotosha maandiko na kufundisha uwongo na hawakuyatii bali waliyaasi maana na malengo yaliyokusidiwa na Maandiko Matakatifu.

 

Kwa Mungu hakuna upendeleo wala msimamo wa njia mbili. Ni ama kutii au kuasi. Kama utazitii na kuzishika amri na imani ya Kristo, utaruhusiwa kuingia kama sehemu ya waliokusudiwa tangu mwanzo, waliochaguliwa na wateule walioitwa waliohesabiwa haki na kutakaswa wakati huu wa Karamu ya Mwanakondoo.

 

Wengine waliosalia ulimwenguni ndipo watajaribu kufanya vita na Kristo, na majeshi ya muungano wa ulimwengu yatapelekwa huko Megido, au bonde jipya la Yezreeli, hadi Armagedoni. Ulimwengu utatiishwa na Shetani pamoja na mapepo yake watafungwa kwa kipindi cha miaka elfu ya Milenia.

 

Maandiko Matakatifu ya Torati ya Mungu yatakuwa yanafundishwa na kila mmoja kati ya wateule kwenye Karamu hii ya Mwanakondoo. Wale ambao hawatazishika Sikukuu zilizoamriwa na Mungu, pamoja na Sabato zake, na Miandamo ya Mwezi Mpya zilizo kwenye Kalenda ya Mungu (Na. 156), na kutuma wawakilishi wao kwenda Yerusalemu, mvua haitanyesha kwa wakati wake muafaka na watakumbwa na magonjwa ya tauni ya Misri (Zekaria 14:16-19).

 

Soma pia jarida la Torati na Amri ya Nne (Na. 256). Kristo anakuja kuwaokoa wale wanaomngoja kwa hamu na makini. Dini potofu za uwongo za imani zilizotungwa na kukubalika hapa ulimwenguni zitakomeshwa na kuangamizwa. Mfumo na imani potofu na mbovu ya Ukristo bandia na wa uwongo ambayo ndiyo yule kahaba Mkuu wa Babeli aliye kwenye kitabu cha Ufunuo itaangamizwa na mnyama mwenyewe.

 

Wateule wa Kanisani watakuwa ni viumbe katika ulimwengu wa roho, baada ya kufufuka kwao, watakuwa wajumbe watakaokwenda ulimwenguni kote kuwahudumia makabila yote ya kidunia na koo zao. Kisha tukio Kuu la Kutoka litatokea na taifa la Israeli litapangiliwa vizuri na kurejeshwa upya kikamilifu huko Mashhariki ya Kati. Tukio la kwanza la Kutoka litafanyika kwa hali isiyo na maana ndani ya tukio hili la Kutoka (Isaya 66:18-24).

 

Soma pia jarida la Kuwaita Watu Kwenda Yerusalemu (Na. 238). Wanawali wapumbavu wangali bado wamechumbiwa na Masihi na wataolewa naye, lakinii wataolewa kwenye Ufufuo wa Pili mwishoni mwa kipindi cha Milenia. Soma jarida la  Ainisho la Ratiba ya Zama na Nyakati (Na. 272). Ufufuo wa Kwanza ndio ulio bora kuliko, na mauti ya pili haina nguvu kwa wateule kwenye Ufufuo ule.

 

Unaweza kufafanua tafadhali ni nani atakayehudhuria kwenye arusi ya mwanakondoo na itafanyika lini?

Jibu: Karamu ya Harusi ya Mwanakondoo imeelezewa kwa kina kwenye sehemu ya II ya jarida la Baragumu (Na. 136). Watakaohudhuria Karamu ya Arusi ni walio Kanisani waliofufuliwa kwenye Ufufuo wa Kwanza.

 

Kuna wale 144,000 na Mktano Mkubwa walioandikwa kwenye Ufunuo 7. Hawa ni wale waliozishika Amri za Mungu na Ushuhuda wa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17: 14:12). Wamefufuka, kama walikuwa wamekwisha kufa tayari, pamoja na wale walio hai watabadilishwa kuwa viumbe katika ulimwengu wa roho na watachukuliwa kwenda Yerusalemu kuwa pamoja na Kristo. Watatawala duniani hapa kwa kipindi cha miaka elfu na kuianda tayari kwa Ufufuo wa Pili.

 

Kwenye Ufufuo huu wa Pili, wale wote waliowahi kuishi watafufuliwa wakwa na miili halisi na watafundishwa kikamilifu na kupewa fursa ya kutubu nay a wokovu. Mwishoni mwa miaka 100, wale watu waliokataa kuzipokea na kutii Torati au sheria za Mungu ndipo wataachyears, those people who have not accepted the Laws of God will simply be alloweiliwa wafe, na watachomwa kwenye Jehanamu, jina ambalo chimbuko lake linatokana na jalala la takataka lililokuwa nje ya mji wa Yerusalemu. Kwa maneno mengine hili linajulikana kama Ziwa la Moto likimaanisha kuwa ni mahala pa kuteketeza mizoga au miili iliyokufa ya wale waliokataa kuukubali mpango wa Mungu kwenye kipindi hiki maalumu cha mwishoni mwa Ufufuo wa Pili na cha Kiti cha Enzi Kikubwa Cheupe cha Hukumu.

 

Kama wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi wanafanya kazi zao kisahihi, hakutakuwa na yeyote atakayepotea. Ni yule mpumbavy na mjinga ndiye atakayeukataa uzima wa milele kwa Sheria za Mungu baada ya kuona kwamba njia nyingine zote zimefanywa kuwa za kilimwengu. Wataponywa wote na kila mmoja atakuwa kwene nia sahihi.

 

Awamu inayofuatia ni ya kuuunganisha Mji wa Mungu. Hii inapelekea Malaika wote wa mbinguni kuwekwa chini ya Kristo kwenye sayari hii, na kisha Kristo atashika hatamu ya kuuongoza ulimwengu wote, akiwamiliki Malaika wote milele. Soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180).

 

Kwa hiyo, kimtazamo, karamu ya arusi itaishia hapo kwa kitambo. Wanawali hawa wenye busara waliolewa kwanza lakini Kristo amechumbia wanawali wapumbavu na wote walitarajia kuingia karamuni pamoja naye, kwa kuwa uchumba ule ukiwa ni arusi kubwa sana. Mtu aliyeingia karamuni au arusini akiwa hakuvaa vazi la arusi alipaswa kutoka nje na kurudi alikotoka na akavae ili awe na fursa kwenye sherehe inayofuatia ya karamu ya arusi. Na ndiyo maana waliitwa “wanawali wapumbavu.”

 

Mchakato huu wa kuyatengeneza mambo yote upya utajiri pia wale malaika walioasi ambao watapewa pia fursa ya kuvikwa vazi jipya na kupewa jina jipya. Itawapasa kwenda kwa kupitia mchakato huo huo alioupitia Kristo. Itawapasa kuwa wanadamu, ili waweze kufufuliwa, kisha ndipo waishi kwa miaka 100 wakiwa kama wanadamu wakiwasaidia wale wote waliowazuia kwenye kipindi chote cha kudumu kwa uumbaji.

 

Soma kwenye majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Nafsi Hai (Na. 92); Hukumu ya Mapepo (Na. 80); Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199); na Ainisho la Ratiba ya Zama na Nyakati (Na. 272).

 

Mji wa Mungu

Nimesikia kukijadiliwa kuwa Mji wa Mungu utakuwepo baada ya miaka 40,000. Naamini kuwa umeandaliwa kutokana na msingi wa maandiko yafuatayo: Kumbukumbu la Torati 7:9; Zaburi 105:8; 1Wafalme 3:4; Luka 1:50. Dhana iliyopelekea kufundishwa hivyo ni kutokana na imani iliyopo kwamba rehema za Mungu zinadumu kwa vizazi 1000 vya wampendao, hivyo basi kuwa sawa wa miaka hii 40,000. Nilidhani kuwa rehema za Mungu zinadumu hata milele na milele. Unaonaje kuhusu hilo?

Jibu: Mji wa Mungu utaletwa mara tu baada ya tukio la Ufufuo wa Pili na cha Hukumu. Kwa nini Mungu asubirie kwa miaka 33,000 kabla ya kuja kwake duniani kuanzisha utaratibu wote mzima wa Mji wa Mungu (soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180). Neno lipasalo kuuita ni la kinadharia tu.

 

Hata hivyo, kama tukiangalia nyuma kwenye historia kwenye matendo na harakati za malaika, walianza uumbaji kwa kipindi cha takriban miaka 40,000 iliyopita na Cro-Magnon inaihesabu tangia wakati hhuu. Inawezekana kabisa utajwaji wa rehema ulienea kwa malaika kwa matendo na harakati zao za wakati wa mwanzoni sana pia. Inahusiana pia na rehema inayoweza kuenezwa hadi kwao kwenye Hukumu, kama tutakavyowahukumu wao (1Wakorho 6:3). Soma majarida ya Hukumu ya Mapepo (Na. 80); Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199); Ainisho la Ratiba ya Zama na Nyakati (Na. 272); Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Wanefili (Na. 154).

 

Kalenda

Kwenye kijitabu kidogo cha Tamko la Msingi wa Imani, kipengele cha 4.2, ukurasa wa 28, kuna palipotaja saa tatu kuwa ni saa 3 asubuhi na saa tisa kuwa ni 9 alasiri. Sielewi iko hivyo kwa nini. Nijuavyo mii ni kwamba siku inaanzia jua linapozama na inaishia pia jua linapozama. Kama ni hivyo, basi saa tatu ingebidikuwa ni saa 3 ya usiku au zaidi yake. Kama kuna inapotaja kwenye saa ya sasa ya ukutani kwamba ni saa 3 ya usiku. Unaweza kunifafanulia jambo hili tafadhali, ni wapi hali hi inakotokea japo kwa ufupi?

Jibu: Kuna namna mbili inayotajwa kuhusu siku. Aina ya kwanza ni ile ya saa ishirini na nne kama unavyosema, lakini Kristo pia alisema “kwani Siku moja haina masaa kumi na mawili?” kwa jinsi hii inamaanisha kuwa ni masaa ya mchana.

 

Saa la kui na mbili kwa kawaida linaanzia saa 6 usiku hadi saa 6 ya mchana, kama tunavyohesabu kwa mujibu wa masaa ya dini ya Kanisa la Roma wanavyohesabu tangu karne ya 19. Usiku pia uligawanywa kwa masaa, lakini mara nyingi yalitajwa kama masaa ya “zamu.” Zamu ya katikati ilijiri kuanzia saa 4 usiku hadi saa 8 alfajiri kwa saa za siku hizi.

 

Saa la kawaida la kwanza la siku ni lile tunalolijua sasa kuwa saa 12 asubuhi, na saa la kwanza la usiku lilikuwa ni saa 12 ya jioni. Kwa hiyo, hesabu ya dhabihu za asubuh na za jioi zilifanyika saa tatu, na ndiyo maana Kanisa lilikusanyika wakati huo siku ya Pentekoste. Roho Mtakatifu aliwashukia majira ya utoaji wa Dhabihu ya Asubuhi. Hii ilikuwa na maana kubwa sana kwa wote waliokuwepo.

 

Utaratibu huo uliendele kutumika hadi hata siku za hivi karibuni. Utaratibu wa kuishika kalenda na nyakati zake vimeainishwa kwenye majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156). Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213) linafurahisha sana jambo hili pia.

 

Unasema kwamba siku ya usiku na mchana masaa kuwa sawasawa maarufu kama ikwinoksi ya majira ya baridi na yalituwa kwenye kuamua kuupata mwezi wa kwanza. Kwani ikwinoksi hii ya majira ya mapukutiko mara zote inaangukia kwenye mwezi fulani tu maalumu au kipindi fulani maalumu kila mwaka?

Jibu: Kuna vipindi viwili tu vya majira kwa mwaka kwenye Biblia. Navyo vinajulikana au kuanza kwa kufuata kutukia kwa hizi siku za Ikwinoksi. Kwa wale walio kama wewe wanaoishi kwenye ncha ya Kaskazini mwa dunia (Sayansi inadaiwa sasa kukubaliana kwamba ncha ya kusini ipo juu, kwa maana ya ulimwengu), yakupasa useme kuwa ni ikwinoksi za majira ya mapukutiko, lakini kwa upande wa Ncha ya Kusini mwa dunia, kuna namna nyingine iliyopo. Siku ya 14 ya mwezi ambayo ni mwanzo wa maadhimisho ya idi ya Pasaka inaangukia kwenye ikwinoksi ya mwezi Machi, na haiwezekani kabisa kutokea siku nyingine yoyote mbali na mwezi huu. Kwa utaratibu huu wa kikanuni, kwa kawaida inafuatia kwamba Siku ya Mwisho ya Mkutano wa Makini ya Sikukuu ya Vibanda inaangukia kabla yake na wakati mwingine baadae kidogo, lakini sio baada ya Ikwiniksi ya mwezi Septemba. Kwa hiyo, majira matatu ya mavuno ya Mungu mara zote yanaangukia kwenye majira ya joto ya upande wa Kaskazini katikati ya hizi Ikwinoksi.

 

Unazihesabuje siku za “Mwezi Mpya?” nimejisomea vitabu vingi sana kuhusu jambo hili. Sikuti chochote kwenye Maandiko Matakatifu kinachoniongoza kujua jinsi ya kuhesabu, ingawaje Sauli, Daudi na Manabii wengine waliijua siku hii. Nauliza swali hili kwa kuwa siku zako zinaonekana kutofautiana siku moja zaidi kuliko kipindi cha mpito wa kuandama mwezi cha kinajimu, nadhani.

Jibu: Hapana. Siku zetu zinatokana na kipimo hicho hicho cha siku ya mpito ya kuandama mwezi cha wataalamu wa Elimu ya Anga na imewekwa sawasawa na kama zinavyoanza siku huko Yerusalemu, jioni hadi jioni inayofuatia. Hivi ndivyo Wasamaria walivyofanya hadi siku za leo, na ndivyo ilivyofanyika kwenye utaratibu wa hesabu za Hekaluni kipindi cha Masadukayo.

 

Ndiyo maana ilijuliana wakati wote kabla. Mwezi Mpya kila mara uliwweza kuhesabiwa kwa kufuata Kanuni zake au Phasis, kama zilivyokuwa jedwali za maji kujaa na kupwa ulimwenguni kote. Hesabu ya wakati wa kupwa maji iliamua siku, sawa na kama yanapokuwa yanajaa. Iliwapendeza Marabi wa Kiyahudi kudhania kwamba tulikuwa wote hatujui ilivyokuwa ikifanyika siku hizo kwa kuwa hawakupenda kushika sheria za Torati ya Mungu bila kuchanganya na mapokeo yao. Katika siku za zamani au za kale zilizokuwa zinafanyika biashara kabla ya kipindi cha Hekalu, vipimo vya nyuzi ulalo za za wima za dunia zilipimwa na ambazo tumezipoteza wakati wa Zama ya Giza iliyoingizwa na iliyojiita kuwa ni Dla Takatifu ya Rumi.

 

Alama ya mwezi mchanga mwandamo ni Kidole cha mungu Ashirat. Alama hii ya mwezi mchanga unaoandama unafanyiza kucha ya kidoleni mwa mungumke anaykusudiwa. Pia ni ishara ya pembe za mungu Sini, au za mungu Hathori akiwa kama mungumke wa urutubisho. Isis pia ni mama wa mungumke na anafuatiwa kwa mbele yake na Horus. Easter au Istar pia ni mama wa mungumke na anafuatiwa kwa mbele yake na kina Attis na Adonis na wengine kadhalika. Ulitumika kama kiashirio cha nyakati na dini mchanganyiko za Kibabeli na Kiashuru na Wamisri waliokuwa wanamuabudu mungu mwezi, Sini na mungumke Easter au Ashirat na Wamisri wote wa zama kati ya Milenia ya pili KK.

 

Ndiyo ilikuwa ibada ya waamini Utatu na mungu mwezi, Sini na habari zake zinachambuliwa kwa kina kwenye jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222). Habari za kalenda zimeandikwa kwa kina kwenye majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156) na Torati na Amri ya Nne (Na. 256). Israeli na Kanisa wamekatazwa kuindama imani ya mungu Sini na Dini au Imani za Mafumbo.

 

Sikukuu, Miandamo ya Mwezi Mpya na Siku Takatifu zilizoagizwa kwenye Biblia na habari zake zinaonekana mara zote kujitokeza kwenye tarehe zinazohesabiwa kutokana na matukio ya idara za wataalamu wa mambo ya nyota. Kalenda zingine zimehesabiwa kwa matukio ya kidini, na huku bado mashirika ya kidini yanayofika kwenye maadhimisho ya Siku Takatifu za namna hii bado yanadai kuwa hizi ni Sikuku Takatifu za Mungu. Ni kwa namna gani au kwa kufuata kanuni zipi tunapata mashiko ya kuamua siku hizi katika siku hizi?

Jibu: Kalenda ya Hekaluni ilihesabiwa kwa kuanzia siku ya mpito ya kutoonekana mwezi na Wasamaria waliuhesabu kwa kuanzia siku ya mpito ya kutoonekana mwezi hata sasa, kama tufanyavyo sisi. Nakala zilizokutikana Uchina zinaashiria kwamba vonyesha kuwa vipindi hivi vya mpito pamoja na matukio ya kupatwa kwa jua na mwezi na matukio mengine ya elimu ya kinyota au unajimu vilihesabiwa tangu milenia ya tatu KK; kwa maneno mengine ni tangu wakati wa Nuhu kwa kweli.

 

Sheree au sikukuu ya Rosh Hashanah ni ya Kibabeli iliyokuwa ikisherehekewa huko Babeli na kuingizw kwenye sikukuu za Kiyahudi zilizoanzishwa au kuingizwa na marabi wa Kiyahudi mnamo karne ya tatu ya siku zetu. Kalenda ya Biblia imeeleweshwa kwa kina kwene jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156) na pia Mwaka Mpya umeainishwa kwa kina kwenye jarida la Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213). Pahala na umuhimu wake kwenye sheria na Torati umeelekezwa kwa kina kwenhe jarida la Torati na Amri ya Nne (Na. 256).

 

Msingi wa kufanya uahirisho wa Kalenda ya Rabi Hilleli, na ambayo imetuama kwenye kuanza kwake kufuatia na sikukuu hii ya Rosh Hashanah, vyote hivyo vimeelezewa kwa kina kwenye jarida la Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho, au Sikukuus? (Na. 195).

 

Je, ushahidi gani tulionao unaotuhakkishia kuwa kalenda ilianzia siku ya mpito wa kutoonekana mwezi?

Jibu: Mchakati rahisi wenye mashiko ndio huu. Mwezi Mpya kwenye mataifa yote mara zote umekuwa ni kipindi kile cha mpito cha wakati wa kutokuonekana mwezi. Imejulikana hadi sasa kuwa ni kipindi hiki cha mpito cha kutoonekana mwezi na mataifa yote na wataalamu wao wa elimu-anga. Dunia na mfumo wake wote unashuhudia kuwa ni kipindi hiki cha mpito cha kutoonekana mwezi na kwa kutumia ali ujazo na kupwa kwa bahari na mwenendo wake.

 

Utaratibu uliokuwa kwenye Hekalu na Zamani ulikuwa ni huu wa kuhesabu tangu kipindi cha giza cha kutoonekana mwezi. Wasamaria walitumia pia utaratibu huu wa kipindi cha kutoonekana mwezi na wangali bado wanatumia hivyo hadi sasa (pia soma jarida la Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213) na majarida ya Mwezi Mpya kwa ujumla pamoja na lile la Kalenda ya Mungu (Na. 156) Mambo haya yamefafanuliwa kwa kina kwenye majarida yenye kichwa hiki cha maneno.

 

Kanisa la Mungu huko Ulaya lilitumia kipindi hiki cha mpito wa kutoonekana mwezi kwa karne nyingi (soma pia jarida la Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170) na la Wasabato wa Transylvania) matatizo yaliyoinuka kwenye imani ya Kiyahudi yalitukea huko Jamnia wakati Mafarisayo waliposhika hatamu na kuanza kuwasha nguzo siku za mwandamo wa mwezi mchanga kwa mintaarafu ya kuadhimisha kulikotokana na hamu na tama zao ya kufanya uahirisho wa kurudi hadi nyuma kwenye Sabato. Matokeo yake, kwa mara ya kwanza Wasamaria walianza kuwasha nguzo siku sahihi ya mpito wa mwezi kutoonekana kutokana na maposhaji mpya ya Mafarisayo. Kuna kinachoitwa misingi mipotofu inayotajwa kwenye imani ya Kiyahudi. Hata hivyo, Wasamaria mara zote walikubali utaratibu wa Hekaluni wa mwezi mpya kuanzia siku ya mpito ya kutoonekana mwezi na kamwe hawaziwashi taa zao kipindi ambacho utaratibu wa hekaluni ulipokuwa unaendeshwa vizuri. Hawakubadilisha kamwe kabisa.

 

Alama ya mwezi mchanga mwandamo imechukuliwa kutoka kwenye ibada za kipagani na iliingia kwenye imani zote mbili, za Kiyahudi na Uislamu kutoka kwenye imani za kipagani pia (soma jarida la Migawanyo Mikuu ya Makanisa ya Washika Sabato (Na. 122). Chanzo chake inatokana na kidole cha mungu Easter au Ashirat au Astarte iliyotumika kama kiashirio cha majira au wakati na imani ya Wamisri na Wababeloni walipokuwa kwenye ushawishi wa ibada za mungu Ishtar kwa muonekano na madhihirisho mbalimbali. Kipindi hiki cha mpito cha kutoonekana mwezi kilikuwa ni mwanzo wa Miezi Mipya kwa kipindi kirefu hata huko Uchina katika millennia ya pili KK. Iwapo kama wataalamu wa elimu ya anga walishindwa kuihesabu na matukio ya kupatwa kwa jua na kwa mwezi, basi waliadhibiwa tangu nyakati za zamani sana (sawa na yasemavyo majarida ya ERE kuhusu Kalenda kuhusu ya China nk).

 

Mafundisho ya kizushi ya Karaite yalianza kuenea kipindi cha Zama za Kati kutokana na kutoelewa na ni utaratibu huu ndiyo ulinaozidi kuenea kama maadhimisho a kijinga na yasiyo na maana hadi sasa. Mtu anaweza kujiuliza swali rahisi tu kwamba: Kama siyo propaganda tu nini basi kwamba Marababi waliitumia kufanikisha mkakatti wa kufanya uahirisho ukubalike ambao Masihi alionyesha haukuwa ukitumika kipindi cha kuanzishwa kwake na ilikuwa ni sababu ya kuingizwa kwa mchezo wa maadhimisho yake na kanuni ilishindwa kufanikiwa kuwakumba watu wengi wa jamii ya Yudea kama mashahidi na kuzidisha shikaji hatamu wao, nu wao, ni ushahidi upi uliopo hapo wa kuhalalisha utaratibu huu wa ahirisho kuadhimisha mwandamo wa mwezi mchanga siyo kuwa unatokana na upagani na imani za Ndama wa Dhahabu?

 

Mitindo ya Kialmanaks (kwa Kirababu inamaanisha kuhesabu) ililetwa na Waanglo Saxons kutoka Mashariki ya Kati walipokuja huko Ulaya wakati wa kuanguka kwa Dola ya Parthian (mnamo karne ya 2 KK), na ambayo ingali inadumu bado ikionyesha kwamba kuna siku hamsini na tisa kwa kila mwezi sawa na mfumo wa Kiarabu, tangu Mwezi Mpya unaokaribiana zaidi na siku ya ikwinoks ya mwezi Machi na ikabakia hivyo hadi katika karne ya kumi na saba huko Uingereza. Mungu aliziumba mbingu ili kufanya majira na nyakati. Hakuhitajiki kutafakari makundi madogo madogo yaliyopotoshwa ya Wayahudi wa kipindi cha Zama Kati ili kuamua mwelekeo wa Kalenda. Imekuwa ni ushuhuda wa watu wote na kwa nyakati zote.

 

Kwa mbinu au mtindo wa kutofautisha maoni kama kwa kadiri ya inavyohusika kuanza kwa siku za miezi mipya, Ningependezwa sana kukijua kile kinachochukuliwa kama msingi wa kuamua siku ya kuanza kwa miezi mipya jinsi ilivyofanywa wakati wa Kristo?

Jibu: "[sikukuu] ya tat uni mwanzo wa mwezi mpya pamoja na jua”. "Philo wa Alexandria [kwenye kitabu chake cha F H Colson (Harvard University Press, Loeb Classical Library, Cambridge, MA, 1937); The Special Laws, II, XI,41]. And in II, XXVI,140 kinasemaa: "Huu ni Mwezi Mpya, au mwanzo wa mwezi mwandamo, ujulikanao kaama kipindi cha katikati ya siku moja ya mpito ya mwezi kutoonekana hadi ya pili, na urefu wa kitu kilichohesabiwa kikamilifu kwa mwelekeo wa kiuanazuoni wa elimu ya anga". (Soma jarida la Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho au Sikukuu? (Na. 195).

 

Mambo mengine ya kuyatilia maanani ni: Kutokana na usomaji wa Injili tunaweza kuona kwamba Kristo alikufa siku ya Jumatano, na alifufuka mwishoni mwa siku ya Jumamosi kuelekea siku ya Jumapili. Tunajua kwamba alikufa saa 9 (saa 9 alasiri) na alikufa kwa siku 3 mchana na siku 3 usiku (Mathayo 12:40). Tunajua pia kwamba Mariamu alikuja kaburini kwake siku ya Jumapili asubuhi (Mathayo 28:1). Kwa hiyo, ukirudi nyuma hadi siku ya 3 za chana na siku 3 za usiku, ni wazi sana kwamba aliuawa siku ya Jumatano tu. Ikitiliwa maanani kwamba Jumatano inaanzia kwanza usiku, na Alhamisi ikawa siku ya kwanza, na angeweza tu kuwekwa kwenye kaburi lake baada ya saa 9 alasiri siku ya Jumatano. Hakuna mashaka pia kwa namna yoyote ile kwamba alikufa siku ya maandalio ya 14 ya mwezi wa Abibu, akiwa kama mwanakondoo wa Pasaka.

 

Kwa vipengele hivyo 2 (yaani kwamba alikufa siku ya 14 ya mwezi wa Abibu, na mwaka ule, siku ya 14 Abibu iliangukia siu ya Jumatano), na tukihesabu kwa kwenda nyuma tunaweza kutarajia kuwa siku ya 1 ya mwezi wa Abibu kuangukia siku ya Alhamisi, ikianzia siku ya Jumatano wakati wa kuzama jua. Kutokana na mwanzo huo, linajitokeza swali kwamba: je, siku ya 1 ya mwezi wa Abibu ilikuwa ni ya mwezi mpya au ya kuandama kwa mwezi mchanga? Kwenye jarida la Nyakati na Majira ya Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159) siku zote zilipewa majira ya mwezi mpya zilikuwa ni mwezi Machi na Aprili tangu mwaka wa 28 BK hadi 33 BK. (Imetolewa na Idara ya Mambo ya Anga iitwayo Her Majesty's Nautical Almanac Office). Jumatano ya yarehe 22 Machi mwaka wa 30 BK saa 20:59 ilikuwa ni mwezi mpya, kuonyesha kwamba Abibu i ilianza wakati wa kuzama jua kwa Jumatano. Hii iikuwa ni siku ya mwezi mpya, na sio ya mwandamo wa mwezi mchanga. Inakuwa na mashiko kwa mwaka wa 30 BK kuwa ni mwaka wa aliosulibiwa Kristo kwa ajili ya Ishara ya nabii Yona (ambayo ilianzia tangu mwaka wa 30 BK na kuishia Abibu 1 ya mwaka 70 BK).

 

Wayahudi wa jamii ya Karaite wamasema kuwa mwezi mpya ni wakati ule wa kuandama kwa mwezi mchanga. Najua kwamba kipindi cha mpito cha kutoonekana mwezi cha wataalamu wa elimu ya anga kuwa ni sahihi sana. Tunawezaje kujua kutokana na Biblia, ni ipi inayokubaliana na maagizo ya YHVH? Tunajua kuwa siku inaanzia wakati wa jua kuzama, lakini kwa kusudi la kila siku ya 1 ya kila mwezi kutumia upigaji wa Baragumu kama mfano, inakuwa ni sahihi kurudi nyuma hadi kwenye uzamaji wa jua uliopita baada ya mwezi mpya? Nadhani kwa mujibu wa jinsi nilivyoambiwa mimi kuhusu ushuhuda wa kuitangaza siku hii na nashangaa waliwezaje kuuona na hata waseme kuwa ilianza tangu siku iliyopita wakati wa kuzama jua. Siku hii yote hadi kuzama kwa jua ni kipindi kitakatifu cha Sabato, kwa hiyo nataka kuwa na uhakika siku tunayoabudu kwa siku hizi.

Jibu: Wayahudi hawa wa jamii ya Karaite ni dini iliyokuwepo katika siku za zama za kati ya Kiyahudi iliyotokana na hazingira ya kutoelewa historia na utaratibu wa Biblia wa Kipindi cha Hekalu. Mataifa yote huanza kuhesabu siku ya Mwezi Mpya kuanzia siku ya Mpito ya kutoonekana mwezi, na walifana hivyo katika kipindi cha Hekalu.

 

Wasamaria bado wanaanza mzunguko wa kalenda yao kwa kuweka kigezo chao siku hii ya mpito ya kutoonekana mwezi, ingawaje walifungamaniba kalenda na ikwinoks ya tarehe 25 Machi katika karne ya tatu KK. Watangulizi wetu kwenye Kanisa la Mungu waliweka kalenda kwa kigezo hiki hii cha kipindi cha mpito kwa miaka elfu. Malumbano yaliyoibuka katika karne ya 20 yalitokana na jaribio la kulikasumbisha itikadi za Kizayoni kanisa na makosa yaliyotokana na imani na mafundisho ya Armstrong.

 

Kama mtu atakwenda kwenye duka la wanasesere na akanunua kijewali cha mviringo, ndipo ataona kuwa mara zote mwezi mpya utaangukia siku hii ya mpito, haijalishi ni nchi gani uliyopo. Neno la “miale ya Mwezi” linatokana na neno “Phasis” ambayo ni Mwezi Mpya. Alama ya mwezi mchanga unaoandama inahusiana na ibada za mungu Mwezi, Sini aliyekuwa maarufu huko Mashariki ya Kati na ambaye alikuwa pia anaabudiwa kwa kumchongea sanamu ya Ndama wa Dhahabu. Soma jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222). Pia soma majarida mengine ya Mwezi na Mwaka Mpya (Na. 213); Kalenda ya Mungu (Na. 156); na Kalenda na Mwezi Mwandamo: Uahirisho au Sikukuu? (Na. 195).

 

Je, unajua kwamba historia hii ni kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa tarehe. Naamini kuwa ilikuwa ni matumizi ambayo yatapaswa kurekebishwa. Watu wengi sana wamekuwa na maono yao yanayoungwa mkono na mwanadamu mwenye chupa ya maziwa tu katiyao na Baba zaidi kuliko Kristo kuwa ni mwombezi wa pekee.

Jibu: Tunajaribu kuyafanya mapenzi ya Mungu na historia ya mwenendo wa majira sio matokeo halisi tunapotilia maanani ukweli wa kwamba kuamua mwanzo wa Mwezi Mpya yanatokana na siku hii ya mpito ya baada au kabla ya utusitusi na kwa hiyo siku imaamuliwa kwa uhusiano wake na Kipindi cha mpito kinachohusiana na utusitusi huko Yerusalemu, na hivyo, siku ile inaamuliwa na kipindi.kwa hiyo, utaratibu wa Muainisho wa Siku wa Kimataifa kwa hakika ni aina ya pili ya kuhesabu. Kuzama kwa jua hadi kuzama tena kwa jua na kipindi cha masaa ishirini na nne kinafanya jumla ya siku moja yenye masaa ishirini na manne ndani na mfumo mmoja wa nyakati iliyopimwa kama siku halisi.

 

Katika kujaribu kuifutilia mbali kalenda ya uwongo, kuna utaratibu mwingine wowote wa kuupata mwezi mpya (wa Abibu) ulionenwa mwaka 1930 na kugawanya mara 100 ya mizunguko (miaka 19) ili kupata “uwezekano” wa kusulibiwa siku ya Jumatano? Kinatokea nini kwenye saa ambayo mzunguko wa Meton unapokoma? Sijaribu kuiweka siku nyingine ya kusulibiwa (au mwaka), bali ni kukitafuta kile ambacho kalenda zingeweza kuashiria kuwa huenda ni katika miaka ya...26-31AD.

Jibu: Uko sahihi kwa hilo kwamba mzunguko wa miaka 19 umekwisha kwa takriban masaa mawili. La msingi ni kujaribu kutumia mizunguko ya mara 100 kufikia siku ya kusulibiwa (tangu mwaka 1931) ilitumiwa na ushirika wa Worldwide Church of God. Walikuta kwamba haikuwa siku ya Jumatano isipokuwa kwenye utaratibu wa mwezi Aprili, na hivyo kuamua siku ya maadhimisho ya Pasaka kulikofanywa tarehe 25 Aprili mwaka 31 BK. Haikuwa kipindi kama hiki cha kabla tangu karne nyingi Kabla ya Kuzaliwa Kristo na kabla ya kipindi cha Hekalu.

 

Sababu iliyowapelekea kufanya hivyo ilikuwa ni kwa sababu waliamua kuwa huduma ya Kristo ilidumu kwa miaka mitatu na nusu ili kujikita na kipande kingine cha unabii wa uwongo. Hii kinyume chake ilisababishwa na kushindwa kwao kupangilia ujenzi wa Hekalu kisahihi, kutokana na makosa ya kitafsiri ya Danieli 9:25 kwenye tafsiri ya biblia ya KJV. Kwa hiyo waliliweka tukio hili mwaka wa 31 na sio mwaka 30 BK, kama maelezo au hadithi ya Biblia inavyoonyesha.

 

Vipindi halisi vya nyakati za Kusulibiwa na kalenda kwenye miaka ya 27-33 BK vimeelezwa kwenye jarida la Majira Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159). Wakati sahihi wa utaratibu na shughuli za Hekalu unakutikana kwenye jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Tena  wa Hekalu (Na. 13).

 

Najua kuwa siku ya 1 Abibu ni Mwaka Mpya wa Kibiblia, lakini tunapouchukulia mwaka wa Yubile unahesabiwa kuanzia siku ya Upatanisho ya mwaka mmoja hadi siku nyingine ya Upatanisho ya mwaka unaofuatia, je tunapaswa kuhesabia mwaka wa utoaji zaka zetu tangua mwezi wa 7? Kwa miaka mingi, wengi wetu tulio kwenye Makanisa ya Mungu tumekuwa tukiyaacha mashamba na bustani zetu zipumzike katika mwaka wa 7, ila tumekuwa hatufanyi hivi kwa wakati huohuo mmoja kama inavyotuagiza Biblia. Je, tunapaswa kuanza kuhesabu mwaka wa 1 baada ya kubatizwa kwetu, au ni kwenye Sikukuu gani ya Vibanda tunayopaswa kuihesabia?

Jibu: Mwaka wa kutoa zaka ni wa namna ileile kama mwaka wa kawaida tu unaoanzia siku ya 1 Abibu. Licha ya maelezo na ufafanuzi kwenye Mishnah, Sabato kwa mujibu wa mzunguko wa Yubile na mwaka wa mwisho wa Sabato uliofanyika mwaka 1998 tangu mwezi wa Abibu (1/1/21/40) hadi mwezi wa Abibu wa mwaka 1999 au 1/1/22/40. Mwaka wa tatu ni mwaka wa utoaji zaka ambao kwao zaka ya pili inatolewa kwenye kanisa ili kuwasaidia maskini na wa kuadhimisha sikukuu malangoni mwetu.

 

Mchakato huu wa mzunguko utaendelea hadi mwaka 2026 katika mwezi wa Saba itakapopigwa baragumu ya kutangazwa kwa siku ya Upatanisho, na mwaka huo utaendelea hadi siku ya Upatanisho ya mwaka 2027, ambao ni mwaka wa Yubile. Tangu siku ya 21 ya mwezi wa Saba wa mwaka wa Yubile ardhi yote itarejeshwa kwa wenyewe, na ndipo harakati za kilimo na kupanda zitaanza kwa ajili ya mavuno ya mwaka wa Kwanza wa Yubile Mpya ya wakati wa Pasaka ya mwaka wa 2028. Habari zii imeandikwa kwa kina kwenye majarida ya Utoaji Zaka (Na. 161); Torati na Amri ya Nne (Na. 256) na lile la Kalenda ya Mungu (Na. 156).

 

Naamini na kuelewa unayofundisha kwenye majarida ya CCG kuhusu Kalenda, bali sielewi jinsi unavyokitumia kipindi cha kutoonekana mwezi. Siku hii ya kutoonekana mwezi inaweza kuishia tangu siku 1.5-3.5 katika Mashariki ya Kati? Pia, ni nini kuhusu uivaji wa shayiri au shayiri mbivu (masuke mabichi) inayoashiria mwanzo wa mwaka, yaani mwezi wa Abibu? Napenda kama ugeitumia Kalenda ya Karaite.

Jibu: Kipindi na utaratibu huu wa siku isiyoonekana mwezi ni mtingo unaotokana na tukio la elimu ya ya kuhesabu miaka mapema na ilihesabiwa hivyo hata kipindi au wakati wa Nuhu. Siku za kila mwaka za Wachina zinaichukulia hii kuwa ilianzishwa kwenye millennia ya tatu KK na mtu aitwaye Hwang Ti, mtu wanayemuita mfalme wa Manjano. Utaratibu wa kuhesabu vipindi hivi vya kutoonekama mwezi na kupatwa kwa jua au mwezi kuwa ni lazima kushindwa kwake kufanya hivyo kuliadhibiwa. Hakuna shaka kuwa taratibu hizo zilitumika na kuhesabiwa kipindi chote cha zama za Hekalu, kama utaratibu huohuo ulitumiwa huko na huko Uchina pia na ulianzishwa na Nuhu. Yaonekana kuwa inawezekana Shemu alitawala akiwa kama kuhani wa Melkizedeki huko Yerusalemu. Ulimwengu wote ulitawaliwa kwa kalenda hii hadi kuanzishwa kwa dini za waabudu jua. Pia tazama kwenye jarida la Melkizedeki (Na. 128).

 

Wasamaria walihesabu kwa kukichukulia kipindi hiki cha kutoonekana mwezi hadi leo, kama tufanyavyo sisi na walivyofanya Masadukayo kipindi cha Hekalu. Walishika huduma za Hekalu kila mara isipokuwa katika miaka tisa chini ya Malkia Alexandra wakati Mafarisayo waliposhika shughuli za Hekalu, lakini hawakuingilia kati suala la kalenda, kama utaratibu wao wa kuanzia siku hii ya kutoonekana mwezi ulikuwa haujaanza. Kanisa limekuwa likichukulia kipindi hiki cha kutoonekana mwezi kwa kipindi cha miaka 2000 sasa. Liliipuuzia na kuikataa kalenda ya Hilleli mwaka 358 na kuichukulia kuwa ni uzushi mpotovu wa Wayahudi. Uzushi wa Karaite ulioibuka kipindi cha zama za kati haukukubalika kabisa na kanisa na mafunmdisho yake yalikuwa kinyume sana nay ale ya kanisa, ni kama ilivyo sasa.

 

Wapagani badi wanalazimishwa kuanzisha majedwali au michoro yao ya mduara yanayolingana na mzunguko wa siku hizi za kutoonekana mwezi na mienzi mwandamo mbali na kalenda ya jua, na Karaites hawakuyachukulia pamoja na wavuzi wasioelewa. Masuke ya kijani ya shayiri, yalikuwa ni masuke yasiyoiva, na yanakatwa yanapokuwa ya kijani na kuhiniwa. Na ndiyo maana yanaitwa “masuke ya kijani.” Ikiwa hujawahi punje hii isiyovunwa basi ungeelewa. Mganda wa Kutikiswa unawakilisha mwanzo wa Malimbuko, ambaye ni Yesu Kristo, aliyekatiliwa mbali akiwa mbichi na wakijani kupungwa kuashiria mwanzo wa Kipindi Maalumu cha kuhesabu Kuelekea kwenye Pentekoste. Tazama jarida la Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa (Na. 106b).

 

Mafundiho mapotofu na ya uwongo ya Karaite yanatokana na hamu au nia ya kukataa mafundisho ya ukenyeufu ya kalenda ya Hilleli, lakini pia kunatokana na hali mbaya ya kutojua historia ya Hekalu na kwa dhahiri kabisa kuwa ni hali ya kutojua kabisa historia ya Kanisa. Nasi pia tumekuwa tukiishika kalenda hii hii kwa kipindi cha takriban miaka 2000 pamoja na kipidi chote cha Hekalu. Tunaijua aina ya kalenda gani ilikuwa inatumiwa Kanisani kipindi cha Matengenezo kama ilivyoandikwa na Rabbi Samuel Kohn kwenye kitabu chake cha Wasabato wa Transylvania (CCG Publishing, USA, 1998). Ushawishi wa Wayahudi ulipelekea kuanzishwa kwa kalenda ya Hilleli baadaye. Kalenda ya Hilleli, pamoja na utaratibu wake wa uahirisho, iliingizwa kanisani karne hii. Mafundisho haya ya kizushi ya Karaite hayakukubaliwa kabisa wala kufuatwa na Kanisa la kweli la Mungu, wala haijawahi kufanyika hivyo. Majarida yafuatayo yana mrengo mmoja wa kufanana: Kalenda ya Mungu (Na. 156); Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213); na Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho au Sikukuu (Na. 195).

 

Pasaka

Unaweza tafadhali kuelezea kwa kina kuhusu kipindi cha wakati muafaka cha Usiku wa Kuuangalia sana na ni mambo gani yunayopasa kuyatenda?

Jibu: Wakati wa kusulibiwa unaelezea ni wa namna gani. Siku ya 14 Abibu, Kristo na mitume aliingia kwenye mahali pa muda kama ilivyohitajika kwenye Kumbukumbu la Torati 16:5-6. Waliuandaa mlo wa maandalizi kwa pamoja na kuanzisha Ushirika wa Meza ya Bwana jioni ile, ambayo kanisa linawajibika kuendeleza kuula usiku ule kila mwaka, na ndivyo lilivyoweza kufanya kwa muda wote wa takriban miaka elfu mbili.

 

Kristo alikamatwa na kuteswa na kusulibiwa. Aliuawa kwenye kipindi kilekile halisi ambacho Mwanakondoo aliuawa kwa ajili ya Pasaka mwishoni mwa siku ya 14 Abibu. Jioni ile ulianza mlo wa Pasaka ambayo kwamba alifanyika kuwa kondoo mbadala. Usiku wa Kuuangalia sana unaanza kwa kula mlo maalumu siku ya 15 Abibu na kanisa linatarajia kuitumia jioni ile kwa kukusanyika na kujifunza au kusoma.

 

Asubuhi waliruhusiwa kurudi makaoni mwao na kuhudhuria ibada ya Siku Takatifu ya Kwanza ya Mikate Isiyoliwa na Chachu. Watu wengine wanaichukulia siku hii kuwa ni usiku unaotumika wa kuangalia sana hadi mapambazuko yake. Matokeo ya kawaida ni kwamba kama mtu akikaa hadi mapambazuko, basi ibada za Siku Takatifu hazitaweza kupangiliwa siku kwa mkoromo wenye mlio mdogo.

 

Hata hivyo, ni vizuri na sahihi sana kwenda kulala mapema ama kuwa ni sehemu tu. Inapasa kutumika kwa matarajio na kwa kumsifu Masihi. Wasamaria wangali bado wanayashika mapokeo haya kila mwaka, na walipoweza waliweza kuadhimisha kwenye Mlima wa Gerizim.

 

Nahitaji kusoma zaidi kuhusu Kanuni ya Kuhesabu siku za kuelekea Idi ya Majuma nay a Mganda wa Kutikiswa. Sielewi kiusahihi hivi ni vitu gani. Nitajisomea wapi kwenye Maandiko Matakatifu kuhusu kipindi sahihi cha kumla Mwanakondoo wa Pasaka? Pia kwa kufanya mdhanio, aya zilizo kwene tafsiri zangu za KJV na NKJV ni za kughushiwa?

Jibu: Hapana, aya hizo zinaelezea mambo kwa mitazamo tofauti na Marko hajaliweka wazi jambo hili. Yohana ameainisha vizuri. Majarida muhimu ni: Kalenda ya Mungu (Na. 156); Siku Takatifu za Mungu (Na. 97); Sadaka ya Mganda wa Kutikisa (Na. 106b); Kanuni ya Kuhesabu Kuelekea Sikukuu ya Pentekoste (Na. 173); Roho Mtakatifu (Na. 117); na Torati na Amri ya Nne (Na. 256).

 

Mimi ni mwanamke mtu mzima ambaye hawezi kuhudhuria kwenye sikukuu ya Pasaka na wengine. Kwa kuwa siwezi kuhudhuria kwenye Sikukuu na kuoshwa miguu yangu, nitakuwa naoshwa kutokana na dhambi zote nizitendazo kila siku kwa njia ya toba? Ni nini basi maana ya alama ya mkate na divai?

Jibu: Torati inawataka wanaume wote kujihudhurisha kwenye sikukuu mara tatu kila mwaka. Wanawake wanaruhusiwa kuiadhimisha Pasaka majumbani mwao, kama watakuwa wanaumwa au wakiwa wazee. Hata hivyo, siku za 14 na 15 Abibu hazitakiwi kulala majumbani au malangoni mwetu kwa mujibu wa Torati (Kumbukumbu la Torati 16:5-7). Yakupasa kuondoka kuoka makaoni mwako na waweza kurudi asubuhi yake, ambayo ni Siku Takatifu ya Kwanza ya Mikate Isiyotiwa Chachu.

 

Ulaji wa Mez ya Bwana unafanyika sambamba na ibada na inaweza kufanyia peke yake. Hata hivyo, inapendekezwa kujihudhurisha kwenye Pasaka ili kwamba mwili wa Kristo uwe pamoja na uweze kukua katika roho. Kama utakuwa umelindwa kwa shuruti ya kimazingira ndipo unaweza pia kushiriki Pasaka mwezi unaofuatia ambao ni Mwezi wa Pili.

 

Katika mwaka wa tatu, sikukuu zinaweza kuadhimishwa majumbani ambao ni mwaka unaotolewa zaka ya tatu, ambayo inatolewa maalumu kwa wasiojiweza au kuwasaidia ndugu walio kwenye uhitaji mwaka huo. Mwaka 2001 utakuwa ni wa utoaji wa zaka hii ya tatu. Soma majarida ya: Torati na Amri ya Nne (Na. 256); Pasaka (Na. 98); Mchakato wa Mlo wa Meza ya Bwana (Na. 103B); Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa (Na. 106b). Kuna mlolongo mwingine wa majarida yanayohusu Pasaka na Mkate Usiotiwa Chachu.

 

Kama tunaishika Pasaka kama Kristo alivyofanya itatupasa kuoshana miguu? Kama ni hivyo, hii inamaana gani?

Jibu. Ndiyo, inatupasa na tunapaswa kuoshana miguu kwenye maadhimisho haya ya Pasaka. Neno lililotumika lilikuwa ni titheni ambalo linamaana ya kujinyenyekesha na kujitoa mtu ili kuwatumikia wenzake ambayo ndiyo tabia na mwenendo unaotupasa kuuendeleza. Soma jarida la Maana ya Kuoshana Miguu (Na. 99). Hii ni sehemu ya mlolongo wa majarida ya Pasaka.

 

Nakumbuka kuwa ushirika wa watakatifu kutoka utoto wangu; lakini ni nini hasa jambo hili na ni vipi na lini limeanza jambo hili?

Jibu: Dhana ya kwamba Ushirika wa Watakatifu ulianzishwa kwa Mlo wa Meza ya Bwana siku ya 14 Abibu, wakati kanisa la Agano Jipya lilikutanika kila mwaka ili kuamsha hali yao katika Roho Mtakatifu. Dhana hii ilienea kwa kufanya utaratibu wa kushiriki ushirika wa meza ya Bwana kila juma kulikofanywa katika karne ya pili, na maji yaliajumuishwa sambamba na mvinyo, jambo linaloonekana kuwa linatokana na imani au dini ya Mithras, kama ilivyokuwa jina la Baba. Wakati huo, mvinyo haukujumuishwa pamoja na makasisi wa Kanisa la Kirumi. Soma jarida la Malumbano na Hoja ya Wakuartodesiman (Na. 277) ili kujisomea kwa kina zaidi kkuhusu malumbano yaliyojiri kwenye karne ya pili na kuendelea.

 

Kanisa

Iwapo kama siu takatifu zote, maadhimisho na mapokeo ya ulimwengu yanatokana na vyanzo vya kipagani, ni siku zipi basi Wakristo wanapaswa kuzitakatifuza na/au kuziadhimsha?

Jibu: Biblia iko wazi sana kwamba ni siku zipi tunazotakiwa kuzishika, nazo ni Sabato, Mwezi Mpya na Sikukuu. Sabato ni Siku ya Saba ya Sabato na sio Siku ya Kwanza ya juma au Jumapili, ambayo imefungamanishwa na utaratibu huohuo wa ibada, kama ilivyo Krismas, inayotokana na dini za waabudu Jua.

 

Kristo na Kanisa walishika maadhimisho yote ya Sabato, Mwezi Mpya na Sikukuu (kama isemavyo Wakolosai 2:16). Sikukuu zenyewe ni: Mwaka Mpya (1 Abibu); Mfungo wa Saumu kwa ajili ya dhambi au Makosa ya Kupotoshwa (7 Abibu); Ushirika wa Meza ya Bwana/Pasaka (14 Abibu); Usiku wa Kuuangalia Sana (15 Abibu); Siku ya Kwanza ya Mikate Isiyotiwa Chachu (15 Abibu); Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa (Jumapili iliyo ndani ya kipindi hiki cha Pasaka na Mkate Usiotiwa Chachu); Siku ya Mwisho ya Mikate Isiyotiwa Chachu (21 Abibu); Idi ya Majuma au Pentekoste (Siku ya Sabato na Jumapili ya siku ya Hamsini yangu siku ya Mganda wa Kutikiswa); Siku ya Upigaji wa Baragumu (Mwezi Mpya wa Mwezi wa Saba)); Siku ya Upatanisho (Siku ya Kumi ya Mwezi wa Saba); Sikukuu ya Vibanda (Inaanzia Siku ya Kumi na Tano ya Mwezi wa Saba); Siku Iliyokuu ya Mwisho au Siku ya Mkutano wa Makini (Siku ya 21 ya Mwezi wa Saba).

 

Hizi ndizo Sikukuu za Bwana. Tutafaidika kwa kusoma majarida ya Kalenda ya Mungu (Na.156); Siku Takatifu za Mungu (Na. 97); Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213); Sikukuu za Mungu Jinsi Zinavyohusiana na Uumbaji (Na. 227); na Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235). Kuna majarida pia yaliyoandikwa kwenye kila Sikukuu zilizotajwa hapo juu.

 

Unamaana gani usemi huu kwamba “hakuna mtu atakayeurithi ufalme wa Mungu” iwapo kama hakuna mtu atakayekwenda mbinguni na kila mtu atafufuliwa na kupewa fursa ya pili? Je, kutakuwa na hukumu nyingine yoyote zaidi ya ile ya kufngwa gerezani katika ulimwengu huu wanayopewa wabakaji na wauaji? Najua kwamba ni mapenzi ya Mungu kuwa asiwepo mwenye mwili atakayepotea, lakini watu wengine ni waovu kupitiliza.

Jibu: Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wa sura yake. Waliumbwa kwa namna hiyo na kupewa uhuru wa kuchagua au kufanya maamuzi. Shetani alikuwa ni kerubi mkamilifu aliyetiwa mafuta. Alichagua kutenda dhambi. Hakuna aliyemuovu kiasi cha kutoweza kuokolewa. Na hii ndiyo sababu iliyomfanya Kristo afe. Hata Shetani atapewa fursa ya kutubu.

 

Kipindi cha ufufuo wa pili kimewekwa kwa ajili ya ukarabati wa hali nzima yote ya mwanadamu. Ni watu wale tu wanaoweza kuona na kusamehe na kuwaelekeza kwa kuwaonya au kuwarudi wengine wanastahili kuingia kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Na ndiyo maana Kristo alisema “Baba wasamehe, maana hawajui watendalo.” Stefano aliomba kwamba wasihesabiwe makosa. Kama kungewezekana, watesaji wakubwa hapo wangeweza kuukataa Wokovu na nusu ya Agano Jipya lisingeweza kuandikwa. Mhemko mkuu wa kitendo cha kumpiga mawe Stefano na shuhuda maalumu alikuwa ni Sauli wa Taso. Tunamjua sasa kama Mtume Paulo.

 

Kanisa lilidhani kuwa alikuwa muovu asiyeweza kubadilika. Ni kweli kwamba Paulo aliwauua au kuwatesa wengi wao ili kuhalalisha nadharia yake. Watu wanaodhani kuwa wengine wanakwenda kuungua motoni jehanamu au wanaotaka iwe hivyo hawafai kuuingia Ufalme wa Mungu. Soma majarida ya: Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na. 199); Hukumu ya Mapepo (Na. 80); Nafsi Hai (Na. 92); Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Mji wa Mungu (Na. 180).

 

Je, Kanisa lina mamlaka yoyote lililopewa kwa namna yoyote ile na Mungu au Yesu Kristo ya kubadilisha mafundisho? Kama ni hivyo, imeandikwa wapi? Pia ni je, Biblia ni mamlaka kamili, au ni mafundisho ya kanisa, maandiko, na mafundisho ndiyo mamlaka kamili?

Jibu: Hapana, kanisa halina mamlaka yoyote ya kuzibadilisha Amri za Mungu. Kristo alisema Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. (Mathayo 5:19).

 

Kristo alianzisha Kanisa lake na kuna aina nyingi za uongozi na utendaji kazi, lakini Bwana ni mmoja. Wamepewa mamlaka ya kuliongoza Kanisa kwa kufunga na kufungua lakini hawana mamlaka ya kubadilisha Sheria au Torati ya Mungu au kupotosha kwa namna yoyote ile.

 

Unaweza kusema kuwa kuna michakato mingi ya kufanyika Mkristo na inaanza kwa kuamini kwamba Kristo alizaliwa na mwanamke bikira na alikufa mtini kwa ukombozi na ondoleo la dhambi?

Jibu: Kama Mkristo, mtakatifu ametajwa kwenye Ufunuo 12:17 na 14:12. Hawa ni wale wazishikao Amri za Mungu na Ushuhuda au Imani ya Yesu Kristo. Mchakato wa kufanyika kuwa Mkristo umeandikwa kwenye Warumi 8:29-30. Wakristo wameitwa na Mungu.

 

Wamakusudiwa na kujulikana tangu mwanzo kwa uweza wake wa Usioshindwa na kitu chochote ili afanane na sura ya Mwaa wake. Wamechaguliwa na kisha kuitwa. Mara tu wanapoitwa na Roho Mtakatifu kwa mujibu wa Uweza usioshindikana wa Mungu, ndipo wanaletwa kwa Kristo na kuandaliwa kwa ajili ya ubatizo. Kisha mara tu baada ya kubatizwa kwenye mwili wa Kristo, Roho Mtakatifu anakuja juu yake akiwa kama malipo stahili yake kwa kupewa roho ya kufanyika mwana.

 

Watafanyika kuwa wana wa Mungu waliozaliwa mara ya pili. Wanahesabiwa haki kwa imani na kuupata wokovu wao, ambao umetolwa bure kabisa kwa neema, kwa kuitii Sheria au Torati ya Mungu kwa matendo. Imani bila matendo imekufa. Wamebadilishwa kwa kupitia Ufufuo wa Wafu wakiwa kama wana wa Mungu na hivyo kutukuzwa. Mchakato huu umeainishwa kwa kina kwenye majarida ya Kuzaliwa Mara ya Pili (Na. 172); Roho ya Kufanywa Wana (Na. 34); Toba na Ubatizo (Na. 52) na Ufufuo wa Wafu (Na. 143).

 

Je, watu walioonyeshwa ukweli na kuukubali wanahukumiwa sasa? Kama watu walioweka mikono yao ili kulima, wanaamua kutembea au kwenda mbali zaidi na kwenda ulimwenguni tena, (na kufa nafsi yake), je hii haisababishi kutenda dhambi isiyosameheka? Je, Mungu anatoa fursa hii ya pili?

Jibu: Biblia inatuambia kuwa tumepewa fursa mbili za kuamua. Tatizo pia lipo kwenye mamuzi na wito. Daudi alitenda dhambi na bado akawa mfalme wa Israeli kwenye Ufufuo wa Kwanza. Dhambi isiyosameheka ni ile ya kumkataa au kumkufuru Roho Mtakatifu. Wale walioteuliwa wako hukumuni sasa. Kama watashindwa watarudi kwenye Ufufuo wa pili au ufufuo wa jumla wa wote wa Wafu. Wale waliojulikana na kukusudiwa na Mungu na kuwachagua anawaita na kuwahesabia haki na kuwatukuza (Warumi 8:29-30). Kwahiyo hawawezi kushindwa kwa kuwa wamechaguliwa akijua hawatashindwa. Walioitwa ni wengi bali wateule ni wachache. Hilo ndilo lengo na hatima yake. Umepewa uhuru wa kuamua. Kama unasikia wito na kuja, bali kushindwa kufanya hivyo sio Mungu anayekusababisha wewe ushindwe au amtoe Roho kutoka kwako. Mapenzi yako mwenyewe au maamuzi yako yanafanya hayo. Baadae chini ya utaratibu mkamilifu zaidi tumepewa sote fursa ya wokovu.

 

Kuitwa au kuchaguliwa, je, hii ni tofauti kati ya wateule na wateule walewale?

Jibu: Hapana. Mteule ni yeye aliyechaguliwa na Mungu. Neno “mteule yuleyule” maana yake ni “mteule halisi”. Neno “mteule” lina maana ya “kuchaguliwa”" au “kuteuliwa.” Mungu huchagua na tumeitwa kwa msingi wa kujulikana kwetu tangu mwanzo. Kuna wengi wanaosikia wito lakini hawajachaguliwa. Wanaangukilia mbali kama ulivyo mfano wa mpanzi. Mungu anajua kuwa watashindwa lakini anawapa Roho Mtakatifu wamuombapo kwa namna yoyote kama alivyoahidi kwa kupitia watumishi wake manabii. Mungu hana upendeleo. Hili ndilo lengo lake zima kwa uhuru wa kuamua na uamuzi kwenye wito wa Mungu.

 

Inaonekana kwamba mapokeo ya Kanisa la Mungu ya kushika Siku Takatifu yanaugeuza Ukristo kwenye uzoefu wa kiakili. Hapo kunatakiwa kuwa na imani, ndoto za kinabii, umoja, furaha, na ushindi na sio suala tu la kutafsiri Maandiko. Nasikia kuhusu dini za siri za Kibabeloni na nasikia kwamba mapepo yanaweza utenda mambo na hata kuponya. Sijawahi kabisa kuponywa na Mungu wala na mapepo bali nimeshagawahi kuumia. Zio wapi ishara hizi za miujiza Kanisani? Yuko wapi Mungu? Hajajidhihirisha kabisa kwangu na simuoni.

Jibu: Inaweza kuwa ni uzoefu tu wa kiakili ukijaribu kuunda ukweli utokanao na viinimacho au ulaghai na maneno ya uwongo ya waamini Utatu. Walishindwa. Wengi hawakujua kile walichokiamini na walijipenyeza na kudharauliwa au kupuuzwa na mawakala wa dini za waamini Utatu.

 

Kanisa letu linaundwa kwa muungano wa bodi ya watu, waliotawanika ulimwenguni kote na kwenye nchi nyingi, waliojitoa kikamilifu na waadilifu wanaojitahidi kumtii Mungu kama alivyoyadhihirisha mapenzi yake kwa kupitia Manabii. Wengi wetu wamekuwa wameumizwa. Wengi wetu tumeponywa, na wengi wetu hawajaponywa pia. Kuna wale walioponywa zaidi kwa kutakaswa zaidi ya wale ambao hawajaponywa bado? Ni Mungu tu ndiye ajuaye jibu lake. Inaonekana kuwa wengi wameiacha njia waliyopo kama kipimo cha kujihesabia kwao haki wakijilinganisha na wengine.

 

Makanisa ya wasika Sabato yamekuwa yakiendendelea kwa kipindi cha miaka elfu kadhaa kupita kwenye kambi za mateso yajulikanayo kama Holocaust kwa kuwa walikuwa wanaishika Sabato, Sikukuu za Mungu na Sheria za Uiajl Vyakula na waliwekwa kwenye daraja la Wayahudi. Kuna kundi na vitengo maalumu vilivyotengwa kwa ajili yao kwenye kambi hizi za mateso. Kulikuwa na mateso ya kuwaning’iniza vichwa chini na kuwanyonga au vyumba vya kuwanyima hewa kwa kile kilichoitwa “Bibelforscher.” “Watafiti” hawa wa Biblia walikomeshwa na kuondolewa. Haukuwa uzoefu tu wa kiakili. Ni wale waliojitoa tu ndio waliishika imani na kufa. Soma jarida la Kazi ya Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170).

 

Washika Sabato wa huko Bektashi waliotokomezwa tu. Mamilioni ya Waarmenia walitolewa nje na kuuawa kwa kuiigwa risasi. Washika Sabato wa Transylvania waliteswa kwa kipindi cha karne nyingi na hata hawakuruhusiwa kumiliki mitambo ya kuchapishia wala chombo cha habari. Waliandia nyaraka zao mara kumi kwa mokono na kuzipeleka nakala hizo kwa kwenye maeneo kusudiwa kumi. Wote walifanya hivyo kwa kuwa walimpenda Mungu na walipenda kumtii na kumheshimu yeye. Unapotendea kazi kile ulichopewa kukielewa, Mungu atakupa mambo zaidi ya kuyajua.

 

Mungu kwa sasa hashughuliki na kuuhukumu ulimwengu huu. Bali bado upo chini ya mungu wa ulimwengu huu, Shetani. Unauona ulimwengu huu karibu ujiangamize kabisa wenyewe kabla ya miaka mingine ishirini ijayo, na itapasa ijengwe tena. Hilo halitakuwa kosa la Mungu. Ataruhusu hili ili kutuonyesha kinachotokea tunapokuwa hatuzitii na tunaziasi Sheria zake. Biblia inasema wazi kitu kimoja: Mkabidhi Mungu njia zako, naye atazithibitisha, hakuna njia nyingine yoyote karibu. Tii kile ulichopewa kwanza na kisha utapata uelewa mwingi zaidi. Kuifia imani si kitu kingine bali zoezi la kiujuzi.

 

Sabato au Jumapili

Ni ushuhuda gani hapo, zaidi ya ukusanyaji wa ujumla uliomchukua Paulo mbali na Yerusalemu kwenye Agano Jipya na kinachoonekana kuwa alikuwa Roma mwaka 150 BK, kwa ibada yoyote ya Jumapili kwenye Kanisa la Karne ya Kwanza?

 

Je, ushahidi huu unawezaje kukanushwa kama ni upotoshaji au uvunjaji wa Sabato na kupelekea kuanza kwa ibada za Jumapili?

 

Ni ushahidi gani ulioko hapa kwenye Agano Jipya na mahala pengine popote kukanusha mtazamo kinyume na kwa Sabato, Mwezi Mpya na Sikukuu za Biblia?

Jibu: Watrinitarian waabudu Jumapili kwa kawaida wanadai kwamba Agano Jipya linaashiria kwamba Wakristo wa jamii ya Kiyahudi walishika siku zote mbili, yaani siku ya saba na siku ya kwanza ya juma na kuzichukulia kama siku takatifu. Hakuna mashaka kwamba Krsto mwenyewe aliishika Sabato na Sikukuu zote, Mwezi Mpya na Siku nyingine zote Takatifu zilizoadhimishwa kipindi cha Hekalu na ndivyo walivyofanya mitume wote wengine. Paulo alihubiri kwenye sinagogi siku ya Sabato. Ilikwa ni kwa ajili hii ndipo aliagiza changizo la kuwasaidia wapendwa wa kanisa la Yerusalemu lifanyike siku ya kwanza ya juma, jambo linalodaiwa na wapotoshaji kwamba Wakristo Wamataifa walikuwa wanakusanyika kufanya ibada siku hii ya kwanza ya juma. Hii inatokana na kulitafsiri vibaya andiko la Matendo 20:7. Hii ilidaiwa kuwa ni kama siku ya pili takatifu na iliitwa siku ya Bwana ili kuitofautisha na Sabato. Wengine hata wanajaribu kudai kwamba huenda ilikuwa ni siku moja tu ya pekee iliyokuwa inatumiwa kuiadhimisha na waongofu Wamataifa. Madai haya ni ya ueongo kabisa. Andiko la Matendo 20 linaitaja inayojulikana kama the mia ton Sabbaton ambayo kama asemavyo Bullinger kuwa ni siku “Sabato ya kwanza kati ya nyinginezo” na inamaanisha kuwa ni juma la kwanza la Mchakato wa Kuhesabu kuelekea Pentekoste tangu siku ya Mganda wa Kutikiswa. Inadhaniwa na kuaminika kuwa ni Siku ya Kwanza ya Juma kwa kuwa inaendana na masomo ya siku ya Jumapili kuifanya iwe namna hiyo. Ni maelezo hayohayo yapo kwenye Yohana kwamba ni siku ya Mganda wa Kutikiswa baada ya kufufuka kwake.

 

Ibada ya Jumapili haikuingia wala kuwepo kanisani hadi mwaka 111 BK kutoka Roma. Wakolosai 2:16 inaonyesha walikuwa wanazishika Sabato na Miezi Mipya na Siku Takatifu na Paulo anasema kwamba mtu na asiwahukumu kwa ajili ya wao kuzishika siku hizi. Kwa hiyo inaweza kuonekana kwamba kanisa la Kolosai lilikuwa linazishika siku hizi na maagizo yote ya Biblia.

 

Uhakika unaotakiwa mara zote kama kigezo ni “Mafundisho ya Mltume Kumi na Mbili” na madai yanayosisitizwa sana yamefanywa kutokana na tarehe zao za mwanzo katika kuanzisha mchakato wa kwenye karne ya kwanza ya kuinganisha na ibada za Jumapili kama inavyosemwa kuhusu Siku ya Bwana na kuendelea kuitaja hivyo hadi siku hizi na kuiona kama kutaniko takatifu na la kuumega mkate (sura ya 14). “Mitume Kumi na Mbili” wanaunganishwa kwenye Katiba ya Mitume na na hueanda wana asili ya kisyria. Tafsiri ya ANF inaiweka hii kwenye Toleo au Gombo la Saba pamoja nao na hata jopo la kitivo cha waabudu Jumapili wanaojadili umahiri na weledi wa kuhesabu na mishikamano. Iwapo kama ingechukuliwa kiuweledi na kiumakini sana kuwa ni kwenye karne ya kwanza, basi ingekuwa kwenye toleo la 1. Sio ni kwa sababu imekuwa ni upotoshaji wa hivi karibuni kusaidia dhana ya ibada za Jumapili pamoja na mafundisho mengine ya kizushi yaliyoingizwa kanisani.

 

Kile kinaoitwa kuwa ni Waraka wa Ignatius kwa Wamagnesians (ANF, vol. 1, p. 63) ni mfano wa kwanza wa rejea hiyo na weledi wa kiusemi wa muundo mrefu zaidi unaoashiria kuwa uliandikwa kwa weledi sana ili kuanzisha matendo ya uko nyuma. Inaonyesha kwamba Sabato ilikuwa inatunzwa pia bali aina ndefu zaidi ni jaribio la kuanzisha dhana ya kuifana Siku ya Nane kuwa Siku ya Bwana, ambayo haipo kabisa kwenye majisifu makubwa ya aina fupi.

 

Rejea inafanywa kwa Pliny kusaidia ibada za Jumapili; hata hivyo, mamlaka ya kanisa yenyewe yanaonyesha kwamba Sabato ilishikwa ulimwenguni kote. Ni katika Roma na Alexandria peke yake kitendo hiki cha undumila kuwili kilifanywa.

 

Justin Martyr (yapata kama 150-154 BK) anaelezea ibada ya kidini ya Wakristo wa kwanza, maadhimisho yao ya sakramenti, nk, katika :siku ya kwanza.” Ni kweli kwamba Justin Martyr anaitaja ibada ya Siku ya Bwana kwenye kitabu chake kijulikanacho kama Utetezi wa Kwanza, yaani First Apology (ANF I, 186) lakini anasema wazi pia kwamba walikuwa wanakusanyika siku za Sabato pamoja na kwenye Mdahalo wake alioufanya na Trypho. Anasema kwamba sheria mpya inakutaka kuzishika Sabato za milele kwa kuzitubia dhambi zote na hivyo kuifanya kila siku kama Sabato (Sura ya 12 ANF I 200). Kwenye Mdahalo wake na Trypho anaonyesha kwamba wanajadili dhana ya Seabato na Sikukuu na inaonekana kwamba malumbano dhidi ya Sikukuu yalitokea Roma katikati ya karne ya pili walipokuwa wanaiigiza sikukuu ya kipagani ya Easter (sura ya XVIII ibid. p. 203). Jumapili iliingizwa pamoja nayo na kwanza iliiondoa au kupotosha maadhimisho ya Pasaka na kuipa nafasi kubwa Easter na kisha ikaiondoa Sabato yenyewe.

 

Justin anashughulikia mapokeo ya Trypho kama vile unywaji wa maji ya moto siku za Sabato. Anasema kuwa anafanya hivyo wakati Trypho alikuwa hafanyi. Malumbano kuhusu mapokeo ya Kifarisayo dhidi ya roho ya sheria katika Kristo. Anaongelea kuhusu ujio wa Masihi huko Yerusalemu na ufungaji wa saumu (Siku ya Upatanisho) kama ulivyoelekezwa na nabii Isaya (58). Hoja ni mtazamo wa watu wa Yuda kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria zaidi kuliko kwa njia ya neema katika Roho Mtakatifu.

 

Mdahalo au malumbano yanajiri ktokana na kushindwa kukubwa na hivi ndivyo ilivyokuwa kwamba Justin alikuwa ameachana na ukweli kwamba Anicetus aliyachukua au kuyaingiza mafundisho mapotofu na yakizushi ya kipagani ya Easter huko Roma na yalienea na kuliharibu kanisa zima. Ili kuyachukulia maandiko haya kuwa yana nguvu zaidi ilimbidi amkemee kwa maneno makali zaidi Anicetus alishutumiwa na Polycarp kwenye Mdahalo wa kwanza kati ya Migahalo ya Wakuartodeciman.

 

Ni Victor tu (takriban mwaka 190-192) tunayemuona kuwa aliishurutisha imani hii huko Roma na malumbano ya Wakuartodeciman yalitokea, na kuligawa kanisa (soma jarida la Malumbano ya Wakuartodeciman (Na. 277)). Polcrates hakuwa na nguvu ya kuisimamisha au kuikataza wakati Polycarp aliyekuwa kabla yake alimudu kuzuia hila hiyo.

 

Irenaeus alikuwa pia kwenye nafasi ya hatari alipokuwa anateuliwa na Smyrna askofu na aliyefundishwa na Polycarp aliyeishika Sabato na Sikukuu zilizoamriwa kama alivyofanya Yohana na mitume wote waliomtangulia hadi kufikia kipindi cha kufa kwake na kuendelea, alijaribu kutunza amani na kina Victor na Polycrates na hii ilishindikana mwaka 192.

 

Ni kwa waandishi wa kipindi cha karibia karne ya pili ambao tunawaona wakiiunga mkono ibada hii ya Jumapili na ikiendelezwa kutokana na shinikizo walililoshinikizwa kutoka Roma. Dionysius wa Korintho aliita kuwa ni “Siku ya Bwana.” Irenaeus wa Lyons ndiye wakati mwingine anayechukuliwa kuwa alidai kuwa Sabato ilikuwa imekoma. Hakuna mahala panapomtaja Irenaeus aliinenea vibaya ay kuitangua Sabato. Anaielezea Sabato kwenye kitabu chake sura ya XXIII. Ni ushahidi gani uliopo wa kumuona kuwa hakuwa anaishika? Anafanya mtofautisho kati ya makanisa mawili ya Yerusalemu kwenye maandiko yake. Moja ni sahihi na nyingine si sahihi.

 

Anaelezea jinsi Kristo alivyoishika kiusahihi na kikamilifu na mitume na wazao wa imani ya Ibrahimu. Anampinga Marcion na kueleza kuwa Kristo aliitimiliza na wala hakuitangua wala kuihalifu sheria (Adv. Haer. VIII, ANF, Vol. 1, pp. 470-471). Anaendelea mbele kwa kuelezea kuwa ilikuwepo lakini mwandishi  mmoja na mmoja aliishia kwenye maagano (ibid. ch IX, p. 472). Hata hivyo, maandiko mengi yaliandikwa baada ya Mtaguso wa baraza la Nicaea yakilenga kuipa kipaumbele Jumapili. Maandiko au kitabu kilichoandikwa na Justin Martyr, kinamtaja Irenaeus akisihi kutopiga magoti kuabudu siku ya Jumapili lakini wakuu wanakubaliana na utajwaji huu wa Jumapili siku ya Pasaka. Siku hiyo ilikuwa ni ya maadhimisho ya Mganda wa Kutikiswa ambayo kwa makosa kabisa waliiiita Easter kama inavyitwa kwa lugha ya Kiingereza (sawa na isemavyo ANF, vol. I, p. 569 and note 9).

 

Injili ya Barnabus inatumika kuonyesha kwa kanisa la kwanza liliabudu siku ya Jumapili (Ep. Of Barn., ANF Vol. 1, pp. 146-147). Hii ilitumika ili kushadidia tabia na mwenendo waliokuwanao mitume na matendo yao. Hata hivyo, Injili ya Barnabus ilidaiwa kuwa iliandikwa na Myahudi wa Alexandria kipindi cha utawala wa Trajan na Hadrian (yapata mwaka 100 BK na kuendelea). Ukweli wa kwamba nia ya Hadrian ya kuujenga mji inaonekana kuwa iliainishwa kwa kina kwenye sura ya 5 (ANF inaunukuu waraka) ikiaashiria kuwa tunaongelea siku za zamani sana za kabla ya mwaka wa 100 BK na kuenda baada ya matatizo yaliyotokea mwaka 135 BK. Ukweli wa kwamba mara nyingi anaonekana au kusikika kama Mmataifa akisalimiwa kwa mshangao na wafafanuzi kwenye ANF. Sababu yake si vigumu sana kuiona. kama Wakristo walikuwa hawathaminiwi kwa kiasi kikubwa sawa na kama ilivyokuwa Sabato na Torati, basi wangefukuzwa na kuchukuliwa kama vuguvugu lililokuwepo la kidini kama wangekuwa hawaneni sawasawa na sheria na ushuhuda (Isaya 8:20). Alexandria kulikuwa ni kitovu cha mhimili wa sera ya uchumi jamii wa Kinostiki na hilo halipaswi kusahauliwa. Pia Sabato ilishikwa kwa uaminifu sana huko Afrika Kaskazini kwa kipindi cha miaka mia nne. Ndiyo maana tunamuona Clement wa Alexandria akiitaja (Strom., ii, 6, ii, 7 etc) na inadhaniwa kuwa ni kutoka kwa Barnabus, Mlawi wa Cyprus. Na ndivyo hata tunavyojionea hata sisi Mnostiki Origen akiielezea kama Waraka wa Kikatoliki (Cont. Cels, i, 63), akiupa heshima yake stahiki (Comm., in Rom., I, 24).

 

Peter wa Alexandria (300 BK) ananukuliwa kama anayesema: "Tunaishika Siku ya Bwana kuwa ni siku ya furaha kwa kuwa yeye alifufuka siku hiyo."

 

Ni kwa sababu hii tunaiona imani ya Kirumi ikigeukia kuwatesa Wakristo ili kufanikisha kuishamirisha ili iweze kufanyika kuwa kama chombo au kifaa cha kutumiwa kufanikisha mikakati ya utawala wa wafalme wa dunia. Constantine alitangaza amri iliyojulikana kama Tangazo la Kuhuvumiliana mwaka 314. Mwaka 318 aliamuru kukaliwe kongamano la mtaguso wa Desposyni. Ndugu wa damu wa Yesu Kristo walidai kwamba Sheria ua Torati ya Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo virejeshwe. Constantine kwa kuombwa na mtume Sylvester, askofu wa Roma, alimpa mamlaka Sylvester kuamuru au aagize kuuawa kwao. Kwenye agizo lililotolewa mwaka 321, Constantine aliitukuza na kuienzi siku hiyo, iitwayo Siku ya Bwana, na kuitambua kuwa ni mojawapo ya siu takatifu kwa Wakristo, na kuamuru kuwa biashara na shughuli zote zifungwe siku hii. Hatimaye, Baraza la Mtaguso wa Nicaea (325 BK) kwenye mchakato wake rasmi ulitoa maelekezo kuhusu aina moya ya ibada ya Kikristo ifanyike siu hii peke yake, na Baraza la Mtaguso wa Laodicea (366) lilikazia kuwa siku hii inayoitwa Siku ya Bwana iwe na maana sawa na Sabato. Kwa hiyo, kwa tangazo na amri ya mfalme na mitaguso iliyoitishwa na kupitishwa katika karne ya nne vililiingiza kwenye Kanisa la Kikristo kwenye Kasumba ya upagani wa Kirumi, mabadiliko yaliyopokelewa na kukubaliwa na kuthibika.

 

Waabudu Jumapili wa Siku hizi wanahoji tofauti iliyopo kati ya siku mbili hizi, yaani Sabato na Siku ya Bwana: Neno “Sabato" limetoholewa kwenye lugha ya Kiebrania liitwalo "Shabua," maana yake "saba," au ni hatima ya mzunguko wa siku saba. Lilichukuliwa ili kumaanisha siku ya saba za juma la Biblia, ambalo wanalitaja kama “Juma la Kiyahudi” (inayoanzia tangu kuchwa kwa jua Ijumaa hadi kuchwa kwa jua Jumamosi). Ndipo kisha wanahoji au kupinga licha ya ukweli wa kwamba Kristo na Mitume walizishika Sabato hizi za kwenye Biblia na Mwezi Mpya na Sikukuu na kwamba ni kwenye kipindi tu cha mtawanyiko wa Wakristo ndipo siku ya mapumziko ilibadilishwa kutoka siku ya saba na kuwa siku ya kwanza ya juma, ili kuifanyia ukumbusho siku aliyofufuka Kristo, na kuipa heshima yake stahiki na kwa hiyo haijawahi kuwa Sabato (ambayo ilimaanisha kwa “usemi wa Wayahudi wa zamani”) na wala Jumapili (ambalo ni neno lenye maana na tafsiri ya kipagani, yaani, "siku ya jua"), bali wao wangali bado wakibisha na kudai hii kuwa ni “Siku ya Bwana.” Haipo kwao na hadhi na maadhimisho sawa nay ale ya Sabato ya Biblia, kama siku ya mapumziko na kuacha kabisa kuzifanya kazi zote ya utumishi au ya kuajiriwa, bali na kuifanya kuwa siku ya kujikuza kiroho na kutafakari na kufanya mambo yaliyo ya harakati za kidini na ni kipindi cha kujiepusha kuyafanya na kuyafuatilia mambo ya kidunia. Madai meingine yanafanywa kutokana na mapokeo potofu ya Mafarisayo ili kuonyesha jinsi ushikaji huu hauwezekani. Ukweli wa kama Kristo aliishika Sabato na siyo Jumapili imepotea kabisa kwao.

 

Makanisa ya Waethiopia na Waabyssinia yalikuwa ya washika Sabato kwa karne nyingi na ushahidi wake unaweza kujadiliwa. Waabudu Jumapili hawazishiki siku Takatifu za Mungu licha ya kuamriwa na kwao zinaonekana kama sheria zisizofaa wala kuutazishika amri zake.u ni kumcha Mungu na kuzishika amri (Mhubiri 12:13). Uzao wa mwanamke ni wale wazishikao amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12).

 

Firsa ipasayo ni rahisi tu.

Mungu ni habadiliki na hana kigeugeu. Kristo ni yeye yule, jana, leo na kesho. Wala habadiliki. Kristo alimpa Musa Torati akiwa kama Malaika wa Uwepo wake. Kristo alizishika Sheria za Mungu maisha yake yote. Alizishika Sabato, Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa sambamba na kuzishika katika roho na kuihubiri injili ya ufalme wa Mungu.

 

Mitume na kanisa la kwanza walishika amri hizi zote na sikukuu za Mungu. Na ndivyo lilivyofanya kanisa kwa kipindi chote cha miaka 2000 bila kushindwa. Limepitia kwenye mateso na kuuawa mamilioni ya waumini wake udhalimu ulofanywa na wale walio kwenye imani potofu za waabudu jua. Kristo anakaribia kurudi na anakwenda kuhimiza umuhimu wa kuzishika Sabato na Mwezi Mpya (Isaya 66:23) na Sikukuu zote zilizoamriwa (Zekaria 14:16-19). Wale watakaopuuzia kuzishika sikukuu watakufa.

 

Sababu zenye mashiko ziko wazi:

Kama Kristo alizianzisha kwa amri ya Mungu; Kama Kristo aliwatuma manabii kwa kipindi cha miaka elfu ili kuwaonya Israeli ili wazishike (soma Amosi 8:5); na kama Kristo na kanisa la kwanza walizishika, na ukweli walizishika; na kama kuna kanisa linalozishika kwa maumivu na vifo kwa takriban zaidi ya miaka 1970, na ambalo bado lipo; na, kama Kristo anakwenda kuhuisha upya umuhimu wake kwa adhabu ya kifo atakaporudi, na kwamba haya ni Maandiko Matakatifu na Maandiko hayatanguki (Yohana 10:34-35): Ndipo sasa kinachofuatia ni kwa sisi wateule kufanya hivyo, na yatupasa pia kuzishika sasa. Ukweli haupingiki.

 

Ni nini basi kuhusu hali iliyopo kwamba Wakristo wengi wanashikilia kuabudu siku ya Jumapili?

Jibu: Ukweli ni kwamba waalimu wa uwongo wanawaambia watu kuwa hawalazimiki wala hakuna sababu kwa wao kuzishika amri za Mungu na hakuna udhuru. Kichwa cha kila mwanaume ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu. Wateule ni wale wazishikao amri za Mungu na Ushuhuda au Imani ya Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12).

 

Mungu alitupatia amri ya nne kwa kupitia kwa watumishi wake manabii na kuwafundisha Israeli kwa kipindi cha miaka arobaini ili kuianikiza mioyontumishi w mwao. Ni kwa nini dunia ilimficha mwanamke jangwani kwa miaka 1260 ya dhiki kuu iliyoandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo? Ni nani basi aliyekuwa akilitesa kanisa? Majibu yake yanapatikana kwenye majarida ya Mgawanyo Mkuu wa Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 122) na Jukumu la Amri ya Nne na Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170).

 

Kristo alisema kuwa walioitwa ni wengi lakini wateule ni wachache. Wateule wamejulikana tangu mwanzo kwa uweza wa milele wa Mungu wa kuelewa kila jambo. Wamejulikana tangu mwanzo, kisha wachaguliwa na kuitwa na kasha wametakaswa na kisha wakatukuzwa. Na ndiyo maana Biblia inasema kwa mifano. Inafanya hivyi ili watu wasiielewe na wakageuka kabla hawajakusudiwa kuitwa. Na ndiyo maana Kristo atakaporudi watamuita Bwana, Bwana, na atawaambia Siwajui ninyi kamwe.... Ndiyo maana alisema: Ukinipenda utazishika amri zangu.

 

Je waabudu siku ya Jumapili hawatakwenda mbinguni?

Jibu: Hakuna hata mmoja wa watu hawa wanaotangatanga visiwani katika “roho” kwenye Jumapili aliyeitwa. Hakuna hata mmoja wao atakayekuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza. Iwapo kama unataka kuwepo kwenye ufufuo wa kwanza, basi zishike amri za Mungu na imani ya Yesu Kristo kwa upendo kama ulivyonenwa kwenye 1Wakorintho 13. Pia soma jarida la Ufufuo wa Wafu (Na. 143).

 

Kama kanisa lilivyomwambia mfalme huko Rumi katikati ya karne ya pili: “Unapowasogelea wale wanaosema kuwa ni Wakristo na kwamba wanapokufa wanakwenda mbinguni basi hao ni Wakristo.” Ni lipi fundisho la kutenganishwa kwa nafsi ya ubinadamu na umbinguni ya Kristo ni kama fundisho la Mpingakristo ilikuwa ni jaribio la kuashiria au kumjua Mkristo wa kweli katia karne ya kwanza na ya ili lingali linaendelea bado kutumiwa kama jaribio la kumuelewa mfuasi wa kweli. Mshika Sabato hii ya Siku ya Saba wa kweli ndiye ishara au alama za kweli za Kanisa hilo.

 

Kwa kusema kweli, Yesu alisema kuwa yeye alikuwa Bwana hata wa Sabato na Paulo aliwaambia kanisa fulani kwamba wanapaswa kuwa waalimu baada ya kwenda kanisani mara nyingi na kuhubiri habari za wokovu na mafundisho kama hayo. Sasa kwangu mimi naona kama ukiisoma Biblia utaijua na kuielewa sawa tu na kama alivyo mhubiri mwingine yeyote. Na kama unasema kuwa sisi, ndiyo tulioitwa, basi tunakuwa wateule kwa kuwa tu Wakristo kwenye Kanisa la Sabato, ambalo hatimaye linatuita sisi kuwa mara zote tuwe tayari kuyafanya mapenzi ya Mungu kama tunavyotakiwa, kama vile kulisha kondoo wake. Je, huwezi kumtoa shimoni mmoja wa kondoo zake hata siku ya Sabato? Je, ni vibaya au dhambi kutenda mema siku ya Sabato? Je, hutakuwa unafanya kazi nguvu siku ya mapumziko? Hata hivyo, hawakuwa makuhani kipindi cha kabla ya Kristo walishughulika kwa kazi ya kuchinja wanyama waliohitajika kwa ondoleo la dhambi na walijua kuwa Kristo atafanyika kuwa mwanakondoo wa sadaka? Kwangu mimi naona kuwa siku zote ni Sabato tu.

Jibu: Kristo alisema: Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka, hata yote yatimie. Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.

 

Kama Kristo aliivunja Amri ya Nne, basi sio Masihi. Alikuwa anatuonyesha jinsi tunavyopaswa kuishika kwa mujibu wa Torati ya Mungu kwa kuwa iliwekwa kwa ajili ya mwanadamu. Mari Kumi ni Amri Kumi tu, na siyo mapendekezo kumi. Inatupasa kupandisha kiwango cha mwenendo na matendo yetu kana kwamba kila siku ni Sabato. Hata hivyo, amri ya Sabato inasimama, na ndani yake kunakamilika Torati yote na Manabii pamoja na Siku Takatifu na kumwabudu Mungu. Soma jarida la (Torati na Amri ya Nne (Na. 256)).

 

Mdahalo wetu na Wakatoliki si kama IWAPO kama inapasa kuzishia amri, bali ni kama wana haki na mamlaka ya KUIBADILISHA Sabato na kuwa Jumapili. Kristo aliishika Sabato, na Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa na Mungu. Hizi zinapatikana kwenye Kalenda ya Mungu. Sabato iliwekwa tangu uumbaji. Mitume na kanisa la kwanza wote walizishika. Kanisa la Mungu limezishika kwa kpindi cha miaka 2000 na waumini wake wameuawa kwa ajili ya ukweli huu. Hebu soma kwenye majarida ya Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170); Malumbano na Hoja za Wakuartodeciman (Na. 277); Mgawanyo Mkuu wa Makanisa ya Washika Sabato (Na. 122); Kalenda ya Mungu (Na. 156); Siku Takatifu za Mungu (Na. 97).

 

Mtazamo wanaouibua wapinga ushikaji wa sheria ulitumiwa kwa mara ya kwanza ili kuipotezea Sabato kutoka Roma, wakati ibada ya Jumapili ilipoingiwa ikitokana na dini potofu za waabudu Jua za huko. Mpango na mtazamo huu haukukubaliwa kabisa na Kanisa la Mungu. Kihistoria, wakati wote inaletwa kama shambulio kwa Kanisa na Torati ya Mungu. Ni mafundisho yaliyoanzishwa na kufundishwa na Mashahidi wa Yehova baada ya baadhi ya waanzilishi wao waliokuwa chini ya kiongozi wao mwanzilishi Russell kujiengua na kutoka kwenye Kanisa la Mungu na kuchukua fundisho hili na kujaribu kulikarabati ili lieleweke na kupendeka zaidi kwa waongofu. Ni uzushi na watahukumiwa kwa kuwafanya wale wanaolifundisha kuwa watakwenda kwenye Ufufuo wa pili wa wafu.

 

Kwa kweli, Shetani hakuwaambia watu hawa uwongo, kwa hilo amewaambia kuwa wataingia kwenye kipindi cha millennia wakiwa kama viumbe walio katika mwili. Hilo ndilo fundisho lao na hivyo ndivyo itakavyotokea kwa wale watakaobalia hai. Hata hivyo, watu hawa watakuwa wanazishika Sabato na Mwezi Mpya (Isaya 66:23), na pia watakuwa wanashika sikukuu za Mungu na kuwapeleka wawakilishi wao huko Yerusalemu. Vinginevyo mvua haitanyesha kwa muda muafaka na hatimaye watakumbwa na baa la njaa au watakumbwa na magonjwa ya tauni (Zekaria 14:16-19). Haya ni Maandiko Matakatifu na Maandiko hayawezi kutanguka.

 

Kwa ukweli hoja hii ni za uwongo sana na za kishetani, kama watu hawa wasiozishika siku zote kama Sabato. Wanafanya kazi siku za Sabato na wanakwenda kuabudu siku za Jumapili, ambavyo ni kinyume kabisa na jinsi Mungu alivyokuamuru ufanye.

 

Hawazishiki wala kuziadhimisha Siku Takatifu licha kuamriwa hivyo na hawaipendi kabisa kweli. Mungu hashughuliki na dunia kwa sasa na ni wazi sana kwamba hashughuliki nao hata wao bado kama unampenda Mungu basi utazishika amri zake. Kiilichobakia ni kumcha Mungu, na kuzishika Amri zake (Mhubiri 12:13). Uzao wa mwanamke ni wale wazishikao amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12).

 

Kama Wakristo walianza kuabudu kwa kuiadhimisha Sabato ya siku ya saba ya juma, kwa nini makanisa mengi wanakutanika siku za Jumapili sasa?

Jibu: Katika karne ya pili ya zama tulizonazo dini za waadhimisha Easter ziliingizwa kutoka kwenye dini na imani za kipagani huko Roma. Haya ndiyo yalikuwa Mabishano ya Wakuartodeciman. Soma jarida la Malumbano ya Wakuartodeciman (Na. 277). Dini ya waabudu Jua ilikuwa ndiyo mhimili mkubwa wa imani hii. Krismas chanzo chake hasa kilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa mungu jua anayehudumu kwenye majira ya baridi kali ya ncha ya kaskazini. Easter ni jina la mungumke Easter na ni mshirika au kimada wa Baali aliyejulikana kama Easter, au Istar, au Astarte. Mungu mfu alikuwa ama Attis kwa upande wa maskazini huko Roma, au Adonis kwa upande wa Mashariki huko Ugiriki na ushawishi wao.

 

Wamisri walimuombolezea Osiris. Hii iliitwa Ijumaa ya kusulibiwa au ya mateso na walisherehekea Kufufuka kwake siku ya Jumapili. Maadhimisho ya kufufuka kwa siku ya mungu Jua kulikuwa ni sehemu ya imani ya dini hii ya mungu wa Utatu. Soma kwenye jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235).

 

Sabato ilipingwa na kushambuliwa na kupingwa vibaya kwanza huko Roma kwa ibada za pamoja na utaratibu wa kutoa komunio siku ya Jumapili, ni kama ilivyokuwa kwenye imani za waabudu jua. Na hii ndiyo sababu inayopelekea kila mwaka Pasaka inaambatana sambamba na maadhimisho ya Easter. Mnamo mwaka 300, baraza la mtaguso wa Elvira liliyanenea vibaya maadhimisho haya, na mwaka 325 imani na maadhimisho ya Easter yalialalishwa na kurasimishwa kwenye Dola yote na imani ya Kibinitarian ya mungu Attis ndipo iliingizwa rasmii kwenye Ukristo. Mwaka 366 baraza la mtaguso wa Laodicea uliipiga marufuku Sabato.

 

Historia ya kipindi cha mpito inakutikana kwenye kitabu kilichoandikwa na Sam Bacchiocchi (cha Kutoka Sabato Hadi Jumapili [From Sabbath to Sunday], Pontifical Gregorian University Press Rome, 1975). Mwaka 381 imani ya Utatu ilibuniwa kwenye Baraza la Mtaguso wa Constantinople na mwaka 451 huko Chalcedon muundo wa imani hii ulikamilika. Wayunitariani, hasahasa wenye asili ya Parthian, waliukataa uzushi huu mpotovu na ndipo vita vikaanza.

 

Wakati wa kuzinduliwa kwa iliyokuwa ikijulikana kama Dola Takatifu ya Rumi, Sabato ilipigwa marufuku na waliokiuka marufuku hii na kuishika waliteswa pasi huruma popote walipoonekana kufanya hivyo (soma jarida la Vita vya Wayunitariani na Watrinitariani (Na. 268)). Dini nyingi zilizoko leo ni matokeo ya kukengeuka huku kutoka kwenye kweli kutokana na mateso au kuteswa kwa makanisa yanayoishika Sabato. Historia yake inakutikana kwenye majarida ya Mgawanyo Mkuu wa Makanisa ya Mungu Yanayoshika Sabato (Na. 122) na Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170). Makanisa mengi ya waabudu Jumapili wameipotezea Pasaka, na kisha kuikataa asili na tabia ya Mungu. Wamefungiwa kwenye mfumo mzima. Na sio ni kuabudu siku ya Jumapili peke yake. Bali ni pamoja na Krismas na Easter, ni pamoja na kumuabudu mungu Utatu. Jisomee hayo zaidi kwenye majarida ya Fundisho la Dhambi ya Asili Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246); Imani za Kuwa Sawa za Kiariani na Uyunitariani (Na. 185); Ubinitariani na Utrinitariani (Na. 76); Kuwa na Hadhi Sawa na Baba (Na. 81); Mteule Kama Elohim (Na. 1) na Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127).

 

Kanisa la kwanza lilifanyaje kuhusu ibada?

Jibu: Wakolosai 2:16 inaonyesha kuwa kanisa lilikuwa linazishika Sabato zote na Miandamo ya Mwezi na Siku zote Takatifu. Inasema kuwa mtu na asiwahukumu kwa kuzishika siku hizo, bila kuzipuuzia. Kitabu cha Matendo kinaonyesha wazi kuwa kanisa zima lilikuwa linazishika sikukuu na Sabato na hapa Miandamo wa Mwezi. Sisi tumedumu kuzishika pia kwa takriban miaka 1971. Waliishika Pentekoste au vinginevyo wasingempokea Roho Mtakatifu (Matendo 2:1). Injili zimechafuliwa kwa kubadilishwa maeneo yanayosema utunzaji huu wa sikukuu, jinsi alivyokuwa anazishika zote Kristo na mitume. Mtume Paulo alizishika nah ii inayatafsiri maandiko yake (Matendo 12:3; 20:6). 1Wakorintho 5:7-8 inaeleza jinsi inavyotupasa kuishika Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.

 

Kanisa liliiadhimisha Siku ya Upatanisho (Matendo 27:9). Huwezi kujua mpango wa wokovu bila kuzijua siku takatifu za Mungu. Kristo alikuwa ndio Pasaka na Mganda wa Kutikiswa. Alituamuru kuiadhimisha Meza ya Bwana kwenye usiku aliosalitiwa ambayo ni siku ya 14 Abibu. Hakuna andiko hata moja lililoibadilisha Sabato na lililoliambia kanisa lisishike Sabato, Miandamo ya Mwezi na Sikukuu, likiwemo andiko la Wakolosai 2:16. Mtume Paulo aliwapangia utaratibu wa kukusanya changizo kuwa ufanyike Siku ya Kwanza ya juma kwa kuwa ilikuwa haikufanyika siku ya Sabato na hili ndilo andiko pekee lililopo na linaloonyesha walikutanika siku ya kwanza ya juma au Jumapili. Na hata siku yenyewe inayoitwa kuwa kuwa ni Siku ya Kwanza ya Juma kwa kweli ni Sabato ya kwanza ya hesabu ya kuelekea kwenye idi ya majuma kwa Kiyunani.

 

Krist alisema usipoula mwili na kuinywa damu yake, huna ushirika naye. Kwenye usiku aliosalitiwa alisema: Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
Vivyohivyo akakitaa kikombe kwenye mlo huo na kusema: Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu. (Luka 22:19-20)

 

Ni kwa wazi kiasi gani inafanyika? Tunaadhimisha Meza ya Bwana pamoja na Pasaka na Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa kuwa imeamriwa. Tunaadhimisha kumbukumbu ya mwanakondoo saa 9 jioni, siku ya 14 Abibu kwa kuwa tumeambiwa tuishike Pasaka nje ya malango yetu kama alivyofanya Kristo na tunakumbuka kuwa katika kipindi hiki ndipo pazia la Hekalu lilipasuka katikati na kufanya iwezekane sisi kuingia Patakatifu pa Patakatifu. Tunakutanika kuadhimisha ukumbusho wa Mganda wa Kutikiswa majira ya saa 3 asubuhi, siku ya Jumapili asubuhi kwa kuwa Kristo ndye alikuwa limbuko na aliingia kwenye Kiti cha enzi cha Mungu wakati huo na akarudi kwa uweza wa Roho Mtakatifu na kufanya iwezekane kwetu sisi kuwa wana wa Mungu. Tangu hapo ndipo tunaanza kuhesabu muda wa kuelekea kwenye Pentekoste na kwenye mavuno yetu. Tunangojea uamsho na urejesho wa Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste saa 3 asubuhi wakati tunapotakiwa kufanya hivyo. Tunamngojea kwa hamu kubwa Masihi tangu kwenye ibada zetu hadi siku ya ukumbusho wa kuzipiga Baragumu.

 

Mungu anatutaka tujitese kwa kufunga saumu ili kuzitesa nafsi zetu pasipo kuwakwaza na kuwataabisha wengine, na kushindana na maadui zetu. Amesema hataisikia saumu kama hiyo wala maombi ya mtu kama huyo. Bali yatupasa kufunga saumu kwa ajili ya kuvunja nira za uovu na kutuweka huru kutokana na matendo ya dhambi, uongo na maovu. Yatupasa kupendana na kusema kweli pasipo hila.

 

Saumu hii ni ya tangu jioni ya siku ya kwanza hadi jioni ya siku ya ili, na inamaanisha kutokula chakula chochote wala kunywa maji kipindi chote cha mfungo huu. Kwa habari ya siku hii ya Upatanisho, ni mfungo wa masaa 24 tangu jioni ya kwanza hadi inayofuatia na kama mtu hatafunga saumu hii, basi ataondolewa mbali kutoka taifa la Israeli, ambalo ni Kanisa lililo chini ya Kristo. Huwezi kuwa Mkristo na ukawa hushiriki mfungo huu wa saumu siku hii (isipokuwa kama itakuwa imethibitika kuwa ni hatari kwake akifanya hivyo).

 

Mitume waliushika mfungo huu na imeandikwa kwenye Matendo 27:9. Saumu unatakiwa kufanywa ukiwa umeosha sura yako na uwe safi, na uvae vizuri na umuombe Mungu na kujisomea maandiko. Kama utawapa chakula wenye njaa na kuwainua na kuwasaidia wanaoonewa basi atakusikia umuombapo.

 

Ikiwa tutaenenda mbele zake kwa unyenyekevu na kujinyima au kuachana na ubatili na kuyanena maovu ya wengine, ndipo atasikia na kutuongezea uwezo wa kuelewa kushughulika nasi kwa wema. Afya yetu itaboreka sana na atatulinda wakati wa ukame. Watu wetu watapajenga mahali palipobomoka, na kisha tutaijenga misingi ya vizazi vingi na tutaitwa wajenzi wa mahali palipovunjika. Mfanya marejesho mapya wa njia za kuishi ndani yake. Safari ya miaka elfu moja inaanzia hapa kwa hatua hii ya kwanza. Soma jarida la Tufundishe Jinsi ya Kuomba (Na. 111).

 

Ninavyojua mimi ni kwamba kulikuwa na mabaraza 4 kwenye historia ya mwanzoni. Kama sikosei, ilikuwa ni mitaguso ya Nicaea, Laodicea, Constantinople, na Chalcedon. Nijuavyo mimi pia ni kwamba kulifanyika mabadiliko mengi sana ambayo yalianzishwa kinyume na imani ya kweli ya kanisa la kwanza kwenye mitaguso hii. Unaweza tafadhali kuelezea japo kwa kifupi kuhusu mabadiliko gani yaliyofanywa kwenye kila mmoja wa mitaguso hii, na ni kwa kiasi au namna gani mabadiliko haya yameiathiri imani halisi nay a kwanza ya kanisa?

Jibu: Kuna mitaguso minne ambayo ni:

Nicaea mwaka 325: Mtaguso huu ulianzisha imani ya Muundo wa Kibinitariani na walimuinua Kristo kuwa ni kama Mungu wa kweli. Mtaguso huu pia ulirasimisha maadhimisho ya Easter, sikukuu iliyoingizwa ikitokea kwenye dini za kipagani za miungu Attis na Adonis na pia ilikuwa ikiabudiwa kwenye dini za Wamisri. Tarehe za kuadhimisha zilitofautiana upande wa Mashariki na Magharibi kwa wafuasi wa miungu hii ya Attis na Adonis. Hii ilibadilika.

 

Kanuni na maazimio ya mtaguso huu zilipotea na kile kilichojulikana kama Tangazo la Ukiri wa Imani la Nicaea kwa kweli ni tangazo la ukiri wa imani la Mtaguso wa Constantinople mwaka 381. Mtaguso wa Laodicea ulianzisha kanoni au sheria 29 zilizotumika kupiga marufuku kuiadhimisha siku ya Sabato na badala yake ikaingizwa Jumapili. Hali hii iliendelezwa na baraza la mtaguso wa Elvira mwaka 300, ambapo walijaribu kuihalilisha Jumapili ichukue rasi mahala pa Sabato, ila ilishindikana baada ya kuanzishwa tena kanisa la mrengo wa Kiyunitariani baada ya mwaka 327 na kutudishwa tena kwa maaskofu wa Kiyunitariani, kulikofanwa na Constantine.

 

Mwaka 358, Wayahudi walianzisha Kalenda mpya ya Hillel na mfumo wa uahirisho. Mwaka 381, baada ya uahirisho wa mzaliwa wa Hispania aitwaye Theodosius na Gratian, Mtaguso wa Constantinople uliitishwa. Imani ya Utatu ilianzishwa na Wakapadokian na waliikubali kwa sehemu.

 

Mwaka 375, Krismas iliingizwa kanisani kutoka Syria na mnamo mwaka 386 imanii hii ilifika hadi Yerusalemu na mungu wa Utatu aliingizwa rasmi na kuanza kuabudiwa kwenye imai ya Kikristo. Mwaka 450-451 huko Chalcedon, imani ya Utrinitari na muundo wake wa imani mpya vilikubalika. Mgawanyiko huu ulipelekea kuanzishwa kwa Kanisa la Coptic, lakini sikukuu za kipagani za Easter na Kristmas ziliingizwa, na katika karne iliyofuatia kulishuhudiwa kuingizwa kwa imani nyingine ya kipagani ya kumuabudu mungumke aliyeingizwa kwa jina la Maria na ibada zake za kusali kwa kutumia shanga, viliingizwa kwa uvamizi huu.

Soma majarida ya Cheanzo cha Krismas na Easter (Na. 235); Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127); Kuendelea kwa Mtindo wa Uplatoni Mamboleo (Na. 17); Kuwa Sawa na Baba (Na. 81); Roho Mtakatifu (Na. 117) na Ubinitariani na Utrinitariani (Na. 76).

 

Ni kina nani walikuwa Mababa wa Kanisa? Niwajuao mimi ni kina Clement, Augustine, Athanasus, Eusebius, nk. Niliiona orodha yao kwenye tovuti ya Wakatoliukuliwa kama mababa wa Kanisa “Katoliki la Roma.”

Jibu: Watu hao walioorodheshwa waliitwa mababa wa Kanisa, kwa maana kwamba walikuwa waalim na wanateolojia wa kanisa waliofundisha imani ya kweli ya kanisa kwenye matawi yake mbalimbali. Kanisa Katoliki la Roma kama tujuavyo sote halikuwepo huko nyuma hadi mwaka 381.

 

Kanisa liliitwa Kanisa Katoliki kwa maana kwamba lilikuwa la ulimwenguni kote, na hawa “mababa” hawakuwa wanakubaliana wote na Roma, na wengine hawakuwa hata na ushirikiano nalo. Tertullian, kwa mfano, mwanzoni alikuwa anashirikiana na Roma, lakini akawa ni wa mrengo wa Wamontana na alipingwa na kuthibitiwa sana na Roma.

 

Irenaeus, askofu wa Lyon, alifundishwa kwenye Shule ya Mtume Yohana chini ya Polycarp wa Smyrna, na hakuwa hata amepangiwa na Roma. Athanasius na Augustine walikuwa kwenye mstari wa walioyashadidia na kuendeleza mawazo mapotofu ya Warumi. Fundiso la Wapinga maazimio ya Mababa wa Nicaea kuhusu asili ya Mungu waweza kuyasoma kwenye jarida la Teolojia ya Mwanzoni Kuhusu Uungu (Na. 127). Hili litakuonysha mtiririko wa kimawazo.

 

Ibada za Kipagani

Hatuini Easter ikitajwa mahali popote kwenye maandiko ya Agano la Kale na kwa hiyo tunapenda kujua chimbuko la sikukuu hii ni nini na neno hili linatokana na nini?

Jibu: Neno Easter ni la Kianglo-Saxon la munumke (soma kamusi ya Oxford Universal Dictionary). Mungumke huyu anaitwa pia Istar au Ostar. Kwenye Biblia anaonyeshwa kuwa ni mwenzi au mke wa Baali kama “Ashtaroth” (SHD 6252). Wakati mwingine, anaitwa pia “Ashteroti.” Sulemani alishiriki ibada za sanamu kwa kuadhimisha sikukuu hizi na kuabudu, yaani sikukuu ya Easter.

 

“Ashtar” ni shina la kina lililopelekea kuitwa kwa jina hili la Easter. Lugha za muungano wa Anglo Saxon ndizo ziliunda kwa pamoja jina hili Ashtar kutoka kwea Israeli wa kale. Watu wa Austria walikuwa na jina waliloiita nchi yao lililoitwa kwa ajili yake mnamo mwaka 996, ambalo lilianzishwa na Ostarrichhi au ufalme wa Ostar. Soma kwenye jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235).

 

Hatuioni Easter kwenye maandiko ya Agano la Kale ikiwa kama miongoni mwa sikukuu za Mungu, tungependa kujua ni wapi wazo la kuabudu na kuiadhimisha siku hii lilitokea?

Jibu: Sikukuu au maadhisho ya mungu mfu ilikuwa ni sehemu ya imani na maadhimisho ya Easter ya Wababeloni. Sikukuu hii ilikuwa inaadhimishwa na waumini wa mungu Attis upande wa Magharibi, na Adonis kwenye ulimwengu wote ulioathiriwa na mafundisho ya Kihellen upande wa Mashariki, na Osiris, na mungu mfu wa Wamisri. Dhana iliyoko ya Kusulibiwa kwa Kristo siku ya Ijumaa na kufufuka kwake Jumapili inatokana na itikadi ilikuwa inafanywa kwenye dini hii potofu. Mti wa msonobari ulikuwa ni mti mtakatifu kwenye dini ya Attis ambao ndio alisulibiwa juu yake.

 

Wakati Ukristo ulipoanza kuwa maarufu na kushamiri huko Roma, wafuasi watiifu wa dini zenye maana za Kisirisiri,a hasahasa dini ya Attis, waliingia kwenye Ukristo na wakaiingiza imani Easter na maadhimisho yake. Maaskofu wa Roma walijaribu kuipinga na kuipiga marufuku mwaka 152 BK chini ya Anicetus bila mafanikio. Bali waliiadhimisha huko na kwenye miaka ya 190-192, Victor aliingiza a kuiruhusu na akaligawa Kanisa. Haya yaliitwa Mambishano ya Wakuartodeciman. Soma kwene jarida la Mabishano ya Wakuartodeciman (Na. 277).

 

Yawezekana kuwa kwamba imani ya Utatu ni aina nyingine ya ibada za sanamu, wakati kwamba tofauti pekee ni kwamba sanamu haziabudiwi ila ni nabii wa Mungu? Inawezakuwa kwamba bado watu ni wajing au hawajui? Ni maana, Wakristo wanasema kuwa Mungu ni mmoja, lakini hudhani kwamba wanamgawanya?

Jibu: Imani ya Utatu inatokana na fundisho la mungu wa Utatu. Kuna watu wengi wasiojua kuwa ni waumini wa Utrinitarian ambao ni waumini wa Kanisa la Utatu, lakini hawayaamini maneno haya. Wangali wakimuabudu bado Mungu mmoja wa Pekee na wa Kweli, ambaye ni Baba, kwa jina la Mwanae Yesu Kristo, na hawamchukulii Kristo kuwa ni Mungu.

 

Wao kwa kweli ni Wayunitarian. Kwenye Kanisa la Kipresbyterian miaka elfu mbili iliyopita, ingekufanya kuwa vigumu sana kutofautisha na Watrinitarian wa kweli. Viongozi wengi wan chi ya Marekani walikuwa wa Yunitarian. Jefferson alidhani na kutamani kuwa angeona nchi yote ya Marekani wakiwa Wayunitarian. La kusikitisha sana ni kwamba tangu siku hizo za imani iliyopendwa yenye kuonewa mashaka, ndipi ilirudi nyuma kwenye nchi iliyopupumbazika. Mababa Wahamiaji walikuwa Wayunitarian, na waliteswa kwa sababu ya kuamini hivi na kwa kuishika kwao Sabato mara tu baada ya kuanzisha kwao koloni. Fundisho la kwamba Mungu na Kristo ni sehemu ya Mungu mmoja huyohuyo, ni fundisho la mungu Attis, na yeyote anayemtenganisha Kristo na ubinadamu au asiyekiri kuwa ni mwanadamu na kwamba si Mungu ana mafundisho ya Mpingakristo. Soma majarida ya Asili ya Mungu ambayo ni Programu ya Kujifunza Biblia (Na. B1); Torati na Amri ya Kwanza (Na. 253) na Amri Iliyokuu na ya Kwanza (Na. 252).

 

Wazo la kuwaomba miungu mingine, au watakatifu na masalia ya wafu, ni ibada ya sanamu kabisa na isingeweza kuvumiliwa kwenye Kanisa la kwanza. Mungu anaichuza mioyo ya watu na anawajua wasiopiga magoti yao kwa Baali. Taifa linalindwa na hali yake ya kawaida ya watu waaminifu. Watakatifu walio kwenye nchi hiyo hulitakasa. (Soma majarida ya Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) na Utakasi Kwa Ajili ya Dhambi Zilizofanywa Pasi Kukusudia (Na. 291).)

 

Mpingakristo

Biblia ilipasa kusema kuwa mpingakristo atakuja na kujaribu kuanzisha mkakati wa kurejesha ushikaji tena wa Torati ya Musa. Unaweza kunipa rejea ya Maandiko Matakatifu yanayosema hivyo?

Jibu: Hakuna andiko kama hilo popote. Wahubiri wa Kiprotestant nchini Marekani wanasema kuwa Mpinhakristo ataanzisha tena mchakato wa kuzishika Amri na Torati ya Musa. Lakini hilo ndilo hakika tunalopasa kulitarajia kufanywa na Kristo kwa mujibu wa maandiko ya Biblia.

 

Kwa mfano, Kristo atarejesha tena ushikaji wa Sabato, na Miandamo ya Mwezi, na sikukuu (Isaya 66:23). Watu wote watawapeleka wawakilishi wao huko Yerusalemu kila mwaka kwenda kuishika sikukuu ya Vibanda, vinginevyo hawatapata mvua kwa wakati wake (Zekaria 14:16-19). Hii inamaana kuwa utazishika Sheria za Mungu na na Sabato zake, vinginevyo utakufa kwa njaa.

 

Unaweza kuniambia mafundisho ya Mpingakristo ni yepi? Pia, je, unadhani kuwa Mpingakristo yungali hai bado?

Jibu: Mafndisho ya Mpingakristo yaleelezewa kwenye 1Yohana 4:1-2. Andiko lililo kwenye Biblia sasa limebadilishwa kulinganisha na lilivyoandikwa kwenye maandiko yake asilia. Andiko sahihi la zamani linapatikana kwenye kitabu cha Irenaeus, Sura ya 16:8 (soma jarida la ANF, Vol. 1, fn. Hadi ukurasa wa 443).

 

Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. 3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo.

 

Socrates Mwanahistoria anasema (VII, 32, p. 381) kwamba kifungu hiki kimepotoshwa na wale walionuia kutenganisha hali ya ubinadamu wa Yesu Kristo kuoka kwenye hali yake ya kimungu. (Soma pia jarida la Msingi wa Imani wa Imani ya Kikristo, Machapisho ya CCG publishing, fourth edition, p. 7 pia kama jarida la  Msingi wa Imani (Na. A1).)

 

Tofauti ilikuja kutoka kwenye mafundisho ya imani na ushikaji wa Easter na ya mungu Attis yaliyojipenyeza kwenye Ukristo. Ni ya imani ya mungu Attis aliyeaminika na kufundishwa kuwa baba na mwana walikuwa ni mungu mmoja, na kwamba huyu mtoto aliuawa lakini uungu wake ulidumu na kubakia. Imani na fundisho hili lilikubalika na kuingizwa kwenye imani ya Kikristo kwa Muundo wa Kibinitaiani kwenye Baraza la Mtaguso wa Niacea, na hatimaye ikapitishwa kuwa Utatu kwenye Baraza la Mtaguso wa Constantinople mwaka 381 kwa juhudi za Wakappadocians.

 

Soma jarida la Teolojia ya Mwanzo ya Uungu (Na. 127) na pia majarida mbalimbali kadhaa yanayofundisha Asili ya Mungu nay a Masihi yanayopatikana kwenye jarida la Utaratibu wa Kujisomea Biiblia (Na. B1). Mpingakristo amekuwa pamoja nasi tangu mwanzo, na fundisho hili liliendelea kanisani na sasa kwa watu wengi wanaojiita Wakristo waamini Utatu.

 

Je, Yesu atakuja kama mwanadamu kiasi cha watu kumdhania kuwa yeye ni Mpingakristo? Watu watakaobaki wanaishi baada ya theluthi moja ya wakazi ulimwenguni wameangamia, je watabahatika kufufuliwa au hata kuwa hai tu na kuwa na miili kama ilivyo sasa na kurudi kwenye mchakato wa ufufuo wa kwanza na wa pili?

Jibu: Malaika wanaweza kuwa na umbo la kibinadamu wakipenda. Viongozi wa utawala wa millennia bado watakuwa wanadamu, watakaokuwa wanawaongoza wanadamu. Israeli watawachagua viongozi wao kama isemavyo Biblia na makuhani wao watakuwepo. Wakati Keisto atakapokuja hapa watamuona na hakuna atakayeona mashaka kama wakati alipokuwa kwanza hapa duniani. Kama watawaambia kuwa yuko jangwani, nk, msiwasadiki. Kila jicho litamuona kama ilivyoandikwa atawatela mataifa yote mahali paitwapo “Armagedoni,” na kuwaangamiza wote. Kutakuwa na matenki ya kutosha na masalia yatakayoachwa kuwakimbia Israeli na mafuta ya kutuia kwa miaka mingi. Chuma kitakuwa ni chanzo cha masalia kwa karne nyingi. Watu wengi watakao pigana naye watakuwa ni wale walio kwenye Ukristo bandia au wa kipagani wa leo, na wafalme wa Mashariki. Kwa hiyo, utakuwa ni mchakato endelevu. Majarida ya Mihuri Saba (Na. 140) na Baragumu Saba (Na. 141) ni ya muhimu sana. Soma pia jarida la Baragagumu (Na. 136) na Mapitio ya Nyakati ya Zama (Na. 272).

 

q