Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[060]
Maswali Yaulizwayo Mara Kwa
Mara
Kwenye Mafundisho ya Biblia
Kuhusu Dini
Zinazofanana
(Toleo
La 1.1 20000730-20030914)
Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Dini Zinazofanana yameorodheshwa
humu ndani.
E-mail: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 2000, 2001, 2003 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote
atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja
ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kupotoshwa kwa Imani…Uislamu, Imani ya Kiyahudi, Ukristo-Gombo
za Bahari ya Chumvi-Umonotheistiki
Imani za Utatu/Uyunitariani…Makanisa machache
yajulikanayo-Usemitiki-Uarianism-Waarians
Ukumene…Mgawanyiko au mpapurano
wa madhehebu
Uislamu…Allah-Ramadhan-Korani-Khalifa-Imamu
Imani ya Kiyahudi…Kalenda ya Hillel
Waprotestanti…Shahada za msamaha wa dhambi-Martin Luther-Aliipingilia
mbali dhana hii
Upagani…Wakristo wanaupinga
Mashahidi wa Yehova…Kitendo cha kutoa damu na kumtia mwingine-Kurudi kwa Kristo-Ufufu
wa wafu-Kushushwa chini kwa Mashahidi wa Yehova
Fundisho kuhusu Roho…Imani kuhusu viumbe kubadilika badilika kwa njia ya
kuzaliwa tena na tena-Nafsi isiyokufa- Msalaba Uliogeuzwa-Wayahudi waliouawa
mauaji ya halaiki ya Holocaust-Desturi ya Kiutetezi…Ubatizo wa
watoto wadogo-Kuzaliwa Mkatoliki/kufa Mkatoliki
Wamormoni…Je, ni imani ya Kikristo-Kuwabatiza wafu-Mavazi matakatifu
Umonastiki au useja…Hiki ni kitu gani
Unostiki…Maana ya Toharani-Mbinguni & jehanamu
Tohara…Watoto
wa kiume wanaozaliwa Wakristo
Ubudha…Lengo
moja na Ukristo-Dalai Lama-Chakras-chombo cha kufanyia uponyaji
Uhindu…Je,
ni fungamano la kikumene-Rig Veda-Sikukuu za kidini
Ushamanism…Inaelezewa
kama Shamani- Roho zinazoachiliwa kutoka Pagatory
Ureemasoni…Ni
dini au klabu Umithrasism…Dini za siri za Kikosmiki
Waadventa
Wasabato…Mafundisho ya uwongo Imani
ya mchanganyiko wa Waashuru na Wababeloni…Kidole cha Ashirat-Bata
bukini-Orodha ya Eponym-Oreb & Zeeb-Mardi Gras-Pinata-Tantara
Uzoroastrianism…Ahriman
Mafundisho
ya Kimafumbo ya Kikristo…Mafundisho ya
Uzuri-Damu Takatifu & Kikombe Kitakatifu-Kaburi la Mtakatifu Yakobo-kipimo
cha nasaba cha DNA-Waherme-Dini ptofu za uwongo
Ukiri wa Imani ya Kikristo…Agizo la Kikatoliki
Imani za Kidini za Kitaifa…Mauaji ya Holocaust na Vatican-Waskochi-Waselti-Nadharia
ya Kigaia-Tara-Nadharia ya machafuko-Baraka za Toronto-maandiko ya Wasumerian
Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara Kuhusu Dini Zinazofaanana
Kuposhwa kwa Imani
Unaweza kunisaidia kunijulisha
misingi ya imani ya dini za Kiislamu, Kiahudi na Kikristo? Mimi nataka pia kulinganisha
nione kama zinafanana au hazifanani.
Jibu: Uislamu ulianzia kwa Adamu, na imani ni ile ile
haijabadilika hadi kwa kina Nuhu, Ibrahimu, na Mababa wa imani. Imani za Kikristo,
Kiyahudi na Kiislamu zinaaminika kuwa zote zimetuama kwenye mrengo wa Biblia na
Torati ya Mungu. Lakini zimejikuta zote zikipoteza mwelekeo wao na kugawanyika
kwa maana ya kushikilia mambo yake kila moja ikiwa imara na thabiti. Tunatarajia
kujionea mambo zaidi na kukabiliana kwenye Vita Kuu ya III ya Dunia.
Gombo za Bahari ya Chumvi zinakomesha utata wa madai ya
Uislamu kwamba nakala halisi ya Biblia yenyewe alisia ilipotea. Maandiko gushi
na makosa ya kiutafsiri yaliyo kwenye tafsiri ya KJV havisaidii kuiimarisha
hoja hii. Imani ya Kiyahudi iliyopo sasa imetokana na uanzishwaji kiupotoe wa
mapokeo uliofanyika kipindi cha baada ya kubomolewa kwa Hekalu, mkakati
uliotuama kwenye mapokeo tu, yanayoifanya Biblia kuwa kituko au kichekesho na
watu mara nyingi husema kinyume na kile ambaho Biblia inakusudia kukisema kwa
kweli. Jua na dini za kimafumbo na imani ya Kinostiki vimeuharibu na kuuathiri
pakubwa sana Ukristo. Makosa yaliyo kwenye Uislamu wa siku hizi yameharibu
uhusiano kati ya Biblia na Korani. Uislamu ulikamilika tu kipindi cha mtume Muhammad
na cha Makhalifa wake Wanne Waliomfuatia. Ulianza kupotoshwa tangu hapo.
Utaweza kujua na kugundua jinsi mambo haya yalipobadilika
usomapo majarida yafuatayo hapa chini: Kristo na Korani (Na. 163); Sabato Ndani ya Kur'an (Na. 274); Ijuma'a: Maandalio ya Sabato (Na. 285); Mwanzo 22, Imani za Kiyahudi, Uislamu na
Kutolewa Sadaka Kwa Isaka (Na. 244). Soma pia mkururu wa majarida ya Torati ya Mungu (Na. L1); Kalenda ya Mungu (Na. 156) na Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235). Utakuja kujionea
mabadiliko makubwa yaliyotokea kipindi hiki cha baada ya kubomolewa kwa Hejalu kwenye
dini zote tatu na upotoshwaji mkubwa uliofanywa na dini tatu zote kwa ushawishi
wa kisiasa.
Sasa, Gombo
hizihizi za Bahari ya Chumvi hatimaye zimetoa hadharani, angau sehemu Ukristo
umerudisha mafundisho mbalimbali au kwa namna ileile, yameimarisha mafundisho
yaliyoaminiwa kwa muda mrefu wakati ushahidi ulipodhihirika kuonyesha ni nakala
gani yenye mafundisho yapi. Tunaone haya yakitokea ndani ya ama Uislamu au imani ya
Kiyahudi?
Jibu: Kwa hiiyo, ugeni kama unavyoonekana, wote wanajaribu
kupuuzia kwa shingo ngumu tu gombo hizi. Uislamu unadai kwa karne kadhaa kwamba
hawahitaji kuzishika sharia za Torati, kwa mintaarafu ilivyo kwenye Biblia, kwa
kuwa hazipo sawa na maandiko asilia yaliyoandikwa na Manabii na Hekalu.
Hivyo basi, sasa tuna uthbitisho, wanaojaribu kuupuuzia
au kukataa ukweli Gombo hizi za Bahari ya Chumvi zinaonyesha tuliyonayo ni
nakala halisi kabisa yenye masahihisho kadha machache ambayo yanajiri yafanyike
kwa kuwa Marabi wa Kiyahudi waligeuza au kupotosha maandiko baada ya kuanguka
kwa Hekalu (kwa mfano, Kumbukumbu la Torati 32:8 ni mojo wapo). Tafsiri ya Talmudi
ya Kiyahudi imepotosha Biblia pia, kwa hiyo wamepofuka na wamefanya hivyo kwa
makusudi kabisa.
Niliambiwa kuwa
dini hizi tatu kuu za Ukristo, Uislamu na ya Kiyahudi zote ni za mrengo wa
kuamini Mungu ni mmoja au Umonotheitiki. Je, ni kweli, na unaweza kunifafanulia?
Jibu: Dini tatu za Ukristo, Uislamu na ile ya Kiyahudi zote zimetuama
kwenye imani moja na ni ya kuamini Mungu mmoja au za kimonotheism. Utheism wa Kirazini,
Biblia, na imani tatu zilizotokea ndani yake kwa hakika zote ni za Kimonothiki.
Tatizo linainuka wakati tunapoona kuibuka kwa ushawishi
au kuingizwa kwa imani zinazotokana na dini za mungu jua na imani za kipagani
za mungu wa Utatu zilizoingizwa ndani yake. Ukristo kwa imani yake ya utatu,
haupo tena kwenye imani na kuabudu Mungu mmoja au umonotheism. Uislamu
unapojijumuisha kwenye imani ya utatu, karibu na asemavvyo Ali, inajiondoa pia
kwenye umonotheism.
Mfumo w imani ya kimonotheism inatuaama kwenye uwepo wa
Mungu wa pekee na wa Kweli, ambaye ndiye pekee asiyeweza kufa wala kupatwa na
madhara na ambaye katika yeye ndipo viumbe wote wanaishi na kushughulika. Kwa hiyo ndiyo umonotheism na huo ndiyo msimamo na
Fundisho kuu la Biblia. Somo hili limefundishwa kwa kina kwenye jarida la Mungu Amefunuliwa, Sura ya 1 Umonotheism wa Kale (Na. G1).
Imani za Utatu au Utrinitarian/Uyunitarian
Ni Makanisa yapi
machache yanayojulikana kama hayapo kwenye mrengo wa Utatu? Imani nyinginezo ni
zipi? Makao yao makuu yako wapi?
Jibu: Kanisa la Kikristo liligawanyika kwenye makundi mawili.
Waamini Mungu kuwa ni mmoja, maarufu kama Wayunitarian na waamini Utatu au
Watrinitarian, mgawanyiko uliojitokeza au kusababishwa na mabaraza ya makanisa
tangu karne ya nne. Kwenye karne mbili za kwanza, kila mmoja alikuwa
Myunitarian akiamini kuwa Kristo alikuwa ni Malaika Mkuu wa Agano la Kale. Watrinitarian
hawakuwepo kwenye Ukristo. Kulikuwa na wapagani huko Roma waliokuwa wakikuwa
wanaabudu Jupiter, Juno, na Minerva Bikira asiye na Doa.
Imani ya Kibinitarian ya waabudu mungu Attis iliingia kwenye
Ukristo kutoka Roma na pia mungu Adonis kutoka mashariki. Imani hii iliingizwa
kwa kuichukuliwa Umaboleo katika karne ya tatu na kwa kufanyika kuwa
Ubinitarian huko Nikea au Nicaea mwaka 325 katika karne ya Nne. Baada ya
kuingizwa imani ya utatu kutoka Constantinople mwaka 381, imani iligawanyika tena.
Iligawanyika pia kwa kuingizwa kwa sikukuu na sherehe za Easter katika karne ya
Pili. Soma kwenye jarida la Hoja na Mabishano ya Quartodeciman (Na.
277) na Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235).
Waamini kuwa Mungu ni mmoja, au Wayunitarian walipigana
vita na waamini Utatu au Watrinitarian kwa kipimdi cha karne kadhaa. Toma jarida la Vita vya Wayunitarian/Watrinitarian (Na.
268). Hawa Wayunitarian walikuwa pia ni washika Sabato. Kwa makosa makubwa
waliitwa Waarian. Familia ya mtume Muhammad walikuwa wa mrengo huu wa washika Sabato.
Kwenye karne ya nne, Kanisa la Abyssinia lilimtuma askofu
wao mkuu Mueses kwenda China akipitia India. Alianzisha Ukristo huko China, ambao
waumini wake walikuwa Wayunitarian washika Sabato. Wengi wa watu hawa waliunda
pia misafara na mjumuiko wa kibiashara na Waarabu ambao walikuwa ni Waislamu.
Watu hawa walikuja kujulikana kama wa Hue Hue. Maelezo yake kwa kina
yanapatikana kwenye jarida la Migawanyo Mikuu ya Makanisa Yanayozishika
Sabato (Na. 122). Washika Sabato wangaliko bado nchini China na idadi yao ni takriban
milioni moja. Wengi wao walilelewa kiroho kwenye imani potofu ya Kisabeliani na
sasa wanatofautiana na mafundisho asilia ya kanisa la kwanza. Wengi wao
humchukulia Yesu kuwa ni Mungu na Baba.
Wakati wa Matengenezo, Kanisa la Wayunitarian
liligawanyika makundi mawili. Moja lilikuwa ni la Wayunitarian wahfidhina,
ambalo lilitokana na makundi ya Kiprotestanti na waliabudu siku za Jumapili
ambayo ni siku ya Wakatoliki. Kundi linguine lilitokea na Kanisa la wa
Waldeansian waliokuwepo hata kabla ya kipindi cha Matengenezo, na walikuwa
washika Sabato. Uzao wao bado wapo huko Ulaya hata leo. Tatizo linaonekana
kwenye majarida ya: Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya
Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170) na Usosiniani, Uariani na Uyunitariani (Na. 185).
Imani hii ya Uyunitariani wa kiafidhina inakataa fundisho
la kwamba Kristo alikuwepo duniani kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi
hapa duniani na, kwa usemi wa kihistoria ni kwamba, ni ubunifu au uvumbuzi
uliotungwa hivi karibuni tu. Imani ya Kiislamu iliendeleza pia dhana hii kwa
ufanisi mkubwa hapo mapema. Sio Uyunitarian wenyewe asilia, au hata mafundisho
ya Kiislamu, wala hata imani ya Kiyahudi ya Kibiblia humkubali Masihi. Historia
ya kile kilichotokea kwenye Kanisa la huko Transylvania inakutikana kwenye
kitabu cha Rabi Samuel Kohn, cha The
Sabbatarians in Transylvania [Wasabato wa Transylvania], CCG Publishing,
USA, 1998. Pia soma jarida la Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Hapa Duniani
(Na. 243) kwa kujipatia dondoo zaidi pamoja na ukiri wa imani wa Wagoths.
Hadi kufikia miongo kadhaa, Makanisa yote ya watunza
Sabato walikuwa sio waamini Utatu au Watrinitarian. Waadventista Wasabato,
yaani wa SDA walijiunga kwenye Utrnitarian, kwa urasmi kabisa mwaka 1978. Kanisa
la Mungu Ulimwenguni Kote, yaani WCG mwaka 1993/4 na Kanisa la Mungu la Siku ya
Saba au Church of God (SD) lenye makao yake makuu huko Denver lilijiunga rasmi
na imani ya Kibinitarian mwaka 1995. Konferensi nyingine nyingi zilijiunga na
imani ya kiditheist.
Makanisa mengine ya Mungu yalitangatanga kutoka
Uyunitarian, kwenda Ubinitarian na Uditheisti. Moja, ambalo ni Christian
Churches of God, ni la Uyunitarian asilia likishikilia imani ya waumini wa
karne ya kwanza. Wayunitarian wa Yuveso ndio wale wanaoitwa wa Yunitarian
wahafidhina, kama ilivyo Halmashauri Kuu ya Makanisa ya Mungu ya huko Georgia.
Nimesikia kuhusu
imani ya Kiarianism, lakini vinginevyo ni Usemi-Arianism, ambayo naiona
ikitajwa mara chache sana tu?
Jibu: Neno Uarianism linatumika ili kuifunika imani ya
Kiyunitarian ambayo inatambua na kuamini kuwa Kristo alikuwepo hata kabla
hajazaliwa rasmi hapa duniani na inajaribu kuirudisha nyuma hadi kwenye kipindi
cha Arius, mzee wa kanisa la Alexandria, na migongano iliyojitokeza kwenye
Halmashauri Kuu ya Mtaguso wa Nikea au Nicaea mwaka 325.
Kitendo ambacho kilitokea pia kwenye malumbano haya,
yaliitwa hoja bandia au dhaifu za Wamakedonia, na pia waliitwa Waarin nusu.
Wengi wa hawa kwenye orodha na matumizi ya maneno yaliyotokana na propaganda za
Watrinitarian. Soma kwenye jarida la Uariani na Usemi-Ariani (Na. 167); Usosiniani, Uariani na Uyunitariani (Na. 185); Ubinitariani na Utrinitariani (Na. 76); Roho Mtakatifu (Na. 117); Kuwa na Ushirika wa Pamoja na Baba (Na. 81) na Kuendelezwa kwa Mtindo wa Uplatoni Mamboleo
(Na. 17).
Je, unaweza
kufafanua kuhusu baadhi ya mikanganyiko kuhusu utambulisho au jinsi ya kuwajuwa
Waariani ulioibuka wakati tunaposoma juu ya malumbano kati ya vikundi vya
Wayunitarian/Waarian na Waathanasian/Watrinitarian?
Jibu: mkanganyiko ulianzishwa kwa makusudi kabisa na
Watrinitarian ili kufanya ienekane kwamba fundisho la Uyunitarian halikuwa ni
lile lililokuwa likifundishwa kwenye Kanisa la kwanza, na lionekane kama lilianzishwa
na Arius ambaye alikuwa ni mzee mwangalizi wa makanisa ya Alexandria. Wakati
mwingine inajulikana pia kama ni Ueusebiani, kwa kuwa Eusebius alikuwa ni
mkubwa sana kwa Arius. Kwa kweli Arius hakuwepo kwenye mtaguso ulioitishwa huko
Nicaea, bali anatajwa tu wakati inapoonekana kuwa muhimu, akiwa kama mshauri
wake kimashiko.
Kulikuweko pia na idadi kadhaa ya maaskofu huko ambao
wote walifundishwa mafunzo na Lucian wa Antiokia, mwanateolojia mkuu wa Kanisa
wa kipindi cha mwishoni mwa karne ya tatu na mwanzoni mwa karne ya nne. Ukweli
wa mambo ni kwamba, Arius alikuwa mmoja tu wa watu waliokuwa kwenye mstari
mrefu wa watu, kutoka kwa Kristo na kwa hata kwa Mitume, ambao wote walikuwa ni
Wayunitarian. Imani ya Utatu au Utritariani lilikuwa ni zao lililoibuka katika
Karne ya Nne.
Kwa hiyo, walikanganya jambo kwa propaganda na kuupa jina
la bandia kuwa ni Uarianism. Na waliupa mafundisho ya kizushi, wakati, kwa
kweli, mababa wote wa wakati wa Ante-Nicene walikuwa ni Wayunitarian kwa
kipindi chote cha karne mbili au miaka mia mbili ya kwanza ya imani.
Justin Martyr, kwenye ukiri wake wa imani ya Kikristo
mbele za Mfalme wa Rumi mnamo mwaka 150, alimuonyesha wazi kabisa Kristo kuwa
ni Malaika wa Yahova aliyempa Musa Torati pale Sinai. Ni vigumu kidogo
kummsingizia Justin na Kanisa la Roma kuwa ni Waarian, wakati Arius hakuwa
amezaliwa katika karne nyingine na nusu. Soma kwenye majarida ya Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127); Kuwa Mmoja na Baba (Na. 81) na Imani za Kisocsniani, Kiariani na Kiyunitariani (Na. 185).
Ukumene
Je, muunganiko wa bandia
kwenye ndama mmoja kwa namna yoyote ile ni unabii wa muungano wa siku zijazo za
mbeleni wa umoja wa kidini utakaozilazimisha dini zote kuungana na kuwa moja?
Tumesikia habari za mipasuko mingi kadhaa iliyotokea hivi karibuni kwenye
madhehebu kadhaa kama vile Walutheri na Wakatoliki. Je, hali hii itaendelea
kama ilivyowahi kutabiriwa kwa Ndama wa Dhahabu?
Jibu: Huenda tuko sahihi. Biblia inasema kuwa ni Siri, Babeli
Mkuu, Mama wa Makahaba. Kwa hiyo, ni kahaba wa kidini wa dini za Siri, ambaye kwamba,
alionyeshwa mfano wake kwa Ndama wa Dhabau, I sehemu yote ya dini hiyohiyo.
Watakusanyika wote pamoja ili kupigana na Masihi lakini wenyewe wataangamizwa
na Mnyama katika siku za mwisho. Israeli ilifanywa kula dhahabu ya ndama kwa
maana ya kuyanywa maji ya ghahabu ambayo kwayo walikuwa wamechanganyishwa
kwayo. Huo ulikuwa ni unabii tu.
Uislamu
Naelewa kikamilifu,
kwamba Waislamu wanamuabudu Allah. Je, huyu ni Mungu wao wa pekee na kama ni
hivyo, walilipataje jina lake?
Jibu: Jina la la Kiarabu, “Allah' ” linatokana na lugha ya
Kiaramu cha Mashariki au Kikaldayo, “Elahh.” Ni neno au juna la umoja na
inakubalika kuwa si jina au neno la uwingi. Ni Mungu wa Pekee na wa Kweli
aliyeandikwa kwenye Biblia yaani, “Eloah.” Ni jina la umoja “Eloah” na kwa
Kikaldayo ni “Elahh” linafanyika kuunda jina la uwingi “Elohim” kwenye lugha ya
Kiebrania na “Elahhin” kwenye Kikaldayo.
“Elohim” linaweza kuwa ni umoja kwenye matumizi na kisha linatumika
kumtaja “mmoja wa Elohim.” Ambayo imetumika kwa habari ya “Eloah” kwa kawaida
anaitwa “ha Elohim” au “Elohim” au “Mungu.” Kwenye Kiyunani, tendo hili
linaendelea kwenye Koine kama “Ho Theos” na “Theos” au kwa kuhojiwa “ton Theon”
na ni “theos” tu ni kumtaja au rejea ya elohim. Kwenye uwingi wa elohim imefanyika
“theoi.” Uislamu unamtambua huyu Mungu wa Pekee wa Kweli Yohana 17:3 kuwa ni
“Allah' ” maana ya jina hili kutokana na chimbuko lake
asilia kwa kweli inamtaja Mungu kama ni “Uweza.” Inakitaja kiambishi cha el, ambacho kinaweza kutumika kwa
kumtaja yeye mwenye nguvu au Mwenyezi na pia kwa kiambishi kinachotaja au
kuonyesha uwingi kama hawa au wale walio
miongoni mwetu. Kwa maana hii ni sawa na ilivyo kwenye Kiebrania na
Kikaldayo na ndivyo ilivyo kwenye Kiaramu na kwingineko. Kwa maana hii, ipo kwenye
umoja tu inapotumika kuwa “hawa au wao.” Hwa hiyo, ni jambo geni kuona
kuwa ni uwingi kwenye kamusi ya fasihi ya SHD 429 ambapo imeandikwa kama ‘elleh kwenye Kikaldayo ila imeunganishwa
kwa muundo kamili wa umoja Eloah. Neno hili ni sawa tu na kama Eloahh au
Elowahh kwenye lugha ya Kiebrania na linamaanisha kumtaja Mungu mmoja wa pekee.
Neno la uwingi la elohim au elahhin linatokana na uwingi kwenye
Kikaldayo isipokuwa kiambishi chenyewe kinapotumika kulifanya lionekane kama Ha elohim linalomaanisha Mungu (kama inavyoonekana kwenye SHD 430 na
maandiko mengine). Kwa hiyo basi Mungu ni nguvu au uweza unaoenea hadi
kwenye viumbe vingine vilivyopo mbinguni na anaendelea kuishi akiwa ni kama wale walio pamoja nasi. Kwa hiyo, jina
hili elohim na yahova yanatumika kwa viumbe wengi kama viumbe wake yeye Mungu
mmoja, wa Pekee na wa Kweli, na wote wanafanya kazi kwa minajiri yake. Dhana ni
sawa na ilivyo kwenye Kikaldayo au Kiebwania au aina zingine mbalimbali
zilizochukuliwa kutoka lugha hizo. Jina Allah’
ni jina linaloonyesha ukweli huu wa Uweza wa aina moja zinazotenda kazi
katikati yetu. Linabeba dhana ya uwingi peke yake kwa namna moja kama muhimu
kwenye nguvu zitendazo kazi kwa minajiri yake na inakuwa na uwezekano wa kuwa
na nguvu zake.
Waislamu hufunga saumu
kwa mwezi mzima (mwezi wa 9 wa mwandamo) kwa hiyo nilikuwa nashangaa iwapo kama
jambo hili lina msingi wowote wa kibiblia? Na kama sivyo, basi, je, Biblia
inawataka Wakristo wafunge saumu kwa mazingira mengine yoyote?
Jibu: Korani inmewaagiza waminio wautunze mwezi wa mfungo. Huu
mi mwezi wa maandalio, ambao umebadilishwa uzito wake na kufwanya kwa
mintaarafu ya imani za kipagani kama ilivyofanyika kwenye sikukuu zote zingine.
Maandimisho ya Kwaresma ni upotoshaji wa mwezi wa Kwanza
tunaotakiwa kuiadhimisha Pasaka sawasawa ilivyoagizwa kwenye Torati au Sheria
za Biblia. Imani ya kipagani iliichukua siku hii, kama inavyoonekana kuwa
ilifanyika kwenye mfungo wa Ramadhan. Maagizo ya biblia yanakwenda kinyume
kabisa na sikukuu hii na Korani inasema tu juu ya kuukumbuka mwezi wa mfungo,
ambao kwa tuujuavyo sisi ni tangu siku ya 1 Abibu Nisani hadi mwisho wa sikukuu
au idi ya Mkate Usiotiwa Chachu, ambapo ni siku ya 21 Abibu.
Mimi ni Mwislamu na
nina sababu ya kujifunza kwa kina yale yaliyoandikwa kwenye Agano la Kale – na
kwa kweli kuyachukulia kama ni kioo cha karibu sana kinachotumiwa kwenye utunzi
wa hadithi nyingi zilizo kwenye Kur’an. Sijui kabisa hata mahali pa kuanzia
kulisoma Agano Jipya. Ni kina nani alioyaandika maandiko haya? Waliishi miaka
mingapi baada ya Yesu? Na yakini, je, Wakristo wote wanayapa uzito ulio sawa
Maagano haya mawili, yaani Agano la Kale na Jipya? Nauliza hivyo kwa kuwa waongofu
wanapenda kujua jambo hili kwa ufasaha mara tu wanapoingia kwenye Uislamu.
Nadhani kwamba tuhitaji dini inayoweka pamoja mitazamo inayofanana ya historia.
Jibu: Majibu yake yanaweza kupatikana pia kwenye Korani.
Wakati lilipoandikwa Agano Jipya, kipindi hicho Maandiko Matakatifu yalikuwa ni
Agano la Kale tu. Agano Jipya ni ufafanuzi wa kusudi la unabii ulioko kwenye
Agano la Kale. Kwa hiyo, ni kama ufafanuzi tu, ni kama ilivyo Korani kuwa ni
ufafanuzi tu wa Sheria au Torati ya Mungu tu na chenyewe.
Kutokana na sura isemayo: Wale waliosimama kwenye madaraja ya vyeo,
tunaona kwamba Ufunuo wa Mungu ulitolewa tangu Adamu hadi Nuhu, na Ibrahimu
hadi Isaka na Yakobo, na Musa na Haruni, na hadi kwa Kristo na Manabii. Muhammadi
na Makhalifa Wanne Aliowaamini Walioendeleza Dini waliujua Uislamu wenyewe na
walijulikana kama Al Islam. Baada ya hapo, Uislamu uliondokana na ukamilifu
wake wa imani yake halisi.
Na ni jambo hilohilo ndilo lililowakuba waliojulikana
kama watu wa Kitabu au wa Maandiko Matakatifu. Habari zao zimesimuliwa kwa kina
kwenye majarida ya Migawanyiko Mikuu ya Makanisa ya Washika
Sabato (No. 122) na Kazi ya Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya
Mungu ya Washika Sabato (Na. 170).
Muhammadi alifundisha na kusisitiza kuishika Sabato na
akasema kwamba yeyote asiyeishika hiyo ni kama nyani mkubwa. Ni sawa tu na
ilivyo kwa Kristo na Mitume, umma wote wa Waislamu kutoka Adamu hadi Kristo
waliishika Sabato. Bali wale waliouamini uwongo waliihalifu na wakaibadili siku
ya kuabudu ya waaminio kuwa Jumapili. Pia waliingiza Easter iliyotumika
kumuabudu mungu-mke wa zamani za kale, aliyewasababishia makundi yote mawili,
yaani Waisraeli na Waarabu na Wana wa Ketura kujikwaa na kumwacha Bwana. Na
vivyohivyo, siku ya Maandalio, iliyojulikana kama Juma’ah ikabadilishwa na
kufanywa kuwa ni Ijumaa ya sala na ibada na ndipo Sabato ikasahauliwa kabisa na
Waislamu. Soma kwenye majarida ya Sabato Ndani ya Kur'an (Na. 274), na pia la Ijuma'a: Maandalio ya Sabato (Na. 285).
Kwa namna hiyohiyo, ndipo watu waongo walivyoiingiza
imani ya Utatu na kuirasimisha katika karne ya Nne. Hii ilisababisha mgawanyiko
mkubwa kwenye imani ya Kikristo. Korani inayataja makundi haya mawili. Watu wa
Kitabu au wa Maandiko wanaonekana kuanzia Sura za II. 105, 111ff., 120, 144;
III: 23, 64ff., 98f.,110ff., 186f., 199; IV. 44f., 123, 153ff., 171; V, 5, 15,
19ff., 59, 65, 68, 77, XXIX: 46; XXXIII: 26 f.; XCVIII 1 hadi mwishoni mwa;
LVII: 29.
Familia ya mtume ilikuwa na nakala ya maandiko ya Biblia.
Tunajua kwamba wakati yalipoandikwa na tunajua kwamba maandiko haya yako sahihi
yote. Gombo za Bahari ya Chumvi zinatuonyesha ni maandi yapi aliyikuwanayo na
aliyoyatumia Mtume, na kwamba yalikuwa ni sawa tu kama ya wakati Kristo na Eloah
habadiliki. Maandiko ya bandia yalibuniwa na yalichukua mahali pa maandiko
asilia ya kweli, na hatimaye, yale maandiko ya kweli yalipotezwa na Makhalifa
waliofuatia baadae, ili kuepuka msisitizo wa kuishika Torati. Ni kama alivyosema
mtume, hawakutakiwa kungojea kipindi cha ibada kipite huku wakiendelea kufanya
biashara siku ya Sabato. Watu wa Kitabu walipewa ulinzi na makhalifa hawa
Waliochaguwa Wauongoze umma, na walijulikana na kuishi na Waislamu pasi na
shida wala kero kabisa hadi kerne hii.
Agano Jipya liliandikwa na watu wa kanisa la karne ya
Kwanza. Mitume kina Mathayo na Yohana waliandika injili zao, na wanafunzi wengine,
Marko na Luka waliandika za kwao. Nyaraka zu maandiko ya Paulo nayo ni sahihi
na Kitabu cha Waebrania kinadhaniwa kilianza kuandikwa pia na Paulo na
kikamaliziwa na mwanafunzi mwingine, huenda alikuwa Barnaba. Yohana anaaminiwa
kuwa ndiye aliyeandika injili, nyaraka na kitabu cha Ufunuo, kwa ufunuo
aliopewa wakati Mungu alipompatia Masihi ufunuo huo.
Historia ya kanoni imeelezewa kwa kina kwenye jarida la Biblia (Na. 164). Hilo litakupa
madondoo zaidi. Watu wenyewe asilia hawa wa kitabu bado wapo hata sasa, lakini
ni wachache sana duniani. Imeandikwa kwenye
korani hivi: “kwa hakika tulimkabidhi Musa Maandiko Matakatifu na
tulisababisha msururu wa wajumbe wafuate baada yake, na tulimpa Yesu mwana wa
Mariamu (Mary) hakika iliyothibitishwa na tulimsaidia kwa Roho Mtakatifu.
Iliwahi kuwa kwamba wakati anapokuja kwenu mjumbe pamoja na kile ambacho ninyi
wenyewe hamkitamani, nanyi mkaendelea kujivuna na baadhi yenu mkaamini na
wengine mkawauwa?”
Je, Allah’ alikuwa ni Mkarimu, Mwenye rehema, Mungu wa
Pekee wa Kweli, aliyaacha hayo kama baadhi ya Maimamu wanavyodai? Au je, hana
nguvu au uweza wa kutosha wa kuyakamata maneno ya mitume na manabii wake kwa
wakati wote?
“Na wanasema mioyo yetu imekuwa migumu. Hapana, lakini
‘Allah’ amewalaani kwa kutokuamini kwao. Kidogo ni kile wanachokiamini.”
Ni kitu gani hiki basi na ni mtu yupi aliyekifanya?
Ameokolewa kwa mchanganyiko wa damu na maji, ambavyo vimetoka upande wa Masihi
ambaye ni Al Tarikh: Nyota mpya ya Asubuhi. Soma kwenye jarida linalohusiana na
jambo hili lenye kichwa kisemacho Kristo na Koran (Na. 163). Marida yaliyo kwenye tovuti ya www.logon.org pia yapo
yaliyoandikwa kwa lugha ya Kiarabu na lugha nyinginezo.
Agano la Kale limefafanuliwa na Agano Jipya, na Korani haiwezi
kueleweka pasipo kutumia Biblia kwa kuwa ni kitabu kinacholenga kuifafanua tu
biblia. Kuna Al Islam moja tu na imetolewa tangu mwanzoni sana na watu wote
wameagizwa kuzishika sharia zake huyu Mungu aliyehai, Eloah au Allah’. Hutoweza
kuwa Mwislamu wa kweli kama huishiki Sabato.
Je, unaweza kunielezea
Khalifa ni kitu gani? Pia ni je, huu ni wadhifa au ni mtu (vyovyote inavyoweza
kuwa), je, inaendelea kufanya kazi hata leo?
Jibu: Ofisi ya Khalifa ilikuwa ndiye mtawala kwenye dini ya
Kiislamu.
Jina hili linatokana na lugha ya Kiarabu la Khalifah ambalo
maana yake ni mrithi. Jinsi linavyotumika na kuandikwa sasa ni Khalif. Kamusi
ya The Oxford Universal Dictionary inasema matamshi yanayofanywa kwa kutumia a ndefu au ya kuvuta ni mbaya.
Ni cheo cha Kiislamu kwa watawala wa kiduania au kisiasa na
kidini wanaochukuliwa kuwa warithi wa huduma ya kitume wa Mtume Muhammadi. Utawala au eneo lake la kiutawala au la ufalme linaitwa
Khalifate.
Makhaliwa wanne wa kwanza waliitwa Makhalifa Wakuu Warithi
Wanne. Baada ya hapo Uislamu ulichukuliwa kuwa umepungua nguvu ya kiteolojia
chini ya Ummayids na Abbasids. Kuna mkururu wa majarida yanayoelezea Uislamu
yaliyowekwa kwenye tovuti yetu ya www.ccg.org na pia ya kuanguka kwa Yerusalemu
mikononi mwa Omari kwenye jarida la Goligotha: Mahali pa Fuvu la Kichwa (Na. 217). Pia soma kwenye jarida la Imani za Kisirisiri Sura ya 5 Uislamu (Na.
B7_5).
Tafadhali unaweza
kumuelezea Imamu alikuwa nani au ni mtu gani sasa na mtu anawezaje kuwa Imamu?
Jibu: Kuna maana mbili na matumizi ya cheo hiki cha Imamu.
Cheo hiki kinamaana ya kwenda au
kutangulia mbele. Pia kinatumika katika kumuweka mtu wakfu ili awe mkuu au
kuhani wa Waislamu Msikitini
Pia kilitumika kama cheo walichopwa viongozi mbalimbali
wa Kiislamu na watemi wakiwemo Makhalifa au wafalme binasfi. Mafundisho ya
kawaida na yaliyokubaliwa kwenye jamii ya Kiislamu yanahitajika au ni muhimu.
Imani ya Kiyahudi
Ni nini
maana ya uahirisho wa kalenda ya Hilleli au ya Kiyahudi?
Jibu. Kalenda ya Hilleli inaahirisha Sikukuu za mwezi wa Saba kwa kuweka
uahirisho, kitendo ambacho kwa mara ya kwanza kabisa kilifanyika mwaka 344 na
marabi wawili wa Kibabeloni na kikaendelezwa na kurasimishwa na Rabi Hilleli II
mwaka 358 BK. Hawakufikia hatma yake hadi katika karne ya kumi na moja. Tangu
karne hii ya kumi na moja, sikukuu ya Rosh Hashanah ambayo ilianzishwa katika
karne ya tatu BK ikitokea Babeli hadi kwenye imani ya Kiyahudi iliyoweka au
kupangilia jinsi ya kuziweka siku za mwezi na imekuwa ikitumika kuwa ni kama
Mwaka Mpya. Mnamo mwaka 2000, kwa mfano, Rosh
Hashanah iliahirisha Siku ya Upatanisho kutoka kwenye Siku yake halisia
ikiibambikia na Sabato ya tarehe 7 Octoba kwa siku mbili ili kwamba siku ya
Upatanisho ianzie jioni ya tarehe 8 Octoba na ifanyike siku ya Jumapili Usiku
na Jumatatu ya tarehe 9 Octoba.
Hii ni siku mbili baadae zaidi ya ilivyo kwenye kalenda
ya hekalu ambayo inaanzia siku zake tangu siku za kutoonekana mwezi na ambayo
ndiyo inaamua kuanza kwa kila mwezi pamoja na mwanzo mwezi wa Mwaka Mpya yaani
mwezi wa Abibu ambao ndio Mwaka Mpya wa kweli na Mwezi wa Kwanza kwa mujibu wa
Sheria au torati ya Mungu. Uahirisho huu unatokea mara nyingi kwenye utaratibu
ule wa kalenda. Soma
majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156); Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213) na Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho au
Sikukuu? (Na. 195).
Wakristo wa kwanza waliichukulia siku ya Upatanisho kama
inavyoonekana kwenye majarida ya Siku ya Upatanisho (Na. 138); na Azazeli na Upatanisho (Na. 214). Jambo muhimu na la kutilia maanani ni kufanya toba na
kurudi kwenye Sheria au Torati ya Mungu.
Uprotestanti
Wengi wa Wanaoamini
dhana ya uahirishaji wanasema kuwa dhambi ni dhambi tu. Je, unaamini kiwango
fulani cha dhambi?
Jibu: Waprotestanti wapo kwenye nafasi mbaya sana kuhusu tabia
ya dhambi. Biblia inasema wazi sana kwamba dhambi ni kile kitendo cha kuzivunja
amri za Mungu (1Yohana 3:4). Hata hivyo, Waprotestanti hawazishiki sheria za
Mungu wala kuzichukulia kuwa kanuni au mwongozo mkuu na wanatumainia mabaraza
yaliyokaa na kutoa miongozo katika Karne ya Nne kwa kuziweka Sheria mbalimbali
na ambazo ziliingizwa kanisani. Walimtumainia Augustine kuwatungia elimu ya
teolojia na mafundisho ambayo yameendelea kutokana na mabadiliko hayo na tafakari
ya mijadala kuhusu Mungu kwa kiwango cha utakatifu.
Na hii ndiyo sababu iliyopelekea kushindwa kwa Matengenezo
ya Waprotestanti. Yaishindwa kwa kuwa mkakati huu wa Matengenezo haukurudi nyuma
zaidi ya kipindi cha Augustine na kuirudisha imani asilia ya kwanza. Kwa hiyo,
hawakuweza kushughulikia uthibiti wa dhambi ma namna yenye ufanisi. Ukiri wote
wa Matengenezo wa Waprotestanti ulizilenga Amri Kumi, lakini wawaishiki Amri ya
Nne na hata ya Kwanza kwa kweli, na wengi wanaivunja hata amri ya pili pia.
Mafundisho yanasema kwamba kama inaivunja amri moja, basi
unazivunja amri zote. Pia, chochote kisichotokana na imani ni dhambi (Warumi
14:23). Kitendo cha kumpendelea mtu pia ni dhambi, na kwa hiyo, kanisa
limepungukiwa na utukufu wa Mungu (Yakobo 2:9). Yohana anasema kwamba kuna
dhambi isiyo ya mauti. Hii inamaanisha kwamba
dhambi tunazozitenda kwenye mzunguko wote wa mwaka, zinasafishwa bure na tunaruhusiwa
kubakia kwenye mwili wa Kristo na kuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza
unaotajwa kwenye Ufunuo 20. Wale wanaotenda dhambi kwa makusudi watakwenda
kwenye ufufuo wa pili wa wafu na watakabiliwa na mauti ya pili. Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi (1Yohana 3:9).
Tofauti hii kwenye dhambi ni mssingi kwa mtazamo kuhusu dhambi
mbaya na ya mauti. Makanisa kongwe ya kale yameweka tofauti kwenye mkakati wa
kupotosha kwa karne kadhaa sasa; hata hivyo, hiyo ilikuwa ndilo fundisho kuu na
la msingi la Kanisa la Agano Jipya. Dhambi ya wazinzi wa Kikorintho ilikuwa ni
kwamba walitolewa kwa shetani ili kwamba uhai wake uweze kuokolewa katika siku
za mwisho (1Wakorintho 5:5). Kwa hiyo, waliondolewa Kanisani na wakawa kwenye hukumu
bado hadi walipotubu. Kwa maneno mengine, ni kwamba walichukuliwa kuwa watakuwa
na sehemu kwenye ufufuo wa pili wa wafu ili waweze kuokolewa huko. Walipewa fursa
ya kutubu inaonekana kwamba walifanya hivyo.
Kuna matawi sasa ya Waantinomiani ambayo yamejichanganya
na Uprotestanti, imani au vuguvugu linalosema kuwa sharia za Mungu zimeondolewa
au zimetanguka zote kabisa (yaani, zimepigiliwa Mtini na kuitafsiri hivyo Wakolosai
2:14), na kwamba hakuwezi kuwa na dhambi kwa ajili hiyo. Mtazamo huu na hisia hii
imeongezeka na kuenea ulimwenguni kote.
Soma kwenye majarida ya Chimbuko la Uvaaji wa Heleni na Vito vya
Thamani vya Dhahabu Katika Siku za Kale (Na. 197); Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235) na pia Ndama wa Dhahabu (Na. 222).
Martin Luther ni
nani? Nijuavyo mimi ni kwamba alikuwa ametengwa na kanisa, lakini hakuwahi
kurudishwa kwenye imani. Kama ni hivyo, ni kwanini alirudishwa kwenye imani?
Je, yeye sio mzushi?
Jibu. Mkakati wa Mtaguso wa II wa Vatican ulikuwas ni
kuyarudisha Makanisa ya Kiprotestanti yawasiliane na Roma na kwa hiyo, Waptotestanti
hawakuwa tu ndugu waliotengwa na sio wazushi.
Mtaguso wa I wa Vatican ulioitishwa na Pius IX ulikuwa na
mkakati wa kulazimisha kutolewa Tangazo lenye Amri lijulikanalo kama Unam Sanctam. Lengo lake lilielezewa kwa
kina kwenye bango kitita. Ufafanuzi huo wa kwenye bango kitita na tafsiri yake
na malengo yake vimeelezewakwa kina kwenye jarida la Theori ya Vita vya Haki (Na. 110).
Ili kufungua majadiliano, ndipo Mtaguso wa II wa Vatican uliitishwa
na John XXIII na uliendelezwa na Paul VI. Kuna bonde kubwa sana kanisani sasa
na ili kuwaridhisha au kuitosheleza mistari iliyotangulia, tangazo la fundisho
jipya ndipo sasa limetolewa na Ofisi Takatifu inayojulikana kama Mkutano
Mtakatifu wa Mafundisho ya Imani.
Hoja za baraza la Inkwizisheni linalofuatia zilitolewa na
John Paul II na inahofiwa kwamba zilielezewa kwa wahusika kwenye kanisa
Katoliki la Roma, kama vile Morris West. Vuguvugu lililopo sasa za kuzirasimisha
kanoni ya John XXIII na Pius IX ni kutuma jumbe zenye kukanganya na kuleta
mgongano kanisani. Mtu mmoja anasema kwamba tunayarudia mapito ya zamani, na
mwingine anasema kwamba tunaendelea na mambo au ustaarabu wa kisasa. Hii
inamaanisha kuwa ni hila wa kisaikolojia. Mkanganyo wenyewe unalenga kuingiza
mabadiliko yasiyokubalika na kisha, kwa wakati huohuo, wayakane mabadiliko
yoyote yanayotokea.
Wale wanaotaka kubadilisha watashushwa, kile mmoja
akijionea au kujipatia jambo analopenda kuliona. Na ndipo kidogokidogo, upande
wa wanaopinga utapikwa kama vyura kwenye maji ya moto. Kwa hapo ndipo tuna
Luther Mzushi, Luther Mtakatifu aliyeliimarisha kanisa, na ambaye ni Luther
mzushi pia. Je, Luther wa kweli na halisi ataweza kusimama tena? Na ndivyo kama
ilivyo Canterbury pia na Waanglikana/Waepiskopalians. Kumbuka, malengo au maazimio ya Canterbury kwa matamko ya
Ratzinger kutoka kwenye baraza la Ikwizisheni la Vatican.
Mwishoni mwa karne ya
20, tetesi ya kujitenga au kumeguka iliibuka kuwa ni kama nguvu kuu na
isiyoonekana kwenye uhai wa dini za Marekani. Wakati huohuo, makanisa ya
Kiprotestanti hayakuachwa mbali na makanisa mengine, lakini kwa aina ya dini
kulikuwa na watu binafsi wasiohitaji imani zilizoanzishwa kimapokeo. Leo watu
wanaonekana wamerithika kuanzisha imani zao wenyewe za kidini, zilizo na
ushabihiano na imani waliyokuwanayo zamani ya inayoendana na desturi iliyo
kwenye jamii, ambazo ziko ili kushurutisha kuwafanya watu wawe na tabia za
kidini maishani mwao. Je, unakubaliana, au unapingana na maneno hayo hapo juu.
Jibu: Watu wetu wamekuwa kila mara wakiteswa na Taasisi zenye
mapokeo ya Kikrisro. Tumekuwa
tukisimama kwenye Biblia tukipitia mateso mengi nay a mara kwa mara. Mauaji ya
kuangamiza ya Holocaust yalibuniwa kwa lengo la kutufutilia mbali sisi pamoja
na Wayahudi pia. Yeyote aliyeamini kwa mujibu wa Biblia peke yake aliteswa na
kile kilicholikana kama imani ya ukristo mkongwe.
Haishangazi kabisa kuona kuwa imani yote ya Biblia
imepotoshwa na kwamba wakati inapokabiliwa na imani ya kweli zaidi au
iliyopungufu katika ukweli na ya zama ya uwazi iliyoshindwa kuendelea. Kwenye
kitabu kilichoandikwa na Rabbi Kohn mwaka 1894 unaweza kuona kwamba ile inyoitwa
imani ya Kikristo ilichotufanyia sisi Wakristo. Waliwaua wanawake wetu haikuu kwa
kuwa walipika kwa mafuta ya bata bukini badala ya kutumia mafuta ya nguruwe na
kwa kuwa walikuwa wanaishika Sabato. Wakati kanisa Katoliki la Roma
liliposimama kuwauwa, ndipo Walutheri walichukua fursa na kuendeleza mauaji
haya (soma kitabu cha Kohn, cha Sabbatarians
in Transylvania [Wasabato wa Translyvania], CCG Publishing, kilichonyambuliwa
zaidi na Cox, 1998).
Historia ya Kanis
la Mungu linaloshika Sabato imeainishwa kwa kina kwenye majarida ya Migawanyo Mikuu ya Makanisa ya Washika Sabato (Na. 122) na Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika
Sabato (Na. 170). Pia soma jarida la Malumbano ya Wakwotadesimani (Na. 277).
Upagani
Kwa nini kuna
Wakristo wengi sana ukilinganisha na Wapagani? Je, sisi sio watu wabaya tunaomwabudu
shetani. Ukichukulia ukweli kwamba, Upagani ulikuwepo hapa miaka mingi sana
kabla ya Ukristo na ni jinsi ya kwamba kuna imani tofauti tofauti kwenye
Ukristo zinaonekana kuwa ni kama za Kipagani. Chukulia mfano wa imani ya
Kikatoliki inayomwabudu Bikira Maria kwa kiwango sawa na Yesu Kristo. Kwenye
dini ya Wawikkani, utakuta kwamba mungumke wao anaweza kufananishwa na huyu
Bikira Maria na mungu wao ni kama huyu Yesu Kristo, ni kwamba tu mungu mke wa
hawa anamzalia mungu wao mume mtoto kila mwaka. Anaishi akiwa hai na kisha
anakufa majira ya Kipupwe ili aweze kuzaliwa tena majira ya Machipuko, ni sawa
tu na kama na majira aliyofufuka Kristo. Nadhani jambo hili linahitaji kufafanuliwa
ili Wakristo wengi kabla hawajaendelea kutoa hukumu kuwahukumu Wapagani.
Jibu: Unaonekana kutoelewa nafasi na hali zenyewe. Unachokifanya ni kinyume na Sheria za Mungu. Chimbuko la
dini yako kinafahamika vyema zaidi na kimeandikwa na kuchambuliwa kwa kima
kwenye tovuti ya www.ccg.org. soma kwenye majarida ya Fundisho Kuhusu Dhambi ya Kwanza Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246) na Fundisho Kuhusu Dhambi ya Kwanza Sehemu ya
2 Kizazi cha Adamu (Na. 248).
Unasemaje kuhusu imani ya Ukatoliki, iko sahihi. Ibada
hizi za kumwabudu Maria kama mungu-mke, mama, ziliingizwa kwenye Ukristo kutokana
na imani za Baali-Easter, zilizoibuka kwenye imani za kipagani kwa mara yake ya
kwanza. Ilikuwa ni imani ya kwanza asilia ya Waaryani. Upagani ni dini
inayotuama kwenye mzunguko wa Siku za utoaji wa Kafara za Wanadamu.
Mungu alikataza imani hii, na sisi, tukiwa kama Wakristo
tumekatazwa kujishirikisha imani hii. Kanisa la Mungu limekuwa likiteswa kwa
kipindi cha miaka elfu mbili sasa kwa kuwa hatukubaliani kuadhimisha wala
kuiamini imani ya Easter ya mungu mfu, awe ni Attis wa Roma, au Adonis wa
Wayunani, au Orisis wa Wamisri. utajifunza zaidi kwenye jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235) ukipenda,
kama ilivyo kwenye jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222).
Kanisa la kweli la Kikristo haliwezi kabisa kuzikubali
sikukuu hizi za kipagani. Kanisa la kwanza kutoka Roma na Constantinople liliingiza
mafundisho ya upotofu kanisani ili kuwashawishi wafuasi wa miungu Attis na
Mithras na Sol Invictus Elagabal, mtindo wa kuabudu kwa wazi na hadharani imani
ya mungu jua, kwenye Ukristo. Chembechembe au ushawishi wa uasetiki wa
Kinostiki viliingizwa pia kwenye Ukristo. Ushawishi wa Kinostiki uliingizwa na
kushirikishwa pia. Tazama jarida la Uvijitariani na Biblia (Na. 183) ili kujifunza mambo hayo.
Mambo haya yote ya kumwabudu mungu wa Utatu vilitokana na
uasi wa Malaika wakiongozwa na Shetani. Roho hiyo ndiyo roho unayoiabudu. Imani
ya Kiutatu na mungu mwenye vichwa vitatu aliyeko mtini ndiye chanzo cha imahi
hii ya kipagani. Ilianzishwa kwa kipindi cha maelfu ya miaka iliyopita. Soma
mkururu wa majarid ya Imani za Kisirisiri
(Na. B7).
Mara tu baada ya kipindi maalumu na kilichowekwa cha
Mungu wa dunia hii kitakapokoma ndipo imani na mfumo huu utakapoanguka na
kukoma. Wafuasi wake huabudu kwenye imani hii wakimwabudu kama mungu-mke, au
Gaia au walio kwenye maumbo mengine, lakini inaonekana kutoka kwenye imani
hiyohiyo ya mungu wa Utatu.
Dunia itakuwanayo imani hii hadi muda mfupi kabla ya
mwaka 2027 kipindi cha kutubu. Kisha marejesho ya ushikaji wa Sheria au Torati
yatarejeshwa na dini hizi hizi wanazoabudu zitaonekana kuwa hazina nguvu kabisa
tena. Dunia inazishika sharia za Mungu tangu wakati huo, vinginevyo itakubwa na
baa la njaa kali ya kuhilikisha kabla ya mfumo wao utakapoishiwa nguvu. Huyu
anayejulikana kama mungu-mke au pepo atatupwa kuzimuni kwa kipindi cha miaka
elfu pamoja na mapepo wengineo.
Dunia itakuwa imeelimishwa au kufundishwa tena kwenye
kipindi cha Ufufuo wa Pili ambacho kwamba wengine wote miongoni mwa wanadamu
waliodanganywa na Shetani na imani hii. Ndyo maana imani ya kurudia rudia
kuzaliwa tena na tena ilianza hapa duani. Ilianzishwa kwa lengo la kuwadanganya
wale walio kwenye ufufuo.
Wataelimishwa au kufundishwa upya na kupewa fursa ya kuelewa
na kutubu. Wanapaswa washukuru sana kwamba tuna Mungu mwenye rehema. Mchawi wa Endori
aliogopa sana alipomuona elohim akipanda kutoka ardhini kama kinavyotuambia
kitabu cha Samweli. Hivyo basi, hata mapepo haya yanajua kuna Mungu mmoja wa
Pekee na wa Kweli na wanatetemeka.
Mara tu, imani hii ya waabudu mungu mama ndipo itakakoma na
kutokomea. Makuhani wanaovaa majoho meusi wajulikanao kama Khemarim wa imani au
dini ya Baali-Easter watatokomea na dunia itawekwa huru kutokana na imani na
ibada za uwongo. Dini za Kisirisiri zinazotokana na dini za Siri za Kibaleloni,
ambayo imefanyika kuwa mwanamke kahaba kwenye sayari hii, haitakuwepo tena.
Dini hizi potofu zingali bado zipo na zinatenda kazi kwa
kuwa zinatoka sehemu hiyohiyo moja na Kuasi kwa Malaika waovu na mungu wa
Utatu. Wakati mwanamke huyu kahaba atakapoangamizwa muda si mrefu sana ujao, upagni
utakuwa na mfufuko tena kwa kitambo, wakati na manma utakavyoangamizwa na watu
wataurudia utoaji Zaka wa kweli wa Mungu na watairudia imani yake pia.
Kila mmoja anahitaji kujisomea imani yake na chimbuko
lake na kutubu. Watakatifu msichukie kabisa tena. Wanachukia kile
kinachofanyika. Mungu hauhukumu ulimwengu bado. Wakati Mashahidi watakapoanza kuhudumu
huko Yerusalemu, tutaiona nguvu ya Mungu ikiishughulikia imani iliyopo hapa
duniani. Tunapaswa kuwapenda watu wote na kuwaombea ili wakombolewe. Ni jambo la
kuogofya sana kuanguka kwenye mikono ya Mungu aliye hai.
Mashahidi wa Yehova
Ilionekana kwamba
Mashahidi wa Yehova ni afadhali wafe kuliko kukubali kutiwa damu ya mtu mwingine.
Je, hii ni dhana ya kibaguzi? Pia ni angiko au maandiko yapi wanayoyatumia
kuzijengea hoja zao za kiimani?
Jibu: Fundisho hili la Mashahidi wa Yehova linatoka kwenye
maandiko ya Biblia yanayokataza kula au kunywa damu. Maandiko haya yanaelezea
maelekezon aliyopewa Nuhu, na pia alipewa Musa. Kwa mfano, kwenye Mwanzo 9:4: “Bali nyama pamoja
na uhai, yaani, damu yake, msile.” Wazo lenyewe linatokana na ukweli kwamba damu ni uhai na iwapo kama
utaichukua damu kutoka kwao, ni sawa tu kutoa uhai mwingine kutoka kwako, kwa
kuichukua damu yao. Huku ni kutojua na upuuziaji wa usomaji wa maandiko usio na
ubaguzi.
Utunzaji mbaya wa damu yenye virusi vya UKIMWI, na vitu
vingine vyenye chembechembe za STDs zenye damu iliyokosewa katika kuisafisha
kwake kumewaacha Mashahidi wa Yehova wakiwa na mlipuo au hamasa zaidi ya
kupinga mambo yao, lakini inakuwa bado ni makosa ya kiutafsiri wa maandiko ya
Maandiko Matakatifu. Amri au agizo la kuto kula damu ni kwamba imewekwa pale
ili kuhakikisha kwamba wanyama wawe wanachinjwa vizuri. Ni juu ya mtu binafsi
kuona iwapo kama atakubali kupata tiba hii au la. Kukubali kufa kwa ajili ya huku
kufanya madai ya kipuuzi ya Maandiko Matakatifu ni uamuzi na uchaguzi binafsi
wa mtu.
Kumlazimisha mtu mwingine afe kwa ajili ya kutojua
kuyatafsiri Maandiko Matakatifu ni jambo linguine tena. Na ndiyo maana baadhi
ya nchi zinaingilia kati na kuwaachia wazazi waamue kwenye mazingira ya tiba ya
uhai au maisha kama mtoto atakufa asipowekewa damu. Mambo haya ya malumbano
yanatokana na mahudhui ya kibinafsi yanayomjiri mtu mwenyewe binafsi.
Suala hili la kumtia mtu damu kwa ruhusa ya wazazi ni
tatizo kubwa sana, kama tohara ya mtoto wa kiume imezuiwa hata kwa hoja au
malumbano makubwa kutoka kwa wanaowapinga watetezi wa Sheria za Biblia, sio kwa
wapagani waliomcha Mungu peke yao bali hata na waamini Utatu pia. Ni vigumu
sana kumpata mtoto aliyekwisha tahiriwa nchini Uingereza sasa na hali
inaongezeka kuwa hivyo. Soma kwenye majarida ya Sheria za Vyakula (Na. 15) na Utakaso na Tohara (Na. 251).
Kutokana na mjadala
na maadhi ya Mashahidi wa Yehova wanaonekana kuwa wanasema kuwa Kristo
alikwisharudi duniani mwaka 1914. Hata hivyo hatuwezi kumuona kwa kuwa yupo
kwenye maumbile ya kiumbe wa kiroho. Wanasema mwaka wa mwisho wa ‘kawaida’
katika historia ulikuwa wa 1913, na mwaka 1914 ulikuwa ni mwisho wa kipindi cha
utimilifu wa mataifa. Je, mwaka huu wa 1914 una maana yoyote kwenye namna ya
kibiblia ya kuhesabu matukio na mkururu wa nyakati? Pia ni kwamba, imakuwaje basi
kwamba sisi sote hatujui kwamba Kristo alikwisha kurudi? Siwezi kudhania kuwa
tukio hili lilikwisha andikwa popote.
Jibu: Ndiyo, tunafahamu na kuzizoea hoja zao. Linatokana na kuelewa
vibaya ya kitu kinachojulikanaa kama unabii kwenye Maandiko Matakatifu.
Waliamua kwamba vita iliyoibuka mwaka 1914 kuwa ni vita ya mwisho wa dunia.
Waliamua kwamba ulikuwa ndiyo mwaka kutimilika kwa kipindi cha miaka 2520, au nyakati
saba kutoka kipindi cha Nebkadneza na cha vita vya Karkemish. Hizi zilikuwa ni
nyakati saba za Nebkadneza kwenye unabii wa Danieli. Kwa bahari mbaya sana, ilikuwa
ni miaka 2518 tu tangu Vita ya Karkemish, ambayo ilikuwa mwaka 605 KK, na
hivyo, waliliweka tukio hili kwenye mwaka 607 KK.
Pia, hawakujua au kuelewa maana ya unabii wa Mikono Iliyovunjika
ya Farao wa kwenye Ezekieli 28-30, na wanadhani kuwa sio sahihi kwa mwaka 1914 badala
ya mwaka 1916, na kuishia hapo tu badala ya kuchukua hadi mwaka 1996. Wala
hawakuyajua matatizo yaliyosababishwa na
wahafidhina wa Kiislamu yaliyopelekea kuunganika tena kwa Kanisa la Kikoptiki
la Misri na Roma na kuanzishwa kwa Misri ikiwa kama nguvu kuu ya uafidhina.
Waliuelewa vibaya au kuukosea unabii kwenye uhusiano wake na nyakati za mwisho
na kwa hiyo, wao, wakaangukia kufanya makosa waliyoyafanya wa SDA walivyofanya
mwaka 1844, na wakabuni maelezo mengine kutetea kushindwa kurudi kwa mwokozi na
kujitetea kutokana na madhara yaliyosababishwa na kosa hilo.
Mkururu way ale yaliyotakiwa wayaelewe vizuri kutokana na
muainisho huo yasome kenye mkururu wa majarida ya: Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95); Anguko la Misri (Na. 36) na Mchanganuo wa Ratiba ya Nyakati (Na.
272).
Nimejionea mara
nyingi sana ukisema kwamba baada ya ufufuo wa wafu tutakuwa ni watu wenye
jinsia. Je, tutawajua watoto wetu na mababu zetu? Niliambiwa kuwa tutakuwa
tukiishi bado kama familia, na hakuna atakayekufa, watoto watawajua mababu zao
waliopita na tutajenga majumba popote tutakapopapenda, na kahalika. Natumai
kwamba umekwisha sikia jambo hili hapo kabla. Je, Mashahidi wa Yehova wamekosea
kuamini na kuwafundisha watu wao hivyo?
Jibu: Mashahidi wa Yehova wamekosea kufundisha hivyo, ni kama
walivyokosea kwenye jinsi mambo yatakavyokuwa kipindi cha Milenia pamoja na
fundisho kuhusu Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Ufufuo wa Kwanza utatokea mwanzoni
mwa Milenia. Watakatifu au wateule wote watafufuka na kisha watafanyika kuwa
viumbe wa kiroho. Watachukua nafasi ya malaika walioasi kwa kipindi cha miaka
1000. Sehemu nyingine iliyosalia ya dunia itaendelea na itafanywa upya. Watu
wataishi na kufa kama kawaida kwenye familia zao.
Dunia itaongozwa au kutawaliwa kutoka Yerusalemu na
Kalenda ya kweli ya Mungu itatumika sambamba na imani asilia ya Mungu. Wale
watakaopinga au kukataa kuzishika Shweria za Mungu, vikiwepo Sabato zake,
Miandamo ya Mwezi Mpya, na Sikukuu zilizoamriwa na mwenyewe, mvua haitanyesha
kwao kwa majira yake muafaka na watakubwa na maradhi ya Misri (Zekaria
14:16-19).
Umuhimu wa watu kuzishika Sheria au Torati ya Mungu
utarejeshwa kwa kuhubiriwa au kufundishwa na Mashahidi. Soma kwenye jarida la Mashahidi (Wakiwemo Mashahidi Wawili) (Na. 135). Kisha ndipo watu watakuja moja kwa moja kwa Baraka au
Laana zilizoandikwa kwenye Kumbukumbu la Torati 28 (soma jarida la Baraka na Laana (Na. 75). Mwishoni mwa kipindi hiki cha milenia ndipo Uasi wa
mwisho utatokea. Wote watakaohusika watakufa na mapepo watapungua na kujigeuza
kwa miili ya wanadamu na watakufa pamoja nao (soma kwenye jarida la Hukumu ya Mapepo (Na. 80).
Kisha ndipo watafufuliwa wote. Kila mwanadamu aliyewahi kuishi,
ambaye hajawa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza, atafufuka kwenye Ufufuo wa Pili
wa Wafu sambamba na mapepo. Hawatakuwa na jinsia wala hawataoa waka kuolewa.
Hakutakuwa na ndoa tena tangu kipindi hiki. Kila mwenye mwili atapewa fursa ya
miaka 100 ya kutubu. Wote watarudiwa au kukemewa, wataongoka na kisha
watabadilishwa miili yao. Wale wanaochagua kufa wataachwa wafe na ndipo
watachomiwa wote motoni na kuangamia kabisa.
Kisha ndipo kifo hakitakuwepo tena, kama watakavyofanywa
manabii wa uwongo pamoja na roho za Mashetani. Shetani atapewa fursa mpya ya
kufanyika kiumbe mpya na roho mpya akifanyika kuwa mwana mpya wa Mungu, ni kama
atakavyofanyiwa pia Hitler, na Papa wa Borgia, na kwa kiumbe yeyote aliyewahi
kuishi hapa duniani. Soma kwenye majarida ya Mchanganuo wa Nyakati za Mpito wa Zama (Na.
272) na Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu (Na.
199).
Mpango wa Mungu ni mkamilifu. Tunamtumikia Mungu wa Kweli
ambaye ni mwenye sifa za Kuelewa Kila Jambo, Mwenye Uweza Wote, Aliyekamilika
kwa Wema na wa Kweli ambaye ndiye Baba wa wote. Yeye anayetakasa na wao
wanaotakaswa wana mwanzo au chimbuko moja tu (Waebrania 2:11). Hatuendi
kumpoteza mtu yeyote.
Kama mmoja wa Mashahidi
wa Yehovah, nimesoma maelezo mengi sana yaliyo kinyume na imani hii ya
Mashahidi wa Yehova. Sikusudii kuipuuza dini ya mtu yeyote na nilikuwa
nashangaa ni kwa nini watu wengi sana wanapenda kuwapuuza wenzao wakiwa kwa
kweli hawajui wanachokiamini hasa. Na kama tunadai ya kwamba tunamtumikia
Mungu, kwa nini basi hatuenendi sawasawa na imani ile tunayodai kuwa
tunaiamini? Wengi wanadai kuwa wanaiamini Biblia, lakini imani zao zikiwa
kinyume kabisa na madai yao. Nimejitahidi kwa kadri niwezavyo kuwapenda watu
wote na wa imani zote, na wa aina zote na kutowabagua. Kama Mungu hana
upendeleo na haonyeshi upendeleo wowote wala hambagui mtu yeyote, basi sisi ni
kina nani hata tunafanya hivyo?
Jibu: Yatupasa kuwapenda majirani zetu kama tunavyojipenda
wenyewe. Hakuna mtu anayejichukia mwenyewe. Hivyo ni kwa nini uwachukie wengine.
Kanisa la Mashahidi wa Yehova (au kwa usahihi zaidi waite
“the Watch Tower and Bible Tract Corporation” yaani Shirika la Uchapishaji na
Ugawaji Vipeperushi vya Biblia la Mnara wa Mlinzi]) lina mtazamo wa uwongo kuhusu
Maandiko kadhaa ya Biblia. Tunakubaliana na mfumo au utaratibu huo kwa upande
mmoja na kiwango cha jinsi isemavyo Sheria ya Mungu na Sabato zake. Tunajua
habari zao na kule zinakotokea na jinsi zilivyofanikiwa kuwa pale walipo sasa.
Tunajua pia kwamba wamefanya namna ya mwitikio na kwamba,
kama kanisa, wamevunjwa moyo na usomaji wowote wa kimtizamo kuliko wao wenyewe
na wamewafanya watu waamini mitazamo hiyo iliyo kinyume kabisa na yasemavyo
Maandiko Matakatifu.
Hamu yetu ya kuirudisha Imani ya kweli ya Ukristo wa
karne ya kwanza kwa watu wote. Ili kufanya hivyo, yatupasa kuakinisha mafundishi
kadhaa ya uwongo yaliyopo kwenye dini nyingi za uwongo. Mashahidi wa Yehova
wanajulikana sana kwa sifa yao ya kushutumu imani za makanisa kongwe ya zamani,
wakidiriki hata kupita mlango mmoja hadim mwingine wakiwashawishi watu wajiunge
nao.
Yohana Mbatizaji hakumung’unya maneno na ndivyo hata
Kristo na ndivyo hata watakavyokuwa Mashahidi watakapokuja hapa. Mashahidi wa
Yehova, kama alivyo mtu mwingine yoyote hapa duniani wataanza kuzishika sharia
za Mungu au vinginevyo watakufa. Hakutakuwa na mjadala wala maafikiano.
Wataanza kushika na kuadhimisha miandamo ya Mwezi Mpya na
Sabato (Isaya 66:23) na Sikukuu za Mungu (Zekaria 14:16-19) na watawapeleka
wawakilishi wao huko Yerusalemu kila mwaka, vinginevyo hawatanyeshewa mvua kwa
majira yake muafaka na wataandamwa na maradhi au tauni ya Misri
vitakavyoruhusiwa kuwasumbua.
Hayo ni Maandiko Matakatifu, na Maandiko hayatanguki.
Soma kwenye jarida la Sheria na Amri ya Nne (Na. 256).
Fundisho Kuhusu Roho
Je, unaamini kuhusu
kiumbe kuzaliwa mara nyingi tena na tena? Ni kwa nini basi kwamba nimekutana na
watu niliowagundua papohapo na kuwa kwenye mahali ambapo walikuwa wanafanana
sana na mimi? Nagundua kuwa Maandiko Matakatifu yanasema kwamba kila mtu yupo
kwa wakati wake fulani (mara moja tu) bali je, kuna uwezekano wowote wa kwamba
mwanadamu anaweza kuwa na wakati mwingine zaidi wa kuishi maishani mwake.
Jibu: Fundisho hili la kuzaliwa mara nyinginyingi ni tunda au
matokeo ya fundisho la Roho au Nafsi hai na ni kinyume kabisa na Biblia.
Uzoelefu tunaouona kwa watu mara nyingi unatokana na kumbukumbu zetu kwa watu,
maelekezo, maneno na mjumuiko. Wacelti pia walikuwa na fundisho hili
lililotokana na imani nyingine za Waryani. Kwa kweli ni makosa
yanayowatumikisha watu. Yatupasa kupambana na matatizo iliyoyasababisha huko India.
Kifilosofia, ilikikuwa ni dini iliyoanzishwa hapo mwanzo wake kabisa ikikusudia
kuondoa ubaguzi wa hali za kiuchumi au rangi na matabaka ya watu kwa kigezo cha
kuwanadharisha watu kuwa kuna mizunguko ya kiumbe kuzaliwa tena na tena, dhadharia
iliyobuniwa na Dini potofu za Kihyperborean. Biblia inafundisha Ufufuo wa Wafu
na uhai wa mara moja na kwamba uhai huo umesababisha kuwepo kwa kvumbe wa
kiroho kwa njia ya aina mbili za ufufuo wa wafu. Msimamo wa biblia imeainishwa
kwa kina kwenye majarida ya Fasi hai (Na. 92); Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Mji wa Mungu (Na. 180).
Sote tunajua kwamba nafsi zetu ambazo haziwezi
kuzaliwa; haziwezi kuwa na mauti; yaani, kuzaliwa kwa mtu ni kule kuumbwa kwa
mwanadamu na kufa kwake kunamaanisha mwili wake kuacha kufanya kazi. Kwa nini
wanasema kuwa Yesu alifufuka na kutoka akiwa hai siku 3 baada ya kuteswa na kuuawa
kwake? Kama nafsi inaachana na mwili baada ya kufa kuna nini kisicho cha kawaida
kwa habari ya Yesu? Ama iwe kama hakufa baada ya kuangikwa mtini au baada ya kufa
kwake, nafsi yake ilimtoka na ikaenda mbinguni?
Jibu: Fundisho la nafsi isiyokufa siyo la Kikristo kabisa. Liliingia kwenye Ukristo
kutoka kwenye dini na imani za Kinostiki na kama zimehuishwa tena kwenye
mafundisho ya Kisocrati. Kwenye karne ya kwanza nay a pili, kama ingemwambia
Mktisto yeyote kuwa ukifa utakwenda mbinguni, basi wangejua kuwa wewe ni
pandikizi na siyo mwenzao. Kwa kweli, Kanisa la Roma
lilimwandikia mfalme mnamo mwaka 150-154 likimwelezea yanayojiri kwenye imani. Pia
waliiandikia Senate. Mwandishi wa Kanisa alikuwa ni Justin Martyr. Pia
aliwaandikia Wayahudi kuhusu Majadilianao yake na Trypho Myahudi (yapata mwaka
80). Justin alimwambia kwamba kama angekutana na watu waliojiita kuwa ni
Wakristo na wanaamini kuwa wakifa watakwenda mbinguni, basi msiwaamini kwa kuwa
hawakuwa Wakristo. Lakini sasa tuna mamilioni ya watu wanaodai kuwa ni Wakristo
lakini wanaamini kuhusu nafsi isiyokufa, na kuhusu mbinguni na jehanamu.
Ukweli wa mambo
ni kwamba Biblia (na hata Koran pia) zinafundisha aina mbili za Ufufuko wa
wafu. Ufufuo wa Kwanza utafanyika atakaporudi Masihi, na wa pili utafanyika
miaka 1000 baadae mwishoni mwa kipindi cha Milenia. Kwenye ufufuo huu wa pili
au ufufuo wa wafu wote, watu wote watafufuka na kuhukumiwa. Utapata hali halisi
itakavyokuwa kwa kujisomea majarida ya: Nasfi Hai (Na. 92); Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Milenia na Dhana ya Unyakuo (Na. 95).
Je, Mtume Petro
anaweza kuwa ndiye aliyebuni matumizi ya msalaba?
Nimeisoma makala
inayoweka taswira ya maelezo ya Rabbi Ovadia Yosef kwamba "waathirika wa
mauaji ya kuangamiza watu ya Holocaust, Wayahudi wote milioni sita, wato hao
maskini wote waliopotea kwenye mikono ya hao watenda maovu Manazi...walikuwa ni
zao la waliozaliwa u[ya tena kutokana na roho za waliotenda dhambi kipindi cha
nyuma na pia na walifanya mbinu zote za mambo ambazo hazijawahi kufanywa, na
walirudia kuzaliwa tena ili kwamba vitu viwekwe sawa" Aina hii ya fikra au
mawazo inatoka wapi? Inaonekana kuwa inaumiza sana kwa wale waliowapoteza
wapendwa wao kwenye mauaji haya ya Holocaust au walioishi kipindi chote cha
kuamriwa kufanyika mauaji haya. Inawezaje nasi amani na furaha kumjia mwanadamu
pamoja na dunia?
Jibu: Dhana ya kuzaliwa mara kadhaa ni upotoshaji wa fundisho
la ufufuo wa wafu. Agano la Kale na Agano Jipya yanafundisha Ufufuo wa Wafu.
Ufufuo wa wote utafanyika kwa kipindi cha miaka 100. Kipindi hicho kitakuwa
kwenye kipindi cha utawala wa milenia wa Masihi. Mpango huu umeandikwa na
kuainishwa zaidi kwenye majarida ya Mcganganuo wa Ratiba ya Nyakati na Zama (Na. 272) na pia jarida la Ufufuo
wa Wafu (Na. 143). Hivyo basi, dunia
itapewa ufufuo kwa wenye mwili na maendeleo yake yameelezewa pia kwenye Ezekieli
sura ya 37.
Kwa upande mmoja, hiki ni kitendo cha kurudiarudia
kuzaliwa ambacho kimechukuliwa na watu hawa ili kuliunga mkono fundisho la
kuzaliwa tena na tena. Moja ya mbinu anazozifanya Shetani ni kulishamirisha
fundisho hili la kuzaliwa tena na tena kwa nyakati mbalimbali na alifanya hivyo
tangu mwanzo. Alijua kwamba wakati watu watakapoamka kenye Ufufuo wa Pili,
tukio litakalowatukia wanadamu wote walioko duniani, kama walidhania kulikuwa
na wakati mwingine wowote utakaokuwa mgumu zaidi kuwashughulikia. Kwa maana
iliyo kweli. Hatutakuwa na muda mwingine wa kuwashawishi watu hawa kwamba wana
fursa hii na kwamba wapo hukumuni wakati ule na kwamba hawataipata fursa
nyingine. Kwa maana ya kwamba watapoteza muda wetu fulani na mchakato wa elimu
ili kuyarekebisha mawazo hayo.
Hakuna ukweli wa kuamini kwamba mauaji ya Holocaust yalikuwa
kwa ajili ya watenda dhambi ambao walikuwa wamezaliwa kwa mara nyingine tena,
na haya ni mafundisho na imani potofu ya Kihindu/Kibudha yanayotokana na sharia
za Dharma na Kharma. Kwa kweli haina uhusiano wowote na Biblia na ni kejeli au matusi
tu makubwa sana kwa walionusurika na mauaji haya ya Holocaust. Dhana iliyoko
nyuma yake ni hii.
1. Wayahudi ni watoto wa Yuda na Yuda ni mmoja ya wateule
waliochaguliwa na Mwenyezi Mungu kwenye jamii ya Waisraeli.
2. Mungu huwalinda watakatifu au wenye haki.
3. Mungu hakuwalinda Yuda kwenye mauaji haya ya holocaust
na kwa hiyo Wayahudi waliokufa hawakuwa wema au watakatifu. Inawezekana kuwa
walikuwa wanatenda dhambi na maovu mengine mengi na dhana ya kwamba watenda
dhambi wote ni budi wadhaniwe kuwa walikuwa wamezaliwa kwa mara nyingine tena ili
wapate mateso ni uwongo mkubwa kabisa.
Mtazamo huu hauna mashiko na wala hauleti maana yoyote
kwa mtu mwenye busara na akili timamu awafukuze Wazungu hadi kwenye nchi
nyingine ili kuziondoa au kuzikomeshilia mbali Sheria za Mungu na wote
wanaozishika. Kuamini kuwa Mungu hakuwa anawalinda Wayahudi kwa kiasi fulani
ndipo ilipowalazimu watu hawa kuingia kwenye mazingira kwa ukweli kwamba walikuwa
kwenye imani ya uwongo ya kuabudu na walipaswa kutubu.
Ukweli ni kwamba mungu wa dunia hii anajaribu kuwaharibu
wateule na kanisa la kweli kwa raslimali za kanisa la uwongo na anajua kwamba
muda wake ni mfupi. Shetani ana wastani wa miaka ishirini na tano ijayo kabla
ya kutupwa kwake kuzimuni. Kwa kipindi hicho atajaribu kuliharibu na hata
kuliangamiza kanisa na Waisraeli na kuwaangamiza kwa kuwafutilia mbali watu
wengi.
Maelezo kama yale ya kiongozi wa Shas yanawasha hamasa na
kusababisha kusiepukike kuwepo kwa vita. Pia yanawapotosha watu kama kwenye
malengo na nia ya Biblia na utaratibu wake.
Mapokeo au Desturi ya Mitume
Hippolytus anayaelezea Mapokeo au desturi ya
Mitume 21:16 (AD 215). Je, unajua anachokiongelea? Maneno yake kuhusu ubatizo
wa watoto wachanga. Ninini maana ya Mapokeo au desturi ya Mitume? Je, ni Kitabu
kilicho kwenye Biblia? Je, kimewekewa vifungu vyake kwenye Biblia kama 21:16.
Jibu: Rejea anayoifanya Hyppolytus kwenye ubatizo ni ANF, Vol. V, p. 236 na haina rejea unayoichukua au kuitaja wewe,
wala haelezei ubatizo wa watoto wachanga hapo. Kuanzishwa kwa ubatizo wa watoto
wadogo inaonekana kuwa kulianza katika karne ya tatu, na tunakuta kuwa makala
au maandiko ya Cyprian kwenye nusu ya pili ya karne ya tatu. Kuliamuliwa kuwa
sheria ya kufanyika tohara siku ya nane isifuatwe, lakini mtoto anaweza kubatizwa
ifikapo siku ya pili au ya tatu (ANF,
ibid., pp. 353ff.).
Haikuwa na desturi
ya mitume kuwabatiza watoto wadogo kutokana na kumbukumbu tunazozijua. Kwa kweli
makala au maandiko yaliyofanywa na
Cyprian ni utetezi wa kwanza na hauonyeshi rejea
yoyote kuonyesha kama kulikuwa na desturi haka hizo kwa kuandika kwake kutetea
ubatizo wa watoto wadogo (cf. ibid., p. 354 Ep. LVIII, 3). Kwa hiyo maelezo ya Hippolytus
yanamashiko na yanapendeza.
Maelezo
yaliyotolewa na Tertullian yanaashiria pia kwamba hiyo haikuwa ni sababu, kama
alivyotangaza kuwa ubatizo unaweza kucheleweshwa hadi watoto watakapokuwa
wameikulia imani na wakiwa wanaweza kumjua Kristo. Anayataja mabishano
yaliyojitokeza kuhusu wasimamizi, nah ii inaashiria kuwa kuanzishwa kwa ubatizo
wa watoto wadogo na wasimamizi wao kulianzia miaka ya kwanza kwanza ya karne ya
tatu na alikuwa anapinga hapa kiutunzi au kiriwaya kwa maandiko ya kimakala
yahusuyo ubatizo (ANF, Vol. III, p.
678). Anasema pia kwamba kipindi cha kabla ya Pasaka kilikuwa kizuri na muafaka
kwa kufanya ubatizo. Kisha baada ya Pentekoste na siku za sikukuu, lakini kila
siku ilikuwa nzuri tu mbali ya siku hizo. Makanisa ya Mungu, yanayofanya ubatizo
wa watu wazima, kila mara yamekuwa yakibatiza kwa namna hii iwe ni wakati wa
maandalio ya Pasaka au kwenye sikukuu.
Irenaeus anasema
kwenye 2:22.4: “Kwa kuwa alikuja kuwaokoa wote kwa njia yake yeye Mwenyewe –
kama, nisemavyo, wale waliozaliwa kwa kupitia yeye wamezaliwa tena katika Mungu
– Watoto wachanga, na watoto wadogo, na wavulana, na vijana, na wazee. Kwa hiyo
yeye anapita kwenye kila umri, anajifanya kuwa mtoto mchanga kwa ajili ya
watoto wachanga; na kwa hiyo anawatakasa wale walio kwenye umri huu…”. Sasa,
Wall pamoja na wengine wanaamini kwamba huu ulikuwa ni usemi wa thamani kwa
kweli kama wa ubatizo wa watoto wachanga kwenye kanisa la kale (ANF, Vol. 1, p. 391 fn. 9). Hata hivyo,
la muhimu hapa na linalojadiliwa ni utakaso, na sio ubatizo. Usomaji wa Agano
Jipya unatuonyesha ni wapi walikuwa watoto wachanga, watoto wakubwa kidogo na
wavulana waliokuwa chini ya wazazi wao. Irenaeus haongelei kuhusu ubatizo wa
watoto wachanga. Anaongelea juu ya utakaso timilifu wa watu wote kwa njia ya
Kristo. Usemi huu haya hivyo hauwataji wanawake, hivyo basi, kupinga kwamba
tunashughulika na uhusiano wenyewe na wa moja kwa moja uliowatenga watu wa
jinsia ya kike kutoka kwenye ubatizo. Kwa hiyo, mjadala unategemea na kile
kinachojulikana na Maandiko kuhusu utakaso wa watoto wachanga.
1Wakorintho
7:12-14 inakuonyesha maana ya kweli ya kile anachokisema Irenaeus na inakuonyesha
kwamba watoto hawabatizwi bali wanawekwa wakfu kuwatakasa wakitokea kwa wazazi
waaminio, ni vivyohivyo kwa mwenzi asiyeamini anatakaswa pale wanapokubali
kuishi na mwenzi aaminiye. Narudia kusema kwamba hakuna ushahidi unaoonyesha au
kuhalalisha ubatizo wa watoto wachanga kama ulifanyika kwenye Kanisa la karne
ya kwanza, wala kama kuna kitu kinachoonekana kama kulikuwa na desturi kama
hiyo ya ubatizo. Agano Jipya, kwa kweli, limeandika matukio mengi ya ubatizo
lakini hakuna hata mfano mmoja wa kubatizwa kwa mtoto pamoja na watu wazima;
rejea muhimu iliyo kwenye Hippolytus. Maandishi mengi ya aina hii yametuama
kwenye nukuu za makosa, au makosa ya kimaandishi au ya kiutafsiri kama tuonavyo
hapa, kuunga mkono mapokeo yaliyofuata baadae ambayo hayana msingi wowote wa
Kimaandiko Matakatifu.
Ndugu alijaribu
kunishawishi kuwa mtu asingeweza kuiamini tu Biblia peke yake, bali unatakiwa
mapokeo ya mitume yanayotokana na 2Wathesaloniake 2:15; ambapo hoja yake ya
msingi ni kwamba msingi ni kwamba “umezaliwa Mkatoloki, na utakufa ukiwa
Mkatoliki, usishangae!” ni kitu gani ambacho Mungu anatuambia tukiamini kwenye
Neno Lake?
Jibu: Ni kipi anachowaambia Mafarisayo? Mmelitangua neno la
Mungu kwa mapokeo yenu. Kile kinachojulikana kama mapokeo ya mitume si kingine
tena bali ni matendo ya mitume. Biblia inasema wazi kwamba: Ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao
hapana asubuhi (Isaya 8:20). Kwa hiyo wale wanaowaendea makasisi na watumishi
wa injili wanaonena kinyume na amri za Mungu na Ushuhuda wa Yesu Kristo. Ndiyo
maana neno lipo kwenye kundi kamilifu kama hiyo, na ndiyo sababu Ukristo sasa
unajikuta ukiwanywa wa kawaida na hauwezi kumbadilisha mtu na unachanganyika au
kufanana na upagani na ushirikina. Ni kwa kuwa umechukua au kutohoa matendo yao
kwa malengo ya kisiasa na kuyaita kuwa matendo ya Kanisa.
Easter inawakilisha mungu-mke wa kipagani wa ibada za
Baali, ambaye Mungu aliwakatazwa kumwabudu wala kumtumikia kwa kupitia
watumishi wake manabii. Lakini siku hizi hii ipo kwenye ibada na maadhimisho ya
makanisa mengi. Kama Yahova ni Mungu, basi mwabuduni yeye, lakini kama Baali ni
Mungu basi mfuateni yeye. Lakini msiyaite haya kuwa ni mapokeo ya Kanisa. Soma
kwenye jarida la Maelezo ya Msingi wa Imani (Na. A1). Haya ndiyo mapokeo na desturi ya kweli au matendo ya
Mitume.
Wamormoni
Je, Mormoni ni dini
ya Kikristo? Najua kwamba wenyewe wanadai hivyo, ni kweli?
Jibu: Swali lako linahitaji ufafanuzi kuhusu ni upi Ukristo wa kweli. Dini ya
Kikristo ni ipi? Biblia inalijibu swali hilo kwenye Ufunuo 12:17 na 14:12. Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake
afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na
ushuhuda wa Yesu.
Amri za Mungu zinalenga kumfanyia ibada Mungu wa pekee na
wa Kweli, ambaye Yesu ndiye aliyemwabudu na ambaye ndiye Baba yake na Baba
yetu. Kristo alizishika Sabato na kuwa ndiyo siku ya Saba ya juma.
Aliishika Pasaka na idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Aliisadhimioha
siku ya Mganda wa Kutikiswa, kama ilivyoagizwa kwenye Walawi 23. Yeye pamoja na
Kanisa la kwanza waliishika Miandamo ya Mwezi Mpya, na Sikukuu ya Pentekoste
kama iliyoagizwa pia kwenye Walawi 23 (soma pia Wakolosai
2:16).
Yeye pamoja na Kanisa la kwanza walishika siku za
kuzipiga Baragumu na siku za Upatanisho zilizoagizwa kwenye Walawi 23. Pia
aliitunza Sikukuu ya Vibanda na Mkutano wa Makini zilizoagizwa kwenye Walawi 23.
Yeye pamoja na mitume walikula vyakula safi na nyama zisizo najisi tu kama
ilivyoagizwa kwenye Kumbukumbu la Torati 14 na Walawi 11. Alianzisha Ushirika
au Mlo wa Meza ya Bwana, ulioliwa siku ya 14 Abibu na alikua siku hiyo akiwa
kama Mwanakondoo wa Pasaka, na pia alituambia kuzishika siku hizo. Alifufuka
toka kwa wafu na Kanisa liliamini kuwa litafufuliwa toka kwa wafu atakaporudi tena.
Hawakuamini kuhusu nafsi kuendelea kuishi, au watu kwenda mbinguni, au motoni.
Hawakuzishika pia sikukuu za kipagani na hata hawakula
pamoja na wale waliokuwa kwenye imani ya wapagani ya Baali-Easter (soma jarida
la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235). Kama Wamormon
wanafanya mambo haya yote, basi watakuwa ni Wakristo wa kweli. Kama hawafanyi
hivyo, basi watakuwa sio Wakristo wa kweli. Unalotakiwa kufanya ni kuhakikisha
kuwa unayafanya haya yote, na kuishi sawasawa na alivyoishi Kristo na mitume wake
walivyoishi, na utakuwa Mkristo wa kweli. Yeyote asiyefanya mambo yaliyoorodheshwa
hapo juu sio Mkristo wa kweli. Tukimpenda yeye, na tuzishike Amri zake.
Nina bwaadhi ya Wamormoni
wanaonitembelea na niliwauliza kuhusu imani yao kuhusu ubatizo wao wa wafu na jinsi
wanavyofuatilia vizazi vilivyopita ili wapate majina ya kuwabatiza. Walionekana
kuwa wanahisi kuwa mtu asiyebatizwa hawaweza kuokolewa. 'Mormo' aliorodheshwa kuwa
ni Mfalme wa Waghouli au wafu wanaoendelea kuishi na Lavey kwenye biblia ya
kishetani. Je, hili ni jina la kimotoni wakati Wamormoni wanapopewa majina yao?
Jibu: Dhana ya kuishi tena kwa wafu ni ya uwongo kabisa na ni
kosa kubwa kuiita kuwa inatokana na mafundisho ya Biblia. Ndiyo, LaVey anamtaja
Mormo kuwa ni mungu wa wafu na inafanana sana na kwamba aina hoo ya utani ilihusishwa
kwenye imani ya Kimormoni tangu kuazishwa kwake. Kwa sasa imekuwa ni
mkanganyiko wa kidini. Jina la Mormon linamaana ya mfuasi wa Mormo mungu wa
Wafu. Na ndiyo maana baadhi yao wanalipinga jina hili. Hata hivyo, wanaainisha
na kukubaliana na mambo yote ya dini hizi potofu za wafu. Wanadhania tu kwamba
wasicheweza kufanya ni kufufua wafu kwa kutumia taratibu za kidini za sikukuu.
Ni njama ya kujua mishabihiano migeni na mabadiliko kwenye
majina na taratibu za kidini za Wamormoni. Mihimili yao ina alama za Freemasoni
na hususan ni za taratibu za kiibada za mafreemasoni wa Kiscoti kwenye maandishi
yao yote ya zamani. Hata mahekalu yao ya zamani na michoro yao vimefanywa kwa
kufanya rejea za mahekalu ya Kimasoni. Gazeti lao la zamani lilikuwa
linaonyesha moja kwa moja harakati za kiokaliti.
Unapaswa kukiona hiki na kuwa na uelewa wa ufreemasoni na
alama na nembo zao ili uweze kuwasifia kiukweli, lakini ni wazi sana kwamba
ilianzishwa na deturi za kidini ya freemasoni wa Kiscochi na ya Kimormoni waliotohoa
desturi za kiutandawazi za kidunia. Hiyo ilikuwa moja wapo ya sababu iliyopelekea
wakashambuliwa na kuuawa na ikawalazimu kukimbia kutoka Missouri. Adhabu
inayotolewa kwa kuzisaliti siri za dini hii ni kifo. Uadilifu wao, kama ilivyo
kwenye imani na taratibu za Wakatoliki wa Roma umeenea na kupita hata kwenye mipaka
ya kitaifa.
Wafuasi wengi wa Kimormoni na hususan wanawake
hawaonekani kuelewa hilo. Maswali mengi hayawezi kujibiwa kwenye maeneo fulani
na muhimu na huenda mengine yanapaswa kushikwa kutoka hadharani pia.
Malaika Moroni aliyetoa Kitabu cha Mormon ana sehemu yake
muhimu kwenye kisanamu cha lugha ya Kiebrania cha herufi “i” che maana maalumu
ya “the” kwa mfano “kabila au watu wa” kwa mfano Waashikenazi wenye maana ya
wana wa Ashikenazi (ambao walikuwa ni wana wa Gomeri). Malaika Moroni ana
sehemu yake kwenye kumuumba malaika wa Wamoroni akitumia
hisia au vitu vinavyokubalika vya neno.
Matukio ni mengi sana kufanyika kuwa ya bahati mbaya.
Yeyote aliyepangilia kuanzishwa kwa dini alikuwa na uelewa mkubwa wa
ufreemasoni na uokaliti na ana kiwango kikubwa sana cha ujanja wa hisia ya
mvuto.
Nimesikia kwamba
Wamormoni huvaa wanayoyaita kuwa ni mavai matakatifu na kwamba wana alama au
michoro wanayochapwa miilini mwao. Je, uvumi huu ni wa kweli? Na kama ni hivyo,
ni nini maana yake mambo haya?
Jibu: Hili ni swali zuri sana. Ufuatao hapa chini ni ushuhuda uliotolewa
na muumini wa zamani na alioiasi dini hii ya Wamormoni wenye kichwa cha somo
cha:
Habari za Msingi Kuhusu
Mavazi ya Hekaluni
“Imekuwa ni muda kitambo sasa (takriban miaka kumi
imepita sasa) tangu niliponunua au kuvaa mavazi haya, lakini licha ya mabadiliko
yoyote yaliyowahi kufanyika tangu hapo, hivi ndivyo nijuavyo: Mavazi ya Hekaluni
yanavaliwa kwa mara ya kwanza baada ya mtu kuwa amepokea “wakfu au nadhiri”
chake cha kwanza cha Hekaluni. Wakati huu wa uwekaji nadhiri wake, mtu huyu
anapewa “jina jipya”, anafundishwa habari au hadithi ya uumbaji wa dinia (kwa
mujibu wa mtazamo wa LDS), na anawekwa nadhiri zinazojiri imani yake, na huku
aikjifunza namna atakavyoingia kwenye Ufalme ulio Bora zaidi, na anapewa maelekezo
kwa vitu vingine. miongoni mwa mambo anayoelekezwa ni uvaaji wa adabu au mzuri
wa mavazi ya Hekaluni. Mavazi haya yanatakiwa yavaliwe ndani ya nguo ya mtu
huyo na kwa nyakati zote, isipokuwa kwenye nyakati zilizotengwa kwa ajili ya utoaji
wa maombi ya mtu mwenyewe, ambapo mavazi haya yanaweza kuonekana na wasiokuwa
waumini au pale yanapoonekana yanaweza kuzuia matendo mengine yasiyo na maana.
Kwa mfano, nilionyesha mahali ambapo mavazi haya yanaweza kuvuliwa wakati wa
kuoga, wakati wa kufanya ngono, matendo mengine kama vile ya kuogelea (ambapo
yangechukuliwa kuwa yamefichwa hata na waogeleaji mahiri na yangeweza kulowa),
na wakati wa kwenda kwenye ofisi ya daktari au hospitalini, ambako yangeweza
kuonekana kirahisi na wasio waumini wenzetu. Wahudumu wa hekalu walielezea kwamba
kulikuwa na mazingira mengine ambayo mavazi haya yanaweza kuvuliwa kwa muda,
yasiyo muafaka kwa mvaaji wa mavazi haya, lakini mavazi haya yalikuwa ni kiini
cha mambo yote mawili, yaani yana ulinzi wa kiroho na wa kimwili, na yanatakiwa
yavaliwe kila wakati kama ikiwezekana. Kwa mfano, haikushuriwa kuyavua
unaposafiri au wakati wa kulala na kulala bila kuwanayo.
Wakati Fulani kwenye ibada ya Kufunga saumu na Uhuhuda,
nakumbuka nilimsikia mtu aliyekuwa mshauri wa idara ya vijana wakati nilipokuwa
kijana wa umri wa miaka ya makumi akielezea jinsi vai lake lilivyomlinda dhidi
ya hatari ya kuumia kimwili. Alikuwa kwenye kituo cha kununua mafuta ya gari au
petrol na alikuwa anatia gesi au mafuta kwenye gari. Gari lake lilikuwa no moja
ya yaliyokuwa yamefungua tangi la kutilia gesi au mafuta akiwa karibu na gari
chini uvunguni mwa kishikio cha pleti namba. Ghafla, gari likaana kurudi nyuma
upande wake na kumbambia katikati ya bampa la gari lake ya bampa la gari la
karibu yake na kwenye usawa wa magoti yake. Alishuhudia kwamba sehemu ya goti
lake ilikwamba katikati ya hizi bampa mbili na goti lilikuwa limefunikwa na
mavazi yake, na lilikuwa “limechubuliwa tu badala ya kuvunjika.” Aliamini kuwa
huu ulikuwa ni ushahidi wa tosha wa nguvu za ulinzi wa mavazi haya. Lakini
haionyeshi wazi kwamba kishindo cha mgongano hakikutosha kuvunja mguu wake? Wakati
kwamba hii ikiwa ni hadithi yake kuu ya pekee kuhusu nguvu za ulinzi zitokanazo
na mavazi nilizowahi kuzisikia, nimeendelelea kuzisikia hadithi nyingine nyingi
kadhaa za michapo, hadithi nyingine zenye utata za vijijini za Wanormon,
zinazonuia “kuikuza imani”. Hadithi moja inatuama kwenye mtu wa LDS ambaye
alikuwa amepigwa na radi. Kina dada wawili wa LDS waliiona radi ikimpiga
katikati ya shamba na wakamkimbilia. Walipomkarinia, waliona kuwa amekufa, na
kuungua vibaya sana usoni kwake, na chini ya mikono yake, na chini ya miguu
yake. “Lakini tazama” dada mmoja anamwambia mwenzake, “kila mahali alipofunika mavazi
mwili wake hapajaungua!” Na kwa kweli, mavazi na ngozi ili chini yake haikuguswa.
Nilidhani kuwa hii ilikuwa ni hadithi ya kukanganya nilipoisikia. Nina
maanisha, aliinuka, kumbe amekufa! Ni tofauti gani hapa iliyofanyika kwa kusema
kwamba sanamu yake ilikuwa na shepu nzuri wakati kichwa chake kimeungua? Huenda
wanahitaji kutengeneza mavazi ya miti...
Kadiri muonekano halisi wa mavazi unapoishia ndipo
zinaonekana kwa kiasi fulani kama toleo la chupi cha aina ya long john yaani
“john mrefu”. Mavazi ya wanaume yana longp senye marinda au mikunjo mifupi na
mishipi ambazo kidogo zimekuwa "zimechongwa" kuliko Fulana halisi za
wanaume. Pande zake za chini zinfika hadi juu ya magoti. Nguo za wanawake ziko
sawa tu na hizo ipokuwa kuna uchaguzi ulio tofauti na upande wa shingoni (imechongwa,
V, au kwa usawa), na kola zimefupishwa kuliko zile za wanaume, zikionekana kama
“kingo za kofia.
wote wawili, yaani wanaume na wanawake wanaingia ndani ama kwa mtindo wa
kipande kimoja ai vipande viwili, na kwa uzito mbalimbali uliotengenezwa na kufanana,
kama vile nailoni, pamba, mchanganiko wa pamba na polista. Mavazi yote ya
Hekaluni ni meupe kabisa, ingawa nimesikia kwamba pia zinatokana na mafuta ya drabu
kwa watu wa LDS jeshini, lakini sijawahi kuona hayo. Mavazi yote ya Hekalu yamewekwa
chapa na kuwekwa alama upande wa kulia kwa matiti yake, nevali, na gotini.
Michoro hii imedariziwa, kwenye vazi kwa uzi mweupe (ingawa kwa habari ya
mavazi ya kijeshi yanaweza kabisa kuwa ni ya uzi wa drabu ya mzeituni.) Michoro
hii inamaanisha vipengele fulani kutoka kwenye sherehe za viapo au nadhiri za
Hekaluni. Waumini wanajulishwa kuwa hawaruhusiwi kunyoa nywele zao. Wala
wasisuke, wala kubadilisha mavazi au nguo zao kwa namna yoyote. Kwa mfano, hayaruhusiwi
kupunguzwa au kufupishwa, kubanwa, au kuruhusu uvaaji wa nguo fupi au jozi ya
kaptula. Isivyo kawaida ni kanuni “isiyobadiliki” inaweza kufanywa kwa waumini
waliokuwa na ulemavu kimwili.
Wakati yanapozaliwa mavazi haya, waumini wanashauriwa
kugawanya maeneo kwa vipande vya kudarizi kwa mkasi na kuzichoma. Michomo hii
inapotoka, nguo zinakuwa hazichukuliwi teba kuwa takatifu, na zinaweza kutumika
kama makapi yenye vumbi, kama na uvaaji wa mavazi.”
--Serratia
Useja au Umonastiki
Umonastisism ni kitu gani na umetoka wapi?
Jibu: Mwanzo wake hasa, umonastiki ulijumuishwa kwa kushirikiana
na dini potofu za mungu Attis na I,ani au dini ya washika Easter ya Asia Ndogo.
Makuhani wa mungu-mke huyu walijulikana kama Essene (usiwachanganye na jamii ya
Qumran ambao Pliny aliwaita hivyo), waliishi maisha ya useja na waliuendeleza na
wengine walijikuta wakihanithika wakiitumikia miungu.
Wakati dini hizi zilipoingia kwenye Ukristo na kupelekea
imani ya Easter pamoja nao, ni sawa tu na itikadi ya kiasetiki ambayo pia
iliingiza imani yake. Wamonastiki wa kwanza, au mtu aliyeaminiwa kuwa alinzisha
msingi wa Umonastiki wa Kikristo, ni Anthony. Athanasius anaaminika kwa uandishi
wa mambo yahusuyo maisha yake, na alifanyika kuwa mashuhuri huenda ni kutokana
na ukweli huo kwenye karne ya nne.
Kumekuwa na mabishano fulani kwa wakati halisi wa maisha
yake, na wengine wamekuwa hata wakipinga uwepo wake. Ukweli wa mambo ni kwamba
Wamonastiki wa kwanza walikuwa ni waasetiki ambao hawakuishi kijamii au mahali
pamoja, kama inavyojulikana sasa. Waliishi kwenye vikundi vidogovidogo, kama
sehemu iliyochanganyika.
Mtindo huu wa maisha kidogokidogo ukafanyika kuwa maarufu
na, katika nyakati ya zama kati. Amri za kimonastiki zilifanyika kuwa mamlaka
kamili na hatimaye, kwenye karne ya ishirini, waliwaondoa mashemasi wa kike na
makasisi waliooa kutoka kwenye majumba ya kitawa na wazee wote na makasisi wa
kanisa kwa ujumla.
Unostiki
Ni nini maana ya Bythus?
Jibu: Bythus ni jina la kuzimuni ya Kinostiki lakini kama
yalivyo mambo mengine yote walionekana kuwa walifanya mgegeuzi juu yake kama
vile ulivyokuwepo kama kuzimuni ya Mungu anayeendelea kutoka urefu usioonekana
na asiyeonekana na asiye na jina wa uwepo halisia wa Aeon ambao walimuita
mkanunishi wa kwanza ambaye ni Muasisi na Bythus.
Hippolytus (vi, 37) anamuelezea Mnostiki Valentinus anayesema
kwamba: Yeye anaye muongelea Plato kuwa ni mfalme wa wote, mtu huyu alidhaniwa
kuwa kama baba na Bythus na ni mkanunishi wa kwanza wa hawa aeons.
Wavalentiniani wanaamini kuwa kuwa mchakato wa kujihimili
mwenyewe. Wabythus waligeuka kuwa mikururu ya jozi za aeons, wakiume na wa
kike, jozi yoyote inayoitwa pleroma. Hawa Aeon walikuwa ni umoja, uliojionyesha
wenyewe kama uwingi.
Unostiki uliofuatia baadae wanawashuhudia kama muunganiko
uwepo wa Mbingu unaoendelea kwenye jozi kutoka Baba Mwenyezi, kila jozi
iliungana na nyingine, ikitokea kwenye ukuu kama inavyokuwa ki undani zaidi
kutoka kwenye chanzo chake (ERE,
Aeons, Vol. 1, p. 149).
Mafundisho ya Syzygies yana aina ya ushabihiano na imani
ya Kimithrai pia na zote mbili zometoholewa kutoka kwenye imani za Kibabeloni,
ambako Unostiki umetokea na ukaingizwa tu kiurahisi (soma ERE, ibid). Kwa hiyo wao pia wana ushirika na imani ya Kishinto ya
Japani, Umahayana Ubudha, Uzoroastriani, Mawazo ya Kiplatoniki, Nguvu za Uphilo
na Ulogoi wa Kitoiki na kadhalika wa kadhalika.
Imani ya Shinto ilianzia huko Kojiki ikituama kwenye
imani kamili kabisa ya miungu mingi yaani upantheism. Ni kama Izanagi na
Izanami wakuu wa kiume na wa kike wameonyeshwa na kuonyeshwa kama ulafi mkubwa
sana. Hawa Aeons wenye kuzaa wanatokana na miungu shabihika.
Kwenye Shule ya Kaskazini ya Adibuddha, Mabudha watano wa
kuwatafakaria sana (Vairochana, Aksobhya, Ratnasambhava, Amitabha, na
Amoghasiddhi) zinaonyesha na kuonyesha mambo matatu na imani ya Kibudha ya kuifanyia
tafakari sana, chimbuko la dunia tamo, ambayo kiufanisi wanafanya ulimwengu. Walifanyika
kuwa mambo matano ya dunia, maji, moto, hewa na nginezo au uhafidhina wa Kibrahma.
Wazoroastrian wanafanana lakini imani ya ukuwili ya waaeon kwenye falme za Nuru
na Giza. Ahuramazda anaongoza ufalme wa Nuru na Ahriman
anauongoza ufalme wa Giza.
Pleroma ya Kinostiki lilikuwa pia jina kwenye mkururu
wote uliotolewa pamoja ambalo hatimaye imetuama kwenye Bythus kwenye uhusino wa
kike kama Tiamat alivyomfanyia Apsu. Hata hivyo, Unostiki hauundi kabisa mfumo
wa kimwili wa homojinazi ya mbadala.
Hippolytus anatuonya sisi kwamba kulikuwa na fursa nyingi
miongoni mwao kuhusu Bythus yenyewe. Wenye kutafakari wengine waliamini kwamba Bythus
kuwa nje ya pleroma wakati wengine wakimchukulia yeye kuwa ndani yake bali ni
kujitenganisha kutoka kwa wengine na Horus ambaye alionekana kama mpaka (soma ERE, Vol. 1, pp. 54-55) na huenda hii
inaweka taswira dini za kisirisiri za Wamisri, na misukumo ya uchumi jamii wa
Kinostiki, kwa mujibu wa Wayunani, inayotuama kwenye imani ya Waalexandria.
Wengine pia wanamuondoa Bythus kutoka kwenye uongozi wa
mkururu na kumfanya kuwa amfuate ogdoad. Wengine walimdhania yeye kuwa ni kama
asiye fungamana, wengine ni kama kiandrojeni au mwenye jinsia. Wengine walimpa
yeye Sige kama mshirika au mwenzi wake na wengine nguvu mbili Mawazo na Utashi.
Uhusiano wa udadisi wa Kinostiki kuhusu Bythus umeonyeshwa
na kuashiria kwa sentensi moja ya tu ya Irenaeus
(ap. Epiphaneus xxxii, 7) "Kwa kuwa wengine wanasema kwamba yeye hajafungandoa
na wala sio mwanaume wala si mwanamke, wala kwa kweli, hana lolote
kabisa." Huenda hii ni rejea inayozua maswali.
Kwa namna nyingine alikuwa ameonyeshwa kwwnyw mitazamo ya
Wabudha wengi aliwa ameinuliwa juu ya vyote vinavyopingana. Utambulisho Wote usio
na Maana; Kiumbe ambaye kwaye hata uwepo wake hauwezi kutabirika. Ni kutokana
na dhana hii ya Kinostiki ambao dini za Kisirisiri zilianzisha na kuendeleza mchakato
wa kimawazo:
"Niliwaona na kuwajua viumbe wote, Byss na Abyss, na
kizazi cha milele cha Utatu Mtakatifu, kizazi na chanzo cha ulimwengu na cha
viumbe wote kwa kupitia Hekima Takatifu" (Jacob Behmen, alinukuliwa na
James, kwenye kitabu chake cha Varieties
of Religious Experience [Uzoefu wa Dini Mbalimbali, p. 411 na pia cha ERE, ibid, p. 55).
Unailinganishaje
imani yako ya Kikristo na mafundisho yako ya desturi za zamani na uhusiano
uliopo kati ya zile za Mashariki ya Kati na zile za Amerika ya Kusini? – Ni
vipi kuhusu mafundisho kuhusu kwenda Mbinguni na Motoni?
Jibu: Inaonekama kuwa hakuna mgongano uliopo kati ya kwa kweli
inachikisema Biblia na kile walichokikuta Wanasayansi kwa kila siku. Mgongano unatuama kwa unachokisema Ukristo wa kisasa na
wa kimamboleo.
Kwa mfano hatuyaamini wala hatujawahi kuyaamini
mafundisho kuhusu kwenda Mbinguni na kuishi milele Motoni. Haya siyo Mafundisho
ya Kikristo. Yaliingizwa kutoka kwenye imani ya Kinostiki kwenye karne ya pili.
Justin Martyr alisema kwenye kitabu chake cha Dialogue with Trypho [Majadiliano na Trypho]
yaliyokusudiwa na Wayahudi kwa niaba ya Kanisa huko Roma kwenye miaka ya 150-155
kwamba yalikuja karibu na watu waliodai kuwa wao ni Wakristo na kusema kwamba
kama wakifa walikuwa wanakwenda Mbinguni, hawakuchukuliwa kuwa ni Wakristo.
Hili lilikuwa ni swali la kumpima mtu ili kumjua kumbaini
kama ni Mkristo wa kweli au kama alikuwa ni Mkristo wa uwongo na ingali bado
inatumika kuwapima Wakristo wa kweli. Fundisho la roho au nasfi kuendelea
kuishi na watu kwenda mbinguni na la watu kuchomwa motoni na kuishi humo milele
sio la kimungu kabisa na ni la kufuru na wakati wote limekuwa likichukuliwa
kuwa hivyo na Kanisa la kweli la Wakristo, Kanisa ambalo ndilo tuliloko sisi.
Mambo haya yameainishwa kwa kina kwenye majarida ya Nafsi Hai (Na. 92); Ufufuo wa Wafu (Na. 143); Milenia na Unyakuo (Na. 95) na Mji wa Mungu (Na. 180). Mafundisho ya Kinostiki na historia yake yamechambuliwa
piwa kwenye majarida ya Wanikolai (Na. 202) na Imani ya Ulaji wa Mbogamboga Tupu Kwenye
Biblia (Na. 183). Utafaidi pia kujisomea majarida ya Wanefili (Na. 154) na Mchanganuo wa Ratiba ya Nyakati-Zama (Na.
272).
Je, ni lazima kwa mtoto
mchanga wa wazazi Wakristo abatizwe au sio lazima?
Jibu: Kitendo cha
kutahiri huenda ni moja ya sharia ya zamani sana ya watu wote waliostaarabika.
Kitendo hiki kinakutikana kwenye makabila yote na sehemu zote (kama
linavyoeleea jarida la Utakaso na Tohara (Na. 251)). Tohara ina matokeo mazuri na ya manufaa hasa kwenye maeneo yenye
hali ya joto ya jangwani ambako inasaidia kuzuia magonjwa. Mbali na hali hiyo, chimbuko
la kitendo hiki linaonekana kuwa na uhusiano wa tofauti na dhana ya kuamini
kuzaliwa tena na tena au inayoamini kuzaliwa tena na mara nyingi kwa kiumbe
mmoja. Tangu siku za zamani sana za zamani, govi la mwanaume aliyetahiriwa
liliwekwa kwenye maeneo ya umbali fulani na uliojulikana kutoka kwenye zakari za
wanaume waliotahiriwa, ama kwenye mapango au kwenye miti pia. Tangu hapo
tunaweza sasa kusema, inaonekana kwamba kitendo cha kutahiri kwa kweli
kinatuama kwenye dhana ya kuzaliwa mara nyingi, tena na tena kwa mtu kwenye
miili ya wazazi wa uzao mbalimbali. Hii inaonekana kuwa imechukuliwa zaidi kuwa
ni kama ni dhana na imani iliyokuwepo kwenye makabila yote ya zamani. Ina jinsi
maalumu ya kuyachukulia kuwa ni dhana ya uwongo kwenye dhambi ya asili au
mwanzo wa dhambi, ikipodanganya kwamba, hutakufa hakika.
Inaonekana kuwa kwa kutoa agizo la kutahiri alipewa Ibrahimu kama ni
laima kwa mtoto anapofikia siku ya nane (wakati mgando wa damu unapoanza
kutokea), kwa kweli Mungu alikuwa anaingilia kati na kutoa maana halisi ya moja
kwa moja ya kukomeshwa kwa matendo ya kipagani. Mungu alisema, “Mini ndimi mwamba
au gumegume lako na ni asili ya ufufuo wako na mwendelezaji w uhai au uzima
wako.” Hivyo ililazimu ifanyike siku ya nane na siyo wakati wa kubalehe, ikiondolewa
kutoka kwenye uume wa mtu na kuuweka kwenye kiwango zawadi iliyotolewa bure na
Mungu kama mshirika wa taifa la Israeli. Mungu alikuwa anapingana na uwongo wa
mafundisho ya roho kuendelea kuishi na lile la mtu kuzaliwa tena na tena,
ambayo ni mafundisho ya kipagani nay a kishetani ya imani za miungu Sin na
Ishtar (kama yasemavyo majarida ya Ndama wa Dhahabu (Na. 222) na Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235)).
Kwenye kanisa la kwanza mjadala kuhusu tohara uliibuka na wale walioitwa
wa mrengo wa Kihelleniki walikataa na kuupinga na waliokuwa kwenye mrengo wa
Kiyahudi waliukubali na kupenda uendelezwe (Matendo 11:2; 15:1,5; 21:21). Mtume
Paulo yeye mwenyewe alikuwa ametahiriwa na, kwa shinikizo la Wayahudi, alimtahiri
Timotheo (Wafilipi 3:5; Matendo 16:3). Aliichukulia hii kama alama ya upendeleo
wa Mungu kwa taifa (Warumi 3:1 ff.). Hata hivyo, kwa habari ya waongofu wa
Mataifa, ilichukuliwa kuwa ni kama si kitu cha lazima (Matendo 15:19 ff.; sawa
na Wagalatia 5:2-4). Paulo aliuchukulia uwepo au kutokuwepo kwa tohara hii ya
mwili kama haikumaanisha kuwa ni agano kati ya mwanaume mtu mzima na Mungu (Warumi
3:30f.; 4:9ff.; 1Wakorintho 7:18f.; Wagalatia 5:6; 6:12f.; Wakolosai 3:11). Kwa
imani Sheria iliwekwa na utakatifu unapatikana kwa njia ya imani. Kwa kuwa wao
wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sharia, bali wanajaribu kujitukuza kimwili kwa
sisi tunaozishika sharia (Wagalatia 6:12ff.). kwa kuwa ni kwa tohara ya kweli
pekee ni kiroho. Kwenye fundisho hili Paulo anamlazimisha tena Yeremia (Yeremia
4:4; 6:10; 9:26; sawa na Kumbukumbu la Torati 10:16; 30:6). Anaruhusu kuwa na
kanuni za kuepukana nazo kwenye mazingira yake maalumu (Matendo 16:3, Wagalatia
2:1).
Dini za wasoamini Utatu waitwao Waariani walikubaliana na Waamini Utatu
au Watrinitariani kwa suala hili. Waamini Utatu au Wakatoliki walitwaa madaraka
muda mfupi tu baada ya hilo mwaka 590 na wakaianzisha iliyokuwa inaitwa Dola
Takatifu ya Rumi. Eugene IV aliwapa rasmi maafisa wa Kanisa Katoliki la Roma
usemi au meno kwenye Tangazo lake lijulikanalu kama Cantate Domino (tarehe 4 Februari 1441). Alidai kwamba ulazima na
kanuni za Torati, hata hivyo ni sahihi kwa muda kitambo, kwamba zilitenguliwa
kwa ujio wake Kristo na kwa sakramenti za Agano Jipya. Kwa hiyo, ubatizo
ulikuja onekana kuwa ni kama umechukua mahala pa tohara.
Kwenye Kanisa la Kikoptiki, ubatizo haukuonekana kama umechukua mahali pa
tohara. Wakati ubatizo wa watoto wachanga ulipoanzishwa, vijana walibatizwa
wakiwa na umri wa siku 40 na wasichana wakiwa na umri wa siku 80. Utaratibu huu
ulifanya taswira hasa hasa kwamba sharia ya utakaso na tohara ya wanaume
ilibakia kwa ujumla (ERE, vol. 4, p.
119). Wakoptiki walikuwa ni sehemu ya Kanisa la Wakristo wa kwanza kabisa la
Kaskazini mwa Afrika lilikuwa nchini Misri. Walijitenga na kile kinachoitwa
kanisa la Kiorthodox yapata mwaka 451 kama matokeo ya mafundisho ya kuibuka
kutoka mitaguso ya (mwaka 381) na Chalcedon (mwaka 451). Inaweza kabisa
kufanyiwa hoja kutokana na ushahidi wa Wakoptiki, kwamba ubatizo haukuonekana
kama ni mbadala wa tohara. Wakati Wakoptiki walipoanza kufanya ubatizo wa
watoto wadogo uliotuama kwenye utofautishaji wa wanaume na wanawake, wanawake
walikuwa bado wakikeketwa, ni kama ilivyokuwa ikifanyika katika Israeli ya
kale. Kwa hiyo, wanaume na tohara yenyewe ilionekana kama ni mambo
yaliyotofauti kwenye tofauti ya utakaso, uliofanya taswira ya tofauti ya
kibiblia.
Tunaweza kuhitimisha kuhusu matendo au imani ya kanisa la kwanza la
Kikoptiki wa kwanza, ambayo yalitendwa pia kwenye dini au madhehebu ya Wasabato
huko Ulaya na Asia Ndogo, kwamba tohara ya watoto wadogo ilichukuliwa kuwa ni
wa muhimu kama sehemu ya taifa la Israeli na Kanisa. Ni wanaume Wapagani tu
ndio hawakulazimika kutahiriwa, wakati walipoingia Kanisani wakiwa watu wazima.
Kwavile kitendo cha kutahiri mwili kilikuwa kinatoa njia ya kutimilika kwa
ubatizo wa kiroho na tohara ya moyo, na kwa kuwa ubatizo wa watoto wadogo
haukuwa ukifanyika kwenye kanisa la kwanza (sawa na lisemavyo jarida la Toba na Ubatizo (Na. 52)), ilifuatia kwamba tohara ya mwili ya
siku ya nane kwa wamtoto wa kiume wanaozaliwa ilikuwa ni ishara ya taifa la
Israeli kama Kanisa. Wakati Kanisani, Wamataifa walikuwa wanawatahiri watoto wao,
kama alivyofanya kila mtu. Kitendo hiki kilikuwa ni cha jumla na hakisemwa
dhidi ya urasmi kwenye imani ya Kikatoliki hadi kwenye karne ya kumi na tano.
Tunaweza kupunguza kutoka kwenye uhusiano wa siku saba za utakaso na matendo ya
tohara ya siku ya saba zinazohusiana na mpango wa wokovu. Siku ya saba ya
utakaso ni taswira ya hatima ya utawala wa milenia na kutakaswa kwa dunia. Siku
ya nane ni taswira ya ufufuo wa mwisho na kufanywa upya kwa wote wenye mwili hapa
duniani, ikiwa kama sehemu ya taifa la Israeli na ambayo ndiyo Mji wa Mungu (sawa
na isemavyo Ufunuo 21:1-3 na jarida la Mji wa Mungu (Na. 180)).
Imani ya Kibudha
Je, unafikiri nini
kuhusu imani ya Kibudha? Je, imani hii ya Kibudha na Ukristo vinaweza kuwa na
lengo moja?
Jibu: Ubudha ni dini ambayo inamuono tofauti. Unapinga uwepo wa
Mungu kwa kiwango kikubwa sana. Ni chimbuko la kile kinachojulikana kama usiku
wa kshatryan Sidartha au Guatama katika karne ya sita KK aliyofundisha na kueleea
mzunguko wa mara nyingi za mzunguko wa Aryan Hindus kama ni falsafa iliyokuwa
imejikita kwa Wayunani iliyobuniwa kwa madhmuni hayohayo kuyaelezea na
iliyofundishwa kwenye Dini za Wahyperborean wa Uingereza na Ulaya.
Ukristo ni imani inayomtegemea na kumwamini Mungu kabisa na
haifundishi kuwa na kitu kingine chochote kabisa cha kukitumainia na wala kuwa
na kitu kingine chochote cha bandia ili wakitumainie. Chimbuko la imani ya
Kibudha limeelezewa kwa kina kwenye jarida la Imani za Kisirisiri Sura ya 7 Ubudha (Na.
B7_7).
Je, unahabari
zozote kuhusu Dalai Lama?
Jibu: Maisha na habari za Tenzin Gyatso, Dalai Lama wa 14
zinakutikana kwenye tovuti ya www.dalailama.com.
Dalai ni neno la Kimongolia ambalo maana yake ni "Bahari"
na Lama ni neno la Kitibeti lenye maana ya "mwalimu wa Kiroho" na kwa
hiyo wanaamini kwamba yeye ni Bahari ya Hekima.
Kwa mujibu wa imani yao, wanaamini kuwa yeye ametokana ma mzunguko wa 14 la
mzunguo wake wa kuzaliwa ki marudio rudio tangu Dalai Lama wa kwanza.
Kuna akina Lama wengi sana huko Tibeti walio kwenye
madaraja mbalimbali ya vueo. Wamechaguliwa kama watoto kwa mujibu wa mafundisho
yao ya kurudia kuzaliwa mara kwa mara na dhana ya kwamba watu wamerudia
kuzaliwa mara kwa mara kwa mujibu wa sharia ya imani ya Dharma. Ni sawa na kama
shubaka kubwa ya salio au deni/malipo au kikombozi ambacho kinawasumbua watu
kwenye mtindo wa uwepo waliodai kustahili kwa sababu ya kile walichokifanya
kwenye maisha yaliyopita.
Sioni talasimu zikitajwa
kwenye Biblia, kwani sio muhimu kuzijua?
Jibu: Suala la talasimu kwenye matatizo halisi ya kimwili
kwenye imani ya Budha na dini zilizopewa ushawishi nazo. Biblia haielezei kuhusu
hizo kwa kuwa hazina umuhimu kwa wokovu wa mwanadamu.
Zinatumiwa kwa uwanja au nyanja fulani ya mzuto wa
kielektroniki lakini hazina madhara kwa kushughulikia mpango wa wokovu na mwili
wa Kristo.
Vipi kuhusu suala
la uponyaji? Kuna vitabu vingi sana vinavyofundisha uponyaji unaotumia talasimu.
Jibu: Suala la uonyaji ni la kiimani. Uponyaji unaouongelea ni
wa taratibu za imani za Kihindu na Kibudha.
Utasitasita kwenye njia mbili hadi lini? Kama Yahova ni
Mungu mfuate yeye lakini kama Baali ni Mungu, basi mfuate yeye.
Imani ya Kihindu
No kwa jinsi ipi
imani ya Kihindu inaonekana kama ni ya kikumene?
Jibu: Imani ya Kihindu ni ya mfumo wa kujumuisha miungu mingi,
ambayo ndiyo maana hasa ya ukumene kwa maana kwamba ina mkusanyiko wa jopo la
miungu kwenye uwingi wake wa kiungu kama unavyodhaniwa au kuonekana kuwa inafaa
kwenye imani yake yenyewe. Haiendani wala kuchukuliana na mifumo mingine
inayokanganya na mijumuisho ya kidunia au kosmolojia.
Na ndiyo maana unazidisha uadui wa kuzichukia misheni za
kuendeleza Ukristo. Imani hii ya Budha ilianzishwa huko India ikiwa ni matokeo ya
tabaka la uhafidhina mgumu na imani au mfumo wa boma wa Kihindu. Uislamu
uliingizwa huko na wapiganaji walioshinda na imani hii ilianzishwa kutokana na
ukweli huo. Kitendo cha kuigawanya India na uadui kulikosababishwa na migogoro
ya kidini kuliendelea hadi kukapelekea vita nyukilia. Haiwezi kuhesabiwa kati
ya dini za “kikumene”.
Mwalimu wangu
anasema kwamba Agano la Kale linaonyesha kuwa imani hii ilikuwepo tangu mwaka 600
KK, lakini hili ni wazo au dhana inayotokana na Rig Veda ambayo ni ya kale
kidogo. Hitimisho, ni kwamba mwandishi wa Biblia aliifanya ituame kwenye imani
za ‘kisirisiri au za kimizimu’ za hapo nyuma. Kama ningejua ni lini Gombo za
Bahari ya Chumvi au Dead Sea Scrolls zilionyesha tarehe za nyuma ilivyoanza (alikuwa
kwa kiasi kikubwa sana analinganisha na matukio ya kitabu cha Mwanzo) ndipo
ningeweza kumwambia kuwa amekosea. Je, unajua?
Jibu: Anakaribia sana na imani ya Kihindu. Rig Veda ilituama kwenye
hadithi potofu za Kimizimu za Kiaryani za Mwanzo wa uumbaji, ambazo
zilichukuliwa na kuingizwa huko India yapata mwaka 1000 KK.
Mungu wa Utatu aliingizwa
huko India mwaka 1700 KK kutoka Ashuru, na wakati huo huo aliingizwa nchini
Israeli na mababa waliokuwa wakiishi Misri. Soma kwenye
kitabu cha Wolperts, cha “Historia Mpya ya India (A New History of India).” Hesabu ya kitarehe ya Biblia ya mwaka 600 KK
ni msukumo mkubwa sana. Soma
kwenye jarida la Biblia (Na. 164). Litakupa tarehe zake na taratibu zake. Miungu ya
Kihindu ina tabia zinazofanana na iliyoandikwa kwenye maandiko ya Kikaldayo/Kiebrania
yaliyoonyesha namna walivyoabudu Mababa wa imani.
Mimi ni Muhindu na
kwa sasa nasoma kwenye Shule ya Kihindu, hapa Bahrain. Nina maswali yafuatayo:
1) Umuhimu wa kusherehekea
sikukuu za kdini za Kitaifa nikiwa nyumbani kwangu au mashuleni?
2) Je, unaweza
kuniambia kuhusu sikukuu ya Kihindu ya Raksha Bandhan na nieleze kwa nini &
inapaswa isherehekeweje ili kuwafanya watoto siyo waifurahie tu bali na
waielewe maana yake pia?
Jibu: Milenia iliyopita wanaume waliacha kuzishika na
kuzisherehekea sikukuu za Mungu na walianzisha aina nyingine za ibada. Utaratibuu
huu ulianzishwa na Mungu ambao ulikuwa ni wa manufaa sana na watu walihitaji
vipindi hivi kwa mapumziko na kujiweka sawa kiroho.
Waaryani walioshambulia India mwaka 1000 KK wakujanazo na
jinsi ya kufundisha kuhusu uumbaji, mafundisho yaliyotuama kwenye ibada za Mashariki
ya Kati na walianzisha huko imani au ibada za Sanskrit zilizotuama kwenye Usemitiki
wa kale au lugha za Kikaldayo.
Michoro ya zamani kwenye desturi au tamaduni za kinasaba zikafanywa
kuwa mungu kwa kupitia ibada za wazee na mababu zao. Sheba au Shiva akafanywa
kuwa ni mungu wa Kihindu. Nuhu au Nu akafanywa Seri Nu yaani mungu wa fedha au
wa utajirisho. Wanefili wakafanywa kuwa Raksasas.
Kutokana na mtazamo huu, dini potofu za kuwaabudu malaika
au za mapepo, mapepo ya kike waliojulikana kama Rakshanis zilianzishwa. Ni
kweli kulikuwa na mapepo wa kike na maroho wa miti. Kisha, na kama walivyokuwa batali,
walikuwa na mapepo au maroho yenye ngozi kwenye yogini au miambani kwa imani ya
Kianimism kama walivyokuwa banasati. Chungu ni pepo mwingine wa mti kutokana na
makabila mengi ya zamani kwenye imani ya Waanimism wa Kihindu.
Sikukuu zilianzishwa na sheria za kidini za hawa waanimisti
na zilichukua mahali pa sikukuu zilizowekwa na Mungu na alizopewa Nabi Nu au
Nuhu wakati dunia ilipoishia kupita kwenye kipindi cha watu kuongezeka. Zilikuwa
ni sikukuu za pili zilizotumika kumfanya mwanadamu apoteze sikukuu halisi na za
kweli za Mungu zilizoachwa na Waaryani kabla hawajaishambulia India na
kuanzisha Uhindu ukiwa kama taasisi tu na hatimaye kuwa imani kamili za kidini.
Sasa, kwenye sehemu ya pili ya swali lako.
Raksha Bandhan ni mila ya Kihindu inayoonyesha upendo na uhusiano
mkuu ulioo kati ya ndugu wanaume na wanawake. Neno Raksha maana yake ni
“Ulinzi,” (limechukuliwa kwenye dhana ya ulinzi dhidi ya mapepo waliotajwa hapo
juu) na Bandhan maana yake ni "kifungo". Inasherehekewa mnamo 'Shravan
sud Poornima' kila mwaka kwa mujibu wa kalenda ya Kihindu. Katika siku hii,
wadada huwafunga kaka zao 'Rakhi' viunoni mwao na kuwaomba kaka zao wawalinde
yanapotokea maafa. Inaaminika kwamba wakati Indra alipokuwa anakwenda kupigana
vita fulani, Indrani alimfunga uzi mkononi mwake ili kumlinda na alifanikiwa na
ndipo desturi hii ilipoanza. Inaaminika sana kuwa, maadhimisho haya ya Raksha
Bandhan ni mahali panapoweka taswira kifungo au makubaliano ya masaidiano haya
kati ya kina kaka na kina dada.
Chimbuko la Raksasas limeelezewa kwa kina kwenye jarida
la Wanefili (Na. 154). Kwa ajili ya
kalenda asilia ya Waaryani soma jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156).
Imani ya Ushamanism
Unaielezeaje imani
ya Kishamani? Sidhani kwamba tuna mengi tuliyoyapoteza, bali tunapotoshwa tu na
watenda Matendo ya Washamani. Ni kitu gani kinachomfanya mtu kuwa ni mtu aliyejitoa
kabisa kwenye imani hii ya Kishaman kwa kweli?
Jibu: Neno Shaman linatokana na neno la Kirusi lililotuama
kwenye lugha ya Tungusian la saman. Chimbuko
lake kabisa hapo mwanzoni na walivyokuwa, walikuwa ni makuhani au makuhani
matabibu wa makabila ya kaskazini mwa Asia. Hapo mwanzoni sana walikuwa ni wa
kianimisti na walitokea kwenye imani za kisirisiri za Mashariki ya Kati na
pembeni mwa nchi ya Urusi. Walianzisha misingi ya kidini ya watu wa jamii ya
Wauraliki/Altaiki, ambayo ilienea pande zote za kaskazini mwa Siberia na Ulaya.
Makundi yaliyokuwa mahiri kwa kuongea lugha nyingi ambayo
yaliyoanzisha mfumo asilia yaliunganisha vikundi vya Waaltaiki wa Kiuraliki
kikiwemo kile cha Kiugriki wa Kifino, Kihungarian/Magyar, Vogul na Manshi,
Manchu/ Tungus, Manchurian, Mongol, Wakorea wa Zamani na Wajapani. Vikundi hivi
vilienea hadi Amerika Kaskazini pamoja na Wahindi wa Marekani. Waliunda misingi
ya ushawishi wa kianimistiki kwenye Ubudha wa Kimahayana.
Mfumo wa imani ya Kishamani imeelezewa vizuri sana kwenye
kitabu cha Mirceau Eliade's cha Ushamanism. Msingi
wa imani yao ni kwamba mzuri yote na mabaya yanayojitokeza kwenye maisha yanaletwa
na maroho au mizimu, ambao wanaweza kushawishiwa tu na Washamani. Hii
inafanyika na Wahindi waishio Kaskazini Magharibi mwa Amerika na watu matabibu
ambao walikuwa ni Washaman sambamba na maeneo mengine ya Asia. Neno Kushamanaizi
maana yake ikikoma kabisa ni kufanya kitendo hiki cha kuzaliwa mara kwa mara na
kwa namna mbalimbali cha washamani na linatafsiriwa kuwa ni kukubaliana na
imani ya Kishamani (Oxford Universal Dictionary).
Wachina waliwakubali lakini waliwachukulia kama unabii
unaotakiwa mtu afafanuliwe kwa lugha ya Shen. Walionekana kama waongo. Lugha ya
Shen inashabihina na neno la Kikaldayo na ambalo ni la Kiarabu la Djinn na
ambalo linamaana ya maroho au pepo.
Hii imewekwa kwenye
sehemu ya Maadhimisho ya mwezi August kwenye kitabu cha: Sikukuu Mahsusi za
Wachina ambazo kwamba kilele chake kinasemekana kuwa ni siku ya 7 ya mwezi
mwandamo, roho za waufu zinatolewa kutoka toharani au purgatory na kutembelea
hapa Duniani. Nagundua kwamba mwezi wa August kwa hakika unaangukia katika
mwezi wa 5 wa mwezi mwandamo lakini kamati ijulikanayo kama Kamati ya Utenganisho
wa Desturi (Cultural Diversity Committee) liliiweka mwezi wa August kwa sababu
zake fulani.
Jibu: Hii inaonekana kuwa hasa ni kama ushawishi wa desturi za
Majesuit tangu wakati wa ushawishi wa Ukatoliki wa Warumi wazamani. Kwa hakika
isingeweza kuingia kutoka kwenye Hue Hue ya Kiislamu au kwa Wasabato, imani
zilizowatangulia kabla yao.
Sikukuu unazozieleza wewe zinatokana na dini potofu
inayowaabudu waliokufa zamani. Sadaka inayotolewa kwa wafu hawa inafanyika
makaburini majira ya baridi na ya kipupwe na inafanywa kwenye “Meza ya
wagonjwa” kwenye kipindi cha majira ya sikukuu.
Hii ilikuwa inafanyika siku ya kwanza, ya tatu nay a kumi
na tano ya mwezi mwandamo wa Kwanza, Sikukuu iliyojulikana kama “Nuru Kuu au
Mbalamwezi Ing’aayo” (ni kama Aprili 6 hivi); siku ya Tano ya mwezi wa Tano,
siku ya kumi na tano ya mwezi mwandamo wa Saba, siku ya kumi na tano ya mwezi
mwandamo wa Nane; siku ya kwanza ya mwezi mwandamo wa Kumi; siku ya mwisho ya
mwaka; na kwenye matukio maalumu kama vile ya ndoa (ERE, vol. 3, p. 731).
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi mwandamo wa Saba
sikukuu maalumu ilikuwa inafanyika kwa “mizimu yenye njaa” ambayo haina ndugu
waliowatolea sadaka. Sadaka za kimapokeo au za desturi zilitolewa wakipewa
zikitolewa na watu kwa ujumla na sio kwa wote wanaotoa kwa moyo wa kujitoa na
wa hiyari. Sadaka hizi zilikuwa na mtu aliyelala chini anayewasihi mizimu
“yatima” hawa ili wasiwadhuru walio hai kwa kuwaumiza.
Dhana ya kuwepo kwa toharani au purgatory ni mojawapo ya
zime zilizoingizwa kwenye ushawishi wa Wakatoliki wa Roma kama zilivyokuwa
kwenye imani hizi potofu, kazi iliyofanywa na Majesuit. Kama kanuni ya jumla,
Wachina waliopendezwanayo wakishawishiwa na Mkanganyiko, walipinga utoaji
kafara wa kuwatolea marehemu hawa na mwakilishi wao mkuu aliyeitwa Chucius wa
karne ya 12 alionea mashaka uwepo huu wa mizimu na imani yake yote. Hawa Hue na
Washika Sabato waliamini kuwa kuna ufufuo wa wafu na walikataa imani hii ya
kuwepo kwa mizimu.
Huenda ushawishi huu unatokea kwenye imani ya zamani ya
Kishamani kuwa una washamani wachache wa Kijapani wanaouadhimisha mwezi wa
wafu. Huenda yaweza kuwa kwamba ilishurutishwa baada ya ujio wa Majesuit wajanja
na watafuta fursa na ndipo imani hii ya kuwepo kwa toharani au purgatory inaonekana
kwenye maandiko ya kumbukumbu ambayo unayataja.
Freemasoni
Je, kwani Freemasoni
ni dini au ni klabu ya siri (ya kijamii) tu ya vijana?
Jibu: Freemasoni ni dini. Kuna matawi au madaraja mawili ya
dini hi: daraja au tabaka au mrengo au tabaka la York
au wa Kimarekani na la mrengo au tabaka la Uskochi. Kundi lililoko Ulaya halina
uhusiano wowote na lile la mrengo wa wanaotumia lugha ya Kiingereza. Kuna ngazi
au vyeo thelathini na tatu na wameenea kwenye maeneo kadhaa mbalimbali.
Kuna mirengo au tabaka mbili, Mrengo au Tabaka Mwekundu
na Mrengo au Tabaka la Bluu au Samawi. Tabaka au Mrengo wa Bluu ndiyo
unaojulikana au wa kawaida na unajiri na mabo ya kimahusiano na watu wengi
hawaingii wala kujiunga kabisa kwenye Tabaka au Mrengo Mwekundu. Tabaka au Mrengo
Mwekundu ni tabaka au daraja la cheo linaloshughulika na mambo ya siri na
kadiri unapopanda madaraja au kupewa vyeo vya juu zaidi ndipo unapozidi kupewa
siri kubwa zaidi ya walo chini yako. Ni dini inayowajumuisha watu wa tabaka la
juu la maisha kwenye jamii. Kuna vitabu vingi sana vilivyoandikwa kuhusu dini
hii.
Imani ya Mithrasism
Nimekuwa nikisoma hivi
karibuni kuhusu Siri za Kikosmiki za Mithras (Cosmic Mysteries of Mithras) na
pia kuhusu imani chache nyingine za kidini. Nakuta kwamba inaonekana kuwa
mfanano kwenye dini ambazo zina namna ya kufanana. Unaweza kuniambia kwa nini
baadhi ya mambo haya yanafanana sana kwenye dini na madhehebu mengi?
Jibu: Wana chimbuko lao la kiimani la dini za waabudu jua.
Imani ya Kimithrai ilikuwa na mtindo wa kipekee wa kuamini miungu ya kiume na
makuhani wake ukilinganisha na dini nyingine zote potofu za waabudu jua kama sol invictus
Mithra. Aina yake ya wazi au ya hadhara ilikuwa ni sol invictus Elagabal. Wanawake
walipewata fursa kwenye dini zenye tabia ya dini za Kisirisiri za Isis na pia
za Attis na Adonis. Nyingi ya hizi zilihusiana na dini za mchanganyiko wa
Waashuru na Wababeloni, ambazo pia zilienea kwa kupitia upagani kama ushamanism.
Na ndiyo maana imani ya Ukristo Mkongwe wanaabudu Mungu
wa Utatu pamoja na sikukuu zao zote zimetokana na dini hizi au kwa maneno
mengine ni kwamba wameziazima au kuzitohoa kutoka kwenye upagani na zingali
bado zikifanana na maadhimisho au sikukuu za kipagani. Zote zomechukuliwa
kutoka kwenye imani hizihizi za Kibabeloni. Soma kwenye majarida ya Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246) na Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235).
Waadventista Wasabato
Nimesikia kwamba Ellen
G. White alitoa unabii wa uwongo na nilishangaa kama hivi ni kweli na ndivyo
ilivyo na ni nabii zipi hizo? Sababu inayonifanya niulize ni kwamba nina marafiki
zangu wengi niwapendao walio kwenye Kanisa hili la Waadventista Wasabato.
Nimeshiriki ibada zao hapo kabla na ingawa sikubaliani na mafundisho yao bali
sijakutana bado na kitu kinachonishawishi nikubali kuwa imani hii ni potofu nay
a uwongo. Pia unasemaje kuhusu imani yao kwamba Malaika Mkuu Mikaeli ni Yesu
jambo ambalo nimelisikia nilipotembelea mara moja ibadani kwao lakini sio kitu
pekee wanachokiamini. Pia ninazijua nabii nyingi za uwongo zinazifundishwa na
jinsi walivyoanza kuwa walianza kama vuguvugu lililoamini kuw kipindi cha
Milenia kingeanza katikati ya miaka ya 1800, bali hiki sicho nnachokikusudia
kukiongelea.
Jibu: Mafundisho ya Kanisa la Waadventista Wasabato hadi mwaka
1978 yalikuwa kwamba Kristo alikuwa ndiye yule Malaika Mkuu ambaye Agano la
Kale linamtaja kuwa ni Mikaeli. Soma kwenye majarida ya Malaika wa YHVH (Na. 24) na Uwepo wa Yesu Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzaliwa Kwake Rasmi Duniani (Na.
243).
Wengi wao bado wanaamini kuwa Kristo ndiye huyo Mikaeli.
Walipuuzwa na kupingwa na Waamini Utatu au Watrinitarian wa imani Katoliki ya
Roma pamoja na familia zao zilizokuwa kanisani. Waliwafundisha imani ya kweli na
wakaielewa imani ya kweli pamoja na asili na tabia ya Mungu. Sasa, kuna
mamilioni kati yao wenye mawazo ya kama waamini Utatu. Ni kweli kabisa kwamba Ellen
G White alikuwa ni nabii-mke wa uwongo. Alifundisha mafundisho ya uwongo kwa
kiasi kikubwa sana kuhusu kipindi cha milenia kwa kuwa alikuwa anajaribu
kuinguza mafundisho ya ulaji wa mbogamboga tupu maarufu kama uvijitariani w
ukosmoloji wa nyakati za mwisho na alishinda na Maandiko Matakatifu mengi
ambayo aliyapuuzia kuyalinganisha na mafundisho yake alikuwa akiyatunga.
Makosa au upotoshaji wake wa kimafundisho pamoja na
upotoshaji wake wa kitafsiri vimeainishwa kwenye majarida ya Milenia na Unyakuo (Na. 95) na pia lile
la Uvijitariani na Biblia (Na. 183) na pia la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188).
Imani ya Kiashuru-Kibabeloni
Kwa kulijibu swali
lihusulo ndama uliyemuongelea mwezi mpevu unaoandama na ‘kidole cha Ashirat.’ Je,
hiki kidole gumba cha waabudu mwezi wakati mwezi ulipokuwa ukififia kama inavyoonekana
mawinguni unapoandama au ni yapi matumizi yake? Mwezi mchanga ulio kwenye
bendera na ni alama kuu na inayojulikana kila mahali leo. Ina maana gani na kwa
nini iko hivyo?
Jibu: Kidole cha Ashirat ni sehemu tu ya imani ya zama kale ya
mchanganyiko wa Waashuru na Wababeloni ya ibada na mkururu wa nyakati. Imani
hii iliingia Misri kwenye dini za Siri za Osiris, Isis na Horus ambazo zinashabihiana
na dini ya Baali-Easter. Inatajwa kama mwezi mchanga, na huu mwezi mchanga
ulionekana kuwa ni alama mungu-mke, Ashirat au Istar. Ilikuwa kama kidole,
mwezi huu mchanga ukiwa ni kucha ya kidole, ikicukuliwa kama watumishi wa Easter
au Ashirat kwenye ibada. Ilitumika hasa kama ndiyo inayolinganishwa kwenye
upangaji wa tarehe kwa kuweka kikomo au mwisho wake na kuadibisha, kama tutakavyoweza
kuona kutokana na tahswira ya kidole cha Ashirat.
Ni ushahidi tosha na wenye maana sana pia kwa mwezi
mchanga, kama ulivyotumika huko Mashariki ya Kati na kwenye utaratibu wa
kutazamia kuuona mwezi waliokuwanao Wayahudi, ambao wapagani waliuchukua kwenye
taratibu za imani zao baada ya kuangushwa kwa Hekalu. Soma sasa kwenye nukuu.
Kwa mujibu wa kitabu cha The Crescent and
the Bull (Mwezi Mchanga na Fahali la Ng’ome) kilichoandikwa na Erich
Zehren, ukurasa wa 190. Kinatuambia kuwa Ta’annek haikuwa ya kidunia mnamo
mwaka 1901 kwa maelekezo ya Ernst Sellin. Maelezo fulani ya kwenye maandiko ya
kale yanasema haikuwepo duniani, pamoja na nyaraka aliyoandikiwa Mfalme wa Taanak,
Ishtarjashar mmoja.
Kifungu kimoja kutoka kwenye waraka wa Jemadari wa
Kimisri kinasema:
“Ninyo nyote mnasikiliza niandikieni kutoka huko, ili
niweze kuelewa jambo hili. Kama kidole cha Ashirat kinajionyesha kwa kujilenga
chenyewe, ningependa nifanye haraka kukitii. Na ndipo mnipe ripoti mimi kuhusu ishara na mabo yote
yaliyopo.”
“Ashirat ANAONYESHAJE kidole chake? Ashirat anafanana
sana na kina Ishtar na Inanna Kidole chake lilionekana tu kwa ndani mawinguni,
ambapo ‘kidole’ kinaweza kuchukuliwa kuwa kinaonekana kwa umbo la mwezi mchanga
unavyoonekana unapikuwa mwishoni mwa mwezi. Barua ya jemadari wa Kimisri,
inasema vyema, inaonyesha siku. Wakati mwezi mchanga unapoikaribia sayari ya Venus
ataitarajia ripoti.” “mawasiliano
haya, ndipo, ni ombi kamilifu la kawaida kimatendo kwa wakati fulani.”
“waraka huu unatoka katikati ya milenia ya pili KK, kuhusu
njipanda kati ya Ibrahimu na Musa”, ukurasa wa 191. Kutokana nah ii tunaona kwamba
karibu ulimwengu wote umefungashwa kwenye imani za kisirisiri za Wababeloni
kwenye imani zao hadi leo.
Je, unajua ni wapi
wazo la Mama Bata na yai la dhahabu inakotokea? Je, hizi ni hadithi za
kuwahadithia watoto zisizo na madhara au zina maana yake fulani?
Jibu: Uhusishwaji wa Bata na imani ya nasfi hai kuendelea
kuishi na imani ya Mungu-Mke inatoka kwenye dini za zama kale za Kimisri. Farao
au mfalme hakuwa huru kufanya mambo yake kama tunavyodhania kuwa ndivyo walivyo
wafalme. Kila jambo la siku zao ilipangiliwa na kuamriwa na hata masaa wanayotakiwa
kufanya ngozo na wanawake pia walipangiwa. Niposa walipangiwa pia kula nyama ya
ndama na bata (kwa mujibu wa kitabu cha Frazer, cha The Golden Bough, iii, 13).
Wakati Farao alipokufa basi hawa bata walitolewa kafara.
Kila Farao alichukuliwa kuwa ni Osiris kama walivyokuwa watu wa kawaida kwenye
dini ya wafu na mtu aliyekuwa amekufa aliitwa Osiris na kadhalika wa kadhalika.
Mungu-Mke Nut alikuwa mama wa Osiris. Kwa hiyo uhusiano ulifanyika. Mungu-mke Isis
na Nephthys walikuwepo kama walivyokuwako kina Anubis na Horus na miungu
wengine maarufu wa Kimisri waliokusanyika wakiizunguka maiti. Waombolezaji
wawili wanawake walikuwepo hapo kuiwakilisha miungu hii ya kike.
Frazer anasema kuwa hawa bata walichinjwa kwenye matanga au
maombolezo haya (maombi waliyokuwa wakiombewa yamewekwa kwenye vi, 15). Osiris alikuwa
ni mungu wa ufufuo kwa namna hiyohiyo ndivyo alivyokuwa Attis pia akijumuishwa
na hiyo kwa upande wa Magharibi na Adonis kwa upande wa Mashariki. Mungu huyu
mfu wa kilimo cha mboga au mchicha kwa kiasi fulani alihusishwa na matendo haya
pamoja na siku ya Matawi kwenye kingo za Siku ya Matawi na kubeba lundo lililofungwa la Matawi huko Ulaya. Matawi
yaliyochomwa kuwa matawi au Mabua yalitumiwa ili kuwawezesha au kuwafanya bata
wazae mayai mengi ikiwa kama ishara ya rutuba (ibid viii, 326).
Tofauti ya jambo hili kwa hiyo imechukuliwa kwa miaka
sasa hadi kupelekea kujitokeza kwa mungu-mke Mama na ishara ya digidigi/goose. Nguruwe alikuwa mtakatifu pia
kwa Apollo na ana ukanunishaji sawa tu huko Ulaya akiwa ni familia ile ile ya bata
bukini.
Kwa hiyo tunarudi kwenye dini za urutubisho na imani ya Easter
(soma jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235)). Pia kuna
hadithi ya mahusiano inayofanana na nakushauri usome jarida la Wanikolai (Na. 202)).
Je, kuna umuhimu gani
wa Orodha ya Kafara za Waashuru?
Jibu: Kwenye elimu ya Kiashuru, hii ni orodha ambapo kazi au
matendo au utendaji kazi wa Waashuru waliipa jina kwa mwaka maalumu wa ofisi.
Kwa hiyo, orodha ya majina ni sawa na orodha tarehe zilizohesabiwa kutoka kwao.
Wakati
tunaposoma habari za Gideoni kwenye Waamuzi 7 na 8 yaonekana kuwa Orebu na Zeebu
kuwa ni wawakilishi wa makerubi 2 walioasi? Je, kuna maana yoyote kuhusu majina
yao yanayotupa sisi dalili au ishara ya nani au kile wanachopaswa kukiwakilisha?
Jibu: Orebu (kwa mujibu wa kamusi ya SHD 6157) inayotamkwa “'arobu” limetikana
na shina la neno lenye maana ya mbu na hivyo kata kwa “nguruwe” na hivyo
linatumika kwa wadudu mbalimbali warukao kama mainzi au nguruwe. Kwa hiyo,
mfalme wa Orebu anaweza kuchukuliwa kama ni Bwana wa Mainzi, ambaye alikuwa pia
ni mungu wa Ekroni.
Je, kuna uhusiano
wowote ule kati ya dini na Mardi Gras? Inaonekana kuwa kuna uhusiano
ninaposikia maadhimisho wa siku hizi, kama zilivyo pia nyinginezo za Jumanne
Nene. Matamasha kwa ujumla, yanaonekana kuwa na uhusiano na maadhimisho ya
kidini. Ifikspo Januari, kuna maadhimisho mengine yanayoitwa Tamasha la majira
ya Baridi, na kisha kuna Gwaride maarufu kuliko yote la kuadhimisha Easter.
Jibu: Ndiyo. Kuna uhusiano kati ya maadhimisho ya Mardi Gras na
dini. Ni tamasha la
zamani linalohusiana na siku ya Matawi. Jumanne ya Wanene inatokana na
maadhimisho ya zamani ya Jumanne ya Matawi. Mwanzoni kabisa, Jumatano ya Matawi
haikuwa na maana nyingine zaidi ya Tamasha au Sikukuu au Maadhimisho ya
Kwaresma. Yalikuwa ni maombolezo ya kuyaombolezea matawi, ambayo yalikuwa yameunguzwa
na majivu yaliyobakia yaliyawakilisha Matawi yaliyounguzwa.
Jina la Jumatano ya Majivu ni caput jejunii. Kuna tofauti ya kiliturjia kati ya caput jejunii na
"initium quadragesimae" jina la Jumapili ya kwanza ya Kwaresma.
Mwanzoni kabisa, wakati imani ya Easter ilipoanzishwa,
sikukuu au maadhimisho ya mungu anayekufa yalianza kwa mfungo wa saumu ya siku 36
kwenye Jumatatu ya baada ya Jumapili ya kwanza ya maombolezo ya Kwaresma (kitabu
cha ERE, kuhusu ‘Lundo la Matawi, Jumanne
ya Matawi’, xi, 477). Baada ya kipindi cha Papa Gregory I aliyeitwa kama Mkuu,
na kuanzishwa kwa Dola Takatifu ya Rumi, ndipo Jumatano ilianzishwa na
ikafanyika kuwa ni moja ya siku nne zilizotengwa maalumu zilizotengwa kwa ajili
ya kufunga saumu ambazo ziliitwa "caput jejunii." Juma la kipindi hiki
linahusiana na Tamasha au maadhimisho ya Mardi Gras. Imani hii ya kuadhimieha siku
ya matawi ilihusiana na ingali bado ikihusiana na juma hili la Tamasha na neno "Carniprivium"
limetolewa kuwa ni Jumapili ya Kwadresma au Quinquagesima.
Mila zilizokuwa zinafanywa huko Uskochi inaonyesha uhusiano
uliopo na “mila au desturi za Wabacchanalian za ufungaji au Matawi yaliyofungwa
na maadhimisho ya Saturnalia iliyopelekea kuibuka kwa sikukuu ya Krismas"
(ERE, p.478). mwanzoni kabisa,
Jumatano ya Majivu ilikuwa ni maombolezo yaliyokuwa yanaandaliwa kumlilia mungu
anayekufa na kifo cha matawi kwenye tamasha.
Frazer ana maelezo mengi na fasaha mno kuhusiana na mila
na desturi zao kwenye kitabu chake cha The
Golden Bough (Jipu la Dhahabu) ukurasa wa iv. 220-221,
na 226ff. Ipo au ilikuwepo hadi karne hii ikiendelea hadi sasa huko Ulaya.
Mwanzoni haikuwa desturi wala maadhimisho ya Wakristo kabisa na chimbuko lake
linatokana na desturi za kipagani ambazo ziliigwa na kuchukuliwa na kuingizwa
kama zilivyo pamoja na sikukuu ya Easter kwenye karne ya pili na ambayo haikuwa
na uwiano au inaendana kikamilifu kabisa hadi mwanzoni mwa karne ya saba na Gregory.
Jumatano ya Majivu haihusiani kabisa na mafundisho na
imani ya Biblia. Mwanzoni ilikuwa ni kumbukumbu ya kukikumbuka kifo cha matawi
ya Bacchanalian. Kwa hiyo, Tamasha hili lilifanyika siku ya Mwisho ya
maadhimisho ya Matawi na Jumanne ya Wanene ni siku ya mwisho kabla ya kuunguzwa
kwenye Jumatano ya Majivu, ambayo haina maana kwa Wakristo au haina maana
yoyote kwao.
Sikukuu au maadhimisho yote haya yana chimbuko lake au
vyanzo vyake kwenye dini za Kisirisiri na zinawaingiza watu kwenye imani na
maadhimisho ya Easter ya Baali-Easter. Utajionea au kujisomea kwenye majarida
ya Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235) na lingine la
Ndama wa Dhahabu (Na. 222).
Kwenye sherehe za
kuadhimisha siku ya kualiwa kwa watoto na hata kwa naadhi ya watu wazima kama
vile sherehe za kuonyesha, pinata zinaonekana kutumika zaidi na zaidi
kuongezeka kwa burudani. Neno hili halionekani kwenye kamusi yangu. Je, unajua
chimbuko la mchezo huu?
Jibu: Mwanzoni kabisa Pinata ilitengenezwa kwa umbo la nguva ingawaje
kwa sasa haitengenezi kila mara kwa umbo hili la nguva. Wakati mwingine
inatengenezwa kwa umbo la nyota yenye ncha sita. Nyota hii ya mungu imechukuliwa
na kuingizwa kuoka kwenye chanzo kile kile kimoja kama ilivyo kwa nguva. Nguva
ni ishara ya mungu-mke Deceto au Ceto au Kato ambaye ni Atargatis anayehusiana
na Wafilisti na dini potofu ya Dagoni pamoja na ile ya Baali-Easter.
Samaki alikuwa ni mtakatifu kwa Atargtis au Derceto kama
alivyokuwa njiwa. Kitendo cha kuyachukua maji na kuyapeleka Hekaluni kutoka
kwenye mabwawa yake kilichukuliwa au kuigwa kutoka kwenye dini hii potofu na
hata imani ya kuita maji matakatifu ilichukuliwa au kuihwa kutoka kwenye imani
potofu ya mungu Baali-Easter. Huu ulikuwa pia ni mwanzo au chimbuko la imani ya
kutokula nyama na kumla samaki peke yake siku ya Ijumaa kuu iliyokuwa
inaaminika kuwa ni siku ya kifo cha mungu huyu aliyejulikana kama Attis au
Adonis au Osiris kutegemea eneo wanalomuombolezea wanavyomuita au kutegemea
lugha iliyokuwa inatumika kwenye maeneo hayo.
Nguva huyu alikuwa anapigwa kwa fimbo ili kumvunja pinata
au mfuko wa mbegu, aliokuwanao ili kwamba mbegu hizo zimwagwe na kumiminikia
ardhini na ili iweze kuzaana. Na ndiyo maana pinata ina vitu vitamu kama peremende ndani yake
vinavyowakilisha mbegu.
Katika siku za zamani waliweka ngozi ya mwanadamu na
kuzipiganayo. Mara nyingi ibada hizi zilifanyika sambamba na utoaji wa kafara
za wanadamu. Maungamo ya Wabacchanalian yameigwa na kuingizwa kutoka kwenye
kitendo hiki kama ilivyoigwa na kingizwa Jumatano ya Majivu ambayo chanzo chake
hakihusiani kabisa na kipindi cha Maombolezo kiitwacho sasa Kwaresma bali zaidi
tu kilikuwa kinamaana ya uchomaji wa Matawi ya Mtende kwenye juma
linalotangulia na iliyofia kwenye Jumanne ya Matawi. Ubebaji wa lundo la Matawi
yaliyofungwa yalipigwa pia huko Ulaya siku hii.
Maelezo kuhusiana na matendo haya yanapatikana kwenye
majarida ya Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235); Pinata (Na. 276); Daudi na Goliathi (Na. 126).
Niliokutananao hivi
karibuni ndio walionisimulia habari za “dini”. Inaitwa Tantra. Nilikwenda na
kuisoma kwenye tovuti. Nilichokipata kutokana na kumchukua mtu huyu na kuperuzi
kwenye tovuti yenyewe, ni kwamba hii ni imani inayotafuta kuunganisha au
kuhusianisha kati ya mambo ya kiroho kwenye mahusiano ya kingono na shauku au
tama ya mwili. Naamini kuwa wanafundisha kwamba mtu anaweza kupata utoshelezi
kamili kwenye hii…maana yake ni matendo ya uzinifu au kwenye ngono ma kwenye
matendo ya kiroho. Lakini kwani hii inaingana kabisa na kile Mungu anachotuambia
sisi?
Jibu: Ndiyo. Yoga wa Kitantriki inafuata mstari huu wa
kutafakari. Sio imani ngeni. Uhusiano wa kingono umekuwa ndiyo msingi wa ibada
za dini potofu za waabudu jua na imani za kisirisiri kwa kipindi cha milenia
sasa. Inafungamanisha imani zote za Baali-Easter kama ilivuo kwenye upotoshaji
wa amri ya tano na mfumo au muundo wa kifamilia.
Soma kwenye majarida ya Torati na Amri ya Tano (Na. 258) na la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) na Mkururu wa majarida ya Sheria au Torati
kwa ujumla: soma jarida la Torati au Sheria ya Mungu (Na. L1).
Imani ya Kizoroastriani
Nimependezwa na
kujua jinsi na mahali ninaweza kukuta kiwakilishi (sanamu au michoro) ya mzimu
wa Kizoroastrian wa aitwaye Ahriman (kama upo mahala fulani popote).
Jibu: Mdiyo, hii siyo katizo rahisi. Kuna machimbo
yanayoaminika ya zamani sana ya Ahriman yenye nyayo ilizokanyaga miguu ya Ahura
Mazda au Ohrmazd. Yapo kwenye “Bonde la Irani la Wafalme” Naqsh-i Rustam.
Ni uwakilisho wa Mfalme Ardashir I (miaka ya 224-241 BK) ikiwa
bado ipo pamoja na pete ya heshima ya kifalme ya Ohrmazd. Kwenye mihuri ya
zamani sana ya Achaemenid, Mungu hakuwa ameonyeshwa kabisa kwa umbo la
mwanadamu na uwakilishi nguvu za duniani ulionyeshwa kama nguvu na hivyo ulionyeshwa
kwa alama au nembo. Kuna picha ya Ardashir iliyotolewa kwenye kitabu cha Elimu ya Mizimu Ilivyoelezewa Kwenye Kitabu
cha Ufafanuzi wa Maneno (Mythology An Illustrated Encyclopaedia, Black Cat,
on p. 43).
Kuonekana kwake kwa mwisho alionao Ahriman anaonekana
kwenye umbo la kibinadamu akiwa na kichwa cha nyoka. Kunaweza kuwa na uchimbaji
wa hivi karibuni kuhusu Ardashir na imetolewa huko Iran na hivyo Oxford na
Cambridge vinaweza kuwa na picha bora zaidi hadi leo za muonekano wake au
michoro siku za mwishoni za Ahriman na Ahura Mazda.
Mafundisho ya Kisirisiri ya Kikristo
Unasemaje kuhusu
mafundisyo ya Kipreterist yanayoonekana kuwa yanatokea kwa nguvu za marehemu?
Sipendi kulishawishi jibu lako, ila naziona fikra hizi za kwamba Kristo
alikwisharudi mwaka 70 AD kama ni ya uzushi wa wapenda maono ambazo hazina msingi
wowote wa Maandiko Matakatifu. Ni upi mtazano wako?
Jibu: Nadhani unachomaanisha hapa ni fikra au mawazo ya wa Wapreterist
wanaosema kuwa Kristo alikwisha rudi tayari, au yupo na anatenda kazi hapa
duniani, wanajenga hoja yao kwamba alikwisha rudi mwaka 70 BK ni ya kipuuzi
kabisa. Mashahidi wa Yehova wanapnekana kuwa na walilitilia chumvi zaidi wazo
hili pia mnamo mwaka 1914.
Kinachosumbua zaidi kuliko vyote ni fikra ya kwamba Kristo
ndiye anayeliongoza au kulitawala Kanisa Katoliki la Roma, na kwamba amekuwepo
tangu lilipoanzishwa. Hii inachukuliwa kuwa ni kipidi cha milenia
kilichoandikwa kwenye Ufunuo 20, ingawaje limedumu kwa kipindi cha hata zaidi
ya hapo. Kama kile kililojukana kama Dola Takatifu la Rumi iliyodumu kwenye
miaka ya 590-1850 (au kwa miaka 1260) lilikuwa ni Utawala wa Mungu hapa
duniani, basi ingekuwa vi vyema kuchagua kufa.
Kristo anasema kuwa kama wakiwaambia kuwa wao ni Masihi,
au wakiwaambia kuwa yuko hapa au yupo kule msiwasadiki (Marko 13:21). Tutamuona
wote akishuka kutoka mawinguni kwa nguvu na utukufu na sote tutakusanyika
pamoja (Marko 13:26-27). Wakati atakaporudi hapa tutaiona dunia hii ikiongozwa
kwa kipindi cha miaka elfu kwa maongozi ya Torati ya Mungu, na watu watakwenda
kujifunza utii kwa ukamilifu wake sawa na ilivyo kwenye Kumbukumbu la Torati 28
(soma jarida la Baraka na Laana (Na. 75) Milenia na Unyakuo (Na. 95)).
Kwenye vitabu kama
vile vya Damu Takatifu na Kikombe Kitakatifu na pia cha mstari wa Damu wa Kikombe
Kitakatifu mambo au pointi za muhimu na za kupendeza zinazoibuka zinahusiana na
kwenye Agano Jipya na kwenye dini kama ilivyo kwa ujumla. Je, unaweza
kunifafanulia ni kwa nini mjina yake ya jumla fikra zao na mawazo yao yalivyo
ya uwongo na kwamba bado unaamini kwamba toleo lako la historia ya kidini ni
sahihi?
Jibu: Ni kwa nini tuwe tukiamini chochote kile? Ni kipi
kinachoifanya Biblia iwe ni ya muhimu sana? Ni vipi hukusu Magitaa na maandiko
mengine? Hebu na tuanzie mwanzoni. Mungu aliziumba na nchi. Alimuumba mwandamu.
Uumbaji wake ulikuwa na malengo. Kama usingekuwa na malengo, ndipo Mungu
angefanya mambo yake kutoka kwenye mabadiliko. Huenda mtu angepinga kwamba sisi
ni mapambo ya kijumi tu kwenye galaksi ya Njia yenye Maziwa. Hatuamini hivyo na
watu wa zamani za kale hawakuamini hivyo kabisa.
Inaaminika kuwa Mungu ana makusudi kwa mwanadamu. Malengo
hayo yanahusiana na hukumu na maisha baada ya kufa. Kama tutahukumiwa basi ni
budi tunahukumiwe kwa kiwango cha usawa. Hivyo yapasa ibakie hivyo na isibadilike
kwenye utendaji kazi wake na kwenye utaratibu au kanuni ya Mungu ni uwingi na
Kristo ni yeye yule, jana, leo na hata milele.
Mungu ana maagizo ya kijamii na kimaadili ili kuyafunua
mapenzi yake na kiwango dhidi ya kile tutakachohukumiwa nacho. Vinginevyo, yeye
atakuwa wa holela na anayewapendelea watu. Pia sharia ni budi ituame kwenye
vigezo fulani kuliko ukweli wa kwamba aliitoa kutokana na ughafla. Kama aliitoa
kutokana na ughafla basi atakuwa ni mtishaji au dikiteta mwingine.
Kwa rekodi zote tulizonazo, Biblia ndiyo inyoendelea
kudumu zaidi na yule aliyeungwa mkono na rekodi za kihistoria na matendo ya
miujiza hasi. Mungu aliyafunua mapenzi yake kwa kupitia watumishi wake manabii.
Tuna ushahidi wa uingiliaji kati ule na unabii wa Mungu unaokuja kuchipua na
kuzaa matunda au kutimilika.
Kanuni ya Biblia ni kwamba unabii ni lazima uendane na
Sheria na Ushuhuda (Isaya 8:20). Vitabu vyote vilivyo ndani ya Biblia
vimekubalika kuwa ni unabii na vinakubalika kuwa ni vitabu vitakatifu na bodi
ya Waisraeli na makuhani ya kuyakubali maandiko na kuyapitisha. Hii ilienea kwa
makanisa yote hata yale yaliyokataa Sheria za Mungu wasizishike hata leo.
Vitabu kam vile cha Damu Takatifu na cha Kikombe Takatifu
havidai kuongelea lolote kuhusu Mungu n wala havifuati sheria na Ushuhuda. Kes
hiyo vinapungua vigezo vya msingi vilivyovuviwa na Mungu kama wasemavyo mitume
wa Agano Jipya na Maandiko kwa ujumla.
Kwa kuvisoma vitabu kama hivi inampasa mtu kukipima kila
kimoja kwa umakini akikilinganisha na jinsi inavyosema Biblia na ndipo
alazimike kuvikataa kwa kuwa sio tu kwamba viko tofauti au haviendani, bali kwa
mambo kama hayo yaliyo magumu kwenye uelewa wowote wa Mpango wa Mungu. Kiwango
hiki kinaweza kutendeka kwenye Korani pia na kwenye vitabu vingine.
Wakati kwango kinapolinganishwa na kile kinachosemwa na
Kurani, ni kama inavyopingwa na kile mahafidhina wa Kiislamu wanachodai kuwa
inasema bali tunakuta kuwa hakuna mlingano na maandiko ya kwenye Biblia na
ndipo tunapoiona kuwa ni uwongo. Hata hivyo, pale tunayoyafuata yale Uislamu wa
siku hizi unapodai kwenye hilo, basi tunakuwa kwenye makosa makubwa.
Kwa hiyo tunalazimika kuyapima na kuyapitia maandishi
yote kwa kile kinachodaiwa na wao na manabii wenyewe na pamoja na mashahidi na
waandishi na pia pamoja na tafsiri na ulinganifu wa vitabu vilivyo kwenye mfumo
wa Maandiko Matakatifu kama yalivyofunuliwa na Mungu kwa manabii. Vivyo hivyo
chochote tunachokindika yapasa kitokane na maagizo ya Torati au Sheria na
Ushuhuda vinginevyo basi hakutakuwa na nuru ndani yake.
Hii ndiyo sababu mambo yote yaliyoenezwa na watu wetu
wamekuwa wakichunguzwa na baraza la kanisa na kuadibishwa ikiwa kutofanana huku
kunakutikana kuwa kuko wazi au dhahiri. Kama utakuta andiko la watu wetu ambalo
linaonekana kuwa linatofautiana na Sheria ya Mungu na Ushuhuda wa Y esu Kristo na manabii tafadhali tujulishe
tujue nasi tutaisahihisha, au tutaifafanua kwa nini haiku sahihi. Tutatoa
ufafanuzi unaokubalika kwa kweli anaouibua mtu kwa suala la kitabaka.
Ni upi ushahidi wa
kwamba kaburi lililovumbuliwa katika karne ya 9 huko Santiago de Compostela, upande
wa kaskazini magharibi mwa Hispania, (Galicia) lilikuwa, kama inavyodaiwa, kuwa
ni kaburi la Mtakatifu Yakobo?
Jibu: Yakobo, askofu wa Yerusalemu na ndugu wa Kristo aliuawa
shahidi mwaka 63 BK na nafasi yake ilichukuliwa na Symeon mwana wa Maria na
Klopa. Kitendo cha kufananisha Desposyni kuruhusu maiti au masalia yake yaondolewe
na yapelekwe Galicia hakina maana.
Kwa imani ya Kikatoliki, Yakobo alikuwa ni mtakatifu
mlinzi wa Galicia na ilikuwa kwa kupitia yeye ndipo watu wa Uhispania walianza
kuwafukuza na kuyarudisha majeshi ya Waislamu. Agizo la Mtakatifu Yakobo wa Compostella
linaweka tarehe kutoka kwenye tarehe iliyofuata baadae na kwa kweli ilikuwa
kiti chenyewe asilia cha agizo au amri. Agizo lenyewe lilikuwa la sehemu mbili,
mwanzoni kabisa huko Leon na Ucle wa Castille.
Usiku wa siku kadhaa wa Santiago ulikuwa na mambo kwenye
falme zote mbili lakini Ferdinand II wa Castile na Alphonse VIII wa Castile wakiirudisha
tena amri waliweka maxingira ambayo vikao vya kutolea maamuzi au amri vilibidi
viwe kwenye nchi au mataifa muhimu husika. Mabishano marefu yaliishia mwaka 1230
wakati Ferdinand III alipounganisha kofia zote mbili za kifalme. Kisha ndipo Ucles wa Cuenca uliteuliwa kuwa ni makao makuu.
Kihekalu cha Mtakatifu Yakobo kililindwa na wao. umuhimu
wa kuendeleza ujenzi wa vijihekalu na sanamu zake zilizojulikana kama za
watakatifu walinzi na juhudi au hamasa za kidini kwenye vita nchini Hispania
viliendeleza hamasa ya kuwa na masalia ya mfupa au ya kiungo kimoja au viwili
na mwili wa yule aliyechukuliwa kuwa ni mtakatifu mlinzi wa Wahispania yalikuwa
ndiyo matokeo yake halisi.
Nimependezwa na
kile ulichowahi kukisema kuhusu Utafiti au Kuchorea Ramani kwa kutumia kipimo
cha nasaba cha DNA. Nimesoma maelezo ya wanasayansi kwenye vitabu vingi, na ni
vingi sana na visivyo na hesabu hadi hapa
nilipo sasa. Hii inafanya hesabu inanifanya nifikie hamasa ya kwamba: Na sasa
TUNAJUA…….kwahiyo kumtazama Mungu! Inaonekana kama mtu anamtumia Mungu peke
yake wakati inapoonekana inafaa kufanya hivyo.
Jibu: Kulikuwa na shindano moja tu kwenye shindano la
mwanadamu na sasa tunaweza kuonyesha ukweli huo kiufasaha sana. Dhamira au
madhara ya ubaguzi yanaweza kuwekwa kwenye mambo mengine yanayoweza tu
kuingizwa kuwa mbadala kwa kitisho cha kutisha zaidi kwenye uhuru wa mwanadamu.
Madhara ya kiuzawa ya nasaba ya familia kadhaa na makabila vinaweza kutengwa au
kuondolewambali na hata familia za kawaida za wanadamu zimeangamizwa kwa dhana
hii.
Haya ni mafundisho yaliyoletwa baadae ya mapepo, yanayokusudia
kukataza au kuzuia ndoa hata siwe ya kweli zaidi. Soma kwenye majarida ya Mafundisho ya Mapepo ya Nyakati za Mwisho (Na. 48) na pia lile la Uvijitariani na Biblia (Na. 183).
Kitendo cha kuweka alama za genome ya mwanadamu kitaibua
matukio ya Mwanzo wa uumbaji yaendelee. Usemi usemao kuwa watakuwa kama elohim
unaeleweka vizuri sasa. Na ndiyo maana Babeli iliangamia na lugha ilitibuliwa.
Wakati
tunapoiangalia orodha ya Mababa wa Kanisa nilimgundua au nilimuona Hermes. Ni
nani mtu huyu na alikuwa anaamini kitu gani na/au alikuwa anafundisha nini?
Jibu: Kimsingi, Hermes si mmoja wa mababa wa kanisa kwa kweli.
Alitajwa kuwa alikuwa ni mmoja kati ya Mababa waliokuwepo kwenye Mtaguso uliojulikana
kama Ante Nicene akipitishwa kutokana na mtazamo wake. Anaitwa Hermes
Trismegistus. Alikuwa anaaminiwa kuwa ni Hermes wa tano au Mercury aliyemuua Argus
na baada ya kufanya hivyo alikimbilia Minsri. Wamisri wanamuita Thoth na
wanauita mwezi wa kwanza baada ya jina lake ambao ni sawa na mwezi wa Septemba.
Aliujenga mji wa Hermopolis na anaabudiwa huko Phenae. Alikuwa
ni mwaamini Mungu mmoja aliyekuwa anafundisha huko Misri kuhusu mungu
asiyejulikana. Ametajwa
kwenye kamusi ya ANF kwenye matoleo
ya 1:289; VII: 15, 210, 215. Hermes wa pili ni Messalian au Eustathian.
Epiphanius anasema kuwa sini hii potofu ilianzishwa kipindi cha utawala wa Constance
lakini Theodoret anasema kuwa zilianza katika nyakati za Valentian.
Mkururu wa vitabu vya Makasisi waliohudumu kipindi cha
baada ya kipindi kinachojulikana kama Post Nicene, Matoleo ya II vol XIV kwenye
ukurasa wa 240 kuna kifungu kinachoelezea kuhusu dini hii. Kulikuwa na catacombi
ya Hermes iliyochimbuliwa karne moja iliyopita kwenye Via Salaria Vetus ng’ambo
au nyuma ya Porta Pinciana (CE vol. II, p. 419, 517). Kuna taarifa chache tu
zinazojulikana kumhusu yeye yaliyohifadhiwa kiasi cha kuonekana kuwa huenda
aliuawa shahidi mnamo mwaka 119 BK. Kizazi cha Waliberia wa Karne ya Nne
kilimtaja yeye kuwa alizikwa kwenye uwanja wa Makaburi wa Kusini mwa Basilla. Basilica
ya chini ya ardhi ya karne ya nne iliijengwa juu ya kaburi. Adrian I (772-95) aliuondpa
mwili wa Hermes na kuupeleka mjini. Chanzo kwa kwanza cha Wakeisto kuhusu catacombi
ya Hermes na masalia ya ss Peter na Hyacinth yaliyokutikana hapo yanachukuliwa
kama huko Guiseppe Marchi 21 Marchi 1845 (CE, Vol. IX, p. 643).
Dini hizi mara
nyingi zinadhaniwa kuwa zilikuwa na ajenda ya siri na kutumia hali ya kuitawala
akili za watu na kuzitumia kama wanavyopenda ili kuwafanya waumini wao wawe
waaminifu na watiifu kwenye dini hizo. Cult ni nini? Kama sio kwamba limetoka
wapi neno ‘cult’ zenye matendo haya?
Jibu: Kalti au Cult ni neno linalotokana na neno Cultus ambalo
linamaana ya kuabudu. Kalti kubwa zaidi ya zote ya Kikristo ni Kanisa Katoliki
la Roma. Limeendeleza maana yake ya kiporojo au kebehi kwa imani za Ukristo
mkongwe walisaidia kuieneza na kuviambukiza vikundi vidogovidogo na kuviwezesha
au kuvifanya viendelee kuamini kinyume au hata vikatae kufuata mrengo wa makanisa
makongwe.
Ni kawaida tu kwenye historia na imani ya Ukristo mkongwe
imekuwa ikirudiarudia kumuua mtu yeyote aliyeonekana kutokubaliana na wale
wanaoichukulia dini kuwa ni kama siasa. Utendaji kazi wa Kalti umeainishwa kwa
kina kwenye jarida la Fikra za Kalti (Na. 74). Mateso
yaliyofanyiwa kanisa la watuza Sabato kama kalti yamekuwa yakifanyika na
kuendelea mara kwa mara tangu pale kalti za waabudu Jumapili ziliposhika hatamu
kama Wakristo walio wengi. Soma jarida la Kazi ya Amri ya Nne Kwenye Historia ya
Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170).
Mauaji ya kuangamiza ya Holocaust yalipangiliwa kwa lengo
la kuwaangamiza na kuwafutilia mbali washika sheria au torati na waamini Biblia
wote waliokuwako huko Ulaya kwenye karne ile. Ilikuwa ni karibu wafanikishe
mkakati huu. Kwa sasa, kuna mambo ya kushangaza au mageni yanayojitokeza
yakilenga kuviangamiza vikundi vidogovidogo. Vikundi vingine vidogo hata
vinajiua au kujinyonga vyenyewe.
Kundi moja nchini Uganda hivi karibuni lilijitebga kutoka
kwenye Kanisa Katoliki la Roma na inadaiwa kwamba lilisema kuwa linataka
kuzirudisha Amri za Mungu. Kisha wafuasi wake walikutwa wamejinyonga kwa kamba
na wengine kujipigilia misumari kwenye jingo la kanisa na ambalo hatimaye
lilichomwa moto na viongozi wao. Hili ni tukio lisilo la kawaida kulisimulia
miongoni mw matukio mengi mengine.
Waco lilijulikana kama kalti ya whacky lakini tunakuta
sasa kwamba mambo mengine yasiyo ya kawaida yalijitokeza huko ambazo
zimewasumbua kwa kiasi kikubwa Wamarekani wengi. Wakristo wa imani Kongwe
wameviua vikundi vidogovidogo visivyo kubaliana nao kwa kutumia zana kalikali
au kwa kutumia mbinu za namna mbalimbali pamoja na vitu vya hatari kwa kipindi
cha karne nyingi sasa. Soma kwenye
kitabu cha but we find now that some extra ordinary things Wasabato wa Transylvania (CCG Publishing 1998.)
Ukiri
wa Imani ya Kikristo
Kwenye swali lililopita ulilitaja
Kabrasha R [“R Document.”] Tafadhali unaweza kufafanua kidogo zaidi kwamba hiki
ni kitu gani? Ni nani aliyeiandika? Ni kipindi gani mjarabu? Je, kuna ukurasa
wa tovuti au chochote kilicho kwenye nakala iliyotafsiriwa kuhusu hiki ili
kwamba tuisome?
Jibu:
Kabrasha R ni nakala iliyojulikana zamani sana ya tangazo la ukiri wa imani ya
kanisa ambalo kutokana nalo ndipo Ukiri wa Imani wa Mitume ulichukuliwa, au na
ambayo ilighushiwa kwa kuwa haikuwa na mashiko na mitume.
Herbert
Thurston alihuisha tena misingi na fikra zake kwenye makala yake aliyoiandika
kwenye kitabu cha fafanuzi kijulikanacho kama Catholic Encyclopaedia aliko andika makala ihusuyo ukiri wa imani.
Inaonyesha wazi sana kwamba kanisa huko Roma, angalau sehemu ya pili ya
mwishoni mwa karne ya pili, lilijitangaza lenyewe kuwa ni Kanisa Takatifu na
siyo Kanisa Katoliki. Lilikuwa ni kanisa la Kiyunitarian likiamini kuwa Kristo
siyo mungu na liliamini kuhusu Ufufuo wa Wafu. Kutokana na kazi ya kurekebisha
iliyofanywa na Tertullian, Roho Mtakatifu alikuwa ni nguvu au uweza tu wa Mungu
na siyo mtu.
Imani za Kidini Kitaifa
Nilisoma maelezo kuhusu kambi za mateso
za Croatia na Vatikan. Nilikuwa na wakati mgumu sana sio wa kuyafikiria matukio
haya. Kwa bahati nzuri mimi ni Mjerumani Mkatoliki kwa kuzaliwa lakini uvunjifu
mkubwa wa Amri ya Pili hauna ubishi. Mbali ya kufunga saumu na kuomba kwa ajili
ya ulimwengu ili utubum na uponyaji wa watu, wenyeji na sayari; na kwa kweli
wamtii Mungu wa Pekee na wa Kweli kuna nini kingine cha kufanya?
Jibu:
Lakutisha mno ni kwamba inaonekana kutokuwa na kujulikana halisi kutoka kwa
watu hawa kwamba kwa kwli walifanya makosa. Tuna ushahidi kuhusu viapo
vitolewavyo mahakama ya sharia kwenye migongano ya vita vya uhalifu kutoka kwa
makasisi hawa wa Kifranciscan. Mmoja alikiri kuwa yeye peke yake aliua watu takriban
44,000 yeye mwenyewe. Na bado tunao makasisi walio kwenye mabara au majukwaa ya
ulimwengu ambao wanaendelea bado kukataa ukweli wa mambo yaliyotokea.
Kulikuwa
na takriban kambi za mateso 15000 na kuliharibiwa kambi huko Ulaya. Wayahudi
hawakutupa msaada wowote kwa kujionyesha kwetu kuwa tunafafana kiimani na yakachukuliwa
kuwa yalikuwa ni mauaji ya kuangamiza ya Holocaust ya Wayahudi peke yao.
Lengo
la mkakati huu lilikuwa ni kuwatokomeza watu wote wasioami Utatu na hususan washika
Sabato wa Ulaya. Ulikuwa ni mkakati wa pamoja wa Wakatoliki wa Roma pamoja na
wenye imani ya Kilutheri. Takriban watu milioni 18 waliuawa. Ulikuwa ni mkakati
wa pamoja uliowajumuisha Kanisa Katoliki la Roma pamoja na Walutheri wa Ulaya
ndio waliofanya hivi. Kambi ya kwanza ya mateso ilitolewa kwa watu wa Afrika
Kusini na wakapewa Kanisa la Kilutheri mnamo Desemba 1932. Hii ni miaka kumi
baada ya kile kinachodhaniwa kuwa kipindi cha mauaji ya kuangamiza ya Holocaust
ya miaka ya 1942-45.
Hii ni sawa kama ile tume ya Ukweli na Maridhiano ya
Afrika ya Kusini. Pasipo ukweli hakuwezi kuwa na upatanisho. Bila Kanisa
Katoliki kukiri yale waliyoyafanya nan i wapi imani yao ilikotoka hakuwezi kuwa
na toba.
Haya hayakuwa ni mauaji ya Holocaust yaliyodumu kwa miaka
mitatu peke yake huko Ulaya. Ni kama unavyoweza kuona kuwa maangamizi haya
yalianzia huko Afrika mwanzoni mwa karne hiyo. Hata hivyo, Mabaraza ya
kuwahukumu na kuwatesa watu yalianza kufanya kazi karne kadhaa zilizopita.
Soma kwenye majarida ya Vita Vya Wayunitarian/Watrinitarian (Na.
268). Soma pia kwenye jarida la Kazi ya Amri ya Nne Kwenye Historia ya
Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170).
Mahakama ya mwisho ya Kuhukumu na Kuwatesa watu ilikuwa kwenye
Himaya za Papa katika miaka ya 1823 na 1946. Watu 200,000 walihukumiwa kifo au
wa- manchani za uhalifu. Watu milioni 1.5 waliwekwa kwenye mahabusu ya mateso
makali na vifungo vya maisha; kulikuwa na kitanzi kabisa kila kona. Watu walishitakiwa
kwa Kilatini na hawakuwa na jinsi ya kujitetea na hawakujua sababu ya
kushitakiwa kwao. Mwana historia wa Kijesuit marehemu Malachi Martin anaelezea
kwa kina jambo hili kwenye kitabu chake cha The
Decline and Fall of the Roman Church [Kudhoofika na Kuanguka Kwa Kanisa la
Roma], pp. 250-254ff. Wakati watu wakiichukulia kura ya maoni kama ni masalia
ya imani na mfumo wa kipapa au kufanyika kuwa sehemu ya hadhara, ya wachache
waliosalia walioruhusiwa kupiga kura ya kuwachagua watu 130, 000 waliochaguliwa
kujiunga kwenye Jamhuri na wengine 3000 peke yao wasio wa kawaida waliotaka
kubakia.
Maaskofu waamini Utatu na wazee wa makanisa
yao walifikia kujaribu kuyaandaa mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994 ambapo
waliweka mikakati, kuonyesha, na kuwalipa watu ili wawaangamize zaidi ya watu 900,000
waliouawa na huenda waliouawa wanafikia idadi kubwa zaidi ya hiyo na hata
yaweza ikawa ni mara mbili yake.
Yatupasa tumgeukie Mungu aliye-hai kwa kuomba na kufunga
na kuzitubia dhambi zetu pamoja na mafundisho yetu ya kizushi pamoja ibada zetu
za sanamu. Yatupasa tupate Amri Kuu ya Kwanza ya kwenye Torati moja kwa moja
hata kabla hatujaendelea kwa kina kwenda kwenye Amri Kuu ya Pili lakini kabla
hatujaipata Amri Kuu ya Kwanza basi yatupasa kuipenda kweli na kuendeleza
shauku halisi ya kuwapenda watu wote.
Kama hatutawapenda majirani zetu tunaowaona basi
tutawezaje kumpenda Mungu tusiyemuona. Umechukua hatua ya kwanza kwenye njia
ndefu hadi kwenye matengenezo mapya.
Waskochi hawakutokea Scotland mwanzo wao.
Ni wapi lilipo eneo lililojulikana kama lilichimbwa chimbuko lao na masalia na waliwezaje
kufika Scotland?
Jibu:
Waskochi wana historia hii hii ya kitabaka kama wa Irish. Hii kwa kweli
inamaana kwamba Waskochi walikuwa (nab ado wapo) Waseltiki. Tukirudi hatua moja
nyuma kutoka kwa Hispania inaonekana kuwa uhusiano wake na Georgia wa huko
Caucasus.
Neno
Iberia (kama ilivyo Latin Iberi) nchi ya Iberi, inatokana na neno la Kiyunani
la Iberes, ambalo lilitumika kwa watu wawili. Mmoja alikuwa ni mtu wa Hispania
na wendine ni wa Iberians, ambao walikuwa ni wa jamii ya Kiasiatiki karibu na
Caucasus.
Wagodelian
walikuwa ni wana wa Yafeti lakini jina Iberi linaonekana kuwa la namna ya
Kiyunani ya Kisemitiki. Biblia inawaita wakazi wa asili wa Hispania Wagodelian kutoka
kwa wana wa Godel. Hawa wa Iberians wanachukuliwa kuwa ni wa uzao wa Basque.
Iberia
ya kale huko Asia ilikuwa eneo lenye wastani wa ile inayojulikana sasa kama Georgia.
Iberian pia ni neno
la Kiingereza cha Katikati la lugha ya Basque, (soma kamusi ya Oxford Universal Dictionary).
Upande wa mbali zaidi wa mashariki tuliona masalia yao
yako kwenye eneo la Urumqi huko Tien Shan katika Uygur Dini ya Kienyeji na ya Wenyeji
(Xinjiang Uygur Zizhiqu) wa Kaskazini Magharibi mwa China.
Maiti zao zilikutwa zikiwa na nguo na mali za thamani kwa
kweli. Walikuwa wanavaa ala za kuwindia za bluu na za samawati pamoja na hizo
walikuwa na ala zilizonolewa pamoja na za michirizi iliyokatisha ya rangu
nyeusi na nyekundu zote zilikuwepo. Wanaume walikuwa warefu hadi futi sita nan
chi sita kwenda juu. Wote walikuwa na nywele za rangi ya kaki (na macho
maangavu ka kizungu?).
Wataalamu wa ushonaji na kufuma nguo wameandika kitabu
chenye kichwa cha habari Mummies of
Urumqi (Maiti za Waurumqi). Kinaelezea masuala ya nguo na kina picha za masala ya miili au maiti.
Wachina waliikuta iliwa imekalishwa ilipogunduliwa kwa muda mrefu hadi mgeni
alipoachiwa kujikwaa juu yao na wanazuoni wa Kichina waliopenda mavumbuzi
yaliyotolewa na kupewa utambulisho.
Je, kuna tofauti
yoyote kati ya Waselti na Waselti wa Kihyperborean? Nimesikia maneno yote
mawili yakitumika lakini sielewi kama kuna ni wamoja au ni makundi tofauti.
Jibu: Neno lililotumika na Wayunani ili kuwataja Waseltiki
waliokuwa upande wa Kaskazini au “juu ya Kaskazini” (yaani Wind)." Walisemekana
kuwa waliishi kisiwani upande wa kaskazini na kwa hiyo tunaongelea Uingereza.
Hawa Waseltiki walijulikana na Wayunani waliopenda
Filosofia na kuichukulia kuwa ni njia ya kujikomboa na kujiweka huru kutoka
kwenye gurudu au mzunguko huu wa kurudiarudia kuzaliwa ambao Waselti walikuwa wamejiunga
na ulimwengu kuuamini katika Milenia ya Kwanza KK.
Habari zao hazijaandikwa kwa ukamilifu sana na huenda
tutafanya hivyo hivi karibuni tu. Soma kwenye majarida ya Vita Vya Wayunitarian/Watrinitarian (Na. 268); Msalaba: Chimbuko Lake na Maana Yake (Na. 39) na lile la Ndama wa Dhahabu (Na. 222). Pia soma kwenye tovuti ya www.Abrahams-Legacy.org.
Unajua nini kuhusu
nadharia ya Gaia? Ni ya kweli? Ni nini mawazo yako? Je, kuna usanii wowote au
mashairi au kitu chochote kutoka kwenye dini au cha kidini kilichotabiriwa au
kunenwa kabla ya kujitokeza kwa dhana au wazo hili?
Jibu: Maandishi ya Gaia yameanikizwa kifilosofia kutoka Parmenides
na mfumo wa mmoja. Plato anaiendeleza hii na mfumo wake wa kiimani umeainishwa
kwa kina kwenye kitabu cha ufafanuzi cha Proclus'
Commentary on Plato's Parmenides.
Dhana ya kuwepo kwa Mama Mungu au Mama wa Dunia inatokana
na imani ya miungu mingi, ambayo chimbuko lake linakutikana kwenye imani ya
kianimisti ya kishamani. Na sasa inaendelezwa kwenye Teolojia Machato sambamba
na Shule ya Kyoto kama ilivyoanzishwa na Hartsehorne na Whitehead.
Tofauti ya Teolojia ijulikanayo kama vuguvugu la Zama
Mpya inatafuta kuiendeleza ikiwa kama theori inayoupinga Uumbaji chini ya uweza
mahiri wa Baba Mungu. Lengo ni kufanya uwingi mtakatifu wa miungu na wa kudumu.
Ni theory ya zamani sana iliyotuama kwenye uwongo wa namna zote mbili yaani
kifalsafa na kiteolojia. Inaunda sasa kwenye nadharia za imani ya ulimwengu kutoka
kwenye Kipigo Longolongo kama ilivyoenezwa kusemwa na Hawking na huenda
Penrose.
Je, neno Tara lina maana
gani linapotumiwa kwenye masuala ya dini?
Jibu: Jina Tara ni la ki Irishi na linakitaja Kilima
Kitakafitu cha Tara kilichopo huko Ireland ambako jiwe hili linaitwa kuwa ni
nguzon ya jiwe la Yakobo kutoka Betheli lililoletwa kupitia Misri na Uhispania
hadi Ireland mnamo mwaka 700 KK na likawekwa hapo. Neno tara (SHD
8652) ni kama mlinda mlango na ambalo pia limechukuliwa kutokana na mtazamo au
maana hii.
Wafalme walikuwa wanavikwa taji wakiwa juu yake wakati
huo. Jiwe hili liliaminika kuwa liliondolewa hapo na likachukuliwa na kupelekwa
hadi Scone iliyoko Scotland na Fergus wakati alipoanzisha shughuli za kitawa na
kiseja kwa Waskochi. Tarehe zilizotolewa ni za kubuni tu na siyo za kweli. Lilichukuliwa
na kupelekwa huko Westminster Abbey na Edward I mwaka 1297.
Wafalme
na Malkia wote wa Uingereza wamekuwa wanavijwa taji zao za ufalme juu yake
tangu wakati huo. Inadaiwa kuwa ni kuwaendeleza Wafalme wa kweli wa Israeli.
Hivi punde tu ndipo lilirudishwa Scotland.
Tara ni jina la kiti cha zamani cha wafalme wa Ireland. Linatokana
na lugha ya Kikaldayo lenye maana ya mlango na ndiyo kasri la ufalme; ambalo ni
lango au kinywa. Hapa ni mahala au uwanja wa wafalme. Maneno yote mawili
yanatumika kwa maana hizi kwenye Biblia.
Pia Tara inaonyesha imani za kimashariki za mungu-mke Tara,
ambaye ameelezewa kwa kina kwenye kitabu cha Cox, cha Mysticism, CCG, 2001.
Ni nini maana ya
kifalsafa ya nadharia tata kwenye sayansi na kwenye dini?
Jibu: Nadharia tata au ya machafuko imetuama kwenye msimamo wa
kwamba hakuna agizo la kulifafanua hapa ulimwenguni. Ulimwengu unajibu mapigo
zaidi kuliko ulivyoshawishiwa kwa shuruti au kwa amri yoyote ile. Amri
isiyofafanuliwa siyo machafuko na haichefui, bali ni kwamba haijafafanuliwa tu.
Nadharia hii ina dalili pana sana kwenye dini kama inavyo maanisha hapo kwamba
hakuna Mungu aliyeamuru kuwepo mfumo au utaratibu.
Kutokana na hii tunapata hamasa inayofanana. Chochote kile kinachotarajiwa ni cha kimaadili. Hakuna
ukamilifu wa kimaadili. Kuhusu sayansi tuna mkururu wa majarida ya sheria,
ambazo zimetuama kwenye maagizo. Sheria au kanuni za Mwendojoto ni muhimu kwa
hiyo.
Jambo hili limefafanuliwa kwa kina kwenye majarida ya Uumbaji: Kutoka Kwenye Nadharia ya Kianthropomorphiki Hadi Kwenye Ile ya
Anthropolojia ya Kitheomorphiki (Na. B5). Vikwazo vya
nadharia ya Machafuko inakutikana kwenye kitabu cha Wanasayansi kama vile kina
Hawking Penrose.
Falsafa ya Causation inahusiana pia na mambo haya. Causation
ni Mwamini umoja kama ilivyoonyeshwa kwenye Uumbaji. Kwahiyo siyo kuzuka na kwa
hakika siyo fujo. Kuoza kwa K Mesons kuliashiria kuwa hii siyo nadharia sahihi.
Soma pia kuhusu Uumbaji. Uteuzi wa kifungu cha kiwango cha sauti ya angani kwa
viwango vya 10 hadi 10 hadi 123 pia kunaipinga au kuitatiza. I,eandikwa:
Mpumbavu amesema moyoni mwake hakuna Mungu.
Ni kitu gani basi
kachojulikana kama “Baraka ya Toronto” na chimbuko lake ni wapi?
Jibu: Ilianzishwa mjini Toronto Canada. Watu walishinikizwa
kwenye namna yao ya kuwaza kwenye ibada zao na waliguswa kichwani na kuanguka
chini wakiwa na hali ya kupagawa au kiwewe au tofauti kwenye maana. Ni fundisho
la uamsho wa Kipentecoste iliyojumuishwa na mafundisho mengine ya kupayuka
payuka kimaneno na yote yanayoendananayo.
Imeainishwa kwa kina zaidi kwenye majarida ya: Swali Kuhusu Kunena kwa Lugha (Na. 109); Kunena kwa Lugha Kuliishia Lini? (Na. 182); Baraka ya Toronto, Ni Muweweseko wa Kupagawa na Mapepo (Na. 149).
Unafikiri nini kuhusu
maandiko ya kale ya Kisumerian yaliyoelezea kuhusu gharia kuu na “Vipande vya
mawe vilivyoandikwa mambo yanayoielezea mashua kubwa iliyotengenezwa kwa
kuamriwa na mfalme aitwaye Ziusudra, aliyekuwa analinda mazao ya mbogamboga na
mbegu ya mwanadamu”? hudhani kuwa huenda Mungu alimuamuru mtu mwingine aijenge
mashua kama Nuhu? Pia ni je, kuna mandiko yoyote ya kale ya lugha ya
Kiebrania yaliyopatikana? Kama jibu lake ni Ndiyo, ni kweli kwamba jina la
Mungu limeandikwa YHWH?
Jibu: Ndiyo, maandiko haya yanapendeza sana. Ziusudra ni aina
ya Kisumerian ya jina. “Tamko la Gilgamesh” inatoa aina ya Kimesopotamian:
“Utnapishtim” (iliyoitwa ni mbali sana). Mtindo wa kimaandiko wa Kiyunani
ulikuwa “Xisouthros.” Yote hayo ni matoleo ya hadithi ya Nuhu.
Kwenye “Tamko la Gilgamesh” wanamnukuu akimuomba mungu
Sin, ambaye ni mungu mwezi. Hili ni chimbuko la neno la Kianglo Saxon kumtaja
mungu sin. (Soma kwenye jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222).) jarida hili lina mambo mengi sana yaliyoainishwa kwa
kina.) Kipimo cha safina kilibuniwa kwa aina yake. Kwenye “Tamko la Gilgamesh” familia
za wafanya kazi zinachukuliwa pamoja nao pia.
Kwenye maandiko ya Kisumerian, unayoyaelezea, Ziusudra anajionyesha
mwenyewe mbele ya kina Anu na Enlil, miungu ya Wasumerian. Andiko hili pia
linatoa tanko la uumbaji wa “watu wenye vichwa vyeusi” (neno lililotumika
kuwataja Wababeloni na Wachina pia kwenye maandiko yao, na hapa lina maanisha ongezeko
la idadi ya watu ulimwenguni kwa ujumla) na ulitanguliwa na kuumbwa kwa
wanyama. Gharika ilidumu kwa siku saba na ilizoa au kufagia vituo vitano vya
dini hizi potofu duniani, ambavyo viliwekwa chini ya miungu na baraza la miungu
huko mbinguni.
Habari hizi zimebuniwa kwa matoleo mengi zaidi au
machache yanayohusu gharika yaliyoandikwa karibu miungu yao yote ya zamani.
Hata hivyo, wanaonyesha undani wa dhana yenyewe ya baraza la elohim na
inavyofanana na hadithi ya gharika kuu na lengo lake. Kuna nakala za hadithi
hiyohiyo ya Nuhu. Nkala ya Kiebrania haiandiki YHWH bali YHVH. Hakukuwa na herufi
“w” kwenye Kiebrania. Vav inatamkwa kama sawa na inavyotamkwa “w” lakini
inaandikwa “V”. maandiko ya zamani hayakuwa na vokali. Kwa hiyo YHVH ni uandishi
sahihi wa andiko hili. Tuna “Lachish Ostracon,” ambao ni uandishi wa kipindi cha
Yeremia. Tafsiri ya kisasa ya Albright imeliandika jina hili kuwa Yahweh. Maandiko
ya Elephantine yaliyotafsiriwa na Ginsberg yanaonyesha shina la uandishi wa neno
halikuwa Yah (liliandikwa Jah kwenye tafsiri ya Kiingereza) bali Yaho na hivyo
andiko hili linakuwa ni Yahova na siyo Yahwe. Limeandikwa YHVH kwenye Kiebrania
asilia. Makabrasha yapo yote kwenye maandiko yaliyoandikwa na James B Pritchard
kwenye kitabu chake cha The Ancient Near
East...(Mashariki ya Karibu ya Zama
Kale), Princeton, 1958.