Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[116]

 

 

 

 

Majina ya Mungu

(Toleo La 2.0 19950306-20000705)

Majina ya Mungu yametolewa na kufafanuliwa. Mazingira ambayo yametumika ni ya muhimu kwenye kuelewa jinsi Mungu anavyotenda na ni kwa nani anayeongea naye.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 2000 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Majina ya Mungu

 


Moja kati ya dhana au nadharia inayokosewa kueleweka vyema kwenye Biblia ni jina la Mungu. Imekuwa ikipotoshwa kwa upande mmoja na makosa ya kuwaaminisha au kuwafundisha waamini Utatu au Watrinitariani ikifuatiwa na karne ya nne, na kwa upande mwingine, kwa kukithi shauku ya imani ya Kiyahudi ili kuilinda imani yao ya Mungu mmoja au Umonotheism dhidi ya mafundisho potofu ya Kitrinitarian pamoja na mamlaka au nguvu kuwili za kiuzushi. Shauku ya kulinda ukuu wa kipekee wa Mungu na kuitetea imani ya Kimonotheism iliyo kwenye mfumo na mafundisho ya Biblia kutokana na makosa na upotoshaji yanayoendelezwa kwenye mafundisho ya Kibinitariani na Watrinitarian kwa uzushi mkubwa na wa nguvu, ulioshuhudia hatimaye imani ya Kiyahudi ikiachana kwa taratibu sana ukweli kuhusu uhalisia na muundo mdogo wa jinsi Mungu alivyowafanyia Israeli. Malaika Mkuu ambaye Elohimu amemhusisha kwenye maandiko. Matokeo mabaya ya jambo hili ni upotoshaji wa baadhi ya maandiko muhimu na kuificha kweli umuhimu wa kiumbe huyu mwakilishi aliyeshughulika na kuwaongoza Israeli kwenye kipindi cho chote cha historia yao. Viumbe hawa wana majina, na majina yao yanaashiria uhusiano wao. Justin Martyr kwenye waraka wake wa First Apology au Utetezi wa Kwanza kwa niaba ya Kanisa aliompelekea mfalme wa Roma anasema kwamba Kristo alikuwa ndiye Malaika wa Mungu kwenye Agano la Kale aliyempa Torati nabii Musa.

 

Kulijua jina la Mungu ni ishara na dalili tosha ya kuielewa vyema Biblia. Makosa makubwa na yaliyozoeleka ya mafundisho potofu kuhusu jina la Mungu yanatokana na kuielewa vibaya Zaburi 83:18.

 

Zaburi 83:18 Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.

 

Jina hili lilikuwa linatamkwa Yahova (halikuwa na herufi J kwenye lugha ya Kiebrania). Viumbe wengi wanachukua jina hili kwa niaba ya yeye Mungu wa Kweli.

 

Andiko hili lenye rejea ya karibu na Kutoka 6:3 na Isaya 26:4. Maandiko haya matatu yalikuwa ndiyo sehemu tatu kwenye tafsiri ya biblia ya Authorised Version ambamo andiko hili lilitafsiriwa na kuchapishwa kwa herufi kubwa na zilizokolea. Andiko la Zaburi 83:18 linaonyesha cheo kingine chenye jina la Yehova aitwaye Elyon au Mungu Aliye Juu Sana. Hiki ni cheo kinachotofautisha kama tutakavyokwenda kujionea. Ni Yehova yuleyule ndiye afanyaye kazi na kuonekana akiwa sawasawa tu pasipo kutofautika. Anayeonekana wazi mwingine ni Yahwe. Huyu pia anakuwa hafanani. Maandiko mawili mengine yanasomeka:

 

Kutoka 6:3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.

 

Isaya 26:4 Mtumainini Bwana siku zote Maana Bwana YEHOVA ni mwamba wa milele.

 

Jina la Mungu ambalo lilikuwa halijulikani na Mababa wa zamani yalikuwa na maana halisi na ndivyo ilivyokuwa pia na madhumuni yake.

 

Jina Yehova (au kwa usahihi wake sana linaitwa Yahova) ni mjumuisho wa jina Elohim nan linamaanisha Elohim na El kwenye Zaburi 83:1. Elohim ni jina la uwingi, ambalo linategemea na jissi linavyotumiwa. Linamaana zote mbili, yaani Mungu mmoja na miungu. Linamaanisha au kumtaka kiumbe mmoja asilia na asiye wa kawaida. Linawataja viumbe wengi wasiojulikana walio kwene Mwanzo 1:26.

 

Mwanzo 1:26  Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Wabinitariani wanajaribu kuhusisha au kuumaanisha usemi huu na viumbe wawili, wajulikanao kama Mungu Baba na Kristo, lakini hata hivyo, jambo hili haliwezekani kupewa maana kubwa ya kuwepo kwa Elohimu wengi na andiko lililo kwenye Ayubu linalowataja wana wengi waliokuwepo wakati wa uumbaji (Ayubu 1:6; 2:1; 38:4-7).

 

Ayubu 1:6 Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.

 

Ayubu 2:1 Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za Bwana.

 

Hawa ni Wana wa Mungu (haElohim). Neno Bwana lililopo hapa linamaana ya Yehova (yaani Yahova). Tafsiri ya biblia ya The Companion Bible lina makala inayofafanua kuhusu jina hili la Yehova kwenye Jarida lake la Nyongeza au Appendix 4, II. Yehova inachukuliwa kumaanisha wa Milele au Mwenye Kusikika. Tafsiri yake ipo kwenye Mwanzo 21:33.

 

Mwanzo 21:33 Ibrahimu akapanda mkwaju huko Beer-sheba, akaliitia huko jina la Bwana Mungu wa milele.

 

Umilele unaoelezewa hapa unatokana na neno la Kiebrania la ‘olam lenye maana ya kipindi endelevu au bila ukomo. Chimbuko la neno Yehova maana yake inaaminiwa kuwa ni Yeye aliyekuwepo na Anayekuja. Kuna tatizo katika kulichukulia jina lililotolewa pale Sinai kulichukulia kuwa lina maanisha Yehova tu, peke yake.

 

Kutoka 3:14 Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO amenituma kwenu.

 

Neno Mimi niko lililoko hapa linamaana ya hayah (%*% SHD 1961) ambalo maana yake ni kuwepo, kuwa au kufanyika kuwa. Tafsiri ya biblia ya the Companion Bible inaonyesha andiko hili kuwa ‘ehyeh ‘asher ‘ehyeh, na imelitafsiri neno hili kuwa Nitakuwa jinsi nitakavyokuwa (au nitakuwa) (soma maandiko yake kwenye ukurasa wa Nyongeza wa 48), hakuna pia kinachomaanisha neno Yehova kuwa ni Yeye atakuwa anaongelewa kwa pamoja na wenginewowote. Wanazuoni wa chuoni Oxford wameonyesha kwenye tafsiri yao ya biblia ijulikanayo kama Oxford Annotated RSV kwamba Yahwe kwa kweli ni muundo wa nafsi ya tatu ya vebu ambayo kwa kweli inamaanisha Yeye anayesababisha kuwa.

 

Kwa hiyo Mungu anajidhihirisha kuwa ni kama Nitakuwa kama nitakavyokuwa kwa kupitia Malaika pale Sinai. Anajulikana na kutajwa kama Yehova (Yahova) ambayo inamaanisha kwa mtindo au umbo la nafsi ya tatu: Anayesababisha kuwa. Wakati mtu yeyote anapotajwa kuwa ni kama Yehova kwa kweli utakuwa unasema kwamba Aliyesababisha kuwa. Na kwa hiyo utakuwa unaunga mkono au kuitabua asili ya usaidizi wa kiumbe yeyote anayenena na wewe. Wayahudi walielewa hilo na Mungu hakuongea nao kabisa na wao; bali walipewa maelekezo yao yote na malaika ambao walikuwa ni wajumbe wake. Wajumbe hao waliitwa Yehova na jina hilo linamaanisha ni Yeye anayesababisha kuwepo, kwa kuwa yeye anayesababisha mambo kuwa hakuwepo kabuisa huko. Unapolielewa neno Yehova unakuwa kila mara unajua kuwa unamtaja mjumbe ambaye ni mtu fulani ambaye hujawahi kumuona au kuongea naye. Neno Yehova lina maana ya moja kwa moja ya Sijawahi kumuona kabisa yeye.

 

Kwa hiyo, jina alililotolewa la kuwa ni MIMI NIKO pale Sinai lilikuwa ni Mimi niko na ambaye nitakuwepo ambao ndiyo ujumbe ambao Mungu aliyempa Malaika huko Sinai. Neno la Mungu lililotafsiriwa kama MIMI NIKO haliku limetumika kabisa tena. Lilitumiwa mara moja tu kwenye Biblia. Neno la Mungu ambalo neno hili limetoholewa kwalo limeandikwa kwa namna au mtindo wa nafsi ya tatu la vebu. Tunajua kutokana na Yohana 1:18: Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua. Hivyo, walilitafsiri tu kuwa ni Mwana pekee ili kuifikia nadharia au wazo la kwamba kulikuwa na mmoja tu aliyezaliwa na Mungu.

 

Ni Mungu pekee ndiye aliyenena na huyo ndiye monogenes theos, yaani Mwana pekee wa Mungu. Kwa maneno mengine ni kwamba Yesu Kristo ndiye pekee aliyenena au kuongea na Mungu. Baba Mungu hajaongea kamwe. Unapoyaona majina haya kwa lugha zote mbili, yaani Kiebrania na Kiyunani ndipo unapata kujua au kuelewa. Tunapata matumizi mamoja tu ya neno moja kumtaja Mungu na kisha tunalitumia jina Bwana na mambo mengine ili kufikiliza. Kuwa na neno moja la Mungu kunatosha sana kwa kuwa hatutaweza kujua kinachofanyika kwa kupitia majina ya Mungu.

 

Andiko linalofuatia kwenye Ayubu ambali linahusika na Jeshi la Malaika ni kwenye Ayubu 38:4-7.

 

Ayubu 38:4-7 Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa na ufahamu. 5 Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake? 6 Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni, 7 Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?

 

Kutokana na andiko hili tunajua kwamba andiko lililo kwenye Mwanzo 1:26 …… Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; linataja kundi la viumbe ambao walikuwepo tangu mwanzo wa kuumbwa kwa dunia; na kwamba kulikuwa na nyota wengi wa asubuhi; na nyota ya asubuhi ni daraja au cheo na sio kiumbe. Kwenye suala hili la mwanzoni mwa kuumbwa kwa dunia kuna nyota wengi wa asubuhi. Kulikuwa na mifumo mingi ya makamanda waliokuwepo wakati wa kuumbwa kwa dunia hii. Hivyo kunajitokeza hoja nyingi hizi zote kwamba kuna nafsi mbili Elohimu na kwamba kuna Mwana mmoja tu wa Mungu. Maandiko hayo yanaonyesha kwamba imani ya Kibinitariani ina uwongo mkubwa sana kama ilivyo ya Kiutatu au Utrinitariani tu na inakwaza uelewa wa hatika yetu na inajaribu kututenganisha na urithi wetu, ambao ni kufanyika kuwa warithi tulio sawa na Kristo na kutawala kama wana wa Mungu na tutatawala tukiwa kama elohimu na eli.

 

Nyota za asubuhi wanazotajwa hapa ni wengi na wakati bado Kristo hajachukua wadhifa wake wa kuwa nyota wa asubuhi wa sayari yetu hii na Shetani alikuwa ni Lusifa bado au mpeleka nuru kama mwana wa asubuhi, nyota ya asubuhi au nyota ya mchana. Yeye ni mungu wa dunia hii na mfalme wa nguvu za anga (2Wakorintho 4:4; Waefeso 2:2).

 

2Wakorintho 4:4 haisemi kwamba Shetani ni theos wa dunia hii pasipo sababu. Waamini Utatu wanajaribu na kusema kwamba tangua Thomas aliposema kuwa ninyi ni kurios na theos wangu kwa Kristo, kwa hiyo basi yeye ni Mungu Babba kwenye mjumuiko wa Utatu. Kwa kweli, Paulo anasema wazi kabisa kwamba Shetani ni theos wa dunia hii. Wote wawili ni theoi: wote wawili ni miungu. Biblia inasema wazi sana kuhusu jambo hilo. Paulo anasema kwenye 1Wakorintho 8:5 kuwa kuna theoi wengi na Mabwana wengi.

 

Kile tunachokiona kuhusu Shetani kimeendelezwa kutoka kwenye Isaya 14:12-17 kunakomtaja kama Lusifa au Mleta Nuru.

 

Isaya 14:12-17 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! 13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.

 

Hawa nyota wa Mungu wanaotajwa hapa ni wana wa Mungu. Nyota ni cheo au daraja. Yeye ni kaburi. Tunakwenda kuwa naye nyota wa asubuhi anayekwenda kuzikwa kaburini.

16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme;

 

Tuna mabadiliko kwenye mazingira ya kicheo hapa kwa mwanadamu.

17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?

 

Hapa tunaona kwamba Lusifa, au mleta nuru, alikuwa mwana wa asubuhi au nyota ya asubuhi au nyota ya mchana. Wadhifa huu wa kicheo amepewa Kristo na aliwashirikisha wateule wake (2Petro 1:19; Ufunuo 2:28; 22:16):

 

Ezekieli 28:14-19 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. 16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto. 17 Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama. 18 Kwa wingi wa maovu yako, katika uovu wa uchuuzi wako, umepatia unajisi patakatifu pako; basi nimetokeza moto kutoka ndani yako, nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi, machoni pa watu wote wakutazamao. 19 Wote wakujuao kati ya kabila za watu watakustaajabia; umekuwa kitu cha kutisha, wala hutakuwapo tena hata milele.

 

Maandiko haya yapo wazi. Vifaa vitakavyotumiwa kumwangamiza Shetani vinakuja kutokana na nguvu za kiroho zilizoko ndani yake, yaani nguvu hizi zinakwenda kuwa ni vifaa vitakavyomwangamiza au vya kuangamizwa kwake. Roho hii haitakwenda kuwepo tena kabisa. Lusifa, nyota wa Asubuhi anakwenda kukoma kuwepo kwake. Anakwenda kufanyika kuwa mwanadamu, akiwekwa kwenye mchakato na kupewa fursa ya kutubu na kisha anakwenda kubadilishwa hulka yake na kuwa kiumbe wa namna nyingine. Njia pekee ya kumtiisha Shetani pamoja na malaika zake waovu ni kwa kuwatoa nje ya hulka au maumbile yao waliyonayo sasa, na kuwapa fursa ya kutubu na kwa suala la Shetani kumfana aingie kwenye mchakato ambao kwao anaweza kutiishwa. Kwa hiyo ndipo anapoweza kufanyika tena kuwa ni nguvu na uweza na ndipo anaweza kutiishwa na kufikia utii kamili na maovu yake yanaweza kuondoka na kisha akarejeshwa kwenye kundi la malaika.

 

Propaganda nyingi zimekuwa zikienezwa kusema kwamba Mungu hatendi haki na kwa kweli ndiye aliyemuumba Shetani awe kama hivi alivyo tangu mwanzo na Shetani hajapewa fursa. Kwa jinsi hiyohiyo, Kristo naye aliumbwa mkamilifu tangu mwanzo na asingeweza kufanya lolote kwa kuwa alikuwa na tabia na asili ya Mungu na Shetani hakuwa nayo na wote ni mchezo uliokusudiwa. Hii ni propaganda ya Kishetani na kama utaangukia kwenye uwongo huo wa kwamba Kristo asingeweza kutenda dhambi na kwamba Shetani asingeweza kufanya jambo lolote jema, basi utakuwa unaifanya kazi ya Shetani kwa niaba yake na kuutendea kazi mfumo wote wa imani ya Utatu unaoendelezwa kusema kwamba kanuni zake ziliimarika, na kwamba Mungu hatendi haki. Mungu hana upendeleo kama tutakavyokwenda kuona.

 

Shetani anakwenda kuangamizwa kabisa na hataweza kuishi, kwa mujibu wa andiko hili. Atakwenda kupunguzwa na kushughulikiwa wakati wa Marejesho mapya na siku ya Hukum (soma majarida ya Hukumu ya Mapepo (Na. 80) na Lusifa, Mbebeba Nuru na Nyota ya Asubuhi (Na. 223)). Vyeo hivi hata hivyo vilikuwepo hata kabla ya kuumbwa kwa dunia na walikuwa wengi. Wana wa Mungu (haElohim) walijihudhurisha mbele za Yehova kama tulivyojionea kwenye kitabu cha Ayubu.

 

Jina au neno Yehova liko kwenye aina mbili zenye maana iliyo tofauti. Ni neno ambalo linaendana pia na majina mengine. Aina mbili zilizo tofauti zipo kwenye jina hili la Yehova (SHD 3068) na jina Yehovi lililo kwenye kamusi (SHD 3069). Kwa kweli yanatofautiana kwa kuonyesha watu wawili wenye kubeba jina hili la kiwdhifa la mwingine na mwingine ni mdogo.

 

Kamusi ya Strong inasema kwamba Yehova ni jina la Kiyahudi la Mungu wa taifa. Utofauti wa Yehovi (au kiuhalisia na sahihi huitwa Yehovi) linatumiwa badala ya kutaja Adonai au Bwana. Huyu ndiye Bwana, Yehovi au ni mkuu kwa Yehova. Nie Yehova elyoni au Yehova wa Majeshi. Jina Yehova linatumika kama neno la kutofautisha. Yehova anayeitwa kuwa Yehova wa Majeshi kama Yehova, ndiye Yehova aliyetajwa kwenye Ezekieli 16:36, 31:10,15; 38:10,14; 39:8. Anayejulikana kama Yehova dabari au neno la Mungu linalojitokezwa kwenye Ezekieli. Adonai Yehovi linatumia kwenye unabii wa Ezekieli 29:8 ambalo linaashiria kutofautisha kati ya neno la Mungu na Yehovi Adonai.

 

Zekaria inaonyesha kwamba kuna tofauti kwenye majina na watu wenyewe (Zekaria 2:3-12).

 

Zekaria 2:3-12 Na tazama, yule malaika aliyesema nami akasimama karibu, na malaika mwingine akatoka ili kuonana naye; 4 naye akamwambia, Piga mbio, kamwambie kijana huyu, na kusema, Yerusalemu utakaliwa na watu, kama vijiji visivyo na kuta, kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo ndani yake. 5 Kwa maana mimi, asema Bwana, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake. 6 Haya! Haya! Ikimbieni nchi ya kaskazini, asema Bwana; kwa maana mimi nimewatawanya ninyi kama pepo nne za mbinguni, asema Bwana. 7 Haya! Ee Sayuni, jiponye, wewe ukaaye pamoja na binti Babeli. 8 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake. 9 Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono wangu juu yao, nao watakuwa mateka ya hao waliowatumikia; nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma. 10 Imba, ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa kati yako, asema Bwana. 11 Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwako. 12 Na Bwana atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi takatifu, naye atachagua Yerusalemu tena.

 

Ni wazi sana kutokana na andiko hili kwamba kuna malaika wawili wanaohusika hapa. Mmoja ni bora na mkuu kwa mwingine na huyu aliyebora zaidi na mkuu ni Masihi kwa kipindi chake cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi hapa duniani. Ananena kwa niaba ya Yehova wa Majeshi aliyemtuma. Aya ya 5 inamtaja kama kwa maana Mimi nasema Bwana lakini kwa kweli inasema kwa kuwa Mimi ni mjumbe wa Yehova (soma kwenye Companion Bible fn. to v. 5). Malaika huyu ambaye no mjumbe wa Yehova ndiye atawaokoa Israeli kutoka kwenye mataifa (aya ya 9) na, kwa hiyo, mataifa mengi yatajua kwamba Yehova wa Majeshi amemtuma kiumbe huyu kwao. Neno mboni ya jicho lake kwa kweli linamaanisha mboni ya jicho langu. Neno “langu” limebadilishwa na kusomeka “lake” na Sopherim kwa likitiliwa maanani neno lililo kama ni kumpunguzia heshima au udhalilishaji kwa Yehova (soma kwenye tafsiri ya Companion Bible fn. Hadi aya ya 8). Mabadiliko haya huenda yalitokana na kwamba neno mboni ya jicho langu limesababisha kufanya lionekane kuwa ni mboni ya jicho la kiumbe mdogo. Mataifa mengi yataunganishwa kwa Bwana (Yehova) katika siku ile. Ataketi katikati yao na watajua kwamba Yehova wa Majeshi amemtuma kwao.kwa maneno mengine ni kwamba huyu Yehova anayetajwa hapa ni malaika aliyetumwa kwa Waisraeli na Yehova wa Majeshi. Malaika huyu au mjumbe wa Yehova wa Majeshi alikuwa ni elohim wa Israeli. Zekaria 12:8 inaonyesha wazi kwamba Malaika wa Yehova alikuwa ndiye elohim na kwamba watakatifu watakuwa pia elohim kama alivyo yeye.

 

Zekaria 12:8  Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.

 

Neno “Mungu” lionekanalo hapa linamaanisha elohim na malaika wa Bwana ni Malaika wa Yehova. Lengo lake liko wazi. Wote wawili, yaani malaika na watu wa nyumbani mwake Daudi (yaani watakatifu) watakuwa kama elohim.

 

Elohim kama ilivyoelezewa hapo nyuma ni jina la uwingi la Mungu. Neno linalosimama kuhusu Mungu kwa umoja ni Eloah. Jina hili linathibitisha haiba ya umoja ya Mungu. Mithali 30:4-5 inaonyesha kwamba ana mwana pamoja na kulitoa jina lake Eloah baada ya kuuliza swali.

 

Mithali 30:4-5 Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake? Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake? Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua? 5 Kila neno la Mungu limehakikishwa; Yeye ni ngao yao wamwaminio.

 

Neno linalosimama kuhusu Mungu kwenye aya ya 5 ni Eloah. Dhana na nadharia kuhusu mwana wa Mungu ni kwamba linaweka wazi kwenye Agano la Kale. Nabii Ezekieli anaonyesha pia dhana hii kwenye andiko lake la sura ya aya ya 21:8-13:

 

Ezekieli 21:8-13 Neno la Bwana likanijia, kusema, 9 Mwanadamu, tabiri, useme, Bwana asema hivi; Nena, Upanga, upanga, umenolewa na kusuguliwa, 10 umenolewa ili kufanya machinjo; umesuguliwa ili uwe kama umeme; basi je! Tufanye furaha? Upanga unadharau fimbo ya mwanangu, kama unavyodharau kila mti. 11 Nao umenolewa usuguliwe, upate kushikwa mkononi; upanga umenolewa, naam, umesuguliwa, ili kutiwa katika mkono wake auaye. 12 Piga kelele, utoe sauti ya uchungu, Ee mwanadamu, kwa maana upanga u juu ya watu wangu, u juu ya wakuu wote wa Israeli; wametolewa wauawe na upanga pamoja na watu wangu, basi, jipige pajani. 13 Kwa maana kuna kujaribiwa; itakuwaje, basi, ikiwa upanga unaidharau hiyo fimbo? Haitakuwapo tena; asema Bwana MUNGU.

 

Usemi ulio kwenye aya ya 9 unatokana na jina Yehova, hata hivyo baadhi ya viambatanisho vyenye matoleo mengine matatu yaliyochapishwa mwanzoni zamani (mijawapo lenye bango kitita za Marabi chini yake) zinasomeka Adonai. Kwene aya ya 13 tunasoma kwamba ni mjumbe wa Yehova Adonai. Hivyo, tunashughulikia kuhusu Yehovi au Yehova mkubwa wa Majeshi na tunaamini kuwa huyu ndiye mwanae ambaye alikuwa ni Masihi. Alipewa fimbo. Upanga unaotajwa kwenye aya ya 11 ilikwenda kwa mfalme wa Babeli akiwa kama mchinjaji lakini bado huu ulikuwa ni upanga uliowekwa kwenye bustani ya Edeni. Hivyo Kristo aliuitimiliza unabii huu. Upanga wa mwanawe ulidharauliwa kwa kusulibiwa. Upanga uliilaumu fimbo na kwa hiyo hata huo upanga hautaweza kuwepo tena. Kwa hiyo kuhusu mwana na kifo chake ni mambo yaliyo wazi sana kwenye maandiko ya Agano la Kale. Masihi ni mdogo kwa Yehova wa Israeli ambaye alitumwa na Yehova wa Majeshi.

 

Andiko hili linahusu kuchinjwa na maangamizo ya Israeli, na kukomshwa kwa ufalme, ambao kwamba siku yake inakujaa ambapo uovu utakoma (aya ya 25). Kwa hiyo ndipo ufalme utakoma hadi atakaporudi Masihi, ambaye haki ni yake (aya ya 27).

 

Muundo wa shina la Jah (au Yaho)

Yehova ni jina moja tu linalomtambulisha Mungu na pia kwa wasaidizi wake wanaolitumia jina lake. Muundo msingi wa kiini cha jina hili ni Jah ambalo pia ni jina linalomhusu na kumtaja Mungu. Yehova wa Israeli hakuwa ndiye mlengwa kwenye maombi au ibada. Mlengwa kwenye maombi ni Yehova wa Majeshi. Jina la Hekalu lilitokana na chimbuko la jina hili likiandikwa na kutamkwa Yaho ambayo ndiyo neno la kale lililomaanisha kuwa ni Jah au Jahh. Hili pia limeorodheshwa kuwa ni kama jina la Mungu kwenye Zaburi.

 

Zaburi 68:4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mtengenezeeni njia ya barabara, Apitaye majangwani kama mpanda farasi; Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.

 

Mahala pa kwanza kujitokeza jina Jah ni kwenye Kutoka 15:2. Hivyo, ni sahihi sana kusema kwamba mfano huu upo kwenye sehemu ya pili au kwenye kitabu cha Kutoka cha Zaburi.

 

Kutoka 15:2 Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.

Huyu Jah anatajwa hapa kama ni Bwana. Dhana ya kuwepo kwa kiumbe anayemiliki au kutamalaki inaonekana. Inatumika kwa mara ya kwanza kwenye Biblia kunahusianishwa hapa na ukombozi. Yeye ni El na ni baba wa hawa elohi.

 

Kisha aya ya 3 inaendlea kusema kwamba Yehova ni ish au mtu wa vita.

 

Kutoka 15:3 Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake

 

Hapa Yehova anaitwa Bwana.

 

Kwa hiyo Sifa zinatolewa kwa jina la Jah, kwenye Zaburi 68:4. Andiko lililo kwenye aya ya 8 linautaja uwepo wa Mungu kwenye Kutoka.

 

Zaburi 68:8 Nchi ilitetemeka Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.

 

Huyu Mungu wa uwepo wake alikuwa ni Malaika wa Yehova. Alikuwa hapa kama pani au uwepo wa elohim au peni-el, Uso wa Mungu. Uwepo ulikuwa pamoja nao jangwani. Andiko hili linamtaja elohim, elohi wa Israeli, Mungu, Mungu wa Israeli.

 

Zaburi 68:17 inaonyesha maana nyingine kwenye ustadi wa kuumba.

 

Zaburi 68:17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu; Bwana yumo kati yao kama katika Sinai, Katika patakatifu.

 

Andiko hili lina maana ile ile na nyingine. Tafsiri ya The Companion Bible inalibaini andiko lisemalo kwamba idadi ya magari ya Mungu aliyoandikwa kwa lugha ya Kiebrania ni mara mbili ya maelfu kumi na makumi elfu mengine, ambayo ni idadi ya milioni ishirini. Andiko hili ni kwa mujibu sawa na elimu ya kame ya ki-tahajia kwenye mgawanyo wa neno (Companion Bible fn.), ambayo ingesomeka Yehova ameshuka kutoka Sinai na kuja kwenye Maskani (Ginsburg, Intr., pp. 161,162). Au kwa kiudondoo au kwa kutupia maneno ingesomeka kuwa ni Yehova aliye katikati yao (yaani ni malaika na magari) [wamekuja kutoka Sinai] na kuingia kwenye Maskani. (Linanisha na isemavyo Biblia.).

 

Tafsiri ya andiko hili imeendelezwa kwenye aya nyingine inayofuatia ya 18.

 

Zaburi 68:18 Wewe umepaa juu, umeteka mateka, Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; Naam, hata na wakaidi, Bwana Mungu akae nao.

Yehova anayetajwa hapa kuwa ameshuka mahala pa juu na kuwapa vipawa wanadamu na hata kwa wale malaika waasi ili kwamba huyu Bwana Mungu au Jah Elohim aweze kuwa pamoja nao. Hii ni rejea ya moja kwa moja ya tukio lililofanyika siku ya kuutoa Mganda wa Kutikiswa utowao siku ya Kwanza ya juma au Jumapili asubuhi saa 3 kamili. Kristo alitolewa kuwa ni sadaka ya Mganda wa Kutikiswa na akapokea vipawa ili awape wanadamu, kipawa kijulikanacho kama Roho Mtakatifu. Kutokana na andiko la Yohana 20:17 Kristo alimhakikishia Mariamu kuwa Anapanda kwenda kwa Mungu na Baba yetu wote. Kwenye Yohana 20:19-22 tunaona kwamba hatimaye alirejea siku hiyohiyo na kuwapulizia pumzi ya Roho Mtakatifu kwa Wanafunzi, akiashiria kukubalika kwake na kuwapa vipawa vilivyoahidiwa kwenye Zaburi 68:18 na kwamba sasa zinatolewa rasmi na Baba kwa Kanisa ili kuanza mchakato wa kuwatuma waende. Siku hii ilianzisha kipindi maalumu cha Hesabu ya kuelekea kwenye Pentekoste ambako ndiko vipawa au karama za Roho Mtakatifu vitatolewa kwa kanisa zima lote. (Soma pia jarida la Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa (Na. 106b)).

 

Jah au kwa usahihi zaidi inaandikwa Yaho ni neno shina ya jina linalomtaja Mungu kwendana na uwakilishi na namna zake. Jah [wa] Elohim ni sawa tu na Yehova wa Majeshi. Yehowa mdogo anatajwa hapa kuwa amewatoa watumwa kutoka utumwani ili kwamba viumbe wote wa namna mbili zote, yaani watiifu na waasi waweze kupatanishwa na Mungu. Kiumbe huyu anayewaokoa au kuwatoa watumwa kutoka utumwani anaonekana kwenye andiko hili na kutajwa kuwa ni Kristo kwa rejea iliyo kwenye Waefeso 4:8 na Ufunuo 13:10. Alipokea vipawa kutoka kwa Mungu na alivitoa kuwapa wanadamu.

 

Waefeso 4:7-8 Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. 8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.

 

Andiko hii linamlenga Kristo na kumtaja kuwa ni malaika aliyetumwa kuwasaidia Israeli. Hapa Paulo anataja tukio la kupaa kama kulivyoelezewa kwenye Zaburi 68:17 lakini hakuondoi somo lenyewe kamili la maana yake kwenye andiko hili.

 

Sambamba nayo, kwenye Ufunuo kunazitafsiri aya hizi kuhusu kuwatoa watumwa au wafungwa utumwani hivi:

 

Ufunuo 13:10 Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.  

 

Ni wazi kabisa kwamba Yehova hapa ni Kristo ambaye pia ni Malaika wa Yehova. Kwa hiyo, Yehova ni jina la uwakilishi tu. Yehova hastahili kuabudiwa. Ni kwa pale anapodhihirishwa tu kuwa ni Yehova elohim au Yehova wa Majeshi anaweza kujulikana au kuchukuliwa kuwa anastahili kuabudiwa. Ni jina la Mungu tu peke yake ambalo linamtaja na kumdhihirisha Baba kwa neno moja ni Eloah. Inampasa Yehova aambatane na maneno mengine au achukuliwe kwenye mstakabala wa kuonyesha mhusika. Kwa hiyo, Mungu Baba anaweza kujulikana tu kama hivyo kwa neno Eloah. Linapotumiwa kwa mtindo wa shina la neno lenyewe la Jah, ndipo lazima iwe kuwa anayetajwa hapo awe ni Mungu.

 

Matumizi ya neno Jah yanawezesha utendaji kazi kwene maandiko. Linatokea kwa takriban mara arobaini na tisa, jambo linaloonekana kuwa ni hitimisho la mizunguko saba. Lina maana yake Fulani na maalumu kama Yehova amefanyika kuwa wokovu wetu. Linakamilisha mara 49 au mizunguko ya kuingilia kwenye Patakatifu pa Patakatifu kwenye mzunguko wa Hamsini ambao ni ishara kamili ya Hekalu la Mungu ambalo sisi ndilo Hekalu lake.

 

Hekalu limeitwa kuwa ni Hekalu la Yaho kutokana na herufi na uandishi wa lugha ya Kiaramu la Hekalu lililoko huko Elephantine (soma kitabu cha Pritchard, cha The Ancient Near East etc., vol I, pp. 278-280). Kwa hiyo Jah linalitaja jina la kale la Yaho lililotumika tangu takriban mwaka 407 KK. Kwa hiyo, namna sahihi ya kimuundo la kiuandishi la Yehova ni Yahova au Yahovih kutegemea kisarufi kilichotumika anapotajwa kiumbe mwenyewe. Linatamkwa Yahowe au Yahowih. Neno Yahweh kwa hiyo ni sahihi sana (soma jarida la Abracadabra: Maana ya Majina (Na. 240)).

 

Umakini ni lazima uchukuliwe katika kumuonyesha au kumwelezea Yahowe kuwa ndiye anayestahili peke kuabudiwa. Vinginevyo kama hataonyeshwa na kueleweka kuwa ni kama Mungu mkuu, Yahovah wa Majeshi ambaye ni Eloah, na hapa ndipo imani juu ya Mungu mmoja inakanganywa na ndipo imani ya Kibinitariani inapoanzia.

 

Jina Yehova au Yahova linajumuishwa na majina mengine kumi. Yamepangiliwa kwa mpangilio sawia na yanatokea kwenye maandiko ya Kiebrania yafuatayo kama hivi:

1.       Yehova-Yire Yehovah ataona au atatupatia mahitaji yetu (Mwanzo 22:14).

2.       Yehova-Ropheka Yehova awaponyaye ninyi (Kutoka 15:26).

3.       Yehova-Nissi Yehova bendera yangu (Kutoka 17:15).

4.       Yehova-Mekaddishkem    Yehova awatakasaye ninyi (Kutoka 31:13; Walawi 20:8; 21:8; 22:32; Ezekieli 20:12).

5.       Yehova-Shalom Yehovah [aletaye] atumaye amani (Waamuzi 6:24).

6.       Yehova-Zeba’oth Yehova wa Majeshi (1Samweli 1:3 na sehemu nyingine nyingi tu).

7.       Yehova-Zidkenu Yehova ni haki yetu (Yeremia 23:6; 33:16).

8.       Yehova-Shamma Yehova yupo hapa (Ezekieli 48:35).

9.       Yehova-’Elyon Yehova Aliyejuu Sana (Zaburi 7:17; 47:2; 97:9).

10.   Yehova-Ro’I Yehova mchungaji wangu (Zaburi 23:1).

 

Zaburi ya Ishirini na Tatu inatumia tabia saba zilizotajwa kwenye majina haya ya Mungu:

Aya ya 1; inaendeleza dhana 1 (Yehova-Yire).

Aya ya 2; inaendeleza dhana 5 (Yehova-Shalom).

Aya ya 3; inaendeleza dhana 2 na 7 (Yehova-Ropheka na Yehova-Zidkenu).

Aya ya 4; inaendeleza dhana 8 (Yehova-Shamma).

Aya ya 5; inaendeleza dhana 3 na 4 (Yehova-Nissi na Yehova Mekaddishkem).

 

Tafsiri ya the Companion Bible ina mkururo wa hoja (Nyongeza 4) kuhusu El kuwa ni muhimu sana na ndiye mwenyezi ingawaje neno lenyewe halijaashiria kuwa hivyo kabisa. Dhana hii kwa kweli ni kama El Shaddai. Matumizi ya neno El yanatumiwa ni kumaanisha kuwa Mungu ana uweza wa kipekee wa Kuelewa kila jambo. Elohim linatumika kwa maana ya kwamba Mungu ni Muumbaji kwa kuwa Mungu anaumba na ameziweka kanuni au sheria na torati mikononi mwa waombezi au wapatanishi. Elohim ni uwingi. El linatumika kama shina kwa maelekezo muhimu ya kumuelezea Mungu. Ni Eloa tu peke yake ambaye ndiye Mung anayependa na ni mmoja peke yake anayestahili kuabudiwa na watu wake (soma pia tafsiri ya Companion Bible. Jalada ya Nyongeza 4). El inadhaniwa kuwa ni Mungu ajuaye mambo yote au kila jambo (limejitokeza kwa mara ya kwanza kwenye Mwanzo 14:18-22) na aonaye mambo yote (Mwanzo 16:13) na anawafanyia kila jambo watu wake (Zaburi 57:2) na ni ambaye kwa yeye mambo yote ya mbinguni nay a kimungu yanahusika (Comp. Bible ibid.). Hata hivyo kuna ukweli kwamba neno El ni shina linalojitokeza kwenye majina na vyeo vinavyoashiria au kuonekana kwamba ni shina tu ambalo kwamba linafanya tofauti ya viwango inayoonekana kwenye vitu ambavyo vinatenda kazi kwa kuwakilisha. Kwa mfano, Malaika wa Yehova pia ni El Bethel au Mungu wa Nyumba ya Mungu. Kwa maneno mengine, inaonesha mamlaka au uweza kwenye muunganiko huo. Ni Eloah t uni namna moja ya uenezi wa kiibada.

 

Eloah ni Elohim wa Elohim; Yeye atiaye mafuta (Zaburi 45:6-7; Waebrania 1:8-9). Eloah ni Mungu Apendaye. Mungu huyu nuyu ndiye anayestahili kuabudiwa na ni kini na mlengwa mkubwa wa Elohim. Huyu ndiye aliyependa na nye aliyependa na ni katika yeye vitu vyote vimekuwapo na viliumbwa (Ufunuo 4:11).

 

Ufunuo 4:11 Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.

 

Huyu ndiye mlengwa na anayestahili kuabudiwa na wazee ishirini na nne na mwana kondoo ambaye ni Masihi (Ufunuo 4:1-5:14). Masihi ndiye mwana na mzaliwa pekee na Eloah ni Baba kutokana na Mithali 30:4-5. Kujitokeza kwake kwa kwanza kwa jina hili kunahusiana na stahili yake ya kuabudiwa (Kumbukumbu la Torati 32:15,17). Linatumika kwa namna tofauti na sanamu naye ndiye Mungu aishiye na aliyehai. Huyu ndiye Mungu ambaye hapatwi na madhara wala hafi (1Timotheo 6:16). Wengine wote wanapata uzima wa milele kutoka kwake kwa mapenzi na maelekezo.

 

El Elyon ni jina linalommaanisha Eloah kuwa ndiye El Aliye Juu Sana. Yeye ni Mungu wa peke na Aliye Juu Sana na ni Baba kama tunavyojua kutokana na lugha ya Kiyunani inayomtaja hivyo kwenye Luka 1:35. El Elyon ni kiumbe aliyeyagawanya mataifa (Kumbukumbu la Torati 32:8). Aliwapa Israeli kama sehemu ya Yehova. Kwa hiyo, Yehova hapa ni Yehova wa Israeli na ni mdogo kwa Eloa au El Elyon. Ni huyu Eloah au Elyon ndiye mlengwa na anayestahili kuabudiwa. Israeli hawabumuabudu huyu elohim mdogo. Tilia maanani kwamba andiko la Kumbukumbu la Torati 32:8 limepotoshwa kwenye maandiko yaliyo kwenye tafsiri ya Masoretic ili isomeke sawasawa na idadi ya Wana wa Israeli zaidi kuliko kama ilivyoandikwa kwenye maandiko yake asilia yasemayo wana wa Mungu au idadi ya malaika (LXX) au eliym au miungu (DSS).

 

Mwanzo 14:18-22 inaonyesha kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye amiliki wa mbingu na nchi na kwamba Melkizedeki ni kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana nay eye mwenyewe hawezi kuwa ndiye huyo Mungu. Mtu hawezi kuwa kuhani anayejitolea dhabihu mwenyewe. Maandiko haya yapasa kulinganishwa na Zekara 6:13 na 14:9.

 

Zekaria 6:13  Naam, yeye atalijenga hekalu la Bwana; naye atauchukua huo utukufu; ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi; na kutakuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi; na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili.

 

Kwa hiyo tunaelewa kwamba kiti cha enzi cha Mungu Aliye Juu Sana anatawala na Masihi kwa kuelekezwa. Muungano wa ufalme mfumo wake unatokana viumbe walio chini ya mapenzi ya Eloah.

 

Zekaria 14:9 Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja.  

 

Yehova (iliyotafsiriwa Bwana) atakuwa mfalme juu ya dunia na ulimwenguni kote. Kisha Yehova atakuwa ni mmoja (ehad) na jina lake litakuwa moja (ehad). Huu umoja unaoainishwa wa utawala wa Yehva ni kwamba Mungu anafanika kuwa yote katika yote na ndani ya yote (1Wakorintho 15:28; Waefeso 4:6).

 

Waefeso 4:6  Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.

 

Kwa hiyo Mungu ni Baba tu na yupo juu ya mambo yote na kila jambo. Kristo amejumuishwa kwenye mahudhui haya.

 

1Wakorintho 15:28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.

 

1Wakorintho 15:28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.

 

Wakati vitu vyote vinapotiishwa chini yake, ndipo hapo mwana mwenyewe atajinyenyekeza kwa Mungu na kukabidhi vitu vyote aliyemkabidhi mambo yote na kuviweka chini yake ili kwamba Mungu afanyike kuwa yote katika yote. Tafsiri ya RSV haiko sahihi ikionekana kutokana na shauku yake ya kukusudia kuyashinda mahitimisho yote na hoja zinazotolewa na wale wasioamini Utatu yaliyochukuliwa kutoka kwenye andiko hili. Mungu atakuwa ndani ya yote kama alivyo ndani ya Kristo.

 

Kwa hiyo, Elyon yupo ulimwenguni kote (Zaburi 83:18). Jina hili la kicheo linakutikana mara 36 au 6 x 6 ambayo inamaana yake fulani inayohusiana na uumbaji wa mambo yote.

 

Shaddai inamaanisha Mwenyezi kwa maana ya kuwapatia watu vitu na mahitaji yao. Limetumika wakati Ibrahimu alipoitwa atoke ili aenende pamoja naye kwenye Mwanzo 17:1. Mtazamo wa kuitwa atoke uliitikiwa na Ibrahimu na unakubalika pia na Kanisa 2Wakorintho 6:18.

 

2Wakorintho 6:17-18 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,

 

Kwa mara nyingine tena tunamtaja Mungu Baba. Neno lililotumika ni El Shaddai.

 

Adon. Ni moja kati ya majina matatu ya kicheo, (ambayo ni Adon, Adonai, Adonim). Kwa ujumla yanaitwa na kutamkwa kama Bwana. Kwa ujumla, yanamaana ya Bwana kama mtawala wa dunia. Inatofautiana na neno Adonai ambalo linatumika kama linachukua mapenzi ya Mungu hapa duniani. (Bwana katika uhusiano wake na dunia Companion Bible ibid.). Vokali inaoonyesha uhusiano wake na Yehova wakati inapotumika na Adon inasikika au kufanya ionekane na kusomeka Adonai. Hii ilifanyika kwa makusudi kabisa kwenye vifungu vya 134 ambavyo vimegeuzwa kwa kupotoshwa na kutolewa kwenye tafsiri ya Massorah (§§ 107-115) (soma poa kwenye tafsiri ya Companion Bible App. 32 ili kupata orodha yake).

 

Adonim ni uwingi wa Adon na haijatumiwa kabisa kwa mwanadamu (Comp. Bible ibid.). Imerahisishwa kwamba huenda Adon anaweza kuwatawala wengine ambao hawapo upande wake. Kwa hiyo, pasipo na kijimakala hicho ingeweza kutumiwa na watu. Bullinger haelezei kwa kina sana na uwingi na umoja kwenye matumizi ya maneno yanayohusiana na viumbe wa mbinguni. Hakuna mashaka kwamba matumizi ya neno Adonai na elohim yalitumika ili kuweka tofauti fulani na maalumu kati ya majina haya mawili ya Yehova na Yehova wa Majeshi. Yehova kama lenyewe lilivyo tu (SHD 3068) ni elohi wa taifa wa Israeli (soma kamusi ya Strongs) na hapaswi wala sio mlengwa wa kuabudiwa. Yehovih (SHD 3069) ni ni mkuu kwa Yehova, ni elohi wa Israeli ambaye pia anaitwa Malaika wa Yehova.

 

Yehova kwa maneno mengine na kama Adonai Yehova anaitwa Bwana Mungu na kwa hiyo ni tofauti na matumizi ya umoja. Kuna maneno mawili yanayoitwa na kumaanisha Bwana Mungu nayo ni Adonai Yehova na Yehova Elohim. Neno moja au jina elohim mara nyingi linatumika kwa malaika na hasahasa Malaika wa Yehova ambaye ni elohim aliyetiwa mafuta kwenye Zaburi 45:6-7 na ambaye ndiye Kristo (Waebrania 1:8-9).

 

Kwa hiyo, Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.

Kwa jinsi hiyohiyo ndipo sisi sote tutakapofanyika kuwa elohim chini ya jina lake na uweza au nguvu zake (Zekaria 12:8) kwenye imani ya Mungu mmoja iliyoko kwenye nadharia ya Biblia. Imeandikwa Mimi nimesema, Ndinyi Miungu; Wana wa Aliyejuu Sana ndinyi nyote na Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka (Yohana 10:34-35). Imani za Kibinitariani/Kitrinitariani zinaknza kuelewa dhana na nadharia kwamba tutatawala pamoja na Mungu.

 

q